Maisha halisi ya Burundi

umelenga mule mule , nafanya kazi in and out bujumbura nipo kigoma ,,, hujakosea mkuu , hasa umalaya . mrundi hana kawaida ya kumkatalia mtu na wanapenda starehe sana . vitu wanavyopenda warundi ni mavazi ,,, chakula kama wali , i mean mchele w kutoka tanzania . hawapendi kufanya kazi wakina mama zaidi ya kufanya vibiashara vya hapa na pale ,,,,, ukiwa disco usishangae mwanamke akakutongoza na ukikubaliana naye ukamuacha na kutongoza mwingine ,,, maisha yako yapo rehani.

kwa sisi wana kigoma , burundi ni sehemu muafaka sana kuendesha maisha , kwani bidhaa zetu tunanunulia burundi hasa mahitaji ya nyumbani mfano ,,, nyama kigoma tanzania kilo tshs6000/7000 ,,, burundi mugina tshs4000,,, maharage kg tz tshs1800 ,,, br tshs1000 . simu ndiyo usiseme bei ya tz na burundi kwa simu ile ile , tofauti unaweza kukuta tshs 30000/=. mwezi jana nimeacha change ya pesa ni tshs 10,000 kwa fr 11,500/=.

tatizo la kupitisha vitu border ndiyo changamoto , vitu vichache hutozwi ushuru wa tra , lakini vikiwa vingi unatozwa ushuru . mchele burundi kilo moja ni fr 3000 wakati sasa hivi kigoma ni tshs 1000-1200 kwa kilo ., ukipitisha mpakani chini ya kilo 100 huo ni wa kula hutozwi ushuru ,, mtu anajitahidi kukata mafurushi madogo madogo kwa kila gari anabeba kilo hata 400 kwa mkupuo . kuna makampuni ya mabasi ya hamza transit , burugo travel na luba express , yanayofanya usafiri bujumbura kigoma .
Kwaiyo fursa zipo nyingi ila nasikia vibaka kila sehemu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwana kabisa niwape pole kwa mihangaiko yenu ya kila siku wana JF.
Kama heading isemavyo hapo juu, mwezi uliopita/Septemba nilifanya ziara ya kitalii nchini burundi, kwa niliyoyakuta ni balaa tupu, very dangerous. Pia kama kuna Warundi humu basi mje mkanushe au myatolee ufafanuzi haya ninayoenda kuyaongea.
1.Hakuna kuoa zaidi ya mke mmoja, hili lilinishangaza sana ndipo nikaamua kulivalia njuga nikaulizia chanzo. Wenyeji waliniambia eti'' ubhanye abhagore bhenshi nta amatogo yachwiye''
2.Zaidi ya 90% ya wafanyakazi wa serikali ni wa chama tawala, wenyewe wanaita IMIGAMBWE. Kwa huku kwetu TZ, Maadili ya viongozi yanakataza wafanyakazi wa serikali kuwa na milengo ya kisiasa, ila kwa Burundi , Waalimu, madaktari, n.k utawakuta kazini wamevaa t-shirt zenye picha ya rais na chama chake cha CMDD-FDD
3.Mishahara ya wafanyakazi ni pasua kichwa, ni nusu ya hapa kwetu, ila watu bado hawagomi na wanachapa kazi. Mfano, Mwalimu wa shule za upili/Secondary school ni chini ya laki 3 Tsh
4.Wafanya kazi wa ndani ni shida tupu, wengine wanaita UBHUBHOYI au UBHUYAYA, yaani mtu unalipwa Tsh 4000/month,duuu pathetic.
5.Vijana wenye nguvu hukimbilia Tanzania katika mikoa ya Kigoma na Kagera kutafuta vibarua vya kulima mashamba, na hii ni kama uti wa mgongo wa kilimo cha mkoa wa Kigoma, Warundi ndio hulima mahekta mengi kwa ujira mdogo huku wao wakiona ni hela nyingi. Mfano, mtu unalima Hekari ya mita 100 kwa Tsh laki 1 then unaona hela nyingi, duuu
5.Mademu wa burundi ni pasua kichwa, zaidi ya 80% wanatumia pombe kama kuonesha Ubitoz. Na ukimtaka tu wewe mnunulie pombe basi, wanawaogopa watz eti ni Malaya/Abhagilanyi duuu, ila ukipiga kiswahili kizuri ukaahidi kumuoa basi yuko tayari, lakini hataki muishi Burundi bali Tz.

Ongezeeni na mengine, karibu kwa mjadala basi matusi nooo

nkobhe255
Hapo kwenye kipimo cha HEKARI YA MITA 100..... Ni kipimo kipya eti
 
Ngoja na mimi nifunguke .............

Burudhi ni nchi masikini sana yaani eneo lenye bata ni kama asilimia 5 tu ya nchi yaani bujumbura (ukubwa wa robo dar ) na vimiji vingine viwili ukubwa wa makambako ,ila bujumbura patamu ,maisha ni cheap sana kutokana na pesa yetu kuwa juu kidogo ya yao tshs 79000= 100,000 br hivyo ukilala lodge ya elfu 25,000 asee ninzuri balaa hadi fridge ,ila burundi centre ni aghali sana mahoteli ,ushauli wangu nendeni NIWAKALI hotel ipo bwiza ,inaulinzi balaa hata ukichukua malaya huingii naye kama hana kitambulisho na wanaki retain hadi uthibitishe uko salama na umeruhusu.
View attachment 922889
USWAZI BWIZA (MANZESE YA BUJUMBURA

View attachment 9228910


Warundi wengi sio waaminifu mfano usipande tax kabla hamjaelewana bei atakutoza bili utakimbia na wagonvi sana ,wakijua ww mtanzania wanajua umekuja kula bata au mnunuzi wa madini kuwa makini sana ,chakula kizuri ni ugali/ndizi na mishkaki yao maalumu inaitwa MICHOPOO inaseviwa na vitunguu vyeupe
View attachment 922892
View attachment 922893
MA-BEACH MAZURI BUJUMBURA

View attachment 922894
View attachment 922895
Hii inaitwa borabora beach ni nzuri balaa ,hapa wanaenda warudi wenye pesa magari utayoona ni latest na makali sana ,nyingine ni sagaplashe hii changanyikeni vitoto vizuri vya uswazi vimejaa wengi wanasura za wastani ila kiuno bonge la zigo ,lakini pia kwa dada zetu huwasifu warundi hususani waliochanganyika na watutsi ni mahandsome sana na wako masculine .

View attachment 922896
kuna club yao nimeisahau jina hii hapa ila nusu ya watu ni wazungu halafu hauruhusiwi kuingia na sandles wala singlet

View attachment 922899

Namengi ya kusema juu ya bujumbura niishie hapo
Funguka mkuu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
29 Reactions
Reply
Back
Top Bottom