Restituta Mbogo: Wakina Mama hakikisheni Wanaume wanaandika majina yenu pindi wanaponunua ardhi

na wanaume tuhakikishe yanaandikwa majina yetu akinamama wanaponunia ardhi na mali myinginezo...au ndio "changu-chetu, chako-chako mwenyewe"...

Ni vyema akapambana ianzishwe sheria kila mali inayotafutwa mkiwa kwenye ndoa badi iandikwe majina ya watoto na mkiachana mali ibaki chini ya mahakama mpaka watoto wafikishe miaka 25.... kama mmeachana hamna watoto basi kila mtu achukue kile alichochuma kwa jacho lake....

Kuwe na mikataba kabla ya ndoa inayosema nani amekuja na nini kwenye ndoa, nani anafanya kazi gani, kila kipato cha mtu kiwe wazi...ili mwisho wa siku kila mtu abaki na chake...na ndoa iwe ni sehemu ya kuburudishana tu na kutafuta watoto.....
 
“Ningependa kutoa ushauri wa jumla kwa wakina mama wa Tanzania, waume zetu wanavyonunua ardhi na sisi tuhakikishe majina yetu yanakuwepo pale pembeni, kwasababu wamama wengi wamekuwa wakidhulumiwa nyumba na mashamba,” amesema Mbunge Taska Restituta.

Mbunge huyo ameongeza kusema kuwa, “Tusiwe wavivu kununua viwanja, tusipende kuwatuma akina baba halafu hawaandiki jina lako unakaa pale kwa miaka 40 unaonekana wewe ni mpangaji,” amesema Mhe. Restituta.
Nanyi mkinunua andikeni majina ya akina baba vivyohivyo!!!
 
Hivi kwanini kwenye Ndoa WANAWAKE akili zao sikU zote wanawazaga Mwanaume tu ndie atakae tangulia Kufa
Uzoefu unawafundisha hivyo katika jamii kwa kutafakari tangu ngazi ya kaya mpaka TAIFA !

Mfano angalia wajane na wagane ni akina nani wengi kwenye jamii ? Anza kwa wanasiasa maarufu na wafanya biashara wakubwa Tanzania !
 
Mbunge wa Viti Maalum Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi, Mhe. Taska Restituta Mbogo, ametoa wito kwa akina mama nchini kuhakikisha wanaume zao wanaandika majina yao wanapokwenda kununua ardhi ili kuepuka matatizo ya baadaye pindi mmoja wao anapofariki dunia.

Mhe. Restituta ametoa ushauri huo wakati akiwasilisha hoja Bungeni, Dodoma na kueleza kuwa wakina mama huwa wana tabia ya uvivu wakuweka majina yao kwenye ardhi ilihali sheria inaruhusu watu wanawake kumiliki ardhi.

“Ningependa kutoa ushauri wa jumla kwa wakina mama wa Tanzania, waume zetu wanavyonunua ardhi na sisi tuhakikishe majina yetu yanakuwepo pale pembeni, kwasababu wamama wengi wamekuwa wakidhulumiwa nyumba na mashamba,” amesema Mbunge Taska Restituta.

Mbunge huyo ameongeza kusema kuwa, “Tusiwe wavivu kununua viwanja, tusipende kuwatuma akina baba halafu hawaandiki jina lako unakaa pale kwa miaka 40 unaonekana wewe ni mpangaji,” amesema Mhe. Restituta.

Naye Mbunge viti maalum Mhe. Sophia Mwakagenda akitoa taarifa bungeni ameungana na hoja iliyowasilishwa na Mhe. Restituta.

“Mhe. Spika lakini waume hawa wanapoenda kununua viwanja hawatuagi, na wakati mwingine ananunua akiwa amefariki bahati mbaya, unashangaa kumbe wake mko sita wakati unajua uko peke yako,” amesema Mhe. Sophia Mwakagenda.
Wabunge wa ccm kuchangia hoja zenye maslahi ya taifa ni 0% ,wao wapo kwa ajili ya matumbo yao tu
 
Dah, Weee jamaaaa
Nyakati hizi kuoa limekuwa jambo la kuogofya sana maana wanawake wameigeuza miili yao kuwa maduka na kujipatia mali.......napata kigugumizi ninapoombwa ushauri wa masuala ya kuoa maana unaweza ukamsababishia kijana wa watu matatizo makubwa sana yatakayomfanya akulaani maisha yake yote..............
 
Wanaume mnaoona kama wake zenu watawaibia au watawafilisi, msiowe. Bakini kuwa ma bachelors, bakini na vimada wenu, zaeni hovyo hovyo kama wanyama pori. Maisha yanaendelea. Familia zenu zitawapeni presha tuu lakini haziwezi kuwalazimisha kuowa. Mambo ya ndoa waachieni wanaume wanaoyaweza na ambao wako tayari kuungana na wake zao wawe kitu kimoja. Hakuna cha kwangu, hakuna cha kwake, vyote ni vyetu pamoja.
 
kwa lile tukio la kufungishwa ndoa ya kimila, kama ndo mimi, wala nisingemuoa.
Upumbavu Sana huu,

Tena UPUUZ Kama huu huu uliwai sababisha nmeish na mke miaka 12 sijafunga nae kabisa Ndoa,

Unakaa zako Unawaza ukishaweka mambo sawa Ubariki ndoa.

Unashangaa mwanamke anakuamsha usiku kukuambia
"Baba D, fanya tufunge ndoa mme wangu. Endapo ikitokea Mungu amekuchukua gafla nitabaki katika mazingira gani"

Unabaki unajiuliza,
"Ina maana uyu mtu anajua kabisa Mimi ndo ntakaetangulia?"

Unaghairi, Unafanya Mambo mengine.

Kuna siku niliwai kukosana na ba mkwe, kisa kunitumia tumia watu wanipush tufunge ndoa.

Ba mkwe anakuita kukuambia
"Mwanangu, fanyeni mfunge Ndoa,
Kuna kesho na keshokutwa Unaweza usiwepo wajukuu wangu uyu akakosa haki zao za msingi"

Nikamjibu TU kwa kifupi Kisha nikaondoka zangu,
"Nikiwa tayar nitakujuza mzee"

sikU moja ikatokea harusi ukweni, tumehudhuria shemej yangu mmoja anafunga Ndoa ya kimila.

Nashangaa Wazee wananiita chumba Cha kumuandaa bwana harusi, nakunikaribisha kiti jirani na bwana harusi mhusika.

Nashangaa kuona wanaingia waandaaji wanaanza kuniandaa Kama alivokua bw.harusi,

Nikamwambia,
"Ebu subiri, Nini kinaendelea hapa"

Wakajibu,
"Tumeelekezwa na mkwe wako tukuandae Kama P na wewe ufunge Ndoa leo leo."

Nikanyanyuka nikatupa makorokoro yao nikaondoka nje.

Niko nje ba mkwe ananifata,
"Vipi kijana mbona umetoka nje wkt Kila kitu Kisha kishaenda sawa"

Nikamwambia,
"Mzee mbona hamkuniandaa kwa zoezi la Ndoa, ninachojua nimekuja hapa kujumuika Kama wanafamilia wengine Kwenye harusi ya shemej yangu"

Akasema,
"Mi mbona mkeo nilimwambia na anajua na maandaliz yote anafahamu"

Nikamuita,
alipokutwa nae akaanza kujiuma Uma eti akajua kwa sababu Nilikua nawasiliana na mzee wake Basi alijua tayar ashaniambia, nikampuuza.

Nikamwambia mzee,
"Kwanza sijawai kufikiri kufunga Ndoa ya kimila, pia siwez kufungia Ndoa ya ukweni nilikooa na pia siwez funga Ndoa bila wazazi wangu au Ndugu zangu kuwepo"

Akasema,
" Sasa itakuaje, na tumeshatumia gharama"

Nikamwambia mzee,
"Mzee wangu Ilo la gharama zenu halinihusu,nnachojua Mimi siwez funga Ndoa sijajiandaa Kama nilivokueleza.
Maandaliz yangu yakiwa tayar nitakueleza na sitegemei kufunga Ndoa ya kimila,ilo sahau kabisa"

Nikapanda zangu usafiri nikarudi zangu KWANGU.

Niliporudi nyumban, na wife akarudi nikamuwakia Sana, nikamwambia
"Kwa mlichokua mnataka kunifanyia uko kwenu. Sitaki kuskia Tena habar za Ndoa nyumba hii, vinginevyo unatafuta ugomvi mkubwa Sana na mimi. hutak kuish na Mimi Basi Rudi kwenu wakakutafutie mwanaume mwingine"

Tangu hapo, Kulikaa kimya Kama Miaka 5 hivi mbele bila habar Tena za kupush Ndoa.

Na ndipo nilipoamua mwenyewe kufunga Ndoa rasmi kabisa ya KIDINI.


MWAKA WA 9 Sasa Kwenye Ndoa Rasmi
 
Leo nilikuwa nafanya research ndogo ya maeneo niliokulia,wababa karibia wote wameshakufa ila wake zao wote wapo hai,hapa nimeangalia familia zaidi ya 20 za majirani zetu,nadhani wanalijua hili kuwa sisi tunatangulia kufa zaidi kuliko wao,ndio maana wanapambana sana inapokuja swala la mali...
Ukweli ni kwamba, baada ya safari ngumu ya kutafuta na kulea watoto wakafikia utu uzima, siku za mwanaume huwa zinaanza kuhesabika.

Ndio maana wazee wa zamani ilikuwa mtoto wa kwanza, hasa wa kiume akielekea au akioa. Nae anaoa mke wa pili. Na kuhamishia kila kitu kwa mke mdogo.

Kwa sababu, wanawake wanajuana. Ndo maana wazungu wanakamsemo kao "it takes a monster to fight a monster". Mkubwa akitaka kukutoa relini, mdogo anajibu mapigo.

Siku chache zilizopita kuna jirani yetu kafariki kwa ukweli uliowazi. Akauawa na mkewe.

Tuishi nao kwa akili.
 
Mbunge wa Viti Maalum Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi, Mhe. Taska Restituta Mbogo, ametoa wito kwa akina mama nchini kuhakikisha wanaume zao wanaandika majina yao wanapokwenda kununua ardhi ili kuepuka matatizo ya baadaye pindi mmoja wao anapofariki dunia.

Mhe. Restituta ametoa ushauri huo wakati akiwasilisha hoja Bungeni, Dodoma na kueleza kuwa wakina mama huwa wana tabia ya uvivu wakuweka majina yao kwenye ardhi ilihali sheria inaruhusu watu wanawake kumiliki ardhi.

“Ningependa kutoa ushauri wa jumla kwa wakina mama wa Tanzania, waume zetu wanavyonunua ardhi na sisi tuhakikishe majina yetu yanakuwepo pale pembeni, kwasababu wamama wengi wamekuwa wakidhulumiwa nyumba na mashamba,” amesema Mbunge Taska Restituta.

Mbunge huyo ameongeza kusema kuwa, “Tusiwe wavivu kununua viwanja, tusipende kuwatuma akina baba halafu hawaandiki jina lako unakaa pale kwa miaka 40 unaonekana wewe ni mpangaji,” amesema Mhe. Restituta.

Naye Mbunge viti maalum Mhe. Sophia Mwakagenda akitoa taarifa bungeni ameungana na hoja iliyowasilishwa na Mhe. Restituta.

“Mhe. Spika lakini waume hawa wanapoenda kununua viwanja hawatuagi, na wakati mwingine ananunua akiwa amefariki bahati mbaya, unashangaa kumbe wake mko sita wakati unajua uko peke yako,” amesema Mhe. Sophia Mwakagenda.
Huyu Mbunge mjinga sana.
Na mchepuko huandika wapi?
 
Hivi kwanini kwenye Ndoa WANAWAKE akili zao sikU zote wanawazaga Mwanaume tu ndie atakae tangulia Kufa
... kuna ukweli wa kisayansi na kijamii kwenye hili. Kisayansi, jini (genes) za kiume ziko weak kuliko za kike hivyo probability ya mwanaume kufa mapema ni kubwa zaidi. Kijamii, ni utamaduni kwamba wanaume huwazidi wenza wao umri.

Ni nadra sana kukuta mke wanalingana au kamzidi mume umri. In most cases wanaume kuwazidi wake zao by 5 to 10 years, even beyond, is very common. Kutokana na umri mkubwa, probability ya mume kufa kabla ya mke ni kubwa.

Pia kijamii, life style ya wanaume inawaweka kwenye risk kubwa ya kufa mapema kuliko wanawake. Kwa mfano, ulevi uliopindukia, uvutaji sigara, wake wengi/vimada na kote huko ni lazima uhudumie pamoja na kubeba kero zao inaongeza msongo wa mawazo hatimaye pressure, visukari, etc.

So, ukichanganya dimensions zote, men are in a high risk to die earlier than women. Wala haihitaji ushahidi wa kisayansi.

Na ukichunguza utakuta lugha za "ukifa nitaishije na watoto" hutolewa zaidi na wake ambao wamezidiwa sana kiumri na waume zao; au wale ambao life style za waume zao zime-deviate sana from normal! Yaani wewe ni kawaida kupotea nyumbani wiki nzima bila maelezo ya kueleweka halafu mke awe na amani; how?
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom