Riwaya ya Kijasusi; Mtoto wa Rais

Oh my God poti sina neno imebaki mwili tu ndo unatetemeka asante sana wanyumbani
 
RIWAYA; MTOTO WA RAIS
Imeandikwa na HalfaniSudy
Simu 0652 212391

Sehemu ya Kumi na Moja

Donald Tengo akahema kwa nguvu, akajaribu kuipiga tena ile namba lakini ilikuwa haipatikami.

"Kuna nini Mheshimiwa Donald?" Balozi Rwekaza aliuliza.

"Wanangu wametekwa!" Donald alisema kwa kulalama.

"Wametekwa? Na nani?"

"Sijajua bado ni kina nani wamewateka. Ila mtekaji amesema nimpigie baada ya nusu saa aniambie nini anataka kutoka kwangu?"

"Safi, tutumie nafasi hii kumnasa mtekaji"

"Kivipi mzee Rwekaza?"

"Tumwite Amanda atusaidie kunasa mahali alipo mtekaji wakati ukimpigia simu. Tukishalijua eneo tunaandaa shambulio la kwenda kuwaokoa watoto wako" Mzee Rwekaza alisema.

"Good Mzee Rwekaza, umewaza vizuri sana. Unajua uwezo wangu wa kufikiri umepungua sana baada ya tukio hili. Mpigie Amanda"

Baada ya dakika kumi Amanda alifika pale sebuleni. Mzee Rwekaza alimuelekeza jambo la kufanya. Amanda alitoa tarakilishi mpakato yake na kuunganisha na simu ya Donald Tengo. Wakati akishughulika akauliza.

"Vipi John alikupigia?" Amanda aliuliza.

"Daah hili tukio limeharibu kabisa uwezo wangu wa kufikiri. Sijawaza kumpigia dereva wala mlinzi wangu. Sijui akili zangu zimeenda wapi? Sijamwambia hata mama yao"

"Usihofu Mheshimiwa Donald. Tulimalize hili kwanza, kisha tuone ilikuwaje watoto wakatekwa"

Baada ya nusu saa kupita, Donald akaipiga ile namba ya mtekaji. Sasa simu ilipatikana.

"Hallo" Donald aliita simuni.

"Habari za sahivi mheshimiwa Donald Tengo" Sauti ya mtekaji ilisema.

"Nzuri kijana, vipi wanang..." Donald Tengo akataka kupoteza muda ili Amanda afanye kazi ya kunasa eneo inapotokea simu ile.

"Najua unachojaribu kufanya mheshimiwa Donald. Na hii inaonesha kwa namna gani usivyowependa wanao"

"Sijakuelewa kijana.."

"Najua unajaribu kuidukua simu hii lakini tambua kuwa hatopata kitu huyo mtu wako" Mtekaji alitoa kauli iliyomchanganya kila mmoja.

Donald Tengo alihamanika. Alichanganywa sana na maneno ya mtekaji.

"Unayafanya yote hayo kwakuwa hujui wanayoyapitia wanao. Nitakapokutumia maiti za wanao ndio utanielewa! Naitwa Daniel Mwaseba!"
Simu ikakatwa.

Mheshimiwa Donald Tengo jasho lilimtoka. Moyo ulimwenda mbio, hakuweza kuvumilia, chozi lilimdondoka.

"Pole sana Mheshimiwa Donald" Mzee Rwekaza alisema.

Donald alimwangalia tu, macho yake yakijitahidi kuzuia machozi.

"Umegundua lolote Amanda?" Mzee Rwekaza akamgeukia Amanda.

"Maajabu, maajabu makubwa sana, mfumo unaonesha mahali ilipopigwa simu hiyo ni hapahapa nyumbani kwako" Amanda alisema akiwa amechoka.

"Tunafanyaje sasa?" Mzee Rwekaza aliuliza.

"Tushamjua mtekaji wa watoto wa Mheshimiwa Donald, tushamjua mtu aliyesababisha ajari ya Alexander na kumteka. Sasa ni kuingia mtaani na kumsaka huyo Daniel Mwaseba. Na tutampata, tutampata tu!!" Amanda alisema kwa hasira.

"Watoto wangu!" Donald Tengo alisema kwa hasira.

"Tutawapata mkuu. Tukimpata Daniel Mwaseba tumewapata watoto wako. Lakini kwanini mlinzi na dereva wako hawajakwambia kitu mpaka sasa?" Amanda aliuliza swali kwa uwoga.

"Wote wamekufa!" Sauti ngeni ilisikika mle ndani. Ulikuwa ugeni wasioutegemea. Alikuwa ni Daniel Mwaseba amesimama katikati ya mlango wa kuingilia sebuleni.

"Nimekufata nyumbani kwako, nimekufata Donald Tengo. Nimeona kwenye simu hatuwezi kuelewana. Nimeona nikufate hapa. Ni kweli nimewashikilia watoto wako wawili, hivyo usijidanganye kufanya ujanja wowote ule. Watauwawa!
Nikwambie tu wakati ninyi mkijaribu kuidukua simu yangu mimi nilikuwa katika harakati za kuingia hapa. Wakati mkiwa katika mchakato wa kuidukua simu iliyounganishwa na mtandao mimi nilikuwa ninamuua mlinzi wako wa mwisho. Sasa ni mimi na nyinyi baada ya kuwauwa walinzi wako nane huko nje.." Daniel alisema kwa kujiamini.

"Unataka nini hasa wewe?" Donald Tengo aliuliza kwa sauti dhaifu.

"Unataka kujua ninataka nini? Ninataka kujua kiongozi wenu wa mpango wa kumuondoa rais Profesa Mark madarakani!!"

Mstuko ulitokea katika sura zote tatu. Hawakutegemea, katu hawakutegemea mipango yao kustukiwa mapema kabisa.

"Nani kiongozi wenu?"

Ukumbi ulikuwa kimya.

"Donald, upo tayari kushuhudia watoto wako wakiuwawa kwa kumficha mkuu wa huu mpango haramu? Sio mwanaume wewe, sio baba, sikuzote baba yupo tayari kufanya lolote lile ilimradi kuiokoa familia yake, laki.." Daniel hakumaliza kuongea. Mdomo wa baridi kutoka katika bastola ya Kizito ulikuwa umemgusa shingoni.

"Mwisho wako! Huu ni mwisho wako Daniel Mwaseba!" Kizito alisema akiwa nyuma ya Daniel.

"Kizito, Daniel kashikilia watoto wangu.."

"Nasi tunamshikilia yeye. Wakiuwawa watoto wako naye tunampeleka kuzimu!" Kizito alisema.

"Amanda njoo umpekue huyu mwanaharam!" Kizito alisema. Amanda alimsogelea Daniel kwa tahadhari kubwa sana. Alimpekua kila sehemu ambayo alihisi kutakuwa na silaha. Akapata bastola tatu, mabomu matatu ya mikono na visu vinne.
"Mpeleke chumba cha mateso tukamuoneshe dunia!"

***

Kule katika nyumba ya Daniel, wakina Martin walikuwa wanashuhudia kila kitu kupitia kamera ndogo aliyoibandika katika kifungo chake cha shati.

"Wanaenda kumtesa Daniel" Hannan alisema kwa majonzi.

"Ndivyo alivyotaka Daniel, kujikamatisha kwa Donald Tengo ili apate nafasi ya kuipata kasiki ya siri. Daniel anajua hawezi kuuliwa kwakuwa bado tunawashikilia wanawe" Martin alisema.

"Atateswa lakini.." Hannan alilalama.

"Ndio maana kavaa ile kamera, akiteswa tutaona kila kitu nasi tutawatesa watoto wake, kisha tutamtumia video ya mateso Donald Tengo. Hawawezi kuendelea kumtesa Daniel" Martin alisema.

"Daniel mbishi sana. Nilimwambia aache huu mpango sio nzuri lakini hakutaka kunisikia. Ona sasa yupo majaribuni. Ule mpango wa awali wa kuwatumia watoto wa Donald Tengo ulikuwa bora sana. Donald angefunguka tu. Asingevumilia kuona watoto wake wanateseka" Hannan alilalama.

"Huu sio muda wa kulalamika Hannan, ni muda wa kuona mipango yetu inaendaje. Ni muda wa kuona tunamuokoaje Daniel endapo mpango wetu wa awali ukifeli. Daniel anatutegemea sana sisi, tukifeli sisi tumemfelisha na yeye. Lazima tuwe imara katika wakati huu kuliko wakati wowote" Martin alisema.

Hannan alivuta pumzi kubwa. Aliuona ukweli katika maneno ya Martin.

"Kuna kitu nilikiona wakati napekua taarifa za Donald Tengo lakini sikuwaambia" Hannan alibadilisha mada.

"Kitu gani hicho uliona Hannan?"

"Ni taarifa niliyoikuta katika mtandao wa siri sana wa majasusi. Na niliamua kuzipeleleza zaidi mwenyewe baada ya kudukua simu ya Magdalena Lema"

"Magdalena Lema? Mke wa rais?" Martin alishangaa.

"Ndio Martin"

"Niambie taarifa gani hizo ulizozipata?"

"Donald Tengo ana uhusiano wa siri wa kimapenzi na mke wa rais!!"

"Unasemaje Hannan?" Martin alishangaa.

"Donald Tengo anatembea n
mke wa rais!" Hannan alirudia.

"Kwanini hukutuambia wakati tupo na Daniel?"

"Niliamua kuthibitisha kwanza taarifa hizi ndipo niwaambie. Lakini kwa bahati mbaya kabla sijawaambia Daniel aliamua mpango mwengine. Mpango wa kujitekesha kwa makusudi ili apate nafasi ya kuipata Kasiki ya siri ya Donald Tengo.."

"Daah hiyo ni siri nzito sana umegundua Hannan. Mke wa Rais kutembea na waziri wa fedha katika Serikali ya mumewe ni bonge la kashfa. Natamani Daniel angekuwepo hapa tuone angekuwa na mawazo gani juu jambo hili" Martin alisema.

"Hapa hayupo Daniel, tupo sisi, tunaweza kufanya kitu ambacho akija Daniel tunaweza kuendelea nacho" Hannan alisema.

"Umewaza kufanya nini Hannan katika suala hilo?"

"Mimi ninaona tumchimbe zaidi Magdalena Lema, huenda tukapata kitu zaidi"

"Sawa Hannan" Martin alikubali.

Hannan alianza kubofya tarakilishi yake, wakati Martin alikuwa makini na picha za kamera ya siri ikiyoonesha chumba cha mateso alicholazwa Daniel Mwaseba.

"Ona, ona Martin.." Martin aliacha kuangalia picha za kamera na kwenda kwa Hannan.

"Umeiona hii picha" Hannan aliuliza.

Martin aliingalia ile picha. Mstuko ulionekana usoni mwake.

"Umeitoa wapi hii picha?" Martin aliuliza.

"Nimempekua mke wa rais katika ukuta wake wa mtandao wa facebook. Hakukuwa na lolote la kumtilia shaka. Nilianza kuangalia picha zake mbalimbali. Ndipo nikaiona picha moja amepiga na mwanamke mmoja. Juu ya picha aliandika

'Rafiki yangu wa siku zote'

Katika picha hiyo alikuwa amemshirikisha huyo mwanamke. Huyu mwanamke kwa majina anaitwa Salma Lungu. Niliamua kumpekua huyu Salma Lungu hukohuko facebook. Baada kuangalia picha kadhaa za Salma ndipo nikaikuta picha hii" Hannan alisema.

Martin aliiangalia kwa umakini ile picha "Bila shaka huyu wa kushoto ni Salma Lungu, anayefatia ni Magdalena Lema, huyu mwengine ni Donald Tengo. Ili kuujua vizuri uhusiano wa Donald na Magdalena lazima tumsake huyu Salma Lungu. Ni nani huyo Salma?" Martin aliuliza.

"Cha kushangaza, nimejaribu kumpekua Salma kwa namna nyingine. Lakini hakuna taarifa zozote zile kuhusu yeye, sehemu yoyote ile"

"Inawezekana vipi kusiwe na taarifa zake mtandaoni. Ila hii sura sio ngeni kwangu, ni kama nimewahi kumuona mahali fulani. Tunafanyaje sasa kumpata?"

"Ngoja niangalie vizuri ukuta wa Facebook wa Salma nione anatuma sana picha akiwa maeneo gani? Huo utakuwa ni mwanzo nzuri wa kumjua zaidi"

"Sawa"

Hannan akapekua kama dakika kumi hivi, kisha akasema
"Njoo uone hii picha Martin"

Martin akasogea katika tarakilishi ya Hannan

"Kuna nini Hannan?"

"Angalia hii sebule, hujawahi kuiona?"

"Aaah hi ni sebule ya ya Donald Tengo, kama tulivyoiona leo katika kamera ya siri aliyoivaa Daniel Mwaseba"

"Naam. Inavyoonesha Salma Lungu na Donald Tengo ni wapenzi pia! Hii aliyoivaa Salma ni gauni ya kulalia, bila shaka siku hii alilala nyumbani kwa Donald Tengo!" Hannan alisema.

"Salma Lungu ni nani haswa?" Hannan alijiuliza kwa sauti ndogo. "Mbona hakuna taarifa yoyote mtandaoni kuhusu Salma Lungu? Nimeangalia hadi katika kanzidata ya vitambulisho vya Taifa, vitambulisho vya kura, hadi RITA katika vyeti vya kuzaliwa. Hakuna taarifa kuhusu Salma Lungu. Ananiumiza sana kichwa. Inamaana hakuzaliwa Tanzania? Hakusoma Tanzania? Ni nani Salma Lungu?" Hannan alisema huku akiipiga kofi tarakilishi yake.

Mara, mwanga ukatokea katika video iliyokuwa inaonesha katika chumba cha mateso alichokuwemo Daniel Mwaseba. Hannan na Martin macho yao yalielekezwa huko.

Video ilionesha mlango ukifunguliwa. Akaingia Amanda akiwa na Kizito.

"Tumekuja kaka. Safari hii tumekuja kivingine, tumekuja kuuliza maswali, nawe utupe majibu. Majibu sahihi ya kila tutakachokuuliza" Kizito alisema.

Daniel aliwaangalia tu huku akiiruhusu kamera yake ikiwamulika wale watu wawili usoni. Alifanya vile makusudi.

"Umemficha wapi Alexander Helb?" Amanda aliuliza.

Daniel alikaa kimya.

Kizito alienda kwenye kabati dogo lililokuwemo mle ndani. Kilikuwa ni chumba kidogo chenye dirisha moja dogo lililokuwa juu kabisa ya kile chumba. Dirisha lisiloruhusu mwanga, hivyo mwanga ulisubiri na mlango ufunguliwe ili mwanga upate kupita.

Ndani ya kabati alitoa waya mdogo ulioambatana na mashine ndogo.

"Kinaitwa kibano hiki, utasema tu wapi ulipomweka Alexander!" Kizito alisema wakati akiunganisha ule waya katika umeme ukutani. Akatoa vyuma viwili virefu, akamvua shati Daniel ili amgusishe vile vyuma. Hapo ndipo wakina Martin walipoteza picha. Kamera ilifunikwa vibaya na lile shati walilomvua.

"Wameitoa kamera?" Hannan aliuliza.

"Hatuwezi kuona kwasasa. Wamemvua shati ili wamtese" Martin alisema.

"Tufanye kama Daniel alivyotuagiza"

***

Kule katika chumba cha mateso wakati wakijiandaa kumtesa Daniel na kibano, ghafla aliingia Donald Tengo.

"Mwacheni, mwacheni, msimfanye kitu" Donald Tengo alisema.

"Kuna nini mkuu?" Amanda aliuliza.

"Angalia" Donald Tengo alimpa simu yake Amanda. Kulikuwa na video fupi, Amanda akaicheza.

"Mimi ni mzalendo kwa Taifa langu. Ujumbe wangu kwako Mheshimiwa Donald ni sasahivi watu wako wako katika harakati za kumtesa Daniel. Nakushauri kawaambie waache mara moja, la sivyo utapokea kichwa cha mwanao mmoja. Nitaanza na Candy!! Naitwa Hannan" Video iliishia hapo.

Wote watatu walitoka nje ya chumba cha mateso jasho likiwatiririka.

Amanda, nini kimetokea?" Donald aliuliza walipofika sebuleni.

"Sijaelewa kwa namna gani watu wake wamegundua kwamba tunataka kumtesa muda huu. Ni mambo ya kushangaza sana" Amanda alishangaa.

"Kuna mambo mawili tu, kati ya hayo moja limefanyika. Aidha Daniel ana kamera ya siri ama ana kinasa sauti!" Kizito alisema.

Donald Tengo alitingisha kichwa kukubaliana nae.

"Mhamisheni katika kile chumba, mpelekeni baharini!!"

Amanda na Kizito walienda katika chumba alichowekwa Daniel, walimfungua kamba na kumpeleka katika chumba kingine. Kilikuwa ni chumba kidogo zaidi, kikiwa hakina dirisha, wala kitu chochote kile ndani yake. Cha kushangaza katikati ya chumba kulikuwa na bomba la maji. Akiwa anatazamwa na midomo miwili ya bastola Daniel alisukwasukwa mle ndani. Kwa umakini mkubwa huku akimwelekezea bastola Daniel alienda katikati ya chumba. Akafungulia lile bomba la maji. Maji mengi yalianza kumwagika mle ndani. Jamaa walifunga mlango na kutoka nje, wakiacha chumba kikianza kujaa maji!

"Mshampeleka baharini?" Donald aliuliza.

"Ndio mkuu" Kizito na Amanda walijibu kwa pamoja.

"Safi, sasa tunaenda kuwasaka wanangu popote pale walipo. Hawa watu wanamtegemea sana Daniel katika mipango yao. Hivyo kumuacha akifa baharini itaturahisishia sisi. Na kama hao wenzake walikuwa wanapata mawasiliano nae kwa kamera au kifaa chochote kile imekula kwao, maana kitakuwa kimesharibiwa na maji" Donald Tengo alisema.

"Ni kweli mkuu. Misheni ya kuwasaka watoto itakuwaje?"

"Ita vijana wa bahari nyekundu kumi. Nitamtumia Dick, yule kijana wetu wa usalama wa Taifa atuambie mahali anapoishi Daniel. Tukishapapata tu tumemaliza mchezo. Watoto wangu lazima watakuwa nyumbani kwa Daniel Mwaseba"

"Hata Alexander atakuwa hapohapo" Kizito alisema.

"Ndio, nilishasahau kuhusu Alexander, kupotea kwa watoto wangu kumeharibu sana uwezo wangu wa kufikiri. Naahidi naenda kuwateketeza vibaya sana hao watu waliowateka wanangu. Watamjua Donald Tengo ni nani! Nahisi hawaujui vizuri upande wangu wa pili. Mimi ni mnyama!" Donald Tengo alisema kwa ghadhabu.

Wote watatu wakajipanga vizuri. Amanda akawapigia simu vijana wa bahari nyekundu, ndani ya robo saa vijana kumi waliwasili wakiwa katika magari mawili. Donald Tengo akampigia simu Dick, mtu wao wanaomtumia katika idara ya usalama wa Taifa kuwapa taarifa. Akawaelekeza nyumbani anapoishi Daniel, wakaelekea huko.

Hannan na Martin walikuwa wamepoteza kabisa mawasiliano na Daniel Mwaseba. Hii iliwapa hofu sana juu ya usalama wa Daniel.

"Tunafanyaje sasa Martin? Daniel hapatikani kwa namna yoyote" Hannan aliuliza.

"Itabidi nimfuate Daniel nyumbani kwa Donald Tengo. Inaonesha Daniel yupo katika hatari" Martin alisema.

"Ni hatari sana kwa wewe kwenda huko. Sitaki kukupoteza na wewe Martin kama nilivyompoteza Daniel. Hawa watoto waliopo hapa hawana thamani yenu nyinyi. Hawana thamani kwangu na hata kwa taifa"

"Hannan, kwenda nyumbani kwa Donald Tengo ni njia pekee ya kumpata Daniel. Pale ni mahali ambapo alipotelea. Na bila shaka ndipo mahali alipo mpaka sasa. Siwezi kumuacha Daniel akiteketea kirahisi kwa namna hii. Licha ya kufanya kazi pamoja kwa muda mrefu lakini Daniel kwangu amekuwa ni kama ndugu. Siwezi kumwacha ndugu yangu akifa kifo cha namna hii, wakati nina uwezo wa kumwokoa. Sitoweza kujisamehe kamwe. Nitaenda kupambana kama ni kufa ni bora na mimi nikafie humo."

"Sawa Martin, mimi nitabaki hapa kuwalinda hawa watoto. Ila usiende hivihivi. Chukua kifaa hiki kitatusaidia katika mawasiliano. Kama utapata tatizo lolote niambie, nitakuwa njiani kuja kukusaidia. Na mimi nife pamoja na ninyi" Hannan alisema kwa hisia.

***

Maji ya baridi yakiyotoka katika bomba, katika chumba alichowekwa Daniel yalikuwa yanamfika katika mabega sasa. Mwanzoni alijaribu kuufungua mlango, lakini utundu wake wa kucheza na milango mbalimbali hapa ulikwama. Mlango wa chuma haukukubali utundu wowote ule. Giza la chumbani, ukichanganya na ubadili mkali wa maji yale yalimtesa sana. Kama wakina Donald Tengo wangerejea na kumuuliza chochote kile, pasi na shaka safari hii angewajibu.

"Mbinu zangu zote hapa zimefika mwisho. Maji haya ya baridi yamezimaliza nguvu zangu. Ninakufa, ninakufa kifo kibaya sana. Ni kweli ninakufa lakini ninaamini wakina Hannan watalimaliza jambo hili, kuhakikisha uhaini huu haufanikiwi, na yoyote yule aliyehusika katika uhaini huu akipelekwa katika vyombo vya dola" Daniel aliwaza wakati maji yakimfikia shingoni.

Wakati huo, Martin Hisia alikuwa anaendesha gari kwa kasi sana. Akielekea katika nyumba ya Donald Tengo. Nusu saa tu ilimfikisha katika nyumba ile ambayo aliamini Daniel alikuwemo. Bila wasiwasi akaenda getini. Akagonga. Akasubiri kama dakika mbili hivi, geti dogo lilifunguliwa, alitoka njemba moja akiwa na bunduki mkononi.

"Wenyewe hawapo.." Njemba ilisema kwa sauti ya kibabe kabla hata hajaulizwa kitu.

"Samahani kaka.." Martin alisema lakini alikatishwa.

"Nimekwambia wenyewe hawapo!" Njemba safari hii alisema kwa ubabe. Na hiyo ndio nafasi aliyokuwa anaisubiri Martin.
Ghafla!
Alimsukumia ndani kwa kutumia kifua chake. Kilikuwa ni kitendo cha ghafla ambacho kilimwacha Njemba akidondoka chini, bunduki yake ikiwa mkononi. Kabla Njemba hajapata nafasi ya kutafakari, Martin alimrukia na kumchoma kisu cha kifua mara mbili. Njemba alitaka kupiga ukelele lakini Martin alimuwahi kwa kumziba mdomo. Sauti yake ikapotelea humo.
Njemba alikata roho.

Martin alienda upande wa kulia wa ile nyumba. Nako kulikuwa na mlinzi aliyekuwa anavuta sigara, bunduki yake ikiwa kaisimamisha ukutani. Kwa haraka akamuwahi risasi moja ya paji la uso kwa bastola yenye kiwambo cha kuzuia sauti. Jamaa akadondoka chini. Martin alizunguka ile nyumba hakuwakuwa na mlinzi mwingine.
Akaingia ndani.

Wakati huo, Donald Tengo akiwa na vijana wa bahari nyekundu walikuwa wanakaribia nyumbani kwa Daniel Mwaseba huko Mikocheni.

"Humu ndani ninaamini ndimo walimo watoto wangu. Kuweni makini kuhakikisha watoto wangu hawapati madhara yoyote yale." Donald Tengo alisema huku wengine wakimsikia kupitia vifaa walivyovaa masikioni mwao.

Na misheni hii ndogo ilianza.

Vijana wa bahari nyekundu walijipanga katika makundi mawili ya watu watano watano. Kundi la kwanza lilipita upande wa mashariki huku wengine wakielekea upande wa magharibi. Donald Tengo, Amanda na Kizito walibaki ndani ya gari huku wakifatilia kwa umakini mkubwa sana kila kitu kinachoendelea.

Baada ya kuhakikisha eneo la nje liko salama, vijana walizama ndani. Silaha zao zikiwa zimetangulizwa mbele. Kwa umakini mkubwa sana walisonga mbele kuifata nyumba ya Daniel Mwaseba. Kwa kutumia funguo maalum walifungua mlango na kuingia ndani. Baada ya dakika tano kifaa cha sikioni cha Donald Tengo kilipata uhai.

"Mkuu tumefanikiwa kuingia ndani lakini hakuna mtu humu ndani?"

"Unasemaje bahari nyekundu?" Donald Tengo aliuliza kwa hamaki.

"Hakuna mtu ndani, tumepekua kila mahali lakini hatujaona mtu. Kuna chumba kimoja tumepekua tumekuta vitu kadhaa vinavyoonesha ni vya Daniel Mwaseba"

"Mmekuta kama kitu gani?"

"Tumekuta nguo na albam ya picha, bila shaka ni za Daniel"

"Ok njoo na hiyo albam ya picha, inaweza kutusaidia. Waweke na zawadi wakutane nayo watakaporudi" Donald Tengo alisema.

Kijana alimwelewa.

Baada ya kuthibitisha kwamba watu wa Daniel hawakuwemo mle ndani walirejea nyumbani.

"Hakuko sawa nyumbani!" Kizito alisema kwa ghadhabu wakiwa kama mita mia moja kufika nyumbani kwa Donald Tengo.

Macho ya Donald nayo yalielekea getini. Aliona geti la nyumba yake likiwa wazi. Ilimpata hofu kuu. Hakutaka kumpoteza Daniel kabla hajawapata wanawe. Walishukia nje, wakatembea kwa tahadhari kubwa wakielekea ndani. Kila mmoja bastola yake ikiwa mkononi. Waliingia mpaka ndani, baada ya kuacha maiti ya mlinzi wake nyuma. Baada ya wale wa awali kuuwawa. Walizunguka nyuma na kukuta maiti ya mlinzi mwengine.

"Adui katoka nje" Kijana mmoja wa bahari nyekundu alisema.

"Kwanini?" Amanda alisema.

"Unaona hizi alama za viatu. Hivi ni viatu vya mvamizi, inaonesha wakati akiondoka" Yule kijana wa bahari nyekundu alisema.

"Twendeni ndani, bado hatujajua uharibifu alioufanya Daniel Mwaseba" Donald Tengo alisema.

Wakaingia ndani, walichokutana nacho huko, wote walibaki midomo wazi.

Sebuleni kulikuwa kumetawanywa vibaya sana. Kila kitu kikiwa hakipo katika mpangilio waliouacha. Friji liligeukia kule, kabati liligeuzwa huku, runinga ilikuwa chini huku makaratasi kadhaa yakiwa yamemwagwa pembeni ya meza ndogo.

Donald Tengo alikimbilia katika chumba ambacho walikiita baharini, alipigwa na butwaa, mlango aliouamini kuliko kitu chochote kile ulikuwa chini. Mlango imara, wa chuma ambao fundi wake alimwaminisha kwamba hakuna atakayeweza kuufungua hapa duniani ulikuwa umefunguliwa. Na ndani ya chumba hiko Daniel Mwaseba hakuwemo. Donald Tengo alichanganyikiwa sana. Kwa kasi alienda chumbani kwake, akachukua rimoti iliyokuwa juu ya feni. Akabonyaza kuelekea ukutani. Ukuta ulisogea, lakini macho yake hayakuamini.

"Wamechukua kasiki yangu ya siri! Oooh tumekwishaaa" Donald Tengo alipiga ukelele mkubwa.
Kwa hakika alikuwa amepatikana!

"Sasa kila kitu kipo mikononi mwake, ushahidi wote anao, huu sio wakati wa vita vya siri tena, ooooh no, Daniel safari hii nikikupata nitakuua mwenyewe, sitojari tena maisha ya watoto wangu!! Lakini amepajuaje mahali hapa nilipoificha kasiki yangu ya siri, amejuaje kama huu ukuta unafunguka? Ni mtu mmoja tu niliyewahi kumwambiai siri hii. Mmoja tu, mpenzi wangu wa maisha Salma Lungu! Je ni yeye ndiye aliyeivujisha siri hii? Haiwezekani, haiwezekani!" Donald Tengo alichukua simu yake na kumpigia Salma Lungu. Simu ilikuwa haipatikani. Na hii ilikuwa ni kwa mara ya kwanza simu ya Salma Lungu isipatikane tangu walipoingia katika mahusiano. Akazidi kuchanganyikiwa.
Akapiga simu kwa Balozi Rwekaza.

"Mzee Rwekaza itisha kikao cha dharura sasahivi" Donald Tengo alisema kwa sauti iliyoambatana na hofu.

"Kuna tatizo gani Donald?" Mzee Rwekaza aliuliza.

"Utajua kwenye kikao.." Donald Tengo alisema na kukata simu.










Itaendelea..
Duh, hii kali, moto, hatari.
Safi sana mtunze na wewe unayepost.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
RIWAYA; MTOTO WA RAIS
Imeandikwa na HalfaniSudy
Simu 0652 212391

Sehemu ya Kumi na Moja

Donald Tengo akahema kwa nguvu, akajaribu kuipiga tena ile namba lakini ilikuwa haipatikami.

"Kuna nini Mheshimiwa Donald?" Balozi Rwekaza aliuliza.

"Wanangu wametekwa!" Donald alisema kwa kulalama.

"Wametekwa? Na nani?"

"Sijajua bado ni kina nani wamewateka. Ila mtekaji amesema nimpigie baada ya nusu saa aniambie nini anataka kutoka kwangu?"

"Safi, tutumie nafasi hii kumnasa mtekaji"

"Kivipi mzee Rwekaza?"

"Tumwite Amanda atusaidie kunasa mahali alipo mtekaji wakati ukimpigia simu. Tukishalijua eneo tunaandaa shambulio la kwenda kuwaokoa watoto wako" Mzee Rwekaza alisema.

"Good Mzee Rwekaza, umewaza vizuri sana. Unajua uwezo wangu wa kufikiri umepungua sana baada ya tukio hili. Mpigie Amanda"

Baada ya dakika kumi Amanda alifika pale sebuleni. Mzee Rwekaza alimuelekeza jambo la kufanya. Amanda alitoa tarakilishi mpakato yake na kuunganisha na simu ya Donald Tengo. Wakati akishughulika akauliza.

"Vipi John alikupigia?" Amanda aliuliza.

"Daah hili tukio limeharibu kabisa uwezo wangu wa kufikiri. Sijawaza kumpigia dereva wala mlinzi wangu. Sijui akili zangu zimeenda wapi? Sijamwambia hata mama yao"

"Usihofu Mheshimiwa Donald. Tulimalize hili kwanza, kisha tuone ilikuwaje watoto wakatekwa"

Baada ya nusu saa kupita, Donald akaipiga ile namba ya mtekaji. Sasa simu ilipatikana.

"Hallo" Donald aliita simuni.

"Habari za sahivi mheshimiwa Donald Tengo" Sauti ya mtekaji ilisema.

"Nzuri kijana, vipi wanang..." Donald Tengo akataka kupoteza muda ili Amanda afanye kazi ya kunasa eneo inapotokea simu ile.

"Najua unachojaribu kufanya mheshimiwa Donald. Na hii inaonesha kwa namna gani usivyowependa wanao"

"Sijakuelewa kijana.."

"Najua unajaribu kuidukua simu hii lakini tambua kuwa hatopata kitu huyo mtu wako" Mtekaji alitoa kauli iliyomchanganya kila mmoja.

Donald Tengo alihamanika. Alichanganywa sana na maneno ya mtekaji.

"Unayafanya yote hayo kwakuwa hujui wanayoyapitia wanao. Nitakapokutumia maiti za wanao ndio utanielewa! Naitwa Daniel Mwaseba!"
Simu ikakatwa.

Mheshimiwa Donald Tengo jasho lilimtoka. Moyo ulimwenda mbio, hakuweza kuvumilia, chozi lilimdondoka.

"Pole sana Mheshimiwa Donald" Mzee Rwekaza alisema.

Donald alimwangalia tu, macho yake yakijitahidi kuzuia machozi.

"Umegundua lolote Amanda?" Mzee Rwekaza akamgeukia Amanda.

"Maajabu, maajabu makubwa sana, mfumo unaonesha mahali ilipopigwa simu hiyo ni hapahapa nyumbani kwako" Amanda alisema akiwa amechoka.

"Tunafanyaje sasa?" Mzee Rwekaza aliuliza.

"Tushamjua mtekaji wa watoto wa Mheshimiwa Donald, tushamjua mtu aliyesababisha ajari ya Alexander na kumteka. Sasa ni kuingia mtaani na kumsaka huyo Daniel Mwaseba. Na tutampata, tutampata tu!!" Amanda alisema kwa hasira.

"Watoto wangu!" Donald Tengo alisema kwa hasira.

"Tutawapata mkuu. Tukimpata Daniel Mwaseba tumewapata watoto wako. Lakini kwanini mlinzi na dereva wako hawajakwambia kitu mpaka sasa?" Amanda aliuliza swali kwa uwoga.

"Wote wamekufa!" Sauti ngeni ilisikika mle ndani. Ulikuwa ugeni wasioutegemea. Alikuwa ni Daniel Mwaseba amesimama katikati ya mlango wa kuingilia sebuleni.

"Nimekufata nyumbani kwako, nimekufata Donald Tengo. Nimeona kwenye simu hatuwezi kuelewana. Nimeona nikufate hapa. Ni kweli nimewashikilia watoto wako wawili, hivyo usijidanganye kufanya ujanja wowote ule. Watauwawa!
Nikwambie tu wakati ninyi mkijaribu kuidukua simu yangu mimi nilikuwa katika harakati za kuingia hapa. Wakati mkiwa katika mchakato wa kuidukua simu iliyounganishwa na mtandao mimi nilikuwa ninamuua mlinzi wako wa mwisho. Sasa ni mimi na nyinyi baada ya kuwauwa walinzi wako nane huko nje.." Daniel alisema kwa kujiamini.

"Unataka nini hasa wewe?" Donald Tengo aliuliza kwa sauti dhaifu.

"Unataka kujua ninataka nini? Ninataka kujua kiongozi wenu wa mpango wa kumuondoa rais Profesa Mark madarakani!!"

Mstuko ulitokea katika sura zote tatu. Hawakutegemea, katu hawakutegemea mipango yao kustukiwa mapema kabisa.

"Nani kiongozi wenu?"

Ukumbi ulikuwa kimya.

"Donald, upo tayari kushuhudia watoto wako wakiuwawa kwa kumficha mkuu wa huu mpango haramu? Sio mwanaume wewe, sio baba, sikuzote baba yupo tayari kufanya lolote lile ilimradi kuiokoa familia yake, laki.." Daniel hakumaliza kuongea. Mdomo wa baridi kutoka katika bastola ya Kizito ulikuwa umemgusa shingoni.

"Mwisho wako! Huu ni mwisho wako Daniel Mwaseba!" Kizito alisema akiwa nyuma ya Daniel.

"Kizito, Daniel kashikilia watoto wangu.."

"Nasi tunamshikilia yeye. Wakiuwawa watoto wako naye tunampeleka kuzimu!" Kizito alisema.

"Amanda njoo umpekue huyu mwanaharam!" Kizito alisema. Amanda alimsogelea Daniel kwa tahadhari kubwa sana. Alimpekua kila sehemu ambayo alihisi kutakuwa na silaha. Akapata bastola tatu, mabomu matatu ya mikono na visu vinne.
"Mpeleke chumba cha mateso tukamuoneshe dunia!"

***

Kule katika nyumba ya Daniel, wakina Martin walikuwa wanashuhudia kila kitu kupitia kamera ndogo aliyoibandika katika kifungo chake cha shati.

"Wanaenda kumtesa Daniel" Hannan alisema kwa majonzi.

"Ndivyo alivyotaka Daniel, kujikamatisha kwa Donald Tengo ili apate nafasi ya kuipata kasiki ya siri. Daniel anajua hawezi kuuliwa kwakuwa bado tunawashikilia wanawe" Martin alisema.

"Atateswa lakini.." Hannan alilalama.

"Ndio maana kavaa ile kamera, akiteswa tutaona kila kitu nasi tutawatesa watoto wake, kisha tutamtumia video ya mateso Donald Tengo. Hawawezi kuendelea kumtesa Daniel" Martin alisema.

"Daniel mbishi sana. Nilimwambia aache huu mpango sio nzuri lakini hakutaka kunisikia. Ona sasa yupo majaribuni. Ule mpango wa awali wa kuwatumia watoto wa Donald Tengo ulikuwa bora sana. Donald angefunguka tu. Asingevumilia kuona watoto wake wanateseka" Hannan alilalama.

"Huu sio muda wa kulalamika Hannan, ni muda wa kuona mipango yetu inaendaje. Ni muda wa kuona tunamuokoaje Daniel endapo mpango wetu wa awali ukifeli. Daniel anatutegemea sana sisi, tukifeli sisi tumemfelisha na yeye. Lazima tuwe imara katika wakati huu kuliko wakati wowote" Martin alisema.

Hannan alivuta pumzi kubwa. Aliuona ukweli katika maneno ya Martin.

"Kuna kitu nilikiona wakati napekua taarifa za Donald Tengo lakini sikuwaambia" Hannan alibadilisha mada.

"Kitu gani hicho uliona Hannan?"

"Ni taarifa niliyoikuta katika mtandao wa siri sana wa majasusi. Na niliamua kuzipeleleza zaidi mwenyewe baada ya kudukua simu ya Magdalena Lema"

"Magdalena Lema? Mke wa rais?" Martin alishangaa.

"Ndio Martin"

"Niambie taarifa gani hizo ulizozipata?"

"Donald Tengo ana uhusiano wa siri wa kimapenzi na mke wa rais!!"

"Unasemaje Hannan?" Martin alishangaa.

"Donald Tengo anatembea n
mke wa rais!" Hannan alirudia.

"Kwanini hukutuambia wakati tupo na Daniel?"

"Niliamua kuthibitisha kwanza taarifa hizi ndipo niwaambie. Lakini kwa bahati mbaya kabla sijawaambia Daniel aliamua mpango mwengine. Mpango wa kujitekesha kwa makusudi ili apate nafasi ya kuipata Kasiki ya siri ya Donald Tengo.."

"Daah hiyo ni siri nzito sana umegundua Hannan. Mke wa Rais kutembea na waziri wa fedha katika Serikali ya mumewe ni bonge la kashfa. Natamani Daniel angekuwepo hapa tuone angekuwa na mawazo gani juu jambo hili" Martin alisema.

"Hapa hayupo Daniel, tupo sisi, tunaweza kufanya kitu ambacho akija Daniel tunaweza kuendelea nacho" Hannan alisema.

"Umewaza kufanya nini Hannan katika suala hilo?"

"Mimi ninaona tumchimbe zaidi Magdalena Lema, huenda tukapata kitu zaidi"

"Sawa Hannan" Martin alikubali.

Hannan alianza kubofya tarakilishi yake, wakati Martin alikuwa makini na picha za kamera ya siri ikiyoonesha chumba cha mateso alicholazwa Daniel Mwaseba.

"Ona, ona Martin.." Martin aliacha kuangalia picha za kamera na kwenda kwa Hannan.

"Umeiona hii picha" Hannan aliuliza.

Martin aliingalia ile picha. Mstuko ulionekana usoni mwake.

"Umeitoa wapi hii picha?" Martin aliuliza.

"Nimempekua mke wa rais katika ukuta wake wa mtandao wa facebook. Hakukuwa na lolote la kumtilia shaka. Nilianza kuangalia picha zake mbalimbali. Ndipo nikaiona picha moja amepiga na mwanamke mmoja. Juu ya picha aliandika

'Rafiki yangu wa siku zote'

Katika picha hiyo alikuwa amemshirikisha huyo mwanamke. Huyu mwanamke kwa majina anaitwa Salma Lungu. Niliamua kumpekua huyu Salma Lungu hukohuko facebook. Baada kuangalia picha kadhaa za Salma ndipo nikaikuta picha hii" Hannan alisema.

Martin aliiangalia kwa umakini ile picha "Bila shaka huyu wa kushoto ni Salma Lungu, anayefatia ni Magdalena Lema, huyu mwengine ni Donald Tengo. Ili kuujua vizuri uhusiano wa Donald na Magdalena lazima tumsake huyu Salma Lungu. Ni nani huyo Salma?" Martin aliuliza.

"Cha kushangaza, nimejaribu kumpekua Salma kwa namna nyingine. Lakini hakuna taarifa zozote zile kuhusu yeye, sehemu yoyote ile"

"Inawezekana vipi kusiwe na taarifa zake mtandaoni. Ila hii sura sio ngeni kwangu, ni kama nimewahi kumuona mahali fulani. Tunafanyaje sasa kumpata?"

"Ngoja niangalie vizuri ukuta wa Facebook wa Salma nione anatuma sana picha akiwa maeneo gani? Huo utakuwa ni mwanzo nzuri wa kumjua zaidi"

"Sawa"

Hannan akapekua kama dakika kumi hivi, kisha akasema
"Njoo uone hii picha Martin"

Martin akasogea katika tarakilishi ya Hannan

"Kuna nini Hannan?"

"Angalia hii sebule, hujawahi kuiona?"

"Aaah hi ni sebule ya ya Donald Tengo, kama tulivyoiona leo katika kamera ya siri aliyoivaa Daniel Mwaseba"

"Naam. Inavyoonesha Salma Lungu na Donald Tengo ni wapenzi pia! Hii aliyoivaa Salma ni gauni ya kulalia, bila shaka siku hii alilala nyumbani kwa Donald Tengo!" Hannan alisema.

"Salma Lungu ni nani haswa?" Hannan alijiuliza kwa sauti ndogo. "Mbona hakuna taarifa yoyote mtandaoni kuhusu Salma Lungu? Nimeangalia hadi katika kanzidata ya vitambulisho vya Taifa, vitambulisho vya kura, hadi RITA katika vyeti vya kuzaliwa. Hakuna taarifa kuhusu Salma Lungu. Ananiumiza sana kichwa. Inamaana hakuzaliwa Tanzania? Hakusoma Tanzania? Ni nani Salma Lungu?" Hannan alisema huku akiipiga kofi tarakilishi yake.

Mara, mwanga ukatokea katika video iliyokuwa inaonesha katika chumba cha mateso alichokuwemo Daniel Mwaseba. Hannan na Martin macho yao yalielekezwa huko.

Video ilionesha mlango ukifunguliwa. Akaingia Amanda akiwa na Kizito.

"Tumekuja kaka. Safari hii tumekuja kivingine, tumekuja kuuliza maswali, nawe utupe majibu. Majibu sahihi ya kila tutakachokuuliza" Kizito alisema.

Daniel aliwaangalia tu huku akiiruhusu kamera yake ikiwamulika wale watu wawili usoni. Alifanya vile makusudi.

"Umemficha wapi Alexander Helb?" Amanda aliuliza.

Daniel alikaa kimya.

Kizito alienda kwenye kabati dogo lililokuwemo mle ndani. Kilikuwa ni chumba kidogo chenye dirisha moja dogo lililokuwa juu kabisa ya kile chumba. Dirisha lisiloruhusu mwanga, hivyo mwanga ulisubiri na mlango ufunguliwe ili mwanga upate kupita.

Ndani ya kabati alitoa waya mdogo ulioambatana na mashine ndogo.

"Kinaitwa kibano hiki, utasema tu wapi ulipomweka Alexander!" Kizito alisema wakati akiunganisha ule waya katika umeme ukutani. Akatoa vyuma viwili virefu, akamvua shati Daniel ili amgusishe vile vyuma. Hapo ndipo wakina Martin walipoteza picha. Kamera ilifunikwa vibaya na lile shati walilomvua.

"Wameitoa kamera?" Hannan aliuliza.

"Hatuwezi kuona kwasasa. Wamemvua shati ili wamtese" Martin alisema.

"Tufanye kama Daniel alivyotuagiza"

***

Kule katika chumba cha mateso wakati wakijiandaa kumtesa Daniel na kibano, ghafla aliingia Donald Tengo.

"Mwacheni, mwacheni, msimfanye kitu" Donald Tengo alisema.

"Kuna nini mkuu?" Amanda aliuliza.

"Angalia" Donald Tengo alimpa simu yake Amanda. Kulikuwa na video fupi, Amanda akaicheza.

"Mimi ni mzalendo kwa Taifa langu. Ujumbe wangu kwako Mheshimiwa Donald ni sasahivi watu wako wako katika harakati za kumtesa Daniel. Nakushauri kawaambie waache mara moja, la sivyo utapokea kichwa cha mwanao mmoja. Nitaanza na Candy!! Naitwa Hannan" Video iliishia hapo.

Wote watatu walitoka nje ya chumba cha mateso jasho likiwatiririka.

Amanda, nini kimetokea?" Donald aliuliza walipofika sebuleni.

"Sijaelewa kwa namna gani watu wake wamegundua kwamba tunataka kumtesa muda huu. Ni mambo ya kushangaza sana" Amanda alishangaa.

"Kuna mambo mawili tu, kati ya hayo moja limefanyika. Aidha Daniel ana kamera ya siri ama ana kinasa sauti!" Kizito alisema.

Donald Tengo alitingisha kichwa kukubaliana nae.

"Mhamisheni katika kile chumba, mpelekeni baharini!!"

Amanda na Kizito walienda katika chumba alichowekwa Daniel, walimfungua kamba na kumpeleka katika chumba kingine. Kilikuwa ni chumba kidogo zaidi, kikiwa hakina dirisha, wala kitu chochote kile ndani yake. Cha kushangaza katikati ya chumba kulikuwa na bomba la maji. Akiwa anatazamwa na midomo miwili ya bastola Daniel alisukwasukwa mle ndani. Kwa umakini mkubwa huku akimwelekezea bastola Daniel alienda katikati ya chumba. Akafungulia lile bomba la maji. Maji mengi yalianza kumwagika mle ndani. Jamaa walifunga mlango na kutoka nje, wakiacha chumba kikianza kujaa maji!

"Mshampeleka baharini?" Donald aliuliza.

"Ndio mkuu" Kizito na Amanda walijibu kwa pamoja.

"Safi, sasa tunaenda kuwasaka wanangu popote pale walipo. Hawa watu wanamtegemea sana Daniel katika mipango yao. Hivyo kumuacha akifa baharini itaturahisishia sisi. Na kama hao wenzake walikuwa wanapata mawasiliano nae kwa kamera au kifaa chochote kile imekula kwao, maana kitakuwa kimesharibiwa na maji" Donald Tengo alisema.

"Ni kweli mkuu. Misheni ya kuwasaka watoto itakuwaje?"

"Ita vijana wa bahari nyekundu kumi. Nitamtumia Dick, yule kijana wetu wa usalama wa Taifa atuambie mahali anapoishi Daniel. Tukishapapata tu tumemaliza mchezo. Watoto wangu lazima watakuwa nyumbani kwa Daniel Mwaseba"

"Hata Alexander atakuwa hapohapo" Kizito alisema.

"Ndio, nilishasahau kuhusu Alexander, kupotea kwa watoto wangu kumeharibu sana uwezo wangu wa kufikiri. Naahidi naenda kuwateketeza vibaya sana hao watu waliowateka wanangu. Watamjua Donald Tengo ni nani! Nahisi hawaujui vizuri upande wangu wa pili. Mimi ni mnyama!" Donald Tengo alisema kwa ghadhabu.

Wote watatu wakajipanga vizuri. Amanda akawapigia simu vijana wa bahari nyekundu, ndani ya robo saa vijana kumi waliwasili wakiwa katika magari mawili. Donald Tengo akampigia simu Dick, mtu wao wanaomtumia katika idara ya usalama wa Taifa kuwapa taarifa. Akawaelekeza nyumbani anapoishi Daniel, wakaelekea huko.

Hannan na Martin walikuwa wamepoteza kabisa mawasiliano na Daniel Mwaseba. Hii iliwapa hofu sana juu ya usalama wa Daniel.

"Tunafanyaje sasa Martin? Daniel hapatikani kwa namna yoyote" Hannan aliuliza.

"Itabidi nimfuate Daniel nyumbani kwa Donald Tengo. Inaonesha Daniel yupo katika hatari" Martin alisema.

"Ni hatari sana kwa wewe kwenda huko. Sitaki kukupoteza na wewe Martin kama nilivyompoteza Daniel. Hawa watoto waliopo hapa hawana thamani yenu nyinyi. Hawana thamani kwangu na hata kwa taifa"

"Hannan, kwenda nyumbani kwa Donald Tengo ni njia pekee ya kumpata Daniel. Pale ni mahali ambapo alipotelea. Na bila shaka ndipo mahali alipo mpaka sasa. Siwezi kumuacha Daniel akiteketea kirahisi kwa namna hii. Licha ya kufanya kazi pamoja kwa muda mrefu lakini Daniel kwangu amekuwa ni kama ndugu. Siwezi kumwacha ndugu yangu akifa kifo cha namna hii, wakati nina uwezo wa kumwokoa. Sitoweza kujisamehe kamwe. Nitaenda kupambana kama ni kufa ni bora na mimi nikafie humo."

"Sawa Martin, mimi nitabaki hapa kuwalinda hawa watoto. Ila usiende hivihivi. Chukua kifaa hiki kitatusaidia katika mawasiliano. Kama utapata tatizo lolote niambie, nitakuwa njiani kuja kukusaidia. Na mimi nife pamoja na ninyi" Hannan alisema kwa hisia.

***

Maji ya baridi yakiyotoka katika bomba, katika chumba alichowekwa Daniel yalikuwa yanamfika katika mabega sasa. Mwanzoni alijaribu kuufungua mlango, lakini utundu wake wa kucheza na milango mbalimbali hapa ulikwama. Mlango wa chuma haukukubali utundu wowote ule. Giza la chumbani, ukichanganya na ubadili mkali wa maji yale yalimtesa sana. Kama wakina Donald Tengo wangerejea na kumuuliza chochote kile, pasi na shaka safari hii angewajibu.

"Mbinu zangu zote hapa zimefika mwisho. Maji haya ya baridi yamezimaliza nguvu zangu. Ninakufa, ninakufa kifo kibaya sana. Ni kweli ninakufa lakini ninaamini wakina Hannan watalimaliza jambo hili, kuhakikisha uhaini huu haufanikiwi, na yoyote yule aliyehusika katika uhaini huu akipelekwa katika vyombo vya dola" Daniel aliwaza wakati maji yakimfikia shingoni.

Wakati huo, Martin Hisia alikuwa anaendesha gari kwa kasi sana. Akielekea katika nyumba ya Donald Tengo. Nusu saa tu ilimfikisha katika nyumba ile ambayo aliamini Daniel alikuwemo. Bila wasiwasi akaenda getini. Akagonga. Akasubiri kama dakika mbili hivi, geti dogo lilifunguliwa, alitoka njemba moja akiwa na bunduki mkononi.

"Wenyewe hawapo.." Njemba ilisema kwa sauti ya kibabe kabla hata hajaulizwa kitu.

"Samahani kaka.." Martin alisema lakini alikatishwa.

"Nimekwambia wenyewe hawapo!" Njemba safari hii alisema kwa ubabe. Na hiyo ndio nafasi aliyokuwa anaisubiri Martin.
Ghafla!
Alimsukumia ndani kwa kutumia kifua chake. Kilikuwa ni kitendo cha ghafla ambacho kilimwacha Njemba akidondoka chini, bunduki yake ikiwa mkononi. Kabla Njemba hajapata nafasi ya kutafakari, Martin alimrukia na kumchoma kisu cha kifua mara mbili. Njemba alitaka kupiga ukelele lakini Martin alimuwahi kwa kumziba mdomo. Sauti yake ikapotelea humo.
Njemba alikata roho.

Martin alienda upande wa kulia wa ile nyumba. Nako kulikuwa na mlinzi aliyekuwa anavuta sigara, bunduki yake ikiwa kaisimamisha ukutani. Kwa haraka akamuwahi risasi moja ya paji la uso kwa bastola yenye kiwambo cha kuzuia sauti. Jamaa akadondoka chini. Martin alizunguka ile nyumba hakuwakuwa na mlinzi mwingine.
Akaingia ndani.

Wakati huo, Donald Tengo akiwa na vijana wa bahari nyekundu walikuwa wanakaribia nyumbani kwa Daniel Mwaseba huko Mikocheni.

"Humu ndani ninaamini ndimo walimo watoto wangu. Kuweni makini kuhakikisha watoto wangu hawapati madhara yoyote yale." Donald Tengo alisema huku wengine wakimsikia kupitia vifaa walivyovaa masikioni mwao.

Na misheni hii ndogo ilianza.

Vijana wa bahari nyekundu walijipanga katika makundi mawili ya watu watano watano. Kundi la kwanza lilipita upande wa mashariki huku wengine wakielekea upande wa magharibi. Donald Tengo, Amanda na Kizito walibaki ndani ya gari huku wakifatilia kwa umakini mkubwa sana kila kitu kinachoendelea.

Baada ya kuhakikisha eneo la nje liko salama, vijana walizama ndani. Silaha zao zikiwa zimetangulizwa mbele. Kwa umakini mkubwa sana walisonga mbele kuifata nyumba ya Daniel Mwaseba. Kwa kutumia funguo maalum walifungua mlango na kuingia ndani. Baada ya dakika tano kifaa cha sikioni cha Donald Tengo kilipata uhai.

"Mkuu tumefanikiwa kuingia ndani lakini hakuna mtu humu ndani?"

"Unasemaje bahari nyekundu?" Donald Tengo aliuliza kwa hamaki.

"Hakuna mtu ndani, tumepekua kila mahali lakini hatujaona mtu. Kuna chumba kimoja tumepekua tumekuta vitu kadhaa vinavyoonesha ni vya Daniel Mwaseba"

"Mmekuta kama kitu gani?"

"Tumekuta nguo na albam ya picha, bila shaka ni za Daniel"

"Ok njoo na hiyo albam ya picha, inaweza kutusaidia. Waweke na zawadi wakutane nayo watakaporudi" Donald Tengo alisema.

Kijana alimwelewa.

Baada ya kuthibitisha kwamba watu wa Daniel hawakuwemo mle ndani walirejea nyumbani.

"Hakuko sawa nyumbani!" Kizito alisema kwa ghadhabu wakiwa kama mita mia moja kufika nyumbani kwa Donald Tengo.

Macho ya Donald nayo yalielekea getini. Aliona geti la nyumba yake likiwa wazi. Ilimpata hofu kuu. Hakutaka kumpoteza Daniel kabla hajawapata wanawe. Walishukia nje, wakatembea kwa tahadhari kubwa wakielekea ndani. Kila mmoja bastola yake ikiwa mkononi. Waliingia mpaka ndani, baada ya kuacha maiti ya mlinzi wake nyuma. Baada ya wale wa awali kuuwawa. Walizunguka nyuma na kukuta maiti ya mlinzi mwengine.

"Adui katoka nje" Kijana mmoja wa bahari nyekundu alisema.

"Kwanini?" Amanda alisema.

"Unaona hizi alama za viatu. Hivi ni viatu vya mvamizi, inaonesha wakati akiondoka" Yule kijana wa bahari nyekundu alisema.

"Twendeni ndani, bado hatujajua uharibifu alioufanya Daniel Mwaseba" Donald Tengo alisema.

Wakaingia ndani, walichokutana nacho huko, wote walibaki midomo wazi.

Sebuleni kulikuwa kumetawanywa vibaya sana. Kila kitu kikiwa hakipo katika mpangilio waliouacha. Friji liligeukia kule, kabati liligeuzwa huku, runinga ilikuwa chini huku makaratasi kadhaa yakiwa yamemwagwa pembeni ya meza ndogo.

Donald Tengo alikimbilia katika chumba ambacho walikiita baharini, alipigwa na butwaa, mlango aliouamini kuliko kitu chochote kile ulikuwa chini. Mlango imara, wa chuma ambao fundi wake alimwaminisha kwamba hakuna atakayeweza kuufungua hapa duniani ulikuwa umefunguliwa. Na ndani ya chumba hiko Daniel Mwaseba hakuwemo. Donald Tengo alichanganyikiwa sana. Kwa kasi alienda chumbani kwake, akachukua rimoti iliyokuwa juu ya feni. Akabonyaza kuelekea ukutani. Ukuta ulisogea, lakini macho yake hayakuamini.

"Wamechukua kasiki yangu ya siri! Oooh tumekwishaaa" Donald Tengo alipiga ukelele mkubwa.
Kwa hakika alikuwa amepatikana!

"Sasa kila kitu kipo mikononi mwake, ushahidi wote anao, huu sio wakati wa vita vya siri tena, ooooh no, Daniel safari hii nikikupata nitakuua mwenyewe, sitojari tena maisha ya watoto wangu!! Lakini amepajuaje mahali hapa nilipoificha kasiki yangu ya siri, amejuaje kama huu ukuta unafunguka? Ni mtu mmoja tu niliyewahi kumwambiai siri hii. Mmoja tu, mpenzi wangu wa maisha Salma Lungu! Je ni yeye ndiye aliyeivujisha siri hii? Haiwezekani, haiwezekani!" Donald Tengo alichukua simu yake na kumpigia Salma Lungu. Simu ilikuwa haipatikani. Na hii ilikuwa ni kwa mara ya kwanza simu ya Salma Lungu isipatikane tangu walipoingia katika mahusiano. Akazidi kuchanganyikiwa.
Akapiga simu kwa Balozi Rwekaza.

"Mzee Rwekaza itisha kikao cha dharura sasahivi" Donald Tengo alisema kwa sauti iliyoambatana na hofu.

"Kuna tatizo gani Donald?" Mzee Rwekaza aliuliza.

"Utajua kwenye kikao.." Donald Tengo alisema na kukata simu.










Itaendelea..
Kali sana, Tengo anashikwa mchana kweupe
 
Riwaya; Mtoto wa Raid
Imeandikwa na Halfani Sudy
0652 212391

Sehemu ya Saba


Masaki; Dar es Salaam.

Katika nyumba moja ya thamani kubwa kulikuwa na kikao cha watu kumi. Waziri wa fedha, mheshimiwa Donald Tengo alikuwa mbele ya watu tisa waliokuwa wamevalia suti za thamani, zenye rangi nyeusi. Kulikuwa na utulivu mkubwa, watu wote wakitega masikio yao kumsikiliza Donald Tengo.

"Karibuni sana wajumbe, hatukuwa na ratiba ya kukutana hapa kwa siku ya leo. Tulikubaliana tutakutana hapa mwisho wa mwezi huu tukiwa tumeimaliza hii kazi, lakini tumekutana hapa kwa dharura. Kuna tatizo kidogo limetokea.
Katika kikao chetu cha mwisho nakumbuka niliwaambia wajumbe juu ya ujio wa Alexander Helb. Jasusi hatari sana kutoka Uholanzi. Ilifanyika kama ilivyopangwa, tulimshawishi Alexander na alikubali kuacha kazi zake huko Uholanzi na kuja kushirikiana na sisi. Tulimuingizia bilioni moja kama malipo ya awali, na tulimwahidi bilioni mbili baada ya kumaliza kazi yetu" Donald akanyamaza kidogo kuacha maneno yake yaingie ubongoni mwa wajumbe.

Baada ya sekunde kadhaa akaendelea,
"Leo asubuhi Alexander aliwasili hapa lakini lilitokea jambo la kushangaza sana pale uwanja wa ndege.
Ni hivi, gari waliyopanda Alexander na Joyce ilipata ajari!" Donald Tengo alinyamaza, akachukua chupa ya maji na kuimiminia mdomoni. Kisha akasema "Mwanzoni tulidhani ni ajari ya kawaida tu, lakini baada ya kufanya uchunguzi wetu tuligundua kwamba ilikuwa ni ajari ya kupangwa, na Alexander alichukuliwa na watu wasiojulikana baada tu ya kutokea ajari!. Na tangu hapo hatujajua mahali alipopelekwa Alexander na watekaji" Donald alimaliza.

"Daah ni habari mbaya sana hiyo kwetu. Alexander alikuwa na umuhimu mkubwa sana kwa hapa tulipofikia. Bila ya Alexander hata kazi ya ZAK ni bure tu. Je, mmejaribu kuisachi simu ya Alexander kujua mahali alipopelekwa?" Mjumbe mmoja aliuliza.

"Tulijaribu kumtafuta mjumbe, Amanda aliifanya hiyo kazi, lakini aligundua kitu cha ajabu sana. Simu ya Alexander ilionekana bado ipo Uholanzi. Hii ilitushangaza sana!" Donald Tengo alisema.

"Hujuma, bila shaka kuna hujuma. Bahati mbaya sana hujuma zimeanza wakati tukiwa ukingoni mwa mpango wetu wa kumuondoa rais Mark madarakani. Sasa, lazima tuhakikishe tunazizima hujuma hizi. Lazima tuhakikishe tunajua wapi alipopelekwa Alexander na kina nani waliomteka? Wote tulikuwepo hapa wakati ukimueleza Alexander juu ya kazi hii. Ulimueleza kuhusu mpango wetu, hivyo kukamatwa kwake ni kuweka rehani siri zetu. Hivyo kuna umuhimu mkubwa sana wa kuhakikisha Alexander anapatikana. Tuwatumie vijana wa bahari nyekundu kumsaka Alexander popote pale alipo!" Mjumbe mwengine alisema.

"Upo sawa Mjumbe, Bahari nyekundu wakiongozwa na Amanda nitahakikisha hawalali hadi watuambie wapi alipopelekwa Alexander, na ni kina nani waliomteka. Kuhusu Alexander kutoa siri hilo hatuna shaka nao. Alexander ni jasusi, sio rahisi kutoa siri kirahisi hivyo." Donald Tengo alisema.

Kikao kiliendelea kwa muda wa saa tatu. Wakapanga. Wakakubaliana. Sasa walianza msako maalum wa kumsaka Alexander Helb, iwe mvua, iwe jua. Awe mashariki, awe magharibi. Awe kusini, awe kaskazini, jasusi Alexander Helb lazima apatikane!!!


***

Ulikuwa ni wakati wa jioni. Jua lililokuwa likiwasulubu wana Sinza mchana nd'o lilikuwa linazama. Sasa Sinza nd'o ilikuwa imechangamka. Baa mbalimbali zilikuwa zimejaa wateja wakiimaliza siku kwa kusindikiza na bia. Makelele ya muziki yalikuwa yanasikika katika baa hizo.

Daniel na Martin walikuwa wamepaki gari yao katika kituo cha mafuta kilichopo Sinza Afrika sana. Macho yao yalikuwa yameelekezwa katika geti la shule ya sekondari ya Kenton. Ulikuwa ni muda ambao walikuwa wanausubiri kwa hamu.

Na dakika waliyokuwa wakiisubiri ikafika. Waliliona gari jeusi likitoka getini.

"Gari tunayoisubiri ni ile pale. Kazi ianze.." Daniel alisema.

"Ndio Daniel, na misheni ianze" Martin alisema huku akishuka katika gari. Akafungua buti la gari na kuitoa pikipiki. Akaiwasha na kuanza kuifuata ile gari, wakati Daniel nae akifata kwa nyuma kwa gari.

Ile gari nyeusi ilifika katika makutano ya Bamaga iliyotoka katika geti la shule ya sekondari Kenton. Gari lilikuwa katika foleni ili waelekee Masaki, nyumbani kwa Donald Tengo. Ghafla, dereva bodaboda mmoja aliikwaruza ile gari karibu na mlango. Ilikuwa ajari ndogo lakini dereva wa gari nyeusi hakuweza kuivumilia.

Pengine kuonesha umwamba wake. Si ni dereva wa waziri!!

Kwa kasi akafungua mlango na kuanza kumfata yule dereva bodaboda. Alipofika alitulizwa, alikutana na hasira ya dereva bodaboda, akala kibao. Mlinzi akiwa ndani ya gari alishuhudia tukio lile. Naye alitoka kwa kasi kwenda kumsaidia dereva.

Lilikuwa kosa,

Kwa kasi Daniel alienda kwenye ile gari nyeusi, bastola ikiwa mbele aliwanyooshea watoto waliokuwa wamekaa katika siti za kati. Kwa ulaini, aliwachukua wote na kuwapeleka katika gari yake wakati wenye gari wakigombana na Martin Hisia. Daniel akaondoka na Candy na Cindy.

Kule ugomvi uliisha baada ya watu kuanza kukusanyika. Dereva wa gari nyeusi akaona isiwe tabu. Yeye na mlinzi wake wakarudi katika gari yao huku wakimruhusu dereva bodaboda aondoke. Walipofika katika gari watoto hawakuwepo!!

Ilikuwa tafrani!!

***

Wakati hayo yakifanyika katika makutano ya Bamaga Sinza. Vijana wa bahari nyekundu, Amanda George akiwa na Kizito Kizito walikuwa katika viunga vya uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere. Kizito aliyekuwa dereva alipaki gari nje uwanja. Wakaingia ndani kuanza kupeleleza chanzo cha ajari iliyotokea asubuhi. Kizito akamwita dereva teksi mmoja, alimtambua kwa sare alizovaa, kitambulisho chake kilionesha kwamba anaitwa David.

"Habari kaka, ninaitwa Musa ni Mwandishi wa habari wa gazeti la uchunguzi la Dukua. Najua unalifahamu gazeti hilo, hutoa habari za kina za kichunguzi kuliko gazeti lolote lile hapa nchini. Huyu ni mwenzangu anaitwa Feriha" Kizito alidanganya.

"Sawa ndugu mwandishi, naitwa David Msomi ni dereva teksi hapa uwanja wa ndege, nina miaka mitano sasa" David alisema.

"David tunahitaji kitu kimoja tu kutoka kwako, kimoja tu na bila shaka tutakulipa vizuri. Kwako tunataka taarifa ili kwetu zikawe habari. Tupo tayari kununua taarifa kwa gharama yoyote ile ili gazeti letu la Dukuo lizidi kuwa juu katika habari za uchunguzi" Kizito alisema.

"Taarifa gani mnataka kaka?" David aliuliza.

"Tunahitaji taarifa kuhusu ajari ya leo asubuhi"

"Ile ya Range rover nyeusi na gari la maji taka?" David aliuliza.

"Naam" Kizito aliitikia.

David aliangalia juu. Alikumbuka vizuri sana ajari iliyotokea asubuhi.

"Kuna kitu gani unakijua juu ya ajari ile ambayo vyombo vingine vya habari hawawezi kukipata?" Kizito aliuliza.

"Mtanilipa sh ngapi nikiwapa taarifa?" David aliuliza.

"Inategemea na uzito wa taarifa yako. Lakini sio chini ya laki moja" Amanda alisema.

David aliwaza sana, kisha akasema " Majuto".

"Unajuta nini David?" Amanda aliuliza.

"Kitu ambacho watu hawakijui ni Majuto, Majuto ndiye aliyesababisha ile ajari ya asubuhi!" David alisema.

"Kivipi?" Kizito aliuliza huku akijifanya kuandika katika karatasi aliyoishika.

"Pesa, nipeni pesa yangu kabisa. Namjua Majuto lazima ataniua! Nipeni pesa ile niondoke kabisa hapa ndipo nitawaambia" David alisema.

Amanda alitoa simu yake. Akapiga sehemu. Akaongea kama dakika tano, kisha akamuuliza David wakati simu ikiwa hewani.

"Una akaunti benki?"

David aliitikia kwa kichwa.

"Niandikie namba ya akaunti yako na jina la benki kwenye simu yako" David akaandika. Akampa Amanda. Amanda akaisoma ile namba kwa aliyekuwa anaongea nae kwenye simu. Akakata simu. Baada ya kama dakika tano simu ya David ikaingia meseji.

'Milioni moja ilikuwa imeingia katika akaunti yake'

"Bila shaka pesa zimeingia, Eeeh tuendelee. Ilikuwaje kuhusu Majuto na ile ajari ya Range rover nyeusi?" Kizito aliuliza.

"Majuto alikata breki ya ile range rover kabla haijatoka. Na hiyo ndio sababu ya ajari ya asubuhi!"

"We ulijuaje?" Kizito aliuliza.

"Nilimwona, nilimwona kwa macho yangu akikata breki za ile gari"

"Umemwambia yeyote yule taarifa hiyo?" Amanda aliuliza.

"Hapana ninyi ni wa kwanza kuwaambia. Hata Majuto mwenyewe hajui kama nilimwona" David alisema.

"Ok tunashukuru sana kwa taarifa yako. Andika namba yako hapa tutakutafuta tukihitaji ufafanuzi zaidi" Amanda alisema.
Kisha wakaagana.

"Kifuatacho?" Kizito aliuliza.

"Msako wa Majuto popote pale alipo!" Amanda alisema.

"Amanda, umemuingizia kweli milioni moja yule kisebengo hahahaha" Kizito alisema huku akicheka.

"Mambo ya mtandao yale. Mwache aende benki ataenda kukutana na salio zero katika akaunti yake hahaha" Amanda alisema huku akicheka.

Majuto! Kijana aliyetumiwa na Daniel Mwaseba anasakwa na vijana wa bahari nyekundu..

Wakati kule, watoto wa Donald Tengo wako mikononi mwa Daniel. Hatua gani itafuata baada ya kuwapata?

Lako Jicho!
 
RIWAYA; MTOTO WA RAIS
Imeandikwa na Halfani Sudy
Simu 0652 212391

Sehemu ya Kumi na Mbili

"Karibuni sana wajumbe. Samahani kwa kuwaita tena kwa ghafla namna hii. Mkiona wito wa haraka namna hii najua nyote mnajua kwamba kuna dharura. Na ni kweli leo kuna dharura.." Donald Tengo alitulia kidogo kuongea ili kila mmoja yamwingie vizuri maneno yake.

"Tangu mwanzo kwa'kweli tumejitahidi sana kufanya kila tuwezalo ili kuhakikisha mipango yetu inakwenda sawa, lakini bado kuna kidudumtu kinatusumbua sana. Kuna adui mpya ameingia katikati ya mipango yetu. Adui huyo mpya ndiye aliyemteka Alexander, pia amewateka watoto wangu wawili wakiwa wanatoka shule. Leo hii alivamia nyumbani kwangu na kufanya uhalifu mkubwa sana na kwa bahati mbaya sana kaondoka na Kasiki yangu yenye siri zetu. Ndani ya hiyo Kasiki kuna siri kubwa sana za huu mtandao wetu, hivyo kwa weledi wa adui yetu ninaamini mambo yetu yatakuwa hadharani, katika mikono yake. La msingi ni kuhakikisha siri hiyo haisogei katika mikono mengine.." Donald Tengo alinyamaza tena na kuwaangalia wajumbe.

"Ni nani huyo adui anayekitafuta kifo kwa nguvu kiasi hicho?" Mjumbe mmoja akauliza.

"Adui yetu anaitwa Daniel Mwaseba. Ni mpelelezi kutoka kitengo maalum ndani ya idara ya usalama wa Taifa. Huyu kijana ni msumbufu sana. Amekuwa akitufatilia kwa siri mimi na Balozi Rwekaza. Na katika ufatiliaji wake amefanikiwa kufika hadi nyumbani kwangu na kuiiba Kasiki yangu yenye taarifa mbalimbali za siri" Donald Tengo alisema.

"Mh. Donald samahani kwa kusema hili. Kwa'kweli umetuangusha sana. Ni wewe pekee ndiye unayestahili lawama zote katika hili. Ulinzi hafifu umemfanya Alexander Helb akamatwe. Ulinzi hafifu umesababisha watoto wako watekwe. Na sasa limezuka hili jipya kabisa. Kasiki ya siri yenye siri zetu inaibiwa? Hiyo ni sawa na kutuvua nguo sisi wote. Unawekaje Kasiki muhimu mahali ambapo pameweza kufikiwa na huyo kijana?" Mjumbe mwengine aliuliza kwa jazba.

"Kasiki niliiweka sio sehemu rahisi kufikiwa, ilikuwa sehemu ya maficho sana. Hadi sasa sijaelewa kwa namna gani Daniel ameweza kupagundua mahali ilipokuwa Kasiki. Lakini wajumbe huu sio muda wa kulaumiana, ni wakati wa kujadiliana kwa kina na kuhakikisha mpango wetu unakamilika. Pia ni lazima tuhakikishe tunaitoa roho ya huyu kijana mfukunyuku" Donald Tengo alisema kwa kirefu.

"Ni kweli kabisa, huu sio muda wa kulaumiana. Huu ni wakati wa kupanga mikakati thabiti. Mimi ninaona kitu muhimu cha kufanya ni kumuua huyo kijana na kuhakikisha taarifa zote zilizopo katika Kasiki tunazipata. Pia ni lazima tuwatumie vijana wetu wa Bahari nyekundu kuhakikisha tunampata Alexander, tunawaokoa watoto wa Donald na kuipata Kasiki yake. Kisha mipango yetu iendelee kama kawaida" Balozi Rwekaza alisema.

"Upo sahihi Balozi Rwekaza ingawa hatujui zitachukua siku ngapi hayo mambo kukamilika. Kumbukeni muda hautusubiri sisi, na jukumu letu kuu ni kuhakikisha mpango wetu unakamilika haraka iwezekanavyo. Hivyo mimi nashauri tuyafanye kazi yote hayo kwa wakati mmoja. Yaani vijana wa Bahari nyekundu wamsake Daniel Mwaseba huku tukitafuta namna ya kumuua Rais Mark!" Mjumbe mwengine alisema

"Uko sahihi mjumbe, lakini, Je kuna mtu mwenye namna yoyote ya kumuua Rais Mark tofauti na ya kumtumia Alexander?" Donald Tengo aliuliza.

Mjumbe mmoja alinyoosha mkono na kuruhusiwa kuongea "Mimi nashauri tutafute muuaji mwengine aje kutekeleza hiyo kazi, kama alivyosema mjumbe kumsubiri Alexander ni kujichelewesha wenyewe, huku mipango yetu ikiendelea kuchelewa" Mjumbe mwengine alisema.

Kikao kiliendelea zaidi ya saa mbili, walikubaliana jinsi ya kutekeleza mipango yao. Baadaye, wajumbe wote walitawanyika kwa njia wanazozijua wao.

***

Daniel Mwaseba na Martin Hisia walikuwa sebuleni. Dakika saba zilizopita walikuwa wamerejea kutoka katika nyumba ya Donald Tengo. Walikuwa wametoka kutekeleza mpango wa hatari sana uliopangwa na Daniel mwenyewe. Mpango wa kujikamatisha ili aingie katika ngome ya Donald Tengo, akisubiri wakina Donald Tengo wafanye kosa lolote lile ili awaadhibu.

Na kweli, walifanya kosa..

"Kuna lolote jipya lililotokea hapa nyumbani?" Daniel aliuliza huku akimwangalia Hannan usoni.

"Nilikuwa nina wasiwasi sana baada ya kuzimika ile kamera. Sikuubariki mpango wako wa kujikamatisha mikononi mwa Donald Tengo. Usithubutu tena kufanya kitu kama hiko. Daniel, wewe ni wa thamani sana kwangu. Kuhusu hapa nyumbani kuna kitu nilikuwa sijakueleza ambacho nimekigundua katika mitandao ya siri ya kijasusi"

"Ni kitu gani hicho ulichogundua?" Daniel aliuliza kwa hamu.

"Katika kutafuta zaidi taarifa za Donald Tengo nimegundua kwamba ana uhusiano wa kimapenzi na Mke wa Rais!...." Hannan alianza kuelezea.

"Madam Magdalena Lema!" Daniel alidakia kabla Hannan hajamaliza kuelezea.

"Ndio," Hannan alisema huku akibonyaza tarakilishi yake.

"Haiwezekani Bwana!" Daniel alikataa.

"Taarifa hizi hata mimi na Martin zilitustua sana tulipoziona awali. Hivyo tulianza kumchimba zaidi Mke wa Rais. Katika uchunguzi wetu tukagundua kuwa rafiki yake mkubwa ni mwanamke mmoja anayeitwa Salma Lungu. Tumejaribu kumchunguza huyo Salma Lungu lakini hatujapata taarifa yoyote kutoka kwake. Hakuna taarifa yoyote katika mtandao juu ya Salma Lungu" Hannan alisema.

"Naona mmekua sasa vijana. Kwa'sasa ninaamini hata siku nisipokuwepo nitakuwa nimeacha watu makini sana wa kufanya uchunguzi. Yaani mmechimba hadi mmegundua kuhusu Salma Lungu?" Daniel alishangaa.

"Daniel, unataka kuniambia unamjua Salma Lungu?" Martin alishangaa.

Daniel alikaa kimya akiwaza.

"Daniel!" Hannan aliita.

"Namfaham Salma Lungu, ni mimi mwenyewe ndiye niliyempandikiza katika nyumba ya Donald Tengo. Alienda pale kama mfanyakazi wa ndani lakini Donald Tengo alimlazimisha hadi wakawa wapenzi. Na huo ndio ulikuwa mpango wangu, kumchunguza Donald Tengo kupitia kwa mtu wake wa karibu, Salma Lungu." Daniel alisema.

"Kumbe huu mpango unaonesha ni wa siku nyingi sana na ulikuwa unaufahamu hata kabla hajagundua kuhusu simu ya Balozi Rwekaza. Ulikuwa unachunguza nini kwa Donald Tengo hapo kabla?" Hannan aliuliza maswali mfululizo.

"Ni kweli, huu mpango wa siku nyingi kidogo. Kulikuwa na taarifa mezani kwetu kwamba Donald Tengo alikuwa anajihusisha kwa siri na mtandao wa madawa ya kulevya, ndio maana nikafanya mpango wa kumpenyeza Salma Lungu katika maisha yake ili kumchunguza" Daniel alisema.

"Nini aligundua Salma Lungu katika upelelezi wake?" Martin akauliza.

"Salma aligundua mambo mengi sana ya siri yanayomhusu Donald Tengo, lakini mambo mawili makubwa ni kweli Donald alikuwa mshiriki katika mtandao wa siri wa Madawa ya Kulevya hapa nchini unaoshirikisha vigogo wakubwa sana. Na kingine aligundua Donald ana uhusiano wa siri wa kimapenzi na Mke wa Rais."

"Kumbe unajua Daniel. Kwanini sasa hajakamatwa kwa kujihusisha na mtandao huo wa Madawa hayo haramu?" Martin aliuliza tena.

"Bado tunakusanya taarifa za kina za kuweza kumtia hatiani Donald Tengo. Na pia tunataka kuhakikisha tunawakamata washirika wake wote katika mtandao huo haramu" Daniel alieleza.

"Kwanini hukutueleza hayo mambo kabla Daniel? na wakati tupo katika misheni moja?" Hannan aliuliza.

"Samahanini sana jamaa zangu. Sikujua kama uchunguzi wetu ungetufikisha huku, pia nilidhani kwamba hapa tupo katika misheni nyingine tofauti na ile niliyoifanya na Salma Lungu!" Daniel alisema.

"Ni nani hasa Salma Lungu? Kwanini hakuna taarifa zake sehemu yoyote ile katika mtandao?" Hannan aliuliza tena.

"Salma Lungu ni Elizabeth Neville! Nilimwingiza Elizabeth katika maisha ya Donald Tengo kwa jina la Salma Lungu. Donald Tengo hakujua kama Salma ni Mpelelezi kutoka kitengo maalum katika idara ya Usalama wa Taifa" Daniel alisema.

"Aisee!" Martin na Hannan walisema kwa pamoja.

"Ndio hivyo ndugu zangu, eeh tuendelee na haya tuliyoyapata kwa Donald Tengo, ilinipasa kwenda katika nyumba ile, maana nilivyoongea na Elizabeth aliniambia kwamba mpango wa kuwatumia watoto wake usingefanikiwa kumfungua Donald Tengo. Donald Tengo ana roho mbaya sana, asingewajari sana watoto wake. Yeye alishauri kwa namna yoyote ile niingie nyumbani kwake na akanielekeza mahali Kasiki ya siri ilipo na jinsi ya kuipata. Na sasa Kasiki tunayo mbele yetu, tuifungue tuone tutapata nini ndani yake?" Daniel alisema.

Martin Hisia aliisogeza ile Kasiki mbele na kuanza kuifungua..

Itaendelea..

Ofa ya leo wanagroup..
Soma msimu huu wa kwanza na wapi wa Mtoto wa Rais kwa sh 3000 tu.
Ni whatsapp 0652 212391

Na Red butterfly inapatikana kwa sh 5000.
Ni Whatsapp 0652 212391
 
RIWAYA; MTOTO WA RAIS
imeandikwa na Halfani Sudy
Simu 0652 212391

Sehemu ya Kumi na Tatu

Martin Hisia aliisogeza ile Kasiki mbele na kuanza kuifungua.

Dakika kumi na tano zilitosha kuiacha wazi Kasiki ya siri ya Donald Tengo. Ilikuwa Kasiki ya chuma ambayo kuifungua kwake ilihitaji ufundi wa kimakinikia na teknolojia. Daniel na Martin walihusika kila palipohitaji makenika wakati Hannan alitumia ujuzi wake wa teknolojia. Kuna muda walitumia moto wa gesi, kuna wakati walitumia risasi ya moto, mwisho Hannan alifanikiwa kuifungia nywila ngumu sana kwa kutumia ujuzi wa teknolojia.

Baada ya Kasiki kuwa wazi, Daniel alianza kutoa vitu vilivyokuwepo ndani ya kasiki ile. Juu kabisa ya Kasiki kulikuwa na pesa nyingi sana za Kimarekani. Walitoa mabunda kumi yaliyokuwa yamewekwa kwa juu na kuyaweka juu ya meza. Yalikuwa ni mabunda ya dola mia moja yaliyofungwa kwa pamoja. Baada ya mabunda kutolewa kwa chini, walikuta mafaili matatu na tiketi ya ndege.

"Kila mmoja ashike faili lake na kulisoma tuone kuna nini ndani ya mafaili haya" Daniel alisema wakati akiyagawa yale mafaili matatu kwa kila mmoja. Kukawa kimya kila mmoja akisoma faili lake, wote majasho yaliwatoka wakati wakisoma mafaili yale.

Nusu saa baadaye walikuwa wamemaliza, walibadilishana yale mafaili na kuanza kusoma tena. Baada ya kumaliza kwa mara ya pili, wakabadilishana tena, wakasoma kwa mara ya mwisho na kumaliza. Wote sasa wakawa wameyasoma mafaili yote matatu kwa wakati mmoja. Daniel akaiangalia ile tiketi, ilikuwa ni tiketi ya ndege ya shirika la ndege la kimataifa la Qatar ikionesha ujio wa mtu aliyeandikwa kwa majina ya mawili, Zayiid bin Khalifa. Kwa mujibu wa tarehe iliyoandikwa katika ile tiketi, ilionesha kwamba huyo Zayiid aliwasili siku tano zilizopita kutoka nchini Iran.

"Hannan, hebu jaribu kutafuta taarifa za huyu Zayiid bin Khalifa, ni nani haswa?" Daniel alisema akimwangalia Hannan.

Harakaharaka Hannan alianza kubofya tarakilishi yake, wakati Daniel na Martin wakisubiri kwa hamu kubwa sana taarifa za Zayiid bin Khalifa. Hawakuwa na wasiwasi wowote ule kwani Hannan alikuwa ni mchawi wa kike wa Kompyuta. Mtu mwenye kuweza kuvunja uzio wowote ule kwenye Kompyuta na kuweza kupata taarifa anayoitaka.

"Zayiid bin Ally bin Khalifa" Hannan alianza kusoma huku uso wake ukiitazama tarakilishi yake " Kwa mujibu wa mtandao wa Magaidi wanaotafutwa kwa siri na Serikali ya Marekani, Zayiid ni mmoja wa watu wanaosakwa sana na nchi hiyo. Zayiid amehusika katika matukio mengi sana ya kigaidi. Lakini tukio aliolifanya hivi karibuni ni kutengeneza kemikali ambazo zimetumika kuuwa wanafunzi hamsini na tatu katika chuo kikuu cha Harvard huko Marekani. Zayiid bin Khalifa ni kijana wa Kiiran mwenye umri wa miaka thelathini na tisa. Anahusishwa pia na mahusiano na kikundi cha kigaidi cha Alqaeda" Hayo ndio yaliyopo katika mtandao wa magaidi wanaotafutwa kwa siri na Marekani.

"Kwanini kuna orodha ya magaidi wanaotafutwa kwa siri? Vita ya magaidi ni ya kimataifa, siyo vita ya nchi mojamoja. Sasa kwa nini nchi ya Marekani wawe na orodha ya magaidi wanaotafutwa kwa siri? Huoni kwamba wangewaweka hadharani ingekuwa rahisi kuwakamata? Mimi ninaamini hata huyu Zayiid zingewekwa taarifa zake hadharani asingeweza kuingia nchini kwetu" Martin alisema huku akimwangalia Hannan.

"Upo sahihi Martin kwa kila ulichosema. Lakini njia hii hufanywa kwa malengo maalum. Marekani wana orodha yao ya magaidi wanaowatafuta kwa siri, lengo lao kuu ni kuondoa taharuki hapa Duniani. Hawapendi Dunia iwe na hofu sana juu ya Magaidi. Lakini pia kuwatafuta kwa siri inawapa uwanja mpana sana wa kuwakamata. Magaidi wanakuwa hawajui nguvu namna gani inatumika kuwasaka, hivyo ni faida kubwa sana kwa Mtafutaji." Hannan alimwelezea Martin.

"Umeelezea vizuri sana Hannan. Sasa turudi kuchakata taarifa za huyo Zayiid bin Khalifa. Donald Tengo ana tiketi ya mtu huyu hatari sana, kwanini tiketi hii iwepo katika kasiki yake ya siri? Ni kwa bahati mbaya? Zayiid ana rekodi mbaya sana za kigaidi, sasa kwanini huyu Zayiid aje hapa Tanzania? Kwa lengo gani? Na kwa'sasa yupo wapi?" Daniel aliuliza maswali mfululizo.

"Daniel umeuliza maswali mazuri sana. Lakini majibu ya maswali hayo yote yapo kwa Donald Tengo pekee. Ni yeye pekee ndiye anajua alipo Zayiid bin Khalifa na yeye pia anajua sababu iliyomleta hapa nchini" Martin alisema.

"Lazima tumsake Donald Tengo haraka iwezekanavyo na kumleta hapa. Tutaitumia siri yake ya kutoka na Mke wa Rais ili kumfungua kila kitu" Daniel alisema.

"Na haya mafaili?" Hannan aliuliza.

"Kama tulivyoona. Hiyo ni mipango ambayo imeshatekelezwa. Inavyoonesha hawa watu wanaweka mafaili ya mipango yao iliyotekelezwa kwa Donald Tengo, sasa tuna kazi ya kusaka mafaili ya mipango yao isiyotekelezwa bado. Lazima tujue mafaili hayo yanakaa kwa nani? Hapa tumepata ushahidi tu kupitia mafaili haya kuwa wao ndio walioiangusha ndege ya abiria ya Coastal na kuuwa abiria wote 356, pia wanahusika na mpango wa wizi mkubwa wa dhahabu huko Geita, na katika hilo faili la tatu tumeona ni wao ndio waliofanikisha mauaji ya Makamu wa Rais, Marehemu Jamal Mlimi. Kazi yetu sasa ni kuchunguza sababu za kufanyika matukio yote hayo matatu, bila shaka, Balozi Rwekaza na Donald Tengo watakuwa na majibu!" Daniel akasema.

Hannan na Martin wakaitikia kwa kutikisa kichwa.

"Sasa Hannan hebu iwashe simu ya Robin tuone kama tutapata chochote?" Daniel alisema.

Hannan akaiunganisha simu ya Robin na tarakilishi yake, akaiweka katika mfumo ambao hata mtu akiitafuta haitaonesha kama ipo mahali pale. Mara zikaanza kuingia jumbe mbalimbali. Hannan alisoma jumbe zote, jumbe ya sita kuingia ndio ilimstua sana.

"Daniel njoo uisome hii meseji" Hannan alisema huku uso wake ukiwa katika tarakilishi.

Daniel alisogea hadi katika meza iliyokuwepo tarakilishi ya Hannan, na kuanza kusoma ujumbe. Ujumbe ulisomeka hivi..

'Robin, vipi umejua mahali mzigo wa ZAK ulipo?'

"Nini kinachokupa shaka juu ya ujumbe huu Hannan?" Daniel aliuliza baada ya kuusoma na kutouelewa.

"Bila shaka huu ujumbe ni fumbo, na kilichonifanya niutilie wasiwasi hivyo ni anuani ulipotoka ujumbe huu"

"Umetokea wapi?" Daniel aliuliza.

"Ujumbe umetoka katika kompyuta iliyopo katika makao makuu ya ujasusi Marekani!"

"C.I.A?" Daniel alishangaa.

"Ndio. Na umetumwa nusu saa iliyopita. Nimeshangaa maana Robin alisema ameacha kazi C.I.A, kwanini ujumbe huu utokee hukohuko C I.A, Bila shaka Robin alitudanganya" Hannan alisema.

"Inavyoonesha Robin aliingia hapa nchini kuusaka mzigo wa ZAK na ndio maana C.I.A wanauliza kama amefanikisha kuupata. Swali la kujiuliza ni mzigo gani huo wa ZAK? Na upo wapi? Cha kukatisha tamaa mtu pekee wa kujibu swali hii amejiua.."Martin alisema kwa kukata tamaa.

"Kwakuwa Robin aliletwa na kina Donald Tengo bila shaka watakuwa wanajua juu ya mzigo wa ZAK. Sasa jukumu letu kuu ni kumsaka Donald Tengo popote pale alipo. Ni yeye pekee ndio tumaini letu" Daniel alisema.

"Kwa tulichomfanyia Donald Tengo lazima sasa atakuwa amejipanga zaidi kiulinzi. Tunahitaji silaha za kutosha katika mapambano haya. Mimi na Martin tutaenda nyumbani kwangu kuchukua silaha kisha tutarudi tena hapa. Hannan hakikisha usalama wa watoto wa Donald. Tunaweza kuwatumia baadae itakapobidi"

"Sawa Daniel, watakuwa salama"

Daniel na Martin wakachukua gari kuelekea nyumbani kwa Daniel Mwaseba.

Itaendelea...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom