Ripoti ya CAG imefichua madudu mengi ya awamu ya tano, kulikuwa na ufisadi wa kutisha

Mada ya 2018

Awamu ya tano imetupa pembeni utaratibu wa zabuni na sasa inaamua na kufanya manunuzi au kuingia mikataba wenyewe kwa amri toka juu...

Rejea hii itatukumbusha siku za usoni na hasa kwa Miradi hii.

1. Uwanja wa ndege chato
2. Vitambulisho vya utaifa
3. Fly overs
4. Bombadier
5. Tenda za ujenzi za TBA n.k
6. SGR
7. Bwawa la umeme

Kwa kumalizia tuu.... nimeandika hayo nikiwa full detailed. Kuna vitu duniani havichiki navyo ni Jua mwezi na ukweli.

MUDA NI HAKIMU WA YOTE!!

Credit kwako Lusungo
Niliwahi kusema kitu cha kuhusu ndege tena nikiwa kigoma hotelini jamaa wakataka kunila nyama kisa namseba vibaya mkuu.
Kuna mturuki alishawahi kufukuzwa baada ya kuwahoji ukweli viongozi wa TRC Juu ya kwanini tunajenga baadhi ya matanuri ya kupitisha reli badala ya kuipitisha njia ya nnje ambayo gharama yake sio kubwa sana?
Muda ni kitu chaajabu sana kwakweli.
 
Siku ya leo sijui tuuiteje huko; Mbaya? Au nzuri sana?

Ripoti ya mkaguzi mkuu wa serikali inayoendelea kusomwa muda huu si kwamba tu inawaweka CCM na watetezi wa mwendazake kwenye wakati mgumu sana, lakini tayari imechefua wananchi wengi kwa kiwango kisichomithilika.

Madudu ya SHUJAA WA AFRIKA yanatisha na kutia kinyaa.

Madudu ya MTETEZI WA WANYONGE Yanatia hasira sana.

Chukulia hili moja BILIONI 3.9 kwenye matengenezo ya ndege moja ambayo HAIKUFAA!

Upinzani uliwahi kusema upigaji wa awamu hii utavunja rekodi, watu wakabeza sana. Lakini wakati ni hakimu mzuri. Uongo hupanda lift lakini ukweli hukwea ngazi. Mahakama ya mafisadi inaweza kuanzia pale kwenye nyumba ya milele ya mwendaAzakwe marehemu hayati.

Huu uozo uliendelea kuwekwa wazi peupe hivi tusishangae kuona siku moja marehemu akalikimbia kaburi lake. N itokee kuna kitu kinaitwa maandamano kifanyike Bila udhibiti imara si ajabu kuwakuta waandamanaji wakilicharaza bakora kaburi la shujaa wa Afrika na kuipopoa mawe picha yake.

Baada ya kusomwa hii ripoti, masikio yote yako kwa Bimkubwa. Je, atasemaje? Watu wamefura kwa hasira. I hope hatawazingua
Mahabusu ziandaliwe za kutosha sasa. Ni zamu ya kubadilisha wapangaji. Karibia kila wizara ina vimeo vya kutisha.
AHSANTENI KWA KUJA


IMG-20210408-WA0100.jpg
 
mama D mwaka huu yamezidi. Hata ukiangalia mh angekuwepo yasingewekwa hadharani kama hivi inavyofanyika sasa. Mwaka jana tu alituambia ATCL imefanya faida ya bil 28. Mwaka huu angekubali CAG aseme hasara ni 60bil kwa miaka 5?
Ngoja tupate report zilizopita ndio tuone yaliyozidi maana kila report ina madudu
 
Shida yetu kubwa ni kwamba tunapojadili haya mambo hatuji na masuluhisho. Na kila mwaka ni yale yale. Upigaji wa kutisha!

Kama jamii tufanye nini ili kuikomesha hali hii? Tunawezaje kuukomesha ufisadi? Kwa nini viongozi wetu wanakuwa hivi? Tufanye nini?

Mwendazake keshalala. Hata tukipopoa mawe na kucharaza bakora kaburi lake hatatusikia. Kimbembe ni kwetu tuliobakia. Ni kweli hatuwezi kuikomesha hali hii?
Jamii ifanye nini ? Hatuna mamlaka yeyote kwenye hii nchi hata kumtoa mbunge.
Ingia barabarani ukutane na form four wanaolipwa posho ya nyumba, usafiri, chakula, umeme wakutandike virungu ufe.
 
Ngoja tupate report zilizopita ndio tuone yaliyozidi maana kila report ina madudu
Labda utafute ya mwaka 2015 au kabla yake. Zote kuanzia 2016 zinaonesha mambo ni shwari. Mamiradi tu yanatekelezwa masgr, JNHP, n.k si unajua tena serikali ya kiongozi wa Malaika😂😂😂
 
Shida yetu kubwa ni kwamba tunapojadili haya mambo hatuji na masuluhisho. Na kila mwaka ni yale yale. Upigaji wa kutisha!

Kama jamii tufanye nini ili kuikomesha hali hii? Tunawezaje kuukomesha ufisadi? Kwa nini viongozi wetu wanakuwa hivi? Tufanye nini?

Mwendazake keshalala. Hata tukipopoa mawe na kucharaza bakora kaburi lake hatatusikia. Kimbembe ni kwetu tuliobakia. Ni kweli hatuwezi kuikomesha hali hii?
Tuliowapa mamlaka au dhamana ya kukomesha hili wanatuangusha, hatuwezi kunyanyuka jamii nzima na kupigana na mafisadi au wabadhirifu, kuna sheria kwa ajili ya kuwawajibisha, tuna mamlaka za juu zenye kuweza kutoa tamko juu ya hawa wanaotumia ofisi za umma kwa manufaa yao, katiba yetu haijatupa wananchi mamlaka ya kuwawajibisha hawa kwa sababu hata kwenye masanduku ya kura wanatufanyia ubadhirifu, simply katiba isipobadilishwa basi haya mambo hayatakwisha, ni muda muafaka hizi ofisi ziwe na watendaji proffesional na sio wanasiasa wa kuteuliwa
Shida yetu kubwa ni kwamba tunapojadili haya mambo hatuji na masuluhisho. Na kila mwaka ni yale yale. Upigaji wa kutisha!

Kama jamii tufanye nini ili kuikomesha hali hii? Tunawezaje kuukomesha ufisadi? Kwa nini viongozi wetu wanakuwa hivi? Tufanye nini?

Mwendazake keshalala. Hata tukipopoa mawe na kucharaza bakora kaburi lake hatatusikia. Kimbembe ni kwetu tuliobakia. Ni kweli hatuwezi kuikomesha hali hii?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom