Ripoti ya uchunguzi dhidi ya Trump kuwekwa wazi wiki hii

Nyendo

JF-Expert Member
Jun 4, 2017
1,174
4,062
Ripoti ya uchunguzi inayolenga kumshitaki Rais Donald Trump wa Marekani, itawasilishwa leo kwa faragha mbele ya wabunge muhimu wakati wabunge wa chama cha Democratic wakizidi kuongeza shinikizo, licha ya azimio la Ikulu ya Marekani, white House kutoshiriki usikilizwaji wa kwanza mbele ya kamati ya mahakama.

Kamati ya usalama iliyo na wingi wa wajumbe wa chama cha Democratic imesema kwamba ripoti hiyo, iliyojumuishwa baada ya wiki mbili za ushahidi itajieleza yenyewe, katika kile mwenyekiti wa kamati hiyo Adam Schiff alichokiita makosa yaliyofanywa na Rais juu ya Ukraine.

Ripoti hiyo inatayarishwa kwa ajili ya wabunge wa kamati kuitathimni kuelekea kura itakayopigwa kesho ya kuipeleka kwenye kamati ya mahakama. Hapo jana Ikulu ya White House iliwaeleza wabunge wa chama cha Democratic kwamba Rais Trump na mawakili wake hawatoshiriki katika mchakato wa uchunguzi wiki hii wakielezea kuwa umekosa misingi ya haki.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom