Riwaya: Mtuhumiwa

SEHEMU YA KUMI NA SITA

Alitupa tena macho upande wa pili wa ile barabara, na kuna gari jingine likawa linapita hivyo hakumuona yule jamaa mwenye tai mpaka lilipopita, ambapo alimuona yule jamaa akiinuka kutoka pale alipokuwa amechutama. Mara moja yule mtu mrefu mwenye koti refu aligundua kitu kisicho cha kawaida. Mkono wa kulia wa yule mtu mwenye tai ulikuwa unatokea nyuma ya bati linalofunika tairi la mbele la gari lile!
Ala!
Yule mtu mwenye tai alisimama kwa sekunde chache zaidi kama mtu anayetaka kuvuka barabara. Kisha taratibu alitumbukiza mikono yake kwenye mifuko ya suruali yake ya buluu, akageuka nyuma taratibu kuangalia upande ambao Jaka na Clara wangetokea, halafu aligeuka tena taratibu na kutazama kule ambapo ilipoegeshwa ile Raum nyeupe.
Hapo yule mtu mrefu mwenye koti refu alijua kuwa yule jamaa alikuwa ni mtaalamu kwenye fani yake kwani alikuwa akigeuka kwa namna ambayo kwa mtu mwingine yeyote angeonekana kuwa ni mtu wa kawaida aliyekuwa akimsubiri rafiki au jamaa aliyechelewa miadi. Katika kugeuka kwake, alikuwa akizungusha mwili wake kutokea kiunoni kuja juu, na wakati akifanya hivyo alikuwa akitupa tupa miguu yake mbele, mara moja au mbili akijaribu kupiga teke vijiwe vidogo vilivyokuwa pale barabarani. Hii ilileta picha kuwa alikuwa akimsubiri mtu, na subira yake ilikuwa inaelekea ukingoni.
Haya yote yaliendelea kutazamwa kwa utulivu wa hali ya juu na yule bwana mwenye kofia pana, kwani naye, kama yule mtu mwenye tai ng'ambo ya pili ya barabara, alikuwa ni mtaalamu kwenye fani yake. Mara ile yule mtu mwenye tai aliinua mkono wake wa kulia na kuangalia saa. Mtu mwenye pama alitabasamu, kwani alielewa ni nini kitafuata baada ya kitendo kile. Yule bwana mwenye tai alishusha mkono wake na kuanza kuvuka barabara taratibu kuelekea kule ilipokuwa imeegeshwa ile Raum.
Jamaa mwenye kofia pana alijua kuwa hakuwa peke yake aliyekuwa akimvizia Jaka siku ile. Yeye
binafsi alijua ni kwa nini alikuwa anamfuatilia Jaka siku ile. Tatizo ni wale jamaa wengine. Wanahusiana vipi na Jaka? Kwa nini hawakutokea siku zote wakaamua kutokea leo? Na jambo alilofanya yule bwana mwenye tai pale kwenye gari la akina Jaka....
Maswali haya yalipita kichwani mwake huku akijaribu kuoanisha matendo ya yule mtu mwenye tai na uwepo wa akina Jaka kwenye eneo lile. Jibu la jumla alilolipata ni kwamba jambo baya sana lilikuwa linaandaliwa...limeandaliwa pale.
Alibaki pale pale alipokuwa amesimama. Jamaa aliingia ndani ya ile Raum na kutulia kando ya dereva. Kinyume na matarajio ya yule bwana mwenye pama, ile Raum iliendelea kubai pale pale, haikuondoka, Aliitazama ile gari na kujikuta akizikariri namba za usajili za gari lile.
Ni jambo gani limefanyika pale?
Kwa nini?
Hakupata jibu. Dakika zilisogea. Nusu saa ilipita. Dakika aribaini na tano. Hakuna badiliko. Ile Raum bado ilikuwa imeegeshwa pale pale na wale watu wawili wakiwa ndani yake.
Sasa wanasubiri nini? Yule mtu alipitisha mkoni chini ya ile Vitara...kwa nini...?
Wakati akiendelea kujiuliza maswali hayo, alizidi kuchanganyikiwa pale alipowaona Jaka na Clara wakitoka nje ya eneo lile la Nyerere Square kuelekea kwenye gari lao huku wakiongea na kucheka kwa furaha, Clara akiwa amebeba kifurushi kidogo bila shaka cha vipochopocho walivyonunua eneo lile.. Aligeukia tena kule kwenye ile Raum. Dereva wa ile gari alikuwa ametoa kichwa nje ya dirisha akiangalia kule ambapo akina Jaka walikuwako. Na hata pale alipokuwa akimtazama, alimuona yule dereva wa Raum akiinamisha uso kutazama saa yake na kuuinua tena uso kuwatazama akina Jaka.
Ina maana gani?
Kama kuna jambo lolote lililoandaliwa pale, basi sasa ndio ulikuwa wakati wa jambo hilo kutokea. Akili ilimwenda mbio...
Kule upande wa pili wa barabara Jaka alikuwa anazunguka mbele ya ile Vitara ili aende upande wa dereva ambao ulikuwa upande wa barabarani. Clara alikuwa amesimama upande wa mlango wa abiria wa gari lile....
Ni nini kitatokea pale?
Na mara alikumbuka.
Ilimjia kichwani mwake kwamba katika nukta moja ya sekunde baina ya kupita gari la kwanza na la pili aliweza kumuona yule mtu mwenye tai akiwa ameinama pale chini, na katika nukta ile macho yake yalikuwa yanautafuta mkono wa kulia wa yule mtu, kwai ilimjia kama anayefunga kamba kw amkono mmoja tu...mkono wa kushoto. Katika nukta moja ile, alihisi aliuona ule mkono wa kulia wa yule mtu ukiwa umeshika tairi la mbele la lile gari...au ulikuwa umefichwa na bati la gari lile linalofunika tairi...?
Aligeuka tena kushoto kwake.
Ile Raum ilikuwa inaondoka taratibu kutoka eneo lile; na sasa alimuona yule mtu mwenye tai, akiwa ndani ya gari akigeuka kutazama pale lilipokuwa gari la akina Jaka. Naye upesi aligeuka tena kutazama kule walipokuwa akina Jaka.
Jaka alikuwa ameegemeza sehemu ya mbele ya mwili wake kwenye boneti la gari lile akipokea funguo za gari kutoka kwa Clara aliyekuwa upande wa pili wa gari lile.
Akili ilizidi kumzunguka jamaa mwenye pama.
Ilikuwa haileti maana....kwa nini yule mtu, ambaye kwa hakika alikuwa akiwasubiri akina Jaka, aamue kuondoka baada ya watu aliokuwa akiwasubiri kutokea...bila ya kuongea nao chochote? Au...?
Hakufikiri zaidi.
Alikurupuka na kutoka kasi kukimbilia kule walipokuwa akina Jaka huku akimwita Jaka kwa kelele na akimpungia mikono ili amuone.
"Jaka...! Jakaaaaaaa! Toka hapoooo....tokeniiiih! Kimbienii....ondokaaaaa...uppeeeesssss!" Yule mtu alikuwa akipiga kelele huku akivuka barabara kuelekea kule walipokuwa akina Jaka.
Jaka aligeuka kwa mshituko aliposikia jina lake likiitwa kwa kelele hadharani. Na hata pale alipogeuka alimuona yule mtu mwenye koti refu akiingia barabarani huku akimkimblia bila kujali magari. Gari moja lilifunga breki kali na kuserereka huku tairi zake zikitoa sauti kali ya msuguano na lami huku honi kali ikirindima. Lile gari lilikuwa linaelekea kumgonga lakini yule mtu aliweka mkono wake wa kulia kwenye boneti la lile gari na kujisereresha juu ya boneti lile na kudondokea upande wa pili wa gari ile. Watu walioshuhudia tukio lile walipiga kelele za woga na mshituko juu ya kitendo kile hali wengine wakibaki midomo wazi na kujishika vichwa. Jamaa hakujali. Aliendelea kuwakimbilia akina Jaka huku akiwapigia kelele kama mwehu.
"Ondoka wewweeeh....! Kimbia...! You are going to die gaddemmiiiitt! Toka...! Hilo gariiii!"
Mara moja alimtambua John Doe. Alimuona alivyokuwa akiwaendea mbio huku akipunga mikono hewani na akipiga mayowe kama mwehu, na alishuhudia kwa mshituko jinsi alivyoruka juu ya boneti la gari lililokuwa kwenye mwendo wa kasi. Alipoona bado John Doe anazidi kuwakimbilia namna ile baada ya kukoswa kugongwa na gari, alijua ni lazima afanye kitu. Alisikia maneno yaliyokuwa yakitoka kinywani mwa yule mtu na aliiona hofu iliyojianika usoni kwa yule jamaa wakati akiwakimbilia namna ile. Jamaa alikuwa hafanyi utani.
Kutokea kule alipokuwa Jaka aligeuka na kuudaka mkono wa Clara na kumvuta pembeni huku na yeye akijisukuma kutoka ubavuni mwa lile gari kuelekea mbele ya lile gari. Clara alipiga kelele za hamaniko bila ya kuelewa kilikuwa kinatokea. Jaka alimkamata kiuno na kujitahidi kumvutia pembeni, mbali na lile gari lao. Walipepesuka vibaya huku raia waliokuwa eneo lile nao wakipiga kelele za kutoelewa.
Sasa John Doe alikuwa karibu sana na walipokuwa wakipepesukia. Jaka alijigeuza mzima mzima na kumkabili yule jamaa mwenye ngumi nzito huku akiwa amemkinga Clara kwa mgongo wake. Alikuwa akijitahidi kuongeza umbali baina yao na John Doe kwa kurudi nyuma huku akimsukuma Clara kwa nyuma. Watu wengi waliokuwa katika eneo lile walitawanyika mbio kila mmoja kwa upande wake bila ya kujua ni nini hasa walichokuwa wanakikimbia.
"Hilo gari hilo weweee...! Gariii! Kaa mbali naloo...ebbo! TOKA HAPOOO! Kimbieniii, Pummm-bbaaavvvv!" John Doe aliendelea kubwata huku akiwakimbilia. Jaka aliduwaa kidogo, na hapo John Doe alienda hewani mzima mzima akiwa ametanguliza mikono yake na kumkumba Jaka kwa kishindo, bega lake la kushoto likijikita tumboni kwa Jaka na wakati huo huo mkono wake wa kushoto uking'ang'ania kiunoni Clara aliyekuwa nyuma ya Jaka. Kwa wahka Jaka alirusha ngumi kwa mkono wake wa kushoto akiamini kuwa jamaa alikuwa anashambulia, lakini yule jamaa jabari aliipangua ngumi ile na hapo hapo akamdaka mkono ule kwa mkono wake wa kulia na wote watatu wakawa wanaelekea kupiga mweleka mzito.
Jaka hakuwa na la kufanya zaidi ya kung'ang'ania koti la yule mtu kwa mgongoni kwa mkono wake wa kulia. Nyuma yake, Clara akajigonga kisigino kwenye ukingo wa barabara na kupoteza kabisa mwelekeo. Alibaki akimng'ang'ania Jaka mgongoni huku akipiga kelele zisizoeleweka.
Msukumo wa yule mtu alivyowaparamia, na kujikwaa kwa Clara, viliwafanya wote watatu waruke hewani na kujibwaga bila mpangilio juu ya meza za wachuuzi wachache waliokuwa kando ya barabara ile. Mayowe yalizagaa wakati wao wakijipigiza chini kwenye vumbi wakisambaratisha meza na bidhaa zilizokuwa juu yake huku wale wachuuzi wakipiga mayowe na kukimbia hovyo. Jaka alikuwa akijaribu kujiinua kutoka pale chini akiwa amemlalia Clara kwa mgongo wake huku yule jamaa akiwa amemlalia kwa tumbo lake juu yake. Lakini kila alivyojaribu kujiinua ndivyo yule jamaa alivyozidi kumkandamiza chini kwa nguvu na ndivyo walivyozidi kumwelemea Clara aliyekuwa chini kabisa akipiga kelele vibaya sana.
Na mara hiyo hiyo mlipuko mkubwa sana ulisikika.
Jaka akiwa amekandamizwa chini na yule mtu aliweza kushuhudia kwa mshituko na kutoamini kukubwa kabisa jinsi gari lao likipasuka kuanzia sehemu ya mbele sanjari na mlipuko ule. Moto mkubwa uliruka hewani na aliliona lile gari likinyanyuliwa zima zima kutoka pale lilipokuwa limeegeshwa na kutupwa hewani huku likisambaratika vipande vipande. Vipande vya vioo vilirushwa huku na huko na kurudi ardhini kama matone ya mvua, vikijeruhi watu waliokuwa wamezagaa eneo lile. Tairi moja lilichomoka na kutupwa angani huku likiwaka moto na kufuka moshi.
Yote haya Jaka aliyaona ndani ya sekunde moja tu.
Macho yalimtoka pima na kinywa kilimchanua pasi sauti kutoka.
Mayowe, vilio na heka heka vilitawala eneo la Nyerere Square asubuhi ile. Watu walikibia huku na kule wakijaribu kuokoa maisha yao bila ya kujua ni wapi hasa palikuwa salama. Katika kelele zao hizo, Jaka alimsikia Clara akipiga mayowe ya woga na maumivu kutokea nyuma yake.
Clara likuwa amelalia mgongo pale chini. Juu alikuwa amelaliwa na mgongo wa Jaka. Juu ya Jaka John Doe alikuwa amelalia tumbo uso wake akiwa ameuficha upande wa kulia wa shingo ya Jaka huku akijikinga kichwa chake kwa mkono wake wa kushoto. Uso wa Jaka ulitokeza juu ya bega la kushoto la yule mtu ukitazama angani.
Na mara nyingine tena kilisikika kishindo kingine kilichotokana na mabaki ya lile gari kujibwaga tena ardhini katikati ya barabara na kulalia ubavu huku likiendelea kuteketea kwa moto. Watu walianza kulikimbilia na kulizunguka, hali wengine wakiwazunguka akina Jaka waliojirundika pale chini.
John Doe alijiinua kutoka pale chini, na haraka Jaka aliyechanganyikiwa naye akakurupuka kutoka pale chini. Alipepesuka na kuanguka tena chini. John Doe alimsaidia Clara kuinuka kutoka pale chini na kumshikilia asianguke kama Jaka. Uso wake ulionekana kutulia na kutokuwa na woga hata kidogo. Hatimaye Jaka aliinuka na kujivuta mpaka pale alipokuwa amesimama Clara huku macho yakiwa yamemtoka pima.
"Oh! Jaka...Jaka...tungekufa leo dear!" Clara alibwabwaja huku akilia. Jaka alimkumbatia kwa nguvu huku akimpigapiga mgongoni.
"Ni kweli. Lakini bado tunapumua...hatujafa...." Jaka alimliwaza huku macho yake yakiangaza huku na kule akimtafuta yule mtu mwenye koti refu ambaye alionekana kuyeyuka kama upepo mara Jaka alipomfikia Clara pale walipokuwa wamesimama. Kwa hakika yule mtu alikuwa amewaokoa kutokana na kifo kibaya sana, na sasa jumla ya maswali yaliyopita kichwani mwake ilikuwa haisemeki. Swali moja lilibaki kuwa kubwa kuliko yote.
Kwa nini?
"Imekuwaje...? Nini kimetokea...?" Alijikuta akibwabwaja peke yake huku akiendelea kutembeza macho kila kona bila ya mafanikio, kundi la mashuhuda liliowazunguka ulilifanya zoezi la kumuona yule mkombozi wao asiyetarajiwa kuwa gumu sana.
"Mlitegewa bomu....na wewe ndiye uliyekusudiwa." Sauti ilimjibu kwa upole kutokea nyuma yake. Aligutuka huku akigeukia kule sauti ilipotokea, na kumuona yule mtu mwenye koti refu. Alikuwa amesimama huku macho yake akiwa ameyaelekeza kule lilipokuwa linateketea lile gari.Yaani jamaa alikuwa amemjibu bila ya kumtazama na hakutaka kumtazama.
"Lakini wewe...? Kwa nini umeni...umetu....mbona... Ah! We' nani kwani...?" Jaka alibwabwaja huku akimkodolea macho yule mtu na akishindwa kabisa kuzipangilia sentesi zake. Mara ving'ora vya magari ya polisi vilisikika, na muda mfupi baadaye magari matatu ya polisi yalifika eneo lile kwa makeke. Askari wa jeshi la polisi waliruka kutoka kwenye magari yale na kuzidi kuwatia hofu wananchi waliojazana eneo lile.

ITAENDELEA
 
SEHEMU YA KUMI NA SABA





Aligutuka huku akigeukia kule sauti ilipotokea, na kumuona yule mtu mwenye koti refu. Alikuwa amesimama huku macho yake akiwa ameyaelekeza kule lilipokuwa linateketea lile gari.Yaani jamaa alikuwa amemjibu bila ya kumtazama na hakutaka kumtazama.
"Lakini wewe...? Kwa nini umeni...umetu..
..mbona... Ah! We' nani kwani...?" Jaka alibwabwaja huku akimkodolea macho yule mtu na akishindwa kabisa kuzipangilia sentesi zake. Mara ving'ora vya magari ya polisi vilisikika, na muda mfupi baadaye magari matatu ya polisi yalifika eneo lile kwa makeke. Askari wa jeshi la polisi waliruka kutoka kwenye magari yale na kuzidi kuwatia hofu wananchi waliojazana eneo lile.
Kwa sauti ya chini huku akiendelea kutazama kule kwenye moto John Doe alimwambia:
"Utakapoulizwa na hao polisi, mimi na wewe hatujaonana. Hujui ni nani aliyekuokoa...t
utaonaoena tena." John Doe alimnong’oneza huku bado akiwa ameelekeza uso wake kule kwenye lile gari lililokuwa likiteketea kwa moto. Kisha aligeuka na kujichanganya kwenye umati wa watu.
Jaka alibaki akiwa ameduwaa. Wala hakugeuka kutazama ni wapi alikuwa akielekea yule jamaa. Macho yake yalikuwa yanatazama mbele ambako askari wawili walikuwa wakielekea pale alipokuwa amesimama na Clara.
"Niachie mimi nijibu maswali yote." Alimnong'oneza Clara ambaye hata hivyo hakuwa katika hali ya kuongea hata kidogo.
"Nyie ndio wenye lile gari?" Mmoja wa wale askari aliuliza mara walipowafikia. Jaka aliafiki kwa kichwa.
"Samahani, naomba tungozane." Yule askari aliwaambia.
Bila ya kutia neno, Jaka alimshika mkono Clara na kumuongoza kuwafuata wale askari. Mmoja wa wale askari alikuwa akiwapangua watu waliojaa eneo lile ili kuwapa njia ya kupita. Walielekezwa kuingia ndani ya gari la polisi aina ya Volkswagen Golf, na hapo hapo hilo gari liliondolewa kwa kasi kutoka eneo lile.
Njia nzima kuelekea huko alipokuwa anapelekwa na wale wana usalama Jaka alikuwa amezongwa na mawazo kuhusu yule mtu wa ajabu aliyeokoa maisha yao kutokana na mlipuko ule. Clara alikuwa akiendelea kulia taratibu akiwa ameegemeza kichwa begani kwake, naye alikuwa akimpapasa kichwa kile kwa kumliwaza huku akili yake ikilitafakari lile tukio.
Lile bomu alikuwa ametegewa yeye, na kama si John Doe kujitolea kuwatahadharisha namna ile, ni wazi yeye na Clara wangekuwa marehemu muda ule.
Sasa ni nani anayetaka yeye afe?
Kwa nini atake kumuua sasa hivi na si wakati wowote kabla ya sasa?
Lile bomu lilikuwa limetegwa saa ngapi?
Ni nani aliyelitega?
Maswali haya yalikuwa yakizunguka tu akilini mwake bila ya kujua ni wapi walipokuwa wakipelekwa na wale wana usalama.
Na wala hakujali.
Bila shaka yule mtu aliyewaokoa na kifo kutokana na bomu lile, ambaye amekuwa akifuatilia nyendo zake kwa siri, atakuwa na ufumbuzi kuhusu mengi ya maswali haya.
Lakini nyuma kabisa ya akili yake, Jaka alijua kuwa tukio lile lilikuwa ni muendelezo wa matukio mengine aliyokutana nayo huko nyuma na ambaya alitamani yawe yamefutika maishani mwake.
Ule mlipuko wa bomu ilikuwa unamuanikia wazi ukweli kuwa hakika lile jinamizi la matukio mabaya aliyokutana nayo akiwa jijini Dar sasa lilikuwa limemfuata rasimi pale Dodoma.
Ni ukweli mchungu sana...na usiokwepeka.
Je niko tayari kuukabili ukweli huu?
Eee Mungu! Hebu nisaidie mja wako...!
Kitabu Cha Pili:
Tuhuma-Mwaka Mmoja Uliopita
Nipashe, Novemba 18
Dar es Salaam
Msichana mmoja,mwanafunzi wa mwaka wa kwanza katika Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam jijini,alifariki dunia hapo jana baada ya kumeza vidonge vingi aina ya Chloroquine.
Msichana huyo aliyejulikana kwa jina la
Mwahija Mlawa (21) alikutwa akiwa amekufa chumbani kwake katika bweni namba saba muda wa saa tano za usiku.
Hata hivyo, mpaka tunapoandika habari hizi ilikuwa bado haijajulikana ni nini hasa ilikuwa sababu ya msichana huyo kuchukua hatua hiyo ya kujiua, jambo linalotokana na kutokuwepo hata na barua iliyoachwana msichana, huyo aliyekuwa akisomea fani ya biashara kuelezea sababu za kujiua kwake.
Kamanda wa polisi wa mkoa wa Dar es Salaam bwana Samson Ramadhani alikaririwa akisema kuwa uchunguzi wa kina utafanyawa ili kugundua sababu za msichana huyo kujiua...
Uhuru. 08 Januari
Dar es Salaam.
Msichana mmoja mwenye umri wa miaka Ishirini na mitatu alifariki dunia huko nyumbani kwao maeneo ya OysterBay,Toure Drive, baada ya kunywa sumu kali aina ya Strichnine.
Kutokana na msemaji wa familia ya binti huyo kutoweza kupatikana mara moja, haikuweza kujulikana iwapo kulikuwa kuna sababu yoyote inayojulikana ya binti huyo kujiua.
Msichana huyo, aliyekuwa akiitwa Margareth Mfinanga, alikuwa ni mwanafunzi wa mwaka wa pili katika Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam akisomea shahada ya kwanza ya Sheria...
Jaka alipiga mwayo mrefu huku akifunua ukurasa mwingine wa gazeti lile. Ingawa na yeye pia alikuwa ni mwanafunzi wa mwaka wa pili katika Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, hakuwa akimjua yule binti aliyeandikwa habari zake kwenye gazeti lile. Hiyo vile vile ilichangiwa na ukweli kwamba wakati yule binti alikuwa akisomea sheria, yeye alikuwa akisomea shahada ya Biashara.
Hakuona habari yoyote ya kuvutia kwenye ule ukurasa mwingine aliofunua na hivyo alipiga mwayo mwingine mrefu na kugeukia kwenye ukurasa wa michezo.
Kwa mbali akilini mwake alikuwa akikumbuka kuwa kuliwahi kutokea tukio jingine la binti mwingine wa pale pale chuoni kujiua kwa kumeza vidonge au sumu, katika siku za nyuma.
Hakulitilia maanani zaidi...
9
Ufukwe wa pwani ya OysterBay jijidi Dar ulikuwa umefurika watu wa aina mbalimbali katika siku ile ya Jumamosi. Mawimbi yalijitupa kwa mbwembwe zote katika ufuko ule na watu wengi waliokuja kujiliwaza katika pwani ile, wakubwa kwa watoto, walionekana kufurahia sana hali ile.
Miongoni mwa waliokuwepo pale ufukweni siku ile alikuwa ni binti mmoja mzuri mwenye umri uliopata miaka ishirini na mitatu hivi. Yeye alikuwa amevaa suruali ya Jeans nyeusi iliyomkaa vizuri sana, na juu alikuwa amevaa fulana ndogo nyepesi iliyoishia juu kidogo ya kitovu chake. Alikuwa amejilaza juu ya kanga aliyokuwa ameitandika pale mchangani chini ya kivuli mwanana cha mmoja kati ya miti michache iliyokuwa imetawanyika katika pwani ile ya kupendeza. Macho yake mazuri alikuwa ameyaelekeza baharini akiwaangalia watu waliokuwa wakiogelea huku uso wake ukifanya tabasamu dogo na hatimaye kuangua kicheko pale alipomshuhudia kijana mmoja miongoni mwa wale waliokuwa wakiogelea akigaragarazwa na wimbi kubwa na kutupwa kando ya bahari ile kabla ya kuibuka akiwa ameenea mchanga kichwa chote.
Yule mvulana alijiinua haraka na kujitosa tena baharini, kabla ya kurudi nchi kavu dakika chache baadaye na kuelekea pale alipokuwa yule binti huku akitabasamu. Alikuwa kidari wazi na chini alikuwa amevaa bukta iliyoishia juu kidogo ya magoti yake, iliyomkamata mwilini mithili ya soksi. Miguuni alikuwa amevaa viatu vya chachacha vilivyoilinda miguu yake kutokana na mawe makali yanayopatikana kwenye sakafu ya bahari ile.
Alimfikia yule msichana na kumuinamia na kumbusu kwenye paji la uso huku akitabasamu, kisha akachukua taulo dogo lililokuwa pale pembeni na kuanza kujifuta yale maji ya bahari. Yule binti alimpenda sana yule mvulana na hakuwa na shaka kuwa na yeye pia alikuwa akimpenda.
“Naona ulifurahi sana pale nilipotupwa na mawimbi, eeenh?” Mvulana alimuuliza kwa utani huku akiketi kando ya yule binti, ambaye binti alicheka kwa sauti huku akijiinua na kuegemea kiwiko cha mkono wake mmoja ili apate kumuona vizuri mpenzi wake.
“Hapana...unajua we’ unapenda sana kujitia ubingwa katika kila kitu...sasa leo bahari imekutoa ushamba...” Binti alimjibu kisha akamcheka zaidi, na Jaka akajikuta akiangua kicheko pamoja naye.
Yule msichana alikuwa anaitwa Moze.
Moze Mlekwa alikuwa ni msichana mwenye sura ya kuvutia sana na Jaka alijiona ni mtu mwenye bahati kubwa kabisa kuwa mchumba wa binti yule aliyemendewa sio tu na vijana wengi wa rika lake bali pia na watu wazima. Moze hakuwa “mweupe” au maji ya kunde kama Jaka, bali yeye alikuwa na weusi fulani ambao haikuwa rahisi kuubainisha moja kwa moja kuwa ni weusi. Ulikuwa ni weusi ulioelekea kwenye rangi kama ya kahawia kidogo.
Baada ya kuvaa suruali yake aina ya jeans ya buluu, Jaka alinyoosha miguu yake na kuugemeza mgongo wake kwenye mti. Moze alijiinua na kumuegemea mpenzi wake kwa mgongo wake hali kisogo chake akiwa amekilaza kifuani kwa Jaka. Jaka alipitisha mikono yake na kuilaza tumboni kwa mpenziwe yule. Walikaa vile kwa muda mrefu wote wakiwa kimya, kila mmoja akifurahia ukaribu wa mwenzake. Nyakati kama hizi huwa ni nyakati zenye hadhi ya ndoto kwao na kila mmoja alihisi furaha isiyo kifani moyoni mwake.
Wakiwa ni wasomi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, wapenzi hawa walikutana kwa mara ya kwanza miaka miwili iliyopita na kuanza mapenzi yao miezi sita baadaye. Wakati Moze alikuwa anasomea shahada ya sheria, Jaka alikuwa anasomea shahada ya uongozi na biashara.
Mapenzi yao yaliota mizizi haraka sana kiasi cha kuwafikishia hatua ya kufunga uchumba rasmi mwaka mmoja baada ya kuanza kwa mapenzi yao.
Wakiwa wamebakisha miezi sita tu kabla ya kumaliza mwaka wao wa pili pale chuoni na kuingia mwaka wa tatu na wa mwisho kwa shahada yao ya kwanza, walikuwa wamedhamiria kufunga ndoa mara tu baada ya kumaliza masomo yao na kuanza maisha mapya kama mke na mume.
Uhusiano wao ule ulikuwa unajulikana na marafiki zao wengi pale chuoni na hata na baadhi ya wahadhiri, na hivyo waliheshimika sana na asilimia kubwa ya wanafunzi wenzao waliowafahamu pale chuoni.
Ilikuwa wakati wakiwa njiani kurejea chuoni jioni ile wakati Moze alipoamua kumueleza Jaka juu ya vituko alivyokuwa akifanyiwa na Joakim Mwaga. Joakim Mwaga alikuwa ni msomi mwenzao pale Chuoni ambaye aliwahi kumtaka Moze kimapenzi hapo awali. Kutokana na tabia yake chafu ya umalaya na uhuni Moze hakumkubalia ombi lake. Joakim hakuwa na mazoea ya kukataliwa na msichana yeyote, na hivyo alikula kiapo mbele ya Moze kuwa ipo siku tu “atamtia mkononi.” Hata habari za urafiki wa Moze na Jaka zilipodhihiri, Joakim aliendelea tu kumfuatafuata kwa kishawishi hiki na kile ili amwache Jaka na awe mpenzi wake.
Moze hakubadilli msimamo wake.
Kwa upande wake Jaka aliyajua yote hayo lakini hakutaka kuyaingilia kwa msimamo kuwa anamwachia Moze mwenyewe aamue ni yupi mpenzi anayemfaa.
Zilipodhihiri habari za uchumba kati yao, ambapo walifanya sherehe ndogo ya kufunga uchumba pale pale chuoni na kuwaalika baadhi ya marafiki zao, wote wawili walitegemea kuwa sasa Joakim Mwaga angekubali kushindwa na kuwaacha waendelee na mapenzi yao bila mashaka yoyote.
Lakini haikuwa hivyo, kwani ndio kwanza Joakim aliongeza vishawishi kwa Moze, na alipoona vishawishi vyake vinazidi kugonga mwamba alianzisha vitisho.
Vitisho vya Joakim vilitokana hasa na uhusiano wake na kundi dogo lenye fujo sana la watoto wa matajiri walioona nyadhifa na utajiri wa wazazi wao kuwa ni sababu ya wao kufanya lolote walitakalo kwa mtu yeyote.
Ingawa baadhi ya wanafunzi wenzao walikuwa wakiwatukuza na kuwanyeyekea Joakim na kundi lake lililoongozwa na kijana mwingine aliyeitwa Anthony Mpoki, au Tony kama mwenyewe alivyopenda kujiita, Jaka hakuwa miongoni mwa haw wenye kuwatukuza wale jamaa. Yeye aliwaona kuwa ni wahuni na wapumbavu waliokwenda pale chuoni kupoteza muda tu. Mara kadhaa aliwahi kujiuliza ilikuwaje hasa hata watu kama wale wakapata nafasi ya kujiunga na Chuo Kikuu kama kile, na mara zote jibu lililomjia kichwani mwake halikuwa la kupendeza hata kidogo.
Kutokana na kundi la Tony kuwa na pesa nyingi za kuchezea tu na kwenda pale chuoni kwa magari ya aina mbalimbali na mapikipiki makubwa, baadhi ya wasichana wasomi wa pale chuoni walionekana kuwapapatikia na kuwanyenyekea sana bila ya kujali tabia zao chafu za kuwadhalilisha na kutowaheshimu wasichana wanaotembea nao.
Jaka alijiuliza ni wapi watakuwa wanapata pesa nyingi namna ile, kwani hata kama wazazi wao walikuwa matajiri kiasi gani, hakuamini kuwa watakuwa wanawapa watoto wao pesa zote hizo ili wachezee tu bila ya sababu maalum.
Hali hiyo ilisababisha Joakim na wenzake wajione kuwa walikuwa wana haki ya kutembea na kuchezea msichana yeyote waliyemtaka pale chuoni bila ya kujali kuwa alikuwa ni mpenzi wa watu au la. Kwa hiyo lilikuwa ni jambo la kushangaza sana kwa Joakim Mwaga kuona kuwa Moze alikuwa anamkataa. Na ilipomdhihiriki
a kuwa kumbe ni Jaka ndiye alikuwa sababu ya yeye kukataliwa, alijenga chuki kubwa sana kwa Jaka.
Moze alimweleza Jaka jinsi Joakim alivyokwenda kumgongea mlango wa chumba chake pale chuoni usiku wa siku iliyopita na kumlazimisha afungue mlango. Baada ya Moze na rafiki yake wanayeishi naye chumba kimoja katika bweni namba tatu kukataa kufungua mlango, Joakim alitishia kuuvunja mlango ule na hakuondoka nje ya mlango ule mpaka Moze alipotishia kupiga kelele za mwizi.
ITAENDELEA
 
SEHEMU YA KUMI NA NANE
Hali hiyo ilisababisha Joakim na wenzake wajione kuwa walikuwa wana haki ya kutembea na kuchezea msichana yeyote waliyemtaka pale chuoni bila ya kujali kuwa alikuwa ni mpenzi wa watu au la. Kwa hiyo lilikuwa ni jambo la kushangaza sana kwa Joakim Mwaga kuona kuwa Moze alikuwa anamkataa. Na ilipomdhihiriki
a kuwa kumbe ni Jaka ndiye alikuwa sababu ya yeye kukataliwa, alijenga chuki kubwa sana kwa Jaka.
Moze alimweleza Jaka jinsi Joakim alivyokwenda kumgongea mlango wa chumba chake pale chuoni usiku wa siku iliyopita na kumlazimisha afungue mlango. Baada ya Moze na rafiki yake wanayeishi naye chumba kimoja katika bweni namba tatu kukataa kufungua mlango, Joakim alitishia kuuvunja mlango ule na hakuondoka nje ya mlango ule mpaka Moze alipotishia kupiga kelele za mwizi.
Jaka alisikiliza habari ile na kubaki kimya kwa muda mrefu bila ya kusema neno.
“Basi mi’ n’taenda kuongea naye ili aache upuuzi wake, sawa?” Hatimaye Jaka alisema, na Moze akajua kuwa Jaka alikuwa amechukizwa na taarifa ile.
“Sawa...lakini msigombane...ongea naye kiungwana tu, sawa...?” Moze alionesha wasiwasi kutokana na jinsi Jaka alivyobadilika kutokana na taarifa ile.
“Usiwe na wasiwasi Moze. Mi’ najua n’taongea naye vipi.”
“Hilo sina shaka nalo kabisa babie…mashaka yangu ni iwapo Joakim anajua jinsi ya kuongeleshwa jambo hilo…unadhani atalipokea vizuri kweli?” Bado Moze alionesha wasiwasi.
“Aaam…yeah…ataelewa tu…” Jaka alimjibu, kisha haraka akamua kubadili maongezi.
“Hey...umesoma Uhuru la jana...? Limeandika habari za binti mmoja aliyejiua pale chuoni...eti anasoma huko huko Laws. ”
“Ah...nimesoma bwana...yule msichana namfahamu sana, alikuwa anaitwa Mage. Masikini Mage, sijui ni kwa nini tu aliamua kujiua...” Moze alijibu kwa masikitiko.
Wakaendelea kimya na safari yao. Walipofika barabara ya Haile Selasie Jaka alisimamisha teksi ya kuwarudisha hadi chuoni. Wakiwa ndani ya teksi ile bado Jaka alionekana kuwa na mawazo mengi. Moze alimuuliza kulikoni.
“Ah, unajua nilikuwa najaribu kutafakari...hivi tukio kama hili si liliwahi kutokea pale chuoni hapo nyuma...?”
“Tukio kama lipi?”
“La msichana wa Chuo Kikuu kujiua. Nakumbuka kuna binti mwingine alijiua pale Chuoni...kama kwenye Oktoba au Novemba hivi ya mwaka jana, sikumbuki sawasawa...”
“Kwa hiyo...?”
“Ah, mi’ sitaki kuamini kuwa vifo hivi vinatokea kwa bahati mbaya tu. Lazima kuna kitu fulani kinaendelea pale Chuoni aisee… na bila shaka kuna uhusiano mkubwa baina kifo cha kwanza na hiki cha sasa hivi. We’ unaonaje?”
“Mi’ sioni chochote zaidi ya kwamba mambo hayo wenyewe ni polisi...na kama umesoma vizuri lile gazeti, utagundua kuwa Kamanda wa Polisi mwenyewe amesema kuwa watafanya uchunguzi wa kina kuhusiana na swala hilo.” Moze alimshushua.
“Labda hujanielewa, ninachomaanisha ni kwamba...”
“Wewe ndiye hujanielewa Jaka. Ninachomaanisha ni kwamba usitake kuingilia kabisa mambo kama hayo mpenzi. Utakuja kujitia kwenye matatizo makubwa bure...halafu ikawa balaa kwetu sote. Naomba usirudie tena kusema jambo hilo mbele ya mtu mwingine yeyote pale chuoni aisee! Tafadhali sana, Okay?”
Jaka alitaka kubisha, lakini akaghairi.
“Ahh...Okay...”
Waliendelea na safari yao wakiwa kimya.
________________
Siku iliyofuata, Jaka alimkuta Joakim katika uwanja wa kuchezea Tennis ndani ya eneo la michezo pale chuoni. Muda ulikuwa ni kiasi cha saa kumi na moja za jioni hivi.
Alijipenyeza miongon mwa wanafunzi wachace waliokuwa wakifuatilia mchezo ule kutokea nje ya uzio ule wa senyenge, na kubaki akimtazama kwa muda wakati yule jamaa wakati akicheza mchezo ule uliopendwa sana na baadhi ya wanafunzi wenzao pale chuoni. Joakim alikuwa mwembamba na mrefu kuliko yeye. Jioni ile alikuwa amevaa bukta ya michezo ya rangi nyeupe na fulana kubwa ya rangi hiyohiyo, huku miguuni akiwa amevaa viatu vyeusi aina ya Reebok bila ya soksi, vyote vikiwa ni vivazi ghali.
Aliendelea kufuatilia mchezo ule mpaka ulipoisha. Joakim alichukua mkoba wake mdogo uliokuwa kando ya ule uwanja waliokuwa wakichezea na kutoa kijitaulo kidogo na kuanza kujifuta jasho huku akiondoka eneo lile. Jaka alisogea hadi kwenye ile senyenge ule upande ambao Joakim alikuwapo, na kumwita kwa sauti. Joakim Mwaga aligeuka, na alipoona kuwa ni Jaka ndiye aliyemwita, aliachia tabasamu la upande mmoja na kumfuata pale alipokuwa kutokea upande wa pili wa senyenge ile.
Walitazamana kwa muda bila ya yeyote kumsemesha mwenzake hali Joakim akiwa ndani na Jaka akiwa nje ya seng’enge ile. Aligundua kuwa umbali baina ya jicho moja la Joakim na jingine ulizidi kidogo ule umbali wa kawaida kama unavyokuwa kwa watu wengine.
“Unasemaje?” Hatimaye Joakim aliuliza kwa jeuri, akivunja ukimya baina yao.
Jaka hakutaka kupoteza muda zaidi.
“Joakim, kwa muda mrefu sasa umekuwa ukimfuatafuata Moze kwa vishawishi kadhaa wa kadhaa kwa nia ya kuvunja uhusiano uliopo baina yangu na yule binti, uhusiano ambao wewe unaufahamu fika...”Alianza kumwambia lakini alimuona Joakim akikenua meno kwa tabasamu la kejeli, ingawa hakusema kitu. Sura yake ilimkumbusha Jaka dume la nyani alilopata kuliona zamani katika mbuga fulani za wanyama hapa nchini.
“...lakini sasa naona unaanza kutupa mipaka na kufikia hatua ya kutoa vitisho na kumfanyia fujo yule binti, jambo ambalo mimi nikiwa kama mchumba wake siwezi kukaa kimya tu na kulifumbia macho...”
“Kwa hiyo...utafanyaje sasa, mchumba?” Joakim alimkatisha kwa jeuri kubwa huku akimkebehi kwa kumwita “mchumba”.
Ingawa hakupendezwa na kauli ile, Jaka alijitahidi kuipuuza. Akaendelea, “…kwa hiyo bwana Joakim mimi ninataka tabia hiyo uiache mara moja. Kwa sababu itakuletea aibu na kukuvunjia heshima yako bure tu. After all, sisi hapa ni watu wazima, na litakuwa ni jambo la aibu sana kwa wasomi wazima kufanya vituko vya watoto wa kidato cha pili, au we’ unaonaje?”
“Aah! Ina maana we’ unataka kunipangia maisha mimi?” Joakim alimjia juu huku akionesha wazi kuwa hakutaka tu kuelewa kile ambacho Jaka alikuwa akimwambia.
“Sikiliza bwana…mi’ najua we’ umezoea tabia ya kuchezea-chezea watoto wa watu. Sasa kuna baadhi wanaopenda kuchezewa kama jinsi unavyopenda kuwachezea...lakini pia kuna wengine ambao hawapendi. Kwa hiyo jambo ninalojaribu kukueleza ni kwamba ingekuwa bora kama ungewaacha kama walivyo wale wachache ambao hawapendi hiyo michezo yako na ukaendelea kuchezea wale wanaopenda, ambao ni wengi sana. Sasa katika hao wachache wasiopenda kuchezewa-chezewa, Moze ni mmoja wapo...na hataki umfuate fuate...”
Yale maneno yalionekana kumuudhi sana Joakim.
“Sasa mi’ nakwambiaje (akamtukania mama yake)…mi’ Moze n’taendelea kumtongoza na n’tamchukua! Mchumba, mchumba…mchumba Mlimani? Chukua taimu kule, fala nini?” Alimkoromea kwa ghadhabu.
Jaka akajua kuwa Joakim alikuwa anaupeleka kusudi ule mjadala kwenye mtafaruku. Kwa vile alikuwa ameshafikisha ujumbe wake, aliamua kuondoka.
“Naamini ujumbe umekufika Joakim…kaa mbali na Moze!” Alimwambia na kugeuka, akaanza kuondoka akimuacha Joakim na ghadhabu zake.
Jokaim aliruka mbele kwa hatua mbili kubwa na Jaka akajikuta uso kwa uso na hasimu wake.
“Hivi wewe unajiona kama nani hata unipangie ni mwanamke gani nitembee naye na yupi nisitembee naye, eennh?” Joakim alimkoromea huku akimtomasa-tomasa kifuani kwa kidole chake na uso wake ukionesha hasira nyingi.
“Kama utatumia akili kidogo tu Joakim, utagundua kuwa nilichofanya ni kukupa ushauri wa busara sana...kuwa tembea na kila mwanamke umtakaye iwapo naye anakutaka, na yule ambaye hakutaki, basi achana naye...ni hivyo tu. Sasa sijui ni kitu gani kinachokufanya wewe uje mbogo kiasi hicho!” Jaka alimjibu kwa utulivu huku akiwa ameingiza viganja vya mikono yake miwili ndani ya mifuko ya jaketi lake la michezo alilokuwa amevaa. Kwa jibu lile wasomi wachache waliokuwa pale karibu waliangua kicheko na kumfanya Joakim ajione mjinga.
“Kkha! Yaani unamaanisha mimi situmii...yaani sina...akili?” Joakim alibwata huku macho yakimtembea. Jaka alijua kuwa pale Joakim alikuwa hatumii akili bali alikuwa akiendeshwa na jazba na pupa.
“Mi’ naona huu mjadala tuuahirishe kwa sasa na tutafute wakati mwingine iwapo utaona kuna haja ya kufanya hivyo Joakim…Lakini kwa upande wangu nadhani ujumbe niliokuletea ni mdogo tu na uko wazi sana.” Jaka alimwambia huku akimpita pembeni na kuendelea kuondoka katika eneo lile. Mashuhuda wakazidi kucheka. Joakim akazidi kujazibika.
“Hey! Bado hatujamaliza! Unaniletea kiburi mimi wewe...?” Joakim aliendelea kubwata wakati Jaka akiendelea na safari yake bila kumjali.
Joakim alimrukia na kumsukuma kwa nguvu. Jaka alianguka huku akilaani kwa sauti. Alijiinua kutoka pale chini akiwa amehamanika, na alikuwa akimgeukia Joakim kwa hasira wakati Joakim alipomuwahi na kumkwida kwa kola ya jaketi lake.
“Hata siku moja usijaribu kunitolea jeuri mie...umesikia wewe?” Joakim alimwambia kwa hasira na kumsukuma tena chini kwa nguvu. Lakini safari hii Jaka naye alikuwa tayari. Kama umeme alimdaka mikono yake na kumvuta nyuma pamoja naye, na hapo hapo akamrusha hewani kwa judo kali. Joakim aliachia ukelele wa taharuki kabla ya kuangukia mgongo kwa kishindo. Haraka sana Jaka alijirusha na kusimama wima na kumgeukia pale alipokuwa akigaagaa.
Joakim alijikurupusha kutoka pale chini na kumkimbilia Jaka kwa ghadhabu huku akiwa ametanguliza mikono yake kwa nia ya kumdaka koo, lakini Jaka alipiga hatua kubwa kumuwahi, kisha akajigeuza huku akimzungushia teke kali sana la nyuma-nyuma na kumshindilia kisigino cha chembe yule hasimu wake. Joakim alijipinda huku yowe la uchungu likimtoka. Alienda chini bila kupenda na kubaki akiwa amepiga magoti pale chini huku akiwa amejishika ile sehemu iliyopata dhoruba, miguno ya maumivu ikimtoka na akiwa anamtumbulia Jaka macho ya kutoamini.
Jaka alibaki akimtazama kwa dharau jinsi alivyokua akiugulia bila namna pale chini, kisha bila ya kusema neno aligeuka kuondoka, akimwacha Joakim akitweta hovyo. Kabla hajafika mbali mmoja kati ya wasomi wenzao wachache walishuhudia tukio lile kwa butwaa alimkimbilia.
“Aisee...! Hivi unajua kuwa umechokoza vita kubwa sana wewe? Unajua wash’kaji zake wakiipata habari hii utakuwa katika “trabo” kubwa sana mshikaji wangu!” Jamaa alimwambia, akimaanisha kuwa Jaka atakuwa kwenye matatizo makubwa pindi kundi la marafiki wakorofi wa Joakim likipata habari za tukio lile.
“Nionavyo mimi ni kwamba yeye ndiye ambaye yuko kwenye “trabo” hivi sasa.” Jaka alijibu kwa kutojali huu akiendelea na safari yake.
Ambalo hakukijua kwa wakati ule ni kwamba kulikuwa kuna “trabo”, yaani matatizo, makubwa zaidi yaliyokuwa yakimsubiri yeye huko mbele kutokana na tukio lile.
Ukweli ni kwamba kuzagaa kwa habari za kipigo alimdondoshea mtukutu Joakim kulimpa umaarufu mkubwa sana Jaka pale chuoni. Umaarufu hu ulikuja kwa namna mbili, ya kwanza ikiwa ni ya kuonekana shujaa na mdiriki aliyeweza kusimama imara dhidi ya mtukutu anayehofiwa na wengi, kiasi kwamba baadhi wa wanafunzi walifikia hatua kwenda kumpongeza kwa tendo lile. Lakini namna ya pili ni kwamba aliondokea kupata umaarufu mkubwa sana miongoni mwa washirika wa mtukutu Joakim Mwaga, hususan kwa kijana aliyeitwa Anthony Wanzaggi, mwanafunzi wa mwaka wa pili katika fani ya elimu ya Kompyuta pale chuoni, ambaye ndiye hasa aliyekuwa kiongozi wa kundi lile ambalo Joakim alikuwa akijihusisha nalo.
Anthony Wanzaggi, au Tony, kama jinsi alivyopenda aitwe, alijulikana sana kutokana na umaarufu na utajiri wa baba yake. Mzee Athanas Wanzaggi alikuwa akimiliki makampuni kadhaa makubwa hapa nchini na ilikuwa inasemekana kuwa Tony alikuwa amewekewa ukurugenzi katika moja ya makampuni hayo.
Kwa upande mwingine, hali ile ilizidisha wasiwasi na mashaka makubwa kwa Moze, ambaye alikuwa anahofia kisasi kutoka kwa Joakim na wenzake dhidi ya Jaka na hata dhidi yake pia.
Jaka alijitahidi kumtoa mashaka kwa kumwambia kuwa Joakim hatarudia tena upuuzi wake kwa kuhofia aibu ya kipigo kingine, na kwamba hakukuwa na sababu ya hao marafiki zake kuingilia katika jambo ambalo wao halikuwa likiwahusu hata kidogo.
“Ah, we Jaka huwajui wale jamaa nakwambia…sijui ni kwa nini, ila jamaa wanapenda sana sifa na kuogopwa. Yaani ningejua hata nisingekwambia kuhusu haya mambo dear…watatusumbua tu hawa. Mi najua!” Moze alilalama.
Jaka alifinya uso kwa tafakuri.
“Ah, okay…basi na tuwe makini tu kuanzia sasa. Hili jambo ilibidi lifikishwe mwisho Moze, na nilitaraji litaisha kwa mazungumzo tu…lakini ndio haikuwa.” Alimwambia.
________________
Anthony Athanas Wanzaggi, au Tony, alifikicha pua yake pana kwa nguvu huku akitikisa kichwa chake kutoka upande mmoja kwenda mwingine. Alifumbua macho yake mekundu na kuinua uso wake kuwatazama wale jamaa waliokuwa chumbani kwake muda ule. Aliwaona kwa mbali huku akihisi kama kwamba macho yake yalikuwa yameingiwa na ukungu fulani.
Alitikisa tena kichwa chake na kukiinamisha huku akiinua mkono wake wa kushoto na kunusa unga mweupe na laini sana uliobakia kwenye mgongo wa kiganja cha mkono ule kwa mkupuo mmoja na ule unga ukatowekea puani mwake na kusambaa kwenye mishipa yake ya fahamu zake. Kwa kutumia kilekile kiganja aliifikicha tena pua yake pana kwa nguvu zaidi huku akiendelea kutikisa kichwa chake, miguno ya kuridhika ikimtoka huku akivuta pumzi nyingi ndani ya mapafu yake. Safari hii alipofumbua tena macho yake kuwatazama wale jamaa, aliwaona vizuri sana. Wale jamaa wawili waliokuwa pamoja naye mle chumbani walikuwa wakimtazama huku wakitabasamu, naye alitabasamu.
“Ee bwana ee...yaani najisikia poa kishenzi mshikaji wangu, you know what I’m sayin’?” Tony aliwataarifu wale wenzake kisha akacheka sana. Wale jamaa nao wakacheka pamoja naye kisha wakagonganisha viganja vya mikono yao kama kihitimisho cha furaha yao.
Walikuwa chumbani kwa Tony pale chuoni katika bweni namba moja ghorofa ya tatu. Wale jamaa wawili walikuwa ni wanafunzi wa mwaka wa pili pale chuoni na ndio waliounda kundi lile lililoogopwa sana pale chuoni wakiongozwa na Tony.
ITAENDELEA
 
SEHEMU YA KUMI NA TISA
“Ee bwana ee...yaani najisikia poa kishenzi mshikaji wangu, you know what I’m sayin’?” Tony aliwataarifu wale wenzake kisha akacheka sana. Wale jamaa nao wakacheka pamoja naye kisha wakagonganisha viganja vya mikono yao kama kihitimisho cha furaha yao.
Walikuwa chumbani kwa Tony pale chuoni katika bweni namba moja ghorofa ya tatu. Wale jamaa wawili walikuwa ni wanafunzi wa mwaka wa pili pale chuoni na ndio waliounda kundi lile lililoogopwa sana pale chuoni wakiongozwa na Tony. Joakim alikuwa bado mgeni katika kundi lile potofu.
Kuvuta na kusambaza madawa ya kulevya kwa “wateja” mbalimbali ndani na nje ya chuo kile ilikuwa ndio kazi yao yakua nfasi ya pili tu kwao. Baadhi ya wasomi wachache pale chuoni walikuwa wameingizwa kwenye mkumbo ule wa kutumia madawa ya kulevya, wengi wao ikiwa ni kinyume na matakwa yao. Baada ya kuingia katika mkumbo ule walikuwa ni kama tongwa walionaswa kwenye ulimbo, na mara kwa mara walipohitaji unga ule haramu waliupata kwa bei ghali sana kutoka kwa wale jamaa wawili waliokuwa na Tony mle ndani usiku ule.
Pamoja na kuwa “wateja” walikuwa wakiupata unga ule wa haramu kila walipouhitaji, hakukuwa na hata mmoja kati yao aliyekuwa akijua ni wapi hasa wale wasambazaji wao walikuwa wakiupata unga ule haramu. Ni wale jamaa wawili tu ndio waliojua kuwa Tony ndiye aliyekuwa akiongoza biashara ile pale chuoni na kuwatuma wao kuisambaza kwa “wateja” wachache walioingia katika ulevi ule kwa kulazimishwa na kwa vitisho hata wakajikuta kuwa hawawezi tena kukaa bila kutumia unga ule.
Wengi wa wateja wa Tony walikuwa ni wasichana.
“Sasa Tony unasemaje kuhusu huyu Jaka...unajua katutia aibu sana?” Mohamed “Muddy” Shomari, mmoja kati ya wale jamaa wawili ambaye naye pia alikuwa ni mtumiaji mzuri wa madawa ya kulevya au “bwimbwi” kama watoto wa mjini walivyozoea kuuita unga ule haramu, alisema.
“Yaa...katutoa nishai kichizi mshikaji!” Jamaa wa pili alithibitisha hoja ya mwenzake, huyu aliitwa Alphonce Ng’ase, na alikuwa mfupi na mkomavu. Mwenyewe alipenda sana kujiita “Al Pacino”, labda kutokana na upenzi wake kwenye ile biashara haramu ya madawa ya kulevya aliyokuwa akiifanya pale chuoni.
“Katutoa nishai sisi au kamtoa nishai Joakim bhana?” Tony aliuliza huku akijishughulisha kuchagua CD ya muziki miongoni mwa nyingi zilizozagaa hovyo mezani kwake pale chumbani.
“Aaah...sasa Joakim si mshiriki wetu bwana? Sasa hivi kila upitapo hapa Chuo stori ni hiyo tu! Lazima na sisi tujibu mapigo kwa niaba ya mshiriki wetu bwana, au unasemaje Ng’ase?” Muddy alimjibu huku akitaka kuungwa mkono na yule mwenzake.
“Yaani hilo ndio mpango mzima mwanakwetu...la
zima na siye tufanyie ya kwetu fala yule, hawezi kutuaibisha namna ile halafu aachiwe tu hivi hivi, nkhaa!” Ng’ase aliunga mkono hoja ile.
“Ah…Joakim nae laini mno yule...tabu yake ni kuwa hatumii “madope” yule mtoto...kama angekuwa anapata “dope” yule angechangamka kidogo.” Tony alilalamika kwa hasira akimaanisha kuwa Joakim alikuwa laini kwa sababu alikuwa havuti unga na ndio maana akapigwa na Jaka. Sio wote katika marafiki wa lile kundi lao waliokuwa wakitumia madawa ya kulevya, na ukitoa Ng’ase na Muddy, wengine wote walikuwa hawajui kuhusu utumiaji na uuzaji wao wa unga ule haramu. Ilikuwa ni siri kali sana ambayo kujulikana na mtu yeyote asiyetakiwa kulimaanisha kifo kwa mtu yule, na kutokana na ugeni wake kundini, Joakim hakushirikishwa kabisa kwenye siri ile.
“Unajua tatizo ni kwamba inatufanya hata sisi tuonekane mabwege mbele ya “wateja”, na hii inatishia usalama wa biashara yetu Tony.” Muddy alichangia. Kauli ile ilikamata umakini wa Tony. Alinyamaza kimya na kubaki akimtazama Muddy kwa muda, kisha akatikisa kichwa kuafikiana naye huku uso wake ukionesha mawazo mazito.
“Good point, man! Basi jamaa itabidi apewe onyo kali sana, you know what am sayin’?.” Alisema kwa sauti ya chini na kunusa tena ule unga wa haramu.
Muddy na “Al Pacino” wakagongesha ngumi zao kufurahia kupita kwa hoja ile.
_________________
Siku mbili baadaye Moze alikuwa akimweleza Jaka, “Wale ni watu wabaya sana Brown...haikuwa busara kabisa kufanya jinsi ulivyofanya kwa Joakim.” Moze hupendelea kumwita Jaka kwa ubini wake, yaani Brown.Walikuwa chumbani kwa Moze, ambapo Rose, mwanafunzi mwenzao aliyekuwa akiishi pamoja na Moze mle chumbani pia alikuwapo. Ilikuwa ni saa tatu za usiku.
“Kwani wewe wasiwasi wako ni nini Moze?” Jaka alimuuliza huku akiielekeza kinywani bilauri ya juisi kabla ya kupiga funda kubwa na kuirudisha mezani bilauri ile ikiwa tupu.
“Mi’ n’na wasiwasi Brown...kila ninapokutana na wale marafiki wa Joakim huwa wananitazama kwa namna ambayo inaashiria kuwa wana lao jambo...” Moze alijibu kwa mashaka.
“Lakini Moze, mi’ naona Jaka hakuwa na budi kufanya jambo alilolifanya, kwa sababu Joakim asingeacha kukufanyia vituko.” Rose alidakia huku akimtazama Moze kwa makini.
“Ah…najua, lakini...naona kama bado mambo hayajaisha haya...”
“Sasa unaonaje kwa muda huu tukiishi kwa furaha mpaka hapo hayo mambo yatakapoamka tena? Muda huo ukifika tutajua tuchukue hatua gani, unaonaje mpenzi?” Jaka alimwambia Moze kwa utaratibu akijaribu kumtoa wasiwasi. Moze alimtazama kwa sekunde kadhaa, kisha akatabasamu.
“Brown kwa kujifanya Van Damme!” Hatimaye alisema na wote watatu wakacheka kwa sauti.
Jaka aliinua Trampeti yake ndogo iliyokuwa pale juu ya meza na kuanza kupuliza taratibu wimbo ambao alijua kuwa Moze alikuwa akiupenda sana. Trampeti ile ilikuwa ni zawadi aliyopewa na Moze katika kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa miezi sita iliyopita. Jaka alikuwa ni hodari sana wa kupuliza ala ile na ilikuwa ni kiburudisho chake kikubwa.
Taratibu nota za wimbo ule zilianza kusikika na Moze na Rose walibaki wakimtazama huku wakiwa kimya. Alikuwa akiigiza kupuliza wimbo wa zamani lakini walioupenda sana ulioimbwa na Roxette, ulioitwa It must have been Love.
Kadiri wimbo ule ulivyokuwa ukiendelea ndivyo Jaka alivyozidi kupata mori na kujisahau kabisa kuwa alikuwa na watu wengine mle ndani hali akiendelea kupuliza Trampeti yake huku macho yake akiwa ameyafumba kwa mdadi. Moze alimwangalia mpenzi wake huku ule wimbo ukimwingia na alihisi raha sana.
Taratibu Jaka aliumalizia wimbo ule huku akifumbua macho yake taratibu kumtazama mpenzi wake. Macho yao yalikutana na waliangaliana kwa mapenzi huku mlio wa Trampeti ile ukimalizikia kwa sauti ya chini. Moze alionekana kulengwa na machozi kwani siku zote wimbo ule alioupenda sana ulimtia msisimko fulani ausikiapo, na huwa anashindwa kuyazuia machozi kutokana na maana ya maneno ya wimbo ule uliokuwa akielezea hadithi ya simanzi ya penzi lililopotea.
Taratibu Rose aliinuka na kutoka nje ya chumba kile bila ya kusema neno na kuwaachia faragha wapenzi wale wawili. Moze aliinuka na kwenda kumkumbatia Jaka kwa mapenzi huku machozi yakizidi kumchoma machoni. Jaka alimpakata mpenziwe mapajani na kumbusu kwenye paji la uso huku kwa mkono wake mwingine akiining’iniza pembeni ile ala yake ya muziki. Aliyaona machozi yaliyokuwa yakipigania kutoka kwenye macho ya mpenzi wake.
“Unalia.”
“Ndio.”
“Sitaki mtu yeyote atupotezee penzi letu, Moze...si Tony wala si Joakim…yeyote yule.”
Moze alitikisa kichwa kukubaliana naye lakini hakusema kitu.
“Kwa hiyo usiwe na wasiwasi, penzi letu halitapotea…halitaisha.”
Moze alimtazama mpenzi wake kwa huba na kumkumbatia kwa nguvu. Jaka alimkumbatia yule binti kwa mkono mmoja huku akiwa bado ameshikilia Trampeti yake kwa mkono mwingine. Nyuso zao zilikutana na kugusana kwa upendo. Walikutanisha midomo yao katika mvuto wa mapenzi na ndimi zao zilipokutana kila kitu kilionekana kusimama, trampeti ikaanguka juu ya zulia lililotandikwa pale sakafuni...
It must have been love, but it’s over now…
It must’ve been good...but I lost it somehow...
Maana ya baadhi ya maneno ya wimbo ule wa Roxette ilikuwa bado vichwani mwao hali wakiwa wakielea katika ulimwengu wa kipekee katika mvuto ule wa kimapenzi.
Bila shaka lilikuwa ni penzi, lakini sasa limekwisha...
(Ni wazi kuwa) ilikuwa vizuri (kuwa na penzi), lakini kwa namna fulani nimelipoteza...
Ni maneno hayo katika wimbo ule ambayo mara nyingi yaliwakumbusha majuto watakayokuwa nayo pindi wakiliachia penzi lao lipotee.
“Penzi letu halitapotea...” Moze aliyarudia maneno ya Jaka kwa sauti ya kunong’ona sana.
“Mmnnhh!” Ndilo jibu pekee lililomjia Jaka kichwani mwake kwa wakati ule huku akizikutanisha tena ndimi zao...
____________________
Kwa kawaida siku za mwisho wa wiki huwa ni siku za burudani mbalimbali kwa wanachuo. Siku hizo wanachuo hupata nafasi ya kwenda kubadili mawazo kwa kujiburudisha katika kumbi mbalimbali za starehe ndani ya jiji la Dar es Salaam. Wanachuo huwa wanajiandalia utaratibu maalum wa kwenda katika moja ya kumbi hizo za starehe kwa gharama nafuu. Wikiendi hii wanachuo walikuwa wameandaliwa kwenda kwenye ukumbi wa disko wa Club Billicanas, ambapo mmoja wa wanamuziki wa kizazi kipya alikuwa anafanya onesho maalumu la kuzindua albamu yake mpya pamoja na video ya moja kati ya nyimbo zake kutoka kwenye albamu yake hiyo mpya.
Wanachuo wengi waliamua kujimwaga kwenye ukumbi ule ili kwenda kujisahaulisha machovu ya wiki nzima ya kusumbua ubongo pale chuoni au “The Hill” kama wenyewe walivyopenda kupaita, wakimaanisha “Mlimani”. Miongoni mwao usiku ule pale Billicanas walikuwapo Jaka na mpenziwe Moze, pamoja na rafiki yao Rose ambaye alikuwa amesindikizwa na Raymond Mloo, rafiki mkubwa wa Jaka ambaye walikuwa wakiishi chumba kimoja katika bweni namba tano pale chuoni.
Raymond alikuwa ni kijana mkimya na mtaratibu kama Rose, na kinyume cha matarajio ya Moze, hakuonesha dalili yoyote ya kutaka uhusiano wa kimapenzi na Rose ingawa Rose mwenyewe alishaonesha kila dalili za kumridhia katika hilo. Raymond hakuwa na uhusiano wa kimapenzi na msichana yeyote pale chuoni na hakuwa na mpango wa kufanya hivyo ingawa aliuheshimu sana uhusiano uliokuwapo baina ya Jaka na Moze.
Jaka alielewa ni kwa nini Raymond hakupenda kujihusisha na maswala ya mapenzi, kwani mara nyingi alipojaribu kumchokoza kuhusu swala hilo jibu lake lilikuwa ni lile lile siku zote.
“Mi’ nawaogopa sana wasichana...kwa sababu msichana anaweza kukupenda sana halafu akaja kukuchukia ghafla kwa jambo dogo tu...na usiombe msichana unayempenda atokee kukuchukia ghafla rafiki yangu, kwani hapo ndipo utakapojuta kuzaliwa. Sasa mimi sitaki ije itokee siku nije kujuta kwa nini nilizaliwa...ndio maana sitaki kabisa michezo na hawa watoto wa kike...”
Lakini pamoja na msimamo wake huo juu ya mapenzi, Raymond hakuonesha dharau hata kidogo kwa akina dada. Na ni tabia yake hiyo iliyojengwa na msimamo wake huo ndio iliyowafanya akina dada kama Rose wazidi kupata hamu ya kuhusiana naye kimapenzi. Jaka aliwahi kumweleza hilo mara kadhaa lakini jibu lake halikubadilika.
“Wanawake ni viumbe hatari sana rafiki yangu, ukijaaliwa kupata mwanamke mwenye tabia tofauti lazima ushukuru sana. Acha kabisa kunishawishi-shawishi kuhusu mambo ya wanawake bwana, kwa sababu wanawake hawatabiriki...sasa ukinishawishi nami nikakubaliana nawe, siku atakaponibadilikia wewe hutaweza kunisaidia hata kidogo rafiki yangu. We’ niache tu!”
Jaka alicheka sana siku alipojibiwa hivyo. Wakati ule hakuwa na namna ya kujua kuwa kuna siku angekuja kuyakumbuka kwa uchungu sana yale maneno.
Yote kwa yote, ulikuwa ni usiku ya furaha sana pale Billicanas. Jaka na Moze walicheza muziki,waliongea na marafiki zao ambao wengine walikuwa hawajaonana nao kwa wiki nzima ingawa walikuwa wakisoma pale pale chuoni. Nje ya ukumbi ule kulikuwa kuna sehemu ya maakuli, zaidi ikiwa ni chipsi, ndizi choma na nyama choma. Basi ndizi na nyama choma vilitafunwa kwa vinywaji baridi, muziki ulichezwa, nyama na ndizi zikatafunwa tena, muziki ukachezwa tena, maongezi yakapamba moto, vicheko vikatawala. Ilikuwa ni burudani iliyotimia. Moze alicheza muziki na Raymond pamoja na baadhi ya marafiki mbalimbali wa Jaka kwa nyakati tofauti huku Jaka akiongea na marafiki zao kadhaa.
Hatimaye wakawa wamebaki peke yao kwenye meza moja ya pembeni mle ukumbini. Rose alikuwa amejichanganya kwenye ukumbi ule na Raymond halikadhalika. Moze alionekana ni mwenye furaha sana na Jaka alifurahishwa na hali ile kwani alijua kuwa wasiwasi wake juu ya kundi la akina Joakim bado ulikuwa haujaondoka.
Bila ya wao kujua, pamoja na jitihada za Jaka kuangaza kwa chati kila kona ya ukumbi ule bila ya mafanikio, furaha na nyenendo zao zote zilikuwa zikishuhudiwa kwa utulivu mkubwa na Alphonce “Al Pacino” Ng’ase na Muddy waliokuwa wamekaa kwenye meza moja iliyojificha kwenye kona nyingine yenye kiza kidogo pale ukumbini.
Baada ya Raymond kuzunguka sehemu mbalimbali za ukumbi ule akiongea na jamaa kadhaa aliojuana nao huku akiendelea kula maraha, aliangalia saa yake na kugundua kuwa muda wao wa kuondoka ulikuwa umekaribia kwani walikubaliana waondoke pale ukumbini ifikapo saa nane na nusu za usiku. Saa yake ilimwambia kuwa muda ulikuwa ni saa nane na dakika kumi...
Huku nyuma, Jaka aliinuka na kumbusu mpenzi wake shavuni, akamuaga kuwa alikuwa anaelekea chooni kujisaidia haja ndogo. Moze aliafiki na kubaki peke yake pale mezani akimsubiri.
Walipoona kuwa Jaka amechukua uelekeo wa maeneo ya msalani, Ng’ase na Mudy walitazamana, na bila kuongea waliinuka kwa pamoja na kumfuata...
 
SEHEMU YA ISHIRINI
Baada ya Raymond kuzunguka sehemu mbalimbali za ukumbi ule akiongea na jamaa kadhaa aliojuana nao huku akiendelea kula maraha, aliangalia saa yake na kugundua kuwa muda wao wa kuondoka ulikuwa umekaribia kwani walikubaliana waondoke pale ukumbini ifikapo saa nane na nusu za usiku. Saa yake ilimwambia kuwa muda ulikuwa ni saa nane na dakika kumi...
Huku nyuma, Jaka aliinuka na kumbusu mpenzi wake shavuni, akamuaga kuwa alikuwa anaelekea chooni kujisaidia haja ndogo. Moze aliafiki na kubaki peke yake pale mezani akimsubiri.
Walipoona kuwa Jaka amechukua uelekeo wa maeneo ya msalani, Ng’ase na Mudy walitazamana, na bila kuongea waliinuka kwa pamoja na kumfuata...
Raymond alimkuta Moze akiwa peke yake pale mezani, na alipomuulizia Jaka Moze akamfahamisha kuwa ameenda kujisaidia.
“Rose…?”
“Naye pia alitowekea huko huko kwenye muziki na mpaka sasa hajarudi.” Moze alijibu.
Raymond aliokota kipande cha nyama kutoka kwenye sahani iliyokuwa pale mezani na kukitupia kinywani. Alitafuna taratibu huku akiangaza huku na kule akijaribu kumtafuta Rose bila ya mafanikio.
“Mi’ naona nikamtafute Rose ili tukija hapa Jaka atakuwa amesharudi tunatimua, au vipi ?”
“Sawa Ray...wazo zuri.”
Raymond akapotelea ukumbini kumtafuta Rose.
________________________
Kule chooni Jaka alifunga zipu ya suruali yake na kugeuka huku akichomekea vizuri suruali akiwa katika hatua ya kutoka pale chooni baada ya kujisaidia.
Hakupiga hatua nyingine zaidi.
Muddy na Alphonce Ng’ase walikuwa wamesimama huku wakimtazama, na mara moja alijua kuwa balaa lilikuwa limemfika, kwani alimkuwa wazi kuwa wale jamaa walikuwa wamemsimamia namna ile kwa nia moja tu, nayo si kumsalimia.
Huku moyo ukimwenda kasi na akili yake ikifanya kazi ya ziada kujaribu kutafuta namna ya kujikwamua, alitupa jicho kulia kwake na hakuona chochote cha kumsaidia. Akatupa jicho kushoto nako akakuta hali ni hiyo hiyo. Aliona ajabu kwa nini walikuwa peke yao mle chooni ambapo kwa kawaida vyoo vya kumbi za starehe huwa haipiti dakika tano bila kuwa na mtu au watu wakijisaidia.
Aliinua macho yake na kuchungulia juu ya mabega ya wale jamaa na kugundua kuwa wale jamaa walikuwa wameufunga mlango ule kwa ndani ili kuhakikisha kuwa Jaka hafanikiwi kutoka mle chooni kabla hawajatimiza azma yao mbaya.
“Oi! Vipi tena tough guy, umeshituka kutuona rafiki zako wapenzi?” Muddy alimuuliza kwa kejeli huku akimsogelea. Jaka alipiga hatua mbele kuuwahi mlango huku akiwapisha wale jamaa.
“Samahani, naomba kupita...”
Alphonce Ng’ase alimdaka koo huku akimkemea kwa ukali.
“Sisi tunaongea na wewe halafu unajidai huelewi sio? Pumbavu!”
Hapo hapo Muddy akamtandika teke kali sana la mbavu, naye akahisi maumivu makali, mguno wa uchungu ukimtoka pasi kupenda. Aliinua mikono yake akijaribu kuuondoa mkono wa Alphonce uliomkaba koo, lakini Alphonce alimwachia koo haraka kabla Jaka hajamgusa na hapo hapo akamshindilia ngumi tatu za haraka haraka, mbili kwenye chembe, na moja ikimpata kwenye taya.
Jaka alilia kwa kipigo kile huku akipepesuka. Muddy aliruka na kumbabatiza teke la kifua lililomsukuma hadi ukutani, ambapo alipigiza mgongo na kisogo chake vibaya sana. Alihisi mlipuko wa kiza ukipita machoni mwake na miguu ikamuwia mizito. Alijitahidi kujizatiti kimakabiliano, lakini maumivu makali kutokea kisogoni kwake yalim[oteza kabisa muelekeo. Na kama hilo halikutosha, wale jamaa waliokuwa wamedhamiria kutompa kabisa nafasi ya kujitetea kimakabiliano walimvurumishia mvua ya mapigo bila ya huruma akiwa amebabatizwa pale ukutani, huku wakimiminiwa matusi kem kem. Nguvu zilimwishia Jaka, na huku akihisi kizunguzungu alidondokea magoti pale msalani, na alikuwa anaelekea kuangukia uso pale sakafuni wakati Alphonce Ng’ase alipomdaka koo. Alibaki akitweta huku uzito wake wote ukiwa umeegemezwa kwenye mkono wa Alphonce Ng’ase aliyemdaka koo. Alijaribu kuuinua uso wake ili amtazame yule jamaa aliyemdaka koo lakini hakuweza kwani macho yake yalimuwia mazito sana.
“Hizo zilikuwa ni salamu kutoka kwa Joakim...na nyingine zitafuata, Pusi wee!” Alphonce alimkoromea, kisha akamwachia na Jaka akaanguka sakafuni kama mzigo. Hapo hapo Muddy alimtandika teke la mbavu lililotoa mguno hafifu kutoka kwa Jaka.
Wale jamaa walibaki wakimwangalia kwa dharau akiwa amelala pale sakafuni kabla ya kugeuka na kutoka nje kimya kimya, wakimwacha Jaka akigaagaa kwenye mikojo na damu pale sakafuni.
Jaka alijaribu kuinuka bila ya mafanikio. Maumivu makali yalimtambaa mwilini na alihisi fahamu zikimpotea upesi mno. Alijaribu kutambaa kuelekea mlangoni huku akitoa sauti za kuomba msaada lakini sauti ilikuwa imemkauka na nguvu zilizidi kumwishia. Hatimaye alidondosha kichwa chake juu ya mkono wake uliolala pale sakafuni kwa kukata tamaa na kubaki akiwa amelala kifudifudi pale chooni bila ya kujali harufu kali ya mikojo na damu nyingi iliyokuwa ikimtoka puani na mdomoni. Akili yake ilitawaliwa na jambo moja tu muda ule...Moze.
Alijua kuwa baada ya kumfanyia yale waliyomfanyia wale jamaa wangeenda kwa Moze...
Sijui watamfanya nini tu maskini Moze wangu huko…
Wazo hilo lilimpa nguvu. Alijikurupusha na kupiga goti moja pale sakafuni huku akihisi maumivu makali mwilini na kichwani. Alipojaribu kuinua mguu wa pili alishindwa na kuanguka tena sakafuni kwa kishindo huku akihisi kiza kikitanda mbele ya macho yake.
Fahamu zikampotea.
_____________________
Kule ukumbini Raymond Mloo aliangalia saa yake kwa mara nyingine tena na kuwageukia Moze na Rose waliokuwa pamoja naye pale mezani.
“Jamani, mbona Jaka amechelewa sana kutoka...” Kabla hajamaliza kauli yake aliwaona Alphonce Ng’ase na mshirika wake wakitokea sehemu za kule msalani kwa mwendo wa haraka hali wakiangaza huku na huko. Mara moja alihisi hatari kwani aliuelewa fika uhasama uliojitokeza baina ya Jaka na Joakim, na alijua kuwa Alphonce na Muddy walikuwa ni marafiki wakubwa wa Joakim.
“Ooooh, Shiiit!” Aliropoka na kutoka mbio kuelekea kule chooni.
Kwa sekunde kadhaa Moze na Rose walibaki wakiwa wamepigwa butwaa pale mezani pasina kuelewa kilichokuwa kinaendelea. Kisha Moze naye akakurupuka na kutoka mbio kumfuata Raymond huku akiita jina la Jaka kwa kelele. Na hata wakati anaendelea kufanya hivyo, alimuona Raymond akitokea sehemu za eneo la kujisaidia wanaume huku akiwa anamburura Jaka kwa taabu. Moyo ulimlipuka na alihisi miguu ikimwisha nguvu. Akasimama palepale alipokuwa, macho yakiwa yamemtumbuka.
Jaka alikuwa ametapakaa damu sehemu ya mbele ya shati lake na jicho lake moja lilikuwa limevimba vibaya.
“Brown...! Brown! Oh, Mungu wangu! Ni nini tena kimetokea sasa?” Alibwabwaja huku akipepesuka kuelekea kule alipokuwa wanatokea Raymond akiwa nusu amembeba, nusu anamkokota Jaka. Baadhi ya wanachuo, wahudhuriaji wengine na wahudumu waliokuwepo pale ukumbini nao walianza kuelekea kule alipokuwa akitokea Raymond kujaribu kutoa msaada na kutaka kujua kilichotokea.
“Gari! Tafuta gari upesi!” Raymond alifoka huku akiendelea kumburura Jaka.
Kufikia hapo Moze na Rose walikuwa wakilia kama wajinga. Muda mfupi baadaye walikuwa ndani ya teksi wakielekea kituo cha afya cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Waliamua kwenda huko kwa kuwa ndipo mahala pekee ambapo walijua kuwa Jaka angeweza kupata huduma bila maswali mengi wala kuhitajika kutoa pesa za matibabu, wakizingatia kuwa wote walikuwa ni wanafunzi wasio na uwezo wa kumudu gharama za matibabu ya hospitali za nje ya chuo kikuu. Teksi ilikuwa inaendeshwa kwa mwendo wa kasi sana kuwarejesha chuoni, Raymond akiwa kiti cha mbele kando ya dereva hali Jaka akiwa amelazwa kwenye kiti cha nyuma akiwa amelaza kichwa chake kwenye mapaja ya Moze na miguu yake ikiwa kwenye mapaja ya Rose. Kutokea kwenye kile kiti cha nyuma, sauti za wale akina dada zilisikika zikilia taratibu.
Jaka alilazwa pale hospitali ya Chuo Kikuu kwa wiki mbili. Ndani ya wiki ya kwanza akiwa pale hospitali alikuwa akipoteza na kurudisha fahamu mara kwa mara kutokana na maumivu makali yaliyotokea kichwani na kwenye mbavu.
Mama yake alikwenda kumuona pale hospitali na alikuwa pamoja na Moze kando ya kitanda alicholazwa mwanaye kwa muda wote huo, ukiachilia mbali nyakati kadhaa ambazo Moze alilazimika kwenda darasani. Katika muda waliokuwa pamoja, Moze alipata fursa ya kumueleza mama Jaka mkasa wote mpaka ikafikia hatua ile.
Mama Jaka alizipokea habari zile kwa masikitiko makubwa.
“Lazima hao vijana wafunguliwe mashtaka Moze, lazima!” Mama Jaka alisema kwa hasira.
“Ni kweli…lakini patahitaji ushahidi mama, na kwa mujibu wa taarifa zilizopo, hakukuwa na mtu yeyote aliyeshuhudia wale vijana wakimpiga Jaka…Ray alimkuta akiwa amelala sakafuni kule msalani akiwa peka yake!”
“Si unasema aliwaona hao vijana rafiki zake Joakim sijui…wakitokea kule kule msalani? Ushahidi gani tena unahitajika hapo?”
“Aliwaona wakitokea usawa wa eneo la msalani, sio msalani kwenyewe!”
Mama Jaka aliuma meno kwa hasira.
“Kwani mwanangu alikutwa akiwa ameibiwa chochote huko msalani alikoachwa baada ya kipigo?” Aliuliza.
“Hapana mama…”
“Sa’ si unaona? Huwezi kusema kuwa hao waliompiga ni vibaka Moze…lazima hao watakuwa ni watu wenye kisasi au ugomvi naye tu! Sasa watu hao ni akina nani kama si hao akina Joakim? Hapa Jaka akipona tu ni kuwafungulia mashtaka…yote yakaelewekee huko huko!” Mama alikuja juu.
Moze alimtazama yule mama kwa muda.
“Sawa mama…lakini, mi’ nasomea sheria ujue. Na ingawa natal asana hawa jamaa wachukuliwe hatua…bado najua ni jinsi gani itakuwa vigumu kuwatia hatiani kwa kosa hili, japo mioyoni mwetu tunajua kuwa ni wao ndio waliohusika…!” Moze alimwambia mkwewe mtarajiwa.
“Tutapambana kisheria tu mwanangu! Hawa jamaa hawawezi kumfanya hivi mwanangu halafu tuwaangalie tu!” Mama Jaka aliazimia.
“Sawa mama. Basi tutakuwa pamoja katika hilo mwanzo mwisho. Nilitaka tu ujue hali halisi ili kupunguza kiwango cha kukatishwa tamaa pindi hitimisho la kesi hii litakapokuwa tofauti na matarajio yetu…” Moze alimalizia.
___________________
Taarifa za kipigo alichopokea Jaka zilimfurahisha sana Joakim. Alikuwa na uhakika kabisa kuwa baada ya kipigo kile, Jaka asingethubutu tena kumletea jeuri na kwamba mtoto Moze angemkubalia matakwa yake kwa kuhofia usalama wa mpenzi wake. Na ndio sababu alishindwa kuyaamini macho yake pale Moze alipofika chumbani kwake na kumwambia kuwa alikuwa ana maongezi na yeye.
Ilikuwa ni kiasi cha saa kumi na moja za jioni hivi, wiki moja tangu Jaka apate kile kipigo na Joakim alikuwa peke yake chumbani akijaribu kujisomea.
“Oh, Ka…karibu Moze...karibu...ingia tu mpaka ndani...” Joakim alimkaribisha Moze huku akianza kuisifu bahati yake. Moze alisimama kando ya mlango ndani ya chumba kile kidogo huku akimtazama kwa ghadhabu. Lile jicho la chuki alilokuwa akitupiwa na Moze lilimfanya agwaye kidogo na abaki akimkodolea macho ya viulizo yule binti.
Walitazamana kwa sekunde kadhaa bila ya yeyote kusema neno.
“Moze...vipi, naona leo umeamua kunitembelea, lakini nakuona kama...” Alianza kuongea, lakini hapo Moze akamkatisha.
“Joakim, kilichonileta hapa ni kitu kimoja tu, nacho ni kukujulisha kuwa iwapo unyama walioufanya rafiki zako kwa Jaka wangu unatokana na mimi kukataa kuwa kimada wako, basi mtu wa kupata adhabu ile alikuwa ni mimi na sio Jaka!”
Joakim alibaki mdomo wazi. Hakutarajia kuambiwa maneno kama yale.
“Ah, Moze…”
“Kitu ninachotaka wewe Joakim ukielewe ni kuwa mimi sikupendi na sitakupenda maisha yangu yote! Kwa hiyo huna utakalofanya ambalo litabadilisha msimamo wangu katika hilo na wala usijidanganye kuwa kuwatuma hao marafiki zako kufanya kitendo cha kijinga na cha kipumbavu kama kile kunaweza kubadilisha msimamo wangu na kunifanya nikubaliane nawe...na kama una mawazo hayo basi nakusikitikia sana Joakim kwani kwa hakika utakuwa ni mwenye kufilisika kibusara!” Maneno yale yalimchoma sana Joakim, lakini sio kama alivyochomwa na chuki ya wazi dhidi yake iliyo jidhihirisha usoni kwa yule mwanadada. Alibaki akimtazama Moze kwa mshangao na woga kwani Moze alikuwa kama mtu aliyepandwa na mashetani.
“Moze… Mimi sio...”
“Funga domo lako Joakim! Mimi sio mpumbavu hata kidogo na wala usijaribu kujidanganya kuwa wewe hukuhusika katika tukio lile...wewe ndio chanzo cha mambo yote haya na ndio maana na mimi nimekuja kwako ili nikupe yangu machache. Liwalo na liwe, mi’ niko tayari!”
“Nakubali Moze, lakini naomba uelewe kuwa mimi...”
“Nyamaza kimya Joakim nikueleze! Mi’ najua kuwa hata tukiwafungulia mashitaka hatutashinda hata kidogo, maana nyie ni watoto wa vigogo. Lakini huwezi kuushinda uthabiti wa moyo wangu na penzi lililomo ndani yake kwa Jaka! Kwa hiyo nimekuja kukueleza ukweli wa moyo wangu Joakim, nao ni kwamba mimi sikupendi! Sikupendi, sikupendi, sikupendi! Na wala sitaki kupendwa na wewe hata kidogo! Sasa kama wewe unadhani unanitaka sana kiasi cha kutaka kuniulia mpenzi wangu, basi leo ndio nimekuja ili unifanye hicho cha maana mno kwako hata utake kumuua mwenzako kwa ajili ya hicho ukitakacho kwangu! Lakini ujue kuwa mimi sikupendi na sitokupenda daima...tumeelewana?”
Heeeh!
Joakim aligwaya maradufu. Aliingiwa na woga wa ajabu kutokana na maneno ya yule binti na jinsi alivyoonesha chuki ya hali ya juu kwake.
“Haya mimi hapa sasa nimekuja! Fanya unalolitaka uniachie mpenzi wangu aishi!” Moze alimfokea kwa hasira huku akimkazia macho yaliyojaa hasira.
“Moze sikiliza...” Joakim aligwaya lakini Moze hakuwa na muda wa kusikiliza.
“Fanya basi, mbona maelezo mengi? We’ si kidume? Onesha basi huo udume wako!”
Tahayari ilimwingia Joakim na alijikuta akikaa kwenye kiti taratibu huku macho yake akiwa ameyainamisha chini.
“We’ si unanitaka sana? We’ si umezoea kila mwanamke unayemtaka ni lazima umpate? Sasa nimekuja ufanye hicho cha muhuimu sana kwako na ambacho huwezi kukipata sehemu nyingine isipokuwa kwangu, eeennh?” Moze aliendelea kumkemea kwa hasira.
Joakim alibaki kimya tu, wazi kuwa hakuwa ameitarajia hali ile.
ITAENDELEA
 
Vita vya panzi furaha kwa kunguru. Huo ugomvi wenu unatupa faida public hebu post na Utata wa 9 Disemba 1& 2, Miss Tanzania, Bondia, Mdunguaji.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SEHEMU YA ISHIRINI
Baada ya Raymond kuzunguka sehemu mbalimbali za ukumbi ule akiongea na jamaa kadhaa aliojuana nao huku akiendelea kula maraha, aliangalia saa yake na kugundua kuwa muda wao wa kuondoka ulikuwa umekaribia kwani walikubaliana waondoke pale ukumbini ifikapo saa nane na nusu za usiku. Saa yake ilimwambia kuwa muda ulikuwa ni saa nane na dakika kumi...
Huku nyuma, Jaka aliinuka na kumbusu mpenzi wake shavuni, akamuaga kuwa alikuwa anaelekea chooni kujisaidia haja ndogo. Moze aliafiki na kubaki peke yake pale mezani akimsubiri.
Walipoona kuwa Jaka amechukua uelekeo wa maeneo ya msalani, Ng’ase na Mudy walitazamana, na bila kuongea waliinuka kwa pamoja na kumfuata...
Raymond alimkuta Moze akiwa peke yake pale mezani, na alipomuulizia Jaka Moze akamfahamisha kuwa ameenda kujisaidia.
“Rose…?”
“Naye pia alitowekea huko huko kwenye muziki na mpaka sasa hajarudi.” Moze alijibu.
Raymond aliokota kipande cha nyama kutoka kwenye sahani iliyokuwa pale mezani na kukitupia kinywani. Alitafuna taratibu huku akiangaza huku na kule akijaribu kumtafuta Rose bila ya mafanikio.
“Mi’ naona nikamtafute Rose ili tukija hapa Jaka atakuwa amesharudi tunatimua, au vipi ?”
“Sawa Ray...wazo zuri.”
Raymond akapotelea ukumbini kumtafuta Rose.
________________________
Kule chooni Jaka alifunga zipu ya suruali yake na kugeuka huku akichomekea vizuri suruali akiwa katika hatua ya kutoka pale chooni baada ya kujisaidia.
Hakupiga hatua nyingine zaidi.
Muddy na Alphonce Ng’ase walikuwa wamesimama huku wakimtazama, na mara moja alijua kuwa balaa lilikuwa limemfika, kwani alimkuwa wazi kuwa wale jamaa walikuwa wamemsimamia namna ile kwa nia moja tu, nayo si kumsalimia.
Huku moyo ukimwenda kasi na akili yake ikifanya kazi ya ziada kujaribu kutafuta namna ya kujikwamua, alitupa jicho kulia kwake na hakuona chochote cha kumsaidia. Akatupa jicho kushoto nako akakuta hali ni hiyo hiyo. Aliona ajabu kwa nini walikuwa peke yao mle chooni ambapo kwa kawaida vyoo vya kumbi za starehe huwa haipiti dakika tano bila kuwa na mtu au watu wakijisaidia.
Aliinua macho yake na kuchungulia juu ya mabega ya wale jamaa na kugundua kuwa wale jamaa walikuwa wameufunga mlango ule kwa ndani ili kuhakikisha kuwa Jaka hafanikiwi kutoka mle chooni kabla hawajatimiza azma yao mbaya.
“Oi! Vipi tena tough guy, umeshituka kutuona rafiki zako wapenzi?” Muddy alimuuliza kwa kejeli huku akimsogelea. Jaka alipiga hatua mbele kuuwahi mlango huku akiwapisha wale jamaa.
“Samahani, naomba kupita...”
Alphonce Ng’ase alimdaka koo huku akimkemea kwa ukali.
“Sisi tunaongea na wewe halafu unajidai huelewi sio? Pumbavu!”
Hapo hapo Muddy akamtandika teke kali sana la mbavu, naye akahisi maumivu makali, mguno wa uchungu ukimtoka pasi kupenda. Aliinua mikono yake akijaribu kuuondoa mkono wa Alphonce uliomkaba koo, lakini Alphonce alimwachia koo haraka kabla Jaka hajamgusa na hapo hapo akamshindilia ngumi tatu za haraka haraka, mbili kwenye chembe, na moja ikimpata kwenye taya.
Jaka alilia kwa kipigo kile huku akipepesuka. Muddy aliruka na kumbabatiza teke la kifua lililomsukuma hadi ukutani, ambapo alipigiza mgongo na kisogo chake vibaya sana. Alihisi mlipuko wa kiza ukipita machoni mwake na miguu ikamuwia mizito. Alijitahidi kujizatiti kimakabiliano, lakini maumivu makali kutokea kisogoni kwake yalim[oteza kabisa muelekeo. Na kama hilo halikutosha, wale jamaa waliokuwa wamedhamiria kutompa kabisa nafasi ya kujitetea kimakabiliano walimvurumishia mvua ya mapigo bila ya huruma akiwa amebabatizwa pale ukutani, huku wakimiminiwa matusi kem kem. Nguvu zilimwishia Jaka, na huku akihisi kizunguzungu alidondokea magoti pale msalani, na alikuwa anaelekea kuangukia uso pale sakafuni wakati Alphonce Ng’ase alipomdaka koo. Alibaki akitweta huku uzito wake wote ukiwa umeegemezwa kwenye mkono wa Alphonce Ng’ase aliyemdaka koo. Alijaribu kuuinua uso wake ili amtazame yule jamaa aliyemdaka koo lakini hakuweza kwani macho yake yalimuwia mazito sana.
“Hizo zilikuwa ni salamu kutoka kwa Joakim...na nyingine zitafuata, Pusi wee!” Alphonce alimkoromea, kisha akamwachia na Jaka akaanguka sakafuni kama mzigo. Hapo hapo Muddy alimtandika teke la mbavu lililotoa mguno hafifu kutoka kwa Jaka.
Wale jamaa walibaki wakimwangalia kwa dharau akiwa amelala pale sakafuni kabla ya kugeuka na kutoka nje kimya kimya, wakimwacha Jaka akigaagaa kwenye mikojo na damu pale sakafuni.
Jaka alijaribu kuinuka bila ya mafanikio. Maumivu makali yalimtambaa mwilini na alihisi fahamu zikimpotea upesi mno. Alijaribu kutambaa kuelekea mlangoni huku akitoa sauti za kuomba msaada lakini sauti ilikuwa imemkauka na nguvu zilizidi kumwishia. Hatimaye alidondosha kichwa chake juu ya mkono wake uliolala pale sakafuni kwa kukata tamaa na kubaki akiwa amelala kifudifudi pale chooni bila ya kujali harufu kali ya mikojo na damu nyingi iliyokuwa ikimtoka puani na mdomoni. Akili yake ilitawaliwa na jambo moja tu muda ule...Moze.
Alijua kuwa baada ya kumfanyia yale waliyomfanyia wale jamaa wangeenda kwa Moze...
Sijui watamfanya nini tu maskini Moze wangu huko…
Wazo hilo lilimpa nguvu. Alijikurupusha na kupiga goti moja pale sakafuni huku akihisi maumivu makali mwilini na kichwani. Alipojaribu kuinua mguu wa pili alishindwa na kuanguka tena sakafuni kwa kishindo huku akihisi kiza kikitanda mbele ya macho yake.
Fahamu zikampotea.
_____________________
Kule ukumbini Raymond Mloo aliangalia saa yake kwa mara nyingine tena na kuwageukia Moze na Rose waliokuwa pamoja naye pale mezani.
“Jamani, mbona Jaka amechelewa sana kutoka...” Kabla hajamaliza kauli yake aliwaona Alphonce Ng’ase na mshirika wake wakitokea sehemu za kule msalani kwa mwendo wa haraka hali wakiangaza huku na huko. Mara moja alihisi hatari kwani aliuelewa fika uhasama uliojitokeza baina ya Jaka na Joakim, na alijua kuwa Alphonce na Muddy walikuwa ni marafiki wakubwa wa Joakim.
“Ooooh, Shiiit!” Aliropoka na kutoka mbio kuelekea kule chooni.
Kwa sekunde kadhaa Moze na Rose walibaki wakiwa wamepigwa butwaa pale mezani pasina kuelewa kilichokuwa kinaendelea. Kisha Moze naye akakurupuka na kutoka mbio kumfuata Raymond huku akiita jina la Jaka kwa kelele. Na hata wakati anaendelea kufanya hivyo, alimuona Raymond akitokea sehemu za eneo la kujisaidia wanaume huku akiwa anamburura Jaka kwa taabu. Moyo ulimlipuka na alihisi miguu ikimwisha nguvu. Akasimama palepale alipokuwa, macho yakiwa yamemtumbuka.
Jaka alikuwa ametapakaa damu sehemu ya mbele ya shati lake na jicho lake moja lilikuwa limevimba vibaya.
“Brown...! Brown! Oh, Mungu wangu! Ni nini tena kimetokea sasa?” Alibwabwaja huku akipepesuka kuelekea kule alipokuwa wanatokea Raymond akiwa nusu amembeba, nusu anamkokota Jaka. Baadhi ya wanachuo, wahudhuriaji wengine na wahudumu waliokuwepo pale ukumbini nao walianza kuelekea kule alipokuwa akitokea Raymond kujaribu kutoa msaada na kutaka kujua kilichotokea.
“Gari! Tafuta gari upesi!” Raymond alifoka huku akiendelea kumburura Jaka.
Kufikia hapo Moze na Rose walikuwa wakilia kama wajinga. Muda mfupi baadaye walikuwa ndani ya teksi wakielekea kituo cha afya cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Waliamua kwenda huko kwa kuwa ndipo mahala pekee ambapo walijua kuwa Jaka angeweza kupata huduma bila maswali mengi wala kuhitajika kutoa pesa za matibabu, wakizingatia kuwa wote walikuwa ni wanafunzi wasio na uwezo wa kumudu gharama za matibabu ya hospitali za nje ya chuo kikuu. Teksi ilikuwa inaendeshwa kwa mwendo wa kasi sana kuwarejesha chuoni, Raymond akiwa kiti cha mbele kando ya dereva hali Jaka akiwa amelazwa kwenye kiti cha nyuma akiwa amelaza kichwa chake kwenye mapaja ya Moze na miguu yake ikiwa kwenye mapaja ya Rose. Kutokea kwenye kile kiti cha nyuma, sauti za wale akina dada zilisikika zikilia taratibu.
Jaka alilazwa pale hospitali ya Chuo Kikuu kwa wiki mbili. Ndani ya wiki ya kwanza akiwa pale hospitali alikuwa akipoteza na kurudisha fahamu mara kwa mara kutokana na maumivu makali yaliyotokea kichwani na kwenye mbavu.
Mama yake alikwenda kumuona pale hospitali na alikuwa pamoja na Moze kando ya kitanda alicholazwa mwanaye kwa muda wote huo, ukiachilia mbali nyakati kadhaa ambazo Moze alilazimika kwenda darasani. Katika muda waliokuwa pamoja, Moze alipata fursa ya kumueleza mama Jaka mkasa wote mpaka ikafikia hatua ile.
Mama Jaka alizipokea habari zile kwa masikitiko makubwa.
“Lazima hao vijana wafunguliwe mashtaka Moze, lazima!” Mama Jaka alisema kwa hasira.
“Ni kweli…lakini patahitaji ushahidi mama, na kwa mujibu wa taarifa zilizopo, hakukuwa na mtu yeyote aliyeshuhudia wale vijana wakimpiga Jaka…Ray alimkuta akiwa amelala sakafuni kule msalani akiwa peka yake!”
“Si unasema aliwaona hao vijana rafiki zake Joakim sijui…wakitokea kule kule msalani? Ushahidi gani tena unahitajika hapo?”
“Aliwaona wakitokea usawa wa eneo la msalani, sio msalani kwenyewe!”
Mama Jaka aliuma meno kwa hasira.
“Kwani mwanangu alikutwa akiwa ameibiwa chochote huko msalani alikoachwa baada ya kipigo?” Aliuliza.
“Hapana mama…”
“Sa’ si unaona? Huwezi kusema kuwa hao waliompiga ni vibaka Moze…lazima hao watakuwa ni watu wenye kisasi au ugomvi naye tu! Sasa watu hao ni akina nani kama si hao akina Joakim? Hapa Jaka akipona tu ni kuwafungulia mashtaka…yote yakaelewekee huko huko!” Mama alikuja juu.
Moze alimtazama yule mama kwa muda.
“Sawa mama…lakini, mi’ nasomea sheria ujue. Na ingawa natal asana hawa jamaa wachukuliwe hatua…bado najua ni jinsi gani itakuwa vigumu kuwatia hatiani kwa kosa hili, japo mioyoni mwetu tunajua kuwa ni wao ndio waliohusika…!” Moze alimwambia mkwewe mtarajiwa.
“Tutapambana kisheria tu mwanangu! Hawa jamaa hawawezi kumfanya hivi mwanangu halafu tuwaangalie tu!” Mama Jaka aliazimia.
“Sawa mama. Basi tutakuwa pamoja katika hilo mwanzo mwisho. Nilitaka tu ujue hali halisi ili kupunguza kiwango cha kukatishwa tamaa pindi hitimisho la kesi hii litakapokuwa tofauti na matarajio yetu…” Moze alimalizia.
___________________
Taarifa za kipigo alichopokea Jaka zilimfurahisha sana Joakim. Alikuwa na uhakika kabisa kuwa baada ya kipigo kile, Jaka asingethubutu tena kumletea jeuri na kwamba mtoto Moze angemkubalia matakwa yake kwa kuhofia usalama wa mpenzi wake. Na ndio sababu alishindwa kuyaamini macho yake pale Moze alipofika chumbani kwake na kumwambia kuwa alikuwa ana maongezi na yeye.
Ilikuwa ni kiasi cha saa kumi na moja za jioni hivi, wiki moja tangu Jaka apate kile kipigo na Joakim alikuwa peke yake chumbani akijaribu kujisomea.
“Oh, Ka…karibu Moze...karibu...ingia tu mpaka ndani...” Joakim alimkaribisha Moze huku akianza kuisifu bahati yake. Moze alisimama kando ya mlango ndani ya chumba kile kidogo huku akimtazama kwa ghadhabu. Lile jicho la chuki alilokuwa akitupiwa na Moze lilimfanya agwaye kidogo na abaki akimkodolea macho ya viulizo yule binti.
Walitazamana kwa sekunde kadhaa bila ya yeyote kusema neno.
“Moze...vipi, naona leo umeamua kunitembelea, lakini nakuona kama...” Alianza kuongea, lakini hapo Moze akamkatisha.
“Joakim, kilichonileta hapa ni kitu kimoja tu, nacho ni kukujulisha kuwa iwapo unyama walioufanya rafiki zako kwa Jaka wangu unatokana na mimi kukataa kuwa kimada wako, basi mtu wa kupata adhabu ile alikuwa ni mimi na sio Jaka!”
Joakim alibaki mdomo wazi. Hakutarajia kuambiwa maneno kama yale.
“Ah, Moze…”
“Kitu ninachotaka wewe Joakim ukielewe ni kuwa mimi sikupendi na sitakupenda maisha yangu yote! Kwa hiyo huna utakalofanya ambalo litabadilisha msimamo wangu katika hilo na wala usijidanganye kuwa kuwatuma hao marafiki zako kufanya kitendo cha kijinga na cha kipumbavu kama kile kunaweza kubadilisha msimamo wangu na kunifanya nikubaliane nawe...na kama una mawazo hayo basi nakusikitikia sana Joakim kwani kwa hakika utakuwa ni mwenye kufilisika kibusara!” Maneno yale yalimchoma sana Joakim, lakini sio kama alivyochomwa na chuki ya wazi dhidi yake iliyo jidhihirisha usoni kwa yule mwanadada. Alibaki akimtazama Moze kwa mshangao na woga kwani Moze alikuwa kama mtu aliyepandwa na mashetani.
“Moze… Mimi sio...”
“Funga domo lako Joakim! Mimi sio mpumbavu hata kidogo na wala usijaribu kujidanganya kuwa wewe hukuhusika katika tukio lile...wewe ndio chanzo cha mambo yote haya na ndio maana na mimi nimekuja kwako ili nikupe yangu machache. Liwalo na liwe, mi’ niko tayari!”
“Nakubali Moze, lakini naomba uelewe kuwa mimi...”
“Nyamaza kimya Joakim nikueleze! Mi’ najua kuwa hata tukiwafungulia mashitaka hatutashinda hata kidogo, maana nyie ni watoto wa vigogo. Lakini huwezi kuushinda uthabiti wa moyo wangu na penzi lililomo ndani yake kwa Jaka! Kwa hiyo nimekuja kukueleza ukweli wa moyo wangu Joakim, nao ni kwamba mimi sikupendi! Sikupendi, sikupendi, sikupendi! Na wala sitaki kupendwa na wewe hata kidogo! Sasa kama wewe unadhani unanitaka sana kiasi cha kutaka kuniulia mpenzi wangu, basi leo ndio nimekuja ili unifanye hicho cha maana mno kwako hata utake kumuua mwenzako kwa ajili ya hicho ukitakacho kwangu! Lakini ujue kuwa mimi sikupendi na sitokupenda daima...tumeelewana?”
Heeeh!
Joakim aligwaya maradufu. Aliingiwa na woga wa ajabu kutokana na maneno ya yule binti na jinsi alivyoonesha chuki ya hali ya juu kwake.
“Haya mimi hapa sasa nimekuja! Fanya unalolitaka uniachie mpenzi wangu aishi!” Moze alimfokea kwa hasira huku akimkazia macho yaliyojaa hasira.
“Moze sikiliza...” Joakim aligwaya lakini Moze hakuwa na muda wa kusikiliza.
“Fanya basi, mbona maelezo mengi? We’ si kidume? Onesha basi huo udume wako!”
Tahayari ilimwingia Joakim na alijikuta akikaa kwenye kiti taratibu huku macho yake akiwa ameyainamisha chini.
“We’ si unanitaka sana? We’ si umezoea kila mwanamke unayemtaka ni lazima umpate? Sasa nimekuja ufanye hicho cha muhuimu sana kwako na ambacho huwezi kukipata sehemu nyingine isipokuwa kwangu, eeennh?” Moze aliendelea kumkemea kwa hasira.
Joakim alibaki kimya tu, wazi kuwa hakuwa ameitarajia hali ile.
ITAENDELEA
Ni kweli kwamba hujaona katazo la mhusika wa hizi riwaya? Ama umeamua kukausha tu kwa kuwa unajua huwezi kufanywa kitu, uko nyuma ya keyboard?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom