HaMachiach
JF-Expert Member
- Dec 15, 2015
- 3,399
- 6,077
RIWAYA: MASHARIKI YA MBALI
KALAMU YA: George Iron Mosenya
SEHEMU YA KWANZA.
Hekaheka zilizoanza takribani majuma mawili na nusu nyuma, zilikuwa zimechochea moto katika siku hii. Ikiwa ni siku moja tu kabla ya tukio lililoleta hekaheka hizo.
Katika jiji la Mainstream kilichokuwa kinazungumzwa zaidi ni kuhusiana na maandamano ya amani kupinga uteuzi wa waziri mkuu ambaye alikuwa akijihusisha na vitendo vya kishoga waziwazi. Licha ya kwamba sheria ya nchi yao iliruhusu uhalali wa vitendo vya ushoga bado wananchi hawakuridhia kabisa kuwa na waziri mkuu shoga. Walikuwa radhi kuishi na mashoga mtaani lakini sio kuwaona katika magari ya serikali wakitimiza wajibu wao.
Walishindwa kutimiza wajibu wao wa kuwa wanaume wataweza kutimiza wajibu wao kama viongozi? Hili lilikuwa swali kuu.
Baada ya kuhamasishana kwa takribani majuma mawili kwa kutumia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii. Maandamano haya yalikuwa habari kubwa sana nchini Semedari.
Mitaa ilingoja kwa hamu sana kuishuhudia siku hiyo ambayo waziri mkuu angepaswa kung’atuka kwa namna yoyote ile. Huku Mashoga na wanaoongoza taasisi zao wakifanya dua zao maandamano yale yasifanikiwe wabaki kuwa na waziri mkuu aliye upande wao.
Siku zikahesabika na hatimaye ikabaki siku moja tu.
Na sasa yalikuwa ni masaa.
_____
Daniel katunzi alikuwa amejifungia chumbani kwake tumbo likiwa linamuuma kwa juhudina kichwa kikigonga kwa fujo sana.
Hakuwa Daniel yule mchangamfu, huyu wa siku hii alikuwa amepooza sana. Wanafamilia kwa ujumla walitambua hali hii na kuhisi huenda anaumwa.
Lakini Daniel ni wa kushindwa kusema angali anaumwa? Hili lilikuwa swali la kila mmoja kujiuliza……
Haikuwa kawaida yake hata kidogo.
Akiwa chumbani Daniel alishindwa kulala kama alivyokuwa ameaga baada ya kushindwa kumaliza chakula, usingizi ulipaa mbali naye.
Alijigeuza huku na kule na kisha akaamua kuufungua mlango na kurejea tena sebuleni.
Chumbani palikuwa hapakaliki!!
Aliikuta familia nzima ikiwa imepooza…. Chakula kikiwa kama alivyokiacha.
“Dany.. unaumwa kijana wangu.” Mama wa familia ile aitwaye Diana alimuuliza kwa upole.
Ni kama swali hilo aliuliza kwa niaba ya familia nzima kwani kila mmoja alitikisa kichwa kuunga mkono.
“Kichwa kinaniuma sana. Na tumbo pia… lakini si kwamba ninaumwa.” Alijibu Daniel Katunzi kwa unyonge.
Jibu lile likawa moja kati ya mastaajabisho ya usiku ule.
Ati! Anaumwa lakini haumwi.
“Unamaanisha nini?”
“Ni kichwa kinauma na tumbo pia lakini mimi najua siumwi.” Alijibu huku akijibweteka katika kochi kubwa la kustarehe lililokuwa jirani naye. Likanesanesa kisha likatulia naye akatulia tuli.
“Kesho nd’o ile siku nadhani.” Alizungumza bila kujulikana kama anauliza ama anaanza kujenga hoja.
“Ndio Dany, kesho tunaingia barabarani… kila mmoja ameandaa bango lake nawe tumekuandalia moja utajichagulia lolote la kuandika. Ikiwa afya itaruhusu basi tutaenda wote. Tena kuandamana ni mazoezi… maana utatembea kidogo walau nawe uuone mji wetu ukijaa watu unavyokuwa. Uone wanavyotabasamu…” Maria, Binti mdogo katika familia ile ya watoto watatu alijibu kwa uchangamfu mkubwa.
“Tabasamu?” Dany alishtuka.
“Mazoezi?” akaujazia uzito mshtuko wake. Na hapo akaketi vyema akiwa anawashangaa wanaomshangaa yeye.
Wakashangaana!
“Napenda kuwashauri tubaki ndani tusiende katika maandamano hayo…” alizungumza akiwa katika mchanganyiko wa huzuni na fadhaa.
“Whaaat! Huo ni usaliti…. Familia yangu haiwezi kufanya dhambi hiyo…” Diana. Mama wa familia aling’aka akiwa wima.
“Daniel…”… Maria alimuita kwa unyonge lakini asiweze kusema lolote hata Daniel alipomtazama.
“Si chini ya miaka mitano ama sita imepita. Lakini kamwe sijaisahau Mashariki ya mbali. Mashariki inayokaliwa na raia kama mimi ambao akili zetu zimeruka na kukaa mashariki, ubongo umelalia mashariki bila kujua magharibi ni wapi sahau kuhusu kusini……” akaweka kituo akameza funda la mate na kuketi vyema akiwa anatazama chini.
“Hali ilikuwa kama hii niionayo kwenu, lakini sababu zetu zilikuwa tofauti. Naona yenu ni sababu dhaifu sana……”
“Sababu dhaifu! Una maana gani, yaani tunaongozwa na waziri aliyeolewa na mwanaume mwenzake halafu unasema ni sababu dhaifu. Semedari ni nchi kubwa sana kiuchumi duniani, haipaswi kuongozwa na mtu dhaifu….” Danstani alizungumza kwa mara ya kwanza katika hali ya kufoka. Huyu akiwa ni kijana mkubwa wa Diana.
DANIEL ANASIMULIA
Tembo walivamia kijiji cha Mafisa, huko Mashariki ya mbali ninapotoka. Uvamizi wao wa kwanza ulianza kwa kuharibu mazao. Wananchi walioharibiwa mashamba wakatoa taarifa katika serikali ya mtaa juu ya hili. Afisa wa serikali ya mitaa yeye hana shamba hivyo hakuguswa na habari hii, akaipokea taarifa na kuiweka katika meza yake kama taarifa isiyokuwa ya msingi. Mashamba yaliendelea kuharibiwa…. Tembo ni mnyama na hana akili…. Alipomalizana na mashamba akaanza kudhuru watu. Watoto wawili walikanyagwa na tembo na kupoteza maisha. Kwa sababu wale watoto hawakuwa wa afisa wa kata aliipokea taarifa na kuiweka katika meza yake kama taarifa ya ziada. Lakini usoni akihuzunika na kutoa pole za dhati kwa wafiwa.
Huzuni ya kinafiki!!
Mtoa taarifa akarejea baada ya siku nne kuulizia maendeleo yoyote kuhusu kuchukua hatua za kiusalama. Afisa akadai kuwa kwa takribani juma zima simu yake haina pesa za kupiga wala kutuma meseji (SMS). Na hapo akaanza kulalamika kuwa mtoa taarifa si mzalendo kabisa, ametoa taarifa lakini hakulipia hata senti tano ya kuchangia wino wa kujaza katika muhuri. Afisa akaenda mbali na kusema kuwa wananchi wanajitazama wao pekee wakipatwa na matatizo lakini hawatazami upande mwingine wa shilingi. Na hapo akatoa hitimisho kuwa wapambane na hao tembo kama watawaweza.
Mtoa taarifa akaondoka akiwa mwenye huzuni sana akawafikishia wakulima wenzake na wananchi waliokuwa katika kijiwe hicho.
Wananchi wakashangazwa sana na majibu yale, kwa jinsi walivyovimba kwa jazba hawakutaka kungoja. Wakaondoka kuelekea nyumbani kwa afisa huyo.
Hawakumkuta ofisini wakamfuata nyumbani kwake. Wakamfokea kwa maneno makali hasahasa ya kulewa madaraka yale madogo na kuwasahau wananchi.
Wakaondoka na jazba zao na kuhamasishana kuwa hawana mtetezi basi watalazimika kujiunda vikundi vikundi na kuyalinda mashamba yao pamoja na familia kwa ujumla.
La mgambo likalia na jambo lenyewe likatangazwa.
Baada ya siku mbili tembo wawili waliuwawa.
Na punde baada ya tembo wawili kuuwawa serikali ikahamia katika kijiji cha Mafisa. Walipouwawa watoto wawili serikali haikutokea hata msibani lakini tembo walipouwawa ikajaa pale kijijini na msako ukaanza wa nani aliwaua tembo.
Afisa wa kijiji kile alipofuatwa akawataja wahusika kuwa ni wale waliomfuata nyumbani na kumfokea, akawapatia majina ya wale waliomwandikia barua mbili ofisi kumpatia taarifa kuwa wamevamiwa na tembo.
Haraka sana wakakamatwa na kudhalilishwa mbele ya familia zao. Ilikuwa ni usiku wengine wakiwa uchi wa mnyama na wengine wakiwa na nguo fupi za kulalia.
Walipigwa sana huku wakishutumiwa kuwa wao ni wawindaji haramu.
Uharamu huo nd’o hatukuwahi kuufahamu, tembo hakung’olewa jino wala pembe yake….. aliuwawa tu.
Mmoja kati ya wale watuhumiwa alipoteza maisha akiwa rumande, polisi wakamtupa mitaroni na kudai kuwa alifanya jaribio la kutoroka wakapambana naye….. nchi ikasikia juu ya wengine sita kuwa wapo ndani na wana majeraha makubwa sana.
Kilio cha Mafisa kikadondosha chozi lake katika ardhi nzima ya Mashariki ya mbali.
Wananchi wakaanza kuhamasishana kuhusu maandamano ya amani kuhakikisha wakazi wale wa Mafisa wanaipata haki yao.
Kilichotokea nd’o kinachoniumiza kichwa hadi leo.
Hatukuwa na silaha, tulijitahidi hata tusitembee na kalamu mifukoni wasije wakasema ni visu vya kisasa. Hata waliokuwa na nywele ndefu tuliwaambia wazinyoe maana hawakawii kusema kuwa lile lundo la nywele limeficha bangi ndani yake.
Tulihakikisha maandamo yetu yanakuwa swafi kuliko namna tujiwekavyo kila tuendapo katika ibada.
Ule usafi tuliojitahidi uwe ukatuachia doa. Ilikuwa ni bahati sana ukivunjwa na kuachwa hai, kuna waliotolewa macho na hadi sasa wanamshukuru Mungu kwa kuwatetea…..
Kama mtu anamshukuru Mungu kwa kung’olewa jicho pekee. Jiulize wasioshukuru ni kipi ,kiliwasibu?
Nilikuwa naziona vita katika runinga lakini kule mashariki ya mbali nilijiona nipo katika vita, niliuona mlipuko wa mabomu na niliona kwa macho na sikio langu lilisikia mtu akiwa anataka kukata roho lugha mpya anayoiongea inavyoumiza kusikiliza hata kama hauelewi asemacho.
Mashariki ya mbali tuliuwawa kwa kujaribu tu kuwatetea wale waliokuwa wanafia rumande bila hatia. Na sio kwamba sisi tulitaka waachiwe huru la! Sisi tulitaka watibiwe wasije kufia rumande kama wenzao. Hilo tu!!!
Nikisema sababu yenu ni dhaifu msinihesabu kama muoga.
Nilishiriki maandamano yale ya amani ambayo yaligeuka vita kati ya wenye silaha na wasiokuwa nazo.
Kwa kifupi huko mashariki ya mbali tulipigana vita ya uonevu.
Shangazi yangu mpole kabisa alikamatwa akiwa katika mgahawa wake na mtoto wake mdogo mgongoni alipigwa na kupoteza maisha mbele ya mtoto wake. Kisa ni cha kuchekesha…..
Alikuwa anamwaga maji barabarani, bahati mbaya iliyoje yale maji yaliyokuwa na masalia kidogo ya ukoko wa ubwabwa yakalifikia gari la polisi lililokuwa likikatiza.
Wakasimamisha gari ghafla na kumvamia wakimlazimisha alioshe gari lile kwa sababu ana dharau.
Shangazi akalifuta gari pale palipoguswa na ukoko, wakamlazimisha aoshe gari lote.
Shangazi akahoji kwanini wanamfanyia vile angali amesema ni bahati mbaya.
Na hata kabla hawajamjibu mtoto wake akaanza kulia, shangazi akamjali mwanaye na hiyo kwao wakaitafsiri kama dharau kwao.
Shangazi aliuwawa!
Naomba muamini kuwa sababu yenu ya kesho ni dhaifu sana.
___________
Ilikuwa ni simulizi ya dakika ishirini na tano, simulizi iliyojenga ukimya wa hali ya juu. Na hata Daniel alipokinyanyua kichwa chake alikutana na uso wa Diana ukiwa umelowana kwa machozi, Maria alikuwa ameuficha uso wake, Danstan alikuwa anajikaza kiume kwa kung’atang’ata meno yake.
“Serikali ilitoa tamko gani kwa ukatili huo” Danstani aliuliza huku akionyesha jazba za waziwazi.
“What’s the https://jamii.app/JFUserGuide!! Ingetoa tamko gani Danstani, labda ingetangaza kuwa IMESHINDA VITA kwa kishindo..” Diana alizungumza huku akishindwa kudhibiti hamaniko lake.
“Daniel mwanangu. Huku kwetu hakuna kitu kama hicho. Tuna uhuru asilimia 100 wa kufanya maandamano kwa lolote ambalo tunaona kwamba halipo sawa. Ni wajibu wetu kuikumbusha serikali kuwa wananchi ni moja ya nguzo kuu katika serikali na tunapaswa kuiwajibisha serikali yetu kila inapokwenda njia isiyokuwa sahihi na bunge likiwa kimya.” Diana alimgeukia Daniel na kutoa ufafanuzi.
Akatoa ufafanuzi zaidi kwa kutoa mifano yakinifu ya matukio kadha wa kadha yaliyowahi kutokea nchini humo.
“Daniel na bado kila siku unasisitiza kuwa unahitaji kurudi Mashariki ya mbali.” Maria alimuuliza kwa unyonge sana.
“Hakika natamani sana kurudi Mashariki ya mbali. Ni huko nilipozaliwa na nitarejea. Si kwa sababu za kuibadilisha nchi bali kula kwa pamoja raha na karaha za ardhi ile.”
“Raha? Kuna raha gani katika nchi inayoua raia wake sasa…” Diana aling’aka
“Juma lililopita nakumbuka niliwasikia mkizungumzia juu ya waziri wa nishati aliyejiuzuru baada ya umeme kukatika bungeni kwa muda wa dakika tano.
Kule kwetu kuna raha ya aina yake, na raha nyingi tunazozipata husababishwa na karaha tunazopitia. Kule kwetu tukisikia waziri kama huyo aliyejiuzuru eti kisa dakika tano kwetu ni kichekesho kikubwa sana, na kwanza ni uzembe mno wa kimaamuzi. Umeme unakatwa kwa siku tatu mfululizo na waziri anapita tunapungia mkono kwa shangwe… sio raha hizo?
Katika hizo siku tatu umeme unapokatika tunatoa kila aina mpya ya matusi kwa taasisi husika, lakini hayo matusi tunaambizana sisi kwa sisi sio kwamba tunawatukana wao. Bado tu huioni raha?
Baada ya hizo siku tatu za umeme kukatika pindi utakaporejea tunaungana kwa pamoja nchi nzima, akina baba kina mama na watoto tunasema kwa pamoja ‘HUOO’. Hujapata tu sababu ya kufurahi?
Na kisha kila mmoja anaendelea na maisha yake, matusi yanaishia hewani na hatutukani tena. Ukijifanya unaendelea kutukana angali umeme umerejea watu wanabaki kukushangaa.
Lazima nitarejea Mashariki ya mbali.” Daniel aliweka kituo katika simulizi yake.
Nyuso za tabasamu zikatawala nyumba ile, Daniel alikuwa amewapa sababu mbili kwa pamoja. Kwanza aliwatupa katika msiba na vilio kisha akazisafisha nyuso zao na tabasamu japo lilikuwa tabasamu la karaha.
Wakaagana kwa mara nyingine wakikiacha kile chakula mezani na kila mmoja kwenda katika chumba chake kuuchapa usingizi.
Akiwa chumbani kaka mkubwa katika familia ile, Danstan alianza kuingiwa na ushawishi wa kuitembelea Mashariki ya mbali.
Hakujua nini maana ya tamanio lake hilo.
NAAAM! RIWAYA hii ya Mashariki ya bali itakuwa ikikujia muda na wakati kama huu kila siku mpaka itakapotimu tamati yake…….
Maoni yako ni muhimu sana!!
KALAMU YA: George Iron Mosenya
SEHEMU YA KWANZA.
Hekaheka zilizoanza takribani majuma mawili na nusu nyuma, zilikuwa zimechochea moto katika siku hii. Ikiwa ni siku moja tu kabla ya tukio lililoleta hekaheka hizo.
Katika jiji la Mainstream kilichokuwa kinazungumzwa zaidi ni kuhusiana na maandamano ya amani kupinga uteuzi wa waziri mkuu ambaye alikuwa akijihusisha na vitendo vya kishoga waziwazi. Licha ya kwamba sheria ya nchi yao iliruhusu uhalali wa vitendo vya ushoga bado wananchi hawakuridhia kabisa kuwa na waziri mkuu shoga. Walikuwa radhi kuishi na mashoga mtaani lakini sio kuwaona katika magari ya serikali wakitimiza wajibu wao.
Walishindwa kutimiza wajibu wao wa kuwa wanaume wataweza kutimiza wajibu wao kama viongozi? Hili lilikuwa swali kuu.
Baada ya kuhamasishana kwa takribani majuma mawili kwa kutumia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii. Maandamano haya yalikuwa habari kubwa sana nchini Semedari.
Mitaa ilingoja kwa hamu sana kuishuhudia siku hiyo ambayo waziri mkuu angepaswa kung’atuka kwa namna yoyote ile. Huku Mashoga na wanaoongoza taasisi zao wakifanya dua zao maandamano yale yasifanikiwe wabaki kuwa na waziri mkuu aliye upande wao.
Siku zikahesabika na hatimaye ikabaki siku moja tu.
Na sasa yalikuwa ni masaa.
_____
Daniel katunzi alikuwa amejifungia chumbani kwake tumbo likiwa linamuuma kwa juhudina kichwa kikigonga kwa fujo sana.
Hakuwa Daniel yule mchangamfu, huyu wa siku hii alikuwa amepooza sana. Wanafamilia kwa ujumla walitambua hali hii na kuhisi huenda anaumwa.
Lakini Daniel ni wa kushindwa kusema angali anaumwa? Hili lilikuwa swali la kila mmoja kujiuliza……
Haikuwa kawaida yake hata kidogo.
Akiwa chumbani Daniel alishindwa kulala kama alivyokuwa ameaga baada ya kushindwa kumaliza chakula, usingizi ulipaa mbali naye.
Alijigeuza huku na kule na kisha akaamua kuufungua mlango na kurejea tena sebuleni.
Chumbani palikuwa hapakaliki!!
Aliikuta familia nzima ikiwa imepooza…. Chakula kikiwa kama alivyokiacha.
“Dany.. unaumwa kijana wangu.” Mama wa familia ile aitwaye Diana alimuuliza kwa upole.
Ni kama swali hilo aliuliza kwa niaba ya familia nzima kwani kila mmoja alitikisa kichwa kuunga mkono.
“Kichwa kinaniuma sana. Na tumbo pia… lakini si kwamba ninaumwa.” Alijibu Daniel Katunzi kwa unyonge.
Jibu lile likawa moja kati ya mastaajabisho ya usiku ule.
Ati! Anaumwa lakini haumwi.
“Unamaanisha nini?”
“Ni kichwa kinauma na tumbo pia lakini mimi najua siumwi.” Alijibu huku akijibweteka katika kochi kubwa la kustarehe lililokuwa jirani naye. Likanesanesa kisha likatulia naye akatulia tuli.
“Kesho nd’o ile siku nadhani.” Alizungumza bila kujulikana kama anauliza ama anaanza kujenga hoja.
“Ndio Dany, kesho tunaingia barabarani… kila mmoja ameandaa bango lake nawe tumekuandalia moja utajichagulia lolote la kuandika. Ikiwa afya itaruhusu basi tutaenda wote. Tena kuandamana ni mazoezi… maana utatembea kidogo walau nawe uuone mji wetu ukijaa watu unavyokuwa. Uone wanavyotabasamu…” Maria, Binti mdogo katika familia ile ya watoto watatu alijibu kwa uchangamfu mkubwa.
“Tabasamu?” Dany alishtuka.
“Mazoezi?” akaujazia uzito mshtuko wake. Na hapo akaketi vyema akiwa anawashangaa wanaomshangaa yeye.
Wakashangaana!
“Napenda kuwashauri tubaki ndani tusiende katika maandamano hayo…” alizungumza akiwa katika mchanganyiko wa huzuni na fadhaa.
“Whaaat! Huo ni usaliti…. Familia yangu haiwezi kufanya dhambi hiyo…” Diana. Mama wa familia aling’aka akiwa wima.
“Daniel…”… Maria alimuita kwa unyonge lakini asiweze kusema lolote hata Daniel alipomtazama.
“Si chini ya miaka mitano ama sita imepita. Lakini kamwe sijaisahau Mashariki ya mbali. Mashariki inayokaliwa na raia kama mimi ambao akili zetu zimeruka na kukaa mashariki, ubongo umelalia mashariki bila kujua magharibi ni wapi sahau kuhusu kusini……” akaweka kituo akameza funda la mate na kuketi vyema akiwa anatazama chini.
“Hali ilikuwa kama hii niionayo kwenu, lakini sababu zetu zilikuwa tofauti. Naona yenu ni sababu dhaifu sana……”
“Sababu dhaifu! Una maana gani, yaani tunaongozwa na waziri aliyeolewa na mwanaume mwenzake halafu unasema ni sababu dhaifu. Semedari ni nchi kubwa sana kiuchumi duniani, haipaswi kuongozwa na mtu dhaifu….” Danstani alizungumza kwa mara ya kwanza katika hali ya kufoka. Huyu akiwa ni kijana mkubwa wa Diana.
DANIEL ANASIMULIA
Tembo walivamia kijiji cha Mafisa, huko Mashariki ya mbali ninapotoka. Uvamizi wao wa kwanza ulianza kwa kuharibu mazao. Wananchi walioharibiwa mashamba wakatoa taarifa katika serikali ya mtaa juu ya hili. Afisa wa serikali ya mitaa yeye hana shamba hivyo hakuguswa na habari hii, akaipokea taarifa na kuiweka katika meza yake kama taarifa isiyokuwa ya msingi. Mashamba yaliendelea kuharibiwa…. Tembo ni mnyama na hana akili…. Alipomalizana na mashamba akaanza kudhuru watu. Watoto wawili walikanyagwa na tembo na kupoteza maisha. Kwa sababu wale watoto hawakuwa wa afisa wa kata aliipokea taarifa na kuiweka katika meza yake kama taarifa ya ziada. Lakini usoni akihuzunika na kutoa pole za dhati kwa wafiwa.
Huzuni ya kinafiki!!
Mtoa taarifa akarejea baada ya siku nne kuulizia maendeleo yoyote kuhusu kuchukua hatua za kiusalama. Afisa akadai kuwa kwa takribani juma zima simu yake haina pesa za kupiga wala kutuma meseji (SMS). Na hapo akaanza kulalamika kuwa mtoa taarifa si mzalendo kabisa, ametoa taarifa lakini hakulipia hata senti tano ya kuchangia wino wa kujaza katika muhuri. Afisa akaenda mbali na kusema kuwa wananchi wanajitazama wao pekee wakipatwa na matatizo lakini hawatazami upande mwingine wa shilingi. Na hapo akatoa hitimisho kuwa wapambane na hao tembo kama watawaweza.
Mtoa taarifa akaondoka akiwa mwenye huzuni sana akawafikishia wakulima wenzake na wananchi waliokuwa katika kijiwe hicho.
Wananchi wakashangazwa sana na majibu yale, kwa jinsi walivyovimba kwa jazba hawakutaka kungoja. Wakaondoka kuelekea nyumbani kwa afisa huyo.
Hawakumkuta ofisini wakamfuata nyumbani kwake. Wakamfokea kwa maneno makali hasahasa ya kulewa madaraka yale madogo na kuwasahau wananchi.
Wakaondoka na jazba zao na kuhamasishana kuwa hawana mtetezi basi watalazimika kujiunda vikundi vikundi na kuyalinda mashamba yao pamoja na familia kwa ujumla.
La mgambo likalia na jambo lenyewe likatangazwa.
Baada ya siku mbili tembo wawili waliuwawa.
Na punde baada ya tembo wawili kuuwawa serikali ikahamia katika kijiji cha Mafisa. Walipouwawa watoto wawili serikali haikutokea hata msibani lakini tembo walipouwawa ikajaa pale kijijini na msako ukaanza wa nani aliwaua tembo.
Afisa wa kijiji kile alipofuatwa akawataja wahusika kuwa ni wale waliomfuata nyumbani na kumfokea, akawapatia majina ya wale waliomwandikia barua mbili ofisi kumpatia taarifa kuwa wamevamiwa na tembo.
Haraka sana wakakamatwa na kudhalilishwa mbele ya familia zao. Ilikuwa ni usiku wengine wakiwa uchi wa mnyama na wengine wakiwa na nguo fupi za kulalia.
Walipigwa sana huku wakishutumiwa kuwa wao ni wawindaji haramu.
Uharamu huo nd’o hatukuwahi kuufahamu, tembo hakung’olewa jino wala pembe yake….. aliuwawa tu.
Mmoja kati ya wale watuhumiwa alipoteza maisha akiwa rumande, polisi wakamtupa mitaroni na kudai kuwa alifanya jaribio la kutoroka wakapambana naye….. nchi ikasikia juu ya wengine sita kuwa wapo ndani na wana majeraha makubwa sana.
Kilio cha Mafisa kikadondosha chozi lake katika ardhi nzima ya Mashariki ya mbali.
Wananchi wakaanza kuhamasishana kuhusu maandamano ya amani kuhakikisha wakazi wale wa Mafisa wanaipata haki yao.
Kilichotokea nd’o kinachoniumiza kichwa hadi leo.
Hatukuwa na silaha, tulijitahidi hata tusitembee na kalamu mifukoni wasije wakasema ni visu vya kisasa. Hata waliokuwa na nywele ndefu tuliwaambia wazinyoe maana hawakawii kusema kuwa lile lundo la nywele limeficha bangi ndani yake.
Tulihakikisha maandamo yetu yanakuwa swafi kuliko namna tujiwekavyo kila tuendapo katika ibada.
Ule usafi tuliojitahidi uwe ukatuachia doa. Ilikuwa ni bahati sana ukivunjwa na kuachwa hai, kuna waliotolewa macho na hadi sasa wanamshukuru Mungu kwa kuwatetea…..
Kama mtu anamshukuru Mungu kwa kung’olewa jicho pekee. Jiulize wasioshukuru ni kipi ,kiliwasibu?
Nilikuwa naziona vita katika runinga lakini kule mashariki ya mbali nilijiona nipo katika vita, niliuona mlipuko wa mabomu na niliona kwa macho na sikio langu lilisikia mtu akiwa anataka kukata roho lugha mpya anayoiongea inavyoumiza kusikiliza hata kama hauelewi asemacho.
Mashariki ya mbali tuliuwawa kwa kujaribu tu kuwatetea wale waliokuwa wanafia rumande bila hatia. Na sio kwamba sisi tulitaka waachiwe huru la! Sisi tulitaka watibiwe wasije kufia rumande kama wenzao. Hilo tu!!!
Nikisema sababu yenu ni dhaifu msinihesabu kama muoga.
Nilishiriki maandamano yale ya amani ambayo yaligeuka vita kati ya wenye silaha na wasiokuwa nazo.
Kwa kifupi huko mashariki ya mbali tulipigana vita ya uonevu.
Shangazi yangu mpole kabisa alikamatwa akiwa katika mgahawa wake na mtoto wake mdogo mgongoni alipigwa na kupoteza maisha mbele ya mtoto wake. Kisa ni cha kuchekesha…..
Alikuwa anamwaga maji barabarani, bahati mbaya iliyoje yale maji yaliyokuwa na masalia kidogo ya ukoko wa ubwabwa yakalifikia gari la polisi lililokuwa likikatiza.
Wakasimamisha gari ghafla na kumvamia wakimlazimisha alioshe gari lile kwa sababu ana dharau.
Shangazi akalifuta gari pale palipoguswa na ukoko, wakamlazimisha aoshe gari lote.
Shangazi akahoji kwanini wanamfanyia vile angali amesema ni bahati mbaya.
Na hata kabla hawajamjibu mtoto wake akaanza kulia, shangazi akamjali mwanaye na hiyo kwao wakaitafsiri kama dharau kwao.
Shangazi aliuwawa!
Naomba muamini kuwa sababu yenu ya kesho ni dhaifu sana.
___________
Ilikuwa ni simulizi ya dakika ishirini na tano, simulizi iliyojenga ukimya wa hali ya juu. Na hata Daniel alipokinyanyua kichwa chake alikutana na uso wa Diana ukiwa umelowana kwa machozi, Maria alikuwa ameuficha uso wake, Danstan alikuwa anajikaza kiume kwa kung’atang’ata meno yake.
“Serikali ilitoa tamko gani kwa ukatili huo” Danstani aliuliza huku akionyesha jazba za waziwazi.
“What’s the https://jamii.app/JFUserGuide!! Ingetoa tamko gani Danstani, labda ingetangaza kuwa IMESHINDA VITA kwa kishindo..” Diana alizungumza huku akishindwa kudhibiti hamaniko lake.
“Daniel mwanangu. Huku kwetu hakuna kitu kama hicho. Tuna uhuru asilimia 100 wa kufanya maandamano kwa lolote ambalo tunaona kwamba halipo sawa. Ni wajibu wetu kuikumbusha serikali kuwa wananchi ni moja ya nguzo kuu katika serikali na tunapaswa kuiwajibisha serikali yetu kila inapokwenda njia isiyokuwa sahihi na bunge likiwa kimya.” Diana alimgeukia Daniel na kutoa ufafanuzi.
Akatoa ufafanuzi zaidi kwa kutoa mifano yakinifu ya matukio kadha wa kadha yaliyowahi kutokea nchini humo.
“Daniel na bado kila siku unasisitiza kuwa unahitaji kurudi Mashariki ya mbali.” Maria alimuuliza kwa unyonge sana.
“Hakika natamani sana kurudi Mashariki ya mbali. Ni huko nilipozaliwa na nitarejea. Si kwa sababu za kuibadilisha nchi bali kula kwa pamoja raha na karaha za ardhi ile.”
“Raha? Kuna raha gani katika nchi inayoua raia wake sasa…” Diana aling’aka
“Juma lililopita nakumbuka niliwasikia mkizungumzia juu ya waziri wa nishati aliyejiuzuru baada ya umeme kukatika bungeni kwa muda wa dakika tano.
Kule kwetu kuna raha ya aina yake, na raha nyingi tunazozipata husababishwa na karaha tunazopitia. Kule kwetu tukisikia waziri kama huyo aliyejiuzuru eti kisa dakika tano kwetu ni kichekesho kikubwa sana, na kwanza ni uzembe mno wa kimaamuzi. Umeme unakatwa kwa siku tatu mfululizo na waziri anapita tunapungia mkono kwa shangwe… sio raha hizo?
Katika hizo siku tatu umeme unapokatika tunatoa kila aina mpya ya matusi kwa taasisi husika, lakini hayo matusi tunaambizana sisi kwa sisi sio kwamba tunawatukana wao. Bado tu huioni raha?
Baada ya hizo siku tatu za umeme kukatika pindi utakaporejea tunaungana kwa pamoja nchi nzima, akina baba kina mama na watoto tunasema kwa pamoja ‘HUOO’. Hujapata tu sababu ya kufurahi?
Na kisha kila mmoja anaendelea na maisha yake, matusi yanaishia hewani na hatutukani tena. Ukijifanya unaendelea kutukana angali umeme umerejea watu wanabaki kukushangaa.
Lazima nitarejea Mashariki ya mbali.” Daniel aliweka kituo katika simulizi yake.
Nyuso za tabasamu zikatawala nyumba ile, Daniel alikuwa amewapa sababu mbili kwa pamoja. Kwanza aliwatupa katika msiba na vilio kisha akazisafisha nyuso zao na tabasamu japo lilikuwa tabasamu la karaha.
Wakaagana kwa mara nyingine wakikiacha kile chakula mezani na kila mmoja kwenda katika chumba chake kuuchapa usingizi.
Akiwa chumbani kaka mkubwa katika familia ile, Danstan alianza kuingiwa na ushawishi wa kuitembelea Mashariki ya mbali.
Hakujua nini maana ya tamanio lake hilo.
NAAAM! RIWAYA hii ya Mashariki ya bali itakuwa ikikujia muda na wakati kama huu kila siku mpaka itakapotimu tamati yake…….
Maoni yako ni muhimu sana!!