BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,832
- 287,782
Posted Date::12/6/2007
Marekani yasubiri kwa hamu ripoti ya BOT
John Stephen na Mwanaid Omary
Mwananchi
SERIKALI ya Marekani imesema inasubiri kwa hamu kubwa ripoti ya tuhuma za ufisadi katika Benki Kuu Ya Tanzania (BoT) ambayo tayari amekabidhiwa Mthibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).
Akizungumza jana na Mwananchi Msemaji wa Ubalozi wa Marekani nchini, Jeffery Salaiz, alisema kati ya mambo muhimu ambayo yanasubiriwa na ubalozi wake ni ripoti za tuhuma za rushwa ambazo zinaikabili benki hiyo.
Salaiz alisema kwa ujumla nchi yake haiwezi kutoa maoni yoyote kuhusu ukimya wa Serikali tangu ilipokabidhiwa ripoti hiyo na Kampuni ya Ernst& Young iliyoofanya ukaguzi katika benki hiyo kufuatia tuhuma za ufisadi zinazoikabili.
Msemaji huyo, alisema wanaisubiri ripoti hiyo kwa sababu Marekani inaamini kwa mtu yoyote atakayebainika kuhusika na tuhuma hizo, atachukuliwa hatua kali za kisheria.
Uongozi wa Serikali ya Tanzania tunaukabali na tunaimani kuwa watu watakaotajwa kuhusika katika ufisadi watachukuliwa hatua. Na kusema ukweli hatuwezi kutoa maoni zaidi kwa sababu ripoti hatujapewa,� alisema Salaiz.
Ukaguzi wa tuhuma za ufisadi ambazo zinazoikabili BoT, ulifanywa na Kampuni ya Ernst& Young katika kipindi cha siku 60 kuanzia Septemba, mwaka huu na kuikabidhi ripoti hiyo kwa CAG.
Mapema mwishoni mwa mwezi uliopita, Waziri wa Fedha, Zakia Meghji alipoulizwa kuhusu ripoti hiyo, alisema bado iko kwa CAG na kwamba hafamu lolote kuhusu kilichomo ndani ya ripoti hiyo kwa sababu hajaiona.
Hadi sasa ripoti iko kwa CAG, sijaipata kama ni suala la maamuzi na nini kilichomo hadi ichambuliwe, nikiipata, nitaipitia, atapewa rais na maamuzi yatatangazwa kwa umma,� alisema waziri huyo.
Mbali na hayo, ripoti hiyo inasubiriwa kwa hamu na Watanzania ili kuona ukweli wa tuhuma za ufisadi ambazo zinadaiwa kufanywa katika Akaunti za Madeni ya Nje (EPA) kwa ajili ya malipo ya vocha mbalimbali.
Kampuni hiyo, awali ilipaswa kuikabidhi ripoti hiyo serikali Novemba 10 baada ya kumalizika kwa siku 60 za kufanya ukaguzi huo lakini haikufanya hivyo na iliiomba serikali wiki tatu kwa ajili ya kuandaa ripoti ambayo ilifanyika London, Uingereza.
Kampuni hiyo, ilipitia mahesabu katika kumbukumbu za vocha za malipo yaliofanywa na BoT katika kipindi cha mwaka 2005/6, kubaini kama kuna ukweli juu ya madai ya ubadhirifu wa fedha katika benki hiyo katika kipindi hicho.
Agizo la kutafuta kampuni ya kukagua vocha hizo na mahesabu ya BoT, lilitolewa na Waziri Meghji Desemba 3, mwaka jana akimtaka CAG kuteua kampuni huru ya wakaguzi wazoefu wenye sifa za kimataifa kupitia baadhi ya kumbukumbu za matumizi ya fedha za benki za mwaka 2005/6 ili kuondoa utata uliopo.
Katika hatua nyingine, Balozi wa Marekani nchini Mark Green amewataka Watanzania kutumia misaada inayotolewa na nchi yake kuzisaidia sekta mbalimbali ipasavyo kwani ni fedha zinazotokana na kodi za wananchi.
Balozi Green aliyasema hayo alipokuwa akikabidhi misaada ya compyuta na vifaa vya maktaba vya thamani ya zaidi ya Sh5 milioni katika shule ya Sekondari ya Kiislam Kionondoni inayomilikiwa na Baraza Kuu La Waislamu(Bakwata).
Marekani yasubiri kwa hamu ripoti ya BOT
John Stephen na Mwanaid Omary
Mwananchi
SERIKALI ya Marekani imesema inasubiri kwa hamu kubwa ripoti ya tuhuma za ufisadi katika Benki Kuu Ya Tanzania (BoT) ambayo tayari amekabidhiwa Mthibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).
Akizungumza jana na Mwananchi Msemaji wa Ubalozi wa Marekani nchini, Jeffery Salaiz, alisema kati ya mambo muhimu ambayo yanasubiriwa na ubalozi wake ni ripoti za tuhuma za rushwa ambazo zinaikabili benki hiyo.
Salaiz alisema kwa ujumla nchi yake haiwezi kutoa maoni yoyote kuhusu ukimya wa Serikali tangu ilipokabidhiwa ripoti hiyo na Kampuni ya Ernst& Young iliyoofanya ukaguzi katika benki hiyo kufuatia tuhuma za ufisadi zinazoikabili.
Msemaji huyo, alisema wanaisubiri ripoti hiyo kwa sababu Marekani inaamini kwa mtu yoyote atakayebainika kuhusika na tuhuma hizo, atachukuliwa hatua kali za kisheria.
Uongozi wa Serikali ya Tanzania tunaukabali na tunaimani kuwa watu watakaotajwa kuhusika katika ufisadi watachukuliwa hatua. Na kusema ukweli hatuwezi kutoa maoni zaidi kwa sababu ripoti hatujapewa,� alisema Salaiz.
Ukaguzi wa tuhuma za ufisadi ambazo zinazoikabili BoT, ulifanywa na Kampuni ya Ernst& Young katika kipindi cha siku 60 kuanzia Septemba, mwaka huu na kuikabidhi ripoti hiyo kwa CAG.
Mapema mwishoni mwa mwezi uliopita, Waziri wa Fedha, Zakia Meghji alipoulizwa kuhusu ripoti hiyo, alisema bado iko kwa CAG na kwamba hafamu lolote kuhusu kilichomo ndani ya ripoti hiyo kwa sababu hajaiona.
Hadi sasa ripoti iko kwa CAG, sijaipata kama ni suala la maamuzi na nini kilichomo hadi ichambuliwe, nikiipata, nitaipitia, atapewa rais na maamuzi yatatangazwa kwa umma,� alisema waziri huyo.
Mbali na hayo, ripoti hiyo inasubiriwa kwa hamu na Watanzania ili kuona ukweli wa tuhuma za ufisadi ambazo zinadaiwa kufanywa katika Akaunti za Madeni ya Nje (EPA) kwa ajili ya malipo ya vocha mbalimbali.
Kampuni hiyo, awali ilipaswa kuikabidhi ripoti hiyo serikali Novemba 10 baada ya kumalizika kwa siku 60 za kufanya ukaguzi huo lakini haikufanya hivyo na iliiomba serikali wiki tatu kwa ajili ya kuandaa ripoti ambayo ilifanyika London, Uingereza.
Kampuni hiyo, ilipitia mahesabu katika kumbukumbu za vocha za malipo yaliofanywa na BoT katika kipindi cha mwaka 2005/6, kubaini kama kuna ukweli juu ya madai ya ubadhirifu wa fedha katika benki hiyo katika kipindi hicho.
Agizo la kutafuta kampuni ya kukagua vocha hizo na mahesabu ya BoT, lilitolewa na Waziri Meghji Desemba 3, mwaka jana akimtaka CAG kuteua kampuni huru ya wakaguzi wazoefu wenye sifa za kimataifa kupitia baadhi ya kumbukumbu za matumizi ya fedha za benki za mwaka 2005/6 ili kuondoa utata uliopo.
Katika hatua nyingine, Balozi wa Marekani nchini Mark Green amewataka Watanzania kutumia misaada inayotolewa na nchi yake kuzisaidia sekta mbalimbali ipasavyo kwani ni fedha zinazotokana na kodi za wananchi.
Balozi Green aliyasema hayo alipokuwa akikabidhi misaada ya compyuta na vifaa vya maktaba vya thamani ya zaidi ya Sh5 milioni katika shule ya Sekondari ya Kiislam Kionondoni inayomilikiwa na Baraza Kuu La Waislamu(Bakwata).