Review: Tanzania kutofaidi kwa madini na gesi asilia Tatizo ni nchi sio kampuni za nje

OLS

JF-Expert Member
Oct 12, 2019
419
669
Baada ya kuisoma kwa uzuri tafiti iliyofanywa na wataalamu wa mafuta na gesi Afika, Polus, A na Tycholiz, W nimekuja na review ya kile ambaco kipo kwenye kazi waliyoifanya mwaka 2019 ikiaangazia uwanja wa madini na gesi asilia nchini Tanzania huku wakionesha namna ambayo nchi inapoteza mbali na kuwa na rasilimali nyingi huku wenyewe wakiwa wameona si vyema kutumia msamiati 'Laana ya rasilimali'

Gesi asilia iligundulika nchini Tanzania mwaka 1974 na kampuni ya AGIP na uchimbaji wake ulianza rasmi mwaka 2004 ambapo Benki ya Dunia ilikadiria kuwa gesi asilia itaifaidisha Tanzania na kuwaondoa wati milioni 11 kutoka katika wimbi la umasikini mkubwa. WAkati huo madini yalikuwa yakiendelea kuchimbwa nchini na hakuna faida ya moja kwa moja iliyokuwa inaonekana kwa wananchi juu ya uchimbaji wa madini hayo.

Wasomi waliaoandika kazi hii ya David Versus Goliath: Tanzania's effeorts to stand up to foreign gas corporations hawakuweza kuweka kisa alichowahi kuandika Kamara Kusupa kuhusu Bulyankulu na visa vingine vya wananchi waliokaribu na migodi ambao walinyanyaswa na kupelekea vifo vya watu kadhaa, kama ambavyo mwaka huu kampuni moja ya uchimbaji ililazimika kuwalipa wahanga wa matukio ya kinyanyasaji

JINSI TANZANIA INAVYOLIWA
Imebainika ya kwamba katika makampuni 1700 ya uchimbaji madini na gesi asilia ni 25% tu ndio wanalipa kodi. Hata Royalties zinazolipwa ni ndogo mno ambazo ni 2.3% ya makusanyo yote ya kodi hiyo ni kwa kipindi cha 1998 hadi 2011. Kibiashara ni kawaida kwa watu kusema hawapati faida lakini wasomi hawa wameonesha kampuni tatu kubwa ambazo mmetoka kuingia nazo mkataba zilipata faida ya USB 37.2 Bilioni mwaka 2017 ambapo wakati huo makusanyo ya kodi ya Tanzania kwa ujumla yalikuwa USD bilioni 7.3. Andiko hili linaonesha ubovu wa mikataba iliyokuwepo ambapo ilifanya Tanzania ipoteza kiwango kikubwa cha fedha kama mapato

Kutokana na arguments zilizokuwepo, watu wengi huwa na lawama kwa vyombo hivyo vya nje kutokana na ukubwa wake na ni kweli ni vikubwa kwa kuwa Mitaji ya kampuni kubwa tatu ni mara 16 ya GDP ya Tanzania, hata hivyo watafiti wanasema tatizo lipo ndani ya nchi na sio nguvu ya nje ya kampuni hizo

MZIZI WA FITNA
Leo tunashuhudia mtanange kati ya Waziri wa Nishati January Makamba na Mkurugenzi wa TPDC kuhusu kiwango cha mafuta kilichopo nchini. Japo hii haikuwa sehemu ya hoja za hao wanazuoni lakini wameweka wazi kwamba kutoa wataalamu wa nishati kutoka Wizara ya Nishati kuwapeleka TPDC kuna walakini kwa kuwa TPDC ni mdogo kwa Wizara ya Nishati ambapo inaweka ulazima wa wao kuripoti wizarani na kushindwa kuchukua maamuzi ya kitaalamu yasiyoathiriwa na siasa

Suala lingine ni kuwa na uwezo finyu wa ku-negotiate kwenye mikataba ya madini, ambapo katika hili watafiti hao wamemtaja Magufuli kuwa alijitahidi kuangalia mikataba na ile iliyokuwa na viashiria vya unyonyaji vilifutiwa leseni na kufanya uchangiaji wa mapato kutoka kwenye madini kwa GDP kupanda

Watu wengi walioko madarakani wana woga, kwenye kutoa taarifa, hali inayokuwa changamoto, i.e wanazuoni wameonesha kuwa walipata shida kukutana na wataalamu kutoka Benki Kuu ya Tanzania kwa kuwa hawakutaka kuonge nao wakati wa tafiti yao

Aidha watu wamewaambia watafit kuwa 'Kukalia ofisi ya umma ni njia fupi ya kupata utajiri' bila shaka hii ni akili iliyo kwa wengi ambapo ubadhirifu umekuwa kwa vichwa vya watumishi wa umma badala ya kuweka maslahi mapana ya taifa. Hoja zao zimeandikwa vizuri na wachumi wa maendeleo Smith and Michael Todaro (2014)

NJIA SAHIHI

Njia ambayo watafiti wameshauri katika kazi yao ni kuongeza uwezo wa kupambana na rushwa, kwa kitu ambacho watafiti wamekiita 'Magufuli Effect' kwa kuongeza uwajibikaji na kupitia upya mikataba ya madini na gesi. Aidha tumeona hivi karibuni masuala mengi yaliyoanzishwa na Magufuli kuhusu madini yakikiukwa ikiwemo kuruhusu usafirishaji wa makinikia ambapo Waziri Mkuu alisema nchi inakuwa imeshapata stahiki yake ambayo kimsingi ni dhahania kwa kuwa haujui kiwango cha madini yaliyoko ili kupata kodi stahiki

Hoja zilizoko kwenye kazi hii ni hoja nzito ambazo zinaendana visuri na hoja za Action Aid kwenye kuzidisha wigo wa kupaa kodi bila kuongeza tozo, ushuru nk wakati vipo fedha nyingi ambazo tunaziacha bila kuchukua stahiki, recently ration ya Tax to GDP haizidi 14 ambapo ukusanyaji kodi ukiwa mzuri hasa kwenye sekta ya madini na gesi hesabu za Action Aid zimeonesha Tax to GDP ratio itapanda hadi kufikia 50% ambapo hatutakuwa tena na haja ya kuomba mikopo kutoka nje

Ni muhimu kuzalisha wataalamu wa kutosha wakuitazama vyema mikataba ili kujua namna bora ya kufaidika kutoka kwenye mikataba hiyo

Kaz iliyokuwa Reveiwed ni Polus, A., & Tycholiz, W. (2019). David versus Goliath: Tanzania’s Efforts to Stand Up to Foreign Gas Corporations. Africa Spectrum, 54(1), 61-72.

Signed

OEDIPUS
 
Umeandika kirefu sana solution moja tu ukitaka kumiliki uchumi wa dunia ikiwemo hayo makampuni makubwa ya Madini na gesi ni kuruhusu watanzania kununua hisa kwenye masoko ya fedha ya kimataifa ambako hayo makampuni yamesajiliwa

Watanzania tungeruhusiwa kusingekuwa na hizo kelele za ohh wanatuibia tungepata mgao kupitia faida

Wengi huuliza kwa nini watanzania wengi maskini wakati tuna Madini na gesi nk jibu rahisi hatujaiunga na uchumi wa dunia kuruhusu watanzania binafsi kununua hisa masoko ya Ulaya na Marekani. Serikali iruhusu hata Kesho Tanzania matajiri wapo na wananchi wa kawaida wapo kibao waweza nunua hisa

Soko la hisa la Tanzania hamna kitu soko maskini sana haluwezi mpa utajiri mtanzania ndio maana unakuta watu hawalichangamkii sana halikomboi mtu kwenye umaskini kama hayo masoko makubwa ya nje ya fedha

Bila kuruhusu tutaendelea kuimba nyimbo hewa kuwa hao wawekezaji wanatuibia na kupinga kisingizio visivyoisha mara mikataba mara sijui nini
 
Umeandika kirefu sana solution moja tu ukitaka kumiliki uchumi wa dunia ikiwemo hayo makampuni makubwa ya Madini na gesi ni kuruhusu watanzania kununua hisa kwenye masoko ya fedha ya kimataifa ambako hayo makampuni yamesajiliwa

Watanzania tungeruhusiwa kusingekuwa na hizo kelele za ohh wanatuibia tungepata mgao kupitia faida

Wengi huuliza kwa nini watanzania wengi maskini wakati tuna Madini na gesi nk jibu rahisi hatujaiunga na uchumi wa dunia kuruhusu watanzania binafsi kununua hisa masoko ya Ulaya na Marekani. Serikali iruhusu hata Kesho Tanzania matajiri wapo na wananchi wa kawaida wapo kibao waweza nunua hisa

Soko la hisa la Tanzania hamna kitu soko maskini sana haluwezi mpa utajiri mtanzania ndio maana unakuta watu hawalichangamkii sana halikomboi mtu kwenye umaskini kama hayo masoko makubwa ya nje ya fedha

Bila kuruhusu tutaendelea kuimba nyimbo hewa kuwa hao wawekezaji wanatuibia na kupinga kisingizio visivyoisha mara mikataba mara sijui nini
Kilichotajwa hapo ni kulipa Kodi stahiki kwa serikali wakati wewe unazungumzia 'redistribution' ya faida inayopatikana kwenye madini. Unachosema hapo ni kwamb, kwa kuwa watu wana hisa za Voda basi voda isilipe kodi, which is not practical thing.

Aidha hakuna mtanzania anayezuiwa kununua hisa kwenye masoko ya nje. Lakini kampuni za nje hazija-list shares zao DSE kwa kuwa soko la ndani halijachangamka. Au niambie sheria gani inamzuia mtu kununua hisa London Stock Exchange, New York Stock Exchange nk
 
Baada ya kuisoma kwa uzuri tafiti iliyofanywa na wataalamu wa mafuta na gesi Afika, Polus, A na Tycholiz, W nimekuja na review ya kile ambaco kipo kwenye kazi waliyoifanya mwaka 2019 ikiaangazia uwanja wa madini na gesi asilia nchini Tanzania huku wakionesha namna ambayo nchi inapoteza mbali na kuwa na rasilimali nyingi huku wenyewe wakiwa wameona si vyema kutumia msamiati 'Laana ya rasilimali'

Gesi asilia iligundulika nchini Tanzania mwaka 1974 na kampuni ya AGIP na uchimbaji wake ulianza rasmi mwaka 2004 ambapo Benki ya Dunia ilikadiria kuwa gesi asilia itaifaidisha Tanzania na kuwaondoa wati milioni 11 kutoka katika wimbi la umasikini mkubwa. WAkati huo madini yalikuwa yakiendelea kuchimbwa nchini na hakuna faida ya moja kwa moja iliyokuwa inaonekana kwa wananchi juu ya uchimbaji wa madini hayo.

Wasomi waliaoandika kazi hii ya David Versus Goliath: Tanzania's effeorts to stand up to foreign gas corporations hawakuweza kuweka kisa alichowahi kuandika Kamara Kusupa kuhusu Bulyankulu na visa vingine vya wananchi waliokaribu na migodi ambao walinyanyaswa na kupelekea vifo vya watu kadhaa, kama ambavyo mwaka huu kampuni moja ya uchimbaji ililazimika kuwalipa wahanga wa matukio ya kinyanyasaji

JINSI TANZANIA INAVYOLIWA
Imebainika ya kwamba katika makampuni 1700 ya uchimbaji madini na gesi asilia ni 25% tu ndio wanalipa kodi. Hata Royalties zinazolipwa ni ndogo mno ambazo ni 2.3% ya makusanyo yote ya kodi hiyo ni kwa kipindi cha 1998 hadi 2011. Kibiashara ni kawaida kwa watu kusema hawapati faida lakini wasomi hawa wameonesha kampuni tatu kubwa ambazo mmetoka kuingia nazo mkataba zilipata faida ya USB 37.2 Bilioni mwaka 2017 ambapo wakati huo makusanyo ya kodi ya Tanzania kwa ujumla yalikuwa USD bilioni 7.3. Andiko hili linaonesha ubovu wa mikataba iliyokuwepo ambapo ilifanya Tanzania ipoteza kiwango kikubwa cha fedha kama mapato

Kutokana na arguments zilizokuwepo, watu wengi huwa na lawama kwa vyombo hivyo vya nje kutokana na ukubwa wake na ni kweli ni vikubwa kwa kuwa Mitaji ya kampuni kubwa tatu ni mara 16 ya GDP ya Tanzania, hata hivyo watafiti wanasema tatizo lipo ndani ya nchi na sio nguvu ya nje ya kampuni hizo

MZIZI WA FITNA
Leo tunashuhudia mtanange kati ya Waziri wa Nishati January Makamba na Mkurugenzi wa TPDC kuhusu kiwango cha mafuta kilichopo nchini. Japo hii haikuwa sehemu ya hoja za hao wanazuoni lakini wameweka wazi kwamba kutoa wataalamu wa nishati kutoka Wizara ya Nishati kuwapeleka TPDC kuna walakini kwa kuwa TPDC ni mdogo kwa Wizara ya Nishati ambapo inaweka ulazima wa wao kuripoti wizarani na kushindwa kuchukua maamuzi ya kitaalamu yasiyoathiriwa na siasa

Suala lingine ni kuwa na uwezo finyu wa ku-negotiate kwenye mikataba ya madini, ambapo katika hili watafiti hao wamemtaja Magufuli kuwa alijitahidi kuangalia mikataba na ile iliyokuwa na viashiria vya unyonyaji vilifutiwa leseni na kufanya uchangiaji wa mapato kutoka kwenye madini kwa GDP kupanda

Watu wengi walioko madarakani wana woga, kwenye kutoa taarifa, hali inayokuwa changamoto, i.e wanazuoni wameonesha kuwa walipata shida kukutana na wataalamu kutoka Benki Kuu ya Tanzania kwa kuwa hawakutaka kuonge nao wakati wa tafiti yao

Aidha watu wamewaambia watafit kuwa 'Kukalia ofisi ya umma ni njia fupi ya kupata utajiri' bila shaka hii ni akili iliyo kwa wengi ambapo ubadhirifu umekuwa kwa vichwa vya watumishi wa umma badala ya kuweka maslahi mapana ya taifa. Hoja zao zimeandikwa vizuri na wachumi wa maendeleo Smith and Michael Todaro (2014)

NJIA SAHIHI

Njia ambayo watafiti wameshauri katika kazi yao ni kuongeza uwezo wa kupambana na rushwa, kwa kitu ambacho watafiti wamekiita 'Magufuli Effect' kwa kuongeza uwajibikaji na kupitia upya mikataba ya madini na gesi. Aidha tumeona hivi karibuni masuala mengi yaliyoanzishwa na Magufuli kuhusu madini yakikiukwa ikiwemo kuruhusu usafirishaji wa makinikia ambapo Waziri Mkuu alisema nchi inakuwa imeshapata stahiki yake ambayo kimsingi ni dhahania kwa kuwa haujui kiwango cha madini yaliyoko ili kupata kodi stahiki

Hoja zilizoko kwenye kazi hii ni hoja nzito ambazo zinaendana visuri na hoja za Action Aid kwenye kuzidisha wigo wa kupaa kodi bila kuongeza tozo, ushuru nk wakati vipo fedha nyingi ambazo tunaziacha bila kuchukua stahiki, recently ration ya Tax to GDP haizidi 14 ambapo ukusanyaji kodi ukiwa mzuri hasa kwenye sekta ya madini na gesi hesabu za Action Aid zimeonesha Tax to GDP ratio itapanda hadi kufikia 50% ambapo hatutakuwa tena na haja ya kuomba mikopo kutoka nje

Ni muhimu kuzalisha wataalamu wa kutosha wakuitazama vyema mikataba ili kujua namna bora ya kufaidika kutoka kwenye mikataba hiyo

Kaz iliyokuwa Reveiwed ni Polus, A., & Tycholiz, W. (2019). David versus Goliath: Tanzania’s Efforts to Stand Up to Foreign Gas Corporations. Africa Spectrum, 54(1), 61-72.

Signed

OEDIPUS
Nimeshangaa kusikia kuwa hili pia ni tatizo kwa nchi kama Canada. Sikujua kama Canada ina reserve ya mafuta kuliko Saudia na Qatar. Lakini mafta hayachangii sana mapato ya serikali.
Nadhani serikali ili ifaidi matunda ya mariasili, inafaa iwepo kampuni ya serikali inayosimamia mavuno yake kama ilivyo Saudia na nchi za Kiarabu.
 
Back
Top Bottom