Rekodi ya matukio: Kilichoikuta CHADEMA kwa Lowassa ndicho kitakachoikuta Yanga kwa Manara

Kibosho1

JF-Expert Member
Dec 12, 2017
2,491
3,997
Kwanza nawaambieni ndugu zangu, dunia ya sasa usikiamini tena kiumbe kinachopumua.

Level ambayo mwanadamu amefikia inafaa kumwamini tu siku ukiona anaingia kaburini kufukiwa.

1. Mwaka 2015 tunakumbuka wanasiasa mahiri na mawaziri wastaaf, Edward Ngoyai Lowassa na Frederick Sumaye. walienda Chadema wakiwa wametukanwa sana, lakini walikuwa kama mbwa waliokuwa wamevaa ngozi za kondoo. Nini Chadema walipata kabla ya miaka mitano?

2.Real Haule Gluck na kigogo2014. huko jamuhuri ya twitter,hakuna watu waliotegemewa kama hawa, walikuwa influencers, wakosoaji, wanahabari n.k walipata mashabiki lukuki na kuamika kama wanaharakati wa kweli kumbe waganja njaa tu. Sasa hivi wako wapi?

3. Haji Sandé Manara. Huyu mnafiki amedhihirishia watanzania kuwa hakuna mwanadamu anaweza kuaminika kwa sasa hata kama akiapa kwa Mungu wake. Manara ameitukama yanga kwa miaka 6,tena maneno mabovu yakuudhi lakini GSM wameona anawafaa, kweli?

Kama ni mashabiki wa Yanga jipangeni kisaikolojia,naawaambia na wekeni alama uzi huu. GSM wao wako kibiashara zaidi ndio maana wamemuajiri huyu Haji kimaslahi, Haji ni mwana Simba kabisa lakini kaeni mkijua maneno sio pointi. Tukutane uwanjani
 
Manara mwanasiasa mpiga domo..
Nyinyi wafuasi lialia ndo mtalia sana..

Manara anapiga hela ..
Hata kwenye vyama watu wanapiga hela
Kwa sasas ndio naamini hivyo,hakuna mtu asieangalia hela kwa sasa. Mapenzi yamebak kwenye nasfi zao tu
 
Back
Top Bottom