RE: Natafuta rafiki wa kike anayeishi kwa matumaini.

Nashukuruni sana kwa kunitia moyo. Mimi najiona mzima kabisa pamoja na kwamba nimeathirika. Nitakuwa na dhambi isiyosameheka kama sitakuwa mkweli kwa hali yangu kwa ninayetarajia kumpata nikidanganya hali yangu. Maana ukidanganya kama binadamu asili yetu ni kurudi vumbini na kama mungu akipenda atatujalia neema yake ya ahera. NAOMBENI KAMA MNAYAFAHAMU MASHIRIKA YANAYOTOA USHAURI WA UHAKIKA MNISAIDIE MAWASILIANO YAO. Shida waafrika tunajificha kuelezea hali zetu. Mama yangu ameishi na virusi kwa takriban miaka 30 sasa na hana hata dalili ya kudhoofu afya yake. Asante.:)
 
Mimi ni kijana wa kiume nina umri wa miaka 20, nimeathirika na ninaishi kwa matumani. Bahati mbaya nilizaliwa na hiyo hali kwani mama na baba yangu ndiyo walikuwa wameshadhirika nilipozaliwa. Kwa bahati mbaya wadogo zangu watatu wote (3), na kaka yangu wameshatangulia mbele ya haki na Baba pia ametangulia mbele ya haki mama bado yupo. Nimeamua kutafuta rafiki wa kike kuanzia miaka 18-22 ili kama itawezekana na kulingani na ushauri wa daktari tuweze kutafuta mtoto maana siku hizi mnaweza kumpata mtoto ambaye hajaadhirika ili ukoo wangu usipotee.Maana inaonyesha historia baba yangu ndiyo inaishia hapa. Kama kuna ambaye yupo radhi naomba tuwasiliaane. Kutokana na hii hali yangu sijawahi kufanya mapenzi tangu nizaliwe. ndugu zangu wamenishauri pia kuwa nitafute rafiki wa kike aliyeadhirika na wao watachukua majukumu ya kutusaidia na kutunza mtoto kama mungu atatujalia endapo nitafanikiwa.
Asanteni
Kikilo

Mkuu, kwanza hongera sana kwa kuvunja ukimya. Wewe ni shujaa hapa JF. Umeokoa watu wengi kwa kusema ukweli, kwani ulikua unaweza kuweka bandiko zuri lenye sifa chungu tele pasi na kuainisha hilo tatizo ulilolisema na kuwavutia Dada zetu ambao nao wanahitaji wachumba hapa JF.

Nakutakia kila la heri umpate mwenza wako mtakae oana na kuzaa watoto wenye siha njema na wewe kuacha mbegu bora duniani itakayomjua M/Mungu kwa imani yako.
 
Pole kijana naamini utampata na usikate tamaa ishi kama wengine na timiza ndoto zako kila mtu anaish kwa hope hapa duniani sie wote twapita
 
kaka we jembe sababu wengi hawajui kinachowamaliza ni msongo wa mawazo na sio vidudu,we niambie unataka wa vigezo vip mi nikusaidie kutafuta
 
Hongera kwa ujasiri na ushujaa ndugu yangu. Sitaki kusema pole kwani inakufanya ujihisi mnyonge.
 
upande wa watoa mada, jamani mwenyewe ndio anaye ishi katika jamii hii yetu na anajitambua ndio maana amespecify nyie mnao sema hata ambaye hana mbona hamna kati yenu aliyesema mm hapa nipo tayari?
Ndugu mkiwa wote mnahali ya kufanana mnawakati mzuri sana wa kufurahia maisha zaidi ya the oposite.
Na mwisho ya yote Ndugu endelea kujitunza ugunduzi wa dawa halisi haupo mbali.
 
MUNGU akutangulie kwa kila jambo kuwa na maambukizo ya vvu si kufa,kifo anapanga yeye aliyetuumba.AMINA
 
Ndio.
Unaweza kufanya mapenzi na mwanamke ambae ameathirika na mkapata mtoto ambae yuko salama bila kipingamizi.
Ilimradi mmoja wenu asiwe na michubuko kwenye uume au ukeni.

Kama ingekuwa kufanya mapenzi na mtu aliyeathirika ni kupata ugonjwa, nadhani leo hii dunia ingekuwa nusu jangwa haswa kwa wapenda kugegeda.

ww unadhan unaweza kufanya mapenz sikuzote bila kupata michubuko????michubukoz are inevitable jomba!!
 
Utampata muombe Mungu

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
wewe ni kijana champion na unajitambua, unajua unachokitaka, hujakubali kuwa mtumwa wa hali yako, keep the spirit boy Mungu yu pamoja nawe. Nakuombea umpate soul mate wako soon.
 
naomba unitoe matongotongo machoni mwangu, kufanya mapenzi na mtu ambaye hajaathirika na mnapata mtoto bila mama kupata maambukizi

haya mambo ni changamoto sana ila yapo embu soma hii story ila ipo kwa kiingereza.

Living together as a serodiscordant couple

Godfrey_Paulina_Mtonga.jpg
CDC Zambia/Karrin Parker

Life was initially tougher for Godfrey and Paulina Mtonga of Lusaka, Zambia. The couple have now been married for 32 years. They have 11 children and 8 grandchildren. In 1994, they went for HIV testing together. Godfrey was positive and Paulina negative.
“The first week was very bad for us,” Godfrey recalls. “The counsellor came to visit us the very next day.” The counsellor kept coming, and the couple decided to stay together. They continued to have a sexual relationship, using condoms from a nearby clinic. Godfrey started taking antiretroviral treatment in 2002. Pauline has remained HIV-negative.
Godfrey Mtonga’s advice to everyone is to get tested. “If you are positive, love each other and take your medicine at the right time. We have lived with our status as a discordant couple for the past 18 years because we support each other.”

nimeipata WHO | Living with HIV when one partner is positive and the other is negative
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom