kimsboy
JF-Expert Member
- Oct 17, 2016
- 8,991
- 17,888
Israel ilitoa msaada wa kijasusi kwa Saudia katika mauaji ya Khashoggi
Imebainika kuwa shirika moja la kijasusi la utawala wa Israel lilitoa msaada mkubwa kwa ufalme Saudi Arabia ili kufanikisha mauaji ya mwandishi habari Jamal Khashoggi ambaye alikuwa mkosoaji mkubwa wa ufalme huo wa kiimla.
Hayo yamefichuliwa na gazeti la New York Times ambalo limeandika kuwa shirika moja la ujasusi wa mitandaoni la Israel lilitumika katika kufuatilia mawasiliano ya simu ya Khashoggi na kuwakabidhi wakuu wa Saudia taarifa zote za mawasiliano ya mwandishi huyo ambaye aliuawa kinyama. Taarifa zinasema shirika la ujasusi wa mitandaoni la NSO Group la Israel lilinasa mawasiliano yote baina ya simu za mkonono za Khashoggi na mpinzani mwigine wa Saudia aliye uhamishoni. Mawasiliano hayo yalinaswa kwa kutumia programu ya Pegasus ya ujasusi ambayo hubadilisha simu erevu au smartphone ya mlengwa kuwa chombo cha ujasusi. Mpinzani Msaudi anayeishi uhamishoni Canada Omar Abdulaziz sasa amewasilisha mashtaka dhidi ya shirika hilo. Katika mashtaka yake anataka pia kuwepo uchunguzi zaidi kuhusu ushirikiano wa kijasusi baina ya Israel na Saudi Arabia pamoja na tawala zingine za kifalme katika Ghuba ya Uajemi.
Jamal Khashoggi, aliyewahi kuwa msiri na mwandani wa aila ya kifalme inayotawala nchini Saudi Arabia, lakini hatimaye akageuka kuwa mkosoaji mkubwa wa utawala wa Aal Saud, aliuliwa na mwili wake kukatwa vipande vipande, alipoingia kwenye jengo la ubalozi mdogo wa nchi hiyo mjini Istanbul, Uturuki mnamo tarehe Pili Oktoba ili kukabidhi hati zake kwa ajili ya mpango wake wa kufunga ndoa.
Imebainika kuwa shirika moja la kijasusi la utawala wa Israel lilitoa msaada mkubwa kwa ufalme Saudi Arabia ili kufanikisha mauaji ya mwandishi habari Jamal Khashoggi ambaye alikuwa mkosoaji mkubwa wa ufalme huo wa kiimla.
Hayo yamefichuliwa na gazeti la New York Times ambalo limeandika kuwa shirika moja la ujasusi wa mitandaoni la Israel lilitumika katika kufuatilia mawasiliano ya simu ya Khashoggi na kuwakabidhi wakuu wa Saudia taarifa zote za mawasiliano ya mwandishi huyo ambaye aliuawa kinyama. Taarifa zinasema shirika la ujasusi wa mitandaoni la NSO Group la Israel lilinasa mawasiliano yote baina ya simu za mkonono za Khashoggi na mpinzani mwigine wa Saudia aliye uhamishoni. Mawasiliano hayo yalinaswa kwa kutumia programu ya Pegasus ya ujasusi ambayo hubadilisha simu erevu au smartphone ya mlengwa kuwa chombo cha ujasusi. Mpinzani Msaudi anayeishi uhamishoni Canada Omar Abdulaziz sasa amewasilisha mashtaka dhidi ya shirika hilo. Katika mashtaka yake anataka pia kuwepo uchunguzi zaidi kuhusu ushirikiano wa kijasusi baina ya Israel na Saudi Arabia pamoja na tawala zingine za kifalme katika Ghuba ya Uajemi.
Jamal Khashoggi, aliyewahi kuwa msiri na mwandani wa aila ya kifalme inayotawala nchini Saudi Arabia, lakini hatimaye akageuka kuwa mkosoaji mkubwa wa utawala wa Aal Saud, aliuliwa na mwili wake kukatwa vipande vipande, alipoingia kwenye jengo la ubalozi mdogo wa nchi hiyo mjini Istanbul, Uturuki mnamo tarehe Pili Oktoba ili kukabidhi hati zake kwa ajili ya mpango wake wa kufunga ndoa.