RC wa Mbeya (CHALAMILA) aagiza waliomtupia mawe DC wapigwe sana hata wakifa sawa tu hawana hasara

MINOCYCLINE

JF-Expert Member
Apr 2, 2015
8,011
16,748
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Albert Chalamila amesema Wananchi wote waliohusika kuushambulia kwa mawe Msafara wa Mkuu wa Wilaya ya Kyela Claudia Kitta na timu nzima ya Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya hiyo watachukuliwa hatua kali kwani walidhamiria kuwaua Viongozi hao.

“Ni mkong’oto usiku kucha, sababu walirusha mawe na walidhamiria kumuua Mkuu wa Wilaya hawa wamechagua kuuawa wao, hili sio kinyume cha Haki ya Binadamu, haki ya binadamu alipaswa kuwa nayo yeye kabla hajampiga au hajaharibu lile gari” RC Mbeya

“Kikosi kazi kisitoke mpaka nione furaha imejaa moyoni, nawaambia ukweli na hapa bado sijakunjua kikosi kingine, hapa Mbeya kuna kikosi kipo Itende vimenyamaza, tunasubiri watu wajikunjue tupige king’ora cha mwisho” RC Mbeya

Chanzo Taarifa: MillardAyo.

Sijui Rais JPM huwa anawaokota wapi hawa Wapuuzi.
 
Ttzo anayewateua

Naanza Kushawishika sasa kuwa huenda hata nae ( Mteuwaji ) wake / wao ana matatizo labda hata ya kuwazidi hawa. Na nilitegemea baada ya huyu RC Kutoa Kauli hii isiyo ya Kibusara na Hekima kabisa kama Kiongozi mwenye Dhamana basi Ikulu ingetoa taarifa rasmi ya Kutengua hiyo nafasi yake. Kauli yake hii haitibu bali ndiyo sasa inazidisha matatizo na hapa Serikali ya JPM itazidi Kuchafuka.
 
Huyo RC ni mgonjwa wa akili ukimsikiliza hakuna kabisa ushirikiano kati ya ubongo wake na mdomo.

Hata pendekezo la Bashiru la kumpeleka shuleni halitadaidia hadi kwanza afikishwe Milembe akiwa amefungwa kamba mikono.

Kiongozi gani mwenye hekima na kujitambua anaweza kufungua mdomo na kutamka maneno hayo.

Huyu kama sheria ingekuwa msumeno angetakiwa kuwa ndani kwa uchochezi. Totally Embecile
 
Yupo Happy na bosi wao bashite.Hovyo kabisa. Mwenzao Gambo kakua kaacha ujinga wao ndio kwanza wanafanya mambo ya kipumbavu kabisa
Nikiambiwa huyu havuti Bangi nitabisha hadi Kiama kitakapokuja rasmi. Ni Mmoja wa Viongozi wa hovyo hovyo ( ukiachia Yule mwingine ) ambayo Serikali hii ya Awamu ya Tano imebahatika Kishetani kuwa nao.
 
Rais naye toka ndege imetiwa korokoroni huko SA haongei tena. Hawa wapumbavu ndio wana pwayuka mambo ya hovyo kabisa. Kuna kengine kule Kigamboni kenyewe kamesema kakikamata vibaka ni.kupiga na kuvunja miguu. Mahakama zina kazi gani sasa?
" Ni mkong'oto usiku kucha, sababu walirusha mawe na walidhamiria kumuua Mkuu wa Wilaya hawa wamechagua kuuawa wao, hili sio kinyume cha Haki ya Binadamu, haki ya binadamu alipaswa kuwa nayo yeye kabla hajampiga au hajaharibu lile gari " RC Mbeya.

Chanzo Taarifa: MillardAyo.

Sijui Rais JPM huwa anawaokota wapi hawa Wapuuzi.
 
" Ni mkong'oto usiku kucha, sababu walirusha mawe na walidhamiria kumuua Mkuu wa Wilaya hawa wamechagua kuuawa wao, hili sio kinyume cha Haki ya Binadamu, haki ya binadamu alipaswa kuwa nayo yeye kabla hajampiga au hajaharibu lile gari " RC Mbeya.

Chanzo Taarifa: MillardAyo.

Sijui Rais JPM huwa anawaokota wapi hawa Wapuuzi.
Hao vichaa wenzake ndiyo anawataka. Hawezi kuwa kichaa peke yake atakuwa bored sana.
 
Maneno aliyosema hayafai kusemwa hadharani kwa kiongozi kama yeye ila hao wahuni waliorusha mawe kwenye gari la mkuu wa wilaya walistahili adhabu kubwa sana kuliko hata aliyosema mhe RC kwa sababu kuu 2

1. Walikuwa na lengo la kudhuru mtu ambayo ni haki ya mtu kuishi pasipo tishio lolote la usalama kwake awe kiongozi au raia wa kawaida.

2. Walikuwa na lengo la kuharibu mali ya serikali ambayo imenunuliwa kwa kodi zetu watanzania hivyo hawana tofauti na wahujumu uchumi wengine
 
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Albert Chalamila amesema wananchi walioshambulia msafara wa Mkuu wa Wilaya ya Kyela Bi.Claudia Kitta, watapewa mkong'oto usiku kucha wa leo na hata wakifa ni sawa tu, maana hata wao walidhamiria kuua.
_
"Ni mkong'oto tu usiku kucha. Kama watakufa sawa tu kwa sababu walidhamiria kumuua Mkuu wa Wilaya, kwahiyo hawa wamechagua kuuawa wao. Na hii sio kinyume cha Haki ya Binadamu. Wao walipaswa kuzifahamu haki za binadamu kwanza kabla hawajampiga DC" amesema Chalamila.
 
Back
Top Bottom