Ripoti ya Utetezi wa Bwawa la Stiegler - Ndiyo Hii? Nimeshindwa Kuisoma...

Mkuu Mzee Mwanakijiji, uzalendo ni pamoja na kuwa na blind faith, kuwa na imani isiotia shaka na matumaini na unaowaamini kwamba wanatupeleka mahala pema hata kama wanatupitisha njia iliyojaa mbigiri, hivyo huna haja kuiosoma na kuielewa muhimu ni kuisoma tuu na kuiamini na sii lazima kuielewa, kama tunavyo mwamini Mungu.
Ujamaa ni imani, aliyepo amekuja kuikamilisha na kuitimiliza ndoto ya Nyerere, tumuaminie na kumpatia kila ushirikiano ili ayaweze katika Yeye amtiaye nguvu.

Heri wewe umeisoma hukuielewa, mimi wala sihitaji kuisoma, nimeisha iamini bila kuisoma kwa kuwaaminia kwa sababu kuhusu Stigler niliisha sema kila kitu hapa
nilisema

Uzalendo wa kweli wa nchi yako ni pamoja na kusupport mipango kamambe
ya maendeleo ya nchi yako hata kama mipango hiyo itasababisha maumivu kwa walio wengi as long as itakuwa na faida kubwa kitaifa huko baadae.
P
 
Mzee Mwanakijiji huwa unawaamini sana wataalamu kutoka Ulaya kwa ripoti zao zilizopambwa?

Oh noooo.. siwaamini kabisa... nawasoma kwa umakini na nauliza kila assumption wanayotoa. Binafsi nilitarajia ripoti hii isiwe ye kisiasa kabisa; ingedeal na facts na facts tupu. Na pale inapotoa mahitimisho basi yatolewe kutokana na facts zilizopo. Siasa waachiwe wanasiasa. Binafsi kama mtu ambaye naunga mkono ujenzi wa bwawa hili hoja za umuhimu, ulazima na uharaka wa kujenga bwawa hili zinasimama peke yake bila kuhangaika na kujibu hoja za watalaamu wa "Ulaya". Unajua kuwa 2 + 2 ni 4. Haijalishi anayejumlisha ni Mchina, Mtumbatu, au Mdigo. Tunaweza kutofautiana kwenye mbili za "nini" na mbili za "nini" zinajumlishwa.
 
Hawa waandishi wana utaalam wowote wa Mazingira?
Nimejaribu kuangalia 'References' walizoweka nione kama wanayo maandishi yoyote katika eneo hilo, sioni hata mmoja wao ambaye maandishi yake yalishachapishwa katika eneo hilo, sikumwona hata mmoja.
LIcha ya hivyo, ningependa kujua competencies zao ni nini... kwa mfano, nimeona jina la Dkt. Kashililah.. ninadhania ni yule yule aliyekuwa Bungeni siyo? Hawa wataalamu wengine ni wabobezi wa maeneo gani ya kitaaluma?
 
Nini maana ya "report", tuanzie hapo?

Kwa uelewa wangu na elimu ndgo niliyonayo;

Report katika project ni kuwa unatoa taarifa ya maendeleo ya project inayoendelea au imekwisha fanyika.

Kwa project inayotegemea kuanza huwa inafanyiwa "feasibility study".

A feasibility study is an analysis that takes all of a project's relevant factors into account—including economic, environmental, technical, legal, and scheduling considerations—to ascertain the likelihood of completing the project successfully.

Yan hapa hakuna cha feasibility study. Ni brabra tu nyingi na vingereza vya shule ya secondary. In short hii ni kama tu maoni ya kundi fulani la watu wamepewa vipesa watunge uwongo wao kujustify ujenz.

Ila hii sio feasibility study ni riwaya ya maoni ya wanasiasa na si wanasayani.
Mr slowly ndo kandika. kila jambo awamu hii imekua politicized,,ni ujïnga mtupu
 
Tumesikia na kusoma juu ya uzinduzi wa "ripoti ya wataalamu" wazalendo. Mimi binafsi naunga mkono ujenzi wa bwawa hili na nilikuwa miunngoni mwa watu waliofurahia sana kuwa hatimaye hili linafanyika... Lakini si kwa utetezi unaojaribiwa kwenye ripoti hii. Nimejaribu kusoma lakini sikufika mbali...

Ila inaitwa ni ya "wataalamu"... seriously... Ningekuwa na kaudikteta kadogo tu Ningeagiza watalaamu hawa wote waende Butimba angalau kwa mwezi mmoja... Kama wangeita ni "utetezi wa kisiasa".. nisingekuwa na matatizo nayo hii ripoti... lakini kuiita ni ya "kitaalamu".. basi neno "utaalamu" limepoteza maana...
Mkuu Mzee wanavillage kutetea uongo na uzandiki ni kazi kubwa sana, lazima utaandika ugoro tu

"Siasa za mabunduki ni ushamba"
 
Hawa waandishi wana utaalam wowote wa Mazingira?
Nimejaribu kuangalia 'References' walizoweka nione kama wanayo maandishi yoyote katika eneo hilo, sioni hata mmoja wao ambaye maandishi yake yalishachapishwa katika eneo hilo, sikumwona hata mmoja.
Mkuu Kalamu, Tanzania ya sasa
hatuhitaji references za wataalamu wazungu katika ripoti zetu za kitaalamu, ripoti zetu sasa zinazingatia uzalendo, maadamu tumeamua kujenga mradi wa HEP wa Stigler, then ripoti zetu zitareflect our political wishes, nakumbuka kwenye hili tulikutana hapa na wote sisi mimi name wewe tulichangia page ya kwanza, ulianza wewe kuchangia post No. 5, nikaja mimi post No.8

Uzalendo wa kweli wa nchi yako ni pamoja na kusupport mipango kamambe
ya maendeleo ya nchi yako hata kama mipango hiyo itasababisha maumivu kwa walio wengi as long as itakuwa na faida kubwa kitaifa huko baadae.
P
 
This is how the blind faith operates
nilisisitiza uzalendo wa aina hii

Uzalendo wa kweli wa nchi yako ni pamoja na kusupport mipango kamambe
ya maendeleo ya nchi yako hata kama mipango hiyo itasababisha maumivu kwa walio wengi as long as itakuwa na faida kubwa kitaifa huko baadae.
P

Mipango kamambe haihitaji kuchezwa mdundiko, kujieleza yenyewe na wengi kama si wote wanaikubali. Kuna tofauti ya kuwa mfurukutwa na mfirigiswa
 
Tunaposema elimu yetu imedidimia kiasi cha kutisha hatueleweki.

Lakini sasa inajionyesha kwamba sio katika elimu pekee ndiko tuliko kwisha. Chukua nyanja nyingine yoyote ile, michezo, siasa, utamaduni, n.k. ambako unaweza kusema tuna nafuu huko. Pengine kudhoofika katika haya nako kunaanzia kulekule kwenye elimu mbovu. Kwa sababu tunakosa misingi ya kuyafanya yote haya, misingi ambayo inatokana na elimu nzuri.

Vyuo vyetu vikuu na wasomi walioko huko. Hebu tafuta machapisho yanayotoka katika vyuo hivyo, hasa katika maeneo ya Sayansi, Uhandisi, na teknologia. Tafuta machapisho katika "journals" zinazotambulika duniani uhesabu ni ngapi zinatokana na wasomi wetu. Sokoine walikuwa wameinuka kidogo hapo siku za nyuma, siku hizi hata wao ni shida tupu!

Siasa inalipa sana Tanzania, na haya ndio matokeo yake. Kila jambo tunataka kulifanya liwe la kisiasa. Hata kucheza mpira wa miguu iwe ni siasa! Hata siasa yenyewe ndio hiyo tunaiua, kwa kuondoa ushindani wa mawazo huru.

Ripoti za Makinikia, Maprofesa wetu wanaweka pembeni ujuzi wao na kufanya mambo ya aibu kabisa, ili waonekane wao ni 'Wazalendo'.

Ni hapa mwisho mwisho wa ngwe ya Kikwete ndipo wale jamaa wa Taasisi ya Kikwete pale Muhimbili walijaribu kujitutumua kidogo kuonyesha wanachoweza kufanya kama wataalam. Kwingine kote, juhudi zipo katika kujiandaa kupata uteuzi wa kisiasa.

Kwa hiyo, ukiona ripoti za wataalam wetu zinazotia aibu na kukatisha tamaa kuzisoma, elewa hiyo ni sehemu ndogo sana inayoonyesha udhaifu wetu mkubwa katika nyanja nyingi.

Inatulazimu turudi katika misingi ya kuimarisha elimu yetu, na utendaji wetu. Tuache kuifanya siasa ndio iwe kila kitu kinachoendesha uhai wa taifa letu.

Sawa, ngoja nitoe sifa za kikorofi na kinafiki: Tanzania wakulima wetu wanazalisha mahindi kwa wingi kuliko wakati mwingine wowote.
Nani anaweza kusema mkulima wa leo ni tofauti sana na yule wa miaka ya Mwalimu Nyerere!
Natambua sana juhudi za "Kilimo Kwanza," lakini kweli kuna uendelevu hapo wa kujivunia?
Ndugu hapo sio swala la ubora wa elimu tu! pia wataalam kutaka kumfurahisha mtawala maana aliepoa anataka kusikia anachopenda tu
 
Tumesikia na kusoma juu ya uzinduzi wa "ripoti ya wataalamu" wazalendo. Mimi binafsi naunga mkono ujenzi wa bwawa hili na nilikuwa miunngoni mwa watu waliofurahia sana kuwa hatimaye hili linafanyika... Lakini si kwa utetezi unaojaribiwa kwenye ripoti hii. Nimejaribu kusoma lakini sikufika mbali...

Ila inaitwa ni ya "wataalamu"... seriously... Ningekuwa na kaudikteta kadogo tu Ningeagiza watalaamu hawa wote waende Butimba angalau kwa mwezi mmoja... Kama wangeita ni "utetezi wa kisiasa".. nisingekuwa na matatizo nayo hii ripoti... lakini kuiita ni ya "kitaalamu".. basi neno "utaalamu" limepoteza maana...
"WATAALAMU" ndio wametufikisha hapa,Ndio hao walioingia mikataba ya KICHIFU MANGUNGO na kuliingiza taifa hasara ya matrilioni.....Naungana na wewe na mimi siisomi hiyo ripoti ya kitaalamu.
 
Tumesikia na kusoma juu ya uzinduzi wa "ripoti ya wataalamu" wazalendo. Mimi binafsi naunga mkono ujenzi wa bwawa hili na nilikuwa miunngoni mwa watu waliofurahia sana kuwa hatimaye hili linafanyika... Lakini si kwa utetezi unaojaribiwa kwenye ripoti hii. Nimejaribu kusoma lakini sikufika mbali...

Ila inaitwa ni ya "wataalamu"... seriously... Ningekuwa na kaudikteta kadogo tu Ningeagiza watalaamu hawa wote waende Butimba angalau kwa mwezi mmoja... Kama wangeita ni "utetezi wa kisiasa".. nisingekuwa na matatizo nayo hii ripoti... lakini kuiita ni ya "kitaalamu".. basi neno "utaalamu" limepoteza maana...
Sasa mkuu kama unasema hujaisoma yote then unaiponda na mbaya zaidi bila hata kutoa hoja za uchambuzi wa taarifa yenyewe! Lakini si shangai inasemekana watz ni wavivu wa kusoma sana vitu vya maana ila kwa udaku hawajambo. Acha siasa isome kwanza then njoo na hoja za kuipinga za kiuchambuzi siyo blabla tu mkuu.
 
12 Reactions
Reply
Back
Top Bottom