Riwaya: Jina langu ni Pheady

KAZI IENDELEE...



"Okey, nitafanya hivyo." Alisema Patrick.
"Haya kwa heri." Aliongea yule mtu wa kwenye simu na kukata.

Patrick aliendelea kukata makali ya Long John huku akiaangalia runinga na baada ya muda akawa amepitiwa na usingizi. Alikuja kushtuka majira ya saa tisa, kilichomshitua usingizini ni mlio wa simu ambao ulisikika. Aliposhtuka Mr Wanna See na mwenzie wamekaa huku wakinywa ile pombe iliyokuwa imebaki kwenye chupa. Akichukua simu na kuweka sikioni bila hata kuwasemesha akina Wanna See.
"Hallo Patrick hapa." Alisema. Baada ya kuslimiana na huyo mtu wa kwenye simu aliendelea kusikiliza kwa makini huku akikunja na kukunjua uso wake. Mara alisikika akisema; "Kwaheri tutaonana saa tatu, nitakupitia nyumbani." Alimaliza kusema hivyo akarusisha simu mahali pake na kuwageukia wenzake akina Wanna See.
"Hallo naona mmenifaidi sana nikiwa nayoyoma na usingizi" Alisema Patrick.
"Ha! Wapi rafiki yangu sisi tumefika muda mfupi tu, tulijua labda umeegesha tu." Alisema yule mwenzake na Wanna See.
"Boss kuna taarifa nimepokea hapa sasa hivi" alisema Patrick akiwa anamuangalia Wanna See.
"Inasemaje hiyo taarifa?" Wanna See aliuliza kwa shauku.
"Yule mtu tuliyekuwa tumemteka ila atuambie wapi alipo Pheady kusudi tupate ile mali aliyochukua kwa marehemu Catto, inasemekana amelazwa zahanati ya MAGAMBO. Alipelekwa usiku na wenzie wawili ambao walimfikisha akiwa hajitambui kutokana na mateso tuliyompa. Inasemekana sio mtu wa kutoka leo Wala kesho labda wenzake walazimishe kumchukua." Alimaliza maelezo Patrick.
"Kama ni hivyo huyo ngio atakayetueleza alipo Pheady, hiyo zahanati ipo sehemu gani? Je ni nzuri ya kuweza kwenda kuchukua mtu bila matatizo? Alihoji Mr Wanna See.
"Sehemu yenyewe ni nzuri sana tu hata mchana unaweza kutoa mtu kwa mkwala na ukaondoka kabla ya askari kufika." Alieleza Patrick.
"Kwa hiyo wewe unasemaje kuhusiana na mpango wa kumpata huyo mtu? Maana wewe ndie mwenyeji unayeyaelewa mazingira yalivyo. Na inatakiwa apatikane haraka kabla hajapeperuka, kumbuka wale nao ni watu wa machale yanaweza yakawacheza wakabadili mchezo wakati wowote na kutuunguzia picha." Kabla hakamaliza kuongea mlango uligongwa wakaingia vijana watano kwa pamoja na kusalimiana baadae wakakaa kwenye sofa zilizokuwa wazi pembeni.

Baada ya kuwa wamekaa Patrick aliwauliza; vipi kuna mafanikio yoyote huko?
"Hakuna, tumejitahidi kila njia lakini mpaka sasa hatujapata fununu zozote kuwahusu. Inaonekana wamejichimbia mahali na hawataki kufanya makosa yoyote yatakayowafanya waonekane. Alafu mjini kulikuwa na vurugu ambazo zimetupotezea wakati kidogo. Machinga wa mtaa wa Makoroboi walianzisha maandamano yaliyoambatana na fujo mpaka FFU ikainhilia Kati. Walikuwa wanaelekea manispaa. Kutokana na hizo vurugu na tishio la kuchoma moto manispaa FFU wametanda mitaa yote iliyo karibu na manispaa." Alisema Gilly.

"Kutokana na maelezo aliyotoa Gilly, mpango wa kumpata mtu wetu leo utakuwa mgumu kidogo. Kwani zahanati ya Magambo ipo jirani tu na manispaa." Patrick alisema huku akimwangalia Wanna See aliyekuwa akimsikiliza.
"Hata kama utakuwa mgumu lakini ni lazima awepo mtu pale aangalie nyendo za hapo alipo huyo mtu. Huenda tukamnasa tunayemtaka akija kumsalimia na hapo tutakuwa na uwezo wa kumufatilia." Alisema wanna See.
"Kwani Kuna habari zozote mlizonazo kuhusiana nao?" Aliuliza Zuberi, maana wao waliingia muda mfupi uliopita, hawakuwa na habari alizopata Patrick.
Patrick aliwaeleza kwa kifupi wakawa wameelewa na kuendelea na mpango ulio mbele yao.

"Kwa hiyo pale inabidi tuweke doria yetu ya kisiri au mmoja wetu augue apelekwe pale kwa matibabu na kuhakikisha analazwa pale kwa usiku wa leo ili tuwe na uhakika na tunachofanya." Alisema yule mwenzake na Wanna See ambaye mda wote alikuwa kimya. Walichangia hoja kuhusiana na mawazo aliyotoa huyo ndugu ambaye jina lake ni Lung'otha mwenye asili ya kizuru huko Afrika ya Kusini. Baadae waliafikiana kuwa Kabla ya kitendo chochote kile inabidi Patrick kwanza akonane na huyo aliyempa habari hiyo ili amfafanulie kwa undani zaidi. Kwa sababu pale ni kazini kwa mtoa habari anaweza kuwa msaada iwapo atatumika vizuri.

Baada ya maafikiano hayo Patrick alionelea aondoke wakati huo maana jioni ilishaanza kunyemelea. Nao akina Wanna See walitaka kwenda kumuona mwenzao ambaye yuko Mwanza Hotel. Kabla hawajaondoka Wanna See alimuambia Patrick asubiri, akaelekea chumbani na kurudi na mkoba wake.

Alifungua na kutoa redio kumi na mbili ndogo za mkononi akasema hizi ni redio za kawaida lakini zina sehemu zetu za siri za mawasiliano. Aliwaonyesha jinsi ya kutumia kama mwenzako akiwa anakutafuta utaona uzi unaotumika kutafuta mawimbi ya sauti unakuwa mwekundu na redio inakoroma kama vile haijashika mawimbi sawasawa. Hivyo unatakiwa kubonyeza sehemu iliyojitokeza kidogo pembeni ya kifufe cha kuongezea sauti na hapo mnaweza kuwasiliana. Kwa miiaka hiyo ilikuwa ni teknolajia mpya hivyo waliifurahia.
Baada ya kutoa maelekezo mafupi aligawa kwa kila mtu. Wote walipokea na kujaribu alafu wakatunza na kila mtu akaendelea na majukumu yake huku wakiwa wameahidiana kukutana saa nne za usiku pale kwa Patrick.

Patrick yeye alitakiwa akonane na mtu aliyempa habari za Kikakika ambaye ni Norack. Alifanya hivyo, kwa sababu ahadi ya kuonana ilikuwa bado ilibidi atumie akili nyingine ya kumpata Norack kwa haraka. Baada ya kuonana nae waliongea kwa kirefu na kukubaliana kuwa Patrick atapeleka mgonjwa pale usiku ili huyo mgonjwa achukue jukumu la kumchunga Kikakika. Hakumueleza ukweli wa mambo lakini kutokana na jinsi Norack alivyokuwa akimpenda hakuhoji zaidi isipokuwa kuahidi kumsaidia. Patrick. Patrick alimpatia pesa kiasi cha shilingi laki moja na kumuambia hiyo ni kwa ajili ya msaada anaoendelea kutoa na ahadi ya kujengewa nyumba ipo palepale. Norack alifurahi na kuongezea kuwa ingekuwa vizuri kama wangefika pale kuanzia saa nne na nusu kwani atakuwa tayari ameishaingia kazini. Baada ya hapo waliagana na kuahidiana kuonana baadae lakini hawataonyesha kujuana. Wakati huo ilikuwa ni saa moja na nusu jioni.

Pamoja na kuwa ahadi yao ya kukutana ilikuwa ni saa nne, lakini ilipotimia saa tatu na robo karibu wote walishawasili kwa Mr Patrick pamoja na yule mzungu mwenzie na Wanna See ambaye hakuwepo mchana. Ni Gilly pekee ndie alikuwa hajafika. Walikuwa waliendelea na mazungumzo ya kawaida huku wakitazama mkanda mmoja wa video uitwao Black Eagle, ile video ilionekana kewapendeza sana maana walikuwa wakijadili matukio yanayotokea humo kwenye video. Ni wakati alipofika Gilly ndipo walipoanza kujadili utendaji wao wa kazi na hiyo ilikuwa ni saa nne kasoro robo.

Baada ya mjadala mrefu kidogo ilikubalika Gilly ndie apelekwe zahanati kama mgonjwa aliyepata mshtuko wa moyo. Na Gilly atakuwa amechukua vifaa vyake vyote muhimu kama unga wa kunusa na kusinzia, bastola ndogo na redio ataachiwa kama wa kusikiliza. Unga unaweza kusaidia iwapo itapatikana njia ya kumtoa huyo mtu lazima awe hana fahamu ili kuhepusha bugudha. Gilly, Zuberi na Patrick waliondoka kwenda kutekeleza mpango huo. Wakati wanaondoka ilikuwa saa nne na dakika kumi na mbili, walipofika zahanati Gilly alijifanya yuko hoi akipumua kwa namna ya ajabu, Zuberi na Patrick walimsaidia kutembea huku wakiwa wameweka mikono yake juu ya mabega yao na kumuongoza mpaka kwenye mlango wa zahanati. Daktari alinyanyua uso wakati wanaingia na kuwaashiria wapite moja kwa moja katika chumba cha kuhudumia wagonjwa.
"Habari za shughuri?" Aliuliza Zuberi baada ya kuwa wameingia ndani na kukaa.
"Salama tu, sijui mgonjwa wenu ana tatizo gani?" Aliuliza daktari.
"Hata hatujui, ni hali iliyomtokea ghafla tu baada ya kupokea taarifa fulani hivyo tunahitaji msaada wako."
Baada ya daktari kusikia hivyo akichukua vipimo vyake na kuanza kumpima, alimaliza kumpima lakini hakuweza kugundua ugonjwa wowote maana alikuta mapigo ya moyo yakienda sawasawa.
"Haonyeshi tatizo la moyo" alisema daktari. Patrick na Gilly huku wakionyesha sura za mshangao walisema kwa pamoja" lakini hali yake unaiona ilivyo"
"Ndio kwa macho anaonekana ni mgonjwa lakini kwa hivi vipimo haonyeshi." Alisema daktari.
"Sasa bwana daktari unatushauri tufanye nini?" Aliuliza Zuberi. Daktari alifikiri kidogo alafu akasema "Nawashauri mumuache hapa kwa uchunguzi zaidi ndio tutakuwa na majibu sahihi ya kinachomsumbua"
"Sawa tutamuacha, sijui malipo yataghalimu kiasi gani cha fedha?" Aliuliza Patrick.
Kabla daktari hajajibu aliingia mlangoni Norack akiwa katika vazi la uuguzi. Aliwasalimia Patrick na Zuberi kisha akaongea daktari kuhusu aina fulani ya dawa ambapo daktari alifungua kabati pembeni yake na kutoa vipaketi vya dawa na kumpa.
"Siwezi kuwaambia malipo kabla sijampatia matibabu hivyo nyie muacheni na kesho njooni ndipo mtapata kujua gharama zinazohitajika." Aliongea daktari baada ya muuguzi kuwa ameondoka.
"Sawa, kwa hiyo sisi tunaondoka tutaonana kesho." Alisema Patrick.
Waliagana alafu Zuberi na Patrick wakaondoka huku wakiwa wamemuacha Gilly hapo zahanati akiwa na vifaa vyake vyote vya kazi. Zuberi na Patrick waliwasili kwa wenzao bila matatizo na kuwaeleza mambo yalivyokuwa huko zahanati, baada ya hapo wakatawanyika na kwenda kulala huku wakiwa wameahidiana kuonana kesho yake saa tatu asubuhi iwapo hakutakuwa na dharura yoyote.
 
KAZI IENDELEE...



"Okey, nitafanya hivyo." Alisema Patrick.
"Haya kwa heri." Aliongea yule mtu wa kwenye simu na kukata.

Patrick aliendelea kukata makali ya Long John huku akiaangalia runinga na baada ya muda akawa amepitiwa na usingizi. Alikuja kushtuka majira ya saa tisa, kilichomshitua usingizini ni mlio wa simu ambao ulisikika. Aliposhtuka Mr Wanna See na mwenzie wamekaa huku wakinywa ile pombe iliyokuwa imebaki kwenye chupa. Akichukua simu na kuweka sikioni bila hata kuwasemesha akina Wanna See.
"Hallo Patrick hapa." Alisema. Baada ya kuslimiana na huyo mtu wa kwenye simu aliendelea kusikiliza kwa makini huku akikunja na kukunjua uso wake. Mara alisikika akisema; "Kwaheri tutaonana saa tatu, nitakupitia nyumbani." Alimaliza kusema hivyo akarusisha simu mahali pake na kuwageukia wenzake akina Wanna See.
"Hallo naona mmenifaidi sana nikiwa nayoyoma na usingizi" Alisema Patrick.
"Ha! Wapi rafiki yangu sisi tumefika muda mfupi tu, tulijua labda umeegesha tu." Alisema yule mwenzake na Wanna See.
"Boss kuna taarifa nimepokea hapa sasa hivi" alisema Patrick akiwa anamuangalia Wanna See.
"Inasemaje hiyo taarifa?" Wanna See aliuliza kwa shauku.
"Yule mtu tuliyekuwa tumemteka ila atuambie wapi alipo Pheady kusudi tupate ile mali aliyochukua kwa marehemu Catto, inasemekana amelazwa zahanati ya MAGAMBO. Alipelekwa usiku na wenzie wawili ambao walimfikisha akiwa hajitambui kutokana na mateso tuliyompa. Inasemekana sio mtu wa kutoka leo Wala kesho labda wenzake walazimishe kumchukua." Alimaliza maelezo Patrick.
"Kama ni hivyo huyo ngio atakayetueleza alipo Pheady, hiyo zahanati ipo sehemu gani? Je ni nzuri ya kuweza kwenda kuchukua mtu bila matatizo? Alihoji Mr Wanna See.
"Sehemu yenyewe ni nzuri sana tu hata mchana unaweza kutoa mtu kwa mkwala na ukaondoka kabla ya askari kufika." Alieleza Patrick.
"Kwa hiyo wewe unasemaje kuhusiana na mpango wa kumpata huyo mtu? Maana wewe ndie mwenyeji unayeyaelewa mazingira yalivyo. Na inatakiwa apatikane haraka kabla hajapeperuka, kumbuka wale nao ni watu wa machale yanaweza yakawacheza wakabadili mchezo wakati wowote na kutuunguzia picha." Kabla hakamaliza kuongea mlango uligongwa wakaingia vijana watano kwa pamoja na kusalimiana baadae wakakaa kwenye sofa zilizokuwa wazi pembeni.

Baada ya kuwa wamekaa Patrick aliwauliza; vipi kuna mafanikio yoyote huko?
"Hakuna, tumejitahidi kila njia lakini mpaka sasa hatujapata fununu zozote kuwahusu. Inaonekana wamejichimbia mahali na hawataki kufanya makosa yoyote yatakayowafanya waonekane. Alafu mjini kulikuwa na vurugu ambazo zimetupotezea wakati kidogo. Machinga wa mtaa wa Makoroboi walianzisha maandamano yaliyoambatana na fujo mpaka FFU ikainhilia Kati. Walikuwa wanaelekea manispaa. Kutokana na hizo vurugu na tishio la kuchoma moto manispaa FFU wametanda mitaa yote iliyo karibu na manispaa." Alisema Gilly.

"Kutokana na maelezo aliyotoa Gilly, mpango wa kumpata mtu wetu leo utakuwa mgumu kidogo. Kwani zahanati ya Magambo ipo jirani tu na manispaa." Patrick alisema huku akimwangalia Wanna See aliyekuwa akimsikiliza.
"Hata kama utakuwa mgumu lakini ni lazima awepo mtu pale aangalie nyendo za hapo alipo huyo mtu. Huenda tukamnasa tunayemtaka akija kumsalimia na hapo tutakuwa na uwezo wa kumufatilia." Alisema wanna See.
"Kwani Kuna habari zozote mlizonazo kuhusiana nao?" Aliuliza Zuberi, maana wao waliingia muda mfupi uliopita, hawakuwa na habari alizopata Patrick.
Patrick aliwaeleza kwa kifupi wakawa wameelewa na kuendelea na mpango ulio mbele yao.

"Kwa hiyo pale inabidi tuweke doria yetu ya kisiri au mmoja wetu augue apelekwe pale kwa matibabu na kuhakikisha analazwa pale kwa usiku wa leo ili tuwe na uhakika na tunachofanya." Alisema yule mwenzake na Wanna See ambaye mda wote alikuwa kimya. Walichangia hoja kuhusiana na mawazo aliyotoa huyo ndugu ambaye jina lake ni Lung'otha mwenye asili ya kizuru huko Afrika ya Kusini. Baadae waliafikiana kuwa Kabla ya kitendo chochote kile inabidi Patrick kwanza akonane na huyo aliyempa habari hiyo ili amfafanulie kwa undani zaidi. Kwa sababu pale ni kazini kwa mtoa habari anaweza kuwa msaada iwapo atatumika vizuri.

Baada ya maafikiano hayo Patrick alionelea aondoke wakati huo maana jioni ilishaanza kunyemelea. Nao akina Wanna See walitaka kwenda kumuona mwenzao ambaye yuko Mwanza Hotel. Kabla hawajaondoka Wanna See alimuambia Patrick asubiri, akaelekea chumbani na kurudi na mkoba wake.

Alifungua na kutoa redio kumi na mbili ndogo za mkononi akasema hizi ni redio za kawaida lakini zina sehemu zetu za siri za mawasiliano. Aliwaonyesha jinsi ya kutumia kama mwenzako akiwa anakutafuta utaona uzi unaotumika kutafuta mawimbi ya sauti unakuwa mwekundu na redio inakoroma kama vile haijashika mawimbi sawasawa. Hivyo unatakiwa kubonyeza sehemu iliyojitokeza kidogo pembeni ya kifufe cha kuongezea sauti na hapo mnaweza kuwasiliana. Kwa miiaka hiyo ilikuwa ni teknolajia mpya hivyo waliifurahia.
Baada ya kutoa maelekezo mafupi aligawa kwa kila mtu. Wote walipokea na kujaribu alafu wakatunza na kila mtu akaendelea na majukumu yake huku wakiwa wameahidiana kukutana saa nne za usiku pale kwa Patrick.

Patrick yeye alitakiwa akonane na mtu aliyempa habari za Kikakika ambaye ni Norack. Alifanya hivyo, kwa sababu ahadi ya kuonana ilikuwa bado ilibidi atumie akili nyingine ya kumpata Norack kwa haraka. Baada ya kuonana nae waliongea kwa kirefu na kukubaliana kuwa Patrick atapeleka mgonjwa pale usiku ili huyo mgonjwa achukue jukumu la kumchunga Kikakika. Hakumueleza ukweli wa mambo lakini kutokana na jinsi Norack alivyokuwa akimpenda hakuhoji zaidi isipokuwa kuahidi kumsaidia. Patrick. Patrick alimpatia pesa kiasi cha shilingi laki moja na kumuambia hiyo ni kwa ajili ya msaada anaoendelea kutoa na ahadi ya kujengewa nyumba ipo palepale. Norack alifurahi na kuongezea kuwa ingekuwa vizuri kama wangefika pale kuanzia saa nne na nusu kwani atakuwa tayari ameishaingia kazini. Baada ya hapo waliagana na kuahidiana kuonana baadae lakini hawataonyesha kujuana. Wakati huo ilikuwa ni saa moja na nusu jioni.

Pamoja na kuwa ahadi yao ya kukutana ilikuwa ni saa nne, lakini ilipotimia saa tatu na robo karibu wote walishawasili kwa Mr Patrick pamoja na yule mzungu mwenzie na Wanna See ambaye hakuwepo mchana. Ni Gilly pekee ndie alikuwa hajafika. Walikuwa waliendelea na mazungumzo ya kawaida huku wakitazama mkanda mmoja wa video uitwao Black Eagle, ile video ilionekana kewapendeza sana maana walikuwa wakijadili matukio yanayotokea humo kwenye video. Ni wakati alipofika Gilly ndipo walipoanza kujadili utendaji wao wa kazi na hiyo ilikuwa ni saa nne kasoro robo.

Baada ya mjadala mrefu kidogo ilikubalika Gilly ndie apelekwe zahanati kama mgonjwa aliyepata mshtuko wa moyo. Na Gilly atakuwa amechukua vifaa vyake vyote muhimu kama unga wa kunusa na kusinzia, bastola ndogo na redio ataachiwa kama wa kusikiliza. Unga unaweza kusaidia iwapo itapatikana njia ya kumtoa huyo mtu lazima awe hana fahamu ili kuhepusha bugudha. Gilly, Zuberi na Patrick waliondoka kwenda kutekeleza mpango huo. Wakati wanaondoka ilikuwa saa nne na dakika kumi na mbili, walipofika zahanati Gilly alijifanya yuko hoi akipumua kwa namna ya ajabu, Zuberi na Patrick walimsaidia kutembea huku wakiwa wameweka mikono yake juu ya mabega yao na kumuongoza mpaka kwenye mlango wa zahanati. Daktari alinyanyua uso wakati wanaingia na kuwaashiria wapite moja kwa moja katika chumba cha kuhudumia wagonjwa.
"Habari za shughuri?" Aliuliza Zuberi baada ya kuwa wameingia ndani na kukaa.
"Salama tu, sijui mgonjwa wenu ana tatizo gani?" Aliuliza daktari.
"Hata hatujui, ni hali iliyomtokea ghafla tu baada ya kupokea taarifa fulani hivyo tunahitaji msaada wako."
Baada ya daktari kusikia hivyo akichukua vipimo vyake na kuanza kumpima, alimaliza kumpima lakini hakuweza kugundua ugonjwa wowote maana alikuta mapigo ya moyo yakienda sawasawa.
"Haonyeshi tatizo la moyo" alisema daktari. Patrick na Gilly huku wakionyesha sura za mshangao walisema kwa pamoja" lakini hali yake unaiona ilivyo"
"Ndio kwa macho anaonekana ni mgonjwa lakini kwa hivi vipimo haonyeshi." Alisema daktari.
"Sasa bwana daktari unatushauri tufanye nini?" Aliuliza Zuberi. Daktari alifikiri kidogo alafu akasema "Nawashauri mumuache hapa kwa uchunguzi zaidi ndio tutakuwa na majibu sahihi ya kinachomsumbua"
"Sawa tutamuacha, sijui malipo yataghalimu kiasi gani cha fedha?" Aliuliza Patrick.
Kabla daktari hajajibu aliingia mlangoni Norack akiwa katika vazi la uuguzi. Aliwasalimia Patrick na Zuberi kisha akaongea daktari kuhusu aina fulani ya dawa ambapo daktari alifungua kabati pembeni yake na kutoa vipaketi vya dawa na kumpa.
"Siwezi kuwaambia malipo kabla sijampatia matibabu hivyo nyie muacheni na kesho njooni ndipo mtapata kujua gharama zinazohitajika." Aliongea daktari baada ya muuguzi kuwa ameondoka.
"Sawa, kwa hiyo sisi tunaondoka tutaonana kesho." Alisema Patrick.
Waliagana alafu Zuberi na Patrick wakaondoka huku wakiwa wamemuacha Gilly hapo zahanati akiwa na vifaa vyake vyote vya kazi. Zuberi na Patrick waliwasili kwa wenzao bila matatizo na kuwaeleza mambo yalivyokuwa huko zahanati, baada ya hapo wakatawanyika na kwenda kulala huku wakiwa wameahidiana kuonana kesho yake saa tatu asubuhi iwapo hakutakuwa na dharura yoyote.
Hongera Mwandishi KAZI IENDELEE
 
KAZI IENDELEE



10
Ilikuwa ni saa moja na kitu nilipostuka usingizini, nilijisikia mchovu sana hii ilitokana na kutokufanya mazoezi kwa muda. Nilimuangalia Sonno aliyelala kitanda cha pembeni yangu yeye alionekana kuamka kitambo kwani alikuwa akivuta sigara.
"Vipi Sonno?" Nilimjulia hali.
"Safi tu, naona kumekucha"alisema.
"Ndio kumekucha na makucha yake alisema na wote tukacheka."
"Leo sikusinzia kwa raha, nilikuwa naota ndoto za ajabu ajabu tu."
"Kwa hiyo inabidi tukae kwa tahadhari huenda kuna mabaya yanaweza kutufika sio?" Niliongea huku nikimtaza usoni.
"Ha!! Wapi ndugu yangu zinaweza kuwa ndoto za kawaida tu, lakini hata hivyo kuwa na tahadhari ni jambo muhimu wale watu wanaweza kuwa wameisha tunusa." Aliongea Sonno.
Baada ya hapo nitoka kitandani kwenda kuoga, nilipokuwa nimemaliza shughuri zote za usafi wa asubuhi. Nilibadiri nguo na kuvaa full jeans huku ndani nikiwa nimevaa mojawapo ya fulana za kuzuia risasi tulizozipata kule kwa Patrick.
Ilipofika saa mbili na nusu Sonno naye alikuwa tayari kishamaliza mambo yote ya usafi, alikuwa kavaa suti huku ndani kavaa fulana ya kuzuia risasi vilevile. Tulitoka chumbani na kwenda sebuleni ambapo tulimkuta dada akiwa kwenye pilika pilika za usafi. Alipotuona aliacha chughuri zake za usafi tukasalimiana na baada ya kusalimiana alitutengea kifungua kinywa nasi tukaanza kunywa.
"Vipi mbona leo mmeamka asubuhi namna hii au mna ahadi muhimu nini?" Aliongea dada wakati sisi tunaendelea na chai..
"Kuna mwenzetu mmoja ambaye inabidi tumuone kabla ya saa nne. Nilimueleza dada.
Tulipomaliza kunywa chai tulirudi chumbani nikachukua simu iliyokuwa pembeni mwa meza na kuzungusha namba 333 ambazo ni namba za yule msichana tuliyeonana nae kule Magnum Club. Baada ya kusubiri kidogo nilisikia simu ikinyanyuliwa alafu ikasikika sauti ya kiume.
"Nani mwenzangu?" Iliuliza
"Samahani kaka naomba kuongea na msichana aitwae Mtuli." Niliongea kwenye simu..
"Subiri kidogo." Ilisikika ile sauti na baada ya muda mfupi ilisikika sauti ya kike.
"Hallo nani mwenzangu?"
"Lyampili." Nilisema kwa kumtega kama ananikumbuka.
"Wewe ndie tulionana Magnum Club?" Niliulizwa.
"Ndio mimi, mambo vipi?" Nilimjibu na kuuliza.
*Haha!!! Mwanaume wewe una laana kweli, alisema kwa kebehi alafu akaendelea. Maana yake nini kuniwwka nikusubiri kama kichaa pale River Side."alimaliza na kuvuta pumzi zilizosikika hata kwenye simu.
"Sio makusudi mpenzi ni kutokana na matatizo yasiyozuilika. Nilimchomekea neno mpenzi nione muitikio wake.
"Matatizo gani yasiyozuilika? Au ulitaka kunipima pumzi zangu?" Alisema kwa sauti yenye hasira kidogo.
"Sikiliza bibie hapa kwenye simu sio mahali pa kulaumiana lililopo ni Mimi na wewe kupanga tuonane wapi." Nilibadilisha mkondo wa maongezi.
"Kwani wewe unasemaje?" Aliuliza.
"Mimi nakusikilizia wewe uniambie una nafasi saa ngapi na ni wapi tuonane" nilieleza.
"Nitapata nafasi saa saba mchana muda wa kwenda kupata chakula." Alisema.
"Muda huo haufai kuonana na wewe, tungefanya jioni baada ya kazi ingekuwa bora zaidi." Nilimueleza.
"Jioni naweza kuwa na shughuri nyingine alafu nikakosa muda." Alisema.
"Sawa lakini kumbuka unaposema tuonane saa saba mimi nahofia kutokuonana maana kuna mambo nafatilia, huenda huo muda nikajikuta sehemu ambayo siwezi kutoka kwa wakati huo hivyo mambo yakawa kama jana. Au wewe unataka tusionane tena." Nilisema.
"Hapana sio hivyo ila hata mimi nilikuwa nakupa hali halisi." Alijibu.
"Kwa hiyo ndio kusema hakuna uwezekano wa kuonana jioni ila kwa muda uliosema tu siyo?" Nilihoji.
"Uwezekano upo ila ni mdogo sana." Alisema.
"Sikiliza Mtuli najua ukiamua uwezekano upo ni kiasi cha wewe kupanga mambo yako na kuangalia muda hata wa nusu saa kwa ajili yangu. Kwani hapo ulipo sio kwamba umeolewa. Kwa hiyo unaponiambia kuwa jioni sio rahisi sikuekewi ila naelewa kuwa huna mpanga wa kuonana na mimi au sio??
"Basi Lyampili tuonane saa tatu usiku pale Jafaries, si unapafahamu? Alisema.
"Ndio." Nilimjibu.
"Sawa, kwa hiyo tuonane hapo saa tatu."Alisema.
"Sawa bibie ila jitahidi usinichomeshe mahindi." Nilisema.
"Hakuna wasiwasi, siwezi kulipiza kisasi kwa jinsi ulivyonifanyia wewe." Alisema wote tukacheka na baada ya hapo tuliagana nikarudisha simu mahali pake alafu nikageuka kumuangalia Sonno niliyemkuta alitabasamu.
"Vipi, naona mambo sio mabaya kwa jinsi unavyomwemwesa." Alisema Sonno huku akicheka.
"Wewe vipi rafiki yangu mbona unanisanifu." Nilisema huku na mima nikianza kucheka.
"Sikiliza Pheady," Sonno alikatisha kicheko na kuanza kuongea; "Inabidi tupange mpango wa kumtoa Kikakika zahanati akaugulie nyumbani au sehemu nyingine na sisi tupotee mji huu. Hata kama Kikakika hajisikii vizuri, matibabu ataendelea kupata kama kawaida. Navyoona kuendelea kumuacha pale zahanati na sisi kuendelea kuwa mji huu Haina maana, tutawanyike na mzigo tuuache mambo yakitulia tuatafanya vitu vyetu" alimaliza kusema Sonno.
"Hakuna matatizo, twende tukamuone alafu tupitie kwa mkuu wa ofisi zetu za hapa. Baada ya hapo tutakuwa na mpango kamili wa mambo yetu." Nilieleza.
"Sawa, twende tukamuone, lakini mimi nafikiri tumpelekee huko huko fulana ya kuzuia risasi vilevile avae kama sisi tulivyovaa." Alisema Sonno.
"Du," wazo zuri sana, inaonekana umekubuhu katika masuala haya." Nilimpongeza, akacheka na kukunja fulana moja na kuweka kwenye mfuko wa kaki.
"Je kuna haja ya kuchukua silaha? Aliuliza Sonno.
"Hakuna haja Kuna sehemu nyingine mbovu leo, maana ni jana tu vijana wa vijana wa Makoroboi waliichachamalia serikali. Kwa hiyo licha ya askari wa upelelezi kuwa mitaani wakitafuta chanzo cha mauaji ya Inspector wa polisi, Catto na wenzake bado Kuna FFU kwa ajili ya ulinzi.
Baada ya kuwa tumemaliza mambo yetu pale nyumbani kwa dada tulipanda gari letu moja kwa moja kwenda kwa Kikakika. Tulipofika maeneo ya manispaa nilimuambia Sonno akaegeshe gari katika maegesho ya sekouture naye akafanya hivyo. Tulishuka pale tukaanza kutembea kuelekea barabara itakayotufikisha huko zahanati kwa Kikakika. Tulitembea kama mwendo wa dakika kama kumi na saba hivi ndipo tulipofika pale zahanati majira ya saa nne. Tulimkuta daktari akiwa katika sehemu yake ya kazi kama kawaida. Tulimsalimiana na baada ya salamu akatuambia mgonjwa wetu anaoendelea vizuri tunaweza kwenda kumuona. Tuliingia chumba cha wagonjwa na kukuta Kikakika akiwa amekaa huku akisoma gazeti.
"Halo Kikakika mambo vipi?" Aliuliza Sonno.
"Safi kiasi," alijibu
"Unajisikiaje rafiki yangu?" Nami niliulizwa.
"Poa kiasi chake." Alijibu.
"Vipi Sasa unaweza kutembea na kufanya mambo yako bila kusikia maumivu sana?" Nilimuuliza.
"Ndio, nilikuwa nawasubili ninyi ili nitoke hapa zahanati kwani siwezi kuendelea kuwa hapa tayari naweza hata kukimbia ikibid"i. Alisema kwa sauti ya utani wote tukacheka.
"Inaonekana wewe ni mpiganaji haswaaa"alisema Sonno.
"Tena mwanaume wa shoka." Niliongezea tukacheka tena.
"Sasa unasemaje tuondoke wote sasa hivi au tukupitie baadae kidogo maana tunataka kwenda kwa mkuu wa ofisi zetu za hapa." Nilimuuliza Kikakika.
"Mimi naona hakuna haja ya kusubiri hapa, twendeni tu." Alijibu Kikakika.
"Hapana wewe tusubiri hapa maana kwenda kwa yule mzee alafu kurudi mpaka tulipo tutakuwa tunakutonesha yaani tunakusumbua na maumivu kutokana na mtikisiko wa gari. Unajua barabara zetu zilivyo mbovu." Alisema Sonno wote tukakubaliana na wazo lake hivyo ikabidi sisi tuondoke alafu tutampitia baadae wakati tukitoka huko.

Tulimuaga na kutoka hapo zahanati kwa kuwa gari tuliegesha mbali na hapo tulianza kutembea kuelekea barabara inayokwenda jengo la manispaa ya Mwanza. Tulipokuwa tumeishavuka kama nyumba tatu hivi kutoka zahanati ilitokea gari aina ya Range Rover ilitokea tunakoelekea. Ilitupita kwa kasi kiasi cha kunishtua na kukumbuka ile Range iliyonikimbiza siku ile tulipomfungia kazi Mr Catto pale Pamba Hostel. Wakati nakumbuka hilo niligeuka nyuma kuangalia na kuona inaegesha pale zahanati tulipotokea. Iliposimama hakuna mtu aliyeteremka ila alitoka muuguzi mmoja akaongea na dereva kwa muda mfupi sana alafu gari ikageuza kwa kasi na kuangalia ilikotokea. Mambo yote hayo niliyaangalia wakati tunaendelea kutembea, tulikuwa tumefika kwenye kona iliyojirani na manispaa hivyo hivyo wakati like gari linageuzwa tulikuwa tunaishia kwenye kona ya nyumba ambayo ilitukinga tusiione ile gari
"Nina wasiwasi na ile gari," nilimwambia Sonno.
"Hata mimi nimekuona jinsi ulivyobafilika nikajua kuna jambo, kidogo nikuulize hata kabla hujasema."

Wakati Sonno anamaliza kuongea like gari lilikuwa linakata kona kushika barabara tuliyopo. Jihadhari nilimuambia Sonno tukiwa pembeni mwa barabara karibu na mtalo wa kupitisha maji iliyokuwa imekauka kutokana na kutokuwepo kwa mvua kipindi hicho. Ghafla niliona midomo mitatu ya bastola ikituelekea kutoka kwenye gari ilipokuwa inatukaribia. Ruka... Nilimwambia Sonno, kumbe na yeye alikuwa ameona. Tuliruka na kuangukia kwenye mtaro wa barabara huku risasi zikivurumishwa upande wetu. Mlio wa bastola haukusikika inaonekana walitumia viwambo vya kuzuia sauti.

Pamoja na kuwa tulikuwa tumewahi kuruka lakini Kuna risasi zilitua kwenye za vifua na tumboni. Tulishukuru kuvaa fulana za kuzuia risasi tulizozichukua kwa Patrick vinginevyo tungekuwa maiti sasa hivi. Vitendo hivyo vilifanyika huku gari likiwa kwenye mwendo kiasi kuwa hawakueza kusimama kuangalia matunda ya kazi yao kwani ilikuwa saa tano tu mchana. Hivyo walihofia kuonwa na watu au hata kuvamiwa na halaiki, Lakini mioyini mwao walihisi wametumiza malengo yao ya kutuua.

Baada ya tukio hilo watembea kwa miguu waliokuwa jirani na sisi walishangaa na sie tuliibuka toka mtaroni na kuanza kutembea kwa kasi kuelekea tulipoegesha gari letu. Walioshuhudia walishikwa na bumbuwazi wakati sie tunatokomea kiaina.
 
KAZI IENDELEE



10
Ilikuwa ni saa moja na kitu nilipostuka usingizini, nilijisikia mchovu sana hii ilitokana na kutokufanya mazoezi kwa muda. Nilimuangalia Sonno aliyelala kitanda cha pembeni yangu yeye alionekana kuamka kitambo kwani alikuwa akivuta sigara.
"Vipi Sonno?" Nilimjulia hali.
"Safi tu, naona kumekucha"alisema.
"Ndio kumekucha na makucha yake alisema na wote tukacheka."
"Leo sikusinzia kwa raha, nilikuwa naota ndoto za ajabu ajabu tu."
"Kwa hiyo inabidi tukae kwa tahadhari huenda kuna mabaya yanaweza kutufika sio?" Niliongea huku nikimtaza usoni.
"Ha!! Wapi ndugu yangu zinaweza kuwa ndoto za kawaida tu, lakini hata hivyo kuwa na tahadhari ni jambo muhimu wale watu wanaweza kuwa wameisha tunusa." Aliongea Sonno.
Baada ya hapo nitoka kitandani kwenda kuoga, nilipokuwa nimemaliza shughuri zote za usafi wa asubuhi. Nilibadiri nguo na kuvaa full jeans huku ndani nikiwa nimevaa mojawapo ya fulana za kuzuia risasi tulizozipata kule kwa Patrick.
Ilipofika saa mbili na nusu Sonno naye alikuwa tayari kishamaliza mambo yote ya usafi, alikuwa kavaa suti huku ndani kavaa fulana ya kuzuia risasi vilevile. Tulitoka chumbani na kwenda sebuleni ambapo tulimkuta dada akiwa kwenye pilika pilika za usafi. Alipotuona aliacha chughuri zake za usafi tukasalimiana na baada ya kusalimiana alitutengea kifungua kinywa nasi tukaanza kunywa.
"Vipi mbona leo mmeamka asubuhi namna hii au mna ahadi muhimu nini?" Aliongea dada wakati sisi tunaendelea na chai..
"Kuna mwenzetu mmoja ambaye inabidi tumuone kabla ya saa nne. Nilimueleza dada.
Tulipomaliza kunywa chai tulirudi chumbani nikachukua simu iliyokuwa pembeni mwa meza na kuzungusha namba 333 ambazo ni namba za yule msichana tuliyeonana nae kule Magnum Club. Baada ya kusubiri kidogo nilisikia simu ikinyanyuliwa alafu ikasikika sauti ya kiume.
"Nani mwenzangu?" Iliuliza
"Samahani kaka naomba kuongea na msichana aitwae Mtuli." Niliongea kwenye simu..
"Subiri kidogo." Ilisikika ile sauti na baada ya muda mfupi ilisikika sauti ya kike.
"Hallo nani mwenzangu?"
"Lyampili." Nilisema kwa kumtega kama ananikumbuka.
"Wewe ndie tulionana Magnum Club?" Niliulizwa.
"Ndio mimi, mambo vipi?" Nilimjibu na kuuliza.
*Haha!!! Mwanaume wewe una laana kweli, alisema kwa kebehi alafu akaendelea. Maana yake nini kuniwwka nikusubiri kama kichaa pale River Side."alimaliza na kuvuta pumzi zilizosikika hata kwenye simu.
"Sio makusudi mpenzi ni kutokana na matatizo yasiyozuilika. Nilimchomekea neno mpenzi nione muitikio wake.
"Matatizo gani yasiyozuilika? Au ulitaka kunipima pumzi zangu?" Alisema kwa sauti yenye hasira kidogo.
"Sikiliza bibie hapa kwenye simu sio mahali pa kulaumiana lililopo ni Mimi na wewe kupanga tuonane wapi." Nilibadilisha mkondo wa maongezi.
"Kwani wewe unasemaje?" Aliuliza.
"Mimi nakusikilizia wewe uniambie una nafasi saa ngapi na ni wapi tuonane" nilieleza.
"Nitapata nafasi saa saba mchana muda wa kwenda kupata chakula." Alisema.
"Muda huo haufai kuonana na wewe, tungefanya jioni baada ya kazi ingekuwa bora zaidi." Nilimueleza.
"Jioni naweza kuwa na shughuri nyingine alafu nikakosa muda." Alisema.
"Sawa lakini kumbuka unaposema tuonane saa saba mimi nahofia kutokuonana maana kuna mambo nafatilia, huenda huo muda nikajikuta sehemu ambayo siwezi kutoka kwa wakati huo hivyo mambo yakawa kama jana. Au wewe unataka tusionane tena." Nilisema.
"Hapana sio hivyo ila hata mimi nilikuwa nakupa hali halisi." Alijibu.
"Kwa hiyo ndio kusema hakuna uwezekano wa kuonana jioni ila kwa muda uliosema tu siyo?" Nilihoji.
"Uwezekano upo ila ni mdogo sana." Alisema.
"Sikiliza Mtuli najua ukiamua uwezekano upo ni kiasi cha wewe kupanga mambo yako na kuangalia muda hata wa nusu saa kwa ajili yangu. Kwani hapo ulipo sio kwamba umeolewa. Kwa hiyo unaponiambia kuwa jioni sio rahisi sikuekewi ila naelewa kuwa huna mpanga wa kuonana na mimi au sio??
"Basi Lyampili tuonane saa tatu usiku pale Jafaries, si unapafahamu? Alisema.
"Ndio." Nilimjibu.
"Sawa, kwa hiyo tuonane hapo saa tatu."Alisema.
"Sawa bibie ila jitahidi usinichomeshe mahindi." Nilisema.
"Hakuna wasiwasi, siwezi kulipiza kisasi kwa jinsi ulivyonifanyia wewe." Alisema wote tukacheka na baada ya hapo tuliagana nikarudisha simu mahali pake alafu nikageuka kumuangalia Sonno niliyemkuta alitabasamu.
"Vipi, naona mambo sio mabaya kwa jinsi unavyomwemwesa." Alisema Sonno huku akicheka.
"Wewe vipi rafiki yangu mbona unanisanifu." Nilisema huku na mima nikianza kucheka.
"Sikiliza Pheady," Sonno alikatisha kicheko na kuanza kuongea; "Inabidi tupange mpango wa kumtoa Kikakika zahanati akaugulie nyumbani au sehemu nyingine na sisi tupotee mji huu. Hata kama Kikakika hajisikii vizuri, matibabu ataendelea kupata kama kawaida. Navyoona kuendelea kumuacha pale zahanati na sisi kuendelea kuwa mji huu Haina maana, tutawanyike na mzigo tuuache mambo yakitulia tuatafanya vitu vyetu" alimaliza kusema Sonno.
"Hakuna matatizo, twende tukamuone alafu tupitie kwa mkuu wa ofisi zetu za hapa. Baada ya hapo tutakuwa na mpango kamili wa mambo yetu." Nilieleza.
"Sawa, twende tukamuone, lakini mimi nafikiri tumpelekee huko huko fulana ya kuzuia risasi vilevile avae kama sisi tulivyovaa." Alisema Sonno.
"Du," wazo zuri sana, inaonekana umekubuhu katika masuala haya." Nilimpongeza, akacheka na kukunja fulana moja na kuweka kwenye mfuko wa kaki.
"Je kuna haja ya kuchukua silaha? Aliuliza Sonno.
"Hakuna haja Kuna sehemu nyingine mbovu leo, maana ni jana tu vijana wa vijana wa Makoroboi waliichachamalia serikali. Kwa hiyo licha ya askari wa upelelezi kuwa mitaani wakitafuta chanzo cha mauaji ya Inspector wa polisi, Catto na wenzake bado Kuna FFU kwa ajili ya ulinzi.
Baada ya kuwa tumemaliza mambo yetu pale nyumbani kwa dada tulipanda gari letu moja kwa moja kwenda kwa Kikakika. Tulipofika maeneo ya manispaa nilimuambia Sonno akaegeshe gari katika maegesho ya sekouture naye akafanya hivyo. Tulishuka pale tukaanza kutembea kuelekea barabara itakayotufikisha huko zahanati kwa Kikakika. Tulitembea kama mwendo wa dakika kama kumi na saba hivi ndipo tulipofika pale zahanati majira ya saa nne. Tulimkuta daktari akiwa katika sehemu yake ya kazi kama kawaida. Tulimsalimiana na baada ya salamu akatuambia mgonjwa wetu anaoendelea vizuri tunaweza kwenda kumuona. Tuliingia chumba cha wagonjwa na kukuta Kikakika akiwa amekaa huku akisoma gazeti.
"Halo Kikakika mambo vipi?" Aliuliza Sonno.
"Safi kiasi," alijibu
"Unajisikiaje rafiki yangu?" Nami niliulizwa.
"Poa kiasi chake." Alijibu.
"Vipi Sasa unaweza kutembea na kufanya mambo yako bila kusikia maumivu sana?" Nilimuuliza.
"Ndio, nilikuwa nawasubili ninyi ili nitoke hapa zahanati kwani siwezi kuendelea kuwa hapa tayari naweza hata kukimbia ikibid"i. Alisema kwa sauti ya utani wote tukacheka.
"Inaonekana wewe ni mpiganaji haswaaa"alisema Sonno.
"Tena mwanaume wa shoka." Niliongezea tukacheka tena.
"Sasa unasemaje tuondoke wote sasa hivi au tukupitie baadae kidogo maana tunataka kwenda kwa mkuu wa ofisi zetu za hapa." Nilimuuliza Kikakika.
"Mimi naona hakuna haja ya kusubiri hapa, twendeni tu." Alijibu Kikakika.
"Hapana wewe tusubiri hapa maana kwenda kwa yule mzee alafu kurudi mpaka tulipo tutakuwa tunakutonesha yaani tunakusumbua na maumivu kutokana na mtikisiko wa gari. Unajua barabara zetu zilivyo mbovu." Alisema Sonno wote tukakubaliana na wazo lake hivyo ikabidi sisi tuondoke alafu tutampitia baadae wakati tukitoka huko.

Tulimuaga na kutoka hapo zahanati kwa kuwa gari tuliegesha mbali na hapo tulianza kutembea kuelekea barabara inayokwenda jengo la manispaa ya Mwanza. Tulipokuwa tumeishavuka kama nyumba tatu hivi kutoka zahanati ilitokea gari aina ya Range Rover ilitokea tunakoelekea. Ilitupita kwa kasi kiasi cha kunishtua na kukumbuka ile Range iliyonikimbiza siku ile tulipomfungia kazi Mr Catto pale Pamba Hostel. Wakati nakumbuka hilo niligeuka nyuma kuangalia na kuona inaegesha pale zahanati tulipotokea. Iliposimama hakuna mtu aliyeteremka ila alitoka muuguzi mmoja akaongea na dereva kwa muda mfupi sana alafu gari ikageuza kwa kasi na kuangalia ilikotokea. Mambo yote hayo niliyaangalia wakati tunaendelea kutembea, tulikuwa tumefika kwenye kona iliyojirani na manispaa hivyo hivyo wakati like gari linageuzwa tulikuwa tunaishia kwenye kona ya nyumba ambayo ilitukinga tusiione ile gari
"Nina wasiwasi na ile gari," nilimwambia Sonno.
"Hata mimi nimekuona jinsi ulivyobafilika nikajua kuna jambo, kidogo nikuulize hata kabla hujasema."

Wakati Sonno anamaliza kuongea like gari lilikuwa linakata kona kushika barabara tuliyopo. Jihadhari nilimuambia Sonno tukiwa pembeni mwa barabara karibu na mtalo wa kupitisha maji iliyokuwa imekauka kutokana na kutokuwepo kwa mvua kipindi hicho. Ghafla niliona midomo mitatu ya bastola ikituelekea kutoka kwenye gari ilipokuwa inatukaribia. Ruka... Nilimwambia Sonno, kumbe na yeye alikuwa ameona. Tuliruka na kuangukia kwenye mtaro wa barabara huku risasi zikivurumishwa upande wetu. Mlio wa bastola haukusikika inaonekana walitumia viwambo vya kuzuia sauti.

Pamoja na kuwa tulikuwa tumewahi kuruka lakini Kuna risasi zilitua kwenye za vifua na tumboni. Tulishukuru kuvaa fulana za kuzuia risasi tulizozichukua kwa Patrick vinginevyo tungekuwa maiti sasa hivi. Vitendo hivyo vilifanyika huku gari likiwa kwenye mwendo kiasi kuwa hawakueza kusimama kuangalia matunda ya kazi yao kwani ilikuwa saa tano tu mchana. Hivyo walihofia kuonwa na watu au hata kuvamiwa na halaiki, Lakini mioyini mwao walihisi wametumiza malengo yao ya kutuua.

Baada ya tukio hilo watembea kwa miguu waliokuwa jirani na sisi walishangaa na sie tuliibuka toka mtaroni na kuanza kutembea kwa kasi kuelekea tulipoegesha gari letu. Walioshuhudia walishikwa na bumbuwazi wakati sie tunatokomea kiaina.
Mdgo mdgo tutafika tu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom