winston20
JF-Expert Member
- Jun 21, 2020
- 1,117
- 2,256
GENGE
EP1
JULAI 15, 1991 DIAMOND JUBILEE
SAUTI KUBWA YA MUZIKI ilisikika kutoka katika ukumbi huo maarufu jijini Dar es salaam, katika kitongoji maarufu cha Upanga. Ni harusi ya kukata na shoka, kati ya Bi. Egra Mwakasimba na Dastani Kihwelo. Mamia, kama si maelfu ya watu waliujaza ukumbi huo. Wakila na kunywa huku wakitunuku zawadi kemkem kwa maharusi hao. Mishale ya saa mikononi mwa waliowengi ilioneshas saa sita kasoro robo usiku. Wenine walisaanza kusimama na kuondoka wakati wimbo huo unaojulikana kama ‘Wifi twende nyumbani’ ukirindima. Maharusi nao walikuwa wima wakitembea kwa mwendo wa maringo na hatua za hesabu kulielekea lango kuu, tayari kwenda kula fungate.
Nje ya ukumbi huo, gari la maharusi lilikwishaandaliwa na kuegeshwa mahala pake. Mercedes Benz E Class,jipya kabisa, toleo la 1990 lilipambwa likapambika. Gari hilo la pesa nyingi lilitolewa zawadi na idara ya Usalama wa Taifa ambapo Dastani Kiwelo alikuwa mwajiriwa mtiifu. Baada ya kuagana na ndugu na marafiki, Dastani, na mkewe Egra wakajitoma ndani ya chombo hicho kipya.
“Ooooh! Gari zuri sana mume wangu!” Egra akasifia mara tu baada ya kupokelewa na kiti cha ngozi laini. Akatazamana na mumewe na kubusiana kisha Dastani akapachika funguo mahala pake na kuliwasha. Ndani ya gari hilo walijiona wao tu, taratibu gari lile likaingia barabarani na kutokomea huku likiwaacha watu wakisindikiza kwa macho. Mazungumzo kati ya mtu na mkewe yalicukua nafasi wakati tairi zikichachafya Barabara ya Ally Hassan Mwinyi mara baada ya kuiacha ile ya Umoja wa Mataifa. Kutoka kwenye redio ya gari hilo, sauti ya mwaDanada Judy Boucher ilikuwa ikisindikiza kwa kibao matata ckinachokwenda kwa jina ‘Mr. Dream Maker’.
“Asante Dastani,” Egra akashukuru.
“Asante nawe pia, umenifanya niwe mwanaume sasa,” Dastani akamjibu mkewe huku akiongeza mwendo kulipita gari la mbele yake.
“Nataka tujenge familia ndogo, yenye upendo na furaha…” Dastani akajibu, alipotaka kulipita gari lingine akasikia honi kali nyuma yake. Akarudisha usukani kushoto na Benzi lile likatii amri. Mazda jekundu likampita kasi. Ndani ya Mazda lile ‘kibanda wazi’ kulikuwa na mwanamke mmoja ambaye ndiye dereva. Mshtuko wa wazi kwa Dastani ukaonekana.
“Vipi honey, mbona umepoa ghafla?” Egra akauliza.
“Hapana, hamna kitu,” akajikaza kiume, Waswahili husema.
“…unanificha, au ndo x wako? Wanaume amna wema!” Egra akalalama na kueukia upande wa pili.
Wanawake bwana! Hapo keshawaza mengine! Dastani akawaza na kupunguza mwendo. Kama mwanausalama, alishajua nini kitatokea kama akiendelea kufuata barabara hiyo. Akili ilimtuma kuchepuka na kuingia kulia kwenye barabara ndogo ya Kaunda, hakufanikiwa.
Kutoka nyuma ya kiti chake aliisi kitu chenye ncha kali kikimchoma pembeni kidogo ya uti wa mgongo. Akatulia huku gari likiendelea kuseleleka taratibu. Egra akaundua hilo, akageuka nyuma na kukutana macho na mtu aliyevaa soksi jeusi kufica uso wake. Alipotaka kupiga kelele akajikuta akipiwa na kiganja kigumu upande wa nyuma wa shingo, akazirai.
“Endelea na barabara hiyo hiyo mpaka nitakapokwambia,” sauti nzito ya mtu huyo ikamwamuru. Dastani akuwa na ujanja, akatenda aliloambiwa na mtu huyo. Kicwani mwake aliendelea kutafakari na kujaribu kukumbuka ni wapi aliisikia sauti hiyo, asipate jibu.
Dakika mbili zilizofuata walifika eneo la Mbuyuni.
“Kunja kushoto!” akaamriwa. Naye akatii na kucuku barabara ya Ruhinde. Mbele kidogo akatakiwa kukunja kulia, akafanya hivyona kuingia Mtaa wa Galu. Mara tu baada ya kukunja ile kona akaliona lile Mazda jekundu limeegeshwa kando.
“Simama hapo!” akaamriwa, naye akatii. Kutoka kwenye vivuli vya miti, wakajitokeza watu wengine watatu, wanaume ambao sura zao alizifahamu vyema. Dastani akateremshwa garini na kusimama chini,
“Umependeza Dastani, suti ya gharama uliyovaa, gari ya kisasa uliyopewa zawadi na wadosi wako… vyote ni kwa sababu ya kutuuza swahiba zako,” mwanaume wa makamo alizunumza huku akiwa kasimama mita chache tu kutoka kwa Dastani.
“Ilikuwaje ukakiuka maagizo Dastani, ata ukasababisha mipango yetu kwenda fyongo? Mpiganaji wetu , komandoo Salimu Manumba akauawa… yote kwa sababu yako. Na wewe mwenyewe kwa mkono wako ukamuua Bambross pale Embassy Hotel, ukachukua nyaraka nyeti na kuwapa mabosi wako. Tulijua u mwema, kumbe fukufuku mchangani. Watu wa aina yako uwa hawastahili kuishi… kwa taarifa yako, ulichokisema kwa mabwana zako ni asilimia kumi tu ya mpango mzima. Usifikiri tulikuwa wajinga kwamba tungeweka kila kitu mbele yako, la hasha! Sasa wewe utakuwa sanduku letu,” yule bwana akamaliza na kuingia kwenye lile Mazda jekundu pamoja na yule mwanamke wa Kizungu. Dastani akarudishwa garini mwake, mara hii, kwenye kiti cha nyuma huku vijana wengine wawili wakikaa upande huu na ule. Egra akiwa bado kwenye mzimio.
Safari yao iliishia Msasani Peninsula, kando kabisa ya Bahari ya Indi kulikuwa na nyumba moja pweke, ya kifahari. Ni katika nyumba hii ndipo, Dastani na mkewe, Egra, walikuwa wakielekea tayari kwa kuuanza usiku wa kwanza kama wanandoa.
“Usiwe na wasiwasi Dastani, fungate mtakula kama kawaida, na mtainjoi harusi yenu ndani ya nyumba ni hii hii,” yule bwana akazungumza. Dastani hakujibu. Yule mwanamke wa Kizungu mwenyue Mazda jekundu akaja na ndoo ya maji mkononi na kummwagia Egra. Egra akakurupuka na kuanza kuhema kwa nguvu na haraka haraka huku akimwita Dastani kwa sauti kali. Makofi mawili aliyozabwa na yule mwanamke yakamnyamazisa na kumwacha akitweta. Dastani, alilishuhudia tukio lile, akauma meno kwa uchungu na hasira.
“Mwacheni mtoto wa watu msimdhuru, haya hayamuhusu…” Dastani akatamka.
“Hatuwezi kumdhuru huyu, hana hatia, ila ataishi na sisi mpaka Munguamchukue mwenyewe, na wewe, malipo ya kazi yako yamefika…” alipomaliza kusema hayo kikafuatia kipigo kikali kutoka kwa wale vijana. Dakika kumi, zilimwachaDastani akiwa chini, hoi bin taabani, kila alipokohoa alitokwa na damu kinywani. Egra alikuwa akilia kwa uchungu kwa kila alipokuwa akitazama kipigo anachoshusiwa mwenza wake. Wale vijana baada ya kumsulubu Dastani, wakamwacha pale chini na kufunua buti la lile Mazda, wakatoa madumu mawili ya petrol na kuinia ndani ya ile nyumba. Dakika tano baadae wakatoka na kumwaga mafuta yaliyobaki kwenye kibaraza na mengine wakalimwagia lile Benz. Haikupita dakika mbili , upande wa baarini ikawasili boti ndogo.
Vijana wawili wakashuka wakiwa wamebeba miili ya watu wawili; mwanamke na mwanaume. Awakuongea na mtu,wakapitiliza ndani ya nyumba ile moja kwa moja. Iliwachukua kama sekunde arobaini hivi, wakatoka.
“Tayari boss,” wakamwambia yule bwana aliyesimama kando ya Dastani. Akawajibu kwa kutikisa kichwa. Akawapa ishara ya kumbeba Dastani na mkewe, wakafanya hivyo na kuwapakia kwenye ile boti. Pamoja nao, wakafuatana na wale vijana wengine.
“Ash to ash!” akatamka yule mwanaume na kuitoa sigara yake kinywani kisha akaitupia pale kibarazani. Moto mkubwa ukalipuka na kuichoma ile nyumba na kuteketeza lile Benzi wakati wawili wale wakipotea mbali ndani ya Mazda lao.
“Mungu amlaze panapomstahili,” yule bwana akatamka.
“Jesca! Moja kwa moja uwanja wa ndege,” akaoneza kusema. Yule mwanamke aliyeitwa kwa jina la Jesca akaitika kwa kichwa.
* * *
2002 Januari
BRUSELS –UBELGIJI
Wingu zito lilitanda katika anga la jiji hilo, barabara zilifunikwa na kwa barafu na kusababisha baridi kali kwa wakaazi wake. Daima kipindi kama hiki cha miezi ya Desemba mpaka Februari, nchi za Ulaya hupitia katika kipindi hiki, winter.
Nje ya jengo refu lenye sakafu thelathini na sita, linalojulikana kama Tour des Finances, gari moja la kisasa aina ya Audi liliingia katika uwanda wa maegesho, chini ya jengo hilo, likiiacha barabara kubwa ya Royale inayokatiza pembezoni mwake.
Kutoka ndani ghorofa ya ishirini na tano, ndani ya ofisi moja nadhifu iliyosheheni vitabu na makabrasha anuai katika rafu zake zinazong’aa kwa polish safi, hatua za mtu anayeujongelea mlango zilisikika pasi na kificho. Zilipofika mlangoni hapo, zikakoma. Sekunde kumi na tano zilizofuata, mlango ukafunguliwa. Kipande cha mwanaume kikaingia ndani. Kabla hajawasha taa kwa minajiri ya kufukuza iza hafifu lililosababishwa na wingu lile; aliona taa ikiwaka yenyewe.akapiwa na mshtuko na kuwai kugeuka upande wa pili ambako kuna swichi nyingine ya kuongoza taa hiyo.
“Usiogope, ni ugeni tu wa kawaida…” sauti ya mwanaume ikasikika upande ule. Yule bwana akashikwa na kigugumizi na kutazamana macho kwa macho na huyo aliyejiita mgeni.
“Wewe ni nani? Na unafanya nini katika ofisi yangu?” kile kipande cha mtu kikauliza uku akivuta kiti na kuketi nyuma ya meza yake kubwa.
“Mimi ni mgeni wako kutoka katika nchi iliyokulea, mpaka ukawa mtu mzima na kuiasi,” yule mgeni akajibu.
“Nani aliyekutuma?”
“Mama yako!” yule mgeni akajibu huku akicezea vidole vyake.
“Hivi ninyi Watanzania mna matatizo gani? Kwa nini ampendi watu wastarehe na maisha yao? Kutwa kucha mnatufuatilia, tuacheni!” akang’aka yule bwana.
“Jiulize! Ni Watanzania wangapi wanaisi Ughaibuni tumekuwa tukiwafuatilia? Kama si wewena washenzi wenzio tu… mngekaa kwa amani kama mngeondoka kwa amani…lakini mlichokifanya mnakijua, na adabu yake mnaijua. Nyote lazima muitumikie adhabu yenu…” yule mgeni akaeleza. Ndani ya mfuko wa ndani ya suti yake akachomoa bahasha ya khaki, juu ilikuwa na mhuri wa serikali.
“Ichane, uisome, nimetumwa na mama yako kukuletea…”
Yule bwana akaichana kwa kitete huku akivuta kamasi jepesi kulirudisa ndani ya pua zake ndogo. Akatulia kuisoma. kijasho chembamba kikamtiririka ilhali ofisi hiyo ilitawaliwa na baridi.
“Wewe ni nani?” akauliza kwa sauti huku akizungusha kiti kumtazama mgeni huyo. Mkono wake wa kuume ukabonyeza kitufe Fulani na kuruusu saraka ya siri kufunuka katika meza hiyo. Akabaki kakodoa macho akiwa haelewi nini cha kufanya.
“Usihangaike Bwana Titus Mwakibinga, bastola yako ninayo, nilikwisaichukua kitambo!”
Yule mgeni akamwambia mwenyeji wake ambaye mara hii alimtaja kwa jina la Titus Mwakibinga. “Umeju-aje ma-ha-li bastola ya-ngu i-li-po?” Titus akauliza kwa kigugumizi uku akipiga ngumi mezani.
“Kwani wewe ulifikiri hapo ni mahala pa siri? Mimi nilisapajua zamani sana, na sikupata tabu kuichukua,” mgeni akajibu.
“Nakuuliza kwa mara ya mwisho… wewe ni nani?” Titus akatupa swali uku akiwa amefura kwa hasira.
“Naitwa Amata Ric, au Kamanda Amata, TSA 1, code 005…” yule mgeni akajitambulisa huku tayari bastola ikiwa mkononi mwake. Titus alipotazamana na bastola ile alijikuta akiisiwa nguvu.
“Mbiyo za panya! Titus, hata kama kosa umelifanya mwaka ’82, hukumu iko palepale. Kama ulifikiri ukitoroka ndiyo utaukwepa mkono wa sheria, basi umeula wa chuya kwa uvivu wa kuchagua. Hukumu ya kesi yenu ilisomwa mwaka 1985, Desemba 28 na Jaji Antoni Mzavas. Wenzi wako walihukumiwa kifungo lakini wewe na wengine wachache mlitoroka nchi. Titus Mwakibinga, umehukumiwa kifo…” Kamanda Amata akamwambia pasi na lepe la tabasamu usoni mwake.
“Mimi sihusiki, serikali imenionea tu,” Titus akalalama.
“Sasa nani anahusika kama si wewe?”.
“Sijui!”
“Hujui? Kama hujui, basi ni mhusika mmoja wapo…” Amata akasema.
“Nooo!” Titus akang’aka mara alipoona bastola ile imeondolewa usalama.
“Kijana, nitakupa pesa nyingi sana,” akasema Titus.
ITAENDELEA
GENGE
EP2
Nooo!” Titus akang’aka mara alipoona bastola ile imeondolewa usalama.
“Kijana, nitakupa pesa nyingi sana,” akasema Titus.
“Sihitaji pesa yako, nimekuja kutekeleza kile nilichotumwa kama ulivyosoma kwenye hiyo hati,” Amata akasema na kumfanya Titus ageuke kutazama mezani. Macho yake yakagonganana neno KIFO, lililoandikwa kwa wino mzito na kupigiwa mstari mwekundu.
“Buriani Titus! Ukishakufa uwatokee wenzio kwenye ndoto uwaambie kuwa nitamuua mmoja baada ya mwingine. Popote watakapokimbilia…” Amata akasema. Kabla Titus hajaongea chochote tayari, risasi moja kutoka kwenye bastola yake mwenyewe, Glock 23, ikatoboa paji la uso. Titus Mwakibinga akajibamiza kitini na kichwa chake kuegemea kushoto. Amata akaipachika bastola ile mkononi mwa marehemu.
Nje ya jengo lile, akatembea taratibu huku mikono ikiwa mfukoninabubblish ikiteketea kinywani mwake, akapita barabara ya Royal kuelekea Best Western Hotel ambako ndiko aliwekeza makazi yake kwa muda akiwa katika operesheni hiyo. Ze Sindiket…
* * *
Ndani ya hoteli ile, Amata alijitupa kitini, akavua glovesna kuziweka juu ya meza ndogo ya kusomea. Akavuta kabrasha lake na kupekua hapa na pale akitazama kinachofuata. Alipojiridhisa na kazi yake akalikunja kabrasha lile na kulitia mkobani.
1981
DAR ES SALAAM
UPEPO MWANANA uliendelea kuvuma. Dirisha kubwa katika moja ya nyumba nyingi katika eneo la Kawe Mzimuni, liliruhusu upepo huo uwafikie wapendanao wawili waliokumbatiana kitandani usiku huo. Muziki laini kutoka katika santuri ya Mbaraka Mwishehe ulikuwa ukiendelea kusikika kwa sauti ya chini. Kelele za mibweko ya mbwa ikamshtua mwanamke aliyelala kitandani hapo. Mwanamke wa Kizigua, mwenye shepu isiyosemeka, akajivuta na kunyoosa mkono wake mpaka sehemu Fulani, uvunguni mwa kitanda hicho. Taa kubwa ya nje ikawaka na kufanya nuru kali ambayo kila kitu kingeonekana.
Mbwa waliendelea kubweka, mwanamama yule akaamka na kukiacha kitanda. Umbo lake la Kitanga likafanya mitetemo ya kuvutia na kuuweka dhahiri shahiri uanamke wake. Akakiacha cumba na kuelekea sebuleni. Wakati mbwa wakiendelea kubweka, mara kelele iliyofanyika kwa mawe matatatu kurushwa batini, ikamshtua mwanaume aliyelala kitandani hapo.
Akaamka na kupapasa upande aliokuwapo mkewe, hayupo. Akajiinua na kuketi kitandani. Nukta hiyo hiyo mkewe akainia chumbani humo na kujitupa kitandani, akavuta suka na kujifunika mwiliwe akikiacha kichwa tu nje.
Yule mwanaume akatoka kitandani na kuchukua shati lake kutoka kwenye henga. Akavuta hatua na kuelekea sebuleni, kasha geti kubwa. Akatoka nje. Nje tu ya geti hilo kuliegeswa Land Rover 109, na vijana wawili walikuwa wameliegemea.
“Vipi kwema?” akawauliza bila kuwasabahi.
“Mr. Chameleon!” mmoja wa wale vijana akatamka, akashusa kiko chake na kukimata vizuri kwa mkono wake wa kulia, “usiku kama huu, hakuwezi kuwa na wema. Twende zetu ofisini, kuna ujumbe wako.
“Oh shit! Hebu niacheni nipumzike na mama yenu kwanza ee!” Chameleon akajibu.
“Ni kweli mzee, ila huna budi kufanya hilo, namba moja anakuhitaji haraka,” yule kijana akamwambia Chameleon. Mzee yule akajishika kiuno, baada ya tafakari ya sekunde kama kumi hivi, akawaaca wale vijana na kuinia ndani. Mkewe alikuwa tayari keshalala fofofo. Dakika kumi zilizofuata, tayari alikuwa ndani ya Kaunda suti. Akamsukasuka mkewe na kumwamsha.
“Aaaa unanikatisha ndoto yangu bwana!” mkewe akasema huku akiamka na kuketi.
“Mi natoka…”
“Unaenda wapi?” akamuuliza mumewe.
“Kazini mara moja!” Chameleon akajibu.
“We na kazi zako, nisakuzowea. Siku hizi hata ndoa hatufaidi, naachwa na kiu tu…” akalalama mwanamke wa Kizigua.
“Usijali mpenzi, ngoja tulitumikie taifa,” akambembeleza.
“Haya nenda kwenye taifa lako unalolipenda ukalitumikie… na taifa hili unaloliacha likivamiwa na waasi usilalamike!” Mkewe akasema. “Aaaaa mama watoto, unafika mbali sasa…”
“Piiiiiiip! Piiiiip!” honi ya gari ikamshtua.
“Haya mammy, tutaonana baadae!”
“Sawa Daddy”.
Wakabusiana, na mzee huyo akaiacha nyumba na kuondoka zake.
* * *
Saa saba usiku, Chameleon alifika Msasani kuliko na makazi ya Rais ambaye wao walimtambua kama ‘namba moja’ kwa kuwa ndioye aliyekuiwa na dhamana ya ulinzi kwa nchi nzima. “Pole!” Rais akamwambia huku akimkaribisa kiti katika ofisi yake ndogo. Ndani ya nyumba hiyo.
“Asante Meshimiwa, nimeitikia wito…” Chameleon akajibu kwa adabu zote.
“Nisichukue muda wako mwingi… kuna taarifa hii hapa ambayo imenifikia jioni ya leo. Sikuifanyia kazi kwanza, kwa sababu nilikuwa naipitia kwa kina,” akamwambia huku akimkabidhi ile karatasi iliyoandikwa pande mbili. Chameleon akaipokea na kuisoma mara kadhaa. Alipomaliza, akaiweka mezani na kumsogezea mkuu wa nchi.
“Kwa hiyo, hata waziri Kibwana Mtokambali anahusika?” Chameleon akauliza.
“Ningekuwa na majibu, nisingekuita. Nataka ufanye uchunguzi… umchunguze waziri
Kibwana na nyendo zake zote. Pia nataka unipe taarifa kamili za hawa maafisa wa jeshi, akiwamo Kepteni Vincent Mwanachia,” Rais akamwambia Chameleon. Naye akajibu kwa kutikisa kichwa juu chini.
“Chameleon, this is confidencial… hakikisha, ndani ya siku mbili, unanipa majibu stahiki,” Rais akasema na kuagana na mwanausalama wake anayemtegemea. Chameleon alitoka ndani ya ile ofisi, akachukua na ile karatasi huku kichwa chake kikiwa kimejaa mawazo ya nini cha kufanya dhidi ya hicho alichoambiwa. Alitazama saa yake, ikamwonesha kuwa ni saa tisa kasoro robo usiku. Akafikiri aende nyumbani kuendelea kuumaliza usiku na mkewe, au aende ofisini kuanza kupana na kupanua juu ya hicho alichoambiwa, akupata jibu. Mawazo yake yakamrudisa kwenye kauli ya mkewe ambayo iliuchoma moja kwa moja moyo wake, ‘…na taifa hili unaloliacha likivamiwa na waasi usilalamike!’
Saa tisa na dakika na dakika tano usiku alikuwa akipita Barabara ya Chole, Masaki akiwa bado ajui sawia ni wapi aelekeako. Katika barabara hii kulikuwa na nyumba kadhaa za vibopa na vigogo wa serikali. Kati ya nyumba hizo, ilikuwamo ya waziri Kibwana Mtokambali. Bwana Chameleone alikuwa na tatizo kubwa moja, akishapewa kazi basi akili yake uwa hailali mpaka kazi ile itimie. Katika barabara ya Chole maeneo ya Oysterbay, Chameleone alikuwa akiendesha moja ya magari yao ya siri katika idara ya Usalama wa Taifa, Volvo. Alipokuwa katika lindi la mawazo, akautuswa na mwanga mkali wa taa za gari lililoingia katika barabara hiyo kutokea ile ya mbele yake. Akapunuza mwendo na kususa ukali wa taa zake, lakini lile ari la mbele yake alikufanya hivyo na kupelekea mwanga ule kumuumiza machoni. Akapunuza mwendo na kueesa kando kidoo akisubiri ari lile lipite. Badala ya kupita, likawasa indiketa ya kulia na kuinia kwenye ujia mfupi ulioishia kwenye lango la nyumba nyumba moja kubwa.
Bahati gani ya mtende kustawi jangwani? Gari lile lilisimama mbele ya nyumba ya mheshimiwa Kibwana Mtokambali. Chameleon akarudisha gari barabarani nakupita pale polepole akiendelea nasafari yake. TB 620, namba za gari zilisomeka namna hiyo. Kwa kamera yake ndogo ya Kirusi aina ya Cimena, akapiga picha lile gari kwa upande wa nyuma likiwa linamalizikia kuingia ndani ya wigo ule. Chameleon, hakuelewa kama gari lile, usiku ule, alikuwa waziri Kibwana mwenyewe akitoka mizunguko au mgeni kaja kumtembelea, hakuna jibu. Akaamua kuegesha gari lake kwenye kona moja mbele yake. Kisha akaamua kurudi kwa miguumpaka usawa wa nyumba ya waziri Kibwana, mwenye dhamana ya ulinzi wa nchi yake.
Ukuta ulioizunguka nyumba hiyo ulikuwa mrefu kiasi, kadiri ya mita tatu hivi na juuye kulikuwa na waya uliozungushwa kwa usatadi mkubwa na kibao kilichosomeka ‘DANGER’ chenye rangi ya njano na maandishi meusi kilining’inia. Akasimama nje ya ukuta huo kwa kuwa mazunumzo ya awali ya maamkiano ya watu hao aliyasikia.
“Hakuna mtu nyuma yako? Maana hii nchi unaijua!” Sauti ya Kibwana ikasikika.
“Aaaa naijua kazi yangu mheshimiwa…”sauti ya pili ikajibu. Chameleone hakuweza kuigundua sauti hiyo kuya ni ya nani. Alichokifanya ni kutega masikio kwa nguvu zote kusikiliza kile kitakachozungumzwa hapo nje.
“Enhe!”Kibwana akaendeleza mazungumzo, ambapo sasa dhahiri shahiri,sauti zao zilikuwa za chini sana.
“Kule kila kitu kipo sawa. Kesho, kijana wetu atafanya maandalizi ya mwisho na wale kuruta wamejiandaa vyema…”
“Mmeshawapa pesa?” Kibwana akauliza kwa kimuhemuhe.
“Tumewapa nusu na nusu nyingine baada ya kazi…”mgeni akajibu.
“Sawa, sasa sikiliza…”
“Enhe!”
“…mpango ubaki vilevile, saa na siku iwe ile ile… Mimi kama nilivyokwambia, kwa kuwa ratiba ya Mzee ninaijua vyema, nitawaambia ni wakati gani mzuri…”Kibwana akasema kwa msisitizo.
“Sawa,we unachotakiwa utuambie masaa sita kabla!” yule mgeni akajibu.
“Sawa, sasa mipango mingine, we pita ofisini kesho kama saa nane hivi!” Ukafuatia ukimya kidogo na baadae milango ya gari ikasikika ikifungwa. Chameleone akajibanza palepale na kulisuudia lile gari likitokomea katika barabara za Masaki.
Hapa kuna jambo kubwa! Akawaza na kujitoa katika ule ukuta. Akaliendea gari lake na kuingia ndani. Mara baada ya kushusha pumzi ndefu, akawasha injini na kuamua kurudi nyumbani kwake kujipanga kwa siku inayofuata.
SIKU ILIYOFUATA
Siku hii haikuanza vizuri kwa wakazi wa jiji la Dar es salaam.mvua kubwa yenye radi kali ilikuwa ikinyesa. Mzee Chameleon akajikuta anashindwa kubanduka kutoka katika kifua cha mkewe. Joto mujarab la mwanamama huyo lilimfanya alale kama motto kitandani hapo.
“Mwenzetu we huendi kazini?” Mkewe akauliza. Chameleone akainua saa yake mezani na kutazama. Loh! Ilikwishatimu saa tatu za asubuhi. Akakurupuka na kuijiweka tayari. Baada ya chai nzito kutoka kwa mkewe, akaingia katika gari lake na kutia injini moto.
Katika taarifa ya siri aliyopatiwa jana yake na Mkuu wa nchi, kulikuwa na orodha ya majina kadhaa ambayo kwayo ilimpasa kuyafatilia. Akiwa na mawazokichwani mwake, alijitahidi kuendesha gari kwa uangalifu. Akaiacha barabara ya Kawe na kukunja kushoto kuifuata ile ya Bagamoyo kuelekea Mwenge. Mita chache mbele, akakunja kushoto na kutazamana na lango kuu la kuingia katika kambi ya jeshi ya Colito, Lugalo.Askari aliyekuwa lindo akalifuata gari hilo na kuuliza maswali mawili matatu, kasha akaliruhusu kuingia. Chini ya mwembe mkubwa, ndani ya kambi hiyo akaegesa gari lake na kuvuta hatua ndogo ndogo kuelekea katika canteen ya maafisa.
Hakukuwa na watu wengi, lakini pia hakupenda kukaa kiti cha peke yake. Hatua zake, zikamfikisha mbele ya meza moja iliyokaliwa na mwaDanada alievalia sare za jeshi. Cheo chake ca Kepteni kilijionesha pasi na kificho kwa nyota tatu zilizojipanga vyema mabegani mwake.
“Hujambo bibie?” akamsabahi na kumtupia tabasamu lenye bashasha. Yule binti aliinua sura yake na kumtazama Chameleone kuanzia juu mpaka chini.
“Salama, karibu!” akajibu, kasha akaendelea kuburudika kwa supu ya kongolo iliyokuwa mbele yake.
“Karibu baba, nikusaidie nini?” ni sauti ya mhudumu iliyomshitua kutoka katika kumtazama afande yule, kepteni wa kike.
“Nipatie kongolo na Pepsi Cola. Itakuwa shin’ ngapi?” akauliza.
“Shilingi kumi na mbili tu,” mhudumu akjibu.
“Pamoja na hii ya Kepteni Zuhura…” akaongeza kusema. Yule afande aliposikia jina lake likitamkwa, akainua uso na kumwangalia huyo alitajaye kwa mara nyingine.
“Shilingi kumi na sita tu,” akajibu.Chameleone akatoa noti ya shilingi kumi kumi, mbili, na kumpatia.
“Hizo shilingi nne ununue bofulo kwa ajili ya watoto,” akamwambia mhudumu, naye akashukuru huku akitokomea jikoni. Mara baada ya kumalizana na yule mhudumu, akarejesha macho yake kwa afande yule.
“Asante kwa ukarimu wako,” Kepteni Zuhura akamwambia Chameleone.
“Karibu. Hivi ndivyo wanaume tunavyopaswa kuwa, nitapenda kutembelea ofisini kwako kabla sijaondoka kambini hapa leo hii…” Chamelleone akamwambia Zuhura.
“Karibu sana, lakini bahati mbaya, mimi sina ofisi…”
“KIvipi?”
“Ofisi yangu ni uwanjani tu,” Zuhura akajibu.
“Unamaanisha nini, wakati cheo chako kinakutaka kuwa ofisini? Wewe si ni ofisa!” Chameleone akazidi kudadisi.
“Ni kweli, ila mimi ni mkufunzi zaidi kuliko kuwa ofisini,” akamjibu.
ITAENDELEA
GENGE
EP3
Unamaanisha nini, wakati cheo chako kinakutaka kuwa ofisini? Wewe si ni ofisa!” Chameleone akazidi kudadisi.
“Ni kweli, ila mimi ni mkufunzi zaidi kuliko kuwa ofisini,” akamjibu.
“Ooh, safi sana! Je naweza kujua ni mkufunzi wa nini? Kama hutojali,” mtu mzima, Cameleone akauliza.
“Mimi ni mkufunzi katika Sanaa ya mapigano ya ana kwa ana. Huwa nakuja kuendesha mafunzo haya kwa vijana walio katika Special Force,” Zuhura akajikuta anabwabwaja bila simile mbele ya Chameleone. Muda huo huo, staftahi yake ikafika, akaagana na mwanamke huyo kasha yeye akaendelea na kuitupia kinywani supu aliyoagiza. Dakika ishirini baadae, akawa tayari nje ya kantini hiyo ya maafisa, akivuta hatua taratibu kuelekea jengo la utawala.
Hatua zake ndefu ndefu zikamfikisha kwenye jengo hilo, ambalo juu ya ukuta kuliandikwa jina Colito. Akasimama kwa sekunde kadhaa kabla ajaingia katika ofisi hiyo ambayo kwayo, mkuu wa kikosi hicho huwapo.
“Shida!” sauti kutoka nyuma yake ikamgutusha.
Chameleon akageuka taratibu ma kumtazama huyo asemaye. Kijana mmoja, mrefu, aliyependeza katika mavazi yake ya kijeshi, mgongoni mwake alikuwa kabeba bunduki kubwa, AK47. Kijana yule alikuwa kasimama imara, hacheki wala hatikisiki. Chameleon akajua wazi kabisa kuwa anasubiri jibu hata kama hajauliza.
“Aaaann nahitaji kumuona, Kepten Baka Baka,” Chameleone akajibu huku akisimama sawa kutazamana na mwanajeshi huyo.
“Bakabaka ndiyo nani?” yule mwanajeshi mwenye cheo cha Koplo akamtwanga swali Chameleon lakini hakujibiwa.
“Ninyi ndiyo tunaowatafuta, yaani tumewapiga kule kwenu Uganda lakini bado mnaendelea kutufuatafuata, sasa leo umejileta.
“Mimi nina shida zangu za ofisini kijana!” Chameleone akajieleza.
“Hakuna, wewe ni jasusi, umetumwa, sasa nakuweka ndani,” yule askari akasema pasi na mzaha. Sura yake tu haikuwa na chembe ya huruma, macho yake mekundu yalieleza wazi hisia zake za ukatili. Akapuliza filimbi iliyokuwa katika mfuko wake wa shati lile la kijeshi kwa mtindo wa pekee. Sekunde chache tu, wanajesi wenine wawili wakawasili.nao walikuwa katika kombati za jeshi, na mabega yao kuja katika viwiko yalivikwa kitambaa cheupe chenye herufi mbili nyekundu, MP yaani Military Police au kwa lugha nyepesi tungesema, polisi wa jeshi. Walipofika pale, yule bwana akawapa ishara tu, hawakuhoji, wakamchukua na kuondoka naye.
Mzee Chameleone akatupwa rumande maalumu ambayo huwekwa wanajeshi watukutu au wenye makosa mbalimbali. Na huwekwa ndani kwa amri ya wakubwa wao kulinana na kosa lenyewe. Lakini yeye aliwekwa humo kwa kutuhumiwa kuwa ni jasusi. Akaingizwa kwenye jengo moja lililojitenga kando kabisa na mengine. Kabla ya kufika katika jengo hilo walipita jirani kabisa na uwanja wa mazoezi na hapo alishuudia mazoezi makali ya Martial Art yakiendelea chini ya Kepteni Zuhura. Alipotazama upande ule, akagongana macho na mwanamke huyo aliyekuwa amesimama akiwatazama vijana wake.
“Songaaaa! Usiangalie wake wa wakubwa, ala!” Mp mmoja akamkaripia na kumsukuma mbele.
“Vua viatu, saa, mkanda, kofia na kama una pesa zote weka hapo kwenye mess tin,”akaamriwa, naye akatii. Alipomaliza kutekeleza hayo akaingizwa kwenye chumba kimoja ambacho ndani yake alikutana na watu wenine wanne. Watu wale wote aliwatambua kuwa ni wanajeshi kutokana na suruali zao za mabakamabaka. Ni yeye tu aliyekuwa amevaa kiraia, suti ya mtindo wa Kaunda.
“Kaa kwanza huko mpaka tutakapokuchukua kwa mahojiano…” MP mmojawapo akamwambia huku akimsukumia ndani na kuupia kufuli mlango huo wa chuma.
“Mzee, umepotea njia?” mmoja wa wale vijana akamuuliza.
“Nilipotea njia, nikajikuta ndani ya kambi, nikakamatwa na kuletwa huku,” akamjibu.
“Pole sana! Wananchi lazima muhesimu kambi na maeneo ya jeshi, na si kukatizakatiza kama mnaenda chooni,” akasema yule mwanajeshi.
“Sasa mbona aliyekuleta amesema usubiri kuhojiwa?” mwingine akadakiza swali.
“Mi sijui taratibu zenu za kijeshi, mi najua jeshi la wananchi, kwa hiyo sikuona shida kupita kuuliza niendako…” Chamelleone akawajibu na wote wakaanua vicheko.
Sekunde chache baadae, ukimya ukatawala kama mwanzo. Mzee Chameleone akiwa amekaa upande mwingine wa chumba kile, alikuwa kimya kabisa, akiwaza na kuwazua. Kwa namna nyingine alionakama amepewa nafasi ya utulivu ya kufikiri juu ya kile anachokifuatilia tofauti na anekuwa ofisini.
“We! Kwa hiyo… mi siwezi kukaa humu, ngoja nikaungane na wengine…” mmoja wa wale vijana wa jeshi akamwambia mwenzake.
“Unasema nini wewe? Mimi siwezi, kamwe, waje hata wakitaka waniue…” yule mwenzake akajibu.
“Wenzetu washakubali, wako nje saa hii…” akasema mwingine kabisa ambaye daima alikuwa kimya.
“Nimeapa kuilinda nchi yangu, na si vinginevyo!” akasema yule wa kwanza. Mara ukasikika mlango wa chuma ukifunguliwa. Yule mwanajeshi aliyesema hawezi kukaa mule ndani, akasimama haraka na kuuendea mlango wa chumba kile, kwa mikono yake miwili akasika zile nondo.
“Afandeee!” akaita.
“Tulia we muasi, wazalendo tupo kazini, kuilinda na kuipigania nchi yetu,” akajibiwa kutoka katika moja ya vyumba vile ambamo labda askari wale au yule aliingia.
Maneno yale yalimvutia sana Chameleone, akatega sikio kusikiliza kwa maana alishajuakuwa watu hao wanaongea kwa mafumbo. Dakika mbili baadae, akasikia michakacho ya miguu ya mwaDanamu anayetembea kwa hatua za haraka haraka kuelekea mlango ule. Wakati huo huo akamwona yule mwanajeshi pale mlangoni akaisogea nyuma kama sentimeta thelathini hivi. Kufuri likafunguliwa.
“Onana na Chatu haraka sana! Dakika kumi zikipita hujamwona, utarudi humu. Hakuna mwingine aliyechoka kukaa humu?” yule aliyefungua akauliza, huku akiwa anachungulia mule ndani. Macho yake yakagongana na ya Chamelleone. Sekunde mbili kama si tatu, akaingia ndani ya kile chumba.
“We raia vipi? Aliyekwambia hii ni selo ya watu kama wewe nani?” yulemwanajeshi akauliza.
“Selo ya raia iko wapi afande?” Chameleone akauliza.
“Atakujibu aliyekuleta!” akasema na kutoka nje huku akibana kufuli lile.
* * *
Baada ya saa sita kupita, Chameleone akatolewa ndani ya kile chumba na kuongozwa mpaka cumba kingine, akawekwa ndani yake na kutakiwa kusubiri hapo. Nusu saa baadae waliinia wanajeshi wawili. Mmoja alivaa kombati iliyopambwa kwa nyota tatu mabeani mwake na mwingine alivaa vilevile isipokuwa yeye alipambwa na v moja na kitambaa cheupe chenye erufi M na P. Yule kepteni akaketi kwenye kiti cha mbao na yule MP akasimama kando kiukakamavu kabisa.
“Wewe ni nani?” yule Kepteni akauliza. Chameleone akamtazama kwa jicho bay asana, hakujibu.
“Unajua hatupo kwenye utani ee, miaka hii nchi yetu imekuwa na maadui wengi sana. Taarifa niliyoipata ni kuwa wewe ni jasusi mmoja wa nchi hizo...”
“Hujakosea, mimi ni jasusi mmoja wa nchi hizo. Sasa siwezi kuzungumza chochote na wewe, namhitaji mkuu wako wa kikosi…” Chameleone akawaambia. Wale wanajeshi wakatazamana na kuanza kucheka.
“Unafikiri mkuu wa kikosi huwa anawasikiliza watu kama ninyi? Wewe tunakupia risasi kwa sababu umeidharau kambi,” yule kepteni akasema.
Ikawa zamu ya Chameleone kucheka, akacheka kwa sauti kubwa, kisha akanyamaza na kuwatazama.
“Nyie, msinifanye mimi mtoto mwenzenu, wewe mwili wako ushaingia risasi ngapi?” yule Kepteni hakujibu. Na Chemelleone akaendelea kusema.
“Kwa taarifa yako, hapa nilipo nina risasi mbili mwilini, hivyo siogopi risasi hizo unazozisema. Ondokeni hapa, mkamwite mwenye cheo cha juu kuliko ninyi wote…” akang’aka Chameleone. Yule kepten akasimama kutoka pale alipoketi na Chameleone akafanya hivyo.
“Mfundishe adabu!” akamwamuru yule MP, naye akamjia mzee yule akiwa tayari na mkanda wa jeshi mkononi, asijue anayemfuata kipumbavu ni nani katika medani ya upianaji. Hatua moja kabla ya kumfikia, yule MP akauzunusha ule mkanda hewani tayari kushambulia. Chameleone aliruka juu kimo cha ng’ombe, pio moja maridadi likamfanya yule kijana azunuke kama pia na kujibamiza ukutani, kisha akaanguka chini kama mzigo. Kepteni akamtazama yule mzee, kisha akamtazama kijana wake pale chini akiwa hana fahamu. Hakuwa na uamuzi mwingine zaidi ya kutoka nje na kuufunga mlango.
Dakika kama tano hivi wakawasili vijana wengine watano waliojazia miili. Wakafunua mlango wa kile chumba wakiwa na uchu wa kutoa kipigo kwa huyo mzee. Awakukuta mtu zaidi ya yule MPakiwa sakafuni. Hawakuamini, wakatafuta mpaka kwenye droo za kabati, hakuna mtu.
Wakambeba yule mwenzao na kumuwahisha hospitalini. Kishapo taarifa zaikafika kwa yule kepteni, hakuamini anachoambiwa. Akasimama kwa gadhabu na kutoka nje, alipofika mlangoni akakutana uso kwa uso na Chameleone aliyekuwa amesimama mkabala na ngazi za kuingilia katika jengo hilo la utawala. Palepale alipokamatiwa mwanzo. Yule kepteni akapatwa na mshtuko, hakujua nini afanye, arudi ofisini au aende kumkabili mzee huyo? Utata.
“Hivi, we mzee ni mzimu?” akamuuliza.
“Njoo unishike, uone kama mzimu una mifupa!” Chamelleone akajibu na kuanza kupanda ngazi.
“Unaenda wapi?” akaulizwa na yule kepteni.
“Ofisini kwako, tena uje bila kuchelewa!” Chameleone akamjibu na kumpita pale aliposimama, akaongoza na kuingia kwenye mlango wa tatu. Yule kepteni kwa woga akarudi ofisini kwake na kumkuta mtu mzima yule amekwishaketi kitini.
“Keti kijana! Kepteni Mwanachia…” akamwambia, na yule kepteni akaketi huku kicwani mwake kukiwa na mawazo lukuki.
Ni nani mtu huyu? Alibaki kujiuliza.
“Kepteni! Kumbuka kuwa hiki ni chombo cha wananchi, yakupasa kukitii kiapo chako, na si vinginevyo. Mbinu zozote chafuchafu kwa maslahi yako na ya wenzako, zitawagharimu maisha,” Chameleone akasimama na Kepteni Mwanachia naye akafanya vivyo hivyo.
“Wewe ni nani?” Mwanachia akauliza.
“Mzimu! Na usiku huu nitakutokea nyumbani kwako,” Chamelleone akamjibu na kutoka nje. Moja kwa moja akaliendea gari lake na kuondoka eneo lile.
* * *
Dakika thelathini baadae, Chameleone aliegesha gari lake nje ya ofisi yake ya siri, maeneo ya Hospitali ya Ocean Road, jirani kabisa naupande wa nyuma wa Ikulu ya Tanzania. Akaingia ndani na kuketi kitini, akiitazama meza yake iliyokuwa pweke muda wote. Kwanza akatua mezani hapo kabrasha alilotoka nalo garini, kisha akaingiza mkono mfukonina kutoa karatasi ndogo, ya rangi nyeupe iliyofifia, akaiweka kando ya kabrasha lile. Akainuka na kuuendea mtungi wa udongo uliokuwa kwenye kona ya chumba hicho. Ndaniye, akachukua Pepsi Cola moja kati ya sita zilizowekwa majini mtungini humo. Akafungua kwakutumia meno, na kurudi tena kitini.
Kilikuwa ni kibanda tu kikuukuu kilichotelekezwa pembeni kabisa mwa hospitali hiyo maarufu sana. Kama ungejaaliwa kukiona kwa nje basi ungesema ni ‘choo kibovu’. Hakikuwa na paa upande mmoja. Mbao zilizooza, ndizo zilionekana wazi waziwe. Upande mwingine kulikuwa na paa la vigae vikuukuu. Nje, pembezoni kidogo, palikuwa na mti mkubwa wa zambarau. Katika kibanda hicho, ndipo mzee huyu, mwanausalama mwaminifu wa serikali, alikuwa akifanyia mambo yake tofauti na ofisi yake ya kawaida ambayo huwa na wenzi wake wengi.
Akakisoma kile kikaratasi vizuri.
Bayankata itakuwa DDC Kariakoo
Usiku wa leo saa 4:00 usikose.
Mpenzio.
ITAENDELEA
EP1
JULAI 15, 1991 DIAMOND JUBILEE
SAUTI KUBWA YA MUZIKI ilisikika kutoka katika ukumbi huo maarufu jijini Dar es salaam, katika kitongoji maarufu cha Upanga. Ni harusi ya kukata na shoka, kati ya Bi. Egra Mwakasimba na Dastani Kihwelo. Mamia, kama si maelfu ya watu waliujaza ukumbi huo. Wakila na kunywa huku wakitunuku zawadi kemkem kwa maharusi hao. Mishale ya saa mikononi mwa waliowengi ilioneshas saa sita kasoro robo usiku. Wenine walisaanza kusimama na kuondoka wakati wimbo huo unaojulikana kama ‘Wifi twende nyumbani’ ukirindima. Maharusi nao walikuwa wima wakitembea kwa mwendo wa maringo na hatua za hesabu kulielekea lango kuu, tayari kwenda kula fungate.
Nje ya ukumbi huo, gari la maharusi lilikwishaandaliwa na kuegeshwa mahala pake. Mercedes Benz E Class,jipya kabisa, toleo la 1990 lilipambwa likapambika. Gari hilo la pesa nyingi lilitolewa zawadi na idara ya Usalama wa Taifa ambapo Dastani Kiwelo alikuwa mwajiriwa mtiifu. Baada ya kuagana na ndugu na marafiki, Dastani, na mkewe Egra wakajitoma ndani ya chombo hicho kipya.
“Ooooh! Gari zuri sana mume wangu!” Egra akasifia mara tu baada ya kupokelewa na kiti cha ngozi laini. Akatazamana na mumewe na kubusiana kisha Dastani akapachika funguo mahala pake na kuliwasha. Ndani ya gari hilo walijiona wao tu, taratibu gari lile likaingia barabarani na kutokomea huku likiwaacha watu wakisindikiza kwa macho. Mazungumzo kati ya mtu na mkewe yalicukua nafasi wakati tairi zikichachafya Barabara ya Ally Hassan Mwinyi mara baada ya kuiacha ile ya Umoja wa Mataifa. Kutoka kwenye redio ya gari hilo, sauti ya mwaDanada Judy Boucher ilikuwa ikisindikiza kwa kibao matata ckinachokwenda kwa jina ‘Mr. Dream Maker’.
“Asante Dastani,” Egra akashukuru.
“Asante nawe pia, umenifanya niwe mwanaume sasa,” Dastani akamjibu mkewe huku akiongeza mwendo kulipita gari la mbele yake.
“Nataka tujenge familia ndogo, yenye upendo na furaha…” Dastani akajibu, alipotaka kulipita gari lingine akasikia honi kali nyuma yake. Akarudisha usukani kushoto na Benzi lile likatii amri. Mazda jekundu likampita kasi. Ndani ya Mazda lile ‘kibanda wazi’ kulikuwa na mwanamke mmoja ambaye ndiye dereva. Mshtuko wa wazi kwa Dastani ukaonekana.
“Vipi honey, mbona umepoa ghafla?” Egra akauliza.
“Hapana, hamna kitu,” akajikaza kiume, Waswahili husema.
“…unanificha, au ndo x wako? Wanaume amna wema!” Egra akalalama na kueukia upande wa pili.
Wanawake bwana! Hapo keshawaza mengine! Dastani akawaza na kupunguza mwendo. Kama mwanausalama, alishajua nini kitatokea kama akiendelea kufuata barabara hiyo. Akili ilimtuma kuchepuka na kuingia kulia kwenye barabara ndogo ya Kaunda, hakufanikiwa.
Kutoka nyuma ya kiti chake aliisi kitu chenye ncha kali kikimchoma pembeni kidogo ya uti wa mgongo. Akatulia huku gari likiendelea kuseleleka taratibu. Egra akaundua hilo, akageuka nyuma na kukutana macho na mtu aliyevaa soksi jeusi kufica uso wake. Alipotaka kupiga kelele akajikuta akipiwa na kiganja kigumu upande wa nyuma wa shingo, akazirai.
“Endelea na barabara hiyo hiyo mpaka nitakapokwambia,” sauti nzito ya mtu huyo ikamwamuru. Dastani akuwa na ujanja, akatenda aliloambiwa na mtu huyo. Kicwani mwake aliendelea kutafakari na kujaribu kukumbuka ni wapi aliisikia sauti hiyo, asipate jibu.
Dakika mbili zilizofuata walifika eneo la Mbuyuni.
“Kunja kushoto!” akaamriwa. Naye akatii na kucuku barabara ya Ruhinde. Mbele kidogo akatakiwa kukunja kulia, akafanya hivyona kuingia Mtaa wa Galu. Mara tu baada ya kukunja ile kona akaliona lile Mazda jekundu limeegeshwa kando.
“Simama hapo!” akaamriwa, naye akatii. Kutoka kwenye vivuli vya miti, wakajitokeza watu wengine watatu, wanaume ambao sura zao alizifahamu vyema. Dastani akateremshwa garini na kusimama chini,
“Umependeza Dastani, suti ya gharama uliyovaa, gari ya kisasa uliyopewa zawadi na wadosi wako… vyote ni kwa sababu ya kutuuza swahiba zako,” mwanaume wa makamo alizunumza huku akiwa kasimama mita chache tu kutoka kwa Dastani.
“Ilikuwaje ukakiuka maagizo Dastani, ata ukasababisha mipango yetu kwenda fyongo? Mpiganaji wetu , komandoo Salimu Manumba akauawa… yote kwa sababu yako. Na wewe mwenyewe kwa mkono wako ukamuua Bambross pale Embassy Hotel, ukachukua nyaraka nyeti na kuwapa mabosi wako. Tulijua u mwema, kumbe fukufuku mchangani. Watu wa aina yako uwa hawastahili kuishi… kwa taarifa yako, ulichokisema kwa mabwana zako ni asilimia kumi tu ya mpango mzima. Usifikiri tulikuwa wajinga kwamba tungeweka kila kitu mbele yako, la hasha! Sasa wewe utakuwa sanduku letu,” yule bwana akamaliza na kuingia kwenye lile Mazda jekundu pamoja na yule mwanamke wa Kizungu. Dastani akarudishwa garini mwake, mara hii, kwenye kiti cha nyuma huku vijana wengine wawili wakikaa upande huu na ule. Egra akiwa bado kwenye mzimio.
Safari yao iliishia Msasani Peninsula, kando kabisa ya Bahari ya Indi kulikuwa na nyumba moja pweke, ya kifahari. Ni katika nyumba hii ndipo, Dastani na mkewe, Egra, walikuwa wakielekea tayari kwa kuuanza usiku wa kwanza kama wanandoa.
“Usiwe na wasiwasi Dastani, fungate mtakula kama kawaida, na mtainjoi harusi yenu ndani ya nyumba ni hii hii,” yule bwana akazungumza. Dastani hakujibu. Yule mwanamke wa Kizungu mwenyue Mazda jekundu akaja na ndoo ya maji mkononi na kummwagia Egra. Egra akakurupuka na kuanza kuhema kwa nguvu na haraka haraka huku akimwita Dastani kwa sauti kali. Makofi mawili aliyozabwa na yule mwanamke yakamnyamazisa na kumwacha akitweta. Dastani, alilishuhudia tukio lile, akauma meno kwa uchungu na hasira.
“Mwacheni mtoto wa watu msimdhuru, haya hayamuhusu…” Dastani akatamka.
“Hatuwezi kumdhuru huyu, hana hatia, ila ataishi na sisi mpaka Munguamchukue mwenyewe, na wewe, malipo ya kazi yako yamefika…” alipomaliza kusema hayo kikafuatia kipigo kikali kutoka kwa wale vijana. Dakika kumi, zilimwachaDastani akiwa chini, hoi bin taabani, kila alipokohoa alitokwa na damu kinywani. Egra alikuwa akilia kwa uchungu kwa kila alipokuwa akitazama kipigo anachoshusiwa mwenza wake. Wale vijana baada ya kumsulubu Dastani, wakamwacha pale chini na kufunua buti la lile Mazda, wakatoa madumu mawili ya petrol na kuinia ndani ya ile nyumba. Dakika tano baadae wakatoka na kumwaga mafuta yaliyobaki kwenye kibaraza na mengine wakalimwagia lile Benz. Haikupita dakika mbili , upande wa baarini ikawasili boti ndogo.
Vijana wawili wakashuka wakiwa wamebeba miili ya watu wawili; mwanamke na mwanaume. Awakuongea na mtu,wakapitiliza ndani ya nyumba ile moja kwa moja. Iliwachukua kama sekunde arobaini hivi, wakatoka.
“Tayari boss,” wakamwambia yule bwana aliyesimama kando ya Dastani. Akawajibu kwa kutikisa kichwa. Akawapa ishara ya kumbeba Dastani na mkewe, wakafanya hivyo na kuwapakia kwenye ile boti. Pamoja nao, wakafuatana na wale vijana wengine.
“Ash to ash!” akatamka yule mwanaume na kuitoa sigara yake kinywani kisha akaitupia pale kibarazani. Moto mkubwa ukalipuka na kuichoma ile nyumba na kuteketeza lile Benzi wakati wawili wale wakipotea mbali ndani ya Mazda lao.
“Mungu amlaze panapomstahili,” yule bwana akatamka.
“Jesca! Moja kwa moja uwanja wa ndege,” akaoneza kusema. Yule mwanamke aliyeitwa kwa jina la Jesca akaitika kwa kichwa.
* * *
2002 Januari
BRUSELS –UBELGIJI
Wingu zito lilitanda katika anga la jiji hilo, barabara zilifunikwa na kwa barafu na kusababisha baridi kali kwa wakaazi wake. Daima kipindi kama hiki cha miezi ya Desemba mpaka Februari, nchi za Ulaya hupitia katika kipindi hiki, winter.
Nje ya jengo refu lenye sakafu thelathini na sita, linalojulikana kama Tour des Finances, gari moja la kisasa aina ya Audi liliingia katika uwanda wa maegesho, chini ya jengo hilo, likiiacha barabara kubwa ya Royale inayokatiza pembezoni mwake.
Kutoka ndani ghorofa ya ishirini na tano, ndani ya ofisi moja nadhifu iliyosheheni vitabu na makabrasha anuai katika rafu zake zinazong’aa kwa polish safi, hatua za mtu anayeujongelea mlango zilisikika pasi na kificho. Zilipofika mlangoni hapo, zikakoma. Sekunde kumi na tano zilizofuata, mlango ukafunguliwa. Kipande cha mwanaume kikaingia ndani. Kabla hajawasha taa kwa minajiri ya kufukuza iza hafifu lililosababishwa na wingu lile; aliona taa ikiwaka yenyewe.akapiwa na mshtuko na kuwai kugeuka upande wa pili ambako kuna swichi nyingine ya kuongoza taa hiyo.
“Usiogope, ni ugeni tu wa kawaida…” sauti ya mwanaume ikasikika upande ule. Yule bwana akashikwa na kigugumizi na kutazamana macho kwa macho na huyo aliyejiita mgeni.
“Wewe ni nani? Na unafanya nini katika ofisi yangu?” kile kipande cha mtu kikauliza uku akivuta kiti na kuketi nyuma ya meza yake kubwa.
“Mimi ni mgeni wako kutoka katika nchi iliyokulea, mpaka ukawa mtu mzima na kuiasi,” yule mgeni akajibu.
“Nani aliyekutuma?”
“Mama yako!” yule mgeni akajibu huku akicezea vidole vyake.
“Hivi ninyi Watanzania mna matatizo gani? Kwa nini ampendi watu wastarehe na maisha yao? Kutwa kucha mnatufuatilia, tuacheni!” akang’aka yule bwana.
“Jiulize! Ni Watanzania wangapi wanaisi Ughaibuni tumekuwa tukiwafuatilia? Kama si wewena washenzi wenzio tu… mngekaa kwa amani kama mngeondoka kwa amani…lakini mlichokifanya mnakijua, na adabu yake mnaijua. Nyote lazima muitumikie adhabu yenu…” yule mgeni akaeleza. Ndani ya mfuko wa ndani ya suti yake akachomoa bahasha ya khaki, juu ilikuwa na mhuri wa serikali.
“Ichane, uisome, nimetumwa na mama yako kukuletea…”
Yule bwana akaichana kwa kitete huku akivuta kamasi jepesi kulirudisa ndani ya pua zake ndogo. Akatulia kuisoma. kijasho chembamba kikamtiririka ilhali ofisi hiyo ilitawaliwa na baridi.
“Wewe ni nani?” akauliza kwa sauti huku akizungusha kiti kumtazama mgeni huyo. Mkono wake wa kuume ukabonyeza kitufe Fulani na kuruusu saraka ya siri kufunuka katika meza hiyo. Akabaki kakodoa macho akiwa haelewi nini cha kufanya.
“Usihangaike Bwana Titus Mwakibinga, bastola yako ninayo, nilikwisaichukua kitambo!”
Yule mgeni akamwambia mwenyeji wake ambaye mara hii alimtaja kwa jina la Titus Mwakibinga. “Umeju-aje ma-ha-li bastola ya-ngu i-li-po?” Titus akauliza kwa kigugumizi uku akipiga ngumi mezani.
“Kwani wewe ulifikiri hapo ni mahala pa siri? Mimi nilisapajua zamani sana, na sikupata tabu kuichukua,” mgeni akajibu.
“Nakuuliza kwa mara ya mwisho… wewe ni nani?” Titus akatupa swali uku akiwa amefura kwa hasira.
“Naitwa Amata Ric, au Kamanda Amata, TSA 1, code 005…” yule mgeni akajitambulisa huku tayari bastola ikiwa mkononi mwake. Titus alipotazamana na bastola ile alijikuta akiisiwa nguvu.
“Mbiyo za panya! Titus, hata kama kosa umelifanya mwaka ’82, hukumu iko palepale. Kama ulifikiri ukitoroka ndiyo utaukwepa mkono wa sheria, basi umeula wa chuya kwa uvivu wa kuchagua. Hukumu ya kesi yenu ilisomwa mwaka 1985, Desemba 28 na Jaji Antoni Mzavas. Wenzi wako walihukumiwa kifungo lakini wewe na wengine wachache mlitoroka nchi. Titus Mwakibinga, umehukumiwa kifo…” Kamanda Amata akamwambia pasi na lepe la tabasamu usoni mwake.
“Mimi sihusiki, serikali imenionea tu,” Titus akalalama.
“Sasa nani anahusika kama si wewe?”.
“Sijui!”
“Hujui? Kama hujui, basi ni mhusika mmoja wapo…” Amata akasema.
“Nooo!” Titus akang’aka mara alipoona bastola ile imeondolewa usalama.
“Kijana, nitakupa pesa nyingi sana,” akasema Titus.
ITAENDELEA
GENGE
EP2
Nooo!” Titus akang’aka mara alipoona bastola ile imeondolewa usalama.
“Kijana, nitakupa pesa nyingi sana,” akasema Titus.
“Sihitaji pesa yako, nimekuja kutekeleza kile nilichotumwa kama ulivyosoma kwenye hiyo hati,” Amata akasema na kumfanya Titus ageuke kutazama mezani. Macho yake yakagonganana neno KIFO, lililoandikwa kwa wino mzito na kupigiwa mstari mwekundu.
“Buriani Titus! Ukishakufa uwatokee wenzio kwenye ndoto uwaambie kuwa nitamuua mmoja baada ya mwingine. Popote watakapokimbilia…” Amata akasema. Kabla Titus hajaongea chochote tayari, risasi moja kutoka kwenye bastola yake mwenyewe, Glock 23, ikatoboa paji la uso. Titus Mwakibinga akajibamiza kitini na kichwa chake kuegemea kushoto. Amata akaipachika bastola ile mkononi mwa marehemu.
Nje ya jengo lile, akatembea taratibu huku mikono ikiwa mfukoninabubblish ikiteketea kinywani mwake, akapita barabara ya Royal kuelekea Best Western Hotel ambako ndiko aliwekeza makazi yake kwa muda akiwa katika operesheni hiyo. Ze Sindiket…
* * *
Ndani ya hoteli ile, Amata alijitupa kitini, akavua glovesna kuziweka juu ya meza ndogo ya kusomea. Akavuta kabrasha lake na kupekua hapa na pale akitazama kinachofuata. Alipojiridhisa na kazi yake akalikunja kabrasha lile na kulitia mkobani.
1981
DAR ES SALAAM
UPEPO MWANANA uliendelea kuvuma. Dirisha kubwa katika moja ya nyumba nyingi katika eneo la Kawe Mzimuni, liliruhusu upepo huo uwafikie wapendanao wawili waliokumbatiana kitandani usiku huo. Muziki laini kutoka katika santuri ya Mbaraka Mwishehe ulikuwa ukiendelea kusikika kwa sauti ya chini. Kelele za mibweko ya mbwa ikamshtua mwanamke aliyelala kitandani hapo. Mwanamke wa Kizigua, mwenye shepu isiyosemeka, akajivuta na kunyoosa mkono wake mpaka sehemu Fulani, uvunguni mwa kitanda hicho. Taa kubwa ya nje ikawaka na kufanya nuru kali ambayo kila kitu kingeonekana.
Mbwa waliendelea kubweka, mwanamama yule akaamka na kukiacha kitanda. Umbo lake la Kitanga likafanya mitetemo ya kuvutia na kuuweka dhahiri shahiri uanamke wake. Akakiacha cumba na kuelekea sebuleni. Wakati mbwa wakiendelea kubweka, mara kelele iliyofanyika kwa mawe matatatu kurushwa batini, ikamshtua mwanaume aliyelala kitandani hapo.
Akaamka na kupapasa upande aliokuwapo mkewe, hayupo. Akajiinua na kuketi kitandani. Nukta hiyo hiyo mkewe akainia chumbani humo na kujitupa kitandani, akavuta suka na kujifunika mwiliwe akikiacha kichwa tu nje.
Yule mwanaume akatoka kitandani na kuchukua shati lake kutoka kwenye henga. Akavuta hatua na kuelekea sebuleni, kasha geti kubwa. Akatoka nje. Nje tu ya geti hilo kuliegeswa Land Rover 109, na vijana wawili walikuwa wameliegemea.
“Vipi kwema?” akawauliza bila kuwasabahi.
“Mr. Chameleon!” mmoja wa wale vijana akatamka, akashusa kiko chake na kukimata vizuri kwa mkono wake wa kulia, “usiku kama huu, hakuwezi kuwa na wema. Twende zetu ofisini, kuna ujumbe wako.
“Oh shit! Hebu niacheni nipumzike na mama yenu kwanza ee!” Chameleon akajibu.
“Ni kweli mzee, ila huna budi kufanya hilo, namba moja anakuhitaji haraka,” yule kijana akamwambia Chameleon. Mzee yule akajishika kiuno, baada ya tafakari ya sekunde kama kumi hivi, akawaaca wale vijana na kuinia ndani. Mkewe alikuwa tayari keshalala fofofo. Dakika kumi zilizofuata, tayari alikuwa ndani ya Kaunda suti. Akamsukasuka mkewe na kumwamsha.
“Aaaa unanikatisha ndoto yangu bwana!” mkewe akasema huku akiamka na kuketi.
“Mi natoka…”
“Unaenda wapi?” akamuuliza mumewe.
“Kazini mara moja!” Chameleon akajibu.
“We na kazi zako, nisakuzowea. Siku hizi hata ndoa hatufaidi, naachwa na kiu tu…” akalalama mwanamke wa Kizigua.
“Usijali mpenzi, ngoja tulitumikie taifa,” akambembeleza.
“Haya nenda kwenye taifa lako unalolipenda ukalitumikie… na taifa hili unaloliacha likivamiwa na waasi usilalamike!” Mkewe akasema. “Aaaaa mama watoto, unafika mbali sasa…”
“Piiiiiiip! Piiiiip!” honi ya gari ikamshtua.
“Haya mammy, tutaonana baadae!”
“Sawa Daddy”.
Wakabusiana, na mzee huyo akaiacha nyumba na kuondoka zake.
* * *
Saa saba usiku, Chameleon alifika Msasani kuliko na makazi ya Rais ambaye wao walimtambua kama ‘namba moja’ kwa kuwa ndioye aliyekuiwa na dhamana ya ulinzi kwa nchi nzima. “Pole!” Rais akamwambia huku akimkaribisa kiti katika ofisi yake ndogo. Ndani ya nyumba hiyo.
“Asante Meshimiwa, nimeitikia wito…” Chameleon akajibu kwa adabu zote.
“Nisichukue muda wako mwingi… kuna taarifa hii hapa ambayo imenifikia jioni ya leo. Sikuifanyia kazi kwanza, kwa sababu nilikuwa naipitia kwa kina,” akamwambia huku akimkabidhi ile karatasi iliyoandikwa pande mbili. Chameleon akaipokea na kuisoma mara kadhaa. Alipomaliza, akaiweka mezani na kumsogezea mkuu wa nchi.
“Kwa hiyo, hata waziri Kibwana Mtokambali anahusika?” Chameleon akauliza.
“Ningekuwa na majibu, nisingekuita. Nataka ufanye uchunguzi… umchunguze waziri
Kibwana na nyendo zake zote. Pia nataka unipe taarifa kamili za hawa maafisa wa jeshi, akiwamo Kepteni Vincent Mwanachia,” Rais akamwambia Chameleon. Naye akajibu kwa kutikisa kichwa juu chini.
“Chameleon, this is confidencial… hakikisha, ndani ya siku mbili, unanipa majibu stahiki,” Rais akasema na kuagana na mwanausalama wake anayemtegemea. Chameleon alitoka ndani ya ile ofisi, akachukua na ile karatasi huku kichwa chake kikiwa kimejaa mawazo ya nini cha kufanya dhidi ya hicho alichoambiwa. Alitazama saa yake, ikamwonesha kuwa ni saa tisa kasoro robo usiku. Akafikiri aende nyumbani kuendelea kuumaliza usiku na mkewe, au aende ofisini kuanza kupana na kupanua juu ya hicho alichoambiwa, akupata jibu. Mawazo yake yakamrudisa kwenye kauli ya mkewe ambayo iliuchoma moja kwa moja moyo wake, ‘…na taifa hili unaloliacha likivamiwa na waasi usilalamike!’
Saa tisa na dakika na dakika tano usiku alikuwa akipita Barabara ya Chole, Masaki akiwa bado ajui sawia ni wapi aelekeako. Katika barabara hii kulikuwa na nyumba kadhaa za vibopa na vigogo wa serikali. Kati ya nyumba hizo, ilikuwamo ya waziri Kibwana Mtokambali. Bwana Chameleone alikuwa na tatizo kubwa moja, akishapewa kazi basi akili yake uwa hailali mpaka kazi ile itimie. Katika barabara ya Chole maeneo ya Oysterbay, Chameleone alikuwa akiendesha moja ya magari yao ya siri katika idara ya Usalama wa Taifa, Volvo. Alipokuwa katika lindi la mawazo, akautuswa na mwanga mkali wa taa za gari lililoingia katika barabara hiyo kutokea ile ya mbele yake. Akapunuza mwendo na kususa ukali wa taa zake, lakini lile ari la mbele yake alikufanya hivyo na kupelekea mwanga ule kumuumiza machoni. Akapunuza mwendo na kueesa kando kidoo akisubiri ari lile lipite. Badala ya kupita, likawasa indiketa ya kulia na kuinia kwenye ujia mfupi ulioishia kwenye lango la nyumba nyumba moja kubwa.
Bahati gani ya mtende kustawi jangwani? Gari lile lilisimama mbele ya nyumba ya mheshimiwa Kibwana Mtokambali. Chameleon akarudisha gari barabarani nakupita pale polepole akiendelea nasafari yake. TB 620, namba za gari zilisomeka namna hiyo. Kwa kamera yake ndogo ya Kirusi aina ya Cimena, akapiga picha lile gari kwa upande wa nyuma likiwa linamalizikia kuingia ndani ya wigo ule. Chameleon, hakuelewa kama gari lile, usiku ule, alikuwa waziri Kibwana mwenyewe akitoka mizunguko au mgeni kaja kumtembelea, hakuna jibu. Akaamua kuegesha gari lake kwenye kona moja mbele yake. Kisha akaamua kurudi kwa miguumpaka usawa wa nyumba ya waziri Kibwana, mwenye dhamana ya ulinzi wa nchi yake.
Ukuta ulioizunguka nyumba hiyo ulikuwa mrefu kiasi, kadiri ya mita tatu hivi na juuye kulikuwa na waya uliozungushwa kwa usatadi mkubwa na kibao kilichosomeka ‘DANGER’ chenye rangi ya njano na maandishi meusi kilining’inia. Akasimama nje ya ukuta huo kwa kuwa mazunumzo ya awali ya maamkiano ya watu hao aliyasikia.
“Hakuna mtu nyuma yako? Maana hii nchi unaijua!” Sauti ya Kibwana ikasikika.
“Aaaa naijua kazi yangu mheshimiwa…”sauti ya pili ikajibu. Chameleone hakuweza kuigundua sauti hiyo kuya ni ya nani. Alichokifanya ni kutega masikio kwa nguvu zote kusikiliza kile kitakachozungumzwa hapo nje.
“Enhe!”Kibwana akaendeleza mazungumzo, ambapo sasa dhahiri shahiri,sauti zao zilikuwa za chini sana.
“Kule kila kitu kipo sawa. Kesho, kijana wetu atafanya maandalizi ya mwisho na wale kuruta wamejiandaa vyema…”
“Mmeshawapa pesa?” Kibwana akauliza kwa kimuhemuhe.
“Tumewapa nusu na nusu nyingine baada ya kazi…”mgeni akajibu.
“Sawa, sasa sikiliza…”
“Enhe!”
“…mpango ubaki vilevile, saa na siku iwe ile ile… Mimi kama nilivyokwambia, kwa kuwa ratiba ya Mzee ninaijua vyema, nitawaambia ni wakati gani mzuri…”Kibwana akasema kwa msisitizo.
“Sawa,we unachotakiwa utuambie masaa sita kabla!” yule mgeni akajibu.
“Sawa, sasa mipango mingine, we pita ofisini kesho kama saa nane hivi!” Ukafuatia ukimya kidogo na baadae milango ya gari ikasikika ikifungwa. Chameleone akajibanza palepale na kulisuudia lile gari likitokomea katika barabara za Masaki.
Hapa kuna jambo kubwa! Akawaza na kujitoa katika ule ukuta. Akaliendea gari lake na kuingia ndani. Mara baada ya kushusha pumzi ndefu, akawasha injini na kuamua kurudi nyumbani kwake kujipanga kwa siku inayofuata.
SIKU ILIYOFUATA
Siku hii haikuanza vizuri kwa wakazi wa jiji la Dar es salaam.mvua kubwa yenye radi kali ilikuwa ikinyesa. Mzee Chameleon akajikuta anashindwa kubanduka kutoka katika kifua cha mkewe. Joto mujarab la mwanamama huyo lilimfanya alale kama motto kitandani hapo.
“Mwenzetu we huendi kazini?” Mkewe akauliza. Chameleone akainua saa yake mezani na kutazama. Loh! Ilikwishatimu saa tatu za asubuhi. Akakurupuka na kuijiweka tayari. Baada ya chai nzito kutoka kwa mkewe, akaingia katika gari lake na kutia injini moto.
Katika taarifa ya siri aliyopatiwa jana yake na Mkuu wa nchi, kulikuwa na orodha ya majina kadhaa ambayo kwayo ilimpasa kuyafatilia. Akiwa na mawazokichwani mwake, alijitahidi kuendesha gari kwa uangalifu. Akaiacha barabara ya Kawe na kukunja kushoto kuifuata ile ya Bagamoyo kuelekea Mwenge. Mita chache mbele, akakunja kushoto na kutazamana na lango kuu la kuingia katika kambi ya jeshi ya Colito, Lugalo.Askari aliyekuwa lindo akalifuata gari hilo na kuuliza maswali mawili matatu, kasha akaliruhusu kuingia. Chini ya mwembe mkubwa, ndani ya kambi hiyo akaegesa gari lake na kuvuta hatua ndogo ndogo kuelekea katika canteen ya maafisa.
Hakukuwa na watu wengi, lakini pia hakupenda kukaa kiti cha peke yake. Hatua zake, zikamfikisha mbele ya meza moja iliyokaliwa na mwaDanada alievalia sare za jeshi. Cheo chake ca Kepteni kilijionesha pasi na kificho kwa nyota tatu zilizojipanga vyema mabegani mwake.
“Hujambo bibie?” akamsabahi na kumtupia tabasamu lenye bashasha. Yule binti aliinua sura yake na kumtazama Chameleone kuanzia juu mpaka chini.
“Salama, karibu!” akajibu, kasha akaendelea kuburudika kwa supu ya kongolo iliyokuwa mbele yake.
“Karibu baba, nikusaidie nini?” ni sauti ya mhudumu iliyomshitua kutoka katika kumtazama afande yule, kepteni wa kike.
“Nipatie kongolo na Pepsi Cola. Itakuwa shin’ ngapi?” akauliza.
“Shilingi kumi na mbili tu,” mhudumu akjibu.
“Pamoja na hii ya Kepteni Zuhura…” akaongeza kusema. Yule afande aliposikia jina lake likitamkwa, akainua uso na kumwangalia huyo alitajaye kwa mara nyingine.
“Shilingi kumi na sita tu,” akajibu.Chameleone akatoa noti ya shilingi kumi kumi, mbili, na kumpatia.
“Hizo shilingi nne ununue bofulo kwa ajili ya watoto,” akamwambia mhudumu, naye akashukuru huku akitokomea jikoni. Mara baada ya kumalizana na yule mhudumu, akarejesha macho yake kwa afande yule.
“Asante kwa ukarimu wako,” Kepteni Zuhura akamwambia Chameleone.
“Karibu. Hivi ndivyo wanaume tunavyopaswa kuwa, nitapenda kutembelea ofisini kwako kabla sijaondoka kambini hapa leo hii…” Chamelleone akamwambia Zuhura.
“Karibu sana, lakini bahati mbaya, mimi sina ofisi…”
“KIvipi?”
“Ofisi yangu ni uwanjani tu,” Zuhura akajibu.
“Unamaanisha nini, wakati cheo chako kinakutaka kuwa ofisini? Wewe si ni ofisa!” Chameleone akazidi kudadisi.
“Ni kweli, ila mimi ni mkufunzi zaidi kuliko kuwa ofisini,” akamjibu.
ITAENDELEA
GENGE
EP3
Unamaanisha nini, wakati cheo chako kinakutaka kuwa ofisini? Wewe si ni ofisa!” Chameleone akazidi kudadisi.
“Ni kweli, ila mimi ni mkufunzi zaidi kuliko kuwa ofisini,” akamjibu.
“Ooh, safi sana! Je naweza kujua ni mkufunzi wa nini? Kama hutojali,” mtu mzima, Cameleone akauliza.
“Mimi ni mkufunzi katika Sanaa ya mapigano ya ana kwa ana. Huwa nakuja kuendesha mafunzo haya kwa vijana walio katika Special Force,” Zuhura akajikuta anabwabwaja bila simile mbele ya Chameleone. Muda huo huo, staftahi yake ikafika, akaagana na mwanamke huyo kasha yeye akaendelea na kuitupia kinywani supu aliyoagiza. Dakika ishirini baadae, akawa tayari nje ya kantini hiyo ya maafisa, akivuta hatua taratibu kuelekea jengo la utawala.
Hatua zake ndefu ndefu zikamfikisha kwenye jengo hilo, ambalo juu ya ukuta kuliandikwa jina Colito. Akasimama kwa sekunde kadhaa kabla ajaingia katika ofisi hiyo ambayo kwayo, mkuu wa kikosi hicho huwapo.
“Shida!” sauti kutoka nyuma yake ikamgutusha.
Chameleon akageuka taratibu ma kumtazama huyo asemaye. Kijana mmoja, mrefu, aliyependeza katika mavazi yake ya kijeshi, mgongoni mwake alikuwa kabeba bunduki kubwa, AK47. Kijana yule alikuwa kasimama imara, hacheki wala hatikisiki. Chameleon akajua wazi kabisa kuwa anasubiri jibu hata kama hajauliza.
“Aaaann nahitaji kumuona, Kepten Baka Baka,” Chameleone akajibu huku akisimama sawa kutazamana na mwanajeshi huyo.
“Bakabaka ndiyo nani?” yule mwanajeshi mwenye cheo cha Koplo akamtwanga swali Chameleon lakini hakujibiwa.
“Ninyi ndiyo tunaowatafuta, yaani tumewapiga kule kwenu Uganda lakini bado mnaendelea kutufuatafuata, sasa leo umejileta.
“Mimi nina shida zangu za ofisini kijana!” Chameleone akajieleza.
“Hakuna, wewe ni jasusi, umetumwa, sasa nakuweka ndani,” yule askari akasema pasi na mzaha. Sura yake tu haikuwa na chembe ya huruma, macho yake mekundu yalieleza wazi hisia zake za ukatili. Akapuliza filimbi iliyokuwa katika mfuko wake wa shati lile la kijeshi kwa mtindo wa pekee. Sekunde chache tu, wanajesi wenine wawili wakawasili.nao walikuwa katika kombati za jeshi, na mabega yao kuja katika viwiko yalivikwa kitambaa cheupe chenye herufi mbili nyekundu, MP yaani Military Police au kwa lugha nyepesi tungesema, polisi wa jeshi. Walipofika pale, yule bwana akawapa ishara tu, hawakuhoji, wakamchukua na kuondoka naye.
Mzee Chameleone akatupwa rumande maalumu ambayo huwekwa wanajeshi watukutu au wenye makosa mbalimbali. Na huwekwa ndani kwa amri ya wakubwa wao kulinana na kosa lenyewe. Lakini yeye aliwekwa humo kwa kutuhumiwa kuwa ni jasusi. Akaingizwa kwenye jengo moja lililojitenga kando kabisa na mengine. Kabla ya kufika katika jengo hilo walipita jirani kabisa na uwanja wa mazoezi na hapo alishuudia mazoezi makali ya Martial Art yakiendelea chini ya Kepteni Zuhura. Alipotazama upande ule, akagongana macho na mwanamke huyo aliyekuwa amesimama akiwatazama vijana wake.
“Songaaaa! Usiangalie wake wa wakubwa, ala!” Mp mmoja akamkaripia na kumsukuma mbele.
“Vua viatu, saa, mkanda, kofia na kama una pesa zote weka hapo kwenye mess tin,”akaamriwa, naye akatii. Alipomaliza kutekeleza hayo akaingizwa kwenye chumba kimoja ambacho ndani yake alikutana na watu wenine wanne. Watu wale wote aliwatambua kuwa ni wanajeshi kutokana na suruali zao za mabakamabaka. Ni yeye tu aliyekuwa amevaa kiraia, suti ya mtindo wa Kaunda.
“Kaa kwanza huko mpaka tutakapokuchukua kwa mahojiano…” MP mmojawapo akamwambia huku akimsukumia ndani na kuupia kufuli mlango huo wa chuma.
“Mzee, umepotea njia?” mmoja wa wale vijana akamuuliza.
“Nilipotea njia, nikajikuta ndani ya kambi, nikakamatwa na kuletwa huku,” akamjibu.
“Pole sana! Wananchi lazima muhesimu kambi na maeneo ya jeshi, na si kukatizakatiza kama mnaenda chooni,” akasema yule mwanajeshi.
“Sasa mbona aliyekuleta amesema usubiri kuhojiwa?” mwingine akadakiza swali.
“Mi sijui taratibu zenu za kijeshi, mi najua jeshi la wananchi, kwa hiyo sikuona shida kupita kuuliza niendako…” Chamelleone akawajibu na wote wakaanua vicheko.
Sekunde chache baadae, ukimya ukatawala kama mwanzo. Mzee Chameleone akiwa amekaa upande mwingine wa chumba kile, alikuwa kimya kabisa, akiwaza na kuwazua. Kwa namna nyingine alionakama amepewa nafasi ya utulivu ya kufikiri juu ya kile anachokifuatilia tofauti na anekuwa ofisini.
“We! Kwa hiyo… mi siwezi kukaa humu, ngoja nikaungane na wengine…” mmoja wa wale vijana wa jeshi akamwambia mwenzake.
“Unasema nini wewe? Mimi siwezi, kamwe, waje hata wakitaka waniue…” yule mwenzake akajibu.
“Wenzetu washakubali, wako nje saa hii…” akasema mwingine kabisa ambaye daima alikuwa kimya.
“Nimeapa kuilinda nchi yangu, na si vinginevyo!” akasema yule wa kwanza. Mara ukasikika mlango wa chuma ukifunguliwa. Yule mwanajeshi aliyesema hawezi kukaa mule ndani, akasimama haraka na kuuendea mlango wa chumba kile, kwa mikono yake miwili akasika zile nondo.
“Afandeee!” akaita.
“Tulia we muasi, wazalendo tupo kazini, kuilinda na kuipigania nchi yetu,” akajibiwa kutoka katika moja ya vyumba vile ambamo labda askari wale au yule aliingia.
Maneno yale yalimvutia sana Chameleone, akatega sikio kusikiliza kwa maana alishajuakuwa watu hao wanaongea kwa mafumbo. Dakika mbili baadae, akasikia michakacho ya miguu ya mwaDanamu anayetembea kwa hatua za haraka haraka kuelekea mlango ule. Wakati huo huo akamwona yule mwanajeshi pale mlangoni akaisogea nyuma kama sentimeta thelathini hivi. Kufuri likafunguliwa.
“Onana na Chatu haraka sana! Dakika kumi zikipita hujamwona, utarudi humu. Hakuna mwingine aliyechoka kukaa humu?” yule aliyefungua akauliza, huku akiwa anachungulia mule ndani. Macho yake yakagongana na ya Chamelleone. Sekunde mbili kama si tatu, akaingia ndani ya kile chumba.
“We raia vipi? Aliyekwambia hii ni selo ya watu kama wewe nani?” yulemwanajeshi akauliza.
“Selo ya raia iko wapi afande?” Chameleone akauliza.
“Atakujibu aliyekuleta!” akasema na kutoka nje huku akibana kufuli lile.
* * *
Baada ya saa sita kupita, Chameleone akatolewa ndani ya kile chumba na kuongozwa mpaka cumba kingine, akawekwa ndani yake na kutakiwa kusubiri hapo. Nusu saa baadae waliinia wanajeshi wawili. Mmoja alivaa kombati iliyopambwa kwa nyota tatu mabeani mwake na mwingine alivaa vilevile isipokuwa yeye alipambwa na v moja na kitambaa cheupe chenye erufi M na P. Yule kepteni akaketi kwenye kiti cha mbao na yule MP akasimama kando kiukakamavu kabisa.
“Wewe ni nani?” yule Kepteni akauliza. Chameleone akamtazama kwa jicho bay asana, hakujibu.
“Unajua hatupo kwenye utani ee, miaka hii nchi yetu imekuwa na maadui wengi sana. Taarifa niliyoipata ni kuwa wewe ni jasusi mmoja wa nchi hizo...”
“Hujakosea, mimi ni jasusi mmoja wa nchi hizo. Sasa siwezi kuzungumza chochote na wewe, namhitaji mkuu wako wa kikosi…” Chameleone akawaambia. Wale wanajeshi wakatazamana na kuanza kucheka.
“Unafikiri mkuu wa kikosi huwa anawasikiliza watu kama ninyi? Wewe tunakupia risasi kwa sababu umeidharau kambi,” yule kepteni akasema.
Ikawa zamu ya Chameleone kucheka, akacheka kwa sauti kubwa, kisha akanyamaza na kuwatazama.
“Nyie, msinifanye mimi mtoto mwenzenu, wewe mwili wako ushaingia risasi ngapi?” yule Kepteni hakujibu. Na Chemelleone akaendelea kusema.
“Kwa taarifa yako, hapa nilipo nina risasi mbili mwilini, hivyo siogopi risasi hizo unazozisema. Ondokeni hapa, mkamwite mwenye cheo cha juu kuliko ninyi wote…” akang’aka Chameleone. Yule kepten akasimama kutoka pale alipoketi na Chameleone akafanya hivyo.
“Mfundishe adabu!” akamwamuru yule MP, naye akamjia mzee yule akiwa tayari na mkanda wa jeshi mkononi, asijue anayemfuata kipumbavu ni nani katika medani ya upianaji. Hatua moja kabla ya kumfikia, yule MP akauzunusha ule mkanda hewani tayari kushambulia. Chameleone aliruka juu kimo cha ng’ombe, pio moja maridadi likamfanya yule kijana azunuke kama pia na kujibamiza ukutani, kisha akaanguka chini kama mzigo. Kepteni akamtazama yule mzee, kisha akamtazama kijana wake pale chini akiwa hana fahamu. Hakuwa na uamuzi mwingine zaidi ya kutoka nje na kuufunga mlango.
Dakika kama tano hivi wakawasili vijana wengine watano waliojazia miili. Wakafunua mlango wa kile chumba wakiwa na uchu wa kutoa kipigo kwa huyo mzee. Awakukuta mtu zaidi ya yule MPakiwa sakafuni. Hawakuamini, wakatafuta mpaka kwenye droo za kabati, hakuna mtu.
Wakambeba yule mwenzao na kumuwahisha hospitalini. Kishapo taarifa zaikafika kwa yule kepteni, hakuamini anachoambiwa. Akasimama kwa gadhabu na kutoka nje, alipofika mlangoni akakutana uso kwa uso na Chameleone aliyekuwa amesimama mkabala na ngazi za kuingilia katika jengo hilo la utawala. Palepale alipokamatiwa mwanzo. Yule kepteni akapatwa na mshtuko, hakujua nini afanye, arudi ofisini au aende kumkabili mzee huyo? Utata.
“Hivi, we mzee ni mzimu?” akamuuliza.
“Njoo unishike, uone kama mzimu una mifupa!” Chamelleone akajibu na kuanza kupanda ngazi.
“Unaenda wapi?” akaulizwa na yule kepteni.
“Ofisini kwako, tena uje bila kuchelewa!” Chameleone akamjibu na kumpita pale aliposimama, akaongoza na kuingia kwenye mlango wa tatu. Yule kepteni kwa woga akarudi ofisini kwake na kumkuta mtu mzima yule amekwishaketi kitini.
“Keti kijana! Kepteni Mwanachia…” akamwambia, na yule kepteni akaketi huku kicwani mwake kukiwa na mawazo lukuki.
Ni nani mtu huyu? Alibaki kujiuliza.
“Kepteni! Kumbuka kuwa hiki ni chombo cha wananchi, yakupasa kukitii kiapo chako, na si vinginevyo. Mbinu zozote chafuchafu kwa maslahi yako na ya wenzako, zitawagharimu maisha,” Chameleone akasimama na Kepteni Mwanachia naye akafanya vivyo hivyo.
“Wewe ni nani?” Mwanachia akauliza.
“Mzimu! Na usiku huu nitakutokea nyumbani kwako,” Chamelleone akamjibu na kutoka nje. Moja kwa moja akaliendea gari lake na kuondoka eneo lile.
* * *
Dakika thelathini baadae, Chameleone aliegesha gari lake nje ya ofisi yake ya siri, maeneo ya Hospitali ya Ocean Road, jirani kabisa naupande wa nyuma wa Ikulu ya Tanzania. Akaingia ndani na kuketi kitini, akiitazama meza yake iliyokuwa pweke muda wote. Kwanza akatua mezani hapo kabrasha alilotoka nalo garini, kisha akaingiza mkono mfukonina kutoa karatasi ndogo, ya rangi nyeupe iliyofifia, akaiweka kando ya kabrasha lile. Akainuka na kuuendea mtungi wa udongo uliokuwa kwenye kona ya chumba hicho. Ndaniye, akachukua Pepsi Cola moja kati ya sita zilizowekwa majini mtungini humo. Akafungua kwakutumia meno, na kurudi tena kitini.
Kilikuwa ni kibanda tu kikuukuu kilichotelekezwa pembeni kabisa mwa hospitali hiyo maarufu sana. Kama ungejaaliwa kukiona kwa nje basi ungesema ni ‘choo kibovu’. Hakikuwa na paa upande mmoja. Mbao zilizooza, ndizo zilionekana wazi waziwe. Upande mwingine kulikuwa na paa la vigae vikuukuu. Nje, pembezoni kidogo, palikuwa na mti mkubwa wa zambarau. Katika kibanda hicho, ndipo mzee huyu, mwanausalama mwaminifu wa serikali, alikuwa akifanyia mambo yake tofauti na ofisi yake ya kawaida ambayo huwa na wenzi wake wengi.
Akakisoma kile kikaratasi vizuri.
Bayankata itakuwa DDC Kariakoo
Usiku wa leo saa 4:00 usikose.
Mpenzio.
ITAENDELEA