Kudo
JF-Expert Member
- Nov 2, 2017
- 1,809
- 6,081
RIWAYA: MVAMIZI
NA; BAHATI K MWAMBA.
SIMU: 0758573660/0656741439.
1:
CHIPIPA, ANGOLA…
Pembezoni kidogo mwa mji mdogo wa Chipa ulioko ndani ya mkoa wa Chipipa nchini Angola, kulikuwa na tukio lililokuwa linaendelea katikati ya giza nene. Tukio ambalo lilikuwa linafanywa kwa siri na umakini mkubwa ndani ya msitu mnene uliozunguka mji ule mdogo, ambao ulitumika kama kituo kikubwa cha uuzaji Almasi kutoka kwenye migodi iliyoko kilomita chache.
Helkopita isiyo na sauti aina ya Chinook H-47K ilikuwa imeganda angani mita mia tatu kutoka usawa bahari. Kwenye mlango mmoja kulikuwa na kamba mbili nene zikining'inia. Sekunde chache baadae kamba zile zilianza kutambaliwa na viumbe ambao walitoka ndani ya helkopita. Viumbe wale walishuka kwa kasi na kwa umakini mkubwa huku silaha zikiwa mikononi mwao, tayari kwa lolote. Viumbe wanane wenye miguu miwili walishuka chini na kwa kutumia kamba na walipofika chini walitikisa kamba mara mbili na helkopita iliondoka huku kamba zikivutwa ndani kwa kasi kubwa.
Baada ya viumbe wenye miguu miwili na mikono miwili kufika chini salama na kuruhusu helkopita iondoke, walikimbia kwa mtindo wa zigizaga kuelekea kwenye kichaka kilichokuwa karibu na pale waliposhukia. Ilipendeza kuwatazama namna walivyokuwa wanakimbia huku silaha zao zikiwa mikononi, kofia vichwani mwao na mabegi yenye uzito wa kilo kumi na tano yakiwa migongoni mwao. Licha ya kuvaa landboot nzito, lakini mikimbio yao haikuwa na vishindo, walikimbia kwa ufasaha na kwa malengo maalumu mithili ya watuhumiwa waendao mahakama ya kijeshi. Ilivutia kuwatizama ijapokuwa wao hawakuwa na lengo la kumvutia yeyote aliyekuwa akiwatizama. Kila mmoja alikuwa na bunduki aina ya M4 carbine 5.56×45mm yenye urefu wa sentimita 36.83 na caliber ya 5.56.
Bunduki zote zilikuwa na telescope stock. Vichwani mwao walivaa kofia za chuma zilizozungushiwa mchipi uliobeba Night gogle ambayo ilikuwa imekaa usawa wa paji la uso wa kila mmoja. Vifuani mwao walivaa tactical vests zenye chest rig, viganja vyao vilifunikwa na glavu za ngozi, huku mikanda yao ikiwa imebana vema viuno vyao na kufunikwa na maga pochi zilizosheheni magazini zenye risasi za kutosha.
Magoti yao yalibanwa vema na protective pads huku mapajani mwao kukiwa na holsters zikiwa zimebana vema bastola zilizoshiba risasi. Kila mmoja sikio lake lilikuwa na wireless earpiece kwa ajili ya kuwasiliana wawapo kwenye jambo lililokuwa limewapeleka maeneo hayo.
Wote wanane walifika kwenye kichaka huku kila mmoja akimlinda mwenzake na hatari yoyote ambayo ingelijitokeza.
“Tuna dakika thelathini za kufanya kilichotuleta huku. Hatutakiwi kuvuka zaidi ya dakika thelathini na mbili. Umakini unahitajika ili tuweze kurejea tukiwa salama.” Mmoja wa makomando aliwambia wenzake huku akijipapasa kwenye mifuko yake na punde alitoa karatasi ndogo, ambayo ilikuwa imechorwa michoro ambayo si rahisi kutafsirika.
Aliitazama karatasi ile kwa nusu dakika kisha aliikunja na, kuirejesha mfukoni huku macho yake yakizunguka kuwatazama wenzake ambao walikuwa wamepiga goti moja chini, mithili ya wafukuza upepo kwenye mbio za mita mia moja. Ni yeye pekee aliyekuwa amesimama.
“Tunahitaji kutumia dakika saba kwa safari ya mwendo haraka kufika kwenye kiota cha miiba. Tutatumia dakika kumi na tano kukipekuwa kiota na kuchukua yai letu na kuondoka.” Aliwambia wenzake huku akibeba vema bunduki yake na kuivaa vema shingoni mwake.
“Kumbukeni kosa moja litatufanya tu…” Alisita kusema huku kwa kitendo cha haraka na wepesi mkubwa, akijirusha chini kwa umakini mkubwa na kutulia huku silaha yake ikiwa tayari kuachia risasi zilizokusudiwa. Kitendo cha yeye kujirusha chini hakukifanya peke yake, wenzake walishakifanya sekunde mbili mbele yake.
Walifanya hivyo baada ya kuhisi kuvunjika kwa kitu mita chache kutoka walipokuwa. Kujirusha kwao kuliambatana na kutambaa chini kwa mtindo maalumu huku wakigawana uelekeo, kulizunguka eneo ambalo walisikia sauti ya mvunjiko.
Sekunde chache zilitosha kulifanya eneo lile liwe chini ya uangalizi mkubwa, huku upekuzi ukifanyika kwa umakini mkubwa kuhakikisha kinafahamika kilichosababisha mlio ule ambao, haukuwa wa bahati mbaya. Masikio yao hayakukubaliana na bahati mbaya, bali ni makusudi kabisa yalifanyika kuitoa ile sauti ya kuvunja kijiti. Umakini wao ulikuwa mkubwa kwa sababu uwepo wao pale ulikuwa ni kwa ajili yao, hawakuwa wametarajia uwepo wa mtu mwingine yeyote.
“Pito!” Komando mmoja aliita na haraka aliyeitwa alisogea pale kwa kasi kubwa.
“Hiki ni nini?” Pito aliulizwa. Hakujibu haraka, badala yake aliinama chini na kuanza kupapasa taratibu na kisha alimtizama aliyemuita.
“Hapa kulikuwa na moto uliozimwa dakika chache zilizopita!” Pito alisema huku akiinuka na kuanza kuangaza kando ya lile eneo.
Makomando wote walisogea pale paliposemekana kuwashwa moto, kila mmoja alijiridhisha kuhusu uwepo wa moto uliozimwa muda mfupi, kabla ya wao kufika pale.
“Change plan!” Komando kiongozi aliwambia wenzake, kisha walibadili uelekeo na kuanza kukimbia kwa kasi ndani ya lile pori lililoshiba miti na nyasi nene. Walikimbia kwa umakini, bunduki mkononi night goggles zikiwa machoni ili kuwawezesha kuona ndani ya giza nene.
Walikimbia umbali wa kilomita moja, kisha Komando kiongozi alinyoosha mkono juu na kuukunja ngumi. Ishara ambayo ilionwa vema na makomando wengine na kilichofuata ni kila mmoja kusimama huku akichukua upande wa kuwalinda wenzake, huku wakimweka Komando kiongozi katikati yao.
Haraka Komando kiongozi alitoa karatasi yenye michoro anayoweza kuitafsri yeye na kuitizama kwa umakini mkubwa. Alipohakikisha ameelewa kilichochorwa kwenye karatasi, alirudisha mfukoni na kuwaambia wenzake..
“Hatupo mbali na kiota cha miiba, ijapokuwa uelekeo huu ni kutokea mbele ya kiota. Kila mmoja anaelewa kipi cha kufanya ili kulifikia yai na kulibeba likiwa salama. Upande wa mbele unachangamoto ambayo tulishaipigia mazoezi, hivyo utekelezaji kwa kuzingatia muda ni….” Alisita kuendeea kuzungumza, haraka alichuchumaa chini na kumtazama jamaa mmoja ambae alikuwa na begi mgongoni likiwa na kifaa maalumu cha kuunganisha mawasiliano baina yao. Si yeye tu aliyemtizama, wengine nao walimtizama na yeye aliinuka haraka na kulitua begi lake. Kisha alitoa kile kifaa alichokuwa amekibeba na kukiweka chini. Alibofya hapa na pale na kuwageukia wenzake.
“Hakuna uingiliano wa mawasiliano. We are safe.” Alisema huku akikifunga.
“Not safe!”Kamanda alikataa huku akimpa ishara Pito.
“Kila mmoja amesikia chafya ikipigwa na hakuna ambae ameipiga miongoni mwetu. It’s a trap!” Alisema huku akihema kwa jaziba. Operesheni ilikuwa mikononi mwake na uhai wa wenzake ulikuwa mikononi mwake. Kusonga mbele wakati kuna mauzauza yameanza kujitokeza, ilikuwa ni kuuza uhai wao kwa bei rahisi. Lakini kurudi nyuma pia ilimaanisha walichoenda kukifanya kitakuwa hakijafanikiwa.
Komando kiongozi alimtizama Pito. Kisha akamshika bega na kumpa ishara kwa kichwa na alipoutoa mkono wake begani, haraka Pito aliondoka pale mithili ya mwizi anavyotoroka katikati ya umati wa watu.
Walibaki makomando saba wakiwa wametulia katikati ya pori nene. Huku kiongozi wao akiwa bado hajapata maamuzi sahihi ya kufanya na alitegemea kupata taarifa sahihi kutoka kwa Pito. Aliobaki nao aliwapa ishara ya kuvua wireless earpiece zilizokuwa masikioni mwao. Kila mmoja aliivua na walibaki kumtazama.
“We are in a killing ground. Kila mmoja awe makini kuhakikisha mwenzake anakuwa salama. Tunabadili uelekeo na kutafuta eneo zuri na salama huku tukingoja ripoti ya Nyoka. Ikiwa ndivyo sivyo, tuna abort mission.” Aliwambia wenzake na kisha alianza kuondoka pale walipokuwa na kuelekea upande mwingine. Kila walichokuwa wanakifanya kilikuwa kinawaweka nje ya muda. Lakini hawakuwa na namna, waliijua thamani yao ndani ya jeshi lao na walijua madhara ya kufanyiwa shambulio la kushitukiza, hasa kutoka kwa adui ambae anajua uwepo wao pale.
Makomando saba walihama eneo huku komando wa mwingine ambae alikamilisha pack ya makomando nane, akiwa yuko msituni akijaribu kunyatia harakati za mtu ambae alikuwa ameingilia mipango yao.
Pito Fizo alikuwa ni komando miongoni mwa makomado wa kutumainiwa. Hakuwa komando tu, alikuwa ni komando mlengaji akiwa amefuzu kwenye shule ya walenga shabaha na kuwa miongoni mwa wanafunzi bora ambao walifaulu kila idara; kuanzia idara ya shabaha, hesabu, mbio na ujifichaji.
Kila mara alikuwa akijumuishwa kwenye pack ya makomando kwa ajili ya misheni nje ya nchi. Ufanisi wake awapo kwenye uwanja wa vita ulimfanya awe miongoni mwa makomando wa kuaminika huku akipewa kipaumbele, upande wa kulenga shabaha. Kuna wakati aliondolewa kwenye orodha ya uwajibikaji kivita na kupelekwa kitengo cha usalama, lakini hakudumu, alikataa na kuomba kurejea kwenye uwanja wa vita.
Aliamini yeye si wa kukimbizana na wahalifu wavivu, ambao walipachikwa majina ya ujasusi; aliamini yeye ameletwa Duniani kupambana na wahalifu wenye silaha nzito katikati ya misitu minene. Alipenda kujificha juu ya miti na kupigwa jua huku akiwa ameshindia matone kadhaa ya maji. Aliona fahari kukimbia katikati ya kiza kinene, huku akiwala vichwa maadui zake na kuwasafishia njia wenzake. Kwake kukaa sehemu moja ndani ya siku mbili akingoja windo, ilikuwa ni kawaida na hakuwahi kujuta kulala juu ya miti au kwenye nyasi akisubiri windo lake likae pahali anapohitaji ili atimize lengo lake.
Maisha ya Pito Fizo yalitawaliwa na hekaheka za msituni kuliko anasa za kidunia. Hakupenda kufanya kazi ya kukaa na kuripoti kambini kila siku. Alipenda kuishugulisha akili yake na mambo ya vita. Kupiga hesabu za kulishinda windo lake, kukimbizana na maadui msituni kwake ilikuwa ni furaha isiyokifani.
Wakati vijana wengine wakishabikia mchezo wa kubeti, yeye alikuwa anabeti maisha yake na maadui. Kila alipokuwa akienda misheni, ndani kwake huacha karatasi yenye pande mbili; upande wake na upande wa adui yake ambapo, hutiki upande wake kama mshindi hivyo akiwa kwenye uwanja wa mapambano, hupigana ili kuokoa mkeka wake na kila arudipo na ushindi huweka rekodi kwenye kitabu chake cha kumbukumbu, kisha huenda kanisani na kusali kwa siku saba mfululizo na kisha huhamia msikitini ambapo, huswali kwa siku saba swala tano. Katika siku zote hizo za kusali na kuswali huambatana na mfungo.
Kwenye maisha yake aliamini kuna Mungu anaemlinda kwenye nyakati zote ngumu anazopita. Lakini alishindwa kujua ni Mungu yupi kwa sababu waisilamu huamini wanae Mungu wa haki na Wakristu nao huamini Mungu wanaemwamini. Pito Fizo aliamua kutumika kote kama shukrani kwa Mungu mmoja anaeabudiwa kwa imani mbili tofauti. Yeye aliamini imani zote ni sawa na zinaabudu Mungu mmoja na hazipaswi kunyosheana vidole. Mara zote alipenda sana kuwaadhibu maadui wanaojificha kwenye mgongo wa dini. Aliamini hao ndiyo wanaoiweka dunia kwenye matatizo kwa kigezo cha udini, huku wakiwa na agenda ya udhalimu nyuma yao.
Alisali na kuswali pia kwa lengo la kumuomba Mungu msamaha, endapo aliua mtu ambae hakuwa dhalimu.
Pito Fizo alipenda vita na aliamini Mungu amemlata Duniani kupigana vita na si kitu kingine. Aliamini uwezo wake wa kulenga shabaha, kupigana na kuwatoroka maadui ni kipaji alichopewa na Mungu. Licha ya kupigana vita, lakini alikuwa ni mtu wa dini haswaa.
Komando Pito Fizo baada ya kuondoka na kuwaacha wenzake, alizunguka eneo walilokuwepo kwa umbali wa mita mia tano kwa pande tatu za Dunia, huku ule upande wa nne akiuacha kwa kuwa wenzake walikuwa upande huo na kama kungelikuwa na tatizo, wangelimtaarifu kupitia vifaa maalumu walivyofunga masikioni mwao. Alizunguka kwa umakini mkubwa lakini hadi anamaliza, hakuwa amefanikiwa kukutana na kitu chochote chenye kutia shaka ijapokuwa, akili yake ilikuwa inaamini kabisa kuna kitu hakikuwa sawa.
Wazo moja likampitia kichwani na haraka aliamua kulifanyia kazi. Aliachana na hizo pande na badala yake aliamua kuelekea upande ambao wenzake waliamua kuutumia kama eneo lao la kimkakati. Aliamua kulikagua eneo hilo na kisha angelirejea kwa wenzake.
Lakini jambo moja ambalo hakujua ni kuwa, eneo alilokuwa anafikiria kuliendea tayari lilikuwa limeshasheheni wenyeji kutisja wa kutisha. Hilo hakujua na wenzake pia hawakujua tayari wameshapokelewa na mwenyeji mwenye macho na mikono ya chupa.
Msitu wa Chipa uligeuzwa duka la roho katikati ya giza nene.
NA; BAHATI K MWAMBA.
SIMU: 0758573660/0656741439.
1:
CHIPIPA, ANGOLA…
Pembezoni kidogo mwa mji mdogo wa Chipa ulioko ndani ya mkoa wa Chipipa nchini Angola, kulikuwa na tukio lililokuwa linaendelea katikati ya giza nene. Tukio ambalo lilikuwa linafanywa kwa siri na umakini mkubwa ndani ya msitu mnene uliozunguka mji ule mdogo, ambao ulitumika kama kituo kikubwa cha uuzaji Almasi kutoka kwenye migodi iliyoko kilomita chache.
Helkopita isiyo na sauti aina ya Chinook H-47K ilikuwa imeganda angani mita mia tatu kutoka usawa bahari. Kwenye mlango mmoja kulikuwa na kamba mbili nene zikining'inia. Sekunde chache baadae kamba zile zilianza kutambaliwa na viumbe ambao walitoka ndani ya helkopita. Viumbe wale walishuka kwa kasi na kwa umakini mkubwa huku silaha zikiwa mikononi mwao, tayari kwa lolote. Viumbe wanane wenye miguu miwili walishuka chini na kwa kutumia kamba na walipofika chini walitikisa kamba mara mbili na helkopita iliondoka huku kamba zikivutwa ndani kwa kasi kubwa.
Baada ya viumbe wenye miguu miwili na mikono miwili kufika chini salama na kuruhusu helkopita iondoke, walikimbia kwa mtindo wa zigizaga kuelekea kwenye kichaka kilichokuwa karibu na pale waliposhukia. Ilipendeza kuwatazama namna walivyokuwa wanakimbia huku silaha zao zikiwa mikononi, kofia vichwani mwao na mabegi yenye uzito wa kilo kumi na tano yakiwa migongoni mwao. Licha ya kuvaa landboot nzito, lakini mikimbio yao haikuwa na vishindo, walikimbia kwa ufasaha na kwa malengo maalumu mithili ya watuhumiwa waendao mahakama ya kijeshi. Ilivutia kuwatizama ijapokuwa wao hawakuwa na lengo la kumvutia yeyote aliyekuwa akiwatizama. Kila mmoja alikuwa na bunduki aina ya M4 carbine 5.56×45mm yenye urefu wa sentimita 36.83 na caliber ya 5.56.
Bunduki zote zilikuwa na telescope stock. Vichwani mwao walivaa kofia za chuma zilizozungushiwa mchipi uliobeba Night gogle ambayo ilikuwa imekaa usawa wa paji la uso wa kila mmoja. Vifuani mwao walivaa tactical vests zenye chest rig, viganja vyao vilifunikwa na glavu za ngozi, huku mikanda yao ikiwa imebana vema viuno vyao na kufunikwa na maga pochi zilizosheheni magazini zenye risasi za kutosha.
Magoti yao yalibanwa vema na protective pads huku mapajani mwao kukiwa na holsters zikiwa zimebana vema bastola zilizoshiba risasi. Kila mmoja sikio lake lilikuwa na wireless earpiece kwa ajili ya kuwasiliana wawapo kwenye jambo lililokuwa limewapeleka maeneo hayo.
Wote wanane walifika kwenye kichaka huku kila mmoja akimlinda mwenzake na hatari yoyote ambayo ingelijitokeza.
“Tuna dakika thelathini za kufanya kilichotuleta huku. Hatutakiwi kuvuka zaidi ya dakika thelathini na mbili. Umakini unahitajika ili tuweze kurejea tukiwa salama.” Mmoja wa makomando aliwambia wenzake huku akijipapasa kwenye mifuko yake na punde alitoa karatasi ndogo, ambayo ilikuwa imechorwa michoro ambayo si rahisi kutafsirika.
Aliitazama karatasi ile kwa nusu dakika kisha aliikunja na, kuirejesha mfukoni huku macho yake yakizunguka kuwatazama wenzake ambao walikuwa wamepiga goti moja chini, mithili ya wafukuza upepo kwenye mbio za mita mia moja. Ni yeye pekee aliyekuwa amesimama.
“Tunahitaji kutumia dakika saba kwa safari ya mwendo haraka kufika kwenye kiota cha miiba. Tutatumia dakika kumi na tano kukipekuwa kiota na kuchukua yai letu na kuondoka.” Aliwambia wenzake huku akibeba vema bunduki yake na kuivaa vema shingoni mwake.
“Kumbukeni kosa moja litatufanya tu…” Alisita kusema huku kwa kitendo cha haraka na wepesi mkubwa, akijirusha chini kwa umakini mkubwa na kutulia huku silaha yake ikiwa tayari kuachia risasi zilizokusudiwa. Kitendo cha yeye kujirusha chini hakukifanya peke yake, wenzake walishakifanya sekunde mbili mbele yake.
Walifanya hivyo baada ya kuhisi kuvunjika kwa kitu mita chache kutoka walipokuwa. Kujirusha kwao kuliambatana na kutambaa chini kwa mtindo maalumu huku wakigawana uelekeo, kulizunguka eneo ambalo walisikia sauti ya mvunjiko.
Sekunde chache zilitosha kulifanya eneo lile liwe chini ya uangalizi mkubwa, huku upekuzi ukifanyika kwa umakini mkubwa kuhakikisha kinafahamika kilichosababisha mlio ule ambao, haukuwa wa bahati mbaya. Masikio yao hayakukubaliana na bahati mbaya, bali ni makusudi kabisa yalifanyika kuitoa ile sauti ya kuvunja kijiti. Umakini wao ulikuwa mkubwa kwa sababu uwepo wao pale ulikuwa ni kwa ajili yao, hawakuwa wametarajia uwepo wa mtu mwingine yeyote.
“Pito!” Komando mmoja aliita na haraka aliyeitwa alisogea pale kwa kasi kubwa.
“Hiki ni nini?” Pito aliulizwa. Hakujibu haraka, badala yake aliinama chini na kuanza kupapasa taratibu na kisha alimtizama aliyemuita.
“Hapa kulikuwa na moto uliozimwa dakika chache zilizopita!” Pito alisema huku akiinuka na kuanza kuangaza kando ya lile eneo.
Makomando wote walisogea pale paliposemekana kuwashwa moto, kila mmoja alijiridhisha kuhusu uwepo wa moto uliozimwa muda mfupi, kabla ya wao kufika pale.
“Change plan!” Komando kiongozi aliwambia wenzake, kisha walibadili uelekeo na kuanza kukimbia kwa kasi ndani ya lile pori lililoshiba miti na nyasi nene. Walikimbia kwa umakini, bunduki mkononi night goggles zikiwa machoni ili kuwawezesha kuona ndani ya giza nene.
Walikimbia umbali wa kilomita moja, kisha Komando kiongozi alinyoosha mkono juu na kuukunja ngumi. Ishara ambayo ilionwa vema na makomando wengine na kilichofuata ni kila mmoja kusimama huku akichukua upande wa kuwalinda wenzake, huku wakimweka Komando kiongozi katikati yao.
Haraka Komando kiongozi alitoa karatasi yenye michoro anayoweza kuitafsri yeye na kuitizama kwa umakini mkubwa. Alipohakikisha ameelewa kilichochorwa kwenye karatasi, alirudisha mfukoni na kuwaambia wenzake..
“Hatupo mbali na kiota cha miiba, ijapokuwa uelekeo huu ni kutokea mbele ya kiota. Kila mmoja anaelewa kipi cha kufanya ili kulifikia yai na kulibeba likiwa salama. Upande wa mbele unachangamoto ambayo tulishaipigia mazoezi, hivyo utekelezaji kwa kuzingatia muda ni….” Alisita kuendeea kuzungumza, haraka alichuchumaa chini na kumtazama jamaa mmoja ambae alikuwa na begi mgongoni likiwa na kifaa maalumu cha kuunganisha mawasiliano baina yao. Si yeye tu aliyemtizama, wengine nao walimtizama na yeye aliinuka haraka na kulitua begi lake. Kisha alitoa kile kifaa alichokuwa amekibeba na kukiweka chini. Alibofya hapa na pale na kuwageukia wenzake.
“Hakuna uingiliano wa mawasiliano. We are safe.” Alisema huku akikifunga.
“Not safe!”Kamanda alikataa huku akimpa ishara Pito.
“Kila mmoja amesikia chafya ikipigwa na hakuna ambae ameipiga miongoni mwetu. It’s a trap!” Alisema huku akihema kwa jaziba. Operesheni ilikuwa mikononi mwake na uhai wa wenzake ulikuwa mikononi mwake. Kusonga mbele wakati kuna mauzauza yameanza kujitokeza, ilikuwa ni kuuza uhai wao kwa bei rahisi. Lakini kurudi nyuma pia ilimaanisha walichoenda kukifanya kitakuwa hakijafanikiwa.
Komando kiongozi alimtizama Pito. Kisha akamshika bega na kumpa ishara kwa kichwa na alipoutoa mkono wake begani, haraka Pito aliondoka pale mithili ya mwizi anavyotoroka katikati ya umati wa watu.
Walibaki makomando saba wakiwa wametulia katikati ya pori nene. Huku kiongozi wao akiwa bado hajapata maamuzi sahihi ya kufanya na alitegemea kupata taarifa sahihi kutoka kwa Pito. Aliobaki nao aliwapa ishara ya kuvua wireless earpiece zilizokuwa masikioni mwao. Kila mmoja aliivua na walibaki kumtazama.
“We are in a killing ground. Kila mmoja awe makini kuhakikisha mwenzake anakuwa salama. Tunabadili uelekeo na kutafuta eneo zuri na salama huku tukingoja ripoti ya Nyoka. Ikiwa ndivyo sivyo, tuna abort mission.” Aliwambia wenzake na kisha alianza kuondoka pale walipokuwa na kuelekea upande mwingine. Kila walichokuwa wanakifanya kilikuwa kinawaweka nje ya muda. Lakini hawakuwa na namna, waliijua thamani yao ndani ya jeshi lao na walijua madhara ya kufanyiwa shambulio la kushitukiza, hasa kutoka kwa adui ambae anajua uwepo wao pale.
Makomando saba walihama eneo huku komando wa mwingine ambae alikamilisha pack ya makomando nane, akiwa yuko msituni akijaribu kunyatia harakati za mtu ambae alikuwa ameingilia mipango yao.
Pito Fizo alikuwa ni komando miongoni mwa makomado wa kutumainiwa. Hakuwa komando tu, alikuwa ni komando mlengaji akiwa amefuzu kwenye shule ya walenga shabaha na kuwa miongoni mwa wanafunzi bora ambao walifaulu kila idara; kuanzia idara ya shabaha, hesabu, mbio na ujifichaji.
Kila mara alikuwa akijumuishwa kwenye pack ya makomando kwa ajili ya misheni nje ya nchi. Ufanisi wake awapo kwenye uwanja wa vita ulimfanya awe miongoni mwa makomando wa kuaminika huku akipewa kipaumbele, upande wa kulenga shabaha. Kuna wakati aliondolewa kwenye orodha ya uwajibikaji kivita na kupelekwa kitengo cha usalama, lakini hakudumu, alikataa na kuomba kurejea kwenye uwanja wa vita.
Aliamini yeye si wa kukimbizana na wahalifu wavivu, ambao walipachikwa majina ya ujasusi; aliamini yeye ameletwa Duniani kupambana na wahalifu wenye silaha nzito katikati ya misitu minene. Alipenda kujificha juu ya miti na kupigwa jua huku akiwa ameshindia matone kadhaa ya maji. Aliona fahari kukimbia katikati ya kiza kinene, huku akiwala vichwa maadui zake na kuwasafishia njia wenzake. Kwake kukaa sehemu moja ndani ya siku mbili akingoja windo, ilikuwa ni kawaida na hakuwahi kujuta kulala juu ya miti au kwenye nyasi akisubiri windo lake likae pahali anapohitaji ili atimize lengo lake.
Maisha ya Pito Fizo yalitawaliwa na hekaheka za msituni kuliko anasa za kidunia. Hakupenda kufanya kazi ya kukaa na kuripoti kambini kila siku. Alipenda kuishugulisha akili yake na mambo ya vita. Kupiga hesabu za kulishinda windo lake, kukimbizana na maadui msituni kwake ilikuwa ni furaha isiyokifani.
Wakati vijana wengine wakishabikia mchezo wa kubeti, yeye alikuwa anabeti maisha yake na maadui. Kila alipokuwa akienda misheni, ndani kwake huacha karatasi yenye pande mbili; upande wake na upande wa adui yake ambapo, hutiki upande wake kama mshindi hivyo akiwa kwenye uwanja wa mapambano, hupigana ili kuokoa mkeka wake na kila arudipo na ushindi huweka rekodi kwenye kitabu chake cha kumbukumbu, kisha huenda kanisani na kusali kwa siku saba mfululizo na kisha huhamia msikitini ambapo, huswali kwa siku saba swala tano. Katika siku zote hizo za kusali na kuswali huambatana na mfungo.
Kwenye maisha yake aliamini kuna Mungu anaemlinda kwenye nyakati zote ngumu anazopita. Lakini alishindwa kujua ni Mungu yupi kwa sababu waisilamu huamini wanae Mungu wa haki na Wakristu nao huamini Mungu wanaemwamini. Pito Fizo aliamua kutumika kote kama shukrani kwa Mungu mmoja anaeabudiwa kwa imani mbili tofauti. Yeye aliamini imani zote ni sawa na zinaabudu Mungu mmoja na hazipaswi kunyosheana vidole. Mara zote alipenda sana kuwaadhibu maadui wanaojificha kwenye mgongo wa dini. Aliamini hao ndiyo wanaoiweka dunia kwenye matatizo kwa kigezo cha udini, huku wakiwa na agenda ya udhalimu nyuma yao.
Alisali na kuswali pia kwa lengo la kumuomba Mungu msamaha, endapo aliua mtu ambae hakuwa dhalimu.
Pito Fizo alipenda vita na aliamini Mungu amemlata Duniani kupigana vita na si kitu kingine. Aliamini uwezo wake wa kulenga shabaha, kupigana na kuwatoroka maadui ni kipaji alichopewa na Mungu. Licha ya kupigana vita, lakini alikuwa ni mtu wa dini haswaa.
Komando Pito Fizo baada ya kuondoka na kuwaacha wenzake, alizunguka eneo walilokuwepo kwa umbali wa mita mia tano kwa pande tatu za Dunia, huku ule upande wa nne akiuacha kwa kuwa wenzake walikuwa upande huo na kama kungelikuwa na tatizo, wangelimtaarifu kupitia vifaa maalumu walivyofunga masikioni mwao. Alizunguka kwa umakini mkubwa lakini hadi anamaliza, hakuwa amefanikiwa kukutana na kitu chochote chenye kutia shaka ijapokuwa, akili yake ilikuwa inaamini kabisa kuna kitu hakikuwa sawa.
Wazo moja likampitia kichwani na haraka aliamua kulifanyia kazi. Aliachana na hizo pande na badala yake aliamua kuelekea upande ambao wenzake waliamua kuutumia kama eneo lao la kimkakati. Aliamua kulikagua eneo hilo na kisha angelirejea kwa wenzake.
Lakini jambo moja ambalo hakujua ni kuwa, eneo alilokuwa anafikiria kuliendea tayari lilikuwa limeshasheheni wenyeji kutisja wa kutisha. Hilo hakujua na wenzake pia hawakujua tayari wameshapokelewa na mwenyeji mwenye macho na mikono ya chupa.
Msitu wa Chipa uligeuzwa duka la roho katikati ya giza nene.