Ridhiwan Kikwete: Mimi si fisadi

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,792
287,994
Ridhiwan Kikwete: Mimi si fisadi

na Charles Mullinda
Tanzania Daima~Sauti ya Watu


MTOTO mkubwa wa Rais Jakaya Kikwete, Ridhiwan Kikwete, amesema hahusiki kwa namna moja au nyingine na tuhuma za ufisadi zinazowaandama baadhi ya makada wa Chama Cha Mapinduzi na viongozi waandamizi wa serikali.

Akizungumza na Tanzania Daima Jumapili jana kupitia simu yake ya kiganjani kuhusu tuhuma ambazo zimekuwa zikielekezwa kwake katika siku za karibuni kuwa mmoja wa watu waliohojiwa na timu iliyoteuliwa na Rais Kikwete kuchunguza watuhumiwa wa wizi wa fedha za EPA pamoja na kukusanya fedha hizo, alisema hajawahi kuhojiwa na timu hiyo.

Ridhiwan alisema tuhuma zinazoelekezwa kwake sasa kuwa katika kipindi kisichozidi miaka miwili ya kuwa kazini amejilimbikizia ukwasi wa kutisha, ikiwa ni pamoja na kumiliki magari na nyumba kadhaa za kifahari, zina malengo ya kisiasa ili kumpunguza nguvu katika kampeni anazoshiriki sasa ndani ya Umoja wa Vijana wa CCM.

Alisema katika kipindi chote alichofanya kazi ya uwakili katika Kampuni ya uwakili ya IMMMA, akiba ya fedha alizonazo benki hazizidi shilingi milioni 10, jambo linalothibitisha kuwa yeye si fisadi wala hajawahi kumuibia mtu.

"Watu wanapenda sana kusemasema, lakini mimi kama nilivyosema, sipendi kusema sema, ndiyo maana niko mbali na vyombo vya habari. Mimi si fisadi, simwibii mtu, nafanya mambo yangu mwenyewe.

"Ninatambua ninachokifanya na nina malengo. Ninachohangaika nacho kwa sasa ni kijishamba changu nilichoachiwa na babu yangu, nataka nikope fedha nikiimarishe. Sina fedha jamani, akaunti yangu haina hata milioni 10. Lakini nayajua madhara ya kuwa mwanasiasa ni kama haya, kuzushiwa. Sitasema kitu na hutanisikia nikisema kitu kuhusu hili," alisema Ridhiwan kwa sauti ya masikitiko.

Ridhiwan ametoa kauli hii ikiwa ni siku chache baada ya kuibuka kwa minong'ono kuwa aliitwa na kuhojiwa na timu ya rais inayochunguza kashfa ya EPA.

Katika minong'ono hiyo, Ridhiwan anatajwa kama mmoja wa watu waliofaidika na fedha zilizochukuliwa Benki Kuu ya Tanzania katika akaunti ya EPA na kwamba katika kipindi kifupi alichofanya kazi amejikusanyia ukwasi wa kutisha, ambao haulingani na umri wake katika ajira.

Taarifa hizo zilieleza kuwa Ridhiwan ambaye hajatimiza hata miaka miwili katika ajira yake, anamiliki mamilioni ya shilingi katika benki mbalimbali nchini pamoja na magari kadhaa ya kifahari, na nyumba za kifahari, ambazo hazilingani na kipato chake, madai ambayo yeye ameyakanusha na kuyahusisha na mapambano ya kisiasa ndani ya chama katika kipindi hiki cha uchaguzi wa viongozi wa UVCCM.

Hata hivyo, Ridhiwan katika kukanusha tuhuma hizo, alisema zinatokana na vita ya kuwania madaraka ndani ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), ambayo imeanza kushika kasi mpya, baada ya kujitokeza kwake kumuunga mkono mmoja wa marafiki zake anayegombea uongozi ndani ya umoja huo.

Ridhiwan alisema uchaguzi huo umembana kwa sababu anatumia muda mwingi kumsaidia rafiki yake aliyejitosa kugombea, kwa kuwa anapata upinzani mkali kutoka katika kambi nyingine ndani ya umoja huo.

Bila kumtaja jina rafiki yake huyo wala nafasi ya uongozi anayowania, Ridhiwan alisema baadhi ya wagombea wanaopambana na rafiki yake wameanza kumzushia tuhuma ili kumtisha aache kumuunga mkono rafiki yake.

"Sipendi kuzungumza na ‘media' (vyombo vya habari), kwa sababu tuko katika mapambano ya uchaguzi mkuu wa UVCCM. Ninapambana chini kwa chini kwa sababu ndivyo zilivyo siasa zetu.

"Kinachonishangaza, watu wananiangalia tofauti kabisa kama vile mimi sipaswi kushiriki katika kampeni au siasa, mimi sigombei, anayegombea ni rafiki yangu na kweli ninamuunga mkono. Ninatumia muda mwingi sana kwa sababu kambi tunayopambana nayo inatoa upinzani mkali kwa rafiki yangu," alisema Ridhiwan.

Akizungumza kuhusu uamuzi wake wa kumuunga mkono rafiki yake huyo alisema, unatokana na kuwa karibu naye kwa muda mrefu tangu wakiwa wanafunzi, na kuwataka wanaodhani kwamba alijiunga na kambi isiyostahili, wafahamu kuwa anamfahamu mgombea huyo tangu wakiwa watoto, hivyo anaamini anaweza kuwa kiongozi wa juu wa umoja huo.
 
Ridhiwan ametoa kauli hii ikiwa ni siku chache baada ya kuibuka kwa minong’ono kuwa aliitwa na kuhojiwa na timu ya rais inayochunguza kashfa ya EPA
.

Kama ni kweli this is not a bad move... unaitwa unajielezaa na unajisafisha/au? etc... anybody can be called.... its not bad... we need this be done even to Mkapa au mtu mwingine yeyote..

Katika minong’ono hiyo, Ridhiwan anatajwa kama mmoja wa watu waliofaidika na fedha zilizochukuliwa Benki Kuu ya Tanzania katika akaunti ya EPA na kwamba katika kipindi kifupi alichofanya kazi amejikusanyia ukwasi wa kutisha, ambao haulingani na umri wake katika ajira.

This too, is also very good..ni minogono..or whatever...tunahitaji majibu..na hililifanyike kwa kila mtuhumiwa pia..na wananchi tuelezwe finaly results. Hili litamuweka mtu mahali sahihi katika nafasi na picha nzima ya uongozi.
 
wewe kijana ridhwan nasikia ni mtoto wa mzee, elewa kuwa hapa tuko kwenye utaifa wetu. na katika utaifa hakuna cha kikwete au mrisho. kama wewe syo fiSADI KARIBU. kama unafikiri babako ni rais na KUWA ATAKUWA NA NA NAFASI FULANI SAHAU. TUTAKUTANA HUKOOO TUNDURU ALUTA KONTINUA. MAPAMBANO NDO BADO , USITEGEMEE UBWECHE.
 
"Watu wanapenda sana kusemasema, lakini mimi kama nilivyosema, sipendi kusema sema, ndiyo maana niko mbali na vyombo vya habari."

Like father like son.
 
Mshahara anapata ngapi na amefanya kazi muda gani tufanye mahesabu ya hizo million chini kidogo ya kumi
 
Oh Shit!!

I wish angezitaja hizo mali zake (Shs milioni kumi na shamba) chini ya kiapo. Ingekuwa ni reference nzuri sana ya kuitumia siku za mbeleni.

But still tumeshapata leads kuhusiana na mali anazodai anazi-own kwa sasa (By June 1st 2008). He can still be quoted in the future kwa kutumia maneno yake haya.
 
“Sipendi kuzungumza na ‘media’ (vyombo vya habari), kwa sababu tuko katika mapambano ya uchaguzi mkuu wa UVCCM. Ninapambana chini kwa chini kwa sababu ndivyo zilivyo siasa zetu. "

Alikuwa anazungumza na nani tena?

Ngoja nisome tena....Mhhh


Hivi mapambano ya kifisadi yanaweza kuwa yapo chini kwa chini? Kajiswali tu

Hii hapa Nyani aliyekufa kuwepo sijui atasemaje..."kwa sababu ndivyo zilivyo siasa zetu. "

Tehe hehehe...
 
O kumbe neno ujamaa na kujitegemea halijafutwa kwenye katiba. Nimesikia eti kuna sheria inayokataza watanzania kuweka pesa nje.. Pia nadhani mke na watoto wa rais wanatakiwa watambuliwe kikatiba.
 
Muungwana anamuandaa mwanaye aje kushika nchi miaka ya baadae. na kwa uzuzu wa makada wataingia kazini ili hilo liwezekane....
 
Hapa kijana anajikanyaga hapendi kuongea na media hapo anafanya nini! ok na kaongea leo karopoka ana < mil10 na shamba ,kama alivyosema mjumbe aliyetangulia we keep this for future reference.
Vinginevyo ana haki ya kushiriki mambo ya chama chake kama watu wengine kuhusu influence yake kama mtoto wa m/kiti wa chama na rais watajuana wenye chama.
 
Hapa kijana anajikanyaga hapendi kuongea na media hapo anafanya nini! ok na kaongea leo karopoka ana < mil10 na shamba ,kama alivyosema mjumbe aliyetangulia we keep this for future reference.
Vinginevyo ana haki ya kushiriki mambo ya chama chake kama watu wengine kuhusu influence yake kama mtoto wa m/kiti wa chama na rais watajuana wenye chama.

kama kaulizwa swali basi ni mapenzi yake ajibu au asijibu ! na kuhusu kutopenda media hiyo choice ya mtu binafsi hasa unapokuwa kwenye lime light, kama dogo anashine jamani sio lazima awe kwenye media, alichokosea dogo ni nini ? au ndo kila kitu anachoongea mtu basi hakifai ?
 
Kazo bado ipoo....na ni mbichi kabisa ngoja tuzidi kuomba subira na muda utajieleza na kubaini mengi mazuri sana kwa ajili ya mustakabali ....wa nchi yetu....
 
Lakini wana JF naskia huyu kijana anatembelea VX sasa ni ya serikali au ya kwake?kama yake gharama yake inazidi hizo 10mill.na ananyumba huko bagamoyo mbona hajasema???Ngoja tumsubili.
 
Waandishi wa habari wa Tanzania ni wavivu sana kufanya homework zao, yani wako too easy kwa hawa public figure. I am not saying kwamba Ridhiwani ana mahusiano na EPA, sema muandishi hakumtwanga maswali muhimu.

Swali la kwanza, Jee ni kweli ulikuwa na enough credential za kuajiriwa na IMMA?

Jee can you be specific kuzitaja hizo qualifications? Jee una uhusiano gani kati yako na Masha?

Jee ni kweli position uliyopata ni kutokana na political influance na sio academic influance?

Jee nini lengo la wewe kuingia kwenye UVCCM? Jee what is your opinion concern CCM party and Tanzania economic?

Jee what changes you thing CCM need to emphasize inorder to boost Tanzanian life standard?

What are the failure of CCM between 2005 to 2008?

What need to be done?

Honest huyu mtoto ni empty suit, yaani ni mweupe kabisa. OOoooohh mungu hawa watoto some of these days watakuja kuchukua position, huyu kijana ni bendera kabisa...... Bado natamani sana kuona kazi zake, i wish
 
Na kwa kuwa ameshasema kuwa hapendi kuzungumza na media, hapo walipompata ndipo walitakiwa kukandamiza kibagamoyo mpaka ajibu maswali yote.

Lakini labda ulikuwa ni mpango maalum wa kumsafisha maana limeongelewa suala la yeye kukanusha tu.
 
Lakini wana JF naskia huyu kijana anatembelea VX sasa ni ya serikali au ya kwake?kama yake gharama yake inazidi hizo 10mill.na ananyumba huko bagamoyo mbona hajasema???Ngoja tumsubili.

Kama ni kweli anazingumzia ana pesa Bank isiyofikia hata 10Mil, ni kiwango kidogo sana hicho wala hapaswi kulaumiwa kwa lolote.

Mambo mengine kama shamba, nyumba,kutembelea VX ni kitu cha kawaida, linaweza kuwa gari la nyumbani huyu ni mtoto wa rais ana masilahi yake serikalini kupitia baba yake. Na pia anafanya kazi nadhani wote tunaofanya kazi tunajua zile njia zetu za tik tak! tik tak! inamaana nazo utautangazia Umma? Tusidanganyane hakuna hata mmoja wetu aliiyendelea bila kucheza makato-style! kazini.

Hata sisi wenyewe wana JF vitu hivi tunavyo shamba, nyumba, gari na pengine hata Akiba ya 50Mil. sasa inamaana tuhojiwe tumevipataje?

Mimi nadhani kama kitu kimekuwa na utata hicho ndicho tukijadili ilikuweka mambo sawa, lakini si'kwa kufuatilia vitu vidogo-vidogo vya kibinafsi hatutakuwa kwenye nia njema ya kurekebisha tabia, bali majungu na kuchimbuana.

Simfahamu Ridhiwan na zungumzia kiujumla....
 
Kama ni kweli anazingumzia ana pesa Bank isiyofikia hata 10Mil, ni kiwango kidogo sana hicho wala hapaswi kulaumiwa kwa lolote.

Mambo mengine kama shamba, nyumba,kutembelea VX ni kitu cha kawaida, linaweza kuwa gari la nyumbani huyu ni mtoto wa rais ana masilahi yake serikalini kupitia baba yake. Na pia anafanya kazi nadhani wote tunaofanya kazi tunajua zile njia zetu za tik tak! tik tak! inamaana nazo utautangazia Umma? Tusidanganyane hakuna hata mmoja wetu aliiyendelea bila kucheza makato-style! kazini.

Hata sisi wenyewe wana JF vitu hivi tunavyo shamba, nyumba, gari na pengine hata Akiba ya 50Mil. sasa inamaana tuhojiwe tumevipataje?

Mimi nadhani kama kitu kimekuwa na utata hicho ndicho tukijadili ilikuweka mambo sawa, lakini si'kwa kufuatilia vitu vidogo-vidogo vya kibinafsi hatutakuwa kwenye nia njema ya kurekebisha tabia, bali majungu na kuchimbuana.

Simfahamu Ridhiwan na zungumzia kiujumla....

Savimbi,

Fidel80 kauliza VX ni la serikali au la kwake? We ushasema Ridhiwani humjui, kwa hiyo swali la Fidel80 huwezi kujibu. Hayo mengine ya kusema mil 10 na shamba ni kitu cha kawaida, hayo umeyaleta wewe!

Na, unaposema wote wanaofanya kazi wanajua zile njia zao za tik tak tik tak, hapo jiongelee mwenyewe. Kuna wengine hata huo mshahara unapigwa panga ukichelewa kazini, achilia mbali kuwa na njia za tiki taka.

Na unaposema ni kitu cha kawaida kwa mtoto wa Rais kuwa na masilahi yake kupitia Baba yake unaonyesha huelewi swala zima la ufisadi. Huo ndio ufisadi wenyewe tunaouongelea.

Kwa kuangalia ulivyo ongea hapo juu, nasema wewe ni fisadi la kutupwa!
 
Kikubwa ni kwamba niliwahi kuandika hapa JF juu ya Ridhwan kumfanyia kampeni rafiki yake kwa kutumia nguvu ya Baba yake, wenye haraka na Keyboard wakaandika mambo lukuki juu ya thread yangu hiyo, anayeweza afanye search ya 'MTOTO WA KIGOGO KUMFANYIA KAMPENI RAFIKI UVCCM'.

Kibaya si yeye kushiriki kampeni ila ni lugha aliyosikika siku moja pale Rose Garden akisema eti "HAWAJUI NGUVU YANGU NITATUMIA RUNGU LANGU" wengi tulikwazwa na hilo rungu gani hilo kama ni kukata majina ya wagombea, kateni sana ila hata kama litabaki jina la mwehu mmoja wallah! Beno ataipata Fresh, mtafute mtu aitwaye Nape, muulize 2003 ilikuwaje.

Tena kwa jinsi wasivyojua kujipanga hali ya kuonekana mtoto wa kigogo anamtaka fulani kwetu sie wa kambi tofauti ni mtaji tosha wala hatutakuwa na maneno mengi ya kuomba kura kwi kwi kwi kwi !
 
The Boy Is Dangerous In Featuere The Family In East Cost Make Sure Make Followup On Him Just Gather Any Thing About Him,in Feature Will Be Of Good Use For The Family,just Amewahi Ku Baka,steal,just Gather Information,
 
loh kumbe bongo kunalipa hivyoo ehh??huyu kijana si ndo aligraduate sijui mwaka jana??!lakini now akaunti yake ina tu milioni tu kadhaa tayari sijui mshahara ni kiasi gani kwa mwezi..au ndo mshahara wake hautumiki kwa any tumizi as zaliwa hela za wananchi via uraisi wa babake???basi hata soda jamaniii??maana anataka kutuambia he saves ol his mshahara
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom