Restaurant gani au wapi wanapika chakula kizuri kwa Dar es Salaam?

Nenda mayor restaurant kariakoo mtaa wa nyamwezi karibu Na msikiti wa makonde zamani ikiitwa zitta restaurant hapo unapatikana Msosi wa nguvu kuanzia breakfast mpaka lunch kila kitu kipo sawa Na vimepikwa kwa ufundi wa hali ya juu mpaka juice ya pale sio mchezo
Hawa wamefunga siku hizi.
Ila pamoja na uzuri wa chakula walikuwa na reasonable price
 
Muanzisha Uzi inategemea unataka chakula cha aina gani. Ukiacha Chef's Pride sehemu nyingine nyingi za kula inategemea ni watu wenye asili ya wapi
Ukienda Zahir, Zitta, Golden Fork, White Rose, Mishi(tmk) utakuta vyakula kama Pilau, Biryan, Wali Nazi, Samaki na kadhaalika vinavutia
Ukienda Break Point, Chang'ombe Village, Rombo Greenview, Mary's, na Miami Ilala hapa utakuta vyakula kama Michemsho, Kuku choma, Nyama choma, Mbuzi Choma, Mtori na Kongoro ndio mwake
Kwa hiyo ukiuliza Restaurant lazima ueleze unapendelea nini ?
Uzuri wa Chef's Pride wanapika vyakula vya aina zote kwa weledi mkubwa sana
 
Back
Top Bottom