Riwaya: Genge

GENGE
EP42

Zile boti zikatawanyika, mbili upande huu na ile nyingine upande mwingine. Boti ya kina Chiba ikageuka na kurudi pale ilipolipuka ile ya jeshi ili kusaidia kama kuna majeruhi yeyote. Wakati Scoba akifanya hivyo. Gina alichumpa ndani ya maji na kuanza kuogelea kuelekea kwenye lile jumba halikuwa mbali sana na wala hakuna aliyemjali.
* * *
Kutoka katika chumba cha chini kabisa, ndani ya jengo lile, Msambamagoya au Big J alimhifadhi Mtokambali kwa ajili ya usalama.
“Ukiona, dakika sitini sijarudi, unaweza kutoroka kwa kupitia njia hii, utatokea kwa Jovanina utajihifadhi hapo kwa muda,” akamwambia rais wake. McTee pamoja na kuwa aikuwa mwanajeshi zamani, alijikuta akitetemeka.
“Tumeshindwa kwa mara nyingine?” akamuuliza Big J.
“Hatuwezi kushindwa, we fanya nilivyokwambia. Ukifanikiwa kutoroka, kajifiche Mauritius na mimi nitaungana nawe huko,” Big J akatoka na kupanda ngazi kulekea juu. Alipojitokeza tu, akakuta hali mbaya, vijana wake aliokuwa akikaa nao kwa ajili ya usalama wote walikuwa sakafuni, damu ilitapakaa huku na kule. Akatazama eneo lile akasikitika. Alitamani awaite wote walio mafichoni waje, mapambano yaanzie hapo, lakini hakuna simu iliyokuwa inatoka. Big J akahisi kuchanganyikiwa, akaiendea ngazi inayopanda juu, akaanza kuikwe, alipokunja kona tu akakutana uso kwa uso na Amata.
Kitendo bila kuchelewa, Kamanda alimsukuma kwa nguvu yule jamaa aliyekuwa akimwongoza kwenda chini. Akampamia Big J. kabla hajafanya lolote akajikuta akipigwa guu la uso. Big J akaanguka chini mzima mzima. Akaivuta bunduki yake kubwa aliyokuwa kaipachika mgongoni. Amata akaruka upande wa pili na risasi zikatawanya kioo kikubwa cha dirisha. Big J akainuka haraka kumkabili mbaya wake. Bandeji yake bado ilikuwa begani na kidonda kilianza upya kutoa damu. Kamanda Amata naye akainuka haraka kujiweka sawa. Akainua chupa ya ua iliyokuwa kwenye kiukuta kidogo na kumrushia mbabe huyo. Hakuangaika kuikwepa, kwa kutumia bunduki ileile akaifumua ikiwa hewani, kisha akamlenga Amata tayari kummaliza.
“Huna ujanjaaaa!” akapiga kelele. Lakini ghafla, Amata akapigwa kikumbo kitakatifu na kuangukia upande mwingine huku risasi zikimiminika pale alipotoka. Gina akajiviringa chini na kumrushia Amata bastola iliyoshiba risasi. Hakufanya kosa, aliwahi kuinuka kiufundi kabisa lakini kabla hajafyatua, alijikuta kapata pigo moja zito lililoitoa bastola ile mkononi.
“Hukumu yako ni kifo,” Amata akamwambia.
“Ha ha haaaaaa hamna kitu, kifo utakishuhudia wewe,” Big J akatamba na kumwendea
Amata kwa kasi. TSA 1 naye akavuta hatua mbili ya tatu, akamkanyaga gotini na kujirusha tiki taka, goti la mguu wa pili likamtandika Big J kidevuni. Amata akatua sakafuni salama salimini kwa miguu miwili. Big J, pande la baba, liakaguna kwa maumivu. Likatema meno mawili.
“Na utaenda motoni kibogoyo…” Amata akamwambia. Gina aliinuka pale alipo, akajiweka sawa na kuingialia mtanange huo.
“Gina kaa pembeni, hii mechi nzito…” Amata akamwambia.
“Hakuna kitu kama hicho, huyu boya tu,” Gina akamtukana, akamsogelea Big J na kumvurumishia mapigo kadhaa ya karate lakini hakuna hata moja lililompata. Akabadilisha mtindo na kujiweka sawa kwa kung-fu, akapiga kata za kutosha za aina zote lakini bado hakuweza kumpata huyo jamaa hata kwa pigo moja. Mzunguko wa mwisho, alidakwa mkono. Big J akauzungusha na kusababisha hitilafu kwenye mifupa. Gina alipiga yowe la uchungu lililomfanya Amata kuhamaki. Akaiwahi bastola iliyokuwa chini lakini kabla hajafika akasikia kishindo kikubwa, akageuka na kushuhudia Gina akibamizika mlangoni na kuanguka hapo ndani. Amata alipokea konde zito, akayumba na kabla hajasimama akapata mateke kadhaa ya haraka haraka, akajaribu kuyakwepa na kujikuta keshafika ukutani. Akajaribu bahati yake, akajiangusha chini makusudi, akajiviringa na kuchukua kipande cha chupa kilichokua hapo chini. Akainuka, pigo lililofuata akalikinga kwa mkono ule wenye chupa, ikadidimia kwenye nyama ya mkono wa Big J. akavuta na kuchana sehemu kubwa ya nyama.
“Aaaaaaaaahhhhh!”
Amata akatumia nafasi hiyo akaruka na kumtadika kifuti cha paji la uso, Msambamagoya akahisi kuchanganyikiwa. Hajakaa zawa alichezea Makonde mazito ya chembe, akakohoa damu. Amata aligeuka mbogo, akaruka hewani na kumtandikaa mateke mawili maridadi kabisa, mwanaume akaenda chini kama mzigo.
“Ulihukumiwa kunyongwa, sasa natimiza hukumu hiyo…” akamwambia.
James hakukubali kufa kijinga, akainuka na kumuwahi Amata, akakosea padogo sana. TSA 1 kwa mikono yenye nguvu akaepa pigo la kifo la Big J, akafanya kama anampita hivi akaudaka ukosi wa shati la jamaa huyo akavuta kwa nguvu akakidaka kichwa, akamvuta chini wakaenda wote Amata akiwa katangulia. Alipofika chini akamgeua na kuikunja shingo yake vibaya. Mifupa ya shingo ya Big J ikaitika. Macho yakamtoka, miguu ikatapatapa, akakaata roho.
Amata hakuamini, akainuaka haraka na kumkimbilia Gina, akamuinua kutoka pale kwenye vipande vya mlango.
“Amekufa?” Gina akauliza.
“Tayari,”
“Nimeumia Amata,” akalalamika huku kajishika eneo la mbavu.
“Msiniue Tafadhali,” sauti ya kike ikasikika kutoka upande wa nyuma. Amata akagaeuka, na kugongana macho na mwanamke mweupe, mwarabu au chotara. Akamtazama kwa sekunde kadhaa. Hassna.
Akamshika mikono na kumkalisha chini, “Gina mlinde,” akatoa amri. Kisha akatoka pale na kushuka ngazi moja, Cabin 4, akavunja mlango na kumkuta Egra kajikunyata kwenye kona ya chumba akiwa kaukumbatia msalaba wa marehemu mumewe.
“Wakati wa kuondoka Egra,” akamwambia na kumshika mkono. Egra hakutaka kuuacha msalaba ule. Amata akaubeba na kuondoka nae mpaka alipo Gina, “mchukue huyo tuondoke,” akamwambia, nao wakatafuta njia ya kutoka nje.
Huko nje tayari wanajesshi walikuwa wameteremka kutoka kwenye boti na kulivamia lile jumba. Watalii ndani ya hoteli walitolewa nje wote na kuwekwa sehemu nyingine kabisa. Kizaazaa. Amata akiwa na Gina, Hassna na Egra walifanikiwa kutoka nje, wakapokelewa na vijana wa JW wenye silaha nzito.
“Kamanda Amata!” Amata akasikia akiitwa na mmoja wa wale vijana, akasimama na kumtazama. Hakumjua kutokana na jinsi alivyojiziba uso. Akajitoa ile barakoa.
“Joseph Rutashobya!” akamtambua. Joru akapiga saluti ya kukubali kwa mara nyingine kazi ya agent huyo wa siri wa serikali.
“Kazi nzuri Joru, hakikisha mmesafisha kila kitu huko ndani, ilakuna siri moja nakupa uifanyie kazi,”
“Yes Kamanda!”
“Katika kijiji cha Bweni kaskazini kabisa ya kisiwa hiki, kuna wanajeshi wetu waasi wamejificha walikuwa wakisubiri hizo silaha kuja kufanya mapinduzi… naomba muashughulikie kwa sharia zenu,”
“Umesomeka!”
“C4, C4,” Joru akaita kwenye redio yake.
“C4 anakusoma,”
“Uelekeo, upande wa kaskazini, kuna mifugo ipo malishoni, tukaichukue kwa njia yoyote tunayoweza,”
“Copy Sir!”
Chopa namba nne likateremka chini na vijana kama kumi walio kamili wakalikwea na kuondoka eneo lile.
Boti ya Scoba ilifika ukingoni kabisa mwa lile jumba, Egra, Hassna wakapakiwa. Gina na Amata wakafuatia. Chiba akateremsha kifaa chake na kukizima bila kurudisha mtandao eneo lile. Wakajifungia ndani. Amata akainua simu ya upepo wanayotumia mara nyingi kama ofisi.
“HOT, HOT,” akaita.
“TSA 1, nakupata,”
“Mission Clear, James Msambamagoya ametekelezewa hukumu yake. Mtokambali amefanikiwa kutoroka tena… tupo salama, tunarejea, ova” akampa taarifa fupi..
“Umesomeka… tukutane shamba operesheni nyingine TNS wameshaingia kazini, over and Out!”


MWISHO

Safi sana..Story Nzuri..

Chapter Closed...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom