RIWAYA: Joto La Mshumaa

SEHEMU YA ISHIRINI..........20
Endelea......................
Ndani ya kijiji cha MPOLONI ambako kijana
KATUNJE alifika baada ya mwendo mrefu kutoka
kule ambako aliwaacha wale wenzake na
kutokomea na kuacha neno la kusema kuwa yeye
kuwa kafariki na lile jitu kule msituni, alifika akiwa
na furushi la majani na magome ya miti ambayo
ilipatikana kule lakini mkono ungine akiwa kashikilia
mche wa ule mti.
Haikujulikana aliubeba kwa lengo la kwenda
kuupanda au laa! Mzee Ukelele alizidi kumsubilia
lakini Katunje alikuwa na hali mbaya sana alikuwa
hajielewi kutokana na kuzidiwa na hali aliyonayo
lakini jambo ambalo lilimsaidia sana ni kule kufika
ndani ya kijiji cha Mpoloni. Akiwa ndani ya kijiji hiko
ndipo baadhi ya watu ambao walishawahi kumuona
katika moja ya nyumba ambayo alikuwa anapita
walianza kumsemasema "banahivi yule si ndio
alikujaga siku moja kuja kumuulizia bwana Ukelele?"
Huyo ambae alikuwa anaulizwa wote walikuwa
wenye umri wa makamo. "Ndio ndio yeye haswa,
sasa unakumbuka tulimlisha nyama yule sasa
hawezi kutupotea kabisa sasa ngoja nianze
kumfuatilia nyumanyuma". Kumbe walikuwa ni wale
watu ambao katunje kwa mara ya kwanza kuja
katika kijiji hiki cha Mpoloni aliweza kukutana na hii
familia ambayo aliweza kuwaomba kama msaada
wa kuelekezwa kwa Mzee Ukelele lakini
alichofanyiwa alipewa chakula chenye nyama ya
mtu.
Yani ni umafia na unyama uliokithiri ambao
hauelezeki kabisa. Basi Katunje alizidi
kuyumbayumba kama mtu ambae alikuwa kanywa
pombe kali. "ngoja kwanza usiende hivihivi yule
pale alipo hajielewi si unamuona sasa kachukue
usinga humo ndani kwenye nyungo ile alafu uje nayo
hapa haraka", Bibi huyo alimtuma mwenzake ambae
hakufanya ajizi kabisa alienda na kurudi na ule
usinga.
"Sasa hapa nenda na huu ukimkaribia tu basi mpige
nao kichwani hizi nywele baada ya hapo atakuwa
akili zake tumemchanganya na hatoweza kabisa
kuona mbele". Yule mtu aliyafanya hayo na kuanza
kumfuatilia bwana Katunje, wakati anaendelea
kwenda Katunje mkono wake ambao ulifungwa na
ile dawa ulianza kumuuma sana ndipo akasimama
"Mh! mkono mbona unavuta sana hapa kuna hatari
inabidi niwe makini sana'
Sasa alianza kwenda huku akiangalia nyuma,
hatimae alipata nguvu na kukimbia na akaondokana
na majanga ambayo aliandaliwa na wale watu
waliokuwa wakimuandama hali ya kuwa
hawamfahamu kabisa. Katunje aliendelea kuyoyoma
na njia ile hadi alipokaribia kwenye nyumba ya Mzee
Ukelele, alishindwa hata kuodikia zaidi alianguka
palepale na kupoteza fahamu.
Wakati huo mzee Ukelele yeye kwa upande wake
alikuwa maeneo ya shambani akipalilia mahindi
yake ambayo yalikuwa yanaonyesha hali nzuri huko
bustanini kwake. Hakuwa anafahamu lolote
kuhusiana na ujio wa bwana Katunje. Kumbe yule
bibi ambae alikuwa anamfuatilia alifika hadi kwenye
nyumba ya mzee Ukelele lakini aliweza kuishia
mbali na pale kutokana na ulinzi mkubwa sana
uliopo pale.
Alibaki kufyonya tuu kisha akageuza njia na kurudi
alikotokea, Kwenye nyumba hiyo alitokea binti
mmoja ambae anajulikana kwa jina la MWAIJA
alitoka nje baada ya kusikia kishindo cha mtu
kudondoka, "Mamaaa huyu kadondoka jamani alafu
babu hayupo hapa..." Aliamua kukimbia sana
kuelekea kule aliko babu yake ili kwenda kumpa
taarifa alimkuta mzee Ukelele akiwa anamalizia na
akijiandaa kurudi nyumbani kwake.
"Babuuu kuna mgonjwa kaanguka pale nyumbani"
"Mgonjwaaa haya twende haraka tukamuone".
Walitembea kwa mwendo wa haraka sana hadi
walipofika kwenye ile baraza walimkuta Katunje "
Aaaah kumbe huyu kijana " Alisema mzee Ukelele
"Babuu unamjua kwani?'' Mwaija aliuliza " Ndio yule
niliyekuambia kuwa atakupeleka kwa mama huyu
ndiko anakotokea anaitwa Katunje, sasa tumpeleke
ndani kwanza kwa ajili ya matibabu". Walisaidizana
kumpeleka ndani kisha wakamlaza matibabu
yaliendelea kuwa mazuri mpaka jioni akawa
amepata nafuu kidogo. Mzee huyo aliyatumia yale
majani pamoja na mizizi kwa kuisugua na kupata
dawa ambayo alimlisha kijana Katunje. "Muda
mchache tu katunje anatapika nyama na kitu kimoja
aina ya Irizi ambayo alilishwa. "Unaona hii ndio
ambayo ingekuua maisha yako mjukuu wangu, lakini
kama ulivyosema walikufuata ni kweli kwani kupitia
hiki kairizi walikuwa wanakuona popote pale ulipo
hivyo ingekuwa rahisi kwao kukukamata.
Siku ya pili yake matibabu yalimalizika na yeye
akawa vyekma kabisa ndipo akaanza kumueleza
kuhusiana na kumjua mtu ambae siku hiyo alikuwa
anamfuatilia Lyoto.
"Sasa naomba unisikilize, dawa hii siku ukifika tu
isugue kwenye jiwe kisha kula nyingine jipake
mwilini mzima wakati unakaribia kulala baada ya
hapo utalala na usiku utamshuhudia nani ambae
alikuwa anamfuatilia mtu wako na ilikuwaje, Pia
baada ya hapo utamuendea na kumhoji akikataa
dawa hii nyingine utaenda pale sehemu ya mwisho
ambayo utaiona kwenye ndoto ambapo waliishia na
huyo mtu akageuza nenda kaifukie hii kwenye moja
ya Mguu wake wa unyayo"
Katunje alikubali na akalipokea kwa mikono miwili
kabisa.
"Alafu itabidi leo hii muondoke na huyu binti
utaenda kumuacha kwa huyo mama aliyekuagiza ni
mtoto wake." Baada ya muda kupita safari ilianza
huku wakiwa wametengenezwa vyema kwa
kutosumbuliwa na mtu yeyote yule kama mwanzo
alivyokakaribishwa na wenyeji wa MPOLONI,
Majira ya usiku wanafika kijiji cha KILIMALONDO
kwa lengo la kutimiza ile ahadi ambayo alidhamilia
kuweza kuifanya kuwa lazima LYOTO apatikane kwa
hali yoyote ile kama yuko hai. Ndipo Katunje
alipomueleza binti huyo wa makamo kama Katunje
kuwa "Mwaija tumefika tayari lakini sasa ni usiku
sana itabidi tukapumzike kwenye nyumba yangu
alafu asubuhi nakupeleka kwa mama yako".
"swa haina shida twende" waliongozana na wakati
huo sasa mvua ikaanza kunyesha na ukizingatia
majumba ya kijiji cha KILIMALONDO, yapo
mbalimbali hivyo upepo wa kibaridi unaingia ndani
ya miili yao bila kizuizi kabisa. walifanikiwa kufika
hadi kwenye kibanda cha Katunje akafungua kisha
wakaingia ndani.
Nyuma iliezekwa kwa nyasi kiasi mahali ambako
palikuwa salama ni kitandani palikuwa hapalowi,
lakini sehemu nyingine nyingi mlikuwa mnalowa
maji yalikuwa yanapenya vyema tu, hivyo iliwabidi
aibu wazitoe kabisa wakalala kitanda hikohiko,
ndipo radi zilianza kuamsha hisia za wawili hao bila
kujijua baridi nalo likaendelea kuchombeza na
kuwafanya wajione kama waliohalalishwa kushikana
na kukamatana, walishasahau kama ni watu wawili
ambao hawakuwa na mahusiano kabla.
Sauti za kimahaba ziliendelea na bwana Katunje
kwa miaka kadhaa hakuwahi kuona ndani hivyo siku
hiyo Mbuzi alifia kwa muuza supu, Walimaliza na
Mwaija akajikuta anajishangaa sana kwa kufanya lile
tendo kwa kijana Katunje, 'Kwa nini nisimtamkie
kuwa nampenda kisha iwe rahisi mimi kuwa nae ili
anisaidie baadhi ya kazi hapa nyumbani' yalikuwa ni
mawazo ambayo alikuwa nayo kijana Katunje.
Asubuhi na mapema kila mmoja anamuonea aibu
mwenzake lakini wakajikuta kila mmoja
anamuonyeshea hisia za kwa nini tusikubaliane
kuoana kabisa. " Mwaija samahani ila muda huu
twende nikupeleke kwa mama yako ukamuone",
Walifuatana wote kwa pamoja hadi kwenye nyumba
ya mama Mwaija.
Kwa bahati mbaya kubwa sana wanamkuta mama
Mwaija kafariki na ilionyesha ni wa muda mrefu
sana tangu afariki, masikitiko yalianza pale hasa
binti Mwaija, alilia sana kwa kufiwa na Mama yake.
Alishindwa kuamini kwa kile ambacho
anakishuhudia. Waliondoka pale na Katunje alienda
kutoa taarifa kwa kiongozi bwana SWAI ambae
taarifa hiyo ilipokelewa na Kijana KIMOLO ambae
kama mlinzi wa mzee huyo aliyejiita mfalme wa
Kilimalondo.
Baada ya mazishi kupita ndipo Mwaija alidai kurudi
nyumbani kwa babu yake, ' Ngoja nitakupeleka
lakini dawa ile ambayo alinipa yule babu sijaifanya
nikiiifanya keshokutwa tunaenda sawa".
Katunje alimuonea huruma sana Mtoto Mwaija
ambae alionekana kutokuwa na furaha kwa wakati
wote, Katunje aliikanda dawa ile kwenye jiwe kama
alivyokaelekezwa na mzee Ukelele na kwa kuwa
ilikuwa ni majira ya kulala alilamba na nyingine
akajipaka, akamuambia na Mwaija nae ajipake tu na
ailambe na wote wakafanya hivyo,
'''Mama mwaija mbona unapenda kufuatilia mambo
yangu kwa nini?
""Wee mzee Kauzibe na mwenzako Udevu ndio
mnahusika kumpoteza Lyoto nyinyi""
"""Mama Mwaija usitake nikufanyie kitu ambacho
hutokuja kusahau maishani mwako"". Mzee Kauzibe
aliongea kwa kupaniki akimueleza mama Mwaija
aliyeonekana kuwa anafuatilia mambo yake, "Hata
kama lakini huniwezi na lazima tukatangaze kesho
wajue kuwa wewe na akiludi katunje haki ya nani
namuambia" Mzee Kauzibe aliondoka hadi kwake
akachukua upinde ambao aliupaka sumu ambayo
huwa anatumia sana katika mambo yake. alifikilia
lakini akaghaili ndipo akafungua kikopo kimoja na
akaanza kukiongelesha kile kikopo ndipo moshi wa
aina yake ukatoka ukaelekea hadi kwenye nyumba
ya mama Mwaija ule moshi ulikuwa kama uchawi
ambao ulimuingia Sehemu za uwazi kama
Masikio,mdomo, puani na ungine ukatambaa
kuingia sehemu za haja zote na hatimae anakufa.
"'Heeeeeiiiiheee heee Mamaaaaa". Katunje alipiga
kelele kubwa sana mpaka pale Mwaija alipoamka,
Mwaija alishangaa kwa nini Katunje kapiga mikelel
kama ile, " Vipi kuna nini?" Aliuliza Mwaija
"Hapana Ndoto tu itabidi tukiamka asubuhi turudi
kwenu ili nikuache kule kwanza sawa!"
Kweli kama kawaida walishakuwa kama wapenzi
sasa walianza safari ya kurudi nyumbani kwa Mzee
Ukelele ili kwenda kumueleza yale aliyoyaona
kwenye ndoto.
Walifika salama kabisa na wakapokelewa ndipo
wakamhadithia yale yaliyotokea kule mpaka mwisho
"Mh! mimi nimewasikia lakini kati yenu nahisi kuna
jambo ambalo mmeshalifanya ila haina shida kijana
naomba umtunze binti yangu aliyebaki baada ya
mama yake kufariki" Aliongea mzee Ukelele "Haina
shida babu
"Eheee vipi kuna ndoto yoyote ambayo umeiota
baada ya kufanya ile dawa?"
"Ndio lakini nimeota kuwa mzee Kauzibe kamuua
mama yake Mwaija kwa uchawi mweusi
ulioambatana na Moto, lakini sikuota ile niliyokuja
nayo yani kuhusu yule binti".
"Sawa kuhusiana na huyo mzee niachie mimi
nitamuonyesha, lakini sasa kama mwaija nae alikual
hiyo dawa basi ndoto kuhusiana na Huyo binti
aliyepotea ataiota huyu kwa hiyo tumsubiri lini
ataota na atuambie nini kaota, kwa hiyo kazi yako
ni kumuuliza kila siku kaota nini".
Katunje akaona bado kazi mbichi.
Ndani ya kijiji kimoja kijulikanacho kwa jina la
KALULU kuna familia moja ilikuwa na kikao
ambacho kilionekana kikao cha maana sana kwani
walikuwa makini sana pindi mtu mmoja akiongea,
Bwana mmoja alisimama na kusema " Jamani sisi
kama wanafamilia wa hapa basi hatuna budi
kusema kuwa hili jambo ni la kwetu sasa inatakiwa
wote kulitekeleza, mada iliyokuwepo hapa kuwa
Mke wangu pamoja na mimi kama mzee UWESU
nipo hapa mbele yenu kusema kuwa tunamhitaji
mwenetu NYAMALI tangu aende kwenye familia ya
mzee MAMBO SASA mpaka sasa kila nikituma
taarifa hakuna inayorudi sasa tuna wasiwasi na huko
aliko."
Kumbe mada ambayo iliwekwa mezani ilikuwa
inamhusu Mama SIKITU ambae kaolewa na bwana
CHITO kwenye familia ya mzee Mambo sasa.
walikubaliana kuwa mwenyekiti wa kijiji cha Kalulu
itabidi asafiri kabisa na aelekee kwenye kijiji cha
SHISHIMO ili kwenda kujua kama mtoto wao
Nyamali atakuwa ni mzima au laah! jambo hilo
lilipita vyema kabisa na ndipo mwenyekiti huyo
alijiandaaa kwa ajili ya kusafiri kwenda kwa bwana
MASANJA ambae ni mwenyekiti wa kijiji cha
Shishimo ili akajue anaweza kulitatua kwa namna
gani ili siku isije kuleta ugomvi baina ya hivi vijiji
viwili.
Siku ya pili yake ndipo mzee Mwenyekiti wa Kalulu
anaingia ndani ya kijiji cha Shishimo ili kuonana na
bwana Masanja.
Walikutana na wakati huo bwana Mapato
anaonekana kujiandaa kama kuhitaji kuondoka pale
kwa mwenyekiti na kwenda mahali pengine.
"Mzee vipi sule unaondoka leo kwa nini usiondoke
kesho?" Masanja alimhoji mapato aliyejulikana kwa
jina la SULE. " Yani hapa nashukuru kwani hapa
mwanga wa kumpata ndugu yangu unaonekana sasa
nataka kwenda kuwataarifu familia kisha nije kwa
awamu nyingine." Ndipo bwana Mapato akawa
anajiandaa na wakati huohuo mwenyekiti wa kijiji
cha Kalulu anaingia.
"Haaaah! rafiki khaaaaa! umepotea sana"
"Si kupotea kazi za kuwatumikia wana kijiji lazima
zituweke mbali kabisa"
walikaa mahali kwa kuwa walijua kuna jambo
ambalo linahitajika kuzungumzwa kwa wakati huo.
"Haya bwana kutoka kalulu nipe habari".
"Habari kubwa ni kuhusiana swala letu la
kuhakikisha uongozi wa kifalme tunaufutilia mbali
na tunauingiza wa uenyekiti, inatakiwa hii kauli
itambae maeneo yote kabla hata hatujaamua kuanza
kutembelea kimoja hadi kingine kwa upande wangu
tayari kampeni hizo zinaendelea baada ya kujua
kuwa ufalme wa kurithishana huwa tunawapata
viongozi wasiojitambua na kuwaacha vijana
pembeni kama sisi tukikaa tu"
Kwa manen aliyokuwa akiyaongea alionekana kuwa
mwenye utimamu mkubwa sana.
"Ni kweli bwana unalolisema "
"Kingine kama unakumbuka mwanakijiji wenu
mmoja anayejulikana kwa jina la CHITO mtoto wa
mzee MAMBO SASA alikuja kuchumbia kule Kalulu,
kwenye familia ya bwana UWESU kwa mtoto wao
NYAMALI unakumbuka?"
Msanja alikaa kimya maana mada hii ya pili kwake
ni ngumu sana kuingilia ovyo. " Haswaaa
nakumbuka vyema sana na hata maandishi yao
hapa tunayo."
"Sasa miaka takribani amchukue ingali Nyamali
yuko binti mpaka sasa hajawahi kurudi nyumbani
japo walikuwa wanaleta taarifa za kumhitaji yeye aje
nyumbani kwa kuwa wazee wake hawawezi
kutembea lakini hakuna majibu yeyote waliyoyapata,
kikubwa wanachotaka kuona kama ni mzima huyo
mtoto wao basi."
Mzee Masanja akakaa akawa anakumbuka siku
moja alipofika Chito
"""Yani mwenyekiti nakuambia leo ni siku ya nne
mke wangu sijamuona, kapotelea wapi sijui lakini
namhisi baba yangu kwa kuwa siku ya kwanza
niliyaona maji yakielekea chumbani kwake siku ya
pili makana na leo yote kwa pamoja asije akawa
anamlisha makana...makana...mke wangu....mke
wangu...mke wangu".
aliwaza na kuwazua hajui nini aseme wakati huo
sauti ya Bwana Chito ikirudia rudia kichwani mwake
kila mara kwa kule kukumbuka kwake. " Bwana
Masanja vipi mbona sikuelewi au kuna chochote
ulichogundua?" Aliuliza bwana huyo kutoka Kalulu.
"Ni kweli lazima niwaze sana kwa hili maana
linanitia shska sana, kukupa taarifa iliyokamili
kutokana sina uhakika wa kile nilichokisikia ila
ningependa kupata taarifa kamili ndipo niweze
kukueleza kila kitu".walikaa kwa muda kidogo kisha
yule mwenyekiti akasema "Sawa basi mimi naomba
niitiwe huyo bwana Chito kwani nadhani anaweza
kunipa maelezo ambayo yanaweza kunipa nguvu
kule niendako kuwapa moyo wale wazazi wake".
Kwa upande wa bwana Masanja ilionekana kama
kikwazo japo haikujulikana kwa sababu gani.
"Itabidi nikupeleke kwa bwana Mambo sasa ili
ukaongee nao kule kwao nadhani itakuwa njema
zaidi". Waliinuka wakati huo tayari bwana Mapato
alikuwa anayasikia hayo yote ambayo walikuwa
wakiyaongea huku akiwa anajiandaa kwa safari ya
kurudi ndani ya kijiji cha BWAWANI. Safari ya
kuelekea kwa bwana Mambo sasa haikuwa na
mafanikio ya uharaka kama walivyoifikilia kwani
hawakufanikiwa kumkuta mtu,
Wakiwa wanaondoka ndipo bwana Mambo sasa
anaonekana kuja kwa haraka kwenye nyumba yake,
baada ya kufika pale aliingia chumbani kwake kisha
akaingia uvunguni na kutoa furushi lake. alitoa
usinga pamoja na irizi nyingi sana za kutosha
ambazo hazikujulikana zinatumika kwenye mambo
gani zaidi. alimuendea Mama Sikitu na kumkokota
hadi kwenye nyungo akaanza kuimba huku na kule
kisha ghafla wapotea, safari yao ilifika kule sehemu
ambayo aliambiwa kuwa anahitajika kumpeleka yule
mtu ambae kamkamata.
Baada ya kumfikisha alisifiwa na kiongozi yule na
kuahidiwa pindi akimleta mjukuu wake hakika
atapandishwa cheo kikubwa sana. "Haaah haaah
haaah! hapa umenifurahisha sana kwa jambo hili,
sasa ujionee nini tunakifanya kwa huyu mwanamke".
Walimvua nguo zote na akabaki uchi wa unyama,
kama alivyozaliwa, walianza kumdhihaki kwa
maneno ya ajabuajabu sana wakati huo akiwa
kafungwa kamba. Mzee Mambo sasa alikuwa hapo
akiwaza jambo moja ambalo alikuwa analikumbuka
kichwani mwake """Babaa...unafikili hii kazi
uliyonayo itakufaidisha kitu gani unaua ndugu yako
wa karibu nani atakuzika au kukusaidia pindi ukiwa
na shida....mama umemuua unadhani hapa kijijini
nani anakupenda kutoka moyoni baada ya kufanya
haya mambo....au unadhani mwisho wa wewe kuua
unapata nini baba mke wangu yuko wapiiii?".
Maneno aliyokuwa akiyakumbuka kipindi
anaambiwa na mtoto wake, aliona kuwa kweli kile
akifanyacho siyo kizuli kabisa na sasa itabidi afanye
jambo lakini kachelewa na pale yupo kwa wakubwa
wake yani mizimu ya NYAMNYENA iko pale hana
sauti mbele yao. Waliendelea kumtesa ndipo mkuu
huyo akachukua kisu na kumfuata alimshika mdomo
kisha akaushika ulimi na kuukata kabisa, damu
nyingi zilimtoka na alishindwa kulia kwani alifanywa
kama zezeta hivi asiyejitambua, Mzee Mambo sasa
aliona huruma kutokana na ule ukatili ambao
alikuwa anafanyiwa mkwewe yani mke wa mtoto
wake.
Hawakuishia hapo walimtoa macho yote huku akiwa
mzima kabisa sijui maumivu ambayo aliyapata
yalikuwa ni ya aina gani jamani, baada ya aliitwa
mzee Mambo sasa akapewa kisu na kuambiwa
sasa amchinje hapo shingoni, alianza kuogopa
kabisa """KIJANA UOGA WAKO UNANIFANYA
NIBADILI MAAMUZI YA KUKUPA NGUVU NA UWEZO
MKUBWA KAMA Nyandu UKATILI WAKO HAPO
NDIPO NAUHITAJI UUFANYE HARAKA SANA"""
Aliongea huyo kiongozi kumuimiza bwana Mambo
sasa afanye harakja kwa jambo lile aliloambiwa.
Vijana walimfungua mama Sikitu aliyeonekana
kuzimia na wakamlaza, mzee huyo kwa mkono
wake mwenyewe anategesha kisu chake kwenye
shingo la mke wa mtoto wake wa kumzaa
mwenyewe, huku akiwa anatetemeka wanamuimbia
wimbo wa ushujaa kumpa nguvu ya kutenda lile
jambo akapitisha kisu kwa nguvu akarudisha kwa
nguvu akafanya hivyo mara kadhaa hakika damu
nyingi sana ziliruka pale na zingine zikamfikia
mwilini mwake kwenye nguo..Alikuwa na wasiwasi
kwa lile ambalo alikuwa analifanya.
Ikatoka kauli nyingine ya kuse,ma sasa amtoe
sehemu za siri za Mama Sikitu kwa haraka bila
kuogopa na bila kuchelewa na bila kukosea, Mzee
huyo alikuwa kama ndondocha ambae alikuwa
anafuata kile alichokuwa akiambiwa, wakati sasa
Mama Sikitu tayari keshakuwa Maiti mzee alitoa
nyeti zake pamoja na vitu alivyoambiwa kuvitoa.
baada ya hapo akapewa nyama iliyotokana na
Mwanadamu huyo na kuambiwa.
"HII ITABIDI UONDOKE NAYO NA UMPATIE
MWANAO AILE AKISHAKULA HATOWEZA
KUKUSUMBUA TENA, KWANI NA YEYE ATAKUWA
MUHUSIKA WA HILI WEWE UMEUA YEYE KALA"".
Baada tya hapo aliondoka baada ya kujihakikishia
yuko vizuri katika mwili hakuna damu yeyote bila
kujua kuwa nyuma ya mgongo wake kuna damu
nyingi sana ambazo hakuziona. alifika nyumbani
anamkuta mtoto wake akimsubiri " Chito mwanangu
vipi mbona umehuzunika yani bado unanituhumu
kuwa nimemchukua mkeo".
Wakati anamkaribia harufu ya mwanamke ikamjia
maana alikuwa akishika nyeti za Mama Huyo kwa
fujo ili aweze kuzikata vyema 'huyu baba katoka
kwa mwanamke alafu hajaoga huyu uzee wote huu
anakuwa malaya hivi duu' Alimshuku baba yake
katoka kwa mwanamke kutokana na ile harufu
iliyokuja.
"Baba unatokea wapi sasa hivi?" Chito aliuliza
"Natokea maporini kuangalia mtego wangu na hiki
ndicho kitoweo cha leo mana tulikuwa wawili na
bwana Nyandu tumegawana huko huko". Chito
alipokea kisha akamuacha baba yake atangulie
ndani alishangaa sana kuona damu nyingi alafu
anatembea akiwa hajiamini, pia harufu ile ndio
inamshangaza sana " Baba kuna mgeni kafika hapa
leo alikuwa anatuulizia sisi"
"Mgeni gani huyo?" "Mwenyekiti kutokan kijiji cha
Kalulu alikuja kufuatilia swala la mtoto wa mzee
UWESU mkwe wangu wanamhitaji mtoto wao
wamuone NYAMALI yaani mke wangu sasa sijui
baba utawaeleza nini hapo mana ushanitia
mashakani kabisa na wanatusubili kwa bwana
MASANJA mana hili jambo limefika kwake na
hatujui kamueleza nini huko kwa hiyo kajiandae
alafu tuende huko"
Ghafla mzee Mambo sasa anadondoka chini na
kuzimia.
Taarifa ya mzee KELEBU iliwafanya kuwa na amani
sana pale kijijini kwani hali ya binti Lyoto iliweza
kuwa salama kabisa, afya yake ilikuwa nzuri baada
ya kupata huduma kutoka kwenye miti ile
aliyokwenda kuichukua kijana BAMUZI mfalme
ambae anatarajiwa kukaa. Mzee huyo alimshauri
Mzee Ngololo kuwa aitishe mkutano wa wanakijiji
wote wa CHAMLO ili kuweza kuelezana baadhi ya
mambo yenye faida katika kile kijiji kwani tabia ya
wanakijiji hao kukataa kujitolea kumsaidia mfalme
kutafuta dawa si nzuri kabisa.
Mzee Ngololo alimuita bwana Mwalami na
kumuelza kitu "Bwana wewe nakupa siri ambayo
niliiweka kwa muda mrefu pia niliona kuitoa
mapema inaweza kuzua utata kwa mambo mawili
kwanza siri yenyewe tulipata taarifa ambayo sina
uhakika nayo kuwa "Mfumo wanataka kuubadilisha
hawataki tena kutawala kwa nja ya ufalme wanataka
kuwa na mwenyekiti ambae atachaguliwa kwa sifa
watakazoleta, pia wakatoa tamko kuwa tupeleke
majina ya vijiji ambavyo vinaongozwa kwa ufalme,
sasa jambo gumu kuwa hapa kijijini watu wanaishi
kwa amani lakini huu mfumo utakuja kumaliza watu,
pili wanasema hawataki kuamini mambo haya ya
mizimu tunayotaka sisi wanataka kuishi kawaida tu
bwana wewe".
"Mbona habari mpya hiyo, imetoka wapi?" aliuliza
bwana Mwalami. " Kiongozi wangu wa habari ndie
alifuata hizo taarifa wakati anatembea kijiji na kijiji
ili kujua yanayojili na kutuletea na hivyo kabahatika
kapitia kijiji cha KALULU kinavyoitwa kpo mbali sana
na mimi sijawahi kufika sasa kesho nadhani
atakuwa anarejea katika moja ya safari zake sasa
atatueleza zaidi kwani nadhani atakuwa huko akipita
kijiji kila kijiji kupata taarifa".
"Basi tusubiri nini cha kufanya baada ya yeye kurudi,
nitajua nini nikushauli lakini mkuu usisahau kuwa
kuna safari ya kwenda mpoloni kuhani msiba wa
kijana yule aliyemsaidia Bamuzi". "Hilo usijali
itapangwa safari kubwa lakini kwanza tumalize hali
ya huyu malkia baada ya hapo tukimkabidhi basi
tutakwenda"
Upande wa binti Naomi akiwa na mama yake
alimueleza kuhusiana na kijana ambae katokea
kumpenda sana kutoka moyoni na anashindwa
kuzuia hisia zake pindi akimkumbuka " Mama kuna
kijana alikuja juzi hapa yani mzuriii huyo,
nimempenda sana mama yani hata kwa kitu
chochote naomba ufanye ili nimpate huyo kijana".
mama yake alimuangalia sana Naomi akaona jinsi
gani anavyoteseka kimapenzi, alimuonea huruma
sana mwanae na mzazi siku zote hapendi kuona
kiumbe alichokitunza tumboni kwa muda mrefu
kinalalamika kwa jambo ambalo linawezekana.
"Mwanangu ebu niambie jina lake unalifahamu?' "
Mama nimelisahau kabisa japo aliniambiaga".
"Sawa ngoja keshokutwa nakwenda kwa Bwana
Ukelele naamini tutafanikiwa sana kwa hilo. Hatimae
siku zilikwenda na keshokutwa ikafika wakafunga
safari ya kwenda kijiji cha MPOLONI, walipofika
hadi kwenye nyumba hiyo ya mzee Ukelele
walimkuta yeye mwenyewe.
walimueleza shida yake na kwa kuwa huwa alikuwa
anakuja sana Mama Naomi ilikuwa rahisi
kukubaliwa 'Mzee huyu mwanangu ana shida na
kumpata mwanaume ambae anampenda sana sasa
naomba umsaidie".
"Naomi unamfahamu jina la huyo mwanaume?" "
Hapana"
"Haya chukua hiki kitu sema kisirisiri alafu taja kwa
sifa zake zote kama jina humjui na itakuwa rahisi
mimi kumjua na mkifika kwenu haitochukua siku
nyingi atakuja hapo." waliondoka wakiwa na imani
kuwa watasaidiwa na mwanaume huyo atakuja
kulealiko Naomi. wakati wao wanaondoka ndipo
Katunje na Mwaija walikuwa shambani ndipo
wakafika wakiwa wamechoka sana.
Mzee huyo alianza kufanya kazi ile lakini
anashangaa kuona Katunje analalamika mkono kuwa
dawa yake inambana kuonyesha kuna hatari fulani,
mzee ukelele akamuuliza " Kijana samahani isije
nakuumiza wewe unamjua NAOMI siku uliyekwenda
Chamlo ulishaonana nae?".
"Ndio babaaa nilikutana nae na ndie ambae
alinipeleka kwa mzee Mwalami..."
"Tobaaaaaaaaa........kumbe ndie wewe anayekuhitaji
huyu mama mpuuzi kweli alafu mjukuu wangu abaki
na nani shenzi " akavurugavuruga mitego yote
ambayo aliweka ili kumfanya mwanaume huyo
kwenda kumfuata Naomi na kumbe alikuwa Katunje
ambae kwa sasa ni mchumba wa Mwaija.
Baada ya siku kupita Mwaija alitamani kwenda
kupajua nyumbani kwa Katunje ambako alimtajia
kuwa ni SHISHIMO "Sawa siku moja tutakwenda
kwani hata mimi nimepakumbuka nyumbani sana ".
Walifurahi sana hasa Mwaija kumpata mwanaume
ambae hakutarajia kama atakuja kumpa raha na
amani moyoni mwake..............
 
SEHEMU YA ISHIRINI NA MOJA.............21
Endelea..............
.................Mzee UKELELE aliamua kuacha kabisa
kuifanya kazi ile ya Mama yake NAOMI aliyekuja
kwa ajili ya kumganya kijana ambae anamhitaji
Naomi basi aweze kurudi ndani ya kijiji cha
CHAMLO. "Kwani vipi babu kuna jambo gani kwani
lililotokea?"
Aliuliza KATUNJE
"Hapana kwani nilitaka kufanya jambo ambalo
lingetutenganisha kati ya sisi na wewe" Mzee huyo
alisema kumuambia kijana Katunje. Jambo hilo
lilifanya kijana huyo kuwa na maswali mengi sana
ambayo hayakuwa na majibu kamili kwenye kichwa
chake. "Sasa babu hapo sijaelewa kuwa kutengana
kwa namna gani yani mimi na nyinyi?"
Katunje hakuwa na amani kwani alikuwa na shauku
ya kujua nini ambacho alikuwa anamaanisha Mzee
huyo. Lakini japo na juhudi zake za kutaka kujua
kile ambacho kipo nyuma ya pazia lakini mzee huyo
alikuwa mgumu kumueleza kiundani zaidi nini
ambacho wale wageni yani mama Naomi na Naomi
mwenyewe walikuwa na shida gani. Katunje na
Mwaija walitoka na kumuacha peke yake mzee huyo
akiendelea na shughuli zake za utengenezaji wa
dawa na mambo yake mengine.
" Mwaija najua bado hatujaanza kujuana vyema
lakini mapenzi yetu unayaonaje?. Aliuliza Katunje
huku akimkodolea macho kwa makini kana kwamba
anataka kummeza kwa hamu iliyotokana na njaa ya
muda mrefu sana.
"Mh! mhhh weee Katunje kiukweli sijui hata
nikuambie nini kwani nakuona kuwa wewe pekee
ndie ambae umebakia katika msaada wangu ndani
ya maisha haya ya sasa na kuhusu mapenzi yangu
mimi na wewe najiona mwenye furaha sana Ehee! je
kwa upande wako".
Baada ya kueleza kipi ambacho moyo wake
unajisikia ndipo na yeye akrudisha swali hilo kwa
mwenzake ili ajue nini na yeye anachojisikia.
"Kweli pia nashukuru sana unajua kuwa bado tuna
safari ndefu sana kwenye mapenzi yetu, alafu mimi
kiukweli bado sina furaha kabisa maishani
mwangu". Katunje aliongea kuwa hana furaha
akimuambia Mwaija ambae alitarajia jibu zuri kama
alilompatia yeye wakati kaulizwa. "Niniii? huna
furaha kipi kinakufanya usiwe na furaha?" Muda huo
wako kjikoni wote wakiandaa chakula cha wakati
huo.
"Sina furaha kweli na sijui furaha yangu itarudi lini
tena kwani, nilikuja hapa kwa sababu ya kumtafuta
ndugu yangu aliyenipotea kwa muda mrefu sasa
yani sijui wapi ambako kaelekea, yani LYOTO
ananiumiza kichwa sana kiukweli mpaka sasa hivi".
"Mwaija nae aliona huruma sana ndipo akainuka na
kukunja upande wa kanga yake na kumfuta chozi
ambalo kijana Katunje alikuwa anamwaga kutoka
kwenye mboni mbili za macho yake. "Pole sana
sikujua kuwa hiko ndicho kinakufanya ukose furaha
ila ngoja tumuulize babu atatusaidia tu na wala
usijali kabisa"
Majira ya usiku kuingia Mwaija alianza kuhangaika
huku na kule akiyumbisha kichwa chake na
kumfanya Katunje aweze kuamka na kumuangalia,
alishtuka baada ya dawa ambayo ipokwenye mkono
wake maeneo ya msuli kumbana kuonyesha kama
kuna hatari kubwa sana iliyopo. Alimuangalia huku
akim shangaa kwa jinsi anavyohangaika huku na
kule.
" huyu si bure itakuwa ni ndoto hii ila inaweza kuwa
ndio ile ndoto ya kumfahamu nani ambae alihusika
na tukio la Lyoto ngoja nimuache kwanza" Aliongea
Katunje baada ya kuhisi kuwa kama ni ndoto basi
itakuwa ile ambayo alihitajika kuiota yeye kuhusiana
na kupotesa kwa Lyoto ila sasa anaiota huyu
Mwaija. Ghafla anashangaa ananyamaza na akatulia
kabisa na ndipo wote wakawa wamelala mpaka
asubuhi ya siku iliyofuata.
Asubuhi na mapema sana Mwaija alimsimulia yote
ambayo aliyaota kwenye ndoto ambayo yalikuwa ni
kama msaada mkubwa katika ile kazi ya kumtafuta
mtu wao.
"Basi tuende tumuelekeze babu inawezekana
akatusaidia kwani yeye mwenyewe alisema pindi
utakavyo ota ndoto hiyo hapo ndipo na sisi
tumuambie kila kitu". waliondoka kutoka kwenye
chumba chao na kumuendea mzee Ukelele ili
kumpa taarifa.
"Hodiii Babuuu, babuuuu " walimuita mpaka pale
alipofungua mlango
"Naam vijana wangu kuna tatizo lolote asubuhi hii?"
Aliuliza kwa shauku kwani ni mzee mwenye
tabasamu kwa muda wote ambao alikuwa nao.
"Ndio baba, usiku nimeiota ile ndoto yote ambayo
ulisema ikitokea tuje kukuambia" Mzee hakika
alianza kufurahi na akawaomba haraka sana waingie
ndani, kweli wote waliingia ndani na wakaanza
kumhadithia huku Katunje akiwa na hamu ya kumjua
nani huyo kwani ndoto haikutaja jina lolote japo
alikuwa na hisia juu ya mtu fulani.
"Sawa hiyo ndoto tayari kwani ilivyoelezwa na mimi
imenisaidia kujua wapi naanzia sasa Katunje
kachukue ile dawa ambayo ulienda kuchukua kule
msituni siku za nyuma".
Alienda kwa haraka sana na kurudi aliagizwa na
maji akachukua kisha vyote akavileta mbele ya
mzee Ukelele. Muda kadhaa alikuwa tayari
keshamaliza kazi yake ya kuiandaa dawa hiyo
muhimu sana kisha akaanza kumpa maelekezo juu
ya matumizi ya yale dawa.
"Sasa hapa naomba mnisikilize kwa makini kwanza
nataka kujua kijijini kwenu unakwenda lini?" Aliuliza
mzee Ukelele "Huko natarajia kwenda siku chache
baada ya kufanikisha kurudisha binti Lyoto". Katunje
akajibu
"Sawa hii dawa itakubidi uioge siku tano asubuhi na
usiku siku tatu ukiwa KILIMALONDO siku moja
ukimtafuta huyo binti siku moja wakati unapanga
kwenda kwenu hapo utamaliza kila kitu".
katunje alipatwa na bumbuwazi kwa jambo lile.
"Sasa babu inakuwaje kwenye swala la huyu mtu
ambae anahusika kwa upotevu wa binti lyoto?"
"Kuhusu hao usijali ndio maana nikakuambia wewe
kaoge kwa hizo siku tatu mimi nitajua pia
nitakukuta hukohuko maana najua itakuwa kazi
ngumu sana nitakuja na kuhakikisha huyo aliyemuua
binti yangu Mama Mwaija basi atanitambua lakini
kumbuka hata kama ukafika usiku wa muda gani
lazima uioge hii dawa pia naomba mzingatie yasije
kuwakuta mabaya kwani mtakuwa mnawindwa
kama nyinyi mnavyowawinda wao".
Walipanga safari ya kurudi tena hadi ndani ya kijiji
cha Kilimalondo ambako alitokea na mambo yote
yalianzia mpaka kumfanya awe pamoja na Mwaija.
Walifika usiku kama kawaida kutokana na umbali
uliopo. walifika kwenye nyumba ya kijana Katunje
lakini katunje anashangaa kuona mazingirz yako
tofauti sana na kawaida ambayo huwa kaizoea.
"Mwaija hapana hapapo salama kabisa hapa"
"Aaah mimi nimechoka nahitaji kwenda kulala"
Mwaija alikuwa kachoka sana lakini Katunje nafsi
yake inakataa kabisa kuingia mule ndani,
haikujulikana kuna nini ndani humo mpaka awe na
wasiwasi namna hivyo, kutokana na kuwepo kwa
mwanamke basi Katunje alikubali na wakaingia
ndani, walisafisha kidogo maeneo yao ya kujidai/
kulala kisha wakajitupa kitandani hiyo yote ilitokana
na uchovu walionao wa safari na kufanya Katunje
kusahau kabisa juu ya kuiandaa dawa na kuoga.
wakiwa usingizini Jogoo anawika kijana Katunje
anasikia sauti ambayo kama inamkumbusha jambo
fulani "''Kijanaaaa, onaaa niniiii unafanyaaaa onaaa
unampotezaaaaa Mwaija....umeshindwa kufuata
masharti.....".
Alikurupuka toka kitandani na akiangalia ubavu
wake wa kushoto ambako alilala Mwaija hayupo
kabisa. aliinuka akakumbuka na ile ndoto ya
asubuhi iliyomueleza kuwa umeshindwa kufuata
masharti.
"Mamaa yangu sijaoga ile dawa sasa Mwaija yuko
wapi jamani...Mwaijaaaaa"
Alikurupuka na kutoka nje ambapo mlango wenyewe
ulifunguliwa na haikujulikana nani ambae alikuwa
kaufungua. alitoka nje huku akiita lakini hakuna
ambae alikuwa anamsikia. Mwaija haonekani kabisa
machoni mwake. Akili iliyomtuma ni kurudi ndani
na kuchukua ile dawa na kwa kwa kulikuwa na maji
aliyaweka kwenye ndoo na kisha akachanganya huku
akiwa na wasiwasi kabisa kwani alikuwa
akitetemeka.
"Jamani mbona haya mambo yananikuta mimi tu"
Alienda chooni wakati anatoka nje anakutana na
mzee Udevu ambae alikuwa anamshangaa sana
kijana huyo kwani alipotea kwa muda kidogo tangu
atoke pale hakujulikana wapi ambapo alikwenda.
"Weee si Katunje weweee umerudi ulikuwa wapi?"
Aliuliza Bwana Udevu huku akimsogelea
"weee mzee komaaa tena usinijie ondoka mbele
yangu shetani wewe na mzee mwenzko KAUZIBE
tena mpe taarifa yani nawachukia nyinyi hamnijui
tu..." Alipandwa na jazba kubwa sana ukizingatia
hawa wazee wawili ndio anawatuhumu alafu
hapohapo mjukuu wa Mwaija kapotea kwa
mazingirz ya kutatanisha. "kijana nakuuliza kwa
upole unaniletea fyongooo unataka kujua nani
mbabe si ndio ngoja wewe mdogo sana ".aliondoka
na huku kijana katunje akaingia chooni na akawa
anajimwagia maji yote yale yenye dawa.
Alivyotoka anasikia sauti ikimuita
"Katunjeeeee ukom wapi jamaniiii?" Akajua fika
kuwa Mwaija karejea ilibidi na yeye afurahi na
kuacha ndoo chini na kumkimbilia kule alikosikia
sauti ya wito. Alimuona akiwa mlangoni akihaha
kumtafuta Katunje "Mwaijaa mimi hapa hunioni".
"Uko wapi Katunje nasikia sauti tuuu jamani"
Alilalamika kuwa yeye anamsikia sauti tu lakini
hamuoni kabisa
"Mwaija mimi mbele yako hunioni kweli Mwaija ebu
nitazame kwanza". Aliendelea kumsisitiza ili aweze
kumuona ukweli Katunje alimkaribia na akaanza
kumshika mkononi pale mlangoni kwao.
"Katunje nahisi kweli unanishika lakini hapa sikuoni
kabisa yani sikuoni mbona uko hivyo vipi jamani
Katunje "
"Mwaija macho yako yameharibika una maana kuwa
hunioni kweli?"
Katunje alianza kutoa chozi likisaidiana na Mwaija
ambae alijihisi mpweke bila kumuona Katunje
akimsikia sauti tu
"Katunje niamini angalia hii ni ndoo uliyotoka nayo
kuoga ina rangi nekundu na ulitoka kuioga ile dawa
si hii lakini wewe sikuoni jamani huniamini"
"Aaaaaah mamaaaa weee sasa nimekuaje mimi
mbona matatizo kila nilifanyalo jamani". Ghafla
ndipo KIMOLO akiwa katika doria yake ya kama
kawaida kumtafutia mzee binti wa kucheza nae kwa
siku hiyo kwani huwa ndio kawaida ya Mzee SWAI
kufanya hivyo, alipokaribia ndipo Katunje
alipomuambia Mwaija jambo.
"Mwaija kama kweli sionekani huyo anayekuja ana
kawaida ya kumtafutia mzee wake Swai wanawake
kama saizi yako sasa akija mimi nipo hapa ongea
nae".
Kweli alifika mpaka pale na akashangaa kumuona
binti mzuri sana katulia kwenye nyumba ya kijana
Katunje na wakati katunje mwenyewe yuko
pembeni.
"Eweee binti mzuri uliyependezwa na Swai wa
Kilimalondo, unaonekana kuwa mgeni na nyinyi
wageni ndio anawataka sana mbona uko peke
yako?"
Katunje alishangaa kuona kuwa yeye haonekani
mpaka anaulizwa Mwaija kwa nini yuko peke yake,
alijishika huku na kule ili ajue nini ambacho
kimemtokea mwilini mwake lakini haikufaa
chochote. " Namsubuli mchumba yangu anakuja"
Alijibu Mwaija.
"Mchumba yako yupo unayemsubili wewe sasa
jiandae twende kwa mzee Swai haraka sana utakula
kila ukitakacho mzee mwenye mali nyingi sana na
asiyejua kutumia nyinyi ndio watumiaji wake".
Katunje alishuhudia jinsi Kimolo anavyolazimisha
kumbeba Mchumba wake. Hakika alikasirika sana
ndipo akampiga ngumi nzito ambayo ilimpeleka
chini kama mzigo utupavyo chini kutoka umbali
mrefu.
Kimolo alishangaa kuwa ngumi inatokea wapi,
alisimama ili ajipange kama jemedari wamzee SWAI
apambane na mtu huyo, wakati upande wa Mwaija
nae alishangaa kuona jamaa kaanguka wakati
alishikwa mkono huku akilazimishwa kutoka pale
aliposimama.
"Mjingaaa wewe mwanamke unadiriki kunipiga mimi
kabisa unanifahamu mimi eeeh?" Swali lake
halikujibiwa na Mwaija bali ilijibiwa na ngumi
nyingine nzito ambayo ilimpelekea kumtoa damu
nyingi puani na mdomoni. Mwaija alishangaa sana
akaamini kweli Katunje yupo ila haonekani kwa hali
ya kawaida kabisa.Hapo ilimbidi bwana Kimolo na
nguvu zake atafute njia ya kukimbilia ili kuokoa
maisha yake huku akiwa na wasiwasi mkubwa sana.
Huku nyuma Kijana Katunje alimsogelea Mwaija na
kumshika mkono ambae Mwaija kwa upande wake
aliona tu mikono yake ikinyanyuka lakini mtu
mwenyewe haonekani.
"Mwaija basi inanibidi na wewe inakubidi ukubaliane
na hali yangu niliyokuwa nayo kwa sasa hakuna jinsi
nahisi kujitambua kwa upande ungine labda inaweza
kuwa sababu ya mimi kumrudisha lyoto wangu"
Mwaija alifuta chozi kisha akamkubalia ndipo
walipoingia ndani.
Mzee udevu ile taarifa akaipeleka kwa mzee
Kauzibe ambae hakuwa na hili wala lile. " Kauzibe
unayajua haya ya asubuhi hii?"
"Yapi hayoo tena ?" aliuliza bwana Kauzibe
"Leo asubuhi wakati naelekea kwa yule ndugu yangu
niliyekuambia jana kuwa ni mgonjwa si nikapita
pale kwa kijana yule Katunje!"
"Eheeee"
"Huwezi kuamini kijana kwanza karudi maana
nimemuona kwa macho yangu haya mawili" Mze
Kauzibe akasimama kwanza "Unasema yaliyo ya
kweli kuwa karudi huyu kijana?"
"ndio kabisaaa"
"Ahsante maana nilikuwa nimembakisha mpuuzi
huyu kwani ananifanya niishi kwa hofu hapa unajua
pia kuwa uongozi wa Ufalme unaanza kufa sasa
ndio maana nataka kuondoa hawa vikwazo vyangu
nije kuwa mwenyekiti"
Aliongea bwana Kauzibe kumpa taarifa kuwa
uongozi wa ufalme unaenda kufa na sasa unaingia
mfumo mpya wa mwenyekiti ambae atachaguliwa
na wanakijiji wake husika.
"Lakini si hayop tu ya kuja yeye kuwa makubwa
sana kuna makubwa aliyoyafanya na ndio
yaliyonileta hapa kwako mpaka sasa"
"yapi tena hayooo?"
"Yani yeye katutukana kwanza, pili anasema sis
ndio wabaya wa hapa kijijini sisi anatuchukia tena
zaidi ya maelezo mpaka nimeogopa kwenda
kumuangalia ndugu yangu yani sijui anachojivunia
kitu gani"
kauzibe alikunja sura na kumshika mkono na
kumeleza kuwa atamtumia vijana ambao
watamfanyia kazi kubwa sana na kumuangamiza
kama alivyoangamia binti Lyoto.
Mzee swai anashangaa kumuona kijana wake
mdomo umevimba damu zinamtoka ilimbidi
amuulize kwanza "Bwana wee nini kimekutokea
huko na mbona hujarudi na mwali yeyote leo?"
"Mfalme wangu bwana nilichokutana na huko wee
acha tu, kuna mtu anapiga lakini haonekani kabisa"
walicheka sana baada ya ksikia hayo maneno
"Sijawahi kuona siku ya maajabu kama ya leo sasa
ngoja siwezi kuacha dharau wakati kila mwanakijiji
hapa anajua kuwa mimi ikifika siku ninayotamani
kumpata mwanamke namchukua na hawakatai sasa
nani ambae kakukataza huyo?".
Walishtushwa baada ya kumuona mzee Kauzibe
kafika pale, "Mkuu nina shida sana naomba vijana
wako wakamuadhibu Kijana Katunje maana
katutukana sana mimi na bwana Udevu".
"Hapo umekuja pazuri sana kinachotakiwa fuatana
na hawa vijana sita wanatosha kumshikisha adabu
na inatakiwa mukimkamata nendeni mbele za watu
alafu mumpige mpaka kifo chake alafu mimi
nitakuja kutoa tamko"
Waliondoka kumfuata bwana Katunje.
Wakati huo katunje tayari yuko ndani "Mwwaija
naomba utulie humu ndani na usitoke mimi hunioni
ila mimi nakuona nitakuwa mlinzi kwako muda
wote, nakuja mara moja".
"Katunje ni bora ukaenda kuniweka nyumbani kabisa
siwezi kuishi hivi mimi" ghafla mlango unafunguliwa
kwa nguvu na vijana hao waliotumwa kazi na bwana
Swai.
"Katunje toka njeee haraka sana tena sana, " katunje
alimficha yule mwanamke chini ya kitanda kisha
yeye akatafuta upenyo kati yao kwa kuamini kuwa
haonekani akapita hadi nje. wale walikagua ndani
humo na hapakuwa na kitu mmoja alipata wazo
kuwa wachome ile nyumba ili kumdhoofisha kijana
katunje.
Kabla hawajatekeleza ilisikika mtu akianguka chini
huku zikimtoka damu kichwani, " jamani mwenzetu
kaanguka chini, kuna kitu kimempiga hapa"
Mmoja wa viajana waliongea lakini haikuchukua
dakika kadhaa, ilisikika kitu kikianguka kwenye
kichwa cha mtu """nduuuu""" na yeye akadondoka
chini na palepale marehemu. hawakuchukua muda
walikimbizana huku wakiwa hawajui wapi ambako
wanakimbilia.
Mzee Kauzibe alikimbia zaidi ya vijana wote
kuogopa yale yaliyowatokea wale alio waona kwa
macho yake wakianguka chini. Lakini mwingine
aliyekamatwa baada ya kupigwa akapewa ujumbe "
nakuomba uende kwa mzee Swai akamueleze kuwa
aachane na kuwaharibu watoto wa kike wa hapa".
kijana huyo alisimama huku akiyumbayumba na
kukimbia zake kwenda kutoa taarifa kama
alivyoambiwa.
MAPATO anaingia kijiji cha BWAWANI kutoka kijiji
cha SHISHIMO ambako alikwenda kwa shida yake
ya kumhitaji bwana Mambo Sasa. Aliona vyema
sana endapo akirudi kwanza nyumbani kujipanga
baada ya kupata taarifa tofauti na ile aliyotarajia.
Alipofika ndani ya kijiji chake alikutana na rafiki
yake bwana SIKUJUA walioachana nae kwa muda
kadhaa wakati yeye nasafiri kwenda Shishimo "
Bwana karibu sana sijui habari za huko utokako
hawajambo?" Sikujua aliuliza baada ya kumkaribisha
Mapato pale kwake.
Mapato alianza kufika kwa rafiki yake kabla hata ya
kufika kwake mwenyewe. "Nashukuru sana na pia
nimefika salama lakini sasa kitu ambacho
nilikiendea kule sikukipata kwani nimekuta
mkanganyiko mkubwa sana". Sikujua alishtuka
kidogo ndipo akainuka na akaenda kufunga mlango
wake ili kuwa na usalama kabisa.
"Sijaelewa ehee mkanganyiko gani huo ambao
uliukuta?"
"Unakumbuka kuwa kule bwawani aliyehitajika ni
bwana Mambo sasa kama tulivyotamka kule ile
siku"
"ndio nakumbuka vyema sana " sikujua alijibu
"Sasa, nimefika kule nikapokelewa na mwenyekiti
ambae alinikaribisha vyema sana baada ya
kumuelezea kuwa nakuja kumuangalia ndugu yangu,
lakini sasa kumbe yule mzee Mambo sasa sio jina
lake bwana wewe"
Sikujua alishtuka tena
"Unasema kuwa....!"
"Ndio hivyo jina lake bwana CHITO" lakini baba
yake anaitwa Mambo Sasa.
Sikujua alikohoa kidogo kisha akaanza kusema
"koh!...koh!...koh!..hapo sasa ndipo nakuja kusema
kuwa kesi ambayo inatukabili kwa SUSU anasema
kuwa sasa anaanza kuwa na kumbukumbu baada ya
kumpiga kipindi kile kumbukumbu inamrejea...sas
a......" Akiwa anafikilia
"Sasas nini tena....?"
"Mapato tunachotakiwa kukifanya ni kuwa kuweka
uwazi kuwa Mambo sasa sio jina lake anaitwa Chito
na ndie ambae alimfanyia unyama Mama Mengi
kwa kumchoma kisu na akamtolosha mwanae sikitu
ili ajulikane kuwa kakamatwa lakini ni mchezo wa
kufanya mambo yake huku akijificha kivuli cha
kupotelewa na mwanae, pia ndie ambae kampiga
SUSU kwa kuwa alimpaga kama ushahidi lakini
susu akasema ukweli mbele ya mwenyekiti
akaamua kumfanyia hayo"
Mapato alibaki kuduwaa...
"yani wee jamaa wewe una mbinu nzuri sana ehee
baada ya hapo"
aliuliza mapato
"Baada ya hapo itatumwa taarifa ya kuitwa yeye
akija si ndio njia ya kupelekwa bwawani
kumaliziwa".
Hapo umecheza vizuri sana sasa ngoja nikafike
nyumbani kwanza". Alifika nyumbani kwake huku
akiwa na bashasha kutokana na ushauri mzuri wa
rafiki yake.
Alipofika kwa mkewe hakika alipokelewa kwa
furaha sana na kuandaiiwa kama mume kisha baada
ya hapo walipumzika baada ya kula chakula. " Haya
mke wangu habari za kuwaacha huku?" aliuliza
bwana Mapato
"Huku salama kabisa yani sijui za huko na
biashara?".
"Mke wangu hakika kule nilifanikiwa kupata,
shamba ambalo tayari lipo kwangu lakini kilichobaki
ni mimi kwenda kulifanyia kazi na lipo kijiji cha
Shishimo kule, haya hakuna jipya tangu nitoke hapa"
Aliuliza
"Mme wangu mwenyekiti alitoa tamko akiwa na
bwana MANUALI kuhusiana na SUSU"
"Ehee...koh!"
"walisema kipindi cha nyuma ajitokeze mwenyewe
aliyemfanyia kitendo kile susu lakini hakujitokeza
kabisa "
"ndio nakumbuka na jinsi wanakijiji wa hapa walivyo
wabaya yani wamemuua mama Mengi hakujitokeza
sembuse huyu kijana kweli!" Mapato alidakia
"Sasa wamesema juzi kuwa SUSU hali yake nzuri
kumbukumbu anazo na nadhani siku hazijatajwa lini
kuwa atasema rasmi ni nani ambae alimfanyia hivyo
vitendo kwa hiyo tunamsubiri hapa ili akimtaja
wanakijiji tuishi kwa amani hapa kwetu". Alimaliza
Mke wa Mapato na kumuacha mapato akiwa hoi
hajielewi,
"Nashukuru sana sasa ngoja niende kwa bwana
Sikujua ili nikamsalimie kwanza si unajua nina
hamu nae rafiki yangu"
Alinyanyuka na kuondoka huku akitembea kwa
mwendo mkali sana ili afike mapema.
Alimkuta rafiki yake huyo akiwa anasuka mkeka
ndipo akamuomba waondoke mapema kwenda kwa
mwenyekiti ambae ataweza kuwasaidia na kujificha
kwa mambp waliyoyafanya.
waliondoka hadi kwa mwenyekiti bwana SEMENI.
"Mwenyekiti tumekuja hapa bwana tuna
mazungumzo ya hapa na pale kwa ajili ya
maendeleo."
"Karibuni alafu sijakuona kwa muda hapa bwana
Mapato ulienda wapi?"
"Mizunguko ambayo nayo imenileta hadi hapa
kwako"
Walianza mazungumzo watatu hao. "Mh! kweli hilo
jambo ni kweli kijana susu anasema anaweza
kuongea ukweli pindi siku akitaka lakini ajataja lini
kasema akiwa tayari anakuja hapa na ataomba
aseme na wanakijiji ili aseme jambpo hilo"
"Sasa sisi tunamjua aliyemfanyia hivyo na
waliofanyiwa hivyo akiwemo mama Mengi"
Mwenyekiti alishtuka akakaa vizuri "Ehee yupi huyo?"
"Kwanza tunaomba ulinzi maana kuja kumsema mtu
hapa inatakiwa moyo ili kesho mtuhifadhi tukipata
taarifa zingine tuje kukuambia mwenyekiti"
Walijiwekea ulinzi kwanza kisha wakaendelea
kuongea kwani bwana Mapato alikuwa muongeaji
mkuu
"Muuaji na msababishaji wa yale yote ni mzee
Mambo sasa"
"Weeeeee....Naniii inawezekana vipi mzee
aliyepotelewa na mwanae na kama ni yeye sasa
nani ambae kamchukua mwanae?"
Aliuliza mwenyekiti kwao ilikuwa rahisi kwani
walishalijadili mapema sana
"Mwenyekiti hili swala nilikuwa nalijua tangu muda
sana, Mzee Mambo sasa alimtorosha mwanae
kipindi kile sikujua aligombana nae akaingilia SUSU,
sasa akaja na kesi nadhani unafahamu mpaka
akaitwa mzee yule, lakini susu alikuwa upande wa
kumtetea sikujua hilo swala likamuuma sana ndipo
akaona arudishe kisasi"
Mwenyekiti alikuwa makini kusikiliza
"Ehee nakusikiliza endelea"
"Sasa baada ya kushindwa kesi akaamua
kumtorosha mwanae kwenda kijijini kwao Shoshimo
alafu huku akaanza mambo yake yule mama Mengi
alimkuta siku moja akipanga njama za kumuua mtu,
mama yule akamsikia lakini akajishtua kitu
kilichomfanya bwana mambo sasa kumuona, Kama
unakumbuka akasema kuwa jioni namsema nani
ambae kampoteza lyoto..."
"Nakumbuka vyema sana"
"Eheeeeh! alienda kumuua shambani alikokuwa
anakata kuni kisha akarudi kwa haraka, haikutosha
lengo lake amuue mzee sikujua na susu watu wake
kwa kuwa huyu niko karibu nae ndipo akamfanikisha
bwana SUSU". Mwenyekiti aliamini kwa asilimia
zote.
"Ujue mwenyekiti kwa nini ili uamini" Mapato
aliendelea
"Ehee"
"Unamjua kwa jina gani yule mzee?" Mapato
alimuuliza sikujua
"Si jina lake hilo la Mzee Mambo sasa!" alijibu
mwenyekiti
"Aaaaaah ha! ha! ha! ha!...hapana, mwenyekiti
haitwi hilo jina kabisa" Mwenyekiti alishangaa zaidi
siku hiyo kwa kuwa habari anazopewa ni
motomoto.
"Lipi tena jamani mnanichanganya"
"Umeniuliza nilikuwa wapi, nilienda Shishimo
kufuatilia mambo yangu lakini ajabu sasa jina
ambalo nililikuta kule kwani nilifanikiwa kumuona
ndio kwake, anaitwa CHITO na nilimkuta siku hiyo
anataka kumkata baba yake panga bwana Mambo
sasa yeye anaitwa Chito".
Mwenyekiti ilibidi shtuke na kusikitika jinsi jamaa
alivyokuwa katili, lakini alionekana kama anafikilia
jambo fulani hivi kutokana na maelezo ya bwana
Mapato " Choitoooo...chitooooo".
"Vipi mwenyekiti?"
"Hili jina la Chito kama nalikumba hivi hebu
ngojaaa" Alikagua katika makarabasha yake na
kutoa daftari moja ambalo lina majina ya wageni
waliowahi kuja pale. kwa bahati alilikuta lile jina.
aliwapa wasome yale maelezo
JINA; KATUNJE
KUTOKA; Kilimalondo
SHIDA; Namtafuta ndugu yangu anaitwa CHITO
Hapo kila mmoja akawa kachanganyikiwa kuona
kuwa jina la bwana Chito kuna mtu alikuja
kumuulizia pale hivyo wakawa wanjiuliza huyu
bwana Katunje anakaa wapi?.
"Sasa hapa ndipo ninapojua kuna kitu kimejificha
kwa sababu huyu kijana tulimtimua kwa hofu ya
watu wageni kufanya uhalifu katika eneo letu bila
kujua kuwa nduguye ni bwana Chito ambae
tulimfahamu kuwa ni Mambo sasa"
Mwenyekiti alijiuliza.
Jambo la kufanya ni kumtafuta kwanza huyu kijana
KATUNJE ili tujue kuwa anajuana nae vipi huyu
muuaji.
"Lakini hapa kuna kijana alikuwa anakujaga kuuza
mbuzi alisema anatokea kijiji cha Kilimalondo sasa
siku akija tutambana ili atuambie kama yupo huyu
kijana".
Alisema bwana Mapato. Hapo ndipo wakatawanyika
na wakajihakikishia kuwa wamemkamata vyema
sana mwenyekiti na wao wataishi kwa raha kabisa
pale.
 
SEHEMU YA ISHIRINI NA MBILI 22
Endelea....................
..................Muda ambao mzee Mambo sasa
alidondoka na kuanguka chini, jambo ambalo bwana
Chito lilimshangaza sana iweje apewe taarifa alaf
ghafla kama ile adondoke chini na kupoteza
fahamu. Haikuweza kujulikana na siku zote damu
nzito kuliko maji, pia baba ni baba hata kama
kakufanyia nini atabaki kuwa mzazi wako tu hisia za
maumivu ya moyo zilimuingia na kumfanya afungue
mlango wa huruma hatimae akainama na kumbeba
baba yake kisha akauelekea mlango wa chumbani
kwa baba yake.
Ajabu ule mlango uligoma kabisa kufunguka mithili
wanafanya mashindano Chito anataka kuufungua
lakini ilionekana kama kuna mtu yumo ndani
anaukandamiza usifunguliwe mlango huo. Lakini
kwa hasira za bwana Chito ili kumuokoa baba yake
alimuachilia chini kwanza kisha akapiga hatua
kuelekea mwichi uliokaribu na mlabo wa nje,
alienda nao moja kwa moja hadi kwenye mlango
kisha akaupiga na ule mwichi ndipo ulipoachia,
alimbeba tena baba yake na kumpitisha chumbani
kwake.
Baada ya kuhakikisha kamuweka vyema,
anastaajabu kuona Moja ya pambo la mwanamke
kwenye kona ya chumba hiko, Wakati anatafuta
uwezekano wa kumsaidia baba yake aliweza
kuelekea ile bangili ambayo huwa inavaliwa zaidi
kwenye mkono. Alifanikiwa kuishika na akawa
anaiangalia kwa makini sana, alikumbuka jambo
"Baba Sikitu unajua kuwa mzee MANYENYE ni fundi
mzuri sana wa kutengeneza Mikufu na bangili za
mikononi?....nahitaji uninunulie ili nipendeze"
Jambo kubwa sana alilokumbuka kipindi anaiangalia
ile bangili ni pale alipokumbuka utani wa mama
Sikitu wakiwa kijiji cha BWAWANI,
"Mme wangu chooonde usiwaangalie wanawake wa
watu walivyopendeza ninunulie na mimi ili nipendeze
kama wao....". Hiyo siku ndipo akamuendea Mzee
Manyenye na akaweza kupata ile bangili.. Chito
alifura kwa hasira sana lile jambo ambalo
analishuhudia pale " Ina maana baba yangu unadiliki
kulala na mke wangu au kama hukulala nae hii ringi
imefikaje huku na wakati siku ya mwisho
nilimvalisha mimi mwenyewe...aiseee hapana
sijakuelewa bado"
Hakika bwana Chito alijawa na hasira ambazo
ilikuwa ngumu kuelezeka. Lakini aliachana na hayo
yote na kuanza kumpulizia baba yake ili apate
kuzinduka lakini huku akiangalia zaidi ile bangili ya
mkewe ambayo kaikuta kwenye chumba cha Baba
yake.
Baada ya masaa kadhaa Mzee mzima Mambo sasa
aliamka huku akishangaa yale mazingira ambayo
kawekwa pale alafu anamuona mtoto wake yuko
pale kitandani akiwa kasinzia. Aliinuka taratibu bila
yeye mwenyewe kufahamu alimuangalia mkononi
alikuwa na ile bangili, aliichukua kisha akaelekea
kwenye sanduku lake akachukua bangili ambayo
inafanana na ile ambayo Chito alikuwa nayo aliweza
kumbadilishia kisha akamlaza yeye sasa pale
kitandani, hakuishia hapo alichukua kaniki yake na
usinga wake.
"Nyamnyena Nyamnyena......Nyamnyena kulumbila
kulumbilolo, Kalilolisema kama lilombilo chito
kuliona alama cha mkewe, kalitafunaye nnyama
kulipingolo asahau kabisaaa". Mzee huyo alikuwa
akiyazungumza maneno ambayo alikuwa
anamaanisha kuwa anaomba mizimu ambayo huwa
wao wanaikubali sana kipindi chote pale
wanapokuwa na shida, Chito kaiona alama ya
mkewe hivyo anaogopa akaja kujua kila kitu na
yeye anampenda sana mwanae sasa anahitaji
asahau kila kitu pale alipo.
Muda wa jioni unaingia hapo ndipo Baba Sikitu
anaamka kutoka kwenye usingizi mzito alishtuka
anaona yuko kwenye kitanda cha baba yake
alishtuka hivyo alijiona mtu ambae hana adabu bila
kukumbuka aliingia mule ndani kwa sababu ipi.
Alielekea kwenye chumba chake huku akiwa na ile
bangili yake, kabla ya usiku anafika bwana
Mwenyekiti MASANJA akiwa ana haraka sana. Mzee
Mambo sasa alikuwa wa kwanza kumuona hivyo
alihitaji kuondoka nje na nyumba yake ili awe mbali
kabisa asiweze kuonana nae, " Mambo sasa
unaenda wapi bwana wakati mgeni wako nimekuja
hapa", Mbio zake hazikusaidia jambo kwani
alishaonekana na mwenyekiti huyo hakuwa na jinsi
aliamua kumsubiri ili amsikilize.
Masanja alifika pale na kuweza kusalimiana wa
kwanza bwana Masanja alimpelekea mkono lakini
bwana Mambo sasa alikataa katakata, " sema shida
yako nina kazi nataka kwenda kuifanya"
Alionekana kuwa na jazba bwana huyo, "Sawa lakini
haya mambo niliyokuja nayo yahitajika mimi na
wewe tukae chini ili tuyazungumze lakini ukiwa
kwenye hali hiyo sielewi nini una maanisha!"
Mwenyekiti alijitahidi kumuelewesha vizuri sana
Baba yake Chito.
"Nimekuambia hivi kama hauna cha kuongea
nitafute siku nyingine kwa sasa siwezi kukusikiliza"
Alionekana bwana Masanja kucheka kwanza kana
kwamba anastaajabu pia haamini kwa yale
anayoyaona. "Mzee unanifahamu mimi vyema,
unajua kuwa mimi kama serikali ambayo naweza
kukushtaki kwa kukataa maelezo yangu wakati
wewe na mtoto wako ndio yanawahusu". Ilimbidi
mwenyekiti atumie cheo chake baada ya ustaarabu
kushindikana.
"Kijana kuwa kiongozi hakuwezi kunitisha mimi au
kama unataka kutishana tuanze wewe bado mdogo
sana haya nakusikiliza sema "
"Taarifa kutoka kijiji cha KALULU kule ambako
mlikwenda kuoa wewe na mtoto wako, kwamba
alikuja mwenyekiti wa kijiji hiko sasa Mzee Uwesu
kama unavyomfahamu na anavyofahamika katoa
kauli kusema kama hamumpeleki mtoto wao yeye
atajua la kufanya lakini kwa ustaarabu aliokuwa nao
mwenyekiti huyo wakakaa kikao kujadili na
ikaonekana kuwa waje hadi hapa kuja kujua
maendeleo,".
Mzee Mambo sasa alishusha pumzi kwanza huku
akionekana kutafakari " Bwana waeleze kuwa mtoto
wao sisi tulimchukua huko kwa mahali kubwa tu
sasa sisi ndio tunajua jinsi gani ya kumtumia kama
kumla nyama au kumfanya nini tunajua sisi kikubwa
mwambie yeye ni mzima"
Jambo ambalo halikumuingia akili bwana Masanja
"Baba wewe ni mtu mzima kuniambia kumla nyama
sishangai kwani unajulikana kijiji kizima kuwa wewe
ni mwanga mkubwa tu ila sasa nakuomba kabla
yule mwenyekiti hajaondoka kesho mumlete
NYAMALI mtoto wao la sivyo nitakudhalilisha mzee
japo nakuheshimu".
Hali ya maelewano haikuwepo tena baina yao kwani
kila mmoja alikuwa anatupia maneno yake kwa
mwenzake ambayo yanaonekana kuvunjika kwa
amani kati yao. "Haaa haaaa! kijana utajisumbua
sana usijaribu kufuatilia mambo ya watu ebu yaache
pia mwenyekiti una tabia ya kuwakaribisha wageni
hapa bila sisi kujua sasa ukome kabisa la sivyo
nitakugeuza kinyago".
Mwenyekiti na yeye hakuwa mjingamjinga kama
mzee alivyomfikilia hakuogopa vitisho vya huyu
mzee kabisa aliendelea kumpa ukweli wake.
"Wewe Mzee nakuambiaje huniwezi, yani hata
hutamaniki kabisa hapa kijijini na yule mpumbavu
mwenzako, unadiliki kumla nyama mkeo wako
wewe mwenyewe wewe ni mtu au mnyama, na hili
swala nitakuja kumuambia Mtoto wako Chito, haya
angalia umemkimbiza mpaka Kijana ambae ni
mfanya kazi sana hapa kijijini kijana mdogo huko
aliko KATUNJE, hufai...."
Mzee Mambo sasa alianza kukasirika baada ya
kuona mwenyekiti anayoyasema yote yana ukweli
asilimia miamoja zote. "Kijana usiongee vitu
ambavyo huna uhakika navyo unajua nini kuhusiana
na mke wangu mjinga wewe"
Mwenyekiti alirudi wakati alikuwa anaondoka na
wakati huo huku ndani bwana Chito anatoka kwenye
usingizi mzito na anasikia sauti ya mwisho ya
bwana Masanja.
"Unadhani sijui siku nikimuona mwanao hakika
namueleza kama uongo unamfahamu mzee
UPENGO unamjua alikufanya nini yule mzee mpaka
sasa huna hata hamu kwenda kijiji chake tena
nimekumbuka ili kukomesha upuuzi wenu wa
kichawi ni kumleta mzee Upengo na kukuambieni
ukweli baada ya kuwapa taarifa wanakijiji na mimi
naenda kumueleza kila kitu Mwenyekiti hapo ndipo
akija mzee uwesu utakuja kujua....."
Mwenyekiti aliondoka zake na huku mzee Mambo
sasa alikuwa akijikuna kichwa baada ya
kukumbushiwa jina hatari sana la Mzee Upengo,
japo haijulikani mpaka sasa kuwa mzee Upengo
alimfanya nini Mzee Mambo sasa mpaka amuogope
kiasi kile.
Aliingia ndani huku akielekea kwenye chumba cha
Chito, wakati huo chito alivyohisi mzee wake
anakwenda alijifunika gubigubi na huku akiazima
usingizi wa ghafla baada ya kuanza kukoroma.
"Huyu umri nao unakwenda analala sana lakini
inabidi nimkomeshe kabisa bwana Masanja
anaweza kuharibu kila kitu, nampenda sana Chito
pamoja na ndugu yake japo sijui wapi yeye kafia
basi urithi wangu huyu ndie ataukamata...alafu
nilikabidhiwa nyama yayaaaaaa ngoja niandae
haraka sana".
Alielekea jikoni japo na uzee wake aliandaa nyama
ya binaadamu tena mkwewe yani mke wa Mwanae
Mama SIKITU aliiandaa vyema na baada ya
maandalizi hayo aliweza kupika chakula kizuri sana,
Muda wa usiku uliingia ndipo Chito alitoka kutoka
usingizini na kufika pale alipoitwa na baba yake.
"Chito unalala sana mwanangu haya mimi nishakula
chakula changu wewe kula mimi naenda kwanza
huku kwa baba yako mdogo narejea sasa hivi?".
Chito alikaa tayari na kuangalia ile mboga jinsi
ilivyonona, akiangalia ugali jinsi unavyoita kwa ajili
ya kuliwa. Alinawa maji kisha akamega tonge la
kwanza alipamba mchuzi tu kisha akala,tonge la pili
akachukua kipande cha nyma lakini akakumbuka
maneno ambayo muda fulani walikuwa wakiongea
baba na Mwenyekiti....
"......Unamuua mkeo alafu unamla nyama.....Unamla
nyama....unamla nyamaa...nyamaaaa....wewe si
mtuuu bali ni mnyamaa....mnyamaaa....kama
unabisha ....Mzee UPENGO.....upengooooo huna
hata hamu kwenda kijijini kwake pumbavu
weeeee........"
Alivyoyakumbuka hayo wakati yeye kajilaza
chumbani aliacha kwanza lile tonge, kisha akajiuliza
"Ina maana nikimpata mzee huyu Mzee UPENGO
nitajua kila kitu na atanisaidia hata kumjua mke
wangu yuko wapi....lakini inaonesha safari ya baba
kwenda kwa rafiki yake yule si ya amani ngoja
nikamueleze Mwenyekiti ajipange na kama
kuondoka kwanza kijijini basi aondoke kwa muda ".
Ndipo akauacha ule ugali na ile nyama japo
alilamba mchuzi kwenye tonge ile ya kwanza,
alinyanyuka na kwenda hadi kwa Mwenyekiti, lakini
kwa bahati mbaya hakumkuta alimkuta mkewe
ambae alipata kumuuliza "Naaam mke wa
mwenyekiti habari yako?'
"Salama sijui za kwenu huko?" aliuliza mke wa
mwenyekiti
"Sisi salama sijui mzee Masanja nimemkuta?"
"Hapa katoka aliniaga alikuja kwenu alivyorudi tu,
akamsindikiza mgeni wake aliyekaja jana sasa
mpaka sasa ajarudi bado labda kapitia kwa watu
wengine kwenye mambo yao ya kubadilisha uongozi
wao". Mzee Chito hakuwa na hamu tena zaidi
aliondoka na kuanza kumtafuta mwenyekiti lakini
hakufanikiwa kumuona. Kwa upande wa Mambo
sasa na rafiki yake waliyoyaongea yalionekana
vitendo vikifanyika.
"Yani maliza kabisa yani nyonga kabisa kazana zaidi
usimpe pumzi ya kupumua kabisa" Aliyasema rafiki
wa Mzee huyo wakati huo bwana Mambo sasa
akinyonga moja ya kitambaa cheusi aina ya kaniki
kwa nguvu zake zote mpaka pale alipoambiwa
basi.
"Walichukua maji na kuyaweka kwenye chombo
kisha akapitisha usinga wake kama mara tatu kisha
ikaonekana sura ya mtu akiwa kwenye baiskeli
kisha anaanguka chini huku akishikilia shingo yake,
mwishowe ana pupapupa kama kuku anayechinjwa
na hatimae anafariki dunia palepale na baiskeli
ikiwa pembeni.
"Hapa sasa tumemaliza kazi hawezi kutusumbua
sasa aende kwa huyo mzee UPENGO, yani
wanamuita nyuki aje kutuamisha makazi uliona
wapi...sasa mambo sasa nenda nyumbani ila
hakikisha mwanao anakula ile nyama uliyoambiwa
na wakubwa wa Nyamnyena sawa?" aliulizwa "
sawaaaa"
Mzee huyo aliondoka kwa mwendo ambao
aliufahamu yeye mwenyewe kwa bahati nzuri bwana
Chito baada ya kushindwa kumpata mwenyekiti
alirudi nyumbani akipiga tafakari za hapa na pale
atamjuaje huyo mzee na atafikaje huko ili akamalize
kazi zake na yeye maana kachoka.
Aliinuka na kuchukua vile vyombo na kwenda kutupa
vilivyomo ndani kama mboga na ugali, mbali kidogo
kisha akaosha.
"Chito habari mwanangu unaendeleaje vipi
umeshakula chakula ?" Chito hakuwa na wasiwasi
wa kujibu "Baba yani sikuamini kama chakula
ulipika wewe mana ile mboga tamu sana yani
sijapata kuona kabisa " Mzee Mambo sasa
alivyopumbazwa akaamini kama kweli mwanae kala
ile nyama maana ndio lengo kuu kuila ile nyama.
Asubuhi na mapema vilio vikasikika kuwa
Mwenyekiti kafariki, hakika jambo ambal;o kila
mmoja alisikitika kupotea kwa mwenyekiti baada ya
kumkuta akiwa kafa kabisa.
Maiti waliikuta ikiwa njiani njia ya kuelekea kijiji cha
KALULU na mke wa Mwenyekiti aliona kuwa hakuna
mwingine ambae kamuua mumewe isipokuwa
Mwenyekiti mwenzake kutoka kijiji cha Kalulu kwani
ndie ambae alimsindikiza wakati anaondoka pale
nyumbani kwake. Kwa hiyo baada ya maziko kesi
iliyopo ni kuwa Kiongozi wa Kalulu kamuua kiongozi
wa Shishimo na hakuonekana kabisa Mzee Mambo
sasa na rafiki yake. Kuna msemo watu husema
(Kuna binti mmoja ambae alikuwa akiishi na bibi
yake. Siku moja Binti huyo alimuuliza bibi yakje
kuwa "Bibi hivi kumloga mtu kwa uchawi na
ukishamloga usijulikane unafanyaje?....
Lilikuwa swali la binti huyo kumuuliza bibi yake
sikiliza jibu la bibi kwa mjukuu alimjibu nini
"Ngoja jua lizame" Ilikuwa siku ya kwanza ilipofika
jioni, binti akamueleza bibi yake " Bibi jua limezama
tayari" lakini bibi neno lake kwa mjukuu wake
lilikuwa lilelile kuwa " Ngoja jua lizame" baada ya
siku tatu nyumba ya jirani walianza kutoelewana
ndipo kauli za hapa na pale walitoleana kauli nzito
ilikuwa """Yani nitakuua kwa chochote kile"""" hapo
ndipo bibi akamuita mjukuu wake na akamuambia "
Kila siku nilikuwa nakuambia ngoja jua lizame sasa
leo limezama" mjukuu akauliza "Mbona mchana
bado..." Bibi huyo akamfunulia ufafanuzi wote kuwa
" Unaposikia watu wanagombana kama hao, na sisi
tukienda kumuua kwa uchawi huyo anayeambiwa
atauliwa na mwenzake hakika sisi hatutoonekan
sawa na usiku kuwa na kiza hatutoonekana nini
tunafanya zaidi ya yule aliyetamka neno
tulilolitekeleza sisi....."
Haya maneno ya juu ni mfano wa kile alichokifanya
mzee Mambo sasa na rafiki yake kumuua
Mwenyekiti lakini anayekuja kujulikana na
kuonekana kama muuaji ni Mwenyekiti wa Kalulu.
Siku moja Chito akiwa na nia ya kwenda kijiji cha
Kalulu kwenda kumuita kiongozi wa kule kutokana
na ile kesi hakutaka kwenda hivi hivi alimuita baba
yake na kumuambia mambo fulani.
"Baba, ujue mimi nakuamini sana wewe kuliko mtu
mwingine hapa"
Mzee huyo aliona kuwa mtoto wake kweli kala
nyama ya mkewe na inamfanya asahau kila kitu
"Mwanangu kweli kabisa"
"Lakini baba kuna mzee mmoja mchawi sana tena
simpendi kiukweli nimemsikia wakimsifia kuwa
mzuri anasaidia yani natamani nimuue ili sifa upewe
wewe baba yangu"
"Anaitwa nani huyo kwani" Aliuliza mzee huyo bila
kujua kama anategwa
"Anaitwa naniiiiii ehee anaitwa UPENGO....upeng
oooo"
Jina hilo lilikuwa kama linazibua masikio yake pindi
likitajwa
"Huyo kumbe hata mimi namsikiaga" " Sasa anakaa
wapi, huyu mzee bhana mana kila sifa anachukua
yeye alafu wewe hupewi sifa wakati unayafanya
mazuri hapa"
"Mwanagu ila si mtu wa kumchezea kabisa anaishi
kijiji kimoja hivi kinaitwa MIPINGONI huyu mtu
kweli ni mchawi wa kutupiliwa mbali"
"Ahaaa kumbe sasa si unajua mimi nimechaguliwa
kwenda kijiji cha Kalulu nikirudi tu nakuja na
tunapanga jinsi ya kummaliza huyu mzee sawa
baba!".
Bwana Chito alimdanganya baba yake kutokana na
udhaifu ambao huwa anamjua kuwa anaudhaifu gani
na akapata jina la sahihi la mahali ambapo anaishi
huyo mzee.
BAMUZI alionekana akiwa na LYOTO huku Bamuzi
akimshika Lyoto begani na kumtembeza kwenye
uwanja ambao ulikuwa maalumu kwa ajili ya
mazoezi ya kurusha mishale kwa vijana ambao
wanafundishwa mapigano. Hakika walionekana
kupendezwa na kila mmoja akiwa na furaha kubwa
sana. Lyoto alikuwa na kumbukumbu chache sana
kutokana na msukumo wa maji na kusafirishwa
umbali mrefu sana, walikuwa wanaenda lakini Lyoto
alisimama na kumuangalia kwa makini sana kijana
Bamuzi.
"Mke wangu najua huwezi kunijua vyema kwa sasa
mimi ni mumeo na utanijua zaidi endapo dawa
mwilini mwako zikifanya kazi." Alimtoa wasiwasi
binti aliyeonekana kuwa mzuri sana pale kijijini
Chamlo zaidi ya Mrembo NAOMI. Wakati
wanacheka na kufurahi huku pembeni wakiwa
wanawake wale ambao wanamhudumia kama
malkia wa pale kwani siku chache tu zijazo hawa
wanawekwa kuwa Viongozi rasmi.
Naomi aliona wivu sana baada ya kumuona Bamuzi
akila penzi zito lenye bashasha ndani yake
lisilokuwa na uchafu wa hasidi na fitina, penzi
ambalo wazungu wanatumia neno quality yani safi
zaidi. Naomi binti wa mama Naomi aliona wivu
uliojaa chuki na ndipo akaelekea nyumbani kwake
kwa mama yake kama kawaida. (Mtoto kwa Mama)
.
"Mama hivi tangu tuende kwa mzee Ukelele mpaka
leo bado haonekani atakuwa kafanya kweli yule
maana naona Bamuzi na kile kisichana kake
wananifanyia makusudi"
Mama huyo alimuangalia sana mwanae huku
akimuonea huruma sana ndipo akamueleza kuwa
"Mwanangu usijali yule mzee namuamini sana ".
Naomi aliondoka na kukutna na wanawake wenzake
ambao walikuwa na mawazo kama ya kwake "Eti
hivi huyu mwanamke ambae kamchukua Bamuzi
akajifanya eti sisi hatuoni yani eheee..."
"Naomi yani mimi nahisi kuwa siku moja tuongee
na yule msichana ambae kaka yake ZWELI
alitangazwa kuwa kafa baada ya kwenda kule
msituni najua atatusaidia sana".
"Mh mwenzangu kweli una mawazo makubwa sana
sikufahamu hilo tutakalolifanya ni kuwa
tunamdanganya kuhusu kaka yake Zweli kuwa
kauliwa ili afanywe sadaka huko, ili wapate ile dawa
ndio maana waliporudi wakatudanganya "
Naomi aliusuka uongo uliofanana na ukweli ili
kuwakosanisha Bamuzi pamoja na Lyoto.
"Yaaaa hapo najua atakasirika na atafanya kile
ambacho tunakitaka eti...kwanza najua leo atakuwa
kwake twende kwanza"
Waliondoka kuelekea kwenye familia ya bwana
Zweli kijana aliyejitolea kufa kwa ajili ya Kiongozi
wake apate ile dawa ya kumtibia mchumba yake.
Walipofika walimkuta ndipo wakamuomba mama
yake Zweli yani huyo binti ili watoke nae kwa muda.
"MWANA, tumekuita hapa kukuambia yale
usiyoyajua!" Naomi aliongea.
"yapi hayo?"
"Kwanza unamuonaje yule mwanamke pale
unapomtumikia kama hana mikono na miguu".
"Paleee yule mwanamke kiukweli anapendwa sana
na Bamuzi tena mpaka raha sana alafu anaongea
vizuri sio mkorofi".
Naomi aliona njia ya kuingilia hapa itakuwa ngiumu
lakini hakukata tamaa alianza kuongea
"Sasa unajua kuwa kaka yako Zweli aliuliwa na
Bamuzi ili afanywe sadaka ya kupata dawa ambayo
itaenda kumtibia yule mwanamke ambae
mnamtumikia yani mimi mpaka nikaanza kulia sana
baada ya kujua hilo yani". Mwana alianza kutoa
chozi na huku wakiendelea kumjaza sumu mpaka
akatamani kupasuka kwa hasira alizo nazo.
"Sasa naomba utusikilize kwanza, tunachotaka
ikiwezekana umuue yule mwanamke na yeye kama
alivyosababisha kaka yako kuuliwa sawa?"
"Sawa Naomi pia nashukuru kwa ushauri wako na
leo jioni naenda kwenye zamu yangu ya kukaa nae,
alafu hapo nifanya ukatili ambao sikuwahi kuufanya
katika maisha yangu......"
Walijua kwa njia ile wamefanikisha kutoa mapenzi
ya wawili hawa.
Wakati huo Mzee MANUALI na Mzee KELEBU
wakiongozwa na mzee NGOLOLO hawa walipanga
safari tayari ya kwenda kijiji cha MPOLONI wakiwa
na lengo la kutoa pole ya msiba kwa kijana yule
aliyejitokeza ba kumsaidia kijana Bamuzi kupata
dawa. Safari ilipangwa wazee hawa watatu pamoja
na kijana Bamuzi waelekee wakiwa na vijana wa
ulinzi wa njiani.
Bamuzi kabla hata ya kwenda alimuita yule
mwanamke aliyejulikana kwa jina Mwana "Mwana
Nakuacha na huyu mke wangu na unajua hali yake
bado haijatengemaa sasa nakuomba sana umtunze
nirudi nikute hali yake iko nzuri au iko
vilenilivyoacha lakini isirudi nyuma nadhani
unanifahamu".
Maneno hayo ya nadhani unanifahamu
yalimuongezea uchungu sana binti huyo na kufikilia
kuwa kweli Bamuzi kamuua kaka yake kwa ajili ya
huyu mwanamke anayepewa amlinde.
Safari ilianza kama kawaida wakielekea kwa Mzee
UKELELE ndani ya Kijiji cha MPOLONI kwa lile
lengo la kwenda kutoa pole ya msiba wa kijana
wake. Huku nyuma sasa binti Mwana anajiuliza kwa
jinsi gani ataweza kumdhuru Lyoto aliyekuwa
hafahamu chochote. aliamua kumpikia kwanza uji
ambao alihitajika kuweka dawa ambayo
ingemuwezesha kuwa na nguvu kama kawaida.
Lakini ajabu alichanganya na vitu mbavyo alikuwa
anavifahamu yeye mwenyewe kwa lengo kuu la
kumuangamiza. alimpelekea, Lyoto lakini hata kabla
hajampatia alidondoka na uji wote ukamwagika na
kwa purukushani ya kujiokoa ulimfikia mikononi na
kumuunguza kiasi Mwana. Hivyo alishindwa
kumuandalia mwingine na hatua yake ya
kumuangamiza kwa njia hiyo ikagonga mwamba.
Muda wa kumpeleka mazoezini alitumia nguvu
kumsukuma mpaka pale lyoto akadondoka na
akawa analalama kwa maumivu, mlinzi mmoja
aliayaona hayo yote ndipo alipomuendea na
kumuonya " Mwana tabia yako imebadilika kwani
huna huruma na mke wa mfalme wako, unadhani
hasira zako zitakupeleka wapi?"
"Hapana kabisa hawa wauwaji wamemuua kaka
yangu kwa ajili ya huyu kinyago sasa ni bora na
yeye afe"
Wakati huo sasa binti huyo alishika mtii mkubwa
ambao alidhamilia kumpiga na kumuua kabisa
apotee duniani, wakati huo Naomi na mwenzake
wakisubiria majibu.
"Hapana haya ubayoyafanya naamini kaka yako huko
aliko atakuwa anaumia sana kwani yeye alijitoa kwa
ajili ya kumsaidia mfalme wako na akajitpoa
muhanga, lakini hayo maneno uliyopandikiziwa na
wenye chuki utakuja kujutia pale tu ukiufahamu
ukweli na wao wakakucheka kwa akili potofu uliyo
nayo"
Mlinzi huyo alitumia kauli nyepesi na nzuri sana ili
kumuelimisha binti huyo aliyekuwa akimsogelea
Lyoto ili ammalize wakati huo lyoto hana nguvu
alikuwa anatoa machozi tu.
"Mwanaaaa achaaa nitakupiga na mkuki kabla hata
hujamgusa huyo mwanamke pia nakuonya usipige
hatua hata moja kumsogelea hufai kabisa na
nakuahidi kukulipoti pindi Bamuzi akifika mnyama
mkubwa wewe unasikiliza utumbo wa watu wasiojua
hata majina yao yana manisha nini tokaaaaa......."
Binti huyo alipigwa na butwaa ndipo mlinzi huyo
alimkamata na kwenda kumuweka ndani ya selo ya
wale watia vurugu na akamuita mwanamke
mwingine kwa ajili ya kuendelea na huduma kwa
Lyoto.
Wazee hao walifika hadi kwa mzee Ukelele na
walishukuru sana baada ya kumkuta akiwa pale
kwake. Walikaribishwa na Mzee huyo alijawa na
furaha kubwa sana baada ya kutembelewa na mkuu
wa kijiji cha cha Chamlo hakika kwake ulikuwa ni
ujio mkubwa sana yani.
"Jamani karibuni sana hapa ndio nyumbani na
elezeni shida yeyote mimi kama nitaiweza
nitawasaidia."
"Kwanza tunashukuru kama unavyoona ujio huu si
wa kukaa sana tunarudi leoleo hata kama usiku
mfano wa baba kaja huku kule mtoto ata lala na
njaaa".
Maneno ya mzee Manuali hayo yaliwafanya kucheka
wote kwa pamoja.
"Sasa Bwana Ukelele hapa tumekuja kutoa pole
kwanza " Mzee ukelele alishangaa
"Pole gani tena jamani mbona sielewi"
"Kuna kijana ambae ulimtuma aje pale nyumbani
kwangu na nimuelekeze kwenye ule msitu sasa
alikutana na huyu kijana wa mfalme bwana Bamuzi
sasa wakati wanarudi kwa bahati mbaya
hawakumuona kwa nyuma ndio maana tukajua
yaliyotokea kule atakuwa kakamatwa, kilichotufanya
tuje huku kutokana na msaada wake kumsaidia
huyu kijana ndio maana tukaja kutoa pole...."
Mzee huyo alifikilia jambo na kujisemea ndani ya
nafsi yake 'Hawa itakuwa wanamtafuta yule kijana
Katunje na nikiwapa taarifa kamili watamfanya
mtoto wangu MWAIJA kukosa mtu wakuishi nae
baada ya mimi kufariki hapana tena afadhali
walivyoondoka'. Yalikuwa ni mafikilio ya mzee huyo.
"Mzee mbona huongei?" aliuliza Mfalme
"Itakuwa anafikilia maumivu ya kufiwa unajua kweli
inauma sana mfalme wetu" Aliongezea Mzee
KELEBU. Baada ya dakika kadhaa ndipo mzee
Ukelele akaona la kusema
"Jamani mnanikumbusha niliyokwisha yasahau,
kwani taarifa nilizipata hata kabla hamjaja, kwani
kweli kaliwa kabisa na pia sasa hivi nimepoa kabisa
msijali na nawashukuru kwa kuja kunipa pole."
Waliagana kwa pamoja kisha wale wazee pamoja
na Bamuzi waliondoka kurudi kijiji cha Chamlo
kuendelea na mabo mengine muhimu ya
maendeleo.
 
SEHEMU YA ISHIRINI NA TATU......23
Endelea..................
............. Bwana Sikujua na Mapato walikutana
baada ya Mapato kuwa na wasiwasi mkubwa sana
wa maisha yake kwani alimfuata jamaa yake huyo ili
kapate kumueleza kitu muhimu sana ambacho
alihisi kinamtatiza, lakini hata bwana Sikujua nae
alijiuliza kipi ambacho kinamsikitisha bwana
Mapato aliishia kumtazama tu kwani hakujua nini
amsaidie
"Bwana sikujua kuna tatizo hapa ambalo kiukweli
nahisi maisha yangu yanaelekea kuwa mwisho"
Alisema bwana Mapato,
"Ehee kivipi tena maana hata ulivyokuja ulionekana
kuwa na jambo ndio maana hata mimi umeniona
nikiwa na wasiwasi sana".
"Kiukweli usiku nimelala lakini nikiwa usingizini
niliota ndoto mbaya sana kabisa"
Alisema bwana Mapato huku akishika tama. "Yani
usiniambie bwana weee ilikuwaje hiyo ndoto?"
"Yani nilikuwa natembea barabarani, sasa nikamkuta
Sikitu..."
"Sikitu tena kwenye ndoto eheee....!"
"Sasa....baada ya kuonana na huyu binti akanijia
karibu alafu akaniambia na wewe nitakuua kwa
mkono wangu mimi mwenyewe kama nilivyomuua
rafiki yako Sikujua...."
Hapo bwana sikujua hakuamini alitamani kukimbia
kabisa pale alipo "Aaaah hakuna bwana sitaki
kabisa swala hilo maana haiwezekani mtu aliyekufa
hawezi kunielezea mimi kuwa kaniua bwana....''
Alilalama sana bwana sikujua huku akitokwa na
jasho la ghafla maana swala la kuambiwa kuwa
Mapato atauliwa kama alivyouliwa yeye lilikuwa
swala gumu sana kwake kukubaliana na hilo.
"Hapa cha kufanya si kupaniki maana hapakuwa na
swala la kuzunguka sana na kulaumiana zaidi ya
hapo ni kuweza kujua nini tunafanya ili kujua
majawabu yake".
Alinywea kabisa bwana Sikujua na akakaa chini huku
akihemwa na mwili wake ukitokwa na jasho.
waliongozana wote kwa pamoja lakini bwana
Mapato akaona kuna sababu ambayo inawezekana
inapelekea yeye kuota zile ndoto za ajabu ajabu
"Lakini bwana sikujua unalionaje swala hili la
kumpata bwana Chito maana nahisi ndio sababu ya
kutokea haya"
"Alafu inawezekana kuwa na ukweli kabisa"
"Unajua kwa nini inatubidi kumtafuta huyu kijana
anayejulikana kwa jina la KATUNJE alafu mwingine
aelekee kijiji cha Shishimo, sasa itakubidi wewe
uende huko kijiji cha Kilimalondo alafu mimi niende
kule kwa Chito na inatubidi tufanye haraka sana na
hili sio swala la kumueleza mtu yeyote kabisa hata
mwenyekiti". "Sasa kwa nini tusimshilikishe
mwenyekiti maana kwa jambo kama hili tufanye
huku tukijificha kwenye mgongo wa mwenyekiti".
Mapato aliona sasa ni swala ambalo lipo na
linahitajika kufanyika,
Wakati wapo njiani walikutana na bwana Manuali
akiwa na Susu, wakiwa wanaongea mambo ambayo
hayakujulikana kwani walikuwa wanaongea kwa
sauti ya chini na ilikuwa inaonekana wanaelekea njia
ya mzee manyenye. Walijiuliza kwa nini na
wanaelekea kufanya nini kule.
"Mapato unahisi, kuwa watakuwa wanaelekea wapi?"
aliuliza sikujua
"Mh! hata mimi sifahamu kabisa, alafu kwani mbona
kimya sana si alisema kuwa siku kadhaa anasema
wale ambao wamemkamata na wakamsababishia
yale mambo sasa mbona kimya mpaka sasa"
"Inawezekana mana lile swala ambalo tumekwenda
kuliongea kwa mwenyekiti limebana kabisa njia zote
sasa hapa tufanye kweli nenda Kilimalondo mimi
naelekea Shishimo sawa!".
safari ambayo iliandaliwa kwa upande wa bwana
Sikujua ilikuwa na madhumuni ya kwenda
kuhakikisha kuwa wanampata kijana Katunje na
bwana Mapato alirudi tena ndani ya kijiji cha
Shishimo ili kuhakikisha anafanikisha pale ambapo
alipaacha.
Kwanza kabla ya yote waliamua kwenda kwa
mwenyekiti ili kumueleza kuhusiana na safari yao
hiyo ina dhamira gani kwao na hata kijiji chao cha
Bwawani.
"Mwenyekiti nakuomba sana kuna jambo ambalo
tunahitaji msaada wako kwetu"
Sikujua alisema kumuambia mwenyekiti
"Ehee lipi hilo ambalo mnahitaji niwasaidie jamani".
"Yani hapa tumeona kujitolea kwenda kuhakikisha
bwana Chito ambae anajulikana kwa jina la Mambo
sasa nakwenda kuhakikisha kumleta hapa na huyu
mwenzangu atahitajika kwenda kijiji cha Kilimalondo
kwa ajili ya kumuona bwana Katunje na
tutakapokuja hapa tunawaleta ili waje kujibia
mashitaka yao".
Mwenyekiti aliwaza kwa muda kidogo alafu akavuta
pumzi ndefu kisha akashusha alafu akawaangalia na
kuwaeleza kile ambacho anakihisi kama ni kizuri
kutokana na maelezo yao.
"Sasa kwanza nashukuru sana kwani sikufikilia kama
mtatokea watu kama nyinyi na kutaka kusaidia
kutokomeza matatizo kama haya kwangu hakuna
wasiwasi kinachotakiwa tuwaeleze wanakijiji alafu
tuwaeleze...."
"....Aaaaahaaa hapanaaa kabisa utaaribu kabisa
endapo ukiwaambia wanakijiji "
"Kwa nini wakati ni jambo zuri...." alishangaa
mwenyekiti
"ndio kwa sababu jua kiuwa miongoni mwa
wanakijiji haohao wapo ambao ni wako pamoja na
bwana huyu sasa akipata taarifa hiyo watakwenda
kumpa na atakimbia"
Mwenyekiti aliwakubali sana kwa hatua moja hadi
nyingine kutokana na maneno ambayo walikuwa
wanaongea.
Hatimae walikubaliana na wakapewa kiasi cha fedha
kwa ajili ya kujikimu ndani ya safari yao.
Kwa upande wa bwana Sikujua siku ya pili yake
alifika ndani ya kijiji cha Kilimalondo mzee huyu ana
sifa moja ambayo huwa anayo, kwanza huwa ni
mcheshi sana pia mjanja kupiliza, Lakini ni mtu
ambae hana huruma kabisa pindi pale unapomkera
kwenye mambo ambayo anahisi kuwa yatamharibia
maisha yake kama tulivyoona mzee Mambo sasa
kipindi yupo bwawani aligombana nae hakuishia
hapo akamteka kiakili kijana susu na kumfanya
apindue ushahidi na akafanikiwa pia akasababisha
matatizo kwa binti Sikitu, baada ya kumbaka na
kumtupa porini, hakuishia hapo alisababisha mauti
kwa mama Mengi kwa kuficha zile siri ambazo
alikuwa nazo mama huyo.
Hapa sasa anaagizwa na rafiki yake kwenda
kuhakikisha uwepo wa kijana mmoja Katunje.
Alikuta kijiji kipo kimya kabisa hapakuwa na
patashika za hapa na pale aliweza kushangaa
kabisa mana si kawaida pindi unapokwenda kijiji
chochote lazima uhisi uwepo wa watu lakini hapo
ilikuwa tofauti kabisa. 'Ina maana hapa kijijini
hapana watu au sijafika kabisa'
Wakati huo anaonekana kijana Katunje akitoka
kwenye nyumba yake hapo ndipo anakutana na
bwana Sikujua lakini sikujua alikuwa anashangaa tu
pindi anapouona mlango umefunguliwa na
kurudishwa bila kumuona mwenyewe. 'Mh! hapa
panaonekana kuwa na hatari mana uchawi njenje
kabisa haya mlango kufunguliwa na unafungwa bila
mtu kuonekana haya tangu lini'
Alipata kujiuliza maswali baada ya kuona ile hali.
Katunje hakuwa na habari kabisa na mgeni huyo
maana hali aliyokuwa nayo ilizidi kumpa wasiwasi
sana alielekea kwa njia ya kwenda kwa mzee
Kauzibe, alitembea moja kwa moja maana alikuwa
na lengo moja tu alifika na kwa bahati nzuri aliweza
kumkuta akiwa na mzee udevu ndipo katunje
alinyemelea na kukaa pembeni yao akiwasikiliza
nini wanachokiongea.
"Sasa, unadhani tunafanyaje maana tangu juzi kile
kipigo haki ya nani sijui hata nifanye nini"
"Lakini sijajua kuwa huyu kijana anatumia nini
maana si kwa hali ile na naamini atatumia njia
nyingi sana kufanya yale anayoyataka">
"Sawa lakini, hivi nilisikia kipindi kile kuwa kuna
binti ambae alikuja nae na wewe ndie ulikuwa
mganga wake ukamtibu mpaka akapona sasa
sijajua mmegombana wapi yani"
Maneno hayo aliyaongea bwana Udevu kumuuliza
bwana Kauzibe. "ni kweli lakini bwana ilikuwa ni
ajali kubwa sana kwanza si unamjua bwana Swai
anapenda vibinti kama umri wa yule na mimi ndie
alinipa nafasi ya kumtafutia ndio maana nikajitahidi
sana kumfanyia matibabu yote mpaka akapona kwa
lengo la baadae nimpelekee bwana Swai...."
"Eheeee ikawaje......?"
"Daaah ndugu yangu siku nilivyogundua kuwa
wanaishi polini ndipo na mimi nikaangaika
kupatafuta sana hatimae nikapafahamu ndipo
nikatafuta njia ya kuingia pale jambo zuri lilikuwa ni
pale ambapo Katunje alitoka hayo maeneo na mimi
nikaenda kule......alinigundua kuwa naenda kwa nia
mbaya ndipo tukaanza kukimbizana mpaka anafika
kwenye lile korongo la maji daaah akaangukia mule
na akafa kabisa...."
Hayo maneno ambayo alikuwa anayaongea bwana
Kauzibe alijimwaga huku akiwa hafahamu kuwa
bwana Katunje anayasikia yote na alikuwa na hasira
sana kuzidi mpaka.
"Alafu mtu kama yule inabidi ushike ile sehemu
ambayo anaitegemea kwa Katunje kumzibidi ni
jambo dogfo sana tunamkamata yule binti anayeishi
nae alafu atajitokeza tu...."
Mala wanahisi pumzi zikihema kwa kasi maeneo
yale waliyokuwepo "Mh! mbona kama kuna mtu
mwingine karibu yetu hapa" "kweli au....."
kabla hata ajamalizia aliipata ngumi ya uso na
palepale akawashika kwa pamoja na kuanza
kuwashikisha adabu huku akiwaomba waeleze wapi
wamemtupa binti LYOTO maana yeye ndio maisha
yake yatakuwa vyema akimuona binti huyo tofauti
na hapo hapakuwa na njia nyingine.
wakiwa katika harakati hizo huku nyumbani
anaonekana bwana Sikujua akiodika kwenye nyumba
ile ambayo alikuwa na wasiwasi nayo pale mwanzo.
"...hodiiiii....hodiiiiiiii wenyeweee"
"Kaaribuuuuu....."
Sauti ya kike ilisikika na ndipo akatokea mwaija,
hakika alishangaa sana baada ya kumuona mgeni
ambae hamfahamu kabisa pale, "karibu nikusaidie
nini mgeni?"
"Ahsante sijui hapa ndipo kwa bwana Katunje?"
Sikujua aliuliza ili apate uhakika kama si pale basi
aelekezwe na huyohuyo.
"Ndio nikusaidie nini....." Mwaija aliuliza huku
akionyesha dalili za kutaka kuingia ndani na kufunga
mlango "Kwanza mimi nimekuja kutoa taarifa kubwa
muhimu sana akija mwambie kaka yake anamtafuta
anayeitwa CHITO na akitaka kumpata aje anitafute
mimi kwenye kijiji cha BWAWANI kule ambako
alikuja kwa mara ya kwanza aniulizie mimi naitwa
mzee Sikujua akinipata hata ndugu yake
atampata....."
Baada ya kutoa taarifa hiyo mzee huyo aliondoka
kuanza kutafuta njia ya kwenda kwao Bwawani.
Aliamini kabisa baada ya kumpa taarifa ile basi njia
rahisi sana yeye kumpata kwani jinsi anavyompenda
kaka yake hatakuwa na ujanja.
kweli kijana Katunje baada ya kuwashikisha adabu
wale wazee na haikujulikana kawafanya nini huko
waliko alirudi nyumbani na kawaida yake ni kupiga
mluzi wa aina yake ili mwaija afahamu kuwa katunje
anarejea na yeye mwaija hutoka nje na kusimama
akisubiria kukumbatiwa kwani hamuoni zaidi ya
kuhisi kuwa kashikwa na mtu na maongezi tu basi.
Baada ya kuhakikisha kuwa ametulia ilimbidi
Mwaija autue mzigo na kumuambia Katunje yale
yote ambayo kaagizwa aseme kwake.
"Nina maswali kabla sijakupa ujumbe wako"
Alisema Mwaija "Haya niulize na nitakujibu pia
kabla ya hayo nina hoja kwanza nataka kukuambia"
"Hapana mimi ndio wa kwanza ngoja nikuulize
ndipo utaongea hoja yako" walikubaliana na ndipo
katunje akawa tayari kujibu kwa kile ambacho
atakuwa analielewa.
"Wewe huko kwenu baba na mama yako wazima?"
"Nilimuacha baba yangu pamoja na kaka yangu
akiwa na mkewe,"
"Sasa hivi wako wapi hao uliowaacha....?"
"Kwa sasa sijui kabisa kwani nilikuwa wa kwanza
kabisa kuondoka pale baada ya baba yangu kumuua
mama yangu ili awe mchawi mkubwa pia niliondoka
mpaka sasa hivi japo niliwahi kupita maeneo ya
kijijini kwetu nikaulizia kaka yangu nikaambiwa
kaama na yeye miaka mingi iliyopita"
"Eheee ulifanya juhudi gani kumtafuta kaka
yako....na anaitwa nani huyo kaka yako?"
".....Mh! leo umeniamulia....kaka yangu anaitwa
CHITO na mkewe anaitwa Nyamali juhudi za
mwisho ziliishia kijiji cha Bwawani ambapo
mwenyekiti alinifukuza na nikaondoka ila ikawa ndio
chanzo cha kumpata binti Lyoto....ukweli ni stori
ndefu na ndie yeye aliyenikutanisha na wewe"
Katunje wakati anajibu maswali alionekana kama
kulia.
"Nyamaza basi kuna mzee mmoja hapa anaitwa
Sikuja alikuja hapa sijui kama unamfahamu?"
"Sikujuaaa.... nahisi sijui ndio yule ambae
nilimuacha hapo nje wakati mimi naelekea kwa
mzee Kauzibe....ila simfahamu kwa hilo jina hata
sura"
"Haya alikuja hapa akauliza hapa ndipo kwa katunje
nikamjibu ndio akasema kuwa akija muambie kuwa
anatafutwa na ndugu yake ndani ya kijiji cha
Bwawani na akija aulizie mtu anayeitwa Sikujua
hapo atampata ndugu yako Chito...."
hakika Katunje alishukuru sana baada ya kupata
taarifa hiyo huku akijisemea kuwa kumbe kaka
yangu ni mzima wa afya kabisa nilijua siku moja
tutakuja kuonana.
Alipewa nafasi ya kuongea na ili mwaija amsikilize.
"Sasa nilitaka uelekee nyumbani kwa baba yako
mimi niaelekea huko kijijini kisirisiri kwanza kusaka
kila kona ya kijiji kwani sasa hivi hawatoniona ndipo
nitamkuta kabisa kaka yangu kama yupo na kama
hayupo basi nitamuulizia huyo mzee ili aniambie.
Walipanga hivyo na mwaija akenda kwa baba yake
na huku kijana katunje akaondoka kuelekea kwa
mzee sikujua.
Upande wa mzee Mapato alishangaa sana baada ya
kufika kwa mwenyekiti Masanja anapewa taarifa ya
kifo chake alilalamika sana, lakini aliweza kupewa
nafasi ya kuishi pale kwa muda.
Chito na yeye kwa jana yake alijiandaa kuondoka
bila kusahau kabisa ile bangili ambayo aliamini
kama ni ile ya mkewe akiwa na lengo la kwenda
kwa mzee Upengo ili akamuulize baadhi ya vitu
fulani, hatimae safari ilianza na yeye akiwa pamoja
na baadhi ya vijana kadhaa ambao walifuatana ili
kwenda kwenye kijiji cha Kalulu, Chito alitembea
huku akiwa na mawazo ya kutaka kujua anaanzia
wapi kwenda kwa mzee huyo Upengo hali ya kuwa
hata klijiji cha Mipingoni hapafahamu anapitia wapi
na anaingilia wapi.
Ilimbidi aweze kuuliza kwa wale ambao wapo nae
safari moja kabla ya kuwauliza aliwataka wamalize
kwanza mada ambayo walikuwa wanaiongelea lakini
haikuwa nyingine zaidi ya ile ambayo wanaenda
nayo kule "Kiukweli hii si nzuri kabisa haiwezekani
kabisa mtu anakuja kukusalimia alafu ukizingatiia
kuwa wote ni marafiki huku tuendako tutajua la
kufanya mpaka aelewe">
Japo wapo kwenye harakati za kwenda huko lakini
bwana Chito alikumbuka kuwa huko ndiko iliko
familia ya Mama Sikitu sasa wakati anaelekea huko
itambidi awe makini sana akiwa huko.
"Jamani naombeni mnisikilize kwanza...."
aliwaomba wamsikilize "Haya mzee tunakusikiliza
kwani wewe ndio mkubwa wa hii safari"
"Ninaomba kuuliza huku tunakokwenda ninawezaje
kukipata kijiji cha mipingoni...." Baada ya kuuliza
lile swali kila mmoja wao alimuangalia mwenzake
kana kwamba wanaulizana baina yao. Ndipo kijana
mmoja akajitokeza na akamuelekeza kuwa
anapafahamu njia ambayo inapitia kwenda huko ila
kwa bahati mbaya hakuwahi kwenda kabisa, Lakini
kwa maneno hayo yalimpa faraja kubwa sana bwana
Chito akiwa na imani kuwa aliko mtu siku zote
hapotei atafanya kila juhudi ili afike huko.
"jamani nina jambo jingine nahitaji mnisaidie huku
tunakokwenda mnaweza kurudi peke yenu pindi
mkiachwa?"
Aliwauliza ili ajue kama akiwaacha na yeye
akaelekea huko je? wataweza kurudi salama wote?
"Huku mimi napajua vyema sana hatuwezi kupotea
kabisa yani na tutarudi wote kwa salama usalimini"
Safari ilizidi kuwa tamu kipindi kile jua sasa limetua
na kuuanza usiku taratibu, wakati wanakaribia usiku
huo na kijiji kwa mbali wanakiona kwani taa
zilikuwa zinaendelea kuonyesha njia ya pale walipo.
Kila mmoja alifurahi sana moyoni mwake baada ya
kupata matumaini ya kupajua pale wanapokwenda
kuwa wanakaribia, Waliona vyema wapumzike
mahala ili asubuhi waamkie kule kijijini kabisa.
Wazo alilitoa Mzee huyo Chito ambae alikuwa na
nia yake ya kutimiza nia yake ya kuwaacha na yeye
akatokomea kupatafuta huko kwa mzee Upengo.
Kila mmoja hakuwa na wasiwasi wa kutorokwa na
hata mawazo ya kuwa mmoja wao atakimbia pale.
Majira machache baada ya watu kulala fofofo
kabisa.
Chito hakusubiri hata sekunde japo na umri wake
wa uzee kumuanza japo sio sana lakini alikuwa na
nguvu zake, alinyanyuka na kuwaangalia wale wote
akahakikisha kuwa wamelala ndipo na yeye
akatafuta njia ya kuongoza katikati ya kijiji kile cha
Kalulu, ilikuwa mwendo kama wa nusu saa hivi
alifika na ukizingatia i usiku alafu hakuna
anayemfahamu zaidi kwa mzee Uwesu ambae ni
ngumu pia kwenda kwani bado hana uhakika wa
wao kumpokea bila kuulizwa mbona umekuja peke
yako mtoto wetu yuko wapi?
Aliamua kukatisha katikati ya kijiji na kwa jinsi
alivyo hakuwezekana kuonwa vyema na kujulikana
na yeyote yule.
Kwa bahati nzuri alimkuta mmoja wa kijana akiwa
na baiskeli akiwa anaelekea mahali lakini
alionekana kuhemwa kama anayetokea mbali sana.
"Ndugu samahani kwanza bwana...unaweza
kunisaidia kuna mahala napatafuta kijiji kimoja
kinaitwa Mipingoni sijui kama unapafahamu?"
Aliuliza Bwana Chito.
"Oooh! tena kwa bahati nzuri sana kuwa mimi
mwenyewe naelekea huko huko, kama hautojali
twende alafu nitakuacha huko ukifika" Mzee Chito
alihofia ile safari lakini alishukuru kwa kuwa safari
yake imefupishwa sana.
"Lakini hatutofika usiku huko?"
"Hapana yani mwendo mchache sana hapa tunafika
". Waliondoka kwa pamoja huku wakiendelea
kupashana habari na kuulizana baadhi ya maswali
ambayo ilionyesha ishara ya kuhitaji kujuana zaidi.
"Mimi naitwa Chito naishi pale Shishimo...."
"Sawa mimi naishi Chamlo, nafanya kazi kwenye
himaya ya mfalme Ngololo sasa nimekuja huku kwa
ajili ya kutafuta habari za nje ya kijiji chetu ili na sisi
tujulinde kwa kile kipindi cha shida kutokea....."
"Chamlo....nakisiki hiko kijiji kipo mbali sana yani"
Kwa bahati nzuri sana wanafika na Bwana Chito
aliweza kuachwa mahali na yule jamaa aliondoka
zake, Giza llilikuwa kubwa sana na watu walikuwa
wamelala na yeye ilimbidi atafute nyumba ambayo
ina sehemu safi ya kujihifadhi, Alianza kuupata
usingizi wa mang`amung`amu kutokana na
mazingira kwake kuwa mageni kabisa yalikuwa
hayaeleweki.
Upande wa bwana Mapato na yeye alipofika kwa
mke wa Masanja ambae ni marehemu na kupewa
ile habari hakika alijifanya kuchanganyikiwa sana,
alipewa nafasi ya kulala huku akiwa na nia ya
kwenda kwa Chito kwao ili akaongee na Chito
amshawishi arudi nyumbani Bwawani ili
amkutanishe na ndugu yake Katunje ambae mwenye
jukumu la kumleta ni Sikujua na kama tulivyosoma
kuwa Katun je alikubali kuja lakini ataanza
kuchunguza uwepo wa kaka yake na asipofanikisha
kumuona ndipo atakubali kumtafuta sikujua ili
aongee nae.
Mapato bila hata kujua usiku huohuo kwa kuwa
ndani ya kijiji cha Shishimo wengi walichangamka
sana hivyoi ngoma za kiasili zilikuwa kawaida kwa
kila siku.
Aliondoka usiku huo baada ya kuufunga mlango
wake taratibu ili asijulikane nini anafanya na wapi
anakwenda. Mzee Mambo sasa na rafiki yake
Nyandu usiku huohuo ujio wa bwana Mapato
waliupata na hawakutaka kuchelewa kwani
walimtambua ni mtu wa aina gani.
"Nyandu yule mtu ambae anatufuatilia anatoka
kwenye kile kijiji cha SONGAMBELE ambacho siku
hizi kinaitwa Bwawani kaja tena baada ya kumuacha
kwa mara ya kwanza...."
Alisema mzee Mambo sasa.
"Sasa yeye kaja kusema nini au kafuata nini na
kamfuata nani?"
"Ukweli kaja na gia ya kumfuata mwanagu ambae
kwa sasa hayupo, ingawaje anaweza kurudi kwa
siku mbili hizi karibuni...."
"Sawa inatakiwa kumkamata alafu atueleze kwa
makini sana kama kuna jambo anajivunia lazima
atupatie....kwanza nenda kamjaribu kama kakomaa"
Nyandu alimueleza mwenzake kuwa aende
kumjaribu kama kakomaa yani kama ana dawa za
kujikinga basi wajue ili waone wanamzibidi au
kumuendea vipi. Baba yake Chito alikwenda haraka
nyumbani kwake na kuweza kulifanya jambo, wakati
huohuo ndugu bwana Mapato hana hili wala lile
alikusanya miguu yake na kuielekeza kwenye njia
iendako kwa bwana Chito, alishangaa sana baada ya
kufika kwenye uwanja wa bwna Chito alikuta kuna
moshi mkubwa sana....ukifuka kutoka ndani, alijua
labda kuna moto unaunguza nyumba alikimbia
haraka hadi pale mlangoni laaa haulaaaaa!....bwana
chito haikuwa bahati yake alisikia vicheko vya
dharau sana
Haa ha ha haaaa.... Haa ha ha haahaaahaaa!..
baada ya hapo pakawa kimya aligeuka nyuma
kutaka kukimbia alichelewa alijikuta anaingia
kwenye mikono ya watu wenye uchu wa nyama.
Alikamatwa na kuingizwa ndani kwa mzee mambo
sasa akiwa hajitambui.
Mzee chito aliendelea kulala kwenye ile nyumba
kwa nje japo kwa mawenge mpaka pale usingizi
ulivyomchukua ki urahisi. Majira ya asubuhi wale
vijana ambao walikuwa pamoja na Chito
walipoamka wakajikuta wako wao bila kuwepo
mwenzao ambae ni mzee Chito. Kila mmoja
alishangaa kivyake na kujiuliza wapi kaelekea.
Mwishowe ile kauli ya kusema yeye kuwa anaulizia
kijiji cha jirani na kuuliza kama atawaacha peke yao
kama wataweza kurudi walihisi kuwa kaelekea huko.
Wao walisonga hadi kwa mwenyekiti wa kile kijiji.
walieleleza shida ambayo imetokea hadi mwisho na
kwa ustarabu tu mzee huyo aliwaelewa na
akawaomba warejeshe majibu kuwa ataomba kukaa
na wazee wa hapo kijijini na yeye atakuja kisha
watajilijadili ili ajulikane nani ambae alifanya hivyo,
pia akasisitiza kuwa waje kutoa taarifa kuwa mzee
uwesu sasa kaamua kuchukua maamuzi magumu
juu ya mwanae litakalompata yeyote kati yao baba
na mtoto atalijua yeye mwenyewe.
Wale vijana walirudi.
Bwana chito katika pitapita yake alifanikiwa
kupelekwa kwa mzee Upengo na akafanikiwa
kuonana nae ana kwa ana. Walikaa chini na chito
akaanza kueleza nini kafuata kule.
"Baba...samahani sana kuja kote huku nimepata
taarifa yako kuwa wewe mzuri sana katika swala la
kuwakomesha wachawi....sasa mimi baba yangu ni
mchawi sana na sitaki aendelee kufanya ile kazi
naomba unisaidie sana".
Mzee huyo aliangalia kwenye kibuyu chake na
kumuonyesha
"Baba yako ni huyu hapa?"
"Ndio huyuhuyu kabisa" Alijibu Chito
"Sasa huyu nilishamtia adabu kwani mwanzo
alikuwa mkali sana huyo anayeshirikiana nae
anaitwa Nyandu...nyandu alikuwa mwanafunzi wa
Baba yako yani baba yako alikuwa mkuu baada ya
mzimu wao wa Nyamnyena....sasa alikuwa
anamfundisha huyu rafiki yake..nilipata taarifa hiyo
miaka mingi iliyopita nikaja pale na kumdhibiti yani
kumfunga kwa miaka kadhaa asijihusishe na
mambo haya...ilisaidia na ndipo nikamtoa na
uchawi kabisa...lakini juhudi za rafiki yako hakika
zinamfanya kurudi kule japo hatakuwa kama
mwanzo....pia huyu baba yako ni mtu mzuri sana
ila tamaa na marafiki wanaomshauri vibaya"
Chito alishtuka sana lakini aliendelea kuuliza
maswali na kumsikiliza kwa makini.
"Sasa kuna siku nilikuuta hii bangili kwwnye chumba
cha baba na hii ni ya mke wangu...." aliitoa na
kumkabidhi
"Hapana kabisa...hii si ya mkeo kabisaaaa"
"Bali ni ya nani?"
"Hii ni bangili ya marehemu mama yako....na kwa
kukuhakikishia aliyetengeneza bangili hii ndio yule
ambae katengeneza bangili ya mkeo...na kuhusu
swala la mkeo sijajua mpaka uhakikishe unaipata
bangili ile ya mkeo ndipo unaweza kuifanyia kazi na
ukajua mkeo yuko wapi mpaka sasa hivi....Lakini
nikuulize swali?"
"Niulize baba ...."
"Hakuna siku ambayo ulikula nyama ambayo
mlikuwa wewe na ndugu yako....pamoja na baba
yako baada ya mama yenu kufa?" Chito alifikilia
kwa umakini ili apate kumbukumbu sahhi
"Nakumbuka sana kwani baada ya hiyo siku mbele
mtafaruku ulitokea pale baada ya mke wangu
kukataa kula"
"Safi... basi ile nyama mliyokula ilikuwa ni nyama ya
mtu ambae ni....."
'"Babaaa usiniambie kama nilikula nyama ya mama
yangu jamani.....mamaaaa nisamehee sikujua kama
nilikuwa nakula mwili wako mama...."
Aliendelea kulia sana kwa maumivu makali hata
kusikiliza tena hakuweza. Baada ya muda aliendelea
"Lazima nikuambie ukweli upate hasira ya kufanya
jambo la kumsaidia baba yako....Juzi napo nadhani
kuna nyama ulikula...hiyo sina uhakika sana kama ni
ya kawaida ila kachukue ile bangili ili....tukiipata ile
na hii ni rahisi kupata mambo mengi sana ambayo
yamejificha na ikiwezekana kuwa kufutilia mbali
kabisa kwa mambo haya..."
"Sasa naomba unisaidie kuwa tukiachana na mke
wangu naomba unieleze kuhusu mtoto wangu na
ndugu yangu katunje".
"Mtoto wako anaitwa nani.....na kapotelea kijiji
gani" Upengo aliuliza.
"Alipotelea kijiji cha BWAWANI, majira ya jioni
wakati sisi tulikwenda kwa mzee Mapato na kisha
tukapitia kwa manyenye baada ya kurudi
hatukumkuta"
"Sasa nisikilize kwa makini hapa nimeona kuwa
mwanao bado mzima na hakika anaishi kwa maisha
ya furaha sana lakini hana kumbukumbu ya kukujua
wewe ni nani zaidi ya ndugu ya mtu mmoja tu
ambae kwa sasa sijamfahamu vyema ni nani na
kujua mtoto wako yuko wapi sijafahamu..."
"Hakika mke wangu akirudi na akasikia hii habari
atafurahi sana....ila mzee kesho kutwa naimani
nakuletea bangili ya mke wangu kwa hali yoyote"
"Sawa safiri salama....sitokupa kinga yoyote
katumie nguvu zako za kawaida ukija hapa wakati
wa kuuwa haya mambo basi ndipo nitakutengeneza
na kuhakikisha kila kitu kinakuwa salama ila
msalime baba yako mwambie nitakuja
kumsalimia....pia jambo la mwisho hata
usiyemzania ndie atakuja kukusaliti"
Chito alipumzika baada ya kuonyesha mahala pa
kupumzika ili jioni aianze safari ya kurudi kijijini
kwao.
Ndani ya kijiji cha Chamlo, wakati wale viongozi
wanarejea wanakuta kwenye moja ya selo kuna
mwanamke ambae ni msaidizi wa binti Lyoto.
Bamuzi alikuwa na hasira sana alijua kuwa kuna
kosa kalifanya alienda kumuangalia mke wake
alimkuta akiwa analia lakini hasemi chochote ilibidi
aombe afungue mlango wa ile sehemu ambayo yule
mwanamke Mwana kafunga na kuanza kuhojiwa.
yule mlinzi aliyasema kila kitu na hatimae Bamuzi
alitaka kuchukua maamuzi magumu lakini Lyoto
alikataa na akasema aachwe hana hatia.
Baada ya siku kadhaa kupita, ndani ya kijiji hiko
majira ya mchana wanashtuka upande fulani wa kijiji
wanaona nyumba inaungua moto bila hata
kuchomwa na mtu. Watu waliangaika sana ili
kuokoa lakini kila walipojaribu kumwaga maji ni
kama walikuwa wanaongeza moto kukua.
Hatimae kila mahali moto ulionekana kutanda na
kijiji kikawa katikati ya moto. Ilikuwa kama laana
kwa jinsi walipoiona hapo ndipo mzee Mwalami
alitumia nguvu zake za uganga akagundua jambo
"Khaaa ili ni aina ya jini kabisa la moto ndio maana
linatema moto na kusababisha maafa. Alienda moja
kwa moja hadi kwa viongozi wake aliwaonyesha
jinsi gani lile jitu lenye sura mbaya linavyohitaji
kuangamiza mahali pale.
Bamuzi alipomuona alilijua ni lile ambalo walikutana
nae kule msituni wakiwa na lengo la kuchukua dawa
na wakakutana ana kwa ana na mmoja wao ambae
ni ZWELI akajitoa muhanga ili kunusuru wengine
sasa linataka kuja ndani ya kijiji chao kufanya nini.
Wana kijiji wote waliombwa kusimama sehemu
moja wasikimbie ovyo kuepusha madhara zaidi.
"Jamani huyu kiumbe ndie ambae nilikutana nae
kule na ndie ambae alimmeza yule kijana ambae
alikuja kutusaidia kule polini." hapo sasa masikio ya
watu yakafunguka na hata yule mwana aliona kuwa
alikuwa anakosea na wale waliomdanganya
walikuwa na nia mbaya kwao na pamoja na Lyoto.
"Lakini mzee Ngololo...inaonekana anashindwa
kuingia ndani ya hiki kijiji kwa kuwa kuna nguvu
kubwa sana hapa ipo laiti bila hivyo, tungeteketezwa
wote sisi...."
"Sasa hiyo nguvu ni ile ya mizimu yertu au" aliuliza
bwana Ngololo
"Hapana kwani siioni kabisa yani kwa hili jini
limezidi nguvu ila anamilikiwa na nguvu ambayo ipo
hapa karibu sana sasa inabidi kufanya haya ....watu
wote waje hapa kwani inaonekana nguvu iko
hapa...pili wa hapa sisi tusitoke kabisa tusubiri
hapahapa....."
"Sasa inatakiwa kuijua hiyo nguvu kama iko kwa
mtu basi tujue tunamlinda vipi asitoke inatubidi
tuffanye hivyo bwana Mwalami"
Ngololo na bamuzi wakishirikiana na Kelebu
walimsii mzee mwalami afanye vile kwa watu
waliopo pale kwa mfalme Mzee huyo aliwaomba
haraka sana mmoja mmoja atoke wakati huo yeye
akiendelea kuangalia kwenye internet yake ya
kienyeji au GPRS ya kienyeji.
Alianza Mwana na baadhi ya wafanyakazi wa pale
lakini ilionekana hawana kwani nguvu iliendelea
kubaki vilevile, akaja Mzee Kelebu nae hapana
akafuatia Bamuzi nae hapana akaja mzee Ngololo
nae hapana wakashangaa ni nani huyo Bamuzi
akaingia ndani na kumchukua Lyoto ili atoke nae nje
kwani walimsahau japo baadhi ya wazee pale
walianza kumchukia.
Kitendo cha yeye kutoka tu kuelekea kule upande wa
moto ambako ulikuwa unaambaa ambaa ajabu zaidi
mzee Mwalami akasema Lyoto katunje ndie
mwenye hizi nguvu hakika ona hapa inapungua na
kule moto unazimika unyewe, hakika ilikuwa ni
jambo la ajabu sana kwao.
Naomi alikuwa pale karibu alipolisikia lile jina la
Katunje alilikumbuka kuwa ndio yule kijana ambae
alikutana nae siku moja na akampenda sana ila jina
lake alilisahau. akawa anajiuliza huyu Lyoto na
Katunje wana uhusiano gani......
Waliamua kumtembeza kila eneo ambalo liliathirika
na moto wa ajabu ndipo kila anapolisogelea lile
eneo hakika moto una zimika kabisa.
Katunje akiwa na hali yake ile ya kutoonekana
aliondoka kwenda kijiji cha Bwawani akiwa na imani
kuwa kaka yake atakuja kumuona kama
alivyoahidiwa na Mzee sikujua bila kujua kuwa
anaitiwa pale kwa nia mbaya kabisa alienda
mwendo wake wa haraka sana lakini akiwa njiani
alishangaa kuona wanyama wanamuangalia na
kumkodolea mcho lakini kwa binadamu hawezi kitu
kama hiko, alijipa imani kuwa labda yupo vile kwa
lengo la kumtafuta ndugu yake na akishamuona
labda inaweza kuwa ni dawa kubwa ya
kupona.......................
 
SEHEMU YA ISHIRINI NA NNE............24
Endelea.....................
.............Safari ya kijana KATUNJE iliendelea
kuelekea ndani ya kijiji cha Bwawani kwa lengo la
kuonana na bwana SIKUJUA kama mualiko wake
ulivyo. Akiwa na imani kubwa kabisa kuwa kaka
yake atafanikiwa kumuona bila wasiwasi Safari hii
alienda akiwa na matumaini hayo.
Kutokana na mwendo ambao alikuwa akiutembea
haikumchukua muda mrefu sana aliweza kukiona
kile klijiji cha Bwawani hapo aliona sasa muda
umefika wa kumtafuta kwanza kaka yake kisha
pindi akishindwa ndipo pale atakapomtafuta mzee
Sikujua kwa lengo la kuonyeshwa kaka yake huyo.
Aliweza kupita kila eneo kutokana na ile hali ya
kutoonekana mbele ya mamcho ya binaadamu.
Alifika mpaka pale kwenye ile nyumba ya
Mwenyekiti bwana Semeni, aliikumbuka sana ile
nyumba kwani siku ya kwanza anafika pale kijijini
aliondolewa kama mbwa tena kwa kufukuzwa na
vijana waliotumwa na Mwenyekiti huyo. 'Ahaa...hapa
ndipo mara ya kwanza niliweza kufukuzwa baada ya
kuulizia kaka yangu ngoja nianze na hapa.'
Wakati anawaza hayo alimuona bwana mzee mmoja
akiwa na kijana wa makamo mwenye umri
unaokimbilia sawa na yeye, alishangaa hivyo
ilimbidi awafuate kisha aweze kupata taarifa
kuhusiana na yale ambayo wanataka kuongea zaidi
na jambo gani ambalo wanataka kulisema na
likamsaidia.
Yule mzee alikuwa ni bwana MANUALI akiwa na
kijana wake SUSU walifika wanafika kwa bwana
Semeni ambaye ni mwenyekiti wa kijiji cha
Bwawani, Ujio wa watu hao ulionkena kuwa ni
washida sana kwani walikuwa na haraka sana jambo
hilo lilimfanya Katunje ahisi jambo ambalo
lingeweza kumsaidia kwa mambo aliyokuja
kuyafuata. Kwa upande wa katunje haikujulikana
kwa nini anafanya jambo lile la siri japo hali yake
inajulikana.
Muelekeo wa Manuali na Susu ulifikia tamati kwenye
ile nyumba ya mwenyekiti bwana Semeni na ndipo
wakabisha hodi mara kadhaa na ndipo mlango
ukafunguliwa ndipo mwenyekiti aliwakaribisha ndani
na akarudisha mlango. Katunje alijiuliza maswali
kadhaa.
'Ina maana humu ndani ndipo pale kwa mwenyekiti,
na kama ndio humu kuna swala gani
linaendelea..ngoja nikasikilize kama nitafanikiwa
kupata jambo lolote'
Mawazo yake yalimtuma kwenda kusikiliza kipi
ambacho wanazungumzia wale waliomo ndani,
alihitaji kufungua mlango kwa kuamini kuwa yeye
haonekani kwa macho ya kawaida ya mwanadamu,
lakini kwa upande wa pili aliona kuwa ataharibu na
akashindwa kupata kile ambacho alitaka kukipata
kwa urahisi, hivyo aliamua kusikiliza kwa kupitia
upenyo ambao ulionyesha yaliyomo ndani na
waliomo ndani japo kwa nadra kuona kila kitu.
waliomo ndani walikuwa watatu yani Mwenyekiti
Semeni, Manuali na Susu. Hawa wote walionekana
kuwa na mawazo ya pamoja kutokana na hali ya
mihemko yao ya kutaka kujua la mwenzake.
Mwenyekiti alianzisha mazungumzo ambayo
yalimfanya kila mmoja kuwa tayari.
"Manuali unajua kuwa muliahidi kuwa kijana wako
atakuwa tayari kumsema yule ambae anasababisha
mauaji na matatizo kama yale yaliyompata yeye
siku kadhaa zilizopita...sasa mpaka sasa kimya"
Aliongea mwenyekiti kwa sauti ya chini ambayo pia
ilimpa shida katu je kusikia maneno yote ambayo
yanazungumzwa.
"Nafahamu lakini nilikuwa kwenye matiubabu yake,
na hapa unaponiona yuko tayari kusema kila kitu
kwani alihitaji aje kukuambia wewe kwanza kabla
hata wanachi hawajapata taarifa hiyo..."
"...lakini kwa taarifa ambayo niliyo nayo kuwa tayari
mtu anayesababisha kaonekana na baadhi ya watu
waliondoka hapa na kwenda kufuatilia huyo mtu
kwa mahojiano zaidi na mmoja karudi nasubiri ripoti
yake tu hapa..."
Susu alionekana kuchanganyikiwa baada ya
kuambiwa yale maneno, na kwa upande wa kijana
Katunje hakuelewa chochote pale alihisi kama
hayamuhusu kabisa ndipo akatoka pale akijinyoosha
huku akijishikashika na kujitathmini kivipi yeye
haonekani upande ungine alifurahi na ungine alikuwa
na huzuni kwa kutojulikana wapi yeye alipo. Ghafla
anakuja bwana Sikujua kwa mwenyekiti huyo jambo
ambalo Katunje alimuangalia kwa makini na
kumfananisha na mtu fulani hivi'
"Huyu jamaa mbona kama nilishamuona kule
nyumbani au ndio mzee Sikujua...ngoja nifuatilia
nadhani kuna jambo nyeti limejificha"
Alirudi pale sehemu ambayo alikuwa anachungulia,
Mzee Sikujua alibisha hodi na kufanya mazungumzo
ya ndani kughairishwa na kusikiliza huyo anayekuja
ndani ni nani. Hatimae anakutana uso kwa uso na
kijana Susu, moyo wake ulipwita mithli ya mpira
udundao mara kadhaa baada ya kupigwa na
mchezaji mahili. Moyo wake uliendelea kutokuwa na
amani kwani alihgisi kila siri imevuja kwa
mwenyekiti na kazi ambayo alikuwa anaifanya basi
kuwa tupu na ukweli umevuja alijiona kuwa mtu
mpumbavu ambaye anasafiria nyota ya bwana Chito
kwa kumsingizia mauaji na matatizo ambayo yeye
ndio msababishaji>
"Bwana Sikujua samahani naomba tutoke hapo nje
ili tuongee nije kumalizana na hawa wengine"
Maneno ya mwenyekiti yalimpa faraja kubwa sana
Sikujua kwa kuhisi kuwa kuna usalama kidogo,
walisogea pembeni na hapo ndipo Kijana katunje na
yeye aliwasogelea karibu kabisa ili apate kusikia
kila kitu kinachoendelea.
"Ehee habari ya safari huko ulikokwenda?"
"Safari ilikuwa salama yenye matumaini na kile
nilichokiendea...." Sikujua alikuwa anaongea huku
akitetemeka kwa hofu kubwa aliyo nayo.
"sasa....ulifanikisha ?"
"..Ndio na nilifika mpaka kilimalondo na nikamkuta
mke wa Katunje ndipo nikampa taarifa kuwa hapa
afike mapema sana na nadhani siku ya leo yuko
njiani". Aliongea hayo huku bila kufahamu kuwa
kijana katunje mwenyewe anayasikia kila neno na
nukta hakuiacha.
"sasa...huyo mwenzako Mapato huko aliko
atafanikiwa kumleta Chito maana ?" Mwenyekiti
aliendelea kuhoji maswali ambayo yalikuwa
yanamsaidia kijana Katunje kufahamu swala zima
linaendeleaje pale.
"Kuhusu Mapato kwenda Shishimo na kumfuata
Chito halina ugumu japo nilikuja kwako kwa hofu
maana siku ya leo imekuwa kubwa hajarudi kabisa
sasa sijajua kipi ambacho kimempata huko...lakini
mwenyekiti huyu Susu na mzee wake wamekuja
kufanya nini huku kwako?"
"Ooooh! hawa wamekuja kuulizia lile swala japo
kwa maelezo yao wanasema tujitahidi na
tukishindwa basi wao watachukua maamuzi
mkononi kwani wanamfahamu". Sikujua aliona
mambo magumu sana ndipo alimuomba kuwa
awaruhusu kwa kuwaambia kuwa wanalishugulikia
jambo lao. Katun je mpaka hapo aliweza kujua
jambo muhimu na kumfahamu kuwa Sikujua na
mwenyekiti si watu wazuri sana pale kijijini.
Aliweza kujua pia kuwa kaka yake anapatikana
kijijini kwao na inambidi afunge safari ya kwenda
ndani ya kijiji hiko. Kabla hata hawajaachana yani
wanaagana, Kijana mmoja maarufu kwa uuzaji wa
mbuzi akiendelea kunadi karibu kwenye nyumba ya
mwenyekiti.
Sauti hiyo ilimfanya susu kutoka mule ndani na kuja
nje ambako aliwakuta Semeni na Sikujua
wkiendelea kuelezana baadhi ya mambo yao. Kijana
huyo alifika pale na kupaki baiskeli yake pembeni
na kuwasalimia, wakati huo Susu aliliona lile tenga
ambalo lilimkumbusha mbali sana.
"Baba...unaona hili tenga langu limekuja tena leo, "
aliongea kwa sauti na kumfanya bwana Katunje
kusogea pale na kuliona lile tenga ambalo na yeye
analikumbuka vyema, haikutosha pia na ile nguo
ambayo mara ya kwanza alimchukua Sikitu ambae
yeye anamfahamu kwa jina la Lyoto kuiona ikiwa
kwenye miguu ya mbuzi huyo"
Kijana yule alistaajabu baada ya kumsikia susu
akisema kuwa tenga lake "Susu unasema tenga lako
hili kivipi?" Aliuliza kijana huyo ambaye ni kawaida
kwake kuja pale baada ya muda kupita.
"Hili tenga lina historia kubwa sana, hili tenga ndio
chanzo ya mambo hapa kijijini bwana.." alikuwa
anaongea kama mtu ambae kapandwa na mizuka.
Waliweza kumshika huku hasa bwana Manuali na
kuondoka nae, kijana Katunje alikuwa anamfahamu
yule kijana kwani wote wanatoka kijiji kimoja ila
ilikuwa ngumu kwake kuuliza chochote kutokana na
hali yake ya kutoonekana. Tenga lile Katunje
analikumbuka vyema sana alipiga mahesabu iweje
lile tenga lizue yale mambo " Kijana yule anasema
tenga lake lakini tenga hili mimi nililichukua
hukuhuku nikambebea Lyoto hadi kilimalondo,
nakumbukla Mfalme SWAI na kijana wake Kimolo
walilichukua kwa nguvu lile tenga....leo lipo hapa
basi mhusika atakuwa yule kijana anayedai tenga
lake kwa nguvu zote"'
Aliona kuwa Susu ndie muhusika mkubwa na yale
yote lakini na huyu mzee Sikujua ana mambo gani
ya siri na mwenyekiti kuhusiana na kaka yake Chito.
Aliyawza mengi sana na upande mwingine aliona ile
hali ya kutoonekana inamsaidia sana kwa baadhi ya
vitu.
Aliamua kuondoka na kuwafuata Susu na mzee
Manuali. akiwa nao njiani Susu alikuwa anaropoka
maneno ambayo yalionekana kuwa ni ya kweli ndani
mwake. Njiani alikutana na kijana Ndunya ambae ni
rafiki wa Susu ambae alimsaidia mzee Manuali
kumkamata Susu vyema. Kuja kwa Katunje karibu
kulimfanya Ndunya ashtuke na atoke pale jambo
ambalo lilimshtua Katunje kwa kuhisi kuwa
anaonekana na huyu jama.
"Wee nani na mbona unawafuatilia hawa..."
Laa haulaaa..kumbe kijana Ndunya anamuona
vyema kabisa. Katunje aliishiwa pozi jambo ambalo
lilimfanya atoweke maeneo yale kwa kukimbia. Wao
walienda hadi kwa mzee Manuali na kumuweka
susu ili kumpa matibabu kwa kuwa walihisi akili
yake haiko sawa kwa nyakati zile.
Baada ya muda kupita Ndunya na Manuali walikaa
pamoja ndipo wakaanza kuongea baadhi ya vitu
ambavyo walikuwa wanavishangaa pale kijijini.
"Baba hivi haya maneno ambayo alikuwa
anayaongea Susu unayachukuliaje..?" Aliuliza ndunya
kumuuliza mzee Manuali. "Hata mimi ndugu yangu
kwani kuna baadhi ya kauli na mambo yanaendana
yani siamini kusema kuwa bwana Chito anayafanya
haya hapana labisa". Wakati huo katunje tayari
kafika nyuma ya nyumba hiyo huku akisikiliza kwa
makini sana yale yote yanayoongelewa.
"Baba labda nikuambie kitu kimoja, hawa wazee
wawili nina wasiwasi kuwa wanahusika kabisa
kutokana na matukio yanayoendelea" "Akina nani
hao"
"Hawaa...sikujua na mapato na si chito kama
wanavyoongea mana mzee chito alivyopotelewa na
mtoto wake Sikitu hakuwa na amani kabisa na
alihitaji aondoke hapa kijijini...lakini kwa uwezo wa
mzee Manyenye alimuambia atulie hapa kwa kuwa
ni mzee Mzuri sana ila sikujua alimfanyia hujuma
akishirikiana na mjukuu wako Susu, ila sijajua
kuhusiana na hili tenga mana kila sehemu ukimkuta
susu kipindi hiko anamuongelea sikujua atagusia
tenga"
Katunje aliushika usemi ambao ulisema kuwa
"..Maana mzee chito alivyopotelewa na mtoto wake
sikitu hakuwa na amani kabisa.." alipata kujiuliza
swali " Ina maana kaka yangu alikuwa na mtoto
ndani ya hiki kijiji, alafu kapotea kwa mazingira gani
jamani mh...ila huyu kijana inabidi niwe karibu nae
anipe mambo mengi sana" Katunje aliamua
kujitokeza mbele yao na lolote liwe lengo aungane
nao ili apate nafasi ya kuyajua mengi zaidi.
Lakini hata kijana Ndunya hakuweza kumuona tena
kama pale mara ya kwanza jambo ambalo lilimpa
nafasi kubwa kijana katunje kujua mengi zaidi.
Aliona vyema siku hiyo kupanga safari ya kwenda
Kwao alikotokea yani Shishimo ili akamfuate kaka
yake kama taarifa inavyosema.
Ndani ya kijiji cha Kalulu anaonekana mwenyekiti wa
kijiji hiko akiwa katikati ya wanakijiji wake baadhi
hasa akiwemo mzee Uwesu ambae alikuwa
anaonekana mwenye huzuni kubwa sana. hakika
huzuni ilitawala kwani ilionyesha kuwa kuna taarifa
ambayo ilifika pale ni ya kusikitisha kwa wote.
"Mimi kama mwenyekiti, ambae nimeipata shutuma
hii hakika sijafanya mauaji haya ambayo
yamesemwa kuwa mimi muhusika...bwana Masanja
hakunisindikiza japo alikuwa na nia ya kunisindikiza
tuliachana ndani ya kijiji chake na mimi nikaelekea
njia ya huku nyumbani kwangu..lakinijambo ambalo
linaloonekana kuwa familia ya bwana chito
wanataka kulificha jambo hili na Uwesu usimpate au
usipate ukweli wowote kuhusiana na mwanao "
Haikuwa siku nzuri kwao kwani mambo hayakuwa
vyema, Ilimbidi bwana Uwesu na mwenyekiti pamoja
na wazee kadhaa na vijana wa pale kijijini waanze
safari ya kwenda kijiji cha Shishimo kwa ajili ya
kujibia kesi ya mauaji ya mwenyekiti wa Shishimo.
Muda huohuo Chito anarudi kutoka kwa Mzee
UPENGO ndani ya kijiji cha MIPINGONI, huku akiwa
na kazi ya kwenda kwa baba yake kuchukua Bangili
ya mkewe ili apate kurudi tena kwa mzee huyo,
Chito alidhamilia hata kumpoteza baba yake kwa
jinsi hasira alizo nazo aliona kuwa ni mzazi ambae
hana faida kwake kabisa kwa yale ambayo huwa
anayafanya ndani ya familia yao.
Aliweza kuingia ndani ya kijiji chao mapema jioni.
Bwana Mambo sasa akiwa na Nyandu ambae ni
rafiki wake wa karibu sana, walionekana kushtuliwa
sana baada ya kuja taarifa kutoka kwa wakuu wao
wanaojulikana kwa jina la Nyamnyena. "Mambo
sasa hapa kuna taarifa imekuja ya kusikitisha na
inatuhitaji kujipanga sana mana vita sasa imeanza".
Mambo sasa alishangaa sana vita kuanza kwa yapi
tena "Bwana unanichanganya vita hii kuwaje sasa
ebu nieleze nipate kuelewa vyema"
"Sawa yani...Nyamnyena wamesema kuwa lile
mzimu wa Lyoto ambalo limepelekwa kumchukua
Mjukuu wako SIKITU linahitaji nguvu ya ziada yani
damu...mana anaonekana yule binti kupata nguvu
za ziada ambazo zinashindana na nyamnyena...."
Mambo sasa alishangaa sana
"Sasa kwa nini usimuambie nyamnyena akasema
wapi huyo binti alipo na akatuambia na sisi
tukaenda kumaliza kazi hiyo?" "Sasa kama
nyamnyena kashindwa kuingia ndani ya kijiji hiko
utaweza wewe kweli hapa cha kufanya kwanza huyu
uliyemshika ukamtupe kule kwao bwawani sasa hivi
na umpotezee kumbukumbu ya kurudi huku ukirudi
tuje kujua tunalifanyaje hili jambo".
Kweli alijiandaa vyema mzee baba wa chito
akaondoka nae mapato hadi kijiji cha Bwawani
ambapo zamani walikuwa wanalifahamu kwa
Songambele, alimuacha huko na kuchukua baadhi
ya vitu ambavyo aliona kuwa vitamfaa kupitia
bwawa lile na kuondoka navyo akimuacha Mapato
akiwa usingizini.
Anarudi nyumbani akiwa hoi baada ya kubadili
mavazi yake ya usiku. Upande wa chito hakuwa
mgumu sana alienda moja kwa moja hadi kwenye
chumba cha baba yake akafungua vitu mpaka pale
alipoikuta bangili ya mkewe na kuishika kwa
umakini na kutoweka zake.
Safari hii aliona vyema kwenda bwawani japo
wanamchukulia kuwa muuaji lakini aliondoka akiwa
na lengo la kumfuata bwana Manyenye ambae ana
ushahidi tosha sana kuhusiana na zile bangili ajue
zaidi kabla hata ajaenda kwa bwana Upengo kule
Mipingoni.
Mambo sasa anarejea nyumbani kwake lakini
anakuta mambo hayako sawa baada ya kukuta
mlango wa nyumba hukufungwa na ndani hakuna
mtu. aakajua fika kuwa chito karudi alipiga mguu
hadi ndani kabisa kwake lakini hakuisi chochote
kabisa ndipo na yeye akaenda kwa rafiki yake
Nyandu kumalizia kazi zao.
Asubuhi na mapema sana Chito akiwa njiani
kuelekea kijiji cha Bwawani na kwa kuwa alikuwa
kajifunika miguo ambayo haikuwa rahisi kujulikana
kwa lengo la kuwa salama zaidi, ilimfanya
kupishana na ndugu yake bila kujuana Katunje
ambae na yeye alikuwa anaelekea kijijini kwao
kumtafuta kaka yake.
Chito alifika moja kwa moja hadi kwa mzee
Manyenye ambapo mzee huyo aliishiwa nguvu
baada ya kumuona mzee mwenzake, kwa kuwa
alikuwa na haraka sana kwa kuhitaji ukweli wa zile
bangili na kama yeye mtengenezaji atataja ukweli
wote.
walisalimiana na wakapata muda wa kuanza
maongezi yao. "Mzee manyenye najua muda mrefu
sana mpaka sasa ila nina mambo yananitatiza
nahitaji taarifa yake zaidi". "Usijali bwana Mambo
sasa" alimuita lile jina ambalo alilitumia mara ya
kwanza.
"Mimi siitwi mambo sasa kama unavyofikilia
ninaitwa CHITO...je unaweza kuniambia mzee
MAMBO SASA wa shishimo unamfahamu vipi?"
Manyenye aliona kama utani kwa yale maelezo
ambayo wanapeana pale kwa kujua utani kumbe
bwana Chito yuko makini sana kwa lile jambo
alitakalo kujua ukizingatia mkewe na mtoto wake
pamoja na ndugu yake hawaonekani na chanzo
kinajulikana na huyu mzee manyenye naingia
kundini.
"Mbona unaniambia maneno ambayo siyaelewi
ndugu yangu kuna shida kwani?"
"Unaikumbuka hii Bangili niliyokuja kuchukua
kwako?" Alimtolea bangili ambayo alimpatia bwana
Manyenye. Mzee huyo aliikumbuka lakini maelezo
yake yalionyesha kupinga ukweli jambo ambalo
hakulifahamu kuwa anahatarisha maisha yake kwani
Chito alichomoa kisu na kumuonyeshea mzee huyo
"Mtoto wangu kapotea ndani ya hiki kijiji, haitoshi
mke wangu kapotea kwa mazingira nisiyoyafahamu.
.haitoshi ndugu yangu kapotea mpaka sasa sijui
wapi alipo, nipo radhi kukuua mzee endapo
hukusema ukweli tupo wawili tu hapa sema ukweli
wako wewe na mzee mambo sasa wa shishimo
mna uhusiano gani kuhusiana na hizi bangili?"
Manyenye hapo ndipo alipoamini kuhusiana na
ukweli na umakini wa Chito kwa yale asemayo
"Ngoja kwanza..ukweli ni kuwa baba yako najuana
nae miaka mingi iliyopita kipindi ambacho nilikuwa
mmoja wa kundi la wachawi la nyamnyena...nil
iondoka kwenye lile kundi nikiwa bado kijana ila
walinitishia sana wakanipa kazi ya kutengeneza
bangili za mauaji, pindi mtu avaapo iwe rahisi kwao
kumuita na kumuua....nilitengeneza ya mama yako
na nikatengeneza ya mkeo lakini niliacha hiyo kazi
kabisa na hapa maisha yangi yako hatarini ndio
maana ukaona kuwa nilikuwa mgumu kukupa
mapema sana "
"Ehee ikawaje sasa mpaka sasa hivi...."
"Mpaka sasa nimejiondoa japo wananifuata...kwani
baba yako jana kaja huku bwawani kumleta bwana
Mapato ambae alikuwa anakufuatilia wewe huko
kwenu alipitia hapa na kunipa kazi ya kutengeneza
kingine japo sijajua kwa ajili ya nani kwa sasa ila
siwezi ni bora hata kufa kuliko kusababisha mauaji"
Maelezo hayo yalimsababisha kuelewa kila kitu
kuwa baba yake kuwa muuaji mkubwa sana. alimpa
mkwara kuwa asije kusema kwa yeyote ujipo wake
yeye.
"Lakini nimemuona ndugu yako alikuwa anakutafuta
pia na wewe" Chito alirudi tena kwa mzee Manyenye
"Ndugu yanguuuu......katunjeeeee"
"Ndio japo hayuko kwenye hali ya kawaida sana
nilimuelekeza kuwa afike kwenu ili iwe rahisi
muungane kupambana na baba yenu aliyeamua
kuwasaliti kwa kuhitaji ufalme wa kichawi kwa
nguvu kwa kupoteza ndugu wa karibu zake">
Chito aliondoka muda huohuo kurudi kwao
shishimo.
Katunje anafika kijijini kwao na kuona mazingira
yamebadilika na hakuna hata wa kumuuliza
kutokana na hali yake na ambayo ana amini kuwa
inamsaidia sana, aliendelea kutembea huku na kule
hadi nyumbani kwake lakini hakukuta mtu na
hakupenda kumuona baba yake kutokana na ujinga
wa mzee huyo.
Chito alifanya juu chini kuondoka na baiskeli hadi
kijijini hapo ambapo pia ilikuwa ngumu kumuona
ndugu yake kulingana na hali aliyokuwa nayo ya
kutoonekana na watu.
Alichoamua akifika mahali anaita jina lake yeye
mwenyewe ili kama yupo karibu ahisi ukaribu wake
na kumuoan kuliko kuita jina la Katunje asije
kumsababishia matatizo. "Chitooooooo...
.chitooooooooo"
Sauti hiyo ilisafiri kwa kasi hadi kwenye ngoma ya
masikio ya katunje na kuanza kuhaha huku na kule
kumtafuta kaka yake kipenzi.
Hatimae katunje anamuona kaka yake akiwa
anapiga yowee la jina lake huku chozi likimtoka kwa
wingi kutokana na uchungu alionao, mana mpaka
muda huo alishajua kuwa mkewe kafariki na mtoto
wake.
katunje alienda kumziba mdomo kaka yake na
kumuambia "Kakaaa mimi hapa katunje huwezi
kuniona kwa hali niliyo nayo ila nakuhitaji kwanza
uamini mimi ndugu yako niliyekutafuta kwa miaka
yote hii nikipata matatizo ya dunia yanayosababishw
a na baba yetu mzee Mambo sasa"
Baada ya muda aliamini kuwa ndie yeye ambae
alikuwa anamtafuta na walikaa mahali huku
wakiongea "Hatuna muda wa kupoteza sasa imefika
muda wa kwenda Mipingoni kwa mzee Upengo
atakusaidia pia na tutalimaliza hili jambo
kabisa......."
Safari ya kwenda Mipingoni ilipangwa kuwa kesho
yake kwani kwa siku hiyo pia ndio sikua mabyo
kikao cha mwenyekiti wa Kalulu anakutana na wazee
wa shishimo ambao wana hasira ya kupotelewa na
Mwenyekiti wao wakihisi kuwa mwenyekiti wa
Kalulu ndio msababishaji..........
 
SEHEMU YA ISHIRINI NA TANO......25
Edelea,,,,,,,,,,,,,,,,,,
.....Chito alikuwa haamini kabisa kama kweli yuko
karibu na ndugu yake kipenzi ambae alikuwa
anamtafuta kwa takribani miaka kadhaa iliyopita,
Hali hiyo ilimfanya kumuangalia kwa ule upande
ambao yupo ndugu yake Katunje japo hakuweza
kumuona kabisa. Sauti ya kwikwi ambazo zilikuwa
zikimtoka Katunje ziliendelea kutoka bila hata
kuonekana kwa wakati huo Katunje alijihisi dhaifu
sana kwa ile hali ambayo alitamani kumuona kaka
yake na yeye akionekana.
Lakini ilishindikana walibaki kuongea kwa sauti
lakini kwa upande wa Katunje aliweza kumuona
kabisa lakini ilikuwa tofauti kwa Chito ambae
alikuwa anasikia sauti tu. "Ndugu yangu kipi
ambacho kimekutokea mpaka uwe hivi sasa hivi?"
"kaka ni historia ndefu sana mpaka sasa hivi bado
furaha yangu haijaja mpaka pale utakaponiona japo
mimi nakuona ". Chito alifikilia kwa makini sana
kisha akamuambia jambo Katunje.
"Katunje hakikisha huku tuendako usiongee kamwe
kuna kikao ambacho nahitaji ukasikilize yale
ambayo wanaongea alafu baadae tukutane hapa ili
kuelekea kijiji cha Mipingoni kwa mzee Upengo
sawa".
"lakini kaka nitawezaje kujua mambo ambayo
sijawahi hata kuyajua hata chanzo". Alihoji ili apate
kufahamu zaidi. "Hapana ndugu yangu wewe nenda
ili ukapate kujua yale ambayo yataongelewa kiufupi
kuna kesi ya mauaji ya kiongozi wetu wa hapa
kauliwa na kiongozi wa kijiji cha Kalulu kule aliko
shemeji yako mengi utayafahamu muda ukifika".
Basi kijana Katunje aliondoka pale alipoelekezwa na
bwana Chito alielekea upande mwingine, pia
hakutaka kabisa kukutana na baba yake kwani
anafahamu yapi ambayo yanaendelea. Chito hakuwa
mwenye kuamini kwa lile tukio lote ambalo
limeendelea pale. Alishukuru sana kwa kila hali
aliona kuwa muda sasa umefika wa kufanikisha yale
ambayo kayapanga.
Majira hayo ambayo yalikuwa yanaendelea na kikao
cha viongozi wa pande mbili yani vijiji viwili
walikutana kuzungumzia yale mambo ambayo
yanamhusu kiongozi wa Kalulu. Katunje nae
alifanikiwa kufika maeneo hayo akiwa na lengo la
kupata habari zote ambazo zitakuwa zinahusu kikao
kizima. Baada ya muda wa kikao chao kuisha ndipo
katunje alirudi kumtafuta kaka yake.
Alimkuta akiwa kajiinamia mahali fulani akiwa
kashika tama. Alienda kumshika begani jambo
ambalo lilisababisha Chito kushtuka kwa kuwa
hakumuona aliyemshika ndipo alihaha lakini katunje
alijieleza kumuambia kuwa yeye ni ndugu yake,
"Haya vipi tayari umefanikiwa kujua hata kitu
kimoja".
"Ndio kaka kikubwa walikuwa wanapanga kumjua
yule ambae alifanya yale mauaji kwa upande wa
baadhi ya watu pale walisema kuna Mzee yule rafiki
wa baba yani Nyandu anahusika sana kwa mauaji ya
hapa na akishirikiana na baba kaka inaniuma kwa
nini baba anakuwa katili hivi".
"Basi ndugu yangu usilie mimi nimeshalia sana na
nikapoa kwani kuna vingine nilivishuhudia
mwenyewe lakini nimelia na nimenyamaza cha
kufanya hapa tuongozane haraka sana yani tusipitie
hata kwa mzee tuondoke moja kwa moja
Mipingoni".
Safari ilianza kabla hata hawajamaliza kijiji mke wa
mwenyekiti ambae alishafariki dunia alimuona Chito
akiwa anaongea peke yake. Alimuita "Chitooo....chi
to"
"Oooh naaam...ndugu habari yako"
"Safi mbona unaongea peke yako njiani kote huku
tangu upo kule nakuona unaongea kama....au
umechanganyikiwa shemeji yangu..."
"Ni kweli....mambo yamekuwa magumu sasa.. vipi
lakini lile swala limeendaje baada ya wao kuja ?"
"Kwanza nilishangaa kwa nini hukuja pale..."
Aliongea mke wa marehemu masanja.
"Mhh! kweli ila ujue kuna kesi kubwa mii mwenyewe
ninayo sasa ningekuja ingekuwa vurugu kubwa sana"
"Kesi ipi tena hiyo..."
"Si unajua kupotea kwa mke wangu mama sikitu
mpaka leo sasa wazazi wake wanamhitaji na
sijaenda kutoa taarifa mpaka pale nitakapopata
uhakika "
"Pole sana... lakini shemeji sikufichi muambie baba
yako kuwa tabia hii aliyo nayo sisi tumemchoka
kabisa kumbe mume wangu aliyemuua ni baba yako
na rafiki yake Nyandu..imeniuma sana sijui kosa ni
nini jamani wamenifanya kuwa mjane sasa hivi
mimi hata umri wako bado unadai aaaah!".
"Basi nyamaza fahamu hata mimi sifurahiki na
jambo hili ambalo baba yangu analifanya nakuomba
uvumilie haya yote yatakwisha kwa sasa nipo na
mgeni naenda nae mahali fulani...."
Aliongea Chito huku akimshika bega kumtoa
wasiwasi. "Una mgeni gani tena?"
"Niko na ndugu yangu ambae nilishakuambia kuwa
kapotea kwa muda na leo nimeonana nae yulee
KATUNJE..."
"Yani chito unaniambia yuko kwa baba yako sasa
hivi?"
"Haaa haaa haa..hapana nipo nae ndio ambae
nilikuwa napita kuongea nae sasa nikirudi nitakuja
kukupa habari zaidi.. ila usije kutoa taarifa hii kwa
mtu yeyote".
Safari yao iliendelea kama kawaida na hatimae
walifika ndani ya kijiji cha Mipingoni na kuitafuta
nyumba ya mzee Upengo kama kawaida yake. "Sasa
katunje hapa tutaanza kumueleza kwanza shida yako
ili kama ataweza kukusaidia basi akusaidie ndipo
tufanye yale yaliyonileta huku" " sawa kaka".
Kabla hata hawajafika hapo walikutana na mtu
ambae bwana Chito alishakutana nae mara ya
kwanza na akampa usafiri hadi ndani ya kijiji hiki,
walisalimiana na akamueleza kuwa " Chito
nimekukumbuka si ndio yule mara ya kwanza
ukaniuliza kijiji hiki na nikakupa msaada!"
"Haswaaaa ndio mimi kabisa ndugu haya hii safari
ya wapi tena?" Chito aliuliza.
"Hiii bwana namalizia shughuli za leo na nadhani
kesho ukinielekeza wapi tukutane tutasalimiana
mana mimi na wee tumekuwa kama ndugu sasa,
baada ya hapo nitarudi nyumbani kwetu CHAMLO
kupeleka taarifa japo nina habari nyeti sana za huko
yani".
"Aaaah nitafurahi sana sasa ngoja tufike na kesho
tukutane hapahapa majira kama ya asubuhi ili
tuongee zaidi unipe mambo mazuri ya kijijini kwenu
labda naweza kushawishika kuhamia huko".
Waliagana na wao wakelekea kwa bwana Upengo.
Mzee upengo walimkuta na akawakaribisha vile
ipasavyo na wote wakakaa lakini mZee huyo
alimsalimia kila mmoja jambo ambalo hata chito
ashangae alimjuaje kama kaja na mtu pale.
"Usishangae uliyekuja nae mimi namfahamu na
nadhani nilishakupaga habari zake kabla haya lete
hizo bangili zote".
Chito alizitoa na akampatia.
Mzee upengo kwa ustadi wake mahili sana
alichofanya ni kuiangalia na kuitambua ile ya Mke
wa Chito alikaa kwa muda sana kisha akaaanza
kusikitika kabisa. Sikitiko hilo lilimfanya chito awe
na mshangao sana iweje afanye vile hakutaka
kukawia ilibidi amuulize swali kwanza.
"Baba mbona unasikitika baada ya kuiangalia hiyo
bangili au sio yenyewe?"
"Hapana ni yenyewe hii ya mama yenu tayari nyota
yake imefifia ina maana kafariki na hii ya mkeo
nyota zake zilizowekwa tayari nayo imefifia yani
kafariki dunia..."
Chito alipatwa na butwaa kubwa sana hakutaka
kuamini kwa jambo ambalo anaambiwa kumbe
muda wote ana hangaika kumbe mtu kafa tayari.
walichukua muda mwingi sana mpaka anyamaze na
bwana Upengo kuendelea. Maneno ambayo alikuwa
anayatoa mzee huyo yalikuwa magumu na makavu
yani maneno ambayo hafichi chochote kwa kupoza
ukali wa maneno.
"Si wafichi baba yako alimpeleka mkeo kwa mchawi
wao mkuu na kule wakamchinja shingo, akapewa
kisu baba yako akaambiwa atoe sehemu za siri
zake zote pamoja na viungo vingine, sehemu za siri
wamezificha mpaka pale zitakapokauka
wamezianika na lengo lao baadae wasage zile
nyama kisha achanjiwe baba yako na atawazwe
kuwa mkuu wa wachawi hapa kijijini na vijiji vyote
ambavyo vinazunguka....si hilo tu alipewa nyama
kisha akaambiwa aje kukulisha wewe...kwa bahati
nzuri madhara uliyoyapata ni madogo sana ambayo
yatatoka kwa kuwa hukula nyama hata moja huo
ndio usalama wako....."
'"Ina maana baba yetu kamuua mke wa kaka yangu
jamani aaah hivi huyu mzee huu ukatili kajifunza
wapi jamani na sisi si ndio atatuua kabisa".
Waliendelea kulia kwa pamoja pale, lakini kwa kuwa
yameshatokea walikubaliana na hali halisi ambayo
ipo pale. Walikabidhiwa baadhi ya dawa a,bazo
zitawasaidia. lakini chito aliendelea kuulizia
kuhusiana na katunje kupona itakuwaje "Katunje
siwezi kumtibia mimi kwa kuwa yupo ambae
kayafanya haya na yeye mwenyewe anamfahamu
inambidi aende kijiji hiko na mtu huyo ataenda
kumsaidia".
Walizidi kumuomba sana mpaka pale
alipowakubalia na ndipo akampa dawa na akaweka
ndani ya maji kisha akaambiwa aende kuyaoga maji
yale, baada ya kuyaoga hakika ilimsaidia na chito
akamshuhudia jinsi ndugu yake alivyo jibaba.
Hapo sasa furaha ilikuwa kubwa na kesho yake
walijiandaa kama kawaida asubuhi walikutana na
yule mtu ambae waliahidiana kukutana pale.
"Sasa umesema unatokea kijiji cha Chamlo...." "
kijiji cha Chamlo...?" Katunje alishangaa sana.
Ndipo Chito na yule jamaa wakashangaa "Katunje
una maana kuwa unakijua hiko kijiji ndugu yangu?'
Aliuliza Chito
"Kama nakifahamu hivi kuna kipindi fulani
nilishawahi kwenda hapo yani nilipita sikukaa sana
kwa mzee mmoja anaitwa MWALAMI niliendaga
kutafuta dawa fulani lakini huko nilikutana na kijana
mmoja anaitwa BAMUZI...."
Alionekana kufurahi yule Mzee waliekutana nae pale
"Hakika anapafahamu kwani hao wote ambao
anawasema ndio wahusika wakuu wa pale kijijini "
Chito aliona sasa ndio muda wa kubadilisha maisha
na kwenda kutafuta maisha sehemu nyingine. " Lkini
uliniambia kuwa kuna habaari mpyanzuri ya kuvutia
kule kwenu ipi hiyo?" Aliuliza chito
"Ahaa kumbe yani habari nilizozipata kuwa kuna
msichana mrembo sana ambae yupo kule na ambae
kaolewa na mtoto wa mfalme Ngololo yani ana
maajabu huyo mwanamke "
"yapi haypo tena?"
"Kwanza kaja pale hasikii vyema, haoni vizuri lakini
sasa hivi kawa msaada mkubwa sana pale kijiini
huwezi kuamini kabisa na pia kawa kivutio kwa kila
mmoja "
"Dah natamani kuja kuishi hapo kijijini kutokana na
mshikamano mliokuwa nao na nakuahidi baada ya
kumaliza mambo yangu nakuja huko na kwa kuwa
huyu ndugu yangu anapafahamu nitakuja nae huyu
anaitwa Katunje bwana ni ndugu yangu sana."
Waliagana na wao wakaelekea kurudi kijiji cha
Shishimo. TUkiwa upande wa mzee Mambo sasa
ana haha hajui nini afanye anaelekea kwa mzee
Nyandu baada ya kupata habari kuwa mambo
yameanza kubadilika na wanahitajika kwenye kikao
na mkuu wao.
Walisafiri kwa usafiri wao wa kila siku na hatimae
wanafika ndani ya pango hilo ambalo huwa
wanakutana kila siku. Mkuu wa pale ambae
anashirikiana na Mizimu ya NYAMNYENA, alikuwa
amegadhbika sana kutokana na hali ambayo ipo
mbele yao. Walitulizwa kwa kukaa kimya wote na
ndipo yeye akasimama kutoka kwenye kiti chake
cha ukuu na ndipo akaanza kusema.
"SIDHANI KAMA MNAWEZA KUTUCHEZEA KWA
NAMNA HII...MJUKUU WAKO SASA KAWA TISHIO
KUBWA SANA KWETU...NA HII INATOKANA NA
KUMUACHA KIJANA WAKO CHITO AJITAMBUE NA
KUJUA NINI AFANYE ONA SASA ANAANZA
KUTUGEUKA SASA NATAKA HUYU CHITO AULIWE
MARA MOJA IWEZEKANAVYO SITAKI MAJADILIANO
ZAIDI YA KUTENDA KAZI HIYO KWA MKONO
WAKO...."
baada ya kumaliza maneno hayo hakika
waliruhusiwa kuondoka lakini mzee huyo hakutaka
kabisa kufanya jambo hilo kwa mtoto wake ambae
anampenda sana alikubali kufanya kwa wengine
lakini si kumuangamiza Chito, lakini kutokana na
ushawishi wa rafiki yake Nyandu hakuweza kukataa
alikubali na ndipo mipango ya kumnasa Chito
ikaanza kuwekwa.
'"Lakini hapa kuna jambo ambalo nalihisi, mke wa
Mwenyekiti anataka kurudisha kisasi sasa twende
kumfuata ili tukamkomeshe..."
Walisambaa kama radi kisha wakamfuata mke wa
mwenyekiti na wakamkamata majira hayo ya
mchana akiwa ndani kwake katulia, Mama huyo
alishindwa afanye nini baada ya kushikwa na kuanza
kutishiwa.
"Naomba utuambie una mpango gani na sisi
unataka kupindua maamuzi yetu hali ya kuwa wewe
ni mgeni hapa kwetu, unatujua vyema sisi?..."
Alizidi kutetemeka baada ya kujiwa mchana kweupe
na wazee hao wakimtishia ndipo akajikuta anapata
ujasiri wa kuropoka hata ambavyo hajaulizwa
kabisa.
"Nakuambiaje nyinyi hamtopona mtakufa kama
mlivyomuua mume wangu...."
Hawakutaka kuchelewa walimlisha vitu vya ajabu
ndipo akaanza kulalama tumbo kuuma sana
akaanguka chini huku akigaa gaa kwa maumivu
neno lake la mwisho lilikuwa ni kuwaambia ukweli
ambao aliona utawafanya kuamini kuwa yale
wanayoyafanya yatakuja kuwaghalimu kwa hatua
moja ama nyingine.
"Chito na katunj,,ee wame..ku.t..na na wat..akuja
kulipiza kisasi cha mambo yenu hayo
mnayoyafanya". Pale pale alifariki dunia.
Kama kawaida yao walichukua sehemu za siri za
mama huyo na wakaondoka kabisa yale maeneo.
Hawakuwa na huruma lakini jambo ambalo
waliondoka nalo pale kuwa Chito na Katunje
wameungana na watakuja kulipiza kisasi kwa
mambo wanayoyafanya.
"Mimi siamini kama katunje ni mzima yeye
kamuona wapi ?" "Achana nae cha kufanya subiri
siku watakayotangaza kuwa ile nyama imekauka na
tayari kwa kusagwa na kufanyiwa utaratibu wako wa
kuwa kiongozi na atakaeleta ujinga tunamaliza "
Bila wao kujua kuwa hayo wanayoyafanya kuwa siku
yake iko mwishoni kabisa.
Katunje aliamua kumsimulia kaka yake wakati wako
njiani historia yake na chito na yeye akamsimulia
jinsi mtoto wake alivyopotea na mpaka sasa
haonekani. "Kaka sasa sijaelewa huyo mtoto alikuwa
ni wa kike?"
"Ndio katunje"
"Sasa, kuna watu nilipofika pale bwawani walikuwa
wanagombania swala la tenga na ikaonyesha kuwa
mzee SIKUJUA anahusika na upotevu wa tenga
sijaelewa hapo?"
"Ndugu yangu....baada ya kupotea kwa mwanangu
kuna kijana anaitwa Susu, huyu alimuazimisha tenga
sikujua la muda sana kwa jana anapotea sikitu na
susu anadai tenga kwa sikujua na hakulipata
kabisa... ajabu muda ulipita anakuja kijana kutoka
kijiji cha Kilimalondo..." " Kaka kilimalondo ndiko
mimi maisha yangu yaliko eheee..."
"Kumbe ndo unakoishi....sasa alikuja na lile tenga
tukashangaa kuona lile tenga ambalo susu lilikuwa
lake na ajabu zaidi mbuzi ambae alikuwa kafungiwa
mule alifungiwa na nguo ya sikitu ambayo aliivaa
kwa mara ya mwisho niliumia sana nikajua
mwanangu bado yupo...."
"Kaka ebu subiri unajua mara ya kwanza kuja
bwawani nilifika kwa mwenyekiti SEMENI
nilijitambulisha kuwa namtafuta kaka yangu anaitwa
Chito ila hawakukufahamu na hatimae wakanifukuza
kabisaaa...." Alisema Katunje
"Ni kweli ujue kwa nini nilikuwa natumia jina la
baba yangu mzee Mambo sasa ndio maana ikawa
ngumu kunipata......."
"Unana sasa baada ya kukimbia nikajikuta nafika
mahali ambapo nilipokuwa nakwenda waliogopa
kunifuata na wakawa wanarudi cha kushangaza
nilikuta damu zikiwa kwenye majani...mbele
nikaona tenga lilee ambalo la susu tena vilevile...."
"Weee katunje usiniambie hivyo...ehee"
"Usiwe na wasiwasi...mbele nikaona nguo ambayo
hata juzi ambapo yule kijana aliyekuja bwawani
kuuza mbuzi wa SWAI namjua alikuja na kitambaa
ya nguo hiyo...Nikaamua kurudi nikachukua tenga
nikabeba na nguo nikaondoka navyo hadi sehemu
moja kuna bwawa..."
"Katunje ulidiriki kufika bwawani yaaa kuna hatari
kubwa sana watu hawatoki salamaa eheee" Chito
aliamua kukaa chini kabisa mana hii taarifa inampa
mwangaza fulani na tukio la kupotea kwa mtoto
wake.
"sasa nikawa nahisi kiu na jasho usoni ndipo
nikataka kunywa maji nataka kuanza tu ikanipata
akili ya wasiwasi nikaangalia nyuma nikamkuta binti
kakonda wadudu wamejaa mwilini yani utadhani ni
mzoga....MPAKA SASA HUYO BINTI NAMTAFUTA
SANA".
'ndugu yangu huyo ni mwanangu anaitwa Sikitu
nakushukuru sana kwa msaada wa kumhudumia
mwanao tena nakushukuru sana itabidi tufanye
juhudi kubwa sana kumsaka mpaka apatikane"
"Kaka unaponiona hapa nimeshindwa ila itabidi
tuende mahali fulani huko nadhani tutaanzia ".
Waliondoka na wakiwa na nia kubwa ya kupitiliza
kwenda kijiji cha Bwawani waelekee Kilimalondo
hadi MPOLONI kwa mzee UKELELE. Hawakutaka
kufika nyumbani kwani wanajua kuwa hakuna faida
yeyote pale wanayoipata kukaa na mtu mkatili.
Safari yao hakika ilifika hadi kijiji cha Bwawani
walichofanya baada ya kugundua kuwa mzee sikujua
kuwa ndie chanzo wa yale yote ndipo walifika
kwenye nyumba yake wakapiga alama ya X na hadi
kwenye nyumba ya Mapato napo wakapiga X
mlangoni wakapiga alama ya muelekeo ambao
ulionyesha njia ya kwenda kijiji cha Kilimalondo,
kwa kuwa ilikuwa ni usiku walifanya hayo na
hawakujulikana.
Safari iliendelea moja kwa moja hadi kijiji cha
Kilimalondo ambapo napo hawakutaka kusimama
sana waliendelea kuelekea njia ya kijiji cha Mpoloni
ambako kutwa mzima walitembea, kutokana na
uchovu walipumzika mahali na ndipo wakaanza
safari na asubuhi na mapema wanaingia kijiji cha
Mpoloni. Mzee Ukelel alikuwa wa kwanza kuwaona
kwani yeye huwa anajiimu mapema sana na kuanza
kufanya kazi za utengenezaji wa dawa zake. Mzee
huyo alifurahi sana kuwaona ndipo aliwakaribisha na
wao wakakubali wito.
Mwaija alikuwa na furaha sana baada ya kumuona
katunje kwa macho yake kuwa karudi salama kama
mwanzo.
"Baba huyu ni kaka yangu anaitwa Chito tumezaliwa
wawili tu, "
"Sawa karibu sana kwetu lakini hii sura kama
naifahamu haijanipotea sana machoni mwangu
kama miaka mingi iliyopita "
"Mh! ukelele unamjuaje huyu kama hivyo labda
useme unamjua baba mana ndie aliyefanana nae. "
"baba yenu anaitwa nani na anaishi wapi"
"Anaitwa Mambo sasa na anaishi..."
"Shishimoooo...." Alimalizia mzee ukelele.
alionyesha kuwa anamfahamu sana huyo mzee.
"Inaonekana mlikuwa mnajuana sana na baba
yangu.
"'Unajua baba yenu ni mtu mbaya sana, hata Katunje
upotevu wa binti Lyoto na hali aliyo nayo anachangia
kwa kiasi kikubwa baba yenu,,,mpaka sasa
nimefahamu wapi anaishi...mimi kuna mzee mmoja
anaitwa Upengo na baba yenu tulikuwa marafiki
ambao tulikuwa na kazi za uganga lakini baba yenu
akacha na akaamua kuwa mchawi kabisa na kipindi
hiko alikuwa na nguvu alitufukuza pale tutafute
mahali pa kuishi kwa hiyo sishangai sana kuhusu
hilo"
Muda ulipita siku zilipita Mzee Ukelel anapoteza
maisha baada ya kupatwa na homa kali sana jambo
ambalo lilikuwa na mshangao mkubwa sana kwa
mwaija ambae anaishi peke yake pale, lakini
Katunje anachukua jukumu la kuwa nae kama
kawaida.
PIa hali ya mwaija inaonyesha rasmi kuwa ni
mjamzito ambae baada ya muda huko akawa mama
mlezi. Walipanga safari ya kwemda kijiji cha
CHAMLO ambako wanaenda kuanza maisha kwa
kuwa yeye ana rafiki yake ambae amempa sifa tele
ya huko kijijini kwao......
 
SEHEMU YA ISHIRINI NA SITA 26
Endelea................
... Safari ilianza ya kusafiri kwa pamoja kwenda
ndani ya kijiji cha CHAMLO, safari hiyo iliambatana
na watu watatu ambao ni KATUNJE, CHITO na
MWAIJA. waliiacha nyumba ya mzee ukelele ambae
ni marehemu kwa wakati huo baada ya kuugua kwa
maradhi yaliyotokana na uzee wake.
Upande wa Mwaija hakuwa na furaha kabisa baada
ya kupotelewa na babu yake pamoja na mama yake
na kwa sasa yuko yeye tu lakini hakuna kitu
ambacho kiliharibika zaidi kwani kijana Katunje
alishashikilia majukumu yote ya kumhifadhi binti
huyo pia ukizingatia ni mjamzito. Safari ilikuwa
ndefu sana kwani katunje pekee ndie anapafahamu,
waliamua kupumzika kwa muda kidogo kisha
waendelee na safari yao.
Njiani walikutana na vikwazo vingi hasa wanyama
hatari lakini kilichowasaidia ni uwepo wa katunje
ambae alikuwa anatumia dawa yake ambayo
kafungwa mkononi kama irizi ambayo kwake
aliamini kuwa inamsaidia kwa kiasi kikubwa sana.
"Katunje unamuona yule nyoka anakuja upande wetu
na hatuna njia ya kumkwepa joka kama hili ambao
ni hatari sana!" Chito aliongea kumueleza ndugu
yake katunje baada ya kuliona joka ambalo
lilionekana kutishia maisha yao kwa wakati huo.
Kiukweli lilikuwa kubwa sana kiasi hata mwaija
alihofu kuuliwa mmoja wao ama wote kwa pamoja.
"Hapana msiogope ngojeni kwanza lisogee
nalikausha sasa hivi" aliyaongea hayo katunje huku
akipandisha nguo yake yani shati lake la mikono
mirefu kisha akaifikia ile kamba iliyozunguka mkono
wake. alianza kuiteremsha taratibu na kadri ilivyozidi
kuteremka ndipo nyoka yule alivyopoteza nguvu
hatimae kupoteza fahamu kabisa. "haya twendeni
huyu kalala tayari" hawakuamini kile kitendo
kilichotokea kwa muda mfupi tu. "katunje yani ile
dawa ambayo babu alikupatia tayari bado unayo
tu?" Chito alimuuliza.
"Ndio ninayo na ndio ambayo imenisaidia sana
katika kumtafuta lyoto na wewe "Eti sijawahi
kukuuliza hivi lyoto ni nani?" Chioto aliuliza "Lyoto
ni yule binti ambae nilikuambiaga muda wa nyuma
huko kuwa alikuwa na matatizo na nikaamua
kumsaidia lakini kutokana na hila za wazee wa
KILIMALONDO wakampoteza na sijui wapi ambako
aliko mpaka sasa " Waliachana na hayo
wakamshika mkono mwaija ambae alikuwa
anaogopa kumtambuka joka lile na wakaongoza njia
ya kuelekea Chamlo.
Ndani ya safari yao ilifikia kikomo baada ya kuona
dalili ya nyumba kuonekana na sauti za ngoma
zikiendelea kurindima, hapo ndipo walipoamini
kuwa wamefika tayari na kikubwa zaidi ni kujongea
taratibu kwa madaha na kufika kule kisha kumtafuta
yule jamaa ambae alijitambulisha ni mtu ambae
anahusika na mambo ya kukusanya habari nje ya
Chamlo na kumletea mzee Ngololo pamoja na
mwanae Bamuzi. "Kaka unaona tumefika tayari sasa
ni kuanza kumtafuta kwa kumuulizia yule mtu"
Katunje alitoa kama maoni yake kwa kaka yake.
"Ndio lakini hatuwezi kuanza kumtafuta mtu kwenye
mji wa watu lazima tumtafute kiongozi wao yani
mwenyekiti ndipo tujue tunampata vipi " Katunje
alikumbuka jambo " hapana kaka huku hawana
mwenyekiti bali wana mfalme lakini kuna mzee
mmoja anaitwa nani nimemsahau ila kwake
napafahamu nilipelekwa na binti mmoja wa hapa".
Walifika ndani kabisa ya kijiji hiko kisha wakaanza
kusambaa huku na kule kutafuta nyumba ya mzee
ambae katunje alimsema.
Kumbe Binti NAOMI hakuwa mbali na maeneo hayo
alifanikiwa kumuona kijana Katunje hakika moyo
wake ulikurupuka sana kiasi haamini kama
ampendae kamjia yeye mwenyewe, aliamini kuwa
mama yake kamsaidia kumleta kijana huyo kwa
wakati maalum. 'haaa siamini kama huyu kijana
kaja kwa ajili yangu, lakini ngoja niende kwa mama
kumueleza kwanza'.
Aliondoka kwa mwendo wa shida kubwa yani
haraka sana kumfuata mama yake. Baada ya
kumfikia kwanza alianza kukatika mauno yake
mbele ya mama yake akimaanisha furaha na yeye
kama binti nzuri kushinda wote pale kijijini na
hakuna hata wa kumfananisha nae. "Mwanangu
umechanganyikiwa sasa hivi...mbona unaonyesha
uzuri wako mbele yangu wakati nafahamu kama
wewe ni mzuri zaidi ya unavyojijua kuna nini?".
Naomi alicheza ngoma yao ya kiasili akifuatisha
ngoma ambayo muda mfupi katunje na chito
waliisikia.
"Mama...kweli naona kama mzee Ukelele kafanya
kazi ya maana.." Mama ilimbidi aache kazi ambayo
alikuwa anaifanya "kaifanya kazi gani mwanangu?"
Naomi alimsogelea mama yake. "Mamaaaa....Yule
kijana tayari kaja nimemuona kwa macho yangu
tena anahangaika mtaani akiwa yeye baba yake na
ndugu yake wananitafuta mama nahisi hivo" Mama
yake naomi alicheka sana kisha akanyoosha mikono
juu kisha akongea lugha fulani "Nyamnyenaaaa..
...ahsante". Kumbe hata huyu mama ni mshirika wa
lile kundi la mzee mambo sasa na Nyandu, hakika
kazi ni kubwa sana kwa watu hawa wawili yani
Chito na Katunje.
Mama huyo aliingia ndani pamoja na katunje kisha
akaonekana anabadilisha nguo zake na kuvaa nguo
za kazi. walikaa kwenye mkao mama na mtoto.
Naomi namuita Nyamnyena kisha umuulize maswali
sawa usiogope" Naomi hakuwa na shida kwani yeye
ndie anahitaji na mama yake ni mtu ambae yuko
bega kwa bega kumsaidia " Ilo tu mama muite
haraka". Alifukiza moshi fulani kwenye moja ya kifuu
kisha mama huyo akajifunika kaniki. ndani ya dakika
kadhaa mama huyo alibadili sauti kabisa na kuwa
ya mwanaume ikiwa na maana tayari nyamnyena
kama mzimu wao kafika mbele yake na yuko tayari
kujua nini shida.
"HAYA SEMA SHIDA YAKO HARAKA BINTIII"
nyamnyena aliongea kwa njia ya mama Naomi
"Nymanyena samahani naomba kuuliza leo kuna
wageni wameingia hapa kijijini sasa sijajua kama
wamekuja kwa jambo gani?" Nyamnyena alikaa kwa
muda kisha akacheka sanaa " BINTI, NAKUSIKITIKIA
SANA UNATAKA KUINGIA KESI AMBAYO
HAIKUHUSU...WALE WAMEKUJA KWA KAZI
MAALUM AMBAYO SISI TUNAPAMBANA
WASIFANIKIWE KWA HARAKA IWEZEKANAVYO..PIA
YULE KIJANA TAYARI ANA MCHUMBA YULE AMBAE
UNAMUONA PIA HAYUKO KWENYE MAWAZO YAKO
KABISA..." Naomi furaha ilipungua na huzuni
ikatawala "Sasa wamekuja kufanya nini na
utanisaidiaje kwani nampenda yule kijana"
Nyamnyena alicheka tena na tena "BINTI, YULE
MALKIA ALIYEOLEWA PALE NA BAMUZI NDIO
FAMILIA YAKE HII ILIYOFIKA NA SISI TUNAMHITAJI
YULE BINTI...CHA KUFANYA TUTAKUPATIA YULE
KIJANA UMPENDAE NA SISI UTUFANYIE KAZI
MOJA TU" Naomi alikaa vyema na kuuliza tena "
Kazi gani hiyo Nyamnyena?" Alianza kunguruma
kama simba mara paka mala sauti ya mwanamke
kisha ikarudi tena ya kiume "TUNATAKA UMVUE ILE
DAWA YULE KIJANA MKONONI, PIA TUNATAKA
SIKU YA TANO WAO KUKAA HAPA UTAPATIWA
DAWA NA KITI WETU UTAMPA YULE MWANAMKE
ALIYEKUJA NAE MIMBA YAKE ITATOKA NA NJIA
RAHISI YA KUIVUA HIYO DAWA...ILA TUMIA AKILI
YA ZIADA".
Hatimae aliondoka kwenye kichwa cha mama huyo
na Naomi akamsimulia kila kitu. " Mwanangu
mpaka sasa tumeingia kesi ambayo haituhusu
kabisaaa ila kwa kupendapenda kwako huko kama
wanaume wengine huwaoni si bora hata ukabaki na
yule kijana aliyekutoa usichana wako" Mama
aliongea kwa jazba huku akipanga njia ya
kukabiliana na swala lile. "Sasa Naomi hakikisha
unawafikia kabla hata hawajafika kwa mfalme mana
akifika kule lazima tuwakose watapewa kinga kubwa
ambayo tutashindwa hata kuwakaribia.
Chito aliusoma ule mji akagundua jambo yeye kama
mkubwa na aliyepewa kinga na mzee Upengo ndani
ya kijiji cha cha MIPINGONI.
Alimdokezea tu Mwaija na Katunje kuwa wawe
makini ndani ya mji ule. Walifika hadi kwa mzee
MWALAMI ambae mwanzo Katunje alifika, Mzee
huyo alikuwa ndani na wao wakaanza kuhodika pale
nje. Mwalami alitoka nje kama kawaida yake
alidhani kuwa ni viongozi wake wanamhitaji.
Kumbuka kuwa watu wa Chamlo hasa viongozi
wanajua kuwa katunje kafariki japo jina hawakumjua
ndio maana wakaongozana kwenda kutoa pole kwa
mzee Ukelele kule MPOLONI, Alivyotoka tu nje
alishtuka sana hata akatupa kisu ambacho alikuwa
anakitumia ndani humo "Babu vipi mimi ni yule
kijana wa Ukelele nimekuja tena?"
"Hapana aaah umetoka kuzimu lini wewe kijana
unakuja kunijaribu sio.."
"Kukujaribu babu au umenisahau...babu umenisahau
kweli mimi ni yule kijana nilikwenda kumsaidia
Bamuzi kufuata dawa leo unanikana ". Katunje
aliongea baada ya kuona kuwa mzee huyo
anachanganyikiwa. "Ngoja nakuja kwanza....nisubiri
" Aliingia ndani mwake kisha akatoka na maji fulani
hivi na usinga hakuamini kama ndio yeye kwani
taarifa yake kuwa kafa. alimpiga usinga na
kumwagia maji kichwani hatimae katunje
akadondoka chini. Chito na Mwaija walishangaa.
"Mzee mwenzangu sikuelewi umemfanya nini ndugu
yangu hali anakuambia ni yeye kama mwanzo
mlikutana vipi ushindwe kumuelewa leo".
"Si hivyo mwenzangu kweli alikuja hapa akitokea
Mpoloni, alifikia kwangu nikamuelekeza huko
alikotaka kwenda lakini wakati wenzake wanarudi
yeye hakurudi na huko kuna mmoja alikufa, sasa
taarifa iliyokuja ni kwamba yeye nae kafa
kachukuliwa na mzimu wa moto, tulipanga safari ya
kwenda mpoloni kutoa rambirambi...kwa ukelele
sasa akatuambia kuwa kweli hajarudi mpaka muda
huo nafahamu kuwa huyu kijana kafa sasa
anapokuja leo ndio wasiwasi wangu kwani hapa
kijijini tumeingiliwa baada ya kuondoka malkia wetu
basi hatuna ulinzi tena...ila kama ni wakawaida
atainuka mda mfupi tu ila kama mmekuja kunijaribu
haki ya nani hainuki...."
Yale maneno yaliwachoma sana ukifikilia chito
furaha yake ni Katunje na mwaija ndio kabisa.
Mwaija hakusita kuliamsha chozi alianguka kwa
katunje na kuanza kulia huku akimuamsha.
"bwana wangu amkaaa usiniache peke yangu ona
babu Ukelele kafa mama yangu kafa na wewe
tegemeo langu unadondoka nitabaki na
nani?.....Katunjeeeeee amkaaaa". Lile neno la
Katunje lilimzibua masikio Mwalami kwani sio geni
kabisa kwake.
"Weee binti katunjee unamjua weeweee!?" Mwalami
aliuliza.
"Sasa huypo katunje si ndio huyu uliyemfanyia hivyo
ndugu yangu kabisa na huyu binti ni mchumba
yake, huyo mzee ukelele unayemsema kafariki dunia
tayari ndio kabaki huyu ambae ni nguzo yake sasa
sijui unamsaidiaje?" Mwalami alitumbua jicho huku
akikumbuka jambo.
""Binti nilikukuta kule mtoni ukiwa ndani ya maji ina
maana maji yamekusafirisha mpaka sehemu
salama..japo hatujui wapi ambako umetokea, yapi
yamekupata pia jina lako nani'' Lyotooo..." Ahaaa
unaona sasa jina lako zuri sasa lyoto ndio jina la
baba yakoo "katunjeeee" Ahaa basi tutakuita Lyoto
katunje".
Hapo alipokumbuka akapata picha fulani hivi.
"Jamani ngoja tumpe dawa hii atainuka sasa hivi
mana hapa kuna mapya nimeyaona samahanini sana
ila ni wasiwasi wa kujilinda tu". Walimnywesha
dawa na hatimae akainuka toka usingizini.
Walimsubiri kwa muda ndipo wote wakaingia ndani
ili kuzuia watu walioko nje wasijue nini kinaendelea
humo ndani na ukizingatia kuwa wao ni wageni
pale.
"Jamani ninataka kuuliza swali je mnamjua binti
anaitwa Lyoto?" Katunje alishangaa huku akikodoa
macho yenye furaha kubwa sana pia hakuamini
kama atalisikia swali zuri zaidi ya fedha maishani
mwake. " Babu mimi ni ndugu yangu wa karibu
sana japo si wa familia lakini ni ndugu yanguambae
kapotea miaka mingi sana namfahamu vyema "
"haya anaitwa lyoto nani?". Mwalami aliuliza.
"Jina la baba yake silifahamu ila nilikuwa natumia
jina hilohilo na hata nahisi lyoto si jina lake kwani
tulimpa kwa kuwa alikuwa hafahamu hata jina lake
kabisa tukaona tumepe lyoto kwa kuwa changamoto
tulizozipitia mpaka anakuwa salama". Katunje
aliongea hilo swala wakati huo chito anavuta picha
anahisi kama ndie mwanae wanaemzungumzia
akianzia kwa katunje kusema kuwa kamkuta
bwawani akiwa karibu na tenga, akikumbuka lile
tenga lilivyozua mgogoro kule kijiji cha BWAWANI,
akikumbuka mengi hadi hapa kuwa kapewa jina la
lyoto lakini si lake asilia aliamua kuingilia kati'
kabla ya kusema Mwalami aliuliza swali "Huyu binti
ninayemfahamu mimi anaitwa LYOTO KATUNJE
huyu dada alipokuamsha pale chini nje aliita jina la
katunje ndio maana nauliza lakini pia binti huyo kwa
mbali sikufichi kafanana na huyu bwana" Mwalami
alisema huku akimnyooshea Chito
"Kweli mimi ndio katunje nadhani kasema hivyo
kwa kuwa kanizoea sana kwa kufanana na kaka
yangu siwezi kuthibitisha kwa sababu kaka yangu
tulipoteana miaka mingi na huyu Lyoto kanipotea
muda mrefu sana " hapo ndipo mzee Chito
akashindwa kuvumilia na akaanza kuyasema yake
yeye yaliyo moyoni na yanayomchanganya.
"Mzee mwenzangu, ndugu yangu katunje pamoja na
shemeji yangu Mwaija...nadhani kuwa ndugu yangu
katunje anafahamu kama binti yangu anaitwa SIKITU
kapotea toka kijiji cha Bwawani sasa ni bora
tukamuone inawezekana akawa ni SIKITU au si yeye
tukamsaidia Katunje kumpata binti huyo" Mwalami
alilipata somo la kutosha sana mpaka akaamini
kuwa cha kwako hakipotei.
"Jamani kwanza inatakiwa tuwe kimya hapa tulipo
humuhumu ndani tusitoke naenda kule kwenye
uongozi mkubwa mana kuna yule mleta taarifa za
kijiji amefika tunaenda kuchambua baadhi ya
mambo kuhusiana na ubadilisho wa uongozi kutoka
kwenye ufalme kuja kwenye ngazi ya mwenyekiti.
nitajitahidi kuliweka hilo swala kisha tujue
tunalitatuaje mana huyo binti analindwa sana hata
mimi nina siku kadhaa sijamuona kabisa "
Mwalami alikuwa anajiandaa kuondoka kama
alivyosema "Sawa lakini ni bora ukamueleza huyo
mleta habari kuwa rafiki zake aliokutana nao kule
Mipingoni tumefika aje huku kutuona!" Mwalami
aliwa ahidi kuwa atarudi na huyo mtu baada ya
mazungumzo.
Mzee Mwalami alifika kwenye kikao cha viongozi
baada ya kuisha kwa ngoma ya furaha aliyopigiwa
mfalme, ndipo wanenguaji wote waliambiwa
wapumzike wakale na kubadilisha nguo zao kwa
ajili ya kusherehekea kwa pamoja. Walikutana
akiwemo na Mzee KELEBU pamoja na wengine
waliohitajika pale. katika ajenda ambazo
walizizungumzia ilikuwepo moja inayomhusu binti
Lyoto kufanya harakati ya kujua wapi anatokea kabla
ya kumpatia uongozi kupitia Bamuzi, jambo ambalo
lilichukua muda sana ni baada ya matatizo ya
kuingiliwa na uchawi mara kwa mara pale walipo.
"Haya tumefahamu baada ya uchunguzi mrefu
tunamkaribisha mpelelzi wa habari aliyefika jana
atueleze yapi mapya yanayoendelea." Alikaribishwa
"Kweli nimefika vijiji husika ambavyo tulivituhumu
kuhusika na huu uchawi, nimegundua kuwa kuna
kijiji kinaitwa Shishimo historia yake kuwa wapo
wasumbufu sana ambao wanadiriki kuua watu ..sasa
sisi vita vyetu ni kuwaendea moja kwa moja najua
wanachojikingia hakina nguvu kama sisi tuliye nae
huyu malkia mpya..pia nimegundua kuwa hapa
kwetu wapo ambao wanashirikiana na kundi hili
ambalo linajiita NYAMNYENA ni kundi la mizimu
mikali sana endapo wakifanikiwa kujua kuitumia
wanasambaratisha kila kitu...sasa ni kutuma jeshi
letu kuwadhibiti.." walimuelewa kwa kila hatua
aliyoisema. Muda wa mambo ya nyongeza ulifika
ndipo mzee Mwalami aliomba nafasi ya kuongea
kwa kirfu kidogo apate kueleweka.
"Jamani mnajua kuwa malkia mimi ndie nilimleta
baada ya kumuokoa......" Mara bamuzi akaingilia
"Kwa hiyo unatakaje sasa...mzee nitakutoa kwenye
cheo ulicho nacho unataka kunitenganisha mimi na
huyu hakuna hata mmoja ambae ataweza mana
tumemhudumia mpaka akafika hapa..." Aliyaongea
ya kuyaongea mpaka wakastaajabu ndipo mzee
ngololo akamtuliza "Kijana kumbuka wewe ni
kiongozi wa baadae tumempa nafasi ya kuongea
muache amalize..."
"haya ahsante..kwanza sifa ya kiongozi lazima awe
na BUSARA, awe na HEKIMA, awe na SUBIRA, hivi
vitakusaidia sana nimekupa dondoo naomba uwe na
hekima kwenye maongezi yako naomba uwe na
busara kwenye maamuzi yako naomba uwe na
subira katika kufanikisha mambo naomba niendelee
kueleza jambo muhimu.....Kipindi namleta hapa
binti tunamjua kwa jina la lyoto hatukujua jina la
baba yake tukamsikia anataja jina la katunje na
tukampachika jina la lyoto katunje si ndio?"
"Ndiooo kabisa mwalami endelea tunakusikiliza"
"Mnakumbuka kijana Bamuzi alienda polini kutafiuta
dawa ya kumtibia Lyoto katunje mnakumbuka?"
"Ndio mwalami tunakumbuka..."
"Sawa, kuna kijana alienda kumsaidia kule je
Bamuzi unamfahamu yule kijana kwa jina lake?"
Mwalami alimuuliza
"hapana simfahamu pia yule kijana alikufa tayari..."
"Sawa najua hamfahamu, anaitwa yule ndie
KATUNJE mwenyewe....kijana hakufa ila alichelewa
kufika mpoloni alipatwa na vikwazo njiani..sasa yule
katunje si baba yake ila alimsaidia tu huyu binti na
msaada wake mkubwa sana kuliko wako wewe
hapa hata punje haufiki...pia kuna wasiwasi
ninaouona kuwa hata baba yake anajulikana
munajua kwa nini?"
"Mzee mwalami hizi habari ni mpya sana...lakini
huyu katunje kama namfahamu nilipita kijiji kinaitwa
MIPINGONI nikamkuta rafiki yangu anaitwa Chito
akiwa na nduguye huyu " Hapo mwalami
akamnyooshea mkono "Ewalaaah! kabisa na huyo
chito unayemsema yupo mimi ndio wageni wangu
wamekuja kukutafuta wewe uliwa ahidi kuwa
utawapokea wapo nyumbani kwangu kule sasa ndio
maana nikasema tuwe na busara kwenye maamuzi "
Kila mmoja pale hakuamini kwa kile anachokisema
mwalami,
"haya maajabu kwelikweli, haya fanya haraka sana
nenda kawaite uwalete hapa haraka mno kabla hata
kabla Lyoto hajaamka ndani akajua kila kitu."
Mzee Mwalami anajiandaa kwenda kuwaita kule
alikowaacha na wakati huo tukumbuke tayari mama
Naomi kamtuma mwanae kwenda kwa mzee
Malami kufanya majambozi ya kuwanasa watu hao.
 
SEHEMU YA ISHIRINI NA SABA 27
Endelea................
Mzee Mwalami, alitoka kwenye kile kikao ili apate
kwenda nyumbani kwake ambako aliwaacha wale
watu. Pia Naomi nae akiwa kwenye harakati hizo
hizo. aliondoka kutoka kwake yani kwa mama yake
na kwenda moja kwa moja kwa mzee Mwalami
ambako alikuwa na asilimia zote kuwa atawakuta.
Alijua hivyo kwa kuwa kipindi ambacho kijana
Katunje alikuja alimpokea yeye na ndie ambae
alimuelekeza kwa mzee huyo.
Umbali wa kutoka kwa mfalme Ngololo kwenda
kwa mzee mwalami haukuwa mbali ukilinganisha na
ule wa kutoka kwa mama Naomi. Utofauti kuwa
Naomi aliwahi kwa kuwa ni kijana na mzee
Mwalami pamoja na uzee wake ilikuwa ngumu
kutembea kwa haraka sana. Naomi alipokaribia
kwenye nyumba hiyo alisikia sauti za watu
wakiongea akafahamu fika kuwa wao wako ndani
alifungua furushi lake na kutoa kibuyu ambacho
alikabidhiwa na mama yake, kwa bahati nzuri mzee
Mwalami anakaribia na anafanikiwa kumuona yule
binti akiyafanya madudu pale kwake. "Pumbavuu
huyu binti hanijui vizuri na nilishamkanya mama
yake hii tabia". Alitembea taratibu kisha alipomuona
kuwa anataka kumwaga ule unga kwenye njia ya
kupitia mlangoni kwake akamshtua.
"Weee weee mwanaharamu...mkubwa wee huna
hata aibu unafanya nini hapo toka harakaa khaaa!"
Naomi alikurupuka kwa kukimbia na kuacha baadhi
ya vitu ambavyo alikuja navyo pale. Mwalami alifika
na kuviangalia na akagundua kuwa ni vya kichawi
"Looh! yani mwanamke mdogo anajihusisha na
mama yake kwenye uchawi sasa hivi navichoma
moto hapa hapa".
Aliingia ndani kwanza na kuwakuta wageni wake
wakiwa kwenye harakati ambazo walikuwa
wakizifanya hasa pale binti Mwaija alipokuwa
akijisikia hali mbaya tumboni mwake. "Jamani kuna
jambo gani tena hapa?" Mwalami aliuliza swali
"Aaah tunashangaa tu anasema trumbo linamuuma
sana hata hatufahamu nini hasa kimempata ".
Mwalami ilimbidi aliache swala la kule kuwapeleka
na ndipo akaanza kushugulika na binti huyo. Huku
na kule waliendelea kutafuta dawa ambayo
itamsaidia apone mapema sana.
Naomi alifika nyumbani kwa mama yake akiwa hoi
taabani. " Mamaaa mwalami kaniona" Naomi
alimuelezea mama yake jinsi gani lile tukio lilitokea
kule. "Kakuona haya mbona mimi nilishakurahisishia
kazi nimeshapiga bao kwa yule binti sasa wewe
unashindwa kumalizia!.." Mama huyo kumbe ndie
kasababisha hali ya binti Mwaija kuwa mbaya sana
akiwa na lengo la kumpoteza maishani mwake.
"Hapana mama nimefika nataka kuanza tu kama
ulivyonielekeza na yeye anatokea ndiopo nikakimbia
na hata hivyo kibuyu na ile dawa nimeiacha..."
Naomi alimhadithia mama yake kuhusiana na ile
dawa na kibuyu kukiacha.
"Mwanangu Naomii umeniuaaa tayarii haaa...haya
nenda haraka ukachukue kabla hata hajaiharibu
fanya haraka mjinga wee muone unakuwa
lizembelizembe sana". Naomi alisafiri tena kurudi
kule ambako anahisi kuwa atakipata au atakikuta
mzee mwalami akiwa kamlindia jambo ambalo ni
ndoto kwa mzee mwalami na watu kama hawa. Lile
lengo lake alilitimiza mapema sana kwani
alikichoma moto pamoja na ile Irizi. Naomi
alipofika pale aliweka mikono kichwani huku akitoa
machozi baada ya kuona vile vifaa vikiwaka moto
mkubwa tu tena wa kutosha usiohitaji kuni wala
kifuu ili kukoleza zaidi ya hapo.
Alirudisha miguu yake kinyumenyume, huku akiwa
haamini kabisa yale anayoyaona "Nitamuambia nini
mama yangu jamani mamaaaaaa". Aligeuza shingo
yake kwa mara ya mwisho kuusindikiza moshi
ambao ulikuwa unafuka pale kisha akaelekeza uso
wake njia ya kwenda kwa mama yake mzazi. Mama
yake Naomi uso wake ulionekana kubadilika na
kuwa rangi nyekundu uliovilia damu hii yote
kutokana na ile hali ambayo imetokea haswa
akihofia maisha yake kuwa mwisho kwa nyakati
ambazo ni mapema sana.
Naomi alifika nyumbani ndipo akapiga magoti ya
kumuomba radhi mama yake huku akitoa chozi la
hisia kujua kwa makosa yale ambayo kayafanya.
"Mama yangu nisamehe kabisa mimi, mzee
Mwalami kachoma morto vile vitu mamaaaa" Mama
Naomi alimtumbulia jicho mwanae "Naomiiii nini
etiii aaaah! nishakufa kabisa hapa ololooo". Baada
ya muda mama huyo alitulia na kumtuliza mwanae
kisha akamuambia "Mwanangu hapa hatuna jinsi
nasubiri maelekezo ya wakuu wa Nyamnyena
watakachokisema ndicho nitakifuata.".
Upande wa Mwalami alipiga jitihada zake zote
mpaka hali ya yule binti ikawa nafuu, " Jamani
naombeni msitoke humu ndani, ngoja niende
kuwaeleza kwanza kuwa imeshindikana na tutaenda
kesho yake pia nitaenda kumuita daktari wa mfalme
aje kumtibia zaidi".
Walimuacha mzee huyo aondoke na wao wakabaki
na mgonjwa wao. "Ndugu yangu katunje, hapa
kijijini nina wasiwasi napo mana ila ngoja tukionana
na huyo binti kama ndie yeye basi tunaondoka nae
kama si yeye hapa sina muda wa kukaa hapa".
Baada ya muda yani jioni sana ndipo mzee
mwalami anafika na kufungua mlango kisha kuingia
ndani na kuwakuta wakiwa wameshika tama
wakimzunguka mwaija. Mzee huyo aliandaa chakula
kilipokuwa tayari walikula wote kwa pamoja.
"Jamani asubuhi tunadamkia kwa mfalme tayari
nimeshamueleza lakini mzee Kelebu kashindwa
kufika kwa sababu alikuwa na shughuli na mfalme".
Majira ya usiku sana Mama Naomi na Naomi
mwenyewe walifika kwa Mzee Mwalami nje ya
nyumba hiyo. "Mwalami choonde sana tunakuomba
uturejeshee vitu vyetu tutakufanyia kwa kila kitu
ambacho utakitaka kwa sasa hivi tunaomba sanaaa
chondeee..." Walikuja kuomba radhi kwa mze huyo
ili waweze kurejeshewa vitu vyao. Mzee Mwalami
aliona kuwa ni upuuzi ambao wanaongea
aliwafukuza kwa kuwaambia kuwa ubishi wao
utawafanya wasitoke salama pale la sivyo
waondoke.Hawakuwa na ubishi waliondoka zao.
Asubuhi na mapema sana katunje anaonekana kulia
sana huku akitamka jina la mwaija, sauti hizo
ziliendelea na kuwaamsha wengine walio lala ndipo
kaka yake chito nae aliamka na kuangalia nini
kimejili. Hakika kumbe mwaija alikuwa tayari
kapoteza maisha. Walikuwa pamoja kutulizana
kwani tayari mwaija ndio hivyo kawatoka, Mzee
Mwalami nae aliwapa pole sana kwa lile tukio
lililotokea.
Waliamua kufanya utaratibu wa kuona nini
wanakifanya lakini kwa muonekano wa bwana
Mwalami alijua kuwa yule binti kauliwa kwa njia ya
kishirikina "Jamani huyu mwanamke wako kafa kwa
uchawi..na utaraibu wake lazima mapema hii azikwe
ili kuwafanya wasimfanye mfu hai tena mana
lilionekana kuwa ndio lengo lao..tukimzika hali kila
mmoja anaona mnazika gogo haki ya nani.."
Walifanya kila njia ndani humo walichimba kaburi
kwa haraka sana na kumzika kimila zao za Chamlo.
Baada ya pale waliombwa wasioneshe dalili zozote
za kufiwa kwani pia ni aibu sana mgeni kufia
kwenye eneo ambalo hata viongozi hawatambui na
alifanya hivyo ili kuwapa kazi wale waliomfanyia ule
unyama kwa makusudi ili wasifanikiwe.
Aliwapanga Katunje na Chito kwa ajili ya kuelekea
kwa mfalme huku akiwapa maneno ya kuwatia
nguvu "Ninachohitaji huku mkifika muonyeshe
hakuna kitu chochote ambacho kimetokea, pili nawa
ahidi kuwa tukirudi huku naenda kuwaonyesha yule
ambae kamuua mwaija". Japo maumivu walikuwa
nayo lakini walikubali kuyaacha na kufuata yale
ambayo yule mzee anayasema kwa kuwa wapo
ugenini.
Binti Lyoto akiwa kwenye chumba chake na binti
Mwana ambae ni kaka wa Zweli. Aliambiwa kuwa
amuandae vyema binti huyo ili akitoka nje onekane
kama mwanamke wa mfalme Bamuzi. Pia lengo
jingine ni kuonana na watu hao wambao wamenadi
kuwa lyoto ni mtoto wao. Bamuzi akiwa na baba
yake mzee ngololo "Baba unafahamu kama huyu
binti anafaida sana hapa kwetu?" " Haswaa
mwanangu ndio maana napenda sana asitoke hapa
kwenda mahali popote. Ghafla anatokea kijana
akiwa kwenye mwendo wa kasi sana, "Nini kijana
wewe unachokimbia kuna uvamizi?" Aliuliza Bamuzi
baada ya kumuona yule kijana akiwa hoi.
"Mkuu kuna watu wameingia ndani ya mipaka yetu
wapo wawili, wanakuja maeneo haya huku kwetu!.."
Bamuzi pamoja na baba yake walisimama huku pia
walinzi wakiwa tayari kwa amri ya kushambulia.
"Kuna watu wawili wamekuja kushambulia....eti
wana silaha hao wawili?" Aliuliza Bamuzi. "sifahamu
kabisa ila wanapoonekana kuwa ni watu hatari sana
mana wana mkuki...".
"walinzi wote hakuna abaki mmoja akiwa na huyu
Mwana akimuangalia Lyoto? na wewe binti
hakikisha kama mzee Mwalami anakuja na hao watu
msiruhusu kumtoa huyu binti mpaka tutakaporudi
sawa?" Hivyo basi mambo yakawa yameiva mzee
Ngololo akiongoza msafara pamoja na mwanae
huku pembeni akiwa bwana Kelebu na matibabu
yake. kwa wanajeshi watakao kuwa majeruhi."
Walitoka pale na walibaki watatu tu akiwemo
Mwana,Lyoto na mlinzi mmoja.. Wakati wao
wanaelekea huko mzee mwalami na wale wawili
wanafika pale wanakuta kimya "Mfalmeee wa
Chamloooo" Ilikuwa kama salamu ambayo alikuwa
anasalimia kama watakuwepo, ndipo mlinzi
akaeleza kuwa hawapo na wameenda mahali.
Walipata kuingia ndani humo. Mungu si Athumani,
Lyoto anatoka ndani na uso kwa uso na Mzee Chito
na Katunje kila mmoja walijikuta wanagongana
majina "Lyootoooo..." Katunje alitamka jina hilo na
chito nae " Sikitu mwananguuuu". Walitazamana
wote na Sikitu au Lyoto nae alivuta kumbukumbu
ndefu sana na kujua kuwa Sikitu ndio jina lake
alinyanyua miguu yake kumfuata Katunje kwa kuwa
ndie wa karibu kumjua mapema lakini Mzee Chito
aliendelea kulitamka lile jina la Sikitu kwa nguvu
zake zote ndipo sauti ya mzazi aliyepambana kwa
udi na uvumba kuhakikisha mwanae anapatikana
ilipenya barabara kwenye masikio ya binti huyo na
kumgeukia mzee chito "Babaaaaa....babaaaaa
mamaaa yuko wapi babaaa?". furaha yenye majonzi
mazito sana ndani yake yaliwakutanisha wana ndugu
hao. "Kaka chitoo huyu ndio huyo mwanao
aliyepotea kwani?" Katunje aliuliza "Ndio ndugu
yangu mwanangu huyuu mwanao huyuu uliyekuwa
unamlinda damu yako hiii" Chito alimsogelea
Katunje na kumuambia "Ndugu hapa tunaondoka
hakuna kusubiri chochote hapa kama mtoto
tumempata.." Mzee mwalami alishtukia hilo swala
lakini aliona awape njia na yeye amzuge mlinzi kule
aliko.
Hatimae wanafanikiwa kutoroka watu wanne
Katunje, chito, Sikitu, mwana na mwalami na yeye
aliunga kuondoka kabisa kile kijiji kwani alihofia pia
kufuatwa na wale wachawi sasa bora aondoke
kabisa kile kijiji. Safari yao ilipita maporini sana
kuogopa wakipita njia kuu watakuwa rahisi
kuonekana. Uande wa huku kwenye ule msafara
Walifanikiwa kuwakamata wazee wawili ambao
hawakuwa wenye madhara sana kwani ndio wale
wazee wa kijiji cha KILIMALONDO na si wengine
bali ni KAUZIBE na UDEVU.
Walikamatwa wale wazee hadi kupelekwa kijijini.
Kwa bahati mbaya wanakuta mlinzi akiwa kalala
fofofo kabisa hajitambui kabisa, Bamuzi humuambii
chochote kuhusiana na Sikitu, alimtafuta kwa
kumuita bila mafanikio ndipo alikuja kumuamsha
mlinzi laaah! alikuwa mbali sana alipoamka
anakutana na banzi la mgongoni na swali juu "
Tumekuacha ulinde watu je wakuwapi hao watu?"
Mlinzi alibahabahabuha hajui nini aseme
"Wamekimbia baada ya kunipa maji nikanywa
nashangaa napata usingizi..." Bamuzi alitaka
kumchoma kisu palepale lakini baba yake
alimkamata na kumtuliza apunguze jazba kwanza.
Wale wazee walihojiwa "Mnatokea wapi na
mmekuja kufanya nini huku?" Mzee Kauzibe kwa
kuwa ni mzee mjanja sana alijibu kwa ufasaha
"Ndugu zetu tunahitaji msaada wenu kwanza,
tumekimbia kijiji cha Kilimalondo baada ya
kutishiwa na kukoswa kuuliwa na kijana mmoja
anaitwa KATUNJE...." Bamuzi na Mzee ngololo
waliinuka "Katunjee?....unamjua wewe katunje?"
"Ndio huyu kijana alibahatika kumpata binti mmoja
ambae alimkuta akiwa na hali mbaya sana kijiji cha
Bwawani kipindi anamtafuta kaka yake Chito.
alivyofika pale huyo binti mimi nilimtibia mpaka hali
yake ikawa njema na tukamuita jina la Lyoto..."
Walizidi kuchanganyikiwa yale mambo kama
yanapangwa litoke hili liingie hili. "Mzee ebu malizia
kwanza hayo maelezo.." Mzee Kauzibe alihisi
jambo. "Sasa pale tuna mfalme anaitwa SWAI akiwa
na kijana wake KIMOLO kama mila zetu huwa Swai
huchagua mwali wa kulala nae sasa ikaangukia kwa
Binti Lyoto na mimi ndie niliyepewa kazi uya
kumpeleka...hapo ndipo ndipo utata ulipoingia
mpaka akatutaka sisi kutuua japo kweli tumekili
makosa yetu na hapa anatutafuta ndio maana
tukakimbilia huku..." Kila mmoja alikuwa hoi
"Poleni sana hapa unamuona huyu kijana kapaniki
kwa sababu ya binti mmoja ambae tulimuokota
mto ule ambao unatokezea kwenu huko kilimalondo
anaitwa lyoto katunje...." "Yani lyoto bado nzima
haki ya nani anapona sana huyu binti...nakumbuka
mimi kwa macho yangu anaangukia korongoni
humo wakati nataka kumkamata...sasa akiniona si
ataniua..."
"Hapana pia huyo katunje na na Chito wapo hapa
kijijini wamekimbia na Lyoto sasa walinzi tafuta
mkiwakuta kamata leta hapa mapema sana
tawanyika" .Walitawanyika na huku wazee hao
waliposikia kuwa wale watu waliowakimbia kule
bado wapo, waliama mapema sana na wao
wakakimbia kurudi kijijini kwao kilimalondo. Mungu
alisaidia wale na msafara wao majira ya usiku
wanapata bahati ya kufika kijiji cha Kilimalondo kwa
tena walijificha pamoja na wingi wote ule wanakaa
kwenye nyumba ya zamani ya Katunje.
"Haya karibuni poleni kwa safari ndefu..vipi kuna
mtu kaumia jamani?" Aliuliza katunje akitaka kujua
hali ya kila mmoja. Wale wazee walijitahidi asubuhi
na mapema ndipo wanafika mana usiku mzima
walikuwa safarini kurudi kijijini kwao kumkimbia
Katunje. Asubuhi na mapema kwa kuwa walijiamini
kuwa wako salama sana ndipo Mwana akakaa na
Sikitu pamoja na wale wengine wakianza
kukumbushiana na kupeana faraja. Ilionekana binti
SIKITU ana waza kitu akivuta taswira avute lakini
kama zinakataa. Walipanga siku ya pili yake ndipo
waondoke, kumbuka tayari binti Sikitu ana nguvu
zile alizopewa kama za umalkia ambazo kokote
kule aliko lazima zitamrudisha kule alikopewa
uongozi akaendelee kutawala. Majira ya usiku mzee
Kauzibe na Udevu walilala nyumba moja tu. Huku
Sikitu akili yake ikimtuma vibaya aliamka usiku
usiku na kwenda kwenye nyumba ya mzee Kauzibe
aliufungua mlango na kuwakuta wakiwa wamelala,
Sikitu alikuwa katili sana kwa muda huo
haikujulikana kwa nini anafanya hivyo mana
Alimtumbukiza kisu mzee Kauzibe na mwenzake
palepale wakaaga dunia na yeye akarejea nyumbani
na kulala kisha wakaendeleza basi la usingizi lifike
mji wa asubuhi,
Kabla jogoo hajawika tayari waliamka wakitaka
kujiandaa kuondoka wapite kijiji cha bwawani
kwenda kumaliza mambo yote kule na akataje
kama anamfahamu nani ambae kasababisha
matatizo yake mpaka wao wanahangaika kwa kiasi
kile kama mbwa walio kosa makazi.
Lakini safari yao ilikatishwa na vilio ambavyo
vilitoka mtaa wa pili. Katunje kwa kuwa ni mwenyeji
pale aliomba yeye aende kutafuta na kujua nini
tatizo ambalo limetokea huko au kuna tafrani gani
ambayo imejitokeza, alishangaa kuona kwenye
nyumba ya mzee Kauzibe mzee ambae alikuwa
anamkubali sana lakini alijawa na tamaa watu
wanalia huku akisikia sauti ya watu wakisema
kachomwa kisu tena wote Kauzibe na Udevu yani
hapa pamearibika cha kufanya tutafute wageni wa
humu.
Aliona litanuka muda si mrefu sana cha umuhimu ni
kwenda kuwaeleza kuwa waondoke mapema kabla
hata swala halijafika kwa mzee Swai. Alikimbia kwa
spidi zote hadi nyumbani kwake "Mnasikia kuna
wazee wawili wamefariki kwa kuchomwa na visu
sasa wanawatafuta wageni....tunatakiwa kwenda
Bwawani sasa hivi wasije kutukamata.....
>>JE SAFARI YA WAO KWENDA BWAWANI Mzee
SIKUJUA na Mzee MAPATO watakuwa salama
Mbele ya SIKITU aliyerudi kwa kasi kwa kuanza
kuwalaza chali wazee waliodiriki kutaka kumkamata
kumpeleka kwa swai.?
 
SEHEMU YA ISHIRINI NA NANE 28
Namba ya watsapp imetolewa kwa lengo ya wale
ambao wanataka kulipia hadithi hii watumiwe wao
wakiwa watsap akiona huku ni ngumu pia na kama
una maswali binafsi na si vinginevyo pia kumbuka
kuwa watsapp sina grupu
Endelea.........
...Waliungana watu wote yani mzee Chito, Mwalami,
Katunje, Sikitu na Mwana kuondoka na kwa kuwa
ilikuwa mapema sana ambapo kwa kijiji hiko ilikuwa
ngumu watu kutembea ovyo na kukutana na watu,
iliwawia ngumu wao kuonekana wakati wanaondoka
pale. Safari ilianza mapema sana huku wakiangalia
huku na kule kuhakikisha kuwa hakuna mtu ambae
atakuwa anawatilia kiwingu, lakini huku nyuma kila
mmoja akiwa na mashaka makubwa hasa yule
Katunje kuhusiana na kifo cha watu wale. "Kaka
unajua kuwa mpaka sasa sijaamini vifo vya wale
watu wawili!". Katunje alikuwa anajiuliza kwa
kumshirikisha kaka yake.
"Kwani unawafahamu hao waliokufa?"
"Haswaaa...nawajua vyema sana ndio mmoja wao
alimsaidia sana Lyoto..aah skitu". "Binadamu tuna u
yama sana haya tuwaachie wenyewe ngoja na sisi
tuelekee nyumbani kwetu". Wakiwa njiani ndipo
mzee Mwalami aliongeza katika hoja ile kwa
kuonyesha kweli wako pamoja. Kwa mwendo
waliokuwa wakitembea hakika sikitu na Mwana
walichoka sana hivyo iliwabidi wapumzike mahali.
Walitafuta mahali ambapo palikuwa kwenye mbuyu
mkubwa sana ambao uliweka kivuli kikubwa sana.
Wakati wanaendelea kupumzika alikuwa anafikilia
sana mambo mengi sana mzee Mwalami kitu
ambacho kila mmoja alikuwa na ulizo juu ya mzee
yule. Lakini bwana Chito hakuwa mzembe aliona
kukaa na kitu moyoni hawezi ilimbidi amuulize
"Mzee Mwalami, mbona uko hivyo sasa jamani
kama una mawazo huku ukimuangalia sikitu". Mzee
mwalami ilibidi apindue shingo yake kisha akacheka
kwanza "Hapana kuna swala nalikumbuka sana
mpaka sasa limenikumbusha zaidi ya zamani".
"Aaaakh bwana hapa sasa kama familia moja
hamna cha kuogopa zaidi ebu ongea kwanza ili
tujue tunakusaidia vipi" Hapo mzee mwalami
alionekana akikaa vizuri kutokana na ile staili
aliyokakaa mwanzo kuona inamchosha sana, kisha
akameza mate yake kwa uchache wa kukosa maji
ya kunywa.
"yani maisha ambayo kapitia Binti yako
Lyoto..mtanisamehe mana ndio jina nimelizoea
sana maisha yake ndio ambayo nilikuwa naishi
mimi nikiwa na miaka midogo sana.." Kila mmoja
pale kasoro mwana na Sikitu ambao walikuwa
wamelala kwa uchovu wa safari za kuunganisha.
"Ehee mapya hayo haya tuambie yapi ambayo
ulikuwa unaishi" Chito alihoji... "Nakumbuka sisi
tulizaliwa watoto wawili, Tulilelewa kwa muda mrefu
sana na wazazi wetu sasa baada ya mama yangu na
baba yangu kuuliwa kwa moto kwa sababu ya
ugomvi wa mashamba sisi tulianza kuishio kwa
tabu sana...Kipindi ambacho ilitokea vita ya vijiji
kugombea ufalme baada ya mfalme wetu kufa na
hakuacha mtoto hata mmoja sasa haikujulikana nani
ambae atachukua ule ufalme...watu walikufa sana
mimi nilianza kumtafuta ndugu yangu nikiwa mdogo
na huyo na alikuwa mdogo japo mimi ndie nilikuwa
wa kwanza kuzaliwa..hakika sikumpata ndugu
yangu na mimi nilibebwa na mzee mmoja ambae ni
Mzee Ngololo akaniondoa pale na kukimbia na
mimi akiwa kanibeba mpaka kijiji kile
chake...sikujua mpaka hapo ndugu yangu wapi
alipo na hata jina lake nimelisahau kwani tulikuwa
wadogo sana na kikubwa zaidi sijui yuko hai au laah
ndio maana nikikumbuka ya sikitu basi nalia sana
mana nilishasahau". Walijikuta wote wanaungana
kulia kiume.
Hadithi ya maisha ya Chito na Katunje yalikuwa
hivyo na yashatimia baada ya kuonana kwao.
Maisha ya Sikitu na baba zake yalikuwa hivyo na
yameshatimia, Walimpa imani kuwa ipo siku
atafanikiwa kumuona kama yuko hai. Pia chito
aliongea mambo mengi sana ambayo yalikuwa
yanahusiana na kile kijiji ambacho kimetokea,vilevile
walimuamsha Sikitu na kumkumbushia yale
yaliyopita kama atakumbuka. Alionekana Sikitu
kumkumbatia baba yake huku akilia kwa majonzi
sana hali hiyo ilionyesha kuwa yuko tayari na kila
kitu anakumbuka lakini hakutaka mzee chito
amueleze swala la mama yake mana itakuwa swala
lingine, lengo la mzee chito kufiuka ndani ya kijiji
cha Bwawani. "haya jamani tuinuke twendeni huko
mana si unajua kuwa muda tuwahi kufika na tujue
tunaenda wapi sasa baada ya hapo". Walisimama
na kila mmoja akiwa na nguvu nyingine ya
kuendelea na safari.
Waliongozana huku wakiwa kimya na kila mmoja
akifikilia maisha baada ya kukimbia kule kijiji cha
Chamlo yatakuwaje. Hatimae wanafanikiwa kukiona
kijiji cha Bwawani na kila mmoja alifurahi ila wale
wawili mzee mwalami na mwana walielekezwa
kuwa safari yao iko pale na itakuwa inatimia na
mambo yote yanaenda kufanyika pale na wale
wazee waliotajwa kuwa ni wasumbufu wanapatikana
pale.
Mzee Mwalami kama mtu mkubwa aliyekula chumvi
au munyu nyingi aliwasimamisha wote na
kuwashauri jambo. "Nawaomba munisikilize kwa
makini sana, nadhani kila mmoja ndani ya kijiji kile
wanajua kuwa SIKITU kafariki si ndio...sikitu
usijisikie huzuni tupo kukomesha upuuzi
waliokufanyia kama unawajua sawa.." "Sawa baba.."
Mzee mwalami aliendela kusema.
"Kinachotakiwa hapa tuingia msituni huku...ili
tujipange hata kutengeneza kitu cha kujihifadhi kwa
siku kama tatu hivi wakati tunaangalia jinsi ya
kuingia mana inahitajika kupasoma pale vizuri
sawa..".Baada ya kusema hayo kila mmoja
alikubaliana na ndipo wakageuza njia na kwenda
ndani ya msitu huo uliokaribu na kijiji hiko.
WAKATI wao wakifanya mipango hiyo. ndani ya kijiji
cha Bwawani watu walionekana kuwa na furaha sana
baada ya kuitwa na mwenyekiti SEMENI na
wakishangilia kwa kupiga ngoma na wanawake
wakicheza kwa furaha. Pale walionekana Mzee
MAPATO na SIKUJUA, walikuwepo pale na wao
wakishangilia sana. Haikujulikana furaha hiyo
imewajia kwa njia gani.
Baada ya muda kupita ngoma ilinyamazishwa na
wote wakakaa kwenye viti vyao huku wengine
wakilegea kwa ulevi wa pombe kali walizokuwa
wanakunywa. "Hayaa nashukuru sana kwa hiki
mlichoonyesha kuwa tuko pamoja sana sasa,
nadhani uadui umejulikana kuwa ulikuwa ni kwa
mzee Chito na ndugu yake katunje sasa tunatakiwa
kuishi kwa raha na furaha sana hatutaki mauaji
yoyote ambayo yalifanyika...sasa kabla sijamaliza
na kuwaacha muendelee na furaha zenu
nimkalibishe mzee Manyenye mzee mkubwa hapa
nimpe nafasi ya kuongea kwanza" Hapo ndipo mzee
wa makamo alijivuta kutoka kwenye kiti chake na
kuja mbele za watu, na kwa kuwa sauti yake ilikuwa
inakwaruza alafu pia ni ndogo sana iliwabidi watulie
kumsikiliza wakitarajia mazuri kutoka kwa mzee
huyo.
"Mimi kama mzee wa hapa napenda kutoa maneno
ambayo yatakayomuuma ajirekebishe mapema..."
Kwa kauli hiyo tu iliwafanya watulie na pawe kimya
kama wamemwagiwa maji ya baridi, ndipo mzee
huyo alianza kuwaangalia sana watu yani hadhira
ambayo anaiongelea ambao muda mfupi wametoka
kwenye furaha na yeye anaonekana kubadilisha
upepo wa furaha zao na kuwa huzuni.
"Nawaomba mnisikilize..najua mmetoka kufurahi
sana kwa neno kuwa hatutaki mauaji yaendelee
mnajua kuwa mwanangu kauliwa...hatuwezi
kufurahika na wauaji wakiwemo humuhumu kijijini.."
samahani mzee ja..." Alikuja juu mwenyekiti kutaka
kumsimamisha kwanza mana anaonekana kupeleka
upepo mahali pengine. "Hapana....kijana usidiliki
kunisimamisha wakati naongea mimi na wazee
waliokufa ndio tulikubali wewe uwe kiongozi...sasa
kuwa na adabu sawa..." Ilimbidi SEMENI awe
mpole ili aishi na watu na kumuacha mzee huyo
nuksi akiongea vitu vikavu.
"Sasa...fahamu kuwa siku zinaisha hapa hakuna
furaha zaidi ya kupumbazana tu...kama mnabisha
mimi nawafahamu wote ambao walimuua sikitu
mtoto wa chito na kumuua mwanangu mpaka sasa
wamenibakishia mjukuu wangu basi...nitajeee?"
Watu waliona kama maajabu ndipo wakasema kuwa
" Mtajeeee?......"
"Hapana siwezi kumtaja naamini wao wenyewe
watajionea na watapata adhabu kubwa sana
mbele..." Aliondoka na kuelekea nymbani kwake na
kuwaacha pale wakiwa hoi hawafahamu nini
kimekuwa ni nini?. siku ilikuwa imetimu kuisha na
usiku ulishaanza kuingia wazee hao wawili walikuwa
na mawazo kwa kila mmoja japo mipango yao
ilionekana kufikia mwisho lakini inagonga mwamba
baada ya mzee Manyenye ambae wanajua hawawezi
hata kumuingia. Majira kama ya saa nane usiku
anaonekana mwanamke akiwa anatembea kwa
mwendo wa maringo sana huku akiwa kashika kitu
ambacho hakikujulikana kwa haraka, mwendo wake
ulionekana kuelekea kwenye nyumba ya mzee
Sikujua, alipofika kwenye nyumba hiyo aliizunguka
kama dakika kadhaa kisha akafika mlangoni,
alionekana kutoa kitu ambacho kilifanana na kibuyu
hivi alionekana akiingiza mkono ndani ya kibuyu
hiko na kupaka kwenye mlango wa mzee huyo,
Ilikuwa ni damu ambayo haikujulikana kaitoa wapi.
Alama aliyoichora hapo ilikuwa ni X ambayo ilikuwa
imekorezwa vyema sana, baada ya hapo aliweza
kurudi kule ambako katokea. Pia kwa mzee Mapato
akiwa kalala alishtuka sana na kuamka "Mh! hii
ndoto mbona inanitishia hivi ngoja ifike asubuhi
nikamueleze bwana sikujua ila mh! mbona yale
maneno ya Manyenye yanaendana na hii ndoto?.
Aliendelea kulala.
Asubuhi na mapema sana mzee Sikujua aliamka
kama kawaida yake alichukua kiti ili aende kuotea
jua la asubuhi alipofungua mlango anataka kuufunga
baada ya kugeuka nyuma anashtuka na stuli
aliyoichukua ilimdondoka chini "Khaaa! hii si uchuro
huu jamani watu wananitaka nini mimi eeeh! wakati
tumeshatoka kwa mwenyekiti na kusema hatutaki
hata kutishiana vifo damu hii imekuja fanya nini na
nani kaiweka ?".Alipatwa na bumbuwazi la ghafla
sana wakati huohuo mzee mapato anaingia pale
anamkuta mwenzake akiwa haamini. " Vipi tena
bwana sikujua?" Mapato aliuliza "Ahhh! bwana
jionee nimeamka asubuhi nakuta hapa kuna damu
sasa sijui hata nani kaweka na akiwa na nia gani!".
"Yerewiiiiiiii.....haaa ndio hayahaya niliyoyaota usiku
jamani tumekwisha kabisa"> Mapato na yeye
alikuwa na yake hapo kwa kushangaa "Una maana
gani kusema hivyo?"
"Sikujua nimelala usiku nikaota kuwa tupo milimani
ambako kuna maporomoko makubwa sana sasa
tukashangaa maji wakati yanatoka milimani kama
kawaida sasa yanaanza kurudi kutoka bondeni na
yanapandisha mlima...kwa kuwa nina ujuzi wa
kutabiri angalau ndoto...nikaona kuwa mambo
yanatubadilikia tena sio kidogo makubwa kabisa
yani...kuona hilo sio tabu nadhani uliyoyafanya kwa
SIKITU yanakurudia na si wewe tu hata mimi....cha
kufanya hapa kesho ni kukimbia tu hatuna jinsi
tena."
Maneno ambayo hayakuwa na kipingamizi kabisa.
walikubaliana na swala la wao kesho yake ambayo
ni siku ya pili kuondoka pale. Taarifa hiyo ilifika
kwa mwenyekiti na kila mwanakijiji aliipata kwa
huzuni sana kuwa yuko hatarini kuuliwa kwa wale
ambao walitafsiri. Upande wa Sikitu na wengine
walikuwa wamemkamata sungura kama watatu
wakimfanyia utaraibu huku baba yake chito
alimuuliza swali " Mwanangu, usiku jana muda flani
sijakuona uliena wapi mana sikuwa na usingizi
mkubwa nilikuwa nawaangalia nyinyi tu.." Chito
aliuliza baada ya kuhisi kutowepo mwanae.
"Hapana baba nilienda mbali kidogo kujisaidia haja
kubwa" " Sawa lakini usijalibu kutoka peke yako
mana usije kukamatwa na wanyama wakali.".
Majira ya usiku kama kawaida, usingizi
ulivyowachukua watu wa Bwawani alionekana binti
yule tena asiyejulikana hata kwa jina. Alifikia
kwenye ile nyumba alichoamua kushika kile kitasa
kwa makini sana hatimae muda mchache sana
mlango ulifunguka kumbuka kuwa Sikitu ana nguvu
ambazo ziliweza kuwasaidia sana watu wa Chamlo
kwa hiyo kwa hili kwake ilikuwa dogo sana.
Aliingia ndani humo akamkuta mzee huyo akiwa
kalala fofofo, alichoamua kutoa kibuyu chake na
kutoa unga ambao alimpulizia puani ulikuwa kama
madawa ya usingizi kwa Sikujua alionekana
kuangusha kichwa kuonyesha hata kama alikuwa
anaweza kuamka akishikwa kwa hapo hatoweza
tena. Aalimfungua nguo ambazo alikuwa kavaa
alimuacha uchi kabisa kama alivyozaliwa. Kwa binti
huyo hakujali kumvunjia heshima mzee huyo
haikujulikana kwa nini anafanya hivyo na ana nia
gani baada ya hapo.
Alichukua tena dawa kisha akampaka kwenye
sehemu zake zote za siri kisha akamvalisha na yeye
akaondoka zake. Kama kawaida bwana Mapato
asubuhi mapema huwa anakuja kwa rafiki yake
Alishangaa sana kuona mpaka muda ule bwana yule
hajaamka na si kawaida yake kabisa. "Bwana huyu
kanywa pombe nyingi sana jana mbona mpaka sasa
ajaamka?" Aliingia ndani na kumkuta kweli akiwa
kalala, alimuamsha kwa haraka ndipo na yeye
akajikuta anakurupuka. "sikujua mbona mpaka sasa
hivi nini unaumwa au". Sikujua anashangaa kama
anahisi mabadiliko yametokea ndani ya mwili wake,
aliingiza mkono wake huku akitoa macho kama
panya kabanwa kwenye mlango "sikujua vipiwe mtu
mzima bwana unashikaje huko..."
"Mamaaaaaaa.....yanguuuu sio yangu hiiiii aah haaa
sio yanguuu jamaniiii..." Mapato alishangaa sio
yangu vipi tena kila akimtuliza sikujua haelewi
kabisa sauti alizokuwa akizitoa zilikuwa kubwa sana
sio yanguuuu... ilibidi ampige na kofi kali amtulize
"Mzee mjinga wee sio yangu sio yangu nini mbona
hueleweki eeeh". Watu waliokuwa wanapita walisikia
hayo maneno waliyokuwa wanaongeailionekana
kama ugomvi..
"Mapato ona sio yangu jamani yangu imekwenda
wapi aaaah!..." Alivua nguo zake na kumuonyesha
uchi wake na kuona uko wa jinsia ya kike tofauti na
yake mwenyewe. "Mamaa yangu haya sasa mengine
kabisa sikujua tumekwisha kabisa sasa hivi..".
Ghafla watu walijaa kwa wingi na hakuwa mbishi
aliwaonyesha watu jinsi ilivyo kwa hekma na busara
mzee Manyenye aliomba asifanye hivyo kwa walio
ona inatosha utakuwa unadhalilisha wengine. cha
kufanya kutulia kujua nini kimefanyika. Walimuita
Mzee Manuali ili asaidie kwani na yeye anayajua
yale mambo kidogo. Baada ya kufika waliingia
ndani alikuwa Mapato, susu,mwenyekiti, manyenye
na sikujua mwenyewe wengine wakitaka kusubiri
majibu hasa Ndunya, wakiwa ndani na muda huo jua
likizama na sikitu wanasubiri siku ijayo waingie
kijijini. "aaah katika kupiga mambo hapa naomba
useme ukweli mana hili sio tatizo dogo dawa yake
kusema yale uliyoyafanya inaonekana kama hii ni
laana"> Mapato alimfinya sikujua asiseme chochote,
Lakini sikujua aliona ni kitu cha kijinga kubaki vile
basi alivyoamua kusema ukweli tu. walitoka nje hadi
uwanjani na kusimama katikati ili aseme kile
ambacho alikuwa nacho kutoka moyoni. Alikuja
mwenyekiti na kusema haifai kwa wakti ule bado
wakishindwa ndipo aseme.
Ilishindikana kusema lolote,
Usiku wa kuamkia siku nyingine Binti yuleyule
alikwenda kwenye nyumba ya mzee Mapato na kwa
mzee huyo alimfanyia yale ambayo kamfanyia mzee
Sikujua. wakati anafanya juhudi ya kuondoka kwa
bahati mbaya hali yake inakuwa mbaya anazidiwa
na kuanguka chini, asubuhi watu walimshangaa
kumuona binti aliyefanana na sikitu hakika
walikimbia sana kwani walijua kama ni mzimu.
Hatimae walimshika baada ya kuhakikisha kuwa
ndie yeye. wakati huohuo Mwalami alifika kwa kuwa
yeye hafahamiki akiwa na katunje wanashuhudia
sikitu akipelekwa kwa mwenyekiti walirudi kwenda
kuwaita wale waliokuwa kule polini. hakika walifika
wote kwa pamoja na ndipo kila mwanakijiji
alishindwa kuamini kama kweli sikitu mtoto wa
chito au Mambo Sasa wapo pale. Ilibidi mambo
yaghailishwe na wapewe nafasi baada ya kupewa na
fasi iliyoombwa na mzee Chito. Haikujulikana hali
ya Mapato ikoje mana mpaka muda ule hakuamka
na sikujua kajifungia ndani kwa aibu aliyoipata. Kila
mmoja pale alikuwa hoi na haamini iliwafanya
kuambizana kila mmoja na eneo hilo walifurika watu
shinda hata siku zote ambazo walikuwa wanaitwa
na kuja pale.
Sikitu alikuwa na hasira sana, huku mzee Manyenye
alimuendea chito na kuongelea nae baadhi ya
maneno fulani ambayo hayakusikika kwa baadhi ya
watu.
"Haya katika mambo ya maajabu ndani ya kijiji hiki
pamoja na la leo hili, Huyu sikitu tulishajua kuwa
kafariki na leo anaonekana....sina mengi mana leo
najua yatatokea makubwa sana haya karibu mzee
manyenye." Mwenyekiti alimkaribisha Mzee
Manyenye.
"Jamani msishangae kwani mwanzo nilishawaambia
kuwa siku ipo kila kitu kitajulikana na niliongea jana
tu ila leo hii tunaona sasa mzee Chito au Mzee
MAMBO SASA karibu sanaa...". Kwa kuwa palikuwa
na heshima zake walitulia na mzee chito akaenda
mbele ya watu hao. wengi wao walikuwa
wanamuangalia Sikitu hawaamini jinsi sasa
alivyokuwa na kuwa mrembo sana.
"Nashukuru sana Mzee wa kijiji Manyenye,
nashukuru sana mwenyekiti Semeni, nashukuru sana
Mzee MANUALI kama yupo.." "Hayupo kuna tatizo
limejitokeza ila muda mfupi anakuja endelea"
Manyenye alimuambia. "Sawa ...Mwenyekiti
unakumbuka ulimfukuza kijana huyu mbele yako
miaka michache iliyopita?...huyu ni
KATUNJE..ndugu yangu mimi aliyenipotea kwa
miaka mingi na tukaonana, nililalamika sana kuwa
mwanangu kapotea hatukujua wapi kaenda kweli
ama si kweli?"
"kweliiiiiiiiii...iiiii.." "Nyamazeni sasa nampa nafasi
mwanangu sikitu aseme kila kitu". Watu walizidi
kunong`ona huku wakimsubiri sikitu akiwa anapanda
pale alipoitwa. "Nawashabahi nyoote..Kabla hata
sijaongea chochote nawataka wafuatao waje mbele
yangu ambao ni SIKUJUA na MAPATO nawatakaa
waje haraka sanaaa" Alikuwa analia sana huku akiwa
analia kwa uchungu.
Watu kama kawaida kwenye mambo kama hayo
huwa hawachelewi, vijana kadhaa walitoka na
kwenda kuwafuata hukohuko waliko, akiwemo na
kijana Ndunya alikwenda kwa mzee Sikujua ambako
anafika tu anakutana na sauti za vilio vya bwana
huyo akiwa na bwana Manuali akiwa anamtuliza bila
kujua kuwa yeye anahitajika sana. "Mzee sikujua
fanya haraka sana unahitajika na mwenyekiti kuna
mkutano wa ghafla kule". Alishtuka kidogo hata
hivyo mzee manuali alimnyanyua huku akiendelea
kumtuliza. Wengine walifika kwa mzee Mapato
ambako walimkuta akitaka kujinyonga kwa ile hali
aliyonayo kwani na yeye jinsia yake ilibadilika.
Walimuondoa kwenye kitanzi na kuondoka nae hadi
kule kwenye kikao. Sikujua alikuwa hoi na tumbo
kuwa na joto baada ya kumuona Sikitu akiwa mbele
yake. Sikitu aliendelea kusema. "Nashukuru kama
mmefika hapa. "
"Mzee sikujua nataka uje useme upuuzi wote
uliofanya..je mzee huna mjukuu kama mimi
unadiliki kutaka kuniua unanibaka sikujua kwa
kudanganya utamsaidia baba yangu...mnashirikiana
kumdhulumu baba yangu mnanitupa polini aaaah
jamaniiiiii utu wako uko wapi jamani...hakika kama
hukusema chochote nakuua sikujuaaaaaaa..."
Alianguka chini kwa hasira ambazo zilimpelekea
kuzimia..........
 
SEHEMU YA ISHIRINI NA TISA 29
Endelea..................
...Ndani ya kijiji cha SHISHIMO mambo hayakuwa
mazuri sana wakati huohuo watu wamechanganyiki
wa ndani ya kijiji cha BWAWANI. Watu walionekana
kuwa na hasira sana kwa kuhisi jambo ambalo kila
mmoja hakutaka kulisikia bila kumuadhibu kabisa
yule msemaji. Wachache walienda kumpulizia
SIKITU baada ya kupoteza fahamu, akili ya mzee
chito ilihama kabisa pale na kuwaangalia sana wale
wazee waliofika ambao nao walikuwa wanaficha
sura zao kwa aibu ambazo walikuwa wanaziona.
Mzee SIKUJUA alipanda kwa woga wote lakini
vijana walimpeleka kwa nguvu zote hadi alipofika
pale juu. Mzee huyo alibaki kulia kama mtoto
mdogo mbele za wanakijiji ambao walikuwa tayari
kumsubiri kwa hamu atoe kile ambacho kaambiwa
aseme. Aliendelea kulia lakini njia ambayo aliiona
kuwa itamsaidia basi alivua suruali yake na kubaki
uchi wa unyama lengo aonyeshe zile nyeti zake
ambazo zimebadilika. watu wakubwa kwa watoto
walifumba macho kutohitaji kuona yale ambayo
anayafanya bwana huyo.
Njia hiyo ilimsaidia sana pamoja na rafiki yake
MAPATO kwani walikimbia ovyo, walishindwa
kuwakimbiza kwani walibaki kuwacheka japo ndani
yake waligundua mambo fulani. Muda ulipita
walikutana baadhi ya wazee wakiwemo bwana
MANUALI, MWALAMI, CHITO, KATUNJE, SEMENI na
MANYENYE. Wakati wanawake waliwaandaa wale
wageni wawili yani Sikitu na Mwana mahala pa
kupumzikia kutokana na hali ya sikitu. Huku wazee
hao walizidi kuongea ndipo mambo mengine
yaliibuka baada ya bwana Mwalami wa Chamlo
kumgundua kuwa Manuali wa bwawani ni ndugu
yake wa damu. jambo hilo lilikuja baada ya kueleza
historia nzima ya chito na katunje, katunje na Sikitu,
chito na sikitu ndipo mzee mwalami akaingizia yake
hapo ndipo hata mzee Manuali alifahamu kuwa ndie
kaka yake kabisa ambao waliachana miaka mingi
iliyopita.
Kila mmoja alifurahi sana walikumbatiana, kwa hiyo
sasa ikawa mzee mwalami si mgeni tena pale na
alichukua jukumu la kumlea Mwana ambae na yeye
alikimbia pamoja nao, "Ndugu zangu nawashukuru
sana kwa kunisaidia kumpata ndugu yangu..alafuuu
yule binti kwa kuwa kijana hapa hana mtu anaweza
akaelewanan nae akamuoa kabisa Mwana"
walicheka baada ya kuingizia yale maswala. Majira
ya usiku na wahenga wanasema kuwa usiku ni
mrefu sana hivyo akili ya SIKITU haikuridhika
kuwaacha wazima wale watu ndipo alipowalaza
fofofo wale aliokuwa nao karibu na yeye akaelekea
kumsaka mmoja hadi mwingine.
Kwa bahati yake alifika kwenye nyumba ya mzee
Sikujua alifungua mlango japo walijitahidi kuubana
aliwakuta wakiwa wote wamelala, binti huyo mzuri
wa moyo aliununua ukatili wa ghafla kabisa ndipo
akamkata kisu cha shingo kila mmoja na hapohapo
akasababisha vifo vyao, damu iliyomwagika kwa
haraka zaidi ikiruka kutoka kwenye miili yao ilimfikia
japo hakujali zaidi. Kwa unyama alioufanya ule
mwili wake ulisisimka kuwaona wale watu awahemi
tena, alijiuliza mara mbilimbili kuwa kama kweli
wamekufa.
Uoga aliokuwa nao alijishtukia jogoo linawika na
yeye hajatoka mule ndani, wakati huohuo usiku
walikuwa wanamtafuta baada ya kugundua kuwa
SIKITU katoroka au kakamatwa kwa awamu nyingine
kama mwanzo. juhudi zao zilizaa matunda baada ya
kumuona asubuhi hiyo binti huyo kwenye nyumba ya
Mzee sikujua, akiwa nje ya nyumba kwenye mlango
akihema huku akiwa ameshikilia kisu chake na
mkono ukitetemeka. Watu ilibidi wamuogope na
wasimsogelee kabisa kwani alionekana si mtu wa
kawaida. Baba yake na Katunje pia walikuja. CHITO
ambae ni baba yake alishika kichwa chake kwa
mikono miwili.
"Mwanangu sikitu umefanya nini tena, mamaaa nini
umefanya huko ndani..." Sikitu alianza kuangua kilio
cha uchungu sana alianza kujongea pale walipo
watu ndipo walianza kumkimbia, wengine wali[pata
nafasi ya kwenda kuangalia ndani nini kakifanya.
Ripoti ilifika kuonyesha kuwa wale wazee wakufa
"Aaaah hakika huyu mwanamke ni muuaji kabisa
kawachinja kabisa wote yani kwishaaaaaaa
woteee.....". Kila mmoja alibaki na majonzi mazito,
vijana walinda ulinzi kama sungusungu wa pale
walimkamata kwa umaridadi mkubwa na kumpeleka
eneo husika ambako huwa wanafungwa watu kama
hao.
Chito, Manuali, mwalami, katunje waliingilia kati lile
swala kuwa wampe nafasi aseme kwanza "Hatuwezi
kumkamata sawa hata kama kafanya mauaji,
tumsikilize maelezo yake ndio ambayo yatamfunga
au kumuacha huru huyu mtuhumwa.." Maelezo ya
mzee Manuali yalitia moyo na kupunguza jazba ya
watu waliokuwa pale. SIKITU alipandishwa kwenye
eneo ambalo kila mmoja alikuwa anaweza kumuona
lengo la kufanya hivyo ili aseme kwa nini kaua watu
wale tena kwachinja kama kuku.
"Haya mimi kama mwenyekiti, nakuomba utueleze
hapa mana tuna kesi nyingi za mauaji na leo wewe
umezifanya dhahiri kabisa tena mwanamke..." Sikitu
hakuogopa jambo mana aliamua lolote liwe kwa
muda ule ila dhamira yake imetimia."Sawa.
..nakumbuka kipindi baba yangu anataka
kunisomesha, alinunua mikorosho kwa mzee
Sikujua.lakini mzee huyo alimsaliti baba kwa
kumuibia mikorosho akiwemo na huyu
mwenyekiti..." Mwenyekiti aliposiikia katajwa aliruka
kwanza toka pale alipo "Weeee....kwangu alikuja na
ushahidi sikumdhurumu kabisa mimi tafadhali..alafu
ongea vitu vyenye ushahidi..."
"Pia..baada ya hapo...mzee sikujua alinitaka mimi
niende kwake, ili nikachukue ujumbe ambao alitaka
kumpa baba kwa kuwa waligombana...Baba na
mama walienda kwa Mapato..mimi nikaenda kwa
sikujua..mzee huyu aliniingiza ndani..akaniziba
mdomo sikuweza kutoa sauti ndipo akaniingiliaaaa
.....aaaah mamaaaaa..." Sikitu alianza kulia huku
akiongea kwa kwikwi..watu walimsaidia kulia kwa
kuwa iliwauma pia kwa yale ambayo kafanyiwa.
Ndipo walimbembeleza ili aendelee.
"..Nilipoteza fahamu kwa kuwa alihalibu usichana
wangu nikiwa bado mdogo,...nilizimia sikujua nini
kinaendelea..nakumbuka niliamka nilijikuta niko
kwenye tenga ambapo mimi nimefunikwa na
kiloba.nilijitahidi nikatoka..nguvu sikuwa nazo njaa
ilinikuta, mwishowe nilizimia tena...Fahamu yangu
ilirudi najikuta niko bwawani..sikujua nani ambae
kanipeleka kule..lakini nikashukuru Mtu akaja
kuniokoa akanitibia nikamfahamu kama
Katunje..mika ilipita alipambana kuwazuia wale
watu waliokuwa na nia kama Sikujua..hatimae
nilipatwa na ajali mtu alinikimbiza kunifanyia
mabaya nikakimbia nikaangukia korongoni...sik
uumia..niliokotwa hadi kijiji kingine ambako
wamenisaidia pia mpaka baba leo niko nae,
sikuona umuhimu wa kuwaacha hawa wazee wawili
wanaoshirikiana kuharibu ndoto za watu...."
Maelezo hayo aliyoyatoa yaliwafungua bongo watu,
kiasi kwamba hata mzee Manyenye alikuja kusema
swala la SUSU na Mama MENGI yaliyowatokea.
Mpaka hapo walimtuliza na wao wakazika wale
watu. Baada ya siku kadhaa familia ya Chito akiwa
na mwanae na nduguye walikaa pamoja, lakini
tatizo lilikuja kwa Sikitu "Babaa...nimevumilia sana
nimechoka.." "Nini tena mwanangu ulichochoka.."
Baba aliuliza
"Nataka kujua mama yangu yuko wapi la sivyo
najiua kesho hutoniona mzima..." Aliongea kwa
jazba mpaka katunje na Chito waliogopa, Ilibidi
wamsimulie ukweli kabisa halisi ambao ulihitajika.
Majonzi yaliendelea kutokatika na yalifanya kama
ndio nyumbani kwake humo. "Baba asikubali
aliyesababisha kupotea kwangu na maisha yangu
kuwa magumu sikumuacha hai.. iweje huyu
aliyempoteza mama yangu nimuache naomba kesho
tuende hukohuko kwa babau la sivyo hutoniona ni
bora na mimi akaniue na si kubaki hali mama yangu
kafa".
Hakika ilikuwa kasheshe yani SIKITU kachachamaa
hataki ujinga tena. hali mama yake hamuoni.
Ndani ya kijiji cha SHISHIMO, mambo yalicharuka
baada ya kijiji kuwaka moto. ulionekana upepo
mkubwa ukivuma maeneo karibia yote jambo
ambalo lilifanya kila mwanakijiji ajiulize kulikoni kwa
siku ya leo. Kwa bahati mbaya zaidi kuwa watu
walionekana kufa baadhi yao miili yao ikiwa
imeanza kutapakaa zaidi na zaidi. Nyumbani kwa
mzee MAMBO SASA akiwa na NYANDU walikuwa
wanaendelea kuimba nyimbo za kichawi, khafla
alijitokeza mtu asiyejulikana wa aiana gani mana
yuko mwenye shepu tofauti na binaadamu wa
kawaida. Baada ya kukaribishwa ndipo akarudi
kwenye umbo lake la kawaida.
"VIJANA....NIMEWATUMA KAZI HAMTAKI
KUFANIKISHA SASA NITAUA KILA MWANAKIJIJI WA
HAPA.KAMA HAMUMLETI SIKITU NAUA KILA
MMOJA..TAARIFA NAWAPENI FUNGENI SAFARI
MKANILETEE SIKITU KABLA HAJAFIKA KWENYE
ARDHI HII.." Jitu hilo lilondoka kimiujiza huku
akiwaacha wale watu wawili wakiwa wanaduwaa
hawajui nini waseme hata. "Umejua ana maanisha
nini?" Nyandu aliuliza "Hapana" "Anamaanisha kuwa
SIKITU huyo anayemuhitaji umtoe kafara..yuko njiani
yani karibu kuja hapa sasa tujipange leoleo
tuangaze anga lote tutazame anakuja kupitia wapi.
Kweli Bila wao kufahamu kuwa sikitu sasa ni mtu
mwingine kabisa kaja kwa njia ya kumaliza upuuzi
wote, usiku kama walivyoahidiana walijipanga
kutazama kila baadhi ya vijiji ambavyo walihisi
kuwa atakuwa karibu, safari yao ilianza ndani ya
kijiji cha KALULU, ambako hawakufanikiwa kuona
kitu Waliongoza kwenye kijiji cha MIPINGONI
ambako nako walikosa lakini kumbe mzee UPENGO
alishawaona wakiwa kwenye rada hizo, alitikisa
kichwa huku akionyesha kuwa ytuko tayari "Hawa
wachawi wanapita anga zangu wananitafuta, huku
kuna nini mpaka waje ngoja sasa niwaendee
kulekule kesho pumbavu zao.."
Walirudi wakasafiri ndani ya kijiji cha bwawani
ambako waliona dalili nyingi za kuwepo sikitu,
walirudi baada ya kujua kuwa kweli wanahitaji njia
ya kumzuia kisha wamkamate akiwa nje ya kijiji
hiko. Asubuhi ambayo ilisemwa familia ya watu
watatu waliondoka Bwawani bila kutoa taarifa na
kuja kwa baba yao, ambae kawaandalia chai ya
asubuhi yenye maumivu. daaah kweli mchawi hana
huruma. Wanaingia ndani ya kijiji hiko tu Sikitu
anapata wasiwasi na katunje nae dawa yake
inambana kuhashiria kuwa kuna hatari kubwa mbele
yao.
Sikitu hakuogopa alipita na kila alipopita ilionekana
kuvunjwa kwa ngome ya kichawi iliyowekwa na
babu yake. Mzee Mambo sasa alishtushwa kuona
ugeni mkubwa hasa kijana Katunje kwa kuwa miaka
mingi hakumuona. Mzee alikuwa mstaarabu wa
usoni alivyoona kuwa mambo magumu alimkimbilia
na kutaka kumkumbatia, katunje alimsukuma kama
si baba yake wa kumzaa. "Mwanagu ulikuwa wapi
mwenzako nilikuwa nakutafutaaa nilimtuma kaka
yako aje kukufuata huyo kweli mnapendana eheee
huyu ndio SIKITU..Sikituuu..sikituuuuuuu" Neno hilo
lililtia shaka mpaka ilikuwa inasoma mara kwa mara
kwenye vichwa vya watu.
"Weee baba mnafiki, mchawi, muuaji hupaswi hata
kuonekana...wee baba nimesikia umemuua mama
yangu na ukatulisha nyama yake, hukutosheka
ukamuua mkweo ukataka kumlisha nyama kaka ona
sasa huyu mwanae analelewa na nani na anamtaka
mama yake...mimi ndio maana niliondoka mapema
sana sikutaka kuoan haya mambo yako..." "Wee
keleleeee pumbavu huna adabu mmekuwa sasa hivi
ngoja niwaonyeshe mana mnanipanda kichwani.......
.." Alianza kuimba na kupuliza filimbi yake mla
Nyandu akaja akawashika kiurahisia sana na
wakaingizwa ndani mwake.
"Mambo sasa haya tumewashika, tumuite
Nyamnyena aje kumchukua sikitu...". Hakumaliza
hata kusema lolote mshale ambao haukujulikana
unatokea wapi, ulisiganisha mbavu za Nyandu
kuanzia upoande wa kushoto hadi wa kulia.,
Palepale alidondoka. Mambo sasa alibaki kutoamini
kabisa. alitaka kukimbia mara mzee upengo
akamkamata "Unaenda wapi wakati nilimtuma
mwanao aje kukupa taarifa kuwa siku yeyote nakuja
kukusalimia sasa unataka kunikimbia jamani kweli
urafiki gani huuu..."
".....Rafiki hawa si watoto wako kwa nini unadiriki
kuwafanyia hivi huoni hata huruma kabisa ebu
badilika najua rafiki yako alikuwa anakudanganya
wewe ni mtu mzuri sana bwana....haya ebu kunywa
hii dawa kwanza.." Alitoa kibuyu akampatia mzee
huyo anywe.
"Ukinywa hiyo inakuondoa ujinga wako wote sasa na
hilo nyamnyena lenu nitalivunja sasa wewe kunywa.
"
"..Hata kama nikinywa niliyoyafanya sipaswi
kusamehewa..ni bora ukaniua mape,a mana nahofia
kuteseka na kuwaona watoto zangu wakiniona
mbaya niliyebadilika..."
"Babaaaa kunywa ile si akili yako baba kunywaaaa
haraka..." Kipindi hiko mingurumo kama ya simba
hivi ikiendelea ndani humo nayo ikisema "MAMBO
SASA UNATAKA KUTUSALITI...HAKIKA USINYWE
HIYO DAWA AHADI YETU WEWE NI KUWA MFALME
WA DUNIA SASA UKINYWA UTAWAUA WENGI
KAMA NILIVYOKUAHIDI MWANZO..."
Mzee huyo, alichanganyikiwa akifanya mkono wake
utetemeke kwa nguvu sana chozi lilimtoka kwa
wingi hajui nini afanye watoto wake pia wakiendelea
kumsii baba yao anywe ile dawa aliyopewa.
"Mambo sasa hatuitaji kukulazimisha kunywa hiyo
kwa ridhaa yako...ila kumbuka kuwa wewe na mimi
tulikuwa kitu kimoja..nikakuacha wewe huko uliko
sasa kama unataka kuwa mfalme wa kichawi
wamalize watoto wako alafu tuone nani ambae
atakuwekea maji ya moto wakati wa baridi au
ukiumwa....fikilia sana mimi sikutaka kukuua kwa
kuwa watoto wako walikuja kuniomba ndio maana
nilimuua huyu anayekushauri ujinga..."
Kwa ujasiri uliokuwa mkubwa sana alikunywa ile
dawa. Ndipo sauti ya lile shetani la kichawi
lilipotamka "UNANIUAAAAAAaaaaa". Mwili wa mzee
huyo ulitokwa na jasho alianguka chini huku akipupa
pupa kama kuku ambae aliyechinjwa na kuachwa
mara moja.
Mwili wake ulijaa mavumbi mengi kwa kuwa ilikuwa
kazi kubwa sana baada ya kunywa mzee wa watu
alihangaika sana mpaka pale alipotulia, Mzee
Upengo alimtikisa kumbe alikuwa kapoteza fahamu
"Msijali atakuwa sawa tu akirudisha fahamu atakuwa
vyema kabisa.."
Walimshukuru sana mzee huyo ambae kaja kujitoa
kwa ajili ya kumsaidia baba yao.
JE AKIAMKA MZEE ''MAMBO SASA'' NINI
KITAFUATA
 
SEHEMU YA THELATHINI 30 (MWISHO)
THE END OF JOTO LA MSHUMAA.
KARIBU "MAISHA HAYA ZAIDI YA KURUTA"
ENDELEA.............
HADITHI ZA Author Mudhihili KWA SASA ZITAKUWA
ZINAPATIKANA SEHEMU MBILI TU KWENYE PAGE
YAKE INAYOITWA Riwaya za Mudhihili NA KWENYE
GRUPU LAKE LINALOITWA Maisha & Hadithi FANYA
HIMA KUWA NDANI YA HIZO SEHEMU MBILI
KUPATA BURUDANI ZAIDI AHSANTENI......
.....Mzee Upemgo alisea kuwa mzee huyo atakuwa
sawa endapo akizinduka muda wa hapo baadae.
Kila mmoja alikuwa kimya sana kutazamia zaidi
majira gani ambayo ataamka. Mzee Upengo
aliwasihi mambo kadhaa ya kuyafanya kabla ya
kuondoka.
"Sasa mnatakiwa kuwa makini sana maana mizimu
ya Nyamnyena itakuwa bado haijaishiwa nguvu na
endapo wakija mimi nitapata taarifa nitakuja mara
moja kuimalizia mbali....alafu huyu akiamka hapa
atakuwa hana nguvu mtampikia uji mwingi sana
ambao mtachanganya na hii dawa muhakikishe
anakunywa sawa?" Waliitikia kwa pamoja wote
watatu na mzee huyo muhimu kwa wakati huo
akaondoka zake. Huku nyuma wakiwa wamebaki
watu watatu yani Katunje Chito na Sikitu, walikaa
kwa pamoja na kupanga kujua wanamsaidiaje zaidi.
"Babaa haya mimi nahitajika kurudi kule ambako
yuko mume wangu Bamuzi siwezi kukaa huku
kipindi chote". Walimshangaa sana baada ya kutoa
ile kauli "Khaah! mwanangu kumbe kule ulikuwa
umeolewa yani bila hata taarifa ila haina shida
utakaa na sisi kwa muda na tutakupeleka huko".
Muda mchache walimsikia mzee Mambo sasa
akiomba maji ya kunywa, roho zao zilifurahi sana
kwani kila kitu waliona sasa kipo sawa bin sawia.
"Mpeni maji huyo haraka sana " Katunje alikwenda
kumpa maji ya kunywa alikunywa yote huku
wakimuandalia uji kama maelezo yalivyotakikana.
Waliweza kutia na ile dawa baada ya kumnywesha
uji wote alidai mwingine walifanya hivyo kama mara
tatu, hakika alipoteza nguvu sana. Siku ya pili
Alikuja mzee Upengo pale na kujua maendeleo ya
mgonjwa huyo.
Kufika kwa bwana huyo Mzee Mambo sasa alijihisi
huzuni sana na aibu kubwa kwani hata akili yake
ilirudi ile ya zamani na kukumbuka yapi kayatenda.
Machozi yalianza kumbubujika kwa wingi huku
akiwaangalia wanawe ambao nao pia walikuwa
wanamuangalia. Mzee huyo Upengo alikuja karibu
na kuchutama na kumsalimia "Habari yako bwana
wewe". Alikuwa anaulizwa lakini alibaki kulia tu,
alimfuta chozi kisha akarudia kumuuliza kwa mara
ya pili "Habari yako mzee Mambo sasa wewe ni
rafiki yangu bwanaaa yaache yaliyopita" Aliitikia kwa
kichwa ndipo mzee huyo akawaita wote na kuwapa
maelekezo.
'Naomba mnisikilize jambo liliobaki ni la huyu mzee
kwenda kule ambako alikuwa anachukulia kazi yani
kwenye mizimu yao akiwa peke yake akachome
yale ambayo yeye aliandaliwa ili baadae awe
kiongozi " Chito alidakia kumuuliza swali "Sasa
hapo mzee huko hakutokuwa na shida akienda peke
yake ?" Mzee upengo alikaa kimya kwa sekunde
kadhaa "Ndio shida ipo sio kubwa sana ila lazima
afanye hivyo kuokoa maisha ya hawa wengine sawa
jamani?" Waliitikia lakini Mzee upengo alimuita
Chito pembeni na kumuambia jambo ambalo
alishtuka kiasi lakini alitulizwa kwa maneno ya
hekima.
Hayakujulikana ni aina gani ya maneno ambayo yeye
kapewa. Mzee huyo alimuendea Mambo sasa na
kumuambia maelezo yale aliyokuwa anayatoa pale
kuwa kesho yake ajiandae na afanye kila njia
achome hiyo mizigo haraka kisha arudi pale na
atakuwa salama kabisa. Mzee Upengo aliondoka na
kuwaacha wale wakiwa pale lakini Chito alionekana
kulia lakini haikujulikana kwa nini yeye analia.
Maandalizi ya kesho yake yalianza walimuandalia
kifungua kinywa kama mzazi wao ndipo asubuhi
hiyo anataka kuondoka lakini aliwaita wote akakaa
nao chini akawaeleza jambo moja ambalo alikuwa
nalo kabla hajaenda.
"Wanangiu samahani sana nawaombeni samahani
kwa yote niliyoyafanya bila hata kujielewa yani kwa
tamaa ambayo ilinikuta. lakini mmefanya jitihada
sana kuniondoa kwenye upuuzi ule..pia mimi nakili
kweli nilishilikiana na rafiki yangu Nyandu kuwauwa
watu tulianzia kwa wazazi wake, kwa mkewe na
mimi nikamuua mama yenu..mpaka mkwe wangu
mama wa mjukuu wangu Sikitu pia nilitumwa
kumuua mjukuu wangu sikitu lakini ikashindikana.
nawaombeni samahani sana jamani na nawahidi
naenda kujitoa lazima nikafanikishe haya yote na
sasa nawaacha kama sitorudi muwe radhi na mimi".
Alimaliza na kuinuka na kuelekea njia ambayo
inaelekea shambani kwake. Walibaki kulia tu na
kuhuzunika sana kwa yale ambayo wanayaona na
waliyasikia kwa macho yao. Hawakuwa na jinsi
walimuombea tu baba yao arudi salama. Mzee
Chito alibaki akiwa hana hili wala lile ndipo akapata
wazo ambalo lilikuwa zuri sana "Sikitu na Katunje
nawaomba niwaambie kitu mnisindikize kijiji cha
KALULUL nimpeleke Sikitu akawaona babu zake na
Bibi pamoja na ndugu wa upande wa mama yake.
Sikitu alifurahi mno, Safari ilianza kuelekea kwa
Wazazi wa Mama wa Sikitu. Safari yao ilichukua
muda mrefu kidogo ndipo wanafika ndani ya kijiji
hiko cha Kalulu. Wanafiuka kwenye nyumba ya Mzee
SUEDI ambapo wanakaribishwa lakini mzee huyo
alipowaona tu alikunja sura na kutaka kuufunga
mlango wake. Chito aliushikilia na kumuomba
kwanza wasikilizwe yapi ambayo anayo yeye na
anataka kumueleza, Alikubaliana na yote lakini kwa
shingo upande, waliitwa familia nzima wakakaa
tayari kusikiliza maelekezo kutoka kwa bwana Chito
na jopo lake, kwa kuwa yeye aliolea pale hivyo kiasi
anajulikana.
Alianza kwa kusema. "Nawaombeni radhi kwa
kutokuja kutoa taarifa yoyote kuhusiana na mtoto
wenu..lakini bila kuficha mengi yametokea yalikuwa
ya kifamilia na niliogopa kuja kutoa ushahidi bila
kuwa na ukweli wowote ule. Naumia sana pindi
ninapowaona nyinyi wazazi na ndugu wa mke wangu
na kuwaambieni kuwa mke wangu kafariki
duniaaaa...." Walishtuka kwa pamoja na ndipo
ugomvi ulianza watu wakisema haiwezekani na
wanamtaka mtoto wao, Mwenyekiti alikuta ugomvi
huo na ndipo alipoingilia na kuweka mambo sawa
na kila mmoja akawa anasikiliza nani anasema kwa
utaratibu.
Lakini sasa kaniachia mtoto huyu hamkumfahamu
anaitwa Sikitu tumepitia mengi lakini
yalisababishwa na baba yangu mpaka sasa
tumefanikiwa kumbadilisha, nimekuja kutoa taarifa
na kuwaonyesha mtoto huyu na saa kiongozi ndani
ya kijiji cha Chamlo kwa mfalme Ngololo na mtoto
wake Bamuzi ndie aliyemuoa huyu.Walimpokea na
hapo walikaa siku mbili baada ya kila kitu
kuishakazi ambayo ilibaki ni kumrudisha Sikitu
ndani ya kijiji cha Chamlo. Safari yao ilianza.
Upande wa mzee Mambo sasa anafanikiwa kulipata
furushi ambalo alielekezwa kulifanyia kazi, na
hatimae analiunguza moto palepale lakini sasa kwa
bahati mbaya siku si nzuri kwake moshi wa vitu
hivyo vinamuathiri na kumteketeza kama vumbi na
kupoteza maisha yake kabisa. Maisha ya Mzee
Mambo sasa na mambo yake yote yanaishia
palepale alipokuwa anachoma na inabaki stori tu
kuwa alikuwapo mzee mambo sasa mwenye
mambo ya kizamani.
Safari ya watu hawa sasa ilianza kwenda kuelekea
ndani ya kijiji cha Bwawani, ambako walipofika
walipokelewa vyema sana kwa vishindo, Wanakijiji
walikusanyana kwa pamoja na kuwapongeza kwa
ushujaa wa kuwavumbua wabaya na hatimae
walikufa kwa ubaya wao kweli mwisho wa zambi
mauti, Mwenyekiti akiwa na jopo la watu wengine
kama Manyenye walimuomba mzee chito abaki pale
kwani wanampenda bado. Alichokisema bwana
Chito kuwa bado wanasafari ndefu ambayo
wakisharudi watarejea pale kwa maisha yao yote,
Bwana Manuali, Susu, Mwalami na Mwana
waliungana kwenye safari hiyo ya kurudi Chamlo.
Walisindikizwa kwa ngoma za ushujaa ambazo
zilichezwa na wanawake wazuri sana. Waliondoka
hadi ndani ya kijiji cha Kilimalondo ambako
walikutana na Mfalme SWAI akiwa na mtu wake wa
karibu sana bwana KIMOLO, Mzee Manuali
alishangaa sana pale kuukuta ufalme alifanya
jitihada za kuwaeleza wanakijiji kuwa hakuna
uongozi wa ufalme ambao unaleta mafanikio zaidi
ya unyaunyasaji na kiongozi ambae hafai basi wao
humuweka kwa kuwa huenda kwa kurithishana.
Wanakijiji wa pale wote waliitwa na mzee huyo
kutoka bwawani alisimama na kuongea nao.
wananchi nawaomba, haya munielewe
Hakika hapa nimetimba, Mengi kuwaelezea
Matatizo mwayachimba, maovu kujiwekea
Usasa unatupita, uzamani kuendekeza
Alikuwa anatumia mashaii kama moja ya lugha
ambayo aliona kuwa itafaa zaidi katika kuelimisha,
lakini sehemu yoyote lazima wabishi na wanaotaka
kuelewa zaidi hutokea ndipo akajitokeza mwana
mama mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Mama
Mwaija kama tunamkumbuka alikuwa ni rafiki
mkubwa sana wa mama Mwaija aliyefariki.
Ni mzuri wa kupaza, sauti kubwa mbele yetu
Mbali sisi tumeanza, na swai ndio kauli yetu
Usijaribu kutubeza, kwa haya mafanikio yetu
Huna kitu cha kusema, wewe ni nani kwetu.
Mzee swai alivyoona kuwa watu ni wabishi alitaka
kuwaeleza zaidi lakini sikitu aliingilia kati na
kuyaongea ya kwake mbele za watu wakubwa yeye
akiwa mdogo mbele yao.
Akina mama sikieni, Na wengine wakubwa pia
Yaliyosemwa sikieni, Mabaya nimepitia
Huo ufalme ebu acheni, mwenyekiti bora pia
Kiongozi asipowapeni, yale mliyoambiwa
Huna budi mtoeni, chagueni mwingine pia
Wanakijiji wa pale walikuwa na vigelele vingi na
uongozi wa mzee swai uliishia pale na wakamuweka
mwenyekiti palepale na akaanza kazi. safari yao
iliendelea kuelekea kwenye kijiji cha Chamlo,
ambako huko kulikuwa na mtafaruku mkubwa sana
juu ya swala la Bamuzi kutokuwa na amani kwa
kuondoka kwa Sikitu. Waliendelea kumtafuta na
kuwa na amani ya kuwa sikitu atakuja kurudi tena.
Mama Naomi hakuendelea kuishi kwani tayari
alikufa kutokana na presha na kukosea masharti
kutoka kwenye ngome yao ya Nyamnyena. Siku
iliyofuata waliingia kwa pamoja wote na furaha
ilikuwa kubwa sana kurudi kwao. Hawakufikilia yale
yote yaliyopita bali waliganga yale yanayoendelea
nao pia walifanya kazi ya kuwashawishi sana wale
watu na kiukweli walikubali na mwenyekiti alipatiwa
bwana Bamuzi. Maisha yalikuwa mazuri Sikitu
alibaki na Bamuzi wake ndani ya kijiji cha Chamlo.
Katunje alimuoa Mwana na Mzee chito aliondoka
akiwa na Katunje na Mwana kuelekea Bwawani, pia
Mzee mwalami manuali na Susu walirudi Bwawani.
Nawapenda nyinyi wote, ndani ya hadithi hii
Nimeimaliza yote, Joto mshumaa hii
Nawashukuru nyote, kupata na wazo hili
Jitahidi kuelewa, pindi pale usomapo.
NAWASHUKURU SANA KWA KUWA PAMOJA NA
MIMI
***MWISHO***
 
SEHEMU YA THELATHINI 30 (MWISHO)
THE END OF JOTO LA MSHUMAA.
KARIBU "MAISHA HAYA ZAIDI YA KURUTA"
ENDELEA.............
HADITHI ZA Author Mudhihili KWA SASA ZITAKUWA
ZINAPATIKANA SEHEMU MBILI TU KWENYE PAGE
YAKE INAYOITWA Riwaya za Mudhihili NA KWENYE
GRUPU LAKE LINALOITWA Maisha & Hadithi FANYA
HIMA KUWA NDANI YA HIZO SEHEMU MBILI
KUPATA BURUDANI ZAIDI AHSANTENI......
.....Mzee Upemgo alisea kuwa mzee huyo atakuwa
sawa endapo akizinduka muda wa hapo baadae.
Kila mmoja alikuwa kimya sana kutazamia zaidi
majira gani ambayo ataamka. Mzee Upengo
aliwasihi mambo kadhaa ya kuyafanya kabla ya
kuondoka.
"Sasa mnatakiwa kuwa makini sana maana mizimu
ya Nyamnyena itakuwa bado haijaishiwa nguvu na
endapo wakija mimi nitapata taarifa nitakuja mara
moja kuimalizia mbali....alafu huyu akiamka hapa
atakuwa hana nguvu mtampikia uji mwingi sana
ambao mtachanganya na hii dawa muhakikishe
anakunywa sawa?" Waliitikia kwa pamoja wote
watatu na mzee huyo muhimu kwa wakati huo
akaondoka zake. Huku nyuma wakiwa wamebaki
watu watatu yani Katunje Chito na Sikitu, walikaa
kwa pamoja na kupanga kujua wanamsaidiaje zaidi.
"Babaa haya mimi nahitajika kurudi kule ambako
yuko mume wangu Bamuzi siwezi kukaa huku
kipindi chote". Walimshangaa sana baada ya kutoa
ile kauli "Khaah! mwanangu kumbe kule ulikuwa
umeolewa yani bila hata taarifa ila haina shida
utakaa na sisi kwa muda na tutakupeleka huko".
Muda mchache walimsikia mzee Mambo sasa
akiomba maji ya kunywa, roho zao zilifurahi sana
kwani kila kitu waliona sasa kipo sawa bin sawia.
"Mpeni maji huyo haraka sana " Katunje alikwenda
kumpa maji ya kunywa alikunywa yote huku
wakimuandalia uji kama maelezo yalivyotakikana.
Waliweza kutia na ile dawa baada ya kumnywesha
uji wote alidai mwingine walifanya hivyo kama mara
tatu, hakika alipoteza nguvu sana. Siku ya pili
Alikuja mzee Upengo pale na kujua maendeleo ya
mgonjwa huyo.
Kufika kwa bwana huyo Mzee Mambo sasa alijihisi
huzuni sana na aibu kubwa kwani hata akili yake
ilirudi ile ya zamani na kukumbuka yapi kayatenda.
Machozi yalianza kumbubujika kwa wingi huku
akiwaangalia wanawe ambao nao pia walikuwa
wanamuangalia. Mzee huyo Upengo alikuja karibu
na kuchutama na kumsalimia "Habari yako bwana
wewe". Alikuwa anaulizwa lakini alibaki kulia tu,
alimfuta chozi kisha akarudia kumuuliza kwa mara
ya pili "Habari yako mzee Mambo sasa wewe ni
rafiki yangu bwanaaa yaache yaliyopita" Aliitikia kwa
kichwa ndipo mzee huyo akawaita wote na kuwapa
maelekezo.
'Naomba mnisikilize jambo liliobaki ni la huyu mzee
kwenda kule ambako alikuwa anachukulia kazi yani
kwenye mizimu yao akiwa peke yake akachome
yale ambayo yeye aliandaliwa ili baadae awe
kiongozi " Chito alidakia kumuuliza swali "Sasa
hapo mzee huko hakutokuwa na shida akienda peke
yake ?" Mzee upengo alikaa kimya kwa sekunde
kadhaa "Ndio shida ipo sio kubwa sana ila lazima
afanye hivyo kuokoa maisha ya hawa wengine sawa
jamani?" Waliitikia lakini Mzee upengo alimuita
Chito pembeni na kumuambia jambo ambalo
alishtuka kiasi lakini alitulizwa kwa maneno ya
hekima.
Hayakujulikana ni aina gani ya maneno ambayo yeye
kapewa. Mzee huyo alimuendea Mambo sasa na
kumuambia maelezo yale aliyokuwa anayatoa pale
kuwa kesho yake ajiandae na afanye kila njia
achome hiyo mizigo haraka kisha arudi pale na
atakuwa salama kabisa. Mzee Upengo aliondoka na
kuwaacha wale wakiwa pale lakini Chito alionekana
kulia lakini haikujulikana kwa nini yeye analia.
Maandalizi ya kesho yake yalianza walimuandalia
kifungua kinywa kama mzazi wao ndipo asubuhi
hiyo anataka kuondoka lakini aliwaita wote akakaa
nao chini akawaeleza jambo moja ambalo alikuwa
nalo kabla hajaenda.
"Wanangiu samahani sana nawaombeni samahani
kwa yote niliyoyafanya bila hata kujielewa yani kwa
tamaa ambayo ilinikuta. lakini mmefanya jitihada
sana kuniondoa kwenye upuuzi ule..pia mimi nakili
kweli nilishilikiana na rafiki yangu Nyandu kuwauwa
watu tulianzia kwa wazazi wake, kwa mkewe na
mimi nikamuua mama yenu..mpaka mkwe wangu
mama wa mjukuu wangu Sikitu pia nilitumwa
kumuua mjukuu wangu sikitu lakini ikashindikana.
nawaombeni samahani sana jamani na nawahidi
naenda kujitoa lazima nikafanikishe haya yote na
sasa nawaacha kama sitorudi muwe radhi na mimi".
Alimaliza na kuinuka na kuelekea njia ambayo
inaelekea shambani kwake. Walibaki kulia tu na
kuhuzunika sana kwa yale ambayo wanayaona na
waliyasikia kwa macho yao. Hawakuwa na jinsi
walimuombea tu baba yao arudi salama. Mzee
Chito alibaki akiwa hana hili wala lile ndipo akapata
wazo ambalo lilikuwa zuri sana "Sikitu na Katunje
nawaomba niwaambie kitu mnisindikize kijiji cha
KALULUL nimpeleke Sikitu akawaona babu zake na
Bibi pamoja na ndugu wa upande wa mama yake.
Sikitu alifurahi mno, Safari ilianza kuelekea kwa
Wazazi wa Mama wa Sikitu. Safari yao ilichukua
muda mrefu kidogo ndipo wanafika ndani ya kijiji
hiko cha Kalulu. Wanafiuka kwenye nyumba ya Mzee
SUEDI ambapo wanakaribishwa lakini mzee huyo
alipowaona tu alikunja sura na kutaka kuufunga
mlango wake. Chito aliushikilia na kumuomba
kwanza wasikilizwe yapi ambayo anayo yeye na
anataka kumueleza, Alikubaliana na yote lakini kwa
shingo upande, waliitwa familia nzima wakakaa
tayari kusikiliza maelekezo kutoka kwa bwana Chito
na jopo lake, kwa kuwa yeye aliolea pale hivyo kiasi
anajulikana.
Alianza kwa kusema. "Nawaombeni radhi kwa
kutokuja kutoa taarifa yoyote kuhusiana na mtoto
wenu..lakini bila kuficha mengi yametokea yalikuwa
ya kifamilia na niliogopa kuja kutoa ushahidi bila
kuwa na ukweli wowote ule. Naumia sana pindi
ninapowaona nyinyi wazazi na ndugu wa mke wangu
na kuwaambieni kuwa mke wangu kafariki
duniaaaa...." Walishtuka kwa pamoja na ndipo
ugomvi ulianza watu wakisema haiwezekani na
wanamtaka mtoto wao, Mwenyekiti alikuta ugomvi
huo na ndipo alipoingilia na kuweka mambo sawa
na kila mmoja akawa anasikiliza nani anasema kwa
utaratibu.
Lakini sasa kaniachia mtoto huyu hamkumfahamu
anaitwa Sikitu tumepitia mengi lakini
yalisababishwa na baba yangu mpaka sasa
tumefanikiwa kumbadilisha, nimekuja kutoa taarifa
na kuwaonyesha mtoto huyu na saa kiongozi ndani
ya kijiji cha Chamlo kwa mfalme Ngololo na mtoto
wake Bamuzi ndie aliyemuoa huyu.Walimpokea na
hapo walikaa siku mbili baada ya kila kitu
kuishakazi ambayo ilibaki ni kumrudisha Sikitu
ndani ya kijiji cha Chamlo. Safari yao ilianza.
Upande wa mzee Mambo sasa anafanikiwa kulipata
furushi ambalo alielekezwa kulifanyia kazi, na
hatimae analiunguza moto palepale lakini sasa kwa
bahati mbaya siku si nzuri kwake moshi wa vitu
hivyo vinamuathiri na kumteketeza kama vumbi na
kupoteza maisha yake kabisa. Maisha ya Mzee
Mambo sasa na mambo yake yote yanaishia
palepale alipokuwa anachoma na inabaki stori tu
kuwa alikuwapo mzee mambo sasa mwenye
mambo ya kizamani.
Safari ya watu hawa sasa ilianza kwenda kuelekea
ndani ya kijiji cha Bwawani, ambako walipofika
walipokelewa vyema sana kwa vishindo, Wanakijiji
walikusanyana kwa pamoja na kuwapongeza kwa
ushujaa wa kuwavumbua wabaya na hatimae
walikufa kwa ubaya wao kweli mwisho wa zambi
mauti, Mwenyekiti akiwa na jopo la watu wengine
kama Manyenye walimuomba mzee chito abaki pale
kwani wanampenda bado. Alichokisema bwana
Chito kuwa bado wanasafari ndefu ambayo
wakisharudi watarejea pale kwa maisha yao yote,
Bwana Manuali, Susu, Mwalami na Mwana
waliungana kwenye safari hiyo ya kurudi Chamlo.
Walisindikizwa kwa ngoma za ushujaa ambazo
zilichezwa na wanawake wazuri sana. Waliondoka
hadi ndani ya kijiji cha Kilimalondo ambako
walikutana na Mfalme SWAI akiwa na mtu wake wa
karibu sana bwana KIMOLO, Mzee Manuali
alishangaa sana pale kuukuta ufalme alifanya
jitihada za kuwaeleza wanakijiji kuwa hakuna
uongozi wa ufalme ambao unaleta mafanikio zaidi
ya unyaunyasaji na kiongozi ambae hafai basi wao
humuweka kwa kuwa huenda kwa kurithishana.
Wanakijiji wa pale wote waliitwa na mzee huyo
kutoka bwawani alisimama na kuongea nao.
wananchi nawaomba, haya munielewe
Hakika hapa nimetimba, Mengi kuwaelezea
Matatizo mwayachimba, maovu kujiwekea
Usasa unatupita, uzamani kuendekeza
Alikuwa anatumia mashaii kama moja ya lugha
ambayo aliona kuwa itafaa zaidi katika kuelimisha,
lakini sehemu yoyote lazima wabishi na wanaotaka
kuelewa zaidi hutokea ndipo akajitokeza mwana
mama mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Mama
Mwaija kama tunamkumbuka alikuwa ni rafiki
mkubwa sana wa mama Mwaija aliyefariki.
Ni mzuri wa kupaza, sauti kubwa mbele yetu
Mbali sisi tumeanza, na swai ndio kauli yetu
Usijaribu kutubeza, kwa haya mafanikio yetu
Huna kitu cha kusema, wewe ni nani kwetu.
Mzee swai alivyoona kuwa watu ni wabishi alitaka
kuwaeleza zaidi lakini sikitu aliingilia kati na
kuyaongea ya kwake mbele za watu wakubwa yeye
akiwa mdogo mbele yao.
Akina mama sikieni, Na wengine wakubwa pia
Yaliyosemwa sikieni, Mabaya nimepitia
Huo ufalme ebu acheni, mwenyekiti bora pia
Kiongozi asipowapeni, yale mliyoambiwa
Huna budi mtoeni, chagueni mwingine pia
Wanakijiji wa pale walikuwa na vigelele vingi na
uongozi wa mzee swai uliishia pale na wakamuweka
mwenyekiti palepale na akaanza kazi. safari yao
iliendelea kuelekea kwenye kijiji cha Chamlo,
ambako huko kulikuwa na mtafaruku mkubwa sana
juu ya swala la Bamuzi kutokuwa na amani kwa
kuondoka kwa Sikitu. Waliendelea kumtafuta na
kuwa na amani ya kuwa sikitu atakuja kurudi tena.
Mama Naomi hakuendelea kuishi kwani tayari
alikufa kutokana na presha na kukosea masharti
kutoka kwenye ngome yao ya Nyamnyena. Siku
iliyofuata waliingia kwa pamoja wote na furaha
ilikuwa kubwa sana kurudi kwao. Hawakufikilia yale
yote yaliyopita bali waliganga yale yanayoendelea
nao pia walifanya kazi ya kuwashawishi sana wale
watu na kiukweli walikubali na mwenyekiti alipatiwa
bwana Bamuzi. Maisha yalikuwa mazuri Sikitu
alibaki na Bamuzi wake ndani ya kijiji cha Chamlo.
Katunje alimuoa Mwana na Mzee chito aliondoka
akiwa na Katunje na Mwana kuelekea Bwawani, pia
Mzee mwalami manuali na Susu walirudi Bwawani.
Nawapenda nyinyi wote, ndani ya hadithi hii
Nimeimaliza yote, Joto mshumaa hii
Nawashukuru nyote, kupata na wazo hili
Jitahidi kuelewa, pindi pale usomapo.
NAWASHUKURU SANA KWA KUWA PAMOJA NA
MIMI
***MWISHO***
Asante ubarikiwe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SEHEMU YA THELATHINI 30 (MWISHO)
THE END OF JOTO LA MSHUMAA.
KARIBU "MAISHA HAYA ZAIDI YA KURUTA"
ENDELEA.............
HADITHI ZA Author Mudhihili KWA SASA ZITAKUWA
ZINAPATIKANA SEHEMU MBILI TU KWENYE PAGE
YAKE INAYOITWA Riwaya za Mudhihili NA KWENYE
GRUPU LAKE LINALOITWA Maisha & Hadithi FANYA
HIMA KUWA NDANI YA HIZO SEHEMU MBILI
KUPATA BURUDANI ZAIDI AHSANTENI......
.....Mzee Upemgo alisea kuwa mzee huyo atakuwa
sawa endapo akizinduka muda wa hapo baadae.
Kila mmoja alikuwa kimya sana kutazamia zaidi
majira gani ambayo ataamka. Mzee Upengo
aliwasihi mambo kadhaa ya kuyafanya kabla ya
kuondoka.
"Sasa mnatakiwa kuwa makini sana maana mizimu
ya Nyamnyena itakuwa bado haijaishiwa nguvu na
endapo wakija mimi nitapata taarifa nitakuja mara
moja kuimalizia mbali....alafu huyu akiamka hapa
atakuwa hana nguvu mtampikia uji mwingi sana
ambao mtachanganya na hii dawa muhakikishe
anakunywa sawa?" Waliitikia kwa pamoja wote
watatu na mzee huyo muhimu kwa wakati huo
akaondoka zake. Huku nyuma wakiwa wamebaki
watu watatu yani Katunje Chito na Sikitu, walikaa
kwa pamoja na kupanga kujua wanamsaidiaje zaidi.
"Babaa haya mimi nahitajika kurudi kule ambako
yuko mume wangu Bamuzi siwezi kukaa huku
kipindi chote". Walimshangaa sana baada ya kutoa
ile kauli "Khaah! mwanangu kumbe kule ulikuwa
umeolewa yani bila hata taarifa ila haina shida
utakaa na sisi kwa muda na tutakupeleka huko".
Muda mchache walimsikia mzee Mambo sasa
akiomba maji ya kunywa, roho zao zilifurahi sana
kwani kila kitu waliona sasa kipo sawa bin sawia.
"Mpeni maji huyo haraka sana " Katunje alikwenda
kumpa maji ya kunywa alikunywa yote huku
wakimuandalia uji kama maelezo yalivyotakikana.
Waliweza kutia na ile dawa baada ya kumnywesha
uji wote alidai mwingine walifanya hivyo kama mara
tatu, hakika alipoteza nguvu sana. Siku ya pili
Alikuja mzee Upengo pale na kujua maendeleo ya
mgonjwa huyo.
Kufika kwa bwana huyo Mzee Mambo sasa alijihisi
huzuni sana na aibu kubwa kwani hata akili yake
ilirudi ile ya zamani na kukumbuka yapi kayatenda.
Machozi yalianza kumbubujika kwa wingi huku
akiwaangalia wanawe ambao nao pia walikuwa
wanamuangalia. Mzee huyo Upengo alikuja karibu
na kuchutama na kumsalimia "Habari yako bwana
wewe". Alikuwa anaulizwa lakini alibaki kulia tu,
alimfuta chozi kisha akarudia kumuuliza kwa mara
ya pili "Habari yako mzee Mambo sasa wewe ni
rafiki yangu bwanaaa yaache yaliyopita" Aliitikia kwa
kichwa ndipo mzee huyo akawaita wote na kuwapa
maelekezo.
'Naomba mnisikilize jambo liliobaki ni la huyu mzee
kwenda kule ambako alikuwa anachukulia kazi yani
kwenye mizimu yao akiwa peke yake akachome
yale ambayo yeye aliandaliwa ili baadae awe
kiongozi " Chito alidakia kumuuliza swali "Sasa
hapo mzee huko hakutokuwa na shida akienda peke
yake ?" Mzee upengo alikaa kimya kwa sekunde
kadhaa "Ndio shida ipo sio kubwa sana ila lazima
afanye hivyo kuokoa maisha ya hawa wengine sawa
jamani?" Waliitikia lakini Mzee upengo alimuita
Chito pembeni na kumuambia jambo ambalo
alishtuka kiasi lakini alitulizwa kwa maneno ya
hekima.
Hayakujulikana ni aina gani ya maneno ambayo yeye
kapewa. Mzee huyo alimuendea Mambo sasa na
kumuambia maelezo yale aliyokuwa anayatoa pale
kuwa kesho yake ajiandae na afanye kila njia
achome hiyo mizigo haraka kisha arudi pale na
atakuwa salama kabisa. Mzee Upengo aliondoka na
kuwaacha wale wakiwa pale lakini Chito alionekana
kulia lakini haikujulikana kwa nini yeye analia.
Maandalizi ya kesho yake yalianza walimuandalia
kifungua kinywa kama mzazi wao ndipo asubuhi
hiyo anataka kuondoka lakini aliwaita wote akakaa
nao chini akawaeleza jambo moja ambalo alikuwa
nalo kabla hajaenda.
"Wanangiu samahani sana nawaombeni samahani
kwa yote niliyoyafanya bila hata kujielewa yani kwa
tamaa ambayo ilinikuta. lakini mmefanya jitihada
sana kuniondoa kwenye upuuzi ule..pia mimi nakili
kweli nilishilikiana na rafiki yangu Nyandu kuwauwa
watu tulianzia kwa wazazi wake, kwa mkewe na
mimi nikamuua mama yenu..mpaka mkwe wangu
mama wa mjukuu wangu Sikitu pia nilitumwa
kumuua mjukuu wangu sikitu lakini ikashindikana.
nawaombeni samahani sana jamani na nawahidi
naenda kujitoa lazima nikafanikishe haya yote na
sasa nawaacha kama sitorudi muwe radhi na mimi".
Alimaliza na kuinuka na kuelekea njia ambayo
inaelekea shambani kwake. Walibaki kulia tu na
kuhuzunika sana kwa yale ambayo wanayaona na
waliyasikia kwa macho yao. Hawakuwa na jinsi
walimuombea tu baba yao arudi salama. Mzee
Chito alibaki akiwa hana hili wala lile ndipo akapata
wazo ambalo lilikuwa zuri sana "Sikitu na Katunje
nawaomba niwaambie kitu mnisindikize kijiji cha
KALULUL nimpeleke Sikitu akawaona babu zake na
Bibi pamoja na ndugu wa upande wa mama yake.
Sikitu alifurahi mno, Safari ilianza kuelekea kwa
Wazazi wa Mama wa Sikitu. Safari yao ilichukua
muda mrefu kidogo ndipo wanafika ndani ya kijiji
hiko cha Kalulu. Wanafiuka kwenye nyumba ya Mzee
SUEDI ambapo wanakaribishwa lakini mzee huyo
alipowaona tu alikunja sura na kutaka kuufunga
mlango wake. Chito aliushikilia na kumuomba
kwanza wasikilizwe yapi ambayo anayo yeye na
anataka kumueleza, Alikubaliana na yote lakini kwa
shingo upande, waliitwa familia nzima wakakaa
tayari kusikiliza maelekezo kutoka kwa bwana Chito
na jopo lake, kwa kuwa yeye aliolea pale hivyo kiasi
anajulikana.
Alianza kwa kusema. "Nawaombeni radhi kwa
kutokuja kutoa taarifa yoyote kuhusiana na mtoto
wenu..lakini bila kuficha mengi yametokea yalikuwa
ya kifamilia na niliogopa kuja kutoa ushahidi bila
kuwa na ukweli wowote ule. Naumia sana pindi
ninapowaona nyinyi wazazi na ndugu wa mke wangu
na kuwaambieni kuwa mke wangu kafariki
duniaaaa...." Walishtuka kwa pamoja na ndipo
ugomvi ulianza watu wakisema haiwezekani na
wanamtaka mtoto wao, Mwenyekiti alikuta ugomvi
huo na ndipo alipoingilia na kuweka mambo sawa
na kila mmoja akawa anasikiliza nani anasema kwa
utaratibu.
Lakini sasa kaniachia mtoto huyu hamkumfahamu
anaitwa Sikitu tumepitia mengi lakini
yalisababishwa na baba yangu mpaka sasa
tumefanikiwa kumbadilisha, nimekuja kutoa taarifa
na kuwaonyesha mtoto huyu na saa kiongozi ndani
ya kijiji cha Chamlo kwa mfalme Ngololo na mtoto
wake Bamuzi ndie aliyemuoa huyu.Walimpokea na
hapo walikaa siku mbili baada ya kila kitu
kuishakazi ambayo ilibaki ni kumrudisha Sikitu
ndani ya kijiji cha Chamlo. Safari yao ilianza.
Upande wa mzee Mambo sasa anafanikiwa kulipata
furushi ambalo alielekezwa kulifanyia kazi, na
hatimae analiunguza moto palepale lakini sasa kwa
bahati mbaya siku si nzuri kwake moshi wa vitu
hivyo vinamuathiri na kumteketeza kama vumbi na
kupoteza maisha yake kabisa. Maisha ya Mzee
Mambo sasa na mambo yake yote yanaishia
palepale alipokuwa anachoma na inabaki stori tu
kuwa alikuwapo mzee mambo sasa mwenye
mambo ya kizamani.
Safari ya watu hawa sasa ilianza kwenda kuelekea
ndani ya kijiji cha Bwawani, ambako walipofika
walipokelewa vyema sana kwa vishindo, Wanakijiji
walikusanyana kwa pamoja na kuwapongeza kwa
ushujaa wa kuwavumbua wabaya na hatimae
walikufa kwa ubaya wao kweli mwisho wa zambi
mauti, Mwenyekiti akiwa na jopo la watu wengine
kama Manyenye walimuomba mzee chito abaki pale
kwani wanampenda bado. Alichokisema bwana
Chito kuwa bado wanasafari ndefu ambayo
wakisharudi watarejea pale kwa maisha yao yote,
Bwana Manuali, Susu, Mwalami na Mwana
waliungana kwenye safari hiyo ya kurudi Chamlo.
Walisindikizwa kwa ngoma za ushujaa ambazo
zilichezwa na wanawake wazuri sana. Waliondoka
hadi ndani ya kijiji cha Kilimalondo ambako
walikutana na Mfalme SWAI akiwa na mtu wake wa
karibu sana bwana KIMOLO, Mzee Manuali
alishangaa sana pale kuukuta ufalme alifanya
jitihada za kuwaeleza wanakijiji kuwa hakuna
uongozi wa ufalme ambao unaleta mafanikio zaidi
ya unyaunyasaji na kiongozi ambae hafai basi wao
humuweka kwa kuwa huenda kwa kurithishana.
Wanakijiji wa pale wote waliitwa na mzee huyo
kutoka bwawani alisimama na kuongea nao.
wananchi nawaomba, haya munielewe
Hakika hapa nimetimba, Mengi kuwaelezea
Matatizo mwayachimba, maovu kujiwekea
Usasa unatupita, uzamani kuendekeza
Alikuwa anatumia mashaii kama moja ya lugha
ambayo aliona kuwa itafaa zaidi katika kuelimisha,
lakini sehemu yoyote lazima wabishi na wanaotaka
kuelewa zaidi hutokea ndipo akajitokeza mwana
mama mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Mama
Mwaija kama tunamkumbuka alikuwa ni rafiki
mkubwa sana wa mama Mwaija aliyefariki.
Ni mzuri wa kupaza, sauti kubwa mbele yetu
Mbali sisi tumeanza, na swai ndio kauli yetu
Usijaribu kutubeza, kwa haya mafanikio yetu
Huna kitu cha kusema, wewe ni nani kwetu.
Mzee swai alivyoona kuwa watu ni wabishi alitaka
kuwaeleza zaidi lakini sikitu aliingilia kati na
kuyaongea ya kwake mbele za watu wakubwa yeye
akiwa mdogo mbele yao.
Akina mama sikieni, Na wengine wakubwa pia
Yaliyosemwa sikieni, Mabaya nimepitia
Huo ufalme ebu acheni, mwenyekiti bora pia
Kiongozi asipowapeni, yale mliyoambiwa
Huna budi mtoeni, chagueni mwingine pia
Wanakijiji wa pale walikuwa na vigelele vingi na
uongozi wa mzee swai uliishia pale na wakamuweka
mwenyekiti palepale na akaanza kazi. safari yao
iliendelea kuelekea kwenye kijiji cha Chamlo,
ambako huko kulikuwa na mtafaruku mkubwa sana
juu ya swala la Bamuzi kutokuwa na amani kwa
kuondoka kwa Sikitu. Waliendelea kumtafuta na
kuwa na amani ya kuwa sikitu atakuja kurudi tena.
Mama Naomi hakuendelea kuishi kwani tayari
alikufa kutokana na presha na kukosea masharti
kutoka kwenye ngome yao ya Nyamnyena. Siku
iliyofuata waliingia kwa pamoja wote na furaha
ilikuwa kubwa sana kurudi kwao. Hawakufikilia yale
yote yaliyopita bali waliganga yale yanayoendelea
nao pia walifanya kazi ya kuwashawishi sana wale
watu na kiukweli walikubali na mwenyekiti alipatiwa
bwana Bamuzi. Maisha yalikuwa mazuri Sikitu
alibaki na Bamuzi wake ndani ya kijiji cha Chamlo.
Katunje alimuoa Mwana na Mzee chito aliondoka
akiwa na Katunje na Mwana kuelekea Bwawani, pia
Mzee mwalami manuali na Susu walirudi Bwawani.
Nawapenda nyinyi wote, ndani ya hadithi hii
Nimeimaliza yote, Joto mshumaa hii
Nawashukuru nyote, kupata na wazo hili
Jitahidi kuelewa, pindi pale usomapo.
NAWASHUKURU SANA KWA KUWA PAMOJA NA
MIMI
***MWISHO***

Safi sana... Story nzuri sana...

Chapter Closed...



Cc: mahondaw
 
Habari mambo naitwa Mr Equator Nimeandika ujumbe huu kuku omba swala moja tu!
Mimi nimetengeza website ya ku share story ambayo ni http://www.equatorstory.com/
Je umekuwa ukipata tabu kupost story zako hapa?
Hili ndo suluhisho lako.
Mimi nataka nkupe nafasi ya kuwa mmoja wapo wa kwanza kutumia hii website
unda account yako na uweze kupost story yako mpya.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom