bioto
JF-Expert Member
- Oct 1, 2017
- 1,261
- 2,095
- Thread starter
- #21
SEHEMU YA ISHIRINI..........20
Endelea......................
Ndani ya kijiji cha MPOLONI ambako kijana
KATUNJE alifika baada ya mwendo mrefu kutoka
kule ambako aliwaacha wale wenzake na
kutokomea na kuacha neno la kusema kuwa yeye
kuwa kafariki na lile jitu kule msituni, alifika akiwa
na furushi la majani na magome ya miti ambayo
ilipatikana kule lakini mkono ungine akiwa kashikilia
mche wa ule mti.
Haikujulikana aliubeba kwa lengo la kwenda
kuupanda au laa! Mzee Ukelele alizidi kumsubilia
lakini Katunje alikuwa na hali mbaya sana alikuwa
hajielewi kutokana na kuzidiwa na hali aliyonayo
lakini jambo ambalo lilimsaidia sana ni kule kufika
ndani ya kijiji cha Mpoloni. Akiwa ndani ya kijiji hiko
ndipo baadhi ya watu ambao walishawahi kumuona
katika moja ya nyumba ambayo alikuwa anapita
walianza kumsemasema "banahivi yule si ndio
alikujaga siku moja kuja kumuulizia bwana Ukelele?"
Huyo ambae alikuwa anaulizwa wote walikuwa
wenye umri wa makamo. "Ndio ndio yeye haswa,
sasa unakumbuka tulimlisha nyama yule sasa
hawezi kutupotea kabisa sasa ngoja nianze
kumfuatilia nyumanyuma". Kumbe walikuwa ni wale
watu ambao katunje kwa mara ya kwanza kuja
katika kijiji hiki cha Mpoloni aliweza kukutana na hii
familia ambayo aliweza kuwaomba kama msaada
wa kuelekezwa kwa Mzee Ukelele lakini
alichofanyiwa alipewa chakula chenye nyama ya
mtu.
Yani ni umafia na unyama uliokithiri ambao
hauelezeki kabisa. Basi Katunje alizidi
kuyumbayumba kama mtu ambae alikuwa kanywa
pombe kali. "ngoja kwanza usiende hivihivi yule
pale alipo hajielewi si unamuona sasa kachukue
usinga humo ndani kwenye nyungo ile alafu uje nayo
hapa haraka", Bibi huyo alimtuma mwenzake ambae
hakufanya ajizi kabisa alienda na kurudi na ule
usinga.
"Sasa hapa nenda na huu ukimkaribia tu basi mpige
nao kichwani hizi nywele baada ya hapo atakuwa
akili zake tumemchanganya na hatoweza kabisa
kuona mbele". Yule mtu aliyafanya hayo na kuanza
kumfuatilia bwana Katunje, wakati anaendelea
kwenda Katunje mkono wake ambao ulifungwa na
ile dawa ulianza kumuuma sana ndipo akasimama
"Mh! mkono mbona unavuta sana hapa kuna hatari
inabidi niwe makini sana'
Sasa alianza kwenda huku akiangalia nyuma,
hatimae alipata nguvu na kukimbia na akaondokana
na majanga ambayo aliandaliwa na wale watu
waliokuwa wakimuandama hali ya kuwa
hawamfahamu kabisa. Katunje aliendelea kuyoyoma
na njia ile hadi alipokaribia kwenye nyumba ya Mzee
Ukelele, alishindwa hata kuodikia zaidi alianguka
palepale na kupoteza fahamu.
Wakati huo mzee Ukelele yeye kwa upande wake
alikuwa maeneo ya shambani akipalilia mahindi
yake ambayo yalikuwa yanaonyesha hali nzuri huko
bustanini kwake. Hakuwa anafahamu lolote
kuhusiana na ujio wa bwana Katunje. Kumbe yule
bibi ambae alikuwa anamfuatilia alifika hadi kwenye
nyumba ya mzee Ukelele lakini aliweza kuishia
mbali na pale kutokana na ulinzi mkubwa sana
uliopo pale.
Alibaki kufyonya tuu kisha akageuza njia na kurudi
alikotokea, Kwenye nyumba hiyo alitokea binti
mmoja ambae anajulikana kwa jina la MWAIJA
alitoka nje baada ya kusikia kishindo cha mtu
kudondoka, "Mamaaa huyu kadondoka jamani alafu
babu hayupo hapa..." Aliamua kukimbia sana
kuelekea kule aliko babu yake ili kwenda kumpa
taarifa alimkuta mzee Ukelele akiwa anamalizia na
akijiandaa kurudi nyumbani kwake.
"Babuuu kuna mgonjwa kaanguka pale nyumbani"
"Mgonjwaaa haya twende haraka tukamuone".
Walitembea kwa mwendo wa haraka sana hadi
walipofika kwenye ile baraza walimkuta Katunje "
Aaaah kumbe huyu kijana " Alisema mzee Ukelele
"Babuu unamjua kwani?'' Mwaija aliuliza " Ndio yule
niliyekuambia kuwa atakupeleka kwa mama huyu
ndiko anakotokea anaitwa Katunje, sasa tumpeleke
ndani kwanza kwa ajili ya matibabu". Walisaidizana
kumpeleka ndani kisha wakamlaza matibabu
yaliendelea kuwa mazuri mpaka jioni akawa
amepata nafuu kidogo. Mzee huyo aliyatumia yale
majani pamoja na mizizi kwa kuisugua na kupata
dawa ambayo alimlisha kijana Katunje. "Muda
mchache tu katunje anatapika nyama na kitu kimoja
aina ya Irizi ambayo alilishwa. "Unaona hii ndio
ambayo ingekuua maisha yako mjukuu wangu, lakini
kama ulivyosema walikufuata ni kweli kwani kupitia
hiki kairizi walikuwa wanakuona popote pale ulipo
hivyo ingekuwa rahisi kwao kukukamata.
Siku ya pili yake matibabu yalimalizika na yeye
akawa vyekma kabisa ndipo akaanza kumueleza
kuhusiana na kumjua mtu ambae siku hiyo alikuwa
anamfuatilia Lyoto.
"Sasa naomba unisikilize, dawa hii siku ukifika tu
isugue kwenye jiwe kisha kula nyingine jipake
mwilini mzima wakati unakaribia kulala baada ya
hapo utalala na usiku utamshuhudia nani ambae
alikuwa anamfuatilia mtu wako na ilikuwaje, Pia
baada ya hapo utamuendea na kumhoji akikataa
dawa hii nyingine utaenda pale sehemu ya mwisho
ambayo utaiona kwenye ndoto ambapo waliishia na
huyo mtu akageuza nenda kaifukie hii kwenye moja
ya Mguu wake wa unyayo"
Katunje alikubali na akalipokea kwa mikono miwili
kabisa.
"Alafu itabidi leo hii muondoke na huyu binti
utaenda kumuacha kwa huyo mama aliyekuagiza ni
mtoto wake." Baada ya muda kupita safari ilianza
huku wakiwa wametengenezwa vyema kwa
kutosumbuliwa na mtu yeyote yule kama mwanzo
alivyokakaribishwa na wenyeji wa MPOLONI,
Majira ya usiku wanafika kijiji cha KILIMALONDO
kwa lengo la kutimiza ile ahadi ambayo alidhamilia
kuweza kuifanya kuwa lazima LYOTO apatikane kwa
hali yoyote ile kama yuko hai. Ndipo Katunje
alipomueleza binti huyo wa makamo kama Katunje
kuwa "Mwaija tumefika tayari lakini sasa ni usiku
sana itabidi tukapumzike kwenye nyumba yangu
alafu asubuhi nakupeleka kwa mama yako".
"swa haina shida twende" waliongozana na wakati
huo sasa mvua ikaanza kunyesha na ukizingatia
majumba ya kijiji cha KILIMALONDO, yapo
mbalimbali hivyo upepo wa kibaridi unaingia ndani
ya miili yao bila kizuizi kabisa. walifanikiwa kufika
hadi kwenye kibanda cha Katunje akafungua kisha
wakaingia ndani.
Nyuma iliezekwa kwa nyasi kiasi mahali ambako
palikuwa salama ni kitandani palikuwa hapalowi,
lakini sehemu nyingine nyingi mlikuwa mnalowa
maji yalikuwa yanapenya vyema tu, hivyo iliwabidi
aibu wazitoe kabisa wakalala kitanda hikohiko,
ndipo radi zilianza kuamsha hisia za wawili hao bila
kujijua baridi nalo likaendelea kuchombeza na
kuwafanya wajione kama waliohalalishwa kushikana
na kukamatana, walishasahau kama ni watu wawili
ambao hawakuwa na mahusiano kabla.
Sauti za kimahaba ziliendelea na bwana Katunje
kwa miaka kadhaa hakuwahi kuona ndani hivyo siku
hiyo Mbuzi alifia kwa muuza supu, Walimaliza na
Mwaija akajikuta anajishangaa sana kwa kufanya lile
tendo kwa kijana Katunje, 'Kwa nini nisimtamkie
kuwa nampenda kisha iwe rahisi mimi kuwa nae ili
anisaidie baadhi ya kazi hapa nyumbani' yalikuwa ni
mawazo ambayo alikuwa nayo kijana Katunje.
Asubuhi na mapema kila mmoja anamuonea aibu
mwenzake lakini wakajikuta kila mmoja
anamuonyeshea hisia za kwa nini tusikubaliane
kuoana kabisa. " Mwaija samahani ila muda huu
twende nikupeleke kwa mama yako ukamuone",
Walifuatana wote kwa pamoja hadi kwenye nyumba
ya mama Mwaija.
Kwa bahati mbaya kubwa sana wanamkuta mama
Mwaija kafariki na ilionyesha ni wa muda mrefu
sana tangu afariki, masikitiko yalianza pale hasa
binti Mwaija, alilia sana kwa kufiwa na Mama yake.
Alishindwa kuamini kwa kile ambacho
anakishuhudia. Waliondoka pale na Katunje alienda
kutoa taarifa kwa kiongozi bwana SWAI ambae
taarifa hiyo ilipokelewa na Kijana KIMOLO ambae
kama mlinzi wa mzee huyo aliyejiita mfalme wa
Kilimalondo.
Baada ya mazishi kupita ndipo Mwaija alidai kurudi
nyumbani kwa babu yake, ' Ngoja nitakupeleka
lakini dawa ile ambayo alinipa yule babu sijaifanya
nikiiifanya keshokutwa tunaenda sawa".
Katunje alimuonea huruma sana Mtoto Mwaija
ambae alionekana kutokuwa na furaha kwa wakati
wote, Katunje aliikanda dawa ile kwenye jiwe kama
alivyokaelekezwa na mzee Ukelele na kwa kuwa
ilikuwa ni majira ya kulala alilamba na nyingine
akajipaka, akamuambia na Mwaija nae ajipake tu na
ailambe na wote wakafanya hivyo,
'''Mama mwaija mbona unapenda kufuatilia mambo
yangu kwa nini?
""Wee mzee Kauzibe na mwenzako Udevu ndio
mnahusika kumpoteza Lyoto nyinyi""
"""Mama Mwaija usitake nikufanyie kitu ambacho
hutokuja kusahau maishani mwako"". Mzee Kauzibe
aliongea kwa kupaniki akimueleza mama Mwaija
aliyeonekana kuwa anafuatilia mambo yake, "Hata
kama lakini huniwezi na lazima tukatangaze kesho
wajue kuwa wewe na akiludi katunje haki ya nani
namuambia" Mzee Kauzibe aliondoka hadi kwake
akachukua upinde ambao aliupaka sumu ambayo
huwa anatumia sana katika mambo yake. alifikilia
lakini akaghaili ndipo akafungua kikopo kimoja na
akaanza kukiongelesha kile kikopo ndipo moshi wa
aina yake ukatoka ukaelekea hadi kwenye nyumba
ya mama Mwaija ule moshi ulikuwa kama uchawi
ambao ulimuingia Sehemu za uwazi kama
Masikio,mdomo, puani na ungine ukatambaa
kuingia sehemu za haja zote na hatimae anakufa.
"'Heeeeeiiiiheee heee Mamaaaaa". Katunje alipiga
kelele kubwa sana mpaka pale Mwaija alipoamka,
Mwaija alishangaa kwa nini Katunje kapiga mikelel
kama ile, " Vipi kuna nini?" Aliuliza Mwaija
"Hapana Ndoto tu itabidi tukiamka asubuhi turudi
kwenu ili nikuache kule kwanza sawa!"
Kweli kama kawaida walishakuwa kama wapenzi
sasa walianza safari ya kurudi nyumbani kwa Mzee
Ukelele ili kwenda kumueleza yale aliyoyaona
kwenye ndoto.
Walifika salama kabisa na wakapokelewa ndipo
wakamhadithia yale yaliyotokea kule mpaka mwisho
"Mh! mimi nimewasikia lakini kati yenu nahisi kuna
jambo ambalo mmeshalifanya ila haina shida kijana
naomba umtunze binti yangu aliyebaki baada ya
mama yake kufariki" Aliongea mzee Ukelele "Haina
shida babu
"Eheee vipi kuna ndoto yoyote ambayo umeiota
baada ya kufanya ile dawa?"
"Ndio lakini nimeota kuwa mzee Kauzibe kamuua
mama yake Mwaija kwa uchawi mweusi
ulioambatana na Moto, lakini sikuota ile niliyokuja
nayo yani kuhusu yule binti".
"Sawa kuhusiana na huyo mzee niachie mimi
nitamuonyesha, lakini sasa kama mwaija nae alikual
hiyo dawa basi ndoto kuhusiana na Huyo binti
aliyepotea ataiota huyu kwa hiyo tumsubiri lini
ataota na atuambie nini kaota, kwa hiyo kazi yako
ni kumuuliza kila siku kaota nini".
Katunje akaona bado kazi mbichi.
Ndani ya kijiji kimoja kijulikanacho kwa jina la
KALULU kuna familia moja ilikuwa na kikao
ambacho kilionekana kikao cha maana sana kwani
walikuwa makini sana pindi mtu mmoja akiongea,
Bwana mmoja alisimama na kusema " Jamani sisi
kama wanafamilia wa hapa basi hatuna budi
kusema kuwa hili jambo ni la kwetu sasa inatakiwa
wote kulitekeleza, mada iliyokuwepo hapa kuwa
Mke wangu pamoja na mimi kama mzee UWESU
nipo hapa mbele yenu kusema kuwa tunamhitaji
mwenetu NYAMALI tangu aende kwenye familia ya
mzee MAMBO SASA mpaka sasa kila nikituma
taarifa hakuna inayorudi sasa tuna wasiwasi na huko
aliko."
Kumbe mada ambayo iliwekwa mezani ilikuwa
inamhusu Mama SIKITU ambae kaolewa na bwana
CHITO kwenye familia ya mzee Mambo sasa.
walikubaliana kuwa mwenyekiti wa kijiji cha Kalulu
itabidi asafiri kabisa na aelekee kwenye kijiji cha
SHISHIMO ili kwenda kujua kama mtoto wao
Nyamali atakuwa ni mzima au laah! jambo hilo
lilipita vyema kabisa na ndipo mwenyekiti huyo
alijiandaaa kwa ajili ya kusafiri kwenda kwa bwana
MASANJA ambae ni mwenyekiti wa kijiji cha
Shishimo ili akajue anaweza kulitatua kwa namna
gani ili siku isije kuleta ugomvi baina ya hivi vijiji
viwili.
Siku ya pili yake ndipo mzee Mwenyekiti wa Kalulu
anaingia ndani ya kijiji cha Shishimo ili kuonana na
bwana Masanja.
Walikutana na wakati huo bwana Mapato
anaonekana kujiandaa kama kuhitaji kuondoka pale
kwa mwenyekiti na kwenda mahali pengine.
"Mzee vipi sule unaondoka leo kwa nini usiondoke
kesho?" Masanja alimhoji mapato aliyejulikana kwa
jina la SULE. " Yani hapa nashukuru kwani hapa
mwanga wa kumpata ndugu yangu unaonekana sasa
nataka kwenda kuwataarifu familia kisha nije kwa
awamu nyingine." Ndipo bwana Mapato akawa
anajiandaa na wakati huohuo mwenyekiti wa kijiji
cha Kalulu anaingia.
"Haaaah! rafiki khaaaaa! umepotea sana"
"Si kupotea kazi za kuwatumikia wana kijiji lazima
zituweke mbali kabisa"
walikaa mahali kwa kuwa walijua kuna jambo
ambalo linahitajika kuzungumzwa kwa wakati huo.
"Haya bwana kutoka kalulu nipe habari".
"Habari kubwa ni kuhusiana swala letu la
kuhakikisha uongozi wa kifalme tunaufutilia mbali
na tunauingiza wa uenyekiti, inatakiwa hii kauli
itambae maeneo yote kabla hata hatujaamua kuanza
kutembelea kimoja hadi kingine kwa upande wangu
tayari kampeni hizo zinaendelea baada ya kujua
kuwa ufalme wa kurithishana huwa tunawapata
viongozi wasiojitambua na kuwaacha vijana
pembeni kama sisi tukikaa tu"
Kwa manen aliyokuwa akiyaongea alionekana kuwa
mwenye utimamu mkubwa sana.
"Ni kweli bwana unalolisema "
"Kingine kama unakumbuka mwanakijiji wenu
mmoja anayejulikana kwa jina la CHITO mtoto wa
mzee MAMBO SASA alikuja kuchumbia kule Kalulu,
kwenye familia ya bwana UWESU kwa mtoto wao
NYAMALI unakumbuka?"
Msanja alikaa kimya maana mada hii ya pili kwake
ni ngumu sana kuingilia ovyo. " Haswaaa
nakumbuka vyema sana na hata maandishi yao
hapa tunayo."
"Sasa miaka takribani amchukue ingali Nyamali
yuko binti mpaka sasa hajawahi kurudi nyumbani
japo walikuwa wanaleta taarifa za kumhitaji yeye aje
nyumbani kwa kuwa wazee wake hawawezi
kutembea lakini hakuna majibu yeyote waliyoyapata,
kikubwa wanachotaka kuona kama ni mzima huyo
mtoto wao basi."
Mzee Masanja akakaa akawa anakumbuka siku
moja alipofika Chito
"""Yani mwenyekiti nakuambia leo ni siku ya nne
mke wangu sijamuona, kapotelea wapi sijui lakini
namhisi baba yangu kwa kuwa siku ya kwanza
niliyaona maji yakielekea chumbani kwake siku ya
pili makana na leo yote kwa pamoja asije akawa
anamlisha makana...makana...mke wangu....mke
wangu...mke wangu".
aliwaza na kuwazua hajui nini aseme wakati huo
sauti ya Bwana Chito ikirudia rudia kichwani mwake
kila mara kwa kule kukumbuka kwake. " Bwana
Masanja vipi mbona sikuelewi au kuna chochote
ulichogundua?" Aliuliza bwana huyo kutoka Kalulu.
"Ni kweli lazima niwaze sana kwa hili maana
linanitia shska sana, kukupa taarifa iliyokamili
kutokana sina uhakika wa kile nilichokisikia ila
ningependa kupata taarifa kamili ndipo niweze
kukueleza kila kitu".walikaa kwa muda kidogo kisha
yule mwenyekiti akasema "Sawa basi mimi naomba
niitiwe huyo bwana Chito kwani nadhani anaweza
kunipa maelezo ambayo yanaweza kunipa nguvu
kule niendako kuwapa moyo wale wazazi wake".
Kwa upande wa bwana Masanja ilionekana kama
kikwazo japo haikujulikana kwa sababu gani.
"Itabidi nikupeleke kwa bwana Mambo sasa ili
ukaongee nao kule kwao nadhani itakuwa njema
zaidi". Waliinuka wakati huo tayari bwana Mapato
alikuwa anayasikia hayo yote ambayo walikuwa
wakiyaongea huku akiwa anajiandaa kwa safari ya
kurudi ndani ya kijiji cha BWAWANI. Safari ya
kuelekea kwa bwana Mambo sasa haikuwa na
mafanikio ya uharaka kama walivyoifikilia kwani
hawakufanikiwa kumkuta mtu,
Wakiwa wanaondoka ndipo bwana Mambo sasa
anaonekana kuja kwa haraka kwenye nyumba yake,
baada ya kufika pale aliingia chumbani kwake kisha
akaingia uvunguni na kutoa furushi lake. alitoa
usinga pamoja na irizi nyingi sana za kutosha
ambazo hazikujulikana zinatumika kwenye mambo
gani zaidi. alimuendea Mama Sikitu na kumkokota
hadi kwenye nyungo akaanza kuimba huku na kule
kisha ghafla wapotea, safari yao ilifika kule sehemu
ambayo aliambiwa kuwa anahitajika kumpeleka yule
mtu ambae kamkamata.
Baada ya kumfikisha alisifiwa na kiongozi yule na
kuahidiwa pindi akimleta mjukuu wake hakika
atapandishwa cheo kikubwa sana. "Haaah haaah
haaah! hapa umenifurahisha sana kwa jambo hili,
sasa ujionee nini tunakifanya kwa huyu mwanamke".
Walimvua nguo zote na akabaki uchi wa unyama,
kama alivyozaliwa, walianza kumdhihaki kwa
maneno ya ajabuajabu sana wakati huo akiwa
kafungwa kamba. Mzee Mambo sasa alikuwa hapo
akiwaza jambo moja ambalo alikuwa analikumbuka
kichwani mwake """Babaa...unafikili hii kazi
uliyonayo itakufaidisha kitu gani unaua ndugu yako
wa karibu nani atakuzika au kukusaidia pindi ukiwa
na shida....mama umemuua unadhani hapa kijijini
nani anakupenda kutoka moyoni baada ya kufanya
haya mambo....au unadhani mwisho wa wewe kuua
unapata nini baba mke wangu yuko wapiiii?".
Maneno aliyokuwa akiyakumbuka kipindi
anaambiwa na mtoto wake, aliona kuwa kweli kile
akifanyacho siyo kizuli kabisa na sasa itabidi afanye
jambo lakini kachelewa na pale yupo kwa wakubwa
wake yani mizimu ya NYAMNYENA iko pale hana
sauti mbele yao. Waliendelea kumtesa ndipo mkuu
huyo akachukua kisu na kumfuata alimshika mdomo
kisha akaushika ulimi na kuukata kabisa, damu
nyingi zilimtoka na alishindwa kulia kwani alifanywa
kama zezeta hivi asiyejitambua, Mzee Mambo sasa
aliona huruma kutokana na ule ukatili ambao
alikuwa anafanyiwa mkwewe yani mke wa mtoto
wake.
Hawakuishia hapo walimtoa macho yote huku akiwa
mzima kabisa sijui maumivu ambayo aliyapata
yalikuwa ni ya aina gani jamani, baada ya aliitwa
mzee Mambo sasa akapewa kisu na kuambiwa
sasa amchinje hapo shingoni, alianza kuogopa
kabisa """KIJANA UOGA WAKO UNANIFANYA
NIBADILI MAAMUZI YA KUKUPA NGUVU NA UWEZO
MKUBWA KAMA Nyandu UKATILI WAKO HAPO
NDIPO NAUHITAJI UUFANYE HARAKA SANA"""
Aliongea huyo kiongozi kumuimiza bwana Mambo
sasa afanye harakja kwa jambo lile aliloambiwa.
Vijana walimfungua mama Sikitu aliyeonekana
kuzimia na wakamlaza, mzee huyo kwa mkono
wake mwenyewe anategesha kisu chake kwenye
shingo la mke wa mtoto wake wa kumzaa
mwenyewe, huku akiwa anatetemeka wanamuimbia
wimbo wa ushujaa kumpa nguvu ya kutenda lile
jambo akapitisha kisu kwa nguvu akarudisha kwa
nguvu akafanya hivyo mara kadhaa hakika damu
nyingi sana ziliruka pale na zingine zikamfikia
mwilini mwake kwenye nguo..Alikuwa na wasiwasi
kwa lile ambalo alikuwa analifanya.
Ikatoka kauli nyingine ya kuse,ma sasa amtoe
sehemu za siri za Mama Sikitu kwa haraka bila
kuogopa na bila kuchelewa na bila kukosea, Mzee
huyo alikuwa kama ndondocha ambae alikuwa
anafuata kile alichokuwa akiambiwa, wakati sasa
Mama Sikitu tayari keshakuwa Maiti mzee alitoa
nyeti zake pamoja na vitu alivyoambiwa kuvitoa.
baada ya hapo akapewa nyama iliyotokana na
Mwanadamu huyo na kuambiwa.
"HII ITABIDI UONDOKE NAYO NA UMPATIE
MWANAO AILE AKISHAKULA HATOWEZA
KUKUSUMBUA TENA, KWANI NA YEYE ATAKUWA
MUHUSIKA WA HILI WEWE UMEUA YEYE KALA"".
Baada tya hapo aliondoka baada ya kujihakikishia
yuko vizuri katika mwili hakuna damu yeyote bila
kujua kuwa nyuma ya mgongo wake kuna damu
nyingi sana ambazo hakuziona. alifika nyumbani
anamkuta mtoto wake akimsubiri " Chito mwanangu
vipi mbona umehuzunika yani bado unanituhumu
kuwa nimemchukua mkeo".
Wakati anamkaribia harufu ya mwanamke ikamjia
maana alikuwa akishika nyeti za Mama Huyo kwa
fujo ili aweze kuzikata vyema 'huyu baba katoka
kwa mwanamke alafu hajaoga huyu uzee wote huu
anakuwa malaya hivi duu' Alimshuku baba yake
katoka kwa mwanamke kutokana na ile harufu
iliyokuja.
"Baba unatokea wapi sasa hivi?" Chito aliuliza
"Natokea maporini kuangalia mtego wangu na hiki
ndicho kitoweo cha leo mana tulikuwa wawili na
bwana Nyandu tumegawana huko huko". Chito
alipokea kisha akamuacha baba yake atangulie
ndani alishangaa sana kuona damu nyingi alafu
anatembea akiwa hajiamini, pia harufu ile ndio
inamshangaza sana " Baba kuna mgeni kafika hapa
leo alikuwa anatuulizia sisi"
"Mgeni gani huyo?" "Mwenyekiti kutokan kijiji cha
Kalulu alikuja kufuatilia swala la mtoto wa mzee
UWESU mkwe wangu wanamhitaji mtoto wao
wamuone NYAMALI yaani mke wangu sasa sijui
baba utawaeleza nini hapo mana ushanitia
mashakani kabisa na wanatusubili kwa bwana
MASANJA mana hili jambo limefika kwake na
hatujui kamueleza nini huko kwa hiyo kajiandae
alafu tuende huko"
Ghafla mzee Mambo sasa anadondoka chini na
kuzimia.
Taarifa ya mzee KELEBU iliwafanya kuwa na amani
sana pale kijijini kwani hali ya binti Lyoto iliweza
kuwa salama kabisa, afya yake ilikuwa nzuri baada
ya kupata huduma kutoka kwenye miti ile
aliyokwenda kuichukua kijana BAMUZI mfalme
ambae anatarajiwa kukaa. Mzee huyo alimshauri
Mzee Ngololo kuwa aitishe mkutano wa wanakijiji
wote wa CHAMLO ili kuweza kuelezana baadhi ya
mambo yenye faida katika kile kijiji kwani tabia ya
wanakijiji hao kukataa kujitolea kumsaidia mfalme
kutafuta dawa si nzuri kabisa.
Mzee Ngololo alimuita bwana Mwalami na
kumuelza kitu "Bwana wewe nakupa siri ambayo
niliiweka kwa muda mrefu pia niliona kuitoa
mapema inaweza kuzua utata kwa mambo mawili
kwanza siri yenyewe tulipata taarifa ambayo sina
uhakika nayo kuwa "Mfumo wanataka kuubadilisha
hawataki tena kutawala kwa nja ya ufalme wanataka
kuwa na mwenyekiti ambae atachaguliwa kwa sifa
watakazoleta, pia wakatoa tamko kuwa tupeleke
majina ya vijiji ambavyo vinaongozwa kwa ufalme,
sasa jambo gumu kuwa hapa kijijini watu wanaishi
kwa amani lakini huu mfumo utakuja kumaliza watu,
pili wanasema hawataki kuamini mambo haya ya
mizimu tunayotaka sisi wanataka kuishi kawaida tu
bwana wewe".
"Mbona habari mpya hiyo, imetoka wapi?" aliuliza
bwana Mwalami. " Kiongozi wangu wa habari ndie
alifuata hizo taarifa wakati anatembea kijiji na kijiji
ili kujua yanayojili na kutuletea na hivyo kabahatika
kapitia kijiji cha KALULU kinavyoitwa kpo mbali sana
na mimi sijawahi kufika sasa kesho nadhani
atakuwa anarejea katika moja ya safari zake sasa
atatueleza zaidi kwani nadhani atakuwa huko akipita
kijiji kila kijiji kupata taarifa".
"Basi tusubiri nini cha kufanya baada ya yeye kurudi,
nitajua nini nikushauli lakini mkuu usisahau kuwa
kuna safari ya kwenda mpoloni kuhani msiba wa
kijana yule aliyemsaidia Bamuzi". "Hilo usijali
itapangwa safari kubwa lakini kwanza tumalize hali
ya huyu malkia baada ya hapo tukimkabidhi basi
tutakwenda"
Upande wa binti Naomi akiwa na mama yake
alimueleza kuhusiana na kijana ambae katokea
kumpenda sana kutoka moyoni na anashindwa
kuzuia hisia zake pindi akimkumbuka " Mama kuna
kijana alikuja juzi hapa yani mzuriii huyo,
nimempenda sana mama yani hata kwa kitu
chochote naomba ufanye ili nimpate huyo kijana".
mama yake alimuangalia sana Naomi akaona jinsi
gani anavyoteseka kimapenzi, alimuonea huruma
sana mwanae na mzazi siku zote hapendi kuona
kiumbe alichokitunza tumboni kwa muda mrefu
kinalalamika kwa jambo ambalo linawezekana.
"Mwanangu ebu niambie jina lake unalifahamu?' "
Mama nimelisahau kabisa japo aliniambiaga".
"Sawa ngoja keshokutwa nakwenda kwa Bwana
Ukelele naamini tutafanikiwa sana kwa hilo. Hatimae
siku zilikwenda na keshokutwa ikafika wakafunga
safari ya kwenda kijiji cha MPOLONI, walipofika
hadi kwenye nyumba hiyo ya mzee Ukelele
walimkuta yeye mwenyewe.
walimueleza shida yake na kwa kuwa huwa alikuwa
anakuja sana Mama Naomi ilikuwa rahisi
kukubaliwa 'Mzee huyu mwanangu ana shida na
kumpata mwanaume ambae anampenda sana sasa
naomba umsaidie".
"Naomi unamfahamu jina la huyo mwanaume?" "
Hapana"
"Haya chukua hiki kitu sema kisirisiri alafu taja kwa
sifa zake zote kama jina humjui na itakuwa rahisi
mimi kumjua na mkifika kwenu haitochukua siku
nyingi atakuja hapo." waliondoka wakiwa na imani
kuwa watasaidiwa na mwanaume huyo atakuja
kulealiko Naomi. wakati wao wanaondoka ndipo
Katunje na Mwaija walikuwa shambani ndipo
wakafika wakiwa wamechoka sana.
Mzee huyo alianza kufanya kazi ile lakini
anashangaa kuona Katunje analalamika mkono kuwa
dawa yake inambana kuonyesha kuna hatari fulani,
mzee ukelele akamuuliza " Kijana samahani isije
nakuumiza wewe unamjua NAOMI siku uliyekwenda
Chamlo ulishaonana nae?".
"Ndio babaaa nilikutana nae na ndie ambae
alinipeleka kwa mzee Mwalami..."
"Tobaaaaaaaaa........kumbe ndie wewe anayekuhitaji
huyu mama mpuuzi kweli alafu mjukuu wangu abaki
na nani shenzi " akavurugavuruga mitego yote
ambayo aliweka ili kumfanya mwanaume huyo
kwenda kumfuata Naomi na kumbe alikuwa Katunje
ambae kwa sasa ni mchumba wa Mwaija.
Baada ya siku kupita Mwaija alitamani kwenda
kupajua nyumbani kwa Katunje ambako alimtajia
kuwa ni SHISHIMO "Sawa siku moja tutakwenda
kwani hata mimi nimepakumbuka nyumbani sana ".
Walifurahi sana hasa Mwaija kumpata mwanaume
ambae hakutarajia kama atakuja kumpa raha na
amani moyoni mwake..............
Endelea......................
Ndani ya kijiji cha MPOLONI ambako kijana
KATUNJE alifika baada ya mwendo mrefu kutoka
kule ambako aliwaacha wale wenzake na
kutokomea na kuacha neno la kusema kuwa yeye
kuwa kafariki na lile jitu kule msituni, alifika akiwa
na furushi la majani na magome ya miti ambayo
ilipatikana kule lakini mkono ungine akiwa kashikilia
mche wa ule mti.
Haikujulikana aliubeba kwa lengo la kwenda
kuupanda au laa! Mzee Ukelele alizidi kumsubilia
lakini Katunje alikuwa na hali mbaya sana alikuwa
hajielewi kutokana na kuzidiwa na hali aliyonayo
lakini jambo ambalo lilimsaidia sana ni kule kufika
ndani ya kijiji cha Mpoloni. Akiwa ndani ya kijiji hiko
ndipo baadhi ya watu ambao walishawahi kumuona
katika moja ya nyumba ambayo alikuwa anapita
walianza kumsemasema "banahivi yule si ndio
alikujaga siku moja kuja kumuulizia bwana Ukelele?"
Huyo ambae alikuwa anaulizwa wote walikuwa
wenye umri wa makamo. "Ndio ndio yeye haswa,
sasa unakumbuka tulimlisha nyama yule sasa
hawezi kutupotea kabisa sasa ngoja nianze
kumfuatilia nyumanyuma". Kumbe walikuwa ni wale
watu ambao katunje kwa mara ya kwanza kuja
katika kijiji hiki cha Mpoloni aliweza kukutana na hii
familia ambayo aliweza kuwaomba kama msaada
wa kuelekezwa kwa Mzee Ukelele lakini
alichofanyiwa alipewa chakula chenye nyama ya
mtu.
Yani ni umafia na unyama uliokithiri ambao
hauelezeki kabisa. Basi Katunje alizidi
kuyumbayumba kama mtu ambae alikuwa kanywa
pombe kali. "ngoja kwanza usiende hivihivi yule
pale alipo hajielewi si unamuona sasa kachukue
usinga humo ndani kwenye nyungo ile alafu uje nayo
hapa haraka", Bibi huyo alimtuma mwenzake ambae
hakufanya ajizi kabisa alienda na kurudi na ule
usinga.
"Sasa hapa nenda na huu ukimkaribia tu basi mpige
nao kichwani hizi nywele baada ya hapo atakuwa
akili zake tumemchanganya na hatoweza kabisa
kuona mbele". Yule mtu aliyafanya hayo na kuanza
kumfuatilia bwana Katunje, wakati anaendelea
kwenda Katunje mkono wake ambao ulifungwa na
ile dawa ulianza kumuuma sana ndipo akasimama
"Mh! mkono mbona unavuta sana hapa kuna hatari
inabidi niwe makini sana'
Sasa alianza kwenda huku akiangalia nyuma,
hatimae alipata nguvu na kukimbia na akaondokana
na majanga ambayo aliandaliwa na wale watu
waliokuwa wakimuandama hali ya kuwa
hawamfahamu kabisa. Katunje aliendelea kuyoyoma
na njia ile hadi alipokaribia kwenye nyumba ya Mzee
Ukelele, alishindwa hata kuodikia zaidi alianguka
palepale na kupoteza fahamu.
Wakati huo mzee Ukelele yeye kwa upande wake
alikuwa maeneo ya shambani akipalilia mahindi
yake ambayo yalikuwa yanaonyesha hali nzuri huko
bustanini kwake. Hakuwa anafahamu lolote
kuhusiana na ujio wa bwana Katunje. Kumbe yule
bibi ambae alikuwa anamfuatilia alifika hadi kwenye
nyumba ya mzee Ukelele lakini aliweza kuishia
mbali na pale kutokana na ulinzi mkubwa sana
uliopo pale.
Alibaki kufyonya tuu kisha akageuza njia na kurudi
alikotokea, Kwenye nyumba hiyo alitokea binti
mmoja ambae anajulikana kwa jina la MWAIJA
alitoka nje baada ya kusikia kishindo cha mtu
kudondoka, "Mamaaa huyu kadondoka jamani alafu
babu hayupo hapa..." Aliamua kukimbia sana
kuelekea kule aliko babu yake ili kwenda kumpa
taarifa alimkuta mzee Ukelele akiwa anamalizia na
akijiandaa kurudi nyumbani kwake.
"Babuuu kuna mgonjwa kaanguka pale nyumbani"
"Mgonjwaaa haya twende haraka tukamuone".
Walitembea kwa mwendo wa haraka sana hadi
walipofika kwenye ile baraza walimkuta Katunje "
Aaaah kumbe huyu kijana " Alisema mzee Ukelele
"Babuu unamjua kwani?'' Mwaija aliuliza " Ndio yule
niliyekuambia kuwa atakupeleka kwa mama huyu
ndiko anakotokea anaitwa Katunje, sasa tumpeleke
ndani kwanza kwa ajili ya matibabu". Walisaidizana
kumpeleka ndani kisha wakamlaza matibabu
yaliendelea kuwa mazuri mpaka jioni akawa
amepata nafuu kidogo. Mzee huyo aliyatumia yale
majani pamoja na mizizi kwa kuisugua na kupata
dawa ambayo alimlisha kijana Katunje. "Muda
mchache tu katunje anatapika nyama na kitu kimoja
aina ya Irizi ambayo alilishwa. "Unaona hii ndio
ambayo ingekuua maisha yako mjukuu wangu, lakini
kama ulivyosema walikufuata ni kweli kwani kupitia
hiki kairizi walikuwa wanakuona popote pale ulipo
hivyo ingekuwa rahisi kwao kukukamata.
Siku ya pili yake matibabu yalimalizika na yeye
akawa vyekma kabisa ndipo akaanza kumueleza
kuhusiana na kumjua mtu ambae siku hiyo alikuwa
anamfuatilia Lyoto.
"Sasa naomba unisikilize, dawa hii siku ukifika tu
isugue kwenye jiwe kisha kula nyingine jipake
mwilini mzima wakati unakaribia kulala baada ya
hapo utalala na usiku utamshuhudia nani ambae
alikuwa anamfuatilia mtu wako na ilikuwaje, Pia
baada ya hapo utamuendea na kumhoji akikataa
dawa hii nyingine utaenda pale sehemu ya mwisho
ambayo utaiona kwenye ndoto ambapo waliishia na
huyo mtu akageuza nenda kaifukie hii kwenye moja
ya Mguu wake wa unyayo"
Katunje alikubali na akalipokea kwa mikono miwili
kabisa.
"Alafu itabidi leo hii muondoke na huyu binti
utaenda kumuacha kwa huyo mama aliyekuagiza ni
mtoto wake." Baada ya muda kupita safari ilianza
huku wakiwa wametengenezwa vyema kwa
kutosumbuliwa na mtu yeyote yule kama mwanzo
alivyokakaribishwa na wenyeji wa MPOLONI,
Majira ya usiku wanafika kijiji cha KILIMALONDO
kwa lengo la kutimiza ile ahadi ambayo alidhamilia
kuweza kuifanya kuwa lazima LYOTO apatikane kwa
hali yoyote ile kama yuko hai. Ndipo Katunje
alipomueleza binti huyo wa makamo kama Katunje
kuwa "Mwaija tumefika tayari lakini sasa ni usiku
sana itabidi tukapumzike kwenye nyumba yangu
alafu asubuhi nakupeleka kwa mama yako".
"swa haina shida twende" waliongozana na wakati
huo sasa mvua ikaanza kunyesha na ukizingatia
majumba ya kijiji cha KILIMALONDO, yapo
mbalimbali hivyo upepo wa kibaridi unaingia ndani
ya miili yao bila kizuizi kabisa. walifanikiwa kufika
hadi kwenye kibanda cha Katunje akafungua kisha
wakaingia ndani.
Nyuma iliezekwa kwa nyasi kiasi mahali ambako
palikuwa salama ni kitandani palikuwa hapalowi,
lakini sehemu nyingine nyingi mlikuwa mnalowa
maji yalikuwa yanapenya vyema tu, hivyo iliwabidi
aibu wazitoe kabisa wakalala kitanda hikohiko,
ndipo radi zilianza kuamsha hisia za wawili hao bila
kujijua baridi nalo likaendelea kuchombeza na
kuwafanya wajione kama waliohalalishwa kushikana
na kukamatana, walishasahau kama ni watu wawili
ambao hawakuwa na mahusiano kabla.
Sauti za kimahaba ziliendelea na bwana Katunje
kwa miaka kadhaa hakuwahi kuona ndani hivyo siku
hiyo Mbuzi alifia kwa muuza supu, Walimaliza na
Mwaija akajikuta anajishangaa sana kwa kufanya lile
tendo kwa kijana Katunje, 'Kwa nini nisimtamkie
kuwa nampenda kisha iwe rahisi mimi kuwa nae ili
anisaidie baadhi ya kazi hapa nyumbani' yalikuwa ni
mawazo ambayo alikuwa nayo kijana Katunje.
Asubuhi na mapema kila mmoja anamuonea aibu
mwenzake lakini wakajikuta kila mmoja
anamuonyeshea hisia za kwa nini tusikubaliane
kuoana kabisa. " Mwaija samahani ila muda huu
twende nikupeleke kwa mama yako ukamuone",
Walifuatana wote kwa pamoja hadi kwenye nyumba
ya mama Mwaija.
Kwa bahati mbaya kubwa sana wanamkuta mama
Mwaija kafariki na ilionyesha ni wa muda mrefu
sana tangu afariki, masikitiko yalianza pale hasa
binti Mwaija, alilia sana kwa kufiwa na Mama yake.
Alishindwa kuamini kwa kile ambacho
anakishuhudia. Waliondoka pale na Katunje alienda
kutoa taarifa kwa kiongozi bwana SWAI ambae
taarifa hiyo ilipokelewa na Kijana KIMOLO ambae
kama mlinzi wa mzee huyo aliyejiita mfalme wa
Kilimalondo.
Baada ya mazishi kupita ndipo Mwaija alidai kurudi
nyumbani kwa babu yake, ' Ngoja nitakupeleka
lakini dawa ile ambayo alinipa yule babu sijaifanya
nikiiifanya keshokutwa tunaenda sawa".
Katunje alimuonea huruma sana Mtoto Mwaija
ambae alionekana kutokuwa na furaha kwa wakati
wote, Katunje aliikanda dawa ile kwenye jiwe kama
alivyokaelekezwa na mzee Ukelele na kwa kuwa
ilikuwa ni majira ya kulala alilamba na nyingine
akajipaka, akamuambia na Mwaija nae ajipake tu na
ailambe na wote wakafanya hivyo,
'''Mama mwaija mbona unapenda kufuatilia mambo
yangu kwa nini?
""Wee mzee Kauzibe na mwenzako Udevu ndio
mnahusika kumpoteza Lyoto nyinyi""
"""Mama Mwaija usitake nikufanyie kitu ambacho
hutokuja kusahau maishani mwako"". Mzee Kauzibe
aliongea kwa kupaniki akimueleza mama Mwaija
aliyeonekana kuwa anafuatilia mambo yake, "Hata
kama lakini huniwezi na lazima tukatangaze kesho
wajue kuwa wewe na akiludi katunje haki ya nani
namuambia" Mzee Kauzibe aliondoka hadi kwake
akachukua upinde ambao aliupaka sumu ambayo
huwa anatumia sana katika mambo yake. alifikilia
lakini akaghaili ndipo akafungua kikopo kimoja na
akaanza kukiongelesha kile kikopo ndipo moshi wa
aina yake ukatoka ukaelekea hadi kwenye nyumba
ya mama Mwaija ule moshi ulikuwa kama uchawi
ambao ulimuingia Sehemu za uwazi kama
Masikio,mdomo, puani na ungine ukatambaa
kuingia sehemu za haja zote na hatimae anakufa.
"'Heeeeeiiiiheee heee Mamaaaaa". Katunje alipiga
kelele kubwa sana mpaka pale Mwaija alipoamka,
Mwaija alishangaa kwa nini Katunje kapiga mikelel
kama ile, " Vipi kuna nini?" Aliuliza Mwaija
"Hapana Ndoto tu itabidi tukiamka asubuhi turudi
kwenu ili nikuache kule kwanza sawa!"
Kweli kama kawaida walishakuwa kama wapenzi
sasa walianza safari ya kurudi nyumbani kwa Mzee
Ukelele ili kwenda kumueleza yale aliyoyaona
kwenye ndoto.
Walifika salama kabisa na wakapokelewa ndipo
wakamhadithia yale yaliyotokea kule mpaka mwisho
"Mh! mimi nimewasikia lakini kati yenu nahisi kuna
jambo ambalo mmeshalifanya ila haina shida kijana
naomba umtunze binti yangu aliyebaki baada ya
mama yake kufariki" Aliongea mzee Ukelele "Haina
shida babu
"Eheee vipi kuna ndoto yoyote ambayo umeiota
baada ya kufanya ile dawa?"
"Ndio lakini nimeota kuwa mzee Kauzibe kamuua
mama yake Mwaija kwa uchawi mweusi
ulioambatana na Moto, lakini sikuota ile niliyokuja
nayo yani kuhusu yule binti".
"Sawa kuhusiana na huyo mzee niachie mimi
nitamuonyesha, lakini sasa kama mwaija nae alikual
hiyo dawa basi ndoto kuhusiana na Huyo binti
aliyepotea ataiota huyu kwa hiyo tumsubiri lini
ataota na atuambie nini kaota, kwa hiyo kazi yako
ni kumuuliza kila siku kaota nini".
Katunje akaona bado kazi mbichi.
Ndani ya kijiji kimoja kijulikanacho kwa jina la
KALULU kuna familia moja ilikuwa na kikao
ambacho kilionekana kikao cha maana sana kwani
walikuwa makini sana pindi mtu mmoja akiongea,
Bwana mmoja alisimama na kusema " Jamani sisi
kama wanafamilia wa hapa basi hatuna budi
kusema kuwa hili jambo ni la kwetu sasa inatakiwa
wote kulitekeleza, mada iliyokuwepo hapa kuwa
Mke wangu pamoja na mimi kama mzee UWESU
nipo hapa mbele yenu kusema kuwa tunamhitaji
mwenetu NYAMALI tangu aende kwenye familia ya
mzee MAMBO SASA mpaka sasa kila nikituma
taarifa hakuna inayorudi sasa tuna wasiwasi na huko
aliko."
Kumbe mada ambayo iliwekwa mezani ilikuwa
inamhusu Mama SIKITU ambae kaolewa na bwana
CHITO kwenye familia ya mzee Mambo sasa.
walikubaliana kuwa mwenyekiti wa kijiji cha Kalulu
itabidi asafiri kabisa na aelekee kwenye kijiji cha
SHISHIMO ili kwenda kujua kama mtoto wao
Nyamali atakuwa ni mzima au laah! jambo hilo
lilipita vyema kabisa na ndipo mwenyekiti huyo
alijiandaaa kwa ajili ya kusafiri kwenda kwa bwana
MASANJA ambae ni mwenyekiti wa kijiji cha
Shishimo ili akajue anaweza kulitatua kwa namna
gani ili siku isije kuleta ugomvi baina ya hivi vijiji
viwili.
Siku ya pili yake ndipo mzee Mwenyekiti wa Kalulu
anaingia ndani ya kijiji cha Shishimo ili kuonana na
bwana Masanja.
Walikutana na wakati huo bwana Mapato
anaonekana kujiandaa kama kuhitaji kuondoka pale
kwa mwenyekiti na kwenda mahali pengine.
"Mzee vipi sule unaondoka leo kwa nini usiondoke
kesho?" Masanja alimhoji mapato aliyejulikana kwa
jina la SULE. " Yani hapa nashukuru kwani hapa
mwanga wa kumpata ndugu yangu unaonekana sasa
nataka kwenda kuwataarifu familia kisha nije kwa
awamu nyingine." Ndipo bwana Mapato akawa
anajiandaa na wakati huohuo mwenyekiti wa kijiji
cha Kalulu anaingia.
"Haaaah! rafiki khaaaaa! umepotea sana"
"Si kupotea kazi za kuwatumikia wana kijiji lazima
zituweke mbali kabisa"
walikaa mahali kwa kuwa walijua kuna jambo
ambalo linahitajika kuzungumzwa kwa wakati huo.
"Haya bwana kutoka kalulu nipe habari".
"Habari kubwa ni kuhusiana swala letu la
kuhakikisha uongozi wa kifalme tunaufutilia mbali
na tunauingiza wa uenyekiti, inatakiwa hii kauli
itambae maeneo yote kabla hata hatujaamua kuanza
kutembelea kimoja hadi kingine kwa upande wangu
tayari kampeni hizo zinaendelea baada ya kujua
kuwa ufalme wa kurithishana huwa tunawapata
viongozi wasiojitambua na kuwaacha vijana
pembeni kama sisi tukikaa tu"
Kwa manen aliyokuwa akiyaongea alionekana kuwa
mwenye utimamu mkubwa sana.
"Ni kweli bwana unalolisema "
"Kingine kama unakumbuka mwanakijiji wenu
mmoja anayejulikana kwa jina la CHITO mtoto wa
mzee MAMBO SASA alikuja kuchumbia kule Kalulu,
kwenye familia ya bwana UWESU kwa mtoto wao
NYAMALI unakumbuka?"
Msanja alikaa kimya maana mada hii ya pili kwake
ni ngumu sana kuingilia ovyo. " Haswaaa
nakumbuka vyema sana na hata maandishi yao
hapa tunayo."
"Sasa miaka takribani amchukue ingali Nyamali
yuko binti mpaka sasa hajawahi kurudi nyumbani
japo walikuwa wanaleta taarifa za kumhitaji yeye aje
nyumbani kwa kuwa wazee wake hawawezi
kutembea lakini hakuna majibu yeyote waliyoyapata,
kikubwa wanachotaka kuona kama ni mzima huyo
mtoto wao basi."
Mzee Masanja akakaa akawa anakumbuka siku
moja alipofika Chito
"""Yani mwenyekiti nakuambia leo ni siku ya nne
mke wangu sijamuona, kapotelea wapi sijui lakini
namhisi baba yangu kwa kuwa siku ya kwanza
niliyaona maji yakielekea chumbani kwake siku ya
pili makana na leo yote kwa pamoja asije akawa
anamlisha makana...makana...mke wangu....mke
wangu...mke wangu".
aliwaza na kuwazua hajui nini aseme wakati huo
sauti ya Bwana Chito ikirudia rudia kichwani mwake
kila mara kwa kule kukumbuka kwake. " Bwana
Masanja vipi mbona sikuelewi au kuna chochote
ulichogundua?" Aliuliza bwana huyo kutoka Kalulu.
"Ni kweli lazima niwaze sana kwa hili maana
linanitia shska sana, kukupa taarifa iliyokamili
kutokana sina uhakika wa kile nilichokisikia ila
ningependa kupata taarifa kamili ndipo niweze
kukueleza kila kitu".walikaa kwa muda kidogo kisha
yule mwenyekiti akasema "Sawa basi mimi naomba
niitiwe huyo bwana Chito kwani nadhani anaweza
kunipa maelezo ambayo yanaweza kunipa nguvu
kule niendako kuwapa moyo wale wazazi wake".
Kwa upande wa bwana Masanja ilionekana kama
kikwazo japo haikujulikana kwa sababu gani.
"Itabidi nikupeleke kwa bwana Mambo sasa ili
ukaongee nao kule kwao nadhani itakuwa njema
zaidi". Waliinuka wakati huo tayari bwana Mapato
alikuwa anayasikia hayo yote ambayo walikuwa
wakiyaongea huku akiwa anajiandaa kwa safari ya
kurudi ndani ya kijiji cha BWAWANI. Safari ya
kuelekea kwa bwana Mambo sasa haikuwa na
mafanikio ya uharaka kama walivyoifikilia kwani
hawakufanikiwa kumkuta mtu,
Wakiwa wanaondoka ndipo bwana Mambo sasa
anaonekana kuja kwa haraka kwenye nyumba yake,
baada ya kufika pale aliingia chumbani kwake kisha
akaingia uvunguni na kutoa furushi lake. alitoa
usinga pamoja na irizi nyingi sana za kutosha
ambazo hazikujulikana zinatumika kwenye mambo
gani zaidi. alimuendea Mama Sikitu na kumkokota
hadi kwenye nyungo akaanza kuimba huku na kule
kisha ghafla wapotea, safari yao ilifika kule sehemu
ambayo aliambiwa kuwa anahitajika kumpeleka yule
mtu ambae kamkamata.
Baada ya kumfikisha alisifiwa na kiongozi yule na
kuahidiwa pindi akimleta mjukuu wake hakika
atapandishwa cheo kikubwa sana. "Haaah haaah
haaah! hapa umenifurahisha sana kwa jambo hili,
sasa ujionee nini tunakifanya kwa huyu mwanamke".
Walimvua nguo zote na akabaki uchi wa unyama,
kama alivyozaliwa, walianza kumdhihaki kwa
maneno ya ajabuajabu sana wakati huo akiwa
kafungwa kamba. Mzee Mambo sasa alikuwa hapo
akiwaza jambo moja ambalo alikuwa analikumbuka
kichwani mwake """Babaa...unafikili hii kazi
uliyonayo itakufaidisha kitu gani unaua ndugu yako
wa karibu nani atakuzika au kukusaidia pindi ukiwa
na shida....mama umemuua unadhani hapa kijijini
nani anakupenda kutoka moyoni baada ya kufanya
haya mambo....au unadhani mwisho wa wewe kuua
unapata nini baba mke wangu yuko wapiiii?".
Maneno aliyokuwa akiyakumbuka kipindi
anaambiwa na mtoto wake, aliona kuwa kweli kile
akifanyacho siyo kizuli kabisa na sasa itabidi afanye
jambo lakini kachelewa na pale yupo kwa wakubwa
wake yani mizimu ya NYAMNYENA iko pale hana
sauti mbele yao. Waliendelea kumtesa ndipo mkuu
huyo akachukua kisu na kumfuata alimshika mdomo
kisha akaushika ulimi na kuukata kabisa, damu
nyingi zilimtoka na alishindwa kulia kwani alifanywa
kama zezeta hivi asiyejitambua, Mzee Mambo sasa
aliona huruma kutokana na ule ukatili ambao
alikuwa anafanyiwa mkwewe yani mke wa mtoto
wake.
Hawakuishia hapo walimtoa macho yote huku akiwa
mzima kabisa sijui maumivu ambayo aliyapata
yalikuwa ni ya aina gani jamani, baada ya aliitwa
mzee Mambo sasa akapewa kisu na kuambiwa
sasa amchinje hapo shingoni, alianza kuogopa
kabisa """KIJANA UOGA WAKO UNANIFANYA
NIBADILI MAAMUZI YA KUKUPA NGUVU NA UWEZO
MKUBWA KAMA Nyandu UKATILI WAKO HAPO
NDIPO NAUHITAJI UUFANYE HARAKA SANA"""
Aliongea huyo kiongozi kumuimiza bwana Mambo
sasa afanye harakja kwa jambo lile aliloambiwa.
Vijana walimfungua mama Sikitu aliyeonekana
kuzimia na wakamlaza, mzee huyo kwa mkono
wake mwenyewe anategesha kisu chake kwenye
shingo la mke wa mtoto wake wa kumzaa
mwenyewe, huku akiwa anatetemeka wanamuimbia
wimbo wa ushujaa kumpa nguvu ya kutenda lile
jambo akapitisha kisu kwa nguvu akarudisha kwa
nguvu akafanya hivyo mara kadhaa hakika damu
nyingi sana ziliruka pale na zingine zikamfikia
mwilini mwake kwenye nguo..Alikuwa na wasiwasi
kwa lile ambalo alikuwa analifanya.
Ikatoka kauli nyingine ya kuse,ma sasa amtoe
sehemu za siri za Mama Sikitu kwa haraka bila
kuogopa na bila kuchelewa na bila kukosea, Mzee
huyo alikuwa kama ndondocha ambae alikuwa
anafuata kile alichokuwa akiambiwa, wakati sasa
Mama Sikitu tayari keshakuwa Maiti mzee alitoa
nyeti zake pamoja na vitu alivyoambiwa kuvitoa.
baada ya hapo akapewa nyama iliyotokana na
Mwanadamu huyo na kuambiwa.
"HII ITABIDI UONDOKE NAYO NA UMPATIE
MWANAO AILE AKISHAKULA HATOWEZA
KUKUSUMBUA TENA, KWANI NA YEYE ATAKUWA
MUHUSIKA WA HILI WEWE UMEUA YEYE KALA"".
Baada tya hapo aliondoka baada ya kujihakikishia
yuko vizuri katika mwili hakuna damu yeyote bila
kujua kuwa nyuma ya mgongo wake kuna damu
nyingi sana ambazo hakuziona. alifika nyumbani
anamkuta mtoto wake akimsubiri " Chito mwanangu
vipi mbona umehuzunika yani bado unanituhumu
kuwa nimemchukua mkeo".
Wakati anamkaribia harufu ya mwanamke ikamjia
maana alikuwa akishika nyeti za Mama Huyo kwa
fujo ili aweze kuzikata vyema 'huyu baba katoka
kwa mwanamke alafu hajaoga huyu uzee wote huu
anakuwa malaya hivi duu' Alimshuku baba yake
katoka kwa mwanamke kutokana na ile harufu
iliyokuja.
"Baba unatokea wapi sasa hivi?" Chito aliuliza
"Natokea maporini kuangalia mtego wangu na hiki
ndicho kitoweo cha leo mana tulikuwa wawili na
bwana Nyandu tumegawana huko huko". Chito
alipokea kisha akamuacha baba yake atangulie
ndani alishangaa sana kuona damu nyingi alafu
anatembea akiwa hajiamini, pia harufu ile ndio
inamshangaza sana " Baba kuna mgeni kafika hapa
leo alikuwa anatuulizia sisi"
"Mgeni gani huyo?" "Mwenyekiti kutokan kijiji cha
Kalulu alikuja kufuatilia swala la mtoto wa mzee
UWESU mkwe wangu wanamhitaji mtoto wao
wamuone NYAMALI yaani mke wangu sasa sijui
baba utawaeleza nini hapo mana ushanitia
mashakani kabisa na wanatusubili kwa bwana
MASANJA mana hili jambo limefika kwake na
hatujui kamueleza nini huko kwa hiyo kajiandae
alafu tuende huko"
Ghafla mzee Mambo sasa anadondoka chini na
kuzimia.
Taarifa ya mzee KELEBU iliwafanya kuwa na amani
sana pale kijijini kwani hali ya binti Lyoto iliweza
kuwa salama kabisa, afya yake ilikuwa nzuri baada
ya kupata huduma kutoka kwenye miti ile
aliyokwenda kuichukua kijana BAMUZI mfalme
ambae anatarajiwa kukaa. Mzee huyo alimshauri
Mzee Ngololo kuwa aitishe mkutano wa wanakijiji
wote wa CHAMLO ili kuweza kuelezana baadhi ya
mambo yenye faida katika kile kijiji kwani tabia ya
wanakijiji hao kukataa kujitolea kumsaidia mfalme
kutafuta dawa si nzuri kabisa.
Mzee Ngololo alimuita bwana Mwalami na
kumuelza kitu "Bwana wewe nakupa siri ambayo
niliiweka kwa muda mrefu pia niliona kuitoa
mapema inaweza kuzua utata kwa mambo mawili
kwanza siri yenyewe tulipata taarifa ambayo sina
uhakika nayo kuwa "Mfumo wanataka kuubadilisha
hawataki tena kutawala kwa nja ya ufalme wanataka
kuwa na mwenyekiti ambae atachaguliwa kwa sifa
watakazoleta, pia wakatoa tamko kuwa tupeleke
majina ya vijiji ambavyo vinaongozwa kwa ufalme,
sasa jambo gumu kuwa hapa kijijini watu wanaishi
kwa amani lakini huu mfumo utakuja kumaliza watu,
pili wanasema hawataki kuamini mambo haya ya
mizimu tunayotaka sisi wanataka kuishi kawaida tu
bwana wewe".
"Mbona habari mpya hiyo, imetoka wapi?" aliuliza
bwana Mwalami. " Kiongozi wangu wa habari ndie
alifuata hizo taarifa wakati anatembea kijiji na kijiji
ili kujua yanayojili na kutuletea na hivyo kabahatika
kapitia kijiji cha KALULU kinavyoitwa kpo mbali sana
na mimi sijawahi kufika sasa kesho nadhani
atakuwa anarejea katika moja ya safari zake sasa
atatueleza zaidi kwani nadhani atakuwa huko akipita
kijiji kila kijiji kupata taarifa".
"Basi tusubiri nini cha kufanya baada ya yeye kurudi,
nitajua nini nikushauli lakini mkuu usisahau kuwa
kuna safari ya kwenda mpoloni kuhani msiba wa
kijana yule aliyemsaidia Bamuzi". "Hilo usijali
itapangwa safari kubwa lakini kwanza tumalize hali
ya huyu malkia baada ya hapo tukimkabidhi basi
tutakwenda"
Upande wa binti Naomi akiwa na mama yake
alimueleza kuhusiana na kijana ambae katokea
kumpenda sana kutoka moyoni na anashindwa
kuzuia hisia zake pindi akimkumbuka " Mama kuna
kijana alikuja juzi hapa yani mzuriii huyo,
nimempenda sana mama yani hata kwa kitu
chochote naomba ufanye ili nimpate huyo kijana".
mama yake alimuangalia sana Naomi akaona jinsi
gani anavyoteseka kimapenzi, alimuonea huruma
sana mwanae na mzazi siku zote hapendi kuona
kiumbe alichokitunza tumboni kwa muda mrefu
kinalalamika kwa jambo ambalo linawezekana.
"Mwanangu ebu niambie jina lake unalifahamu?' "
Mama nimelisahau kabisa japo aliniambiaga".
"Sawa ngoja keshokutwa nakwenda kwa Bwana
Ukelele naamini tutafanikiwa sana kwa hilo. Hatimae
siku zilikwenda na keshokutwa ikafika wakafunga
safari ya kwenda kijiji cha MPOLONI, walipofika
hadi kwenye nyumba hiyo ya mzee Ukelele
walimkuta yeye mwenyewe.
walimueleza shida yake na kwa kuwa huwa alikuwa
anakuja sana Mama Naomi ilikuwa rahisi
kukubaliwa 'Mzee huyu mwanangu ana shida na
kumpata mwanaume ambae anampenda sana sasa
naomba umsaidie".
"Naomi unamfahamu jina la huyo mwanaume?" "
Hapana"
"Haya chukua hiki kitu sema kisirisiri alafu taja kwa
sifa zake zote kama jina humjui na itakuwa rahisi
mimi kumjua na mkifika kwenu haitochukua siku
nyingi atakuja hapo." waliondoka wakiwa na imani
kuwa watasaidiwa na mwanaume huyo atakuja
kulealiko Naomi. wakati wao wanaondoka ndipo
Katunje na Mwaija walikuwa shambani ndipo
wakafika wakiwa wamechoka sana.
Mzee huyo alianza kufanya kazi ile lakini
anashangaa kuona Katunje analalamika mkono kuwa
dawa yake inambana kuonyesha kuna hatari fulani,
mzee ukelele akamuuliza " Kijana samahani isije
nakuumiza wewe unamjua NAOMI siku uliyekwenda
Chamlo ulishaonana nae?".
"Ndio babaaa nilikutana nae na ndie ambae
alinipeleka kwa mzee Mwalami..."
"Tobaaaaaaaaa........kumbe ndie wewe anayekuhitaji
huyu mama mpuuzi kweli alafu mjukuu wangu abaki
na nani shenzi " akavurugavuruga mitego yote
ambayo aliweka ili kumfanya mwanaume huyo
kwenda kumfuata Naomi na kumbe alikuwa Katunje
ambae kwa sasa ni mchumba wa Mwaija.
Baada ya siku kupita Mwaija alitamani kwenda
kupajua nyumbani kwa Katunje ambako alimtajia
kuwa ni SHISHIMO "Sawa siku moja tutakwenda
kwani hata mimi nimepakumbuka nyumbani sana ".
Walifurahi sana hasa Mwaija kumpata mwanaume
ambae hakutarajia kama atakuja kumpa raha na
amani moyoni mwake..............