Riwaya: Ngoma Ngumu

Kudo

JF-Expert Member
Nov 2, 2017
1,809
6,081
RIWAYA; NGOMA NGUMU
NA: BAHATI K MWAMBA
SIMU: 0758573660/0624155629

NAIROBI, KENYA…

Kulikuwa na mabishano makubwa ndani ya nyumba moja ya kifahari, katikati ya jiji la Nairobi. Kulikuwa na familia inayoongozwa kwa misingi ya kihuni na ukorofi uliyotukuka. Familia ambayo iliamua kuliteka jiji la Nairobi na kuliweka chini ya himaya yake; rushwa ikiwa ni silaha yao kubwa, pale ambapo vyombo vya usalama huonekana kuingilia mipango yao.

Familia hiyo ilikuwa inaongozwa na vijana watano waliorithi mikoba ya mzee wao, ambae alikuwa anasota gerezani. Vijana nao waliamua kujigawa kiuongozi, kulingana na umri wao; yaani mwenye uongozi wa juu alikuwa ni yule wa kwanza kuzaliwa, kisha uongozi ulifuata kwa waliofuatia.

Wakati wote huwa wanashauriana, lakini mwenye maamuzi ya mwisho ni kaka yao, ambae walipenda kumuita ‘MHISANI’ yaani mwenye nguvu ya kutenda.

Tofauti na siku zote ambapo maamuzi hutolewa kulingana na daraja la umri na, maamuzi ya mwisho hayapingwi, lakini siku hii maelewano yalikosekana ndani ya nyumba. Maelewano ambayo yalitibuliwa na kijana mmoja tu, huku wengine wanne wakiwa wamekubaliana cha kufanya. Wenzake walipojaribu kumsihi asiwe mbishi, alitishia kujiondoa kwenye hilo kundi la kihuni(genge), huku akiwaahidi kuwa, ataitawala Nairobi peke yake na wasije kujaribu kuingia kwenye mgogoro nae, watajuta.

Nyumba ilizizima, ubaridi ukawaingia wenzake. Walimfahamu vema mdogo wao wa mwisho, alikuwa ni mtu wa mipango isiyoshindwa, lakini waliogopa zaidi kwa sababu, ni yeye ndiye aliyekuwa kiongozi wa vijana wote waliokuwa wanawafanyia kazi. Hiyo ilimaanisha, wahuni wote wa Nairobi, walimsikiliza yeye tu na, hata makundi mengine ambayo yaliutaka utawala wa Nairobi, walishindwa kutawala kwa sababu yake. Vijana walimtii na walimheshimu, pia alikuwa amepandikiza vijana wake wengi kwenye makundi mengine na kila kilichopangwa huko, yeye alikijua na kukifanyia kazi kabla, hakijaleta madhara.

Hilo liliwatisha ndugu zake ambao wao walikuwa wanaongoza vitengo vingine kama vile; kukusanya madeni na kukopesha watu, kuingiza na kutoa mizigo ya magendo, kusimamia pesa inayoingizwa na kutolewa kwenye kundi na vitengo vingine vilivyotosha kuongozwa na watu watano.

Iliwatisha zaidi kwa sababu jambo walilokuwa wanabishania, walikuwa wamelipanga na kulifuatilia zaidi ya miaka sita, hivyo mmoja kutaka kujiondoa ilimaanisha, watarudi nyuma tena kwenye utekelezaji.

“Ok! Ugomvi uishe bwana mdogo, hatuna haja ya kugombana huku tukiwa na lengo moja sote. Kaka zako tunakusikiliza, lakini leo ni mara ya mwisho kukubali kukusikiliza, siku nyingine inabidi usikilize amri ya waliokutangulia. Hii si familia ya kambare eti kila mmoja anandevu.” Kiongozi wa familia aliongea kwa mamlaka, huku akiwatupia macho wenzake ambao nao walikuwa wanamtazama mdogo wao kwa hila. Haijawahi kutokea amri ya mdogo ikafuatwa na wakubwa, lakini siku hiyo ilibidi iwe.

“Sina kingine ninachoweza kusema zaidi ya kile ninachokisimamia..” Alinyamaza kidogo na kuwatazama ndugu zake ambao walikuwa kimya wakimsikiliza.

“Vijana wangu hawataweza kuifanya kazi yenu.” Alinyamaza tena na alipotaka kuendelea kuzungumza, alikatishwa na kaka yake mkubwa kabisa, waliemwita Mhisani.

“Kwa nini unasema hawawezi wakati mna kila kitu? Mnasilaha, pesa na ushawishi! Sasa kwa nini kazi hii kwenu ionekane ngumu wakati hadi ramani imepatikana na imebaki kufanyiwa kazi tu?”

“Silaha, pesa na nguvu si mafanikio. Ili tufanikiwe katika hili, tunahitaji kutumia akili nyingi sana wakati wa utekelezaji, pia usiri ikiwa ni nguzo muhimu sana kwenye suala hili”

“Kwa hiyo una maaanisha, kundi lako lote halina watu wenye akili? Litakuwa ni kundi ambalo halina siri?”

“Akili ni jambo moja, usiri ni jambo lingine. Kumbukeni tunawatu wetu na maadaui tunaohumohumo.”
“Kwa hiyo unataka tufanye nini?”

“Hii kazi apewe mtu mwingine kabisa, sisi tubaki wafuatiliaji na watoa msaada kila inapohitajika!” Bwana mdogo alizungumza, lakini wenzake walibaki kumshangaa na wasielewe. Aliendelea kuongea.

“Kwa jinsi jengo lilivyo, inahitaji itumike nguvu kubwa sana ili kufanikisha tunachokitaka, pia itatuchukua muda mrefu sana kupata tunachokitaka na inawezekana kabisa tusikipate kirahisi na tukaishia kurushiana risasi na maofisa wa jeshi. Tusipokuwa makini, tutamfuata Baba Gerezani.”

Ukimya ukapita, kisha mmoja aliyeitwa Amolo aliuliza…

“Kwa hiyo tufanye nini? Kwa maana naona unazunguka tu!”

Mdogo wao aliyeitwa Kamonga, alitoa picha tatu na kuzirusha kwenye meza, kisha alikaa kimya bila kusema kitu, wenzake walibaki wamezubaa na wasijue alimaanisha nini.

Alipoona hawamuelewi, aliwambia..

“Tizameni hizo picha kisha tujadili kinachotakiwa kufanywa kwenye mpango wetu.”

Walizichukua zile picha na kuzitizama kwa umakini mkubwa, kila picha ikiwa imeandikwa jina la mhusika na nchi anayopatikana.

“Una maana gani kutupa picha hizi?” Mhisani alimuuliza.

“Nina maanisha mmoja kati ya hao jamaa anaweza kuifanya hiyo kazi vizuri bila kelele na ikafanikiwa, hivyo tuanze kuchagua na sifa zao nadhani mnazifahamu, maana si wageni kwetu” Kamonga alifafanua.

“Una maanisha kazi hiyo ifanywe na mtu mmoja!?” Mhisani aliuliza kwa mshangao.

“Ili ikamilike ni lazima ifanywe na kichwa chenye kuwaza vema, lakini tukiifanya kwa kutumia nguvu, hakuna tutakachoambulia kabisa!”

“Duh! Ni vema tuachane na hili jambo!”

“Kama mnataka kuachana nalo, mimi nitalifanya peke yangu na nisiulizwe lolote.”

“Bwana mdogo acha jeuri! Hii ni kwa masilahi yetu wote na kiburi si uungwana hata chembe!” Mhisani alionya.

“Let’s make it brothers!” Amolo aliingilia kati huku akijiweka vema kwenye kiti, kisha aliwatizama wenzake wote ambao walimpa usikivu.

“Hili jambo tulifanye kwa misingi ya sheria zetu!” Alinyamaza kidogo huku akimtupia jicho la husda mdogo wake, Kamonga. Kisha aliendelea.

“Sheria zipo wazi kabisa; endapo jambo litafanywa kwa kulazimishwa na mmoja miongoni mwetu, adhabu yake huwa ni kifo mbele ya jopo letu.” Alinyamaza baada ya kuona Kamonga alitaka kukatisha maelezo yake, alimruhusu.

“Lakini kanuni hiyo inaruhusu jambo hilo kufanyika endapo lililolazimishwa, halitofanikiwa.” Kamonga alifafanua kanuni hiyo.
“Upo sahihi kabisa!” Amolo aliafiki.

“Basi tukubaliane kuteua mmoja kati ya hao jamaa, aweze kutufanyia kazi yetu kwa ufanisi unaohitajika.”

“Basi sawa! Mimi nampendekeza huyo jamaa mwenye sare ya jeshi la polisi.” Amolo alisema huku akiitupa mezani picha aliyokuwa ameshika. Wenzake waliichukua na kuipitisha machoni mwao kwa mtindo wa kupokezana.

“Mh! Sajenti Nyau!?” Tindo ambaye alikuwa kimya muda mrefu, aliuliza kwa mshangao huku akiwatizama ndugu zake, ambao na wao walikuwa wanamtupia jicho la kulikoni. Tindo aliendelea kuzungumza, baada ya wenzake kukaa kimya.

“Huyu jamaa ni ofisa wa jeshi la polisi hapa Kenya, japo hutusaidia kazi zetu kwa ufasaha, lakini sina hakika kama tunahitaji kumkabidhi kazi kubwa namna hii.”

“Kwa nini?” Mhisani aliuliza.

“Kwa sababu ni mtu anaeongozwa na tamaa ya pesa. Anaweza kuuza hata huu mpango kwa wabaya wetu” Tindo alijibu swali aliloulizwa.

“Kwa hiyo unamaanisha tuachane nae?” Amolo aliuliza.

“Kama mtaniunga mkono, tuachane nae!”

“Mimi sikuungi mkono!” Mhisani aliingilia kati. Wenzake walibaki kumtazama, wakingoja maelekezo zaidi.

“Sajenti Nyau ni fundi haswaa! Pia ni mkenya mwenzetu na anatufahamu vema kabisa na hajawahi kutuchoma serikalini. Nikimsifia, sifa zake zitajaa hapa na itoshe kusema tu, Sajenti Nyau anatosha kabisa. Hao mamluki wa nchi za nje, hawatufai kwa sasa!” Alifafanua.

“Hata Mimi naona Sajenti Nyau hatoshi kufanya kazi hii. Hana sifa. Naomba ikipendeza, apewe Gomba, huyo jamaa wa Uganda. Ni profesheno. Anaweza kutuletea hiyo plate.” Atumba, ambae alikuwa ni mkubwa akimfuata Mhisani, alisema huku akiitupa picha ya Gomba mezani. Wenzake walimtazama, walihitaji kumsikiliza zaidi. Aliendelea kusema.

“Kumbukeni tunaenda kuiba Benki. Na hatuibi pesa, tunaiba plate namba tano. Na kila mtu anajua hiyo plate ilivyo na umuhimu na namna inavyolindwa. Sasa mtu kama Nyau, ataharibu kabisa, matokeo yake tutaikosa na mipango yetu ya muda mrefu, itakuwa kazi bure.”

“Kwa hiyo unataka kusema Gomba anazosifa za kuweza kuiba hiyo plate?” Mhisani alimuuliza.

“Hakika anaweza, anazosifa zote. Akili,nguvu, ufundi ni miongoni mwa sifa kubwa za Gomba.”

“Vipi kuhusu tamaa, hawezi kutudabo kurosi kweli?”

“Sijawahi kusikia akituhumiwa kwa hilo jambo.”

“Kwa hiyo huna hakika?”

“Hapo kweli sina hakika!”

“Basi tupige kura!”
Wote wanne walikubaliana kupiga kura, lakini wa tano ambae ndiye wa mwisho, alikuwa kimya akiwatizama. Walipiga kura na matokeo yakawa; Nyau kura mbili na Gomba kura mbili, huku Kamonga akiwa hajashiriki kupiga kura, ikatakiwa apige kura, ili kuamua kati ya Gomba au Nyau, ni yupi ambae angelipewa kazi ya kuiba plate namba tano, kwenye Benki ya Umoja.

“Tunaingoja kura yako bwana mdogo!” Mhisani alifoka, huku akimtizama Kamonga kwa macho makali.

“Hao mliowachagua si chaguo langu, bali chaguo langu ni huyu hapa!” Alisema huku akiitupa picha mezani, wenzake waliitupia macho, kisha walimtizama.

“Zuki Gadu!?” Amolo aliuliza kwa mshangao.

“Yes, huyohuyo. Huyo ndiye anaeweza kuifanya kazi hii. Mwenyewe hupenda kuijiita Miguu ya kuku, akipita haachi nyayo, wala sauti ya vishindo vyake, haisikiki” Kamonga alisema huku akisimama na kuzungusha shingo yake, mbele ya kaka zake.
“Wewe ulomjuaje huyu jamaa?” Atumba alimuuliza.

“Miguu ya kuku aliwahi kuwa mlinzi wa Baba, hivyo anatufahamu vema, pia anauwezo mkubwa sana wa kufanikisha mambo yake. Anafaa kwa kazi hii” Kamonga alijibu kwa uhakika.

“Sasa mlinzi binafsi ataweza kweli kashikashi za serikali? Unatushangaza bwana mdogo” Mhisani aliongea bila kuficha wasiwasi wake.

Ulikuwa mtihani mkubwa, majina matatu mezani, lakini lilihitajika jina moja tu ili kazi ifanyike. Kazi nzito na ya hatari. Ilihitajika plate namba tano kutoka Benki ya Umoja, Benki yenye ulinzi kuliko Benki zote ndani ya jiji la Nairobi.

Hakika ilikuwa ngoma ngumu
...
Mwandishi; Bahati Mwamba.
Simu; 0656741439/0758573660/0624155629.

ENDELEA KUWA NAMI
 
RIWAYA; NGOMA NGUMU.

NA; BAHATI K MWAMBA.


SEHEMU YA PILI.

, walihitaji kumsikiliza zaidi. Aliendelea kusema.

“Kumbukeni tunaenda kuiba Benki. Na hatuibi pesa, tunaiba plate namba tano. Na kila mtu anajua hiyo plate ilivyo na umuhimu na namna inavyolindwa. Sasa mtu kama Nyau, ataharibu kabisa, matokeo yake tutaikosa na mipango yetu ya muda mrefu, itakuwa kazi bure.”

“Kwa hiyo unataka kusema Gomba anazosifa za kuweza kuiba hiyo plate?” Mhisani alimuuliza.

“Hakika anaweza, anazosifa zote. Akili,nguvu, ufundi ni miongoni mwa sifa kubwa za Gomba.”

“Vipi kuhusu tamaa, hawezi kutudabo kurosi kweli?”

“Sijawahi kusikia akituhumiwa kwa hilo jambo.”

“Kwa hiyo huna hakika?”

“Hapo kweli sina hakika!”

“Basi tupige kura!”
Wote wanne walikubaliana kupiga kura, lakini wa tano ambae ndiye wa mwisho, alikuwa kimya akiwatizama. Walipiga kura na matokeo yakawa; Nyau kura mbili na Gomba kura mbili, huku Kamonga akiwa hajashiriki kupiga kura, ikatakiwa apige kura, ili kuamua kati ya Gomba au Nyau, ni yupi ambae angelipewa kazi ya kuiba plate namba tano, kwenye Benki ya Umoja.

“Tunaingoja kura yako bwana mdogo!” Mhisani alifoka, huku akimtizama Kamonga kwa macho makali.

“Hao mliowachagua si chaguo langu, bali chaguo langu ni huyu hapa!” Alisema huku akiitupa picha mezani, wenzake waliitupia macho, kisha walimtizama.

“Zuki Gadu!?” Amolo aliuliza kwa mshangao.

“Yes, huyohuyo. Huyo ndiye anaeweza kuifanya kazi hii. Mwenyewe hupenda kuijiita Miguu ya kuku, akipita haachi nyayo, wala sauti ya vishindo vyake, haisikiki” Kamonga alisema huku akisimama na kuzungusha shingo yake, mbele ya kaka zake.
“Wewe ulimjuaje huyu jamaa?” Atumba alimuuliza.

“Miguu ya kuku aliwahi kuwa mlinzi wa Baba, hivyo anatufahamu vema, pia anauwezo mkubwa sana wa kufanikisha mambo yake. Anafaa kwa kazi hii” Kamonga alijibu kwa uhakika.

“Sasa mlinzi binafsi ataweza kweli kashikashi za serikali? Unatushangaza bwana mdogo” Mhisani aliongea bila kuficha wasiwasi wake.

Ulikuwa mtihani mkubwa, majina matatu mezani, lakini lilihitajika jina moja tu ili kazi ifanyike. Kazi nzito na ya hatari. Ilihitajika plate namba tano kutoka Benki ya Umoja, Benki yenye ulinzi kuliko Benki zote ndani ya jiji la Nairobi.

“Awezaye kuifanya kazi hii ni Miguu ya kuku, achaneni na Sajenti Nyau na huyo jamaa mwingine.” Kamonga aliendelea kuwashawishi wenzake.

“OK! Tuamue kwa kusema, wote ni wazuri. Je, tutampa vipi mzuri zaidi?” Amolo aliamua kufupisha mjadala.

“Nadhani tuyachambue maongezi yao. Mtu makini hupimwa kwa weledi wa ulimi wake.” Tindo alishauri.

“Inaweza kuwa njia nzuri, lakini ni kama tunacheza kamari tu.” Amolo alionesha wasiwasi wa njia iliyoshauriwa.

“Ndugu zangu, kama tunautaka utajiri, ni vema tukamtumia Miguu ya kuku. Hawa wengine nadhani wanafahamika vema kabisa, sioni umuhimu wa kuwapigia simu. Tunaweza kuwapigia, ikawa ni njia moja wapo ya kufanya tukafuatiliwa tunachopanga kufanya hapa Nairobi. Hili jambo libaki kuwa siri ya familia tu.” Kamonga aliongea kwa sauti, huku akipigapiga meza kuonesha msisitizo wake.

Ukimya ukashika hatamu, kila mmoja aliwaza lake. Ilikuwa ni ngumu kumwamini mtu mmoja, kufanya kazi ngumu na ya hatari namna ile. Ilikuwa ni vema waifanye wenyewe, kwa sababu walikuwa na; pesa, nguvu kazi ya vijana wao watiifu pia, walikuwa na vifaa vyote ambavyo vingelihitajika kukamilisha kazi yao.

Hili jambo la mpango wao uliyowagarimu muda na pesa nyingi, kufanywa na mtu mmoja, huku wao wakiwa washuhudiaji, lilikuwa linawaungurumisha matumbo.

“Anyway, tumpe kazi Miguu ya kuku. Akifeli ni rahisi sisi kumkataa na kwa nguvu tulionayo, ni rahisi kumkataa na tukaendelea na mpango wetu kwa njia nyingine” Mhisani aliamua kumaliza mjadala kwa kukubaliana na matakwa ya mdogo wake wa mwisho, ambae alipendekeza namna ya kukamilisha wizi ndani ya benki ya umoja.

“Lete namba zake za simu tumpigie” Amolo alisema huku akitoa simu yake mfukoni.

“Huyu jamaa mambo ya kazi huwa anatumia email ama Threema, simu ni kwa maongezi ya kawaida tu.” Kamonga alimwelekeza kaka yake.

“Duh!” Amolo aliguna huku akifungua viboksi vya simu yake, kisha alitafuta kikasha cha email na kukifungua na kuingiza anuani aliyotajiwa, kisha akatuma ujumbe mfupi uliyosomeka; ‘NEEDED!’

Alitulia kidogo na kupokea ujumbe kutoka kwa Miguu ya kuku. Ulisomeka; ‘SYMPATHY or ELSE?’

Amolo alimgeukia Kamonga na kumwonesha ule ujumbe.

“Mjibu Sympathy” Kamonga alimwelekeza.

Haraka Amolo alituma majibu kama alivyoelekezwa. Sekunde chache ujumbe ulijibiwa kwa swali.

‘5W?’ Ujumbe ulisomwa kwa sauti. Wote hawakuelewa alimaanisha nini, isipokuwa Kamonga pekee ndiye aliyetambua ilikuwa na maana gani, haraka aliamua kuwaelekeza wenzake kwa namna alivyoelewa.

“Hiyo inatumiwa na wanausalama kumhoji mtuhumiwa ama shahidi, pia ni somo kwa waandishi wa habari, linalowaongoza kupembua habari zao.” Alinyamaza kidogo na kisha aliendelea.

“….5W hutumika kuhoji, yaani husimama badala ya maneno; When, Where, Why… Hivyo nadhani anahitaji kujua sisi ni nani, tuko wapi, kwa nini tunamhitaji.”

“Kwa hiyo tumjibu vipi sasa!”

“Jitambulishe!”

Amolo aliingia kikashani na kumwandikia ujumbe uliyosomeka hivi; ‘SADON BROTHERS!’

Sekunde chache baadae, ujumbe wao ulijibiwa kwa maneno machache tu.

‘THREEMA,UXC!’ Amolo aliusoma tena kwa sauti, ni kama alihitaji kufafanuliwa ulivyomaanishwa ujumbe ule.

“Anahitaji kupigiwa kupitia threema!” Kamonga alisema huku akichukua simu yake na kuingunisha na runinga kubwa iliyokuwa ukutani, kisha alipekua kikasha cha Threema kwenye simu yake na kupiga kwa njia ya mtandao. Iliita kidogo na kupokelewa upande wa pili na sura ya mtu aliyekuwa amekaa sofani, ilijaa kwenye runinga kubwa iliyokuwa kwenye kile chumba kilichokuwa kimebeba ndugu watano.
Walikuwa wanaonana mubashara na Zuki Gadu p.a.k Miguu ya Kuku.

“Kuna kazi ya kufanya ndani ya siku tatu zijazo.” Mhisani alianza kuzungumza.

“Kazi hiyo ni nyepesi, lakini ni ngumu vilevile, kwa sababu inahitajika kumwaga damu ikibidi, ama kutumia akili nyingi ili kuweza kuifanikisha.” Alimeza mate na kuendelea.

“Ndani ya Benki ya Umoja, kuna plate za kutengeneza pesa. Zipo plate tisa, ila sisi tunahitaji plate moja tu, ambayo ni plate namba tano.”

“Umoja Bank, plate namba tano!” Miguu ya kuku alisema huku akichezea kompyuta yake, iliyokuwa mapajani. Punde akageuka na kusema.

“Nitahitaji kiasi cha milioni mia nne, kukamilisha kazi hii!”

Sadon Brothers walitazamana kwa mshangao, hawakuwa wametarajia kutajiwa kiasi kikubwa cha pesa kwa wizi pekee.

“Mbona pesa nyingi sana bwana!” Tido alisema kwa kuhamaki.

“Ni kawaida yangu kutoza pesa hiyo kulingana na uzito wa kazi, hivyo ni juu yako; kukubali ama kukataa na kuzima dili”

“Duh! Hii kiboko!!”

“Ninazo dakika mbili za kuzungumza na nyinyi, hivyo ni vema mkajielekeza kwenye mada.” Aliwambia bila kupepesa macho yake.

“Lakini unahakika utaweza kufanya kazi hiyo!?” Mhisani alimuuliza.

“Nipe kazi, nikishindwa itafahamika. Unachotakiwa kufanya ni, kuniwekea nusu ya malipo, kisha nusu utamalizia nikikamilisha kazi yako”

“Ok! Unakaribishwa Nairobi!”

“Ahsanteni! Lakini nina ombi moja!”

“Tunakusikiliza bwana Zuki!”

“Naomba nusu ya mpango wenu, muuvujishe bila kusema mnapotaka kutenda tukio na tukio la aina gani.”

“Heh!!” Jamaa walipigwa na mshangao. Wao walitegemea kufanya kwa siri, lakini sasa wanaambiwa wavujishe mpango huo.

Mtihani!!
 
Hii kweli ni ngoma ngumu boss Kudo na mitaa ya Nairobi inaenda kushangazwa na kiumbe anaetembea bila kuacha alama "Miguu ya Kuku".
 
Miguu ya kokoriko a.k.a Jogoo wa Congo hapa tena, Ikiwa ni katika Viunga vya Jiji la Nairobii
 
RIWAYA; NGOMA NGUMU.

NA; BAHATI K MWAMBA.


SEHEMU YA TATU.



Sadon Brothers walitazamana kwa mshangao, hawakuwa wametarajia kutajiwa kiasi kikubwa cha pesa kwa wizi pekee.

“Mbona pesa nyingi sana bwana!” Tido alisema kwa kuhamaki.

“Ni kawaida yangu kutoza pesa hiyo kulingana na uzito wa kazi, hivyo ni juu yako; kukubali ama kukataa na kuzima dili”

“Duh! Hii kiboko!!”

“Ninazo dakika mbili za kuzungumza na nyinyi, hivyo ni vema mkajielekeza kwenye mada.” Aliwambia bila kupepesa macho yake.

“Lakini unahakika utaweza kufanya kazi hiyo!?” Mhisani alimuuliza.

“Nipe kazi, nikishindwa itafahamika. Unachotakiwa kufanya ni, kuniwekea nusu ya malipo, kisha nusu utamalizia nikikamilisha kazi yako”

“Ok! Unakaribishwa Nairobi!”

“Ahsanteni! Lakini nina ombi moja!”

“Tunakusikiliza bwana Zuki!”

“Naomba nusu ya mpango wenu, muuvujishe bila kusema mnapotaka kutenda tukio na tukio la aina gani.”

“Heh!!” Jamaa walipigwa na mshangao. Wao walitegemea kufanya kwa siri, lakini sasa wanaambiwa wavujishe mpango huo.

Mtihani!!

“Mbona kama unataka tufanye kile ambacho hatukufikiria? Pia unataka kufanya kazi hii ionekane ngumu kupindukia!” Amolo alisema huku akijikuna kichwa chake kwa hofu ya kilichosemwa na Miguu ya kuku.

“Hakuna namna! Itabidi iwe hivyo ndugu zangu. Wizi wa benki ni tofauti na wizi mwingine. Akili yako ndiyo ushindi wako!” Zuki Gadu p.a.k Miguu ya kuku, aliendelea kushawishi.

“Kwa nini unataka mpango uvuje?” Mhisani alimuuliza.

“Nataka vyombo vya ulinzi na usalama, vikae chonjo nchi nzima, kisha nitumie makosa yao kutekeleza ninalowaza.”

“Mimi nadhani tukupe mikakati ya namna ya kutekeleza jambo letu. Tutakupa ramani na baadhi ya maelekezo kuhusu benki ya Umoja, kisha fanya kazi kwa urahisi zaidi.”

“Hapana! Mmenipa kazi, acheni nifanye kazi nitakavyo, msiniongoze. Mkakati wenu bakini nao, fanyeni mkakati wangu.”

“Kwa hiyo huo mkakati wako ni kututaka tuuvujishe mpango wetu?”

“Hivyo ndivyo itakiwavyo!”

“Tusipotekeleza itaathiri vipi mpango wako?”

“Inaweza kuniondolea ufanisi wangu, pia inaweza kuchukua muda mrefu zaidi kukamilika, kuliko ambavyo ingevuja!”

“Hii kali aisee!” Mhisani alisema huku akiwageukia wenzake, ambao nao walikuwa wamesimama wakishangaa maelekezo ya mtu wao.

“Sawa, tutakutafuta dakika tatu zijazo.” Amolo alisema huku akikata mawasiliano na kumpa simu Kamonga.

Baada ya kuachana na Miguu ya kuku, Sadon brothers, walibaki peke yao ndani ya chumba cha mikutano, ndani ya jumba lao la kifahari. Walitazamana bila kusemeshana, huku kila mmoja akiwaza lake kichwani.

Ilikuwa ni ngumu kumwamini Miguu ya kuku, lakini haikuwa rahisi pia kufanya ile kazi peke yao. Vichwa viliwauma; mpango walouhitaji, pia walihitaji kufanya kazi na mtu wa nje ya kundi lao.

“Tufanye nini ndugu zangu!” Mhisani aliwauliza wadogo zake.

“Nadhani tumempata mtu sahihi, hatuna haja ya kujiuliza mara mbilimbili. Zuki Gadu, ni sahihi kuifanya kazi hii.” Kamonga aliendelea kuwashawishi wenzake.

“Hapa tatizo siyo Zuki, hapa tatizo ni kuvujisha mpango serikalini. Ni ngumu kulitekeleza hilo jambo!”Tindo aliongea kwa msisitizo.

“Kwanza tunakubaliana na gharama anazozihitaji?” Amolo aliwauliza wenzake.

“Hiyo ni pesa ndogo sana aliyoihitaji. Tatizo bado lipo kwenye kuvujisha mpango.” Mhisani alijibu.

“Tumpe pesa, ila tusivujishe mpango wetu uliyotugharimu pesa nyingi kukamilika. Hatuwezi kuuza gharama zetu kirahisi namna hiyo.” Amolo nae aliongezea.

“Naona tuuvujishe mpango kwa kumruhusu yeye mwenyewe auvujishe awezavyo, lakini tusivujishe mikakati yetu hata chembe!” Kamonga alishauri. Wenzake walimtizama.

“Upo sahihi! Tumpe hiyo kazi peke yake!” Tindo aliafiki.

“Na iwe hivyo!” Amolo nae alikubali, huku akimtizama Mhisani, ambae nae alitikisa kichwa chake kukubali kilichozungumzwa.

Haraka walimuunganisha Miguu ya kuku kwa njia ya mtandao.

“Kila ulichohitaji kitafanyiwa kazi, lakini kwa shariti moja tu!” Mhisani alimwambia Zuki Gadu p.a.k Miguu ya kuku.

“Nawasikilizeni!” Miguu ya kuku aliitikia.

“Tunaomba uvujishe mpango huo kwa njia zako.”

“Itabidi muongeze dau la pesa!”

“Eeh!!”

“Yes! Kwa sababu sijui mkakati wenu ulivyo, zaidi najua mnataka plate namba tano. Sijui mlivyokuwa mmejipanga kufanikisha hilo”
“Kwa hiyo tukiongeza dau, utavujisha mpango wako na si wetu?”

“Ndivyo ilivyo!”

Sadon Brother’s, walitazamana, kisha wakaafiki kuongeza dau. Ilikuwa rahisi kuafiki kwa sababu, mpango wao ulikuwa salama kuvuja.

“Sawa, ujapohitaji usaidizi, tuko tayari wakati wowote!”
Miguu ya kuku alifikiria kidogo, kisha akasema..
“ Haina ubaya! Lakini acheni nifanye kazi yangu kadri niwezavyo. Nyie mkae kimya na angalieni yatakayokuwa yanajiri. Msiingilie lolote.”

“Haina neno! Unakaribishwa Nairobi!” Mhisani alijibu na kumkaribisha Miguu ya kuku.

“Great!” Miguu ya kuku alijibu na kutoka hewani.

Baada ya Miguu ya kuku kutoka hewani, ndugu watano walibaki peke yao. Walijadili mambo machache, kisha walisambaratika na kila mmoja, alienda kuendelea na majukumu yake ya kujimaarisha zaidi kwenye kitengo chake.

DAR ES LAAM….

Miguu ya kuku aliweka simu yake pembeni, kisha aliegemea kwenye sofa na kutazama juu. Mawazo mengi yalipita kichwani mwake. Wazo moja lilikuwa zito zaidi kuliko mawazo mengine. Lilikuwa ni wazo ambalo lilimtia hofu kubwa.

“Nimefanya kazi nyingi, lakini sijawahi kuiba benki. Na kinachonitisha zaidi ni ulinzi ulioko kwenye mabenki, hasa ndani ya benki.” Alijisemea taratibu huku akijaribu kujenga picha kichwani mwake, kwenye baadhi ya mabenki makubwa nchini Tanzania.

“Hii ni kazi ngumu sana aisee!” Alisema huku akiishika laptop yake iliyokuwa mbele yake, juu ya meza. Aliparaza kidogo na ukatokea mchoro(picha) wa jengo refu lenye ghorofa zaidi ya kumi nane. Jengo lile lilinakishiwa kwa vioo, kuanzia chini hadi juu.

“Kazi ipo duh!” Alijisemea huku mkono mmoja ukiwa kidevuni na macho yake yakiwa yametulia kulitizama jengo lile. Aliendelea kulichunguza kwa umakini sana, huku akili yake ikifanya kazi kubwa kutafakari.

“Mara zote benki huwa zinakuwa chini kabisa ya majengo marefu namna hii!” Alijisemea huku akichezesha mshale wa kuongoza, kuelekea upande wa chini wa lile jengo.

“Kama ipo huku chini, ina maana, wanamiliki basement yote na huko ndiko iliko vault ya kuhifadhia pesa na vault ya kuhifadhia hizo plate!” Alijisemea tena huku akiendelea kuizungusha picha ya jengo refu, lililopewa jina la Patrice Lumumba, huku likiwa chini ya umiliki wa Nssf.

Wakati alipokuwa akiendelea kupitia picha kadhaa za jengo lile, kuna kitu kingine aligundua na kitu kile kilimtia woga wa wazi kabisa na aliwaza kutema ndoano, endapo alichokuwa amegundua kingelikuwa sahihi.

Haraka alianza kutafuta picha za satellite ili aweze kujiridhisha na kile alichokuwa amekigundua na kukitilia wasiwasi.
Jengo la Patrice Lumumba lilikuwa ni jengo refu sana na lenye uwekezaji mkubwa jijini Nairobi. Lilikuwa ni jengo ambalo lilijengwa kwa upekee sana. Lilikuwa ni jengo refu pekee maeneo ya Upper hill, huku kukiwa hakuna jengo lingine lau lenye ghorofa moja kwenye ule mtaa.

“Kwa nini ipo hivi?” Alijiuliza huku akizidi kumakinika na picha alizokuwa anazishuhudia kupitia kompyuta mpakato iliyokuwa mbele yake. Alizidi kuyatalii kwa macho maeneo jirani na jengo la Patrice Lumumba. Hapo ndipo mwili ulimsisimka zaidi.

Kwa nini!

Kwa sababu, jengo lile lilizungukwa na maeneo nyeti sana, ambayo si rahisi mtu kuyagundua, japokuwa mengine yalifahamika kirahisi. Jengo lile lilikuwa lipo katikati ya vikosi vya jeshi na vile vya usalama wa raia.

Mashariki mwake kulikuwa na makao makuu ya jeshi la kujitegemea, huku Magharibi kwake kukiwa na kituo kikuu cha polisi cha Nairobi. Upande wa kaskazini kulikuwa na kambi ya kikosi cha anga(Moi air base), na upande wa kusini kukiwa na makao makuu ya chama tawala.

“Sasa nimeelewa ni kwa nini jengo hili limeota peke yake bila kuruhusu majengo mengine ya aina hiyo! Huu utakuwa ni mtaa wa kimkakati hapo nchini Kenya!” Alijisemea huku akijishika kichwani kwa kujikwarua. Nywele ziliwasha kwa hofu ya kile alichokuwa anakiwaza.

“Mbona hii kazi inataka kunionjesha umauti?” Aliwaza huku akianza kutafuta umuhimu wa benki ya Umoja ndani ya nchi ya Kenya.

Kulikuwa na maelezo mengi sana kuhusu benki hiyo, lakini hayakumuingia akilini, yalikuwa ni maelezo mepesi kuliko alivyotarajia.

“Maelezo haya, hayawezi kufanya nchi iweke hapo zile plate za fedha!” Alisema huku akitikisa kichwa na kuchukua simu iliyokuwa pembeni yake. Alitafuta jina alilohitaji, kisha alipiga na kuzungumza kile alichotaka kuzungumza. Lakini alichojibiwa, kilimfanya afikirie kuwapigia Sadon Brothers, na kuitema kazi aliyopewa.

Yalikuwa ni maelezo ya kuogofya kwa binadamu mwenye moyo wa nyama, ilihitaji kiumbe kisicho na damu kuvumilia na kuendelea kushikilia dili gumu namna ile. Dili lenye kuuza roho
.
.
.
.
.
MWANDISHI; BAHATI K MWAMBA.

SIMU; 0758573660/0624155629.

.
ENDELEA KUWA NAMI.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom