Ripoti za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Mwaka wa Fedha 2019/2020

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,797
11,959
Salaam Wakuu,

Hapa chini ni Muhtasari wa ripoti za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Mwaka wa Fedha 2019/2020

===
Mhe. Naghenjwa Kaboyoka (Mb), Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya PAC; Mhe. Grace Tendega (Mb), Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya LAAC; Mhe. Daniel Sillo (Mb), Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Bajeti; Mhe. Japhet Hasunga (Mb), Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya PAC; Mhe. Suleman Zedy (Mb), Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya LAAC; Mhe. Omary Kigua (Mb), Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Bajeti; Ndugu Wanahabari; Watumishi Wenzangu wa Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi;

NAWASALIMU KWA JINA LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA.

1.0 UTANGULIZI

Ndugu Wanahabari,​

Awali ya yote napenda kutanguliza shukurani kwa Mwenyezi Mungu aliyetupa uzima na afya njema kuweza kuiona siku hii ya leo. Pia, ninawashukuru kwa kuitikia wito wa kuja kusikiliza muhtasari wa masuala yaliyojitokeza kwenye kaguzi zangu za Mwaka wa Fedha 2019/20.

Ndugu Wanahabari,​

Mnamo tarehe 28 Machi 2021 nilitimiza jukumu langu la kikatiba kwa mujibu wa Ibara ya 143 (4) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977 (iliyorekebishwa mwaka 2005), inayonitaka kuwasilisha ripoti za ukaguzi za kila mwaka kwa Mhe. Rais kabla au ifikapo tarehe 31 Machi kila mwaka.

Ndugu Wanahabari,​

Kwa mujibu sheria ya ukaguzi, ripoti hizi zinakuwa tayari kwa matumizi ya umma zinapowasilishwa bungeni ambapo tukio hilo limefanyika leo kwa Mawaziri husika kuwasilisha ripoti hizi ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hivyo, natumia fursa hii kuujulisha umma kwa ufupi mambo mbalimbali yaliyojitokeza kwenye ukaguzi nilioufanya kwa Mwaka wa Fedha 2019/20.

Ndugu Wanahabari,​

Kabla ya kuwajulisha muhtasari wa mambo muhimu yaliyojitokeza kwenye ukaguzi nilioufanya kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 naomba niongelee kwa kifupi Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi na mchakato wa ukaguzi wenyewe kwa manufaa yenu na manufaa ya wananchi kwa ujumla.

Ndugu Wanahabari,​

Ofisi ya Taifa ya ukaguzi ni miongoni wa ofisi katika nchi hii ambazo zina mifumo madhubuti ya utendaji kazi. Ofisi hii inafanya kazi kwa kuzingatia misingi ambayo imekuwa ikijengwa tangia kuanzishwa kwa ofisi ya CAG Mnamo tarehe 1 Julai 1961 hadi sasa. Misingi na Mifumo hii inafanya kazi kwa usahihi kabisa, hivyo si rahisi mtu yeyote awe CAG ama msaidizi wake kuivuruga misingi hii. Ukaguzi ni mchakato unaohusisha watu wengi sana hadi kuona ripoti zinatoka na hakuna mtu mmoja anayeweza kufanya maamuzi kuhusu nini kiandikwe kwenye ripoti; kazi hii hufanywa na watu wengi sana kwenye mnyororo wa ukaguzi.

Ndugu Wanahabari,​

Ofisi hii ni mwanachama wa Shirikisho la Taasisi Kuu za Ukaguzi Duniani yaani INTOSAI. Pia ofisi hii ni mwanachama wa umoja wa Taasisi Kuu za Ukaguzi kwa Afrika kwa Nchi zinazozungumza Kiingereza yaani AFROSAI E. Hizi Taasisi zote hufanya ufuatiliaji wa jinsi ofisi hii inavyofanya kazi kwa kuzingatia viwango vya Kimataifa na miongozo tuliojiwekea.

Ndugu Wanahabari,​

Kwa misingi, umakini pamoja na miongozo, imeifanya ofisi hii kuwa Mkaguzi wa Umoja wa Mataifa kwa miaka 6 na sasa ni Mkaguzi wa Nje wa Kamisheni ya Usafiri wa Anga Afrika (AFCAC) kuanzia Mwaka huu hadi Mwaka 2022/23. Pia imekuwa miongoni mwa Wakaguzi wa Nje wa Kamisheni ya Afrika (Umoja wa Afrika – AU) kuanzia mwaka huu. Pia ni Mkaguzi wa EAC na SADC; na kazi hizi zinafanyika kwa umahiri na weledi mkubwa.

Hivyo hii ni ofisi inayozingatia weledi, miongozo, kanuni za ukaguzi pamoja na viwango vya kimataifa vya ukaguzi katika kuikagua Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Mujibu wa Katiba na Sheria pamoja na ukaguzi wa Taasisi za Kimataifa ambazo tunapata fursa ya kuzikagua.

Ndugu Wanahabari,​

Mchakato wa kukagua Taasisi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania huanza mnamo mwezi Mei ya kila mwaka kwa mujibu wa kalenda yetu ya ukaguzi. Inapofika mwezi Januari mwaka unaofuata huwa tunakamilisha zoezi la ukaguzi kwenye field na kuanza kuandaa ripoti za ukaguzi. Kwa maana hiyo taarifa hii ambayo leo nawapa muhtasari wake, ukaguzi wake ulianza mnamo mwezi Mei 2020 na kazi za field zilimalizika mwezi Januari 2021 na kuanza kuandaa ripoti hizi. Mapema mwezi wa Machi ripoti hizi zilienda kwa mchapishaji kwa ajili ya kuchapishwa na kuwa tayari ambapo tarehe 28 Machi 2021 niliziwasilisha kwa Mh Rais.

Ndugu Wanahabari,​

Mtakumbuka kwamba niliteuliwa kuingia ofisi hii mnamo Mwezi Novemba 2019, hivyo hii ni taarifa yangu ya kwanza ambayo nimeisimamia kuanzia planning hadi kumalizika kwa ripoti na kuwasilishwa kwa Mh Rais na kisha leo kuwasilishwa Bungeni.


2.0 RIPOTI ZILIZOWASILISHWA

Ndugu Wanahabari,​

Baada ya utangulizi huo, sasa niingie kwenye taarifa yenyewe.

Ripoti zilizowasilishwa leo bungeni ni 21 zinazojumuisha masuala mbalimbali yaliyojitokeza katika Ukaguzi nilioufanya kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni 2020 kwa Taasisi nilizozikagua ambazo ni kama ifuatavyo:
  1. Ripoti ya Ukaguzi ya Serikali Kuu;
  2. Ripoti ya Ukaguzi ya Mamlaka za Serikali za Mitaa;
  3. Ripoti ya Ukaguzi ya Mashirika ya Umma;
  4. Ripoti ya Ukaguzi ya Miradi ya Maendeleo;
  5. Ripoti ya Ukaguzi wa Ufanisi;
  6. Ripoti ya Ukaguzi wa Mifumo ya TEHAMA;
  7. Ripoti ya ufuatiliaji wa mapendekezo yaliyotolewa katika ripoti za Ukaguzi wa ufanisi kwa miaka iliyopita; na
  8. Ripoti 14 za ukaguzi ufanisi zinazohusu sekta mbalimbali.

Ndugu Wanahabari,​

Ripoti 14 za Ukaguzi wa Ufanisi (Performance Audit) katika maeneo mbalimbali ni kama ifuatavyo:

  1. Ukaguzi wa Ufanisi juu ya Usimamizi wa Usafi wa Masoko ya Vyakula;
  2. Ukaguzi wa Ufanisi juu ya Usimamizi wa udhibiti wa Mafuriko;
  3. Ukaguzi wa Ufanisi juu ya Uandikishaji na Utoaji wa Vitambulisho vya Taifa;
  4. Ukaguzi wa Ufanisi juu ya Matengenezo ya Magari na Mitambo ya Serikali;
  5. Ukaguzi wa Ufanisi juu ya Usimamizi wa Ununuzi wa Pamoja wa
  6. Magari ya Serikali na Usambazaji wa Mafuta; vi. Ukaguzi wa Ufanisi juu ya Usimamizi wa Mifumo ya Kudhibiti Ubora wa Vyakula Vinavyosindikwa Nchini;
  7. Ukaguzi wa Ufanisi juu ya Usimamizi wa Ujenzi wa Majengo ya Vituo vya Huduma za Afya Nchini;
  8. Ukaguzi wa Ufanisi juu ya Usimamizi wa Mali zilizotelekezwa;
  9. Ukaguzi wa Ufanisi juu ya Utekelezaji wa Udhibiti wa Uhamishaji wa Bei ya Mauziano ya Bidhaa au Huduma Baina ya Makampuni yenye Mahusiano;
  10. Ukaguzi wa Ufanisi juu ya Ufuatiliaji na Usimamizi Wa Miradi ya Ujenzi Kwenye Sekta ya Elimu Inayotekelezwa kwa Njia ya ‘Force Account’;
  11. Ukaguzi wa Ufanisi juu ya Udhibiti wa Uchafuzi Unaotokana na Taka za Plastiki kwenye Bahari na Maziwa;
  12. Ukaguzi wa Ufanisi Kuhusu Utekelezaji wa Mradi wa Awamu ya Pili ya Ujenzi wa Miundombinu ya Mabasi Yaendayo Haraka Dar es Salaam;
  13. Ukaguzi wa Ufanisi juu ya Usimamizi wa Misamaha ya Kodi ya kwenye Miradi Ya Uwekezaji; na
  14. Ukaguzi wa Ufanisi juu ya Utekelezaji wa Mradi wa Uzalishaji Sukari wa Mbigiri.

3.0 MWENENDO WA HATI ZA UKAGUZI

Ndugu Wanahabari,​

Aina ya Ripoti
Jumla ya Hati
Hati zinazoridhisha
Hati zenye shaka
Hati mbaya
Kushindwa kutoa maoni
Mamlaka ya
Serikali za Mitaa
185​
124​
53​
8​
0​
Mashirika ya Umma
165​
162​
3​
0​
0​
Serikali Kuu
243​
235​
6​
2​
0​
Vyama vya siasa
17​
4​
4​
0​
9​
Miradi ya
Maendeleo
290​
275​
15​
0​
0​
Jumla
900
800
81
10
9
Asilimia
100
89
9
1
1

Kwa Mwaka wa Fedha 2019/20 nimetoa jumla ya Hati 900 za Ukaguzi; ikiwa ni hati 243 za Serikali Kuu, 185 Mamlaka za Serikali za Mitaa, 165 Mashirika ya Umma, 290 Miradi ya Maendeleo na 17 Vyama vya siasa. Kati ya hizo, Hati zinazoridhisha ni 800 (sawa na asilimia 89); Hati zenye shaka ni 81 (sawa na asilimia 9); Hati mbaya ni 10 (sawa na asilimia moja); na nilitoa hati tisa za kushindwa kutoa maoni (sawa na asilimia moja). Jedwali hapa chini linaonesha mchanganuo wa hati hizo.

MCHANGANUO WA HATI ZA UKAGUZI WA HESABU KWA MWAKA 2019/20

Ndugu Wanahabari,​

Katika mwaka wa fedha 2019/20 nilishindwa kukagua Balozi/Misheni 43 kutokana na kushindwa kusafiri kwa sababu ya ugonjwa wa Covid-19. Aidha, sikukamilisha ukaguzi wa mashirika ya umma 11 kwa sababu hayakuwasilisha taarifa za hesabu wakati wa ukaguzi. Mashirika ambayo sikuweza kuyatolea maoni ya ukaguzi ni haya yafuatayo:

NaShirika
1​
Hospitali ya Taifa ya Muhimbili
2​
Kampuni ya Mbolea Tanzania
3​
Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya
4​
Mfuko wa UTT AMIS/PID
5​
Kampuni ya Magazeti ya Serikali
6​
Shirika la Posta Tanzania
7​
Shirika la Reli la Tanzania
8​
Kampuni ya Simu Tanzania
9​
Shirika la Umeme Tanzania
10​
Soko la Bidhaa Tanzania
11​
Taasisi ya Mifupa Muhimbili

Nitoe wito kwa Menejimenti, Bodi za Wakurugenzi na Maafsa Masuuli wa Taasisi hizo hapo juu kuhakikisha wanatimiza matakwa ya Kikatiba na Kisheria kwa kuhakikisha kwamba wanawasilisha hesabu kila mwaka kwa ajili ya kutolewa maoni ya kikaguzi. Pia wale ambao hutakiwa kufanya marekebisho ya hesabu ili kuhakikisha wanazingatia viwango vya kimataifa vya kutengeneza hesabu, warekebishe kisha wazilete ndani ya muda ili niweze kutoa hati na kutimiza matakwa ya Ibara 143(2)(c) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 (kama ilivyorekebishwa mwaka 2005) badala ya kutoziwalisha kwa kuona kwamba watapata hati wasiyoipenda.

Ndugu Wanhaabari,​


Kwa Mwaka huu nimetoa Hati Mbaya kwa taasisi zifuatazo:
  1. Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga
  2. Halmashauri ya Wilaya ya Singida
  3. Halmashauri ya Wilaya ya Itigi
  4. Halmashauri ya Wilaya ya Igunga
  5. Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge
  6. Halmashauri ya Wilaya ya Urambo
  7. Halmashauri ya Wilaya ya Momba
  8. Halmashauri ya Manispaa ya Tabora
  9. Tume ya UNESCO.
  10. Hospitali ya Rufaa ya Mkoa, Morogoro.

Ndugu Wanahabari,​

Hati zenye shaka zimetolewa kwa taasisi zifuatazo:

MCHANGANUO WA TAASISI ZILIZOPATA HATI ZENYE SHAKA

NA.
JINA LA TAASISI
KUNDI
1.Wakala wa Usimamizi wa Maendeleo ya Elimu (ADEM)Serikali Kuu
2.Wakala wa Huduma za Manunuzi Serikalini (GPSA)Serikali Kuu
3.Wakala wa Taifa wa Utafiti wa Nyumba Bora na Vifaa vya Ujenzi (NHBRA)Serikali Kuu
4.Hospitali ya Rufaa ya Mkoa, ShinyangaSerikali Kuu
5.Hospitali ya Rufaa ya Mkoa, Sumbawanga RukwaSerikali Kuu
6.Hospitali ya Rufaa ya Mkoa, TemekeSerikali Kuu
7.Chuo Kikuu cha Dar Es SalaamMashirikay ya Umma
8.Chuo cha Diplomasia (CFR)Mashirika ya Umma
9.Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA)Mashirika ya Umma
10.Halmashauri ya Wilaya ya BuhigweMamlaka za Serikali Za Mitaa
11.Halmashauri ya Wilaya ya ButiamaMamlaka za Serikali Za Mitaa
12.Halmashauri ya Wilaya ya SongeaMamlaka za Serikali Za Mitaa
13.Halmashauri ya Manispa ya Kigoma/UjijiMamlaka za Serikali Za Mitaa
14.Halmashauri ya Wilaya ya UkereweMamlaka za Serikali Za Mitaa
15.Halmashauri ya Wilaya ya BuchosaMamlaka za Serikali Za Mitaa
16.Halmashauri ya Wilaya ya KorogweMamlaka za Serikali Za Mitaa
17.Halmashauri ya Wilaya ya MbogweMamlaka za Serikali Za Mitaa
18.Halmashauri ya Wilaya ya SihaMamlaka za Serikali Za Mitaa
19.Halmashauri ya Jiji la ArushaMamlaka za Serikali Za Mitaa
20.Halmashauri ya Wilaya ya BahiMamlaka za Serikali Za Mitaa
21.Halmashauri ya Wilaya ya BariadiMamlaka za Serikali Za Mitaa
22.Halmashauri ya Wilaya ya BiharamuloMamlaka za Serikali Za Mitaa
23.Halmashauri ya Wilaya ya BukombeMamlaka za Serikali Za Mitaa

24.Halmashauri ya Wilaya ya BundaMamlaka za Serikali Za Mitaa
25.Halmashauri ya Wilaya ya ChamwinoMamlaka za Serikali Za Mitaa
26.Halmashauri ya Wilaya ya ChembaMamlaka za Serikali Za Mitaa
27.Halmashauri ya Wilaya ya ChunyaMamlaka za Serikali Za Mitaa
28.Halmashauri ya Jiji la Dar es SalaamMamlaka za Serikali Za Mitaa
29.Halmashauri ya Wilaya ya GeitaMamlaka za Serikali Za Mitaa
30.Halmashauri ya Wilaya ya HanangMamlaka za Serikali Za Mitaa
31.Halmashauri ya Wilaya ya IrambaMamlaka za Serikali Za Mitaa
32.Halmashauri ya Wilaya ya IringaMamlaka za Serikali Za Mitaa
33.Halmashauri ya Manispaa ya IringaMamlaka za Serikali Za Mitaa
34.Halmashauri ya Wilaya ya KakonkoMamlaka za Serikali Za Mitaa
35.Halmashauri ya Wilaya ya KaragweMamlaka za Serikali Za Mitaa
36.Halmashauri ya Wilaya ya KasuluMamlaka za Serikali Za Mitaa
37.Halmashauri ya Mji wa KasuluMamlaka za Serikali Za Mitaa
38.Halmashauri ya Wilaya ya KilindiMamlaka za Serikali Za Mitaa
39.Halmashauri ya Wilaya ya KiloloMamlaka za Serikali Za Mitaa
40.Halmashauri ya Manispaa ya KinondoniMamlaka za Serikali Za Mitaa
41.Halmashauri ya Wilaya ya KishapuMamlaka za Serikali Za Mitaa
42.Halmashauri ya Wilaya ya KondoaMamlaka za Serikali Za Mitaa
43.Halmashauri ya Mji wa KondoaMamlaka za Serikali Za Mitaa
44.Halmashauri ya Wilaya ya KongwaMamlaka za Serikali Za Mitaa
45.Halmashauri ya Mji wa KorogweMamlaka za Serikali Za Mitaa
46.Halmashauri ya Wilaya ya KwimbaMamlaka za Serikali Za Mitaa
47.Halmashauri ya Wilaya ya LiwaleMamlaka za Serikali Za Mitaa
48.Halmashauri ya Wilaya ya MkingaMamlaka za Serikali Za Mitaa
49.Halmashauri ya Wilaya ya MpwapwaMamlaka za Serikali Za Mitaa
50.Halmashauri ya Wilaya ya MsalalaMamlaka za Serikali Za Mitaa
51.Halmashauri ya Wilaya ya NamtumboMamlaka za Serikali Za Mitaa

52.Halmashauri ya Wilaya ya NgorongoroMamlaka za Serikali Za Mitaa
53.Halmashauri ya Wilaya ya NyasaMamlaka za Serikali Za Mitaa
54.Halmashauri ya Wilaya ya NzegaMamlaka za Serikali Za Mitaa
55.Halmashauri ya Mji wa NzegaMamlaka za Serikali Za Mitaa
56.Halmashauri ya Wilaya ya RoryaMamlaka za Serikali Za Mitaa
57.Halmashauri ya Wilaya ya SengeremaMamlaka za Serikali Za Mitaa
58.Halmashauri ya Manispaa ya SingidaMamlaka za Serikali Za Mitaa
59.Halmashauri ya Manispaa ya TemekeMamlaka za Serikali Za Mitaa
60.Halmashauri ya Wilaya ya TunduruMamlaka za Serikali Za Mitaa
61.Halmashauri ya Wilaya ya UshetuMamlaka za Serikali Za Mitaa
62.Halmashauri ya Wilaya ya UvinzaMamlaka za Serikali Za Mitaa
63.Mfuko wa Afya-Halmashauri ya MonduliMiradi ya Maendeleo
64.Mfuko wa Afya-Halmashauri ya Mji wa MafingaMiradi ya Maendeleo
65.Miradi ya Maendeleo
66.Mfuko wa Afya-Halmashauri ya Wilaya ya KaragweMiradi ya Maendeleo
67.Mfuko wa Afya-Halmashauri ya Wilaya ya ItigiMiradi ya Maendeleo
68.Mfuko wa Afya-Halmashauri ya Wilaya ya UramboMiradi ya Maendeleo
69.Mfuko wa Afya-Halmashauri ya Wilaya ya NzegaMiradi ya Maendeleo
70.Mfuko wa Afya-Halmashauri ya Wilaya ya BundaMiradi ya Maendeleo
71.Mfuko wa Afya-Halmashauri ya Wilaya ya ButiamaMiradi ya Maendeleo
72.Mfuko wa Afya-Halmashauri ya Wilaya ya UshetuMiradi ya Maendeleo
73.Mfuko wa Afya-Halmashauri ya Wilaya ya MaguMiradi ya Maendeleo
74.Mfuko wa Afya-Halmashauri ya Wilaya ya ShinyangaMiradi ya Maendeleo
75.Mfuko wa Afya-Halmahsuri ya Wilaya ya KakonkoMiradi ya Maendeleo
76.Mfuko wa Afya-Halmashauri ya Wilaya ya LongidoMiradi ya Maendeleo
77.Mfuko wa Afya-Halmashauri ya Wilaya ya MusomaMiradi ya Maendeleo
78.United Democratic Party (UDP)Chama Cha Siasa
79.Chama Cha Kijamii (CCK)Chama Cha Siasa
80.Civic United Front (CUF)Chama Cha Siasa
81.National League for Democracy (NLD)Chama Cha Siasa


4.0 TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MAPENDEKEZO YALIYOTOLEWA MIAKA ILIYOPITA

Ndugu Wanahabari,​

Katika ripoti za Ukaguzi wa Hesabu za Serikali kwa miaka iliyopita, nilitoa mapendekezo mbalimbali yanayolenga kuimarisha usimamizi wa rasilimali za umma pamoja na kuboresha ukusanyaji wa mapato.

Katika ukaguzi wangu wa mwaka huu, nilifanya tathmini ya utekelezaji wa mapendekezo yaliyotolewa miaka iliyopita; kati ya mapendekezo 8,740 yaliyotolewa miaka iliyopita, mapendekezo 2,610 sawa na asilimia 30 yametekelezwa kikamilifu. Mapendekezo 2,662 sawa na asilimia 30 utekelezaji wake unaendelea. Aidha, mapendekezo 2,292 sawa na asilimia 26 utekelezaji wake haujaanza; mapendekezo 751 sawa na asilimia 9 yamerudiwa; na mapendekezo 426 sawa na asilimia 5 yamepitwa na wakati. Jedwali hapa chini linafafanua mchanganuo wa utekelezaji wa mapendekezo ya ukaguzi.

TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MAPENDEKEZO YA UKAGUZI​

Aina ya Ripoti
Jumla Kuu
Yaliyo tekelezwa
Kikamilifu
Utekelezaji unaendelea
Yasiyo tekelezwa
Mapendekezo yaliyorudiwa
Yaliyopitwa na wakati
Mamlaka ya
Serikali za Mitaa
15​
6​
0​
5​
4​
0​
Mashirika ya Umma
116​
25​
36​
52​
0​
3​
Serikali Kuu
5,483​
1,508​
2,003​
1,211​
502​
259​
Miradi ya
Maendeleo
3,126​
1,071​
623​
1,024​
245​
164​
Jumla
8,740
2,610
2,662
2,292
751
426
Asilimia
100
30
30
26
9
5

Ndugu Wanahabari,​

Pia, niwape tathmini ya utekelezaji wa mapendekezo yaliyotolewa kwenye kaguzi tano za ufanisi katika kipindi cha mwaka 2016 kama inavyoainishwa kwenye Jedwali hapa chini.

HALI YA UTEKELEZAJI WA MAPENDEKEZO YALIYOTOLEWA KWENYE KAGUZI ZA UFANISI

Ripoti ya Ukaguzi wa Ufanisi
Mapendekezo
Jumla Kuu
Yaliyo tekelezwa
Kikamilifu
Yaliyo tekelezwa
Kiasi
Yasiyo tekelezwa
Yaliyopitwa na wakati
Utekelezaji wa Masharti ya Mahitaji ya Ndani na Uhakiki wa Gharama Rejeshi Unaotokana na
Makubaliano ya
Mgawanyo wa Uzalishaji
10​
0​
6​
3​
1​
Usimamizi wa Takwimu za Jiofizikia na Jiolojia ya Mafuta na Gesi nchini
Tanzania
16​
8​
5​
3​
0​
Usimamizi wa Mchakato wa Utoaji wa Mikataba ya Utafutaji, Uendelezaji na
Leseni za Gesi Asilia
12​
0​
9​
3​
0​
Ufuatiliaji wa Uzingatiaji na Utekelezaji wa Sera,
Sheria na Kanuni zinazohusu Shughuli za Utafutaji wa Petroli nchini Tanzania
15​
13​
1​
0​
Usimamizi wa
Uendelezaji wa Rasilimali Watu katika Sekta ya
Mafuta na Gesi Asilia
10​
0​
5​
5​
0​
Jumla
63
9
38
15
1
Asilimia
100
14
60
24
2

Kwa ujumla, utekelezaji wa mapendekezo niliyotoa hauridhishi ikizingatiwa kuwa ni asilimia 14 tu ya mapendekezo yote yaliyotolewa yametekelezwa kikamilifu; hivyo, jitihada zaidi zinahitajika kukamilisha utekelezaji wa mapendekezo yote.

Ndugu Wanahabari,​

Napenda nichukue nafasi hii kumshukuru sana Mh. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa maelekezo yake aliyoitoa siku nakabidhi hizi ripoti kwamba wahusika watekeleze mapendekezo ambayo nimekuwa nikiyatoa. Utekelezaji wa mapendekezo na ushauri ninaoutoa utasaidia kuimarisha mifumo ya udhibiti wa ndani na hivyo kuongeza mapato na kupunguza matumizi ya Serikali kwani hoja zingine zimekuwa zikijirudia kwa kuwa wahusika wanaacha tu kutekeleza mapendekezo na ushauri ninaoutoa.


5.0 MATOKEO YA UKAGUZI KWA MWAKA WA FEDHA 2019/2020

Ndugu Wanahabari,​

Naomba sasa niwape matokeo ya ukaguzi nilioufanya mwaka unaoishia tarehe 30 Juni 2020.

5.1 MATOKEO YA UKAGUZI WA SERIKALI KUU

5.1.1 Mwenendo wa Deni la Serikali​

Deni la Serikali hadi kufikia tarehe 30 Juni, 2020 lilikuwa Sh. trilioni 56.76 ambapo deni la ndani lilikuwa Sh.trilioni 15.52 na deni la nje ni Sh. trilioni 41.24 ikiwa ni ongezeko la Sh. trilioni 3.65 sawa na asilimia saba ikilinganishwa na deni la Sh. trilioni 53.11 lililoripotiwa Mwaka wa Fedha 2018/19. Ongezeko hilo linajumuisha Sh. bilioni 652 za deni la ndani na Sh. trilioni 3 za deni la nje.

Hadi tarehe 30 Juni 2020 deni la serikali lilikuwa linahimilika.

5.1.2 Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)​

Kwa mwaka 2019/20, Mamlaka ya Mapato Tanzania ilikusanya Sh. trilioni 17.92 dhidi ya makisio yaliyowekwa ya Sh. trilioni 19.41, hivyo kuwa na upungufu wa makusanyo kwa Sh. trilioni 1.49 sawa na asilimia nane ya jumla ya makisio ya makusanyo.

Ndugu Wanahabari,​

Mamlaka ya Mapato ilikuwa na changamoto mbalimbali katika ukusanyaji mapato kama ifuatavyo:

Bidhaa zinazopita kwenda nchi jirani zenye ushuru wa forodha wenye thamani ya Sh. bilioni 5.14 hazikuthibitishwa kutoka nchini​

Katika ukaguzi wangu wa bidhaa zinazopita nchini kuelekea nchi jirani kupitia mipaka ya forodha ya Tunduma, Kasumulu, Rusumo, Kabanga, Mutukula, Namanga, Holili na Kigoma kwa kuangalia mfumo wa TANCIS na nyaraka za kusafirishia sikuthibitisha kuwa bidhaa zenye makadirio ya kodi ya forodha Sh. bilioni 5.14 zilitoka nchini.

Mafuta yaliyopitiliza muda wa kukaa nchini ambayo yalipaswa kwenda nchi jirani yenye ushuru wa forodha Sh. bilioni 12.14​

Katika mapitio ya mafuta yanayopita nchini kwenda nchi jirani nilibaini yafuatayo:

Lita milioni 2.47 za mafuta zenye makadirio ya ushuru wa forodha wa Sh. bilioni 1.97 yalibaki nchini bila kusafirishwa kwenda nchi zilizokusudiwa kwa muda uliopangwa wa siku 30.


Lita milioni 14.08 za mafuta zenye ushuru wa forodha unaokadiriwa kufikia Sh. bilioni 10.43 zilizoshushwa Tanzania Bara kwa ajili ya kusafirishwa kwenda Zanzibar tangu Julai 2019 hazijaondoshwa kwa muda uliopangwa wa siku 21. Kwa mujibu wa sheria ya forodha, mafuta yanayokaa nchini kwa zaidi ya muda uliopangwa yanapaswa kurasimishwa kwa matumizi ya ndani na hivyo kutozwa ushuru unaotakiwa.

Kodi zilizoshikiliwa na kesi zilizopo katika mamlaka za rufaa za kodi Sh. Trilioni 360 na Dola za marekani milioni 181​

Nimebaini kuwa Mamlaka ya mapato imekuwa na kesi 1,097 za muda mrefu katika Mamlaka za Rufaa za Kodi zenye thamani ya Sh. trilioni 360 na dola za Kimarekani milioni 181 kama inavyoonekana katika jedwali hapa chini

KESI ZILIZOKUWEPO KATIKA MAMLAKA ZA RUFAA ZA KODI HADI TAREHE 30 JUNI 2020​

Mamlaka za Rufaa za Kodi
Idadi ya Kesi
Kodi zilizoshikiliwa kwenye Mapingamizi
(Sh.)
(Dola za
Marekani)
Mahakama ya Rufaa
20​
176,832,218,835​
150,137,310​
Baraza la Rufaa za Kodi
94​
2,681,308,049,509​
23,451,738​
Bodi ya Rufaa za Kodi
983​
357,223,517,421,771​
7,841,204​
Jumla
1097
360,081,657,690,120
181,430,252
Chanzo: Taarifa ya mapato ya Mamlaka 2019/20 na bodi za rufaa 2019/20​

Ucheleweshaji wa Utatuzi wa Mapingamizi ya Kodi Sh. Bilioni 38.78​

Nilibaini uwepo wa mapingamizi 44 yenye kodi ya thamani ya Sh. bilioni 38.78 katika Idara ya Walipakodi Wakubwa, Idara ya Upelelezi wa kodi na Idara ya kodi za Ndani ambayo hayajatatuliwa kwa muda unaotakiwa kama ilivyoainishwa katika Mkataba wa huduma na mlipa kodi ya mwaka 2017. Kucheleweshwa kwa utatuzi wa mapingamizi ya kodi kunaathiri malengo ya ukusanyaji wa kodi kwani mapingamizi haya yanafunga kiasi kikubwa cha kodi.

Kutokusanywa kwa Ushuru wa Forodha kwa Magari na Bidhaa (mitambo) Zilizoingizwa Nchini kwa Muda ambazo Hazijaondolewa Baada ya Muda Kuisha​

Nilibaini magari 936 yaliyoingizwa nchini kwa muda kupitia mipaka ya forodha ya Namanga, Holili, Tarakea, Mtambaswala na Sirari yamebaki nchini kwa zaidi ya muda ulioruhusiwa bila uthibitisho wa maombi ya waingizaji kuongezewa muda.

Pia, nilibaini bidhaa (mitambo) zenye thamani ya Sh. bilioni 20.25 na ushuru wa forodha Sh. bilioni 1.24 zilizoingizwa kwa muda nchini kupitia mipaka ya Namanga, KIA, Holili na Bandari kavu hazijaondolewa baada ya kumalizika kwa muda ulioruhusiwa kuwapo nchini, wala hazijarasimishwa kwa matumizi ya ndani kama sheria ya forodha inavyoelekeza.

5.1.3 Jeshi la Zimamoto na Uokoaji

Akaunti ya masurufu ya Jeshi la Zimamoto ilitumika kupitishia malipo batili ya Sh. milioni 261.35​

Nilibaini Sh. milioni 261.35 ziliwekwa kwenye akaunti ya masurufu ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji katika mojawapo ya benki za biashara kwa vipindi tofauti. Hata hivyo, Menejimenti ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji haikutambua vyanzo vya fedha hizo na hakukuwa na mawasiliano yoyote yaliyofanywa na benki kuhusuiana na mapokezi ya fedha hizo.

Pia, nilibaini kuwa, Kiasi hicho cha fedha kilichukuliwa na Mtunza Fedha wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kutoka katika akaunti hiyo kwa vipindi tofauti kwa kutumia nyaraka za fedha za kughushi.

Aidha, nilibaini kuwa, usuluhishi wa taarifa za benki kwenye akaunti ya masurufu haukufanywa kwa kipindi cha kuanzia tarehe 1 Julai 2019 hadi tarehe ya kukamilisha ukaguzi. Hii ni kinyume na Kanuni Na. 162 (1) ya Kanuni ya Fedha za Umma ya mwaka 2001 ambayo inahitaji taarifa za fedha za benki zifanyiwe usuluhisho angalau kila mwezi.

Hali Hii inaashiria udhibiti dhaifu wa mifumo ya ndani kwenye usimamizi wa fedha katika akaunti za benki za Jeshi la Zimamoto na Uokoaji.

5.1.4 Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA)​

Nilibaini kuwa, TGFA ililipa jumla ya Sh. bilioni 3.92 mnamo tarehe 14 Februari na 26 Aprili 2018 ikiwa ni gharama za huduma ya matengenezo makubwa ya ndege aina ya Fokker 28-5H-CCM ya mwaka 1978. Hata hivyo, wakati wa ziara yangu kwenye hifadhi ya ndege za Serikali Dar es Salaam mnamo 19 Agosti 2020, nilibaini kuwa ndege hiyo ilikuwa haifanyi kazi na ilikuwa imetelekezwa tangu mwaka 2015. Aidha, niligundua kuwa, TGFA iliwasilisha suala hili Wizara ya Fedha na Mipango ikiomba ifanyike tathmini ya kina juu ya ndege hiyo ili kuweza kuishauri Serikali juu ya uamuzi sahihi wa hatua za kuchukua.

Hata hivyo, ninaona uamuzi wa kuwekeza fedha za walipa kodi zenye thamani ya Sh. bilioni 3.92 kufanya ukarabati mkubwa wa ndege bila kufanya tathmini ya kina ya gharama na faida haukuwa sahihi, na hivyo, kusababisha hasara kwa taifa.

5.1.5 Wakala wa Huduma za Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) Makusanyo ya kivuko ambayo hayajapelekwa benki na hayapo kituoni Sh. 81,194,650

Nilibaini kuwa Kituo cha Kivuko cha Magogoni kilikusanya jumla ya Sh. bilioni 5,757,041,950 ikiwa ni tozo za kivuko kwa kipindi kilichoanzia tarehe 1 Julai 2019 hadi 30 Juni 2020. Hata hivyo, kati ya pesa zilizokusanywa, ni Sh. 5,675,847,300 ndizo zilizowekwa kwenye akaunti ya Benki inayosimamiwa na Makao Makuu ya TEMESA, ikiacha jumla ya kiasi cha Sh. 81,194,650 kikiwa bado hakijawekwa benki hadi muda wa ukaguzi, tarehe 31 Julai 2020. Aidha, nilibaini kuwa kiasi hicho cha fedha ambacho hakikuwekwa benki pia hakikuwa kwenye himaya ya kituo. Kwa maoni yangu, fedha hizi ambazo hazijawekwa benki kuna uwezekano kwamba zimetumiwa vibaya au kutumiwa katika shughuli zingine.

Mfumo Usio Madhubuti wa Tiketi za Kielektroniki Katika Kituo cha Feri cha Magogoni – Sh. Bilioni 2.594​

Nilibaini kuwa TEMESA iliuza jumla ya tiketi 21,447,004 zenye thamani ya Sh. bilioni 5.76. Hata hivyo, ni tiketi 9,122,690 tu zenye thamani ya Sh. bilioni 3.16 ndizo zilizothibitishwa na mashine (scanned) na kuacha jumla ya tiketi 12,324,314 zenye thamani ya Sh. bilioni 2.60 zikitumika bila ya kuthibitishwa na mashine (not scanned).

Ni maoni yangu kuwa, tiketi hizo zinaweza kutumika tena na kusababisha serikali kupoteza mapato.

5.1.6 Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA)

Usimamizi Usioridhisha wa Kadi za Kutengenezea Vitambulisho vya Taifa Sh. Bilioni 3.399​

Mnamo tarehe 21 Aprili 2011, NIDA iliingia kwenye Mkataba na M/s IRIS Corporation Berhad ya Malaysia (Supplier) kwa ununuzi wa bidhaa na vifaa vya utekelezaji wa mfumo wa Kadi za Taifa kwa kutumia teknolojia ya kisasa kwa gharama ya Dola 149,956,303. Muda wa mkataba uliisha tokea tarehe 14 Machi 2018 (miaka mitatu nyuma) bila ya kuongezwa kwa muda.

Ukaguzi wangu wa mkataba huu umebaini kuwa kulikuwa na makubaliano ya kusambaza kadi 25,000,000 mpaka kipindi cha Ukaguzi, Novemba 2020, nilibaini kwamba msambazaji aliwasilisha kadi 13,735,728 tu. Aidha, uchambuzi wangu ulibaini kwamba, kati ya kadi zilizowasilishwa, NIDA imetumia kadi 6,180,015 kutengeneza vitambulisho vya taifa na kubakiza kadi 5,084,257 zikiwa hazijatumika.

Hata hivyo, nimebaini kuwa kati ya kadi 5,084,257 zilizobakia, ni kadi 4,657,500 tu ndizo zilikuwa zimehifadhiwa kwenye bohari, huku kadi 426,757 zenye thamani ya Sh. 3,399,973,019[1] zikiwa zimeharibika na hazifai kwenye matumizi ya kutengeneza vitambulisho vya taifa. Licha ya menejimenti ya NIDA kueleza kuwa imetuma barua kwenda kwa mkandarasi (IRIS) ili afanye usuluhisho wa kadi zilizoonekana na matatizo na kubadilisha na kadi mpya ni maoni yangu kuwa kuna hatari ya NIDA kupata hasara ikiwa IRIS atashindwa kubadilisha kadi hizo ambazo hazifai kutokana na kukosekana kwa mkataba halali kati ya NIDA na M/s IRIS Corporation Berhad.


5.1.7 Wakala wa Umeme Vijijini (REA)

Nguzo za Umeme Zenye Kasoro Zilizowekwa Mkoani Lindi Sh. Bilioni 1.07​

Mnamo tarehe 17 Julai 2017, REA iliingia mkataba wenye namba: AE/008/2016-17/HQ/G/09-Lot 4 na M/s State Grid Electrical & Technical Work Ltd kwa ajili ya kuweka umeme vijijini katika mkoa wa Lindi (awamu ya III) kwa bei ya kandarasi ya Sh. 20,878,061,665.12 na Dola za marekani 4,794,467.15 (ikijumuisha kodi ya ongezeko la Thamani). Muda wa kuisha kwa mkataba ulikuwa tarehe 25 Juni 2020 lakini uliongezwa mpaka tarehe 31 Desemba 2020.

Kwenye ukaguzi wa mkataba huu, nilibaini kuwa mkandarasi aliweka nguzo za umeme 6,541 zenye thamani ya Sh. 2,965,562,433.33 katika mkoa wa

Lindi. Hata hivyo, wakati wa kutembelea mradi mnamo Oktoba 2020 niliona

kwamba kati ya nguzo zilizowekwa, nguzo za umeme 2,612 (40%) zenye thamani ya Sh. 1,065,696,000 zilikuwa na nyufa. Mbali na hivyo, mkandarasi hakuwa amebadilisha nguzo hizo zenye kasoro. Hii ni kinyume na Kifungu 23.6 cha GCC kinachomtaka mkandarasi kusahihisha au kubadilisha bidhaa au sehemu ya vifaa ikiwa bidhaa hizo au vifaa vimeshindwa kufaulu jaribio au ukaguzi.


5.1.8 Ofisi ya Mwendesha Mashtaka wa Serikali

Kutokutumiwa kwa Fedha Zinazotokana na Mali Zilizotaifishwa na Kurejeshwa Serikalini - Sh. Bilioni 51.521​

Nilipitia uendeshwaji wa Akaunti ya fedha zinazotokana na mali zilizotaifishwa na kurejeshwa Serikalini zilizo chini ya Mkurugenzi wa Mashtaka hadi kufikia tarehe 30 Juni 2020. Nilibaini kuwapo kwa bakaa ya fedha Sh. bilioni 51.521 kutokana na kesi zilizomalizika katika mahakama mbalimbali kwa kipindi cha miaka 6 na zaidi kama ilivyooneshwa kwenye jedwali hapa chini.

BAKAA YA FEDHA ZILIZO KATIKA AKAUNTI YA FEDHA ZA MALI ZILIZOTAIFISHWA NA KUREJESHWA SERIKALINI​

Namba ya
Akaunti
Jina la Akaunti
Bakaa hadi kufikia tarehe 30 Juni
2020
9921161271Akaunti ya Fedha za Mali zilizo taifishwa na kurejeshwa serikalini
15,264,026,469.22​
9921169817Mkurugenzi wa Mashtaka
18,567,255,515.53​
9931209531Akaunti ya Fedha za Mali zilizo taifishwa na kurejeshwa serikalini Dola za Marekani 7,741,633.92 @Sh 2,285.0891 kwa kiwango cha kubadilisha fedha tarehe 30 Juni
2020
17,690,323,286.78​
Jumla 51,521,605,271.53
Chanzo: Taarifa za Benki

Kutotumiwa kwa bakaa ya fedha katika akaunti kunasababishwa na kutokuwapo kwa sheria na kanuni za kudhibiti matumizi ya fedha itokanayo na mali zilizotaifishwa na kurejeshwa serikalini.

Ni maoni yangu kuwa, kuwapo wa fedha zisizotumiwa kwa sababu ya kukosekana kwa Muongozo au mfumo wa kisheria kunaweza kusababisha matumizi mabaya ya Fedha za umma na ucheleweshaji wa maendeleo ya umma.

5.1.9 Masuala Mtambuka

Kutorejeshwa kwa Fedha Zilizokopwa na Wizara Sh. Bilioni 4.083​

Nilibaini kuwa wizara mbali mbali zilikopa jumla ya Sh. bilioni 4.083 kutoka mifuko maalumu mitatu bila ya kurudisha kiasi hicho kama ilivyoelezewa kwenye Jedwali hapa chini.

FEDHA ZILIZOKOPWA NA WIZARA​

Na. Jina la Mfuko Kiasi
kilichokopwa (Sh.)
Taasisi iliyokopeshwa
1Mfuko wa Uwezeshaji wa Maendeleo ya Madini
(EMDF)
521,831,816.56​
Wizara ya Madini
2Akaunti ya Mfuko wa
Barabara-TAMISEMI
3,442,788,003.52​
OR - TAMISEMI
3Mfuko wa Maji Taifa Wizara ya Maji
119,293,355.00​
Wizara ya Maji
Jumla 4,083,913,175.08
Chanzo: Barua ya mapungufu kwa menejimenti

Ni maoni yangu kwamba, kutokurudishwa kwa fedha zilizokopwa na Wizara kunaathiri utekelezaji wa shughuli za Mifuko Maalumu, hivyo fedha hizo zirejeshwe ili kutekeleza shughuli zilizopangiwa.

Malipo Yenye Nyaraka Pungufu – Sh Bilioni 13.061​

Katika ukaguzi wa mwaka huu, nimebaini malipo yenye thamani ya Sh. bilioni 13.061 ambayo hayakuwa na nyaraka za kujitosheleza kinyume na Kanuni 95 (4) ya Kanuni za Fedha za Umma, 2001 kama inavyoonyeshwa kwenye Jedwali hapa chini.

Taasisi zenye malipo yenye nyaraka pungufu​

Na. Taasisi Kiasi (Sh.)
1.Wakala Wa Huduma Za Misitu Tanzania (TFS)
200,061,021​
2.Wakala wa Ndege za Serikali (TGFA)
451,457,684​
3.Shirika la Uzalishaji Mali la Magereza
530,446,323​
4.Bodi ya Mfuko wa Barabara (RFB)
87,738,385​
5.Wakala wa Majengo Tanzania (TBA)
46,083,900​
6.Shirika la Mzinga
3,584,216,021​
7.Hospitali ya Rufaa ya MkoaTemeke
172,156,483​
8.Wakala wa Taifa wa Utafiti wa Nyumba Bora na Vifaa vya Ujenzi (NHBRA)
101,242,748​
9.Wakala Wa Barabara Za Vijijini Na Mijini (TARURA)
72,860,000​
10.Kituo cha Mafunzo ya Takwimu cha Afrika Mashariki
(EASTC)
98,097,349​
11.Hospitali ya rufaa ya mkoa wa Dodoma
257,424,600​
Hospitali ya rufaa ya mkoa wa Tabora
139,210,000​
12.Jeshi la Zimamoto na Uokozi – Fungu Na. 14
1,766,605,227​
13.Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali – Fungu Na. 16
74,719,150​
14.Tume ya Taifa katika Shirika la Umoja wa Mataifa
linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) –
Fungu Na. 18
138,003,604​
15.Jeshi la Wananchi wa Tanzania – Fungu Na. 38
605,695,511​
16.Wizara ya Mambo ya Ndani – Fungu Na. 51
36,495,728​
17.Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na
Watoto – Fungu Na. 53
143,564,642​
18.Idara ya Huduma za Uhamiaji – Fungu Na. 93
11,200,000​
19.Ikulu - Fungu Na. 20
46,548,534​
20.Msajili wa Vyama vya Siasa – Fungu Na. 27
7,823,000​
21.Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
– Fungu Na. 34
97,087,278​
22.Wizara ya Katiba na Sheria – Fungu Na. 41
61,050,292​
23.Tume ya Taifa ya Uchaguzi – Fungu Na. 61
1,545,034,285​
24.Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu –
Fungu Na. 65
6,735,600​
25.Sekretarieti ya Mkoa Geita
15,323,383​
26.Sekretarieti ya Mkoa Kagera
36,903,658​
27.Sekretarieti ya Mkoa Mara
18,650,000​
28.Sekretarieti ya Mkoa Simiyu
20,000,000​
29.Sekretarieti ya Mkoa Iringa
5,315,441​
30.Sekretarieti ya Mkoa Katavi
5,651,088​
31.Sekretarieti ya Mkoa Rukwa
21,756,360​
32.Sekretarieti ya Mkoa Ruvuma
5,327,000​
33.Sekretarieti ya Mkoa Mbeya
32,487,500​
34.Sekretarieti ya Mkoa Geita
1,652,898,617​
35.Ofisi ya Rais ya Usimamizi wa Nyaraka na Utunzaji wa
Kumbukumbu – Fungu Na. 04
6,000,000​
36.Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia - Fungu Na. 46
29,175,569​
37.Tume ya Kuzuia UKIMWI - Fungu Na. 92
15,538,680​
38.Sekretarieti ya Mkoa Mara
18,650,000​
39.Sekretarieti ya Mkoa Mwanza
22,062,858​
40.Sekretarieti ya Mkoa Dar es Salaam
213,011,595​
41.Sekretarieti ya Mkoa Mtwara
15,000,000​
42.Sekretarieti ya Mkoa Lindi
5,580,000​
43.Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi – Fungu
Na. 48
424,757,390​
44.Sekretarieti ya Mkoa Tanga
4,737,000​
45.Sekretarieti ya Mkoa Shinyanga
86,362,063​
46.Tume ya Taifa ya mipango na matumizi ya Ardhi – Fungu Na.
3
5,110,000​
47.Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa – Fungu
Na. 56
119,275,653​
Jumla
13,061,131,220

Chanzo: Barua ya mapungufu kwa menejimenti

Ni maoni yangu kuwa chanzo cha kuwa na matumizi yenye nyaraka pungufu ni kuwa na mfumo dhaifu wa udhibiti na Maafisa Masuuli kushindwa kuchukua hatua stahiki kwa maafisa wanaosababisha udhaifu huu. Ninaamini kuwa hii inaweza kuwa ishara ya kufanyika kwa matumizi ya udanganyifu na mabaya. Mawanda yangu ya Ukaguzi yalizuiwa hivyo sikuweza kuthibitisha uhalali wa malipo yaliyofanyika.



[1] Gharama ya kila kadi ni Dola za Marekani 3.452 sawa na Sh. 7,967 kwa kiwango cha kubadilisha fedha za kigeni cha BOT mnamo tarehe 30 June 2020; hivyobasi, kadi 426,757 mara Sh. 7,967 ni sawasawa na Sh. 3,399,973,019
 

Attachments

  • Ripoti_ya_Ukaguzi_wa_Mashirika_ya_Umma_2019_20.pdf
    18.9 MB · Views: 40
  • Ripoti_ya_Ukaguzi_wa_Mifumo_ya_TEHAMA_2019_20.pdf
    5.5 MB · Views: 30
  • Ripoti_ya_Ukaguzi_wa_Miradi_ya_Maendeleo_2019_20 (1).pdf
    17 MB · Views: 35
  • Ripoti_ya_Ukaguzi_wa_Serikali_Kuu_2019_20 (1).pdf
    26.3 MB · Views: 28

Matumizi Yaliyofanywa Nje ya Bajeti - Sh. Bilioni 29.659

Katika ukaguzi wa mwaka huu, nilifanya ukaguzi wa usimamizi wa bajeti kwa taasisi mbalimbali na kubaini kuna malipo yenye thamani ya Sh. 29,659,851,120.98 yaliyofanywa nje ya bajeti kinyume na Kanuni 46 (3) ya Kanuni za Fedha za Umma, 2001 iliyorekebishwa 2004 kama inavyooneshwa kwenye Jedwali hapa chini.

Taasisi zilizofanya matumizi nje ya bajeti

Na Taasisi Kiasi (Sh.)
1Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo
(TASUBA)
153,603,589​
2Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS)
2,054,266,378​
3Shirika la Uzalishaji Mali la Magereza
2,234,644,183​
4Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori
Tanzania (TWMA)
204,473,000​
5Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA)
165,850,921​
6Mfuko wa Taifa wa Maji - Wizara ya Maji
110,838,982​
7Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini
(TARURA)
327,777,685​
8Tume ya Taifa katika Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na
Utamaduni (UNESCO) – Fungu Na. 18
4,760,000​
9Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
– Fungu Na. 62
38,150,000​
10Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,
Wazee na Watoto – Fungu Na. 53
257,906,556​
11Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,
Wazee na Watoto – Fungu Na. 52
24,024,009,125​
12Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na
Walemavu – Fungu Na. 65
50,477,500​
13Sekretarieti ya Mkoa Songwe
33,093,200​
Jumla
29,659,851,119
Chanzo: Barua ya mapungufu kwa menejimenti

Ununuzi uliofanyika nje ya mpango wa mwaka wa ununuzi Sh. Bilioni 15.129

Kifungu Na. 49(3) cha Sheria ya Ununuzi wa Umma ya mwaka, 2011 kinaagiza Taasisi za ununuzi kuzingatia Mpango wa ununuzi wa Mwaka. Hata hivyo, katika ukaguzi wa Wizara, Idara, na Sekretarieti za Mikoa, Taasisi saba zilibainika kufanya ununuzi wa vifaa na huduma wenye thamani ya Sh. 15,129,146,553 nje ya mpango wa mwaka wa ununuzi. Kwa kuwa ununuzi huu ulifanyika nje ya mpango wa mwaka wa ununuzi, hali hiyo ilipelekea matumizi nje ya bajeti ya Taasisi husika. Upungufu huu ulitokana na udhaifu kwenye maandalizi ya mpango wa ununuzi na bajeti katika Taasisi husika. Jedwali hapa chini linaonesha Taasisi zilizofanya ununuzi nje ya mpango wa ununuzi wa mwaka.

Taasisi zilizofanya ununuzi nje ya mpango wa ununuzi wa mwaka

Fungu Taasisi Maelezo
Kiasi (Sh)
53Wizara ya Afya,
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na
Watoto
Ununuzi wa Huduma za
Ushauri na Ulinzi
131,192,986​
14Jeshi la Zimamoto na UokoajiUjenzi wa
Majengo ya Ofisi na Makazi
2,709,297,900​
99Wizara ya Mifugo na Uvuviwa na
2,428,349,273​
34Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.Ununuzi wa huduma za
Ulinzi
177,798,040​
61Tume ya Taifa ya
Uchaguzi
Ununuzi wa
Magari Ishirini
(20)
1,373,706,909​
79Sekretarieti ya Mkoa wa MorogoroUnunuzi wa mbegu za mahindi na vifaa vya Ujenzi
93,453,152​
N/AMamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)Ununuzi wa vifaa vya Ofisini, vilainishi na mafuta ya magari,
ukarabati wa magari pamoja na huduma za
bima na usafi
8,215,348,293​
Jumla
15,129,146,553
Chanzo: Taarifa ya Ukaguzi kwa Menejimenti 2019/20

Ikilinganishwa na mwaka 2018/2019, kuna ongezeko la Sh 11,523,371,141 kwa ununuzi uliofanyika bila ya kufuata Mpango wa Ununuzi wa Mwaka. Katika mwaka wa 2018/19 jumla ya taasisi saba zilifanya ununuzi wa bidhaa na huduma zenye thamani ya Sh 3,605,775,412 nje ya Mpango wa Ununuzi wa Mwaka.

Matumizi Yasiyo na Tija - Sh. 453,782,820

Katika ukaguzi wangu nilibaini kuwa Wizara mbili zilifanya matumizi kiasi cha Sh. 453,782,820.35 ambayo hayana tija kama inavyooneshwa kwenye Jedwali hapa chini.

MALIPO YASIYO NA TIJA

Na. Taasisi
Kiasi (Sh.)
Maelezo
1​
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,
Wazee na Watoto
– Fungu Na. 52
Gharama ya kuchelewa kuondosha mizigo bandarini ambayo ni magari 50 ya wagonjwa na pikipiki 50.
2​
Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi – Fungu Na. 64)
2,627,318.35​
Malipo ya adhabu kwa kuchelewa kupeleka makato ya watumishi Mfuko wa Hifadhi ya
Jamii.
Jumla 453,782,820.35
Chanzo: Taarifa ya Ukaguzi kwa Menejimenti 2019/20
Ninaamini kuwa, matumizi yasiyo na tija hutokana na mfumo wa udhibiti wa matumizi usioridhisha. Bila ya kuwa na mfumo madhubuti wa udhibiti wa matumizi ya fedha, Serikali itaendelea kupata hasara kutokana na matumizi ambayo yangeweza kuepukika.

Hati za Malipo Ambazo Hazikuwasilishwa Wakati wa Ukaguzi - Sh. Bilioni 2.638

Hati za malipo zenye jumla ya Sh. 2,638,372,956.12 katika taasisi nne hazikuwasilishwa kwa ajili ya ukaguzi hivyo sikuweza kujiridhisha uhalali wa malipo hayo. Kwa mujibu wa kanuni ya 18 (1)(f) na (2) ya Kanuni za Fedha za mwaka 2001, malipo ambayo nyaraka zake hazijawasilishwa ni hasara ya fedha na yanapaswa kujumuishwa kwenye taarifa ya Hasara ya Mhasibu Mkuu wa Serikali.

Hati za Malipo ambazo Hazikuwasilishwa Wakati wa Ukaguzi​

Na. Taasisi
Kiasi (Sh.)
1​
Jeshi la Wananchi wa Tanzania – Fungu Na. 38
2,293,308,795​
2​
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto – Fungu Na. 52
95,691,921​
3​
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki – Fungu Na. 34
72,853,524​
4​
Tume ya Taifa ya Uchaguzi – Fungu Na. 61
176,518,715​
Jumla
2,638,372,955
Chanzo: Taarifa ya Ukaguzi kwa Menejimenti 2019/20

Ni maoni yangu kuwa chanzo cha kutokuwasilisha hati za malipo ni kuwa na mfumo dhaifu wa udhibiti na Maafisa Masuuli kushindwa kuchukua hatua stahiki kwa maafisa wanaosababisha udhaifu huu. Ninaamini kuwa hii inaweza kuwa ishara ya kufanyika kwa matumizi ya udanganyifu na mabaya. Mawanda yangu ya Ukaguzi yalizuiwa hivyo sikuweza kuthibitisha uhalali wa malipo yaliyofanyika.

Mapungufu Kwenye Uidhinishaji wa Malipo – Sh. Bilioni 3.233

Ukaguzi huu pia umebaini kuwa taasisi saba zilifanya malipo yenye jumla ya Sh. 3,233,703,014 bila ya hati za malipo husika kuidhinishwa.

Kukosekana kwa saini za waidhinishaji wa malipo kwenye hati za malipo kumesababishwa na udhaifu kwenye mifumo ya udhibiti katika uandaaji na uidhinishaji wa hati za malipo. Kuna hatari kuwa watumishi wasio waaminifu wanaweza kutumia fursa hii kutumia vibaya na kujinufaisha. Jedwali hapa chini linaonyesha Taasisi zenye dosari hiyo.

Taasisi zenye Dosari kwenye Kuidhinisha Malipo​

Na.
Taasisi
Kiasi (Sh.)
1​
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii,
Jinsia, Wazee na Watoto – Fungu Na. 52
42,362,000​
2​
Tume ya Taifa katika Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) –Fungu Na.18
1,989,440​
3​
Msajili wa Vyama vya Siasa –Fungu Na. 27
10,489,624​
4​
Tume ya Taifa ya Uchaguzi –Fungu Na. 61
119,207,203​
5​
Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu –Fungu Na. 65
20,155,000​
6​
Sekretarieti ya Mkoa Simiyu
2,270,000​
7​
Jeshi la Wananchi wa Tanzania –Fungu Na.
38
3,037,229,747​
Jumla
3,233,703,014

Chanzo: Taarifa ya Ukaguzi kwa Menejimenti 2019/20

Ikilinganishwa na mwaka uliopita, idadi ya taasisi zenye dosari hii imepungua kutoka taasisi nane hadi saba wakati kiwango kimeongezeka kutoka Sh. 719,479,937.89 hadi Sh. 3,233,703,014.33. Hii inaonesha kuwa menejimenti husika zinatakiwa kuboresha mifumo ya udhibiti ili kuhakikisha kuwa malipo yanaidhinishwa ipasavyo.

Vifaa na Mali Zilizolipiwa Lakini Hazikupokelewa - Sh. Bilioni 6.826

Katika taasisi za serikali kuu nilizokagua, nilibaini ununuzi wa vifaa na mali zenye thamani ya Sh. bilioni 6.826 zilizoagizwa na kulipiwa lakini hazikupokelewa. Makubaliano yalibainisha kuwa ununuzi ulipaswa kukamilika kati ya wiki mbili hadi miezi mitatu lakini wazabuni walishindwa kutekeleza matakwa ya mikataba. Taasisi zilizohusika na ununuzi usiopokelewa zimeorodheshwa kwenye Jedwali hapa chini:

VIFAA NA MALI ZILIZOLIPIWA LAKINI HAZIKUPOKELEWA​

Fungu Taasisi Maelezo Kiasi (Sh.)
1.​
Wizara ya Afya,
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na
watoto
Ununuzi wa Magari Tisa (9) kupitia Wakala wa Huduma za Ununuzi Serikalini (GPSA)
1,090,654,835​
2.​
Wizara ya Mifugo na UvuviUnunuzi wa Magari mawili na Pikipiki tatu kupitia Wakala wa Huduma za Ununuzi
Serikalini (GPSA)
380,000,000​
3.​
Ofisi ya Waziri Mkuu- Kazi, Vijana, Ajira na
Watu wenye Ulemavu
Ununuzi wa Magari matano kupitia Wakala wa Huduma za Ununuzi Serikalini-GPSA
1,022,290,162​
4.​
Sekretarieti ya Mkoa wa ArushaUnunuzi wa vifaa vya umeme
41,134,760​
5.​
Tume ya Taifa ya mipango na matumizi ya ArdhiUtengenezaji wa Kanzi data
41,000,000​
6.​
Wizara ya Afya,
Maendeleo ya Jamii,
Wazee, Jinsia na
Watoto
Ununuzi wa vifaa vya
Hospitalini
4,251,751,270​
Jumla 6,826,831,027

Mapungufu Katika Uendeshaji wa Akaunti ya Masurufu - Sh. Bilioni 6.805

Nimekagua shughuli za akaunti ya masurufu kwa Taasisi tofauti na kubaini kuwa Sh. bilioni 6.805 zimelipwa kupitia akaunti ya benki ya masurufu kwa ajili ya kazi mbalimbali katika taasisi tano ndani ya mwaka. Katika kukagua nilibaini kuwa taasisi zilikuwa hazina daftari la fedha lililotunzwa wala taarifa za usuluhisho wa kibenki wa kila mwezi iliyoandaliwa. Hii ni kinyume na kanuni ya 162 (1) ya Kanuni za Fedha za Umma ya mwaka 2001 ambayo inahitaji bakaa ya kila akaunti ya benki kama inavyooneshwa katika taarifa ya fedha za benki isuluhishwe na taarifa za usuluhisho za kibenki na bakaa za kitabu cha fedha angalau kila mwezi. Taarifa za usuluhisho za kibenki zitunzwe au kurekodiwa katika kitabu cha fedha. Orodha ya taasisi zenye mapungufu zimeoneshwa kwenye Jedwali hapa chini.

MAPUNGUFU YALIYOJITOKEZA WAKATI WA KUIENDESHA AKAUNTI YA BENKI YA MASUFURU
NA. FUNGU Taasisi Maelezo
Kiasi (Sh)
1 29Wizara ya
Mambo ya Ndani
–Idara ya
Magereza
Akaunti namba ya
Masurufu 0150211137700 ambayo ipo benki ya CRDB.
409,344,179​
NA. FUNGU Taasisi Maelezo
Kiasi (Sh)
2 44Wizara ya Viwanda na
Biashara
Benki akaunti namba.
50510032036 ya NMB na akaunti namba 0150211156000 ya CRDB Benki.
232,590,000​
3 46Wizara ya Elimu
Sayansi na
Tecknologia
Akaunti ya Masurufu
namba
0150211138700
iliyopo CRDB
Azikiwe Premier
3,015,357,893​
4 56Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za MitaaAkaunti ya Masurufu ya NMB
2,101,469,012​
5 100Wizara ya MadiniUchukuwaji wa fedha kutoka katika akaunti ya masurufu jumla ya Sh.
1,046,203,019.96 ilitumika kulipa moja kwa moja wazabuni na
makandarasi,
kinyume na sheria na kanuni
zinazohitajika
1,046,203,019​
Jumla
6,804,964,103
Chanzo: Barua ya Mapungufu kwa Menejiment 2019/20

Sababu za kutotunza daftari la fedha la akaunti ya masurufu na maandalizi ya taarifa ya usuluhisho wa kibenki wa kila mwezi hazikufahamika. Hali hii huleta ugumu katika kufahamu ukweli na usahihi wa miamala ya fedha iliyofanyika na bakaa zilizoripotiwa.

Ninatoa angalizo katika mapungufu yaliyojitokeza kwenye udhibiti wa ndani kwa taasisi, ambayo yanaweza kusababisha makosa, ubadhirifu na matumizi mabaya ya fedha za umma.

Kutokulipwa kwa Madai ya Wakandarasi, Wahandisi Washauri na Watoa Huduma - Sh. Bilioni 783.392

Nilibaini kuwa Wakala nne za Serikali zilikuwa na madai ya malipo ya Sh. bilioni 783.39 kutoka kwa wakandarasi, washauri na watoa huduma. TANROADS ilikuwa na deni[1] kubwa lenye thamani ya Sh. 770,119,541,338.75 kutoka kwa wakandarasi na wahandisi washauri kutokana na kuchelewa kupata fedha za kutekeleza miradi kutoka Hazina. Maelezo yameoneshwa kwenye Jedwali hapa chini.

MALIPO YALIYOCHELEWA KULIPWA YA WAKANDARASI, WASHAURI NA WATOA HUDUMA

Wakala
Maelezo
Kiasi (Sh.)
Wakala wa Barabara
Tanzania (TANROADS)
Madai ambayo hayajalipwa ya wakandarasi na washauri
770,119,541,338.75​
Wakala wa Majengo
Tanzania (TBA)
Madai ambayo hayajalipwa ya wasambazaji wa vifaa vya
ujenzi
1,144,426,032.65​
Wakala ya Usambazaji Maji na Usafi na Mazingira Vijijini
(RUWASA)
Madai ambayo hayajalipwa ya wakandarasi na washauri
12,002,403,927.95​
Wakala Wa Barabara Za Vijijini Na Mijini
(TARURA)
Madai ambayo hayajalipwa ya wakandarasi na washauri
125,805,436.00​
Jumla
783,392,176,735.35

Chanzo: Barua ya mapungufu kwa menejimenti

Ni maoni yangu kwamba, ucheleweshaji wa kulipa madai haya kunaongeza hatari ya kuongezeka kwa gharama za miradi kutokana na riba inayotozwa kwenye malipo yaliyochelewa na kwa hivyo kuongeza mzigo wa gharama kwa walipa kodi.

Kushindwa Kutoza Fidia ya Kuchelewesha Kazi - Sh Bilioni 7.511

Ukaguzi wangu umebaini kuwepo kwa Taasisi ambazo zimeshindwa kutoza fidia ya kuchelewesha kazi (liquidated damages) kinyume na Kanuni 112 (1) ya Kanuni za Ununuzi wa Umma za Mwaka 2013. Kwa ujumla nimebaini Sh.

bilioni 7.511 kama fidia ya kuchelewesha kazi hazikutozwa. Jedwali hapa chini linafafanua zaidi.

KUSHINDWA KUTOZA FIDIA YA KUCHELEWESHA KAZI

MKOA
JINA LA MRADI
MKATABA NA.
GHARAMA YA MKATABA (Sh.)
UCHEL
EWES

HAJI
(SIKU)
TOZO YA FIDIA (Sh.)
KageraUjenzi wa Mradi wa maji kijiji cha KakunyuLGA/038/RWS
SP/18/2013/2
014
875,845,000​
312​
116,349,600​
KigomaUjenzi wa Mradi wa Maji Vijiji vya Kaseke, Kimbwela na NyamoliLGA/043/2016 /2017/W/15
1,163,496,000​
539​
174,524,400​
MtwaraUjenzi wa Mradi wa maji kwa Kijiji cha MkwitiLGA/087/WS/
2017/2018/w/
16
3,271,950,518​
100​
327,195,051​
NjombeUjenzi wa Mradi wa maji Igando- KijombeLGA/153/2017 /2018/W/01
12,437,407,360​
49​
609,432,960​
DSM​
Ujenzi wa Barabara ya Makutano – Natta (Sanzate) (50 km): Kipande cha 1TRD/HQ/1032 /2012/13
54,594,286,488​
629​
5,459,428,648​
DSM​
Ujenzi wa Barabara ya mabasi yaendayo haraka: Kipande cha 1.
USD 3,144,025​
704,281,552​
DSM​
Ujenzi wa Barabara ya mabasi yaendayo haraka: Kipande cha 1.TRD/HQ/1038 /2016/17
USD 3,144,025​
226​
120,610,962​
Jumla
7,511,823,173​

Tozo ya Riba kwa Ucheleweshwaji wa Malipo ya Wakandarasi - Sh. Bilioni 14.985

Nilibaini miradi inayotekelezwa maeneo mbalimbali nchini ilikuwa na tozo ya riba kiasi cha Sh. bilioni 14.985 (Jedwali hapa chini) kama adhabu ya kuchelewesha kulipa hati za madai ya wakandarasi (IPCs) kinyume na masharti ya mikataba.

TOZO YA RIBA KWA KUCHELEWESHA MALIPO YA WAKANDARASI BILIONI 14.985

JINA LA MRADI
Riba ya kuchelewa kufanya malipo (Sh.)
Mradi wa Maendeleo ya Reli Tanzania (TIRDP)
2,197,609,697​
Mradi wa Ujenzi wa Barabara ya Kimataifa Arusha-Taveta/HoliliiVoi
1,847,308,621​
Mradi wa Uboreshaji Usafiri wa Mjini Dar es Salaam (DUTP)
666,979,087​
Programu ya Kusaidia Sekta ya Usafirishaji (TSSP)
3,466,386,456​
Ujenzi wa reli ya Kisasa SGR kipande cha Kwanza (DSM – Makutupora)
2,983,064,867​
Mabasi yaendayo Haraka -Mkandarasi Mshauri-Kipande cha kwanza
54,288,759​
Mabasi yaendayo Haraka -Mkandarasi-Kipande cha kwanza
30,307,636​
Mabasi yaendayo Haraka -Mkandarasi-Kipande cha pili
49,263,362​
Mabasi yaendayo Haraka -Mkandarasi Mshauri-Kipande cha pili
9,789,534​
Mradi wa Kimataifa wa Kunganisha Nishati wa Kenya na Tanzania (KTPIP)
132,499,311​
Mradi wa Upanuzi wa Barabara ya Morogoro (Kimara – Kibaha)
304,244,580​
Mradi wa Ujezi wa Miundombinu ya Mabasi yaendayo Haraka
143,641,656​
Mradi wa Usambazaji Maji Same-Mwanga-Korogwe
3,100,217,731​
Jumla
14,985,601,297
Tozo hizi zinaongeza gharama za miradi na ni malipo ambayo hayana tija.

Usimamizi Usioridhisha wa Dhamana za Mikataba - Sh. Bilioni 35.145

Ukaguzi wangu wa shughuli za Wakala Tendaji umebaini kuna usimamizi usioridhisha wa dhamana zenye thamani ya Sh. bilioni 35.145 kama inavyoelezewa hapo chini:

Nimebaini Wakala tatu zilitekeleza miradi ya ujenzi bila ya kuwapo kwa dhamana ya utendaji (Performamnce Security) zenye thamani ya Sh. bilioni 25.70 kinyume na Kifungu 60.1 cha GCC.

Niligundua kwamba, wakala nne zilifanya malipo ya awali yenye thamani ya Sh. bilioni 9.44 kwa wakandarasi na washauri elekezi bila dhamana ya kibenki (Adance Bank Gurantee) kinyume na Kifungu 59.1 cha GCC. Jedwali hapo chini linaonesha Wakala ambazo zinatekeleza miradi bila ya dhamana.

Wakala zinazotekeleza miradi bila ya dhamana

Na.
Wakala
Dhamana za utendaji (Sh.)
Dhamana za malipo ya awali (Sh.)
Jumla
1​
Wakala wa
Barabara Tanzania
(TANROADS)
12,584,887,052​
9,192,035,264​
21,776,922,316​
2​
Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA)
153,000,000​
153,000,000​
3​
Wakala wa
Huduma za Misitu
(TFSA)
49,001,105​
49,001,105​
4​
Wakala Wa
Barabara Za
Vijijini Na Mijini
(TARURA)
781,075,886​
50,000,000​
831,075,886​
5​
Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA)
12,335,711,590​
12,335,711,590​
Jumla
25,701,674,528
9,444,036,369 35,145,710,897
Chanzo: Barua ya mapungufu kwa menejimenti

Kwa kuzingatia yaliyotajwa hapo juu, nina maoni kwamba usimamizi duni wa dhamana za mikataba unaweza kuzihatarisha Wakala kupata hasara iwapo wakandarasi watashindwa kutekeleza makubaliano ya kimkataba au kutekeleza kazi.

5.1.11 Kaguzi Maalumu Kwenye Taasisi za Serikali Kuu

Ndugu Wanahabari,

Nilifanya kaguzi maalumu katika Wizara, Idara na Wakala mbalimbali za Serikali na matokeo yake ni kama yafuatayo:

a) Wakala wa Huduma za Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA)

Ndugu Wanahabari,

Nilifanya ukaguzi maalumu ndani ya Wakala wa Huduma za Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) na kubaini mapungufu yafuatayo:

Hasara Kutokana na Kughushi Kodi za Zuio - Sh. 709,152,607.07

Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) ilipeleka hundi 429 zilizofungwa zenye thamani ya Sh. 1,894,988,144.28 kwa ajili ya malipo mbalimbali kwenye mojawapo ya benki ya kibiashara. Kati ya hundi zilizowasilishwa, hundi za jumla ya Sh. 1,069,249,601.13 zilikuwa ni kwa ajili ya malipo ya kodi ya zuio kwenda kwa Kamishna wa Kodi za Ndani (Mamlaka ya Maopato Tanzania). Wakati wa ukaguzi, Benki hiyo iliwasilisha hundi 368 za TEMESA zenye jumla ya Sh. 1,746,186,740.42 kati ya Hundi 429 zilizoombwa wakati wa ukaguzi. Benki hiyo haikuwasilisha Hundi 61 zenye thamani ya Sh.148,801,403.86 kwa kuwa ilishindwa kuzipata.

Baada ya kuzipitia Hundi zilizowasilishwa, nilibaini kuwa hundi 142 zilizofungwa zenye thamani ya Sh. 709,152,607.07 kati ya 368 zilizowasilishwa kwa ajili ya kumlipa Kamishna wa Kodi za Ndani zilibadilishwa na kuwa hundi za wazi (open cheques) na kulipwa kama fedha taslimu Sh. 585,531,414.53 kwa Mtunza Fedha wa TEMESA, na Sh. 61,898,037.46 zililipwa kwa kampuni mbili na Sh. 61,632,155.08 zililipwa kwa watu wengine watatu.

TEMESA ilithibitisha kuwa haikuwa na mahusiano yoyote ya kibiashara na kampuni pamoja na watu waliolipwa. Katika uchunguzi wangu, nilibaini kuwa ubadhirifu huu ulifanywa kwa ushirikiano mkubwa baina ya wafanyakazi wa benki hiyo na baadhi ya maafisa wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA). Mtunza Fedha wa TEMESA hakuandaa namba za utambuzi wa malipo ya kodi ili kutambua malipo ya kodi za zuio. Mtunza fedha wa TEMESA alikuwa akighushi saini za watoa fedha, na benki hiyo ilikuwa haifanyi uhakiki wa saini ili kuthibitisha uhalisi wa saini za waidhinishaji wa TEMESA waliopo kwenye taarifa za benki. Katika mahojiano, maafisa wa benki hiyo walieleza kuwa walikuwa wakiwasiliana na mojawapo wa watia saini aliyethibitisha kuwa Mtunza Fedha huyo aliruhusiwa kuchukua fedha taslimu kwa kutumia Hundi zilizofungwa.

Ukweli huu unapingana na taratibu za kibenki kwa kuwa sio rahisi kwa hundi zilizofungwa kulipwa fedha taslimu bila ya ufuatiliaji wa kina au uwasilishaji wa hundi mpya zilizokuwa wazi zinazoweza kuchukua fedha taslimu. Kwa kuwa maafisa wa Benki hiyo walifahamu kuwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ilikuwa ikipokea malipo ya kodi ya zuio kwa kutumia namba za utambuzi za malipo ya kodi, ni dhahiri kuwa kitendo cha Mtunza Fedha kuweza kulipa kodi ya zuio kwa fedha taslimu kiliiashiria benki hiyo kuwa kulikuwa na ishara za wizi, na wangeweza kuwasiliana na mteja wao, TEMESA. Kwa ukweli huo, ni dhahiri kuwa mifumo ya udhibiti ya ndani ya benki hiyo ilikuwa dhaifu, hivyo, kusababisha ubadhirifu wa kodi za zuio, jumla ya Sh. 709,152,607.07, uliofanywa na Mtunza Fedha wa TEMESA.

Kodi za Zuio Zilizokusanywa na TEMESA na Kutowasilishwa TRA - Sh. 866,160,442.04

Nilibaini kuwa zaidi ya Sh. 709,152,607.07 zilikusanywa na TEMESA kama kodi ya zuio na kuchukuliwa kinyume na utaratibu na Mtunza Fedha TEMESA. Pia, wakati wa ukaguzi nilibaini kuwa hundi 57 kwa ajili ya malipo ya kodi ya zuio kwa Kamishna wa Kodi za Ndani zenye thamani ya Sh.164,107,502.97 kutoka kwa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) hazikuwasilishwa kwa Benki hiyo kwa ajili ya malipo. Kati ya Hundi hizo, TEMESA iliwasilisha hundi nne tu kwa ajili ya ukaguzi na hundi 53 zilizobaki zenye thamani ya Sh. 155,182,550.45 hazikuwasilishwa kwa ajili ya ukaguzi. Kati ya hundi nne zilizowasilishwa, TEMESA ililipa hundi moja ya Sh. 7,099,668 mwezi Julai 2020.

Hivyo, ninathibitisha kuwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) haikupokea malipo ya kodi ya zuio ya jumla ya Sh. 866,160,442.04; ikiwa ni kiasi cha Sh. 709,152,607.07 kilichochukuliwa na Mtunza Fedha wa TEMESA na Hundi 53 zenye thamani ya Sh. 157,007,834.97 zilizoandaliwa na TEMESA na hazikuwasilishwa kwenye benki hiyo ili ziingizwe kwenye akaunti ya TRA.

Ni maoni yangu kuwa, mifumo ya udhibiti ya ndani ya benki hiyo ilishindwa kubaini saini zilizoghushiwa na kuruhusu hundi zilizofungwa kufunguliwa na kulipwa fedha taslimu. Pia, mifumo ya udhibiti wa ndani ndani ya TEMESA, ikijumuisha ukosefu wa ueledi kwenye kuandaa taarifa za usuluhishi wa kibenki na kutokuwapo kwa mgawanyo wa majukumu, ndiyo chanzo kikubwa cha ubadhirifu huu.

b) Wizara ya Maliasili na Utalii

Ndugu Wanahabari

Nilifanya ukaguzi maalumu ndani ya Wizara ya Maliasili na Utalii na kubaini dosari zifuatazo:

Usimamizi usioridhisha wa Mfuko wa Tozo ya Maendeleo ya Utalii Sh. Bilioni 34.985

Nilibaini kuwa Sh. Bilioni 6.875 zililipwa kutoka kwenye Mfuko wa Tozo ya Maendeleo ya Utalii bila ya idhini ya Afisa Masuuli kinyume na Kanuni za fedha. Pamoja na haya, nilibaini matumizi ya jumla ya Sh. Bilioni 16.363 bila ya kuwa na Hati za Malipo. Pia, yalibainika matumizi mengine ya jumla ya Sh. Bilioni 11.157 ambayo hayakuwa na nyaraka toshelezi. Halikadhalika, Sh. Milioni 89 zilitumiwa na Makumbusho ya Taifa matumizi yasiyoendana na shughuli za utalii.

Pia, ukaguzi wangu ulibaini kuwa kiasi cha Sh. Milioni 500 kililipwa na Shirika la Hifadhi la Taifa (TANAPA) moja kwa moja kwa Bodi ya Utalii ya Taifa bila kupitia kwenye akaunti ya Tozo za Maendeleo ya Utalii. Hii ni kinyume na Kanuni ya 9 (1) na (2) ya Kanuni za Tozo za Maendeleo ya Utalii za mwaka 2013.

Aidha, nilibaini kuwa hadi kipindi cha ukaguzi, Kamati ya Ushauri ya Mfuko haikuwa imeundwa, kinyume na Kanuni Na. 9 (3) na 9 (4) (a-g) ya Kanuni za Tozo za Maendeleo ya Utalii za mwaka 2013. Mapungufu hayo yanaonesha kuwa, akaunti ya Tozo hizo haikusimamiwa ipasavyo na Mkurugenzi wa Utalii na Mhasibu ambapo walitoa fedha bila ya idhini ya Kamati ya Ushauri na Afisa Masuuli wa Wizara kufahamishwa.

Kwa maoni yangu, Mkurugenzi wa Utalii na Mhasibu waliokuwa wanahusika na usimamizi wa Mfuko wa Makusanyo ya Tozo za Maendeleo ya utalii walitumia vibaya fedha za tozo za utalii jumla ya Sh. bilioni 34.98 kinyume na Kanuni ya Tozo za Maendeleo ya Utalii za mwaka 2013.

Mapungufu katika Uanzishwaji na Uendeshaji wa Tamasha la Urithi – Sh. Bilioni 2.09

Katika Ukaguzi wangu wa Tamasha la Urithi ili kukuza utalii na urithi wa kitaifa niliambiwa kuwa Kamati iliyoundwa iliidhinisha bajeti ya Sh.1.60 kwa ajili ya utekelezaji wa hafla hiyo. Hata hivyo, bajeti hiyo haikuwasilishwa kwa ajili ya ukaguzi.

Kupitia ukaguzi wangu, nilibaini kuwa hakukuwa na mpango wa utekelezaji wa Tamasha la Urithi. Kutokana na kukosekana kwa mpango wa utekelezaji ulioidhinishwa, nilibaini kuwa Wizara ya Maliasili na Utalii iliomba wakala zake nne[2] kuchangia jumla ya Sh. Bilioni moja ambazo hazikuwa kwenye bajeti zao ili kuwezesha kufanyika kwa Tamasha hilo. Ili kuongezea bajeti hiyo, Wizara ya Maliasili na Utalii ilichangia Sh. Milioni 299, na Mfuko wa Tozo wa Maendeleo ya Utalii ulichangia Sh. Milioni 270.84; jumla ya Sh. Bilioni 1.57 zilipatikana ili kufanikisha utekelezaji wa tamasha hilo ambapo fedha zote hizi hazikuwa kwenye bajeti za Wizara na Taasisi husika.
Wakati wa Utekelezaji, nilibaini kuwa Kituo cha televisheni cha Clouds na Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) walilipwa jumla ya Sh. Milioni 629.70 na Sh. Milioni 201.46, mtawalia, kwa ajili ya kuonesha matangazo ya Tamasha la Urithi. Hata hivyo, hakukuwa na risiti za kielektroniki zilizotolewa kuthibitisha kupokelewa kwa malipo hayo.

Aidha, kodi ya zuio ya Sh. milioni 31.49 na Sh. Milioni 10.07 kutoka Kituo cha Televisheni cha Clouds na Shirika la Utangazaji wa Taifa (TBC) haikukatwa katika malipo yaliyofanyika.

Vile vile sikupewa ushahidi unaoonesha kuwa manunuzi ya huduma za matangazo kutoka Shirika la Utangazaji wa Taifa (TBC) na Kituo cha televisheni cha Clouds zilipatikana kwa njia ya ushindani na usawa.

Pia, nilibaini kuwa jumla ya Sh. Milioni 487.26 zilipelekwa kwenye Taasisi saba[3] kwa ajili ya utekelezaji wa Tamasha la Urithi. Hata hivyo, hakukuwa na nyaraka zilizowasilishwa kwa ajili ya ukaguzi ili kuthibitisha matumizi hayo. Kadhalika, nilibaini matumizi ya Sh. Milioni 585.52 yaliyolipwa na Mhasibu wa Mfuko wa Tozo ya Maendeleo ya Utalii bila ya kuwa na nyaraka toshelezi; hivyo, nilishindwa kuthibitisha uhalali na usahihi wa malipo hayo.

Aidha, nilibaini kuwa Wizara ya Maliasili na Utalii ililipa Sh. Milioni 140 kwa Kampuni ya Wasafi kwa ajili ya wasanii ambao wangetangaza Utalii wa ndani katika mikoa sita ya Dar es Salaam, Mwanza, Arusha, Moshi, Iringa, na Dodoma. Hata hivyo, hakukuwa na mkataba wowote uliosainiwa kati ya Kampuni ya Wasafi na Wizara ya Maliasili na Utalii. Hivyo, sikuweza kuhakiki wigo wa kazi pamoja na huduma zilizotolewa na kampuni ya Wasafi.

Pia, kulikuwa na maagizo ya Waziri wa Maliasili na Utalii yakielekeza malipo kwa Kampuni ya Wasafi. Katika mahojiano na Waziri huyo, alikiri kuwa Kampuni ya Wasafi iliomba zabuni ya kutangaza tamasha hilo kwenye mikoa iliyotajwa na kutoa maagizo ya kufanya malipo hayo. Ni maoni yangu kuwa, kiasi cha Sh. Milioni 140 kilicholipwa kwa kampuni ya Wasafi kufuatia maelekezo ya Waziri wa Maliasili na Utalii hakiendani na Sheria za Matumizi ya Fedha za Umma.

Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (TANAPA) na Mamlaka ya Hifadhi Ngorongoro (NCAA) Zilifadhili Tamasha la Upandaji wa Mlima Kilimanjaro bila ya Kuwapo Kwenye Bajeti - Sh. 171,998,045

Mnamo tarehe 28 Septemba 2019, Waziri wa Maliasili na Utalii alizindua shindano lililoitwa Kigwangalla Kili Challenge la mwaka 2019 lililolenga kuhamasisha watu kupanda Mlima Kilimanjaro. Shindano hilo lilitumia jumla ya Sh. milioni 172 zilizotolewa na NCAA (Sh. Milioni 114.50) na TANAPA (Sh. Milioni 57.50) bila kuwa katika bajeti zao za Mwaka wa Fedha 2019/20. Pia, nilibaini kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, kupitia kaimu Katibu wake, alizielekeza NCAA na TANAPA kufadhili shindano hilo.

Fedha iliyotolewa na TANAPA ililipwa kwa Kampuni ya Utalii ya Ahsante Tours and Safaris Sh. 57,498,045 kwa ajili ya gharama za malazi za wapandaji mlima. Hata hivyo, hakukuwa na ushahidi ulioonesha kuwa Kampuni ya Ahsante Tours and Safaris ilipewa kazi hiyo kwa njia ya ushindani. Pia, hakukuwa na mkataba wa kazi hiyo uliowasilishwa kwa ajili ya ukaguzi.

Ni maoni yangu kuwa, maagizo yaliyotolewa na Waziri kupitia Katibu wake yalikiuka Sheria ya fedha za Umma na Kanuni za Maadili za Utumishi wa Umma. Maagizo haya yalisababisha TANAPA na NCAA kutumia Sh. Milioni 172 nje ya bajeti iliyoidhinishwa. Ufadhili wa shindano hili umepunguza utekelezaji wa shughuli za TANAPA na NCAA ambazo zilikuwa zimetengwa kwenye bajeti kwa maslahi ya umma.

Matumizi ya Ofisi ya Waziri Kugharamiwa na Mamlaka ya Hifadhi Ngorongoro (NCAA) na Wakala wa Huduma za Misitu (TFS) Kupitia Maagizo Sh. Milioni 148.23

Nilibaini kuwa, Kaimu Katibu wa Waziri wa Maliasili na Utalii alitoa maagizo kwa Mamlaka ya Hifadhi Ngorongoro (NCAA) na Wakala wa Huduma za Misitu (TFS) kulipia matumizi ya Ofisi ya Waziri Sh. Milioni 92.30 na Sh. Milioni 55.93 kwa niaba ya Wizara ya Maliasili na Utalii, mtawalia. Taasisi hizo hazikuwa na bajeti ya malipo hayo; na ukaguzi wangu ulibaini baadhi ya shughuli za taasisi zilizowekwa katika mipango yao hazikutekelezwa.

c) Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi

Ndugu Wanahabari,​

Nilifanya ukaguzi maalumu ndani ya Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi na kubaini mapungufu yafuatayo:

Fedha kwa Ajili Upangaji wa Ardhi Zilizotumika Kinyume na Malengo - Sh. Milioni 69.04

Ukaguzi wangu ulibaini kuwa Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi ilifadhili matumizi ya mkutano wa Bodi ya Mkurugenzi kwa gharama ya Sh. 69,041,415.46 kutoka kwenye fedha zilizotolewa na Ofisi ya Makamu wa Rais ili kutekeleza shughuli za upangaji matumizi ya ardhi katika wilaya za Nyasa, Mbinga, Ludewa, Makete na Kyela. Shughuli za upangaji na matumizi ya ardhi katika wilaya zilizotajwa hazikufanyika hadi wakati wa ukaguzi wangu mnamo mwezi Mei 2020; na Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi haijarejesha fedha hizo.

Mapungufu Yaliyoibuliwa Kwenye Usimamizi wa Mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) - Sh. Milioni 19.77

Wakati wa utekelezaji wa mipango ya ardhi inayohusiana na Mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP), nilibaini kuwa mmoja wa maafisa wa Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi alitumia jumla ya Sh. 5,630,000 ambazo hazikuwa kwenye bajeti. Pia, Sh. 5,580,000 zilitumika zaidi ya bajeti iliyoidhinishwa na mmoja wa maafisa bila idhini ya Mkurugenzi Mkuu. Pia, nilibaini kuwa kiasi cha Sh. 8,560,000 kilichukuliwa na mmoja wa wafanyakazi wa Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi kwa kutekeleza shughuli za upangaji wa matumizi ya ardhi katika vijiji kumi[4] vya Wilaya ya Chato kwa kudanganya idadi ya siku zinazostahili kulipwa kwa walengwa waliohudhuria mafunzo.

Mapungufu Yanayohusiana na kughushi Nyaraka za Malipo Sh. Milioni 160.78

Ukaguzi wangu ulibaini yafuatayo kuhusiana na kughushi nyaraka za malipo: mmoja wa maafisa alighushi mihuri ya Wenyeviti watano[5] wa vijiji na Aaafisa Kata wa Mkoa wa Singida na kujipatia kiasi cha Sh. milioni 12.81. Afisa mwingine alijipatia kiasi cha Sh. Milioni 16.84 kwa kudanganya tarakimu za malipo kwenye hati za malipo za vijiji vitatu[6] vya Wilaya ya Magu. Afisa mmoja alibadilisha kiasi na siku za malipo na kudanganya idadi ya walengwa wanaostahili kulipwa na kujipatia Sh. milioni 16.27 katika vijiji vitano[7] vya Wilaya ya Mkalama na kijiji cha Sigili wilayani Nzega. Afisa mwingine katika Wilaya ya Igunga alighushi siku za malipo na kujipatia Sh.

milioni 7.12; na afisa mwingine huko Uvinza alighushi majina ya walengwa, saini, pamoja na siku zao za malipo na kujipatia Sh. Milioni 7.93 kinyume cha sheria.

Pia, nilibaini kuwa maafisa sita katika wilaya saba[8] walighushi saini za walengwa na kujipatia jumla ya Sh. Milioni 38.16. Pia, nilibaini ushirikano kati ya wafanyakazi wanne kutoka Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi, mmoja kutoka Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) na wawili kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba, na Maendeleo ya Makazi ambao walidanganya siku za malipo na kujipatia kiasi cha Sh. Milioni 61.65 huko Wilaya ya Kondoa, Kiteto, Muheza, Handeni, Makete, Nyasa, Mbinga na Uvinza.

Mapungufu Yanayohusu Uwasilishaji wa Stakabadhi za Udanganyifu - Sh. 88,280,060

Wakati wa kukagua uhalali wa Hati za Masurufu, nilibaini kuwa stakabadhi kutoka kwa wauzaji wa mbao za matangazo zilighushiwa na maafisa sita na kujipatia jumla ya Sh. 44,122,000 katika wilaya saba[9]. Zaidi ya hayo, afisa mmoja katika Wilaya za Uvinza aliwasilisha stakabadhi za nyumba za kulala wageni zilizokuwa za udanganyifu na kujipatia kiasi cha Sh. 1,230,000, kinyume cha sheria.

Pia, nilibaini kuwa stakabadhi za huduma ya kunakili nyaraka za Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi zilighushiwa na maafisa wawili katika Wilaya za Muleba na Misenyi na kujipatia Sh. 3,853,500. Kadhalika, nilibaini kuwa, afisa mmoja aliwasilisha stakabadhi za kughushi za gari lililokodiwa katika Wilaya ya Mbinga na kujipatia kiasi cha Sh. 3,200,000. Vilevile, nilibaini maafisa tisa wa Tume walighushi stakabadhi za kielektroniki na kujipatia sh. 35,874,560.

5.2 MATOKEO YA UKAGUZI WA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA

5.2.1 Masuala Mtambuka

Ndugu Wanahabari,

Katika ukaguzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa nilibaini mapungufu yafuatayo:

Mapato Yaliyokusanywa Lakini Hayakupelekwa Benki - Sh. Bilioni 18.769

Nilipitia taarifa za makusanyo za Mamlaka za Serikali za Mitaa 135 na kubaini kuwa Sh. bilioni 18.769 (Jedwali hapa chini) zilikusanywa kutoka vyanzo mbalimbali, hata hivyo hakuna ushahidi unaoonesha kuwa kiasi hicho kiliwasilishwa benki. Hii inaashiria usimamizi hafifu wa mapato. Kutopatikana kwa nyaraka zinazoonesha mapato yaliyokusanywa yalipelekwa benki kulinizuia kujiridhisha kuhusu uhalali, usahihi na ukamilifu wa kiasi cha mapato kilichokusanywa na kuwekwa kwenye taarifa za fedha za halmashauri husika.

MAPATO YALIYOKUSANYWA LAKINI HAYAKUPELEKWA BENKI

Na. Jina la Halmashauri
Kiasi (Sh)
Na.
Jina la Halmashauri
Kiasi (Sh)
1
H/MJ Mbulu
2,039,000​
69​
H/W Buchosa
56,811,384​
2
H/W Kigoma
2,583,094​
70​
H/W Buhigwe
57,156,802​
3
H/W Korogwe
2,942,726​
71​
H/W Uvinza
59,597,985​
4
H/M Bukoba
3,528,974​
72​
H/W Kilolo
63,989,470​
5
H/W Mpimbwe
3,775,716​
73​
H/W Kibondo
66,706,739​
6
H/W Nachingwea
4,122,000​
74​
H/M Singida
67,232,600​
7
H/W Mkalama
4,187,000​
H/W Namtumbo
68,991,361​
8
H/W Rombo
4,202,800​
76​
H/M Moshi
70,789,850​
9
H/W Karatu
4,442,000​
77​
H/W Rungwe
72,318,800​
10
H/M Tabora
5,142,393​
78​
H/W Nsimbo
74,600,882​
11
H/M Kigamboni
5,570,100​
79​
H/MJ Tarime
76,920,602​
12
H/J Tanga
5,632,008​
80​
H/W Serengeti
78,731,287​
13
H/W Bukoba
5,830,150​
81​
H/W Ushetu
79,264,500​
14
H/W Babati
6,044,900​
82​
H/W Itilima
80,342,191​
15
H/MJ Nanyamba
6,253,002​
83​
H/W Muheza
81,818,843​
16
H/W Ngorongoro
7,065,000​
84​
H/W Chato
82,377,623​
17
H/W Tandahimba
7,693,860​
85​
H/M Ubungo
89,950,589​
18
H/W Ikungi
8,010,700​
86​
H/MJ Mbinga
90,282,275​
19
H/MJ Kasulu
8,040,838​
87​
H/W Karagwe
93,363,635​
20
H/W Gairo
10,581,240​
88​
H/W Kibaha
95,280,180​
21
H/W Simanjiro
11,034,900​
89​
H/W Musoma
95,315,392​
22
H/W Singida
11,399,119​
90​
H/W Madaba
96,075,740​
23
H/W Mkuranga
11,919,312​
91​
H/MJ Newala
96,902,738​
24
H/W Same
12,484,755​
92​
H/W Chalinze
103,867,866​
25
H/W Hai
13,921,175​
93​
H/W Arusha
104,301,097​
26
H/W Kondoa
14,461,300​
94​
H/W Ngara
108,235,400​
27
H/MJ Korogwe
16,722,600​
95​
H/W Kasulu
112,729,941​
28
H/W Rorya
16,873,547​
96​
H/W Kyela
112,922,112​
29
H/W Mwanga
17,787,295​
97​
H/MJ Ifakara
114,871,590​
30
H/W Tarime
20,143,338​
98​
H/W Bunda
117,655,791​
31
H/W Ruangwa
20,188,465​
99​
H/W Chunya
118,295,759​
32
H/J Mbeya
21,993,806​
100​
H/W Siha
123,494,150​
33
H/W Kyerwa
22,896,527​
101​
H/M Kinondoni
124,319,563​
34
H/W Muleba
24,800,765​
102​
H/W Sikonge
125,460,990​
35
H/M Morogoro
27,323,045​
103​
H/W Chamwino
126,060,358​
36
H/MJ Masasi
27,588,206​
104​
H/W Nyang’hwale
130,219,000​
37
H/W Igunga
28,671,260​
105​
H/MJ Bariadi
152,226,864​
38
H/W Manyoni
28,780,724​
106​
H/W Mbarali
152,299,380​
39
H/W Kwimba
28,802,113​
107​
H/W Mbeya
156,468,750​
40
H/W Bagamoyo
28,915,500​
108​
H/W Sumbawanga
159,395,414​
41
H/W Moshi
29,985,933​
109​
H/W Kilindi
167,571,047​
42
H/W Handeni
30,699,961​
110​
H/W Iramba
177,252,941​
43
H/W Mufindi
32,056,375​
111​
H/W Kalambo
177,307,200​
44
H/W Geita
32,133,993​
112​
H/W Kaliua
184,222,913​
45
H/W Monduli
32,861,911​
113​
H/W Bariadi
196,661,100​
46
H/W Nkasi
33,669,060​
114​
H/MJ Ilemela H/M
215,299,798​
47
H/W Nzega
33,807,975​
115​
Kahama
227,862,083​
48
H/W Longido
34,350,445​
116​
H/W Kilwa
230,105,631​
49
H/M Mpanda
37,568,100​
117​
H/W Butiama
237,671,385​
50
H/W Nyasa
38,069,529​
118​
H/W Mafia
274,588,634​
51
H/W Ludewa
41,213,594​
119​
H/M Lindi
332,552,737​
52
H/W Msalala
41,881,908​
120​
H/M Temeke
334,526,813​
53
H/W Kishapu
42,356,544​
121​
H/M Shinyanga
355,076,958​
54
H/W Mbinga
42,643,923​
122​
H/W Bahi
364,107,100​
55
H/W Itigi
43,099,712​
123​
H/W Uyui
383,433,317​
56
H/W Maswa
43,290,704​
124​
H/W Sengerema
414,149,569​
57
H/W Ileje
44,382,926​
125​
H/W Ukerewe
421,774,882​
58
H/W Misungwi
45,451,550​
126​
H/W Kongwa
478,264,480​
59
H/W Busega
45,970,521​
127​
H/M Kigoma/Ujiji
484,390,575​
60
H/W Mkinga
47,117,423​
128​
H/W Biharamulo
497,080,570​
61
H/W Meru
48,161,880​
129​
H/W Chemba
583,877,152​
62
H/W Urambo
48,317,356​
130​
H/J Arusha
669,167,891​
63
H/W Kiteto
48,340,250​
131​
H/W Kilosa
692,408,213​
64
H/W Lindi
52,224,929​
132​
H/W Songea
936,662,871​
65
H/W Meatu
52,615,216​
133H/W Missenyi
1,259,017,214​
66
H/W Newala
52,660,314​
134​
H/W Shinyanga
2,625,885,159​
67
H/J Dar es Salaam
26,693,900​
135​
H/W Rufiji
189,249,365​
68
H/W Liwale
105,465,348​
Jumla
18,769,299,624

Mapato Yaliyokusanywa Nje ya Mfumo wa LGRCIS - Sh. Bilioni 1.337

Nilipitia taarifa mbalimbali za ukusanyaji wa mapato katika Halmashauri 22 na kubaini kiasi cha Sh. bilioni 1.34 kilikusanywa kwenye leseni za biashara na vyanzo vinginevyo nje ya mfumo wa mapato kama inavyooneshwa kenye Jedwali hapa chini.

JEDWALI: MAPATO YALIYOKUSANYWA NJE YA MFUMO

Na
Jina la Halmashauri
Kiasi (Sh)
Na
Jina la Halmashauri
Kiasi (Sh.)
1
H/W Wang'ing’ombe
3,981,700​
12​
H/Mji Korogwe
18,534,660​
2
H/W Monduli
5,479,000​
13​
H/W Kishapu
20,668,838​
3
H/W Longido
5,812,500​
14​
H/W Tandahimba
34,578,750​
4
H/W Nanyumbu
7,517,000​
15​
H/W Moshi
34,941,800​
5
H/Mji Kahama
9,054,600​
16​
H/W Rombo
51,115,059​
6
H/W Njombe
10,729,000​
17​
H/W Bunda
55,655,510​
7
H/W Karatu
11,482,413​
18​
H/W Babati
67,344,531​
8
H/W Mbulu
14,154,850​
19​
H/W Kilwa
67,868,700​
9
H/W Musoma
15,056,000​
20​
H/W Msalala
86,594,000​
10
H/M Tabora
16,801,062​
21​
H/M Shinyanga
159,950,750​
11 H/W Mkinga
18,408,000​
22​
H/Jiji Arusha
621,334,869​
Jumla
1,337,063,592
Mapato yanayokusanywa nje ya mfumo yanaweza kutumiwa vibaya na wakusanyaji bila kugundulika kwa kuwa hayaonekani kwenye mfumo hivyo kutoa mianya ya upotevu wa mapato. Pia, makusanyo yanayofanyika nje ya mfumo yanaongeza hatari ya watumishi au wakusanyaji kujihusisha na vitendo vya rushwa na ubadhirifu.

Miamala ya Sh. Bilioni 4.792 Iliyofutwa Kwenye Mfumo wa Mapato bila kuwa na Viambatisho Muhimu

Nilipitia marekebisho ya miamala kwenye mfumo wa mapato katika halmashauri 35 na kubaini kuwa kiasi cha Sh. 4,792,502,078 kilifutwa kwenye mfumo bila kuambatishwa nyaraka muhimu za marekebisho hayo; na wakati mwingine marekebisho hayo hayakuidhinishwa na Mweka Hazina au Afisa Masuuli, kinyume na Agizo la 37(6) la Randama ya Fedha za Serikali za Mitaa ya Mwaka 2009.

Miamala iliyofutwa kwenye mfumo wa mapato bila kuwa na viambatisho inaoneshwa katika Jedwali hapa chini.

Na. Jina la Halmashauri
Kiasi (Sh.)
Na. Jina la Halmashauri
Kiasi (Sh.)
1 H/W Tunduru
1,210,981,227​
19H/M Sumbawanga
45,478,900​
2 H/W Siha
624,153,964​
20H/W Urambo
36,613,598​
3 H/W Nanyumbu
497,991,938​
21H/W Kilolo
34,754,281​
4 H/W Kilindi
320,033,902​
22H/W Ruangwa
32,379,700​
5 H/W Kasulu
297,066,660​
23H/M Kigoma-Ujiji
31,301,318​
6 H/W Liwale
258,737,465​
24H/MJI Kasulu
28,696,931​
7 H/W Nyasa
242,833,600​
25H/W Handeni
15,562,504​
8 H/W Namtumbo
191,935,660​
26H/W Busokelo
14,063,170​
9 H/M Songea
184,370,128​
27H/W Buhigwe
13,681,473​
10 H/M Tabora
149,385,887​
28H/W Shinyanga
12,239,000​
11 H/W Bahi
74,906,064​
29H/W Mpwapwa
10,722,000​
12 H/W Songea
72,464,000​
30H/W Kyela
10,605,558​
13 H/W Mbinga
66,095,877​
31H/JIJI Tanga
10,602,250​
14 H/W Kakonko
64,651,714​
32H/W Mufindi
7,401,250​
15 H/W Bariadi
63,040,546​
33H/W Mbeya
7,067,154​
16 H/W Ulanga
57,933,852​
34H/W Mlimba
4,374,104​
17 H/W Nsimbo
51,352,326​
35H/W Kongwa
3,184,184​
18 H/W Morogoro
45,839,893​
Jumla
4,792,502,078

MIAMALA ILIYOFUTWA KWENYE MFUMO WA MAPATO BILA KUWA NA VIAMBATISHO

Miamala inayofutwa bila kuwepo kwa viambatisho muhimu inaongeza hatari ya kutumika vibaya kwa mapato ya Mamlaka za Serikali za Mitaa, kwa kuwa miamala ya fedha zilizokusanywa kihalali inawezafutwa kwenye mfumo na hatimaye fedha hizo kutumika kwa matumizi yasiyo kusudiwa.

Mapato Ambayo Hayakukusanywa Kutoka Kwenye Vyanzo Mbalimbali - Sh. Bilioni 30.86

Nilipitia taarifa mbalimbali za mapato zinazotokana na Mfumo wa Mapato (LGRCIS) na kubaini kuwa Sh. bilioni 30.86 hazikukusanywa katika Mamlaka ya Serikali za Mitaa 124 kutokana na mauzo ya viwanja, ukodishaji wa vibanda, leseni za biashara, leseni za vileo na vyanzo vingine. Hali hii inaonesha kuwa Halmashauri hazikuwa na ufanisi wa ukusanyaji mapato.

Mapato ya Sh. 179,539,936 Yaliyokusanywa na Kutumika Kabla ya Kupelekwa Benki

Nilipitia taarifa mbalimbali za makusanyo na kubaini kwamba halmashauri 4 zilitumia kiasi cha Sh. 179,539,936 kama marejesho ya fedha zilizotumika kwa shughuli mbalimbali kabla hazijapelekwa benki kinyume na Agizo la 37(3) na (9) la Randama ya Fedha za Serikali za Mitaa ya Mwaka 2009 linalozuia kutumia fedha zilizokusanywa kabla ya kupelekwa benki. Kutumia fedha za mapato ya ndani kabla ya kupeleka benki kunaongeza uwezekano wa fedha hizo kutumika kwa shughuli zisizokusudiwa na hivyo kuongeza hatari ya matumizi mabaya ya fedha za umma. Orodha ya Halmashauri zilizotumia fedha kabla ya kupelekwa benki ni kama zinavyoonekana kwenye Jedwali hapa chini

FEDHA ZA MAPATO YA NDANI ZILIZOTUMIKA KABLA YA KUPELEKWA BENKI

Na. Jina la
Halmashauri
Kiasi (Sh.) Na. Jina la Halmashauri Kiasi (Sh.)
1. H/W Sumbawanga
154,164,250​
3.H/W Masasi
7,174,000​
2. H/W Kaliua
14,048,800​
4.H/W Ngara
4,152,886​
3. Jumla
179,539,936

Mapato ya Sh. Bilioni 2.345 Yaliyokusanywa na Mawakala na Hayakuwasilishwa Serikalini

Nilibaini jumla ya Sh. Bilioni 2.345 zilizokusanywa na mawakala mbalimbali katika Halmashauri 18 hakikuwasilishwa kwenye mamlaka hizo. Kitendo hiki ni kiashiria cha kuwepo kwa ubadhirifu wa mapato hayo. Jedwali hapa chini linaainisha Halmashauri ambazo mawakala hawakuwasilisha fedha.

MAPATO YALIYOKUSANYWA NA MAWAKALA AMBAYO HAYAKUWASILISHWA


Na Jina la Halmashauri Kiasi (Sh.) Na Jina la Halmashauri Kiasi (Sh.)
1 H/W Ushetu
1,440,889,650​
10H/M Iringa
23,860,100​
2 H/Mji Makambako
434,675,164​
11H/M Ilala
22,946,760​
3 H/W Ulanga
100,450,739​
12H/W Tunduru
20,036,054​
4 H/W Igunga
82,339,496​
13H/JIJI Tanga
19,825,264​
5 H/W Muheza
38,467,000​
14H/W Wang'ing’ombe
15,090,445​
6 H/W Hanang’
36,821,538​
15H/M Lindi
12,900,000​
7 H/W Kisarawe
31,090,466​
16H/W Kibiti
7,062,231​
8 H/W Kwimba
28,819,950​
17H/MJI Babati
5,540,000​
9 H/M Shinyanga
23,932,141​
18H/W Babati
1,096,500​
Jumla
2,345,843,498

Mawakala kutowasilisha mapato kwa wakati kunasababishwa na menejimenti za Halmashauri kutokuwa makini katika kuwasimamia mawakala; hali hii inaweza kupelekea upotevu wa fedha za umma.

Miamala ya Sh. Bilioni 35.997 ya Wadaiwa Mbalimbali Ambayo Haijasuluhishwa Kwenye Mfumo

Nilipitia taarifa mbalimbali zinazotokana na mfumo wa ukusanyaji mapato katika halmashauri 67 na kubaini kwamba kiasi cha Sh. bilioni 36 kilikuwa hakijawasilishwa na wadaiwa wanaokusanya mapato kwenye vyanzo mbalimbali. Kuwepo kwa wadaiwa ambao hawajawasilisha mapato kutokana na kutofanya usuluhishi ni kinyume na agizo la 29(2) la Randama ya Fedha za Serikali za Mitaa ya Mwaka 2009 linalomtaka Mweka Hazina kufanya usuluhishi kwa wakati. Jedwali hapa chini linaonesha wadaiwa ambao miamala yao haikusuluhishwa.

WADAIWA MBALIMBALI AMBAO MIAMALA YAO HAIKUSULUHISHWA KWENYE MFUMO

Na.
Jina la
Halmashauri
Kiasi (Sh)
Na.
Jina la
Halmashauri
Kiasi (Sh.)
1​
H/MJI Babati
4,252,890​
35H/W Makete
96,746,893​
2​
H/W Karagwe
6,973,707​
36H/W Hai
105,197,047​
3​
H/MJI Nzega
12,788,114​
37H/W Moshi
110,712,582​
4​
H/W Nsimbo
16,163,297​
38H/Mji Masasi
115,155,297​
5​
H/W Rungwe
18,141,278​
39H/M Ilala
117,456,100​
6​
H/W Korogwe
19,166,330​
40H/W Nzega
124,102,635​
7​
H/W Handeni
19,350,544​
41H/W Nyasa
129,039,498​
8​
H/W Kibiti
21,265,050​
42H/Mji Geita
130,600,847​
9​
H/W Masasi
23,280,251​
43H/W Mpanda
133,001,769​
10​
H/W Longido
24,343,955​
44H/W
Nachingwea
141,841,282​
11​
H/W Pangani
24,827,904​
45H/W Same
150,463,186​
12​
H/W Tandahimba
24,850,534​
46H/W Songea
174,624,200​
13​
H/W Kiteto
26,338,864​
47H/M Morogoro
189,137,940​
14​
H/M Songea
26,615,666​
48H/W Chemba
194,989,020​
15​
H/W Bukombe
28,076,104​
49H/W Simanjiro
197,995,300​
16​
H/Jiji Mbeya
28,137,367​
50H/W Mbozi
214,832,707​
17​
H/W Kasulu
28,193,795​
51H/W Siha
242,747,150​
18​
H/Mji Bariadi
41,014,664​
52H/W Nanyumbu
250,176,085​
19​
H/W Bumbuli
42,786,225​
53H/W Mbogwe
268,490,389​
20​
H/Mji Mafinga
46,060,208​
54H/W Busokelo
289,263,996​
21​
H/W Kilindi
46,591,500​
55H/W
Namtumbo
335,285,397​
22​
H/W Mwanga
49,429,000​
56H/W Morogoro
346,256,817​
23​
H/W Mkinga57H/W Mlele
379,381,653​
24​
H/W Newala
60,626,199​
58H/Jiji Arusha
516,009,298​
25​
H/W Iringa
64,316,266​
59H/Mji Ifakara
522,221,823​
26​
H/W Muheza
64,892,351​
60H/W Meru
552,430,585​
27​
H/Mji Handeni
67,068,042​
61H/M Iringa
577,618,675​
28​
H/W Busega
70,822,000​
62H/W Momba
583,092,186​
29​
H/W Mvomero
75,362,396​
63H/M Mpanda
620,189,563​
30​
H/Mji Tunduma
82,774,602​
64H/Mji Korogwe
647,221,005​
31​
H/W Mbinga
84,419,482​
65H/W Mlimba
788,658,256​
32​
H/W Gairo
89,610,516​
66H/W Hanang’
1,045,646,733​
33​
H/W Maswa
91,198,412​
67H/Jiji Dar es
Salaam
24,225,812,741​
34​
H/M Moshi
94,712,000​
Jumla
35,997,956,890
Mamlaka za Serikali za Mitaa zilishindwa kufikia lengo la ukusanyaji wa mapato kutokana na kushindwa kukusanya kiasi ambacho kilichokuwa kwa wadaiwa ambao miamala yao ilikuwa haijasuluhishwa, hivyo kushindwa kutekeleza shughuli mbalimbali zilizokuwa zimepangwa. Pia, uwepo wa mapato yasiyowasilishwa kutokana na kutofanya usuluhishi kunaongeza hatari ya wakusanya mapato wasio waaminifu kutumia vibaya kiasi kilichokusanywa.

Mikopo Iliyotolewa kwa Vikundi vya Wanawake, Vijana na Watu Wenye Ulemavu Isiyorejeshwa - Sh. Bilioni 27.790

Nilikagua mikopo iliyotolewa kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kwa mwaka wa fedha ulioishia 30 June 2020 katika Halmashauri 130 na kubaini mikopo kiasi cha Sh. bilioni 27.790 bado hakijarejeshwa. Hii inaonesha kwamba Halmashauri husika hazikufuatilia kwa ukaribu marejesho ya mikopo kutoka kwa vikundi kulingana na makubaliano. Orodha ya halmashauri zenye mikopo ambayo haijarejeshwa zinaoneshwa katika Kiambatisho Na. 4.

Fedha za Mapato ya Ndani Sh. Bilioni 33.96 Hazikupelekwa Kwenye Miradi ya Maendeleo

Tathmini yangu ya ulinganisho wa bajeti na kiasi halisi cha matumizi ya maendeleo umebaini Mamlaka 95 za Serikali za Mitaa zilikusanya mapato ya ndani kiasi cha Sh. bilioni 200.99, hivyo jumla ya Sh. bilioni 93.22 (sawa na asilimia 40 hadi 60) zilipaswa kupelekwa kwenye miradi ya maendeleo. Hata hivyo, kiasi cha Sh. bilioni 59.26 tu ndicho kilichohamishiwa kwenye akaunti za maendeleo kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo na kuacha kiasi cha Sh. bilioni 33.96. Mamlaka tatu za Serikali za Mitaa hazikuweza kabisa kupeleka fedha za mapato ya ndani kwenye miradi ya maendeleo kwa asilimia 100 na zingine 41 kati ya 95 zilipeleka chini ya asilimia 50.

Malipo Yenye Thamani ya Sh. Bilioni 5.54 Yasiyoambatishwa Risiti za Kielekitroniki

Kinyume na Kanuni ya 55(1) ya Kanuni za Usimamizi wa Kodi (za jumla) za Mwaka 2016, nimebaini kuwa halmashauri 58 zimeshindwa kuwasilisha risiti za kielekitroniki baada ya kuzitaka kuonesha risiti za manunuzi yenye jumla ya Sh. bilioni 5.54 kama inavyoainishwa kwenye Jedwali hapa chini. Tabia hii inachochea wafanyabiashara kukwepa kodi na kupelekea ukusanyaji mdogo wa mapato ya Serikali.

MALIPO YASIYO AMBATISHWA RISITI ZA KIELEKITRONIKI​

Na. Halmashauri Kiasi (Sh.) Na Halmashauri
Kiasi (Sh.)
1H/W Babati
35,557,530​
30H/W Mkalama
198,762,039​
2H/W Buhigwe
37,375,000​
31H/W Moshi
14,381,980​
3H/W Bumbuli
158,747,346​
32H/M Moshi
16,956,132​
4H/W Busokelo
36,584,255​
33H/M Mtwara-Mikindani
2,704,525​
5H/W Chamwino
36,274,700​
34H/W Mwanga
9,444,170​
6H/W Chunya
28,707,656​
35H/Jiji Mwanza
252,310,826​
7H/Mji Ifakara
18,642,714​
36H/W Namtumbo
175,396,368​
8H/W Igunga
5,856,500​
37H/Mji Nanyamba
3,472,400​
9H/W Ileje
19,935,938​
38H/W Ngorongoro
4,619,000​
10H/W Iramba
18,650,288​
39H/W Nkasi
122,694,353​
11H/W Itigi
10,713,906​
40H/W Nzega
13,838,600​
12H/W Kalambo
112,031,331​
41H/Mji Nzega
5,629,700​
13H/W Kaliua
93,372,900​
42H/W Pangani
25,613,938​
14H/W Karagwe
127,967,000​
43H/W Rombo
97,318,156​
15H/W Kibaha
50,617,999​
44H/W Rufiji
5,055,300​
16H/Mji Kibaha
22,384,823​
45H/W Sengerema
20,406,035​
17H/W Kigoma
4,929,753​
46H/W Serengeti
22,755,204​
18Kigoma-Ujiji
38,712,984​
47H/W Shinyanga
5,304,000​
19H/W Kilindi
95,018,508​
48H/W Siha
134,829,471​
20H/M Kinondoni
193,647,400​
49H/W Sikonge
138,850,356​
21H/W Kisarawe
71,095,816​
50H/W Songwe
133,358,224​
22H/W Kiteto
28,171,302​
51H/M Tabora
64,669,135​
23H/W Kondoa
26,750,489​
52H/Jiji Tanga
40,158,654​
24H/W Korogwe
159,160,760​
53H/W Tarime
59,677,648​
25H/Mji Korogwe
28,870,178​
54H/W Tunduru
31,984,103​
26H/W Lushoto
33,070,000​
55H/W Ukerewe
89,634,542​
27H/W Mbozi
20,350,683​
56H/W Ushetu
1,409,688,866​
28H/W Mbulu
10,330,000​
57H/W Uyui
33,262,338​
29H/Mji Mbulu
64,661,496​
58H/W Wanging’ombe
820,194,149​
Jumla
5,541,159,468


Malipo ya Bidhaa, Kazi au Huduma Zenye Thamani ya Sh. Bilioni 1.561 Ambazo Hazikupokelewa

Kinyume na Kanuni iliyotajwa hapo juu, nilibaini kuwa halmashauri 24 zililipa Sh. bilioni 1.561 kwa manunuzi ya bidhaa, lakini bidhaa hizo hazikuwa zimepokelewa na halmashauri husika. Orodha ya halmashauri na thamani ya bidhaa ambazo hazikupokelewa zinaoneshwa kwenye Jedwali hapa chini

ORODHA YA HALMASHAURI ZENYE MALIPO KWA BIDHAA AMBAZO HAZIKUPOKELEWA​

Na.
Jina la
Halmashauri
Kiasi (Sh.)
Na. Jina la Halmashauri
Kiasi (Sh.)
1. H/W Tarime
366,512,812​
2.H/M Kinondoni
48,620,725​
14.H/W Nyasa
42,335,036​
3.H/M
Sumbawanga
24,562,000​
15.H/W Sengerema
106,219,293​
4.H/W Chamwino
36,397,500​
H/W Karatu
40,313,638​
5.H/Mji Kibaha
387,757,726​
17.H/Jiji Dodoma
9,875,000​
6.H/W Itigi
10,776,760​
18.H/W Mkalama
46,256,000​
7.H/W Nkasi
2,090,000​
19.H/W Iringa
12,738,214​
8.H/W Mpwapwa
9,948,799​
20.H/Mji Nanyamba
109,462,960​
9.H/M Bukoba
20,000,000​
21.H/W Kasulu
20,499,000​
10.H/W Igunga
12,251,500​
22.H/W Hanang’
68,777,094​
11.H/W Uyui
14,851,766​
23.H/Mji Makambako
74,182,872​
12.H/W Kakonko
42,421,456​
24.H/M Morogoro
46,055,250​
13.H/W Mbogwe
8,405,000​
Jumla
1,561,310,401


Miamala Yenye Viashiria vya Udanganyifu ya Thamani ya Sh. Milioni 614.505

Miamala ya kidanganyifu ni ile inayosababisha upotevu wa fedha za umma ama kwa malipo hewa, miamala isiyo ya kweli, au kwa ufujaji wa mapato yaliyokusanywa. Ukaguzi uliofanyika kwenye malipo kwa wadai mbalimbali na makusanyo ya mapato kwa mwaka huu wa ukaguzi ulibaini malipo na makusanyo yenye viashiria vya udanganyifu yenye thamani ya Sh. Milioni 614.51 kwenye Halmasahuri za Wilaya tisa kama inavyooneshwa kwenye Jedwali hapa chini

MIAMALA YENYE VIASHIRIA VYA UDANGANYIFU​

Na Halmashauri Maelezo ya Muamala
Kiasi (Sh.)
1.
H/W NkasiManunuzi yenye udanganyifu ya vifaa vya ujenzi vya hospitali ya wilaya
21,557,000​
Marekebisho ya gharama kwenye nukuu ya bei na hati ya madai yenye udanganyifu
2,220,000​
2.
H/W BuhigweManunuzi yaliyoambatishwa stakabadhi za kielekitroniki zenye kutia shaka
34,720,000​
3.
H/W KakonkoUfujaji wa mapato yaliyokusanywa
31,493,000​
Malipo ya mishahara yenye shaka kwa wakusanya mapato56,126,092
4.
H/M TaboraMiamala yenye shaka inayohusisha kughushi kumbukumbu za kihasibu
40,014,591​
Fedha zilizorejeshwa kutoka kwenye malipo ya madiwani ambazo hazijawekwa benki6,790,000
5.
H/W KorogweWizi wa vifaa vya ujenzi wa hospitali ya wilaya
12,757,910​
6.
H/W MbingaWizi wa mapato yaliyokusanywa
270,046,700​
7.
H/W MuhezaStakabadhi za kielekitroniki zenye udanganyifu zilizotolewa na wazabuni
123,817,600​
8.
H/W LongidoUpotevu wa mapato yatokanayo na leseni za biashara
2,970,000​
9.
H/W
Mvomero
Wizi wa dawa, vifaatiba na vifaa vya ofisi
11,992,670​
Jumla
614,505,563
Miamala hii imefanyika kutokana na udhaifu katika udhibiti wa ndani wa halmashauri na halmashauri husika kushindwa kufanya tathmini ya vihatarishi vya udanganyifu ili kubaini na kuzuia kutokea kwake.

Makato ya Mishahara ya Sh. bilioni 5.079 ambayo Hayajawasilishwa Kwenye Taasisi Husika

Nilibaini kuwa Mamlaka 46 za Serikali za Mitaa zilishindwa kuwasilisha jumla ya Sh. bilioni 5.079 za makato ya wafanyakazi katika taasisi husika. Miongoni mwa fedha ambazo hazikuwasilishwa ni Sh. bilioni 3.919 za mifuko ya hifadhi ya jamii.

Hali hii ya kutowasilisha makato haya ya mishahara kwa wakati imepelekea Serikali kupata hasara ya kulipa riba inayofikia kiasi cha Sh. bilion 2.76 katika Mamlaka 7 za Serikali za Mitaa. Kwa maoni yangu, fedha hizi zingeweza kutekeleza miradi au huduma zingine kwa manufaa ya umma. Jedwali hapa chini linaonesha muhtasari wa kiasi ambacho hakijawasilishwa hadi kufikia Juni 2020.

MAKATO YA MISHAHARA YA THAMANI YA SH. BILIONI 5.079 AMBAYO HAYAKUWASILISHWA KWA TAASISI HUSIKA

Jina la Taasisi
Kiasi (Sh.)
Mamlaka ya Mapato Tanzania
149,872,690​
Mifuko ya Hifadhi ya Jamii
3,919,411,819​
Makato mengine
1,010,660,933​
Jumla
5,079,945,442
Sambamba na hilo, Halmashauri ya Jiji la Dodoma haikuwakata wachezaji 40 wa timu yake ya mpira wa miguu kiasi cha Sh. 13,617,700 ikiwa ni kodi ya mapato kutoka katika mishahara yao. Hali hii imesababisha upotevu wa mapato ya Serikali.

Miradi Ambayo Haikukamilika Sh. Bilioni 184.006

Nilibaini miradi mbalimbali isiyokamilika yenye thamani ya Sh. bilioni 184.006 katika Halmashauri 101. Hii ilisababishwa na kutolewa kwa fedha pungufu za miradi, usimamizi na ufuatiliaji usioridhisha wa menejimenti za Halmashauri, kutelekezwa kwa miradi kwa muda mrefu pamoja na ushiriki usiotosheleza wa jamii katika utekelezaji wa shughuli za miradi. Hali hii inapelekea upotevu wa fedha za umma na jamii kutokupata manufaa yaliyokusudiwa. Maelezo ya Halmashauri zenye miradi ambayo haijakamilika yanaonyeshwa katika Kiambatisho Na. 1.

Kutokamilika kwa miradi husika kwa wakati kunaweza kupelekea ongezeko la bei za vifaa vya ujenzi kutokana na madhara ya mfumuko wa bei; na jamii zinazolengwa kuchelewa kunufaika na huduma kwa wakati kama ilivyokusudiwa.

Miradi Ambayo Haikutekelezwa Sh. Bilioni 14.903

Nilibaini utekelezaji wa miradi yenye thamani ya Sh. bilioni 10.550 katika Mamlaka za Serikali za Mitaa 26 kutoanza kwa wakati licha ya uwepo wa fedha za utekelezaji wa miradi husika. Kutotekelezwa kwa miradi kulisababishwa na ucheleweshwaji wa fedha ambazo zilitolewa kati ya tarehe 26 na 30 Juni 2020 ambapo ulikuwa ni mwisho wa mwaka wa fedha.

Aidha, kazi zilizopangwa kutekelezwa kwenye Halmashauri 6 zenye thamani ya Sh. bilioni 4.353 hazikutekelezwa kutokana na kutotolewa kwa fedha na Hazina. Halmashauri ambazo hazikutekeleza miradi zinaoneshwa katika Kiambatisho Na. 2.

Hali hii inaashiria kutofikiwa kwa malengo hivyo kupelekea halmashauri kushindwa kutimiza majukumu yake ya kutoa huduma kwa wananchi.

Miradi Iliyokamilika Lakini Haitumiki Sh. Bilioni 18.328

Wakati wa ukaguzi, nilibaini miradi iliyokamilika yenye thamani ya Sh. bilioni 18.328 katika Halmashauri 40 lakini haikuwa ikitumika kama ilivyokusudiwa. Hii inaonesha kuwa thamani ya fedha za miradi husika haipatikani na kuna hatari ya kuharibika kwa miradi hiyo. Ufafanuzi zaidi unatolewa katika kiambatisho Na. 3.

Mikataba yenye Thamani ya Sh. Bilioni 25.561 Haikufanyiwa Upekuzi wa Kisheria

Nimebaini mikataba minne katika halmashauri tatu ambayo haikufanyiwa upekuzi na mikataba miwili katika Halmashauri ya Mji Makambako na Halmashauri ya Wilaya ya Wanging'ombe ambayo ilipekuliwa kabla ya mwajiri kukubali ofa ya wakandarasi. Mapungufu yaliyobainika katika upekuzi wa mikataba yanaoneshwa kwenye Jedwali hapa chini.

MAPUNGUFU YALIYOBAINIKA KATIKA UPEKUZI WA MIKATABA

Halmashauri
Jina la Mradi
Namba ya Mkataba
Gharama ya Mkataba (Sh.)
Mapungufu
H/W MpandaUjenzi wa mradi wa
kusambaza maji katika Kijiji cha
Kabungu
LGA.099/2017
/2018/W/WAT
ER/02/Lot 1
634,810,489​
Haukupekuliwa na
Mwanasheria wa Halmashauri
H/W KigomaUjenzi wa mradi wa
kusambaza maji katika Vijiji vya
Kaseke,
Kimbwela na
Nyamoli
LGA/043/2016 /2017/W/15
1,163,496,000​
Haukupekuliwa na
Mwanasheria
Mkuu wa
Serikali.
H/W
Wanging'ombe
Ujenzi wa mradi wa maji wa Igando-
Kijombe
LGA/153/2017 /2018/W/01
12,437,407,360​
Mikataba
ilipekuliwa
kabla ya
halmashauri mkandarasi kukubaliwa ofa
H/W
Makambako
Ujenzi wa mradi wa
kusambaza
maji wa
UsetuleMahongole
LGA/166/2018 /2019/W/01
7,996,231,305​
H/W
Mkuranga
Ujenzi wa mradi wa maji MwanambayaLGA/012/WS/
2017/2018/w/
01-02
2,347,737,221​
Haukupekuliwa na
Mwanasheria
Mkuu wa
Serikali.
Ujenzi wa mradi wa visima vya maji katika Kijiji cha
Mkerezange
LGA/012/WS/
2017/2018/w/
01-03
981,996,310Haukupekuliwa na mwanasheria wa halmashauri.
Jumla
25,561,678,685
Kwa maoni yangu, kutofanya upekuzi wa mikataba kunaziweka halmashauri katika hatari za kisheria na kunaweza kuhatarisha thamani ya fedha kwa miradi hiyo. Aidha, barua za kukubali ofa ni sehemu ya mikataba hivyo lazima ifanyiwe upekuzi kwa kuwa inahusisha bei ya mkataba baada ya kusahihishwa na masharti mengine kwa mzabuni aliyeshinda kuyatekeleza. Hivyo, inaweza kusababisha wazabuni waliofanikiwa kushindwa kuwajibikaji ipasavyo.

Dosari Zilizojitokeza Zaidi Katika Manunuzi ya Mwaka wa Fedha 2019/20

Nimebaini dosari mbalimbali za manunuzi katika mamlaka za Serikali za Mitaa, kati ya dosari hizo, manunuzi yasiyo na ushindani ndio kasoro inayoongoza ambapo halmashauri 57 zilifanya manunuzi ya Sh. bilioni 9.14 bila ya ushindani wa bei kama zilizoorodheshwa katika Jedwali hapa chini.

Dosari zote zilizoorodheshwa zimejadiliwa katika aya zinazofuata pamoja hatua za marekebisho zilizochukuliwa na Serikali.

DOSARI ZILIZOJITOKEZA ZAIDI KATIKA MANUNUZI YA MWAKA HUU

Na.
Dosari Zilizobainika
Idadi ya H/Shauri
Kiasi (Sh.)
1.Manunuzi yasiyo na ushindani
57​
9,143,192,259​
2.Vifaa vilivyonunuliwa na kupokelewa bila kukaguliwa au kupimwa
44​
3,103,120,807​
3.Manunuzi na tuzo za zabuni bila idhini ya bodi za zabuni
39​
6,948,439,587​
4.Manunuzi kutoka kwa wasambazaji bila mikataba ya makubaliano kutoka Mamlaka ya
Usimamizi wa Manunuzi ya Umma
39​
5,130,195,752​
5.Manunuzi yaliyofanywa kupitia pesa taslimu
24​
752,071,479​
6.Malipo ya bidhaa, kazi au huduma ambazo hazikupokelewa
24​
1,561,310,401​
7.Manunuzi ya bidhaa na huduma bila mkataba mdogo
17​
676,005,295​
8.Manunuzi yaliyofanyika nje ya mpango wa manunuzi wa mwaka ulioidhinishwa na halmashauri
17​
5,012,044,504​
9.Kutowasilisha ripoti za kila mwaka za utekelezaji wa ununuzi kwa PPRA
17​
1,828,187,880​
10.Kununuliwa kwa vifaa zaidi ya mahitaji ya halmashauri
11​
586,458,238​
11.Matengenezo ya magari ambayo hayajapitishwa TEMESA
10​
153,057,506​
12.Nyaraka za manunuzi zinazokosekana kwa ajili ya ukaguzi
9​
3,662,901,212​
Jumla
38,556,984,920

Malipo ya Sh. Bilioni 5.793 Yaliyofanywa Bila ya Vipimo Wala Kuthibitishwa na Wasimamizi wa Miradi

Kanuni ya 243(2) ya Kanuni za Manunuzi ya Umma za Mwaka 2013 inazitaka taasisi kuidhinisha malipo kwa kuzingatia vipimo na kwa vipindi au hatua zilizoelezwa katika mkataba. Hata hivyo, nilibaini katika halmashauri 24 malipo ya kazi za ujenzi zenye thamani ya Sh. bilioni 5.793 yalifanywa bila vipimo wala uthibisho wa mhandisi. Hali hii inaweza kusababisha malipo kwa kazi ambazo hazikufanyika.

ORODHA YA HALMASHAURI ZENYE MALIPO YALIYOFANYWA BILA VIPIMO WALA KUTHIBITISHWA NA WASIMAMIZI WA MIRADI

Na.
Jina la
Halmashauri
Kiasi (Sh.)
Na
.
Jina la
Halmashauri
Kiasi (Sh.)
1.H/M Temeke
2,355,636,382​
2.H/W Itigi
529,171,878​
14.H/W Kalambo
64,896,280​
3.H/W Buchosa
392,897,238​
15.H/W Masasi
61,036,760​
4.H/W Uvinza
353,443,477​
16.H/W Korogwe
39,640,720​
5.H/M Songea
343,980,659​
17.H/Mji Nanyamba
35,295,000​
6.H/W Mlimba
337,500,000​
18.H/M Kinondoni
31,620,171​
7.H/W Chunya
326,843,491​
19.H/W Mpimbwe
30,013,375​
8.H/W Nkasi
175,778,504​
20.H/W Newala
27,914,000​
9.H/W Momba
167,306,900​
21.H/W Bagamoyo
22,426,000​
10.H/Jiji Mbeya
162,000,000​
22.H/M Tabora
12,594,977​
11.H/W Nachingwea
146,340,805​
23.H/W Kakonko
9,504,789​
12.H/M Lindi
94,000,000​
24.H/W Uyui
5,000,000​
13.H/M Sumbawanga
68,777,000​
Jumla
5,793,618,406

Miradi ya Ujenzi yenye Thamani ya Sh. Bilioni 3.458 Haikujumuisha Kwenye Mipango ya Manunuzi ya Mwaka Iliyoidhinishwa

Nilikagua mipango ya mwaka ya manunuzi na kubaini kuwa mikataba miwili yenye thamani ya Sh. bilioni 3.46 haikujumuishwa kwenye mipango ya manunuzi ya mwaka ikimaanisha miradi ilitekelezwa bila mipango. Jedwali hapa chini linaonesha orodha ya miradi iliyotekelezwa ambayo haikuwepo katika mipango ya manunuzi.

MIRADI ILIYOTEKELEZWA AMBAYO HAIKUWEPO KATIKA MIPANGO YA MANUNUZI

Mkoa
Halmashauri
Jina la Mradi
Namba ya Mkataba
Gharama ya Mkataba (Sh.)
RukwaH/W
Sumbawanga
Ujenzi wa bwawa la maji Kijiji cha Ikozi awamu ya IILGA/097/2017/2018 /WS/W/05
2,943,086,780​
GeitaH/W BukombeLGA113/2017/2018/ RWSSP/03 LOT II
514,915,618​
Jumla
3,458,002,398
Kwa maoni yangu, utekelezaji wa miradi isiyopangwa yenye thamani ya Sh. Bilioni 3.46 unaweza kusababisha mchakato mbovu wa manunuzi na matumizi yasiyopangwa. Mbali na hilo, inaweza kusababisha kushindwa kutekeleza miradi iliyopangwa na kutengewa bajeti.

Miradi yenye Thamani ya Sh. Bilioni 23.376 Ilitekelezwa Bila Washauri na Kusababisha Ucheleweshaji wa Huduma ya Maji kwa Jamii

Katika ukaguzi wa majalada ya mikataba ya miradi iliyochaguliwa, nimebaini halmashauri mbili zilitekeleza mikataba mitatu yenye thamani ya Sh. bilioni 23.38. Katika miradi hii, washauri hawakuhusika kuhakiki miundo ya miradi na kusimamia utekelezaji wake. Hali hii ilisababisha kuongezeka kwa muda (miradi ilichukua miezi 19 hadi 30 kutoka miezi 6 hadi 12 iliyopangwa) wa miradi kwa sababu ya kusimamishwa kwa kazi na kushindwa kukabili mabadiliko ya mawanda, wakati, na matokeo kinyume na maagizo. Orodha ya miradi iliyotekelezwa bila washauri inaoneshwa katika Jedwali hapa chini.

MIRADI INAYOTEKELEZWA BILA WASHAURI

Halmashauri
Jina la Mradi
Namba ya Mkataba
Gharama ya Mkataba
(Sh.)
Tarehe ya
Kuanza Na
Kumaliza Ujenzi
H/W
Sumbawanga
Ujenzi wa bwawa la maji Kijiji cha Ikozi awamu ya IILGA/097/20
17/2018/W
S/W/05
2,943,086,780​
02.10.2018 -
01.04.2019
50​
H/W
Wanging'om be
Ujenzi wa mradi wa maji Igando - KijombeLGA/153/20
17/2018/W
/01
12,437,407,360​
09.07.2018 -
08.07.2019
20​
H/M
Makambako
Ujenzi wa mradi wa maji Vijiji vya Usetule na MahongoleLGA/166/20
18/2019/W
/01
7,996,231,305​
23.05 2019 -
22.11.2019
17​
Jumla
23,376,725,445
Kwa maoni yangu, kutekeleza miradi bila washauri kumesababisha kusimama kwa kazi ili kusubiri wataalamu kutoka Wizara ya Maji na Umwagiliaji kwa sababu ya kutokuwepo kwa wataalamu wakati wa utekelezaji wa mradi. Vilevile, imechangia kuchelewesha kukamilika kwa miradi kwa zaidi ya miezi 13 na hivyo kuchelewesha huduma ya maji kwa walengwa.

Kushindwa Kukidhi Mawanda ya Ukaguzi Kutokana na Kukosekana kwa Kumbukumbu za Manunuzi – Sh. Bilioni 3.021

Wakati wa ukaguzi, nilibaini baadhi ya mazingira ambayo yanaonesha udhaifu katika usimamizi wa kumbukumbu za manunuzi ndani ya Mamlaka za Serikali za Mitaa. Udhaifu mkubwa ulionekana hasa katika utunzaji wa kumbukumbu za manunuzi na usimamizi wa mikataba ambapo majalada ya manunuzi na mikataba ilikosa baadhi ya nyaraka muhimu.

Kwa mfano, nilibaini katika halmashauri sita manunuzi yenye thamani ya Sh. bilioni 3.02 yakiwa hayana nyaraka mbalimbali za kuyathibitisha. Kwa maana hiyo, wigo wangu wa ukaguzi ulikuwa mdogo, na sikuweza kuthibitisha uhalali wa manunuzi haya. Orodha ya halmashauri ambazo kumbukumbu za manunuzi zilikosekana inaoneshwa katika Jedwali hapa chini.

HALMASHAURI AMBAZO KUMBUKUMBU ZA MANUNUZI ZILIZOKOSEKANA

Na. Jina la Halmashauri
Kiasi (Sh.)
1.H/W Mlele2,195,082,530
2.H/W Madaba
442,078,923​
3.H/W Tarime
234,144,400​
4.H/M Songea
80,891,880​
5.H/Mji Tunduma
61,311,095​
6.H/W Ushetu
7,200,000​
Jumla 3,020,708,828

Ucheleweshaji wa Nyongeza ya Mishahara na Kupandisha Madaraja

Nilipitia mafaili ya watumishi pamoja na Mfumo wa LAWSON wenye taarifa mbalimbali za watumishi na kubaini watumishi 7,992 katika Mamlaka 14 za Serikali za Mitaa hawakupandishwa madaraja ingawa walikuwa na sifa kwa mujibu wa Kanuni za Kudumu za Utumishi wa Umma kama inavyoonekana kwenye Jedwali hapa chini.

MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA ZENYE UCHELEWESHAJI WA NYONGEZA YA MISHAHARA NA KUPANDISHA MADARAJA


Na.
Jina la Halmashauri
Idadi ya Watumishi
1.H/W Bagamoyo
891​
2.H/W Hai
1,176​
3.H/W Kakonko
18​
4.H/Mji Kasulu
155​
5.H/W Manyoni
10​
6.H/W Mbozi
826​
7.H/W Mbulu
730​
8.H/W Moshi
1,848​
9.H/M Moshi
1,523​
10.H/W Mtwara
34​
11.H/W Newala
164​
12.H/W Siha
590​
13.H/W Singida
22​
14.H/W Ukerewe
5​
Jumla
7,992

Kushindwa kupandisha madaraja na kutoa nyongeza ya mishahara kwa wakati kwa watumishi wa umma husababisha utendaji duni katika utoaji wa huduma na hii huhatarisha nia njema ya Serikali ya kutoa huduma bora kwa wananchi.

Mikopo Iliyopindukia kwa Watumishi bila Kudhibitiwa na Mamlaka za Serikali za Mitaa

Uchambuzi uliofanywa katika Mamlaka 35 za Serikali za Mitaa ulibaini watumishi 3,038 waliokuwa wakipokea chini ya 1/3 ya mishahara yao. Utaratibu huu wa kukopa usiodhibitiwa unaweza kuathiri utendaji wa watumishi na kuathiri utendaji wa jumla wa Mamlaka za Serikali za Mitaa. Aidha, nilibaini kuwa hali hii ilichangiwa na ulipaji wa deni la Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu ambapo mnufaika hukatwa asilimia 15 ya mshahara.

Katika hali isiyo ya kawaida, pia nilibaini watumishi 8 katika Mamlaka 6 za Serikali za Mitaa ambao kila mwisho wa mwezi hawapati kiasi chochote cha mshahara. Mamlaka hizo na idadi ya watumishi ni H/Jiji Arusha (1), H/W Kiteto (1), H/W Njombe (1), H/M Temeke (1), H/W Rombo (3) na H/W Same (1).

Ninapata wasiwasi na ustawi wa watumishi hawa katika kupata mahitaji yao muhimu kama vile chakula, mavazi na malazi. Hali hii inasababisha watumishi kutumia muda wa kazi kwa shughuli zao binafsi ili kujipatia kipato cha ziada, hali inayoweza kudumaza utoaji wa huduma kwa jamii.

Kutokulipwa Madai ya Watumishi wa Umma Sh. Bilioni 359.36

Ukaguzi wangu ulibaini uwepo wa madai ya Sh. bilioni 331.52 kwenye Taasisi 80 za Serikali Kuu na Sh. bilioni 27.84 kwa Mamlaka 36 za Serikali za Mitaa, hivyo kuwa na jumla ya madai yanayofikia Sh. Bilioni 359.36.

Hasara itokatokanayo na kukataliwa kwa madai ya fedha za Bima ya Afya Kiasi cha Sh. bilioni 4.46

Tathmini niliyofanya katika zahanati, vituo vya afya, na hospitali katika Mamlaka 60 za Serikali za Mitaa nilibaini uwepo wa madai yaliyokataliwa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ikiwa ni gharama za matibabu kwa wagonjwa wanaotumia huduma za bima ya kiasi cha Sh. bilioni 2.28 na sh.bilioni 2.18 kwa Hospitali za Rufaa 26 kutokana na makosa katika ujazaji wa taarifa za wagonjwa pamoja na kutozingatia taratibu kama vile idhini batili, kutozingatia miongozo ya matibabu, kutoonesha vipimo vya utambuzi, na kuingizwa kwa huduma ambazo hazikuwa katika Mfuko. Madai yaliyokataliwa yanaathiri uwezo wa zahanati, vituo vya afya na hospitali katika kutoa huduma za afya kwa jamii kwani hii ni sawa na kutoa huduma za matibabu bure.

Mashauri dhidi ya Mamlaka za Serikali za Mitaa yenye jumla ya Sh. bilioni 123.97 na Madai ya Halmashauri Dhidi Watoa Huduma Yaliyoko Mahakamani Kiasi cha Sh. bilioni 13.40

Mamlaka za Serikali za Mitaa 117 kati ya 185 zilikuwa zinadaiwa kutokana na mashauri yaliyo mahakamani yenye thamani Sh. bilioni 123.97; na Mamlaka za Serikali za Mitaa 60 zilikuwa na mashauri ya madai mahakamani ya jumla ya Sh. bilioni 13.40 dhidi ya wadau wake.

Madeni tarajiwa yanaweza kuleta athari kubwa kwenye rasilimali fedha za Mamlaka za Serikali za Mitaa, kama vile gharama za uendeshaji wa mashauri na hatari ya kulipa kiwango kikubwa cha pesa baadaye kutokana na halmashauri kushindwa kesi. Hali hiyo ikitokea inaweza kuathiri utoaji endelevu wa huduma za jamii.


5.2.2 Ukaguzi Maalumu Mamlaka za Serikali za Mitaa

Ndugu Wanahabari,

Nilifanya kaguzi Maalumu kwa Halmashauri 64 ili kuangalia mwenendo wa Halmashauri hizi katika kukusanya mapato na kutekeleza miradi mbalimbali. Kaguzi hizi ziliangazia kipindi cha Miaka ya Fedha 2017/18 hadi 2019/20. Katika kaguzi hizo nilibaini mapungufu yafuatayo:

Mapato Ambayo Hayakukusanywa Kutoka Vyanzo Mbalimbali vya Mapato ya Ndani Sh. bilioni 60.805

Katika ukaguzi maamlu kwa kipindi cha mwaka wa fedha wa 2017/18 hadi 2019/20 ukaguzi nilibaini kuwa jumla ya Halmashauri 42 hazikuweza kukusanya mapato kiasi cha Sh. bilioni

60.805 kutoka vyanzo mbalimbali, vikijumuisha kodi za vibanda vya Halmashauri, madeni kutoka kwa mawakala wa ukusanyaji mapato ya ndani, Leseni za biashara zisizolipiwa na malipo yanayotokana na ukusanyaji wa Taka ngumu; kama ilivyoanishwa katika Jedwali hapa chini

Kwa maoni yangu, upotevu huu wa mapato unatokana na udhaifu wa mamlaka husika kushindwa kufuatilia na kuhakikisha wadaiwa wote wanalipa madeni yao kwa wakati na kuchukua hatua stahiki kwa wanaoshindwa kutimiza wajibu wao wa kulipa.

MAPATO AMBAYO HAYAKUKUSANYWA KUTOKA VYANZO MBALIMBALI VYA MAPATO YA NDANI

Na. Mkoa Jina la Halmashauri
Kiasi (Sh.)
1Dar es SalaamH/Manispaa Kinondoni
28,996,482,240​
2MwanzaH/Jiji Mwanza
6,674,588,103​
3ArushaH/Jiji Arusha
5,096,082,536​
4TangaH/Jiji Tanga
3,571,460,410​
5RukwaH/W Sumbawanga
3,464,662,856​
6Dar es SalaamH/Jiji Dar es Salaam
2,529,445,783​
7TangaH/Mji Korogwe
1,855,512,000​
8IringaH/W Kilolo
1,250,418,957​
9DodomaH/W Kongwa
861,484,756​
10ManyaraH/W Kiteto
625,779,028​
11KilimanjaroH/Manispaa Moshi
609,742,907​
12KilimanjaroH/W Same
570,828,500​
13SongweH/W Mbozi
466,336,477​
14MwanzaH/W Magu
450,839,043​
15DodomaH/W Chamwino
370,121,628​
16KageraH/W Karagwe
342,154,922​
17NjombeH/W Makete
295,118,952​
18DodomaH/Jiji Dodoma
268,991,230​
19Dar es SalaamH/Manispaa Ilala
241,235,806​
20RuvumaH/Manispaa Songea
210,319,829​
21KigomaH/W Uvinza
206,031,703​
22TaboraH/ManispaaTabora
199,556,934​
23ArushaH/Wilaya Karatu
194,512,788​
24SimiyuH/W Bariadi
164,089,366​
25PwaniH/W Bagamoyo
135,430,352​
26KataviH/Manispaa Mpanda
134,515,000​
27TangaH/W Mkinga
126,632,060​
28ShinyangaH/Mji Kahama
104,678,353​
29MaraH/W Rorya
99,511,249​
30TaboraH/Mji Nzega
96,727,295​
31MaraH/Manispaa Musoma
88,690,000​
32ManyaraH/W Mbulu
74,726,150​
33DodomaH/W Chemba
73,121,393​
34KigomaH/W Kasulu
59,314,231​
35NjombeH/W Njombe
58,948,704​
36LindiH/W Kilwa
51,175,024​
37ArushaH/W Meru
40,988,000​
38MbeyaH/W Busokelo
39,344,000​
39KigomaH/W Buhigwe
31,549,418​
40SingidaH/W Itigi
29,572,710​
41SingidaH/W Mkalama
19,828,000​
42RuvumaH/W Nyasa
16,203,900​
43Geita MjiH/Mji Geita
8,752,750​
Jumla
60,805,505,343

Mapato ya Ushuru wa Huduma Ambayo Hayajakusanywa na Halmashauri Sh. Bilioni 8.457

Katika ukaguzi maalumu kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2017/18 hadi 2019/20 nilibaini kuwa Halmashauri 21 zilishindwa kukusanya mapato ya ushuru wa huduma kiasi cha Sh. bilioni 8.457 kama inavyoonyeshwa kwenye Jedwali hapa chini. kutokana na shughuli mabalimbali za kiuchumi zilizofanyika ndani ya halmashauri husika.

Kwa maoni yangu, upotevu huu wa mapato unatokana na udhaifu wa mamlaka husika kushindwa kufuatilia vyanzo vya mapato ikiwemo ushuru wa huduma ili kujua kampuni na wadau wote wanaoendesha shughuli za kiuchumi ndani ya maeneo yao ya kiutawala na kuhakikisha kuwa yanalipa ushuru kadri ya matakwa ya Sheria ya Fedha ya Serikali za Mitaa, Na. 9 ya 1982, (Ilivyorekebishwa 2000) inayosema kwamba mapato na rasilimali za Halmshauri ya Wilaya yatajumuisha mapato yote yaliyotokana na huduma zitolewazo na kupokelewa na taasisi, kwa kiwango kisichozidi 0.3 asilimia ya mapato hayo, baada ya kutoa kodi ya ongezeko la thamani na ushuru wa bidhaa.

Nashauri mamlaka husika ziongeze nguvu katika kufuatilia na kujua mapato halisi ya Taasisi zinazofanya kazi au kutoa huduma ndani ya maeneo yao ya kiutawala ya halmashauri husika kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), ili waweze kukusanya mapato stahiki toka katika taasisi hizo.

MAPATO YA USHURU WA HUDUMA AMBAYO HAYAJAKUSANYWA NA HALMASHAURI

Na. Jina la Halmashauri Kiasi
1H/Manispaa Ilala
3,075,963,095​
2H/Mji Kahama
1,211,482,633​
3H/W Kilosa
962,165,908​
4H/Mji Geita
654,935,880​
5H/W Kilolo
618,071,741​
6H/Manispaa Songea
501,276,586​
7H/W Rungwe
459,091,770​
8H/W Bagamoyo
191,997,408​
9H/W Rorya
163,468,114​
10H/Manispaa Mpanda
140,022,735​
11H/W Kibondo
111,026,052​
12H/W Magu
72,215,601​
13H/W Makete
67,421,870​
14H/W Kilwa
51,175,024​
15H/W Kiteto
49,363,229​
16H/W Nyasa
44,924,745​
17H/W Kongwa
39,051,604​
18H/ManispaaTabora
23,077,333​
19H/W Same
10,910,631​
20H/W Njombe
5,172,040​
21H/W Mkinga
5,140,065​
Jumla 8,457,954,064

Mapato yaliyokusanywa na mawakala kupitia Mfumo wa LGRCIS ambayo hayakuwasilishwa Benki Sh. bilioni 23.879​

Matokeo ya ukaguzi uliofanyika katika Mamlaka 59 za serikali za mitaa yanaonesha kuwa kwa kipindi cha miaka ya fedha 2017/18 hadi 2019/20, makusanyo ya jumla ya Sh. bilioni

23.879 kutoka vyanzo mbalimbali vya mapato ya ndani yalibainika kutowasilishwa benki kutokana na udhaifu wa mfumo wa udhibiti wa ndani. Hii ni kinyume na Agizo la 50 (5) la Memoranda ya Fedha za Serikali za Mitaa ya mwaka 2009.

Muhutasari wa mapato yaliyobainika kutowasilishwa benki kwa kila halmashauri ni kama inavyooneshwa katika Jedwali hapa chini.

MAPATO YALIYOKUSANYWA NA MAWAKALA KUPITIA MFUMO WA LGRCIS AMBAYO HAYAKUWASILISHWA BENKI​

Na.
Jina la Halmashauri
Kiasi (Sh.)
1H/M ya Kinondoni
5,983,799,498​
2H/Jiji Dar es Salaam
1,677,018,980​
3H/J la Arusha
1,256,788,700​
4H/W ya Songea
1,011,379,373​
5H/W ya Chemba
769,172,024​
6H/W ya Itilima
714,457,233​
7H/W ya Kilosa
713,695,590​
8H/W ya Kasulu
612,853,913​
9H/W ya Mbozi
603,530,832​
10H/W ya Meru
557,829,134​
11H/M ya Ilala
552,456,653​
12H/W ya Kilwa
512,210,970​
13H/J la Mwanza
496,153,502​
14H/W ya Kongwa
490,603,427​
15H/M ya Temeke
478,520,015​
16H/W ya Makete
476,584,694​
17H/Jiji la Tanga
444,269,885​
18H/W ya Kibondo
430,336,652​
19H/W Morogoro
420,872,288​
20H/W ya Sumbawanga
418,116,333​
21H/M ya Iringa
409,051,598​
22H/Ma ya Shinyanga
406,591,529​
23H/W ya Rungwe
370,279,219​
24H/J la Dodoma
347,781,513​
25H/W ya Momba
338,643,215​
26H/W ya Uvinza
318,728,573​
27H/W ya Siha
288,691,349​
28H/W ya Itigi
283,782,266​
29H/M ya Lindi
271,893,261​
30H/M ya Songea
229,251,495​
31H/W ya Masasi
167,984,487​
32H/M ya Mpanda
155,173,450​
33H/W ya Kilolo
146,542,908​
34H/W ya Chamwino
139,550,670​
35H/M ya Moshi
134,044,850​
36H/W ya Kiteto
118,918,000​
37H/W ya Sikonge
115,255,248​
38H/W ya Nyasa
115,028,471​
39H/W ya Bariadi
111,085,799​
40H/W ya Karagwe
109,472,791​
41H/W ya Karatu
80,214,500​
42H/M ya Kahama
78,764,853​
43H/W ya Mbulu
74,726,150​
44H/W ya Buhigwe
74,223,744​
45H/M ya Singida
47,658,041​
46H/M ya Musoma
46,732,360​
47H/M ya Tabora
34,789,687​
48H/W ya Nyang’wale
33,299,341​
49H/W ya Njombe
32,858,050​
50H/W ya Magu
29,552,820​
51H/W ya Korogwe
27,375,492​
52H/M ya Morogoro
24,528,420​
53H/W ya Mkinga
21,462,486​
54H/Mji wa Nzega
19,108,030​
55H/W ya Bukoba
15,182,040​
56H/W ya Same
13,393,755​
57H/W ya Mkalama
11,605,250​
58H/M ya Sumbawanga
9,974,650​
59H/W ya Babati
6,044,900​
Jumla
23,879,894,957

wa maoni yangu, haya ni mapato halisi ya Serikali yaliyochepushwa na kutumiwa kwa matumizi binafsi kwa njia ya ubadhilifu. Nashauri mamlaka husika washirikiane na TAKUKURU kuhakikisha wahusika wanawajibika kurejesha fedha walizochukua au wanafikishwa kwenye vyombo vya sheria kujibu mashitaka.

Hati za Malipo ya Sh. Bilioni 5.796 Ambazo Hazikuwasilishwa kwa Ajili ya Ukaguzi

Mchanganuo wa nyaraka za malipo ambazo hazikuwasilishwa kwa ajili ya ukaguzi wangu katika Jedwali hapa chini.

HATI ZA MALIPO AMBAZO HAZIKUWASILISHWA KWA AJILI YA UKAGUZI

Na. Jina la Halmashauri
Kiasi
1H/W Rorya
976,942,815​
2H/W Kilosa
815,376,829​
3H/Manispaa Kinondoni
540,605,920​
4H/W Itigi
482,116,753​
5H/W Morogoro
387,671,740​
6H/W Njombe
286,049,700​
7H/W Bariadi
267,859,305​
8H/Manispaa Ilala
241,235,806​
9H/Manispaa Singida
239,071,596​
10H/W Mbozi
222,822,766​
11H/W Kasulu
214,683,142​
12H/W Siha
194,832,334​
13H/W Kibondo
162,556,940​
14H/Manispaa Iringa
162,438,044​
15H/Manispaa Sumbawanga
153,401,656​
16H/Jiji Arusha
135,774,270​
17H/W Rungwe
119,774,590​
18H/W Kilwa
103,287,218​
19H/W Uvinza
70,186,700​
20H/W Kongwa
19,638,400​
Jumla
5,796,326,524


[1] TANROADS ilikua na deni la Sh. 624,677,604,000 lililoripitiwa katika taarifa za fedha zinazoishia tarehe 30 Juni 2020, kati ya deni hilo, Sh. 593,785,965,000 ni deni linalotokana na madai ya wakandarasi na washauri. Hatahivyo, mpaka wakati wa ukaguzi tarehe 16 Novemba 2020, madeni ya wakandarasi na washauri yaliongezeka mpaka Sh. 770,119,541,338.75, ikiwa ni ongezeko la Sh. 176,333,576,338.75 (30%) kwa muda wa miezi minne.
[2] TANAPA (Sh. 250,000,000), TFS (Sh. 250,000,000), NCAA (Sh. 250,000,000) and TAWA (Sh. 250,000,000)
[3] NMT (Sh. 115,020,000), Arusha (Sh. 130,000,000), Dodoma (Sh. 24,338,000), Dar es Salaam
(Sh.77,900,000), Mwanza (Sh. 60,000,000), Arusha (Sh. 30,000,000) na BASAZA (Sh. 50,000,000)
[4] Nyambogo, Nyambiti, Makurugusi, Mkungo, Busalala, Ilemela, Musasa, Kasala, Mikonto na Kamanga
[5] Nkwae, Ntondo, Mrama, Madamigha, na Ifombou,
[6] Iseni, Nyang’hanga, na Lumeji
[7] Nyahaa, Mpambala, Lugongo, Mkiko na Munguli
[8] Makete, Chemba, Mbinga, Handeni, Nyasa, Kiteto na Muheza
[9] Mbogwe, Chato, Singida, Mkalama, Nzega, Muleba na Igunga
 
5.2.2.1 Halmashauri ya Manispaa Ya Bukoba

Kutopokelewa kwa Vifaatiba Kutoka Bohari ya Dawa (MSD) Vyenye Thamani ya Sh. Bilioni 1.08

Kwa mwaka wa fedha 2017/18 hadi 2019/20 Halmashauri kupitia vituo vya afya Kishanje, Katoro na Maruku ilipokea vifaa tiba vyenye jumla ya Sh. 347,103,250. Vifaa tiba hivi ni sehemu ya jumla ya vifaa tiba vyenye thamani ya Sh. 1,431,928,830 vilivyopaswa kupokelewa kutoka Bohari ya Madawa (MSD) kwa ajili ya huduma ya dharura ya uzazi na watoto wachanga (CEmONC) ambapo kila kituo kilipaswa kupokea vifaa vyenye thamani ya Sh. 477,309,610. Kwa mantiki hiyo nilibaini kuwa vifaa ambavyo havijapokelewa hadi ukaguzi wangu unakamilika vina thamaani ya Sh. 1,084,825,580. Kutokupelekwa kwa vifaa tiba hivyo kunasababisha majengo mengi yaliyojengwa kushindwa kuanza kutoa huduma kwa wananchi kwa wakati.

5.2.2.2 Halmashauri ya Wilaya Ya Nkasi

Kutorejeshwa kwa fedha ya malipo ya awali Kiasi cha Sh. bilioni 1.08 baada ya Mkandarasi Kufutiwa Usajili

Katika Mwaka wa Fedha 2017/18, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi ilimlipa mkandarasi M/s Fally Enterprises Ltd kwa ajili ya mradi wa maji wa Mpasa na Isale Sh. bilioni 1.50, ikiwa ni gharama ya malipo ya awali. Ilibainika kuwa mkandarasi alifutiwa usajili wa kandarasi kwa barua yenye kumb. Na. C6/1224/8/2002/17 ya tarehe 19/10/2019. Kati ya kiasi alichopewa kama malipo ya awali Halmashauri ilifanikiwa kurejesha toka kwa mkandarasi Sh. milioni 416.45 tu hivyo Halmashauri haikufanikiwa kurejesha kiasi cha Sh. bilioni 1.08.

Mabadiliko ya nyongeza ya gharama ya mikataba bila idhini ya Mlipaji Mkuu wa Serikali Sh. bilioni 10.58

Nilibaini nyongeza yenye jumla ya Sh. bilioni 10.58 kwa wakandarasi waliotekeleza miradi ya maji. Mradi wa maji wa Isale Sh. bilioni 2.46 mradi wa maji wa Mpasa Sh. bilioni 1.25 na mradi wa maji wa Kamwanda Sh. bilioni 6.86. Nyongeza hiyo ilipitishwa kwenye kikao cha Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango cha tarehe 10/06/2017, na si Katibu Mkuu Wizara ya Fedha (Mlipaji Mkuu wa Serikali), kinyume na matakwa ya kanuni ya 110(4) ya Kanuni za Ununuzi wa Umma za Mwaka 2013 (zilizorekebishwa 2016), inayotaka taasisi kupata kibali cha Mlipaji Mkuu wa Selikali kabla ya kufanya nyongeza ya gharama ya mkataba.

Manunuzi Kutoka Kwenye Biashara za Watumishi wa Halmashauri Sh.182,004,440

Halmashauri ilifanya manunuzi ya vifaa vya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya na vituo vya afya vyenye thamani ya Sh. 182,004,440 kutoka katika biashara mbalimbali zinazomilikiwa na watumishi wa Halmashauri. Miongoni mwao ni Mhasibu Msaidizi na Mtunza Fedha Mkuu (Main Cashier), na mwingine ni Mwenza wa Kaimu Mhandisi wa Ujenzi wa Halmashauri, hali hii inaweza kuleta mgongano wa kimaslahi na kupelekea kuwepo na upendeleo katika mchakato wa manunuzi.

Hasara iliyotokana na Malipo kwa Kazi Ambazo Hazikutekelezwa Sh. bilioni 2.36

Nilibaini kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi ilifanya malipo ya kiasi cha Sh. bilioni 2.36 kwa makandarasi kwa kazi ambazo hazikutekelezwa, kati ya fedha hizo Sh. bilioni 1.23, zililipwa kwenye miradi 17 ya maji, mradi wa umwagiliaji, mradi wa bwawa na mradi wa chumba cha ubaridi (Cold room) na Sh. 1.13 zililipwa zaidi ya kiwango cha mkataba katika miradi 17 ya maji na miradi miwili ya barabara, hivyo kusababisha hasara kwa Halmashauri. Malipo haya yalifanyika katika kipindi cha mwaka wa fedha 2016/17 na 2017/18.

Malipo ya Usanifu na Usimamizi wa Miradi ya Maji Kulipwa kwa Kampuni ya Mtumishi wa Wizara ya Maji Sh. 255,825,327

Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi ilifanya malipo ya Sh. 255,825,327 kwenda kwa mkandarasi M/s O&A Co. Ltd, kwa ajili ya usanifu na usimamizi wa Mradi wa maji wa Kabwe, King'ombe, Tambaruka na Kisula, mradi wa maji wa Itete, Mtakuja, Katongolo, Msilihofu, Ntuchi, Kitosi, Nkata, Chala A na C, Mpasa na Mlambo na mradi wa maji wa Mkinga na Matala. Nilibaini mmoja wa wamiliki (wanahisa) wa kampuni hiyo ni mtumishi wa Wizara ya maji katika Kitengo cha Oparesheni na Matengenezo. Hii inaonesha mgongano wa maslahi na kuminya usawa katika mchakato wa manunuzi. Hata hivyo mpaka kufikia Aprili 2020 miradi ya kijiji cha Matala haukutoa matokeo chanya kutokana na mapungufu katika usanifu uliofanywa na kampuni hiyo.

Wakandarasi Kutekeleza Miradi ya Sh. Bilioni 8.02 Bila Kuwa na Usajili wa Kisheria

Uongozi wa Halmashauri uliingia mikataba yenye jumla ya thamani ya Sh. bilioni 8.02 na kampuni ambayo hayana usajili wa kisheria. Miongoni mwa kampuni hizo ni M/s Fally Enterprises Ltd aliyesaini mkataba wa Sh. bilioni 7.49 kwa ajili ya mradi wa maji wa Isale, bila kuwa na usajili wa bodi ya wakandarasi(CRB), katika mwaka wa fedha 2016/2017 hadi 2018/2019 kwa vipindi tofauti halmashauri ililipa jumla ya Sh. 376,006,229 kwa M/s Ngejito Group Ltd, M/s Isunta Carpenters Group na Rehema Selemani Mwenda, kwa ajili ya ujenzi wa barabara za Namanyere, ununuzi wa samani za vituo vya afya na ununuzi wa vifaa vya ujenzi wa hospitali ya Wilaya, bila kuwa na usajili wa BRELA na mwaka wa fedha 2016/2017 na 2017/2018, Halmashauri katika vipindi tofauti ilifanya malipo ya jumla ya Sh. milioni 150.63 kwa wazabuni kwa ajili ya manunuzi ya vifaa mbalimbali, bila ya kuwa na usajili wa mlipa kodi toka TRA (TIN No.)

5.2.2.3 Halmashauri ya Jiji la Arusha

Malipo ya Fidia ya Ardhi Kufanyika Kabla ya Taarifa ya Uthamini Kuandaliwa na Kupitishwa na Mthamini Mkuu wa Serikali Sh. 243,000,000

Timu ya ukaguzi maalum ilibaini kuwa Halmashauri ya Jiji la Arusha ilifanya malipo ya Sh. 243,000,000 kwa fidia ya eneo la kituo cha afya Muriet kabla ya taarifa ya uthaminishaji wa eneo hilo kuidhinishwa na Mthamini Mkuu wa Serikali. Ukaguzi ulibaini kuwa taarifa hiyo iliandaliwa mwezi Juni, 2018 na iliidhinishwa na Mthamini Mkuu wa Serikali tarehe 20 Agosti, 2018 wakati malipo yalifanyika kati ya mwezi Februari na Mwezi Aprili, 2018.

Manunuzi Yaliyoidhinishwa na Wajumbe Wawili Kati ya Watano wa Bodi ya Zabuni Sh.289,043,152

Mapitio ya nyaraka za manunuzi yaliyofanywa na Halmashauri ya Jiji la Arusha yalibaini manunuzi ya jumla ya Sh. 289,043,152.16 yaliyofanywa kupitia ‘circular resolution’ ambazo ziliidhinishwa na wajumbe wawili (2) badala ya watano (5) kinyume na matakwa ya Kanuni ya 58(1) ya Kanuni za Manunuzi ya Umma za mwaka 2013. Kanuni ya 58(4) ya Kanuni hizo inaelekeza maamuzi yafanywe baada ya kupitishwa na zaidi ya nusu (wajumbe 3) ya wajumbe wa bodi ya zabuni.

Uwekezaji usio na Tija kati ya Halmashauri ya Jiji la Arusha na kampuni ya Happy Sausage katika Kampuni ya Arusha Meat Company Limited (AMCL).

Ukaguzi maalum ulibaini kuwa tarehe 29 Novemba 1986 Ofisi ya Ardhi Mkoa wa Arusha ilipima viwanja eneo la Sakina Arusha na kugawa kiwanja Na 1 kwa Halmashauri ya Manispaa ya Arusha (Kwa sasa Jiji). Tarehe 6 Desemba 1986 Halmashauri ilipewa haki ya kumiliki (Offer of Right of Occupancy) kiwanja Na. 1 Kitalu “FF” chenye ukubwa wa hekta 10.879 na tarehe 19 Oktoba, 1994 ilipewa Hati miliki ya kiwanja hicho kwa muda wa miaka 99.

Ukaguzi maalumu ulibaini kuwa tarehe 9 Januari, 1993 Halmashauri ya Manispaa ya Arusha (Jiji) iliingia makubaliano na Kampuni ya Happy Sausage Limited (HSL) ya kuendesha kwa ubia kiwanda cha nyama, Arusha Meat Company Limited (AMCL). Sehemu ya tatu (3) ya makubaliano hayo ilieleza kuwa Manispaa ya Arusha itamiliki asilimia 49 ya hisa sawa na Sh.14,700,000 na Happy Sausage itamiliki asilimia 51 sawa na Sh.15,300,000. Sehemu ya nne

(4) ya makubaliano hayo ilikubalika kuwa wakurugenzi wa bodi watakuwa sita (6); watatu (3) kutoka Halmashauri ya Manispaa na watatu (3) kutoka Happy Sausage Ltd. Pia sehemu ya tano ilikubalika kuwa masuala yote yanayoihusu kampuni yatajadiliwa kwa pamoja na kufanyiwa maamuzi ya pamoja kati ya Halmashauri ya Manispaa ya Arusha na Kampuni ya Happy Sausage Ltd.

Hata hivyo mapitio ya utekelezaji wa makubaliano hayo yalibaini mapungufu yafuatayo:

Kiwanja cha Halmashauri ya Jiji la Arusha kumegwa na kutengenezwa Kiwanja Na.2 Kitalu “FF” na kumilikiwa na Kampuni ya Happy Sausages Ltd isivyo halali

Maamuzi ya kuuzwa na kuwekwa rehani kwa mali (ardhi) ya kampuni ya Arusha Meat Company Limited (AMCL) ambayo hayakuridhiwa na Halmashauri ya Manispaa ya Arusha licha ya kuwa ni mwanahisa wa kampuni hiyo.

Halmashauri kushindwa kurasimisha umiliki wa Hisa 3420 kutoka Hanns Seidel Foundation zilizohamishiwa katika Halmashauri ya Manispaa ya Arusha.

Halmashauri kutoshirikishwa kwenye maamuzi mbalimbali yanayohusu uendeshaji wa Kampuni ya Arusha Meat Company Limited (AMCL).

Malipo ya Ziada kwa Manunuzi ya Ardhi bila Mkataba na bila Kupitishwa na Vikao vya Kudumu vya Halmashauri Sh. 30,940,000

Kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2017/18 Halmashauri ya Jiji la Arusha ilifanya makubaliano ya kununua eneo la ekari moja (1) kutoka kwa mwananchi kwa bei ya Sh.50,000,000. Hata, hivyo baada ya kufanya malipo ya fedha kwa mujibu wa makubaliano, muuzaji aliwasilisha barua ya malalamiko tarehe 27 Desemba, 2017 akidai kupunjwa kiasi cha Sh.30,940,000 kutokana na ardhi aliyoiuzia Halmashauri. Kiasi hiki cha fedha za nyongeza kililipwa kupitia hati ya malipo namba 702001V1801800 ya tarehe 9 Januari, 2018 bila ya uwepo wa mkataba wa nyongeza (addendum) na bila taarifa ya uthamini wa ardhi ili kujua thamani halisi ya eneo husika. Kwa madai hayo mapya Halmashauri ya Jiji la Arusha ilinunua ekari moja kwa Sh. 80,940,000

5.2.2.4 Halmashauri ya Jiji la Dar Es Salaam

Ununuzi wa ‘excavator’ wenye shaka Sh.359,862,240

Katika mwaka wa fedha 2019/20, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam iliingia makubaliano na mzabuni kupitia mkataba Na.LGA/018/2019/2020/G/22, wenye thamani ya Sh. 359,862,240 kununua excavator’ kwa ajili ya dampo la Pugu Kinyamwezi. Manunuzi haya yanatia shaka kutokana na mzabuni huyo kutokuwa na leseni ya uuzaji wa Mitambo. Mzabuni huyo alikuwa na leseni ya ukodishaji wa mitambo kama inavyothibitishwa na nakala ya leseni yake ya biashara Na. B 3190519 ya tarehe 26 Juni, 2019.

Kutokamilika ujenzi wa zahanati katika kata ya kipunguni kutokana na upotevu wa fedha Sh. 74,093,000

Mapitio ya jalada IMC/JW.12/1 la maendeleo ya Kata ya Kipunguni na Daftari la makosa ya kinidhamu yalibaini kuwa Afisa Mtendaji wa Kata ya Kipunguni na mtia saini wa akaunti ya maendeleo ya Kata ya Kipunguni walikutwa na kosa la upotevu wa fedha Sh. 74,093,000 zilizotolewa kwa ajili ya ujenzi wa Zahanati ya Kata ya Kipunguni. Upotevu huo ulisababisha mradi wa ujenzi kutokukamilika.

5.2.2.5 Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni

Kutorejeshwa kwa Fedha Zilizolipwa Kama Mkopo wa Mshahara (Salary Advance) kwa Mwalimu wa Timu ya Mpira wa Miguu Inayomilikiwa na Manispaa ya Kinondoni Sh. 33,000,000

Katika kipindi cha Mwaka wa Fedha 2019/2020 Halmashauri ilimpatia mkopo wa mshahara (salary advance) wa Sh. 33,000,000 mwalimu wa timu ya mpira wa miguu (Kocha) inayomilikiwa na Manispaa, ya Kinondoni (KMC FC) kupitia hundi Na. 000368 ya tarehe 21 Juni, 2019. Mpaka ukaguzi huu unakamilika Mwezi Agosti, 2020, mkopo huo ulikuwa bado kurejeshwa.

Malipo ya Uzoaji Taka Yaliyolipwa Zaidi ya Gharama ya Makubaliano Kimkataba Sh. 162,500,000

Halmashauri ya Manispaa iliingia Mkataba Na. LGA/017/2018-2019/HQ/NC/01 na timu ya mpira wa miguu (KMC-FC), kwa kazi ya uzoaji wa taka, kwa gharama ya Sh. 216,000,000 kwa muda wa miezi kumi na mbili (12), kuanzia Januari 2019 hadi Januari 2020.

Hata hivyo, ukaguzi maalumu ulibaini kuwa, Halmashauri ya Manispaa iliilipa timu ya mpira wa miguu ya Kinondoni (KMC-FC) Sh. 378,500,000 na kusababisha malipo ya zaidi juu ya makubaliano ya mkataba kwa Sh. 162,500,000.

Malipo ya Ununuzi wa Magari ya Kuzolea Taka Usiozingatia Taratibu za Manunuzi Sh. 352,928,349

Ukaguzi maalumu ulibaini kuwa Halmashauri ya Manispaa ilifanya ununuzi wa magari mawili (2) ya uzoaji taka kutoka kwa kampuni ya GF Truck & Equipment Ltd, kwa gharama ya Sh. 352,928,349. Hata hivyo, ilibainika kuwa kulikuwa na ukiukwaji wa taratibu za manununuzi ya magari hayo ikiwemo:

Kufanya manunuzi ya magari bila kuomba kibali cha ununuzi wa magari kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, kinyume na waraka wa Hazina Na. 3 wa 11 Novemba, 2014 wenye Kumb. Na. CJA.233/362/01

Kufanya manunuzi ya magari bila kupitishwa na Bodi ya Zabuni na bila kuomba na kupewa vipimo (specification) vya magari kutoka Wizara ya Ujenzi na kisha kuwasilisha vipimo hivyo pamoja na kibali toka Ofisi ya Waziri Mkuu, kwa Mtendaji Mkuu Wakala wa Manunuzi Serikalini (GPSA), kwa ajili ya ununuzi wa magari husika.

Kutumia fedha za mfuko wa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kununua magari hayo, kiasi cha Sh. 102,000,000 ambazo hazikurejeshwa hadi ukaguzi unakamilika mwezi Agosti, 2020 ni ukiukwaji wa sheria.

Mapungufu ya kimkataba kati ya Manispaa na Oysterbay Villa Yaliyosababisha Hasara ya Sh. 218,091,820

Ukaguzi wangu ulibaini kuwa tarehe 13 Disemba, 2007 Manispaa iliingia mkataba na mwekezaji Oysterbay Villa, kwa ajili ya kujenga majengo manne yenye jumla ya vyumba 40, kwa ajili ya upangishaji kwa makubaliano kuwa mwekezaji atamiliki 75% sawa vyumba 30 ya mradi huo na Manispaa itamiliki asilimia 25% sawa na vyumba 10. Ujenzi ulikamilika tarehe 06 Agosti 2010 na vyumba kukabidhiwa Halmashauri ya Manispaa tarehe 16 Machi, 2019.

Aidha, kuanzia Septemba, 2010 mpaka ukaguzi huu unafanyika Agosti, 2020, Halmashauri ya Manispaa ilitarajiwa kuwa imekusanya Sh 246,930,120 kutokana na upangishaji vyumba 10 kwa bei ya Sh. 2,057,751 kwa miezi 120, tangu ujenzi ulipokamilika. Hata hivyo ni Sh.28,838,300 tu zilizolipwa na wapangaji waliongia mikataba na Manispaa, kuanzia 18 Machi, 2019 na hivyo kusababisha hasara ya Sh 218,091,820 kutokana na kitendo cha mwekezaji kutokukabidhi sehemu inayomilikiwa na Manispaa kimkataba kwa wakati tangu tarehe 6 Agosti 2010.

Malipo ya Vibarua Yasiyostahili Sh. 284,850,000

Katika kipindi cha Mwaka wa Fedha 2019/2020, Halmashauri ya Manispaa ilifanya malipo ya Sh. 284,850,000 kwa ajili ya kuwalipa vibarua wa usafi wa barabara na kuzoa taka. Hata hivyo kulikuwa na ukiukwaji wa taratibu za malipo kutokana na nyaraka zilizoambatanishwa kuwa na kasoro mbali mbali ikiwamo; hati za malipo kutoambatana na daftari la kuonyesha siku walizofanya kazi vibarua; sahihi za vibarua kutofautiana ikilinganishwa kati ya nyaraka za malipo ya vibarua (payroll) moja na nyingine ingawa majina ni yale yale; barabara walizofanyia usafi kutotajwa; kukosekana uthibitisho wa wenyeviti wa Serikali za Mitaa na wasimamizi wa vibarua husika, unaothibitisha kufanyika kwa zoezi la usafi/kuzoa taka na kukosekana kwa dokezo lililotoka idara tumizi kwenda kwa Mkurugenzi Mtendaji kuomba malipo.

5.2.2.6 Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo

Kutokukusanywa kikamilifu kwa ushuru wa mazao ya misitu Sh. Bilioni 2.142

Nilibaini kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo haina mfumo au utaratibu mahsusi unaoweza kusaidia kujua bei ya mauzo ya nguzo na idadi ya nguzo zinazouzwa na kampuni zinazojihusisha na uchakataji wa mbao na mauzo ya nguzo. Kwa sababu hiyo nilibaini kuwa, kati ya jumla ya ushuru uliotakiwa kulipwa na kampuni wa Sh. 3,141,829,191 kwa muda wa miaka mitatu ya fedha kuanzia 2017/18 hadi 2019/20, Halmashauri ilikusanya kiasi cha Sh. 1,000,000,000 pekee na hivyo kushindwa kukusanya kiasi cha Sh. 2,141,829,196 ikiwa ni 5% ya mauzo baada ya kupunguza gharama za usafiri.

5.2.2.7 Halmashauri ya Manispaa ya Iringa


Fedha za Matazamio za Miradi ya Mpango wa Uboreshaji Miji katika Serikali za Mitaa (ULGSP) kutumika kinyume na matumizi yake Sh. bilioni 1.08

Nilikagua malipo yaliyokuwa yakifanywa kwa wakandarasi katika utekelezaji wa miradi ya Halmashauri ya Manispaa ya Iringa na kubaini kuwa jumla ya Sh. 1,078,815,035 zilikatwa kama fedha za matazamio kwa miradi ya Mpango wa Uboreshaji Miji katika Serikali za Mitaa (ULGSP) kwa kandarasi. Kati ya fedha hizo zilizokatwa, jumla ya Sh. 812,433,893 zilipelekwa kwenye akaunti ya amana ya Halmashauri na Sh. 266,381,142 zilikatwa kwenye malipo na kuachwa kwenye akaunti ya Maendeleo ya Halmashauri. Nilipitia salio lililopo katika akaunti ya Amana na Akaunti ya Maendeleo ya Halmashauri na kubaini kuwa Akaunti ya Maendeleo ilibakiwa na bakaa la Sh. 34,024 wakati akaunti ya Amana ilikuwa na bakaa la Sh. 4,336,888 tu. Ukaguzi wangu ulibaini pia kuwa fedha za matazamio hazikuwa zimelipwa kwa wakandarasi waliokatwa fedha hizo kwani sikuweza kupata ushahidi wa malipo hayo. Kwa mantiki hiyo ni wazi kuwa jumla ya Sh. 1,078,815,035 zilikuwa zimetumika katika matumizi mengineyo.

5.2.2.8 Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe

Malipo yaliyofanywa kwa mkandarasi bila uthibitisho wa thamani ya kazi zilizofanyika Sh. 88,440,305.90

Nilibaini kuwa katika mwaka wa fedha 2017/2018, Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe ilifanya malipo ya Sh. 88,440,305.90 kwa Mkandarasi kwa ajili ya mkataba wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Buhigwe. Hata hivyo, nyaraka za malipo zilizotumika kumlipa mkandarasi huyo, hazikuambatana na mchanganuo wa kazi zilizofanywa na vipimo (measurement sheets), ili kuthibitisha kiasi cha malipo yaliyostahili kulipwa.

Malipo yaliyofanyika kwa mzabuni asiyekuwa na mkataba na Halmashauri Sh. 23,792,000.


Katika mwaka wa fedha 2019/2020, Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe iliingia mkataba na mzabuni kwa ajili ya kutengeneza na kuweka milango katika jengo la Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kwa gharama ya Sh. 23,792,000. Hata hivyo, malipo yalifanyika kwa mzabuni mwingine ambaye hakuwa na mkataba na Halmashauri hiyo.

5.2.2.9 Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

Kutowasilishwa kwa Mkataba Wenye Thamani ya Sh. Bilioni 12.631 na Nyaraka za Kuthibitisha Mchakato wa Zabuni ya Ujenzi wa Barabara ya Tubuyu, Nanenane na Maelewano

Nilishindwa kukagua mikataba miwili yenye thamani ya Sh. 12,630,868,635, iliyosainiwa baina ya Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro na mkandarasi M/s Group Six International Ltd, akishirikiana na Lukolo Company Ltd na nyaraka za mchakato wa zabuni ya mradi wa kuinua hadhi ya barabara za Tubuyu (km 2.4), Nanenane (km 1.6), na Maelewano (km 0.6) yenye namba LGA/079/2016-2017/HQ/W/04 ambayo haikuwasilishwa kwenye ukaguzi japokuwa nilifanya jitihada mbali mbali za kupata nyaraka hizo.

5.2.2.10 Halmashauri ya Wilaya ya Magu


Malipo ya Kazi Hewa Kutokana na Udanganyifu Katika Vyeti vya Malipo (Payment Certificates) Sh. 656,555,186

Nilibaini kuwa katika mwaka wa fedha 2016/17 hadi 2019/20, Halmashauri ya Wilaya ya Magu ilifanya malipo ya Sh. 1,157,904,440 kwa mkandarasi zaidi ya kiasi alichostahili kulipwa cha Sh. 501,349,253, kutokana na udanganyifu wa kazi zilizofanyika katika Cheti namba 3 (Sh. 11,603,511), Cheti namba 4 (Sh. 51,186,031), Cheti namba 5 (Sh. 101,777,013), Cheti namba 6 (Sh. 225,434,500) na Cheti cha kukamilisha kazi namba 7 (Sh. 266,554,131). Kukosekana kwa usimamizi bora katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo, kumechangia uwepo wa malipo ya jumla ya Sh. 656,555,186 kwa kazi hewa.

5.2.2.11 Halmashauri Manispaa Jiji la Mwanza

Kutofanya Kazi kwa Kituo cha Redio ‘City FM Mwanza’ Licha ya Kuwekeza Sh. 102,574,467

Mnamo mwaka 2010, Halmshauri ya Jiji la Mwanza liliwekeza kiasi cha Sh. 102,574,467 katika kuanzisha redio ya “City FM Mwanza”. Hata hivyo, redio hii ilizimwa mwaka 2017 na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kupitia barua yenye Kumb.Na.DB.96/188/02/86, kwa sababu mawimbi yake yalikuwa yanaingiliana na mawasiliano ya ndege. Hadi ukaguzi unakamilika mwezi wa nane 2020, bado redio ilikuwa imefungwa, hivyo kutokwepo kwa thamani ya fedha kwa kiasi cha Sh. 102,574,467 iliyowekezwa.

5.2.2.12 Halmashauri Mji wa Kahama

Hasara Iliyopatikana kwa Kuwalipa Wazabuni Fedha Nyingi Kuliko Walizokusanya Katika Chanzo cha Mapato Yatokanayo na Ukusanyaji Taka Sh. 290,804,106

Katika kupitia mikataba baina ya Halmashauri ya Mji wa Kahama na na wazabuni, vikundi na watu mbalimbali kwa ajili ya kukusanya taka ngumu pamoja na tozo zake, pamoja na kupitia taarifa kwenye mfumo wa LGRCIS, nilibaini kuwa chanzo hiki cha mapato kilikusanya jumla ya Sh. 678,184,550 na kuwalipa wazabuni na vikundi vilivyohusika na ukusanyaji taka ngumu kiasi cha Sh. 968,988,656, hivyo kusababisha hasara ya Sh. 290,804,106.

Upotevu wa Fedha za Mapato ya Ndani ya Halmashauri Yaliyotumiwa na Mtunza Fedha wa Halmashauri Baada ya Kuwasilishwa Kwake na Wakusanya Mapato Sh. 141,606,500

Nilibaini kuwa jumla ya kiasi cha Sh. 141,606,500 kilichokuwa kimekusanywa na wakusanya mapato, kilitumiwa na mtunza fedha wa Halmashauri ya Mji wa Kahama kwa matumizi yake binafsi. Kati ya fedha hizo, kulikuwa na kiasi cha Sh. 98,779,700 kilichokusanywa na mkusanya mapato mwenye namba ya utambulisho (Payer’s ID) 203300028237 na mkusanya mapato mwenye namba ya utambulisho 203300028235 aliyekusanya Sh. 42,826,800.

Gharama Zilizozidi Uhalisia wa Kazi Sh. 76,950,000

Nilibaini kuwa jumla ya Sh. 76,950,000 zililipwa kimakosa kwa wakandarasi wanaotekeleza miradi katika Halmashauri ya Mji wa Kahama. Kati ya fedha hizo, kiasi cha Sh. 61,280,000 zililipwa kwa Mkandarasi alietekeleza mradi wenye mkataba namba

GA/155/2019/2020/CSR-BARRICK/W/51 ulioingiwa mnamo tarehe 17 Mei, 2020 kwa ajili ya kukarabati stendi ya CDT na barabara zake, ambapo ilibainika kuwa eneo lililopaswa kujazwa mawe kwa mujibu wa mkataba lilikuwa kubwa kuliko eneo halisi lililofanyiwa kazi. Aidha, Mkandarasi Audacity Intercom (T) Ltd mwenye mkataba LGA/155/2018/2019/W/01 alilipwa jumla ya Sh. 15,670,000 zaidi baada ya kuzidisha baadhi ya vipengele vilivyokuwa katika mkataba.

5.2.2.13 Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga

Malipo Yaliyofanywa kwa Wakandarasi Zaidi ya Gharama ya Mkataba Sh. Bilioni 2.449

Nilibaini kuwa Halmashauri ya Manispaaa ya Shinyanga ilifanya malipo mbalimbali ya jumla ya Sh. 2,449,991,166.5 zaidi ya kiwango kilichoainishwa kwenye mikataba, yaliyolipwa kwa wakandarasi na wasimamizi wa miradi mbalimbali. Kiasi cha Sh. 2,263,685,478 kililipwa zaidi kwa kampuni ya Jassie & Company Ltd (JASCO) kutokana na kubadilisha vipengele vya mkataba wakati wa kuomba malipo ya ujenzi wa barabara ya lami. Pia, kiasi cha Sh. 49,331,800 kililipwa zaidi ya stahili kwa Mhandisi Howard Humphreys Tanzania kwa ajili ya kusimamia ujenzi wa barabara za lami, huku kiasi cha Sh. 136,973,888.5 kikiwa ni malipo zaidi ya kiasi stahili kwa Jassie & Company Ltd (JASCO) kwa ajili ya mkataba wa ujenzi wa barabara za lami.

Hadi kufikia Agosti, 2020, fedha hizo hazikuwa zimerejeshwa katika Akaunti ya Benki ya Halmashauri na hivyo kusababisha hasara kwa Halmashauri.

5.2.2.21 Halmashauri ya Wilaya ya Momba

Mshauri Mwelekezi kulipwa Sh. 88,505,340 Mara Mbili kwa Kazi Ambazo Hastahili Kulipwa

Nilibaini kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Momba ilimlipa asilimia 30 Mshauri Mwelekezi M/s MUST Consultancy Bureau, kiasi cha Sh. 88,505,340 kwa hati ya malipo namba 903114V1900659 ya terehe 10 Januari, 2019 kwa ajili ya kuandaa na kuwasilisha taarifa ya awali (inception report). Pia Halmashauri ilimlipa tena Mshauri Mwelekezi asilimia 30 ya makubaliano ya Sh. 88,505,340 kwa hati ya malipo Na. 903114V1901505 ya terehe 08 Mei, 2019, kwa ajili ya uandaaji wa taarifa ya usanifu wa awali pamoja na gharama za mradi, kazi zinazoonekana kufanana.

5.2.2.22 Halmashauri ya Manispaa ya Tabora

Malipo ya Fedha za Matazamio zaidi ya Kiasi Kilichokatwa Sh. 212,262,734

Katika kipindi cha mwaka wa fedha 2018/2019 na 2019/2020, Halmashauri ya Manispaa ya Tabora ilimlipa mkandarasi kiasi cha Sh. 630,003,259.39 kama marejesho ya fedha za matazamio (retention money) badala ya Sh. 417,740,525 iliyokatwa awali na hivyo kupelekea malipo zaidi ya Sh. 212,262,734, kinyume na Sharti la 50.2 la Masharti ya Jumla ya Mkataba Na. LGA/124/2016/2017/W/02/LOT10 wenye gharama ya Sh. 8,222,664,626.25, kwa ajili ya ujenzi wa mradi wa maji uliotekelezwa katika kijiji cha Hedaru.

5.2.2.23 Halmashauri ya Jiji la Tanga


Matofali Yaliyotolewa kwa Wateja Zaidi ya Kiwango Walicholipia Sh. 56,371,200

Ukaguzi maalumu ulibaini kuwa kuanzia tarehe 3 Septemba, 2018 hadi tarehe 5 Julai, 2020, wateja 11 walilipia jumla ya matofali 129,467 na kuchukua matofali 164,699 hivyo kusababisha tofauti ya matofali 35,232 yenye thamani ya Sh. 56,371,200 kuchukuliwa zaidi ya kiwango kilicholipiwa, na ikiwa matofali hayo hayatalipiwa, hiyo itakuwa ni hasara kwa Halmashauri.

Manunuzi Yaliyofanywa kwa Mtumishi wa Halmashauri Sh 120,970,000

Katika kupitia malipo yaliyofanywa kwa wazabuni mbali mbali wa Halmashauri katika mwaka wa fedha 2019/20 ilibainika kuwa jumla ya Sh. 120,970,000 zililipwa kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya ujenzi, mchanga na kokoto katika kutekeleza miradi ya ujenzi katika Halmashauri. Uhakiki wa Kampuni iliyotoa huduma hiyo kwa Halmashauri kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na upembuzi wa taarifa mbalimbali za Halmashauri ulibaini kuwa, mzabuni aliyetoa huduma hiyo kwa Halmashauri ni mtumishi wa Halmashauri aliyeko idara ya manunuzi. Ununuzi wa vifaa mbalimbali kutoka kwa mtumishi wa kitengo cha manunuzi cha Halmashauri unaweza kusababisha Halmashauri kukosa haki ya kupata bei shindanishi.

Kutotumika kwa Muda Mrefu Mashine ya Kufyatua Matofali Iliyonunuliwa kwa Gharama ya Sh.130,000,000

Katika Mwaka wa Fedha 2018/2019, Halmashauri kupitia TISS Na. 50000392 ya tarehe 8 Machi, 2019, ilinunua mashine ya kufyatua matofali yenye thamani ya Sh. 130,000,000. Mashine ilipokelewa kwa hati ya mapokezi Na. 0041 ya tarehe 15 Machi, 2019. Kufanya kazi kwa mashine hii kulihitaji uwepo wa mashine ya kubebea mizigo (forklift) ili kubeba tofali kutoka kwenye mashine na kupelekwa eneo la kupangia kwa ajili ya kukaushwa. Ukaguzi ulibaini kuwa hadi wakati wa Ukaguzi huu tarehe 11 Agosti, 2020 ikiwa ni takribani miezi kumi na sita tangu kununuliwa kwa mashine hiyo ya kufyatulia tofali, ilikuwa haijaanza kutumika kwa sababu Halmashauri haikuwa imenunua mashine hiyo ya kubebea mizigo. Kwa maoni yangu, hali hii ilisababishwa na kutofanyika kwa upembuzi yakinifu wa mahitaji stahiki kabla ya kuibuliwa miradi na kuanza utekelezaji. Kitendo hicho kinaweza kupelekea uharibifu wa mashine hiyo, kuchakaa na kusababisha hasara kwa Halmashauri.

Vifaatiba Vilivyolipiwa Lakini Havijafikishwa Kituo cha Afya Duga Sh. 175,679,500

Katika Mwaka wa Fedha 2019/20, Halmashauri kupitia hati ya malipo Na.862018V1901710 ya tarehe 1 Machi, 2019 ililipa Sh. 200,000,000 Bohari ya Dawa (MSD) kwa ajili ya vifaa tiba vya kituo cha afya Duga. Hata hivyo, kati ya kiasi kilicholipiwa, vifaa tiba vyenye thamani ya Sh. 24,320,500 tu ndivyo vilivyopokelewa hadi tarehe 3 Agosti, 2020. Vifaa Tiba vyenye thamani ya Sh. 175,679,500 vilibainika kutofikishwa Kituo cha Afya Duga, ikiwa ni zaidi ya siku 480 tangu tarehe ya malipo.

Ninapendekeza kwamba menejimenti ya Halmashauri ya Jiji la Tanga inapaswa kufuatilia MSD ili kuhakikisha vifaa tiba hivyo vinaletwa. Kwa kuongezea, hatua stahiki zichukuliwe dhidi ya wafanyakazi wa Halmashauri waliotajwa katika ripoti maalum ya ukaguzi kwa madhaifu yaliyobainishwa. Vilevile, ninapendekeza menejimenti ya Halmashauri kuimarisha udhibiti wa ndani juu ya mambo yote yaliyojitokeza katika ukaguzi.

5.2.2.24 Halmashauri ya Manispaa ya Songea

Kuondolewa kwa Wazabuni Wenye Bei za Chini Bila Sababu za Msingi na Kusababisha Hasara ya Sh. Bilioni 2.143.

Ukaguzi ulibaini Kamati za tathmini kwa mikataba Na. LGA/103/2017/2018W/43 - Ujenzi wa Stendi Mpya ya Mabasi Kata ya Tanga na Na. LGA/103/2017/2018W/54 wa Ujenzi wa Barabara za Manispaa ya Songea, uliwaondoa wazabuni wenye bei za chini katika hatua za awali (Preliminary Stages) kwa kigezo cha kutowasilisha nyaraka za uthibitisho wa mlipa kodi (Tax clearance) kwa Mamlaka ya Mapato (TRA) kwa ajili ya uhakiki wa nyaraka hizo. Menejimenti ya Halmashauri ilishindwa kuwasilisha nyaraka za zabuni zilizowasilishwa na wazabuni hao walioondolewa kwenye mchakato na hivyo haikuthibitisha uhalali wa wakandarasi hao kuondolewa.

Aidha, mapitio ya taarifa ya ufunguzi wa zabuni ya Mkataba Na. LGA/103/2014/2015/W/02 yalibaini kuwa, Mzabuni M/s Lukolo Company Ltd, alipewa kandarasi ya ujenzi wa barabara za lami kwa Sh.14,320,586,464 bila ya kuwasilisha nakala ya hati ya uthibitisho wa mlipa kodi iliyoidhinishwa na Mamlaka ya Mapato (TRA), ambayo ilikuwa ni Kigezo Stahiki (Eligibility Criteria) cha kumuwezesha mzabuni kushiriki kwenye mchakato wa manunuzi kama ilivyotumika katika kuwaondoa kandarasi wengine katika Kandarasi za ujenzi wa kituo cha mabasi na ujenzi wa barabara. Kuondolewa kwa wazabuni hao waliokuwa na bei za chini ya Sh.15,007,703,160 katika hatua za awali, ukilinganisha na bei kwenye mkataba ya Sh.17,149,419,155, kumesababisha Serikali kupoteza Sh. 2,143,715,995.

Kutowasilishwa kwa Nyaraka za Zabuni na Taarifa za Tathmini ya Miradi yenye Thamani ya Sh. Bilioni 39.501

Menejimenti ya Halmashauri ya Manispaa ya Songea, ilishindwa kuwasilisha ripoti za tathmini na zabuni zilizowasilishwa na wazabuni mbalimbali, kwa miradi 12 ya ujenzi na usimamizi yenye thamani ya Sh. 39,501,461,526, kwa ajili ya ukaguzi. Hivyo kumnyima Madhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kushindwa kutimiza majukumu yake.


5.3 MATOKEO YA UKAGUZI WA MASHIRIKA YA UMMA

Ndugu waandishi wa Habari,

Katika ukaguzi wa mapato katika Mashirika ya Umma nilibaini yafuatayo:

Kutofuata viwango vya malipo vilivyoidhinishwa katika utoaji wa huduma

Katika Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), nilibaini kuwa, mamlaka ilitumia viwango vya chini vya ushuru katika tozo za kushusha na kupakia mizigo kwenye meli (Stevedoring) na tozo za kutoa mzigo kutoka kwenye gati hadi kwa mteja (shorehandling) kwa pamoja zilitozwa Dola za Kimarekani 8 badala ya 10; na tozo za maegesho ya meli katika eneo la bandari (Dockage/buoyage) yalitozwa Dola za Kimarekani 10 badala ya 15 kwa uingizaji na usafirishaji wa bidhaa nje. Hii ni kinyume na tozo za bandari zilizopangwa kutumika katika bandari zilizopo katika maziwa zilizotolewa Januari 2018.

Katika Bodi ya Usanifu wa Majenzi na Upimaji (AQSRB), nilibaini kuwa katika Mwaka wa Fedha wa 2019/20, AQSRB ilitoza kiasi pungufu Sh. milioni 21.02 katika kusajili miradi 14 yenye thamani ya Sh. bilioni 143 kinyume na tozo zilizoidhinishwa kwa ajili ya usajili wa miradi.

Udhaifu Katika Usimamizi na Udhibiti wa Mapato ya Kodi za Pango

Chuo cha Taifa cha Sukari (NSI), kina nyumba 123 za makazi zilizo katika muundo na ukubwa tofauti ambazo ziliingiza mapato ya kodi ya pango ya Sh. milioni 111.24 kwa mwaka 2019/20. Hata hivyo, nilibaini kutokuwepo kwa mikataba ya upangishaji kati ya NSI na wapangaji 123. Na makusanyo ya mapato yalifanyika bila kutumia ankara za Mfumo wa Kielektroniki wa Ukusanyaji wa Mapato ya Serikali (GePG), na hakukuwa na viwango vya kodi vilivyoainishwa kwa kila aina ya nyumba. Kitendo hiki kinatoa mianya ya upotevu wa mapato.

Katika Shirika la Masoko la Kariakoo (KMC), nilibaini usimamizi hafifu wa mapato ya ukodishaji wa pango; Soko lilitakiwa kukusanya Sh. milioni 597.54 kwa wapangaji 963 kulingana na taarifa za kitengo cha biashara kwa kiasi cha Sh. 1,700 kwa mpangaji mmoja kwa siku moja. Lakini zilikusanywa Sh. milioni 285.22 na Sh. milioni 312.32 hazikukusanywa. Hii inaashiria kuwa Shirika la Masoko la Kariakoo linapoteza mapato kutokana na usimamizi hafifu wa wapangaji.

TPA ilikodisha ardhi (Ukanda wa Bandari ya Mtwara) kwa EPZA mwaka 2014, kwa kipindi cha miaka 33, ada ya kukodisha ya miaka kumi ya Dola za Kimarekani milioni 3.6 ilitakiwa kulipwa kabla. EPZA ililipa Dola za Kimarekani milioni 1.51 tu na Dola za Kimarekani milioni 2.09 hazijalipwa. Pia, TPA ilikodisha ardhi (Bandari za Ndumbi) kwa TANCOAL Energy Limited (TEL) mwaka 2012. TEL ilitakiwa kulipa kodi kabla kila robo mwaka, hata hivyo, hadi mwaka 2019/20, TEL haikuwa imelipa kiasi cha Sh. milioni 745.79 ambazo imelimbikiza tokea mwaka 2012.

Makusanyo ya Mapato Nje ya Mfumo wa Kielekroniki wa Ukusanyaji wa Mapato ya Serikali (GePG) Sh. bilioni 7.23

Nilibaini taasisi sita (Jedwali Na. 65) zilikusanya mapato yanayofikia Sh. bilioni 7.12 nje ya mfumo wa GePG kinyume na matakwa ya sheria. Kitendo hiki kinatoa mianya ya upotevu wa mapato.

JEDWALI NA. 1: TAASISI NA MASHIRIKA YALIYOKUSANYA MAPATO BILA KUPITIA MFUMO WA GEPG

NaTaasisi/Shirika Kiasi (Sh. milioni)
1
Chuo cha Taifa cha Sukari (NSI)
111.24​
2
Chuo cha Teknolojia (DIT)
731.73​
3
Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Morogoro (MORUWASA)
16.79​
4
Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Dawa (NIMR)
6,251.23​
5
Bodi ya Kahawa Tanzania (TCB)
5.28​
6
Shirika la Posta Tanzania
114.51​
Jumla
7,230.78
Chanzo: Taarifa za makusanyo ya mapato

Ubadhirifu wa kifedha wa Sh. Bilioni 3.93 katika Mamlaka ya Bandari Tanzania

Nilibaini vitendo vya ubadhirifu katika Bandari ya Mwanza na Bandari ya Kigoma. Katika Bandari ya Mwanza, Sh. bilioni 3.27 zilitolewa katika akaunti ya benki ya TPA iliyopo CRDB kupitia miamala 737. Vitabu vya fedha havikuonesha hati za malipo na pia matumizi ya fedha hizo hayakuoneshwa.

Katika Bandari ya Kigoma, Sh. milioni 655.90 zilitolewa kutoka benki kwa kutumia hundi 30 bila kuwa na hati za malipo kuthibitisha malipo yaliyofanywa, na hundi hazikusajiliwa kwenye daftari la udhibiti wa hundi, na vipande 5 vya hundi havijaonekana katika daftari la udhibiti wala katika taarifa za benki. Nyaraka kama vitabu vya hundi, hati za uhamishaji fedha na taarifa za bodi ya zabuni hazikutolewa kwa uchunguzi zaidi.

Pia, katika Bandari ya Kigoma, nilibaini ukosefu wa ripoti za mapato za kila siku ili kuhakiki ripoti za mapato ya kila mwezi kwa kipindi cha miezi 7. Hivyo, sikuweza kuhakiki ukamilifu na usahihi wa mapato yaliyokusanywa kwa kukosekana kwa hati za msingi za mapato.

Taasisi Zenye Wadaiwa Sugu Sh. Trilioni 1.01

Baadhi ya Taasisi na Mashirika ya Umma yana kiasi kikubwa cha madai. Kati ya Mashirika ya Umma 165 ambayo niliyakagua, nilibaini mashirika 66 yenye madai ya muda mrefu yanayofikia kiasi cha Sh. trilioni 1.01 (sawa na 70%) ya madai yote. Aidha, kwa kiasi kikubwa madai hayo yanatokana na huduma mbalimbali zilizotolewa kwa wateja. Pia, nilibaini kuwa 14% sawa na Sh. bilioni 203.96 ya madai hayo yameishapendekezwa kufutwa. Angalia Kiambatisho Na. 7

Mwenendo wa Uwekezaji wa Mitaji katika Kanda Maalumu za Uwekezaji

Kifungu Na 4 cha Sheria ya EPZA ya mwaka 2012 kinaeleza malengo ya kuanzisha Kanda Maalumu za Uwekezaji ikiwa pamoja na kuvutia na kuchochea uwekezaji kwa ajili ya kuuza bidhaa za viwanda nje ya nchi.

Hata hivyo, katika mapitio yangu, nilibaini kushuka kwa uwekezaji wa mitaji mipya katika kanda maalumu kwa kipindi cha miaka mitano (5) kuanzia mwaka wa fedha 2015/16 mpaka mwaka 2019/20 (Rejea Kielelezo hapa chini). Kwa mfano, katika mwaka wa fedha 2019/20 kiasi cha mtaji kilichowekezwa kilikuwa kidogo ukilinganisha na miaka mingine, ambapo idadi ya miradi mipya ilikuwa ni miradi mitano (5) yenye kiasi cha mtaji wa dola za marekani milioni 59.86 (Rejea Kielelezo hapa chini).

MWENENDO WA UWEKEZAJI WA MITAJI MIPYA KATIKA KIPINDI CHA MIAKA MITANO
kati ya leseni 14 zilizoombwa katika mwaka wa fedha 2019/20. Wawekezaji hao 14 ambao hawakupata leseni walipanga kuwekeza kiasi cha dola za marekani milioni 590.94.

Hata hivyo, EPZA ilieleza kuwa kushuka kwa kiasi cha uwekezaji pamoja na mambo mengine kunachangiwa na vibali kwa ajili ya kuwekeza kutoka taasisi zingine za Serikali. Taasisi hizo za Serikali ni pamoja na NEMC, Wizara ya Ardhi, Mamlaka ya Ajira, Uhamiaji na TRA.

Pia, inachangiwa na kutokuruhusiwa kwa wawekezaji kuuza zaidi ya asilimia 20 katika masoko ya nchi za jumuiya ya Afrika Mashariki.

Mwenendo wa uwekezaji katika Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC)

Katika mapitio yangu ya taarifa za mwaka na kanzi data ya wawekezaji katika Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) nilibaini kushuka kwa idadi ya miradi inayosajiliwa na TIC katika kipindi cha miaka mitano (5) kuanzia mwaka 2015/16 mpaka mwaka 2019/20. Kwa mfano idadi ya miradi iliyosajiliwa na kituo mwaka 2015/16 ilikuwa ni 420, wakati katika kipindi cha mwaka 2019/20 ilikuwa ni 219, hivyo idadi hiyo ya miradi katika miaka hii imepungua kwa asilimia 48. Pamoja na kushuka kwa idadi ya miradi, pia nilibaini kushuka kwa kiasi cha mitaji pamoja na idadi ya nafasi za kazi zinazotokana na uwekezaji kama inavyonyeshwa kwenye Jedwali hapa chini.

Aidha, kupungua kwa idadi ya miradi mipya pamoja na mambo mengine kunatokana na mabadiliko ya Sheria ya Fedha ya mwaka 2015 ambayo iliondoa baadhi ya vivutio vya kodi kwa wawekezaji, kwa mfano kuondoa vivutio vya kodi katika upanuzi wa miradi kutoka katika kundi la miradi inayopaswa kupewa vivutio vya kodi.

JEDWALI NA. 2: KUSHUKA KWA IDADI YA MIRADI INAYOSAJILIWA NA TIC

Maelezo
2015/16 2016/17 2017/2018 2018/2019 2019/2020
Miradi ya uwekezaji
iliyosajiliwa
420​
352​
274​
272​
219​
Kiasi cha mitaji mipya kilichowekezwa (MilioniDola za Marekani)7,716.39
2,777​
2,285​
2,577.57​
1,853.47​
Nafasi za ajira zilizotengenezwa kufuatia uwekezaji mpya
63,223​
26,051​
33,702​
48,102​
32,115​
Chanzo: Taarifa ya utendaji ya TIC ya mwaka 2019/20

Aidha, kushuka kwa idadi ya uwekezaji kuna athari kubwa kwa Taifa, kwani kunapunguza fursa ya ajira, kodi, ujuzi pamoja na usambazaji wa Teknolojia.

Mapungufu katika kusimamia Masurufu Sh. Bilioni 9.40

Nilifanya mapitio ya masurufu kwa mwaka 2019/20 ambapo nilibaini mashirika 29 yalikuwa na masurufu yafikiayo Sh. bilioni 9.40 ambayo yalikuwa hayajarejeshwa mpaka mwishoni mwa mwaka yakiwa yamezidi siku 14 baada ya kukamilika kwa kazi. Nilibaini pia kuwa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) kiliripoti masurufu katika hesabu zake kama matumizi katika taarifa zake za fedha wakati hayo yalikuwa bado hayajarejeshwa.

Niligundua kuwa Mashirika hayajaweka mkazo juu ya urejeshaji wa masurufu ikiwa pamoja na kufanya makato kupitia mishahara ya watumishi husika. Ni imani yangu kuwa masurufu ambayo hayajarejeshwa yanaweza pelekea hasara ya fedha za umma. Lakini pia inachelewesha kutambua ama matumizi au mali zitokanazo na matumizi ya masurufu hayo katika vitabu vya hesabu na hivyo kusababisha kutoa taarifa zenye upungufu wa matumizi hali kiasi cha wadaiwa kikiwa kikubwa wakati shughuli zilizotekelezwa kwa masurufu zilikwisha kamilika.

Ninapendekeza kuwa Mashirika ya Umma yaweka msisitizo katika udhibiti wa masurufu yasiyorejeshwa na kuhakikisha masurufu yanarejeshwa kwa muda muafaka na hatua za kurejesha zinafuatwa pale ucheleweshwaji unapojitokeza ikiwa pamoja na kukata masurufu hayo kwenye mishahara ya watumishi husika.

Miamala Isiyo na Viambatisho Sh. Bilioni 4.954

Nilibaini mashirika tisa (9) ya umma ambayo yaliingia gharama zenye jumla ya Sh. bilioni 4.954 katika kutekeleza shughuli mbalimbali lakini gharama hizo zilikosa vielelezo vya kutosha kuhalalisha malipo hayo kama yalivyoainishwa kwenye Kiambatisho Na. 6. Mapungufu haya yanasababishwa na udhaifu katika udhibiti wa ndani wa taasisi katika utunzaji wa nyaraka za malipo yanayofanywa katika kutekeleza majukumu ya taasisi hizo.

Kutorejesha Mikopo ya NSSF kutoka kwenye SACCOS Sh. Bilioni 14

Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) linadai mikopo ya Sh. bilioni 28.8 kutoka kwenye Vyama vya Kuweka na Kukopa (SACCOS) vipatavyo 134 hadi kufikia tarehe 30 Juni 2020. Nilibaini kuwa, vyama 14 vilivyokopeshwa Sh. bilioni 14 havifanyi marejesho ya mikopo. Hali hii inasababisha hasara kwa NSSF na ukosefu wa fedha za kugharamia kazi zingine.

Deni la Watumishi wa Mikataba Ambalo Halijalipwa kwa Muda wa Zaidi ya Miaka Minne Sh. Bilioni 2.31

Nilibaini kuwa Chuo Kikuu cha Dar es salaam kilikuwa na deni la Sh. bilioni 2.31 mpaka kufikia tarehe 30 Juni 2020 ikiwa ni malimbikizo ya kiinua mgongo kwa watumishi wake ambao mikataba ya kazi ilikuwa imeisha kwa kipindi cha mwaka 2016 na miaka ya nyuma ya hapo. Nilifahamu kuwa kiinua mgongo hulipwa na Serikali na Chuo kilionesha deni hilo katika vitabu vyake lakini hakikuonesha kama kinaidai Serikali fedha hizo.

Ni maoni yangu kuwa deni hili lilisababishwa na ufuatiliaji mdogo wa menejimenti ya chuo katika kuhakikisha Serikali inalipa madeni hayo.

Kuendelea kuwa na madeni ya watumishi waliomaliza mikataba yao kwa muda mrefu si tu huwafanya watumishi hao kuhangaika bali pia fedha hupoteza thamani kutokana na kupita kwa muda na hivyo kutokuwa na thamani iliyotarajiwa wakati wa kulipwa.

Akaunti za Benki zilizokuwa zinafanya kazi bila ya kuwa katika Taarifa za Chuo Kikuu cha Dar es Salaam

Katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam nilibaini akaunti 21 za benki zikiwa na kiasi cha jumla ya Sh. bilioni 1.5 kufikia tarehe 30 Juni 2020. Miamala mbalimbali ilifanyika katika akaunti husika, lakini taarifa za akaunti hazikuripotiwa katika taarifa za fedha za Chuo. Kitendo hiki kinatoa mwanya wa matumizi mabaya ya fedha kutoka kwenye akaunti hizo.

Mashirika ya umma yasiyokuwa na bodi za wakurugenzi

Nilibaini Mashirika 30 kutokuwa na bodi za wakurugenzi, kati ya hayo, 20 hayana bodi kwa muda wa chini ya mwaka mmoja, tisa (9) hayana bodi kwa zaidi ya mwaka mmoja na moja halina bodi kwa miaka miwili. Mbali na kukosekana kwa bodi katika taasisi hizi, pia mashirika matano (5) yanaongozwa na kaimu wakurugenzi wakuu kama inavyoainishwa kwenye (Kiambatisho Na.14)

Kukosekana kwa Bodi kwenye taasisi hizi kunazorotesha ufanisi wa mashirika haya pia husababisha kuchelewa kwa kutolewa maazimio na utekelezaji wa maamuzi muhimu ya kimkakati ikiwa ni pamoja na uidhinishaji wa miongozo, kanuni na sera.

Wingi wa idadi ya vikao vya bodi za wakurugenzi

Nimebaini uwepo wa Mashirika saba (7) yaliyofanya vikao vingi vya bodi kwa mwaka wa fedha 2019/20, kinyume na Waraka wa Msajili wa Hazina Na 12 wa mwaka 2015 unaotaka Mashirika ya Umma kufanya vikao vinne vya bodi kwa mwaka. Mashirika hayo yalifanya vikao kuanzia tisa (9) hadi 13 kama ilivyoainishwa kwenye Jedwali hapa chini. Hali hii inaongeza gharama za uendeshaji kwa taasisi hukusika.

JEDWALI: TAASISI ZENYE VIKAO VINGI VYA BODI

Na. Jina la Taasisi Idadi ya Vikao
1
Shirika la Wakala wa Meli Tanzania
13​
2
Benki ya Posta Tanzania
11​
3
Shirika ya Nyumba la Taifa
11​
4
Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano Tanzania
11​
5
Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania
10​
6
Chuo cha Kumbukumbu cha Mwalimu Nyerere
9​
7
Chuo Kikuu cha Mzumbe
9​

Kampuni Tanzu Zilizopata Hasara

Kuna jumla ya kampuni tanzu tano (5) zilizopata hasara. Hasara hii kwa kiasi kikubwa, ilisababishwa na kutofanya vizuri kwa biashara au uwekezaji unaofanywa na Kampuni hizo. Hasara iliyopatikana katika kampuni tanzu hizi ni kama inavyoainishwa kwenye Jedwali hapa chini.

JEDWALI NA. 3: KAMPUNI TANZU ZILIZOPATA HASARA

Na.
Jina
Wawekezaji (Mashirika ya
Umama) na Asilimia ya umiliki
Jumla ya
Kiasi-
Uwekezaji
(Sh bilioni)
Hasara
2019/20
(Sh bilioni)
1
Kampuni ya MkulaziNSSF (94%), Shirika la Magereza (PCS) (6%)
52.59​
4.72
2
Kituo cha Uwekezaji cha APC
21.88
5.17
3
Kampuni ya
Uwekezaji ya NHC &
PPF
NHC (50%)/PSSSF (50%)
6.40​
1.38
4
Kampuni ya TTCL PesaShirika la Simu Tanzania
(TTCL) (99%), Msajili wa
Hazina (1%)
2.48​
0.41​
5
Kampuni ya kiwanda cha bidhaa za ngozi cha Kimataifa cha KilimanjaroPSSSF (86%)/Shirika la Magereza (PCS) (14%)
68.12​
2.95​

Kampuni ya Ndege Tanzania

Nilifanya ukaguzi wa kiutendaji (Startegic and Operational Efficiency) kwenye Kampuni ya Ndege Tanzania na kubaini yafuatayo:

Hadi kufikia tarehe 30 Juni 2020, Serikali ilikuwa imenunua ndege 8 kwa gharama ya Sh. Trilioni 1.028 katika juhudi ya kuifufua Kampuni ya Ndege Tanzania.

Ndege hizo zinamilikiwa na Wakala wa Ndege za Serikali na ATCL huzikodisha.

Pamoja na kununua ndege, kwa miaka mitano yaani kuanzia 2015/16 hadi 2019/20 Serikali imeisaidia Kampuni ya Ndege kiasi cha Sh. Bilioni 153.711 kwa ajili ya shughuli za uendeshaji na maendeleo.

Kampuni ya Ndege imekuwa ikitengeneza hasara kwa miaka 5 mfululizo na mwaka huu ilitengeneza hasara ya Sh. Bilioni 60.246. Kwa miaka mitano imetengeneza hasara ya Sh. Bilioni 153.542

Hata hivyo nilibaini changamoto zifuatazo ambazo zinatakiwa kushughulikiwa ili kuimarisha utendaji wa Kampuni ya Ndege:

Bodi ya Wakurugenzi haina mjumbe hata mmoja ambaye ana uzoefu kwenye masuala ya usafiri wa anga.

Wakati wa changamoto ya Corona (Covid 19) ndege nyingi zilikuwa zimesimama lakini ATCL ilikuwa inatozwa gharama za ukodishaji bila kujali kwamba ndege zilikuwa hazifanyi kazi kutokana na changamoto ya Covid 19. Hii inatokana na ukweli kwamba Mkataba wa ukodishaji kati ya TGFA na ATCL hauna kipengele cha Force majure. Katika kipindi kati ya Machi 2020 na Juni 2020 ATCL ilitozwa na TGFA kiasi cha Sh. Bilioni 15.464 kwa ajili ya ukodishaji wa ndege.

ATCL imerithi madeni makubwa ambayo hutozwa riba, kwa Mwaka wa Fedha 2019/20 ATCL imetozwa riba ya Sh. Bilioni 12.497.

Kutokana na madeni hayo, inakuwa vigumu kwa ndege za ATCL kusafiri kwenda nje ya nchi kwani zinaweza kukamatwa

Kuna changamoto ya viwanja vya ndege hapa nchini kiasi kwamba ndege za ATCL haziwezi kuruka usiku na pia kuna viwanja ambavyo ndege haziwezi kutua zikiwa zimechukua abiria kwa uwezo wake.

Hatari ya kutoweka kwa vivutio vya utalii katika eneo la Hifadhi ya Ngorongoro

Nilibaini kuwapo kwa athari kubwa za kiikolojia na kimazingira zinazohatarisha kuharibika kwa ikolojia na kutoweka kwa wanyamapori katika eneo hilo. Shughuli za kibinadamu zinazoendelea ndani ya eneo la hifadhi zinaathiri maisha ya wanyamapori na zinaharibu miundombinu ya kiikolojia inayosaidia maisha ya viumbe hai katika eneo hilo. Hadi wakati wa ukaguzi mwezi Septemba 2020, bado hapakuwa na maamuzi ya kusitisha shughuli za kibinadamu ambazo zinaendelea kufifisha maisha ya wanyamapori na mazingira ya eneo la hifadhi.

Pia, nilibaini kuwa, idadi ya watu wanaoishi katika eneo hilo iliongezeka kutoka takribani 8,000 miaka ya 1950 hadi kufikia zaidi ya watu 93,000 (Sensa ya mwaka 2017). Idadi ya mifugo iliongezaka na kufikia zaidi ya 750,000 kutoka 250,000. Pia, nilibaini tamaduni za jamii zinazoishi ndani ya hifadhi zimebadilika kutoka wafugaji wa kuhamahama wasio na makazi ya kudumu na kuwa jamii za wafugaji zilizoanzisha makazi ya kudumu ambapo kwa sasa kuna vijiji 25 ambavyo baadhi yake vimekuwa miji na kujengwa nyumba za kisasa bila kuzingatia masharti ya uhifadhi; na zimejengwa shule 25 na vituo vya afya 11 kwa ajili ya kuboresha huduma za kibinadamu ndani ya eneo la hifadhi. Shughuli za kibinadamu zimechangia kwa kiasi kikubwa kuharibika kwa mazingira ya eneo la hifadhi na kusambaa kwa magugu vamizi.

Zaidi ya asilimia 75 ya eneo la Bonde la Ngorongoro na sehemu kubwa ya eneo la Ndutu yametapakaa magugu vamizi. Haya ni maeneo muhimu zaidi kwa malisho na makazi ya wanyamapori katika Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro. Pamoja na juhudi za Wizara ya Maliasili na Utalii kuunda timu ya kufanya mapitio ya matumizi mseto ya Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro tangu mwaka 2018, bado Serikali haijafanya maamuzi juu ya nini kifanyike kunusuru eneo hilo.

Endapo hali ya sasa itaendelea hivi, ikolojia ya Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro itaharibiwa na kushindwa kusaidia maisha ya viumbe hai katika eneo, hali inayoweza kuhatarisha hadhi ya NCA katika orodha ya urithi wa dunia.

Uchimbaji wa Madini katika Hifadhi ya Misitu Bila Kibali – Sh. 614,153,600

Nilibaini kuwa kampuni inayoitwa M/s Ward Investment Company Ltd inaendesha mashine ya kuchimba na kusaga miamba kwa ajili ya kufanya biashara katika Hifadhi ya Msitu ya Chigongwe tangu mwaka 2002, bila kuwa na kibali kutoka kwa TFSA.

Aidha, kampuni hiyo ina leseni ya madini kutoka Wizara ya Madini, ambapo leseni hiyo ni moja ya sharti la kuomba kibali kutoka TFSA. Hata hivyo, Kampuni ya M/s Ward Investment Company Ltd ilishindwa kuomba kibali kutoka TFSA; hivyo, kukosa kigezo cha kuendesha shughuli za uchimbaji katika Hifadhi ya Misitu ya Chigongwe kwa miaka 18. Tatizo hili linaleta wasiwasi kuhusu ni jinsi gani limeachwa kuendelea bila kudhibitiwa kwa miaka 18.

Uchimbaji katika hifadhi ya msitu bila kibali umeinyima TFSA mapato ya miaka 18 yenye thamani ya Sh. 614,153,600 kwa sababu ya kutokukusanywa kwa ushuru uliotajwa chini ya Kanuni ya 29 (1) ya Udhibiti wa Misitu, 2004 (marekebisho ya mwaka 2017). Pia, nina wasiwasi juu ya hali ya mazingira katika eneo hilo kwa sababu ya ukosefu wa mpango wa usimamizi wa mazingira ambao ni muhimu katika kuhakikisha utunzaji wa mazingira.


Ukaguzi Maalumu Katika Mamlaka ya Bandari Tanzania

Ndugu Wanahabari,

Nilifanya kaguzi maalumu kadhaa katika Mamlaka ya Bandari Tanzania na kubaini mapungufu yafuatayo:

Upotevu wa Mapato kwa kutoa Msamaha Usiostahili wa Dola za Marekani 979,126.59 kwa Kampuni ya Saruji ya Mbeya

Tarehe 30 Aprili 2018 menejimenti ya Mamlaka ya Bandari Tanzania ilipeleka kwenye Bodi ya Usimamizi maombi ya msamaha wa Dola za Marekani milioni 1.52 kuiombea Kampuni ya Saruji Mbeya kwa ajili ya wateja wake walioko Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wanaosafirisha saruji kupitia Bandari ya Kasanga. Kampuni ya Saruji Mbeya ilieleza sababu kuwa, wateja hao walipata changamoto ya kukosa meli za kuja Bandari ya Kasanga kuchukua shehena ya saruji iliyokuwa imeagizwa na hivyo kupelekea shehena hiyo kuharibika. Mnamo tarehe 17 Aprili 2019 kupitia azimio la Bodi ilitoa msamaha wa asilimia 100 kama ilivyoombwa. Kampuni ya Saruji ilipaswa kulipa Dola za Marekani 50,000 kama gharama za utunzaji na Dola za Marekani 7,226 kwa ada tu ya kuondoa shehena. Ukaguzi wangu uliangalia ukweli wa msamaha uliotolewa na uligundua shehena ya tani 1,445.2 (mifuko 28,904) ambayo ilioharibika katika Bandari ya Kasanga ilikuwa na malimbikizo ya gharama ya Dola za Marekani 543,224.66 iliyostahili kutolewa msamaha. Hata hivyo, maombi ya msamaha yaliyopelekwa katika Bodi mnamo tarehe 14 Aprili 2019 yalikuwa ya Dola za Marekani milioni 1.52 yakijumuisha madeni ya saruji iliyoharibika ya Dola za Marekani 543,244.66 na gharama za utunzaji Dola za Marekani 979,126.59 kwa shehena zilizosafirishwa kutoka Bandari ya Kasanga katika kipindi za Januari 2013 na Oktoba 2017 na hakukuwa na hasara iliyopatikana na hivyo kutostahili msamaha.

Kuchukulia shehena nzima ya tani 1445.2 kama imeharibika na kutoa msamaha wa dola za Marekani milioni 1.52 badala ya gharama sahihi ya Dola za Marekani 543,244.66 kuliisababishia Mamlaka ya Bandari Tanzania upotevu wa mapato wa Dola za Marekani 979,126.59.

Matumizi Mabaya ya Fedha na Ubadhirifu wa Malipo ya Sh. Bilioni 3.76

Ukaguzi wangu wa malipo ulibaini mapungufu yafuatayo:

Jumla ya malipo ya Sh. milioni 604.77 yaliandikwa kama malipo kwa wazabuni mbalimbali lakini nilibaini fedha hizo zililipwa kwa wafanyakazi wa Bandari ya Kigoma baada ya kutolewa benki. Katika kutekeleza hili, maofisa husika walitumia hundi wazi zilizosainiwa kabisa kwa madhumuni ya malipo ya dharura. Malipo yote yalifanyika bila ya hati za malipo na viambatisho vingine.

Jumla ya Sh. milioni 375.46 zililipwa kwa mzabuni ambaye hakuwa na mkataba wa kusambaza bidhaa zozote kwa Bandari ya Kigoma kwa mwaka wa fedha 2017/18 na 2018/19.

Sh. bilioni 2.19 zilitolewa benki bila hati za malipo. Hati za malipo zilizowasilishwa wakati wa ukaguzi hazikulingana na hundi zilizotumika kutolea fedha hizo benki. Kukosekana kwa hati za malipo husika zinazoonesha walipwaji au kiasi cha fedha kilichokuwepo mwishoni mwa mwaka wa fedha 2017/18 na 2018/19, kwa maoni yangu, kiasi hicho kilitumika kwa ubadhirifu.

Jumla ya malipo 81 ya Sh. milioni 355.45 yalifanywa bila hati za malipo na viambatisho vyake.

Jumla ya hati za malipo 34 za Sh. milioni 227.19 hazikuwa na viambatisho vinavyothibitisha malipo hayo; hivyo sikuweza kuthibitisha uhalali na usahihi wa malipo hayo.

Usimamizi Dhaifu katika Uhamishaji wa Fedha na Makadirio ya Mtiririko wa Fedha Katika Bandari ya Kigoma

Waraka Namba 5 wa 2016/17 kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu ulizitaka idara zote za makao makuu na bandari zote kuwasilisha makadirio ya mtiririko wa fedha kila mwezi kwa Mkurugenzi wa Fedha kabla ya kupelekwa kwa Mkurugenzi Mkuu kutoa idhini ya matumizi. Hakuna malipo yaliyotakiwa kufanyika bila idhini ya Mkurugenzi Mkuu.

Kupitia ukaguzi, nilibaini mapungufu yafuatayo:

Katika miaka 2017/18 na 2018/19 kiasi kilichoombwa na Bandari ya Kigoma ni zaidi kwa Sh. milioni 303.64 ya kiasi kilichoidhinishwa cha Sh. bilioni 7.25

Kiasi kilichotumwa Bandari ya Kigoma ni zaidi kwa Sh. bilioni 2.67.

Sh. milioni 325.86 zilitumwa Bandari ya Kigoma bila kuombwa.

Sh. milioni 128.43 zilitumwa mara mbili ili kumlipa mzabuni ambapo Sh. milioni 128.43 zilitumika kumlipa mzabuni na kiasi kilichosalia cha Sh. milioni 128.43 hakikuwa na maelezo ya kwanini kilibaki kwenye akaunti ya Bandari ya Kigoma. Kiasi hiki ni sehemu ya fedha zilizotumwa zaidi ya zilizoidhinishwa kama ilivyoelezwa hapo juu yaani Sh. bilioni 2.67.

Kitendo cha fedha kutolewa zaidi ya makadirio yaliyoidhinishwa kinaonesha kuwepo kwa udhaifu katika udhibiti wa kutoa na kusimamia matumizi ya fedha.

Utumaji wa fedha bila ya udhibiti na uidhinishaji ndio umesababisha ubadhirifu wa fedha katika Bandari ya Kigoma.

Ufutwaji wa Wadaiwa bila Idhini Sh. Bilioni 1.96

Kupitia taarifa za fedha za miaka 2017/18 na 2018/19 nilibaini uwepo wa masahihisho yaliyopelekea kufuta wadaiwa wa Mamlaka ya Bandari Tanzania wenye jumla ya Sh. bilioni 1.96 bila idhini ya Bodi ya Usimamizi. Pia, hakukuwa na maelezo kutoka kwa menejimenti ya kwa nini madai hayo yalifutwa.

Masahihisho hayo inawezekana yalifanyika kwa makusudi ili kufuta wadaiwa ili kuficha ubadhirifu wa fedha.

Nilibaini pia masahihisho batili ya Sh. bilioni 10.41 na masahihisho yasiyokuwa na vielelezo ya Sh. bilioni 14.56.

Ninapendekeza Mamlaka ya Bandari Tanzania:

Iimarishe udhibiti wa ndani wa masahihisho ili kuhakikisha yanafuata taratibu zote kama ilivyoainishwa katika kanuni za fedha;

Ichukue hatua za kinidhamu na kisheria dhidi ya maofisa waliohusika kufuta wadaiwa na kuhakikisha wadaiwa hao wanarejeshwa na mapato yanakusanywa.

Wadaiwa Sugu wa Muda Mrefu sh. Bilioni 1.84 na Dola za Marekani 311,904

Nilibaini kuwepo kwa wadaiwa sugu wa tangu 2012/13 na 2014/15 wa Dola za Marekani 311,904 na Sh. bilioni 1.84 mtawalia ambapo madeni hayo yamekuwapo kwa muda mrefu katika Bandari ya Kigoma. Kati ya wadaiwa hao kulikuwa na jumla ya Sh. milioni 921.80 ambazo ni wadaiwa waliokuwa hawaendelei kufanya kazi na Mamlaka; na kwa wazabuni waliokuwa wakiendelea kufanya kazi na Mamlaka hakukuwa na mipango yoyote ya kukusanya madeni hayo.

Hasara Sh. Milioni 951.78 Katika Ujenzi wa Gati la Sibwesa Katika Ziwa Tanganyika

Tarehe 19 Mei 2015 Mamlaka ya Bandari Tanzania iliingia mkataba na Kampuni ya Saxon Building kwa ajili ya ujenzi wa Gati la Sibwesa katika Ziwa Tanganyika kwa muda wa miezi 12 wenye thamani ya Sh. bilioni 3.45. Mwanzoni kazi hii ilitarajiwa kukamilika tarehe 20 Aprili 2016 ambayo baadaye muda uliongezwa na kuwa 30 Juni 2018.

Hata hivyo, nilibaini mzabuni aliyepewa zabuni hii hakuwa na sifa kwa kuwa Bodi ya Usajili wa Wakandarasi ilimsajili kufanya kazi zenye thamani isiyozidi Sh. bilioni 1.5 na hivyo kupelekea kutostahili kupewa mkataba huo. Hali hii ilisababisha ucheleweshaji wa utekelezaji wa mkataba ambapo hadi tarehe 30 Juni 2020 Mamlaka ya Bandari Tanzania haikuwa imekabidhiwa mradi huo.

Kanuni ya 112(1) na (2) ya Kanuni za Manunuzi ya Umma za Mwaka 2013 (kama zilivyorekebishwa mwaka 2016) inataka kutoza adhabu ya kuchelewa kukamilisha kazi kwa kiasi cha kati ya asilimia 0.1 na 0.15 ya thamani ya mkataba. Nilibaini Mamlaka ya Bandari Tanzania ilishindwa kutoza adhabu ya asilimia 0.1 ya thamani ya bei ya mkataba na hivyo kusababisha upotevu wa mapato wa Sh. milioni 325.26.

Pia, nilibaini kiasi cha fedha Sh. milioni 634.2 kilitumwa kwa ajili ya kulipa hati za madai ya malipo namba 11 hadi 14 zilizogushiwa kabla ya kukamilika kwa kazi, ambapo Sh. milioni 626.51 zilitumika kufanya malipo yasiyostahiki ambayo kazi yake haikuidhinishwa na Sh. milioni 7.68 zilibakia kwenye akaunti ya Bandari ya Kigoma bila maelezo yoyote. Ufuatiliaji duni wa utekelezaji wa miradi ndiyo uliosababisha upotevu huo wa mapato kwa kiasi cha Sh. milioni 951.78.

Mfumo wa Enterprise Resource Planning (ERP)

Maagizo yaliyotolewa na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali yaliitaka Mamlaka ya Bandari Tanzania kuboresha mifumo ya kusimamia ukusanyaji wa maduhuli kwa njia ya kielekitroniki ili kuleta ufanisi katika utendaji wake ili kuongeza mapato. Menejimenti ya Mamlaka ya Bandari Tanzania ilitekeleza maagizo hayo kwa kusimika mfumo wa ERP ili kuwezesha kusimamia kwa ufanisi rasilimmali-watu, fedha na shughuli zingine. Mnamo tarehe 31 Octoba 2019, Katibu Mkuu Kiongozi aliniomba kufanyika ukaguzi wa namna mchakato wa zabuni na utekelezaji wa mkataba wa usimikaji wa mfumo wa ERP katika Mamlaka ya Bandari Tanzania ilivyofanywa.

Kwa kuzingatia barua hiyo, kupitia Kifungu cha 29 cha Sheria ya Ukaguzi wa Umma ya Mwaka 2008 nilianzisha Ukaguzi Maalumu tarehe 14 Juni 2020 ili kubaini ukweli juu ya taarifa zilizowasilishwa. Ukaguzi wangu ulibaini mapungufu yafuatayo:

Hasara ya Sh. Milioni 655.58 Kutokana na Kuingia Mkataba na Mzabuni Asiye na Sifa

Mnamo tarehe 14 Julai 2010, Mamlaka ya Bandari Tanzania iliingia mkataba na Kampuni ya

Soft Tech Consultant kwa ajili ya Ununuzi na Usimikaji wa mfumo wa ERP kwa Sh. milioni 694.14 kwa muda wa miezi saba (7). Nilibaini mapungufu yafuatayo katika ununuzi na utekelezaji wa mkataba huo:

Mzabuni hakuwa na sifa zinazostahili, ambapo mfumo ulioletwa haukuwa na kipegele cha udhibiti wa bajeti, bajeti kuu na uhasibu wa gharama na pia ulikosa sehemu ya shughuli za forodha kama mkataba ulivyotaka. Hata hivyo, Mamlaka ya Bandari Tanzania ilimtunuku mkataba pamoja na mapungufu yaliyoonekana.

Mamlaka ya Bandari Tanzania ilikuwa imeshatumia kiasi cha Sh. milioni 600.44 baada ya kukabidhiwa mfumo huo tarehe 30 Juni 2011 ambapo nilibaini mfumo haukuweza kutumika kwa sababu ya mapungufu yalioonekana. Hivyo, matumizi hayo ni hasara kwa Mamlaka ya Bandari Tanzania kwa sababu ilidibi ianze upya manunuzi kwa ajili ya mfumo huohuo.

Mamlaka ya Bandari Tanzania iliingia hasara ya dola za marekani 31,860 (Sh. milioni 55.15) iliyotokana na ulipaji wa gharama za mafunzo mara mbili kwa wafanyakazi.

Kushindwa kwa Mamlaka ya Bandari Tanzania kuomba ushauri kwenye Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-Government) katika utayarishaji wa manunuzi kama matakwa ya Kifungu 4.2.1 cha Mwongozo juu ya Matumizi, Ufanisi, na Usalama wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) uliotolewa Julai 2012 na mapungufu katika uongozi na ufatiliaji wa manunuzi na utekelezaji wa mkataba ndio mambo yaliyosababisha hasara ya Sh. milioni 655.58 kwa Mamlaka.

Hasara ya Dola za Marekani Milioni 2.26 kutokana na utekelezaji wa mkataba kutomalizika

Manamo tarehe 30 Oktoba 2015 Mamlaka ya Bandari Tanzania iliingia mkataba na mzabuni mwingine; Kampuni ya ‘Twenty Third Centrury Systems’ kwa ajili ya manunuzi ya kusambaza, kusimika, mafunzo, na kuanzisha mfumo wa SAP-ERP kwa dola za Marekani milioni 6.64. Nilibaini mapungufu yafuatayo katika manunuzi na utekelezaji wa mkataba huo:

Bodi ya Wazabuni hawakuidhinisha zabuni hiyo bali mfanyakazi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania aliidhinisha ambapo ni kinyume na Kifungu cha 33(1) (C) cha Sheria ya Manunuzi ya Umma ya Mwaka 2011 na Kanuni ya 185 ya Kanuni za Manunuzi ya Umma ya Mwaka 2013 (kama ilivyorekebishwa mwaka 2016).

Mamlaka ya Bandari Tanzania ilichagua mzabuni asiyestahili ambaye alidhihirisha kutokuwa na vigezo vya kifedha na kitaalamu pamoja na kuweka vipengele vipya katika masharti ya malipo ambavyo havikuwepo wakati wa manunuzi.

Mzabuni alileta vifaa vibovu; na alisimika mfumo wa zamani kinyume na matakwa ya mkataba.

Mzabuni alichelewesha utekelezaji wa mkataba. Hali hii ilipelekea Mamlaka ya Bandari kusitisha mkataba mnamo tarehe 21 Machi 2019, mzabuni akiwa ametekeleza asilimia 42 tu ya kazi yote, lakini akiwa ameshalipwa asilimia 70 ya mkataba sawa na dola za Marekani milioni 4.63 ambapo ilipelekea Mamlaka kupata hasara ya dola za Marekani milioni 1.86 ambayo ililipwa zaidi ya kazi iliyofanyika.

Mamlaka ya Bandari iliingia mkataba Na. AE/016/2017-18/CTB/C/14 kwa dola za Marekani 433,011 na mshauri wa kujitegemea kwa ajili ya kutoa huduma ya kukagua mfumo uliowekwa iwapo uko sawa na matakwa ya mkataba. Mkataba huu ni hasara kwa Mamlaka kwa sababu kama Mamlaka ingekuwa na umakini kuanzia mwanzo mkataba huu usingekuwepo.

Mapungufu katika manunuzi na usimamiaji katika utekelezaji wa mkataba ndio ulisababsha hasara kwa Mamlaka ya Bandari Tanzania.

Kutowasilisha Kodi ya Zuio Dola za Marekani 410,817.31

Katika utekelezaji wa mkataba Na. AE/016/2014-15/CTB/G/39, nilibaini mzabuni alilipwa jumla ya dola za Marekani milioni 1.63 katika nyakati tofauti lakini Mamlaka ya Bandari haikukata wala kuwasilisha kodi ya zuio ya dola za Marekani 410,817.31 kinyume na Vifungu vya 83 na 84 vya Sheria ya Kodi ya Mapato, hivyo kuinyima Serikali mapato.

Udhaifu Katika Mchakato wa Manunuzi kwa Mzabuni Mpya

Mnamo Agosti 2019 Mamlaka iliingia mkataba Na. AE/016/2018-19/CTB/NC/16 na mzabuni mwingine kampuni ya SAP East Africa Limited wa dola za Marekani 997,647 kwa ajili ya kumalizia usimikaji wa mfumo ambao haukutekelezwa katika mikataba ya nyuma. Nilibaini mapungufu yafuatayo katika mchakato huo wa manunuzi:

Mamlaka ilichagua mzabuni ambaye hakuwa na vigezo vya kifedha ambapo ni kinyume na Kanuni ya 206(1) (2) ya Kanuni za Manunuzi ya Umma za Mwaka 2013 (kama zilivyorekebishwa mwaka 2016);

Mkataba ulipelekwa kwa Mwanasheria Mkuu baada ya kusainiwa na pande zote na utekelezaji wake kuanza ambapo ni kinyume na Kanuni ya 59(1) ya Kanuni za Manunuzi ya Umma ya Mwaka 2013 (kama ilivyorekebishwa mwaka 2016); na

Mzabuni hakuleta dhamana ya utekelezaji wa kazi ambapo ni kinyume na Kanuni ya 29(1) ya Kanuni za Manunuzi ya Umma Na 446 ya Mwaka 2013 (mama zilivyorekebishwa mwaka 2016).

Hadi kufikia Juni 2020, usimikaji wa mfumo wa ERP ulikuwa haujakamilika tangu mchakato ulivyoanza mwaka 2010. Kutozingatia Sheria ya Manunuzi ya Umma ya Mwaka 2011 na Kanuni zake za Mwaka 2013 (kama zilivyorekebishwa mwaka 2016), na udhaifu katika usimamizi wa utekelezaji wa mikataba ndio sababu kuu ya ucheleweshaji wa kumalizika kwa mkataba huo.



MAPUNGUFU KATIKA UTEKELEZAJI NA UKAMILISHAJI WA MIRADI YA MAJI


Ndugu Wanahabari

Nilifanya ukaguzi katika miradi mbalimbali ya maji hapa nchini na kubaini yafuatayo:

Miradi ya Maji Iliyotelekezwa yenye Thamani ya Sh. Bilioni 1.126

Nimebaini miradi miwili ya maji yenye yenye thamani ya Sh. bilioni 1.126 katika Halmashauri za Kigoma Ujiji na Ikungi ambayo imetelekezwa na wakandarasi kwa kipindi cha miezi 6 hadi miezi 34 mpaka wakati wa ukaguzi kama inavyoonekana kwenye Jedwali hapa.

MIRADI ILIYOTELEKEZWA NA WAKANDARASI KWA ZAIDI YA MIEZI SITA

MKOA
OFISI YA WILAYA
JINA LA MRADI
NAMBA YA MKATABA
GHARAMA YA MKATABA
(Sh.)
Kigoma Kigoma-ujijiUjenzi wa Mradi wa maji
Mgumile
LGA/042/2013-2014/12
721,438,645​
Singida IkungiUjenzi wa Mradi wa maji Kijiji cha MtunduruLGA/146/2018/2019/W/ 02
405,007,269​
Jumla
1,126,445,914
Hali hii inaathiri upatikanaji wa huduma ya maji kwa jamii iliyolengwa.

Ongezeko la Gharama Kwenye Huduma ya Mkandarasi Mshauri - Sh. Bilioni 8.6

Nilikagua miradi ya maji katika Miji ya Kigoma, Lindi na Sumbawanga na kubaini ongezeko la gharama ya mkandarasi Mshauri Kampuni ya LAHMEYER GKW Consult GmbH ya Ujerumani kwa Sh. bilioni 8.6 kutoka Sh billion 4.60 hadi Sh. bilioni 13.26. Ongezeko hili lilitokana na kuongezeka kwa muda wa mkataba kwa miezi 46 kutoka tarehe 11 Aprili 2013 hadi tarehe 10 Februari 2017.

Kuchelewesha Utekelezaji wa Miradi ya Maji – Sh. Bilioni 40.066

Nimebaini uwepo wa miradi ya maji 20 ambayo imechelewa kukamilika yenye gharama ya Sh. bilioni 40.07 (Kiambatisho Na. 11) inayotekelezwa na RUWASA. Hali inayopelekea kuchelewesha huduma ya maji kuwafikia wananchi. Pia, inaweza kuongeza gharama za mradi.

Fedha za Miradi ya Maji Kiasi cha Sh. Bilioni 2.216 Zilizotumika kwa Matumizi Mengine

Nilibaini Halmashauri 14 zilikata Sh. bilioni 2.216 kutoka katika malipo ya wakandarasi kama fedha za matazamio na kuzitunza katika akaunti ya amana. Hata hivyo, baadaye fedha hizo zilitumika kwa matumizi mengineyo yasiyohusiana na ujenzi wa miradi ya maji kama zinavyooneshwa kwenye Jedwali hapa chini na hazikuwa zimerejeshwa mpaka wakati ukaguzi huu unakamilika.

JEDWALI: MATUMIZI FEDHA ZA MIRADI YA MAJI KINYUME NA MALENGO YALIYOKUSUDIWA​

Halmashauri
Kiasi (Sh.)
Maelezo
H/W Rorya
146,932,728​
Fedha za matazamio hazikuhamishwa kwenda RUWASA
H/W Meru
126,520,954​
Fedha za matazamio hazikuhamishwa kwenda RUWASA
H/W Siha
40,998,021​
Fedha za Usimamizi wa miradi hazikuhamishwa kwenda RUWASA
H/W Kilosa
193,051,360​
Fedha za matazamio hazikuhamishwa kwenda RUWASA
H/W Morogoro
325,329,093​
Fedha za matazamio hazikuhamishwa kwenda RUWASA
H/M Singida
265,766,172​
Fedha za matazamio hazikuhamishwa kwenda RUWASA
H/W Kibondo
22,000,000​
Fedha za mradi wa maji Mgoboka zimetumika kulipa gharama za umeme zilizotakiwa kulipwa na Mamlaka ya Maji Kibondo Mjini
H/W Kasulu
195,382,273​
Fedha za matazamio hazikuhamishwa kwenda RUWASA
H/W Kongwa
220,151,459​
Fedha za matazamio hazikuhamishwa kwenda RUWASA
H/W Mbulu
170,028,525​
Fedha za matazamio hazikuhamishwa kwenda RUWASA
H/W Kiteto
76,282,058​
Fedha za matazamio hazikuhamishwa kwenda RUWASA
H/W Itilima
201,252,801​
Matumizi ya fedha za matazamio katika Akaunti ya Amana
H/W Sumbawanga
164,091,492​
Fedha za matazamio hazikuhamishwa kwenda RUWASA
H/W Njombe
68,858,405​
Fedha za matazamio hazikuhamishwa kwenda RUWASA
Jumla
2,216,645,340

Ujenzi wa Miradi ya Maji Yenye Thamani ya Sh. Bilioni 4.709 Isiyofanya Kazi

Nimebaini miradi yenye thamani ya Sh. bilioni 4.709 katika Halmashauri 11 isiyofanya kazi ya kutoa huduma ya maji kutokana na miundombinu ya mabomba kutelekezwa, kutoendelezwa kwa miradi baada ya mikataba kuvunjwa na uharibifu utokanao na majanga ya asili, kama ilivyoelezewa katika Kiambatisho Na. 5.

Kuchelewa Kutekeleza na Kukamilisha Miradi ya Maji Yenye Thamani ya Sh. Bilioni 32.486

Nimebaini matukio 42 ambapo ukamilishwaji wa miradi yenye thamani ya Sh. 32.486 umecheleweshwa, kinyume na vifungu vya mikataba ambavyo vinahitaji miradi kuanza na kukamilika kwa wakati uliowekwa katika mikataba husika. Maelezo zaidi yanaonekana katika Kiambatisho Na. 13.

Kwa maoni yangu, ucheleweshaji wa malipo, utekelezaji wa miradi kwa kasi ndogo, usanifu duni wa miradi na kutunuku zabuni kwa wakandarasi wasio na vigezo stahiki imezuia jamii husika kunufaika na miradi hiyo. Hii pia imeziweka Halmashauri kwenye hatari ya kuongezeka kwa gharama za miradi kunakoweza kusababishwa na mabadiliko ya bei.

Mikataba Iliyotekelezwa bila ya Kuwapo kwa Dhamana za Utendaji Sh. Bilioni 14.578

Nimekagua Majalada ya Mikataba katika Ofisi tano za Wilaya za RUWASA na kubaini kuwa mikataba yenye thamani ya Sh. 14,578,220,387 ilitekelezwa bila dhamana za utendaji kama inavyoonekana katika Jedwali hapa chini.

Jedwali: Mikataba Iliyotekelezwa bila Dhamana za Utendaji

MKOA
OFISI YA WILAYA
NAMBA YA MKATABA
MAELEZO YA MKATABA
GHARAMA YA MKATABA (Sh.)
NjombeNjombeUjenzi wa mfumo wa kusambaza maji katika vijiji vya
Usetule-Mahongole
LGA/166/2018/201 9/W/01
7,996,231,305​
MtwaraMasasiUkarabati wa Mradi wa maji vijiji vya Mwena hadi LiloyaLGA/083/2016/201 7/W/21 LOT 01
4,471,710,595​
SingidaIkungiUjenzi wa mfumo wa kusambaza maji katika Kijiji cha MtunduruLGA/146/2018/201 9/W/02
405,007,269​
DodomaMpwapwaUjenzi wa Mradi wa kusambaza maji katika kijiji cha KidengeLGA/023/2016/201 7/W/21
1,070,460,729​
KataviTanganyikaUjenzi wa Mradi wa kusambaza maji katika kijiji cha KabunguLGA.099/2017/201
8/W/WATER/02/Lo
t 1
634,810,489​
Jumla
14,578,220,387
Chanzo: Taarifa ya Ukaguzi kwa Menejimenti 2019/2020


Kwa maoni yangu, kukosekana kwa hati za dhamana za utendaji kunaiweka RUWASA katika hatari ya kupoteza rasilimali zake kwa miradi inayoendelea endapo wakandarasi watashindwa kutekeleza kikamilifu mikataba au wakisitisha utekelezaji wa miradi husika.

Mikataba Yenye Thamani ya Sh. Bilioni 25.561 Haikufanyiwa Upekuzi wa Kisheria

Nimebaini mikataba minne katika halmashauri tatu ambayo haikufanyiwa upekuzi na mikataba miwili katika Halmashauri ya Mji Makambako na Halmashauri ya Wilaya ya Wanging'ombe ambayo ilipekuliwa kabla ya mwajiri kukubali ofa ya wakandarasi. Mikataba hiyo imeainishwa kwenyeJedwali hapa chini.

MAPUNGUFU YALIYOBAINIKA KATIKA UPEKUZI WA MIKATABA

Halmashauri
Jina la Mradi
Namba ya Mkataba
Gharama ya Mkataba (Sh.)
Mapungufu
H/W MpandaUjenzi wa mradi wa kusambaza maji katika Kijiji cha KabunguLGA.099/20
17/2018/W/
WATER/02/
Lot 1
634,810,489​
Haukupekuliwa na
Mwanasheria wa
Halmashauri
H/W KigomaUjenzi wa mradi wa kusambaza maji katika Vijiji vya Kaseke, Kimbwela na
Nyamoli
LGA/043/20
16/2017/W/
15
1,163,496,000​
Haukupekuliwa na Mwanasheria
Mkuu wa Serikali.
H/W Wanging'ombeUjenzi wa mradi wa maji wa
Igando-Kijombe
LGA/153/20
17/2018/W/
01
12,437,407,360​
Mikataba ilipekuliwa kabla ya halmashauri mkandarasi kukubaliwa ofa
H/W MakambakoUjenzi wa mradi wa kusambaza maji wa Usetule-
Mahongole
LGA/166/20
18/2019/W/
01
7,996,231,305​
H/W MkurangaUjenzi wa mradi wa maji
Mwanambaya
LGA/012/W
S/2017/201
8/w/01-02
2,347,737,221​
Haukupekuliwa na Mwanasheria
Mkuu wa Serikali.
Ujenzi wa mradi wa visima
vya maji katika Kijiji cha Mkerezange
LGA/012/W
S/2017/201
8/w/01-03
981,996,310Haukupekuliwa na mwanasheria wa halmashauri.
Jumla
25,561,678,685


Kwa maoni yangu, kutofanya upekuzi wa mikataba kunaziweka Halmashauri katika hatari za kisheria na kunaweza kuhatarisha thamani ya fedha kwa miradi hiyo.

Mikataba iliyotunukiwa kwa wakandarasi wasio na vigezo/sifa stahiki yenye thamani ya Sh. bilioni 6.91

Nilikagua zabuni zilizowasilishwa na ripoti za tathmini za zabuni 14 katika Halmashauri tisa na kubaini mikataba ya thamani ya Sh. bilioni 6.91 ilipewa wakandarasi wasiostahili.

Kwa maoni yangu, tuzo za mikataba kwa wakandarasi wasiostahili, kumechelewesha kukamilika kwa miradi. Kutowajibika ipasavyo kwa kamati za tathmini, kunaweza kusababisha kutofikiwa kwa thamani ya fedha kwa miradi inayotekelezwa.

Mikataba yenye thamani ya Sh. bilioni 3.236 iliyosainiwa na kutekelezwa na kampuni za ubia zisizosajiliwa

Mapitio ya majalada ya mikataba na nyaraka za zabuni yalibaini kuwa, Halmashauri tatu ziliingia mikataba yenye thamani ya Sh. bilioni 3.236 na kampuni zenye ubia ambao haujasajiliwa kama Sheria ya Usajili wa Makandarasi inavyotaka, kama invyoonekana kwenye Jedwali hapa chini.

MIKATABA ILIYOSAINIWA NA KUTEKELEZWA NA KAMPUNI ZA UBIA ZISIZOSAJILIWA

Halmashauri Namba
ya
Mkataba
Maelezo ya Mkataba Gharama ya Mkataba (Sh.) Maelezo
H/W MkingaLGA/133
/20132014/WS
/W/05
Ujenzi wa miundombin u ya maji
katika kijiji cha Parungu
Kasera
955,818,325Kampuni iliyopewa kandarasi ya
M/s Eker Co. Ltd Joint Venture M/s Daman Construction Co. Ltd haijasajiliwa
H/W KibondoLGA/041
/HQ/WS
DP/MKAB
/2017-
18/03
Ujenzi wa mradi wa
maji kijiji cha
Mukabuye
1,021,088,581Hati ya usajili wa ubia ilioyotolewa na CRB iliisha muda wake tarehe 30 Disemba, 2018 hivyo ilihitaji kuhuishwa. Hata hivyo, ubia haukuhuisha usajili huo.
H/W RungweLGA/071
/2016/20
17/RDC/
W/10
LOT 03
Mradi wa
Maji Masoko
(skimu ya
Lufumbi na
Masoko)
1,260,061,273Kampuni iliyopewa kandarasi
MSUKWA GENERAL ENTERPRISES
CO. LTD JV KIBAHA BUILDING AND CIVIL CONTRACTORS Ltdhawakuwa na cheti cha usajili wa ubia wao toka Bodi ya wakandarasi na walipewa kazi zilizozidi uwezo wao
Jumla 3,236,968,179
Kwa maoni yangu, kutoa zabuni kwa Wakandarasi wasiosajiliwa kunaziweka Halmashauri katika hatari ya kupoteza fedha kutokana na uwezekano wa fidia ya Sh. 323,696,818 (Asilimia 10 ya gharama ya mkataba). Aidha, mwenendo huu unaweza kusababisha hasara zaidi, endapo itatokea migogoro ya kisheria itokanayo na Mkandarasi kushindwa kutekeleza mkataba.

Kukosekana kwa Nyaraka Timilifu za Miradi ya Maji Zenye Thamani ya Sh. Bilioni 9.152

Nilibaini matumizi ya Sh. bilioni 9.152 kwa ajili ya miradi ya maji 21, ambayo hayakuweza kuthibitika, kwa sababu Halmashauri zilishindwa kuwasilisha nyaraka za matumizi husika. Mahojiano yaliyofanyika kati ya timu ya ukaguzi na uongozi wa Halmashauri husika yalibaini kuwa, nyaraka hizo hazikuweza kuwasilishwa kwa ajili ya ukaguzi kwa sababu baadhi ya nyaraka hizo zilikuwa TAKUKURU na nyingine hazikuweza kupatikana kwa ajili ya utunzwaji dhaifu, kama inavyoonekana katika Jedwali hapa chini.

KUKOSEKANA KWA NYARAKA TIMILIFU ZA MIRADI YA MAJI KWA AJILI YA UKAGUZI

Mkoa
Halmashauri
Jina la Mkandarasi na Namba ya Mkataba
Nyaraka zilizokosekana
Kiasi (Sh.)
Kagera H/W BukobaLGA
035/W/RWSSP/FY2013/
2014/01(4) Yell Limited
Nyaraka mbalimbali za mchakato wa kumpata mkandarasi zilikuwa TAKUKURU
596,804,000.00​
Mara H/W RoryaMaginga Business Holding Co. Ltd na National Services
Construction
Department
Hati za malipo
976,942,815.00​
Manyara H/W MbuluM/s Jemason Investment
Co. Ltd-
LGA/061/WKS/2013/201 4/WSDP/NC/12,
M/s PNR Services LtdLGA/061/2011/2012/WS​
DP/NC/LOT 1,
M/s Dabenco Enterprices
Ltd-
LGA/061/2011/2012/WS
DP/NC/LOT 3,
M/s Nyangera
Construction-
LGA/061/WSDP/NC/01
na M/s UNEE (T)
Investment Company Ltd JV Yumbaka Eng. and
General Works-
LGA/061/WKS/2013/201
4/WSDP/14
Nyaraka mbalimbali
mchakato wa
mkandarasi
za kumpata
4,986,894,343.00​
Kigoma H/W KasuluM/s Earth Plan
Contractor Company Ltd
Hati za malipo
31,487,338.47​
Tabora H/W SikongeUjenzi wa mradi wa chujio la maji katika bwawa la Igumila lililopo kijiji cha Kapumpa Kata ya Kitunda
Ujenzi wa mradi wa kusambaza maji katika kijiji cha Usunga
Ujenzi wa mradi wa kusambaza maji katika Kijiji cha Msuva
Ujenzi wa mradi wa kusambaza maji katika Kijiji cha Utimle.
Ujenzi wa mradi wa kusambaza maji katika Kijiji cha Nyahua.
Upanuzi wa mradi wa maji wa kijiji cha Ipole kwenda Kijiji cha
Kabanga.
Nyaraka zote zinazohusiana na miradi 6 iliyotajwa ya mwaka
2019/20
1,097,724,216.87​
Pwani H/W
Bagamoyo
M/S Sife General
Enterprises Ltd-
BDC/2013/2014/WT/03,
Coast Belt Construction
Co. LTD-
BDC/2012/2013/03,
Nyaraka zote za utaratibu wa manunuzi
1,462,179,801.00​
Jonenac Construction
Co. LTD-
BDC/2013/2014/WT/04,
M/S Chakwale Company
Ltd-
LGA/014/2015/2016/QT
/W/17 na
M/S Sea Shoe Civil
Works-
LGA/014/2016/2017/QT
/W/R/02
M/S Sea Shoe Civil
Works-
LGA/014/2017/2018/QT
/W/R/01
Jumla
9,152,032,514.34


5.5 USIMAMIZI WA MIRADI YA KIMKAKATI

5.5.1 UJENZI WA RELI YA KISASA (SGR) KUTOKA DAR ES SALAAM HADI MAKUTUPORA KIPANDE CHA KWANZA NA CHA PILI

Raia wa kigeni kufanya kazi nchini bila vibali

Nilibaini raia wa kigeni 586 kati ya 924 walioajiriwa kwenye kipande cha kwanza (1) cha ujenzi wa reli ya kisasa hawakuwa na vibali vya kufanya kazi nchini. Pia kwenye kipande cha ujenzi cha pili (2); raia wa kigeni 952 kati ya 1,484 kutokuwa na vibali vya kufanya kazi nchini. Hii ni kinyume na kifungu cha 9 (2) (a) cha Sheria za Ajira za Raia wa Kigeni ya mwaka 2015

Kutozingatiwa kwa kupata vibali vya kazi kulisababisha kutolipwa kwa ada ya vibali vya kazi inayofikia Dola za Kimarekani 1,538,000.

Ongezeko la Dola za Kimarekani milioni 11.22 kama gharama za usimamizi wa mradi kipande cha kwanza (fungu la 1) baada ya mradi kuchelewa kukamilika.

Shughuli za ujenzi wa mradi wa SGR kipande cha 1 zilitakiwa kuchukua miezi 30 kuanzia tarehe 2 Mei 2017 na kumalizika tarehe 1 Novemba 2019. Kutokana na ucheleweshaji wa utekelezaji wa mradi, tarehe ya kukamilisha mradi ilibadilishwa hadi tarehe 21 Aprili 2021 ikiwa ni nyongeza ya miezi 18. Ongezeko hili limepelekea gharama ya ziada ya mhandisi mshauri jumla ya Dola za Kimarekani milioni 11.22 inayokadiriwa kuwa Sh. bilioni 26.03.

5.5.2 UJENZI WA MRADI WA UMEME WA JULIUS NYERERE

Kutowekwa kwa mfumo wa kutoa uchafu kwenye Bwawa na kwenye njia za maji kuelekea kwenye mitambo ya kuzalisha umeme

Nilibaini Mkandarasi hakutekeleza matakwa ya mwajiri yaliyomtaka kuweka mfumo wa kudhibiti uchafu kutuama ndani ya bwawa la hifadhi ya maji kwa kuweka mifumo ya kuruhusu uchafu kutiririka nje ya bwawa la maji. Ukosefu wa mifumo ya kutoa uchafu huashiria hatari ya kuathiri uimara wa bwawa kwa sababu ya mmomonyoko wa msingi wa bwawa na kuongezeka kwa kina cha mkondo wa chini wa mto. Pia, huweza kufanya umwagiliaji kuwa mgumu kwa maeneo yaliyo baada ya bwawa.

Aidha, uchafu unaweza kuingia kwenye njia za maji yanayoenda kwenye mtambo wa kufua umeme na hivyo kusababisha athari kama vile kulika kwa mapanga ya mitambo ya kufua umeme (turbines), kupunguza ufanisi wa mtambo wa kufua umeme pamoja na kusababisha gharama za mara kwa mara za kubadilisha mapanga katika mitambo ya kufua umeme.

Wafanyakazi muhimu wa mkandarasi kutokuwa na vibali halali vya kazi

Nilibaini raia wa kigeni 46 kati ya 91 (sawa na asilimia 51) kutokuwa na vibali vya kufanya kazi nchini kinyume na matakwa ya Sheria za Ajira za Raia wa Kigeni ya mwaka 2015. Kutozingatiwa kwa kupata vibali vya kazi kulisababisha kutolipwa kwa ada ya vibali vya kazi inayofikia Dola za Marekani 25,300.

Kutokuwapo kwa upembuzi wa kina uliohuishwa

Mradi wa umeme wa JNHPP una malengo mengi kwa ajili ya matumizi ya maji. Hivyo basi, utekelezaji wake unapaswa kufuata Sheria ya Umeme ya mwaka 2008, Sheria ya Umwagiliaji ya Kitaifa ya mwaka 2013, Sheria za Usimamizi ya Vyanzo vya Maji ya mwaka 2009 na 11 Vifungu 20(2) na 20(3) Sheria ya Umwagiliaji ya Kitaifa 2013, Sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya 2004. Sheria hizi zote zinaelezea uhitaji wa kuwapo kwa upembuzi yakinifu kabla mradi haujafadhiliwa na kutekelezwa. Kwa hali hii, Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kupitia Mhandisi Mshauri na Msimamizi wa Mradi (TECU) kama mwakilishi wa mwajiri lilitarajiwa kupitia upya na kuhuisha upembuzi yakinifu uliofanyika hapo awali na kupata mapitio mapya ili kuitumia taarifa hiyo katika kuandaa usanifu wa kina wa kila shughuli ya Mradi wakati wa ujenzi.

Hata hivyo, nilibaini kuwa, Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) lilishindwa kuhuisha vipengele vyote vya upembuzi yakinifu uliofanyika awali. Badala yake, lilitegemea upembuzi yakinifu ambao ulifanywa katika miaka ya 1970 na 1972 na kampuni ya M/S Norconsult (ya Norway) pamoja na Mpango mtambuka wa mradi na ripoti ya uchunguzi wa kiufundi uliofanywa na kampuni ya M/S Hafslund na M/s Norplan (wote kutoka Norway) ambayo iliweza kuhuisha vipengele vya taarifa ya upembuzi yakinifu. Hii ilifanyika miaka ya 1980.

Vipengele vikuu vilivyohuishwa ni pamoja na tathmini ya athari za mazingira (EIA), usanifu wa kiufundi na utafiti wa jiolojia na utafiti wa kiutaalamu wa ufanisi wa miamba. Vipengele ambavyo havikufanyiwa mapitio na kuhuishwa ni pamoja na utafiti wa kiuchumi na kifedha wa mradi, tafiti za kuwepo kwa maji na uendeshaji endelevu wa mradi.

Maafisa waandamizi kutoka Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na TECU walieleza kwamba, upembuzi yakinifu uliofanyika katika miaka ya 1970 ulionesha kwamba mradi unawezekana kitaalamu, kiuchumi na kifedha. Maafisa waliongeza kuwa kutokana na uharaka wa kuanza utekelezaji wa mradi, taarifa za upembuzi za awali hazikuweza kupitiwa upya zote ili kuzihuisha. Sehemu ya tafiti ambazo hazikupitiwa upya ni pamoja na zile za kiuchumi na kifedha, upatikanaji endelevu wa maji, tabia ya miamba na usanifu wa kiuhandisi.

Yapata takribani miaka 50 tangu tafiti za upembuzi yakinifu zilipofanyika mwaka 1970, Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) lilipaswa kufanya stadi za upembuzi yakinifu ili zitoe mwongozo kwenye usanifu wa ujenzi wa mradi unaoendelea kutekelezwa. Inakuwa ni vigumu kuthibitisha juu ya uendelevu wa mradi, hasa kwa upatikanaji wa vyanzo vya maji, ili kusaidia mradi kuzalisha umeme kwa misimu yote ya mwaka.

5.5.3 MRADI WA MIUNDOMBINU YA MABASI YAENDAYO HARAKA JIJINI DAR ES SALAAM

Kituo cha Mabasi Kariakoo hakikujengwa kama michoro ilivyoelekeza

Nilibaini kituo cha mabasi cha Kariakoo kutojengwa kama mchoro ulivyoonesha kwa kujenga fremu ya aina tofauti na iliyoidhinishwa na kusababisha malipo ya ziada ya Sh. milioni 234.37. Baada ya kuhoji uhalali wa malipo ya ziada, mshauri elekezi alirudisha Sh. milioni 130.89 kama sehemu ya malipo yaliyozidi na kuacha kiasi cha Sh. milioni 103.48 ambacho hakijarejeshwa.

Aidha, nilibaini kuwa nguzo zilizojengwa kwenye kituo hicho zilikuwa fupi kuliko kimo kilichotakiwa kwenye michoro ya usanifu na michoro ya kina na kusababisha malipo ya ziada ya Sh. milioni 91.14. Baada ya ukaguzi wangu, Sh. milioni 83.43 kati ya Sh. milioni 91.14 zilirejeshwa na mkandarasi na kuacha kiasi cha Sh. milioni 7.71 ambacho hakikurejeshwa.


5.6 MATOKEO YA UKAGUZI WA MIFUMO


Ndugu Wanahabari,

Pia nilifanya ukaguzi wa Mifumo katika maeneo mbalimbali na kubaini yafuatayo:

Mapungufu katika mfumo wa MUSE

Nimekagua Mfumo wa Malipo Serikalini (MUSE), ambao ni mfumo uliotengenezwa na wataalamu wa ndani ili kuwa mbadala wa mfumo wa kihasibu uliokuwa ukitumika awali, yaani IFMS Epicor, na kubaini mapungufu yafuatayo:

Utoaji na urudishwaji wa masufuru hurekodiwa na kuripotiwa kabla ya kurekodiwa kwenye hati ya malipo na kukamilika kwa hatua za malipo.

Mfumo haurekodi taarifa za karadha (prepayment) kwenye leja ndogo (sub ledgers).

Uwepo wa bakaa kwenye “control accounts” (suspense accounts na control accounts) ambazo hazikuainishwa kwenye taarifa ya fedha.

Watumiaji wa mfumo (wahasibu) hawawezi kuhakiki miamala wanayofanya kabla ya kutuma miamala kwenye vitabu vya fedha (posting transations in books of account).

Mfumo kutofuata muongozo wa kimataifa wa ukaguzi katika sekta za umma (IPSAS), unaoelekeza matumizi kutambulika pindi huduma inapotolewa na si malipo yapofanyika. Nimebaini mfumo unazuia miamala kufanyika na kurekodiwa endapo hakuna bakaa katika kifungu husika cha matumizi.

Mapungufu haya hupelekea makosa katika taarifa za fedha, yanayopelekea urekebishaji unaohitajika kufanyika nje ya mfumo. Hivyo, kusababisha kupungua kwa ufanisi na usahihi katika uandaaji wa taarifa za fedha.

Nimekagua mfumo wa manunuzi ungamanifu wa ki-eletroniki (TANePS) unaondeshwa na Mamlaka ya Manunuzi ya Umma (PPRA). Mfumo huu ulitengenezwa na mzabuni European Dynamics, ukaguzi wangu umebaini mapungufu maeneo yafuatayo:

Utekelezaji wa Mkataba usioridhisha

Nimepitia taratibu za upatikanaji na utengenezaji wa mfumo nikiangazia uwezo wa Mamlaka ya Manunuzi ya Umma (PPRA) katika nyanja za kiufundi, kutoa msaada wa watumiaji, na usimamizi wa mfumo ambapo nimebaini mambo yafuatayo:

Mamlaka ya Manunuzi ya Umma (PPRA) haina uwezo wa kitaalamu wa kuchukua na kuundesha mfumo kwani mpaka wakati wa ukaguzi huu mnamo Septemba 2020 bado Mamlaka ya Manunuzi ya Umma ilikuwa ikimtegemea mzabuni yaani European Dynamics katika kufanya maboresho ya mfumo. Hali hii imesababishwa na ushirikishwaji hafifu wa wataalamu wa TEHAMA wa Mamlaka katika kubuni na kutengeneza mfumo kama ilivyohitajika katika mkataba.

Mnunuzi wa mfumo yaani Mamlaka ya Manunuzi ya Umma (PPRA) hajapokea hatimiliki ya mfumo (Intellectual Property), na pia nimebaini kuwa PPRA haijapatiwa umiliki wa “source code” za mfumo ingawa muda wa udhamini “warranty period” uliisha miaka miwili iliyopita kinyume na kifungu GCC 15.4 cha mktaba. Hii imepelekea PPRA kushindwa kufanya maboresho ya mfumo bila kumshirikisha mzabuni.

Kukosekana kwa maelezo ya kina juu ya mafunzo waliyofanyiwa wataalamu wa PPRA kama ilivyoelezwa katika mpango wa usimamizi wa mabadiliko (Change Management Plan – D13), ibara ya 2.4 kuwa “Kutakuwa na mafunzo ya kina kwa wataalamu wa PPRA na wafanyakazi wengine watakaoisaidia Mamlaka ya Manunuzi ya Umma (PPRA) kutekeleza majukumu ya kusimamia uendeshaji wa mfumo wa TANePS.

Mamlaka ya Manunuzi ya Umma (PPRA) haina mpango ulioidhinishwa unaoonesha mkakati wa kuchukua umiliki na uendeshaji wa mfumo kutoka kwa mzabuni.

Uwepo wa mifumo mingi inayofanya kazi zinazofanana

Katika ukaguzi wangu wa mifumo, nilibaini uwepo wa mifumo inayofanya kazi zinazofanana kama ifuatavyo.

Wizara ya Ardhi ina mifumo mitatu inayotumika kusimamia shughuli za ardhi: Mifumo hiyo ni MOLIS ambayo inatumika katika Manispaa za Kigamboni, Temeke, na Ilala; MOLIS v3 ambayo inatumika katika mikoa mingine nje ya Dar es salaam; na ILMIS ambayo inatumika katika manispaa za Kinondoni, Ilala, Ubungo, Temeke na Kigamboni.

Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) imetengeneza mifumo kadhaa ili kuboresha shughuli zinazofanywa na wizara hiyo. Hata hivyo nimebaini kwa namna moja au nyingine mifumo hii inafanya kazi zinazofanana au kushabihiana kama nitakavyoainisha:

Planrep: Mfumo unaotumika katika kupanga, kubajeti, kutoa taarifa katika Halmashauri; na TiMES: Mfumo wa Ufuatiliaji na tathmini katika Halmashauri (LGAs). Ufuatiliaji na tathmini ni sehemu ya mchakato wa Bajeti. Hivyo basi, Planrep ukiwa ni mfumo wa bajeti ulitakiwa kuwa na moduli ya ufuatiliaji na tathmini badala ya kuwa na mfumo tofauti ambao unaongeza gharama za usimamizi na matengenezo.

Mfumo wa Taarifa za Shule (SIS): Mfumo unatumika kukusanya takwimu za shule kama vile mahudhurio ya wanafunzi na maendeleo, idadi ya wanafunzi, walimu, na vitabu; na mfumo wa Sensa ya Kila mwaka ya shule (ASEC): Mfumo unaotumika katika kukusanya takwimu kutoka shule za msingi, sekondari, na elimu ya watu wazima kwa kutumia dodoso maalumu. Mifumo hii miwili tofauti hukusanya takwimu za shule ambazo zinaweza kufanywa na mfumo mmoja.


IFT-MIS: Mfumo wa kusimamia uratibu na kuweka kumbukumbu za ufuatiliaji wa matumizi ya fedha katika Halmashauri, na utekelezaji wa mapendekezo na maagizo ya CAG, PPRA na LAAC; na GARI-ITS: Mfumo unasimamiwa na Mkaguzi Mkuu wa Ndani unatumika kufuatilia hali ya utekelezaji wa matokeo ya ukaguzi katika taasisi zote za Serikali pamoja na Halmashauri. Hii ni mifumo miwili tofauti ambayo ina jukumu la kufuatilia utekelezaji wa mapendekezo ya CAG, PPRA na LAAC katika Halmashauri.

Uwepo wa mifumo tofauti inayotumiwa kutimiza kusudio moja ni matumizi mabovu ya rasilimali, na huongeza ugumu wa usimamizi, matengenezo, na msaada kwa watumiaji.

Kushindwa kufuatilia Gharama za Utengenezaji wa Mifumo

Ndugu waandishi wa Habari,

Pamoja na muelekeo chanya unafuatwa na Serikali katika kuhakikisha utengezaji na uendelezaji wa mifumo ya Serikali unafanywa kwa kutumia watalaamu wetu wa ndani, ili kuhakikisha Serikali inakuwa na udhibiti wa kutosha katika mifumo yake na pia kukwepa gharama kubwa ambazo huenda zingelipwa kwa makampuni binafsi. Hata hivyo nimebaini mapungufu katika kufuatilia na kuweka kumbukumbu za gharama za utengenezaji wa mifumo.

Kwa mfano katika ukaguzi wangu wa mifumo ya TEHAMA katika Wizara ya Fedha na Mipango nilibaini kuwa wizara ina jumla ya mifumo ya TEHAMA 17 iliyotengenezwa kwa kutumia wataalaamu wa ndani lakini nilipoomba gharama zilizotumika katika utengenezaji wa mifumo uongozi wa wizara haukuweza kunipatia mchanganuo wa gharama husika.

Aidha, mapitio yangu ya mradi wa kutengeneza mfumo wa kieletroniki wa usimamizi wa taarifa za mapato (TeRMIS) wa TARURA nilibaini kuwa gharama ya utengenezaji mfumo hazijulikani kwa sababu ya kukosekana kwa utaratibu mzuri wa ufuatiliaji wa gharama hizo.

5.7 MATOKEO YA UKAGUZI WA UFANISI

Ukaguzi wa Ufanisi Kuhusu Utoaji wa Huduma za Matengenezo ya Magari ya Serikalini Ukaguzi wangu ulibaini yafuatayo:

Mfumo wa Usimamizi wa Taarifa za Matengenezo ya Magari yanayomilikiwa na Serikali haufanyi kazi ipasavyo kuwezesha upatikanaji wa huduma za matengenezo ya magari zenye tija. Mfumo haukusanyi, hauhifadhi, na hauchakati taarifa kamili zinazowezesha upatikanaji wa huduma za matengenezo ya magari zenye tija na gharama nafuu.

Kumekuwa na utekelezaji hafifu wa kazi za utengenezaji wa magari katika maeneo yanayohusu ubora, ufanisi wa kiutendaji na usimamizi wa fedha. Mapungufu hayo yameathiri kiwango na kiasi cha ubora wa kazi za matengenezo ya magari na ufanisi katika usimamizi wa fedha ambapo katika mwaka wa fedha 2019/20 takribani Sh. Bilioni 11.3 ya fedha zilizotokana na matengenezo ya magari hazikukusanywa sawa na asilimia 28 ya mapato yote yaliyozalishwa.

Ukaguzi wa Ufanisi juu ya Ununuzi wa Magari ya Serikali kwa Pamoja na Usambazaji wa Mafuta

Ukaguzi wangu ulibaini yafuatayo:

Wakala wa Huduma ya Ununuzi Serikalini (GPSA) haikusambaza Mafuta ya Magari kwa Taasisi za Serikali kwa Bei Nafuu kama ilivyotarajiwa

Ukaguzi ulibaini kuwa, ingawa Wakala (GPSA) haulipi baadhi ya gharama za kibiashara kama vile kodi ya kampuni na mishahara ya wafanyakazi kama makampuni mengine ya biashara ya mafuta, bado Wakala inauza mafuta kwa Taasisi za Serikali kwa kutumia bei elekezi inayotolewa na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA). Hali hii ilionekana katika mikoa yote 6 iliyotembelewa wakati wa ukaguzi, ambapo GPSA iliuza mafuta kwa bei ya juu ya rejareja ya EWURA kama makampuni mengine ya mafuta.

Hii ilitokana na Wakala kukosa matanki makubwa ya kutunzia mafuta ambayo yangewezesha Wakala kununua mafuta kwa wingi kutoka kwa muagizaji mkuu wa mafuta nchini kama yanavyofanya makampuni mengine ya mafuta; badala yake Wakala umekuwa ukinunua mafuta kutoka kwa makampuni ya mafuta ya ndani kwa bei za jumla na kuyasambaza kwa Taasisi za Serikali kutumia bei elekezi za EWURA.

Ukaguzi wa ufanisi katika usimamizi wa mali zilizotelekezwa

Ukaguzi wangu ulibaini yafuatayo:

Benki Kuu ya Tanzania haikuhakikisha kuwa Benki zote za Biashara zilizofanya kazi Tanzania kwa zaidi ya miaka 15 zinawasilisha mali zilizotelekezwa. Hadi kufikia Juni, 2020 jumla ya Sh. bilioni 2.5 kutoka benki za kibiashara zilikuwa zimewasilishwa Benki Kuu na benki 3 kati ya 26 (sawa na asilimia 11.5) ya Benki zilizopaswa kufanya mawasilisho hayo, kama ilivyoanishwa na Sheria ya Benki na Taasisi za Kifedha ya mwaka 2006 (BAFIA, 2006).

Hadi kufikia Juni 2020, Benki Kuu haikuwa imeondosha au kutumia kiasi chochote cha mali za kifedha zilizoripotiwa, kiasi cha Sh. bilioni 12.25 kutokana na ukosefu wa mamlaka ya kisheria. Matokeo yake Serikali haijaweza kutumia kiasi hicho cha fedha zilizowasilishwa kutoka benki za biashara na taasisi za fedha kwa njia ya mtandao wa simu kwa matumizi yenye tija.

Ripoti ya ukaguzi wa ufanisi kuhusu usimamizi wa vituo vya kutolea huduma za afya

Ukaguzi wangu ulibaini yafuatayo:

Kuchelewa kukamilisha ujenzi wa vituo vya kutolea huduma za afya nchini. Ukaguzi ulibaini vituo 333 kati ya 447 sawa na asilimia 74 ya vituo vya kutolea huduma za Afya vilivyojengwa nchini katika mwaka wa fedha 2015/16 hadi 2019/20 vilicheleweshwa kukamilika kwa miezi 12 hadi 40. Pia, Hospitali za Wilaya 67 kati ya 68 (sawa na Asilimia 99%) zilizojengwa nchini, zilichelewa kukamilika. Vile vile, ujenzi wa vituo vya kutolea huduma za afya 33 kati ya 35 sawa na Asilimia 94 ya vituo vilivyotembelewa ulichelewa kukamilika kwa muda wa miezi 2 hadi 36.

OR-TAMISEMI haikuwa na utaratibu wa kutosha wa kudhibiti ubora wa ujenzi wa vituo vya kutolea huduma za afya vilivyojengwa: OR-TAMISEMI haikuwa na utaratibu wa kutosha wa kudhibiti ubora kutokana na ukweli kwamba, vituo vya afya 34 kati ya 35 sawa na Asilimia 97 ya Vituo vya Huduma za Afya vilivyotembelewa katika Halmashauri za Wilaya 14, havikufanya vipimo vya uchunguzi wa ubora wa vifaa vya ujenzi vilivyonunuliwa. Pia, hali hii ilidhihirishwa na uhaba wa Wahandisi wa wastani Asilimia 75 ya Wahandisi wa Wilaya, Manispaa na Jiji na kutokuwa na usimamizi wa kutosha wa kazi za ujenzi kwa sababu ya ukosefu wa fedha za usimamizi katika Sekretarieti za Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa.

Ukaguzi wa ufanisi kuhusu ufuatiliaji wa miradi iliyotekelezwa kwa njia ya ‘Force Account’ katika Sekta ya Elimu

Ukaguzi wangu ulibaini yafuatayo:

Halmashauri zimeshindwa kuwajengea uwezo watumishi wake ili kuweza kusimamia miradi inayotekelezwa kwa njia ya ‘Force Account’ kama ilivyodhihirishwa na mambo yafuatayo:

Kulikuwa na ucheleweshaji katika kutekeleza miradi ambapo miradi 10 kati ya 22 iliyokaguliwa haikukamilika kwa wakati.

Vipimo vya kubaini ubora wa vifaa vya ujenzi katika miradi 12 kati ya 17 havikufanyika. Pia, kazi ya kusimamia miradi ilifanywa na Wahandisi wasio na sifa.

Baadhi ya majengo yaliyokamilika hayakutumika kwa madhumuni yaliyokusudiwa kwa mfano vyumba vya madarasa kutumia kama stoo na bwalo kutotumika kabisa.

Ukaguzi wa ufanisi juu ya utekelezaji wa mradi wa uzalishaji wa sukari mbigiri

Ukaguzi wangu ulibaini yafuatayo:

Mbolea na dawa za kuulia wadudu zenye thamani ya Sh. 241,889,000 zilitolewa ghalani ila hapakuwa na maelezo ya namna ambavyo mbolea hii ilitumika.

Miwa iliyopita muda wake wa mavuno ilionekana katika vitalu mbalimbali kwenye shamba la Mbigiri ikiwa imeharibika na kupoteza thamani yake ya kiuchumi.

Makisio ya hasara iliyotokana na gharama za uzalishaji wa miwa hiyo ni kiasi cha Sh. 379,338,245.

Visima vinne (4) katika shamba la Mbigiri kitalu E3, D2, E4 na F4 vilichimbwa lakini havitumiki kwa sababu havina uwezo wa kutoa maji ya kutosha kwa shughuli za umwagiliaji. Pia, nilibaini kuwa Mkandarasi aliondoka eneo la kazi licha ya kuwa alishalipwa Sh. 81,500,000 sawa na asilimia kumi 10% ya gharama zilizoainishwa kwenye mkataba.

Kampuni ya Mkulazi ilishindwa kusimika mtambo wa kuchakata sukari kwa wakati na kusababisha benki ya Azania kusitisha kutoa mikopo kwa wakulima wa nje kiasi cha Sh. 1,797,050,000 ambazo zingewawezesha wakulima hao kukidhi gharama mbalimbali za kuzalisha miwa.

Tangu kuanzishwa kwake Kampuni ya Mkulazi haijasajiliwa kwa ajili ya kodi ya ongezeko la thamani. Kampuni iliingia mikataba 52 yenye thamani ya Sh. 50,279,515,851.70 na mikataba hiyo imejumuisha kodi ya ongezeko la thamani yenye kiasi cha Sh. 7,669,756,655.34 katika mwaka wa fedha 2017/18 to 2019/20 ambazo zingeweza kutumika kwa shughuli nyingine.

Kampuni Hodhi ya Mkulazi ilimlipa mkandarasi kiasi cha Sh. 397,020,000 kama malipo ya maandalizi bila kuwa na vielelezo vya vipengele vilivyolipwa.

Ndugu Wanahabari

Masuala niliyowasilisha kwenu ni muhtasari wa mambo machache niliyoyaona ni muhimu zaidi kuwafahamisha. Hata hivyo, Ripoti nilizokabidhi Bungeni zina mambo mengi zaidi na ushauri wa kina kwa kila suala kwa lengo la kuongeza uwajibikaji na usimamizi wa rasilimali za umma. Ni matumaini yangu kwamba mtapata muda wa kuzisoma na kuzichambua ili kuwaelimisha wananchi mambo mbalimbali yaliyojitokeza katika kaguzi nilizozifanya.



Charles E. Kichere

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Dodoma​

8 Machi 2021​

 
CLOUDS nao wachukuliwe hatua.

TAKUKURU chukueni hatua kwa viongozi, hakuna kuoneana aibu.

nitashangaa sana kama hatua hazijachukuliwa, wafikishwe mahakamani.

Fedha zetu za walipa kodi zinapigwa mchana kweupe milioni 629.9 halafu hatua zisichukuliwe?!!!
 
HENRY_KILEWO_on_Instagram:_“Tulisema_wazi_kuwa_2020_hakukuwa_na_Uchaguzi_kulikuwa_na_uchafuzi_...jpg


Je, Dr Mahera ambaye ni Mkurugenzi wa uchaguzi anayo majibu ya hili? Iliwezekanaje hela hii kuliwa mbele ya hotuba nzito ya Rais kama hii?

 
Hii mijizi na jizi lenzie la wachafu naona wanashindana katika mapambio ya kumuwin mama yaendelee kula fedha za wanyonge .
 
Bashiru,Polepole,Mdee,Bulaya,Matiko,Mwakagenda,Silinde,Makonda,Sabaya na washenzi wengine wengi wakiongozwa na dikteta uchwara mwenyewe.

Nimewahi sema hapa awamu ya dikteta itavunja rekodi ya ufisadi kuliko awamu zote ukiziunganisha kwa pamoja.
 
Back
Top Bottom