Regina Lowassa awapa mbinu BAWACHA kuing’oa CCM

12143312_544907869018244_4888291860371228965_n-620x308.jpg


BARAZA la wanawake wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (BAWACHA) wametakiwa kuungana na kuweka mipango mikakati ya nguvu ili kuhakikisha wanaiondoa CCM madarakani katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2020 Kauli hiyo imetolewa leo na Mama Regina Lowassa alipokuwa akizungumza na wanawake wa baraza hilo katika mkutano wao wa kikao cha ndani na kikao cha kazi kilichofanyika mjini Dodoma.

Amesema juhudi za akina mama wa Chadema zilizofanyika katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 zilikuwa na nguvu kubwa hivyo kuna kila sababu ya kuongeza nguvu zaidi ili kuhakikisha akina mama wanagombea nafasi mbalimbali kuanzia ngazi ya tawi hadi taifa.

“Kwa sasa akina mama wenzangu kinachotakiwa ni kushikamana na kuwa na mikakati ya pamoja ili kuhakikisha mapambano ya kuing’oa CCM madarakani yanafanikiwa.

“Hakuna sababu ya kugombana wala kutofautiana ,wala kutegeana katika kufanya kazi, umefika wakati sasa wa kuanza nikakati ya pamoja katika kujenga chama,kujengeana uwezo pamoja na kutokuwa waoga katika kufanya maamuzi.

“Ni ukweli usiopingika katika uchaguzi wa mwaka 2015 CCM ilikuwa na wakati mgumu sana kwani akima mama mlionesha ujasiri mkubwa na mlifanya kazi nzuri na matokeo yake yalionekana,sasa uchaguzi umekwisha ni wakati wa kujipanga na kusonga mbele zaidi ili kuhakikisha CCM inaondoka madarakani ili kuwapa unafuu watanzania ambao wameteseka kwa muda mrefu sasa kutoka na na chama hicho kuwa na mfumo kandamizi” amesema Mama Lowassa.

Naye Halima Mdee, Mwenyekiti wa BAWACHA akifungua kikao cha kazi cha baraza hilo amewataka akina mama kuhakikisha wanafanya kazi kwa ujasiri na kuhakikisha wanapata nafasi mbalimbali katika ngazi za maamuzi.

Mdee ametolea mfano wa mkutano wa baraza kuu la Chadema Taifa na kueleza kuwa katika baraza hilo watoa maamuzi wengi walikuwa wanaume jambo ambalo linaonesha wazi kuwa akina mama wengi hawajitokezi kugombea nafasi mbalimbali za kimaamuzi.

Kutokana na hali hiyo sasa napenda kuwahamasisha wabunge wote wa Viti Maalum, kuhakikisha wanatafuta majimbo na kutafuta nafasi mbalimbali za maamuzi badala ya kuwa na hofu na kujiona kana kwamba zipo nafasi mbalimbali ambazo zinafaa kugombewa na na wanaume na siyo wanawake


Mbona Regina Lowass naye anafanya siasa kama Bulembo na hakuna aliyemzuia. Siasa za.bongo ni unafiki mtupu.
 
Hizo mbinu kwanini asingempa mumewe hadi akapigwa chini na Kikwete dodoma na hatimaye kugalagazwa na Magufuli kwenye uchaguzi mkuu.

..sasa na wewe hukuona kuwa Mzee Lowassa alikuwa mgonjwa taabani hawezi kukampeni?

..Magufuli alipaswa kupata ushindi wa tsunami ukizingatia kwamba mpinzani wake alikuwa hasemi chochote kwenye majukwaa.

..Labda muombe CDM walete mgonjwa mwingine kugombea 2020, vinginevyo u have to brace yourself for a very tough campaign.
 
Ngoja nyumbu waone unasema mgombea wao alikuwa mgonjwa taabani:D.

..that is one issue that very few ppl want to revisit.

..Lowassa did not put up any fight during 2015 campaign.

..his performance during those campaign was very uninspiring yet he lost by 2 mil votes only.

..Tatizo ni kwamba CDM wako so fixated kuwa waliibiwa kura, na hakuna mtu mwenye kufikiri kuwa kama mgombea wao wa Uraisi angekuwa imara huenda chama as a whole kingefanya vizuri(ubunge & uraisi).

..Pia hakuna anayefikiria 2020 mgombea wa aina gani awe ndiye mpeperusha bendera wa CDM.
 
12143312_544907869018244_4888291860371228965_n-620x308.jpg


BARAZA la wanawake wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (BAWACHA) wametakiwa kuungana na kuweka mipango mikakati ya nguvu ili kuhakikisha wanaiondoa CCM madarakani katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2020 Kauli hiyo imetolewa leo na Mama Regina Lowassa alipokuwa akizungumza na wanawake wa baraza hilo katika mkutano wao wa kikao cha ndani na kikao cha kazi kilichofanyika mjini Dodoma.

Amesema juhudi za akina mama wa Chadema zilizofanyika katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 zilikuwa na nguvu kubwa hivyo kuna kila sababu ya kuongeza nguvu zaidi ili kuhakikisha akina mama wanagombea nafasi mbalimbali kuanzia ngazi ya tawi hadi taifa.

“Kwa sasa akina mama wenzangu kinachotakiwa ni kushikamana na kuwa na mikakati ya pamoja ili kuhakikisha mapambano ya kuing’oa CCM madarakani yanafanikiwa.

“Hakuna sababu ya kugombana wala kutofautiana ,wala kutegeana katika kufanya kazi, umefika wakati sasa wa kuanza nikakati ya pamoja katika kujenga chama,kujengeana uwezo pamoja na kutokuwa waoga katika kufanya maamuzi.

“Ni ukweli usiopingika katika uchaguzi wa mwaka 2015 CCM ilikuwa na wakati mgumu sana kwani akima mama mlionesha ujasiri mkubwa na mlifanya kazi nzuri na matokeo yake yalionekana,sasa uchaguzi umekwisha ni wakati wa kujipanga na kusonga mbele zaidi ili kuhakikisha CCM inaondoka madarakani ili kuwapa unafuu watanzania ambao wameteseka kwa muda mrefu sasa kutoka na na chama hicho kuwa na mfumo kandamizi” amesema Mama Lowassa.

Naye Halima Mdee, Mwenyekiti wa BAWACHA akifungua kikao cha kazi cha baraza hilo amewataka akina mama kuhakikisha wanafanya kazi kwa ujasiri na kuhakikisha wanapata nafasi mbalimbali katika ngazi za maamuzi.

Mdee ametolea mfano wa mkutano wa baraza kuu la Chadema Taifa na kueleza kuwa katika baraza hilo watoa maamuzi wengi walikuwa wanaume jambo ambalo linaonesha wazi kuwa akina mama wengi hawajitokezi kugombea nafasi mbalimbali za kimaamuzi.

Kutokana na hali hiyo sasa napenda kuwahamasisha wabunge wote wa Viti Maalum, kuhakikisha wanatafuta majimbo na kutafuta nafasi mbalimbali za maamuzi badala ya kuwa na hofu na kujiona kana kwamba zipo nafasi mbalimbali ambazo zinafaa kugombewa na na wanaume na siyo wanawake


Naona ameibuka baada kazi ya kumuhudumia Mgonjwa wake kupungua, sasa hata Mgonjwa anatembea vizuri bado kuongea tu, sasa ugonjwa umehamia kwake!
 
Wa 2020 si ni Lissu, au..?

..at least u r 100% sure that TL will put up a very spirited fight.

..tatizo ni kwamba anybody else akiwekwa na Magufuli ata kampeni kwa kuogopa-ogopa.

..And one weakness that Uchwara has is that he has nver been " punched ".

..Sasa CDM needs a candidate who is fearless and has no respect for Uchwara, a candidate who is gonna come out of the gates swinging.
 
Mr.Junior

hata mimi nimeona fb wanazungumzia kuhusu huyo aliyepgwa kofi na mkuu wake. Cjui ni nan
 
Tatzo la watanzania tushaweka mawazo yakua ccm haiwez ondoka madarakan, why? Con cha ajabu ccm ikiondoka madarakan
 
Unajua tukiwa tunaongea kwa kuzihaki sio kuziri tukumbuke tume ya uchaguzi iko ktk mfumo upi tusijisifu tuko vizuri uchaguzi ni mpambano tuyaheshimu mawazo ya huyu mama kwani yeye yuko ndani ya uwanja
 
Mbona hakuweza kumsaidia Mzee Lowassa kuingia ikulu 2015?
Kuweka mtandao ni jambo chanya sana. Ikumbwe vuguvugu la maendeleo sehemu nyingi duniani huanzishwa na Wanawake. Pia Roma hakujengwa siku moja.
Uchanguzi wa 2015 , baada ya kuwa na UKAWA , ilileta changamoto kubwa sana kwa CCM . Hivyo wakiboresha mbinu( ingawa hata CCM nao huenda wakazinduka) wataleta ushindani mkubwa na hata kuweza kushinda uchanguzi wa 2020. Nani ajuaye?
 
Kuweka mtandao ni jambo chanya sana. Ikumbwe vuguvugu la maendeleo sehemu nyingi duniani huanzishwa na Wanawake. Pia Roma hakujengwa siku moja.
Uchanguzi wa 2015 , baada ya kuwa na UKAWA , ilileta changamoto kubwa sana kwa CCM . Hivyo wakiboresha mbinu( ingawa hata CCM nao huenda wakazinduka) wataleta ushindani mkubwa na hata kuweza kushinda uchanguzi wa 2020. Nani ajuaye?
Uishinde ccm? Unaota huku unatembea wewe
 
Back
Top Bottom