sexologist
JF-Expert Member
- Dec 5, 2010
- 2,283
- 976
Ndg wana jamvi.. Salam nyng kutoka Shinyanga..
Leo nilikuwa mmoja wa maelfu ya waandamanaji waliojitokeza mjini Kahama.
Watu walikuwa ni wengi haijawahi tokea.. Hali ya usalama ilikuwa tulivu sana, ilikuwa ni amani tu.. Viongozi wa CDM waliokuwepo ni Mh. Mbowe, Ndg. Mwita Waitara, M/kiti wa chama mkoa na wa wilaya, Mbunge viti maalum Manyara, Mweka hazina wa chama taifa na wengne sikuwatambua.
Mabango yalikuwa ni mengi sana, na baadhi yake yalisomeka kama ifuatavyo:-
"BORA UKIMWI KULIKO KIKWETE".. "TUNATAKA UMEME WA BUZWAGI".. "JK NA NGELEJA UZENI WAKE ZENU MUILIPE DOWANS".. "TUNATAKA KATIBA MPYA"... "TUNAPINGA KUPANDA KWA BEI YA BIDHAA" nk..
Viongozi wote wa CDM waliokuwepo waliongea.. Mambo makubwa ni pamoja na kukubaliana kufanya maandamano mpaka Buzwagi kuwaambia wawekezaji waisaidie Kahama kimaendeleo.. Mh. Mbowe alitumia muda mwing kujibu hotuba ya JK ya jana.. Kikubwa alichosema ni kwamba maandamo ndio silaha pekee ya CDM kutumia nguvu ya umma kuikumbusha serikali wajibu wake kwa wananchi.
Nashukuru.
Naomba kutoa hoja.
Leo nilikuwa mmoja wa maelfu ya waandamanaji waliojitokeza mjini Kahama.
Watu walikuwa ni wengi haijawahi tokea.. Hali ya usalama ilikuwa tulivu sana, ilikuwa ni amani tu.. Viongozi wa CDM waliokuwepo ni Mh. Mbowe, Ndg. Mwita Waitara, M/kiti wa chama mkoa na wa wilaya, Mbunge viti maalum Manyara, Mweka hazina wa chama taifa na wengne sikuwatambua.
Mabango yalikuwa ni mengi sana, na baadhi yake yalisomeka kama ifuatavyo:-
"BORA UKIMWI KULIKO KIKWETE".. "TUNATAKA UMEME WA BUZWAGI".. "JK NA NGELEJA UZENI WAKE ZENU MUILIPE DOWANS".. "TUNATAKA KATIBA MPYA"... "TUNAPINGA KUPANDA KWA BEI YA BIDHAA" nk..
Viongozi wote wa CDM waliokuwepo waliongea.. Mambo makubwa ni pamoja na kukubaliana kufanya maandamano mpaka Buzwagi kuwaambia wawekezaji waisaidie Kahama kimaendeleo.. Mh. Mbowe alitumia muda mwing kujibu hotuba ya JK ya jana.. Kikubwa alichosema ni kwamba maandamo ndio silaha pekee ya CDM kutumia nguvu ya umma kuikumbusha serikali wajibu wake kwa wananchi.
Nashukuru.
Naomba kutoa hoja.