BWANKU M BWANKU
JF-Expert Member
- Jan 12, 2019
- 328
- 414
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Ridhiwani Kikwete Jana Alhamisi Machi 24, 2022 alikuwa Mgeni rasmi kwenye Ufunguzi wa maonyesho makubwa ya Viwanda vinavyozalisha Nishati kwa kutumia Teknolojia mbalimbali.
Ufunguzi wa maonyesho hayo yaliyoandaliwa na Kampuni ya Expo Group Limited yamefanyika kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee Jijini Dar es Salaam na yanalenga kuwasaidia Wananchi kutumia bidhaa mbalimbali zilizopo kwenye maeneo yao kuzalisha Nishati.
Naibu Waziri Kikwete amesema maonyesho hayo ni mazuri kwa Taifa hasa kwa Vijana na yatasaidia sana kujifunza kutumia sekta mbalimbali kama za madini, gesi, nishati mbalimbali na kuzitumia kutengeneza ajira na kupata kazi.
"Nimepewa heshima ya kufungua maonyesho ya BuildExpo2022 inayofanyika Diamond Jubilee, Dar es Salaam Tanzania. Nimetumia nafasi hiyo kuwakaribisha wana maonyesho Tanzania na kuwaeleza kwa kina utayari wa Rais wetu Mhe. Samia Suluhu Hassan kushirikiana nao kukuza Uchumi wa Nchi na kuimarisha Mashirikiano baina ya Nchi zetu. Nchi zaidi ya 24 zimeshiriki. Alisema Mhe. Ridhiwani Kikwete.
#SSH #MamaAnapigaMwingi
Ufunguzi wa maonyesho hayo yaliyoandaliwa na Kampuni ya Expo Group Limited yamefanyika kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee Jijini Dar es Salaam na yanalenga kuwasaidia Wananchi kutumia bidhaa mbalimbali zilizopo kwenye maeneo yao kuzalisha Nishati.
Naibu Waziri Kikwete amesema maonyesho hayo ni mazuri kwa Taifa hasa kwa Vijana na yatasaidia sana kujifunza kutumia sekta mbalimbali kama za madini, gesi, nishati mbalimbali na kuzitumia kutengeneza ajira na kupata kazi.
"Nimepewa heshima ya kufungua maonyesho ya BuildExpo2022 inayofanyika Diamond Jubilee, Dar es Salaam Tanzania. Nimetumia nafasi hiyo kuwakaribisha wana maonyesho Tanzania na kuwaeleza kwa kina utayari wa Rais wetu Mhe. Samia Suluhu Hassan kushirikiana nao kukuza Uchumi wa Nchi na kuimarisha Mashirikiano baina ya Nchi zetu. Nchi zaidi ya 24 zimeshiriki. Alisema Mhe. Ridhiwani Kikwete.
#SSH #MamaAnapigaMwingi