Riwaya : Kichaa

KICHAAA

ZUBERY R. MAVUGO.

[MR...FEELLING]

NO: 35

ENDELEA.

Sijisemei mimi namsemea mwanangu nakadhalika. Makala zile japo zilikuwa katika kalamu tena ya mkaa lakini mke wangu alizitunza na niliporejea kutoka jela nilihakikisha nazituma kwenye magazeti.

Nilifuhi na mwanangu pamoja na familia yangu, nikiwa kama muandishi niliweza kubaini kumbe rafiki yamgu Maganga alikuwa akishirikiana na wauaji pamoja na wafanya biashara haramu katika utetezi wake aliwatetea mahakamani watu wale. Nilipogundua hilo ilibidi ni muonye lakini katu hakukubali onyo langu na hata nilipomwambia kuw nitamshitaki alinicheka na kunisihi kuwa nisijifanye najua kuandika kila jambo kwani mambo mengine yanaweza kunigharimu. Kwakuwa sikupenda haki iende hivi hivi ndipo nilipoanza kumfuatilia na kumuandika badala yake nilizuiwa hata kutuma habari nilizoziandika kuhusu yeye, nilipouliza sababu sikupewa. Nilipojifanya king'ang'anizi nilifukuzwa kazi kwa kosa lakujitia kiherehere, nilikaa bila kazi na Maganga aliendelea kufanya ujinga wake, kwakuwa nilikuwa muandishi ambae kwa wakati huo jamii ilinihitaji sana na baadhi ya makampuni walikuwa wakisoma kazi zangu.

Ndipo nilipoletewa mkataba wa kuandika makala mbalimbali huko ndiko nilipojaribu kufichua uovu wa rafiki yangu yule, lakini nako pia nilitiomuliwa utadhani nilikuwa mkosaji kumbe mfumbuaji macho wa wananchi. Niliamua kwenda polisi huko nako sikupata msaada zaidi ya mimi mwenyewe kuteswa kwa kuwekwa ndani. Nilikuwa nikiifahamu sheria vizuri hivyo niliona jambo lile lakuwekwa ndani bila kosa ni uonevu wa maaskali, nilipotoka kwa dhamana nikapitiliza mahakamani na kwenda kumshtaki rafiki yangu Maganga ambae alikuwa akipokea rushwa kutoka kwa watu haramu na kuwatetea.

Kuna wengi walikamatwa na madawa ya kulevya lakini yeye aliwatetea kupitia hongo aliyopatiwa, alipokea rushwa hata kwa wauaji kitu ambacho kilinifanya nimuone mnyama. Nilipoenda mahakamani nilionekana kuwa sina ushahidi wa kutosha ingawa nilikuwa hadi na uthibitisho wa picha mbalimbali nilizompiga kipindi akipokea rushwa. Zaidi nilishauriwa kuwa niachane na mambo hayo kwani kazi yangu nikupiga picha pindi raisi au kiongozi wa serikali anapo toa ahadi kwa wananchi lakini sikupiga picha mambo kama yale. Pia waliniambia kuwa nisipede kujiingiza katika mambo yasiyo nifaa kwani itakuja kupelekea nijiingize matatizoni, mimi muandishi wa habari hivyo sina mamlaka ya kuingilia masuala ya polisi na mahakama.

Hapo niliamini kweli Maganga alikuwa akishirikiana na watu wenye mtandao mkubwa sana. Nilijisemea kuwa sikati tamaa mpaka nimuweke ndani, hapo nilimfuatilia na kumpiga picha tena akiwa anawasaidia walanguzi wa madawa ya kulevya, pia nika mpiga picha kipindi anapokea rushwa kisha nikajisemea kuwa swala hili lazma niliweke wazi kwa wananchi iliwatambue kabisa mambo yaliyokuwa yakifanywa na wale ambao wao wamewapa kipaumbele na kuaamini kuwa wanaweza kuwa saidia. Niliiweka habari ile gazetini na ikasambaa mtaani, watu wakajionea lakini chakushangaza baada ya siku mbili nilishangaa chapisho lililofuata kutoka gazeti hilohilo nililotumia likiwa lime kanusha habari yangu huku likinichafua vilivyo kwakusema kuwa huo nimpango wngu wa kumuharibia sifa mwanasheria mchapa kazi. Mchana wa siku hiyo mke wangu aliniita nakuniambia kuwa ni bora nitafute kazi nyingine kuliko hiyo ya uandishi kwani alihisi inapoenda kunipeleka ni kubaya sana.

''Hebu angalia, mtoto wetu ndio kwanza hata miaka kumi na oja hajatimiza istoshe mie mkeo ni mjamzito kwasasa we unadhani kwa kazi hiyo ya kutengeneza mabifu na wenye pesa tunaweza kufika?, najua unapenda haki na niwajibu wako kufichua maovu yatendwayo na watu pasina kujali. Lakini unadhani kwa hali hii tutafika?'' Alongea mengi sana mke wangu siku hiyo huku akinionesha gazeti lile lililotumika kunichafua na kumsafisha maganga.

Nilichukuwa muda wangu kufikiria ndipo nilipokumbuka kuwa ni heri ningesoma Linguistics niliyo shauriwa na marehemu Faraythati kuliko fani ile ya uandishi wa habari ambayo nilikazaniwa na Maganga niisome. Niliona, Faraythat alikuwa ana macho ya kuona mbali kwani kazi ile ndio iliyopelekea mimmi na rafiki yangu kukosana.

Ningekuwa mwalimu, ningewafundisha wanafunzi lugha na wakaelewa kisha nikachukuwa mshahara na nisikosane na Maganga zaidi tungesaidiana na kila mmoja angekuwa na maisha yake kuliko muda huo ambao nilikuwa nikiishi kwa bifu. Naam, niliona kazi ya uandishi hainifai, ndipo usiku wa siku ile nikiwa na mkewangu huku nikimuuliza juu ya biashara ambayo angependa nifanye kwani nilikuwa nina pesa katika akaunti yangu ambayo ingeweza nisaidia kufanya mambo yangu vizui tu. Mpka kwenye majira ya saa saba usiku tayari tulikuwa tumepata jibu, usiku huohuo ndipo walipoingia watu ambao mwanzo sikuwafahamu, watuwale walinipiga na kuniulia mwanangu pamoja na mfanyakazi wangu huku nikishuhudia kwa macho yangu mawili wakimbaka mke wangu.

Sikuwa na lakufanya zaidi ya kulia tu kwa uchun gu, mke wangu alianguka chini nami nikajua moja kwa moja atakuwa amepoteza maisha, watu wale walinmifuata pale na ndepo walipo nidokeza kuwa kazi ile walitumwa na Maganga kwani alishanionya sana lakini siku taka kusikia hivyo siku ile nio ilikuwa siku yangu ya kupoteza maisha iliniende nikafanye kazi yangu ya uandishi huko ahera. Mmoja wao alinyanyua rungu na kunipiga nalo. Na hapo ndipo mwanzo wa mimi kusahau kila kitu.

Nakumbuka nilitoka ubungo hadi hapa Mwanza kwa ajili ya kuja kutafuta maisha yangu. Sikuwa na kumbuka kama niliacha mke huko wala chochote lakini nilikuwa nina picha moja tu ambayo ndio ilikuwa ikinikumbusha mambo fulani niliyowahi kuyafanya maishani mwangu lakini kiukweli sikuwa nikiweza kuyaelezea kwani yalikuwa yakija na kupotea tu. Nilipoanza kuishi maisha yangu nililichagua jalala na kuhisi huko ndiko kunaweza kunisaidia mimi nisiyekuwa na makazi ya kuishi na hivyo ndivyo ilivyokuwa hadi leo hii nadhani ndio nimejitambua kwani sikuwanikijielewa kabisa kwa lolote lile.
*****

Mavugo alimaliza kuhadithia kumbukumbu ile hospitali na kuwaacha wote wakiwa na majonzi mengi, yote kwa yote walifurahi na kumshukuru Mungu kwa kuwapa ambacho hawakuwahi kukiomba.

Bila dokta Endrew kumuta Mavugo , na bila Mwambe kumuhitaji Neema, pia bila Mama Musa kuugua basi watu wale ilikuwa ni vigumu sana kukutana. Hakika Mungu hashindwi na chochote, kiwe kigumu ama chepesi. Mungu, hufanya vitu vya kushangaza sana ambavyo huleta mazingatio ya hali ya juu sana. Anaweza kukupa mtihani iliatoe fundisho au onyo kwa binadamu ambao mioyo yao imesha kata tamaa na kuamini kuwa Mungu hayupo. Ewe ndugu yangu, kaka, dada uliye hospitali ukilia kwa kukosa matibabu usimlaumu Mungu kwa kudhani kuwa hayupo na wewe au amekutenga sana. Mungu hufanya yote hayo kwa sababu zake, kama aliweza kumuokoa Mavugo ambae hakuwa na anachokikumbuka katika maisha yake basi hashindwi kukuokoa wewe ambae una ikumbuka familia yako kwa kuhangaika na kuhakikisha nyumbani hawashindi njaa. Jina la Mungu lihimidiwe.

Naam, wote kwa pamoja walitoka na kwenda hadi nyumbani kwa Devi hata walipofika huko, walipanga jinsi ya kuwakamata wale wote waliyosababisha Mavugo kuwa katika hali ile. Hilo halikuwa Tatizo kwa Waziri Mwambe ambae alifanya kazi hiyo nndani ya siku tatu tu na wote waliyompelekea Mavugo, kupoteza mwanae pamoja na kunajisiwa kwa mke wake yule ambae ilikuwa bado kidogo tu ampoteze mwanae aliyekuwa tumboni.

Maganga pamoja na wapuuzi wenzake walipatiwa hukumu ya kunyongwa hadi kufa kwani hawakufaa kabisa kuonekana katika uso wa dunia hii. miasha kati ya Mavugo na mkewe yaliendelea vizuri kama yalivyokuwa zamani huku akiwa chini ya usimamizi wa waziri Mwambe.

MWEZI MMOJA BAADAE.

'' Musa kwasasa sina hata chembe ya hisia nawewe. Kwa mambo yote yaliyotokea nimejikuta nikikuona kuwa wewe ni zaidi ya kaka kwa upande wangu tafadhali niruhusu nikuite Kaka na mapenzi yetu yasibaki hata kwa historia kwani mimi nawewe ni zaidi ya ndugu sasa.'' Aliongea Kisura huku akiwa amekaa kwenye moja kati ya makochi makubwa yanayo patikana sebuleni mwa kina Musa.

'' Usijali hata mimi nakuchukulia kama Dada yangu kufuatia ukaribu wa wazazi wetu. Tafadhali naomba unisamehe kwa kukufanya mpenzi ilhali wewe ni dada yangu. Labda zaidi tumshukuru Muumba kwani hakuruhusu tufanye chochote ambacho kinge tupelekea kujutia katika maisha yetu. Nakupenda sana dada yangu.'' Alijibu Musa, pia hakusita kumueleza kisura kuwa yule Neema ndio mpenzi wake wa halali. Wote kwa pamoja walifurahi sana na kutaniana, huku kwa wakati ule Neema akiwa Dar-es-salaam huko kwa waziri ambako ndiko alipokuwa akilelewa kwa muda huo.
............................ .................................

'' Mavugo, hakika wewe ni mwanamume wa kweli. Nimejaribu kupitia historia yako ya maisha na misimamo yako mbalimbali nimeamini hilo. Kumbe wewe hukuwa kichaa bali mwalimu uliye letwa na Mungu kwa ajili ya kuja kunifundisha mimi Endrew kuwa kusoma sana si kujua kila kitu. Umenifanya niuone uwezo wa Mungu mbele ya macho yangu, nashukuru sana kwa hilo. Ama kukutana kwetu kulikuwa na maana kubwa sana.'' Aliongea Docta Endrew pindi alipokuwa ametembelewa na Mavugo pamoja na mke wake MRS. Mavugo ama Mama Musa kama alivyojulikana. Mama yule ni daktari mkubwa sana lakini aliamua kuiacha shughuli ile kufuatia m,atatizo yaliyompata katika maisha yake. Aliirejesha furaha yake baada ya kuungana na familia yake tena kwa namna ya tofauti zaidi.

''Dokta Endrew. Nadhani unakumbuka kuwa niliwahi kukuambia hakuna binadamu asiye kachaa. Utakuwa umeamini kupitia maajabu haya ambayo kiukweli Mungu ameyatenda mahala pake. Waingereza huwa wanatabia ya kufanya uchunguzi huku wakijipatia ma vyeo ya sayansi lakini kamwe muafrika hana tabia hiyo na ndio maana huwa na imani kuwa kila kilichopo ni kwa ajili ya uthibitisho wa kuwa Mungu yupo. Uwepo wa mashariki na magharibi ndio chanzo cha kukuaminisha wewe kuwa jua huzama na kuchmoza, ilhali wana sayansi husema kuwa juwa huwa palepale isipokuwa dunia ndio huzunguka. Hakika uongo umekuwa ukweli, macho ya binadamu yameparazwa na misemo ya kisasa, huku masikio yao yakisikiliza kile kinachoitwa utandawazi na kusahau kuwa upo tangu dunia kuwekwa katika hii anga.

Kama wewe huamini, hebu nenda katizame milima jinsi ilivyo simamihwa utabaini kuwa hakuna isubiricho bali ni kiama. Ingetosha kabisa mbingu ikaoza na kuanguka kama ifanyavyo miti lakini Mungi kutimiza ubora wa utofautishaji ameipa miti majani na kuni nyima mimi binadamu yote hayo ni kutufanya tuamini kuwa hana ashindwalo. Kabla sijanyanyua mguu wangu na kurejea kulitumikia kampuni langu la magazeti ambalo nimepatiwa na ndugu yangu bwana Mwambe nataka nikupe kauli yangu ya hitma isemayo kuwa;

Binadamu yeyote ana maana yake kuwepo katika hii dunia na anamsaada mkubwa kwa binadamu mwenzake iwe kifikra au kifedha. Hivyo usimdharau yatima kwa kupungkiwa wazazi, usimdharau, kichaa kwa kupungukiwa ufikiri, usimkebehi masikini kwa kukosa chakula, usimuogope tajili kwa kuwa na mali. Hakuna mbora kati ya binadanu mwenzake zaidi ya mchaMungu pekee.'' Aliongea Mavugo kisha akachukuwana na mkewe hadi kwenye gali lao na baada ya kulipanda moja kwa moja wakaelekea nyumbani kwao.

Maisha ya Mavugo yakawa mazuri huku akipendwa na kuheshimiwa na wananchi wote wachukia uovu. Magazeti yake yaliuzika sana nchini kutokana na ubora wa waandishi aliyo waajili wakiwemo waandishi wa Hadithi za masimulizi ambao wao aliwalipa kwa kiwango cha juu sana kwani wao ndio walikuwa wakifanya magazeti yake ya uzike na kwa kasi sana. Wote kwa pamoja wakaishi maisha ya raha mustarehe huku shida wakiisikia na kuitatua kwa baadhi ya watu. Alifungua kituo cha kulelea watoto yatima na kujitolea magari katika hospitali mbalimbali za serikali hapa nchini. Na hivyo ndivyo alivyoendelea kuishi katika maisha yake yote.

MWISHO.
Chapter closed...

Story nzuri sana...

Ingawa Mavugo anaaikitisha sana kwa kujaribu kujiua sababu ya mwanamke tena mara mbili, kwa kitanzi na sumu...

Hujafa hujaumbika, we all demand respect...


Ahsante Madame S


Cc: mahondaw
 
RIWAYA: KICHAA.

Na: ZUBER R. MAVUGO.

N0. 01.

Njaa, iliendelea kulisumbua tumbo lake na kumpelekea kuanza kujipitisha maeneo ya ma'ntilie, huku akiamini kuwa shibe yake ipo mikononi mwao.

"mmh, mmh, mmh, puu. Lalalalala. Toka! Hebu tutolee kichefu chefu hapa," Ni baada ya mtu huyo kufika kwenye moja kati ya migahawa ipatikanayo maeneo ya Igoma ndani ya jiji la Mwanza, sauti moja ya mwanamama muuza mgahawa ndio iliyatoa maneno hayo yenye kuonesha kukereka kwa uwepo wa mtu fulani maeneo yale.

"Bado hunisikii. Eti, eee," Alibwata tena, huku mate yake yakishindwa kujizuia kubakia mdomoni na kujikuta yaki mwaga cheche zilizokuwa zikimfuata kijana ambae maneno hayo yalimuhusu yeye. Kijana yule ni kama hakuwa mwenye kusikia maneno yale, si.. Kwamba hana masikio. Laa! Hasha, bali pindi yalipomfikia yalipita sikio moja na kuelekea jingine.

"We.. Kichaa, unajifanya hausikii, si,ndio? Mnatoka huko makwenu mmefanya uchawi au kuiba mmelogwa halafu mnakuja mjini kuwa kero kwetu. Hebu toka, kabla sijakufanyia kitu kibaya." Mama yule aliendelea kumfukuza yule kijana kwa maneno lakini ndio kwanza kijana yule aliendelea kutabasamu huku meno yake machafu yakipata ruksa ya kuonekana maeneo yale.

"Anhaa! Kumbe unanicheka eti ee! Kwahiyo hapa nafanya upuuzi. Ngoja nikuoneshe," Aliongea mama yule huku miko yake akiwa ameiweka kwenye kiuno chake ambacho amekipiga kanga nzuri yenye maandishi ya bezo.

"Asia?," Aliita mama yule na baada ya yule muitwaji kuitika. Akasema, "Niletee hilo sufuria lenye maji ya moto hapa. Nataka ni muoneshe huyu mbwa," Asia, alitii amri na kuleta sufuria hilo. Kwa kuwa lilikuwa la moto, alishindwa kulibeba bila kuweka kitu cha kuzuia hali ile. Aliamua kuchana boksi na kulitengeneza vizuri kisha akalishikamanisha na sufuria lile, baada ya hapo akaliinua na kumpelekea Mama yule.

"Mwanaharamu mkubwa wewe. Unataka kuleta gundu mida hii.. Mbwa wewe." Alitamka maneno yale, kisha akayasindikiza maneno yake na maji ya moto yaliyompata vilivyo kijana yule.

Masikini, kijana yule, aliangua kilio kama cha mbwa mwizi. Sasa alishindwa kustahimili maumivu aliyonayo na kujikuta akikimbia hovyo mfano wa mbwa aliepigwa jiwe la kichwa.

"Hicho ndicho chakula chako. Mbwa mkubwa we... Na bado, allaaa!! Ukichaa peleka milembe, mjini kila mtu yupo timamu bwana." Maneno yale ya bila huruma ya ubinadamu yaliendelea kutoka mdomoni kwa mama yule bila hata haya. Aliendelea kujisifu kwa kuhisi amemkomesha binadamu mwenzake na kusema.

"Hatorudia tena. Wewe mbwa mwenyewe ukimwagia maji kiasi hicho, harudi tena. Ije yeye binadamu? Na akirudi basi atakuwa na roho ya paka. Halo, halo. Analeta ujiwe mbele ya nyundo. He,he,he,he. Ndo.. Basi tena." Baada ya kutamba kwa maneno yake pamoja na vidole vyake alivyovichezesha huku mkono mmoja akiwa kauweka kiunoni. Alirudi na sufuria lake ndani ya mgahawa huo, kisha akateka maji ya mengine na kuyachemsha.

"Mamaaa! Mammaaa! Nakufa! Nakufaaa. Yalaaaa!" Kijana yule alipiga kelele za uchungu wa maumivu huku akiendelea kukimbia hovyo bila kujielewa. Ingawa alikuwa na minywele mingi iliyochakaa, ngozi yenye ukurutu uliokomaa nakuwa kama machacha, ngozi hiyo ilifunikwa na madaso ambayo zamani yalikuwa nguo. Madaso hayo, yalichanika kila mahali, kwa harakaharaka usingeshindwa kumuita kichaa mtu yule, maana hata usowake, ulipambwa na poda ya jalala aina ya majivu, pamoja na mafuta ya oil.

Naam, alikuwa ni kichaa. Nadhani hata mama yule aliempa adhabu hiyo ya maji ya moto. Alimpa kwa sababu alijua kijana yule ni kichaa. Akashtaki wapi wakati Mahakama yake ni jalala? Akamlilie nani wakati wazazi wake ni mbwa wapatikanao mtaani? Nani wakumsaidia kijana huyo ambae hata hatathamani.

Ni njaa pekee ndiyo iliyompelekea kufanyiwa hivyo. Wakati wewe ukisikia njaa unakimbia mapema nyumbani kwako na kupata chakula, au unaenda mgahawani. Kumbe kuna wengine wanapata adhabu ya kuunguzwa na kutengenezewa majiraha kisa njaa zao.

Masikini, kijana yule aliendelea kukimbia huku maji yale yakiwa yameachia hatamu ya umoto na kusababisha maumivu yasiyo mithilika. Hapohapo jiraha kubwa lililoambatana na uvimbe kutokana na kuunguzwa kwa maji lilijijenga kuanzia, mkono wakushoto, ubavuni hadi mguuni. Aliendelea kukimbia hivyohivyo huku akiita neno 'MAMAA' na wala mama yake asije.

Wengi waliomuöna barabarani walimzomea wengine wa kimcheka na kumthihaki, huku wachache wakimtumia kwenye mada zao. Hakuna hata mmoja aliemsaidia kichaa yule japokuwa alikuwa akiomba msaada.

Alikimbia na kwenda kujitupa jalalani. Hakuwa na mahala pengine pakujisitili zaidi ya jalalani. Huko akakutana na watoto ambao nao walivalia madaso kama yeye huku wakiokota vyuma chakavu, pamoja na kina mama waliochafuka kwa kutafuta chakula ambacho hutupwa jalalani hapo. Watu wale masikini ndio walikuwa msaada wake, walimfuata na kumbeba, ingawa kila walipomvuta nguo, waliishia kubakiwa na kipande cha nguo hiyo kutokana na kuisha kwake. Lakini hilo halikuwafanya waache kumbeba na kumsogeza pembezoni mwa jalala lile.

Walipomsogeza pembeni, mapema tu wakaanza kumpatia huduma ya kwanza ya kishamba. Bora wangekuwa na asali ilikumpaka huenda ingesaidia, hawakuwa na dawa yeyote zaidi ya mchanga uliopatikana maeneo yale ya jalala. Walimpakaa mchanga ule wenye chembechembe za uchafu kisha wakamuhitaji apumzike iliasiendelee kuyahisi zaidi maumivu.

"Mpumzishe kwa lazima." Aliongea mama mmoja aliekuwa amesimama huku akiendelea kukiadhibu kichwa chake kwa kukikuta kutokana na muwasho aliokuwa akiupata;muwasho wa mmba pamoja na chawa katili.

"Sawa, maana inabidi apumzike tu." Alijibu mama mwingine ambae yeye alikuwa bize na kufukuza inzi maeneo ya kidonda. Kisha mama yule akaiacha kazi ile kwa nukta, na kupeleka mkono wake hadi kwa maeneo ya shingoni mwa kichaa yule ambae sasa alikuwa akipiga mikono yake chini pamoja na paji lake ilikupolea maumivu kama alivyodhani. Mama yule, aliigusa gusu shingo ya kichaa yule iliyojaaliwa ukurutu mgumu, na nikama alikuwa akitafuta mshipa fulani. Hata alipoupata aliuzimisha kiustadi wa hali ya juu na palepale kichaa yule alipoteza fahamu.

Ingawa njia ile ina madhara, lakini ndio njia pekee iliyopatikana kwao. Hawakuweza kumpeleka mgonjwa hosipitali akachomwe sindano ya ganzi iliasihisi uchungu au sindano ya usingizi kutokana na kutokuwa na pesa. Walilitambua hilo na walijua wazi hata kama wangempeleka hospitali, asingepata msaada wa aina yoyote ile zaidi ya kuangaliwa kwenye benchi kwa kebehi kama inzi mla mavi. Kwao, waliona njia pekee ya kutuliza maumivu ni kumfanya mgonjwa azimie kwa muda. Kumbe wakati wewe unapopata jiraha na kupigwa ganzi, au sindano ya usingizi. Kuna wengine ambao hata hiyo sindano hawaipati badala yake wanapata nyenzo za hatari.

"...we mama, leta hiyo siso kabla sijakuharibia hapa." Ni sauti ya ukali iliyotoka kinywani mwa mtoto mwenye umri wa miaka kumi na nne, maeneo ya jalala hilo. Sauti hiyo isiyojali utofauti wa miaka iliendelea kukoroma. Mama alieambiwa atoe chuma chakavu, alionesha kama kutosikia sauti ile ya dharau tena ukizingatia mtoaji wa sauti ile ni mtoto ambae anauwezo mkubwa sana wa kumzaa. Alifikiria endapo atampa chuma kile chakavu basi ataikosa pesa il-hali nae anashida chungu nzima, hivyo aliona uamuzi wa yeye kuwa nunda ndio pekee utamsaidia mbele ya mtoto yule.

"..we maza nunda sio? Nakwambia leta hapa hiyo siso." Aliendelea kutoa amri mtoto yule utadhani anaongea na mtoto mwenzake kumbe ni mama mzima. Mtoto yule alikuwa ana ngozi chafu iliyojaa ukurutu;ngozi ambayo hakuivika shati kutokana na ukosekanaji wa mashati juu ya hali duni aliyonayo. Huku chini akiwa amevaa kaptula iliyotoboka na kupelekea makalio yake yaliyopauka na kupata sugu kutokana na kukaliwa bila heshima yaonekane vilivyo pasina uficho.

"We... Mtoto wa mbwa, hebu kuwa na adabu pamoja na heshma. Wakubwa husalimiwa mjinga wewe, na sio kutolewa amri za siso tu." Aliongea mama yule kauli iliyohifadhi hasira za wazi juu ya kuchukia amri za mtoto yule mdogo ambae kwa kumuangalia tu. Anashindwa hata kumfananisha na watoto wake kutokana na umri mdogo alionao.

"Afu.. We, maza takuharibia sasa hivi. We sema kama hutaki kunipa hiyo siso uone kama siichukui kwa nguvu. Heshima unaijua wewe? Kama ungekuwa na heshima ungekuja huku jalalani? Acha ujinga. Wenye heshima na adabu wapo majumbani kwao wakipikia waume zao na kuosha watoto wao. Wewe upo huku jalalani halafu unaitaji heshima, sijui adabu. Hebu lete hiyo siso, mpuuzi mkubwa."

Mtoto yule alimkwapua mama kile chuma chakavu, kwa kuwa mama yule hakukubaliana na ile hali ya kunyakuliwa kirahisi chuma ambacho angekiuza na kupata pesa. Ndipo alipoamua kumvaa mtoto yule na kumng'ata vilivyo maeneo ya tumboni kwa kutumia meno yake yasioujua mswaki badala yake yanakijua chakula chajalala. Chakula ambacho kina bakteria waliojificha na wanaoonekana bila hata hadubini.

"Unaning'ata. Ayaah! Niachie mbwa wewe." Alibwata mtoto yule baada ya meno ya mama kuzama vilivyo kwenye ngozi yatumbo lake. Mama yule alisikia kilio cha mtoto yule, lakini hakini hakuhtaji kumuachia mpaka hapo atakapo hakikisha karejeshewa chuma chake iliakauze na kupata pesa.
Hapo mtoto yule akajihami kwa kumpiga mama yule na kile chuma kichwani. Kitendo kile kilimpelekea yule mama kuanguka chini huku damu nyingi zikimtoka na palepale alipoteza maisha.

Hakuna aliebaki maeneo ya jalala lile. Si, wakinamama waliokuwa wakimsaidia kichaa pembezoni mwa jalala, wala machokoraa waliokuwa wakijitafutia riziki. Wote walikimbia ilikuepuka kubambikiziwa kesi na maafande. Hata yule mtoto nae alitimka. Hapo ulibaki mwili wa mama yule. Pamoja na kichaa aliekuwa pembezoni.

Masaa kadhaa yalipita, hatimae yule kichaa alizinduka, kumbe muda huo ndio maafande walikuwa wanafika kwenye eneo la tukio. Walimbeba mama yule na kumbwaga kwenye gari kisha wakamchukua yule kichaa yule na kumsukumia ndani ya gari bila kujali jeraha lake.

"Afande, huyu mjinga ndio tuna mbebesha kesi ya mauaji." Aliongea afande mmoja.

"Huyu lazma itaijibu serikali, kwanini ameua." Alipokeza afande mwingine. Kisha maafande hao wakaingia wote kwa pamoja ndani ya gari.

Yule kichaa alisikilizia maumivu maradufu ya alivyo yapata kabla, kusukumwa na maafande wale kulimpelekea yeye kutonesha jeraha lake na kuyahisi maumivu makali yasiyo na ganzi. Alipiga ukelele kila maumivu yalivyozidi kuongezeka.
1

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom