Ridhiwani Kikwete na Nukuu za Hayati Mwl. Nyerere

zubedayo_mchuzi

JF-Expert Member
Sep 2, 2011
4,873
1,216
Ridhiwani Kikwete "Makosa yetu mengine hutokana na woga; woga unaotuzuia kumlaumu mkubwa japo tunajua kuwa kakosa, au kumtetea mdogo anayelaumiwa na wakubwa japo tunajua kuwa hana makosa.

Na msingi wa woga ni ubinafsi. Pengine huwa tunaogopa sisi wenyewe kulaumiwa au kupata hasara fulani. Pengine twaweza kuwa hatuna cheo chochote ambacho tunaogopa kupoteza; pengine huwa hatuna wala tamaa yoyote ya kupata cheo fulani. Lakini woga unaweza kutokana na tamaa ya kila binadamu kupendwa na binadamu wenzake.

Sisi wote tunayo tamaa hii, au sivyo tusingekuwa binadamu. Woga huu huweza ukamfanya mtu kuvumilia maovu, hasa kama maovu yale yanatendwa na walio wengi kwa walio wachache, au yanatendwa na wakubwa kwa wadogo. Kwa kuogopa kuwaudhi wengi tunawaacha watende makosa bila kuwasahihisha, wasije wakatuchukia. Huu ni ubinafsi mbaya sana." Julius Nyerere, Tujisahihishe, 1962.

SOURCE ;Ridhiwani Kikwete | Facebook
 
sasa si aende akaongee na mshua maneno hayo kuliko kuja kututamkia huku wakati anaelewa ni nani wa kumueleza hizo cheche zeke....rubbish kabisha!!
 
utumbo wake hapa..babake ndo matapioshi matupu kwa nini asimwambie wakiwa wanajadili mipango yao ya hoteli yao pale morogoro stend au akiwa anawasilisha mauzo ya wiki ya DAR LIVE...
 
tatizo la huyu kijana, akiona watu wanachangia negatively hiyo post yake, next week utamsikia akikana hiyo page kuwa kuna watu wanatumia jina lake
 
Haya mafesibuku siyaamini kabisa..........imagine sasa hivi Balali yuko huko wakati ni marehemu.....anaweza asiwe Riz1 wa kweli huyu
 
Haya mafesibuku siyaamini kabisa..........imagine sasa hivi Balali yuko huko wakati ni marehemu.....anaweza asiwe Riz1 wa kweli huyu

ngoja tuvute subira kidogo utasikia tu mara acaunt ya riz 1 ya fb wame ihack .Kama ilivyo kuwa kwenye account za twetter na fb za mama yake.
 
Ridhiwani Kikwete "Makosa yetu mengine hutokana na woga; woga unaotuzuia kumlaumu mkubwa japo tunajua kuwa kakosa, au kumtetea mdogo anayelaumiwa na wakubwa japo tunajua kuwa hana makosa.

Na msingi wa woga ni ubinafsi. Pengine huwa tunaogopa sisi wenyewe kulaumiwa au kupata hasara fulani. Pengine twaweza kuwa hatuna cheo chochote ambacho tunaogopa kupoteza; pengine huwa hatuna wala tamaa yoyote ya kupata cheo fulani. Lakini woga unaweza kutokana na tamaa ya kila binadamu kupendwa na binadamu wenzake.

Sisi wote tunayo tamaa hii, au sivyo tusingekuwa binadamu. Woga huu huweza ukamfanya mtu kuvumilia maovu, hasa kama maovu yale yanatendwa na walio wengi kwa walio wachache, au yanatendwa na wakubwa kwa wadogo. Kwa kuogopa kuwaudhi wengi tunawaacha watende makosa bila kuwasahihisha, wasije wakatuchukia. Huu ni ubinafsi mbaya sana." Julius Nyerere, Tujisahihishe, 1962.

SOURCE ;Ridhiwani Kikwete | Facebook
kawaida sana......
 
All in all! hiyo quotation imenisisimua sana! ina ukweli mtupu haijalishi nani kaitupia kwenye hiyo account yake!
 
Back
Top Bottom