MakinikiA
JF-Expert Member
- Jun 7, 2017
- 5,011
- 6,542
Maelezo ya picha: Refa akionesha kadi nyekundu
Maafisa wa polisi na wale wa huduma ya ambyulansi waliitwa ili kuingilia kati. Refa huyo kwa jina Satyam Toki, 28 anafanya uamuzi wa kuwasilisha mshtaka mahakamani.
Klabu hiyo ya Sporting de Mundial inasema kwamba mchezaji huyo ameondolewa katika klabu hiyo na kwamba atapatiwa matibabu ya kiakili.
SatyamToki ni mkufunzi na refa
''Tunashutumu kitendo hicho cha kutisha'', waliongezea katika mtandao wao wa Twitter.
Toki alisema kwamba alimuomba mchezaji huyo mara kadhaa kutumia lugha nzuri na kuwacha kulalamika, kabla ya kumuonya.
Alianza kutoka na kuelekea katika eneo la wachezaji wa ziada wa timu yake na alipokuwa akiondoka alinitishia kwamba ataniona baada ya mechi, Toki alisema.
''Ni wakati huo ndiposa nilimpatia kadi nyekundu na kunipiga ngumi usoni''.
''Karibu anasisababishie upofu kwa sekunde chache, na baadaye nilianza kutokwa damu.
Kushambuliwa kwa Satyam Toki kulinaswa na kamera ya uwanjani