Ripoti madai ya sumu Mto Mara zina utata, zimetofautiana, wataalam wamezichambua

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,308
5,458
Juzi kati niliona memba humu JF akiandika juu ya taarifa za kemikali zenye sumu kutoka mgodini zilivyoharibu mazingira kwenye Mto Mara na kusababisha vifo vya samaki na pamoja maji kuwa meusi.

Baadaye habari hiyo ikasambaa na kuwa kubwa mwisho Serikali ikiingilia kati na kufanya uchunguzi kuhusu taarifa hizo.

Ripoti ya awali ikatolewa, wakagusia kuwa hakuna sumu bali ni mafuta ndiyo maana Oksijeni ikawa ndogo kwenye maji, wakasema wanaendelea kuchunguza kwa nini maji yamekuwa meusi.

……………………

NANUKUU KILICHOSEMWA SIKU HIYO…
“Akizungumza na waandishi wa habari Machi 12, 2022 jijini Mwanza, Mkurugenzi wa Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Victoria (LVBWB), Renatus Shinhu ametaja vijiji vilivyoathirika kutokana na uchafuzi huo kuwa ni Kirumi, Kwibuse, Marasibora, Ketasakwa na Ryamisanga.

“Uchunguzi wa kimaabara umeonesha mambo mawili ikiwemo kuwepo kwa kiwango kikubwa cha mafuta kuliko kiwango kinachokubalika kwa mujibu wa viwango vya ubora wa maji Tanzania (TZs 2068:2017),” amesema Shinhu.

MWISHO WA KUNUKUU


…………………….

Sasa baada ya ripoti hiyo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Selemani Jaffo akaunda kamati maalum ya kitaifa kuchunguza chanzo cha mabadiliko katika Mto Mara yaliyosababisha maji ya mto huo kubadilika rangi na kuwa nyeusi.

Ndipo ripoti hiyo ya leo Jumamosi Machi 19, 2022 ikatolewa ikiwa na sababu nyingine tofauti, yenyewe ikisema kuwa eti wingi wa kinyesi cha ng’ombe na mkojo ndiyo sababu ya maji kuwa meusi na hatimaye kusababisha vifo vya Samaki wengi.

Inafikirisha kidogo, sasa kufikia hapo tumuamini nani, wale waliosema Samaki wanakufa kwa sababu ya mafuta kuwa mengi tena wakataja kabisa kuwa ni Dizel na Petrol, hawa wengine wanatuaminia kinyesi…

…………………….

NANUKUU RIPOTI YA KAMATI MAALUM YA KITAIFA ILIYOUNDWA NA SERIKALI
Akitoa matokeo ya uchunguzi Jumamosi Machi 19, 2022 mjini Musoma, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Profesa Samuel Manyele amesema kuwa hali hiyo imetokana na kuwepo kwa kiwango kikubwa cha kinyesi cha mifugo mtoni pamoja na uozo wa mimea ndani ya mto hasa mimea vamizi kama vile magugu maji na matete.

Amesema kuwa hali hiyo ilisababisha kupungua kwa kiasi kikubwa kiwango cha oksijeni ndani ya mto na hivyo maji kubadilika rangi na kuwa na harufu mbaya huku samaki wakikosa chakula na hivyo kusababisha vifo vyao.

MWISHO WA KUNUKUU


…………………………………..

Baada ya hapo nimewatafuta wataalamu wawili wa masuala ya ufugaji, mmoja ni kutoka Serikalini na mwingine ni sekta binafsi na kuwauliza kuhusu uwezekano wa samaki kufa wengi kutokana na kinyesi na mkono wa ng’ombe, hawa hapa wanafafanua…


Mtaalam wa kwanza
“Kwa kawaida kinyesi cha ng’ombe huwa ni sehemu ya chakula kwa Samaki na viumbe wengine kwenye maji, ndiyo maana kwenye mabwawa yanayofuga Samaki huwa ni kawaida kuona wafugaji wakitumia kinyesi hicho kwa ajli ya chakula cha Samaki.

“Ikitokea kwenye bwawa unalofugia kinyesi kikawa kingi kupitiliza kinaweza kusababisha kukosekana kwa oksijeni kutokana na kuziba njia kwa juu, hali hiyo ikiendelea kwa muda inaweza kusababisha samaki wakafa kweli.

“Lakini kwa sehemu kama mto au ziwa au bwawa kubwa mara nyingi kinyesi kikiwa kingi kinasambaa hivyo kinayeyushwa, tena kwenye mto au ziwa ni ngumu zaidi kusema kinyesi kimeziba na kukosekana kwa oksijeni.

“Ni ngumu kuona kinyesi kimeziba oksijeni kwenye mto wakati unajua maji ni mengi na kadiri kinyesi kinavyoingia kwenye maji ndivyo kinavyosambaa.

“Kingine ni kuwa kama kweli hali hiyo imetokea unatakiwa kujiuliza imetokea kwa muda gani, yaani imechukua muda mrefu kiasi gani hadi hali hiyo ikatokea, kama ni ndani ya muda mfupi basi hilo ni tatizo lingine, kama ni muda mrefu inamaanisha mlundikano huo ulitakiwa kuonekana mapema na siyo ghafla.

“Kitaalam ikitokea samaki wengi wamekufa kwenye mto au ziwa au bahari ndani ya muda mfupi basi hapo kuna tatizo, ama kuna sumu au kuna kemikali ambao haziendani na samaki.”


Mtaalam wa pili
“Inapotokea kuna magugu au majani mengi kwenye maji kisha kukawa na kinyesi kingi kinajaa kwenye maji, oksijeni itakosekana na itahatarisha maisha ya samaki.

“Hilo linaweza kutokea lakini iwe ni katika sehemu ndogo ya maji ambayo inakuwa na mrundikano wa vitu nilivyoeleza hapo juu, lakini kusema tu ni kinyesi na mkono, swali ni kuwa hali hiyo imetokea kwa muda gani yaani namaanisha mrundikano umechukua miezi mingapi?

“Kingine kinachonipa wasiwasi kuhusu hiyo ripoti ni kuwa maji yamekuwa meusi, hilo kitaalamu sina hakika nalo, ingekuwa imetokea kwenye kibwawa kidogo nisingekuwa na wasiwasi, lakini maji kuwa meusi kwenye mto kisa mikojo na kinyesi nafikiri nahitaji kujifunza zaidi kutoka kwa hao wataalam.”

Pia soma...
Madai ya sumu Mto Mara kutoka migodini, wananchi wazuiwa kutumia maji, kula samaki, uvuvi, Serikali yatoa tamko
Vifo vya Samaki Mto Mara: Kamati ya Dharura yaundwa kuchunguza Samaki wanaodaiwa kufa kwa Sumu
 
Juzi kati niliona memba humu JF akiandika juu ya taarifa za kemikali zenye sumu kutoka mgodini zilivyoharibu mazingira kwenye Mto Mara na kusababisha vifo vya samaki na pamoja maji kuwa meusi....kidogo nisingekuwa na wasiwasi, lakini maji kuwa meusi kwenye mto kisa mikojo na kinyesi nafikiri nahitaji kujifunza zaidi kutoka kwa hao wataalam.”
Mkuu kiufupi hapo tumepigwa.
 
NANUKUU RIPOTI YA KAMATI MAALUM YA KITAIFA ILIYOUNDWA NA SERIKALI
Akitoa matokeo ya uchunguzi Jumamosi Machi 19, 2022 mjini Musoma, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Profesa Samuel Manyele amesema kuwa hali hiyo imetokana na kuwepo kwa kiwango kikubwa cha kinyesi cha mifugo mtoni pamoja na uozo wa mimea ndani ya mto hasa mimea vamizi kama vile magugu maji na matete...
Kiukweli Prof. huyu achunguzwe kwa possibility ya kuwa compromised!.
Kinyesi cha ngombe ni chakula cha samaki na ni soluble in water, hakuna kinyesi chochote cha ngombe kuua Samaki!.

Sii wengi wanafahamu jinsi makampuni makubwa ya madini yalivyo tayari to spend billions kujisafisha kuliko kushitakiwa kwa kumwaga sumu ardhini.

hawakuanza Leo, kwa wanaokikumbuka kisa cha mto Tigiti.

This is not the first time wataalamu wetu kuwa compromised. Ngoja na mimi nijipange kuandika bonge la IJ.
huko nyuma niliwahi kuuliza


Hivyo nashauri wataalamu wetu hawa wachunguzwe!.
P
 
Tumeanza Rasmi Sarakasi na Michezo ya Maigizo ht kwa issue sensitive...hizi sarakazi zote kumlinda nani?and why wanatoa report za hovyo km hivi, au wanahisi we are fools hatujui kua kinyesi ni chakula cha samaki?

Au hao ng'ombe wapo mkoa wa Mara tu, mikoa mingine ng'ombe wao wanatumiaje mito?au Mkoa wa Mara wameanza kufuga mwaka huu?

Mtu anatoa report ambayo haileti mantiki na bado yupo ofcn...kwa maslai ya nani?
 
Tumeanza Rasmi Sarakasi na Michezo ya Maigizo ht kwa issue sensitive...hizi sarakazi zote kumlinda nani?and why wanatoa report za hovyo km hivi, au wanahisi we are fools hatujui kua kinyesi ni chakula cha samaki...
Inashangaza sana, tena mtoaji wa ripoti ni PROFESA
 
Pascal Mayala

Mtu mwelewa, mtu ujulikanaye unaandika bila kuwa na ushahidi wala kufika field?

1. Unajua maji yatokayo ktk Mgodi wa BARRICK NORTH MARA sio meusi?

2. Unajua watu walio~upstream hawakuathirika na madhara ya uchafuzi wa maji ya Mto Mara?

3. Unajua maji meusi yapo ktk ardhi oevu ambayo ipo mbali na discharge point ya mgodi!?

4. Unajua kuwa mifugo haikuwa ndani ya maji kabla ya mvua kubwa kunyesha?

5. Unajua kuwa utafiti umefanywa sehemu tofauti duniani kuhusu ng'ombe anazalisha samadi kiasi gani kwa siku? Utafiti wa karibuni ni wa mwaka 2020 Kenya ulioonesha huzalisha hadi kilo 25 kwa siku?

6. Unajua samadi huzalisha hewa ya methane (wanaotumia mitambo ya biogas wanafahamu) ambayo ikichanganyika na maji huzalisha hewa ya carbon dioxide ambapo mchakato wake huhusisha oxygen kutumika hivyo kupingua Dissolved Oxygen ktk maji?

7. Unajua kuwa Kamati Maalum ya Kitaifa ya Kuchungiza Chanzo cha Uchafuzi wa Maji ya Mto Mara imetaja sababu mbili; Natural Causes na Human Activities? Ni kwa nini hutaki kuzungumzia NATURAL CAUSES?

8. Unajua kuwa kina cha mto ni kati ya mita tisa hadi 12? Unajua kuwa kina cha maji ni mita tatu hadi nne tu huku zinazobaki hadi kufika riverbed ni mrudikano wa uozo wa viumbehai vilivyokufa?

9. Unajua kuwa mwezi Februari 2022 kiwango cha maji yaliyokuwa yanapita mtoni ni chini ya mita ya ujazo moja kwa sekunde? Lakini kati ya tarehe 24/02 hadi 27/02/2022 mvua zilizonyesha upstream zilisababisha maji kuongezeka hadi kufikia mita za ujazo sita kwa sekunde?

10. Unajua wingi huo wa maji uliharibu equlibrum iliyokuwepo ktk ardhioevu hivyo kusababisha mvurugo wa mrundikano wa uozo?

11. Unajua kuwa mvurugano wa uozo ulisababisha kuonekana kwa utando wa mafuta (biogenic) juu ya maji?

12. Unajua mvurugano ulisababisha baktrea wanaochochea kuoza kuongeza matumizi ya oksijeni hivyo kuimaliza?

13. Unajua ardhi oevu imevamiwa na magugu ambayo yanakaribia kuufunika mto wote hivyo kupunguza kiwango cha Dissolved Oxygen ktk maji?

14. Unajua kuwa sampuli za matope (sediments), maji na samaki zilichukuliwa na kuwasilishwa ktk maabara kwa ajili ya vipimo? Unajua hakuna madini tembo (heavy metals) zilizoonekana?

15. Unajua hakuna binadamu aliyeathirika kwa kutumia maji ay samaki waliovuliwa ktk maji ya mto mara?

16. Unajua kuwa taarifa za mto kuchafuka ilitolewa tarehe 06/03/2022 na hadi leo (19/03/2022) bado uchafuzi unaendelea.

17. Unajua kuwa bwawa la majisumu (TSF) ya mgodi lina uwezo wa kuhifadhi lita 800,000 tu. Kumbuka uchafuzi umeripotia tarehe 06/03/2022 na hadi leo (19/03/2022) yasingeweza kuwa yanaendelea kutiririka?

18. Unajua vipimo vya papo kwa papo (in situ parametres) ktk discharge point ya mgodi zinaonesha kuwa maji ni salama?

NB: Umepigwa na kitu kizito kwani ulitegemea taarifa iwalaumu BARRICK NORTH MARA GOLD MINES - NYAMOGO ili upate labda faida binafsi au ya kisiasa. Kwa kukosa kwako fursa kumekufanya uanze UZUSHI.

Bazazi ni Bazazi na si bazazi!
Kiukweli Prof. huyu achunguzwe kwa possibility ya kuwa compromised!.
Kinyesi cha ngombe ni chakula cha samaki na ni soluble in water, hakuna kinyesi chochote cha ngombe kuua Samaki!.

Sii wengi wanafahamu jinsi makampuni makubwa ya madini yalivyo tayari to spend billions kujisafisha kuliko kushitakiwa kwa kumwaga sumu ardhini.

hawakuanza Leo, kwa wanaokikumbuka kisa cha mto Tigiti.

This is not the first time wataalamu wetu kuwa compromised. Ngoja na mimi nijipange kuandika bonge la IJ.
huko nyuma niliwahi kuuliza


Hivyo nashauri wataalamu wetu hawa wachunguzwe!.
P
 
Pascal Mayala

Mtu mwelewa, mtu ujulikanaye unaandika bila kuwa na ushahidi wala kufika field?
...
Tukiachana na hayo uliyo mention je kwanini ripoti zitofautiane?

Kuna mmoja katiyao ametudanganya? Kwanini atudanganye? Nani yuko nyuma ya huo uongo?
 
Pascal Mayala

Mtu mwelewa, mtu ujulikanaye unaandika bila kuwa na ushahidi wala kufika field?

1. Unajua maji yatokayo ktk Mgodi wa BARRICK NORTH MARA sio meusi?

2. Unajua watu walio~upstream hawakuathirika na madhara ya uchafuzi wa maji ya Mto Mara?

3. Unajua maji meusi yapo ktk ardhi oevu ambayo ipo mbali na discharge point ya mgodi!?

4. Unajua kuwa mifugo haikuwa ndani ya maji kabla ya mvua kubwa kunyesha?

5. Unajua kuwa utafiti umefanywa sehemu tofauti duniani kuhusu ng'ombe anazalisha samadi kiasi gani kwa siku? Utafiti wa karibuni ni wa mwaka 2020 Kenya ulioonesha huzalisha hadi kilo 25 kwa siku?

6. Unajua samadi huzalisha hewa ya methane (wanaotumia mitambo ya biogas wanafahamu) ambayo ikichanganyika na maji huzalisha hewa ya carbon dioxide ambapo mchakato wake huhusisha oxygen kutumika hivyo kupingua Dissolved Oxygen ktk maji?

7. Unajua kuwa Kamati Maalum ya Kitaifa ya Kuchungiza Chanzo cha Uchafuzi wa Maji ya Mto Mara imetaja sababu mbili; Natural Causes na Human Activities? Ni kwa nini hutaki kuzungumzia NATURAL CAUSES?

8. Unajua kuwa kina cha mto ni kati ya mita tisa hadi 12? Unajua kuwa kina cha maji ni mita tatu hadi nne tu huku zinazobaki hadi kufika riverbed ni mrudikano wa uozo wa viumbehai vilivyokufa?

9. Unajua kuwa mwezi Februari 2022 kiwango cha maji yaliyokuwa yanapita mtoni ni chini ya mita ya ujazo moja kwa sekunde? Lakini kati ya tarehe 24/02 hadi 27/02/2022 mvua zilizonyesha upstream zilisababisha maji kuongezeka hadi kufikia mita za ujazo sita kwa sekunde?

10. Unajua wingi huo wa maji uliharibu equlibrum iliyokuwepo ktk ardhioevu hivyo kusababisha mvurugo wa mrundikano wa uozo?

11. Unajua kuwa mvurugano wa uozo ulisababisha kuonekana kwa utando wa mafuta (biogenic) juu ya maji?

12. Unajua mvurugano ulisababisha baktrea wanaochochea kuoza kuongeza matumizi ya oksijeni hivyo kuimaliza?

13. Unajua ardhi oevu imevamiwa na magugu ambayo yanakaribia kuufunika mto wote hivyo kupunguza kiwango cha Dissolved Oxygen ktk maji?

14. Unajua kuwa sampuli za matope (sediments), maji na samaki zilichukuliwa na kuwasilishwa ktk maabara kwa ajili ya vipimo? Unajua hakuna madini tembo (heavy metals) zilizoonekana?

15. Unajua hakuna binadamu aliyeathirika kwa kutumia maji ay samaki waliovuliwa ktk maji ya mto mara?

16. Unajua kuwa taarifa za mto kuchafuka ilitolewa tarehe 06/03/2022 na hadi leo (19/03/2022) bado uchafuzi unaendelea.

17. Unajua kuwa bwawa la majisumu (TSF) ya mgodi lina uwezo wa kuhifadhi lita 800,000 tu. Kumbuka uchafuzi umeripotia tarehe 06/03/2022 na hadi leo (19/03/2022) yasingeweza kuwa yanaendelea kutiririka?

18. Unajua vipimo vya papo kwa papo (in situ parametres) ktk discharge point ya mgodi zinaonesha kuwa maji ni salama?

NB: Umepigwa na kitu kizito kwani ulitegemea taarifa iwalaumu BARRICK NORTH MARA GOLD MINES - NYAMOGO ili upate labda faida binafsi au ya kisiasa. Kwa kukosa kwako fursa kumekufanya uanze UZUSHI.

Bazazi ni Bazazi na si bazazi!
Zazazi tulia.
Ukweli utajulikana tu
 
Tumeanza Rasmi Sarakasi na Michezo ya Maigizo ht kwa issue sensitive...hizi sarakazi zote kumlinda nani?and why wanatoa report za hovyo km hivi, au wanahisi we are fools hatujui kua kinyesi ni chakula cha samaki...
Prof anakua compromised kirahisi wakati Hali hiyo inaweza leta madhara makubwa kwa binadamu ikiwemo kifo kwa watu wataokula samaki hao.

Ndio nchi yetu ilipofikia hapa
 
Hii Nchi ingefuta kitu kinacho itwa profesar maana ndo wanatuangusha sana iwe kwenye uchunguzi n.k sjui ndo mfumo wa elimu ulivyo ndo unazalisha watu kama hao
 
Tukiachana na hayo uliyo mention je kwanini ripoti zitofautiane?

Kuna mmoja katiyao ametudanganya? Kwanini atudanganye? Nani yuko nyuma ya huo uongo?
Hii nayo ni hoja muhimu, ijibiwe, kwa nini ripoti ziwe tofauti?
 
Pascal Mayala

Mtu mwelewa, mtu ujulikanaye unaandika bila kuwa na ushahidi wala kufika field?

1. Unajua maji yatokayo ktk Mgodi wa BARRICK NORTH MARA sio meusi?

2. Unajua watu walio~upstream hawakuathirika na madhara ya uchafuzi wa maji ya Mto Mara?

3. Unajua maji meusi yapo ktk ardhi oevu ambayo ipo mbali na discharge point ya mgodi!?

4. Unajua kuwa mifugo haikuwa ndani ya maji kabla ya mvua kubwa kunyesha?

5. Unajua kuwa utafiti umefanywa sehemu tofauti duniani kuhusu ng'ombe anazalisha samadi kiasi gani kwa siku? Utafiti wa karibuni ni wa mwaka 2020 Kenya ulioonesha huzalisha hadi kilo 25 kwa siku?

6. Unajua samadi huzalisha hewa ya methane (wanaotumia mitambo ya biogas wanafahamu) ambayo ikichanganyika na maji huzalisha hewa ya carbon dioxide ambapo mchakato wake huhusisha oxygen kutumika hivyo kupingua Dissolved Oxygen ktk maji?

7. Unajua kuwa Kamati Maalum ya Kitaifa ya Kuchungiza Chanzo cha Uchafuzi wa Maji ya Mto Mara imetaja sababu mbili; Natural Causes na Human Activities? Ni kwa nini hutaki kuzungumzia NATURAL CAUSES?

8. Unajua kuwa kina cha mto ni kati ya mita tisa hadi 12? Unajua kuwa kina cha maji ni mita tatu hadi nne tu huku zinazobaki hadi kufika riverbed ni mrudikano wa uozo wa viumbehai vilivyokufa?

9. Unajua kuwa mwezi Februari 2022 kiwango cha maji yaliyokuwa yanapita mtoni ni chini ya mita ya ujazo moja kwa sekunde? Lakini kati ya tarehe 24/02 hadi 27/02/2022 mvua zilizonyesha upstream zilisababisha maji kuongezeka hadi kufikia mita za ujazo sita kwa sekunde?

10. Unajua wingi huo wa maji uliharibu equlibrum iliyokuwepo ktk ardhioevu hivyo kusababisha mvurugo wa mrundikano wa uozo?

11. Unajua kuwa mvurugano wa uozo ulisababisha kuonekana kwa utando wa mafuta (biogenic) juu ya maji?

12. Unajua mvurugano ulisababisha baktrea wanaochochea kuoza kuongeza matumizi ya oksijeni hivyo kuimaliza?

13. Unajua ardhi oevu imevamiwa na magugu ambayo yanakaribia kuufunika mto wote hivyo kupunguza kiwango cha Dissolved Oxygen ktk maji?

14. Unajua kuwa sampuli za matope (sediments), maji na samaki zilichukuliwa na kuwasilishwa ktk maabara kwa ajili ya vipimo? Unajua hakuna madini tembo (heavy metals) zilizoonekana?

15. Unajua hakuna binadamu aliyeathirika kwa kutumia maji ay samaki waliovuliwa ktk maji ya mto mara?

16. Unajua kuwa taarifa za mto kuchafuka ilitolewa tarehe 06/03/2022 na hadi leo (19/03/2022) bado uchafuzi unaendelea.

17. Unajua kuwa bwawa la majisumu (TSF) ya mgodi lina uwezo wa kuhifadhi lita 800,000 tu. Kumbuka uchafuzi umeripotia tarehe 06/03/2022 na hadi leo (19/03/2022) yasingeweza kuwa yanaendelea kutiririka?

18. Unajua vipimo vya papo kwa papo (in situ parametres) ktk discharge point ya mgodi zinaonesha kuwa maji ni salama?

NB: Umepigwa na kitu kizito kwani ulitegemea taarifa iwalaumu BARRICK NORTH MARA GOLD MINES - NYAMOGO ili upate labda faida binafsi au ya kisiasa. Kwa kukosa kwako fursa kumekufanya uanze UZUSHI.

Bazazi ni Bazazi na si bazazi!
Umetoa maswali ya kitaalam sana, sijui kama Mayala atakuelewa.

Mimi sikufika field wakati huu lakini naufahamu mto Mara unakopita, nafahamu mabwawa ya maji sumu ya Barrick yaliko, nafahamu chemicals zinazotumika kwenye gold recovery processes na chemistry yake.

Niliposikia tu juu ya hali ilivyo mto Mara, kisha nikasikia baadhi ya watu wasiojua chochote wakihusisha hali hiyo na mgodi wa North Mara, nilieleza wazi kuwa hiyo ni hoja ya wajinga wasiojua chochote. Hakukuwa na uwezekano kabisa eti chemikali za sumu zisafiri toka North Mara mpaka Mto Mara, bila ya kuwa na maafa ya binadamu au mifugo kwenye maeneo ambayo kemikali hizo zingekuwa zimepita.

Kemikali ambayo ni sumu inayotumika ni Sodium Cyanide, lakini kemikali hii sumu yake hudumu kwa muda mfupi. Ingeweza kusababisha madhara ya vifo vya wanyama, binadamu, ndege hata samaki kwenye discharge point lakini siyo isafiri kilometa nyingi, halafu kote ilikotokea isilete madhara, madhara yakatokee kilometa nyingi, na kwa samaki tu, na siyo kwa viumbe wengine.

Watu hawajui, hata magugu maji yakitanda mengi, husababisha vifo vya samaki. Ndani ya ziwa Victoria, karibia kila mwaka, kuna samaki huwa wanakufa. Haitangazwi kama janga kwa sababu huwa ni neema kwa wavuvi, hibeba hiyo mizoga ya samaki, na kuwauza kama vile ni samaki wamevuliwa kwa njia za kawaida.
 
Juzi kati niliona memba humu JF akiandika juu ya taarifa za kemikali zenye sumu kutoka mgodini zilivyoharibu mazingira kwenye Mto Mara na kusababisha vifo vya samaki na pamoja maji kuwa meusi.

Baadaye habari hiyo ikasambaa na kuwa kubwa mwisho Serikali ikiingilia kati na kufanya uchunguzi kuhusu taarifa hizo.

Ripoti ya awali ikatolewa, wakagusia kuwa hakuna sumu bali ni mafuta ndiyo maana Oksijeni ikawa ndogo kwenye maji, wakasema wanaendelea kuchunguza kwa nini maji yamekuwa meusi.

……………………

NANUKUU KILICHOSEMWA SIKU HIYO…
“Akizungumza na waandishi wa habari Machi 12, 2022 jijini Mwanza, Mkurugenzi wa Bodi ya Maji Bonde la Ziwa Victoria (LVBWB), Renatus Shinhu ametaja vijiji vilivyoathirika kutokana na uchafuzi huo kuwa ni Kirumi, Kwibuse, Marasibora, Ketasakwa na Ryamisanga.

“Uchunguzi wa kimaabara umeonesha mambo mawili ikiwemo kuwepo kwa kiwango kikubwa cha mafuta kuliko kiwango kinachokubalika kwa mujibu wa viwango vya ubora wa maji Tanzania (TZs 2068:2017),” amesema Shinhu.

MWISHO WA KUNUKUU


…………………….

Sasa baada ya ripoti hiyo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Selemani Jaffo akaunda kamati maalum ya kitaifa kuchunguza chanzo cha mabadiliko katika Mto Mara yaliyosababisha maji ya mto huo kubadilika rangi na kuwa nyeusi.

Ndipo ripoti hiyo ya leo Jumamosi Machi 19, 2022 ikatolewa ikiwa na sababu nyingine tofauti, yenyewe ikisema kuwa eti wingi wa kinyesi cha ng’ombe na mkojo ndiyo sababu ya maji kuwa meusi na hatimaye kusababisha vifo vya Samaki wengi.

Inafikirisha kidogo, sasa kufikia hapo tumuamini nani, wale waliosema Samaki wanakufa kwa sababu ya mafuta kuwa mengi tena wakataja kabisa kuwa ni Dizel na Petrol, hawa wengine wanatuaminia kinyesi…

…………………….

NANUKUU RIPOTI YA KAMATI MAALUM YA KITAIFA ILIYOUNDWA NA SERIKALI
Akitoa matokeo ya uchunguzi Jumamosi Machi 19, 2022 mjini Musoma, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Profesa Samuel Manyele amesema kuwa hali hiyo imetokana na kuwepo kwa kiwango kikubwa cha kinyesi cha mifugo mtoni pamoja na uozo wa mimea ndani ya mto hasa mimea vamizi kama vile magugu maji na matete.

Amesema kuwa hali hiyo ilisababisha kupungua kwa kiasi kikubwa kiwango cha oksijeni ndani ya mto na hivyo maji kubadilika rangi na kuwa na harufu mbaya huku samaki wakikosa chakula na hivyo kusababisha vifo vyao.

MWISHO WA KUNUKUU


…………………………………..

Baada ya hapo nimewatafuta wataalamu wawili wa masuala ya ufugaji, mmoja ni kutoka Serikalini na mwingine ni sekta binafsi na kuwauliza kuhusu uwezekano wa samaki kufa wengi kutokana na kinyesi na mkono wa ng’ombe, hawa hapa wanafafanua…


Mtaalam wa kwanza
“Kwa kawaida kinyesi cha ng’ombe huwa ni sehemu ya chakula kwa Samaki na viumbe wengine kwenye maji, ndiyo maana kwenye mabwawa yanayofuga Samaki huwa ni kawaida kuona wafugaji wakitumia kinyesi hicho kwa ajli ya chakula cha Samaki.

“Ikitokea kwenye bwawa unalofugia kinyesi kikawa kingi kupitiliza kinaweza kusababisha kukosekana kwa oksijeni kutokana na kuziba njia kwa juu, hali hiyo ikiendelea kwa muda inaweza kusababisha samaki wakafa kweli.

“Lakini kwa sehemu kama mto au ziwa au bwawa kubwa mara nyingi kinyesi kikiwa kingi kinasambaa hivyo kinayeyushwa, tena kwenye mto au ziwa ni ngumu zaidi kusema kinyesi kimeziba na kukosekana kwa oksijeni.

“Ni ngumu kuona kinyesi kimeziba oksijeni kwenye mto wakati unajua maji ni mengi na kadiri kinyesi kinavyoingia kwenye maji ndivyo kinavyosambaa.

“Kingine ni kuwa kama kweli hali hiyo imetokea unatakiwa kujiuliza imetokea kwa muda gani, yaani imechukua muda mrefu kiasi gani hadi hali hiyo ikatokea, kama ni ndani ya muda mfupi basi hilo ni tatizo lingine, kama ni muda mrefu inamaanisha mlundikano huo ulitakiwa kuonekana mapema na siyo ghafla.

“Kitaalam ikitokea samaki wengi wamekufa kwenye mto au ziwa au bahari ndani ya muda mfupi basi hapo kuna tatizo, ama kuna sumu au kuna kemikali ambao haziendani na samaki.”


Mtaalam wa pili
“Inapotokea kuna magugu au majani mengi kwenye maji kisha kukawa na kinyesi kingi kinajaa kwenye maji, oksijeni itakosekana na itahatarisha maisha ya samaki.

“Hilo linaweza kutokea lakini iwe ni katika sehemu ndogo ya maji ambayo inakuwa na mrundikano wa vitu nilivyoeleza hapo juu, lakini kusema tu ni kinyesi na mkono, swali ni kuwa hali hiyo imetokea kwa muda gani yaani namaanisha mrundikano umechukua miezi mingapi?

“Kingine kinachonipa wasiwasi kuhusu hiyo ripoti ni kuwa maji yamekuwa meusi, hilo kitaalamu sina hakika nalo, ingekuwa imetokea kwenye kibwawa kidogo nisingekuwa na wasiwasi, lakini maji kuwa meusi kwenye mto kisa mikojo na kinyesi nafikiri nahitaji kujifunza zaidi kutoka kwa hao wataalam.”
CLUE NO 1: JE, kuna mgodi wowote within a radius of 50-100km?
 
Ukweli ni kwamba hizo sumu zinatiririshwa kutoka mgodini, kwa maana nyingine hatua za kisheria zinapaswa kuchukuliwa...

NEMC wanatuabisha sana...
 
Back
Top Bottom