Na Ezekiel Kamwaga
Imechapwa 26 May 2010
ALIPOUAWA mtawala wa Urusi, Nicholaus II, 17 Julai 1918, mauti hayakumfika yeye peke yake. Aliuwawa na watoto wake watano; Alexei, Olga, Maria, Tatiana na Anastasia.
Hata mkewe wake, Alexandra, daktari wake, nao waliuawa pamoja naye. Nicholaus II aliuwawa kwa kupigwa risasi na wale waliojipachika jina Bolshevik wapinzani wa utawala wa kifalme wa Urusi.
Hasira ya wananchi wa Urusi ilikuwa kwa ukoo wote wa kifalme. Kama Wakomunisti wale wangepata nafasi wangetekeza ukoo mzima wa mtawala huyo.
Baada ya Bolshevik kumiminia risasi Nicholaus na familia yake, mabinti wale wanne walikuwa hawajakata roho. Kwa sababu kila mmoja alikuwa amevaa vidani na nguo zilizodariziwa kwa almasi kiasi kwamba risasi hazikuweza kupenya milini mwao.
Walichokifanya wauaji, ni kuwasogelea karibu mabinti hao Olga, Maria, Tatiana na Anastasia kisha kuwaua kwa kuwakata vichwa kwa kutumia mapanga na mashoka!
Ni ukatili ambao ni vigumu kuueleza kwa binadamu wa kawaida. Na hii ndiyo hatari ambayo naiona kwa wanasiasa ambao wanajitahidi kuingiza familia zao kwenye ulingo wa siasa.
Kinachotokea ni kwa jamii nzima kuichukia familia nzima badala ya mtu mmoja.
Kwanza niseme mapema kwamba mimi si miongoni mwa watu wanaopinga watoto wa wanasiasa kuingia katika siasa hususani katika mwaka wa uchaguzi kama huu.
Roho yangu haisononeki kabisa kwamba Amani Abeid Karume, amekuwa rais wa Zanzibar nafasi ambayo baba yake, Abeid Amani Karume aliishikilia kwa miaka nane.
Wala sitakuwa na shida iwapo, Balozi Ali Abeid Karume na Dk. Hussein Mwinyi watakuja kuwa marais ama wa Zanzibar au Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Aidha, siwezi kuwa na kinyongo iwapo, January Makamba, Kippi Warioba, Ridhiwani Kikwete, Nape Nnauye, John Mongella, Dk. Mwele Malecela, Makongoro Nyerere, Mohammed Moyo, Vita Kawawa na wengine, watabahatika kupata utukufu ambao wazazi wao walikuwa nao huko nyuma.
Kusema kwamba hawafai kwa sababu tu, baba zao walikuwa wanasiasa ni kuwaonea. Hii ni sawa na kupingana na asili. Kila mmoja anastahili kujiandikia historia yake.
Tatizo langu kubwa lililopo kwa viongozi wetu, ni kule kutaka kuchomeka watoto wao, ambao hawana uwezo wa kuongoza. Kwamba mtu anapanda vyeo kwa sababu ya wadhifa wa baba yake.
Kama Amani Karume ana sifa na uwezo wa kuwa rais, hakuna sababu ya kutompa nafasi. Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alisema, Tusichague rais kwa kutokana na kabila lake, dini yake au ukoo anaotoka.
Lakini pia hatuwezi kukataa kuchagua kiongozi kwa kuwa tayari baba yake alishika nafasi hiyo.
Kwenye fani nyingine, kwa mfano kwenye mpira, mtoto atapata mafanikio tu iwapo atakuwa na uwezo. Kwamba Ngassa anaweza kucheza Yanga kwa sababu alikuwa na uwezo.
Kama angekuwa hajui kucheza mpira kama mimi, asingepangwa Yanga hata kama baba yake angekuwa Imani Madega. Ndiyo maana watoto wa Pele hawapangwi kwenye timu ya Brazil. Kama mtu hana uwezo, hawezi kupangwa.
Kwenye siasa, mtu ambaye alikuwa hafahamiki wala kujulikana, ghafla anapanda vyeo na kuwa na ushawishi mkubwa mara mzazi wake au ndugu yake anapokuwa na madaraka ! Hapa ndipo kwenye matatizo.
Nicholas aliuawa kwa sababu hakuwa kiongozi mzuri. Alifanikiwa tu kuwa mtawala wa Urusi kwa sababu baba yake, Alexander III alikuwa Mfalme na alipokufa yeye akamrithi.
Katika kitabu cha Guns of August, mwanahistoria Barbara Tuchman aliandika kwamba mfalme Alexander III alikuwa hajampa mafunzo yoyote mwanaye (Nicholaus) kuhusu mambo ya utawala.
Alikuwa amepanga kumpa mwanaye huyo mafunzo rasmi atakapokuwa ametimiza umri wa miaka 30 lakini kwa bahati mbaya mfalme akafariki wakati mtoto ana umri wa miaka 26.
Kwa hiyo, kwa sababu tu Nicholaus alikuwa mtoto wa mfalme, akapewa fursa ya kurithi bila ya kujua kitu kuhusu utawala.
Katika kitabu hicho, Tuchman anaeleza tukio moja kumhusu Nicholaus, kwamba wakati alipopewa taarifa za awali kuhusu mashambulizi yaliyokuwa yakifanywa na Wakomunisti hao, aliisoma taarifa hiyo na kisha kuiweka mfukoni kabla ya kuendelea kucheza tennis. Hakufanya lolote!
Ni vema, katika mwaka huu wa uchaguzi, wanasiasa wetu wakawa makini sana katika namna ambavyo wanahusisha familia zao na mambo ya siasa.
Kama mtu alikuwa si lolote wala si chochote kabla baba au mama hajawa rais au waziri mkuu, anakuaje kila kitu wakati baba anapokuwa mkubwa?
Uongozi unahusu ugawaji na matumizi ya rasilimali za taifa. Ni vema, kwa kiongozi na familia yake, akafahamu wananchi wanapomka wanakuwa na uchungu sana na matumizi ya rasilimali zao.
Kama kiongozi anaona mkewe au mwanaye ana sifa na uwezo wa kuwa kiongozi, ni vema akamruhusu ili asilinyime taifa uongozi murua.
Lakini, atakuwa anafanya jambo la hatari sana kama ataruhusu watu wake wa karibu kutumia cheo na ushawishi wake kujiingiza kwenye mambo ya nchi.
Hapa atakuwa anaiingiza familia yake katika matatizo makubwa bila ya kufahamu. Wakati utakapofika wa yeye kuondoka madarakani, afahamu hataondoka peke yake, ataondoka na familia yake.
Na kama walifanya vibaya, afahamu kwamba ataandamwa, yeye na familia yake, kwa kiwango ambacho kuna kipindi hakuna mtu wa familia huyo atapenda kutumia ubini wao kujitambulisha.
Kabla kiongozi hujamruhusu mwanao au mkeo kuingia kwenye siasa wakati wewe ni mtawala, ni vizuri ujiulize ni kwa nini hawakuingia kwenye siasa kabla hujawa kiongozi.
Kwamba inakuaje ghafla wanakuwa na sifa za uongozi baada ya wewe kuwa madarakani? Mbunge wa Njombe, Dk. Ndembela Ngunangwa, alikemea hilo kwa kuuliza: Walikwina walikuwa wapi - kabla ya wewe kuwa madarakani?
Kimsingi hili ni jambo rahisi sana kulifanya. Hakuna sababu ya viongozi wetu kuingiza familia zao kwenye matatizo. Makosa yao yanaweza kusamehewa na kizazi cha jana na leo.
Nani ajuaye kizazi cha kesho kitakuwa na maamuzi gani?
Source:
Mwanahalisi.
Mtazamo: Waungwana waheshimiwa wa kesho kabla hamjakimbilia zaidi mjiulize maswali yafuatayo:-
a. Baba au Mama yako mzazi aliyekuwa kiongozi alifanya yepi mema kwa watanzania???
b. Je mimi (mtoto wa muheshimiwa) ninaweza kuyaendeleza yale mazuri???
c. Je yale mabaya ya mzazi vipi yanaweza kutibiwa? na mie nitaweza kuyatibu????
d. Ni mifano gani ambapo wananchi walipochoka wameamua kuchukua sheria mikononi mwao kwasababu ya kurithishana???
Kumbuka sio kila anayezaliwa katika ukoo lazima arithi alichokuwa nacho mzazi kwani elimu, uongozi ni vitu mungu humbariki mtu na sio mtu kuzaliwa nacho!!!!
Imechapwa 26 May 2010
ALIPOUAWA mtawala wa Urusi, Nicholaus II, 17 Julai 1918, mauti hayakumfika yeye peke yake. Aliuwawa na watoto wake watano; Alexei, Olga, Maria, Tatiana na Anastasia.
Hata mkewe wake, Alexandra, daktari wake, nao waliuawa pamoja naye. Nicholaus II aliuwawa kwa kupigwa risasi na wale waliojipachika jina Bolshevik wapinzani wa utawala wa kifalme wa Urusi.
Hasira ya wananchi wa Urusi ilikuwa kwa ukoo wote wa kifalme. Kama Wakomunisti wale wangepata nafasi wangetekeza ukoo mzima wa mtawala huyo.
Baada ya Bolshevik kumiminia risasi Nicholaus na familia yake, mabinti wale wanne walikuwa hawajakata roho. Kwa sababu kila mmoja alikuwa amevaa vidani na nguo zilizodariziwa kwa almasi kiasi kwamba risasi hazikuweza kupenya milini mwao.
Walichokifanya wauaji, ni kuwasogelea karibu mabinti hao Olga, Maria, Tatiana na Anastasia kisha kuwaua kwa kuwakata vichwa kwa kutumia mapanga na mashoka!
Ni ukatili ambao ni vigumu kuueleza kwa binadamu wa kawaida. Na hii ndiyo hatari ambayo naiona kwa wanasiasa ambao wanajitahidi kuingiza familia zao kwenye ulingo wa siasa.
Kinachotokea ni kwa jamii nzima kuichukia familia nzima badala ya mtu mmoja.
Kwanza niseme mapema kwamba mimi si miongoni mwa watu wanaopinga watoto wa wanasiasa kuingia katika siasa hususani katika mwaka wa uchaguzi kama huu.
Roho yangu haisononeki kabisa kwamba Amani Abeid Karume, amekuwa rais wa Zanzibar nafasi ambayo baba yake, Abeid Amani Karume aliishikilia kwa miaka nane.
Wala sitakuwa na shida iwapo, Balozi Ali Abeid Karume na Dk. Hussein Mwinyi watakuja kuwa marais ama wa Zanzibar au Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Aidha, siwezi kuwa na kinyongo iwapo, January Makamba, Kippi Warioba, Ridhiwani Kikwete, Nape Nnauye, John Mongella, Dk. Mwele Malecela, Makongoro Nyerere, Mohammed Moyo, Vita Kawawa na wengine, watabahatika kupata utukufu ambao wazazi wao walikuwa nao huko nyuma.
Kusema kwamba hawafai kwa sababu tu, baba zao walikuwa wanasiasa ni kuwaonea. Hii ni sawa na kupingana na asili. Kila mmoja anastahili kujiandikia historia yake.
Tatizo langu kubwa lililopo kwa viongozi wetu, ni kule kutaka kuchomeka watoto wao, ambao hawana uwezo wa kuongoza. Kwamba mtu anapanda vyeo kwa sababu ya wadhifa wa baba yake.
Kama Amani Karume ana sifa na uwezo wa kuwa rais, hakuna sababu ya kutompa nafasi. Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alisema, Tusichague rais kwa kutokana na kabila lake, dini yake au ukoo anaotoka.
Lakini pia hatuwezi kukataa kuchagua kiongozi kwa kuwa tayari baba yake alishika nafasi hiyo.
Kwenye fani nyingine, kwa mfano kwenye mpira, mtoto atapata mafanikio tu iwapo atakuwa na uwezo. Kwamba Ngassa anaweza kucheza Yanga kwa sababu alikuwa na uwezo.
Kama angekuwa hajui kucheza mpira kama mimi, asingepangwa Yanga hata kama baba yake angekuwa Imani Madega. Ndiyo maana watoto wa Pele hawapangwi kwenye timu ya Brazil. Kama mtu hana uwezo, hawezi kupangwa.
Kwenye siasa, mtu ambaye alikuwa hafahamiki wala kujulikana, ghafla anapanda vyeo na kuwa na ushawishi mkubwa mara mzazi wake au ndugu yake anapokuwa na madaraka ! Hapa ndipo kwenye matatizo.
Nicholas aliuawa kwa sababu hakuwa kiongozi mzuri. Alifanikiwa tu kuwa mtawala wa Urusi kwa sababu baba yake, Alexander III alikuwa Mfalme na alipokufa yeye akamrithi.
Katika kitabu cha Guns of August, mwanahistoria Barbara Tuchman aliandika kwamba mfalme Alexander III alikuwa hajampa mafunzo yoyote mwanaye (Nicholaus) kuhusu mambo ya utawala.
Alikuwa amepanga kumpa mwanaye huyo mafunzo rasmi atakapokuwa ametimiza umri wa miaka 30 lakini kwa bahati mbaya mfalme akafariki wakati mtoto ana umri wa miaka 26.
Kwa hiyo, kwa sababu tu Nicholaus alikuwa mtoto wa mfalme, akapewa fursa ya kurithi bila ya kujua kitu kuhusu utawala.
Katika kitabu hicho, Tuchman anaeleza tukio moja kumhusu Nicholaus, kwamba wakati alipopewa taarifa za awali kuhusu mashambulizi yaliyokuwa yakifanywa na Wakomunisti hao, aliisoma taarifa hiyo na kisha kuiweka mfukoni kabla ya kuendelea kucheza tennis. Hakufanya lolote!
Ni vema, katika mwaka huu wa uchaguzi, wanasiasa wetu wakawa makini sana katika namna ambavyo wanahusisha familia zao na mambo ya siasa.
Kama mtu alikuwa si lolote wala si chochote kabla baba au mama hajawa rais au waziri mkuu, anakuaje kila kitu wakati baba anapokuwa mkubwa?
Uongozi unahusu ugawaji na matumizi ya rasilimali za taifa. Ni vema, kwa kiongozi na familia yake, akafahamu wananchi wanapomka wanakuwa na uchungu sana na matumizi ya rasilimali zao.
Kama kiongozi anaona mkewe au mwanaye ana sifa na uwezo wa kuwa kiongozi, ni vema akamruhusu ili asilinyime taifa uongozi murua.
Lakini, atakuwa anafanya jambo la hatari sana kama ataruhusu watu wake wa karibu kutumia cheo na ushawishi wake kujiingiza kwenye mambo ya nchi.
Hapa atakuwa anaiingiza familia yake katika matatizo makubwa bila ya kufahamu. Wakati utakapofika wa yeye kuondoka madarakani, afahamu hataondoka peke yake, ataondoka na familia yake.
Na kama walifanya vibaya, afahamu kwamba ataandamwa, yeye na familia yake, kwa kiwango ambacho kuna kipindi hakuna mtu wa familia huyo atapenda kutumia ubini wao kujitambulisha.
Kabla kiongozi hujamruhusu mwanao au mkeo kuingia kwenye siasa wakati wewe ni mtawala, ni vizuri ujiulize ni kwa nini hawakuingia kwenye siasa kabla hujawa kiongozi.
Kwamba inakuaje ghafla wanakuwa na sifa za uongozi baada ya wewe kuwa madarakani? Mbunge wa Njombe, Dk. Ndembela Ngunangwa, alikemea hilo kwa kuuliza: Walikwina walikuwa wapi - kabla ya wewe kuwa madarakani?
Kimsingi hili ni jambo rahisi sana kulifanya. Hakuna sababu ya viongozi wetu kuingiza familia zao kwenye matatizo. Makosa yao yanaweza kusamehewa na kizazi cha jana na leo.
Nani ajuaye kizazi cha kesho kitakuwa na maamuzi gani?
Source:
Mwanahalisi.
Mtazamo: Waungwana waheshimiwa wa kesho kabla hamjakimbilia zaidi mjiulize maswali yafuatayo:-
a. Baba au Mama yako mzazi aliyekuwa kiongozi alifanya yepi mema kwa watanzania???
b. Je mimi (mtoto wa muheshimiwa) ninaweza kuyaendeleza yale mazuri???
c. Je yale mabaya ya mzazi vipi yanaweza kutibiwa? na mie nitaweza kuyatibu????
d. Ni mifano gani ambapo wananchi walipochoka wameamua kuchukua sheria mikononi mwao kwasababu ya kurithishana???
Kumbuka sio kila anayezaliwa katika ukoo lazima arithi alichokuwa nacho mzazi kwani elimu, uongozi ni vitu mungu humbariki mtu na sio mtu kuzaliwa nacho!!!!