padlock
JF-Expert Member
- Jul 18, 2013
- 328
- 496
Vichwa vya watu wengi ni kuhisi kwamba namna binti huyu alivyoachiwa amefanywa vibaya, yaani Uibe, upatikane ushahidi na vielelezo kisha vyote hivyo viwekwe wazi, Useme alieweka wazi amekosea?? wakati anaulizwa mbele ya wazee wake na kadamnasi ya mashangazi sijui wajomba alivyokuwa anakataa?? Je hilo nalo ni somo lakuhitaji Masters kuwa Huyu Binti ni mSaliti na Muongo?? Yaani unakana huku ukiweka collabo na Jina la Mungu Mara Yesu bila kujua unapalilia makaa ya mawe. Huwezi kufanya mambo yale yale kwa njia zile zile utegemee majibu Tofauti. Me nadhani majibu aliyokuwa anayatafuta ndio aliyoyapata tena alistahili vema kabisa. Kila unachokifanya kina Gharama yake (Everything you do has its price). Siku zote anayeanza haonekani Mbaya bali anayemaliza. Wakati mtoa maada anaelezea visa vya huyu binti naona wengi walikuwa wanasahau, ila wanakumbuka Namna jamaa alivyo Backfire madhila, dharau, usaliti na uongo woote wa Huyu binti. Hapo ndipo wamepakumbuka tu.Mwanamke ambaye namuwekea si chini ya laki 2 kila wiki, hiyo sio ya kula wala mavazi, ni vocha na matumizi yake binafsi, gari yake muda wote ina mafuta, nikamfanya kuwa Malkia kuliko mama angu mzazi, anatokea mama mmoja humu anasema mimi katili, katili gani duniani anaweza kufanya mambo km haya niliyomfanyia huyu binti, tamaa zimepita kiasi kila hela anaitaka, haridhiki, elfu 70 sijui laki inamtoa iman, tuweni serious kdg nyie.
Wakati Mahusiano yanaanzishwa Binti aliepewa alert kabisa, kama ngoma ilikuwa nzito ilibidi tu akae Pembeni ya Mchezo kuliko Kupotezea muda mtu. Unapendwa, unajaliwa, unathaminiwa, unapatiwa Heshima na vigezo vyote kama Mke still unarandaranda, Hii naiita "DHARAU" na dawa ya Hii ni Kiburi. Ukiwa mtu wa kutafuta shari basi jua Malipo yako yatakuwa shari tu.
Nadhani Pigo alilopata huyu Binti ni Funzo ktk Maisha yake, na ninaona Kama Haikutosha kabisa, Ilibdi dozi iwe nzito kuliko hii, Nadhani Alitakiwa atumike kama Extreme Bad Example. So wakati anaendelea kujiskia Vibaya asidhani hafai, Anapaswa kutambua Anafaa kuendelea kutumika kama Mfano mbaya kwa wengine.