Riwaya: Siri

SIRI
Season 2
Episode 13
Mtunzi Patrick CK Edger kaka alibaki ndani ya
mawazo mengi baada ya
kuzungumza na Sayid Omar
“Analosema Sayid ni jambo la
msingi sana.Nadhani wakati
umefika wa mimi kutangaza nia
yangu ya kutaka kugombea urais
katika uchaguzi mkuu ujao.Nina
mtaji mkubwa wa wafuasi.Wengi
wananiamini sana hasa vijana
ambao wana imani kubwa
kwangu.Tukio hili la kutakakuuawa kwa sumu nalo ni mtaji
mkubwa litaniongezea kura nyingi
nitakapoamua kugombea.Sayid
yuko sahihi huu ni wakati wangu
wa kuchukua kiti cha urais.Lakini
nitaweza kupewa nafasi ya
kuteuliwa na chama changu
kugombea urais? Akajiuliza
“Sina hakika kama wanaweza
wakanipa nafasi hiyo kwani kuna
watu ndani ya chama ambao tayari
wamekwisha panga safu za uongozi
na mimi sina nguvu kubwa ndani
ya chama hivyo sina hakika kama
ninaweza kupewa nafasi ya
kupeperusha bendera ya
chama.Ngoja niombe ushauri kwa
Stanley katibu wangu ambaye ndiye mshauri wangu mkuu”
akawaza Edger na kumtafuta
Stanley katika mtandao akampata
na kumpigia simu
“Edger is that you?Nimepatw
ana mshangao mkubwa.Nimetafuta
sana naman ya kuwasiliana nawe
lakini nimeshindwa kupata
mawasiliano ya huko.Nimejaribu
kuwasiliana hata na balozi wetu
Israel lakini hakuna mafanikio
yoyote.Siamini kama
ninazungumza nawe.Vipi
maendeleo yako?
“Mungu mkubwa Stanley
ninaendelea vyema kama
unavyoniona”akasema Edger
“Edger sijui niseme nini nabaki tu namtukuza Mungu kwani huu ni
muujiza kwangu.Sikutegemea
kabisa kukuona ukiwa katika hali
hii” akasema Stanley
“Stanley sina muda mrefu
sana,kuna jambo la msingi nataka
kukueleza ambalo siwezi
kumueleza mtu mwingine zaidi
yako ila naomba ibaki kuwa siri
yako” akasema Edger
“Edger you can trust me”
akasema Stanley
“Stanley chanzo cha ugonjwa
wangu ni sumu.
“Oh my God!! Stanley akastuka
“Ndiyo Stanley.Kwa mujibu wa
madaktari niliwekewa sumu
ambayo ilipitia kwenye ngozi.Wanahisi aidha nilipuliziwa
sumu hiyo au niliogea sabuni yenye
sumu.Kwa mujibu wa maelezo ya
madaktari ni kwamba aina hii mpya
ya sumu hutumiwa sana katika
mauaji ya kimya kimya kwa sababu
huwa ni vigumu kugundulika kwa
haraka.Kilichonisaidia mimi
nikaweza kukaa muda mrefu hadi
nikaweza kufika huku Israel ni
dawa nilizopewa ambazo ziliweza
kuipunguza nguvu ile sumu na
kunifanya niendelee kuishi kwa
muda mrefu,hata hivyo kulikuwa
na baadhi ya sehemu za mwili
ambazo zilikuwa zimeathiriwa na
sumu ile hivyo ikawabidi madaktari
wanifanyie upasuaji wa kuondoa sehemu zote zilizoonesha kuwa
zimeharibiwa na sumu ile
kali.Nashukuru Mungu kwa sababu
operesheni ile ilifanikiwa na kwa
sasa ninaendelea vizuri sana.”
Kimya kikapita cha sekunde
kadhaa.
“Stanley? Edger akaita
“Nipo Edger.Taarifa hii
imenistusha mno.Sikutegemea
kama chuki ingeweza kufikia hatua
hii.Ni akina nani unawahisi
wanaweza kuhusika na kitendo
hicho cha kutaka kukuua?akauliza
Stanley
“Mpaka sasa siwafahamu
wahusika lakini naamini ni
mtandao wa mafisadi ninaopambana nao ndio waliofanya
jambo hili.” Akasema Edger
“Edger hatuwezi kuwaacha
watu hawa wafanye watakavyo
hapa nchini kana kwamba hakuna
sheria,hatuwezi kuwaacha
waendelee kuzitafuna rasilimali za
nchi bila kujali masikini walio
wengi.I’m not scared of them,are
you? Stanley akauliza huku akiwa
amekasirika sana
“Stanley kamwe siwezi
kuwaogopa watu
hawa.Tunachopaswa kufahamu ni
kwamba watu hao wana nguvu na
wana uwezo wa kufanya lolote lile
bila kuchukuliwa hatua,tukitaka
kupambana nao tubadili mbinu za mapambano.Kuendelea
kuwaandika gazetini ,kuwasema
bungeni bado haisaidii.Kwa nguvu
walizonazo hata kama
tukiwafikisha mbele ya sheria
watashinda tu.Hii ndiyo sababu
iliyonifanya nifikiri kubadili mbinu
ya upambanaji”
Stanley akakaa kimya kidogo
halafu akauliza.
“Umepanga tutumie njia gani
mpya ya mapambano?
Edger akavuta pumzi ndefu na
kusema taratibu
“Nataka nigombee urais wa
Tanzania”
“Sijasikia vizuri,unasemaje?
Stanley akauliza “Nataka nigombee urais wa
Tanzania katika uchaguzi mkuu
ujao wa Urais.” Edger akarudia
tena.
“Edger are you sure? Stanley
akauliza baada ya tafakari ya
sekunde chache
“Yes I’m very sure.Nimefikiria
sana na nimeona hiyo ndiyo njia
pekee ya kuniwezesha mimi na
wale wote walio mstari wa mbele
katika mapambano kuwa na nguvu
ya kupambana na wahujumu wa
uchumi.Umeogopa kusikia hivyo?
“Sijaogopa Edger.Nimefurahi
kupita maelezo.Siku zote hata mimi
nimekuwa nikifikiria kukueleza
suala kama hilo lakini sikuwahi kukusikia hata siku moja ukitamka
kuwa una ndoto za kuwa rais wa
Tanzania kwa siku za
usoni.Nimefurahi kwa kuwa kile
nilichokuwa nakiwaza kwa muda
mrefu kimetimia.Ninabaki
ninamtukuza Mungu na kuamini
kwamba yote hii ni mipango
yake.Kama hawa jamaa
wasingefanya jaribio la kukuua
usingekuwa na mawazo ya kuwania
urais”
Edger akatabasamu na
kusema.
“Stanley ni kweli sikuwahi
kuota kama iko siku nitafikiria
kuwania urais wa Tanzania.Lakini
kwa jambo walilonifanyia sioni sababu ya kutokufanya
hivyo.Nitagombea urais na kama
nikifanikiwa kushinda nitakuwa na
nguvu kubwa ya kupambana na
hawa jamaa ambao wamekaa juu ya
sheria.Pamoja na maamuzi hayo
lakini sitegemei mambo kuwa
mepesi.Najua nitakumbana na
vikwazo vingi sana lakini kwa
sababu nimekwisha weka nia ni
lazima niitimize” akasema Edger
“Nakubaliana nawe
Edger.Lazima utakumbana na
wakati mgumu sana.lakini kitu
ninachoweza kukuhakikishia kuwa
nchi italipuka kwa furaha kubwa
pale watakaposikia kuwa unataka
kugombea urais wa Tanzania.Kwa taarifa yako tu ni kwamba nchi yote
ilizizima pale ilipotangazwa
kwamba umepatwa na ugonjwa wa
ghafla.Nakosa neno la kueleza hali
iliyokuwapo.Kazi zilisimama kwa
muda hasa baada ya taarifa
kusambaa kuwa umefariki
dunia.Hii yote ni dalili ya wazi ya
kukubalika kwako katika jamii”
Edger akastuka na kuuliza
“Ina maana kulikuwa na taarifa
kuwa nimefariki dunia?
“Ndiyo Edger.Taarifa
zilisambaa kuwa umefariki dunia
na hivyo kuzusha taharuki
kubwa.Huwezi amini kazi
zilisimama.Ilipotoka taarifa kuwa
unaletwa Dar es salaam kwa matibabu zaidi,vijana kwa mamia
wakajazana uwanja wa ndege
kuhakikisha kama taarifa ile ni ya
kweli au la.Kwa ufupi naweza
kukuhakikishia kuwa unapendwa
mno Edger.Ndiyo maana sipati
picha ya jinsi itakavyokuwa pale
watakaposikia kuwa unagombea
urais”
“Du ! sikuwa naelewa chochote
juu ya kilichotokea huko nyumbani
kipindi cha ugonjwa wangu.Hata
malaika wangu aliyetumwa kuja
kuniokoa hakunieleza jambo hilo”
akasema Edger
“Malaika yupi? Akauliza
Stanley
“Kuna malaika anayeishi ambaye ameyatoa muhanga maisha
yake kwa ajili ya kuhakikisha kuwa
ninapona.Amepambana kufa na
kupona kwa ajili yangu.Bila yeye
kwa sasa jina langu lingekuwa
katika orodha ya marehemu.Ni mtu
muhimu sana kwangu ambaye sioni
ni kitu gani ninachoweza kumlipa
katika maisha yangu yaliyobaki”
Edger akasema kwa hisia kali
“Ni nani huyo aliyepambana
kufa na kupona kuyaokoa maisha
yako?
“Anaitwa Dr Olivia
Themba,binti wa bilionea Agrey
Themba.Huwezi amini huyu ndiye
shujaa wangu”
“Edger unapomtaja Dr Olivia unaonekana kuwa na hisia kali
sana,ukaribu wenu ni ule wa
daktari na mgonjwa wake au ni
zaidi ya hapo?
Swali hili lilimfanya Edger
“Stanley ukaribu tulionao ni
ule ukaribu wa daktari na mgonjwa
wake,lakini kila ninapokuwa naye
karibu najihisi tofauti kabisa.Nahisi
kuna kitu ndani yangu”akasema
Edger
“Nifafanulie vizuri Edger
unahisi nini?Stanley akauliza
“Nahisi kuna kitu kip kati
yetu.Sijawahikuwa na hisia hizi
hapo kabla” Edger akajibu kwa
sauti iliyotulia.
“Edger sijawahi kukusikia ukimsifia mwanamke hii ni mara ya
kwanza nakusikia unatamka
kwamba unahisi kitu kwa Dr
Olivia.Usiniambie tayari umetokea
kumpenda” akasema Stanlye huku
akitoa kicheko kidogo
“Stanley siwezi kukuficha
nahisi tayari nimeanza
kumpenda”akasema Edger.Stanley
akavuta pumzi ndefu halafu
akasema
“Edger wewe ni rafiki yangu
mkubwa,licha ya urafiki wetu mimi
ni katibu wako unaniamini sana na
unanishirikisha katika kila jambo
hivyo nataka nikushauri jambo la
muhimu sana na ninakuomba
uupokee ushauri wangu” akasema Stanley
“Nakusikiliza Stanley”
akasema Edger
“Edger nakushauri haraka
sana yaondoe kichwani mwako
mawazo au hisia zote unazoanza
kuzijenga kuhusiana na huyo
mwanamke Dr Olivia Themba.Stay
far away from her.”akasema
Stanley
“Stanley kama ninataka
kuwania urais itanilazimu nifunge
ndoa.Nitakuwaje rais wakati sina
ndoa?Muhimu sana niwe na mke na
kwa sasa mwanamke ambaye
ninamuona anafaa kuwa mke
wangu ni Dr OIivia.Amepigana kwa
ajili yangu na nina hakika kama akiwa mke wangu atakuwa ni mke
bora na ana sifa zote za kuwa mke
bora”
“Edger liweke kwanza
pembeni suala hilo usilipe uzito
wowote kwa sasa na jaribu
kuziepuka hisia zinazoanza
kujengeka za kumpenda Dr Olivia”
akasema Stanley
“Stanley I don’t know…I real
don’t know.I’m confused.”Akasema
Edger
“Please Edger try to avoid her
as soon as you can.That’s my
advice”
“Stanley I real don’t know….Ila
ninachokuomba kwa sasa,fanya
uchunguzi wa kina juu ya mchakato wa kuwania urais ndani na nje ya
chama unavyokwenda,nataka kujua
ni akina nani wamekwisha onyesha
nia ya kutaka kuwania nafasi
hiyo,kesho unipe ripoti
kamili”akasema Edger
“Sawa Edger ,nitafanya hivyo
ulivyoelekeza.Kesho tutazungumza
kwa kirefu zaidi.Ila zingatia
maneno niliyokueleza”
“Ahsante Stanley uwe na usiku
mwema”akasema Edger na kukata
simu,akavuta pumzi ndefu na
kuzama katika dimbwi la mawazo.
“Stanley ninamuamini sana ni
katibu wangu na ndiye mshauri
wangu mkuu pia lakini kwa hili
alilonieleza leo amenichanganya
sana.Tayari nimekwisha anza kuona kila dalili za moyo wangu
kuangukia kwa Dr Olivia.Sikuwahi
kujihisi hivi hapo kabla.Kwa nini
ananizuia nisimpende Dr Olivia?
Kuna chochote anakifaamu kuhusu
Dr Olivia ambacho kinaweza
kumfanya awe na wasi wasi naye?
Kesho nitakapozungumza naye
nitamuuliza kama kuna sababu
yoyote ambayo inaweza kunizuia
mimi kumpenda Dr Olivia.Milango
ya moyo wangu tayari imeanza
kufunguka na kumkaribisha Dr
Olivia na kuna kila dalili kwamba
tunaendana kwa kila kitu.Kumkosa
mwanamke kama yule ni kosa la
jinai labda kama kuna sababu
kubwa na ya msingi sana”akawaza
Edger
************** Judy aliyasikiliza na
kuyarekodi mazungumzo yote ya
Edger kaka na Stanley na baada ya
kumaliza mazungumzo yao,akaanza
kuyasikiliza tena upya kwa umakini
mkubwa.
“Nadhani mazungumzo haya
pia yanafaa kutumwa Dar es salaam
ili wayafanyie kazi mara
moja.Wanatakiwa kuanza
kumfuatilia Stanley ambaye
anaonekana ni mtu wa karibu na
wa muhimu sana wa Edger na
ndiye anayemtegemea katika
mambo mengi.Hii ni kazi ya watu
wa Dar es salaam.Mimi kazi yangu
ni kutafuta taarifa na kuwatumia” akawaza Judy na kabla ya kutuma
akampigia simu Paul
“Paul nimenasa tena
mazungumzo mengine kati ya
Edger na mtu mmoja anaitwa
Stanley ambaye ni katibu wake na
mtu wake wa muhimu
sana.NInawatumia maongezi yao
mtajua wenyewe nini cha kufanya”
akasema Judy na kuyatuma
maongezi yale ya Edger na Stanley
aliyokuwa amerekodi.
Baada ya kuyapokea
mazungumzo yale Paul akiwa na
timu yake wakayasikiliza kwa
makini sana.Waliyarudia tena zaid
ya mara tatu hadi kila mmoja
aliporidhika. “Nadhani Donald Nkebo
anapaswa kuyasikiliza
mazungumzo haya halafu atatoa
maelekezo.Tutamtumia haya
mazungumzo ya Edger na Stanley
lakini haya mazungumzo ya Edger
na Sayid hatutamueleza kwa sasa”
Akasema Paul
“Kwa nini tusimueleze
Paul?Kuna umuhimu afahamu
Edger ni mtu wa namna gani”
“Nina sababu zangu kwa nini
hatutamueleza Donald Nkebo
kuhusu Sayid.Guys tumekuwa
tunafanya shughuli hizi kwa miaka
mingi lakini wakati umefika wa
kupumzika na kufanya mambo
mengine makubwa ya maendeleo hivyo basi tulieni niacheni mimi
niwaondoe katika
umasikini.Yawezekana hii ikawa ni
kazi yetu ya mwisho kuifanya”
akasema Paul na kumpigia simu
Donald.
“Hallo Paul,habari ya usiku
huu? Akasema Donald Nkebo baada
ya kupokea simu
“Nzuri kabisa mkuu” akajibu
Paul.
“Nipe ripoti Paul kuna
chochote mmekipata?
“Ndiyo mkuu.Judi amefanikiwa
kunasa mazungumzo ya simu ya
Edger kule Israel”
“Good job.Hayo ndiyo mambo
ninayoyataka.Amezungumza na nani?
“Tumefanikiwa kunasa
mazungumzo kati ya Edger na mtu
mmoja aitwaye Stanley.Huyu ni
mtu wake muhimu sana.Nakutumia
maongezi hayo sasa hivi uyasikilize
halafu utupe maelekezo nini cha
kufanya”akasema Paul
“Sawa Paul tuma sasa hivi”
akajibu Donald Nkebo akionekana
kuwa na shauku kubwa ya kutaka
kufahamu nini Edger
amezungumza na Stanley
Baada ya kutumiwa
mazungumzo yale Donald
akayasikiliza kwa umakini
mkubwa.Akachukua chupa ya
pombe kali akaimimina katika glasi akanywa funda kubwa na kusema
kwa sauti ndogo
“Mheshimiwa rais anapaswa
ayasikilize maongezi haya.Naamini
hapa tumegusa penyewe.Edger
anataka kuwania urais! Naamini
rais jasho litamtoka”akawaza
Donald Nkebo na bila kukawia
akachukua simu na kumpigia rais
Dr Evans Mwaluba.
“Donald” akasema Dr Evans
“Mheshmiwa Rais habari za
usiku huu”
“Nzuri kabisa Donald.Simu
yako ya usiku huu inaashiria kuna
jambo la muhimu sana” akasema Dr
Evans
“Mheshimiwa Rais,kuna jambo muhimu sana ambalo huna budi
kulifahamu.Yule binti tuliyemtuma
Israel kufanya kazi ya
kumchunguza Edger tayari
ameanza kazi na kuna
mazungumzo ambayo tayari
ameyanasa kati ya Edger na mtu
mmoja aitwaye Stanley ambaye
anaonekana nimtu wake wa karibu
sana.Ni maongezi muhimu ambayo
ni vizuri ukayasikiliza kwanza
halafu tujadiliane nini cha kufanya”
akasema Donald Nkebo
“Sawa Donald nayasubiri”
akajibu Dr Evans.
Baada ya muda mfupi Donald
akamtumia Dr Evans mazungumzo
yale ya Edger na Stanley.Dr Evans akaanza kuyasikiliza kwa makini
sana.Akarudia tena zaidi ya mara
moja kusikiliza maongezi yale
“Edger anafikiria kutaka kuwa
na mahusiano na Dr Olivia?
Akajiuliza baada ya kuriudia
kuyasikiliza mazungumzo yale
“Hili haliwezekani.Siwezi
kukubali hili likatokea.Olivia ni
binti wa Agrey ambaye ni rafiki
yangu mkubwa na ninamchukulia
kama binti yangu pia.Kitendo
chochote cha kuanzisha mahusiano
na Olivia ni kumuweka katika
hatari kubwa malaika yule na
kumuharibia maisha yake.Hili
jambo linapaswa kuepushwa
haraka sana” akawaza Dr Evans akionekana kujawa hasira
“Kingine alichonistua huyu
jamaa ameamua agombee
urais.Donald Nkebo alikuwa sahihi
kwamba huyu jamaa kutokana na
mtaji mkubwa wa wafuasi alio nao
anaweza akaamua kugombea urais
na sasa yametimia.Edger anataka
kugombea urais.Huyu kijana
akiachwa atakuja kuwa hatari
sana.Nina imani ndani ya chama
hataweza kupata nafasi kwani hana
nguvu kubwa na kwa kuwa
amekwisha weka nia ya kuwania
urais anaweza akaenda katika
vyama pinzani na huko anaweza
akapitishwa haraka sana kugombea
urais na atakuwa ni kikwazo kikubwa sana kwangu”Dr Evans
akatolewa mawazoni baada ya
simu ya Donald Nkebo kuita.
“Mheshimiwa rais umeyasikia
maongezi hayo?akauliza Donald
“Nimeyasikiliza
Donald.Mmefanya kazi nzuri sana
na endeleeni kufuatilia kila kitu
kuhusu huyu jamaa.Kuna
maelekezo ambayo nataka
kuyatoa.Kwanza ni kuhusiana na
kitu alichokizugumza kwamba
anakusudia kuanzisha mahusiano
kati yake na Dr Olivia.Donald sitaki
kusikia jambo hili
linafanikiwa.Edger akae mbali
kabisa na Dr Olivia.Donald nataka
uweke mkazo mkubwa sana katika hilo na uhakikishe mtu wako
aliyeko kule Israel anafanya kila
linalowezekana kuhakikisha Edger
anaondoa wazo la mahusiano na Dr
Olivia.Umenielewa? akauliza Dr
Evans
“Mheshimiwa rais usihofu
nimekuelewa”
“Kuhusu lile wazo lake la
kutaka kuwania urais tunatakiwa
kufuatilia sana kujua kila
anachokipanga.Kwa kuwa huyu
Stanley ndiye mtu wake wa karibu
mfuatilieni huyo na mjue
wanapanga mipango gani ndipo
tuweze kuamua nini tufanye lakini
kwa sasa nataka ulishughulikie hilo
la Edger kutaka kuanzisha mahusiano na Olivia”akasema
DrEvans
“Mheshimiwa rais nina
wazo.Kwa nini tusiache Edger awe
na mahusiano na Dr Olivia?Kama
wakiwa katika mahusiano itakuwa
rahisi sana kwetu kuweza
kumfuatilia Edger na
kummaliza”akasema Donald
“Donald that’s something I
cant allow to happen.Edger akiwa
na mahusiano na Olivia itakuwa
vigumu kummaliza Edger
kwanilazima tumuumize na Olivia
vile vile kitu ambacho sitaki
kitokee.Olivia ni mtoto wa rafiki
yangu mkubwa na mimi
ninamchukulia kama mwanangu vile vile kwa hiyo sitaki kuona
anaingia katika hatari yoyote.Olivia
ni mwanamke msomi na anatakiwa
kuwa na mume
bora,msomi,mwenye uwezo na siyo
mwanasiasa kama yule kijana!!
“Mr President.We have
to………” Donald alitaka kusema
kitu lakini rais hakutaka ushauri
wowote
“Donald are you going to do as
I say or I do it my way!! Akafoka Dr
Evans
“Samahani mheshimiwa rais
nimekuelewa lakini hili ni suala
letu na tunatakiwa tuliendee
taratibu na kwa umakini
mkubwa.Ukilishughulikia wewe mwenyewe utaharibu kila kitu.Let
us handle this Mr
president”akasema Donald Nkebo
“Donald ninataka Dr Olivia
arudi nyumbani haraka sana na hilo
pekee ndilo suluhisho.There is
must be a very huge gape between
that good for nothing Edger and
Olivia! Akasema Dr Evans
“Mheshimiwa rais ukifanya
hivyo utakuwa umeharibu
kabisa.Ni wazi wataanza kujiuliza
umejuaje habari hizi na hivyo
tunaweza tukamuweka Judy
matatani.Hebu pumzika kwa usiku
huu halafu kesho asubuhi tutajadili
nini cha kufanya.”akasema Donald
“Sawa Donald naomba hiyo
 

Similar Discussions

13 Reactions
Reply
Back
Top Bottom