MAHANJU
JF-Expert Member
- Aug 26, 2014
- 5,244
- 7,966
Hivi hili suala kwa mtu makini kabisa ukifikiria kwa umakini wa dhati kabisa huwezi kuona kua hizi ni siasa tu? Ni nani atakayekubali kusulubiwa kwa sababu ya maagizo ya bosi wake? Kama haya mambo yalijadiliwa na baraza la mawaziri kwa maagizo ya wakulu, hawa mawaziri,wanasheria na maofisa wengine wa Serikali kipindi hicho waliotajwa walikua na maamuzi gani ya kutia saini kwenye mikataba bila ya kuagizwa? Ni nani alikua na maamuzi ya kufanya jambo la kitaifa bila baraka za bosi wa nchi?
Tunasema kwa Uchungu kabisa kua Walioliingiza taifa kwenye mikataba mibovu washughulikiwe huku tunasema tusiwataje mabosi wao wala kuwaingiza kwenye sakata hilo, hawa wanaotakiwa kuwajibika walikua na uwezo gani kuyakataa maagizo ya mabosi wao? Are we serious? Tunapata uchungu juu ya hili kivipi ilihali tunaziba njia za kuwashughulikia? Kwanini tusiziite kua ni siasa hizi?
Kuna mashaka makubwa juu ya utekelezwaji wa maagizo ya kamati, uthubutu utatoka wapi hapa? Kama suala ni katiba kuwalinda mabosi hao kwani amendment inatumia muda gani na kupata maazimio ya bunge?
Ni lini Serikali ya CCM ambayo ndio inalelewa na wahusika wakubwa waliolipoteza taifa ikawashughulikia? Inawezekanaje? Kwanini tusiite kua hizi ni siasa? Watanzania uelewa wetu unatupa shida sana!
Tunasema kwa Uchungu kabisa kua Walioliingiza taifa kwenye mikataba mibovu washughulikiwe huku tunasema tusiwataje mabosi wao wala kuwaingiza kwenye sakata hilo, hawa wanaotakiwa kuwajibika walikua na uwezo gani kuyakataa maagizo ya mabosi wao? Are we serious? Tunapata uchungu juu ya hili kivipi ilihali tunaziba njia za kuwashughulikia? Kwanini tusiziite kua ni siasa hizi?
Kuna mashaka makubwa juu ya utekelezwaji wa maagizo ya kamati, uthubutu utatoka wapi hapa? Kama suala ni katiba kuwalinda mabosi hao kwani amendment inatumia muda gani na kupata maazimio ya bunge?
Ni lini Serikali ya CCM ambayo ndio inalelewa na wahusika wakubwa waliolipoteza taifa ikawashughulikia? Inawezekanaje? Kwanini tusiite kua hizi ni siasa? Watanzania uelewa wetu unatupa shida sana!