Elections 2010 Revealed: Timu ya Kuchakachua Matokeo ya Nec ni Hii? (CLOSED: Ushahidi unahitajika)

Status
Not open for further replies.

pangamawe

Member
Jan 18, 2009
8
0
Ujumbe umefutwa (nakala ipo), ulikuwa unataja majina ya watu moja kwa moja bila kuwa na ushahidi wa wazi. JF HAIPO kumchafua mtu bila kuwa na uthibitisho wa kauli. Mwanzisha hoja akija na ushahidi tutaendeleza mjadala huu.

JF Administration
 
Nyie wana CHA DEMU mbona mnafikiri sana katika kuibiwa kwa kura na si kujiamini katika ushindi???? Unajua mfa maji haachi kutapatapa... Kama kweli CHA DEMU ina uhakika wa kushinda uchaguzi mkuu hiyo 31 October, basi na isubiri matokeo na si kushupalia kuibiwa kwa kura.
Swali langu ni kwamba... Hivi kigezo cha kujua mtu anakubalika ni nini? wingi wa mkusanyiko wa watu ktk mhadhara? Kusoma sana JF na kutuma hoja? au ni nini? Tusiwe wachochezi wa mambo yasiyo na msingi na kupata kisingizio cha kuhatarisha amani ya nchi yetu hapo baadae.
Sipendi nasema sipendi kuona visingizio vya kutaka kuleta fujo na uvunjifu wa amani.

Nawakilisha Oktoba 31
 
WEWE CAIN WE WAKILISHA TU CCM KWASABABU UNA KULA KUPITIA CCM,ILA UJUE TU MTI MKUBWA UKIDONDOKA LAZIMA KISHINDO KISIKIKE ILA SASA SISI CHADEMA HATUOGOPI KISHINDO NA UTAENDELEA KUTEMBELEA NDALA NA CCM YAKO.:dance::dance::dance::dance::dance::dance::dance::dance:ENDELEA KUPIGA MAYOWE.
 
Uwizi huo utafanyika katika mazingira yepi?, na wakati wizi huo utakapofanyika mawakala wa vyama husika ambao watahusika mojakwamoja katika usimamizi wa zoezi la upigaji kura watakuwa wapi?. Hizi ni hisia tu za watu ambao wameona kuwa wanaelekea kushindwa katika uchaguzi wa 2010
 
Kwa mtu mwenye uelewa mzuri akisoma taarifa hii kwa makini atagundua kuwa taarifa hii imepikwa tu na haina ukweli na imeungwaungwa tu na mambo mengi .Kwamba haina mtiririko na facts zinazojitosheleza kuwa taarifa kamili na watu wakaamini kwamba ni taarifa sahihi. Kututajia majina ya baadhi ya maafisa usalama siyo kigezo cha kwamba taarifa hii ni sahihi,kwa sababu maafisa usalama tunaishi nao mitaani na tunakunywa nao kwenye mabaa na tunashirikiana nao katika mambo mengi tu ya kijamii na tunawajua kwa majina pia.
 
'',kwa sababu maafisa usalama tunaishi nao mitaani na tunakunywa nao kwenye mabaa na tunashirikiana nao katika mambo mengi tu ya kijamii na tunawajua kwa majina pia''. Hiyo sio sababu kwa sababu kazi wanazozifanya huzijui pia maafisa usalama kuwa katika ofisi za Nec hilo pia ni jukumu lao kujua kila linalofannyika
 
Uwizi huo utafanyika katika mazingira yepi?, na wakati wizi huo utakapofanyika mawakala wa vyama husika ambao watahusika mojakwamoja katika usimamizi wa zoezi la upigaji kura watakuwa wapi?. Hizi ni hisia tu za watu ambao wameona kuwa wanaelekea kushindwa katika uchaguzi wa 2010

Bobishimkali wewe ni zaidi ya mkali.
Hawa Cha Demu wanatapatapa tu kwani hakuna wanaloweza. Hawajazuiwa kuweka mawakala wao lakini wanapiga pumba tu kuhusu kuibiwa kura. Nawaambia hata hao mawakala wao watawasuta baada ya uchaguzi kuonyesha jinsi CCM itakavyokuwa imeshinda.
Chonde chonde tu msiwarudi mawakala wenu...

Nawakilisha Oktoba 31
 
Hii nimeitoa ndani ya thread ya "Njama za kuiba kura jamani hizi hapa", sababu naona watu wengi hawapita kule, kuna ukweli juu ya tuhuma hizi??
 
Hii nimeitoa ndani ya thread ya "Njama za kuiba kura jamani hizi hapa", sababu naona watu wengi hawapita kule, kuna ukweli juu ya tuhuma hizi??


Kipindi hiki yatasemwa mengi hata ya kutunga ili kuonyesha kwamba wapinzani wanaonewa. Nani atadhibitisha haya nashindwa hata kuchangia kwani naweza kuhukumu kumbe ni maelezo ya kutungwa ili kuichafua taasisi hiyo
 
Na pengine majina yenyewe ni ya kutunga kwani ni vigumu kujua mambo ya ndani ya Idara ya usalama wa Taifa kutokana na asili ya kazi yao.
 
Na pengine majina yenyewe ni ya kutunga kwani ni vigumu kujua mambo ya ndani ya Idara ya usalama wa Taifa kutokana na asili ya kazi yao.
Majina yana ukweli ndani yake maana hao watu nami nawafahamu baadhi yao.
 
Uchaguzi mkuu wa mwaka huu unanikumbusha mwaka 1995 Mrema alipojitangaza kwamba katumwa na Usalama wa Taifa kugombea Urais kumbe anataka kupata kura za wananchi kiulaini. Kuwasingizia Usalama wa Taifa si mambo yaliyoanza leo. Marando naye kaja na yake kujiweka karibu na usalama wa Taifa? mwaka huu tutasikia mengi kila mtu akiihusisha usalama wa taifa ili kutimiza malengo yake.
 
niko ndani ya TISS, narudia niko ndani ya TISS hayo majina ni sahihi na kuna watu wawili huyu kikula na nzowa tunawatafutia dawa.wameikumbatia ccm...

tayari nimefanikiwa kupata karatasi feki za kupigia kura nitaziweka hapa ili umma ujue nini kinaendelea.
 
Kutaja majina ya watu si kigezo pekee kwamba taarifa ni ya kweli. Watanzania tuwe makini kudadisi na kudadavua taarifa zingine zina malengo ya kuchafua hali ya hewa.
 
Mama Porojo, majina yote yaliyotolewa ni watu wanaofahamika kabisa na kinachonishangaza ni kuwa watu hao wamekaa kimya hawajakanusha.

Wote waliotajwa na tena kwa nafasi zao ni sahihi kabisa, kama imetungwa mbona hawakanushi? Inawezekana kuna ukweli ndani yake.
 
wale vijana wa IT ni kweli walifanikiwa ku-access remotely database server kwani walipata public ip-address ambayo ni 80.74.107.38 lakini tumefanikiwa kuzuia hilo lisienedelee hapo jana na sasa hawaweze kufika kule kwenye server
 
Hii kitu imezunguka sana kwenye e-mail kiasi kwamba credibility yake inaweza kuwa na utata!! Lakini habari ndiyo hiyo!!!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom