Re: Uteuzi wa wakuu wa mikoa na wilaya wanajeshi wastaafu nini athari zake

Technician

JF-Expert Member
Mar 30, 2010
841
222
Mikoa na Wilaya nyingi zinaongozwa na wanajeshi wastaafu katika nchi maskini iliyoko daraja la tatu la umaskini duniani,third world,Nini FAIDA na HASARA/ATHARI ya uongozi wa wastaafu wa Kijeshi katika kuongoza serekali ya kiraia Tanzania.
Je,Amri wanazotoa katika kuhakikisha sheria za uwajibikaji katika Nyanja za utendaji zinafuatwa au amri za kijeshi hazitekelezeki tena uraiani.
Je,Ufisadi unaotokea katika idara nyingi za serekali hazikaguliwi na hawa wastaafu wa kijeshi .
Nijuavyo mimi idara inayoongozwa na Mwanajeshi ni idara ambayo inatakiwa kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha nidhamu ya kazi ni hali ya juu,je,Tanzania hiyo ipo?
Kiongozi wa Nchi anapotokea Jeshini na kujiunga uraiani na kuanza harakati za kisiasa maana yake ni nini hasa,kutetea maslahi ya nani na kwa mtizamo gani.
Wanajeshi wa Tanzania wako katika kundi gani la kuwakomboa watanzania kwasababu wako ndani ya nchi ya Tanzania.
Fedha na rasilimali za Tanzania zinapoibiwa na makundi ya watu ndani ya nchi jeshi linakaa upande gani?
Tanzania ni nchi ngumu sana kuishi kama una roho nyepesi.
Umaskini uliokithiri na elimu duni ni ishara tosha kazi aliyoifanya muasisi wa Taifa hili Mwalim Nyerere haikufanikiwa ukiachia mbali Siasa ya ujamaa na kujitegemea,Azimio la arusha,azimio la musoma na mengineyo.
 
Back
Top Bottom