Ripoti ya Sky News kuhusu Magufuli na COVID-19

Hoja ya kuwa "kwani wewe una korona au unamjua aliyekufa kwa korona?" ni hoja isiyo na mashiko kwa sababu wakati Watu wanakufa kule Wuhan au Marekani haikumaanisha kuwa lazima kila mtu aambukizwe hiyo korona au afiwe na jirani ndo imaanishe kuwa korona ipo!

Hoja ya maana ni vipimo kwa wengi, uwazi wa kutangaza takwimu ndo tutajua picha nzima ya hali ya korona nchini.

Hii habari ya kuwa sijawahi kung'atwa na nyoka na sijamuona nyoka maeneo haya kwa hiyo nyoka hawapo ni logical fallacy ya kutisha sana!
Ukiacha hizo takwimu huko kwa wenzetu tulikuwa tunasikia hospitali zimezidiwa kwa wagonjwa na wengine mpaka wakajenga hospitali za dharura na tulikuwa tunasikia hadi sehemu za kuhifadhi maiti zilijaa. Hiyo ndio athari za corona mbali na kujua takwimu.
 
Kuuliza si ujinga lakini kuna swali la kijinga kama lako. Wewe na sampuli za aina yako mna tatizo kubwa sana la uelewa. Nchini Tanzania ugonjwa unaoongoza kwa kuua ni malaria. Au hata na hilo utabisha? Sasa nifahamishe ni nani kati ya vilaza wenzio kafa kwa malaria? Nani kafa mtaani au katani kwa malaria? Acha kuparamia usoyajua. Praise n worship team kwa hili ni usiku wa giza!

Tunaongelea Corona au Malaria? Tanzania wajinga wengi ni wale wanaofikiri wanajua mambo kama wewe. Sababu mzungu amesema, basi lazima afuatwe, hata kama anachosema hakina tija. Waliojifungia ndani, sasa hivi maambukizi yameenda juu mpaka inatisha.
And yet, bado tunabeza maamuzi sahihi ambayo Uongozi wa Tanzania ulichukua.
 
Na kama kweli kwamba Watu wanadondoka basi hata humu jukwaani Watu wangeadimika.

Hapa ninapoishi Majirani wote wapo fiti, siku nikisikia Majirani Watatu wameaga Dunia kwa kufuatana basi ndio nitashtuka.
 
Watu walishatishwa wakatishika na serikali ikaamua kuachana na testing. Waganga na wauguzi wakaogopa hata kupokea wagonjwa; watu wakawa wanaugua lakini hawaendi ‘spitali’ kwa kuhofia wataambiwa wana korona. Kwa hiyo hakuna ‘spitali’ yenye mgonjwa wa korona na hospital attendance imepungua kupita maelezo kiasi kwamba watu wanaweza kufa kwa magonjwa mengine kwa kushindwa kwenda ‘spitali’ ambapo wanaweza ambiwa wana korona.

Kwa hali ilivyo watu wanaweza kuugua korona na kufa kisha isemwe kuwa wamekuwa kwa pneumonia au ugonjwa wowote ule lakini siyo covid19 sababu wanasiasa wamesema haupo. Mind you, mwongozo wa wizara ya afya kuhusu covid19 haujabadilika; madaktari wasema kweli bila hofu au unafiki wanaweza kukuambia ukweli usiopendwa na wanasiasa.

Hata PM jan on ITV kasema korona haipo! Je ni kweli korona haipo?

Tuchukue tahadhari:
1. Tudumishe social distance.
2. Tunawe mikono kwa sabuni na maji tiririka.
3. Kama ni lazima uwe kwenye misongamano isiyoepukika vaa barakoa.
4. Kula mlo kamili
5. Fanya mazoezi yanayokutoa jasho ku improve cardiovascular endurance.

Korona bado ipo lkn inaepukika!

Tuchukue tahadhari!
Una Akili fupi
 
Afadhali umejizungumzia wewe, ok, sasa wewe mwenyewe uko kwa mabeberu, utapatia wapi ndugu? ndugu zako wanadedi kimya kimya, unadhani wakivuta kuna Wa kunyanyua domo lake kua kavuta na hio kitu? Thubutu yake!

ataambiwa au kuandikiwa kua ni kwa changamoto za upumuaji, jifanye unajitangazia hio kitu ndio utawajua hao unaowapamba!

Nikwambie tu watu tunaishi kwa kudra za god basi!
Acha unafiki wewe bwana. Kipindi corona ilipoingia Tz kila mtu aliona idadi ya vifo ikiongezeka regardless ya kile kilichokuwa kikitangazwa. Lakini baada ya ugonjwa kudhibitiwa sasa hivi hata idadi ya misiba mtaani imerejea kama zamani kabla ya corona.

Narudia: Kuweni wazalendo acheni unafiki. Corona imedhibitiwa Tanzania, hata kama mbinu zilizotumika hazijawakosha wafuasi wa mabeberu na mabosi wenu.
 
Inawezekana wapo wengi tu wakuzungukao walio na hiyo corona.

Lakini si ajabu haijawaathiri kiasi cha wao kuugua na kushindwa kuendelea na shughuli zao za kila siku.

Na hilo ndo jambo ambalo nimekuwa nikilisema tokea mwanzo. Kwamba, coronavirus si hatari kama tunavyoaminishwa!

Maana, ingekuwa ni hatari kama isemavyo, ingeonekana tu!!

Na bila shaka tulijua kuwa siyo hatari ndiyo maana tulipuuza tangu mwanzo! Ndiyo maana tukaamua kuacha kupashana taarifa za ugonjwa!
 
Na katika kukazia kuwa corona haipo Tz leo balozi mpya wa marekani ameenda ikulu kujitambulisha na hakuwa na barakoa
TeheheteheeeeeView attachment 1525377
IMG_20200802_160549_8.jpg


Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
 
Tunaongelea Corona au Malaria? Tanzania wajinga wengi ni wale wanaofikiri wanajua mambo kama wewe. Sababu mzungu amesema, basi lazima afuatwe, hata kama anachosema hakina tija. Waliojifungia ndani, sasa hivi maambukizi yameenda juu mpaka inatisha.
And yet, bado tunabeza maamuzi sahihi ambayo Uongozi wa Tanzania ulichukua.
Corona tumeimaliza kwa sababu hatukujifungia? Sema tulifanya nini? Maamuzi gani sahihi na nani aliyachukua?
 
M
Acha unafiki wewe bwana. Kipindi corona ilipoingia Tz kila mtu aliona idadi ya vifo ikiongezeka regardless ya kile kilichokuwa kikitangazwa. Lakini baada ya ugonjwa kudhibitiwa sasa hivi hata idadi ya misiba mtaani imerejea kama zamani kabla ya corona.

Narudia: Kuweni wazalendo acheni unafiki. Corona imedhibitiwa Tanzania, hata kama mbinu zilizotumika hazijawakosha wafuasi wa mabeberu na mabosi wenu.
Mbinu zipi zilizotumika? Kwa nini wanaoendelea na corona hawaji kujifunza hapa?
 
Corona tumeimaliza kwa sababu hatukujifungia? Sema tulifanya nini? Maamuzi gani sahihi na nani aliyachukua?
Yes. Hatukuiogopa imesepa zake. Duniani, ni Tanzania na Sweden tu hawakuingiza utapeli wa lockdown.
Angalia US sasa hivi cases zimeongezeka. And all the countries that lied the solution to the pandemic, was lockdown.
Do you what to know what we have done for Corona? Tulimuomba Mwenyezi Mungu atunusuru waja wake maana sio science wala lockdown ingetusaidia
 
Hili la Corona hata Maxence Melo aliungana na mabeberu kufunga ofisi za JamiiForums lakini wabishi tuliendelea na harakati za kuuza mikate stand ya ubungo bila barakoa maana maombi ni zaidi ya barakoa zakishenzi zilizoletwa na mabeberu. Tunamshukuru muumba kwakuwa tuko hai mpaka sasa na vibaraka wa mabeberu wanazidi kuaibika hasa baada ya mabeberu kutuweka ktk orodha ya nchi zenye uchumi wakati wa chini.
 
Yes. Hatukuiogopa imesepa zake. Duniani, ni Tanzania na Sweden tu hawakuingiza utapeli wa lockdown.
Angalia US sasa hivi cases zimeongezeka. And all the countries that lied the solution to the pandemic, was lockdown.
Do you what to know what we have done for Corona? Tulimuomba Mwenyezi Mungu atunusuru waja wake maana sio science wala lockdown ingetusaidia
Wengine hawaombi tena ipasavyo? Mitume wa Yesu walimwomba, bila aibu, awafundishe kuomba. USA na kwingineko wanaona aibu kumwomba yesu JPM awafunze sala ya kutokomeza korona??
 
Hawawezi kurudi tena kuongelea swala hili.

Mabeberu hao hawatutakii mema hata siku moja.

Mshambulizi wetu kaucheza na bao kalifunga... majirani zetu wamebaki kutafuta mpira na mpaka sasa hawauoni
Preta
 
Back
Top Bottom