Kumbe hujui unachoongea.
Akili yako imeshapumbazwa na ushabiki. Pole sana...
marcopolo mbona hujibu unayoulizwa,hatupo kwa majibu ya short answerz kama tupo primary weka hoja na uitete acha kuwa na majibu general
Kumbe hujui unachoongea.
Akili yako imeshapumbazwa na ushabiki. Pole sana...
Kumbe hujui unachoongea.
Akili yako imeshapumbazwa na ushabiki. Pole sana...
Ah!!!!!!!!! Kwamba Dr analipia kadi yake hatuwezi kuamini. Hiyo ni propaganda tupu. Tumeipuuza. Kikubwa tutamshauri aiweke kwenye maktaba ya CDM pamoja na za wengine ambao wasingependa kutia kiberiti za kwao kama kumbukubu ya walipokuwa watumwa wa magamba.Changamoto kwa wana wa magamba ikiwa mnadhani doctor anawasaidia kelele za nini???????? Hapa CDM mtu yeyote anayesaidia ukombozi wa taifa hili anakaribishwa. Na anatizamwa kwa kazi na ufanisi wake.Ushahidi gani zaidi unaohitajika zaidi ya maneno yake mwenyewe aliyotoa ya kukiri?
Kumbe hujui unachoongea.
Akili yako imeshapumbazwa na ushabiki. Pole sana...
Mkuu Tumaini Makene sisi ambao siyo verify user Kama ZeMarcopolo kazi yetu ni kutukana na kuingia mitini ndio maana hawezi kujibu hoja za mohamed Mtoi kwasababu siyo kipimo chakeMkuu ZeMarcopolo
Kamanda Mtoi amekutaka ujibu hoja, mbona unakimbia?
Kama Slaa anaona umuhimu wa kuitunza kadi yake, kwanini amekuwa mstari wa mbele kukusanya kadi za CCM za wenzake na kuzichana na kuchoma moto? Kwahiyo kadi yake yeye iheshimiwe ila za wengine zichomwe moto???
Vilevile, kuwa na kadi ni one thing na kuilipia ada ni another thing. Kuilipia ada ni kumaanisha kuwa Slaa ni mwanachama HAI wa CCM.
Mnaweza kutafuta spin na porojo mbalimbali, lakini wenye akili wameshaelewa kinachoendelea kama jinsi alivyosema Dr. Slaa mwenyewe kuwa "akiba haiozi".
Mkuu ZeMarcopolo
Kamanda Mtoi amekutaka ujibu hoja, mbona unakimbia?
Umbumbumbu mwingine ni wa kujitakia. Jambo liko wazi kabisa na wala porojo za Ndimara haziwezi kujibu maswali ya msingi ambayo ni
1. Kwanini Slaa alindelea kulipia kadi?
2. Katiba ya CHADEMA inakataza waziwazi umiliki wa kadi mbili, je kwanini Katibu Mkuu wa chama awe mwanachama wa vyama viwili kwa siri?
3. Aliposema "akiba haiozi" alimaanisha nini? Kama Slaa amejiwekea akiba hiyo, anamshauri mwana CHADEMA "wa kawaida" ajiwekee akiba gani???
Kama Slaa anaona umuhimu wa kuitunza kadi yake, kwanini amekuwa mstari wa mbele kukusanya kadi za CCM za wenzake na kuzichana na kuchoma moto? Kwahiyo kadi yake yeye iheshimiwe ila za wengine zichomwe moto???
Vilevile, kuwa na kadi ni one thing na kuilipia ada ni another thing. Kuilipia ada ni kumaanisha kuwa Slaa ni mwanachama HAI wa CCM.
Mnaweza kutafuta spin na porojo mbalimbali, lakini wenye akili wameshaelewa kinachoendelea kama jinsi alivyosema Dr. Slaa mwenyewe kuwa "akiba haiozi".
Ndimara!!!!!!!!!!! Ah!!!!!. Yule kada wa CCM?
Mkuu tunaitika ndiyo kwa taswira uliyoonesha hapa juu. Lakini kwa kuwa kiukweli sisi wengine hatutaki hata kusikia harufu ya JAMAA WA KIJANI basi ni vizuri kiongozi wetu na kipenzi Dr wa ukweli na wana CDM wote wenye kadi za Magamba wazikabidhi kadi hizo ili zihifadhiwe kwenye maktaba itakayoanzishwa na CDM makao makuu. Hakika tusidharau wingu linaloendelea maana lina athari zake kisiasa. Pili siungi mkono hata kidogo kwa hao wanojiita viongozi wa BAVICHA na matamko yao, ninafahamu chama kina mfumo wake wa kujadili mambo yake hivyo tulitarajia hao jamaa kufuata nidhamu hiyo. Wakumbuke yaliyowapata NCCR mageuzi na baadaye TLP miaka ya 2007 na kuendelea. Tusingependa yatokee CDM. Ni lazima viongozi wawe na nidhamu. Na wajiulize hayo matamko yanamfaidisha nani hasa???
dr slaa huwa hakusanyi kadi ya mtu yeyote ili ikachomwe.bali zinapelekwa na watu wenyewe ili zikachomwe baada ya kuchoshwa na ccm na serekali yake.ni sawa na kutupa jongoo na mti wake.
zeemarcopolo hajui anayoongea nimemwmbia atoe proof naona anjing'ata kucha labda tumpe mda.
Repetitive.Sikuwahi kukata kadi ya chama hicho.
Sikuwahi kuwa na kadi ya TANU.
Na hicho nacho ulishakisema.Lakini nina kadi ya Umoja wa Vijana wa TANU (Tanu Youth League - TYL).
Lakini bado nina kadi yangu ya TYL.
Mkuu, hapo kwenye kulipia si kweli. Aliyeleta madai hayo anapaswa alete na uthibitisho.Siioni mantiki ya ndimara katika hili maana haina majibu ya maswali mama ya kumiliki kadi za vyama viwili na anazilipia zote huku yeye akiwa mstari wa mbele kukusanya za wenzake hadharani
Mkuu.
Tulia kidogo maana unaonekana una mhemko sana! Haya mambo yanahitaji akili iwe sober na objective ndio tujadiliane. Lakini pia yanahitaji critical thinking and visionary analysis.
1.Una ushahidi kuwa Dr Slaa anailipia/amelipia kadi ya ccm? Kama ndio weka ushahidi twende sawa maana great thinkers hawana tabia ya kuzomoka bila ushahidi.
2. Umesema "katiba ya chadema hairuhusu mtu kuwa na kadi mbili" (sema ni ibara gani acha kuleta majibu ya jumla). Lakini pia naona hapa una maanisha kadi kwa maana ya kadi tu au uwanachama wa chama kingine? (Kumbuka kuwa mtu una ruhusiwa kuwa mwanachama wa chama kimoja tu! Haijasemwa kuwa usiwe na kadi tingine maana walijua kuwa huenda mtu akahama kutoka chama kimoja kwenda chama kingine)
3. Amesemea wapi kuwa hakiba haiozi? Na jee mtu akisema hakiba haiozi akili ya kawaida inakushughulisha kutaka kujua zaidi ya hapo au umeangalia kwa miwani ya kadi peke yake?
Unachotakiwa kukijua.
1. kisheria kadi unayo inunua kwa pesa zako ni mali yako si mali ya chama. Ukihama chama au kuacha kuilipia ni haki yako/ridhaa yako kubaki nayo, kuichoma, kuitupa au kuihifadhi. Hakuna mtu anayeweza kukudai kadi uliyo nunua kwa pesa zako.
2. Kadi ambayo si mali yako ni kama kadi za benk, au kitambulisho cha kazi. Hizi zinakuwa mali ya benki au mali ya waajiri. Ukiacha kazi moja ya sharti kubwa ni kurejesha kitambulisho hicho.
Kama hivyo ndivyo fungua milango yako ya fahamu bila kuwa na chembe ya propaganda na uruhusu tafakuri tunduizi (critical thinking) kichwani mwako.
Karibu kwa hoja.
acha maneno mengi tunza kadi yako ya CCM kama atunzavyo katibu wako si unajua usitupe mbachao kwa msala upitao.Slaa anazingatia sana huu msemo namsifu kutunza kadi na uhai wa kadi hiyo kwa miaka 17!