Slave
JF-Expert Member
- Dec 6, 2010
- 5,314
- 2,635
Mambo vp wajomba natumai mpo poa.jamani hili jukwaa naona linazidi kuwa pana zaidi.ukijaribu kuchunguza utaona mada kubwa zinazojadiliwa ni ama mambo ya computer au mambo ya simu. Na modem.japo hivi vitu vinauwiano wa ki matumizi na vinavyotegemeana.mimi nilikuwa na wazo tujadiliane tuone kama kuna umhimu wa kumuomba moderator atutenganishie kurasa iwepo page ya computer na iwepo ya mobile phone.ili member aweze kuingia sehemu anayoona atapata anachohitaji.mfano hapa kuna DOWNLOADZ ni sehemu ambayo mtu inamuongoza kujua anachokwenda kukutana nacho. Kama nipo sawa unga mkono kama sipo sawa eleza kwa nini. nawakilisha