Reuben Ndege kavae viatu vya jasiri uingoze njia

mayowela

JF-Expert Member
Nov 2, 2014
2,124
1,744
Nimepatwa na furaha sana baada ya kuona taarifa kwenye ukurasa wako wa mtandao wa Instagram ukiufahamisha umma/mashabiki kuwa kwa sasa umerejea CMG, Clouds Media Group, imekuwa furaha kwa wengi ila hofu kwa wengi pia.

Reuben Ndege almaarufu Nchakali, ulipikwa Clouds na jasiri marehemu Ruge ukawa zao bora na hatimae SCANAD wakaona hapana wakakukaribisha na kukupa nafasi uuoneshe uuma upande wako wa creativity uko vipi.

Ukiwa SCANAD ulipaza sauti na wachache hawakuelewa ila walioko kwenye tasnia ya Advertisement waliumia kichwa na kuwaza haya madini huyu mtu anayatoa wapi, Kampuni kubwa umeshiriki kuandaa kampeni za bidhaa kwa njia ya matangazo, Coca Cola, Vodacom, Tigo, Kvant, Chai Bora, etc.

Naweza sema uzalendo na Upendo ulionao Clouds ndio umekurejesha na ni heshima kwa Ruge huko aliko anatabasamu nakuona viatu vyake mvaaji amepatikana,sidhani kama umeangalia sana maslahi, kama ni maslah SCANAD naamin walikuwa na uwezo wa kukuretain kwa nafasi uliokuwa nayo na ungebaki ila la hasha.

Wengi walijiuliza viatu vya jasiri angevaa nani, na jina lako lilikuwa midomoni mwa kila mtu naona ule msemo wa Sauti ya watu ni sauti ya Mungu umejidhihirisha, kapambane na tukutakie kila kheri wale waliohisi Mawingu imefika Mwisho nadhani wameanza kuona ndio kwanza Imezaliwa upya.

Kila la heri Reuben Ndege (Nchakali).
 
Back
Top Bottom