Riwaya: Ngoma Ngumu

RIWAYA; NGOMA NGUMU.

NA; BAHATI MWAMBA.

SIMU; 0758573660/062415629

SEHEMU YA NNE


“Kwa hiyo huo mkakati wako ni kututaka tuuvujishe mpango wetu?”

“Hivyo ndivyo itakiwavyo!”

“Tusipotekeleza itaathiri vipi mpango wako?”

“Inaweza kuniondolea ufanisi wangu, pia inaweza kuchukua muda mrefu zaidi kukamilika, kuliko ambavyo ingevuja!”

“Hii kali aisee!” Mhisani alisema huku akiwageukia wenzake, ambao nao walikuwa wamesimama wakishangaa maelekezo ya mtu wao.

“Sawa, tutakutafuta dakika tatu zijazo.” Amolo alisema huku akikata mawasiliano na kumpa simu Kamonga.

Baada ya kuachana na Miguu ya kuku, Sadon brothers, walibaki peke yao ndani ya chumba cha mikutano, ndani ya jumba lao la kifahari. Walitazamana bila kusemeshana, huku kila mmoja akiwaza lake kichwani.

Ilikuwa ni ngumu kumwamini Miguu ya kuku, lakini haikuwa rahisi pia kufanya ile kazi peke yao. Vichwa viliwauma; mpango walouhitaji, pia walihitaji kufanya kazi na mtu wa nje ya kundi lao.

“Tufanye nini ndugu zangu!” Mhisani aliwauliza wadogo zake.

“Nadhani tumempata mtu sahihi, hatuna haja ya kujiuliza mara mbilimbili. Zuki Gadu, ni sahihi kuifanya kazi hii.” Kamonga aliendelea kuwashawishi wenzake.

“Hapa tatizo siyo Zuki, hapa tatizo ni kuvujisha mpango serikalini. Ni ngumu kulitekeleza hilo jambo!”Tindo aliongea kwa msisitizo.

“Kwanza tunakubaliana na gharama anazozihitaji?” Amolo aliwauliza wenzake.

“Hiyo ni pesa ndogo sana aliyoihitaji. Tatizo bado lipo kwenye kuvujisha mpango.” Mhisani alijibu.

“Tumpe pesa, ila tusivujishe mpango wetu uliyotugharimu pesa nyingi kukamilika. Hatuwezi kuuza gharama zetu kirahisi namna hiyo.” Amolo nae aliongezea.

“Naona tuuvujishe mpango kwa kumruhusu yeye mwenyewe auvujishe awezavyo, lakini tusivujishe mikakati yetu hata chembe!” Kamonga alishauri. Wenzake walimtizama.

“Upo sahihi! Tumpe hiyo kazi peke yake!” Tindo aliafiki.

“Na iwe hivyo!” Amolo nae alikubali, huku akimtizama Mhisani, ambae nae alitikisa kichwa chake kukubali kilichozungumzwa.

Haraka walimuunganisha Miguu ya kuku kwa njia ya mtandao.

“Kila ulichohitaji kitafanyiwa kazi, lakini kwa shariti moja tu!” Mhisani alimwambia Zuki Gadu p.a.k Miguu ya kuku.

“Nawasikilizeni!” Miguu ya kuku aliitikia.

“Tunaomba uvujishe mpango huo kwa njia zako.”

“Itabidi muongeze dau la pesa!”

“Eeh!!”

“Yes! Kwa sababu sijui mkakati wenu ulivyo, zaidi najua mnataka plate namba tano. Sijui mlivyokuwa mmejipanga kufanikisha hilo”
“Kwa hiyo tukiongeza dau, utavujisha mpango wako na si wetu?”

“Ndivyo ilivyo!”

Sadon Brother’s, walitazamana, kisha wakaafiki kuongeza dau. Ilikuwa rahisi kuafiki kwa sababu, mpango wao ulikuwa salama kuvuja.

“Sawa, ujapohitaji usaidizi, tuko tayari wakati wowote!”
Miguu ya kuku alifikiria kidogo, kisha akasema..
“ Haina ubaya! Lakini acheni nifanye kazi yangu kadri niwezavyo. Nyie mkae kimya na angalieni yatakayokuwa yanajiri. Msiingilie lolote.”

“Haina neno! Unakaribishwa Nairobi!” Mhisani alijibu na kumkaribisha Miguu ya kuku.

“Great!” Miguu ya kuku alijibu na kutoka hewani.

Baada ya Miguu ya kuku kutoka hewani, ndugu watano walibaki peke yao. Walijadili mambo machache, kisha walisambaratika na kila mmoja, alienda kuendelea na majukumu yake ya kujimaarisha zaidi kwenye kitengo chake.

DAR ES LAAM….

Miguu ya kuku aliweka simu yake pembeni, kisha aliegemea kwenye sofa na kutazama juu. Mawazo mengi yalipita kichwani mwake. Wazo moja lilikuwa zito zaidi kuliko mawazo mengine. Lilikuwa ni wazo ambalo lilimtia hofu kubwa.

“Nimefanya kazi nyingi, lakini sijawahi kuiba benki. Na kinachonitisha zaidi ni ulinzi ulioko kwenye mabenki, hasa ndani ya benki.” Alijisemea taratibu huku akijaribu kujenga picha kichwani mwake, kwenye baadhi ya mabenki makubwa nchini Tanzania.

“Hii ni kazi ngumu sana aisee!” Alisema huku akiishika laptop yake iliyokuwa mbele yake, juu ya meza. Aliparaza kidogo na ukatokea mchoro(picha) wa jengo refu lenye ghorofa zaidi ya kumi nane. Jengo lile lilinakishiwa kwa vioo, kuanzia chini hadi juu.

“Kazi ipo duh!” Alijisemea huku mkono mmoja ukiwa kidevuni na macho yake yakiwa yametulia kulitizama jengo lile. Aliendelea kulichunguza kwa umakini sana, huku akili yake ikifanya kazi kubwa kutafakari.

“Mara zote benki huwa zinakuwa chini kabisa ya majengo marefu namna hii!” Alijisemea huku akichezesha mshale wa kuongoza, kuelekea upande wa chini wa lile jengo.

“Kama ipo huku chini, ina maana, wanamiliki basement yote na huko ndiko iliko vault ya kuhifadhia pesa na vault ya kuhifadhia hizo plate!” Alijisemea tena huku akiendelea kuizungusha picha ya jengo refu, lililopewa jina la Patrice Lumumba, huku likiwa chini ya umiliki wa Nssf.

Wakati alipokuwa akiendelea kupitia picha kadhaa za jengo lile, kuna kitu kingine aligundua na kitu kile kilimtia woga wa wazi kabisa na aliwaza kutema ndoano, endapo alichokuwa amegundua kingelikuwa sahihi.

Haraka alianza kutafuta picha za satellite ili aweze kujiridhisha na kile alichokuwa amekigundua na kukitilia wasiwasi.
Jengo la Patrice Lumumba lilikuwa ni jengo refu sana na lenye uwekezaji mkubwa jijini Nairobi. Lilikuwa ni jengo ambalo lilijengwa kwa upekee sana. Lilikuwa ni jengo refu pekee maeneo ya Upper hill, huku kukiwa hakuna jengo lingine lau lenye ghorofa moja kwenye ule mtaa.

“Kwa nini ipo hivi?” Alijiuliza huku akizidi kumakinika na picha alizokuwa anazishuhudia kupitia kompyuta mpakato iliyokuwa mbele yake. Alizidi kuyatalii kwa macho maeneo jirani na jengo la Patrice Lumumba. Hapo ndipo mwili ulimsisimka zaidi.

Kwa nini!

Kwa sababu, jengo lile lilizungukwa na maeneo nyeti sana, ambayo si rahisi mtu kuyagundua, japokuwa mengine yalifahamika kirahisi. Jengo lile lilikuwa lipo katikati ya vikosi vya jeshi na vile vya usalama wa raia.

Mashariki mwake kulikuwa na makao makuu ya jeshi la kujitegemea, huku Magharibi kwake kukiwa na kituo kikuu cha polisi cha Nairobi. Upande wa kaskazini kulikuwa na kambi ya kikosi cha anga(Moi air base), na upande wa kusini kukiwa na makao makuu ya chama tawala.

“Sasa nimeelewa ni kwa nini jengo hili limeota peke yake bila kuruhusu majengo mengine ya aina hiyo! Huu utakuwa ni mtaa wa kimkakati hapo nchini Kenya!” Alijisemea huku akijishika kichwani kwa kujikwarua. Nywele ziliwasha kwa hofu ya kile alichokuwa anakiwaza.

“Mbona hii kazi inataka kunionjesha umauti?” Aliwaza huku akianza kutafuta umuhimu wa benki ya Umoja ndani ya nchi ya Kenya.

Kulikuwa na maelezo mengi sana kuhusu benki hiyo, lakini hayakumuingia akilini, yalikuwa ni maelezo mepesi kuliko alivyotarajia.

“Maelezo haya, hayawezi kufanya nchi iweke hapo zile plate za fedha!” Alisema huku akitikisa kichwa na kuchukua simu iliyokuwa pembeni yake. Alitafuta jina alilohitaji, kisha alipiga na kuzungumza kile alichotaka kuzungumza. Lakini alichojibiwa, kilimfanya afikirie kuwapigia Sadon Brothers, na kuitema kazi aliyopewa.

Yalikuwa ni maelezo ya kuogofya kwa binadamu mwenye moyo wa nyama, ilihitaji kiumbe kisicho na damu kuvumilia na kuendelea kushikilia dili gumu namna ile. Dili lenye kuuza roho.

Miguu ya kuku alikuwa amempigia simu mtu wake wa karibu, mtu ambae hufanya nae kazi kila inapotakiwa kufanya kazi. Huyu mtu alikuwa ni kiongozi wa kanisa ndani ya jiji la Nairobi. Mtu huyo aliitwa Mchungaji Emmanuel, alikuwa na jina lake la kazi za siri alizokuwa anafanya. Alikuwa ni muuzaji wa silaha, huku akitumia mgongo wa kanisa, kama kivuli cha kuifanya biashara yake hiyo, iliyokuwa imeshamiri sana nchini Congo na sasa alikuwa Nairobi kama sehemu ya kupanua mtandao wake.

Wengi walimfahamu kwa jina la Mchungaji Emmanuel, lakini Miguu ya kuku alimfahamu na pia alipenda kumuita Bob Rando. Mtu mwenye taarifa nyeti za kila nchi anayoitembelea. Mtu ambae alikuwa ni mfanikishaji mkubwa wa mipango yake.

“Nambie Zuki!” Mchungaji Emmanuel p.a.k Bob Rando, alianza kuongea baada ya kupokea simu.

“Safi Bob!” Miguu ya kuku alijibu.

“Najua umenipigia utakuwa upo mzigoni kama kawaida yako!”

“Hakika hujakosea Bob! Niko hapo Nairobi, lakini roho inasita kuendelea na jambo langu!”

“Mh! Leo hiyo!? Kama roho inasita, achia dili. Uhai ni muhimu zaidi kwa sasa”

“Tatizo jamaa wameshafanya malipo ya awali, kitu ambacho kitanibana ni kanuni zangu, nikipokea huwa sirudishi hadi nikamilishe kazi”

“Kanuni zipo ili zivunjwe komredi”

“Hujakosea! Lakini kanuni zangu hazina kipengele cha kuvunjwa!”

“Basi, fanya hiyo kazi kama huwezi kuivunja. Vaa mabomu, ingia mzigoni!”

“Ngoja nione hadi mwisho itakuwaje”

“Naamini akili yako bado haijachoka kuvunja mitego yote! Upo wewe ni zaidi ya mwanajeshi Zuki!”

“Sawa kwa kunipa nguvu upya, naomba unipe msaada kidogo kabla sijaja Nairobi”

“Kila siku nipo kwa ajili yako! Wewe ni zaidi ya ndugu. Wakati wote nipo kwa ajili yako, hadi siku nitakapoiaga Dunia!”

“Maneno mazito sana unaongea Bob! Naomba unisaidie kudukua jengo la Patrice Lumumba na ikibidi, unipe na unyeti wa Benki ya Umoja.”

“Taarifa zake unazihitaji lini?”

“Hata kama unazo sasa hivi, nipe.”

“Nipe nusu saa!” Bob Rando alisema na kukata simu.

Miguu ya kuku alipumua peke yake, huku akiigeukia laptop yake. Kisha akaanza kusoma mikakati ya kifedha kutoka wizara ya fedha ya Kenya. Aliamua kusoma mikakati hiyo, kwa kuwa alijua kuna kitu kitakuwa kimepangwa na nchi ya Kenya kuhusu mipango fedha.

“Plate namba tano, haiwezi kuwa na umuhimu kiasi hicho kama ingelikuwa haina jambo nyuma yake. Lazima kuna kitu kinachowasukuma hawa jamaa kuiba hii plate!” Alijisemea huku vidole vyake vikicheza kwa kasi kubwa na macho yake yakiwa makini, kutizama kilichokuwa kinapita kwenye kompyuta yake.

Wakati alipokuwa akizipita ripoti kadhaa, hatimae alikutana na ripoti ambayo iliamsha hisia fulani kichwani kwake. Ripoti ilitolewa na katibu wa wizara, ripoti ilihusu mpango wa serikali kuchapa shilingi mpya, ambayo itaziba mianya ya wahujumu uchumi ambao wameondoa pesa kwenye mzunguko na kupelekea kuwe na hali ngumu ya uchumi. Ripoti ile iliendelea kubainisha kuwa; lengo la kufanya vile ni, kuwafanya watu walioondoa pesa kwenye mzunguko, kurejesha pesa hizo ili kuendana na matumizi mapya ya shilingi mpya.

“Sasa hiyo plate na hili jambo vinaingilianaje?” Alijiuliza huku akiwa ameganda na asijue la kufanya.

“Hawa jamaa wanataka kuihujumu nchi yao bila shaka!” Alijisemea huku akiendelea kuperuzi habari nyingine.

“Nchi za wenzetu huko, haya makundi ya kihuni huwa yanamiliki uchumi wa nchi, yawezekana na hawa wanataka kulitenda hilo hilo nchini mwao!” Alijiwazia.

“Lakini hainihusu! Kazi yangu ni kutekeleza tu!” Alisema kwa sauti huku akiichukua simu yake iliyokuwa inaita pembeni yake.

“Unauhakika, unataka kufanya hili jambo?” Bob alianza kwa swali baada ya mwenzake kupokea simu.

“Ni lazima nilifanye komredi!”

“Sasa sikia; ile Benki ya Umoja ni benki ya biashara, lakini ipo kwenye mikono ya serikali kwa asilimia zote. Yaani ile pale ni tawi la benki kuu, japo wananchi hawajui lolote, zaidi wanajua ni benki ya kibiashara tu. Lakini kikubwa zaidi, ile benki ndiyo yenye hazina yote ya nchi. Ina maana kwamba; hata vipande vya madini vimehifadhiwa pale ina maana, ile ndiyo roho ya nchi. Na kulithibitisha hilo, lile jengo limejengwa kwenda chini ghorofa mbili, na huko ndiko mzigo unaoutaka umehifadhiwa. Lakini…”

“Lakini nini Bob!”

“Huko chini, kuna ofisi za Usalama wa nchi na ina maana, kunalindwa saa ishirini na nne tena ulinzi mkali kuliko unavyodhani.

“Duh! Una maanisha, vault ipo kwenye hizo ghorofa za chini?”

“Exactly! Mzigo upo huko.”

“Duh!”

“Lakini ngoja nikusaidie jambo moja.”

“Lipi hilo?”

“Lile ni jengo la kibishara na huwa kunapangishwa kwa mtu yeyote mwenye kampuni kubwa. Ukishapanga, utaelekezwa kuitumia benki ya umoja kufanya kila muamala wako. Ikiwa na maana, unakuwa chini ya uangalizi bila wewe kujua.”

“Kwa hiyo una maana nipange huko juu, kisha nifanye uhuni wangu kirahisi?”

“Hakika umewaza vema!”

“Mimi naona haijakaa sawa! Unaonaje nikitafuta ajira kwenye moja ya kampuni zilizopanga humo?”

“Yes!” Bob aliitikia kwa furaha, jambo lililomshangaza Zuki p.a.k Miguu ya kuku.

“Sikia Zuki, kwenye ghorofa ya tatu, kuna kampuni ya ulinzi ya Dop. Kampuni ile huajiri watu mbalimbali wenye uzoefu na wenye ujuzi mbalimbali. Kampuni ile ndiyo inayosafirisha pesa zote za Umoja benki, lakini pia ni kampuni ambayo huajiri mafundi umeme na watu wa huduma ya kwanza. Hivyo ni wewe na uamuzi wako, uwe fundi umeme, au uwe mtoa huduma ya kwanza na uokozi kwa dharura!”

“Naweza kuwa yeyote kati ya hivyo, lakini nafasi ya kupata kazi ipo? Maana kwa harakaharaka naona hiyo ni kampuni ya wanausalama wenyewe”

“Wewe usiwaze, mathalani wamekubali kupokea mtu yeyote ili wafiche ukweli wao, utapata kazi kupitia mimi. Mimi ndiye Mchungaji Emmanuel bwana!” Bob Rando alimalizia kwa kucheka kwa sauti kubwa.

“Haya poa bwana Pastor!” Miguu ya kuku alisema na kukata simu huku akitabasamu.

“Huwa sipendi sana kuzunguka na kazi moja, kwa muda mrefu, ila hii inaonekana itanilia wakati wangu kuliko nilivyodhani” Alijisemea huku akinyanyuka na kuelekea chumbani kwake.
.
.
.
.
.
MWANDISHI; BAHATI K MWAMBA.
 
Kudo ushauri wangu tu mzee,toa tangazo kwamba unatoa vipande mfano vitano halafu itakuwa inauzwa,lakini hii ya kutoa moja unakaa wiki tatu sidhani kama unatutendea haki washabiki wako,tukiuliza hujibu,sio mambo mzee!
 
Kudo ushauri wangu tu mzee,toa tangazo kwamba unatoa vipande mfano vitano halafu itakuwa inauzwa,lakini hii ya kutoa moja unakaa wiki tatu sidhani kama unatutendea haki washabiki wako,tukiuliza hujibu,sio mambo mzee!
Jamaa ana group na mimi ni member, so mcheck kwenye namba zake kule anauza baadhi ya riwaya mkuu. Ingawa kwa hii story hata kwenye group imefikia hapa hapa.
 
Kudo usitufanyie hivyo,kuwa na ahadi za kizungu,ukiahidi halafu umepata dharula tujuze jamaa yetu!
 
“Kwa hiyo huo mkakati wako ni kututaka tuuvujishe mpango wetu?”

“Hivyo ndivyo itakiwavyo!”

“Tusipotekeleza itaathiri vipi mpango wako?”

“Inaweza kuniondolea ufanisi wangu, pia inaweza kuchukua muda mrefu zaidi kukamilika, kuliko ambavyo ingevuja!”

“Hii kali aisee!” Mhisani alisema huku akiwageukia wenzake, ambao nao walikuwa wamesimama wakishangaa maelekezo ya mtu wao.

“Sawa, tutakutafuta dakika tatu zijazo.” Amolo alisema huku akikata mawasiliano na kumpa simu Kamonga.

Baada ya kuachana na Miguu ya kuku, Sadon brothers, walibaki peke yao ndani ya chumba cha mikutano, ndani ya jumba lao la kifahari. Walitazamana bila kusemeshana, huku kila mmoja akiwaza lake kichwani.

Ilikuwa ni ngumu kumwamini Miguu ya kuku, lakini haikuwa rahisi pia kufanya ile kazi peke yao. Vichwa viliwauma; mpango walouhitaji, pia walihitaji kufanya kazi na mtu wa nje ya kundi lao.

“Tufanye nini ndugu zangu!” Mhisani aliwauliza wadogo zake.

“Nadhani tumempata mtu sahihi, hatuna haja ya kujiuliza mara mbilimbili. Zuki Gadu, ni sahihi kuifanya kazi hii.” Kamonga aliendelea kuwashawishi wenzake.

“Hapa tatizo siyo Zuki, hapa tatizo ni kuvujisha mpango serikalini. Ni ngumu kulitekeleza hilo jambo!”Tindo aliongea kwa msisitizo.

“Kwanza tunakubaliana na gharama anazozihitaji?” Amolo aliwauliza wenzake.

“Hiyo ni pesa ndogo sana aliyoihitaji. Tatizo bado lipo kwenye kuvujisha mpango.” Mhisani alijibu.

“Tumpe pesa, ila tusivujishe mpango wetu uliyotugharimu pesa nyingi kukamilika. Hatuwezi kuuza gharama zetu kirahisi namna hiyo.” Amolo nae aliongezea.

“Naona tuuvujishe mpango kwa kumruhusu yeye mwenyewe auvujishe awezavyo, lakini tusivujishe mikakati yetu hata chembe!” Kamonga alishauri. Wenzake walimtizama.

“Upo sahihi! Tumpe hiyo kazi peke yake!” Tindo aliafiki.

“Na iwe hivyo!” Amolo nae alikubali, huku akimtizama Mhisani, ambae nae alitikisa kichwa chake kukubali kilichozungumzwa.

Haraka walimuunganisha Miguu ya kuku kwa njia ya mtandao.

“Kila ulichohitaji kitafanyiwa kazi, lakini kwa shariti moja tu!” Mhisani alimwambia Zuki Gadu p.a.k Miguu ya kuku.

“Nawasikilizeni!” Miguu ya kuku aliitikia.

“Tunaomba uvujishe mpango huo kwa njia zako.”

“Itabidi muongeze dau la pesa!”

“Eeh!!”

“Yes! Kwa sababu sijui mkakati wenu ulivyo, zaidi najua mnataka plate namba tano. Sijui mlivyokuwa mmejipanga kufanikisha hilo”
“Kwa hiyo tukiongeza dau, utavujisha mpango wako na si wetu?”

“Ndivyo ilivyo!”

Sadon Brother’s, walitazamana, kisha wakaafiki kuongeza dau. Ilikuwa rahisi kuafiki kwa sababu, mpango wao ulikuwa salama kuvuja.

“Sawa, ujapohitaji usaidizi, tuko tayari wakati wowote!”
Miguu ya kuku alifikiria kidogo, kisha akasema..
“ Haina ubaya! Lakini acheni nifanye kazi yangu kadri niwezavyo. Nyie mkae kimya na angalieni yatakayokuwa yanajiri. Msiingilie lolote.”

“Haina neno! Unakaribishwa Nairobi!” Mhisani alijibu na kumkaribisha Miguu ya kuku.

“Great!” Miguu ya kuku alijibu na kutoka hewani.

Baada ya Miguu ya kuku kutoka hewani, ndugu watano walibaki peke yao. Walijadili mambo machache, kisha walisambaratika na kila mmoja, alienda kuendelea na majukumu yake ya kujimaarisha zaidi kwenye kitengo chake.

DAR ES LAAM….

Miguu ya kuku aliweka simu yake pembeni, kisha aliegemea kwenye sofa na kutazama juu. Mawazo mengi yalipita kichwani mwake. Wazo moja lilikuwa zito zaidi kuliko mawazo mengine. Lilikuwa ni wazo ambalo lilimtia hofu kubwa.

“Nimefanya kazi nyingi, lakini sijawahi kuiba benki. Na kinachonitisha zaidi ni ulinzi ulioko kwenye mabenki, hasa ndani ya benki.” Alijisemea taratibu huku akijaribu kujenga picha kichwani mwake, kwenye baadhi ya mabenki makubwa nchini Tanzania.

“Hii ni kazi ngumu sana aisee!” Alisema huku akiishika laptop yake iliyokuwa mbele yake, juu ya meza. Aliparaza kidogo na ukatokea mchoro(picha) wa jengo refu lenye ghorofa zaidi ya kumi nane. Jengo lile lilinakishiwa kwa vioo, kuanzia chini hadi juu.

“Kazi ipo duh!” Alijisemea huku mkono mmoja ukiwa kidevuni na macho yake yakiwa yametulia kulitizama jengo lile. Aliendelea kulichunguza kwa umakini sana, huku akili yake ikifanya kazi kubwa kutafakari.

“Mara zote benki huwa zinakuwa chini kabisa ya majengo marefu namna hii!” Alijisemea huku akichezesha mshale wa kuongoza, kuelekea upande wa chini wa lile jengo.

“Kama ipo huku chini, ina maana, wanamiliki basement yote na huko ndiko iliko vault ya kuhifadhia pesa na vault ya kuhifadhia hizo plate!” Alijisemea tena huku akiendelea kuizungusha picha ya jengo refu, lililopewa jina la Patrice Lumumba, huku likiwa chini ya umiliki wa Nssf.

Wakati alipokuwa akiendelea kupitia picha kadhaa za jengo lile, kuna kitu kingine aligundua na kitu kile kilimtia woga wa wazi kabisa na aliwaza kutema ndoano, endapo alichokuwa amegundua kingelikuwa sahihi.

Haraka alianza kutafuta picha za satellite ili aweze kujiridhisha na kile alichokuwa amekigundua na kukitilia wasiwasi.
Jengo la Patrice Lumumba lilikuwa ni jengo refu sana na lenye uwekezaji mkubwa jijini Nairobi. Lilikuwa ni jengo ambalo lilijengwa kwa upekee sana. Lilikuwa ni jengo refu pekee maeneo ya Upper hill, huku kukiwa hakuna jengo lingine lau lenye ghorofa moja kwenye ule mtaa.

“Kwa nini ipo hivi?” Alijiuliza huku akizidi kumakinika na picha alizokuwa anazishuhudia kupitia kompyuta mpakato iliyokuwa mbele yake. Alizidi kuyatalii kwa macho maeneo jirani na jengo la Patrice Lumumba. Hapo ndipo mwili ulimsisimka zaidi.

Kwa nini!

Kwa sababu, jengo lile lilizungukwa na maeneo nyeti sana, ambayo si rahisi mtu kuyagundua, japokuwa mengine yalifahamika kirahisi. Jengo lile lilikuwa lipo katikati ya vikosi vya jeshi na vile vya usalama wa raia.

Mashariki mwake kulikuwa na makao makuu ya jeshi la kujitegemea, huku Magharibi kwake kukiwa na kituo kikuu cha polisi cha Nairobi. Upande wa kaskazini kulikuwa na kambi ya kikosi cha anga(Moi air base), na upande wa kusini kukiwa na makao makuu ya chama tawala.

“Sasa nimeelewa ni kwa nini jengo hili limeota peke yake bila kuruhusu majengo mengine ya aina hiyo! Huu utakuwa ni mtaa wa kimkakati hapo nchini Kenya!” Alijisemea huku akijishika kichwani kwa kujikwarua. Nywele ziliwasha kwa hofu ya kile alichokuwa anakiwaza.

“Mbona hii kazi inataka kunionjesha umauti?” Aliwaza huku akianza kutafuta umuhimu wa benki ya Umoja ndani ya nchi ya Kenya.

Kulikuwa na maelezo mengi sana kuhusu benki hiyo, lakini hayakumuingia akilini, yalikuwa ni maelezo mepesi kuliko alivyotarajia.

“Maelezo haya, hayawezi kufanya nchi iweke hapo zile plate za fedha!” Alisema huku akitikisa kichwa na kuchukua simu iliyokuwa pembeni yake. Alitafuta jina alilohitaji, kisha alipiga na kuzungumza kile alichotaka kuzungumza. Lakini alichojibiwa, kilimfanya afikirie kuwapigia Sadon Brothers, na kuitema kazi aliyopewa.

Yalikuwa ni maelezo ya kuogofya kwa binadamu mwenye moyo wa nyama, ilihitaji kiumbe kisicho na damu kuvumilia na kuendelea kushikilia dili gumu namna ile. Dili lenye kuuza roho.

Miguu ya kuku alikuwa amempigia simu mtu wake wa karibu, mtu ambae hufanya nae kazi kila inapotakiwa kufanya kazi. Huyu mtu alikuwa ni kiongozi wa kanisa ndani ya jiji la Nairobi. Mtu huyo aliitwa Mchungaji Emmanuel, alikuwa na jina lake la kazi za siri alizokuwa anafanya. Alikuwa ni muuzaji wa silaha, huku akitumia mgongo wa kanisa, kama kivuli cha kuifanya biashara yake hiyo, iliyokuwa imeshamiri sana nchini Congo na sasa alikuwa Nairobi kama sehemu ya kupanua mtandao wake.

Wengi walimfahamu kwa jina la Mchungaji Emmanuel, lakini Miguu ya kuku alimfahamu na pia alipenda kumuita Bob Rando. Mtu mwenye taarifa nyeti za kila nchi anayoitembelea. Mtu ambae alikuwa ni mfanikishaji mkubwa wa mipango yake.

“Nambie Zuki!” Mchungaji Emmanuel p.a.k Bob Rando, alianza kuongea baada ya kupokea simu.

“Safi Bob!” Miguu ya kuku alijibu.

“Najua umenipigia utakuwa upo mzigoni kama kawaida yako!”

“Hakika hujakosea Bob! Niko hapo Nairobi, lakini roho inasita kuendelea na jambo langu!”

“Mh! Leo hiyo!? Kama roho inasita, achia dili. Uhai ni muhimu zaidi kwa sasa”

“Tatizo jamaa wameshafanya malipo ya awali, kitu ambacho kitanibana ni kanuni zangu, nikipokea huwa sirudishi hadi nikamilishe kazi”

“Kanuni zipo ili zivunjwe komredi”

“Hujakosea! Lakini kanuni zangu hazina kipengele cha kuvunjwa!”

“Basi, fanya hiyo kazi kama huwezi kuivunja. Vaa mabomu, ingia mzigoni!”

“Ngoja nione hadi mwisho itakuwaje”

“Naamini akili yako bado haijachoka kuvunja mitego yote! Upo wewe ni zaidi ya mwanajeshi Zuki!”

“Sawa kwa kunipa nguvu upya, naomba unipe msaada kidogo kabla sijaja Nairobi”

“Kila siku nipo kwa ajili yako! Wewe ni zaidi ya ndugu. Wakati wote nipo kwa ajili yako, hadi siku nitakapoiaga Dunia!”

“Maneno mazito sana unaongea Bob! Naomba unisaidie kudukua jengo la Patrice Lumumba na ikibidi, unipe na unyeti wa Benki ya Umoja.”

“Taarifa zake unazihitaji lini?”

“Hata kama unazo sasa hivi, nipe.”

“Nipe nusu saa!” Bob Rando alisema na kukata simu.

Miguu ya kuku alipumua peke yake, huku akiigeukia laptop yake. Kisha akaanza kusoma mikakati ya kifedha kutoka wizara ya fedha ya Kenya. Aliamua kusoma mikakati hiyo, kwa kuwa alijua kuna kitu kitakuwa kimepangwa na nchi ya Kenya kuhusu mipango fedha.

“Plate namba tano, haiwezi kuwa na umuhimu kiasi hicho kama ingelikuwa haina jambo nyuma yake. Lazima kuna kitu kinachowasukuma hawa jamaa kuiba hii plate!” Alijisemea huku vidole vyake vikicheza kwa kasi kubwa na macho yake yakiwa makini, kutizama kilichokuwa kinapita kwenye kompyuta yake.

Wakati alipokuwa akizipita ripoti kadhaa, hatimae alikutana na ripoti ambayo iliamsha hisia fulani kichwani kwake. Ripoti ilitolewa na katibu wa wizara, ripoti ilihusu mpango wa serikali kuchapa shilingi mpya, ambayo itaziba mianya ya wahujumu uchumi ambao wameondoa pesa kwenye mzunguko na kupelekea kuwe na hali ngumu ya uchumi. Ripoti ile iliendelea kubainisha kuwa; lengo la kufanya vile ni, kuwafanya watu walioondoa pesa kwenye mzunguko, kurejesha pesa hizo ili kuendana na matumizi mapya ya shilingi mpya.

“Sasa hiyo plate na hili jambo vinaingilianaje?” Alijiuliza huku akiwa ameganda na asijue la kufanya.

“Hawa jamaa wanataka kuihujumu nchi yao bila shaka!” Alijisemea huku akiendelea kuperuzi habari nyingine.

“Nchi za wenzetu huko, haya makundi ya kihuni huwa yanamiliki uchumi wa nchi, yawezekana na hawa wanataka kulitenda hilo hilo nchini mwao!” Alijiwazia.

“Lakini hainihusu! Kazi yangu ni kutekeleza tu!” Alisema kwa sauti huku akiichukua simu yake iliyokuwa inaita pembeni yake.

“Unauhakika, unataka kufanya hili jambo?” Bob alianza kwa swali baada ya mwenzake kupokea simu.

“Ni lazima nilifanye komredi!”

“Sasa sikia; ile Benki ya Umoja ni benki ya biashara, lakini ipo kwenye mikono ya serikali kwa asilimia zote. Yaani ile pale ni tawi la benki kuu, japo wananchi hawajui lolote, zaidi wanajua ni benki ya kibiashara tu. Lakini kikubwa zaidi, ile benki ndiyo yenye hazina yote ya nchi. Ina maana kwamba; hata vipande vya madini vimehifadhiwa pale ina maana, ile ndiyo roho ya nchi. Na kulithibitisha hilo, lile jengo limejengwa kwenda chini ghorofa mbili, na huko ndiko mzigo unaoutaka umehifadhiwa. Lakini…”

“Lakini nini Bob!”

“Huko chini, kuna ofisi za Usalama wa nchi na ina maana, kunalindwa saa ishirini na nne tena ulinzi mkali kuliko unavyodhani.

“Duh! Una maanisha, vault ipo kwenye hizo ghorofa za chini?”

“Exactly! Mzigo upo huko.”

“Duh!”

“Lakini ngoja nikusaidie jambo moja.”

“Lipi hilo?”

“Lile ni jengo la kibiashara na huwa kunapangishwa kwa mtu yeyote mwenye kampuni kubwa. Ukishapanga, utaelekezwa kuitumia benki ya umoja kufanya kila muamala wako. Ikiwa na maana, unakuwa chini ya uangalizi bila wewe kujua.”

“Kwa hiyo una maana nipange huko juu, kisha nifanye uhuni wangu kirahisi?”

“Hakika umewaza vema!”

“Mimi naona haijakaa sawa! Unaonaje nikitafuta ajira kwenye moja ya kampuni zilizopanga humo?”

“Yes!” Bob aliitikia kwa furaha, jambo lililomshangaza Zuki p.a.k Miguu ya kuku.

“Sikia Zuki, kwenye ghorofa ya tatu, kuna kampuni ya ulinzi ya Dop. Kampuni ile huajiri watu mbalimbali wenye uzoefu na wenye ujuzi mbalimbali. Kampuni ile ndiyo inayosafirisha pesa zote za Umoja benki, lakini pia ni kampuni ambayo huajiri mafundi umeme na watu wa huduma ya kwanza. Hivyo ni wewe na uamuzi wako, uwe fundi umeme, au uwe mtoa huduma ya kwanza na uokozi kwa dharura!”

“Naweza kuwa yeyote kati ya hivyo, lakini nafasi ya kupata kazi ipo? Maana kwa harakaharaka naona hiyo ni kampuni ya wanausalama wenyewe”

“Wewe usiwaze, mathalani wamekubali kupokea mtu yeyote ili wafiche ukweli wao, utapata kazi kupitia mimi. Mimi ndiye Mchungaji Emmanuel bwana!” Bob Rando alimalizia kwa kucheka kwa sauti kubwa.

“Haya poa bwana Pastor!” Miguu ya kuku alisema na kukata simu huku akitabasamu.

“Huwa sipendi sana kuzunguka na kazi moja, kwa muda mrefu, ila hii inaonekana itanilia wakati wangu kuliko nilivyodhani” Alijisemea huku akinyanyuka na kuelekea chumbani kwake.

NAIROBI, KENYA.

Zilikuwa zimepita siku tatu tangu Zuki Gadu p.a.k Miguu ya kuku, aingie jijini Nairobi. Alifikia kwenye hoteli ya Pama. Hoteli ambayo ilikuwa umbali mfupi kutoka lilipokuwa jengo la Patrice Lumumba. Katika siku zote hizo ambazo alikuwa kwenye hiyo hoteli, alikuwa ametumia muda mrefu kulichunguza vizuri jengo lile refu. Alizingatia zaidi ulinzi uliyokuwa upande wa chini ‘Basement’.

Kwa haraka aligundua kulikuwa na walinzi saba ambao walikuwa wanalinda pale benki. Walinzi wawili kati ya hao saba, walikuwa wanalinda eneo la kuegesha magari, walinzi wengine wawili, walikuwa wanalinda upande wa nje ambao ulikuwa na ngazi za kuelekea kwenye ghorofa za juu, bila kupita basement, ambako kulimilikiwa na umoja benki. Walinzi wengine wawili, walikuwa wanalinda eneo la mlango na mlinzi mmoja, alikuwa ndani ya benki.

“Ulinzi wa hapa si mchezo aisee!” Alijisemea huku akivuta kiti na kukaa kwenye meza iliyokuwa ndani ya mgahawa, uliyokuwa mita chache kutoka lilipokuwa jengo la Patrice Lumumba.

Dakika moja baadae, mhudumu alimfuata na kumpa orodha ya vyakula vilivyokuwa vinapatikana wakati huo.
Miguu ya kuku alichagua supu ya samaki na chapati tano. Mhudumu aliondoka kwenda upande wa jikoni, kuleta alichoagizwa.

Wakati mhudumu anaondoka, Miguu ya kuku yeye, aliamua kuendelea kufanya jambo lililokuwa limempeleka pale. Alizungusha macho yake ndani ya ule mgahawa, mithili ya mtu aliyekuwa anamtafuta mgoni wake.

Watu wengi waliokuwa pale ndani, walikuwa bize kushugulikia vyakula vyao huku baadhi wakionekana kuzama kwenye mazungumzo na wengine wakiperuzi kwenye simu janja zao. Lengo lake halikuwa kuwatizama watu hao, bali, alihitaji kuwaona watu ambao walikuwa ni zaidi ya wateja kwenye ule mgahawa.

Licha ya jicho lake kumfikia kila mmoja lakini hakuweza kumtilia shaka yeyote.

“Haiwezi kuwa rahisi namna hiyo. Hapa ni lazima kutakuwa watu wanaotizama nyendo za wapita njia.” Alijiwazia huku akiendelea kuzungusha kichwa chake kila pande ya ule mgahawa.

Wakati akiwa kwenye upelelezi; mhudumu alirejea akiwa na sinia la kiamsha kinywa alichoagizwa.

“Karibu!” Mhudumu alimwambia huku tabasamu la kheri likiwa limeupamba uso wake.

“Ahsante sana mrembo!” Miguu ya kuku alimjibu huku akiinuka na kwenda kunawa.

Alipomaliaza, alirejea kwenye na kuanza kufakamia chakula kilichokuwa mezani. Hakuhitaji kutumia dakika nyingi kulijaza tumbo, alihitaji kuwahi kufanya jambo moja zaidi ili kufanikisha kile kilichikuwa kimempeleka pale.

Dakika tano zilimtosha kumaliza supu na chapati zake tano, kisha alienda kunawa na kurejea alipokuwa. Baada ya kuketi, alizungusha macho yake pale mgahawani. Aliporidhika na utulivu uliokuwepo, alitoa mkebe kwenye mfuko wa suruali yake. Mkebe ule ulikuwa umehifadhi paketi mbili za sigara, aina ya safari.

Alitoa paketi moja na kuifungua, kisha alichomoa pisi moja ya sigara na kuibana kwenye vidole vyake vya mkono wa kulia na kurejea kuifunga paketi kisha, aliirejesha kwenye mkebe na kurudisha mfukoni. Tofauti na mawazo ya wengi kuhisi alitoa sigara pekee, yeye alikuwa ametoa na kitu kingine cha ziada. Alikuwa ametoa kitu chenye ufanano na mdudu vule.

Alichukua sigara na kuiweka kwenye mfuko wa shati, huku macho ya watu waliokuwa wamechukizwa na utoaji wa sigara eneo kama lile, wakimpotezea baada ya kuona hana mpango wa kuivuta. Lakini jambo moja hawakuelewa; wakati alipokuwa akiweka sigara kwenye mfuko, ni wakati huohuo alipodondosha kile alichokuwa amekichukua kwenye paketi ya sigara, kwa uficho.

Baada ya kuhakikisha kimetua chini kwa namna aliyokuwa ameikusudia, alitoa simu yake mfukoni na kuanza kuperuzi taratibu, huku mkono wake mmoja ukitoa pesa na kumpa mhudumu aliyekuwa amesimama kando yake, akingoja malipo ya huduma aliyotoa.

Alilipa pesa iliyohitaji, kisha alirejesha macho yake kwenye simu yake huku masikio yake yakizisikia hatua za mhudumu akiondoka mbali nae.
Dakika moja baada ya kuwa bize na simu yake, kile alichokidondosha chini kilipata uhai na kuanza kujongea ndani ya mgahawa. Kilitembea kila sehemu iliyokusudiwa kisha kilirejea pale alipokuwa Miguu ya kuku. Aliinama na kukiokota kisha alikiweka mfukoni mwake na kunyanyuka kuelekea kwenye hoteli aliyofikia.

Alipofika ndani ya chumba alicholipia, alitoa simu yake kisha alimalizia kwa kukitoa kile kidubwasha chenye umbo ufanano na mdudu vule. Alibofya simu yake mara kadhaa na kile kidubwasha, kilianza kumweka. Kilimweka mara saba na kuzima kabisa.

Miguu ya kuku alipumua kwa nguvu, huku akikuna kidevu chake bila kutarajia.

“Aisee! Hapo mgahawani pekee, kuna watu saba wenye silaha! Hii ni zaidi ya Benki kwa kweli!” Alijisemea kwa sauti huku macho yake akiwa ameyaelekeza kwenye kile kidubwasha kilichokuwa kitandani. Kilikuwa ni kifaa maalumu cha kuhisi silaha iliyofichwa, huhesabu idadi ya silaha na pia kilikuwa na uwezo wa kutoa taarifa endapo kungelikuwa na mlipuko maeneo ya karibu. Miguu ya kuku alipewa kifaa kile wakati alipokodiwa kufanya misheni huko South Afrika. Misheni ambayo ilimkutanisha na jasusi wa Israel aliyemzawadia kifaa kile na vingine vingi vya aina ile.

“Kuiba ndani ya hii Benki kunahitaji umakini sana, la sivyo nitaingia kaburini kabla ya wakati wangu.” Alijisemea huku akikunjua laptop yake na kuiwasha, kisha alianza kusoma vitu kadhaa kuhusu majengo ya Benki na namna yanavyohifadhi mali zake.

Katika pekuapekua zake, aligundua mara nyingi kila benki huwa inakuwa na sehemu maalumu za kuhifadhia ambazo huitwa ‘Vault',sehemu hizi huwa zinakuwa na ulinzi wa kieletroniki. Ukiachilia mbali ulinzi wa aina hiyo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom