Riwaya: Kikosi cha Kisasi

iddy eba

JF-Expert Member
Aug 28, 2015
575
1,169
KIDOKEZO
Ni nani hasa anayewaua viongozi wa wapigania uhuru? Kwa nini viongozi hawa wameuawa wengi zaidi Kinshasa kuliko mahali pengine popote katika Afrika? Je, hatua gani zichukuliwe ili kupambana na kukomesha uhalifu huu usiokuwa na kifani?.
Naam. Umoja wa Nchi Huru za Afrika umepata jibu la masuala yote hayo na mengine. Ni Willy Gamba tena. Nyota ya Afrika na mpelelezi maarufu asiyekubali kushindwa - katika mapambano ya kutisha na kumwaga damu.
Safari hii Willy hakupambana na vikundi vya wanafunzi wa ujasusi bali ni miamba kamambe iliyojidhatiti kutenda uovu bila kujulikana. Ni mapambano ya mafahali, maana Willy naye si mchezo, na vurumai iliyotokea iliukumba mji wa Kishasa katika wimbi la misukosuko ambayo kamwe haitasahaulika.
Usalama wa viongozi wa wapigania uhuru Kusini mwa Afrika ulikuwa umetishiwa, kwani kulikuwa kumetokea mauaji ya viongozi hawa katika nchi mbalimbali za Afrika. Umoja wa Nchi Huru za Kiafrika (OAU) haukuweza kuvumilia hali hii, hivyo ulikata kauli kuwasaka wapinga mapinduzi hawa na kuwafagilia mbali ili kukomesha vitendo hivi vya kijahili.
Willy Gamba mpelelezi maarufu wa Afrika alijikuta amechaguliwa na OAU kuongoza kikundi cha wapelelezi wa Kiafrika cha kuwasaka na kuwatokomeza majahili hawa.
Kinsasa mji mkuu wa Zaire na mji unaosifika kwa starehe zake katika Afrika ulijikuta ni uwanja wa mapambano kati ya vijana wapiganaji shupavu wa Kiafrika wakiongozwa na Willy Gamba na wapinga mapinduzi wa Afrika wakiongozwa na Kaburu Pierre Simonard. Ndipo patashika ambalo halijawahi kutokea katika Afrika liliwaka moto katika mji huu ambalo halijatokea lisahaulike katika historia ya mapambano dhidi ya wapinga mapinduzi wa Afrika


ITAANZA PUNDE
 
SURA YA KWANZA
LUSAKA
"Tafadhali sikilizeni, huyu ni rubani Mwanakatwe ninafurahi kuwafahamisheni kuwa tunakaribia uwanja wa ndege wa Lusaka ambapo ndipo patakuwa mwisho wa safari yetu, Ni matumaini yangu pamoja na wafanyakazi wenzangu kuwa mmefurahia safari yetu mliyosafiri na Shirika la ndege la Zambia, na tunawakaribisheni tena kusafiri nasi mpatapo safari. Sasa fungeni mikanda yenu tayari kwa kutua, asanteni,"
Abiria wote ndani ya ndege hii walifunga mikanda yao tayari kwa kutua. Wale waliokuwa karibu na madirisha waliangalia chini kuiona Lusaka ilivyo kwa juu. Kweli ilitoa picha ya kupendeza sana. Wakati abiria wengine wakijishughulisha na mambo hayo kulikuwa na abiria wanne ambao mara kwa mara walikuwa wanaziangalia saa zao kana kwamba wanachelewa kitu fulani. Mara tu rubani alipotoa taarifa wawili wao waliangaliana. Ingawa abiria hawa walikuwa hawakupandia sehemu moja lakini wawili wao walikuwa wakifahamiana. Wawili walikuwa wamepandia Khartoum Sudan na wawili Dar es Salaam Tanzania. Wawili kati ya watu hawa wanne walikuwa Mawaziri wa Ulinzi kutokana katika nchi hizi mbili na walikuwa wakifahamiana vizuri sana. Ingawaje walikuwa bado hawajapata fursa ya kuzungumza lakini kila mmoja wao alihisi sababu ya kuwepo kwa mwenzake katika safari hii. Watu waliokuwa wameandamana na Mawaziri hawa ni Wakurugenzi wa Upelelezi wa nchi zao.
Abiria hawa ambao walitegemewa kusafiri katika daraja la kwanza, walikuwa wamesafiri katika daraja la kawaida na hakuna abiria wenziwe wala wafanyakazi wa ndani ya ndege waliowatambua kuwa ni akina nani kwani hata hati zao za kusafiria (passport) walizokuwa wakitumia zilikuwa za kawaida tu.
Ndege ilipokuwa imetua abiria walitelemka na kuelekea ofisi za uhamiaji na ushuru wa forodha. Hawa watu wanne walipita sehemu hizi bila matatizo, ingawaje mara kwa mara waliziangalia saa zao kwa wasiwasi kidogo kana kwamba wanazidi kuchelewa kitu. Waliweza kupita kwa urahisi zaidi kwa sababu hawakuwa na mizigo mingi ila mikoba tu ya kawaida.
Walipotokeza nje ya jengo la Uwanja wa ndege walipokelewa na madereva wa teksi waliokuwa tayari kupata abiria wa kupeleka mjini. Hawa watu wanne waliingia ndani ya teksi iliyokuwa karibu na mmoja kati yao akaamru.
"Mjini haraka sana".
"Mpita kuti amadala?" aliuliza dereva teksi katika lugha ya Kinyanja.
"Hatujui kilugha sisi," alijibu mmoja wa watu hawa.
"Nyinyi ni wageni?".
"Ndiyo".
"Nilikuwa na maana mjini niwapeleke sehemu gani?".
"Kwacha House".
Ajabu ni kwamba muda wote huo hawa watu walikuwa hawajasalimiana wala kusemeshana. Kutokana na ukimya na namna ya watu hawa walikuwa na haraka isiyo kifani, kwa hiyo dereva alivuta kasi ili kusudi aweze kuwaridhisha abiria wake. Sharti kama angejuwa ni watu gani aliowabeba asingekubali kwenda mwendo aliokuwa akienda. Maana hawa Mawaziri wawili wa Ulinzi walikuwa ni wanakamati wa kamati ndogo ya usalama ya Kamati ya Ukombozi ya Umoja wa Nchi Huru za Kiafrika.
Hii kamati ndogo ya usalama ilikuwa na wanakamati kutoka nchi nane na mara hii wanakamati hawa walikuwa wameitwa kwenye mkutano wa dharura na wa siri mjini Lusaka, ambako Mwenyekiti wa kamati hii ndiko alikuwa anatoka. Habari walizokuwa wamepelekewa wanakamati hawa kwa njia ya simu zilikuwa zimewataka wanakamati hawa wafike Lusaka kwenye kikao hicho cha dharura ambacho kingefanyika Jumamosi saa kumi jioni wakiwa pamoja na Wakurugenzi wa upelelezi wa nchi zao kwa sababu ya tatizo la mawasiliano wanakamati hawa ndio walikuwa wa mwisho kufika mjini Lusaka. Wanakamati kutoka nchi nyingine walikuwa tayari wamewasili.
Wakati dereva wa teksi anaegesha gari, kwenye maegesho ya Kwacha House ilikuwa yapata saa kumi unusu mchana ambayo ilikuwa inamaana walikuwa wameisha chelewa muda wa nusu saa. Mmoja alimlipa dereva na wao nusu wakikimbia walielekea mlango wa mbele wa Kwacha House.
Kwa mara ya kwanza toka wakutane ndipo waziri wa ulinzi wa Tanzania aliwasalimu, "Habari zenu, poleni na safari tumechelewa lakini si sana, Sisi salama, natumaini watakuwa wanatungoja, hata hivyo sisi tumejitahidi sana kufika kama walivyopanga," Alijibu Waziri wa Ulinzi wa Sudan huku wakiwa wamefika meza ya mapokezi ya Kwacha House. Kabla hata hawajazungumza na msichana aliyekuwa amekaa kwenye hiyo meza alitokea kijana mmoja bila hata kuwauliza akawaambia "Wazee twendenui huku," Na wao bila kuuliza walimfuata, "Mmekuwa mnangojewa kwa hamu sana mkutano bado haujaanza," Huyu kijana aliwaeleza huku akipanda ngazi za ghorofa ya kwanza. Walimfuatana wakiwa bado na hiyo hali yao ya wasiwasi maana walikuwa hawajui mkutano huu ulioitwa kiajabu ulikuwa wa nini.
"Chumba hiki ndicho cha mkutano," aliwaeleza yule kijana huku akifungua na wao bila kusita wakaingia ndani. Ndani ya chumba hiki cha mkutano mlikuwa na meza kubwa ya mkutano ambayo tayari watu kumi na wawili walikuwa wamekaa huku wakiizunguka meza. Mtu mmoja ambaye alikuwa anafanya idadi ndani ya hiki chumba cha mkutano kuwa kumi na tatu alikuwa amesimama dirishani akiangalia chini barabarani. Kanakwamba alikuwa akihesabu magari yaliyokuwa yakipita hapo chini. Hata walipokuwa wakiingia hawa wanakamati wengine, bado aliendelea kuangalia, huko chini kanakwamba alikuwa hakusikia kishindo cha kuingia kwao.
Hawa wanakamati walioingia walikaa kwenye nafasi zao na kushiriki katika kilichokuwepo ndani ya chumba hiki, huku kila mtu akionekana kuwa mwenye mawazo mengi sana. Baada ya kupita kama dakika tano hivi, huyu mtu aliyekuwa amesimama kwenye dirisha aligeuka na kuangalia chumbani. Huyu alikuwa ndiye Mwenyekiti wa kamati ya Ukombozi ya Umoja wa Nchi Huru za Kiafrika. Alienda mpaka kwenye meza akavuta kiti akakaa, kisha akavunja kimya kilichokuwamo chumbani kwa kusema, "Ndugu Wanakamati, inabidi nitoe shukrani zangu kwenu nyote kwa kuweza kuitikia mwito wa kuhudhuria hiki kakao cha dharura cha kamati ya usalama ambacho kimeitishwa kinamna yake. Nilikuwa na wasiwasi mwingi kuwa huenda wanakamati wengine wangeshindwa kufika kwa muda uliopangwa. Hii inazidi kutudhihirishia kuwa Afrika ni moja na umoja wa Afrika unazidi kukomaa siku hadi siku" Alinyamaza kido kiasi cha kupitisha mate, halafu akaendelea "Vile vile ningependa kuwakaribisha Wakurugenzi wa Upelelezi ambao kwa kawaida si wanakamati wa kamati hii, kuwa mtakuwa na haki ya kupiga kura kama wanakamati wa kawaida. Nafikiri tumeelewana mpaka hapo."
"Tumeelewa," walijibu wanakamati kwa pamoja. Kila mtu alionyesha sura ya uchu wa kutaka kujua hasa ajenda ya mkutano huu. Huku akiwa amekunja uso aliendelea. "Ndugu wanakamati, nasikitika kuwaeleza kuwa hiki kikao chetu si cha kawaida na ndiyo sababu kimeitishwa kwa siri kwa maana haikutakiwa ijulikane kuwa kikao hiki kimeitishwa kutokana na jambo lenyewe ambalo limefanya kikao hiki kiwepo kutokana na jamno lenyewe ambalo limefanya kikao hiki kiwepo. Ni jinsi hii mhitasari wa maneno yatakayoamjadiliwa na kuamriwa katika mkutano huu hautachukuliwa.
Hii ina maana itabidi sisi wote tusikilize kwa makini na yote tutakayoyasikia tuyaweke moyoni mwetu, yawe siri yetu," Chumba cha mkutano kilikuwa kimya kabisa isipokuwa sauti ya Mwenyekiti peke yake. Alipokuwa amefikia hapa sura ya kila mtu ilionyesha mshangao wa jinsi mkutano ulivyokuwa ukiendeshwa huku wengine mioyo yao ikipiga haraka haraka kwa shauku ya kutaka kujua jambo lenyewe.
"Ndugu wanakamati." Mwenyekiti aliendelea kwa sauti ya huzuni. "Naamini mmesikia tukio lililotokea mjini Kinshasa Zaire juzi usiku na kutangazwa jana," aliwaangalia huku baadhi yao wakitingisha vichwa kuonyesha kuwa walikuwa na habari kisha akaendelea, "Tumepata habari kuwa aliyekuwa rais wa shirikisho la vyama vya wapigania uhuru Kusini mwa Afrika ndugu Edward Mongo ameuawa huko mjini Kinshasa Zaire baada ya gari alilokuwa akitembelea kutegwa bomu ndani ya mtambo wake na kuripuka. Yeye alikuwa ametokea Libreville Gabon ambako alikuwa akihudhuria mkutano wa umoja wa Matafa kuhusu kuzuia Ufaransa kuiuzia Afrika Kusini dhana za kivita na kuisaidia kutengeneza silaha za Nyuklia. Na alikuwa amepita mjini Kinshasa kwa mazungumzo na serikali ya Zaire kuhusu hali iliyoko Kusini mwa Afrika, Na kabla ya kufanya mazungumzo hayo, ndugu Mongo alikufa juzi usiku kwa mripuko wa bomu lililotegwa ndani ya injini ya gari aliyokuwa amepewa kutembelea. Jambo hili limesikitisha wakuu wa nchi huru za Afrika, kwa maana kifo cha ndugu Mongo kina maana ya pigo kubwa kwa ushirikiano wa vyama vya wapigania uhuru Kusini mwa Afrika! Hii inaonyesha waziwazi kuwa ni njama za makaburu na vibaraka wao kutaka kuvunja harakati za ukombozi zinazofanywa na wapigania uhuru Kusini mwa Afrika. Ni dhahiri kuwa kumuua ndugu Mongo wamejipalia mkaa, lakini kitendo kama hiki hatuwezi kukiruhusu kiendelee.
Kwa jinsi hii ndugu wanakamati, kikao hiki cha dharura kimeitishwa kusudi kitafute dawa ya kukomesha vitendo kama hivi na vile vile kutafuta jinsi gani tunaweza kuwapa fundisho hawa wanaohusika na kitendo kama hiki kuwa sasa Afrika iko macho na haitaki kuchezewa. Hili ndilo jukumu tumepewa na wakuu wa nchi huru za Afrika na hatuna budi kulitekeleza," alimaliza huku akiwatazama wajumbe kikamilifu.
"Ndugu Mwenyekiti, bado haijaeleweka sawasawa hasa kuhusu inatakiwa tufanye nini?. Kwa kweli jambo hili ni la kusikitisha sana na hata wakati natoka nyumbani niliacha baraza la mawaziri limekutana kuzungumzia tukio hili. Kwa hivi jambo tutakalozunguzia au kuamua hapa lina maana kuwa ndiyo utakuwa msimamo wa nchi huru za Afrika. Kwa jinsi hii, ndugu Mwenyekiti, tunaomba utueleze suala hili kinaganaga kusudi tuweze kulielewa sawasawa na pindi tutakapotoa maamzi yalingane na matakwa ya nchi huru za Afrika", alitoa rai mjumbe kutoka Kenya.
Wajumbe wengine walitingisha vichwa, kuonyesha kuwa na wao walihitaji ufafanuzi zaidi. Akijibu hoja hiyo, Mwenyekiti alisema, "Ndugu wanakamati, nadhani itabidi nifafanue jambo hili kwa kutoa historia fupi juu ya matukio ya namna hii na nini kimefanyika katika jitihada za kuyazuia.
"Miaka mitatu iliyopita kumetokea matukio ya mauaji kwa viongozi wa wapigania uhuru na tukio hili la juzi linakuwa la sita kwa muda wa miaka mitatu. Tukio la kwanza ambalo lilitokea mwaka juzi lilitokea mjini Dar es Salaam ambapo Mkuu wa ofisi wa Wapigania Uhuru iliyoko mjini hapo ndugu Leon Fadaka aliuawa kwa bomu baada ya kupokea kifurushi kilichokuwa kimetumwa kwake kwa njia ya posta na wakati alipokuwa akikifungua kililipuka kwani ndani yake kuliwa na bomu na alikufa pale pale. Uchunguzi ulifanyika ikabainika kuwa kifurushi hili kilikuwa kimetumwa kwake kwa njia ya posta kutoka mjini Kinshasa. Serikali ya Zaire ilijaribu kuchunguza jambo hili lakini bila ya mafanikio. Mwaka huo huo wa juzi baada ya miezi sita tangu kuuawa kwa ndugu Fadaka, kulitokea tukio lingine la namna hiyo hiyo hapa mjini Lusaka, baada ya Mkuu wa ofisi ya wapigania Uhuru ya hapa naye kupata barua kutoka mjini Paris Ufaransa na mara alipokuwa akifungua bahasha, kukatokea mripuko ambao ulimuua papo hapo.
Tukio hili lililaaniwa vikali kote Ulimwenguni lakini hakuna mtu wala kikundi cha watu kilichokamatwa bali lawama ziliwaangukia makaburu na vibaraka wao kuwa ndiyo tu wangeweza kuhusika na vitendo hivi. Matukio mengine matatu yametokea mwaka jana. Tukio la kwanza mwaka jana lilitokea mjini Lagos Nigeria, wakati ndugu Nelson Chikwanda ambaye alikuwa mwakilishi wa wapigania uhuru katika ofisi njema za Umoja wa nchi huru za Afrika iliyoko mjini hapo alipigwa risasi na mtu asiyejulikana. Uchunguzi mkali ulifanyika lakini hakuna lolote lililotambulika.
Miezi mitatu baada ya tukio hili huko Lagos, ofisi ya wapigania uhuru iliyoko mjini Nairobi ililipuliwa na wafanyakazi watatu akiwemo ndugu Nene ofisa wa juu katika ofisi hiyo aliuawa. Tukio la mwisho mwaka jana lilitokea tena mjini Kinshasa wakati Afisa wa juu katika Jeshi la wapigania uhuru Meja Komba Matengo alipokutwa ameawa ndani ya Hoteli Tiptop chumbani mwake. Yeye alikuwa amewasili mjini hapo kuhudhuria kikao cha kamati ya ukombozi ya nchi huru za Afrika kilichokuwa kikizunguzia kuunganishwa majeshi ya wapigania uhuru Kusini mwa Afrika. Na ndugu wanakamati tukio la mwisho kufikia sasa ni hili ambalo limetokea juzi. Naamini nyote mnakumbuka hatua ambazo zimechukuliwa kujaribu kuhakikisha usalama wa ndugu hawa wapigania uhuru. Mpaka sasa tumefaulu kutegua mabomu kadhaa yaliyokuwa yametumwa kwa wapigania uhuru kadhaa kwa njia ya barua ama vifurushi jambo hili tumeweza kufuzu kwa sababu barua zote au vifurushi vinavyotumwa kwa watu hawa vinafunguliwa kwanza na wataalam kutoka idara ya usalama ya kila nchi ambapo ofisi hizi zilizopo. Lakini jinsi ya kuzuia matukio mengine kama lilile lililotokea Lagos, Kinshasa, TipTop Hoteli na hili la juzi inakuwa vigumu sana kuyazuia.
Hata hivyo, hatuna budi kujihami, kwani hatuwezi kukaa tu huku ndugu zetu wakiuawa huku na kule ili kusudi harakati za ukombozi wa Kusini mwa Afrika ziweze kusimama. Kwa hivi, ndugu wanakamati, tuko hapa ili tujadiliane ni njia gani tuzitumie katika kujihami. nafikiri nimeeleweka vya kutosha," alimalizia Mwenyekiti.
Mkutano ulishikwa na ukimya wa kama dakika tano hivi huku kila mjumbe akizingatia mambo yote yaliyokuwa yameelezwa. Mjumbe wa Zambia ambaye kwa kawaida huwa ndiye Mwenyekiti wa kamati hii ndiye alikuwa wa kwanza kuvunja kimya hiki kwa kusema, "Ndugu Mwenyekiti na ndugu wanakamati wenzangu, kusema ukweli jukumu hili tulilopewa ni jukumu gumu sana. Ni gumu kwa sababu inabidi kikao hiki kiamue nini kitu gani kitendeke dhidi ya mauaji haya ambayo yanatokea kwa ndugu zetu wapigania uhuru. Ingawaje suala hili ni gumu lakini hatuna budi kulitatua maana tumeaminiwa na viongozi wa nchi zetu na ni matumaini yangu lolote tutakaloliamua hapa ndiyo utakuwa uamzi wa Afrika. Ndugu wanakamati, matukio haya kama yalivyoelezwa na ndugu Mwenyekiti, Utaona ya kwanza yanatokea katika nchi zetu zilizo huru. Ingekuwa habari nyingine kama matukio haya yangetokea kwenye uwanja wa mapambano kwani jambo kama hili lingeweza kueleweka. Lakini utaona kuwa tunapigwa vita nyumbani kwetu. Hii ina maana tumeshindwa kuwalinda hawa ndugu zetu? Suala sasa ni tufanye nini? Kwa upande wangu naonelea ya kwamba inabidi tutafute kiini cha matukio haya, kwani tukishapata kiini chake itakuwa rahisi kupata ufumbuzi. Mpaka sasa hivi tumefahamishwa kuwa matukio mawili yametokea mjini Kinshasa, moja Dar es Salaam, moja hapa Lusaka, moja Nairobi na moja Lagos. Tukio la mjini Dar es Salaam linasemekana limetokana na kifurushi kilichokuwa kimetumwa kwa njia ya posta kutoka mjini Kinshasa, Zaire. Uchunguzi huu unatuonyesha wazi wazi kuwa tukio la Dar es Salaam kilikuwa mjini Kinshasa, kwa hiyo hii inatupa idadi ya matukio matatu kati ya sita yakiwa yametokea mjini Kinshasa Zaire. Ndugu wanakamati, kutokana na hali hii, inaonekana waziwazi kuwa mjini Kinshasa kuna mambo na kama uchunguzi halisi ukifanywa mjini hapo huenda tukapata kiini hasa cha mauaji haya. Kwa hivi ni rai yangu kuwa utumwe ujumbe kutoka kwenye kamati hii ukaonane na wakuu wa serikali ya Zaire, uzungumzie juu ya jambo hili, ukiwa unaomba serikali ya Zaire ifanye upelelezi kabambe juu ya matukio hayo. Ni imani yangu kuwa kwa kufanya hivi tutapata ufumbuzi wa jambo hili. Sijui wanakamati wenzangu mnasemaje," alimaliza.
Mjumbe wa Sudan aliinua kichwa na kwamwangalia Mwenyekiti akionyesha sura ya kutaka kusema kitu. Mwenyekiti ambaye naye alikuwa akimwangalia alimtingishia kichwa kumuashiria aendelee. Hivyo alianza kwa kusema, "Ndugu Mwenyekiti na ndugu wajumbe, kusema kweli mzigo tuliopewa ni mzigo mzito lakini kama walivyokwisha sema walionitangulia hatuna budi kuubeba. Ningependa kuunga mkono maelezo ya ndugu mjumbe aliyemaliza kusema kabla yangu, maelezo ambayo nisingependa kuyarudia kwani naamini yameeleweka vizuri sana. Kweli mtu yeyote anaweza kuona mjini Kinshasa kuna matatizo na ingefaa zaidi uchunguzi ufanyike mjini hapo juu ya matukio haya. Ingawa makubaliano ya suala hili inabidi uchunguxi ufanyike lakini namna alivyotoa maoni ndugu mjumbe mimi nina maoni tofauti na yeye jinsi ambavyo uchunguzi huu ungefaa ufanyike. Ndugu wajumbe ni matumaini yangu kuwa mtakubaliana na mimi kila tukio la namna hii linalotokea katika nchi yoyote lazima upelelezi wa hali ya juu ufanyike kusudi yeyote anayehusika aweze kukamatwa na kutiwa hatiani. Hivi ndivyo nchi zote zilizopatwa na baraa la aina hii zimejitahidi kufanya, ingawaje bila mafanikio maalumu. Mwisho wa kila upelelezi umekuwa ni lawama tu kwa Afrika Kusini na vibaraka wake. Kwa jinsi hii ndugu wajumbe kutuma ujumbe ukazungumze na serikali ya Zaire ili kuongeza jitihada katika upelelezi wake kuhusu matukio haya, itakuwa sawa na kuiomba kufanya kitu ambacho imekwisha kifanya, kwani mimi naamini kwa dhati kuwa Zaire imekuwa ikifanya kila iwezavyo kusudi iweze kuwakamata hawa wauaji, ingawaje bila mafanikio. Kwa hivi naonelea kuwa Zaire inahitaji msaada katika upelelezi wake msaada ambao unabidi utoke nje ili kuimarisha nguvu za wapelelezi wa nchi hiyo.
Kwa hiyo nato oni kuwa kiundwe kikosi cha wapepezi kitakachotoka katika Nchi Huru za Kiafrika ambacho kitaenda Zaire kikasaidiane na wapelelezi wa Zaire ni bahati nzuri kuona kuwa katika mkutano huu, wakurugenzi wa upelelezi wa nchi huru nane za Kiafrika wako hapa na wanaweza kutusaidia kitaalam jinsi ya kuunda kikosi hiki," alimaliza huku akipigiwa makofi ya kumpongeza kwa maoni yake, vile vile ikionyesha wajumbe wengi waliafiki maoni yake. Kwa mara ya kwanza minong'ono ilisikika katika chumba hiki, Mwenyekiti aliikatisha minong'ono hii kwa kusema.
"Ndugu wajumbe mnanipa moyo kwa kuona kuwa jambo ambalo limekuwa nikilifikiria siku nyingi na kunisumbua rohoni siku nyingi leo limeweza kusemwa na nyinyi kabla hata mimi mwenyewe sijalisema. Nilikuwa nachelea kulisema awali nikiwa na mawazo kuwa huenda lingeweza kupingwa, lakini ni furaha iliyoje kuona jambo hili limeshangiliwa na wajumbe wote, ni kweli kabisa ya kuwa wakurugenzi wa upelelezi mmeitwa katika mkutano huu ili muweze kutusaidia kitaalam ni jinsi gani tunaweza kuunda "Kikosi cha Kisasi" kikosi kidogo na chenye kufaa. Kabla sijasema mengi naonelea niwaachie uwanja wataalam waweze kutushauri kabla hatujafikia uamzi kamili,"
Mkurugenzi wa Upelelezi wa Nigeria ndiye alikuwa wa kwanza kusema, "Asante sana ndugu Mwenyekiti na ndugu wajumbe. Kikao hiki mimi ni mara yangu ya kwanza kuhudhuria na, nakihudhuria wakati hasa ambapo nahitajika kukihudhuria kikamilifu katika matatizo yanayoikabili Afrika kwa wakati huu. Ni wazo zuri sana kuunda "Kikosi cha Kisasi" ambacho kitasaidia katika kutafuta na kukipiga vita kikosi kingine cha maadui wa Afrika. Mawazo yaliyokwisha tolewa kuwa baada ya kikosi hiki kuundwa kiende Kinshasa kikasaidiane na idara ya usalama ni jambo la busara. Lakini kwa upande wangu kutokana na ujuzi wangu katika mambo ya upelelezi, mimi naonelea kuwa baada ya kuunda kikosi hiki si vizuri kikasaidiane na idara ya usalama ya Zaire bali kiende huko kikijitegemea na wala kisijulikane kabisa na mtu yeyote nchini Zaire kama kuna kikosi kama hiki. Nikisema hivi sina maana kuwa siiamini sserikali ya Zaire, bali ni kufuatana na hali yenyewe ya kazi ya kipelelezi ilivyo. Jinsi watu wachache Afrika watakavyoweza kufahamu kuwepo kwa kikosi hicho ndivyo kitakavyokuwa na nafasi nzuri ya kuweza kufanikiwa. Kwa maana inabidi ieleweke wazi kuwa adui tunayepigana nae ana nguvu na ujuzi wa hali ya juu na ndiyo sababu watu maarufu sita wameweza kuuawa bila kushika au kuawa mtu hata mmoja kwa upande wa wauaji. Kutokana na tukio lililotokea mjini Lagos nimejifunza mengi kwani upelelezi wa tukio lote ulifanyika chini yangu. Kwa hivyo nathubutu kusema kuwa hili ni kundi la wauaji wa hali ya juu sana na wana mipango ya hali ya juu sana. Kiupelelezi hata mimi nahisi mjini Kinshasa kuna mizizi ya matukio haya. Kwa kifupi basi ni maoni yangu kuwa kwanza lazima tuunde kikosi cha wapelelezi wa hali ya juu sana katika Afrika, pili kikosi hiki kiwe na watu wachache sana, tatu kitakapokwenda Zaire kiingie kisirisiri na kifanye kazi zake kwa siri kama kikundi cha maadui kinavyofanya kazi kisiri, na serikali ya Zaire isijulishwe kabisa juu ya kikosi hiki kwa sasa huenda mpaka hapo baadaye itakapokuwa lazima (Zaire haikuwa mojawapo katika nchi nane za kamati ya usalama) na mwisho lazima kikosi hiki kiundwe haraka iwezekanavyo na kiwe kimefika Zaire wakati bado kuna moto wa kifo cha ndugu Mongo,' alimalizia.
Wakurugenzi wengine wote wa usalama kutoka katika nchini nyingine walikubaliana na maoni hayo yote ya mwenzao. Lililokuwa limebaki sasa juu ya kikao kuzungumzia uundwaji wa kikosi chenyewe. "Ndugu wanakamati, inaonekana tumepiga hatua za haraka sana katika kutafuta ufumbuzi wa tatizo hili," alisema Mwenyekiti. "Lilopo sasa ni kuzingatia maoni yaliyotolewa na kuyashughulikia kikamilifu kufuatana na vile mkutano utakavyokubaliana na maoni hayo. Kwa sababu tumekubaliana kuwa lazima kikosi kiwe tayari wakati bado kuna moto wa kifo cha ndugu Mongo huko Zaire, hii ina maana hatuna nafasi ya kuchagua watu ili tukawafundishe waje waunde kikosi hiki, bali inatubidi tupate watu ambao tayari yamekwisha pata ujuzi wa juu katika upelelezi, kutoka katika nchi mojawapo za Kiafrika na kuunda kikosi hiki kutokana nao. Suala sasa ni kwamba je, tunao watu kama hawa Afrika. Ikiwa suala hili litajibiwa sina shaka tatizo letu litakuwa limekwisha," alimaliza Mwenyekiti huku akiwaangalia wanakamati mmoja baada ya mwingine.
Mkutano kwa mara nyingine uliingiwa na minong'ono kati ya kila Waziri na Mkurugenzi wake wa Upelelezi mingong'ono hii iliendelea karibu nusu saa, ubishi ukizuka hapa na pale kati ya Waziri na Mkurugenzi wake. Kisha mjumbe wa Tanzania aliinua kichwa na kutoa kohozi la kujitayarisha kusema. Wengine waliposikia ishara hii walinyamaza na kumwangalia wakingojea kusikia atasema nini, naye alianza, "Ndugu wajumbe, sina budi kutoa shukrani zangu kwenu nyinyi kwa kuwa tayari kunisikiliza. Vilevile ningependa kutoa furaha yangu jinsi mkutano huu unavyoendeshwa na jinsi ambavyo wajumbe waliowahi kusema, wameweza kusema kwa moyo wa Afrika moja na wala si kwa nchi binafsi kwa sababu hii hata mimi nasikia mori na ninathubutu kuwaeleza kuwa serikali ya Tanzania inaye mtu ambaye akipata msaada wa mtu mmoja au wawili pamoja na baraka za Afrika Huru anaweza kuitekeleza kazi hii kwa kiasi kikubwa sana. Mtu huyu amewahi kufanya shughuli za namna hii kubwa kubwa, na kama ndugu wajumbe mnakumbuka juu ya karatasi za wapigania uhuru zilizoibiwa jijini Dar es Salaam na kuweza kukamatwa mjini Nairobi mtu aliyewezesha jambo hili lifanikiwe ndiye ninayemwelezea. Ujuzi wake ni wa hali ya juu sana na ni imani yangu kuwa anaeleweka vizuri kwa wakurugenzi wa upelelezi, hasa kwa jina.
"Ndiyo tunamfahamu sana, hata sisi tulikuwa tunamzungumzia huyo huyo," alidakia Mkurugenzi wa Upelelezi wa Kenya.
"Sina shaka ni Willy Gamba," alitamka Mkurugenzi wa Upelelezi wa Ghana.
"Ndiye hasa nilikuwa namzungumzia," alijibu mjumbe wa Tanzania.
Mkutano ulinza kumzungumzia huyu mtu aitwaye Willy Gamba, sifa zake zote zilielezwa mbele ya mkutano na Mkurugenzi wa Upelelezi wa Tanzania na mkutano kwa ujumla ulikubaliana kuwa mtu huyu angefaa apewe jukumu hili.
"Nafikiri ndugu wanakamati tumefikia uamzi juu ya suala hili kwa sasa mimi naonelea jambo hili tunawaachia Wakurugenzi wa Upelelezi wakae na walishughulikie. Huyu mtu Willy Gamba tumeamua ndiye ataongoza "Kikosi Cha Kisasi" na mambo mengine yote yatatengenezwa na hawa wakurugenzi ambao ni wataalam, itabidi tuonane tena kesho saa kumi na mbili jioni hapa hapa. Hii itawapa nafasi nyinyi wataalam kutayarisha mambo yote na kuhakikisha kuwa tuonanapo kesho Willy Gamba nae awe amefika hapa. Kwa sasa hivi tufunge mkutano, nyinyi mtapanga muda wenu wa kukutana, nafasi zenu za kulala zimetayarishwa, kila mtu aondokapo hapa apite mapokezi kuna dereva na ofisa usalama kwa kila mwanakamati. Ni matumaini yangu kuwa tuonanapo kesho jioni mambo yatakuwa yameshughulikiwa kikamilifu. Itakuwa tu kupokea taarifa kamili na mambo ya kuanza. Asante sana."
Mwenyekiti alifunga mkutano na kuangalia saa yake ambayo ilionyesha ni saa mbili unusu za usiku wa siku hii ya Jumamosi.
ITAENDELEA 0784296253
 
Tunasubiri muendelezo kwa hamu baadhi yetu tulivisoma vitabu hivi waqt uleeeee lakini ndio hivyo tena pana baadhi ya matukio tumeyasahau sasa kujikumbusha sio ubaya.
 
Dah umenikumbusha mbali aisee na hii hadithi.mpaka kitabu nilikuwa nacho ila sijui baadae nilikitupia wapi.nilikuwa sili,siongei na mtu nakesha kusoma hii hadithi.mtunzi kila akitoa kingine lazima nikipate.hadithi zake ndio zilinifanya nipende hadithi za upelelezi.in real life nilitamani angalau kufanya kazi usalama wa taifa. Matokeo yake haikuwa hivyo.nimeishia kubeba boksi
 
SURA YA PILI
DAR ES SALAAM
Mjini Dar es salaam, kama ilivyo katika miji mingine yoyote Ulimwenguni, kulikuwa kumejaa pilikapilika siku hii ya jumamosi usiku. Saa tano hizi za usiku pilikapilika zilikuwa bado nyingi sana. Watu wengi waliokuwa wameanza starehe za Jumamosi mapema mchana walikuwa wanarejea nyumbani kupumzika, wakati wengine waliokuwa wameanza starehe jioni, walikuwa wamo katikati ya sherehe na wakati ule ule walikuwa na kundi jingine ambalo ndipo lilikuwa linaanza pilikapilika za sherehe saa tano hizi.
Katika msululu wa magari yaliyokuwa kwenye barabara ya Morogoro yakitokea mjini kuelekea sehemu ya Ubungo, mlikuwa na gari moja aina ya 'Colt Gallat Coupe' nambari TZ 300130 ambayo ndani yake mlikuwa na kijana mmoja nadhifu sana na msichana mmoja mrembo sana, ambao walikuwa katikati ya ubishi.
"Mimi nakwambia twende Mlimani Park," alisema yule kijana.
"Nieleze kwa nini tusiende Safari Resort?" Aliuliza yule msichana.
"Bendi mpya ipo pale ya Zaire."
Yaani wewe unafuata upya wa bendi au bendi yenyewe ilivyo."
"Basi Lolita mpenzi, tutakwenda Safari Resort," alijibu yule kijana huku akiongeza mwendo wa gari.
"Lakini usije ukawa umeudhika, ee Willy mpenzi."
"La hasha, ningekuwa sikuridhika ningekuambia, bila kusita." Kusema kweli magari mengi yalikuwa yakielekea kwenye klabu moja maarufu sana iitwayo Resort iliyoko sehemu ya Kimara. Kwa hivi baada ya watu hawa kukubaliana kwenda kustarehe usiku huu huko Safari Resort walielekea moja kwa moja mpaka kwenye klabu hiyo. Walipoingia ndani ya klabu hii walikuta watu tayari walikuwa wamejaa. Muziki ulikuwa ndipo umepamba moto.
"Loo Willy rekodi hiyo mimi naipenda," alisema Lolita mara tu walipoingia ndani,
"Twende tukacheze alijibu Willy. Bila hata kutafuta mahala pa kukaa kwanza waliingia kwenye uwanja wa kucheza na kuanza kulisakata rumba.
Baada ya rekodi hii kwisha, walitoka na kuanza kutafuta mahala pa kukaa.
"Willy karibu huku," Meneja wa klabu alimkaribisha. Meneja wa klabu hii alikuwa amemwona Willy wakati akiingia, na kwa sababu alikuwa akimheshimu sana, alimtafutia mahala pa kukaa ili asipate taabu kutafuta.
"Asante sana Rajabu, hujambo lakini?"
"Mimi sijambo, je wewe?"
"Alhamdulillahi Mungu anasaidia".
"Oh, samahani bibie tabia yangu inataka kuwa mbaya kwa kutokusabahi kwanza, hujambo?"
Rajabu alimsalimia Lolita huku akiwakalisha kwenye meza aliyokuwa amewatayarishia.
"Sijambo mimi" alijibu Lolita huku akiketi.
"Ngoja niwajulishe, huyu ni Lolita rafiki yangu," alimjulisha Lolita kwa Rajabu, "Na huyu ni rafiki yangu vile vile ndiye Meneja wa hapa," alimjulisha Rajabu kwa Lolita.
"Nafurahi kukuona," Rajabu alimwambia Lolita.
"Na mimi pia nafurahi kukuona" alijibu Lolita.
Kisha Rajabu aliwaagizia vinywaji, "Sijui bibie utapendelea kunywa nini?".
"Nafikiri itanifaa safari".
"Na wewe Willy?".
"Na mimi hiyo hiyo itanifaa kwa kuanzia."
Vinywaji viliagizwa na Rajab akaondoka.
"Willy," Lolita aliita kwa mshangao, Willy akajua kwanini?.
"Mara nyingi huwa nafika hapa kiasi cha kwamba huyu meneja amenizoea."
"Ndiyo sababu ulikuwa hutaki kuja huku au sivyo?"
"Nilitaka libadilisha mazingira kidogo."
"Mahala pazuri sana miye huwa napasikia tu sijawahi kufika, rekodi za bendi hii huwa nazisikia tu ndani ya redio, ama kweli anapiga sana."
"Ni mahala pazuri sana."
Vibywaji vilifika na kuanza kunywa huku wakiwa mara kwa mara wakiondoka kwenda kulisakata rumba.
Kiasi cha saa saba hivi usiku, wakati Willy na Lolita wakilisakata rumba uwanjani Willy alimuona Rajabu akielekea mezani kwao ambayo ilikuwa tupu. Alitazama kule na huku akionyesha dalili kuwa alikuwa akiwafuata.
"Nadhani Rajabu anatufuata," Willy alimwambia Lolita.
"Umemwona wapi?" aliuliza Lolita huku akiendelea kucheza.
"Yuko pale mezani kwetu."
"Ina maana wewe unacheza na huku ukiangalia mezani petu!"
"Inabidi nifanye hivyo Lolly mpenzi, maana hakuna mtu anayelinda meza yetu, anaweza kutokea mhuni au mlevi akanywa pombe yetu au akamwaga. Vile vile anaweza akatokea mtu anayechukia wewe au mimi akatuwekea sumu ndani ya pombe yetu,"
"Usiseme hivyo Willy, mimi sina mtu anayenichukia kiasi hicho. Lo ondoa wazo kama hilo."
"Huwezi kujua, dunia ya siku hizi imejaa fitina tupu. Hebu twende tukamwone huenda anatuhitaji naona kama ana wasiwasi hivi!"
Kwa shingo upande Lolita alikubali kuondoka maana muziki waliokuwa wakiucheza ulikuwa muziki taratibu uliokuwa ukiliwaza mioyo ya wachezaji na wasikilizaji wote hawa waliokuwa katika mapenzi.
"Kuna simu yako ofisini kwangu", Rajabu alimwambia Willy kwa shauku walipomkaribia.
"Asante" Willy alijibu kisha akamgeukia Lolita ambaye alikuwa akimwangalia kwa mshangao akamwambia, "Mpenzi, ningoje nikasikilize simu mara moja."
"Nani anakupigia simu saa saba hizi za usiku?" Aliuliza Lolita.
"Nitamjuaje kabla sijaisikia simu yenyewe?" Alijibu Willy.
"Amejuaje kama uko hapa? Je kama tungeebda Mlimani Park?".
"Nitajuaje kuwa amejua niko hapa kabla sijasema naye Loly mpenzi?"
"Haya baba nenda", alijibu Lolita kwa sauti ya kutoridhika.
"Wasichana watu wa ajabu sana, kwa mawazo yake anafikiri simu hii inatoka kwa msichana mwingine", alilalama Willy huku wakielekea ofisini kwa Rajabu.
Msichana akikupenda sana basi ujuwe amejawa na wivu juu yako, lakini hata hivyo Willy kama msichana hakuonei wivu ujuwe hakupendi. Hii inaonyesha waziwazi kuwa msichana huyu anakupenda sana", alisema Rajabu huku wakiingia ndani ya ofisi.
Bila kumjibu Rajabu, Willy aliiendea simu na kuinua.
"Helo, nani mwenzangu?" aliuliza.
"Unastarehe tu mwenzetu, leo una chuma kipya nini?" alijibiwa.
"Aah Maselina uko wapi?"
"Nipo nyumbani kwangu, nimejaribu Mlimani Park sikupata ikabidi nijaribu hapo, vipi muziki hapo."
"Muziki safi tu, natumai hukunipigia saa hizi kuniuliza muziki hapa ukoje." alijibu Willy kwa sauti nzito.
"Usiwe mkali baba, kwa taarifa yako kama ulikuwa na mipango ya starehe na hicho chuma ulichonacho basi sahau. Nimepata simu muda mfupi uliopita toka kwa Chifu, kwa hiyo njoo hapa kwangu haraka iwezekanavyo nina salamu zako maalumu," alijibu kwa sauti ya utani.
Lakini kwa sababu Willy alikuwa akimwelewa sana Maselina, uso wake ulionyesha kuwa ulikuwa umezingatia vizuri sana ujumbe huu.
"Asante sana, nakuja," halafu akamgeukia Rajabu, Sisi sasa tutaondoka"
"Vipi kuna matatizo nyumbani mbona haraka hivi baada ya kupata hiyo simu?"
"Hapana, hakuna matatizo yoyote ila kumefika wageni nyumbani, nilikuwa nimeacha ujumbe kuwa wakifika wakati wowote nielezwe."
"Aisii, basi karibu tena wiki ijayo, mlete huyu mrembo tena maana hajastarehe vizuri leo."
"Bila shaka nitamleta".
"Oke Willy niagie na mrembo huyo."
"Asante, nitakuagia. Kwa heri."
"Kwa heri asante", waliagana kwa kupeana mikono.
Alipokuwa akirudi kwenye meza yake, mawazo yake tayari yalikuwa kazini yakifikiri salamu zake kutoka kwa Chifu zitakuwa salamu za namna gani.
Alipofika mezani pake alimkuta Lolita anazozana na kijana mmoja aliyekuwa anataka kwenda kucheza naye kwa nguvu.
"Vipi ndugu mbona unakuja kufanya fujo hapa?" alimuuliza huyo kijana.
"Siyo fujo ila tu na mimi nataka kupata fursa ya kucheza na mrembo huyu itakuwaje tukuachie wewe ufaidi vyote peke yako?" Yule kijana alijibu kwa dharau. Willy alimwangalia akagundua kuwa tayari alikuwa ameishalewa vibaya sana.
"Twende zetu Loly, achana naye huyu kisha lewa."
"Afadhali umekuja mapema alitaka kunivuta kwa nguvu", alijibu Lolita huku akisimama.
"Haya kaka nenda kafaidi peke yako. Lakini nakupa onyo usije na mrembo kiasi hiki siku nyingine lazima nitakufanyia fujo," alisema yule kijana.
"Sawa mshindi ni wewe," alijibu Willy kwa dharau huku wakiondoka akiwa amemkumbatia Lolita kiunoni.
Macho ya watu wengi yaliwaangaza huku wakidiliki kusema.
"Lo, kweli vijana hao wanapendeza kwa uwili wao", kusema kweli vijana hao walikuwa wanapendeza sana. Kuchaguana walikuwa wamechaguana. Willy alikuwa mwenye sura ya kupendeza sana. Mavazi yalikuwa yakimkaa kama vile alizaliwa nayo kwa hivyo yalimfanya azidi kupendeza kiasi ambacho kila mtu aliyemuona alikiri kuwa alikuwa kijana nadhifu sana. Kwa jinsi hii haikuwa vigumu kwa Willy kuwa na uhusiano mzuri na wasichana wengi. Kwa upande wa mapato Willy alijulikana kuwa kijana mwenye kipato cha juu. Watu wengi hawakuelewa hasa alikuwa akifanya kazi gani, ila tu walijuwa alikuwa anashughulikia biasahara akiwa kama wakala wa makampuni ya nchi za nje katika Tanzania. Kwa hivi kusafirisafiri nchi za nje ambapo huyu kijana alikuwa akifanya mara kwa mara kuliweza kueleweka vilevile. Lakini ukweli wenyewe ni kwamba kijana nadhifu huyu hakuwa mfanyabiashara ila alikuwa mpelelezi maarufu katika Afrika jina lake kamili akiitwa Willy Gamba, ila watu wengi walijua jina lake la kwanza, kwa hiyo kila mtu alimwita kwa jina la Willy.
Msichana aliyekuwa amefuatana naye usiku huu alikuwa msichana rafiki kati ya rafiki zake wasichana wachache aliokuwa nao mjini Dar es Salaam. Msichana huyu alikuwa akifanya kazi na shirika la Reli Tanzania kama mwandishi muhtasi.
Kati ya wasichana wazuri mjini Dar es Salaam huyu msichana alikuwa mmoja wao, kwani alikuwa mrembo hasa. Alikuwa na umbo zuri kiasi cha kwamba kila apitapo watu humwangalia. Toka chini hadi juu alitosheleza kuitwa mrembo kwa kila hali. Kwa hiyo vijana hawa walipoonana hawakuwa na budi kupendana, kwani kwa uwili wao walipendeza sana kwani walionekana kama mapacha.
"Simu ilikuwa inatoka wapi?" aliuliza Lolita.
"Ilikuwa ni simu ya kikazi."
"Mteja wangu mmoja wa Lusaka amefika kuniona. Alipofika amepiga simu kwa mwandishi muhtasi wangu ambaye alianza kunitafuta mpaka amenipata. Kwa hivi inanibidi nikamuone sasa," Willy alidanganya.
"Kwanini usingoje kesho, yanini kumfuata usiku huu," Lolita aliendelea kudadisi,
"Unajua tena shughuli za kikazi, wateja wangu ni wafanyabiashara kama unionavyo mimi, kwa hiyo anaweza kuwa anasafiri kesho asubuhi huenda ndiyo maana ananihitaji haraka hivi," alizidi kudanganya.
"Lo, mwandishi wako lazima awe na kazi sana, kuamshwa usiku hivi na kuanza kukutafuta! Je kama na yeye angekuwa ameenda kustarehe huyo mteja wako angekupataje?" Lolita aliuliza.
"Kama mimi niko nje lazima mwandishi wangu yuko nyumbani na kama yeye yuko nje mimi niko nyumbani, hii ni sheria yetu ya kazi maana kazi yetu tunaweza kuhitajiwa na wateja wetu saa yoyote ofisini au nyumbani."
Walielezana yote haya huku wakielekea mjini wakirudi kutoka Kimara, "Sasa Loly mimi nitakupeleka mpaka nyumabani kwangu, halafu mimi nitakwenda nikaonane na huyu mgeni, mara moja nitakukuta."
"Lakini usikawie, eh Willy mpenzi."
"USiwe na wasiwasi, nitarudi mara tu nimalizapo mazungumzo." Kwa sababu saa hizi za usiku magari huwa hakuna, iliwachukuwa muda mchache kufika nyumabani kwa Willy, sehemu ya Upanga. Walipofika nyumbani, Willy alifungua nyumba wakaingia ndani.
"Mpenzi nenda kapumzike mimi nitarudi sasa hivi."
"Willy mpenzi, usikawie." Alilalamika Lolita huku Willy akimvuta na kumpa busu motomoto walikaa hivi kwa dakika mbili hivi ndipo akamwachia.
"Kalale Loly, nakuja sasa hivi," Willy alisema na kuondoka aliingia ndani ya gari lake akawasha moto kuelekea sehemu ya Mikumi ambako ndiko Maselina alikuwa akiishi. Wakati akielekea kwa Maselina, Willy alimfikiria sana Maselina. Alimfikiria kuwa msichana shupavu sana katika kazi yake. Maselina alikuwa mwandishi wa siri wa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Tanzania ambaye kiofisi alijulikana kama Chifu. Alikuwa na umri upatao miaka ishirini na sita (26) na alikuwa ameisha fanyakazi katika idara hii kwa muda wa miaka sita. Kwa ajili ya ushupavu wa kazi yake baada ya kuwa na idara hiyo kwa muda wa miaka mitatu aliweza kuchaguliwa kuwa mwandishi wa siri wa Chifu. Bado alikuwa hajaolewa na ilikuwa vigumu kujuwa ni kwa sababu gani kwani kama ni kwa uzuri alikuwa mzuri wa kutosha na kama ni kwa tabia alikuwa na tabia nzuri sana. Wafanyakazi wenziwe walifikiri kuwa huenda kazi aliyokuwa akiifanya ilimfanya asiweze kuolewa kwani kazi kama ile kwa mwanamke aliyeolewa ingekuwa ngumu kuitekeleza, Hata Willy alikubaliana na mawazo haya. Kila Maselina alipokuwa akiulizwa na marafiki zake juu ya suala hili la kuolewa alitabasamu tu na kusema, "Muda wangu wa kuolewa bado haujafikia", Willy na Maselina walikuwa wakielewana sana kikazi na kuelewana huku kulijenga urafiki wa aina yake kati yao. Watu wengi walifikiri kuwa walikuwa katika mapenzi lakini ukweli ni kuwa hata siku moja wazo hilo haliingia mawazoni mwao ingawaje siku zingine walikuwa wakienda kwenye starehe pamoja. Ili kuueleza urafiki kati ya Willy na Maselina nitaeleweka vizuri nikisema urafiki huu ulikuwa kama wa mtu na dada yake.
Ilikuwa saa nane za usiku wakati Willy aliposimamisha gari mbele ya nyumba ya Maselina. Taa ilikuwa ikiwaka sebuleni iliyoonyesha kuwa Maselina alikuwa macho akimsubiri Willy, "Karibu Willy, inakuchukua mwaka kutoka Kimara kufika hapa au ilibidi ukakifiche hicho chuma chako kabla ya kuja hapa!".
"Hauko mbali sana na ukweli," alijibu Willy huku akiingia ndani na Maselina alirudishia mlango.
Maselina alikwenda kufungua barafu akatoa chupa ya Konyagi na vpande vya barafu na ndimu akatenga bilauli mbili na kuweka Konyagi kwa ajili ya Willy na akatayarisha nyingine kwa ajili yake mwenyewe.
"Nimepata simu kutoka kwa Chifu, masaa machache yaliyopita," alieleza Maselina huku akiketi kitako, "Anakutaka ufike Lusaka kabla ya kesho mchana. Ameeleza kuwa kuna jambo muhimu sana kiasi cha kwamba unaweza ukahitajika kusafiri bila kurudi hapa Dar es Salaam. Kwa hivi ameamru kuwa ufanye safari yako kamili kamili kabisa. Hii Willy ina maana kuwa kuna safari nyingine kabambe inakungoja maana kufuatana na maelezo ya Chifu inabidi uende ukiwa na vyombo vyako vyote. Kuna ndege ya jeshi la Zambia ambayo ilifika hapa kuchukua mizigo yao, tayari mipango imeishafanywa uondoke nayo. Rubani wa ndege hiyo anazo habari kuwa atakuwa na abiria ambaye anahitajiwa kuhudhuria mkutano wa bodi ya wakurugenzi ya Tazara ambao unaendelea huko mjini Lusaka. Kwa hivyo utasafiri kama mfanyakazi wa Tazara hadi Lusaka ambapo utaonana na Chifu kwa maagizo zaidi. Ndege itaondoka saa nne asubuhi kwa hiyo nenda ukajitayarishe. Jina lako alilopewa rubani huyo ni Marko Mabawa, Meneja wa Shirika la Reli la Tazara. Nimempigia Wilson simu anakutayarishia hati ya kusafiria kwenda Lusaka kwa jina hilo ambayo ataileta moja kwa moja kwako asubuhi hii ya leo. Mambo mengine yamebaki juu yako kutekeleza. Je una swali kutokana maelezo hayo?" (Hapa Maselina alipumzika huku akimwangalia Willy kwa matumaini).
"La hasha", Willy alijibu, "Nafikiri nimekuelewa kwa ufasaha kabisa. Lililobaki ni dukuduku moyoni mwangu kuna nini huko Lusaka, maana hata jinsi Chifu alivyoitwa na kuondoka ilikuwa kiajabu ajabu. Hata hivyo nitapiga moyo konde nikayajuwe nitakapofika. Hii ina maana nimeitwa peke yangu?".
"Bila shaka, maana sikupata maelekezo ya mtu mwingine ila wewe tu", Maselina alijibu.
"Asante Maselina, mimi naondoka nikajitayarishe, kama kukwa na jambo lolote zaidi unaweza kunipata nyumbani kwangu kabla ya hiyo saa nne".
"Vizuri Willy, mimi ninakuombea safari njema uende salama Mungu awe nawe upate kurudi salama. Kama mara hii ni safari nyingine ya hatari ninakuomba ukajiangalie vizuri usije kupata madhala ya aina yoyote. Uwe ukikumbuka kuwa kila siku mimi nitakuwa pamoja nawe katika sala zangu, ukiwa na imani hiyo naamini utarudi salama maana Mungu anasema aombaye atapewa na vilevile husema anamsaidia anayejisaidia. Kwa hiyo kwa sababu tunaombea usalama wako ni matumaini yetu kuwa Mungu atakupa usalama kwa sababu wewe kila wakati unajisaidia vilevile Mungu atakusaidia.
"Asante kwa kunipa maneno ya kunipa moyo, ndiyo sababu Maselina sintaweza kukusahau hata kwa siku moja maisha mwangu kwa kufuatana na maneno ambayo huwa ukinipa kila ninapokuwa nikikaribiwa na safari kabambe", Willy alimaliza kinywaji chake akaagana na Maselina ambaye alimsindikiza hadi kwenye gari lake.
"Kwa heri Willy."
"Kwa heri Maselina," waliagana huku Willy akiondosha gari lake na kumpeperushia Maselina busu . Maselina alibaki pale nje ameshikwa na butwa na huku akisikia uchungu moyoni mwake kwa vile Willy alikuwa yumo mbioni kwenda katika safari zake za hatari.
Willy naye alishikwa na wasiwasi kuwa safari hii kwenda Lusaka ingezaa safari nyingine ya hatari.Lakini kwa vile Willy hatari ndiyo ilikuwa shughuli yake kidogo alikuwa akisikia roho ya furaha kujua kuwa alikuwa anakwenda kwenye safari nyingine ambayo ingeweza kuzaa hatari ila tu kilichokuwa kikimtia wasiwasi ni hatari za namna gani atakazo pambana nazo, maana safari hii ilikuwa ya kiajabu ajabu kufuatana na vile Chifu alivyo kuwa ameondoka na sasa alikuwa akimwita yeye Willy afike Lusaka upesi iwezekanavyo.
Willy aliwasili nyumbani kwake na kumkuta Lolita anagalagala tu kitandani bado hajalala.
"Mbona hulali Loly mpenzi?"
"Nitapataje usingizi bila ya wewe kuwa karibu nani? Nilikuwa ninakungoja kwa shauku sana.
Njoo basi unibembeleze nipate usingizi." Willy alikata shauri apate usingizi ingawaje wa muda mfupi kwa hivi alichojoa nguo zake tayari kwa kulala.
"Mgeni wako umempata", aliuliza Lolita huku akuwa amemkumbatia Willy.
"Nimeonana naye, na tumezungumza vya kutosha. Na katika mazungumzo yetu itanibidi asubuhi hii niende safari Lusaka." Lolita alishituka kidogo na kuanza kulalamika.
"Aah Willy usiende kesho, hata hatujafaidi "week-end" hii wewe unapanga safari! Ngoja utaenda jumatatu".
"Haitawezekana Loly, hata mimi ningependa nipumzike nawe "week-end" hii lakini inabidi niwe Lusaka kabla ya saa kumi mchana maana inabidi nionane na mteja wangu mmoja ambaye itambidi aondoke Lusaka Mjini Kuelekea Ulaya, kwa hiyo inanibidi nimuwahi kabla hajaondoka.
Usiwe na wasiwasi mimi nitarudi mara tu baada ya kuonana naye."
"Haya baba mimi siwezi kukulazimisha. Sogea basi unikumbatie vizuri." Willy alizima taa, akajisogeza na kumkumbatia Lolita vizuri.
Ilikuwa yapata saa kumi na mbili asubuhi Willy alipoamka na kuanza kujitayarisha. Lolita naye aliamka huku pombe bado zikiwa kichwani na usingizi ukiwa bado unamuelemea, lakini ilimbidi aamke kusudi aweze kumtengenezea Willy kifungua kinywa.
"Lala tu Loly mpenzi, mimi nitashughulika mwenyewe,"
Willy alimueleza alipomuona macho yake yakiwa mazito yamejaa usingizi.
"Hata ngoja nikutengenezee Chemsha kinywa, kama ni kulala nitalala wakati utakapoondoka.
"Hiari yako mama"
"Asante" alijibu Lolita huku akielekea jikoni. Willy alichukua mkoba wake maalumu wa kwa safari za namna hii na kuanza kuupakia. Alifungua sehemu ya uficho ya mkoba huu ambayo ikifungwa hakuna mtu anaweza kutambua kama kuna nafasi ya kutia vitu katika sehemu hiyo.
Alimchungulia Lolita na kumuona yupo jikoni akijishughulisha na kutengeneza chai. Aliendelea kufunguwa kabati lake, kisha akafunguwa saraka iliyokuwa ndani ya kabati na kutoa bastola tatu, fulana mbili zisizopenyezeka kwa risasi za bunduki, mabunda ya risasi na vitu vingine vingi vya kuweza kumsaidia wakati wa hatari kisha akaiweka ndani ya sehemu ya ufuko wa mkoba wake na kufunga.Baada ya kupakia vitu hivi aliingia kuweka vitu ambavyo mfanya biashara yeyote anategemea kuwa navyo safarini. Wakati akiwa katika pilikapilika hizi simu ililia na akaenda kuisikiliza.
"Hallo nyumbani kwa Gamba hapa,"
"Nani mwenzangu?"
"Wewe unataka kuzungumza na nani?"
"Naomba kuzungumza na ndugu Marko Mabawa"
"Subiri tafadhali," Willy alijibu huku kwa sauti nzito.
"Mimi ni rubani Josiah Banda wa Jeshi la anga la Zambia, Nadhani una habari zangu!"
"Aaa ndugu Banda habari za asubuhi?"
"Ni nzuri tu, je wewe,"
"Mimi salama. Habari zako nimepata na mimi niko katika pilika za kujitayarisha, nitakuwa uwanja wa ndege mnamo saa tatu hivi," alimweleza.
"Fanya mapema kidogo maanna tulikuwa tuondoke saa nne, lakini tumeamriwa sasa tuondoke saa tatu,"
"Sawa basi, "Willy alijibu, mimi nitakuwa hapo uwanjani kati ya saa mbili na saa mbili na nusu."
"Haya vizuri asante, tutaonana wakati huo."
"Asante kwaheri' alijibu Willy na kukata simu. Baada ya simu hii aliendelea na kutayarisha vitu vyake vya safari. Alipokuwa tayari, Lolita naye alikuwa ameandaa meza tayari kwa chemsha kinywa. Wote walikaa na kuanza kustafutahi.
"Nitaenda na gari mpaka uwanja wa ndege na nitamuachia kijana mmoja wa ofisini kwangu ambaye atakuletea. Unaweza kutumia gari mpaka hapo nitakaporudi," Willy alimweleza Lolita huku wakiendelea kula.
"Kama ni hivyo ngoja basi mimi nikusindikize hadi uwanja wa ndege na mimi nitarudi na gari,"
"Hapana, wewe pumzika tu maana hadi sasa bado hujalala."
"Wewe Mbona ndiye kabisa hujalala." Lolita alisema huku akimwangalia kwa macho ya kurembua.
"Mimi nimeisha zoea, usinitilie wasiwasi."
"Kama utakavyopenda Willy"
"Vile vile ningefurahi kama ungekuwa unakuja kuangalia nyumba mara moja moja hadi nitakaporudi."
"Ina maana utakaa sana."
"Hapana, lakini huwezi kujua mambo ya safari hii naweka kama tahadhari tu."
Kidogo walisikia gari linasimama nje. Willy alienda kufunguwa mlango akakuta ni Wilson.
"Karibu ndani," Willy alimkaribisha.
"Asante nimekuletea Pasi yako, mimi nakwenda," alijibu Wilson huku akiwa na wasiwasi kama kawaida yake kila aonanapo na Willy.
"Usiende, maana utanisindikiza hadi uwanja wa ndege. Gari lako acha hapa, utalichukuwa utakaporudisha gari langu." Waliingia ndani lakini Wilson alikataa kukaribia mezani huku akimkodolea macho Lolita ambaye alikuwa amevaa vazi la usiku.
Baada ya kustafutahi Willy na Lolita waliingia chumba cha kulala kwa mazungumzo mafupi.
"Oke Loly mpenzi, mimi ninakwenda tutaonana nitakaporudi."
Bila kumjibu Lolita alimng'ang'ania mabegani kwa kuanza kumpa busu kali sana lililochukuwa kama dakika tatu.
"Haya kwaheri Willy," Lolita aliaga taratibu huku mwili wake ukitetemeka.
"Asante, usiwe na wasiwasi mimi nitarudi upesi itakavyowezekana." Walitoka nje ya chumba.
"Twende zetu Wilson" Willy alisema huku amebeba mkoba wake ambao ulionekana mdogo sana, lakini huku ulikuwa umebeba mambo makubwa. Lolita aliwasindikiza mpaka kwenye gari, na walipoondoka alibaki machozi yakimtoka.
Willy alifika uwanja wa ndege kiasi cha saa mbili na dakika ishirini na kusimamisha gari lake kwenye lango la sehemu ya ndege za Jeshi la Tanzania.
"Wilson asante sana na sasa unaweza kurudi."
"Asante, safiri salama."
Kwenye lango alikuta mwanajeshi aliyekuwa kwenye zamu.
"Mimi ni Marko Mabawa ni abiria wa ndege ya Jeshi la Zambia," alijitambulisha.
"Ahaa wanakusubiri nenda kwenye ndege ile pale," askari alisema huku akionyesha kwa kidole ilipokuwa ndege ya Jeshi la Zambia. Alipofika alikuta Rubani Banda anamsubiri na baada ya kumaliza taratibu zote za safari za hapo kiwanjani waliingia ndani ya ndege tayari kwa kuruka kuelekea Lusaka, Zambia.
ITAENDELEA
 
35 Reactions
Reply
Back
Top Bottom