Riwaya: Janga

RIWAYA: JANGA
MTUNZI: richard MWAMBE



“Samahani sana, sikujua kama moshi unakudhuru,” akamwambia na kumpulizia tena, Majoti akahisi kama anakabwa, akakosa pumzi, macho yakawa mazito, akazidiwa na kuchukuliwa na usingizi mzito. Gina akavaa fulana yake, akainua mkoba wake na kupotelea nje. Tayari ilikuwa saa tano usiku alipokuwa nje ya hoteli hiyo.
SEHEMU YA 17
AFISI NDOGO
“Vipi, yuko wapi?” Madam S akamwuliza Amata.
“Yupo kwenye usaili, tumsubiri kidogo atachelewa,” Kamanda akamjibu Mada S.
Dkt. Jasmine akatua lile faili mezani na kulisukuma kwa Madam S huku akitikisa kichwa chake.
“Vipi?”
“Nimeelewa, lakini ili nijue kila kitu kilivyo sina budi kuchukua sampuli ya ngozi ili kujua kiuhalisia nini sababu. Lakini Madam, ina maana Mkemia Mkuu hajapata hili swala? Maana kama liko mahakamani basi ilipaswa ahusishwe upande wa serikali,” Jasmine akauliza.
“Kesi ya ngedele hiyo,” Madam akajibu kwa kifupi.
“Sawa, sasa inabidi tufanye hivyo, naomba niifanye kazi hii kesho asubuhi,” akaomba.
“Bila shaka! Sasa waweza kwenda kupumzika, na kazi yetu kesho itaanzia hapa,” Madam akasema na Jasmine akainuka kitini.
Jasmine akawaacha wawili hao nay eye akaondoka zake kwa maana ni siku hiyohiyo alikuwa amefika kutoka Marekani. Kamanda Amata na Madam S wakaendelea na mazungumzo yao juu ya mikakati hasa ya kutatua kadhia hiyo.
Gina alwasili ofisini saa sita usiku na kumkuta Madam S na Amata wakimsubiri, akaketi na kuwatazama watu hao.
“Umepata kazi?” Kamanda akamuuliza.
“Nimeambiwa kesho nipeleke CV zangu kwa Bwana Momba kule Utumishi,” akajibu. Akafungua mkoba wake na kumkabidhi Madam S ile mashine ya kurekodi sauti. Mwanamama huyo akaichukua na kuipachika kadi yake kwenye kompyuta ya mezani, akaiwasha na wote wakaanza kusikiliza mazungumzo ya Gina na Majoti. Mazungumzo hayo yalionekana wazi kuwafumbua macho, Madam S akawa akiandika vitu kadhaa kwenye kidaftari chake kidogo.
Iliwachukua saa kama tatu hivi kusikiliza mazungumzo hayo mpaka mwisho.
“Mh! Sasa naweza kuunganisha picha, Shekibindu kauawa, nataka kujua nani kapanga mpango, naomba tuonane asubuhi saa tatu hapa,” akawaambia.

11
Siku iliyofuata…
JAJI SHEKIBINDU AHUJUMIWA, gazeti la Mbalamwezi liliandika namna hiyo kwenye kurasa yake ya juu kabisa, kila aliyesoma habari hiyo alivutiwa na kuangalia nani mwandishi, na hakuna aliyeamini kwa kuona kuwa aliyandika habari hiyo ni Mustafa Bashiru. Kusfikia saa tano asubuhi nakala zilikuwa zimeisha na bado kila mmoja alikuwa ana hamu nalo.
Ngishu alilikunja gazeti lile na kulitupia mezani, akawatazama vijana wake, akashusha pumzi ndefu na kuwasha sigara hata kama hakuwa mvutaji.
“Huyu mtu yupo, ina maana hata jana alikuwapo mahakamani? Kwa maana jinsi habari hii ilivyoandikwa inaonesha wazi kuwa alikuwepo,” akawaambia wengine.
“Mbona hatukumwona?” Kebby akauliza.
“Kichwa kinaniuma sana, naona kama mzigo huu unatuelemea, naomba mwanze tena kumtafuta na apatikane,” Ngishu akawaambia.
“Sawa!” wakajibu kwa pamoja na kuondoka katika kijisebule hicho. Kama kuna siku ambayo Ngishu alihisi akili yake imechanganyika na damu ilikuwa hii. Alijitupan kitini, akainamisha kichwa chake na kutulia kimya kabisa akijaribu kuyapishanisha mawazo yake, la huku kupeleka kule na la kule vivyo hivyo.
HOSPITALI YA MUHIMBILI
Daktari Jasmine aliingia kwa mganga mfawidhi wa hospitali hiyo kubwa nchini, pamoja naye alifuatana na Kamanda Amata. Baada ya kuonana na mganga huyo alipewa kibali cha kuikagua miili ile kwa ajili ya vipimo zaidi. Walivuta hatua na kupita katika vijia vya kupitia watu kuelekea kwenye mawodi lakini wao hawakuelekea huko.
Kwenye mlango mkubwa wa kuingia katia chumba cha kuhifadhi maiti walikutana na mabishano ya watu kadhaa. Kulikuwa na akina mama wawili na akina baba watatu wakibishana na mhudumu wa chumba hicho kuhusu kuchukua mwili wa ndugu yao kwenda kuuzika.
“Hivi mnanielewa, hili hapa ni andiko la zuio, miili isichukuliwe mpaka amri ya serikali, kuna uchunguzi unafanyika…”
“Uchunguzi gani bwana we!” mama mmoja akang’aka na wakati huo Jasmine na Amata walikwishafika mlangoni pale.
“Jamani hili siyo eneo la mabishano,” Jasmine aliingilia kati.
“Tena we daktari ndiyo unyamaze kabisa, mgonjwa wangu hata diripu hamjamwekea mpaka kapoteza uhai, mmekalia rushwa tu, yaani nchi hii, kama huna pesa unakufa unajiona,” yule mama aliongea mpaka akaanza kulia. Wenzake wakamtuliza na kumsogeza pembeni.
“Wewe ndiye Shabani Mtemanyongo?” Amata akauliza.
“Ndiyo mimi,” akajibu. Jasmine na Amata wakajitambulisha kwake na kumwonesha kibali cha kufanya kazi hiyo kilichosainiwa na Mganga Mkuu na kutoka jeshi la polisi. Kijana yule mwenye macho mekundu, aliyekuwa ndani ya suti safi na chupa la pombe mkononi mwake akawakaribisha katika ofisi yake kwanza. Amata akaitazama ofisi hiyo kwa mapana na marefu wakati Shabani akiongea na Jasmine lugha zao za kitaalamu. Ukutani mwa ofisi ile kulikuwa na picha nyingi sana, tofauti na ofisi za kawaida ungeweza kuona picha za viongozi au watu mashuhuri na kalenda zikiwa zinaning’inia, hapa ilikuwa ni tofauti kabisa. Ukutani kulikuwa na mapicha ya maiti za kila aina, kulikuwa na kalenda ya zamani lakini kwenye eneo la tarehe kulikuwa na karatasi nyeupe iliyoandikwa ‘unaijua siku ya kufa kwako?’.
“Afande usishangae kaka, hata wewe siku moja utakuja hapa, utalala raha mustarehe,” akamtania Amata.
“Unawezaje kuishi humu?” Amata akamuuliza.
“Kama wewe unavyoishi duniani,” Shabani akajibu huku akinyanyuka, “Dokta njoo huku mama!” akaita. Jasmine akainuka na kumfuata akiwa na mkoba wake wa kazi ulioshehni zana zinazotakiwa. Amata naye akainuka kuwafuata.
“We bwana mdogo huku hakukufai, tuache sisi tunaojua kifo ni nini,” Shabani alimwambia Amata kisha akaendelea na safari yake huku chupa ya pombe ikiwa mkononi. Wakati wao wapo huko ndani Kamanda Amata akawa anapekua ile ofisi kiutaalamu sana ili kuona nini na nini vipo. Hakukuwa na la maana zaidi ya magazeti mengi sana ya Mbalamwezi, akayapekua harakaharaka na kugundua kuwa magazeti hayo yote yalikuwa na habari za kadhia ile mpaka la siku hiyo nalo alikuwa nalo.
Ana uhusiano gani na hili swala? Akajiuliza na kujikuta akizidi kupekuwa haraka haraka, katika moja ya droo akakuta picha kama tisa hivi za watu tofauti, lakini kilichomshtua na kumshangaza ni picha ya chini kabisa, ilikuwa ya Jaji Shekibindu, marehemu. Amata akahisi baridi mwili mzima, nyele zikamsimama akashindwa kuelewa. Akachomoa simu yake na kuzipiga picha moja baada ya nyingine, alipohakikisha kamaliza, akazirudisha haraka na wakati huohuo akasikia sauti za watu wakija katika chumba hicho.
“Pole, tulikuacha peke yako,” Jasmine alikuwa wa kwanza kumwambia Amata.
“Haina tabu mi nilikuwa nainjoi tu hapa,” akajibu. Punde kidogo Shabani naye akaingia na kuketi upande ule wa pili, mazungumzo machache yakatawala kisha wakaagana na kuondoka zao.
Wakiwa ndani ya gari, Amata alimuuliza Jasmine kama amefanikiwa, akahakikishiwa kuwa kila kitu kipo sawa na safaroi ilikuwa ni kuelekea Shamba ambapo kuna chumba kidogo cha uchunguzi anachokitumia daima daktari huyu.
“Una uhakika na unachokisema? Au unachokifikiri?” Mheshimiwa Kalembo alimuuliza Ngishu.
“Ndiyo, hakuna mtu mwingine wa karibu anayeweza kusikia mazungumzo yetu kama siyo Alinda,” Ngishu akajibu. Maneno haya yakamwingia Kalembo, akatulia kimya na kufikiri jambo.
“Nakubaliana nawe kwa asilimia za kutosha kwa sababu ni siku ileile ambayo Mustafa alipotea si ndiyo?”
“Ndiyo!”
“Basi litafanyiwa kazi haraka sana, nitakupa taarifa,” Kalembo akamwambia Ngishu, “Enhe haya na huyo Kebby aliuawa?” akaongeza swali.
“Ah kama ni kweli alipewa kitisho, basi muuaji ni mwoga, lakini katumia namba ya marehemu,” Ngishu akaeleza.
“Sikiliza Ngishu, kila kukicha mambo yanakuwa mengi, sasa nini mwisho wa sakata hili?” akauliza kwa wasiwasi.
“Mambo yetu ni machache tu, kumsaka Mustafa na kumuua pia huyo aliyemuua Boban lazima tumlipizie kisasi.
Mara simu ya Ngishu ikaita, akaitoa mfukoni na kuiweka sikioni.
“Kebby!” akaita.
“Asee Ngsihu, ile gari ya majuzi, Ford Ranger tumeioana hapa mitaa ya Azania Front,” Kebby alitoa taarifa.
“Na aliyemo ndani mmemwona?”
“Yeah! Na picha tumempiga,”
“Mmefanya vyema, nitumie kwenye simu mara moja labda nitamtambua,” Ngishu akamwambia Kebby na kukata simu.
“Mheshimiwa nikuache,” akamwambia Kalembo.
“Na huyu inakuwaje, mi naona mumbane tu,” Kalembo akauliza.
“Usaijali hilo tutalifanya jioni,” Ngishu akajibu huku akitoka katika ofisi ile.
Ngishu akatoka afisini na kumwacha Kalembo bado akiwa anamalizia kazi zake mbalimbali, nje ya afisi hiyo, kabla hata hajaingia katika gari yake akamwona Alinda akiwa kasimama na kijana mmoja aliyevalia sweta lenye kofia kubwa, usoni mwake alikuwa na miwani ya jua. Akawatupia macho na taratiu akaingia katika gari yake na kuufunga mlango huku kioo kikiwa chini kiasi Fulani na kumruhusu kuendelea kuwaona watu hao.

Alinda mara baada ya kutoka ofisini alasiri ile, alijikuta akisimamishwa na mtu asiyemjua, mweusi wa wastani, mrefu mwenye nywele nyingi, miwani nyeusi na mustache uliostawi vyema chini ya pua yake. Alipogeuka nyuma kumtazama na kugundua kuwa hamjua, na kumwona jinsi alivyo, aliongeza mwendo kwa maana alimwogopa. Na yule mtu naye akaongeza mwendo kumfikia, kutokana na urefu wake haikumchukua muda akamkata mkono, akihakikisha watu hawagundua tukio hilo. Akamvuta kando na kumtazama usoni.
“Usiogope, mimi ni rafiki yako, nimejibadili tu,” yule mtu akamwambia.
Alinda akamtazama asimjue, “We n’nani?” akamtupia swali.
“Mustafa!” yule mtu akajibu.
Mwanadada huyo akamtazama tena bila kummaliza.
“Usinitafute, utaniletea matatizo,” Alinda akamwambia.
“Usiwe na wasiwasi, kwanza hakuna atayejua kuwa mimi ni yule, unajua kwa nini nimekutafuta?” Mustafa akamwuliza.
“Sijui, kwanini,”
“Nataka unioneshe wale ulionambia kuwa wanataka kuniua, siwezi kujificha siku zote kwani sina pesa za kuniweka huko,” Mustafa akamwambia Alinda.
“Mh! Wewe, we elewa hivyo nilivyokwambia, kama unataka kuwafikisha kwenye vyombo vya dola … mh, sijui maana kwa kazi yako adui wengine ni wakubwa,” akaeleza.
“Sikuelewi!”
“Mustafa…”
“Niite Jack,” Mustafa akasema.
“Ok, Jack, ni hivi, mimi nilikupa taarifa tu kwa kuwa nilipita sehemu nikasikia wanazungumza habari hiyo,” Alinda akamwambia.
“Unaniweka katika mazingira magumu,”
“Najua lakini nitafanyeje, na wakijua tu kuwa nimekupa hiyo taarifa watanidhuru,”
“Ina maana unawajua?”
“Niliwaona siku moja,” Alinda akamwambia huyo kijana na mara hiyo macho yake yakagongana na Ngishu upande wa pili wa barabara. Akahisi moyo wake ukimlipuka, almanusura aanguke, akajikaza kikike na kushusha pumzi ndefu. Mustafa akakiona kitendo hicho, akamkazia macho huyo binti na kisha kugeuza uso wake kuangalia upande wa pili, yaani nyuma yake na ndipo alipomwona Ngishu, hakumtilia maanani, akarudisha macho kwa Alinda, hayupo. Alipmtzama tena Ngishu, tayari keshaingia kwenye gari. Moyo wa Mustafa ukaanza kupiga kwa fujo akajikuta katikati ya dimbwi la sintofahamu. Akaamua kujiondo taratibu labda angeweza kumwona yule mwanamke wapi kaenda au kaingia ili amwulize ni kwa nini kashtuka na kuondoka baada ya kumwona huyo mtu.
Ngishu mara tu baada ya kuketi ndani ya gari akayarudisha macho kwa wale watu na kumwona yule kijana peke yake, binti hayupo, na yeye machale yakamcheza. Mara akamwona mtu yule akitoka taratibu eneo lile na kuingia upande wa pili nyuma ya supamaketi ya Imalaseko. Akawasha gari na kueleke upande ule ule, alipoipita ile supamaketi, akakunja kulia na kumwona yule kijana akiingia katika gari moja ndogo nyeupe na kuondoka, akaamua kuifuata ajue ni wapi itaishia.
Ndani ya gari …
Alinda alipomaliza tu kufunga mkanda, mlango wa nyuma yake ukafunguliwa na Mustafa akaingia.
“Jack utaniletea matatizo Jack!” akalalama.
“Ondoa gari anakuja!” Mustafa akamwambia Alinda. Yule msichana akaondoa gari na kuingia barabarani bila kutazama, kelele za misuguano ya matairi na barabara zilisikika huku matusi yakiporomoshwa na madereva wengine walsimamisha gari zao ghafla.
“Tunaenda wapi?” akamuuliza.
“We nuache hapo mbele mi najua pa kwenda!” Mustafa akamwambia Alinda. Mita kama mia saba hivi kwenye msongamano wa magari, Mustafa akafungua mlango na kutoka nje, akajipekua mfukoni na kumtupia kadi ya kibiashara kupitia dirishani.
“Hili likiisha unitafute, kuna zawadi yako,” akamwambia kisha akapotelea kwenye msongamano wa magari. Alinda akashusha pumzi ndefu na kuisoma ile kadi, haikuficha jina la mmiliki. Akaichukua na kutia mkobani kisha akaondoa gari maana ziliruhusiwa.
Ngishu alikutana na pingamizi barabarani, akashindwa kuingia kwa wakati, akaipoteza gari ya Alinda.
“Shiiit!” akapiga ukulele na kupiga ngumi kwenye usukani wa gari hiyo, nukta hiyo hiyo simu yake ikaita, alipoinyakua akagundua kuwa ni ujumbe mfupi wa picha ‘MMS’, akaifungua na kukutana na picha kijana shababi aliyevalia kitanashati akiwa kama anatoka kwenye gari ambayo hakuiona jina lake lakini aliweza kuitambua rangi yake, akaondoa ile meseji na kupiga namba hiyo ya Kebby.
“Hello, nimeiona picha, tutamfanyia kazi huyo mtu, sasa kuna jipya huku, naomba juu chini tumtie mkononi Alinda, niwakute hapo hapo,” akamwambia kisha akageuza gari na kurudi kwa barabara aliyokuja nayo. Haikumchukua muda alikutana na vijana wake, wakaingia kwenye gari na kuondoka, moja kwa moja mpaka mwananyamala.
“Mnaona nyumba ileeeee!” Ngishu akawaonesha.
Wote wakaitikia kwa vichwa kuwa wameiona.
“Pale ndipo anapoishi Alinda, mumnase kabla hajaingia ndani,” akatoa maelekezo. Kisha wakasogeza gari yao mahali ambapo wangemwona mwanamke huyo akiingia nyumbani kwake. Hawakukosea, wakati wanafika tu eneo hilo, waliiona gari ya Alinda ikikunja kona na kuchukua barabara ambayo ingemfikisha nyumbani kwake.
Mara ghafla Subaru nyeupe ikasimama mbele yake, vijana wawili waliovalia sox usoni wakateremka na kumuwahi, wakavuta kitasa cha mlango, umefungwa, mmoja akapiga ngumi kwenye kioo, kikatawanyika. Alinda akarudiwa na akili, akaweka gia R na kukanyaga mafuta, ile gari ikarudi nyuma kwa nguvu, na mmoja wa vijana hao ambaye alikuwa akijaribu kufyatua loki ya mlango huo aiangushwa vibaya na ile gari ikarudi nyuma na kugonga nguzo ya umeme, hakujali, alikunja kona kali na kuingia barabarani mara upande wa pili gari ya mchanga ikatoke na kuigonga vibaya ile ya Alinda, ikaikanyaga boneti na kulifumua vibaya. Alinda alijibamiza kwa nguvu kwenye usukani, vipande vya kioo cha mbele vikaruka na kumuumiza vibaya. Akasikia kelele za watu na honi za magari, kishavyote vikaanza kufifia na kiza kinene kikambeba kikichanganyika na usingizi mzito.

SHAMBA
Jasmine akiwa na karatasi kama mbili hivi mkononi mwake, aliketi kitini huku mbele yake kukiwa na Madam S pamoja na Kamanda Amata. Wote wawili walikuwa wakimsubiri kwa hamu daktari huyo maana walijua wazi kuwa majibu ya vipimo vyake yangewapa mwanga wa kipi ni kipi.
“Yes Dokta!” Madam alianza. Jasmine akakohoa kidogo na kuzibwaga zile karatasi mezani.
“Nimechunguza sampuli ya ngozi ya mmoja wa marehemu na pia nimechunguza baadhi ya vipodozi tajwa ambavyo nimevinunua mwenyewe dukani. Bila shaka ndani ya jelli na losheni hizo nimekuta kuna viambato ambavyo serikali ilikwisha piga marufuku na viwanda vyake vilikwishasimamaishwa uzalishaji hapa Tanzania, sasa inaoneaka kwa sasa vipodozi hivi vinaingizwa kutoka nje, viambato nilivyovigundua ni Steroids ambayo hujulikana kama Clobetasol Proprionate, Hydrocrotis One na Triamcinolone. Sasa binadamu akitumia vipodzi vyenye kemikali hizi madhara anayoyapata ni pamoja na kuvimba mwili, muwasho, ngozi kuwaka moto, ngozi kukatikakatika, kubabuka, kuwa nyeupe isiyokuwa ya kawaida, zaidi ya hapo hupata madhara kwenye mifupa, kizunguzungu pamoja na madhara mengine mengi ikiwamo kichwa kuuma sana,” Jasmine akawaambia Amata na Madam S, akazifunga zile karatasi na kumpa bosi wake. Madam S akazipokea na kuziweka vizuri.
“Ina maana, idara ya upimaji wa viwango haijaona hili, maana haya makopo yote ukiyaangalia yana nembo ya viwango ina maana yamepitishwa kwa matumizi ya binadamu, kuna nini hapa?” Kamanda Amata akauliza kwa mashaka. Madam S akamtazama kijana huyo huku akitikisa kichwa kumaanisha amelielewa vyema swali hilo.
“Amata, Jasmine, hapa kuna kazi ngumu nimeelewa nini kinaendelea,” Madam akazungumza, “Sasa tunafanyaje?” akamtupia swali Jasmine.
“Nahitaji kuonana na madaktari wa hospitali hizi ili nipate majibu ya vipimo vya marehemu hawa na kisha nioanishe na kile nilichonacho,” Jasmine akaeleza.
“Zaidi ya hapo, inabidi tuimulike hii idara ya viwango, kuna kitu si kidogo ni kikubwa,” Amata akaongeza.
“Tunaanzia wapi?” Madam akauliza, “Maana hawa washenzi nataka kuwabana kabla kesi haijasomwa kwa mara nyingine.
“Jasmine aanzie hospitali kama alivyosema, na mimi nitaendelea nilipo,” Amata akatoa ushauri na wote wakakubaliana nao.
Kebby akakung’uta mkoba wa Alinda aliounyakua kwenye eneo la ajali, kulikuwa na simu kubwa ya kisasa, vipodzi kadhaa, pedi na vikolokolo vingine, akiwa katika kuweka kando begi hilo ndipo akaiona ile kadi ya kibiashara, akaichukua na kuisoma.
Mustafa Bashiru
Gazeti la Mbalamwezi.
Pamoja na maelezo hayo kulikuwa na namba za simu na mawasiliano mengine, akamkabishi Ngishu.
“Mzee kazi imeisha!” Kebby akamwambia Mhindi koko huyo huku akimkabidhi ile kadi.
“Aaaa ha ha ha ha basiiii, kazi imekwisha, huyu anakamatika le oleo na tunamchinjiliza mbali,” Ngishu akasema.
“Sasa tutafute mwanamke mzuri mwenye sauti tamu, ajisanye ni Alinda, kisha ampigie wakutane mahali atakuja tu,” Kebby akatoa ushauri na kila mmoja akaukubali, mkakati ukaandaliwa tayari kwa kumnasa mwanahabari huyo.

12
Pambazuko la aiku iliyofuata lilimkuta Kamanda Amata ndani ya ofisi ya gazeti la Mbalamwezi akiwa uso kwa uso na Mkurugenzi wa gazeti hilo.
“Kwa kweli, mi sijui hata huyu mtu yuko wapi,” yule mkurugenzi alimwambia Amata kutokana na swali aliloulizwa.
“Sikiliza, jana mmetoa habari ambayo imeandikwa na Mustafa ina maana mna mawasiliano naye,” Amata akamwambia Mkurugenzi yule, swali hilo lilimshtua kwa kuwa hakulitegemea na kweli gazeti lililopita alichapa habari ya mtu huyo. Hakuwa na ujanja.
“Nililetewa habari kwenye bahasha,”
“Na nani?”
“Mi simjui, lakini kwa namna fulani kashahabiana na Mustafa,” yule mkurugenzi akajibu.
“Sikiliza, mimi ni afisa wa polisi, na tunamtafuta mtu huyu kwa usalama wake, hivyo mara tu utakapomuona kaja tena hata kama si yeye, nipe taarifa haraka, maana maisha ya mwandishi huyu yapo hatarini, tunahitaji ushirikiano wako,” Amata akamwambia yule Mkurugenzi na kisha akasimama tayari kwa kuondoka.
Alipoagana na mwenyeji wake, mlangoni akakutana na mtu ambaye sifa zake ni zile alizoambiwa. Mrefu, mweusi, ana nywele ndefu na mustachi wenye afya. Kamanda Amata akamtazama haraka kwa jicho lake la tatu, akagundua kuwa mtu huyo kajivika mustachi wa bandia kwani uliinama kidogo upande mmoja. Akili yake ikamwambia kitu, hata hivyo hakusimama akaendele na safari yake mpaka kwenye maegesho akaingia garini na kusubiri. Dakika kama kumi na tano hivi alimwona yule mtu akitoka katika jingo lile la Mbalamwezi na kutaka kuingia kwenye gari moja ndogo iliyochoka kiasi.
Mustafa kwenye muonekano wa kibandia, hakupanda ile gari na moja kwa moja alikiendea kibanda cha magazeti na kukutana na habari iliyosisimua mwili wake.
MAJAMBAZI YAMVAMIA MTUMISHI WA WIZARA, habari hii ilimvuta akaisoma lakini almanusura aanguke baada ya kuona kuwa aliyevamiwa ni Alinda, mtu ambaye jana tu walikuwa pamoka kwa upande mwingine ni kama malaika wake. Akanunua lile gazeti na kulielekea gari alilkuja nalo. Ghafla akasimama na kuchukua simu yake, akaiangalia, ikampa mshangao. Namba iliyokuwa ikiita ni ya Alinda, na habari aliyoisoma ilimhusu mwanadada huyo. Haraka akaipokea na kupokelewa na sauti inayofanana na ile ya Alinda lakini ilikuwa chini kiasi. Mustafa akajua labda kwa kuwa ana maumivu hawezi kuongea vyema. Sauti ile ilimwelekeza Mustafa kuwa afike nyumbani kumwona kwani ameruhusiwa na pia ana habari nyeti ya kumpa.
Kamanda Amata akajua kwa vyovyote kuna jambo ambalo limemchanganya kijana huyo, akaifuata gari yake mara tu baada ya Mustafa kuingia barabarani.
Ngishu akamtazama Kebby, kisha akaitazama tena ile picha kwenye simu.
“Ushawahi kumwona?” Kebby akauliza.
“Hapana, sijawhi kumwona lakini nashindwa kujua kwa nini anataka kujiingiaza katika mzozo huu!” Ngishu akamwambia Kebby.
“Anaweza kuwa polisi,” Kebby akasema kwa mashaka.
“Ni kweli sasa huyu ni kuimfutilia mbali kwa risasi moja tu,” Ngishu akamwambia kijana huyo.
“Ngishu! Vijana wanasema wameshamtega Mustafa Mwananyamala…”
“Oh good! Twende zetu huko huko, kumbuka leo ni kumuua tu na si kumwachia aheme,” Ngishu akasisitiza, wakaingia garini na kuondoka kwa kasi kuelekea Mwananyamala.
“Mwanaharamu huyu, leo lazima iwe zamu yake,” Kebby naye akang’aka huku akibadili gia na kuiacha Barabara ya Gerezani na kuchukua ile ya Msimbazi kuelekea Fire. Akiwa kasi katika barabara ya Morogoro, Kebby akasikia simu yake ikiita, akainyakuwa kwa mkono wa kushoto huku ule wa kulia ukiendelea kukamata usukani. Alipoitazama akakutana na namba ya Boban marehemu, akahisi moyo wake ukiganda kwa ubaridi. Akafyatua kitufe cha kupokelea na kuiweka sikioni.
KITABU CHA ‘MPATANISHI’ KINAPATIKANA
DAR ES SALAAM, DUKA LA KONA YA RIWAYA, PIGA SIMU 0655428085
MBEYA , DUKA LA FANANI NA HADHIRA, PIGA SIMU 0754091481
“Aaaa ha ha ha ha! Jana nilikudanganya tu, lakini sasa tutakutana mchana huu,” sauti ya upande wa pili ikamwambia. Kebby akawasha indiketa na kutoa gari nje ya barabara.
“We mpumbavu vipi! Hujui tunapoteza muda?” Ngishu akang’aka.
“Ngishu, nimepokea hii simu namba ya Boban,”
“Unasema!” Ngishu akashangaa na kuichukua ile simu, alipotazama simu zilizoingia kweli akaikuta ya mwisho ni ya Boban. Hakusita, akaipiga, ikaita na kuita lakini haikupokelewa.
Kamanda Amata akatabasamu, akabadili gia na kuongeza mwendo. Watakoma, nitawafanyia mchezo huu mpaka wachanganyikiwe, Amata akawaza na kusonya. Akahakikisha haipotezi gari ya Mustafa. Walipofika Kinondoni kwenye taa za kuingia Barabara ya Kawawa, gari ya Mustafa ikapita, gari mbili za kati zikasimamishwa.
“Aaaaa come on!” akapiga ukulele na kujaribu kuitoa gari nje ili aingilie upande wa pili, a wapi! Tayari gari zilibana kila upande. Dakika tano baadae wakaruhusiwa kupita, Amata akakamata Barabara ya Mwinyijuma kwa kasi kubwa kuelekea Mwananyamala ilhali hajui wapi hasa mtu huyo aendako. Ford Ranger ilifanya ovateki za hatari barabarani na kila mtu akatahayari kwa mwendo huo. Alipofika Komakoma akapunguza mwendo na kutembea taratibu, mara ghafla kwenye kioo chake cha kulia akaiona ile Subaru nyeupe ikija kasi, akawasha indiketa na kuitoa gari yake nje ya barabara. Ile Subaru, ikampita halafu mbele kidogo ikasimama na kurudi nyuma mpaka pale gari ya Amata iliposimama. Ngishu akashuka na kuifuata ile gari, Amata akshusha kioo taratibu baada ya kumuona Mhindi huyo, ambaye sasa ni mara ya kwanza anakutana naye uso kwa uso. Ngishu akasimama pale dirishani na kumtazama Kamanda Amata, na Amata naye akafanya vivyo hivyo.
“Ukiendelea kunifuata fuata nakuua!” Ngishu akamwambia Amata kisha akamwonwsha kidole cha kati.
“Umeshaua wangapi mpaka sasa?” Amata akauliza huku akipandisha kioo.
Mustafa alifika Mwananyamala pasi na kujua wapi anatakiwa kuelekea, akapunguza mwendo ili aweze kupiga simu kwa mwenyeji wake, akiwa katika harakati hizo aistuka kioo cha gari yake kikitawanyika vibaya. Akayumba barabarani na kutoka nje ya barabara, akajaribu kuiweka gari yake vizuri lakini hakufanikiwa alipojikuta akipokea jiwe lililotua kichwani mwake na kumwachia jeraha kubwa, damu zikaanza kummwagika, maera mlango wa gari hiyo ukafunguliwa kwa ghafla, akavutwa nje na kuangushwa chini. Akajitahidi kuinuka lakini teke kali ikatua usoni na kumtupia upande wa pili.
Nukta hiyo hiyo ile Subaru ikaibuka eneo la tukio, Ngishu akafungua mlango na bastola mkononi, la haula! Kabla hajafanya lolote, gari yake kishindo kikubwa kikasikia, ile Subaru ikagongwa na gari la taka taka, Kebby ambaye bado alikuwa hajatoka katika gari akajikuta akibanwa vibaya mpaka akashindwa kupumua, Ngishu akasukumwa na kubwagwa kando, mshike mshike.
Watu wakaanza kusogea eneo hilo baada ya kusikia kile kishindo, ndani ya gari la takataka, Amata akashuka haraka, na kumwona Ngishu akijiweka sawa na bastola yake, Amata akaruka sarakasi maridadi na risasi zilizotoka kwenye bastola ya Ngishu zikamkosa, naye akatua kifuani mwa Mhindi huyo kwa miguu yote miwili na kumpeleka chini. Ngishu alianguka chini huku bastola ikimtoka mikononi.
“Tat! Tat! Tat! Tat!” risasi mfululizo zikapigwa hewani, Amata akajitupa chini akaviringika mpaka kwenye gari bovu lililosimama eneo hilo na kujificha huku akishuhudia wale jamaa wakikokotana na kuingia kwenye Regius nyekundu, wakapote a zao. Akajitokeza na kumuwahi Mustafa pale chini, akaiendea gari ya jirani na kuchomoa funguo zake zisizoshindwa, akafungua na kuimtupia Mustafa siti ya nyuma, yeye akakaa nyuma ya usukani na na kuondoka kwa kasi mpaka eneo la Komakoma alikoiacha gari yake, akamshusha Mustafa na kumpakia kwenye Ford kisha wakatokomea.

ITAENDELEA.
 
RIWAYA: JANGA
MTUNZI: richard MWAMBE


“Tat! Tat! Tat! Tat!” risasi mfululizo zikapigwa hewani, Amata akajitupa chini akaviringika mpaka kwenye gari bovu lililosimama eneo hilo na kujificha huku akishuhudia wale jamaa wakikokotana na kuingia kwenye Regius nyekundu, wakapote a zao. Akajitokeza na kumuwahi Mustafa pale chini, akaiendea gari ya jirani na kuchomoa funguo zake zisizoshindwa, akafungua na kuimtupia Mustafa siti ya nyuma, yeye akakaa nyuma ya usukani na na kuondoka kwa kasi mpaka eneo la Komakoma alikoiacha gari yake, akamshusha Mustafa na kumpakia kwenye Ford kisha wakatokomea.
Daktari Jasmine na Gina walikuwa katika hospitali ya Amana, kikao cha dharula kilifanyika ndani ya afisi hiyo. Wanawake hao walijitambulisha kuwa wanatoka ofisi ya Mkemia Mkuu. Daktari wa hospitali hiyo aliwasikiliza hoja zao na kuzipitia tafutishi za Jasmine.
“Kiukweli, haya yaliyogunduika huko ndiyo haswa yaliyokuwa yakiwapata wagonjwa hawa mpaka wamekufa,” Mganga yule akakubaliana na Jasmine. Kisha baada ya mazungumzo hayo walipita kwenye wodi ya akina mama kutazama hali ya mgonjwa mmoja aliyesalia. Baada ya kumuona na Jasmine kuzungumza na ndugu wa mgonjwa walirudi afisini na kuweka mambo fulani mezani. Mganga mkuu wa hospitali ile alieleza kwa kirefu sana juu ya tatizo hilo.
“Kwa nini tangu kipindi hicho hakutoa taarifa hata wizarani tu?” Gina akachomeka swali ambalo lilionesha wazi kumbabaisha yule daktari. Jasmine alimtazama swahiba wake lakini hakumsemesha lolote.
“Taarifa tumetoa na sampuli ndiyo hii iliyokuja kwenu,” akajibu.
“Ok dokta, nashukuru kwa ushirikiano wako, tutawasiliana kama tutahitaji mengi zaidi,” jasmine aliaga.
Wakapeana maikono, wanawake wale wakaondoka kutoka katika ile hospitali na kurudi katika gari yao. Gina akiwa nyuma ya usukani, sura yake ilisawajika kwa hasira na mawazo, Jasmine alimtazama na kisha akashindwa kujizuia.
“Vipi shost?” akamwuliza.
“Kuna vitu nchi hii vinaudhi sana, hivi kweli watu wanakufa halafu wengine wanaona kawaida tu!” akamjibu.
“Utafanyaje sasa, ndiyo Afrika yetu hiyo, pesa ina thamani kuliko maisha,” Jasmine akajibu huku akifunga mkanda wa usalama. Gina wakati anawasha gari, simu yake inayotumia satellite ikaita kwa fujo, akaichukua na kutazama kwenye kioo, akatabasamu.
“TSA 5, nipe mpya!” akaitika kwa mtindo wa kikazi zaidi, maana simu hiyo inapoita basi huwa ni ujumbe wa kikazi zaidi.
“Mustafa Bashiru tunduni, safari Shamba,” Amata akaijibu simu hiyo na kukata ile simu. Akamtazama Jasmine na kumtolea tabasamu hadimu kabisa.
“Mbona umefurahi sana?” Jasmine akauliza.
“Sasa kazi inaanza Jasmine, kama kuna mtu tuliyekuwa tukimtafuta ni huyu Mustafa, anajua siri kubwa sana katika hili, Amata amampata na sasa anaelekea Shamba,” akamwambia.
“Oh! Safi sana,” Jasmine naye akalifurahia hilo, safari ikaanza kueleakea Shamba.
“Aaaaaiiiggghh!!!” Kebby akapiga ukelele wa maumivu.
“Tulia kaka, we mwanaume!” Kadoda akamwambia Kebby wakati wakijaribu kumpa huduma ya kwanza katika majeraha yake.
“Mshenzi yule, atanitambua,” Ngishu akapiga kelele ya hasira huku akizunguka huku na kule ndani ya banda hilo ambalo hutumika kama maficho yao.
Baada kufanikiwa kujiokoa katika tukio lile, Ngishu na wenzake moja kwa moja walikimbilia bandani, kila mmoja alitahayari kwa kile kilichotukia, hawakutegemea. Kwao walihesabu ni mafanikio kwa kumpata Mustafa badala yake wakakutana na kitu wasichotegemea.
“Yule mshenzi ni nani?” Kadoda akauliza.
“Mi sijui, lakini sasa nimeona kuwa si mtu wa kumdharau, lazima tumfungie kazi, atapatikana tu, yaani kachokoza nyuki,” Ngishu aliendelea kuongea na muda huo huo mlango wa siri ukafunguliwa na mtu mmoja mwenye mwili akaingia katika banda hilo.
“Poleni sana vijana, imekuwaje?” Kalembo akawauliza. Ngishu akasimulia kisa kizima ambacho kilimwacha mtu mzima kinywa wazi. Akiwa kavaa sox kujiziba uso, Kalembo alisikitika sana juu ya hilo, akamtazama Kebby aliyekuwa na hali mbaya akipumua kwa shida, akamgeukia tena Ngishu.
“Huyo mtu yukoje?” akamwuliza.
“Ah sijawahi kumwona kabla,” Ngishu akajibu na kuitafuta picha katika simu yake, akamwonesha Kalembo, “Labda unaweza kumjua,” akaongeza kusema.
“Hapana, sijawahi kumwona. Anaweza kuwa mpelelezi, labda!” Kalembo akawaambia vijana wa ke huku akimpa simu Ngishu.
“Kama ni mpelelezi si mambo yataharibika?” Kadoda akauliza.
“Hapana, dawa yao naijua. Muandaeni Kebby afikishwe kwenye matibabu kwa daktarai wetu, halafu Ngishu tuonane baadae kwenye ukumbi wa mkutano,” Waziri Thomas Kalembo akaondoka katika banda lile na kuwaacha vijana wale wakimwandaa mwenzao kwenda kwa daktari.
Kamanda Amata akaegesha gari pembezoni mwa Barabara ya Ally Hassan Mwinyi, karibu na njia panda ya kwenda Agha Khan, akageuka kumwangalia Mustafa, akamwona bado anatweta kwa nguvu.
“Ulikuwa unakufa, mshukuru Mungu wako,” Amata akamwambia.
“Asante kwa kuniokoa,” Mustafa akajibu na wakati huohuo kioo cha gari kikagongwa kwa konzi, Amata akashusha kioo.
“Tayari,” Scoba akamwambia Amata kutokea upande wa nje. Kamanda akafungua mlango na kuteremka nje, kisha akaufungua ule wa nyuma na kumwambia Mustafa ateremke.
“Mfuate huyo!” akamwambia na Mustafa akamfuata Scoba mpaka kwenye Land Cruiser V8 yenye rangi nyeusi na vioo vyeusi, akamwingiza siti ya nyuma na kumfungia, kisha yeye akarudi na kuketi nyuma ya usukani. Akavuta droo ya gari hiyo na kuto sox jeusi.
“Vaa hii tafadhali,” akamwambia. Mustafa akahamaki kwa kile alichopewa, sox jeusi, lililotobolewa matundu mawili. Akalitazama na kisha kulivaa kama alivyotakiwa kufanya. Haikumchukua dakika tatu tangu gari ile kuondoka, Mustafa alibebwa na usingizi mzito, usingizi usio na ndoto wala mang’amung’amu.

BUSHTRACKER
Tangu waanze kukutana hapo katika hoteli hiyo kupanga mambo yao na mara nyingine kujikuta wakisema kuwa ni kikao cha daharula, basi walikuwa wanakosea, hiki cha siku hii ndicho hasa kikao cha dharula kwa jinsi kilivyoitishwa. Kila mjumbe wa kikao alikuwa na kimuhemuhe cha kujua kulikoni, mara hii walikutana karibu wote hata wale ambao wao kazi yao ilikuwa ni kupata maagizo tu, kila mmoja alikuja kwa wakati wake na sasa walikuwa watatu ndani ya chumba hicho. Ankhit, Suleiman na Kalembo.
Waziri huyo aliwapa taarifa fupi ya hayo yaliyotukia upande wa pili mchana wa siku ile, kila mmoja akawa na ushauri wake katika nini cha kufanya ili kulinda maslahi yao. Mara hii dhana ya kutumia ‘rushwa’ ilionekana kukosa mashiko kutokana na kwamba kila kitu kingekuwa hadharani ndani ya muda usiojulikana.
“Ndiyo hivyo!” Kalembo akamaliza.
“Tutampataje huyo mtu?” Suleiman akauliza.
“Kwa kweli sijui, kinachonitia wasiwasi nikuwa, huyu Mustafa yuko wapi kama vijana wetu wamemkosa? Je kama huyo waliyepambana naye ni askari mpelelezi na kamchukua Mustafa, si mambo yameharibika? Huyu bwege atasema mpaka asiyoyajua,” Kalembo akaeleza kwa uchungu.
“Hapana jua kitu hiyo!” Ankhit akawatuliza.
“Nikwambie kitu Ankhit?”
“Ee ambiya mimi nasikia,”
“Nimeshafanya uchunguzi wa wapi mtu huyo kapelekwa, lakini vituo vyote vya polisi hayupo, sasa yuko wapi?” Kalembo akamwambia Mhindi huyo. Ankhit alionekana wazi kuchanganyikiwa hasa kwa kusikia jibu hilo, maana kwa mpango wake alitaka wajue kahifadhiwa wapi ili ikiwezekana wamfanyia mauaji huko huko, wao waliamini hakuna kisichowezakana chini ya jua.
“Sasa hakikisheni mnajiweka vizuri, ila msiwe na wasiwasi, mimi nipo, ni mtu mkubwa serikalini, nitahakikisha naliweka sawa na business zetu zitaendelea kama kawaida,” akawatia moyo.

