RIP Credo Celestine - IFM lecturer

luckman

JF-Expert Member
Oct 11, 2010
1,211
371
Kwa wale waliosoma IFM miaka ya kuanzia 2000 watakuwa wanamfahamu sana mr credo celestine, ameaga dunia ghafla baada ya kupanda pressure na kuanguka, alipofikishwa hospitali muhimbili madaktari walisema damu imevujia ndani kwanye ubongo, alipofanyiwa operation ya kufyonza hiyo damu madaktari walisema imefanyika successful, but very unfortunately hakutoka icu hadi mauti yalipomfika jumapili iliyopita na jumanne tulimsafirisha kwenda sengerema kwa mazishi ambayo yamefanyika alhamisi, ameacha mke na watoto watatu! binafsi namkumbuka, pamoja na kuwa ndugu yangu alikuwa rafiki yangu sana! credo ni taa iliyozimika ghafla! bwana ametoa na bwana ametwaa, jina lake libarikiwe
,
tuungane na familia kuwapa pole katika kipindi hiki kigumu sana.
 
mi nilijua maneno ya watu bwana RIP Credo sio pombe mama maana huyu jamaa alikuwa pombe mpaka class..
 
RIP Mwalimu wangu mpendwa. Ninauenzi mchango wako kipindi chote cha maisha yangu ya kusoma IFM
 
RIP Credo Celestine nakumbuka ulivyokuwa unatupiga msasa Statistics na namba kwa ujumla nikiwa 1st year 1997/1998.Sidhani kama kuna mtu aliyekuwa anamchukia huyu marehemu kwa namna alivyokuwa mpole na asiyependa makuu. Wala hakuwa anatunga mitihani ya kukomoa hata wasiokuwa wataalamu wa hesabu walikuwa wanachomoka kwenye mtihani wake.Kiufupi alikuwa aina sahihi ya waalimu katika higher learning institutions.
 
Hivi nyie mnazijua sifa za mtu kuwa Lecturer au mnaosha vinywa tu hapa? Mtu ana masters eti Lecturer.
 
Hivi nyie mnazijua sifa za mtu kuwa Lecturer au mnaosha vinywa tu hapa? Mtu ana masters eti Lecturer.
<br />
<br />
tena sio lecturer ni senior lecturer kujua kwanini kapewa hicho cheo kamuulize Prof G D Mjema sawa
 
RIP CREDO tusianze kmhukumu akiwa mfu kama ulijua ni mgonjwa na ataondoka na wengi ungemsema mapema tukamsuta.
 
Hivi nyie mnazijua sifa za mtu kuwa Lecturer au mnaosha vinywa tu hapa? Mtu ana masters eti Lecturer.

Hebu tuambie nani anastahili kuitwa Lecturer? nimefundishwa na mwalimu mwenye Masters -Financial Analysis katika masters level ambaye alikuwa anakuwa refered kama Lecturer sasa sijui nayo ilikuwa haiko sawa! Anyway IFM wakati wetu kulikuwa Senior Lecturer ambao walikuwa wana Masters tu cha muhimu ilikuwa kama wanafundisha na ku-fanya research tu na publications. Sasa sijui kama una tatizo na hilo pia!
 
watu bwana marehemu alishatangulia kwa amani huko alipoenda nyie mnaanza kumchambua kweli wanadamu hatuwezekaniki
 
Hebu tuambie nani anastahili kuitwa Lecturer? nimefundishwa na mwalimu mwenye Masters -Financial Analysis katika masters level ambaye alikuwa anakuwa refered kama Lecturer sasa sijui nayo ilikuwa haiko sawa! Anyway IFM wakati wetu kulikuwa Senior Lecturer ambao walikuwa wana Masters tu cha muhimu ilikuwa kama wanafundisha na ku-fanya research tu na publications. Sasa sijui kama una tatizo na hilo pia!
hata toutorial assistants mnawaita lectuturer.
Google uone lecturer ana sifa sipi. Mwenye masters anaweza kuwa promoted kuwa lecturer based on work experience kwa maana ya muda aliokaa kazini akifundisha pamoja na maandiko aliyoandika. Otherwise ni assisstant lecturer tu
 
hata toutorial assistants mnawaita lectuturer.
Google uone lecturer ana sifa sipi. Mwenye masters anaweza kuwa promoted kuwa lecturer based on work experience kwa maana ya muda aliokaa kazini akifundisha pamoja na maandiko aliyoandika. Otherwise ni assisstant lecturer tu

Nimekuuliza wewe badala ya kujibu unataka ni-google! kwani nimekwambia sijui kama kuna search engine? otherwise nafikiri umeeleweka na pia marehemu inawezekana alikuwa ana-qualify kuitwa Lecturer kwa vigezo hivyo hivyo ulivyovisema!
 
Hivi nyie mnazijua sifa za mtu kuwa Lecturer au mnaosha vinywa tu hapa? Mtu ana masters eti Lecturer.

Wewe unazijua??. Ukweli ni kwamba mtu anaweza kuwa Lecturer akiwa na masters, depending on 1. The number of years he has involved himself in teaching activities, 2. The number of publications and the associated scores, 3. The number of books or chapters in a book written etc.
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom