Revenue collection ya serikali 80% inatoka Dar? Nimechanganyikiwa kabisa na hili

kibaravumba

JF-Expert Member
Dec 21, 2012
6,635
7,005
Pamoja na mikoa mingine kuwa na kilimo chote cha korosho, chakula kama mpunga, mahindi, ufuta, alizeti n.k. hivi vyote ni bure tu kwani havilimwi Dar!

Tunaona migodi mikubwa ya dhahabu Geita, Bulyanhu, Buzwagi, North Mara, Tanzanite Mirerani, migodi ya makaa ya mawe, Mwadui diamond, gesi ya mtwara; vyote hivi si kitu ukiviweka pamoja bado ni kama tone tu ukilinganisha na uzalishaji wa Dar!

Michango ya wafanyakazi wa serikali na sekta binafsi kwa nchi nzima ni kidogo sana ukiichukua yote kwa pamoja ukilinganisha na zinazokusanywa Dar! Hili limenitisha!

Mifugo mingi kama ng'ombe, Mbuzi, kuku n.k. Mbuga za wanyama, utalii, samaki wa ziwa Victoria, mbona inaniwia vigumu kuelewa?

Zile tochi zote na faini za magari huku mikoani, nchi yenye watu milioni 50, faini hizi ni kidogo ukilinganisha na inayolipwa na watu wanaokadiriwa kuwa milioni sita tu wa Dar!

Hii lugha sijaielewa kabisa na kwa ujinga wangu nimeogopa sana kwa umaskini mkubwa uliopo mikoani, licha ya raslimali nyingi zilizoko huku.

Mwenye kunifafanulia naomba anisaidie. Kumbe inawezekana Dar hawapendelewi kimaendeleo, ni haki yao iwapo 80% ya mapato ya Serikali yanatoka Dar.
 
Bandari ndugu ndiyo inafanya yote iwe hivyo!We fikiri mafuta,magari,pikipiki,dawa,mabati,vifaa vya kilimo kama matrekta,mbegu,kalamu,samaki,sukari,nguo,vipuri na mizigo mingine mingi inayoelekea nchi jirani vyote vinalipiwa kodi Dar kwasababu ya bandari!

So kila mkoa,wilaya mpaka kijiji vinaichangia Dar mapato!
Hata hizo korosho na mazao mengine zikitaka kusafirishwa zinapitishwa bandari ya DSM!
Bila bandari nchi hii ingekuwa ICU!
 
Bado haijakaa akilini kabisa.Ina maana nchi zisizo na bandari wanaishije?
Bandari ndugu ndiyo inafanya yote iwe hivyo!We fikiri mafuta,magari,pikipiki,dawa,mabati,vifaa vya kilimo kama matrekta,mbegu,kalamu,samaki,sukari,nguo,vipuri na mizigo mingine mingi inayoelekea nchi jirani vyote vinalipiwa kodi Dar kwasababu ya bandari!
So kila mkoa,wilaya mpaka kijiji vinaichangia Dar mapato!
Bila bandari nchi hii ingekuwa ICU!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukweli ulio wazi, utalii ndo unaingiza pato kubwa kuliko pahala popote. Hawawez sema ila ndo ukweli

Sent using Jamii Forums mobile app

Hii sekta ina pato kubwa sana labda amesema kutokana na kipind hiki ambapo shughuli nying za kitalii zimefungwa na mchango wake kwa sasa ni mdogo ikilinganishwa na kabla ya hili janga.

Kwa taarifa za miaka ya nyuma kidogo nakumbuka mwanza ilikua ni miongoni mwa chanzo kikubwa cha pato la taifa bila kuisahau Arusha kwhyo nmeshtuka kwa hizo 80% za mheshimiwa.
 
Bandari ndugu ndiyo inafanya yote iwe hivyo!We fikiri mafuta,magari,pikipiki,dawa,mabati,vifaa vya kilimo kama matrekta,mbegu,kalamu,samaki,sukari,nguo,vipuri na mizigo mingine mingi inayoelekea nchi jirani vyote vinalipiwa kodi Dar kwasababu ya bandari!
So kila mkoa,wilaya mpaka kijiji vinaichangia Dar mapato!
Hata hizo korosho na mazao mengine zikitaka kusafirishwa zinapitishwa bandari ya DSM!
Bila bandari nchi hii ingekuwa ICU!
Yani 80% ya mapato ya nchi hii inatoka Dar kwasababu ya Bandari?
 
Yani 80% ya mapato ya nchi hii inatoka Dar kwasababu ya Bandari?
Inawezekana kabisaa!Hebu angalia hapo mkoani ulipo ni bidhaa ngapi katika matumizi yako hazipita katika bandari ya DSM!Ukianza na usafiri,hiyo petrol na magari yote nchini hupitia hapo!Njoo kwenye bidhaa zote kutoka viwanda vya nje hupitia hapo!

Bado tukitaka kusafirisha madini,mazao,malighafi nk kwenda nchi za mbali tunapitishia dar!Viwanda vingi nchini viko hapo hapo Dar au ukanda huo wa pwani!Soko kuu la hisa nchini liko Dar!Sasa hapo unategemea nini?
 
MFANO NENDA UGANDA ALAFU UKIRUDI NDO UTAJUA TULIPO
Bandari ndugu ndiyo inafanya yote iwe hivyo!We fikiri mafuta,magari,pikipiki,dawa,mabati,vifaa vya kilimo kama matrekta,mbegu,kalamu,samaki,sukari,nguo,vipuri na mizigo mingine mingi inayoelekea nchi jirani vyote vinalipiwa kodi Dar kwasababu ya bandari!
So kila mkoa,wilaya mpaka kijiji vinaichangia Dar mapato!
Hata hizo korosho na mazao mengine zikitaka kusafirishwa zinapitishwa bandari ya DSM!
Bila bandari nchi hii ingekuwa ICU!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bandari ndugu ndiyo inafanya yote iwe hivyo!We fikiri mafuta,magari,pikipiki,dawa,mabati,vifaa vya kilimo kama matrekta,mbegu,kalamu,samaki,sukari,nguo,vipuri na mizigo mingine mingi inayoelekea nchi jirani vyote vinalipiwa kodi Dar kwasababu ya bandari!
So kila mkoa,wilaya mpaka kijiji vinaichangia Dar mapato!
Hata hizo korosho na mazao mengine zikitaka kusafirishwa zinapitishwa bandari ya DSM!
Bila bandari nchi hii ingekuwa ICU!

Unaelewa vipi unapoambiwa utalii unachangia 25% ya pato la nchi hii? Lakini ukiangalia utalii kwa sehemu kubwa sio Dar. Kwa maneno marahisi ni kuwa data za uchumi nchi hii ni za kupika.
 
Unaelewa vipi unapoambiwa utalii unachangia 25% ya pato la nchi hii? Lakini ukiangalia utalii kwa sehemu kubwa sio Dar. Kwa maneno marahisi ni kuwa data za uchumi nchi hii ni za kupika.
Mkuu unaweza kuta mgeni analipia siku atazokaa nchini wizara ya mambo ya nje,wakati huo huo wizara iko Dar!Japo ni mtalii anaenda Arusha,tayari anaacha hela ya kuishi nchini Dar,huko anakoemda kutalii analipa expenses nyingine kulingana na eneo!Halafu tofautisha kati ya pato la taifa na revenue!
 
Umeuliza swali moja la msingi sana. Kuna wakati tuliambiwa Dodoma imeipiku Dar kwa mapato, watu wakauliza, inakuwaje? Au tunavyoambiwa asilimia 80-85 sijui ya watanzania wako kwenye sekta ya kilimo, hii nayo ni kweli?

Kama wengine wanavyouliza, tumekuwa tunaambiwa utalii ni sekta inayoongoza kwa kuingiza mapato ya kigeni, na hii yenyewe ni questionable kwa sababu binafsi sidhani kama utalii wa nchi hii utaweza kuishinda sekta ya madini.

Turudi kwenye kulipa billioni 700 kila mwezi kwa madeni ya nje tuliyoambiwa juzi. Haya ni madeni gani wakati miradi mingi tumekuwa tunaambiwa tunalipa kwa fedha zetu za ndani.

Maswali ni mengi, lakini kuna uwalakini katika takwimu tunazopewa.
 
Back
Top Bottom