Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,983
- 10,804
Riwaya: MUME GAIDI
Mwandishi: ATUGANILE MWAKALILE
Imeletwa kwenu na: BURE SERIES
SEHEMU YA 1
Ilikuwa ni kipindi cha mvua za masika, na siku hiyo mvua ilikuwa inanyesha. Kijana Patrick alikuwa ndani na mama yake bi. Deborah, hoja ya Patrick ilikuwa ni moja tu kuhusu baba yake mzazi.
PATRICK: Mama, hivi kwanini hutaki kuniambia ukweli kuhusu baba yangu.
DEBORAH: Mwanangu ni historia ndefu sana, tafadhari usinikumbushe.
PATRICK: Mama, mimi ni kijana mkubwa sasa. Niambie ukweli, baba yangu ni nani? Hayo machungu yako, machungu gani? Ninachotaka mimi ni kumjua baba yangu tu.
DEBORAH: Hii ndio tabu yenu watoto wa kiume.
Mara Patric akainuka na kuelekea nje.
DEBORAH: Jamani mwanangu, unaenda wapi na mvua hii?
PATRICK: Kutembea.
DEBORAH: Kutembea na mvua utalowa mwanangu, halafu humu ndani hakuna hata mwamvuli.
PATRICK: Unanijali eeh!!
DEBORAH: Ndio nakujali mwanangu.
PATRICK: Kama kweli unanijali, ungenitajia baba yangu ni nani.
DEBORAH: Siwezi mwanangu siwezi.
PATRICK: Ndio hapo unaponikera mama, haya bhana badae.
DEBORAH: Jamani Patrick.
Patrick hakujali chochote, alitoka nje na kuondoka.
Deborah alikuwa na siri nzito juu ya mtoto wake Patrick, hakutaka kuusema ukweli kwa kipindi hicho, alijua wazi ukweli huo utamsononesha sana Patrick.
Deborah akiwa amesimama mlangoni na kumuangalia mwanae akitokomea kwenye mvua, mara akamuona dada yake aliyeitwa Marium akiwa anakuja na mwamvuli.
MARIUM: Vipi? Mbona umesimama mlangoni halafu namuona Patrick akitokomea mvuani.
DEBORAH: Dada we acha tu, karibu ndani kwanza.
Akamkaribisha dada yake ndani na kuzungumza nae hili na lile. Akamueleza na nia ya Patrick hadi kuondoka vile kwa hasira.
MARIUM: Debo, hunabudi kumueleza Patrick ukweli. Watoto wa kiume na baba zao mdogo wangu.
DEBORAH: Mmmh!!
MARIUM: Mbona unaguna sasa? Si umwambie tu Patrick kama baba yake ni Jumanne, na aende akamtafute huko Dar.
DEBORAH: Dada, hujui chochote kuhusu mimi na Patrick.
MARIUM: Inamaana hata Jumanne si baba yake? Ulizaa na mwanaume mwingine Deborah, sasa nimeelewa sababu kubwa ya Jumanne kukuacha wewe.
DEBORAH: Dada, usilolijua ni sawa na usiku wa giza.
MARIUM: Sawa, endelea kukaa na siri yako moyoni, nadhani utaitoa kaburini siku utapokufa.
DEBORAH: Jamani dada!!
MARIUM: Ndio hivyo Deborah.
Wakaongea mambo mengine ila Deborah akaendelea kubaki na siri yake moyoni.
Badae, mwanae Patrick alirudi akiwa amelewa sana kwahiyo akapitiliza kulala.
Kesho yake asubuhi, Patrick alikuta mama yake akiwa amemuandalia supu, baada ya kunywa alirudi na kukaa tena na mama yake kumuuliza vizuri.
PATRICK: Mama ni kweli unanijali sana, tena unanipenda sana ila ingekuwa vyema kama ningemjua na baba yangu.
DEBORAH: Patrick mwanangu, ni historia ndefu sana kuhusu baba yako.
PATRICK: Jana nilienda kwa mamdogo Anna, nae ameniambia kuwa inawezekana baba yangu akawa Jumanne. Je huyo Jumanne ni nani? Na je ni kweli ndiye baba yangu?
DEBORAH: Hapana Patrick, Jumanne si baba yako mwanangu.
PATRICK: Jamani mama, sasa baba yangu ni nani? Je ni yule tuliyekuwa tunaishi nae Arusha bwana Maiko?
DEBORAH: Hata Maiko si baba yako.
PATRICK: Sasa baba yangu mimi ni nani? Nahitaji kujua mama, nahitaji kutambua. Hata kama ulibakwa hadi kunipata mimi, niambie tu mama.
DEBORAH: Unapofikia ni pabaya huko Patrick, mi sijawahi kubakwa.
PATRICK: Sasa mbona baba yangu humjui?
DEBORAH: Ipo siku nitakwambia ukweli wote, ila sio sasa.
PATRICK: Mama, ni kweli umenisomesha. Umenilea vyema ila kumbuka kwamba kumjua baba yangu ni haki yangu, haijalishi alikutenda mambo gani mama ila nina haki ya kumjua.
DEBORAH: Sawa mwanangu, nitakueleza tu. Ipo siku utaujua ukweli wote Patrick.
Patrick alijiona hana umuhimu wa kuendelea kuishi nyumbani tu bila ya kufanya kazi maalum. Ikabidi atafute kazi na kuamua kupanga safari ya kwenda kwani alipata kazi kwenye mkoa wa Morogoro.
Patrick akasafiri bila ya kumuaga mama yake, kwa madai yake kuwa amempa adhabu mama yake ya kutomtajia baba yake.
Wakiwa njiani, basi lao likapata ajali kwani liligongwa na lori na kupinduka. Watu waliumia sana, haikuwezekana kuendelea na safari tena.
Majeruhi wakabebwa na kupelekwa hospitali, baada ya matibabu Patrick akaamua kurudi kwa mama yake. Kwakweli Deborah alimuhurumia sana mwanae.
PATRICK: Naomba unisamehe mama, najua yote hii ni laana ya kuondoka bila ya kukuaga mama yangu.
DEBORAH: Usijari mwanangu, cha muhimu hapa ni uzima wako tu mwanangu.
Patrick aliendelea kujiuguza mpaka pale alipopona kabisa. Ila ile kazi ya Morogoro haikuwepo tena kwani muda mrefu uliku umepita.
Patrick akaamua kutafuta kazi tena, na safari hii akapata kazi mkoani Arusha. Akahitajika kwenda huko, akaamua kumuaga mama yake.
DEBORAH: Ila mwanangu, huko Arusha mi sikuamini kabisa.
PATRICK: Kwanini mama?
DEBORAH: Sababu ya Maiko.
PATRICK: Mama usijali, kwanza hata sipakumbuki anapoishi huyo bwana. Siwezi kwenda mama.
DEBORAH: Najua ulimzoea Maiko kama baba yako, ila Maiko ni mtu asiyefaa kabisa mwanangu.
PATRICK: Mama, tumeondoka Arusha tangia nikiwa na miaka sita. Siwezi kumjua tena huyo Maiko, wala yeye hawezi kunikumbuka mama.
DEBORAH: Nakuhurumia mwanangu, ukimuona mkimbie kabisa. Atakufundisha tabia mbaya. Ila nakuombea kheri mwanangu.
PATRICK: Sawa mama usijali, huko Arusha nitafanya kilichonipeleka tu. Na pia nitakuwa nakuja huku Mwanza kukuona mama yangu.
DEBORAH: Sawa mwanangu, ila kuwa makini sana na Maiko, ni mtu hatari sana huyo.
PATRICK: Sawa mama, ingawa nae sijui alikufanya nini?
DEBORAH: Hiyo ni siri yangu mwanangu, ila jitenge nae.
PATRICK: Sawa mama nimekuelewa.
DEBORAH: Nakupa baraka zangu zote mwanangu.
PATRICK: Asante mama, najua nitakaporudi utakuwa tayari kunitajia baba yangu.
DEBORAH: Mmh na wewe, kila mara baba baba kama wimbo wa Taifa!
PATRICK: Ni wajibu wangu kumjua mama.
DEBORAH: Sawa mwanangu, ipo siku nitakwambia ukweli.
Deborah na mwanae wakaongea mengi kwani kesho yake asubuhi ndio ilikuwa siku ya safari, siku ya Patrick kuiacha Mwanza na kwenda Arusha kikazi.
Alfajiri na mapema, Patrick akasindikizwa na mama yake hadi kituo cha mabasi na kumuacha Patrick akiwa ndani ya basi akielekea Arusha.
Safari ilikuwa ni ndefu sana, hadi muda ambao Patrick alifika Arusha alijihisi akiwa na uchovu mwingi. Wazo pekee alilopata kichwani kwa muda huo ni kutafuta nyumba ya wageni ambayo atapumzikia siku hiyo.
Akiwa pale stendi, mara kuna mtu akamshika bega, Patrick alipogeuka akapatwa na kitu cha ajabu sana.
Mwandishi: ATUGANILE MWAKALILE
Imeletwa kwenu na: BURE SERIES
SEHEMU YA 1
Ilikuwa ni kipindi cha mvua za masika, na siku hiyo mvua ilikuwa inanyesha. Kijana Patrick alikuwa ndani na mama yake bi. Deborah, hoja ya Patrick ilikuwa ni moja tu kuhusu baba yake mzazi.
PATRICK: Mama, hivi kwanini hutaki kuniambia ukweli kuhusu baba yangu.
DEBORAH: Mwanangu ni historia ndefu sana, tafadhari usinikumbushe.
PATRICK: Mama, mimi ni kijana mkubwa sasa. Niambie ukweli, baba yangu ni nani? Hayo machungu yako, machungu gani? Ninachotaka mimi ni kumjua baba yangu tu.
DEBORAH: Hii ndio tabu yenu watoto wa kiume.
Mara Patric akainuka na kuelekea nje.
DEBORAH: Jamani mwanangu, unaenda wapi na mvua hii?
PATRICK: Kutembea.
DEBORAH: Kutembea na mvua utalowa mwanangu, halafu humu ndani hakuna hata mwamvuli.
PATRICK: Unanijali eeh!!
DEBORAH: Ndio nakujali mwanangu.
PATRICK: Kama kweli unanijali, ungenitajia baba yangu ni nani.
DEBORAH: Siwezi mwanangu siwezi.
PATRICK: Ndio hapo unaponikera mama, haya bhana badae.
DEBORAH: Jamani Patrick.
Patrick hakujali chochote, alitoka nje na kuondoka.
Deborah alikuwa na siri nzito juu ya mtoto wake Patrick, hakutaka kuusema ukweli kwa kipindi hicho, alijua wazi ukweli huo utamsononesha sana Patrick.
Deborah akiwa amesimama mlangoni na kumuangalia mwanae akitokomea kwenye mvua, mara akamuona dada yake aliyeitwa Marium akiwa anakuja na mwamvuli.
MARIUM: Vipi? Mbona umesimama mlangoni halafu namuona Patrick akitokomea mvuani.
DEBORAH: Dada we acha tu, karibu ndani kwanza.
Akamkaribisha dada yake ndani na kuzungumza nae hili na lile. Akamueleza na nia ya Patrick hadi kuondoka vile kwa hasira.
MARIUM: Debo, hunabudi kumueleza Patrick ukweli. Watoto wa kiume na baba zao mdogo wangu.
DEBORAH: Mmmh!!
MARIUM: Mbona unaguna sasa? Si umwambie tu Patrick kama baba yake ni Jumanne, na aende akamtafute huko Dar.
DEBORAH: Dada, hujui chochote kuhusu mimi na Patrick.
MARIUM: Inamaana hata Jumanne si baba yake? Ulizaa na mwanaume mwingine Deborah, sasa nimeelewa sababu kubwa ya Jumanne kukuacha wewe.
DEBORAH: Dada, usilolijua ni sawa na usiku wa giza.
MARIUM: Sawa, endelea kukaa na siri yako moyoni, nadhani utaitoa kaburini siku utapokufa.
DEBORAH: Jamani dada!!
MARIUM: Ndio hivyo Deborah.
Wakaongea mambo mengine ila Deborah akaendelea kubaki na siri yake moyoni.
Badae, mwanae Patrick alirudi akiwa amelewa sana kwahiyo akapitiliza kulala.
Kesho yake asubuhi, Patrick alikuta mama yake akiwa amemuandalia supu, baada ya kunywa alirudi na kukaa tena na mama yake kumuuliza vizuri.
PATRICK: Mama ni kweli unanijali sana, tena unanipenda sana ila ingekuwa vyema kama ningemjua na baba yangu.
DEBORAH: Patrick mwanangu, ni historia ndefu sana kuhusu baba yako.
PATRICK: Jana nilienda kwa mamdogo Anna, nae ameniambia kuwa inawezekana baba yangu akawa Jumanne. Je huyo Jumanne ni nani? Na je ni kweli ndiye baba yangu?
DEBORAH: Hapana Patrick, Jumanne si baba yako mwanangu.
PATRICK: Jamani mama, sasa baba yangu ni nani? Je ni yule tuliyekuwa tunaishi nae Arusha bwana Maiko?
DEBORAH: Hata Maiko si baba yako.
PATRICK: Sasa baba yangu mimi ni nani? Nahitaji kujua mama, nahitaji kutambua. Hata kama ulibakwa hadi kunipata mimi, niambie tu mama.
DEBORAH: Unapofikia ni pabaya huko Patrick, mi sijawahi kubakwa.
PATRICK: Sasa mbona baba yangu humjui?
DEBORAH: Ipo siku nitakwambia ukweli wote, ila sio sasa.
PATRICK: Mama, ni kweli umenisomesha. Umenilea vyema ila kumbuka kwamba kumjua baba yangu ni haki yangu, haijalishi alikutenda mambo gani mama ila nina haki ya kumjua.
DEBORAH: Sawa mwanangu, nitakueleza tu. Ipo siku utaujua ukweli wote Patrick.
Patrick alijiona hana umuhimu wa kuendelea kuishi nyumbani tu bila ya kufanya kazi maalum. Ikabidi atafute kazi na kuamua kupanga safari ya kwenda kwani alipata kazi kwenye mkoa wa Morogoro.
Patrick akasafiri bila ya kumuaga mama yake, kwa madai yake kuwa amempa adhabu mama yake ya kutomtajia baba yake.
Wakiwa njiani, basi lao likapata ajali kwani liligongwa na lori na kupinduka. Watu waliumia sana, haikuwezekana kuendelea na safari tena.
Majeruhi wakabebwa na kupelekwa hospitali, baada ya matibabu Patrick akaamua kurudi kwa mama yake. Kwakweli Deborah alimuhurumia sana mwanae.
PATRICK: Naomba unisamehe mama, najua yote hii ni laana ya kuondoka bila ya kukuaga mama yangu.
DEBORAH: Usijari mwanangu, cha muhimu hapa ni uzima wako tu mwanangu.
Patrick aliendelea kujiuguza mpaka pale alipopona kabisa. Ila ile kazi ya Morogoro haikuwepo tena kwani muda mrefu uliku umepita.
Patrick akaamua kutafuta kazi tena, na safari hii akapata kazi mkoani Arusha. Akahitajika kwenda huko, akaamua kumuaga mama yake.
DEBORAH: Ila mwanangu, huko Arusha mi sikuamini kabisa.
PATRICK: Kwanini mama?
DEBORAH: Sababu ya Maiko.
PATRICK: Mama usijali, kwanza hata sipakumbuki anapoishi huyo bwana. Siwezi kwenda mama.
DEBORAH: Najua ulimzoea Maiko kama baba yako, ila Maiko ni mtu asiyefaa kabisa mwanangu.
PATRICK: Mama, tumeondoka Arusha tangia nikiwa na miaka sita. Siwezi kumjua tena huyo Maiko, wala yeye hawezi kunikumbuka mama.
DEBORAH: Nakuhurumia mwanangu, ukimuona mkimbie kabisa. Atakufundisha tabia mbaya. Ila nakuombea kheri mwanangu.
PATRICK: Sawa mama usijali, huko Arusha nitafanya kilichonipeleka tu. Na pia nitakuwa nakuja huku Mwanza kukuona mama yangu.
DEBORAH: Sawa mwanangu, ila kuwa makini sana na Maiko, ni mtu hatari sana huyo.
PATRICK: Sawa mama, ingawa nae sijui alikufanya nini?
DEBORAH: Hiyo ni siri yangu mwanangu, ila jitenge nae.
PATRICK: Sawa mama nimekuelewa.
DEBORAH: Nakupa baraka zangu zote mwanangu.
PATRICK: Asante mama, najua nitakaporudi utakuwa tayari kunitajia baba yangu.
DEBORAH: Mmh na wewe, kila mara baba baba kama wimbo wa Taifa!
PATRICK: Ni wajibu wangu kumjua mama.
DEBORAH: Sawa mwanangu, ipo siku nitakwambia ukweli.
Deborah na mwanae wakaongea mengi kwani kesho yake asubuhi ndio ilikuwa siku ya safari, siku ya Patrick kuiacha Mwanza na kwenda Arusha kikazi.
Alfajiri na mapema, Patrick akasindikizwa na mama yake hadi kituo cha mabasi na kumuacha Patrick akiwa ndani ya basi akielekea Arusha.
Safari ilikuwa ni ndefu sana, hadi muda ambao Patrick alifika Arusha alijihisi akiwa na uchovu mwingi. Wazo pekee alilopata kichwani kwa muda huo ni kutafuta nyumba ya wageni ambayo atapumzikia siku hiyo.
Akiwa pale stendi, mara kuna mtu akamshika bega, Patrick alipogeuka akapatwa na kitu cha ajabu sana.