Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,988
CCM kama ilivyo sasa haiwezi kuokoleka
Na M. M. Mwanakijiji - Imechapwa 18 August 2009
Gumzo
KUNA watu ambao kwa makosa ya fikra zao na kiburi cha utamu wa madaraka, hasa wale waliopigwa ganzi ya "utukufu wa kisiasa," wanaamini kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kitadumu madarakani milele.
Hawa, wamejiaminisha katika upotovu wao kuwa CCM kitadumu milele na kitaendelea kuwa kama kilivyo sasa. Hawa ni wa kuwekewa mikono na ikibidi kupepewa huku wanavutwa masikio.
CCM ni mazao ya binadamu, ni chombo kilichoundwa na wanadamu; kimeongozwa na kinaongozwa na binadamu na kutokana na hilo tu peke yake, CCM kinakuwa ni chombo kinachoweza kuharibika, kuvunjika, kuporomoka na kwa hakika kabisa chaweza kuzama.
Hakuna ustadi wa mwanadamu unaoweza kufanya kazi zake zisiwe na makosa milele. Katika uelewa wetu huu mdogo wa kibinadamu ni kazi za Mungu tu ambazo hazina makosa.
Hivyo ninaposikia mtu anasema kwamba CCM itatawala milele, na kumtumbulia macho kama mjusi aliyekoswakoswa na mlango. Na pale ninaposikia kuna wana poropaganda wa CCM ambao "wanaitetea CCM kuwa ni chama safi na kina mafisadi wanne tu," ninafumba macho yangu kwa mshtuko.
Kama ningekuwa karibu na mtu huyo, ningemtingisha ili atoke katika usingizi wake uliochanganyika na ulevi wa madaraka.
Malumbano tunayoyasikia sasa na kugongana kunakoendelea hivi sasa ndani ya chama hiki na tutashuhudia zaidi miezi michache ijayo, yanatoa ushahidi wa jambo moja kubwa kuwa CCM kiko matatani na hakuna mtu wa kuiokoa.
Wale wanaogongana ndani ya CCM leo hii, hawagongani kwa sababu ya tofauti za kiitikadi (karibu wote hawana); wanagongana zaidi kuhusu maslahi yao ndani ya chama. Makundi yote yaliyopo ndani ya CCM leo yanatuhakikishia kuwa hayawezi kudumu ndani ya chama hichohicho yakiendelea kuongeza upana, ukali na uzito wa tofauti zao.
Gazeti toleo na. 150
Na M. M. Mwanakijiji - Imechapwa 18 August 2009
Gumzo
KUNA watu ambao kwa makosa ya fikra zao na kiburi cha utamu wa madaraka, hasa wale waliopigwa ganzi ya "utukufu wa kisiasa," wanaamini kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kitadumu madarakani milele.
Hawa, wamejiaminisha katika upotovu wao kuwa CCM kitadumu milele na kitaendelea kuwa kama kilivyo sasa. Hawa ni wa kuwekewa mikono na ikibidi kupepewa huku wanavutwa masikio.
CCM ni mazao ya binadamu, ni chombo kilichoundwa na wanadamu; kimeongozwa na kinaongozwa na binadamu na kutokana na hilo tu peke yake, CCM kinakuwa ni chombo kinachoweza kuharibika, kuvunjika, kuporomoka na kwa hakika kabisa chaweza kuzama.
Hakuna ustadi wa mwanadamu unaoweza kufanya kazi zake zisiwe na makosa milele. Katika uelewa wetu huu mdogo wa kibinadamu ni kazi za Mungu tu ambazo hazina makosa.
Hivyo ninaposikia mtu anasema kwamba CCM itatawala milele, na kumtumbulia macho kama mjusi aliyekoswakoswa na mlango. Na pale ninaposikia kuna wana poropaganda wa CCM ambao "wanaitetea CCM kuwa ni chama safi na kina mafisadi wanne tu," ninafumba macho yangu kwa mshtuko.
Kama ningekuwa karibu na mtu huyo, ningemtingisha ili atoke katika usingizi wake uliochanganyika na ulevi wa madaraka.
Malumbano tunayoyasikia sasa na kugongana kunakoendelea hivi sasa ndani ya chama hiki na tutashuhudia zaidi miezi michache ijayo, yanatoa ushahidi wa jambo moja kubwa kuwa CCM kiko matatani na hakuna mtu wa kuiokoa.
Wale wanaogongana ndani ya CCM leo hii, hawagongani kwa sababu ya tofauti za kiitikadi (karibu wote hawana); wanagongana zaidi kuhusu maslahi yao ndani ya chama. Makundi yote yaliyopo ndani ya CCM leo yanatuhakikishia kuwa hayawezi kudumu ndani ya chama hichohicho yakiendelea kuongeza upana, ukali na uzito wa tofauti zao.
Gazeti toleo na. 150