Rich Dad Poor Dad by Robert Kiyosaki (Wapi ntapata hiki kitabu kwa Hapa Dar?)

AVO28

Senior Member
Jan 4, 2018
140
240
IMG_0884.JPG


Pengine hili sio jukwaa sahihi kwa chapisho hili lakini ninhependa kufahamishwa tu kwa hapa dar wapi nnaweza pata kitabu hicho cha Robert Kiyosaki? Na pia nkipewa na bei ntashkuru sana.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vinauzwa barabarani tu mkuu . Mfano nenda pale mcity gate kama unaelekea ubungo upande ule kuna majamaa wanauza vitabu chini waulize watakuwa nacho


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Ntajaribu kuwacheki mkuu japo sina uhakika sana kama watakua nacho.


Sent using Jamii Forums mobile app
Posta City Center karibu kila meza ya muuza vitabu kipo.

Nenda Samora Avenue kutoka kwenye Sanamu kama unaenda JMall upande wako wa kulia jirani na Computronics, Copy Cat, Sapna kwa mbele kuna duka la vitabu la TPH uyavipata vibgi tu.

Nadhani bei yake ni elfu kumi na kitu. Sikumbuki.
 
Au toka hapo kwenye Sanamu hiyo Samora nenda jengo la BIMA (NIC House) unakunja kulia unaenda Wizara ya Ujenzi mkono wako wa kulia huo huo panapo tazamana na geti la ujenzi jamaa wanauza vitabu used na vipya kibao utapata.

Au hiyo hiyo Samora unatoka Habari Maelezo unaenda Sanamu hapo mbele kuna wauza vitabu karibu na Mokha City, JD Pharmacy unataka kukunja kwenda New Africa au NBC utavikuta kibao.
 
Au Posta mpya jamhuri street mbele ya Imalaseko Supermarket ukitokea Benjamin Mkapa NSSF tower kuna eauza vitabu wengi hapo nje utavikuta.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom