RE: Toa sababu kumi Kwanini Kikwete Asijiuzuru kwa Mauaji na Uhuni huu

QUALITY

JF-Expert Member
Sep 27, 2010
853
115
Wana JF mimi nimekuwa nafuatilia kwa makini matukio mbalimbali hapa nchini namna polisi (watanzania wenzetu) wanavyochinja watanzania wenzetu kwa visingizio mbalimbali. Tunakumbuka haya mauaji ya Tarime (north mara) tangu mgodi umeanza ikiwa ni pamoja na wizi wa maiti usiku; mauaji ya Arusha ya mandamano, mauaji ya wachimbaji kule penye tanzaniate (Tanzania one); huko kwenye mashamba ya wawekezaji Manyara na Huko mikoa ya kusini. n.k;

Bado Kikwete anaona anaongoza nchi? watu wote wakiuawa, ataongoza nini? Anahitaji watu wangapi wauawe ili aseme kuwa "Sasa najiuzuru?" kama anaona kusema nimejiururu ni vigumu basi aseme nimejivua gamba la Urais. Hatuhitaji Rais anayekaa kimya wakati maisha ya watanzania (innocents) wanauawa kinyama.

Aliyeenda kwa mguu mgodini (anayedaiwa kuiba mchanga wenye mali) anapigwa risasi na kuuawa; aliyeiba mabilioni mengi ya epa, anaambiwa arudishe jina halitajwi. Aliyeiba kidogo anafungwa jela!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Namshauri Kikwete ajiuzuru sasa hivi
 
Back
Top Bottom