SIRI PART2: MTUNZI PATRICK CK
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 10 : EPISODE 10
Edwin Mbeko aliwasili
ikulu alikoitwa na Rais.
“Edwin karibu
sana.Nashukuru umefika kwa
wakati” akaanzisha maongezi
Dr Fabian
“Nashukuru sana
mheshimiwa Rais”
“Nimetaka uje asubuhi hii
tuzungumze kwa sababu nina
ratiba ndefu siku ya leo.Nina
ugeni wa marais wa Uganda na
jamhuri ya kidemokrasia ya
Congo.Tutakuwa na kikao
muhimu sana hivyo
mazungumzo yetu yatakuwa
mafupi sana” akasema Dr
Fabian
“Edwin nimekuta hapa
kuja kukujulisha rasmi
kwamba kuanzia sasa wewe
utakuwa ndiye mkurugenzi
mkuu wa SNSA.Umekaimu
nafasi hii kwa miaka mitatu na
umefanya kazi nzuri sana
hivyo kwa mamlaka yangu
nimekuteua kuwa mkurugenzi
mkuu na msaidizi wako
nitamteua hapo baadae”
akasema Dr Fabian
“Mheshimiwa Rais
umenistua sana.Sikutegemea
kabisa ama ungeweza kuniteua
kushika nafasi hiyo” akasema
Edwin
“Unastahili nafasi hiyo”
akasema Dr Fabian
“Nashukuru mno
mheshimiwa Rais kwa kuniona
ninafaa”
“Unafaa Edwin.Umekuwa
katika nafasi ya ukaimu kwa
miaka mitatu na hakujawahi
kutokea tatizo lolote.Nilifanya
makosa makubwa kuamua
kumleta mtu ambaye haijui
vyema idara ile na tazama
mambo yaliyotokea.Ndani ya
siku mbili tu ambazo Annabel
amekuwa katika nafasi ya
ukurugenzi yametokea mambo
ya ajabu sana.Ameingiza watu
wasio watumishi wa
idara.Vimetokea vifo vya
wafanyakazi wawili n.k.Kama
angeendelea kwa mwezi
mzima sifahamu nini
kingetokea hivyo sitaki tena
kumuona katika idara
ile.Ulifanya vizuri sana
kutumia kanuni kumuondoa
katika nafasi yake.”
“Mheshimiwa Rais
ninashukuru sana kwa uteuzi
huu na ninakuahidi kufanya
kazi iliyotukuka
kabisa”akasema Edwin
“Edwin nataka ukafanye
kazi .Nataka nchi iwe salama”
akasema Dr Fabian
“Usiwe na hofu
mheshmiwa Rais.Idara yetu
hailali watu wanafanya kazi
saa ishirini na nne kuhakikisha
nchi inakuwa salama”
“Good.Kubwa nililokuitia
hapa ni hilo la kukupa hiyo
taarifa nzuri” akasema Dr
Fabian
“Mheshimiwa rais kwa
mara nyingine ninashukuru
sana na ninakuahidi kazi
nzuri.Hata hivyo nina swali
dogo kama utaniruhusu
kuuliza”akasema Edwin na Dr
Fabian akaitazama saa yake
kisha akasema
“Uliza”
“Ni kuhusiana na tukio la
jana usiku.Uliniambia mtu
ambaye alivamia ofisi zetu
anaitwa Mathew Mulumbi.Ni
nani huyo mtu?
“Mathew Mulumbi hata
mimi simfahamu vyema lakini
wanaomfahamu wanadai
aliwahi kufanya kazi katika
idara ya ujasusi kabla ya
kuanza kujishughulisha na
biashara zake binafsi.Licha ya
kuacha kazi katika idara ya
ujasusi lakini inadaiwa
Mathew ameendelea kufanya
kazi za ujasusi kwa
kujitegemea na inasemekana
miaka mitatu iliyopita
alishiriki katika misheni ya
kuwakomboa mateka
waliotekwa na kundi la IS na
mmoja wa mateka hao akiwa
ni mtoto wa Rais aliyemaliza
muda wake kwa bahati mbaya
katika misheni hiyo inadaiwa
alifariki dunia lakini kwa
mshangao mkubwa Mathew
ameibuka wiki hii kutoka
kusikojulikana.Mambo
anayoyaongea na kuyafanya
yanatia shaka sana kama kweli
ni binadamu wa kawaida au ni
mzimu unatuchezea.Kwa
mfano jana aliwezaje kutoka
ndani ya jengo lile bila
kuonekana? Akauliza Dr
Fabian
“Mheshimiwa Rais hata
sisi tumejiuliza alitokaje ndani
ya jengo lile bila
kuonekana?Lakini
mheshimiwa Rais bado kuna
kitu kimoja nataka
kukifahamu kama
itakupendeza “
“Sema Edwin usiogope”
“Nataka kufahamu chanzo
cha taarifa ile ya Mathew
kuingia ndani ya jengo letu”
akasema Edwin
“Ni Annabel”
“Annabel?Edwin
akashangaa
“Ndiyo.Yeye ndiye
aliyeniambia kwamba
anamsaidia Mathew kuingia
ndani ya ofisi zenu na ndipo
nikakupigia.Hiyo ni moja ya
sababu kubwa iliyonifanya
nikamuondoa katika nafasi ile
ya ukurugenzi”
“Mheshimiwa Rais
Annabel alikueleza Mathew
alikuja kutafuta nini katika
ofisi zetu?akauliza Edwin
“Hakunieleza sababu za
kumsaidia Mathew kuingia
SNSA”
“Mheshimiwa rais
utaniwia radhi lakini kwa hiki
alichokifanya Annabel na
Mathew wamekwisha ingia
kwenye orodha ya watu hatari
kwa usalama wa nchi.Annabel
japo amekuwa mkurugenzi wa
SNSA kwa siku mbili lakini
ameyafahamu mambo mengi
ya idara,tayari amezifahamu
siri nyingi za usalama wa nchi
na kama amemsaidia Mathew
kuingia ndani ya ofisi zetu ni
wazi kuna siri wanazitafuta na
watajaribu kila njia hadi
wafanikiwe lengo lao” akasema
Edwin
“Unalolisema Edwin ni la
kweli kabisa.Tayari Annabel
amekwisha onekana kuwa
hatari hivyo tunatakiwa
kuanza kummulika na kujua
mwenendo wake.Nitakuita
tena kesho tutalizungumza hili
kwa kirefu zaidi” akasema Dr
Fabian huku akinyanyuka
kitini
“Kwa heri mheshimiwa
rais,jivinjari ikulu mara ya
mwisho kwani kabla ya
machweo leo tayari utakuwa
umerejea kwa muumba wako”
akawaza Edwin wakati
akiagana na Rais
MAISHA NA KIFO CHA MELANIE CHUMA
SEASON 10 : EPISODE 10
Edwin Mbeko aliwasili
ikulu alikoitwa na Rais.
“Edwin karibu
sana.Nashukuru umefika kwa
wakati” akaanzisha maongezi
Dr Fabian
“Nashukuru sana
mheshimiwa Rais”
“Nimetaka uje asubuhi hii
tuzungumze kwa sababu nina
ratiba ndefu siku ya leo.Nina
ugeni wa marais wa Uganda na
jamhuri ya kidemokrasia ya
Congo.Tutakuwa na kikao
muhimu sana hivyo
mazungumzo yetu yatakuwa
mafupi sana” akasema Dr
Fabian
“Edwin nimekuta hapa
kuja kukujulisha rasmi
kwamba kuanzia sasa wewe
utakuwa ndiye mkurugenzi
mkuu wa SNSA.Umekaimu
nafasi hii kwa miaka mitatu na
umefanya kazi nzuri sana
hivyo kwa mamlaka yangu
nimekuteua kuwa mkurugenzi
mkuu na msaidizi wako
nitamteua hapo baadae”
akasema Dr Fabian
“Mheshimiwa Rais
umenistua sana.Sikutegemea
kabisa ama ungeweza kuniteua
kushika nafasi hiyo” akasema
Edwin
“Unastahili nafasi hiyo”
akasema Dr Fabian
“Nashukuru mno
mheshimiwa Rais kwa kuniona
ninafaa”
“Unafaa Edwin.Umekuwa
katika nafasi ya ukaimu kwa
miaka mitatu na hakujawahi
kutokea tatizo lolote.Nilifanya
makosa makubwa kuamua
kumleta mtu ambaye haijui
vyema idara ile na tazama
mambo yaliyotokea.Ndani ya
siku mbili tu ambazo Annabel
amekuwa katika nafasi ya
ukurugenzi yametokea mambo
ya ajabu sana.Ameingiza watu
wasio watumishi wa
idara.Vimetokea vifo vya
wafanyakazi wawili n.k.Kama
angeendelea kwa mwezi
mzima sifahamu nini
kingetokea hivyo sitaki tena
kumuona katika idara
ile.Ulifanya vizuri sana
kutumia kanuni kumuondoa
katika nafasi yake.”
“Mheshimiwa Rais
ninashukuru sana kwa uteuzi
huu na ninakuahidi kufanya
kazi iliyotukuka
kabisa”akasema Edwin
“Edwin nataka ukafanye
kazi .Nataka nchi iwe salama”
akasema Dr Fabian
“Usiwe na hofu
mheshmiwa Rais.Idara yetu
hailali watu wanafanya kazi
saa ishirini na nne kuhakikisha
nchi inakuwa salama”
“Good.Kubwa nililokuitia
hapa ni hilo la kukupa hiyo
taarifa nzuri” akasema Dr
Fabian
“Mheshimiwa rais kwa
mara nyingine ninashukuru
sana na ninakuahidi kazi
nzuri.Hata hivyo nina swali
dogo kama utaniruhusu
kuuliza”akasema Edwin na Dr
Fabian akaitazama saa yake
kisha akasema
“Uliza”
“Ni kuhusiana na tukio la
jana usiku.Uliniambia mtu
ambaye alivamia ofisi zetu
anaitwa Mathew Mulumbi.Ni
nani huyo mtu?
“Mathew Mulumbi hata
mimi simfahamu vyema lakini
wanaomfahamu wanadai
aliwahi kufanya kazi katika
idara ya ujasusi kabla ya
kuanza kujishughulisha na
biashara zake binafsi.Licha ya
kuacha kazi katika idara ya
ujasusi lakini inadaiwa
Mathew ameendelea kufanya
kazi za ujasusi kwa
kujitegemea na inasemekana
miaka mitatu iliyopita
alishiriki katika misheni ya
kuwakomboa mateka
waliotekwa na kundi la IS na
mmoja wa mateka hao akiwa
ni mtoto wa Rais aliyemaliza
muda wake kwa bahati mbaya
katika misheni hiyo inadaiwa
alifariki dunia lakini kwa
mshangao mkubwa Mathew
ameibuka wiki hii kutoka
kusikojulikana.Mambo
anayoyaongea na kuyafanya
yanatia shaka sana kama kweli
ni binadamu wa kawaida au ni
mzimu unatuchezea.Kwa
mfano jana aliwezaje kutoka
ndani ya jengo lile bila
kuonekana? Akauliza Dr
Fabian
“Mheshimiwa Rais hata
sisi tumejiuliza alitokaje ndani
ya jengo lile bila
kuonekana?Lakini
mheshimiwa Rais bado kuna
kitu kimoja nataka
kukifahamu kama
itakupendeza “
“Sema Edwin usiogope”
“Nataka kufahamu chanzo
cha taarifa ile ya Mathew
kuingia ndani ya jengo letu”
akasema Edwin
“Ni Annabel”
“Annabel?Edwin
akashangaa
“Ndiyo.Yeye ndiye
aliyeniambia kwamba
anamsaidia Mathew kuingia
ndani ya ofisi zenu na ndipo
nikakupigia.Hiyo ni moja ya
sababu kubwa iliyonifanya
nikamuondoa katika nafasi ile
ya ukurugenzi”
“Mheshimiwa Rais
Annabel alikueleza Mathew
alikuja kutafuta nini katika
ofisi zetu?akauliza Edwin
“Hakunieleza sababu za
kumsaidia Mathew kuingia
SNSA”
“Mheshimiwa rais
utaniwia radhi lakini kwa hiki
alichokifanya Annabel na
Mathew wamekwisha ingia
kwenye orodha ya watu hatari
kwa usalama wa nchi.Annabel
japo amekuwa mkurugenzi wa
SNSA kwa siku mbili lakini
ameyafahamu mambo mengi
ya idara,tayari amezifahamu
siri nyingi za usalama wa nchi
na kama amemsaidia Mathew
kuingia ndani ya ofisi zetu ni
wazi kuna siri wanazitafuta na
watajaribu kila njia hadi
wafanikiwe lengo lao” akasema
Edwin
“Unalolisema Edwin ni la
kweli kabisa.Tayari Annabel
amekwisha onekana kuwa
hatari hivyo tunatakiwa
kuanza kummulika na kujua
mwenendo wake.Nitakuita
tena kesho tutalizungumza hili
kwa kirefu zaidi” akasema Dr
Fabian huku akinyanyuka
kitini
“Kwa heri mheshimiwa
rais,jivinjari ikulu mara ya
mwisho kwani kabla ya
machweo leo tayari utakuwa
umerejea kwa muumba wako”
akawaza Edwin wakati
akiagana na Rais