SHAMBA
Usiku wa siku hiyo
Mustafa Bashiru alizinduka kutoka katika usingizi mzito majira ya saa saba usiku, aliangaza macho yake huku na kule asijue wapi alipo. Mwanga mkali sana wa taa kubwa iliyokuwa juu ya kitanda cha chuma kama cha upasuaji liliyasumbua macho yake. Hakajaribu kujigeuza akakuta mikono yake imefuingwa kwa vyuma maalumu vilivyo katika kingo za kitanda hicho. Alipojitikisa kwa nguvu vile vyuma vikafyatuka na kurudi ndani, akawa huru, akaweza kunyayua mikono na pia miguu. Muda huohuo na ile taa ikazimika. Giza nene likatawala kile chumba, Mustafa akaona nuru hafifu upande wa pili, akajitoa kitandani na kusogea kule ambako kunaonekana ile nuru, kioo, hakukuwa na njia. Mara taa za awaida zikawaka na hapo hakuweza kuiona ile nuru tena, mlango ukafunguliwa, akashtuka na kugeuka kutazama. Macho yake yakatua kwa vijana wawili, wote akawatambua, mmoja ni yule aliyemwokoa katika mikono ya wabaya wake kule Mwananyamala na mwingine ni aliyemchukua kutoka pale Upanga. Ila hakuwajua majina yao.
“Mustafa Bashiru!” Scoba akaita na kijana huyo akaitika kwa kichwa, “Njoo huku!” akamwita na kisha wakatoka wote watatu mpaka katika chumba kingine. Chumba kitupu, chenye meza moja, na viti vitatu vya chuma.
“Msinitese jamani tafadhali, mi kila kitu nitawaambia,” Mustafa aliongea kwa kitetemeshi.
“Usiogope Mustafa, sisi hatupo hapa kwa ajili ya kukutesa, tunataka tufanye mazungumzo ya kirafiki, mazungumzo yetu, na majibu yako yataokoa taifa hili,” Kamanda Amata akamwambia Mustafa na kumtuliza.
Scoba akaja na magazeti na kumwekea mezani, matoleo kama matano hivi ya gazeti la Mbalamwezi.
“Haya magazeti yote yana habari iliyoandikwa kwa mkono wako Mustafa, nahitaji unisomee gazet moja baada ya jingine kisha tuzungumze machache, wewe utatuambia yako unayoyajua, na sisi tutakwambia yetu tunayoyajua,” Amata akamwambia. Mustafa akavuta yale magazeti na kuyaweka mbele yake. Mustafa akasoma habari ya kwanza iliyozungumzia uingizwaji wa vipodozi hatari, alipoimaliza akafunga gazeti na kuliweka kando.
“Una uhakika gani kama vipodzi hivyo ni vya sumu?” Amata akauliza.
“Nimefanya uchunguzi mara baada ya kutokea vifo hivyo, niliwahi kuongea na wagonjwa kabla ya vifo vyao na majibu yao yalifanana hasa katika jeli na losheni walizotumia, baada ya kufuatilia bishaa hiyo katika maduka ya vipodozi, nikagundua kuwa havikuwa na muda mrefu tangu vimeingia nchini kutoka nje. Na pia aina hiyo ya vipodozi ilikwishakatazwa kuingia au kutengenezwa nchini,” Mustafa akajibu.
“Nikikwambia kwamba habari uliyoandika ni ya uongo, utakubali au utakataa?”
“Ninakataa kwa sababu kama ni ya uongo kwa nini waliniteka, wakanipiga sana na kunambia nifunge kinywa changu kwani mara nyingine wangeniua,” Mustafa akaongea kwa jazba.
“Walikuteka?” Amata akauliza.
“Ndiyo!”
“Unawajua waliokuteka?” Amata akaongeza swali.
“Hapana, walficha nyuso zao, lakini ninachokumbuka, mkubwa wao ni mnene, anaonekana ni mtu mwenye pesa na alama paekee niliyoikariri kwake ni kovu, ana kovu kubwa mguuni maana siku hiyo alivaa kaptula,” akaeleza na zaidi ya hapo alieleza jinsi alivyotekwa na mpaka kujikuta hospitali.
“Ok, ulijuaje kama waliokuteka walifanya hivyo kwa sababu ya habari hii au jambo hili?” swali lingine likatua kwa Mustafa.
“Si kwamba nafikiria tu, ni kuwa nina uhakika, ijapkuwa nilikuwa na hali mbaya lakini niliikariri sentensi hii nanukuu ‘Hili ni onyo, nakuacha hai, ukijifanya mjanja wa kuandika tena kinachohusiana na hivyo vipodozi sijui nini nitakushughulikia, kunguni wewe!’ maneno haya yananipa uhakika wa hili,” akaeleza huku machozi yakimtiririka.
Baada ya maswali na majibu hayo, Mustafa akatakiwa kusoma habari ya pili, hii ilisisimua zaidi ni juu ya utata wa ajali iliyochukua maisha ya Jaji Shekibindu.
“Niliandika habari hii baada ya kutoka hospitali na kuifanyia uchunguzi, kwa nini jaji afe siku moja kabla ya kusoma hukumu? Na nikioanisha na yale yaliyonitukia mimi, bila shaka, kuna uhusiano mkubwa sana katika hili,” akaeleza baada ya swali aliloulizwa.
Amata akamtazama Scoba kisha akavua pumzi ndefu na kurudisha macho yake kwa Mustafa ambaye alikuwa amenyamaza kimya ila alionekana kkuwa na mawazo mengi.
“Umeshawahi kukutana na Jaji Shekibindu kabla?” Scoba akauliza.
“Ndiyo, niliwahi kumhoji mara tu baada ya kesi hiyo kusomwa kwa mara ya mwisho, ila aliniomba nisiandike habari ile kabisa, bali ibaki kuwa siri yangu. Mbaya zaidi Jaji Shekibindu aliniambia niiandike tu kama yeye atakuwa amekufa, maana alionekana wazi kuwa anajua atakufa, mahojiano yangu nay eye yapo kwenye tape recorder yagu,” Mustafa akaeleza na habari hii ya sasa iliutia joto moyo wa Amata.
“Hiyo recorder ipo wapi?”
“Nyumbani,”
Wamemuua, akawaza na kuinama chini kwa sekunde kadhaa.
“Ok, na katika habari ya juzi ni ni wewe mwenyewe uliiandika au la?”
“Ipi?”
“Hii hapa,” Scoba akamsogezea gazeti lililobaki na Mustafa akapitisha jicho na kutabasamu.
“Hakika Shekibindu kahujumiwa, kwani nina uhakika kama angehukumu kesi hii basi ingekuwa ni kilio kwa hawa wafanyabiashara dhalimu, ila kwa kuitishwa tena uchunguzi upya, hapa kuna jambo,” akawaambia.
“Swali la mwisho. Mwananyamala ulikuwa ukienda kufanya nini?” Amata akauliza.
“Nilipigiwa simu na msichana mmoja anaitwa Alinda, alinitaka nimwone huko,” akajibu.
“Alinda ni nani kwako?”
“Alinda ndiye aliyenipa taarifa ya kuwa natafutwa niuawe, nay eye ndiye akanitaka mimi kutoroka haraka,” akajibu.
“Ina maana yeye anawajua wauaji,” Scoba akadakia kwa kauli ya shaka.
“Sidhani kwa sababu alinambia tu kuwa kawasikia sehemu wakiniongelea, na ndipo akanitafuta,”
“Nikikwambia kuwa Alinda ni jambazi, na alikupigia simu uende ili uuawe, utakubali au utakataa?” Amata akauliza.
“Nakataa,”
“Kwa nini?”
“Kwa sababu ni jana yake jioni alivamiwa na majambazi, hata alivyonipigia simu alionekana kuwa hakuwa na hali zuri,” Mustafa alipoeleza hilo alikuwa kama kawapa daraja watu hao kuunganisha matukio hayo na lile lililotokea huk Mwananyamala ambalo magazeti yameandika siku hiyo.
Kamanda Amata na Scoba wakatazamana na kuongea kwa ishara za macho kisha Amata akatoka ndani ya chumba hicho, na Scoba akamchukua Mustafa na kumpeleka katika chumba kingine kabisa chenye kitanda kidogo, kiti kimoja na friji ya vinywaji.
“Hii itakuwa nyumba yako kwa muda!” akamwambia na kumfungia humo kisha yeye kuondoka.
Mahojiano ya Mustafa na TSA yalichukua takribani saa nne, mpaka wakati akiingizwa katika chumba cha kupumzikia, tayari saa ya ukutani ilikuwa inakariia kunesha kuwa ni saa kumi na mbili kasoro robo asubuhi.
Chumba kidogo kiliwakutanisha wote watano, huku vikombe vya kahawa vikiendelea kumiminiwa matumboni mwao. Ilikuwa ni wakati wa kuweka taarifa pamoja.
“Kwanza namkaribisha Chiba, pole sana kwa safari ndefu na kazi nzito,” Madam S alianza namna hiyo na kila mtu alirudia kumkaribisha mwenzi wao huyo maana hakuwapo nchini kwa takribani miezi miwili kutokana na majukumu ya kikazi nje ya nchi.
Baada ya hapo zilitumika saa nyingine mbili kuweka taarifa zote pamoja ili kupata mwanga wa wapi pa kunazia katika kumaliza janga hilo. Gina aliwasilisha tafutishi zake alizozipata kutoka kwa Majoti, walipozichanganya na majibu ya Mustafa wakapata jibu kuwa Jaji Shekibindu ameuawa kwa asilimia tisini. Na sakata zima lipo kwenye mikono ya wakubwa na ndiyo wanaolipeleka namna hiyo.
“Madam umeona kazi hiyo?” Amata akauliza.
“Nimeelewa vema kabisa, na ninachotaka sasa ni kujua nani na nani kati ya hao vigogo yuko nyuma ya hili,” Madam akaeleza.
“Ukishwajua?” Chiba akapandikiza swali linguine, “Maana mara nyingi tu tumegundua kuwa wanahusika na kadhia mbalimbali, serikali imewafanya nini?” akaongeza swali.
“Usemalo Chiba ni sahihi kabisa, mara nyingi tu, si mara moja, ushahidi unaonekana kabisa, waziri Fulani anahusika lakini hachukuliwi hatua. Hatuna la kufanya kwa hilo wanangu, sisi tutimize wajibu wetu kisha tuikabidhi serikali yenyewe itajua nini cha kufanya,” akamaliza.
“Hapa kuna mlolongo wa watu wengi, na lazima wote wawe chini ya ulinzi, watu wa idara ya vipimo hawawezi kuniaminisha kuwa wamepima wakakuta vipodozi hivyo ni salama, no!” Jasmine naye akaongeza kusema.
“Na bandarini vinaingiaje?” Gina akadakiza.
“Nchi hii ina uozo kila kona, rushwa imekuwa janga la taifa, wasiwasi wangu ni kuwa hawa wanyonge watakapjua kuwa wanaikosa haki yao, itakuwaje?” Madam naye akaongezea, “Sisi kama wanausalama tunajitahidi sana kuweka mambo sawa, lakini hawa wa juu wanatuumiza, hawaoni kama tufanyalo ni la muhimu kwao, wao kazi yao ni kutumbua pesa na kuwafunga vinywa wanaotaka kusema wazi kama akina Mustafa,” Mada akaongea kwa hasira na kuinuka kitini huku akiwaacha vijana wake wakiwa bado wanamsikiliza.
“Safari hii ni maamuzi magumu tu wanangu!!!” sauti ya Madam ikasikika kutoka kwenye korido.
“Ok bibi sasa akili yake imeshachoka, tuingie kazini tumalize sakata hili, hapa lazima TAKUKURU ihusike kuchunguza idara ya viwango, bandari, na mahakama na kila anayehusika tutahakikisha hatua stahiki zinachukuliwa. Tupo kwa ajili ya Watanzania, kama hatuna bunduki za kupigana tutatumia kalamu na maneno yetu makali kuwaangusha kutoka huko waliko,” Amata akawaambia wenzake na kuwapanga katik vikoi kazi vya wawili wawili.
“Gina naomba uwe na Chiba, mumtafute huyu Alinda alipo mkimpata anatakiwa aletwe kituo cha polisi kati kwa mahojiano, naomba mwende maana mnajua utaratibu wote wa kufanya,” Kamanda Amata, akamaliza kusema na kuwataka wawili hao kuondoka asubuhi hiyo kwa kazi. Chiba na Gina wakatoka na kuliacha jumba hilo.
“Daktari Jasimini hata kama wewe ni daktari sasa utakuwa TSA 3 halisi, utaongozana na Scoba hakikisheni Mkurugenzi wa idara ya Viwango anafikishwa polisi kati leo hii kwa mahojiano. Makini?”
“Makini!” wakajibu nao wakajiandaa na kuondoka zao. Ndani ya jumba lile alibaki Kamanda Amata na Madam S pamoja na Mustafa katika chumba chake cha siri. Kamanda Amata akabaki pekee kwenye meza ile kubwa, sekunde chache baadae, akainuka na kueleke ofisi maalumu ambayo Madam S alikuwa akiitumia pindi awapo katika jumba hilo. Akaingia na kumkuata mwanamama huyo katingwa na kompyuta yake.
“Enhe umefikia wapi na zako zako?” akamwuliza huku bado akiwa kakodolea macho kwenye chombo hicho.
“Yeah wameshaondoka kwenye majukumu,” akajibu.
“Nimewaona! Sasa kinachofuata…”
“Wawapate hao ninaofikiri hawana budi kubanwa ili watuambie ukweli kama kuna rushwa na ni yuko nyuma yake,” Amata akajibu.
“Sawa Amata, nategemea taarifa yote kutoka kwako, mi sitoki hapa leo,” Madam akamwambia.
Ndani ya nyumba binafsi Mtaa wa Ally Khan jirani kabisa na shule ya Zanaki, Kebby alikuwa kapata matibabu ya majeraha yake na kupumzishwa. Ngishu na vijana wenzake walikuwa eneo hilo, simu ya marehemu Boban ilikuwa mkononi mwake muda wote, haiikupigwa wala yeye alipopiga haikupatikana.
“Ataingia mkononi mwenyewe tu! Safari hii simuachii roho yake,” akawaambia vijana wake ambao kila mmoja alionekana kuwa na mawazo lukuki. Mara simu yake ikaita, akaitazama, ‘Boss’ akaipokea.
“Uje haraka ofisini tuyaweke sawa mambo yetu,” sauti ya upande wa pili ikamwambia na simu ile ikakatika.
Ngishu akaondoka na gari yake kuelekea huko alikokuwa akiitwa, hapakuwa mbali sana, ilimchukua kama nusu saa tu kuwasili, akaegesha gari na kuteremka. Akakweza ngazi chache na kuifikia afisi hiyo ya serikali, siku hii hakukuwa na wakumkaribisha maana Alinda hakuwepo kazini, akapitiliza mpaka katika afisi hiyo nyeti na kuketi bila ya kukaribishwa.
“Ngishu! Maana hata tukisalimiana tutapteza muda, kuna kazi mbili kubwa za kufanya, na ni ngumu ambazo pindi umalizapo tu huna budi kuondoka nchini,” Kalembo akamwambia kijana huyo.
“Kazi gani mkuu?”
“Kama ile ile uliyoifanya kwa Shekibindu,” Kalembo akamwambia.
“Asassination?” akauliza kwa sauti ya chini.
“Yap!”
“Nani?”
“Alinda, kwa maana najua huyu mwanamke yupo jirani sana na mimi hapa, kama itatokea akabanwa huyu anaweza kuniharibia kila kitu…”
“Sawa,” Ngishu akamkatisha, “Huyo tu?” akaongeza swali.
“Kuna mwingine, Bwana Kajaze, Mkurugenzi, huyu naye hana budi kuondolewa maana anajua siri ilipo,” Kalembo akamwambia.
“Sawa Mkuu, nimekupata,” Ngishu akaitikia.
“Ikiwezekana, kazi hiyo ikamilike leo jioni ili usiku uondoke na ndege ya kukodi, katika hili usiwahusishe vijana wako, fanya wewe vmwenyewe maana ukiwahusisha utakuwa umeongeza nafasi ya misheni hii kugundulika, mimi nitakulinda kwa cheo change serikalini kwa lolote na mambo yakitulia tu utarudi nchini,” Kalembo akasema.
“Sawa nakuhakikishia hilo kuwezekana leo, na je usiku huo nitaelekea wapi?”
“Breki ya kwanza itakuwa Lusaka, kisha kutoka pale tutajua nini tunafanya ili utoke nje ya Afrika,” akamhakikishia.
“Timamu, Mkuu, tutaonana baadae,” Ngishu akajibu na kusimama, akampa mkono boss wake na kupotelea nje.
The time is now! Ngishu akawaza akiwa ndani ya gari yake, akaitazama saa ya mkononi, inakimbilia saa tano za asubuhi. Ngoma haifiki usiku, mchana huu huu lazima kitu kiwake, mi ndiyo Ngishu wa Kumar, kwangu pesa kwanza maisha baadae, akazidi kuongea moyoni mwake huku mwendo wa gari yake ukiwa wa kasi sana. Moja kwa moja akaiacha Barabara ya Nyerere na kuikamata ile ya Chang’ombe, mbele akaingia Barabar ya Mbozi na kusimama katika moja ya godown kubwa kabisa la kampuni ya kutengeneza maplastiki. Hapa ndipo alipokuwa akiishi kijana huyu mwenye macho mekundu ya kulegea, ambaye ukatili ulikuwa ndani ya damu yake na alitekeleza hilo muda wowote ambao pesa ingekaa mbele yake.
Ndani ya chumba chake kikubwa, alichukua begi dogo lililosheheni zana za kazi, akatoka na kuondoka zake.
Kabla ya kuanza kazi yake hiyo, akawasili eneo la Magomeni na kuchukua chumba katika gesti moja tulivu, akatumia muda huo kujibadili muonekano wake, kuanzia sura, ndevu, mavazi na kila kitu, kisha akatulia ndani kusubiri wahudumu hao wabadilishane zamu ili akitoka wasimshangae.
MWANANYAMALA
Alinda hakwenda kazini siku hii, ruhusa yake ya matibabu ilimfanya abaki nyumbani tu kupumzika. Ndani ya chumba chake cha kulala alitulia kimya kabisa akitazama mchezo wa kuigiza katika luninga yake. Hakuwa na simu, maana ilipotea katika tukio lile la kuvamiwa kwake. Akili yake ilikuwa ikiwaza na kuwazua, akatamani atoroke, lakini angesema kaenda wapi kwa bosi wake, akatulia.
Akiwa kwenye lindi la mawazo akasikia hodi ikibishwa kutoka mlango mkubwa wa mbele, moyo wake ukaanza kwenda mbio, hakujua nani anagonga. Akajikausha kimya, mbisho ule ukaendelea mwisho akaona liwalo na liwe, akajiinua taratiu na kuchukua fimbo yake ya kutembelea ambayo alipewa hospitali kutokana na mshtuko wa mguu wake. Akavuta hatua mpaka kwenye mlango akihakikisha wan je hamsikii hatua zake. Akavuta pazia kwa chati na kuona gari ndogo ya polisi imesimama nje, moyo wake ukapoa, akafungua mlango na kujitokeza.
Uso kwa uso akakutana na kipande cha mwanamke mbele yake, kikiwa ndani ya jinzi na fulana nyekundu yenye picha ya Madonna.
“Mimi ni afisa wa polisi, naitwa WP Emile, bila shaka naongea na Bi. Alinda,” akajitambulisha.
“Ndiyo, Alinda Rweyemamu,” akajibu.
Yule WP akato hati ya kumtaka mwanamke huyo katika kituo kikuu cha polisi kwa mahojiano.
“Mahojiano yanahusu nini?” Alinda akauliza.
“Kama wewe ulivyo hujui, nami pia sijui, hivyo jiandae twende na baada ya yote, tutakurudisha,” yule WP akamwambia Alinda naye akarudi ndani na kujiandaa kisha wakatoka pamoja katika gari hiyo na kuelekea mjini. Ndani ya gari hiyo siti ya nyuma, Alinda aliketi kati ya watu wawili asiyowajua, mmoja mwanamke na mwingine mwanaume, yeye katikati. Yule WP aliyemchukua alikuwa mbele na simu yake ya upepo huku kwenye usukani kukiwa na kijana mmoja mwenye sare za kipolisi. Wote walikuwa kimya kabisa kiasi kwamba hali ile ilimtia mashaka Alinda, lakini alijifariji kwa kusikia simu ya upepo ya WP yule ikiwasiliana na wengine, hapo akajua kweli yuko mikononi mwa polisi.
Ni muda ule ule tu, Ngishu alifanikiwa kuwasili katika eneo hilo, kutokana na maelekezo ya majirani alifika bila sahaka na kukikabiri nyumba ya Alinda, akaegesha gari na kuuendea mlango, hakubisha hodi, yeye alifungua kwa funguo yake na kuingia nkatika sebule hiyo ndogo. Sauti ya TV ilimwalika chumbani, akavutab hatua fupifupi ambazo hazikufanya ukelele wowote. Akaufikia mlango wa chumba hicho na kuchungulia, kitanda tupu. Akasukuma mlango, akaingia ndani, hakuna mtu zaidi ya kitanda kilichovurugwavurugwa. Lakini juu yake kulikuwa na karatasi moja ndogo, akaichukua na kuisoma.
Nisipoonekana tena,
Nimechukuliwa na watu waliodai kuwa ni polisi, lakini sina imani nao.
Nimepelekwa Kituo cha polisi cha Kati.
Ngishu akaiweka tena ile karatasi kitandani na kutazama hapa na pale, akaingiza mkono mfukoni na kuitoa simu ya mwanadada huyo akaiweka juu ya ile karatasi na kutoka.
“Shiiit! Mambo yataharibika sasa,” akajisemea na kuwasha gari, kisha akaondoka kasi pasi na kujua wapi anaelekea. Ngishu aimpa taarifa boss wake kuwa Alinda ameondolewa nyumbani na kupelekwa polisi. Kama ilivyomchanganya yeye na Kalembo naye alichanganyikiwa kwa jinsi iyo hiyo, ofisi aliiona ndogo.
“Yaani jitahidi kama waweza ummalize kwa njia yoyote ile, mambo hapo lazima yaharibike kama hatutamdhibiti mapema,” Kalembo alimwambia Ngishu.

ITAENDELEA
--------------------------------------------
 
RIWAYA: JANGA
MTUNZI: richard MWAMBE

“Shiiit! Mambo yataharibika sasa,” akajisemea na kuwasha gari, kisha akaondoka kasi pasi na kujua wapi anaelekea. Ngishu aimpa taarifa boss wake kuwa Alinda ameondolewa nyumbani na kupelekwa polisi. Kama ilivyomchanganya yeye na Kalembo naye alichanganyikiwa kwa jinsi iyo hiyo, ofisi aliiona ndogo.
“Yaani jitahidi kama waweza ummalize kwa njia yoyote ile, mambo hapo lazima yaharibike kama hatutamdhibiti mapema,” Kalembo alimwambia Ngishu.

ENDELEA…….

Wakati uo huo…
Scoba na Jasmine walifika katika ofisi ya Mkurugenzi wa Idara ya Viwango, pamoja nao walifuatan ana vijana wawili wa jeshi la polisi waliovalia kiraia. Ndani ya afisi hiyo Bwana Kajaze alikuwa hana hili wala lile, kazi zilikuwa zikiendelea kama kawaida. Akagutushwa na sauti ya Katibu wake ikimwambia kuwa kuna ugeni.
“Waruhusu,” akatoa kibali na vijana wale wakaingia ndani.
“Sisi ni askari polisi,” wakajitambulisha na kuonesha vitambulisho vyao.
“Sawa kariuni mnataka nini?” Kajaze akaanza kuweweseka maana alijua hapo hakuna msamaha kwani hajawahi kutembelewa na vijana hao hata siku moja.
Wae vijana hawakuwa na maneno mengi, walimwonesha hati ya yeye kutakiwa kituoni kwa mahojiano, hakupinga, aliinuka na kuweka vitu vyake vizuri kisha akaongozana na vijana hao mpaka kwenye gari waliyokuja nayo, hii haikuwa ya polisi, ilikuwa ya kiraia tu. Ndani ya gari hiyo akakutana na watu wengine wawili, mmoja mwanmke na mwingine mwanaume, wakmweka kati na wale wengine wakaingia siti za mbele na kuondoka.
Kamanda Amata na Madam S waliwasili katika kituo cha polisi cha kati asubuhi hiyo kwa kazi maalum ya mahojiano na watu hao. Gina aliwapa taarifa kuwa Ainda tayari keishafikishwa kituoni hapo hivyo wanaweza kufika kwa ajili hiyo. Amata akaegesha gari vizuri na kuteremka. Katika ngazi za jingo hilo wakapokelewa na Inspekta Simbeye na moja kwa moja wakaingia ofisini mwake.
“Asante kwa msaada wako!” Madam akamwamia mzee yule.
“Usijali Sellina, ndiyo kazi zetu hizi,” akajibu, “mtuhumiwa wenu keshafika, ila mmoja bado mpaka sasa, lakini wapo njiani,” akawaambia.
“Ok, nafikiri tunaweza kuanza na huyu huyu kwanza,” Madam akapendekeza, wakakubaliana na kutoka mle ndani. Chumba kikubwa, chenye meza na kiti cha chuma, zaidi ya hapo hakukuwa na kitu kingine chochote. Alinda aliketishwa juu ya kiti kile, kisha Gina akaingia peke yake huku kichwani mwake amevaa kifaa maalumu cha mawasiliano. Ndani ya chumba hicho wakawa wao wawili tu. Amata, Madam S, Chiba na Simbeye walikuwa katika chumba kingine ambacho walisikia yote yaliyozungumzwa ndani ya chumba cha mahojiano, na pia waliweza kuwasiliana na Gina kwa kifaa kile kama wangetaka kujua chochote cha ziada.
Gina akamtazama Alinda ambaye macho yake yalitona kwa machozi.
“Usilie Alinda, hakuna kibaya kitakachokupata, ila tunataka kujua jambo kutoka kwako, mimi naitwa Rose Msasalage, ni afisa wa polisi hapa hapa,” akajitambulisha kwa uongo kama kawaida yake. Alinda akainua uso na kumtazama mwanamke huyo aliyekaa juu ya meza hiyo kwa kalio moja.
“Unaitwa nani? Niambie historia ya maisha yako kwa kifupi,” akamwambia. Alinda akameza mate na kutazama huku na kule.
“Naitwa Alinda Rweyemamu, Mhaya kutoka Kagera. Nimezaliwa mwaka 1983 huko Kamachumu, nikasoma Shule ya Msingi Kamachumu na Sekondari Makongo Dar es salaam. Baada ya hapo nikajiunga na chuo cha Utumishi Magogoni, nilipomaliza chuo nikaajiriwa serikarini katika wizara ya Mali asili baadaye nikahamishiwa Wizara ya Usafirishaji na ndipo nafanya kazi hadi sasa,” akajieleza.
“Hujanmbia kama umeolewa au la,”
“Sijaolewa, wala sina mchumba,” akajibu.
“Unafahamiana vipi na Mustafa Bashiru?” Gina akauliza.
Alinda akakaa kimya kwa nukta kadhaa kisha akamwangalia Gina na kumjibu.
“Namfahamu kwa kuwa yeye ni mwandishi wa habari, na mimi ni mpenzi sana wa kusoma gazeti la Mbalamwezi”.
“Umeshawahi kuonana naye uso kwa uso?” Gina akazidi kuchimba.
“Ndiyo,”
“Mara ngapi na lini?” swali linguine.
“Mara moja, ila mara nyingine alikuja mtu aliyejifanya ni yeye, ila sina uhakika naye,” Alinda akajibu bila wasiwasi.
“Sasa unajua yuko wapi?”
Alinda akanyamaza kimya na kutafakari swali hili, hakujibu akanyamaza na kumezwa na mawazo. Gina akasubiri jibu asipate, akamtazama Alinda na kumwona analia.
“Niambie kama a-me-ku-fa!!” Alinda akaanza kulia kwa sauti akitaka kujuzwa habari za mtu huyo.
“Alinda jibu swali, usilie,” Gina akambembeleza.
“Sijui alipo, tangu nimeonana naye ni kama siku tatu au nne hivi,” akaeleza.
“Mara ya mwisho umempigia simu lini?”
“Nimempigia simu Mustafa mara moja tu na hiyo ni zaidi ya wiki moja na nusu ilopita na ndiyo ikawa mara yangu ya kwanza kuonana naye,” Alinda akazidi kueleza ukweli.
“Mkaongea nini?”
Swali hili likamfanya Alinda kunyamaza tena, akakohoa na kupiga moyo konde, maana aljua wazi kuwa sasa anakaribia kusema ukweli zaidi.
“Nilimwambia atoroke mjini kwa kuwa kuna watu wanataka kumuua,” Alinda alipojibu hivyo, Gina akasimama kutoka kwenye ile meza na kuiegemea kwa kuishika kwa mikono yake miwili.
“Habari hizo ulizipata wapi?” Gina akauliza huku akionesha macho makali kwa mwanadada huyo.
Liwalo na liwe, kama nimeamua kumwokoa basi wacha iwe, akawaza Alinda na kujibu.
“Nilisikia wakiongelea hilo pale afisini kwetu, kuna mgeni huwa anakuja mara kwa mara na bosi wangu hunambia kuwa nisimruhusu mtu mwingine kuingi kama mgeni huyo atakuwa ndani. Siku hiyo nilitaka nijue hasa ni nini wanachokiongea, ndipo nikamsikia Mheshimiwa akimpa maagizo kijana huyo, sikuweza kuvumilia nilitoka na kuichukua namba yake afisini kwao nikampigia na kumpa hiyo taarifa”.
“Enhe endelea nini kikatokea,”
“Mustafa alinielewa na nahisi alikwenda kujificha maana hakuonekana na hata habari zake hazikuandikwa. Juzi nikakutana naye katika sura tofauti nje tu ya afisi yetu, wakati tukiongea ndipo yule mgeni alipotuona na kutufanyia fujo, hapo nikajua kuwa hata mimi nitakuwa hatarini kama watakuwa wamejua kuwa nimetoa hiyo siri, jioni yake nikapata ajali karibu kabisa na nyumbani baada ya kuvamiwa na watu waliovalia sox usoni,” akaeleaza.
“Simu yako iko wapi?” Gina akauliza.
“Kwenye tukio hilo nahisi iliibwa pamoja na mkoba wangu,” akajibu.
Upande wa pili wa chumba kile, Madam S na jopo lake wakawa wakisikiliza kila jambo kwa hatua, Chiba akiwa anarekodi kwenye mashine yake ndogo ya kidijitali.
“Ina maana simu aliyopigiwa Mustafa jana hakuwa Alinda?” Madam S akamwuliza Amata.
“Itakuwa. Labda wameitumia simu hiyo baada ya kuiiba ili kumnasa,” Amata akajibu kisha wakaendelea kusikiliza mahojiano.
“Unamjua vizuri huyo kijana aliyekuwa akiongea na Mheshimiwa?” Gina akauliza.
“Ndiyo, anaitwa Ngishu,”
“Zaidi ya hapo, nani mgeni mwingine anyekuja hapo ambaye una wasiwasi naye?”
“Huwa mara nyingi wanakuja wafanyabiashara, Ankhit na Suleiman na vikao vyao huwa ni virefu sana,” Alinda akajibu.
“Unafikiri kwa nini Mustafa anaka kuuawa?” Gina akazidi kuchimba.
“Itakuwa kutokana na habari zake alizoandika siku hizi,”
“Zipi? Hizi za kuhusu vipodozi?” Gina akampa swali tata.
“Ndiyo!” Alinda akajikuta akijibu na kisha akjishangaa mwenyewe kwa kutoa macho.
“Unaniaminisha na unaliaminisha Jeshi la Polisi kuwa Waziri wa Mambo ya Anga Mheshimiwa Thomas Kalembo anashirikiana na wafanyabiashara katika uingizwaji vipodozi vya sumu?”
“Nahisi,” Alinda akajibu huku machozi yakianza kumtoka upya.
“Asante sana!” Gina akamaliza kumhoji na kutoka ndani ya chumba kile, kisha akaingia WP yule aliyemleta na kumtoa Alinda ndani ya chumba kile, akamwingiza kwenye ofisi fulani na kumhifadhi huko.
“Yale yale Madam!” Amata akamwambia Madam S.
“Sure!” akaitikia.
Baada ya mahojiano yale Madam S, Kamanda Amata, Gina na Chiba walikutana katika chumba kingine na kujadiliana mawili matatu na wakati huohuo, Scoba na Jasmine wakaingia, nyuso zao zilikuwa zikionesha wazi kiuwa kuna jambo limewapata njiani. Madam S aligundua hilo na kabla hajauliza chochote, Amata akawa wa kwanza.
“Vipi, kuna usalama huko?”
“Hapana tumepata ambush moja mbaya sana, tumefanikiwa kuchomoka,” Scoba akajibu huku akihema harakaharaka.
“Kuna madhara?” Gina akauliza.
“Hapana, mtu wetu tunaye, jamaa wanaonekana walidhamiria kumuua nahisi wanataka kupoteza ushahidi,” Jasmine akaeleza. Kamanda Amata akahisi damu inakimbia mwilini mwake, akaona sasa mambo yanaanza kunoga, kuna haja ya kuingia ulingoni kwa mapambano.
“Kuna mengi nyuma ya hili Madam!” Jasmine akasema.
“Naona, poleni sana. Vipi mtu wetu yupo katika hali gani?” akauliza Madam.
“Amepata mshtuko kwa lile tukio, lakini muda kidogo atakuwa sawa,” Jasmine akajibu.
“Ok”.
Bwana Kajaze aliwekwa katika chumba cha peke yake, baada ya dakika kadhaa alikuwa sawa kabisa. Mlango wa chumba hicho ukafunguliwa, Amata akaingia na kisha ukafungwa tena nyuma yake. “Pole sana Bwana Kajaze, tumekuita hapa mara moja tu kwa mazungumzo mafupi, usihofu pindi tukimaliza utarudi kuendelea na majukumu yako ya kulijenga taifa,” Amata akamwambia.
“Asante sana, name nimekuja kwa sababu nimejua kuwa ni mahojiano ya kawaida,” Kajaze akajibu na kujiweka sawa kitini.
“Bwana Kajaze, naomba unambie historia yako kwa kifupi,” Amata akaanza hivyo, Kajaze akajieleza historia yote ya maisha yake alikotoka na mpaka alipofikia.
“Ni hivyo tu,” akamaliza kwa kusema hivyo.
“Sawa, waliokuleta hapa wamekwambia kwa nini?”
“Hapana!” akajibu.
“Sasa kuna wimbi la vipodozi vyenye kemikali mbaya zenye sumu vipo madukani, vipodozi hivyo ambavyo serikali imevipiga marufuku miaka kasha nyuma na viwanda vyake kufungwa, vimerudi tena kwa kasi ya ajabu, naomba unieleze ifara yako yenye dhamana ya kukagua kila kinachotakiwa kutumiwa na binadamu kama ni salama au si salama, inajua juu ya hili?” Amata akamjuza na kumwuliza.
“Hapana, vipodozi gani hivyo?” kajaze akakana lakini wazi alionekana kuchanganyikiwa kwa swali hilo.
“Inakuwaje idara yako haijui ilhali vipo dukani na vina nembo ya ubora?”
Swali hilo likampa kigugumizi Yule bwana, akajikuta anashindwa kujibu na kubaki katumbua macho pasi na kusema lolote. Amata alikuwa akitembea huku na kule katika chumba hicho kidogo akisubiri jibu kutoka kwa mkurugenzi huyo. Alipoona kimya akasimama na kumtazama na kumwona jinsi alivyolowa jasho.
“Kwa ukimya huo inamaanisha unajua kila kitu, na si ajabu umekula rushwa ili upitishe mali hiyo itumike na wananchi. Tazama,” Amata akato picha kadhaa za wale wanawake jinsi walivyoharibika ngozi na kumwekea mezani, “Umeona, wote hawa wamekufa kwa sababu ya tama yako ya utajiri wa haraka haraka. Sema ukweli juu ya hili, ukificha hakika leo utabaki humuhumu,” Amata akamwambia.
“Aaaaaa come on!” Kajaze akajikuta aking’aka kasha kumwemwesa midomo huku akimwangalia Amata.
“Ni-ni-samehe afande!” akaongea kwa taabu.
“Nikusamehe kwa lipi?”
“Ni kwe-kweli ninajua…”
“Enhe…”
“Ni biashara ya kigogo afande!” akasema. Amata akatikisa kichwa kuonesha kuwa amehafikiana na jibu hilo, akasogea jirani kabisa na ile meza.
“Biashara ya kigogo?” Amata akauliza.
“Ndiyo afande, ya kigogo…”
“Sasa mbona mi najua kuwa ni ya Ankhit na Suleiman wale Waarabu sijui Wahindi,” Amata akaendelea kuhoji kwa stahili ya mazungumzo ya kirafiki.
“Kiukweli, mi hao siwajui, mi ninachojua ni ya kigogo, yeye ndiye aliyetushinikiza sisi tuipitishe,” akaeleza.
“Akawapa pesa?”
“Ndiyo, akatupatia pesa, Shilingi Milioni Hamsini tasilimu,” Kajze akajibu na kuongeza na idadi ya fedha aliyopewa.
“Kwa hiyo umepokea rushwa?”
“Ndiyo afande,” akajibu.
“Ok, swala lako litashughulikiwa na wahusika wa rushwa sio mimi. Ni kigogo gani mwenye hiyo hiyo biashara ambaye anateketeza wananchi?” Amata akmtwanga swali Kajaze. Ukimya ukachukua nafasi yake kwa nukta kadhaa.
“Ni Mheshimiwa Waziri wa Usafirishaji?”
“Anaitwa nani?”
“Thomas Kalembo,” akajibu.
“Asante sana kwa majibu yako mazuri na msaada wako kwa jeshi la polisi, sina swali zaidi nakuachia huru isipokuwa, nitakuhitaji muda wowote itakapobidi,” Amata akamwambia huku akikiacha kile chumba. Mara baada ya kutoka, wakaingia wale askari wawili na kumtoa Kajaze mle ndani wakamwamishia kwenye chumba kingine cha kupumzika.
Ndani ya chumba maalumu, TSA walikutana kwa mjadala mfupi.
“Tumeshajua mkono ni wa nani,” Madam akasema.
“Kila mara yuyu huyu anakutikana kwa nini hashughulikiwi?” Chiba akauliza kwa msisitizo.
“Ninaanza kuwa na wasiwasi Madam, inawezeka kuna mkono mzito kuliko huu tunaouona kila mara, haiwekani mtu huyu akingiwe kifua katika kila jambo,” Amata akalalamika.
“Yaache hayo hayakuhusu, nafikiri tuko tayri kuondoka, kazi ziendelee jioni kikao chetu kitakuwa AGI Investment, kikao cha wawekezaji,” Madam akamaliza na kusimama, kasha wengine wakafuatia kwa kufanya vivyo hivyo.

13
“Sikiliza Ngishu, hao washenzi lazima wameshatuharibia tu, hatuna cha kuwafanya lakini timiza nililokuagiza, iwe adhabu yao,” Waziri Kalembo alikata simu na kuitupia mezani huku akisonya kwa hasira.
Ngishu akaegesha gari jirani kabisa na kituo cha Railway, haikupita muda mlango wa gari hiyo ukafunguliwa, Kadoda akajitoma ndani.
“Sikia Kadoda, nimekuita wewe kwa kuwa nakuona waweza kuficha siri, kuna kazi nataka kuifanya kasha unanipeleka uwanja wa ndege mara moja, kaa kwenye usukani,” akamwambia huku yeye akihamia kiti cha abiria. Kadoda akakamata usukani na kusikiliza maelekezo. Utapita kwa mwendo wa wastani hapo kituo cha polisi nataka nifanye shambulizi moja la kushitukiza kasha utatimua mbio kufuata Barabara ya kutokea Railway Gerezani, pale tutaiacha hii gari na kuchukua nyingine ipo tayari tuelekee uwanja wa ndege, sawa?”
“Sawa kaka!”
Ngishu alitupa jicho kule kwenye mlango mkubwa wa kituo cha polisi akaona watu wake wakitolewa ndani tayari kwa safari.
“Ok, now, go!!” akamwamuru Kadoda huku tayari Short Gun Double Barell ikiwa mkononi.
Daktari Jasmine na Kajaze wakatangulia kutoka na vijana wawili wa polisi huku nyuma yake tu Alinda alikuwa akiongozwa na Yule WP. Kamanda Amata naye alivuta hatua akiwa na wengine tayari kwa safari, wakisindikizwa na Inspekta Simbeye. Barabara inayopita mbele ya kituo hicho haikuwa na magari mengi kwa muda huo.
Bwana Kajaze akasita kupiga hatua, akarudi ngazi moja juu na kumwacha Jasmine na wale vijana chini. Alisita baada ya kuiona ile gari iliyotaka kuwafanyia ajali wakati wakija, kabla hajafungua kinywa kusema kitu, alishuhudia kioo cha nyuma kikishuka na midomo pacha miwili ya bunduki ikijitokeza.
Risasi mbili za kwanza kutoka zikamlenga sawasawa Kajaze na kuishia kifuani kwake.
“Chiniiiiiiiii!!!!!!” Amata kutoka nyuma akapiga kelele na kumkata ngwala Alinda, wakaenda chini. Mkono wa Amata ukakamata ukosi wa fulana ya Yule WP naye akaenda chini pamoja nao. Risasi nyingine zikakosa shabaha na kumpata kijana wa polisi mkononi, kizaazaa. Amata akainuka haraka alipoona ile gari ikiongeza mwendo kutokomea. Akaruka hewani na kuwapita wote hapo katika ngazi, akatua mbele yao, akatazama kushoto, kulia, akaona pikipiki ya askari wa usalama barabarani imeegeshwa, akaiendea na kutua juu yake, automatic. Akabonya switch na kupiga norinda, akaizungusha ile Honda na kuikamata barabara ya Railway kuifukuza ile gari huku akiliza king’ora kuomba njia na madereva hawakuwa na hiyana, walipisha.
“Ongeza mwendo, mshenzi huyu anatufuata!” Ngishu akamwambia Kadoda, naye akabadili gia na ile gari ikaongeza mwendo, akawa akifanya ovateki mbaya na kusababisha watu barabarani kupiga kelele. Kadoda akaingia kichochoro hiki na kile.
“Nimeshampoteza huyo,” Kadoda akamwambia Ngishu.
“Safi sana kijana, tuiache hii hapa,” Ngishu akamwambia dereva wake, kasha wakateremka haraka na kuikimbilia ile gari iliyokuwa imeegeshwa hapo Klabu ya Railway. Wakiwa katika kuvuka barabara, Kadoda akaona kitu ambacho kilimshangaza na hakukitegemea, akasimama barabarani ghafla.
“Ngishuuuuuuu!!!!!!” akapiga kelele na wakati huo kelele za tairi za gari kusugua barabara zikasikika na kufuatiwa na kishindo kizito. Ngishu akasimama kumwangalia Kadoda, hakumwona.
Kabla hajakaa sawa, akasikia mlio mzito wa pikipiki juu yake, akainua uso kuangalia upande huo, macho yake yaliiona tairi ya pikipiki ikitua usoni.
Kamanda Amata aikuwa hewani kalinyanyua pikipiki hilo kwa ufundi kabisa na kutua tairi ya mbele usoni kwa Mhindi huyo, akashuka naye chini. Ngishu akapiga kelele za uchungu huku akibwagika chini, kisha akaanza kutambaa.
Amata akalizima lile lipikipiki na kuliacaha chini kasha akamwahi mtu wake, Ngishu akasimama haraka na kumkabili TSA 1. Pigo la kwanza kutoka kwa Ngishu likatua kifuani mwa Amata, akapepesuka na kukaa sawa, Ngishu akaruka hewani na kuichanua miguu yake kumtandika adui yake lakini akakutana na mjanja kamanda Ama akajivuta mbele hatua moja na kumpotezea shabaha kijana huyo, kasha akawa nyuma yake. Ngishu alipotua akakutana na pigo takatifu lililopiga kwenye uti wa mgongo, akasukumwa mbele, kabla hajasimama akajikuta kachotwa mtama na kwenda hewani, kisha Amata akamsindika teke moja maridadi upande wa sikio.
Mhindi Yule akatua chini kama mzigo huku akiguna guno la uchungu, akajaribu kusimama akashindwa, akatema damu.
“Mshhhenz… koh! Koh! Koh! Shenzi… unaniua?” Ngishu akaongea huku akikohoa, akajitahidi na kufanikiwa kusimama, akachomoa kisu na kutikisa mkono wake, kile kisu kikafyatuka na haraka akamvamia Amata. Kwa kasi ya ajabu Amata akaachia konde zito lililomrudisha nyuma yule Mhindi koko kabla hajakaa sawa, teke moja likatua kwenye usawa wa kiuno na mara kishindo kikubwa kikasikika upande wa pili wa barabara. Ile gari waliyoiacha Ngishu na Kadoda ikalipuka na kupaishwa juu ikatua katika gari nyingine nayo ikashika moto. Kishindo kile kikamfanya Amata aruke upande wa pili na sekunde mbili tatu zilizofuata, akakoswakoswa na risasi, kutazama huku na kule zilipotokea risasi zile, akamwona Kadoda akiwa chini barabarani na bastola mkononi huku watu wakitawanyika kwa kukimbia. Alipojiandaa kufyatua tena, hakufanikiwa, Amata akashuhudia kichwa cha Kadoda kikifumuka vibaya.
Kijana mmoja wa polisi aliifanya kazi hiyo kwa umakini sana mara tu baada ya kuwasili eneo lile. Kutoka pale chini, Amata akainuka haraka na kujifuta damu iliyokuwa ikitoka kwenye kona ya kinywa chake.
Ngishu akadakwa na vijana wa polisi, akatiwa pingu akiwa hajiwezi na kutupiwa kwenye defender, kwenye maeneo na matukio kama haya daima TSA hawapendi kuonekana hivyo hutoroka haraka. Gina akawasili na kumchukua Amata akamwingiza kwenye gari wakondoka kwa kasi.
“Kajaze!”
“Kapelekwa Hindu Mandar, hali yake ni mbaya,” Gina akajibu huku akizidi kutokomea na kuacha kizungumkuti huko Klabu ya Railway.
“Washenzi hawa, wanataka nini? Safari hii… siwaachi,” Amata akalalamika huku akijifuta vumbi kwa kitambaa kilichokuwa ndani ya gari hiyo. Baada ya dakika kama kumi na tano hivi, walisimama mbele ya mlango mkubwa wa hospitali hiyo, hawakuteremka, bali mlango ulifunguliwa na Jasmine akaingia ndani.
“Upo ok Jasmine?” Amata akauliza.
“Yeah, niko sawa sijui wewe uliyejitosa msambweni,”
“Niko ok…”
“Yule mshenzi vipi?” akamtupia swali.
“Mmoja kafa na mwingine hali yake mbaya, mshenzi yule lazima akaseme yote labda afe,” Amata akaongea kwa uchungu huku akijipiga ngumi pajani.
Akiwa afisini kwake, Mheshimiwa Waziri Thomas Kalembo akawa akijaribu kupiga simu ya Ngishu, haikupatikana, akajaribu na kujaribu, wapi, akashindwa afanyeje. Bahati mbaya au nzuri hakuwahi kuwa na namba ya vijana wa Ngishu isipokuwa Kebby peke yake ambaye naye hali yake ilikuwa tete.
Hata nikimpigia Kebby haitasaidia, akawaza. Adhuhuri hiyo kwake ikawa nzito sana, akazama mawazoni na mara simu yake ya mezani ikaita, akiinua na kuiweka sikioni. Ilikuwa simu kutoka kwa Ankhit.
“Hello Kalembo!”
“Hello comrade!” akaita.
“Asee niko hapa Hindu Mandar Napata habari baya kabisa,” Ankhit akamwambia Kalembo.
“Habari mbaya? Ipi hiyo?”
“Ngishu mekufa kabia, polisi iko naua yeye,” akaongea huku akitazama huku na kule kama kuna anayemsikia akiwa amesahau kabisa kuwa tayari alikuwa ndani ya gari yake.
“Shiiiiit!” Kalembo akajikuta akipiga kelele kwenye simu.
“Tuonane mara moja Bushtracke bana, hii hali nakuwa bay asana sasa,” Ankhit akamwambia swahiba wake na kuikata simu ile. Akawasha gari na kuondoka zake.
AGI INVESTMENT
“Pameanza kunoga!” Madam akawaambia vijana wake.
“Haswaaaaa!!!” Gina akachomekea.
Kikosi kizima cha TSA kilikutana katika afisi hizi, hii ilikuwa ni moja ya mbinu zao za kujadili mambo ili kuwapoteza kama kuna wanaowafuatilia.
“Thomas Kalembo tena,” Amata akamwambia Madam.
“Sasa katika hili, namwona Jaji Tulabayo pia, lakini huyu tumwache kabisa tuone hatima ya kesi ni ipi, hata Kalembo tusimguse, tumbane Ngishu tuwakamate vibaraka wote kasha tutulie kama hakuna lililotokea, tuone nini atakiamua katika kesi hiyo,” Madam akawaambia vijana wake.
“Upo sawa Madam, kisha hapo ndiyo tumtie mbaroni Jaji Tulabayo ikibidi, na kuhusu Waziri je?” Amata akaongeza swali.
“Huyo utaratibu wetu ni uleule, tutapeleka ripoti kwa Rais yeye ataamua juu yake,” Madam akamalizia.
“Sawa, inaeleweka,” wakajibu.
“Kuanzia sasa tukitoka hapa, kazi hii imesitshwa rasmi, mpaka ukipata au mkipata taarifa nyingine kadiri ya nafasi ya kila mmoja, ila tu Mustafa arudishwe uraiani usiku huu, Alinda naye arudishwe uraiani, nimemaliza,” Madam akavunja mkutano.
“Maadam leo mpo afisini kwangu, basi mpate na vinywaji kidogo,” Gina akawaambia na kuiendea jokofu ndogo iliyo hapo hapo ofisini na kuwapatia vinywaji wageni wake.
Baada ya hapo kila mmoja akatawanyika na kusubiri amri nyingine kama walivyoahidiwa na Madam S.
Mustafa Bashiru, akahisi kelele za watu wanaoshangilia zikimsumbua masikioni mwake, kwa taabu akajaribu kufumbua macho yake, yakawa mazito, akajigeuza na kufanikiwa akajikuta kifudifudi, alipofumbua macho akajikuta kalala juu ya zuria jekundu lenye manyonyoya, akili ikaanza kumrudia taratibu. Akakumbuka kuwa zuria hilo lipo nyumbani kwake Segerea, alipoangaza macho akagundua kuwa yupo ndani ya nyumba yuko.
Nimerudi nyumbani, nimerudije? Akajiuliza. Akajitahidi kusimama na kujikuta mwili wake ukiwa mdhoofu, akajaribu kuvuta hatua, akayumba na kutaka kuanguka, akajiwahi kujidaka kwenye meza kubwa ya chakula. Nani hawa? Akajiuliza, bado hakupata jibu. Mustafa akajivuta na kuelekea chumbani kwake, kila kitu kilikuwa sawa kama alivyokiacha siku ya mwisho karibu wiki moja na nusu iliyopita. Alipohakikisha hilo, akaingia bafuni kuoga ili apate nguvu, kisha akarejea sebuleni mara hii akiwa na nguvu. Akaichukua simu yake na kuiangalia kama kuna mwito wowote ulioingia, hakuna, akaitazama namba iliyompigia kutoka kwa Alinda akaiona, akapata hamu ya kuipiga ili amjulie hali, lakini moyo wake ukasita kabisa.

ITAENDELEA
 
RIWAYA: JANGA
MTUNZI: richard MWAMBE

Nimerudi nyumbani, nimerudije? Akajiuliza. Akajitahidi kusimama na kujikuta mwili wake ukiwa mdhoofu, akajaribu kuvuta hatua, akayumba na kutaka kuanguka, akajiwahi kujidaka kwenye meza kubwa ya chakula. Nani hawa? Akajiuliza, bado hakupata jibu. Mustafa akajivuta na kuelekea chumbani kwake, kila kitu kilikuwa sawa kama alivyokiacha siku ya mwisho karibu wiki moja na nusu iliyopita. Alipohakikisha hilo, akaingia bafuni kuoga ili apate nguvu, kisha akarejea sebuleni mara hii akiwa na nguvu. Akaichukua simu yake na kuiangalia kama kuna mwito wowote ulioingia, hakuna, akaitazama namba iliyompigia kutoka kwa Alinda akaiona, akapata hamu ya kuipiga ili amjulie hali, lakini moyo wake ukasita kabisa.
Akatafuta namba ya mkewe akaiona, alipotaka kuipiga tu, simu ya mezani ikaita, akaiacha ile yake ya mkononi na kuifuata ile nyingine huku moyo wake ukiwa na hofu kuu.
“Hello,” akaita na kutulia kimya.
“Mustafa Bashiru, upo huru, endelea na kazi zako kama kawaida, endesha maisha yako kama kawaida, usihofu, walioitafuta roho yako wako mikononi mwa polisi. Usiandike lolote katika uliyoyaona na kuyashuhudia siku hizi,” ile simu ikakatika. Mustafa akavuta pumzi na kujitupa kwenye kochi.
BAADA YA SIKU TATU
Siku hiyo haikuwa nzuri kwa upande wa Jasmine maana asubuhi hiyo alishuhudia Bwana Kajaze akikata roho katika hospitali hiyo ya Hindu Mandar. Aliumia sana kwa sababu bado kuna taarifa alikuwa anazihitaji kwa mtu huyo. Akiwa bado anashangaa kando ya kitanda hicho huku mke wa marehemu akiwa kazimia kwa kifo cha mumewe, alihisi akiguswa bega, akageuka na kumwona muuguzi wa hospitali hiyo.
“Jana usiku, marehemu alisema nikupatie karatasi hii,” akamkabidhi na kisha akapita kuendelea na taratibu za kuuhifadhi mwili. Jasmine akatoka nje taratibu na kuingia kwenye gari yake huku akifuta machozi. Akainua simu na kumpa taarifa Madam S, kasha akatakiwa kurudi Ofisi ndogo mara moja.
Madam S akamkaribisha Jasmine ndani na kumketisha kitini.
“Vipi?” akamwuliza.
“Amekufa,” Jasmine akajibu kasha ukimya wa sekunde kadhaa ukapita kati yao. Daktari huyo akatoa ile karatasi ambayo bado alikuwa hajaisoma, akaikunjua na kuiweka mezani, ilikuwa na maandishi machache tu.
“Nini hiyo?”
“Nimepewa na muuguzi kasema marehemu alitaka nipewe kama ataaga dunia, na ndivyo ilivyokuwa,” akamsogezea Madam kasha yeye akajiegemeza vizuri kitini.
Nawaomba msamaha Watanzania wote kwa sababu kwa saini yangu vipodozi hivyo vyenye kemikali viliingia madukani, lakini ukweli ni kwamba uchunguzi wa kitaalamu ulituonesha kuwa havisatahili. Siwezi kuiomba samahani serikali kwa sababu viongozi walilmo ndani yake ndiyo wanaoendesha biashara hizo haramu, wanatulazimisha kusaini mikataba mibovu kama hii kwa pesa kidogo na vitisho vingi. Katika hili yupo Mheshimiwa Waziri Thomas Kalembo, wafanyabiashara maarufu Ankhit na Suleiman. Zaidi ya hapo Jaji Tulabayo amepewa pesa nyingi sana ile apindishe sheria n kuiuza hati ya hukumu, isitoshe kontena hiyo ilitoka bila ushuru kwani katika kikao cha mgawanyo wa pesa sote tulikuwepo wakati bado Shekibindu akiwa hai.
Ni vigumu kuamini lakini kuna kontena ishirini na nane bandarini na zinafanyiwa utaratiu wa kutolewa kimagendo mara tu baada ya kesi hii ambayo watu hawa wamejitabiria ushindi.
Watanzania wanisamehe lakini vyombo vya dola vishughulike na watu kama sisi, wala na walisha rushwa.
Buriani.
Madam S akaitua ile karatasi, akavuta kabrasha lile lililohifadhiwa jalada la swala hilo, akaiti ndani yake na kuliweka mahala pake. Akaketi na kujiegemeza kitini.
“Kwa kuwa uliporudi sikukupa mapumziko, sasa nenda mapumziko kwa wiki mbili, hili swala tutalitazama huko mbeleni,” Madam akamwambia Jasmine, akato kitabu chake chenye fomu za kujaza, mwanadada huyo akajaza na alipomaliza akazisaini na zikagongwa muhuri.
“Ikitokea dharula nitakuita kama itabidi,”
“Sawa!”
WIKI MBILI BAADAE
Siku moja kabla Mahakama haijakaa kumaliza kesi ya vipodozi ambayo maelfu ya Watanzania walikuwa wakiisubiri kwa hamu. Madam S na kamanda Amata walikutana falagha kwa mazungumzo. Asubuhi hiyo kabla hata hajaenda ofisini alimwita kijana huyo nyumbani kwake kwa mazungumzo. Wakiwa mezani wanapata kifungua kinywa na mazungumzo yao yaliendelea.
“Tafutishi zote zimekamilika Amata, sasa vipi kuhusu kesho?” Madam akauliza.
“Si tumeshaambiwa kuwa lazima washinde, sasa nini hapo unafikiri kitatokea?” Amata akajibu kwa swali pia.
“Takukuru wameshambaini Tulabayo kwa rushwa, wanasubiri amalize hili tu nao wampandishe kizimbani,” Madam akamwambia Amata.
“Hapo kazi ipo, peke yake?”
“Hapana na wengine kama sita hivi,”
“Na vipi Mheshimiwa waziri?”
“Hilo tumwachie Rais mwenyewe, keshasema hivyo,” Madam S akajibu.
“Sasa sikiliza Amata nimekuita hapa kwa kazi moja tu, kulea ujinga nimechoka, kumbuka sisi tupo kwa ajili ya usalama wa taifa hili. Hukumu ya Jaji Shekibindu ilikuwa sahihi sana kwa watu kama hawa, lakini kwa mazingira ya rushwa hukumu ya Jaji Tulabayo haitatenda haki kwa wanyonge,” Madam akameza mate na kuendelea, “fununu nilizozipata ni kuwa kuna maandamano yamepangwa kufanyika endapo mahakama itawabeba watu hawa kwa mara nyingine,” akatulia na kunendelea kunywa chai.
“Duh! Hapo kazi, inamaanisha wananchi wameshachoka kupokwa haki yao…”
“Ndiyo maana yake,” Madam akadakia.
“Kwa hiyo?” Amata akauliza.
“Hatima ya kila kitu iko mikononi mwetu kuanzia sasa, lazima Tulabayo asome hukumu ya Shekibindu,” Madam akasisitiza huku akipiga ngumi yake nene mezani.
“Huoni kama tutakuwa tunaingilia madaraka ya mhimili mwingine? Au umefikiri ni njia gani tutumie?” Amata akawa na wasiwasi.
“Ni kumshinikiza, inapobidi lazima tuingilie kati maswala ya kiusalama kama haya, kumbuka maamuzi mabaya hapo kesho yatahatarisha usalama wa taifa,” akaeleza.
“Sawa nipe mpango kazi mama yangu,”
“Nataka Tulabayo afanye lile alilotaka kufanya Shekibindu, na wewe ndiye ninayetaka uhakikishe hilo linafanyika, asante,” Madam Sellina akamaliza na kuendelea na staftahi yake. Kamanda Amata alijua na alimuelewa sana bosi wake, akishasema asante, maana yaje ni kwamba hataki nyongeza ila wekafanye kazi. Mazungumzo mengine yakaendelea kwa muda wote ambao walikuwa mezani hapo.
Mchana wa siku hiyo Alinda alikuwa akiendelea na majukumu yake kama kawaida afisini, huku bosi wake akiwa afisi ya upande wa pili. Tangu arejee kazini, hakuwa na mahusiano mazuri sana na bosi wake huyo. Yeye alishajua nini kinaendelea, hivyo hilo halikumpa taabu sana. Mlango ukafunguliwa na watu wawili anaowajua sana wakaingia. Hawa walikuwa Ankhit na Suleiman, akawakaribisha na kuwaongoza kwenye afisi ya Kalembo.
“Alinda, sasa sisi tuna kikao, na hapa hatuna kazi nyingine leo, waweza kwenda nyumbani kama unajisikia,” Waziri Kalembo akamwambia katibu wake ikiwa ni moja ya mbinu za kumfanya asisikie kile wanachozungumza. Msichana huyo hakupingana na agizo la mheshimiwa, akafunga mkoba wake na kuondoka.
“Sasa mlikuwa mnaogopa nini, nilishawaambia hii serikali ni yetu, hatuwezi kufanywa lolote, kwani zile kampeni za urais kampuni zenu si zimechangia mabilioni ya pesa, sasa nani atawagusa, aliuejifanya mnoko tulishampeleka,” Kalembo akawaambia wale magabacholi.
“Kweli kabisa bana kubwa, hiyo hatuna wasiwasi nayo, lakini sasa ile bidhaa imefika usiku, na sasa ipo Hoteli ya New Afrika,” Ankhit akamwambia Kalembo.
“Ooh, safi sana! Sasa anatakiwa afanye kazi hiyo tu, kwa maana hawa jamaa wameshatuharibia sana,” Kalembo akasisitiza.
“Maelekezo yote anayo na picha anazo na kazi hiyo kasema ni ndani ya saa ishirini na nne tu itakuwa imekamilika,” Suleiman akakazia.
“Sawa, basi kesho ni siku yetu ya ushindi, na kuanzia kesho kutwa mzigo tunatoa bandarini na kuusambaza nchi nzima. Ahah! Hah! Hah! Hah! Pesa kedekede,” Kalembo aifurahi sana baada ya kuyaweka mambo yote tayari.
Akiwa njiani kuekea nyumbani kwake, simu ya Alinda ikaita kutoka ndani ya mkoba wake, akaupekua na kuichukua, alipotazama jina la anayepiga akakuta ni Mustafa.
“Helllo” akaita
“Hello Alinda, nimekuwa na roho mbaya sana sijakutafuta siku zote hizi, hakika leo ningependa tupate chakula cha jioni pamoja,” Mustafa akamwambia binti huyo.
“Aaaa Mus’ acha hizo bwana, kwani hujui kama mi napika nyumbani? Halafu itakuwaje ukirudi kwak na kumwambia wifi kuwa umeshiba wakati yeye kakuandalia mahanjumati?” Alinda akamwambia.
“Aaaa shaka ondoa, wewe ni mtu muhimu sana katika maisha yangu, sina budi kukushukuru na isitoshe nina zawadi yako,” akamwambia. Moyo wa Alinda ukaruka chogo chemba baada ya kusikia tu zawadi.
“Ok Mus’ wapi tukutane na saa ngapi? Si unajua mi sina gari siku hizi,” Alinda akamwambia.
“Unaonaje tukikutana Jacaranda? Nitakuchukua kwa gari yangu wala usihofu,”
“Bila shaka!”
Kila mmoja kwa upande wake alfurahi kukutana usiku huo, na kila mmoja alijenga taswira ya jinsi gani utakuwa usiku huo.
HOTELI YA NEW AFRICA
“Basi mpaka hapo kuna nini kingine?”
“Wamekwisha, na watakufa pamoja,” Jalal Nabi akazima kifaa chake maalumu chenye uwezo wa kunasa simu za watu. Akiwa ndani ya chumba hicho katika hoteli hiyo, alikutana na Kebby ambaye ndiye hasa alikuwa wa kumpa maelekezo haya na yale na kumpeleka hapa na pale kwa kuwa yeye alikuwa ni mgeni jijini.
SHAMBA
Chiba akashusha pumzi na kujiegemeza kitini, akaweka mikono yake kichwani na kuivua headphone kubwa iliyokuwa masikioni mwake. Akainua simu yake ya mkononi na kupiga mahala fulani kasha akawkea sikioni.
“Hey Mr. kuna keki tamu ajabu, naomba tuonane sasa hivi hapo ng’ambo,” akamaliza kusema na kutulia kidogo.
“Copy!” akajibiwa. Na wakati huohuo akaondoka ndani ya jumba hilo na kupotelea mjini. Ilmchukua nusu saa tu kuvuka na kuibukia upande wa pili yaani Magogoni. Akaegesha gari jirani kabisa na kituo cha daladala na kusubiri hapo. Sekunde kumi nyingi, mlango ukafunguliwa na Amata akaketi katika kiti cha abiria.
“Kaka mchezo bado mbichi,” Chiba akamwambia Amata.
“Wacha we!”
“Sikia hii,” akamwambi huku akimpa kifaa maalumu cha kusikilizia Kamanda Amata akakivaa na kusikiliza kilichomo humo. Dakika moja baadae akakitua kifaa kile, akamwangalia Chiba kwa jicho la husuda.
“Kaka umeokoa maisha, Madam anakusubiri nenda mwenyewe, mi nina kazi nyingine ila hii nayo nitaifungia kazi,” akamwambia na kuteremka kwenye gari. Wakaachana, Chiba akaelekea afisi ndogo huku Kamanda Amata akienda afisini kwake maana alikuwa na kazi nzito.
Kamanda Amata akawasili afisini kwa ken a kumkuta Gina akiwa ametingwa na kazi zake za uchunguzi.
“Ulinambia huji leo kipi kimekusibu?” akamwuliza Amata.
“Kuna dharula moja ambayo lazima niishughulikie sasa hivi ikae sawa,” akamjibu huku tayari akiwa amekwishawasha kompyuta yake kubwa aina ya Apple. Akachambua mafaili kadhaa ambayo aliyahitaji na kuanza kuyaprinti. Alipomaliza alikuwa na kitini chenye karatasi kama thelathini hivi zilizochapwa pande zote mbili na kufanya kurasa kuwa sitini. Akaziweka vizuri na kumpa Gina ili azibane na kupata kitu kama kitabu kimoja. Gina naye akafanya hivyo na kutengeneza vitabu vingine viwili, jumla yake vikawa vitatu.
“Kazi tayari boss!” Gina akamwambia Amata huku akimwekea mezani.
“Asante sana!” Akajibu na kuyapitia yote, akahakikisha yako sawa. Kamanda Amata sasa akawa na hukumu nzima ya marehemu Jaji Shekibindu.
Hii ndiyo hukumu ya kesho, akawaza huku akichukua vitini vile na kujiandaa kuondoka, hatua kama saba hivi zikamfikisha mlangoni, akasimama.
“Vipi?” Gina akauliza.
“No! moyo wangu umesita kidogo, naona kama kuna hatari, hebu nipe manati yangu, jaza mawe ya kutosha,” akamwambia Gina. Msichana huyo, mrembo, akavuta mtoto wa meza na kuchukua bastola moja, akaijaza risasi na kumpatia.
“Kamata kijana!” akamwambia. Amata akaichukua ile bastola na kuitazama, Magnum 22, bastola ya kizamani kidogo lakini bado ilikuwa katika hali nzuri. Akaisunda kwenye kiuno chake na kutoka taratibu katika jingo hilo. Nje ya jengo hilo akaiacha gari yake na kuiendea ile ya Gina, akaingia na kuketi nyuma ya usukani, akawasha na kusubiri kidogo kuangalia kama kuna lolote, hakuna, akaondoa gari ile na kuingia barabarani kuelekea Ofisi Ndogo. Akiwa bado yuko njiani, akahisi kitu chenye ncha kali kikimgusa kwenye mbavu zake. Hakutikisika, akatulia na kupunguza mwendo.
“Usipunguze mwendo, endelea kwenda na fuata maelekezo,” sauti nzito ya kiume ikamwambia kwa lugha ya kiingereza. Amata akajua kwa vyovyote amepatikana na hana ujanja.
“Fuata gari hiyo ya njano inayokuovateki, ukileta utundu wako tu nakumaliza,” ile sauti ikmwamuru. Amata akaiona gari hiyo ya njano ikimpita kwa upande wa kulia akaanza kuifuata huku akili yake ikifanya kazi harakaharaka za nini cha kufanya. Kila alipojaribu kujitikisa alihisi kile kitu kikimchoma, akajua hapo hakuna masihara, akatulia na kuendelea kufuata ile gari.
Chiba na Madam S walisubiri sana afisini wasimwone Amata. Wakajaribu kupiga simu zake zikawa zinaita tu pasi na kupokelewa. Maswali yakaanza kutawala vichwa vyao. Chiba akapiga simu mara ya tatu haikupokelewa.
“Kamanda hayuko salama!” akamwambia Madam S huku akiinuka na kuiweka sawa bastola yake. Madam S akampigia simu Gina akampata na kumwuliza, akajibiwa kuwa mtu huyo keshatoka afisini pale saa nzima iliyopita, naye akapagawa kwa kuambiwa kuwa hajafika Ofisi Ndogo. Gina akatoka nje ya jengo na kuikuta gari ya Amata ikiwa maegeshoni, na ya kwake hakuikuta. Akajua wazi kuwa kama Amata ametekwa basi hiyo ilikuwa atekwe yeye, chozi likaanza kumtoka, akarudi juu afisini na kuchukua bastola zake mbili zikiwa zimejaa risasi sawasawa, akateremka chini na kuingia kwenye Ford Ranger ya Amata na kuondoka kuelekea Ofisi Ndogo.
MABWEPANDE
Kamanda Amata aliongozwa hadi kwenye shamba kubwa lenye msitu mnene wa miti, akaamuriwa kuingiza gari humo naye akafanya hivyo. Ndani ya shamba hilo akatakiwa kuendelea mbele kiasi kwamba akijikuta katikati ya miti mirefu na mbele yake kulikuwa na banda kubwa kama ghala.
“Simama hapo, shuka tartibu huku mikono ikiwa kichwani,” akaamriwa naye akafanya hivyo na kusimama nje. Kebby akamsogelea na kuchomoa bastola kiunoni mwake kasha akamsona na kumtemea mate usoni. Akiwa bado kasimama akapigwa na kitu kizito kisogoni, akaanguka mzima mzima kama furushi. Usingizi mzito ukamchukua na kumpeleka ulimwengu wa mbali.
Madam S na vijana wake walikuwa wametawanyika kila upande ili kujua fununu yoyote juu ya wapi alipo Kamanda Amata, wasijue. Siku hiyo waliona saa zinaenda haraka sana tena zilikuwa hazitoshi. Wote wakiwa wameshapata taarifa juu ya kuingia kwa muuaji wa kukodi kutoka India, hakuna hata mmoja aliyekuwa na raha kabisa.
Jalal Nabi, alichambuliwa na Chiba kwenye mtandao kuwa ni muuaji anayeijua kazi yake, anayeweza kuua bila kufanya madhara. Akiambiwa huyu afe na presha inakuwa hivyo hivyo, huyu afe kwa ajali vivyo hivyo, huwa hakosei na hakuwahi kukosea.
Kitendo cha kundi la Thomas Kalembo kuzidiwa maarifa na TSA, liliwatia hasira Kalembo na washirika wake na hapo ndipo walipoamua kumfungia kazi Amata na mkewe yaani Gina pasi na wao akina Kalembo kujua kuwa ni nani wanaocheza nao mchezo huo wa kifo.
Jalal Nabi naye alikuwa ni mjanja maradufu, mara nyingi ameweza kuvikwepa vihunzi vya wanausalama mbalimbali duniani, kwake yeye kazi hii aiyopewa ni kama alikuja likizo tu, hakuiona uzito wake.
Jua lilitua na kubadilisha mandhari ya jiji la Dar es salaam kutoka mchana na kuukaribisha usiku. Madam S na vijana wake bado walikuwa kapa kabisa, hakuna hata kifaa kimoja chenye uwezo wa kutambua uelekeo wa TSA 1 kilichofanya hivyo.
Katikati ya usiku mnene, Amata akarudiwa na fahamu, akili yake ikaana kufanya kazi taratibu huku macho akiyafungua kwa chati kuangalia kama kuna yoyote. Kwa mbali alisikia redio ikiimba muziki wa zamani, akatabasamu rohoni. Na ni sekunde hiyo hiyo akasikia mlango wa bati ukifunguliwa na mwanga ukafika mpaka pale alipo.
“Hawajaamka tu?” sauti nzito ikauliza na ndipo akatambua kuwa hayuko peke yake.
“Bado hawa wawili huyu mwanamama keshaamka anasubiri fungate,” sauti nyingine ikasikika kutoka kwenye giza nene hatua chache tu kutoka pale alipokuwapo Amata.
“Pwaaaaa!!!!” maji ya baridi sana yakawamwagikia.
“Amka!” sauti kali ikasikika kasha teke moja zito likatua ubavuni mwa Amata, akaguna kwa maumivu. Taa ikawashwa, ndipo akajua kuwa wapo watatu yaani yeye, akamwona Alinda na Mustafa. Kutoka mlango mwingine akatoka Jalal Nabi na kusimama mbele yao.
“Watieni disprini ila huyu mwanmke mwacheni kwanza,” akaamuru na kilichofuata hapo ni kipigo cha mbwa mwizi. Dakika kama kumi hivi zilikuwa ni za kipigo, Mustafa alikuwa hoi kuliko Amata kutokana na kuwa yeye hakuwa mtu wa mazoezi hivyo hakuweza kustahimili.
“Stop!” akawazuia nao wakasimama pembeni, “Kilichonileta hapa ni kuwauwa tu, na si kingine, lakini kabla ya hilo nataka niwaoneshe kitu kimoja, ahah! Hah! Hah! Hah!” Jalal akaongea na kucheka na ndipo Amata akaigundua sauti ile kuwa ni iliyokuwa ikimwamuru kwenye gari.
“Mleteni huyo mwanamke!” akaamuru.
Alinda akaiuliwa na kusogezwa pale jirani, akataka kumbusu kinywani, akatemewa mate. Kofi lililomtoka Jalal lilimpeleka Alinda chini, Mustafa kwa hasira akatamani ajichomoe kutoka kwenye zile kamba lakini wapi. Kamanda Amata yeye alikuwa akiangalia ni wapi watakose ili afanye yake. Kebby akasogeza magunia matatu.
“Humu ndimo makaburi yenu yalimo, waharibifu nyie,” akasindikiza na sentensi hiyo.
“Sasa tunambaka huyu mwanamke huku nanyi mnaona, show ikiisha ndip tunawaua, mmesikia wapumbavu nyie?” Jalal aliongea kwa kiingereza chake cha lafudhi ya Kihindi. Alinda akachukuliwa kwa nguvu, wakaanza kumvua nguo. Kelele alizokuwa akipiga msichana Yule hata kama ungekuwa umezimia ungeamka tu. Kitendo kile cha udhalilishaji Amata hakuweza kuvumilia. Wakati bado wanakurupushana kumvua nguo, Jalal alikuwa kasimama pembeni akicheka, Kebby akapita jirani na miguu ya Amata. Akasimama na kumtazama Amata, akasogea jirani kabisa, uso kwa uso.
“Tunakula mzigo na mtashuhudia kwa macho yenu,” akamwambia. Kamanda Amata akamtandika kichwa kimoja maridadi, Kebby akapepesuka na kubwagika chini. Kitendo kile, Jalal hakukitegemea, akachomo sime yake na kumwahi Amata, akampelekea pigo moja, Kamanda akajaribu kuepa ka shida kutokana na zile kamba akashindwa, lakini ule muepo ukafanya lile sime litue kwenye kamba, zikakatika. Akamsukuma kwa nguvu Mustafa, naye akampamia Alinda wakaangukia upande wa pili, Amata akaruka sarakasi na alipotua chini akamshushia pigo moja zito Yule kijana aliyekuwa akiendele kumgombania Alinda, naye akaenda chini akiwa hana uhai.
“Enh! It seems you are a professional …” Jalal akamwambia Amata. Kamanda hakujibu, akasimama kimya akitazamana na Mhindi yule. Kebby akajiinua na kumnyatia Amata, naye akajifanya kama hajajua hivi huku Jalal akiwa kajiandaa kwa mapigano. Kebby akamvamia Amata kutoka nyuma, Kamanda akamkepa kidogo na kumakamata mkono, akamzungusha na kumweka mbele yake, mapigo matatu ya karate yakamvunja mgongo. Jalal akatumia mwanya huo kumvamia, Amata akawa mwenpesi, akamwinua Kebby na kumsukumia kwa Jalal. Loh! Sime la Mhindi huyo likadidimia tumboni mwa Kebby.
Amata akaenda hewani na alipkuja kutua, akapeleka mapigo kama kumi hivi Jalal akayapangua yote kwa ufundi wa hali ya juu. Hapo zikatokea piga nikupige za ana kwa ana. Wakatulia na kuanza kuviziana tena. Jalal akajua kuwa kakutana na mpiganaji, na Amata naye akajua vivyo hivyo.
Kutoka pale chini Mustafa akajivuta na kuokota liubao lililokuwa na misumari, akalsogea kwake na kusubiri muda ufike.
Jalal Nabi, alijikunjua na kuanza kupeleka kipigo kwa kasi ya ajabu, Amata akajitahidi kupangua mapigo yale, mengine akabahatisha na mengine yakampata na kumweka katika hali mbaya. Alipokuja kuachiwa, alianguka kama mzigo na kujikuta hawezi hata kuinuka, akajitahidi na kujitahidi, Jalal akamkanyaga mgongoni.
“Aaaaaaah! Sasa ni mwisho, hakuna mtu aliyewahi kuuzwa mkononi mwangu akatoka hai,” Jalal akaongea kwa kujigamba huku akiwa bado guu lake kalikandamiza mgongoni mwa Amata. Kamanda akahisi kuwa kakanyagwa na katapila kwa maana hakuweza hata kujitikisa.
Mustafa, pamoja na maumivu alokuwa nayo, akainuka kwa haraka na kumkung’uta Jalal kwa ule ubao, lakini akashangaa kijana huyo kaudaka ule ubao pasi na kuangali nyuma, lakini msumalei mmoja ulitoboa kiganja chake. Nafasi yiyo hiyo ndiyo akaitumia Amata, akajigeuza ghafla na kufanikiwa, pigo moja akiwa bado chini likatua kwenye korodani, Jalal akapiga kelele. Amata akajibetua na kusimama wima. Jalal akamjia kwa kasi huku akiizungusha mikono yake na kutoa sauti kama paka au chui. Amata akaruka juu na kuichanua miguu yake, teke la kwanza likamtandika shavuni Jalal hakuyupa, akajibu pigo kwa kumpiaga Amata kwenye mshipa wa paja. Amata akatua chini na kukosa uzania wa kusimama, akaanuka na kubiringita huku Jalal akimfuata.
Laiti Mhindi yule angejua hila ya Amata asingemfuata. Kamanda Amata aliuwahi mwilin wa Kebby na kuugeuza kasha akamtia ngwala Jalal naye akakosa uelekea na kujikuta akitua juu ya sime lile lile lililodinda mgongoni mwa Kebby.
“Kemcho mami!”
Sime lake mwenyewe likamtoa uhai bila kutegemea. Kamanda Amata hakutegemea kabisa kama kaweza kumkata pumzi mtu Yule, maana aliona wazi kazidiwa uwezo kila kona lakini tu akili ndiyo ilimfanya ashinde mchezo huo. Akaajivuta mpaka alipo Mustafa, Ainda akainuka na kumdaka Amata wakasaidiana kukokotana mpaka nje ya banda hilo. Akawaonesha gari yake na wote wakaingia humo, Amata akafungua droo ya gari hiyo akatoa fulana moja ya Gina akampa Alinda avae maana hakuwa na nguo upande wa juu baada ya marehemu wale kuilarua. Kasha akachukua kiboksi fulani, akafungua na kutoa sindano ambayo ndani yake ilikuwa na dawa tayari, akajidunga kwenye msuli wa mkono, na kutulia kama dakika mbili hivi, akarudiwa na nguvu zake za awali. Akachukua sindano nyingine akamdunga Mustafa, naye dakika hizo hizo akarudiwa na nguvu yake kama awali.
Amata akahakikisha kila kitu kipo sawa, akawasha gari na kuondoka katika msitu ule.

ITAENDELEA
 
RIWAYA: JANGA
MTUNZI: richard MWAMBE

Akawaonesha gari yake na wote wakaingia humo, Amata akafungua droo ya gari hiyo akatoa fulana moja ya Gina akampa Alinda avae maana hakuwa na nguo upande wa juu baada ya marehemu wale kuilarua. Kasha akachukua kiboksi fulani, akafungua na kutoa sindano ambayo ndani yake ilikuwa na dawa tayari, akajidunga kwenye msuli wa mkono, na kutulia kama dakika mbili hivi, akarudiwa na nguvu zake za awali. Akachukua sindano nyingine akamdunga Mustafa, naye dakika hizo hizo akarudiwa na nguvu yake kama awali.
Amata akahakikisha kila kitu kipo sawa, akawasha gari na kuondoka katika msitu ule.
***
SIKU ILIYOFUATA
Simu ya Madam S ikaita, akaichukua na kuitazama namba akaifahamu mara moja.
“Upo sawa Kamanda?”
“Nipo sawa, tutaongea Madam, sasa naelekea Mahakamani,” akamwambia na kukata simu. Madam S hakuamini kama ameongea na kijana wake ambaye usiku uliyopita hakulala usingizi kwa ajili ya kupotea kwake.
Kamanda Amata akaegesha gari yake nje ya jingo hilo la mahakama, akavaa miwani yake vizuri, akachukua kijibegi chake na kuvuta hatua kuingia ndani ya jingo hilo. Hakupata tabu kuipata afisi ambayo Jaji Tulabayo alikuwa tayari akijiandaa kwenda kwenye kesi.
“Mheshimiwa Jaji, nina mazungumzo mafupi na wewe kama utaniruhusu,” Amata akamwambia huku akimwonesha kitambulisho halisi cha kazi yake. Tulabayo akabaki kimya kama kapigwa shoti ya umeme, aliporejewa na fahamu akamjibu.
“Muda umekwisha kijana, tuonane baada ya shughuli hii”.
“Najua hilo, lakini ninachotaka tuzungumze ni juu ya hilo hilo, dakika chache, naomba uketi,” Amata akatumia ukali, na kuufunga mlango kwa ndani. Tulabayo akaketi kitini na Amata upande wa pili.
“Kama nitakuwa nimevunja taratibu za mahakama na ninastahili kushtakiwa hata kufungwa basi niko tayari baada ya kulimaliza hili,” akafungua mkoba wake na kuto faili moja na kuliweka mezani, “Naomba unipe hukumu yako unayoisoma leo,” akamwambia. Jaji Tulabayo akiwa anatetemeka, akampatia faili linguine Amata.
“Sasa sikiliza, najua na tunajua kuwa umepokea rushwa nzito sana kutoka kwa hawa wafanyabiashara na kigogo mmoja wa serikali, hukumu hii umeipindisha na kuwapendelea wao, hatutaki hicho kitokee. Hiyo niliyokupa, ni hukumu iliyoandikwa na Jaji Shekibindu, tunataka isomwe hiyo na si hii,” Amata akamaliza. Akachukua faili la ile hukumu ya Tulabayo akaitia mkobani na kusimama.
“Nakutakia kazi njema, ukifanya vingine tu, nakupoteza leo hii hii,” alipomaliza kusema hayo, akaufungua mlango na kuondoka zake. Akinua mkono wake na kutumia saa yake kupeleka ujumbe kwa Madam S.
“Nimemaliza sehemu yangu, sasa tusikilize hukumu”.
Madam S akakata kile kijimkanda kutoka katika simu yake na kukitia kwenye mfuko wa suruali aliyovaa. Ndani ya ukumbi wa Mahakama, Gina aliingia kama mwandishi wa habari huku wengine wote wakiwa wamebaki kwenye magari yao wakisikiliza kila kitu kupitia kamera maalum ambayo Gina aliiweka mle ndani. Nusu saa ikapita Jaji Tulabayo hakuingia mahakamani. Mpaka dakika hiyo alikuwa akisubiriwa yeye tu, watuhumiwa walikwishafika na kila kitu kilikuwa tayari. Minong’ono ikaanza kusikika miongoni mwa watu waliokuwepo ndani ya ukumbi wa Mahakama.
***
Upande mwingine wa jiji, Mheshimiwa Waziri Kalembo alikuwa akihangaika kupiga simu ya Kebby bila mafanikio, akajaribu kutafuta kila aina ya mawasiliano ikashindikana, mara mlango wa ofisi yake ukafunguliwa, Alinda akajitokeza na kumsalimu kigogo huyo. Badala ya kuitikia Kaman kawaida yake, akajikuta anakodoa macho, haamini anachokiona mbele yake.
Yeye alikuwa tayari amehesabu kuwa Alinda, Mustafa na Amata watakuwa marehemu muda huo. Mtu kweli au mzimu? Akajiuliza, kasha akainuka na kutoka nje ya ofisi, akaingia katika gari yake na kumwamuru dereva ampeleke shambani haraka sana. Toyota V8 ilifungua mapafu yake na kwenda kwa mwendo wa kasi kuelekea Mabwepande. Haikuwachukua muda wakawasili na kuingia katika uga huo wa ardhi anayoimiliki mheshimiwa.
“Weka gari hapa,” akamwambia dereva kasha yeye akatembea kwa mwendo wa harakaharaka kuelekea ndani ya ghala kubwa. Alipofungua tu mlango ule wa chuma, akakutana na harufu kali ya damu iliyoganda.
“Mh!” akaguna.
Akasogea tena taratibu na kuona kitu ambacho hakukielewa. Ni watu au kitu gani? Akajiuliza, alipoona hakielewi sawasawa kutokana na giza ndani ya ghala hilo, akaisogelea swichi iliyokuwa jirani kabisa na ule mlango aliyoingilia, akaishika kile kidubwasha cha kuwashia, akafikiria na kuacha, kasha akaufunga ule mlango na kuondoka.
“Kila kitu kipo sawa?” dereva wake akamwuliza.
“Hapana, nahisi kama kuna vitu vyangu vimeibwa, inabidi nikachukue poisi waje kuchunguza,” akamjibu dereva wake na kuketi tayari kwa safari.
***
“Kooooorrrrrrrrtttttttttt!!!!!!” iliposikika sauti hiyo watu wotw wakasimama na Jaji Tulabayo akaingia ndani ya ukumbi ule wa Mahakama, akapanda kwenye kijukwaa chake na kuketi nyuma ya meza kubwa iliyochongwa kwa mbao safi, na kunakshiwa ka maua maua, mbele ya meza hiyo kulikuwa na picha kitu kama mzani ambacho daima humaanisha usawa wa kisheria. Akaketi na wengine wote wakaketi.
Mwendesha mashitaka akasimama akiwa amependeza ndani ya suti yake nyeusi iliyotanguliwa na shati safi jeupe. Kabla hata hajaaanza kusoma shitaka lile, macho yake yakagongana na Gina, akajihisi anapata ganzi mwilini, hasira zikaanza kumtawala kichwa chake akamkumbuka mwanamke huyu aliyemlaza usingizi kule Hoteli ya Serena na kumwacha uchi kitandani.
The devil is here again! ‘shetani liko hapa kwa mara nyingine’ akawaza.
“Mwendesha mashitaka!” Jaji Tulabayo akamshtua Danstan Majoti kwa maana alikwishajisahahu na akili yake ikahamia kwa Gina. Kijana huyo akasoma mashitaka yote kama ilivyo ada, alipomaliza zikafuata itifaki za kimahakama kasha ikawa nafasi ya Jaji kutoa hukumu na kuimaliza keshi hiyo.
Katika hali isiyo ya kawaida, Jaji tulabayo alikuwa amelowa jasho mwili mzima, akisoma kwa sauti ya kitetemeshi hati ile ya hukumu. Ilmchukua dakika arobaini na tano kukifikia kipengele kile ambacho ndiyo mwisho wa kila kitu.
“… Mahakama imeamuru, vipodozi vyote vilvyo madukani viondolewe mara moja na wamiliki wa maduka hayo walipwe gharama ya hasara watakayopata. Vilevile kontena zote zilizopo bandarini zinazosadikiwa kuwa na vipodozi hivyo ziteketezwe chini ya uangalizi wa jeshi la polisi. Kutokana na uthibitisho wa idara ya viwango ya serikali kuwa si kontena zote zilizoathirika na mahakama imejiridhisha na hilo, inawatia hatiani Bwana Ankhit na Suleiman na kuwahukumu kifungo cha miaka kumi na tano jela au faini ya shilingi Milioni kumi na tano kila mmoja inayotakiwa kulipwa papa hapa…”
Baada ya hukumu hiyo ndefu, Jaji Tulabayo akafunga faili lake, akainama kidogo kushusha pumzi na kasha akasimama na watu wote wakasimama. Akatoka katika ukumbi wa mahakama na kurudi katika kile chumba alichokuwa mwanzo.
“Umefanya nini Mheshimiwa Tulabayo?” Sauti ya Amata ikasikika kutoka katika kochi kubwa ndani ya chumba hicho.
“Ulitaka nifanye nini kijana? Kila mtu ana namna ya kuendesha kesi yake, Shekibindu aliona hivi na mimi nikaona vile,” akajibu kijeuri.
“Asante kwa nuamuzi wako, asante kwa kuwapa uhuru rafiki zako, kumbuka sheria ni msumeno, inakata huku na kule,” Amata akamaliza na kutoka.
“Nenda bwana, usiniumize kichwa saa hii,” Tulabayo akamwambia Amata huku akimwangalia kijana huyo akipotelea koridoni.
Amata akarudi garini na kuondoka taratibu katika viwanja vya mahakama hiyo huku akishuhudia nje ya mahakama hiyo vurugu ya wananchi kuikataa kabisa hukumu hiyo. Vijana wa FFU walikuwa wakihaha kupiga mabomu ya machozi huku na kule kuwatawanya vijana hao waliobeba mabango makubwa yenye picha za watu walioathiriwa na vipodozi vile.
Madam S akainua simu yake na kuwataarifu vijana wake kuwa huko nje hakufai, hakupitiki kutokana na watu hao.
“Nimemwabia kuwa hiki alichokifanya ni kuhatarisha usalama wa taifa,” Amata akajibu ujumbe ule.
Katika Barabara ya Maktaba na ile ya Bibi Titi, kulijawa na watu, akina mama waliokuwa wakilia kwa uchungu, wakigalagala chini huku wengine wakivua nguo zao kuonesha wanatoa laana kwa serikali yao. Vijana wa FFU walijikiuta wakizidiwa nguvu, pande zote ikaonekana bado watu walikuwa wakiandamana kuja eneo hilo huku wakiimba nyimbo za maazishi na kubeba masanduku yenye picha za marehemu.
Kamanda Amata akateremka kwenye gari na kusimama nje ambako ni moshi tu wa mabomu ya machozi na harufu ya baruti.
Pale wanyonge wanapoikosa haki yao… akawaza na kugeuka kuondoka.
“Unaelekea wapi?” Madam akamuuliza kwa kutumia kifaa chake maalumu alichokiweka sikioni.
“Naenda kumwona Jaji Tulabayo, aje ashuhudie hiki kinachoendelea,” akajibu huku akizikwea ngazi na kuingia ndani Mahakama hiyo, katika moja ya vikorido akapishana na kijana mmoja ambaye sura yake haikuwa ngeni sana lakini hakukumbuka kamuona wapi. Wakatazamana na kupishana hakuna aliyemsalimu mwenzake. Amata akawahi na kufika katika mlango wa afisi ya mheshimiwa Yule, akaingia ndani na kumkuta ameketi kana kwamba anaandika jambo fulani.
“Mheshimiwa! Twende ukashuhudie huko nje,” akamwambia lakini Tulabayo hakushtuka akabaki katulia pale pale, akamwendea na kumgusa paji la uso kumwinua, amekufa.
“Shiiiiittttt!” akang’aka na kutoka mle ndani haraka akawahi, akapita kwa mwendo wa haraka haraka, akatoka nje na kuketi ndani ya gari yake.
“Tunaomba wananchi mtulie!” sauti kutoka kwenye kipaaza sauti ikasikika, na moja ya gari iliyokuwa ikipepea bendera ya taifa, ilifunguliwa juu na akajitokeza Waziri Mkuu. Umati ule ukatulia.
“Kilio kimefika, nilikuwa afisini kwangu lakini imenibidi kuja hapa, ninachowaomba ndugu zangu, mama zangu. Kweli haki yenu inapindishwa siku hadi siku, na hili linasababishwa na viongozi walafi, wapenda pesa…”
“NDIYOOOOOO!!” wakaitikia.
“Sasa basi, ili twende sawa, fanyeni hivi, undeni kamati ndogo ya watu watano ambayo itawawakilisha ninyi na kukata rufaa ili kesi hii isikilizwe upya,” Waziri Mkuu alipomaliza kusema hayo umati wote ukalipuka kwa shangwe, watu wakaanza kutawanyika huku wanasheria wakijitokeza kuunda kamati hiyo bila kuchelewa.
***
Mheshimiwa Waziri wa Usafirishaji alituma askari polisi kutoka kituo cha kati kwenda katika shamba lake huko Mabwepande kufanya uchunguzi, wakateremka na kuweka sawa bunduki zao. Wakiwa katika harakati za kuingia ndani ya ghala hiyo, simu ya upepo ya kiongozi wao ikakoroma.
“Krrrroo! Krrroooo! Nyuki, nyuki,” ikaita.
“Unasomeka,” akajibu Yule kiongozi.
“Hakikisha, usishike kitu chochote, hata swichi ya taa, hakikisha mnafanya ukaguzi kwa kutumia tochi za simu zenu, ova!”
“Copy!!”
Ndani ya jingo lile wale askari wakagundua zile maiti tatu, mbili zikiwa pamoja katika sime na mojaikiwa pembeni, wakapiga picha kila kitu na kupita kwenye mavyumba tofauti na kukagua kila kilichomo. Hakukuwa na cha maana zaidi ya zana za kilimo. Baada ya kujiridhisha wakampa taarifa Mkuu wa Kikosi, naye akampa taarifa waziri huyo.
Taarifa ya kuuawa Kebby na Jalal Nabi iliwamaliza nguvu kabisa watatu hawa, yaani Kalembo, Ankhit na Suleiman. Lakini bado waziri huyo akawahakikishi usalama wao kuwa wasiogope kwani yeye anajua nini atafanya kuwakingia kifua.
***
Ndani ya afisi za AGI Investment, TSA walikutana kutathmini hali nzima ya kesi ile. Pembeni yao luninga ilikuwa ikionesha habari mbalimbali. Mara matangazo yakakatika na maandishi makubwa BREAKING NEWS yakajitokeza. Mwanadada mmoja akapeperusha habari ya kifo cha Jaji Tulabayo, wakaonesha picha mbali mbali za uhai wake Jaji huyo.
“Taarifa zinasema bado haijabainika chanzo cha kifo hicho na uchunguzi unaendelea,” ikamaliza taarifa hiyo iliyokuwa ya dakika tano tu.
“Amata!!” Madam akaita, “Amata umeua, kwa vyovyote, wewe mtoto mi nakujua sana, sasa umefanya nini?” akafoka.
“Hapana Madam! Nimemkuta keshakufa,” akaeleza.
“Hapana, tuliache hilo,” Madam akasema, “Kama ni wewe, safari hii utashughulikiwa…”
“Madam mi sio mpumbavu siwezi kuua mtu kama yule kwa wakati ule,” Amata naye akafoka, kikao kile kikakwa katika mtafaruku, Madam S alibadilika kabisa na kuwa mkali, mwisho akaamua kuondoka zake akimtaka TSA 1 kumpa maelezo ya kutosha juu ya hilo.
“Shiiiiit!” akang’aka Amata na kujitupa kitini kwa nguvu huku sura yake ikiwa imejikunjakunja kwa hasira.
***
“Hii nchi yetu bwana, haya yote yamekwisha,” Kalembo alikuwa akiongea kilevi huku akielekea katika ghala yake huko Mabwepande.
Ukimya ulitawala kila upande, akashuka na kwenye gari na kutembea taratibu akiyumbayumba kwa pombe aliyokuwa akinywa, akaufikia mlango.
“Sisi ndiyo wenye nchiiiiiiiiiiii, tutaila na kuitafuna tutakavyo, mtaandamana weeee, haki yenu ng’o! haki inanunuliwa sheria inauzwa, Watanzania wenzangu vipi?” akaendelea kubwabwaja akiwa peke yake eneo lile.
“Na kesho asubuhi yuleeeeeee Nairobi kula bata na wadau wangu, mnachoma kontena moja, nay ale ishirina saba je, pesa bado ipo!” akaongea huku akipapasa funguo ni ipi ya mlango huo. Alipoipata akafungua na kuingia ndani akapapasa kwa shida na kuipata swichi akabofya kuwasha taa.
Sekunde ile ile alipobonyeza ile swichi, mlipuko mkubwa ukatokea, ukafumua ghala yote, ukateketeza kila kitu, Kalembo akajikuta anashindwa kukimbia kutokana na ulevi ule, akaanguka chini, akajitahidi lakini moto ukamfikia na kumteketeza kama mali nyingine zilizokuwa humo.
Jeshi la zimamoto likawasili lakini hawakuwahi kuokoa chochote ndani ya ghala hilo, zaidi walikuta mwili ule uliokakamaa kwa moto na kuungua vibaya.
OFISI ZA GAZETI LA MBALAMWEZI
Mustafa aliketi kwenye kompyuta na habari tatu muhimu za kuuza gazeti siku inayofuata.
MAHAKAMA YATOA HUKUMU TATA akasoma kichwa hicho na kukikata, kwamba hakipendezi.
Sasa niipe kichwa gani? Akajiuliza.
MWISHO WA UBAYA AIBU, akaandika nacho akakata maana hakuridhika nacho.
HUKUMU YA ANKHIT NA SULEIMAN, WANANCHI WAPAZA SAUTI, akakisoma na kukubaliana nacho kasha akaendelea kuandika vichwa vidogodogo chini yake kuisindikiza habari hiyo.
HUKUMU YA ANKHIT NA SULEIMAN, WANANCHI WAPAZA SAUTI
Yaambatana na vifo vyenye utata
Rushwa yadhihirika kuwa ni janga la taifa
Akina mama walaani serikali
Waziri Mkuu aokoa jaazi
Baada kuandika habari hiyo kwa marefu na mapana, akaiwasilisha kwa mhariri naye hakuwa na shaka, akaitumbukiza kiwandani tayari kuchapa gazeti hilo.

* MWISHO *

aASANTENI KWA KUWA NAMI
 
Kwa mahitaji ya RIWAYA nyingine kali kutoka kwa Richard MWAMBE
Kama vile
MPATANISHI
HARUFU YA KIFO
TUFAA JEKUNDU
CRONOC 7
MKONO WA JASUSI
JIUE MWENYEWE
n.k
Wasiliana nae kwa namba 0753264025
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom